RC KUNENGE AGEUKA MBOGO, AWAJIA JUU WATUMISHI WANAOKUTWA NA TUHUMA MBALIMBALI
DKT.SENGATI KUKUTANA NA FAMILIA ZINAZOTELEKEZA WAZEE WAO
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akiongea na baadhi ya wazee waliofika katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Shinyanga na kujadiliana nao kuhusu masuala mabalimbali yahusuyo wazee hao.
Baadhi ya wazee wa Mkoa wa Shinyanga wakisikiliza hoja mbalimbali za viongozi wa mkoa wa Shinyanga jana mkoani Shinyanga.
MKUU wa mkoa wa Shinyanga Dkt Philemon Sengati amehaidi kulifanyia kazi suala la wazee wanaotelekezwa na watoto wao kwa kuitisha vikao vya familia kwa lengo la kuzitaka familia hizo kubeba jukumu la kutunza wazee lakini pia kurejesha mahusiano yao.
Dkt. Sengati alitoa ahadi hiyo baada ya baadhi ya wazee wa Mkao wa Shinyanga kudai kuwa baadhi yao wametekelezwa na watoto wao na wengine kuachiwa kulea wajukuu na watoto wao ambao wana nguvu za kutosha kuwatunza watoto pamoja na wazee.
Dkt. Sengati alisema hayo jana alipofanya kikao cha pamoja na wazee wa mkoa wa Shinyanga ikiwa ni hatua yake muhimu ya kukutana na kusikiliza makundi tofauti ya jamii katika Mkoa wa Shinyanga.
Adha Dkt. Sengati aliwambia wazee hao kuwa ataendelea kuimarisha mabaraza ya wazee mkoani humo kwani baadhi ya mabaraza hayo hayafanyi kazi vizuri na kuziagiza Halmashauri za Mkoa wa Shinyanga kufanyia kazi changamoto za kibajeti ili wazee hao waweze pia kupata mikopo ya Halmashauri kama ilivyo kwa makundi mengine.
‘’Tutaendelea kushughulikia changamoto za kibajeti hasa ile asilimia mbili ambayo huwa ni lazima itengwe kutoka mapato ya ndani kwa lengo la kuwahudumia wazee kama kundi maalum lakini imekuwa haiwekwi na kwa namna moja au nyingine mmekuwa hamuipati.’’Aliongeza kiongozi huyo wa Mkoa wa Shinyanga.
Aidha Dkt. Sengati ametaka kila mwana Shinyanga kujielimisha lakini pia kutoa elimu kuhusu mira na desturi na imani potofu ya mahuaji ya wazee na kuwa na mtazamo chanya kwa kundi hili la wananchi hodari.
Katika hatua nyingine Dkt. Sengati alizitika Halmashauri za Mkoa wa Shinyanga kuendelea kuelemisha wazee hao namna bora ya kupata mikopo kutoka katika Taasisi za fedha na Halmashauri ili wazee waweze kijihimarisha kiuchumi na kuchangia katika Maendeleo ya Taifa.
Naye Mzee Mohamedi Mkambala mkazi wa Manispaa ya Shinyanga alimwambia Mkuu wa Mkoa kusaidia wazee katika suala zima la kimatibabu kwani wazee hao mara kwa mara wamekuwa wakiandikiwa madawa ambayo yamekuwa hayapatikani hospitalini.
‘’Kuhusu suala la Afya wazee wanapewa dawa za bure lakini wamekuwa wakiandikiwa kwenda kununua dawa izo hela watapata wapi wakati wana andikiwa dawa za bure?Alihoji Mzee Mkambala.
Katika madai tofauti tofauti ya wazee hao Bi. Judithi Kalwalala aliangazia suala la usalama na kuomba msaada wa Jeshi la Polisi kuingilia kati kwani vibaka wamekuwa wakivamia nyumba zao wakiwa wamevalia madera na kuwabia mali zao huku wakijua hakuna wanaume wakuwalinda.
Dkt. Sengati jana alifanya kikao cha pamoja na wazee wa mkoa wa Shinyanga ikiwa ni hatua yake muhimu ya kukutana na kusikiliza makundi tofauti ya jamii na atakutana na makundi mengine kama hayo kwa lengo la kuona namna bora kufanyia kazi matatizo ya wananchi mkoani Shinyanga.
UBALOZI WA FINLAND WACHANGIA PICHA, VITABU MAKUMBUSHO YA TAIFA
UONGOZI INSTITUTE KUWAPIKA VIONGOZI WA UMMA NA WATEULE RAIS
*Serikali yaeleza kutotegemea viongozi kwenda kinyume na maadili na haki baada ya mafunzo hayo
Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
WAZIRI wa nchi, ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mohammed Mchengerwa amesema kuwa viongozi wote walioteuliwa wakiwemo wakuu wa Mikoa, Wilaya pamoja na Wakurugenzi lazima wapitie mafunzo wa Uongozi yanayotolewa na Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute) taasisi ambayo imekuwa ikiwaandaa na kuwapika viongozi ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia haki, maadili na weledi.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akizundua bodi ya tatu ya wakurugenzi ya Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute,) Waziri Mchengerwa amesema, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alitoa maelekezo hayo kwa viongozi wote wa Umma wakiwemo wakurugenzi, wakurugenzi wasaidizi, wakurugenzi wa Wizara, viongozi walioteuliwa na Mawaziri kupata programu za mafunzo maalumu ya uongozi kutoka Taasisi ya Uongozi ambayo imerejesha sifa ya kupika viongozi.
'' Ili watendaji wafanye kazi kwa weledi katika nafasi zao walizoteuliwa na wanazozitumikia wakiwemo vijana lazima wapite katika mikono ya Taasisi ya Uongozi ili watumikie nafasi zao kwa kuzingatia maadili, haki na weledi.'' Amesema.
Waziri Mchengerwa amesema, Hakuna kiongozi yeyote wa Umma na kuteuliwa ambaye hawatapitia mafunzo hayo na hawategemei baada ya mafunzo hayo viongozi hao kwenda kinyume na haki na maadili wa uongozi katika utekelezaji wa majukumu yao.
Pia amesema, Bodi ya wakurugenzi wa Taasisi ya Uongozi iliyozinduliwa leo imesheheni wataalamu wa elimu na viongozi wabobevu ambao watashirikiana na Taasisi hiyo ambayo Serikali inatambua mchango wake wa kuikuza Taasisi ya Uongozi ndani na nje ya nchi.
kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute,) na Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC,) Dkt. Stergomena Tax amesema, bodi mpya ya Taasisi ya Uongozi inamshukuru Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania kwa uteuzi huo na watafanya kazi na kuhakikisha wanafikia lengo kuu la kujenga viongozi watakaoleta maendeleo endelevu nchini.
Dkt. Tax amesema, Wanatambua umuhimu wa viongozi mahiri na watasimamia jukumu hilo katika kuhakikisha viongozi wanajengwa katikla miiko ya maadili na kutekeleza majukumu yao kwa weledi zaidi.
''Sio kwamba viongozi hawapo....Wapo ila mambo yanabadilika kila siku lazima viongozi waende na maendeleo ya kidunia.'' Amesema Dkt. Tax.
Awali akieleza majukumu ya Taasisi hiyo Afisa Mtendaji wa Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute,) Dkt. Kadari Singo amesema, Taasisi hiyo ina jukumu kubwa la kuandaa na kuendesha mafunzo kwa viongozi, kuendesha majadiliano ya kisera na kufanya tafiti za kisera, kutoa ushauri wa kitalaam na kuzisaidia taasisi mbalimbali pamoja na viongozi wake katika kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute,) ilianzishwa Julai, 2010 kwa malengo ya kuwa na kituo cha utalaam wa juu cha kuendeleza viongozi barani Afrika kwa kuanzia nchini Tanzania, Kanda za Afrika Mashariki na hatimaye Afrika nzima.
RAIS SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA MWENYEKITI WA MAKAMPUNI YA WILMAR INTERNATIONAL, IKULU DAR ES SALAAM

Makinda amrithi Salim Ahmed Salim HKMU


Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Kumbukumbu cha Hubert Kairuki (HKMU), John Ulanga akimvalisha kofia Mkuu mpya wa Chuo hicho, Anne Makinda kama ishara ya kumsimika rasmi kwenye nafasi hiyo. Makinda anachukua nafasi ya Salim Ahmed Salim. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Afya na Elimu la Kairuki, Kokushubila Kairuki.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki (HKMU), Spika mstaafu Anne Makinda akiongoza kwenda kwenye hafla ya kumsimika rasmi kuwa mkuu wa chuo hicho jana jijini Dar es Salaam Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, John Ulanga na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Afya na Elimu
WAZIRI SIMBACHAWENE AITAKA POLISI KUDHIBITI UTOAJI, UKAGUZI WA SILAHA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kulia) akimsikiliza Kamishina wa Polisi wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, CP Benedict Wakulyamba, akizungumza katika Kikao cha Wajumbe wa Bodi ya Tatu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, jijini Dodoma, leo, kabla ya Bodi hiyo haijazinduliwa. Waziri huyo ameitaka Polisi kudhibiti Utoaji na ukaguzi Nchini na pia ishirikiani na sekta binafsi za ulinzi ili kuweza kuimarisha ulinzi na usalama wa Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto), akimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Tatu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, Toyi Ruvumbangu, jijini Dodoma, leo, kabla ya Waziri huyo hajaizindua Bodi hiyo. Waziri huyo ameitaka Polisi kudhibiti Utoaji na ukaguzi Nchini na pia ishirikiani na sekta binafsi za ulinzi ili kuweza kuimarisha ulinzi na usalama wa Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kulia), akimsikiliza Katibu wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), John Massawe, jijini Dodoma, leo, kabla ya Waziri huyo hajaizindua Bodi hiyo. Waziri huyo ameitaka Polisi kudhibiti Utoaji na ukaguzi Nchini na pia ishirikiani na sekta binafsi za ulinzi ili kuweza kuimarisha ulinzi na usalama wa Nchi. Katikati ni Kamishina wa Polisi wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, CP Benedict Wakulyamba.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (katikati aliyekaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Tatu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi, jijini Dodoma, leo, baada ya Waziri huyo kuizindua Bodi hiyo. Ameitaka Polisi kudhibiti Utoaji na ukaguzi Nchini na pia ishirikiani na sekta binafsi za ulinzi ili kuweza kuimarisha ulinzi na usalama wa Nchi. Wapili kushoto waliokaa ni Kamishina wa Polisi wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu, CP Benedict Wakulyamba. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
NMB YAKABIDHI SERIKALI HUNDI YA ZAIDI YA BILIONI 21.7
SERIKALI IPO TAYARI KUPOKEA MAONI YA WADAU ILI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU - WAZIRI NDALICHAKO

SERIKALI KUFUNGA KAMERA ZA USALAMA DODOMA
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka(wapili kushoto), akisikiliza maelezo ya Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Polisi Chang’ombe kutoka kwa Mrakibu Mwandamizi wa Polisi, Zakaria Senso baada ya Uwekaji wa Jiwe la Msingi wa Ujenzi wa kituo hicho leo, kinachojengwa katika Kata ya Chang’ombe, jijini Dodoma.Wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Ramadhani Kailima.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde (wapili kulia), akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka mifuko ya saruji ikiwa ni mchango wake katika Ujenzi wa Kituo Kipya cha Polisi Chang’ombe lengo ikiwa kudhibiti uhalifu katika maeneo ya Changombe.Wapili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Ramadhani Kailima.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
*************************
Abubakari Akida, Dodoma
Serikali imedhamiria kufunga kamera za usalama katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dodoma kwa lengo la kupunguza uhalifu ambao umeanza kushamiri katika maeneo ya jiji hilo baada ya Serikali kuhamia Dodoma huku wimbi la watu likichagiza hali hiyo ya uhalifu.
Hayo yamesemwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka wakati wa Hafla ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Kituo cha Polisi Chang’ombe kinachojengwa katika eneo la Chang’ombe, jijini Dodoma.
Adhma hiyo ya kujenga kituo imekuja baada ya matendo ya uhalifu ikiwemo uporaji, ubakaji, udhalilishaji, matumizi ya dawa za kulevya kushamiri katika maeneo ya Chang’ombe hali inayopelekea wananchi wa maeneo hayo kuishi kwa wasiwasi wakihofia matendo hayo ya uhalifu.
“Maeneo mengi ya jiji la Dodoma tutafunga kamera za usalama barabarani, hatuwezi kuwa na jiji ambalo polisi wetu wanakimbizana na wahalifu muda wote, tutatumia teknolojia hiyo kudhibiti uhalifu wa aina mbalimbali, Dodoma ni Makao Makuu ya nchi lazima pawe salama nawashauri wahalifu watafute shughuli nyingine ya kufanya hapa si salama tena kwa kazi zao” alisema Mtaka
Akizungumzia Ujenzi wa Kituo hicho cha Polisi, Mkuu wa Mkoa huyo aliwataka wananchi kushirikiana na serikali kuhakikisha kituo hicho ujenzi wake unakamilika mapema ili kianze kutoa huduma za kiusalama katika maeneo hayo.
“Chang’ombe inakua inahitaji kituo kikubwa kitakachofanya kazi saa ishirini na nne ili wafanyabiashara na wananchi wafanye shughuli zao kwa muda wote na sio biashara zifungwe kwa kuhofia uhalifu, sasa kazi ya serikali sio kukwambia ufunge biashara yako muda gani kazi ya serikali ni kukulinda ili kuwepo na uhuru wa kutoa huduma, kwahiyo wananchi tushirikiane ili kituo kimalizike haraka” alisema Mtaka
Akizungumza kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Naibu Katibu Mkuu Ramadhani Kailima alisema wizara imetoa kiasi cha shilingi milioni 10/= kama mchango wake katika ujenzi wa kituo hicho na kikikamilika kitaweza kutoa huduma mbalimbali ikiwemo upelelezi wa matukio, upelekaji wa majarada ya kesi kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka ambayo yatapelekwa mahakamani kwa hatua za kisheria.
Katika hafla hiyo Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini, Anthony Mavunde alichangia papo hapo mifuko hamsini ya sementi kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho na kumkabidhi Mkuu wa Mkoa Anthony Mtaka.
SERIKALI YAJIPANGA KIMKAKATI KUVUTIA WAWEKEZAJI NCHINI - WAZIRI MKUMBO
Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
SERIKALI imesema imejipanga kisera na kutoa huduma muhimu na sheria rafiki zinazokidhi na kuvutia wawekezaji wa nje na ndani ya nje ya nchi ili kuwezesha ukuaji wa biashara ndani ya bara la Afrika na nje ya nchi.
Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Viwanda na Biashara Prof. Kitila Mkumbo wakati akizindua kongamano la uhusiano baina ya maeneo maalumu ya uwekezaji na uchumi wa ndani lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi Tanzania (Uongozi Institute,) pamoja na Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA,) na kuwakutanisha wawekezaji wa ndani na nje na kujadili namna ya kuunganisha maeneo muhimu ya uwekezaji na uchumi wa ndani pamoja na kuangalia namna ya kushirikisha wawekezaji wa ndani hasa wajasiriamali.
prof. Mkumbo amesema, katika kuhakikisha uchumi wa nchi unashindana kimataifa Serikali na taifa kwa ujumla linaendelea kujiunga na jumuiya mbalimbali za kikanda na kimataifa ili kushindana kimataifa kama ilivyoelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan juu ya msingi wa kuimarisha biashara ndani ya Afrika na nje ya mipaka kwa kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kukuza uchumi wa taifa.
''Serikali imejipanga kisera, huduma muhimu katika maeneo ya uwekezaji, skills muhimu katika elimu ili kwenda na matakwa ya soko kwa ujumla pamoja na sheria za kodi katika kuhakikisha uwepo wa uzalishaji wenye tija katika maeneo ya viwanda.'' Amesema.
Aidha amesema, Serikali imejipanga Katika ujenzi wa mitaa ya viwanda "Industrial parts" pamoja na kutangaza fursa za uwekezaji katika maeneo ya uwekezaj ya Kurasini, Bagamoyo na Benjamin Mkapa mkoani Dar es Salaam.
Kwa upande wake kaimu mtendaji mkuu wa Mamlaka ya Maeneo Maalumu ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA,) John Mnali amesema mamlaka hiyo imekuwa ikitekeleza majukumu katika maeneo ya uwekezaji kwa niaba ya Serikali kwa kuhakikisha maeneo yote ya uwekezaji yanapata huduma muhimu hasa miundombinu ya maji, umeme na barabara pamoja na kutoa leseni za uwekezaji kwa wawekezaji hao.
Amesema, wamekuwa wakishirikiana na Wizara ya viwanda na biashara pamoja na wadau wengine wa uwekezaji kwa kuhakikisha wanayafikia mafanikio kwa kiwango kikubwa na hadi sasa wamesajili kampuni zipatazo 176 zenye uwekezaji wa dola za kimarekani bilioni 2.5 na watanzania 58198 wamenufaika kwa kupata ajira za moja kwa moja hadi kufikia Machi, 2021.
Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi (Uongoz Institute,) kwa kushirikiana na EPZA liliwakutanisha wawakilishi wa Serikali za mitaa, wawakilishi wa biashara ndogondogo na kati, kampuni za uwekezaji, Taasisi za Fedha, Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara.
Benki ya UBA yatoa vitabu vya fasihi kwa vituo vya watoto yatima Dar es Salaam
Mkutano Mkuu Wadau wa Kahawa: Serikali Yaviasa Vyama Vya Ushirika Matumizi Bora Ya Mikopo, NBC Yaelezea Suluhisho.
MSISUBIRI DAKTARI AWAANDIKIE MAFANYE MAZOEZI- DKT MGAYA
Na Avila Kakingo


NMB ups its stake in Zanzibar’s tourism as hoteliers unite
Zanzibar. NMB Bank Plc is upping its stake in Zanzibar tourism in an effort to play an increasingly important role in the growth of the most important economic sector in the Isles’ economy.
Through its involvement with the newly-formed Hotel Association Zanzibar (HAZ), NMB Bank Plc said at the weekend that apart from several tourism-related products that were already on offer in Zanzibar, the lender was also bringing several others in the coming few weeks.
“You shall recall that we launched our E-Commerce Payment Gateway and our UnionPay products right here in Zanzibar. The products are meant to aid transactions associated with tourism. With our partnership with HAZ, we are soon going to do much more, including a special card for tourists,” said the bank’s chief of retail banking, Mr Filbert Mponzi.
He was speaking during an event to officially launch HAZ which was graced by Zanzibar’s Second Vice President, Mr Hemed Suleiman Abdulla.
With its bancassurance products, the bank has entered into partnerships with ten insurance firms, including the Zanzibar Insurance Corporation.
“If taken seriously in Zanzibar, this could offer a lasting solution to such accidents as fire that raze hotels time and again and other risks associated with the tourism sector…Hotels could look up to using bancassurance to mitigate risks associated with damage of properties such as hotels, boats and yacht among others,” he said.
NMB Bank Plc’s ATM machine that has the ability to exchange foreign currency will soon be set up at Amani Karume International Airport Zanzibar.Gracing the event, Mr Hemed Suleiman Abdulla said the coming of HAZ should help to invigorate the tourism industry which had been facing several challenges associated with the Covid-19 pandemic.
“HAZ members should also join hands with the government in preparing a comprehensive recovery plan,” he said.
He said when he inaugurated the House of Representatives in November last year, President Dr Hussein Mwinyi assured investors that his country would leave the doors open for their engagement in creating jobs in line with the government’s Blue Economic model.
HAZ, he said, must work with Zanzibar Association of Tourism Investors (Zati) and Zanzibar Association of Tour Operators in promoting the Isles’ attractions globally.According to the HAZ chairman, Mr Paolo Rosso, last year, Zanzibar received 528,425 tourists who earned the country a total of $426 million in forex earnings.
There were 582 hotels with a total of 9,860 rooms in Zanzibar.
Tourism accounted for 82.1 percent of Foreign Direct Investment (FDI) in Zanzibar, he said, noting that each year, ten new hotels were being built in the Isles, each consuming $30 million in average investment.
“The amount that each tourist spends in Zanzibar has also gone up from an average of $80 per day in 2015 to $206 in 2020,” he said.
HAZ will be the principal voice of all hotels in Zanzibar on issues pertaining to the sectors’ engagement with the government and other agencies.
NMB Bank employees in a group photo with the guest of honor and HAZ Board of Directors.
NMB Bank Chief of Retail Banking receives a certificate of appreciation from Zanzibar’s second vice president, Hon. Hemed Abdulla to recognize the bank’s role towards the development of the tourism sector in the isles.
NMB Bank Chief of Retail Banking, Filbert Mponzi speaks during the launch of Hotel Association of Zanzibar at an event held in the isles over the weekend.
NMB Bank Chief of Retail Banking, Filbert Mponzi welcomes Zanzibar’s Second Vice President, Hon. Hemed Suleiman Abdulla who was the guest of honor at the launch event.
Shule ya sekondari Academic Achievement yafanya mahafali ya kidato Cha sita.
Mbunge wa Mchinga mkoani Lindi, Salma Kikwete amehimiza wanafunzi kusoma masomo ya sanyansi na hisabati akisema ni muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Alisema mafanikio katika masomo ya sayansi na hisabati ndiyo yakatayotengeneza nguvu kazi nzuri na madhubuti ya kuleta maendeleo ya uhakika.
Mama Salma alieleza hayo jana katika hotuba yake iliyosomwa na mbunge mstaafu, Zakia Meghji wakati wa mahafali ya kwanza ya kidato cha sita ya shule ya sekondari ya Academic Archievement Open School (AAOS) ya Dar es Salaam. Shule hiyo ya kimataifa inatumia mfumo Cambridge katika utoaji wa elimu yake.
Katika mahafali hayo, mke huyo wa rais mstaafu, Jakaya Kikwete, “masomo ya sayansi ndiyo yanayochochea maendeleo na maisha ya watu, ujenzi wa barabara, umeme, kompyuta yote kazi ya uanasayansi,” alisema.
Katika hatua nyingine, alieleza kufurahishwa na namna shule hiyo ilitilia mkazo masomo ya sayansi na hisabati, akiwataka kuendelea kukaza buti katika kufundisha masomo hayo kwa wanafunzi kwa maslahi Taifa.
Meghji aliupongeza uongozi wa shule kwa hatua hiyo, akisema ina miaka miwili lakini imeonyesha mafanikio makubwa, huku akiwataka kutombweta katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Kitu kitakachoweza kuwarudisha nyumba ni endapo ufundishaji na uendeshaji wa shule hautakuwa mzuri. Lakini kwa taarifa yenu ilivyo na nilivyotembelea shule sitegemei matatizo hayo kujitokeza,” alisema Mama Salma katika hotuba yake ilisomwa na Meghji.
Aliwataka viongozi na wafanyakazi wa AAOS kuwa na ushirikiano na mshikamano katika uendeshaji wa shule hiyo, ili kufikia malengo yao na kwamba hakuna jambo litakaloharibika bali mafanikio.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa AAOS, Rana Ahmed Saada, shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali katika kujiendesha ikiw ni pamoja kuchelewesha kwa majibu ya kutambuliwa na kituo chao cha mitihani ya Cambridge na Baraza la Taifa la Mitihani (Necta).
“Tumejitahidi kuandika barua ya kuomba kutambuliwa kama kituo cha mtihani cha Cambridge ili vyeti vya wanafunzi wetu vitambuliwe kitaifa wanapoitimu mitihani yao lakini hatujajibiwa hadi sasa. Lengo letu ni kufungua fursa kwa wanafunzi wa kitanzania na mataifa mengine kusoma vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi,” alisema Rana.
Alisema shule hiyo ilianzishwa mwaka 2019 kama shule huria, lakini wana mpango wa kuanzisha program za ufundishaji kwa wanafunzi QT pamoja na watahiniwa binafsi.
Wanafunzi wa kiume Sekondari ya Academic Achievement wakiwa wanaimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza mahafali ya kuhitimu kidato cha Sita.
Wanafunzi wa kike Sekondari ya Academic Achievement wakiwa kwenye mahafali ya kuhitimu kidato cha Sita.
Mbunge mstaafu Zakia Meghji akiwa katika mahafali ya shule ya sekondari Academic Achievement akiwa na (kushoto) mkurugenzi wa shule ya Academic Achievement Rana Saada (kulia) ni Mshauri na Msimizi shirika la Maendeleo (WAMA) Johari Kandoro.
Wasanii watia fora uzinduzi wa UMISSETA LEO




Rais Samia azungumza kwa njia ya simuna Rais Xi Jinping wa China.
PSSSF, BENKI YA AZANIA WAINGIA MAKUBALIANO KUUZA NYUMBA,VIWANJA KWA MKOPO WA RIBA YA ASILIMIA 10
MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma(PSSSF) pamoja na Benki ya Azania wameingia makubaliano yatakayowezesha wanachama wa mfuko huo na wananchi wengine kukopa kwenye benki hiyo kwa kupata riba nafuu.
Akizungumza leo Juni 21,2021 mkoani Dar es Salaam,Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Hosea Kashimba amesema taasisi hizo zina dhima ya kuhakikisha wanaendana na azma ya Serikali ya kutekeleza kwa vitendo malengo yaliyomo kwenye dira ya Taifa ya 2025.
Na vipaumbele vya Ilani ya CCM inayohimiza kupatikana kwa huduma bora za afya, elimu , maji,makazi na umeme mijini na vijijini ambapo lengo lake kuu ni kustawisha maisha ya kila mtanzania.
"Ikumbukwe PSSSF kupitia jukumu lake la kisheria la uwekezaji umeendelea kutekeleza miradi ya kuuza nyumba za gharama nafuu pamoja na viwanja vya makazi.Madhumuni ya miradi hii ni kuwezesha wafanyakazi ambao ni wanachama wa mfuko na watanzania kwa ujumla kupata makazi bora na salama.
"Kwa kununua nyumba na viwanja vilivyopima kwa kulipia kwa njia rafiki ikiwemo mikopo ya makazi , aidha mradi wa nyumba za gharama nafuu upo katika Mkoa wa Dar es Salaam , Morogoro, Shinyanga, Tabora ,Mtwara na Iringa.
"Pia mradi wa viwanja vya gharama nafuu upo mikoa ya Ruvuma ,Kagera, Tabora Iringa,Katavi Morogoro ,Dar es Salaam, Kigamboni kule Kimbiji ,Rukwa, Lindi na Mtwara."amesema.
Hivyo ametumia nafasi hiyo kuwashukuru benki ya Azania akiwemo Mkurugenzi Mtendaji na timu yake kwa kuwa wa kwanza kuonesha utayari wa kushirikiana nao kukubali kutoa mikopo hiyo yenye riba na masharti nafuu.
Ameongeza kwa kufanya hivyo wanatekeleza azma ya Serikali ya kuongeza idadi ya wafaidika wa mikopo kwa ajili ya makazi bila mzigo wa riba kwa kuendelea kushusha viwango vya riba hadi kufikia kiwango cha asilimia 10 kwa mwaka ambacho ni kiwango nafuu.
"Miongoni mwa maeneo yaliyoonesha mafanikio katika dira ya uwekezaji ya mwaka 2025 na Ilani ya CCM ni kuendelea kushusha kwa riba iliyokuwepo ya kati ya asilimia 21 hadi asilimia 25 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 13 na 18 mwaka 2020.
PSSSF na Benki ya Azania tumekuwa mstari wa mbele kuhakikisha azma hii inatekelezwa kwa vitendo,kupitia makubaliano haya wananchi watafaidika kwa kukopesha nyumba na viwanja,hivyo kuimarisha na kuweka mazingira wezeshi kwa wananchi walioko maeneo yote nchini ili wawe na makazi bora na kutimiza kauli mbiu ya Serikali nyumba bora kwa wananchi wote inawezekana.
"Makubaliano haya yatamuwezesha mkopaji kulipa mkopo wake taratibu huku akiendelea kutimiza majukumu mengine ya kimaisha.PSSSF na Benki ya Azania tumeenda hatua zaidi kwa kuhakikisha tunawalinda wakopaji dhidi ya majanga kama vile moto , mafuriko, kimbunga na majanga mengine ya kibima wakati wote wa mkopo ili kulinda thamani ya uwekezaji ambao umefanywa,"amefafanua.
Kashimba amesema benki ya Azania imeshaandaa utaratibu wa kibima ili kuwalinda wakopaji dhidi ya majanga hayo na kwamba mteja atakapokamilisha mkopo wake atakabidhiwa hati yake ya nyumba na benki ya Azania.
"Muda wa marejesho ya mkopo huu ni kipindi kisichozidi miaka 15 kwa mkopo wa nyumba na miaka miwili kwa mkopo wa kiwanja .Masharti mengine ya msingi kwa mkopaji ni kuweka asilimia 10 ya thamani ya mkopo au mali yenye thamani hiyo kwa dhamana ya mkopo.
"Kiwango cha juu kabisa ambacho mteja anaweza kukopeshwa ni asilimia 90 ya thamani yote ya nyumba au kiwanja.Aidha taratibu zote na maelekezo ya masharti na vigezo vingine vya mkopo utakavyopatikana vitatolewa kwa wakopaji pindi watakapofika kwenye ofisi za PSSSF na Benki ya Azania,"amesema.
Aidha jumla ya nyumba 192 na viwanja 886 vyenye hati vitakuwa sokoni na vitauzwa kwa njia ya mkopo wenye riba nafuu utakaotolewa kwa wanachama na wananchi wote kwa kutegemea vigezo na masharti mepesi yaliyowekwa.
Amesema utaratibu wa kuviona, na kutoa mikopo utaratibiwa kupitia ushirikiano kati ya PSSSF na benki ya Azania pamoja na benki nyingine zitajitokeza baadae kwa kuzingatia idadi ya nyumba na viwanja.
"Mikoa ambayo nyumba za miradi zipo ni Dar es Salaam eneo la Chanika Buyuni, ambalo lina nyumba 106.Morogoro eneo la Lukobe nyumba moja, Tabora eneo la Usule kuna nyumba 25 ,Mtwara eneo la Mang'amba nyumba sita ,Shinyanga eneo la Ibadakuli nyumba 46, na Iringa eneo la Mawelewele kuna nyumba nane.
"Aidha nyumba ziko za aina nne zenye ukubwa tofauti kuanzia nyumba za vyumba viwili hadi vyumba vinne , bei ya nyumba ni kati ya Sh.milioni 36 hadi Sh.milioni 61 kulinagana na aina na ukubwa wa nyumba husika.
"Bei hizi zimejumuisha kodi ya ongezeko la thamani yaani VAT .Makubaliano haya na benki ya Azania ni pamoja na uuzaji wa viwanja kwa njia ya mkopo ambapo vinapatikana mikoa ya Ruvuma viwanja 128.
"Kagera viwanja 192,Tabora kiwanja kimoja ,Iringa viwanja vinne, Katavi viwanja 50, Morogoro kiwanja kimoja ,Singida viwanja 211, Dar es Salaam eneo la Kigamboni kule Kimbiji viwanja 87,Rukwa viwanja 54,Lindi viwanja 70 na Mtwara viwanja 70"amesema.
Amesisitiza viwanja hivyo vina hati na vina ukubwa kati ya mita za mraba 450 hadi mita za mraba 1500 na vinapatikana kwa kati ya Sh.2500 hadi Sh.15000 za mita za mraba.Hata hivyo mfuko huo bado una uhuru wa kuuza kwa muuzaji mwingine.
Pia PSSSF itaendelea kuandaa mipango kama hiyo ya kuwapatia wanachama wake fursa ya kumiliki makazi yao pindi wakiwa bado kwenye ajira.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Azania, Bw. Charles Itembe...amesema benki yao inaona faraja kuwa sehemu ya mradi huo mkubwa na kwamba benki hiyo ilikuwa ya kwanza na kinara wa ukopeshaji wa nyumba kwa riba nafuu.
"Kwa hiyo ni jambo ambalo tunauozoefu nalo kwa miaka mingi sana,tulikuwa ni benki ya kwanza kabisa kutoa mikopo ya nyumba toka miaka 2005 na mwaka 2016 wakati benki nyingine zikiwa bado hazijaanza kufanya kazi hiyo.
"Ukiangalia benki hii kwa kiasi kikubwa huduma ya mikopo ya nyumba imechukua asilimia kubwa, hivyo kwetu hili si jambo la kwenda kuiga bali tumeshalifanya na wengi wamefaidika hasa wafanyakazi wa sekta ya umma ukiondoa wa sekta binafsi.
"Na jambo hili kimsingi limetujengea heshima kubwa mtaani, ukisikia watu wengi wana nyumba za kuishi watakwambia ni kwasababu ya benki ya Azania, hivyo watanzania wanaokwenda kuomba mikopo ya nyumba au viwanja, basi benki hiyo iko tayari kuwahudumia, na mikopo hiyo inatolewa kwa riba ya asilimia 10.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Azania, Bw. Charles Itembe wakisaini makubaliano yatakayowawezesha wananchama wa PSSSF na wananchi wengine kukopa fedha kwenye Benki ya AZANIA kununua nyumba za gharama nafuu na viwanja zilizojengwa na Mfuko sehemu mbalimbali nchini.Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Azania, Bw. Charles Itembe wakibadilishana nyaraka za makubaliano yatakayowawezesha wananchama wa PSSSF na wananchi wengine kukopa fedha kwenye Benki ya AZANIA kununua nyumba za gharama nafuu na viwanja zilizojengwa na Mfuko sehemu mbalimbali nchini.Wanaoshuhudia pichani kulai ni Mkurugenzi wa Mipango PSSSF Fortunatus Magambo na kushoto ni Meneja Mwandamizi wa Wateja Binafsi Jackson Lolai Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bw. Hosea Kashimba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Azania, Bw. Charles Itembe wakiwaonesha Waanishi wa Habari (hawapo pichani) nyaraka za makubaliano yatakayowawezesha wananchama wa PSSSF na wananchi wengine kukopa fedha kwenye Benki ya AZANIA kununua nyumba za gharama nafuu na viwanja zilizojengwa na Mfuko sehemu mbalimbali nchini.Picha ya pamoja
TAARIFA YA KUUZWA KWA SHAMBA
Shamba lenye jumla ya Heka 165 ambalo tayari limeishapimwa linauzwa .
Mahali: Shungumbweni, Mkuranga karibu na Kiwanda cha Chumvi Neel Salt
Bei: Shamba hilo linauzwa kwa kila Heka moja ni shilingi 1,500,000/= (Milioni moja na Laki tano)..
Umbali: Kilomita 5 kutoka baharini, Kilomita 26 kutoka barabara kuu ya Dar-Lindi, (Unaweza Ingilia kwa njia ya Kibada-Mwasonga pia).
Shamba lina miti ya mikorosho iliyopandwa kwa heka 20,Mianzi,kisima cha maji safi mita 72, kinatoa lita 20,000 kwa saa.
Kwa aliye SERIOUS kununua anakaribishwa sana.
KWA MAWASILIANO ZAIDI 0763000053