MWILI WA ALBERT MANGWEA ULIVYOPOKELEWA EAPOT
↧
↧
Tendwa Akipa Usajili wa Kudumu Chama Kipya cha 21, CHAUMMA
Baadhi ya wanachama cha CHAUMMA pamoja na viongozi wao wakishangilia baada ya kupewa usajili
Wanachama wakionesha cheti cha usajili kwa wanahabari
Tendwa akikabidhi cheti cha usajili CHAUMMA
Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, John Tendwa (kulia) akizungumza na wana CHAUMMA
Gari la Mwenyekiti wa muda wa CHAUMMA, Wallance Mayunga likiondoka baada ya hafla ya usajili
========= ======== ==========
Tendwa Akipa Usajili wa Kudumu Chama Kipya cha 21, CHAUMMA
Na Thehabari.com
MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amekipa usajili wa kudumu Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) huku akivitaka vyama vya siasa kufuata sheria na kuepuka kuwa vyanzo vya vurugu na uchochezi wa migogoro.
Tendwa ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akiwakabidhi cheti cha usajili wa kudumu viongozi wa chama kimpya cha kinachojulikana kama Chama cha Ukombozi wa Umma.
Alivitaka vyama vya siasa kuhakikisha vinatimiza malengo yao ya kushika dola na hata kama itashindikana kwao, basi kuhakikisha wanapata nafasi za uwakilishi wa wananchi zikiwemo za udiwani, ubunge pamoja na uongozi wa serikali za mitaa kwa mujibu wa taratibu za nafasi hizo.
Alisema kwa sasa vipo vyama vya siasa ambavyo licha ya kuwa na usajili wa kudumu na uongozi mzuri usio na migogoro vimeshindwa kutimiza malengo ya msingi ya chama kwa kushika nafasi za uwakilishi maeneo anuai kwa mujibu wa utaratibu.
“…Vyama hivi unakuta hawana mbunge, hawana diwani, hawana viongozi serikali za mitaa, kijiji na kwingineko lakini ukiangalia wana viongozi wazuri hawana migogoro ndani ya chama, haya sio madhumuni ya chama cha siasa,” alisema Tendwa.
Aidha aliwataka viongozi wa CHAUMMA kuhakikisha wanajipanga vizuri ili waweze kutimiza malengo ya chama na kuwawakilisha wananchi maeneo mbalimbali ya uongozi kisiasa. Alisema katika mapendekezo mapya ofisi yake inafikiria kuanza kuvipunguza vyama ambavyo licha ya kuwa na usajili havifanyi chochote kama ilivyo kwa madhumuni ya kuanzisha chama.
“Sheria inafanyiwa marekebisho, chama kikikaa ndani ya miaka mitano hakijafanya chochote tunafikiria kukifuta, kiongozi wa chama akitukana miezi sita unafungiwa kwa muda…maana hatuwezi kuruhusu matusi, vurungu na masuala mengine yasiokuwa na msingi ndani ya vyama vya siasa,” alisema Tendwa.
Hata hivyo amesema katika mapendekezo yao ya mabadiliko ya katiba wamependekeza mambo mengi ikiwemo sasa kuruhusu vyama kujiunga na kufanya shughuli za siasa kama ilivyo kwa nchi za Kenya, Afrika Kusini, Lethoto na nchini Namibia.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa cheti cha usajili wa kudumu Mwenyekiti wa muda wa CHAUMMA, Wallance Mayunga alisema wamejipanga vizuri katika kuwatumikia wananchi na chama chake kinatambua changamoto zilizopo nchini katika uongozi, utendaji na utawala hivyo kina nia ya kuleta mabadiliko.
Nafasi ya Katibu Mkuu wa muda wa CHAUMMA inashikiliwa na Shaffii Abed huku Hamad Tao akiwa ni miongoni mwa wanachama waanzilishi wa nchama hicho.
↧
Absalom Kibanda arejea nchini,apokelewa kwa kishindo
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa habari na wanaharakati wakisubiri kumpokezi ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.
Waandishi wa habari na wanaharakati wakimsubiri kumpokea Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda.
Baadhi ya wapiga picha wakiwa Uwanja wa Ndege wakati wa mapokezi ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom kibanda.
Mjumbe wa Bodi wa Jukwaa la wahariri, Theophil Makunga akimlaki Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Absalom Kibanda alipowasili leo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Afrika Kusini kwa matibabu.
Kibanda akiwasili leo.
Absalom Kibanda (katikati)
Umati wa waandishi wa habari pamoja na wanaharakati wakiwa katika mapokezi ya Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri.
↧
LIVE NEWZ KUTOKA IRINGA;KIKOSI CHA ZIMA MOTO CHAZIDI KUTOA ELIMU JUU YA TAHADHARI YA MOTO
Kikosi cha zima moto kimeendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa kinga na tahadhari ya moto katika meneo mbalimbali ya makazi ya watu ikiwemo sehemu ya kuufanyia biashara.
Akizungumza Kamanda wa kikosi cha zimamoto mkoa wa Iringa KENEDY KOMBA, amesema kuwa lengo la kufanya hivyo ni kuondoa kero kwa wananchi ili wafahamu ni kitu gani wanalipia pamoja na manufaa yake.
Amesema zoezi hilo hufanyika kila mwaka wa fedha wa serikali kuanzia julai I mwaka husika mpaka mwaka unaofuata juni 30.
Aamesema kuwa mbali na kutoa elimu pia kuanzia tarehe 1 mwezi wa kumi mwaka jana walikuwa wakifanya zoezi hilo pamoja na ukusanyaji wa madhuhuri ya serikali na muda wake umekwisha na kwa wale wote watakaokuwa hawajakamilisha sheria itachukua mkondo wake.
Aidha amesema kuwa kwa wale ambao hawajafikiwa wafike wenyewe katika ofisi ya kamanda wa zimamoto na kwa wale ambao wamefikiwa na wamepewa hati ya malipo wanapaswa kufahamu kuanzia sasa ndani ya siku saba watafikishwa mahakamni.
Kwa upande wa wamiliki wa vyombo vya usafiri amesema kuwa kodi yao inakatwa kupitia tra na baada ya kukatwa pesa hizo wanatakiwa kufika katika ofisi ya kamanda wa zimamoto na uokoaji ili kukaguliwa na kupewa ushauri vifaa gain vinafaa kuwekwa katika vyombo hivyo na namna ya kutumia vyombo hivyo na ili kuthibitisha kama umekaguliwa unapewa fomu maalum.
↧
GrooveBack Jmosi Hii East 24-Arcade(Mikocheni)
↧
↧
WANAFUNZI WA CHUO CHA KIJESHI CHA MAWASILIANO WATEMBELEA MAKAO MAKUU YA VODACOM KWA MAFUNZO ZAIDI
Mkuu wa Idara ya uendeshaji- uhandisi wa Vodacom Tanzania,Bw.Andrew Lupembe,akifafanua jambo kwa baadhi ya wanafunzi wa chuo cha kijeshi cha mawasiliano cha jijini Dar es Salaam,wakati walipofanya ziara ya kimafunzo makao makuu ya Ofisi za Vodacom Tanzania.
Mkuu wa kitengo cha maendeleo rasilimaliwatu wa Vodacom Tanzania,Bw.Conrad Msoma,akielezea jambo kwa baadhi ya wanafunzi wa chuo cha kijeshi cha mawasiliano cha jijini Dar es Salaam,wakati walipofanya ziara ya kimafunzo makao makuu ya Ofisi za Vodacom Tanzania.
Mkuu wa kozi ya Mawasiliano wa jeshi la wananchi (JWT) katika Chuo cha Mgulani jijini Dar es Salaam, Luteni Moshi Masawani akiuliza swali njinsi Kampuni ya Vodacom inavyoendesha huduma ya mawasiliano, wakati walipofanya ziara ya kimafunzo makao makuu ya Ofisi za Vodacom Tanzania.
Mkuu wa Idara ya uendeshaji- uhandisi wa Vodacom Tanzania Bw.Andrew Lupembe,akifafanua jambo kwa baadhi ya wanafunzi wa chuo cha kijeshi cha mawasiliano cha jijini Dar es Salaam, baada ya kufika katika moja ya kituo cha kurushia mawasiliano cha Vodacom kilichopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.Wakati walipofanya ziara ya kimafunzo makao makuu ya kampuni hiyo.
Mkuu wa Idara ya uendeshaji-uhandisi wa mtandao wa Vodacom Tanzania,Bw.Andrew Lupembe,akiwaelezea jambo baadhi ya wanafunzi wa chuo cha kijeshi cha mawasiliano cha jijini Dar es Salaam, Wakati walipofanya ziara ya kimafunzo makao makuu ya kampuni hiyo.
Mkuu wa kitengo cha uendeshaji wa mtandao wa Vodacom Tanzania,Bw.Andrew Lupembe,akiwaonyesha mitungi ya gesi ya kisasa ambayo inatumika kuzima moto wanafunzi wa chuo cha kijeshi cha mawasiliano cha jijini Dar es Salaam, Wakati walipofanya ziara ya kimafunzo katika moja ya kituo cha kurushia mawasiliano cha Vodacom kilichopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.
↧
Bharti Airtel yasaidia kuondoa umaskini kupitia mradi wa Millenium Village
Meneja huduma kwa jamii wa Airtel Hawa Bayumi akiongea wafanyakazi wa afya wa mradi wa millenium village wakati akikabithi simcards 240 zitakazowasaidia wafanya kazi hao kuwasiliana kwa bei nafuu na kutoa huduma kwa wakazi wa Mbola Tabora.akishuhudia ni Mkurugenzi wa mradi huo Dr Gerso Nyadzi na wafanyakazi wengine wa mradi huo
Meneja Huduma za Jamii wa Aitel Tanzanaia- Hawa Bayumi akikabidhi SIM card 240 za mtandao huo kwa Meneja Mkuu wa Mradi wa Millenium Village ulioko Mkoani Tabora- Dr Gerson Nyadzi. Mradi huu unalenga katika kuboresha huduma za afya na elimu vijijini kupitia technolojia ya mawasiliano. Kulia ni afisa mauzo wa Airtel kanda ya ziwa Charles Elisante, na Meneja wa Airtel money kanda ya ziwa Violet Gyumi. Hafla
ya makabidhiano ilifanyika mkoani Tabora
======== ======== ========
Bharti Airtel yasaidia kuondoa umaskini kupitia mradi wa Millenium Village
* Mradi huo kutoa elimu kwa wafanyakazi wa afya kwa kupitia
huduma za mawasiliano
* Yawawezesha wafanyakazi 240 kuwasiliana kwa gharama nafuu za pekee.
* Airtel unasaidiana na mradi huu wa millennium village
katika nchi 6 za Afrika
Dar es Salaam Juni 04 2013: Kampuni ya Bharti ("Airtel") inayoongoza
kwa kutoa huduma za mawasiliano inayoendesha shughuli zake katika
ndani ya nchi 20 barani Afrika na Asia, leo imethihirisha thamira yake
ya kufikia malengo ya Millenium kwa kushirikiana na kampuni ya
Erickson katika mradi maalum ujulikanao kama Millenum village
inayoendeshwa katika nchi 6 za Afrika ikiweko Tanzania.
Mradi huo umeundwa na taasisi ya Earth Institute kwa dhamira ya
kutimiza baadhi ya malengo ya Milenia kwa kuelekeza ufumbuzi wa
kiubunifu zaidi katika maeneo ya vijijini huku ikishirikiana kwa
ukaribu zaidi na kampuni ya simu za mkononi Airtel barani Afrika
Airtel imesaidia mradi wa millennium village katika mkoa wa Tabora kwa
kutoa huduma za mawasiliano zitakazowawezesha watu kupata elimu kuhusu maswala ya afya kwa urahisi.
Airtel imetoa namba ya dharura itakayopigwa bila kutozwa gharama yoyote na kuwawezesha watoa huduma za afya na wagonjwa kuwasiliana kiurahisi zaidi. Mradi wa millennium Vilage unasaidiwa na Airtel katika nchi 6 ambazo Airtel inafanya biashara zake. Nchini Tanzania mradi wa millinium village umeanzishwa katika eneo la Mbola mkoani Tabora na kusambaa katika maeneo mengi na kufikia zaidi ya vijiji 20 vilivyopo katika eneo lenye mita za mraba 700msq likiwa na wakazi 30,0000 waishio katika wilaya ya Uyui Tabora.
Mpaka sasa mradi huu umekuwa na mafanikio makubwa, zaidi ya watu
500,000 katika nchi 11 zilizoko kusini mwa jagwa la sahara Afrika
wamefaidika ambapo hadi kufikia mwisho wa mwaka 2011 asiliimia 90 ya
vijiji vilikuwa vimesha unganishwa na mtandao wa simu
Vile vile ndani ya mradi huu kuna kipengele cha Connect to Learn,
chenye ushirikiano baina ya Earth Institute Chuo kikuu cha Columbia ,
Ericsson and Bharti Airtel Africa, ulioanzishwa katika shule zilizopo
ndani ya mradi wa millennium village na kuwafikia walimu na wanafunzi
zaidi ya 5,000 katika nchi za Ghana, Tanzania, Uganda na Kenya.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Bwana Sunil Colaso
alisema" Airtel ina dhamira ya kugusa maisha ya watu si tu kwa kutoa
huduma za mawasiliano zenye gharama nafuu lakini pia kuwazifikia
jamii za chini zenye uhitaji wa technologia katika kuendeleza na
kukuza maisha yao, ambayo ndio lengo lililotufanya kushirikiana na
Earth Institute pamoja na Erickson kusaidia mradi huu wa millennium
village.
Ushirikiano huu unatupelekea kufikia malengo ya mradi wa millennium
village ya kushughulikia changamoto za umasikini katika maeneo mengi
ikiwemo Kilimo, elimu, afya, miundo mbinu, usawa katika jinsia na
kukua kwa Biashara. Tunafurahi kuwa sehemu ya mabadiliko na tunaahidi
kuisaidia jamii nchini Tanzania.
Akiongea wakati wa halfa ya kupanua mradi wa millennium village katika
kijiji cha Mbola mkoani Tabora, Meneja Huduma Jamii wa Airtel bi Hawa
Bayumi alisema" tunafurahi kuendelea kutimiza dhamira yetu ya kutoa
huduma za mawasiliano zenye gharama nafuu katika vijiji mbalimbali
Tanzania . leo tunaonyesha kwa vitendo dhamira yetu na kuwapatia
wafanyakazi 240 huduma za mawasiliano ili kuuendesha mradi huu wa
millennium village kirahisi. Airtel pia imetoa namba ya dharura
ambayo itaboresha upatikanaji wa huduma za afya ikiwemo huduma za
dharura na elimu ya afya katika kijiji cha Mbola"
"Huduma ya mawasiliano tuliyoitoa kwa wafanyakazi 240 ni pamoja na
kupigiana simu kwa gharama nafuu zaidi (CUG), ujumbe mfupi wa bure
pamoja na huduma ya internet ilikuwezesha mawasiliano kati yao na
jamii" aliongeza Bayumi
Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha huduma kwa jamii katika nchi za
Afrika zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara Bi Margaret Kositany,
alisema" ni imani yetu kwamba kwa kuboresha mawasiliano kutawezesha
kuleta ufanisi katika huduma zetu za afya na kufanya mawasiliano ya
karibu kati ya wauguzi na wagonjwa kuwa ya rahisi, kutoa elimu kwa
jamii kupita mitandao na kuongeza uelewa wa elimu kwa njia ya
mtandao kwa watoto wa shule."
Mbali na mradi wa Millennium Villages , Airtel Tanzania iko mstari
wa mbele katika kusaidia shule za secondari nchini kwa kuwapati nyenzo
za kufundishia ikiwemo vitabu. Tangu kuanzishwa kwa mradi wa 'Airtel
Shule Yetu' zaidi ya shule 900 nchini zimefaidika na kupata vitabu
kutoka Airtel.
↧
Mamia wajitokeza kumuaga msaani albert Mangweha leo viwanja vya Lidaz club jijini dar,kuzikwa morogoro kesho.
Gari iliyobeba mwili wa Marehemu Albert Mangweha (ya pili nyuma) ikiongozwa na gari ya polisi,tayari kwa kuanza safari ya kuelekea mkoani Morogoro,ambako anatarajiwa kuzikwa kesho.
Waombolezaji wakiondoka kwenye viwanja vya Lidaz Club tayari kuelekea Mkoani Morogoro,ambako marehemu anatarajiwa kuzikwa huko hapo kesho.
Baadhi ya Waombolezaji wakiwa kwenye viwanja vya Lidaz Club,wengine wakitoka kuaga mwili wa msanii huyo.
Baadhi ya Ndugu,Jamaa na marafiki wakiaga mwili wa Marehemu Albert Mangweha.
Sanduku leneye mwili wa Marehemu Albert Mangwea likifunikwa mara baada ya waombolezaji kupita kumuaga kwa mara ya mwisho kwenye viwanja vya Lidaz Club,kinondoni jijini Dar.
Waombolezaji wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri uwanjani.
Mtangazaji wa Clouds FM,B Dozen akitangaza live kwenye maombolezo ya kumuaga Marehemu Albert Mangweha mapema leo kwenye viwanja vya Lidaz Club.
Watu wakiendelea kuaga mwili wa Marehemu Albert Mangweha.
Wasanii wa bongofleva wakijadiliana jambo.
Wasanii wa Bongo Movie wakitafakari jambo.
Msanii TID akihojiwa kwa ufupi kuhusiana na kifo cha Marehemu Mangweaha.
↧
TBL YANG'ARA KILELE SIKU YA MAZINGIRA DAR
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadick akimkabidhi tuzo Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Doris Malulu baada ya kampuni hiyo kuibuka mshindi wa kwanza kwa kusaidia utunzaji wa mazingira,katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani, yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Zakheim, Mbagala, Dar es Salaam leo. Wanaoshuhudia ni Ofisa wa Afya na Usalama Kazini wa TBL, Ismail Kalema (wa pili kulia) na Meya wa Temeke wa Manispaa ya Temeke, Maabad Hoja.
Mratibu wa Afya na Usalama Kazini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Daud Lwila (katikati), akionesha tuzo ya cheti baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadick kwa kuwa kampuni ya kwanza kusaidia utunzaji wa mazingira katika kilele cha maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani,yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Zakheim, Mbagala, Dar es Salaam
Wafanyakazi wa TBL, wakiwa na tuzo hiyo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Sadick akiwa katika picha ya pamoja na taasisi zilizozopewa tuzo Mazingira. Kushoto ni Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu.
Doris Malulu na ImailKalema wa TBL wakiwa pamoja na wananchi walishiriki kwenye maadhimisho hayo.
Wasanii wa Bendi ya Mjomba, wakitumbuiza kwa sarakasi wakati wa maadhimisho hayo.
Mjomba Band ikitumbuiza katika maadhimisho hayo.
↧
↧
MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA ZANZIBAR;tatizo la uchafu wa mazingira laathiri sekta ya kilimo na uvuvi.
Tatizo la uchafuzi wa Mazingira katika Visiwa vya Zanzibar limeathiri kwa kiasi kikubwa sekta ya Kilimo na Uvuvi na kwamba juhudi za pamoja zinahitajika kuinusuru Zanzibar ili kukabiliana na hali hiyo.
Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais Fatma Abdulhabib Fereji wakati alipokuwa akizungumza na Wananchi na Wanafunzi kutoka maeneo mbali mbali ya Zanzibar huko Victoria Garden Mjini Unguja katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani.
Amesema hali hiyo imetokana na Wananchi kuchafua mazingira kwa kukata Mikoko,kuchimba mchanga pembezoni mwa fukwe hali ambayo imeifanya bahari kupanda juu kwenya mashamba ya wakulima na kuhatarisha kilimo.
Ameongeza kuwa Wakulima wa Mwani wamekuwa wakikosa mavuno mazuri kutokana na kupanda kwa joto la bahari nakupelekea mwani wao kufa ambapo kwa upande wa Wavuvi hulazimika kwenda maeneo ya mbali kuvua kwavile mazalia ya samaki nayo hufa kutokana na joto la bahari kuwa kubwa.
“Tuna shuhudia kuanguka kwamiti ya kudumu na majengo mbali mbali kutokana na mmong’onyoko wa fukwe, kupotea maeneo ya kilimo kutokana na kuingiliwa na maji ya bahari, na hata kuathirika maji ya kunywa katika visima nayo yanaathiriwa na maji ya chumvi”, alisema Waziri Fereji.
Alisema hali hiyo hivi sasa haiwezi kuachwa iendelee kama ilivyo, bali Serikali na wananchi waipinge kwa nguvu zote ili kuepuka maafa hayo.
Alisema juhudi kubwa inayofanywa na Serikali ni kuihamasisha na kuielemisha jamii juu ya umuhimu wa kuifadhi mazingira na kuwataka wananchi washiriki katika matukio mbalimbali ikiwemo Midahalo na mashindano ya kuhifadhi mazingira.
“Hali ya mazingira yetu ilivyo hivi sasa hatuwezi kuiacha ikaendelea kama ilivyo,hivyo juhudi za pamoja za hali na mali zina hitajika kuazia ngazi ya Dunia Taifa,Wilaya ,Shehia hadi mwananchi mmoja mmoja kuinusuru Dunia pamoja na nchi zetu kutokana na hali mbaya ya mazingira tulio nayo”, aliongeza kuseama Waziri.
Nae Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Zanzibar Hamza Rijal amesema sababu iliyopelekea uharibifu wa mazingira ni kuwepo kwa matumizi mabaya ya viwanda Vidogo vidogo, ambapo amesema kuwa kuwepo kwa Sheria ya Mazingira inayokidhi haja ya wakati uliopo inaweza kupunguza tatizo.
Madhimisho hayo yaliambatana utoaji wa zawadi wa pesa taslimu kwa wanafunzi walifanya vyema katika kuandaa utenzi , mchezo wa kuigiza na ngoma za asili ambapo Ujumbe wa mwaka huu ni Fikiria .kula .Weka .
Na Miza Othman-Maelezo Zanzibar 5/6/2013
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
↧
MAKAMU WA RAIS DKT. BILLAL AONGOZA KILELE CHA SIKU YA MAZINGIRA KITAIFA NAMANYERE MKOANI RUKWA LEO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akihutubia wananchi katika viwanja vya sabasaba Mji mdogo wa Namanyere Mkoani Rukwa katika kuhitimisha siku ya mazingira duniani ambayo kitaifa imefanyika Mkoani Rukwa leo tarehe 05.06.2013. Katika hotuba yake hiyo alisisitizia juu ya uhifadhi wa mazingira kwa kutunza vyanzo vya maji, milima na misitu ya asili, kuhifadhi ardhi na kupanda miti katika maeneo yaliyoathirika na usafi wa mazingira kwa ujumla.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akikagua kitalu cha miche ya miti mbalimbali ya mjasriamali ndugu Kidevu (kushoto) katika maonyesho kwenye kilele cha siku ya mazingira kitaifa Mkoani Rukwa katika Mji mdogo wa Namanyere wilayani Nkasi leo tarehe 05.06.2013, Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akisoma moja ya vitabu vya uhifadhi wa mazingira wakati akikagua banda la maonyesho la Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira kwenye kilele cha siku ya mazingira kitaifa Mkoani Rukwa katika Mji mdogo wa Namanyere wilayani Nkasi leo tarehe 05.06.2013, Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt. Rajab Mtumwa Rutengwe. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mohammed Gharib Billal akimkabidhi kikombe na cheti Ndugu Leonard Kapini Makamu mwenyekiti Halmashauri ya Mji Mpanda kwa Halmashauri hiyo kuwa mshindi wa kwanza kitaifa katika usafi wa Miji nchini. Zawadi nyengine waliyopewa ni Pikipiki moja. Jiji la Nyamagana limekuwa la kwanza kitaifa na Manispaa ya Moshi ikiwa Manispaa ya kwanza kitaifa katika usafi wa Mazingira mwaka huu 2013.
Baadhi ya viongozi na wafanyakazi wa Halmashauri ya Mji Mpanda wakifurahia kwa pamoja ushindi kwa halmashauri yao kuwa ya kwanza kitaifa katika usafi wa Miji nchini mwaka 2013. Halmashauri hiyo imezawaidiwa cheti, kikombe na pikipiki moja.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akikagua mtambo asilia wa kuzalisha umeme kwa kutumia upepo uliobuniwa na mjasiriamali kutoka Mkoani Rukwa wa kampuni ya Ulaya Hydro and Windmill Technology (Kulia), Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya na Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akisalimiana na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima mara baada ya kuwasili kwa helkopta katika viwanja vya Sabasaba katika Mji mdogo wa Namanyere Wilayani Nkasi kwa ajili kushiriki katika kilele cha siku ya mazingira duniani ambayo kitaifa imefanyika Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akipanda mti wa kumbukumbu katika kampeni ya uhifadhi wa mazingira mbele ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi leo tarehe 05.06.2013 ikiwa ni kuadhimisha siku ya mazingira duniani ambayo kitaifa imefanyika Mkoani Rukwa.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Billal akizindua kwa kuwasha mashine mpya ya maji katika bwawa la maji Mphiri ambalo ni chanzo kikuu cha Maji katika Mji mdogo wa Namanyere Wilayani Nkasi leo tarehe 05.06.2013. Serikali imetenga jumla ya Tshs bilioni nne (4) kuendeleza chanzo hicho muhimu ambacho asili yake ni chemchem.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa akihutubia wananchi ambapo alikemea uharibifu wa vyanzo vya maji na kuwaasa wanasiasa kutofanya siasa zitakazopelekea kuhatarisha uhai wa vyanzo vya maji kwani umuhimu wa maji hauna mbadala.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza kuwatambulisha baadhi ya viongozi wakuu waliohudhuria maadhimisho ya siku ya mazingira duniani yaliyofanyika kitaifa Mkoani Rukwa.
Naibu Waziri wa Afya Dkt. Seif Suleiman Rashid akiwataja washindi mbalimbali wa usafi wa mazingira kitaifa katika ngazi ya majiji, manispaa, miji na wilaya ambao walipewa zawadi mbali mbali. Walioongoza ni Halmashauri ya Jiji la Nyamagana (Majiji), Halmashauri ya Manispaa ya Moshi (Manispaa), Halmashauri ya Mji Mpanda (Miji) na Halmashauri ya Wilaya Njombe (Wilaya).
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima akizungumza katika maadhimisho hayo. Kushoto ni Msema Chochote (MC) machachari ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mhe. Moshi Chang'a.
MC Machachari ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mhe. Moshi Chang'a akisherehesha mambo kwa ufasaha kabisa. Nyuma yake ni kundi la taarab la TOT ambalo limekuwa likinogesha sherehe hizo.
Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Iddi Hassan Kimanta na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Ndugu Galikunga wakijadili jambo katika maadhimisho hayo. Hawa ndio viongozi wakuu wa Wilaya ya Nkasi na wenyeji wa maadhimisho ya siku hiyo ya mazingira kitaifa mwaka huu 2013.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira Dkt. Terezya Luoga Huvisa akicheza muziki na kundi la Tanzania One Theatre (TOT) waliokuwepo kutumbuiza katika maadhimisho hayo. TOT wakiongozwa na muimbaji wao mahiri Khadija Kopa "Heshima Pesa Shkamoo Makelele".....
Baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa wakiwa katika banda lao la maonesho. (Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa - rukwareview.blogspot.com)
↧
MALI ZA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA ZAKAMATWA NA DALALI WA MAHAKAMA
Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya Udalali ya Flamingo, Nyalila Noel akipandika hati ya mahakama katika basi la Shirikisho la soka Tanzania (TFF), ambayo inaruhusu kukamatwa kwa mali za shirikisho hilo.
Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya Udalali ya Flamingo, Nyalila Noel akibandika hati ya mahakama katika basi la Shirikisho la soka Tanzania (TFF), ambayo inaruhusu kukamatwa kwa mali za shirikisho hilo.
Dereva la basi dogo la TFF (kulia), akisoma hati ya mahakama iliyotolewa kwa ajili ya kukamatwa kwa mali za TFF kutokana na deni la sh. milioni 51 linazodaiwa na Safina Holding.
Hati ya mahakama.
Sasa tunafunga na kuondoka nalo.
Wafanyakazi wa Jay Ambe Break Dowan wakichakalika na ufungaji wa basi la TFF tayari kwa ajili ya kuondoka nalo kutokana na deni wanalodaiwa na Safina Holding.
Gari dogo aina ya Toyota Crown lenye namba T 643 BJW likiwa limezuia gari la Jay Ambe Break Down lisitoke katika lango kuu la kutoka na kuingia katika Ofisi za TFF, baada ya mali za shirikisho hilo kukamatwa na dalali wa mahakama.
Hati ya kukamata mali za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ikiwa imebandikwa katika basi kubwa aina ya Youtong kwa ajili ya utekelezaji
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah akizungumza na waandishi wa habari wakati wa sakata hilo.
Na Mwandishi Wetu
UONGOZI wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), leo umejikuta kwenye wakati mgumu baada ya madalali wa Kampuni ya Flamingo Auction Mart, kutinga katika ofisi za shirikisho hilo na kukamata baadhi ya mali zake ili zipigwe mnada kufidia deni wanalodaiwa.
Shirikisho hilo linadaiwa na Safina Holding ya jijini Dar es Salaam zaidi ya sh milioni 50, baada ya kuwaweka katika hoteli ya kampuni hiyo maeneo ya Kijitonyama, waamuzi wa michuano ya Kombe la Kagame mwaka 2012.
Sakata hilo liliweza kudumu kwa muda wa saa nne kuanzia saa tano asubuhi na kudumu hadi saa tisa mchana, baada ya TFF kukubali kulipa sh milioni 20 kati ya sh 51,507,012 zilizokuwa zikidaiwa.
Awali, madalali hao wa Flamingo, walifika Ofisi za TFF, Karume Ilala na kujadiliana na Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Angetile Osiah na kushindwa kufikia muafaka, hali iliyowalazimu kuita gari maalumu ‘break down’ mali ya Jay Ambe na kulifunga basi dogo aina ya Toyota Coaster.
Baada ya gari hilo kufungwa ili likokotwe kupelekwa ‘yadi’ ya Flamingo, mlinzi wa TFF aliamua kukimbilia geti la kutokea na kulifunga na kuwafanya madalali hao washindwe kutoka nalo.
Jambo hilo lilizidisha sintofahamu na kuwafanya baadhi ya watu kuingia ndani kushuhudia kinachoendelea, huku maofisa wa Flamingo wakihangaika kuwasiliana na Jeshi la Polisi kwa ajili ya kupatiwa msaada wa kuweza kutekeleza amri ya mahakama.
Usumbufu huo wa kuzuia madalali wasitekeleze amri halali ya mahakama, ulisababisha kero kwa watu mbalimbali waliofika Karume, kwa kushindwa kuingia ama kutoka katika ofisi hizo.
Wakati majadiliano yakiendelea, zilipatikana taarifa kuwa TFF wameomba walipe sehemu ya fedha wanazodaiwa kwa ahadi ya kumalizia zilizobaki, ili magari yake yasichukuliwe, hali iliyomfanya dereva wa gari lililozuia mlango kwenda kuliondoa na kuruhusu shughuli zingine kuendelea.
Ilipofika saa tisa mchana, Osiah alijitokeza na kuwaeleza waandishi wa habari kuwa wamemuagiza mhasibu akachukue fedha benki.
Akizungumzia adha hiyo, Osiah alisema wao hawakujua kama tukio hilo litatokea, kwa kuwa barua waliyokuwa nayo haikueleza hivyo, na kudai kushangazwa na hatua hiyo, wakati barua kutoka Flamingo ikionekana kuchanganya tarehe ya zoezi hilo kufanyika.
Osiah alisema walipata nguvu za kugoma magari hayo yasichukuliwe kutokana na kugundua kuna makosa ya tarehe katika barua hiyo, huku akikiri kudaiwa sh milioni 28.
“Sisi tunadaiwa mil 28/-, ila mambo ya kimahakama ndio maana ikafikia hiyo na pia tumewashangaa sana Safina, badala ya mambo tuyamalize wenyewe, wao wanayakuza na fedha hizo zilitokana na hifadhi ya waamuzi katika michuano ya Chalenji,” alisema Osiah.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Flamingo, Deogratius Luziga, alisema wao walifikia hatua hiyo ya kutaka kuondoka na magari hayo kama amri ya mahakama ilivyowaagiza na kudai kuwa tatizo kubwa ilikuwa ni dharau za Osiah na kuwa angefanya hivyo toka awali wasingechukua muda wote huo katika zoezi hilo.
“Tumekubaliana mara baada ya kutuomba sana, tumekubali watangulize milioni 20/- kwanza, halafu milioni 31/- watamaliza ndani ya siku 14, kwani hii mahakama inaruhusu na bila hivyo, tutafanya kama tulivyokusudia kwa kuwa bado ni mali yetu sisi,” alisema Luziga.
Awali, Osiah alionekana kuchanganyikiwa na kuwasihi madalali hao kuachana na zoezi hilo la kuchukua magari hayo.
“Naombeni muache kufanya hivyo ambavyo mnataka kufanya, mimi sasa hivi namwambia mhasibu wetu mwende naye benki akawape fedha zenu zote jamani, msifanye hivi,” alisihi Osiah.
↧
RAIS KIKWETE AENDELEA NA ZIARA YAKE YA KIKAZI NCHINI SINGAPORE LEO
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika mkutano wa kwanza wa ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na Singapore ulioandaliwa leo Juni 5, 2013 katika hoteli ya Swissotel jijini Singapore
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na wawekezaji wa Singapore leo Juni 5, 2013 katika hoteli ya Swissotel jijini Singapore.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kitabu alichopewa na Wakurugenzi wa NEWater plant baada ya kutembelea mitambo yao ambayo inatoa huduma ya maji masafi kwa nchi ya Singapore baada ya kuyachuja na kuyasafisha kutoka vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na baharini, maji ya mvua na maji taka.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitambulishwa kwa baadhi ya Watanzania Waishio Singapore alipokutana nao leo Juni 5, 2013 katika hoteli ya Swissotel jijini Singapore
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Watanzania Waishio Singapore alipokutana nao leo Juni 5, 2013 katika hoteli ya Swissotel jijini Singapore
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipiga picha ya kumbukumbu na Watanzania Waishio Singapore alipokutana nao leo Juni 5, 2013 katika hoteli ya Swissotel jijini Singapore. Kulia ni balozi wa Tanzania nchini Singapore Injinia John Kijazi.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na mwenyeji wake Rais wa Singapore Dkt Tony Keng Yam alipokutana naye katka Istana (Ikulu) ya Singapore leo Juni 5, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete za ujumbe wake wakitembezwa kuangalia bandari ya Singapore
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Istana (Ikulu ya Rais) leo Juni 5, 2013 huku mwenyeji wake Rais wa Singapore Dkt Tony Keng Yam akiwa pembeni yake baada ya kumlaki
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na mwenyeji wake Rais wa Singapore Dkt Tony Keng Yam alipokutana naye katka Istana (Ikulu) ya Singapore leo Juni 5, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake Rais wa Singapore Dkt Tony Keng Yam alipokutana naye katka Istana (Ikulu) ya Singapore leo Juni 5, 2013
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na mwenyeji wake Rais wa Singapore Dkt Tony Keng Yam alipokutana naye katka Istana (Ikulu) ya Singapore leo Juni 5, 2013.PICHA NA IKULU
↧
↧
NATIONAL WORLD BLOOD DONORS DAY 2013, THEME: GIVE THE GIFT OF LIFE, DONATE BLOOD
World Blood Donor Day, celebrated on 14 June every year, serves to raise awareness of the need for safe blood and blood products and to thank voluntary unpaid blood donors for their life-saving gifts of blood.
With the slogan "Give the gift of life: donate blood", this year’s campaign, the 10th anniversary of World Blood Donor Day, will focus on the value of donated blood to the patient, not only in saving life, but also in helping people live longer and more productive lives.
In Tanzania National World Blood
D onor day to be held in Mara Regional on 14
th June, 2013, at MKENDO Ground and The Guest of hanour will be the Minister of Health and Social Welfare Hon
Dr Hussein Ali Mwinyi (MP)
.
.
Theme for this year event is Every Blood Donation is the Gift of life. Also this year celemony will be celebrated in National blood Transfusion service (NBTS) zonal centers such Mbeya, Dar-es-Salaam, Mtwara, Kilimanjaro, Tabora. for furher information contact 0712612000.
Rafiki wa Damu Salama is a new born
a blood donation platform initiated for young Tanzanian, aims to address and alleviate the blood issue in Tanzania by encouraging Individual Youth and Active Youth Organizations with the core element as Regular voluntary non-Remunerated blood donation (the youth platform of a safe and sustainable blood donation) and health promotions.
a blood donation platform initiated for young Tanzanian, aims to address and alleviate the blood issue in Tanzania by encouraging Individual Youth and Active Youth Organizations with the core element as Regular voluntary non-Remunerated blood donation (the youth platform of a safe and sustainable blood donation) and health promotions.
The Main Focuses of the Platform are:
- EMPOWER Youth Participation on Blood Donation
- ELIMINATE wrong perceptions concerning Blood Donation among Youth
- SUSTAIN Youth Blood Donors and Blood Ambassadors
↧
UJUMBE WA KIKOMUNISTI CHA VIATNAM WATUA DAR ASUBUHI HII
Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akiwa na Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Kimomunisti Cha Viatnam (CPV), Hoang Binh Quan, baada ya ujumbe wa CPV kuwasili asubuhi hii kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Quan na ujumbe wake wanatarajiwa kuwa na mazungumzo na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana baadaye leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es salaam, Ramadhani Madabiba.
Balozi wa Vietnam Tanzania, NguyenThien akimtambulisha Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Kimomunisti Cha Viatnam (CPV), Hoang Binh Quan kwa katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Martin Shigela (kulia) baada ya kushuka katika ndege, kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu wa NEC ya CCM, Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akiwatambulisha kwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Kimomunisti Cha Viatnam (CPV), Hoang Binh Quan, viongozi wa CCM aliofuatana nao katika mapokezi hayo, wakiwa chumba cha mapumziko Uwanja wa Ndege wa JN.
Dk.Asha-Rose Migiro na mgeni wake, wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa mgeni huyo na viongozi wengine wa CCM, wakati wamapokezi kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JN, Dar es Salaam.
Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akizungumza na Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Kimomunisti Cha Viatnam (CPV), Hoang Binh Quan, baada ya kumpokea kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere asubuhi hii. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
↧
Mpigie Kura Feza Kessy abaki kwenye Jumba la Big Brother
↧
NGUMI KUPIGWA SIKU YA TAMASHA LA MATUMAINI
Bondia Thomas Mashali (kulia) akitia saini ya dole gumba kwenye mkataba wa kupambana kwa ajili ya kuchangia elimu siku ya Tamasha la Usiku wa Matumaini litakalofanyika Julai 7, mwaka huu katika uwanja mpya wa Taifa jijini Dar. Mashali atacheza na Bondia Patrick Amote kutoka Kenya. Tamasha hilo litawashilikisha wasanii mbalimbali pamoja na wabunge. Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akisaini mkataba kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya katika Tamasha la Usiku wa Matumaini.Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Thomas Mashali akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Patrick Amote katikaTamasha la Usiku wa Matumaini.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akisaini mkataba kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya katika Tamasha la Usiku wa Matumaini.Kushoto ni Rais wa TPBO, Yasin Abdallah.
Thomas Mashali akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Patrick Amote katikaTamasha la Usiku wa Matumaini.
Bondia Francis Miyeyusho (kulia) akipokea sehemu ya fedha za maandalizi kwa ajili ya mpambano wake na Bondia Shadrack Muchanje kutoka Kenya.
Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
↧
↧
UJUMBE WA VIETNAM WAWASILI NCHINI EO
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula akimpa zawadi ya sanamu ya twiga iliyotengenezwa kwa vyuma chalavu, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, wakati wa chakula cha mchana kwenye mgahawa wa Akemi, jijini Dar es salaam. Sanamu hiyo ni ubunifu unaofanywa na kikundi cha walemavu jijini Dar es salaam (Picha zote na Bashir Nkoromo)
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha katika hoteli ya Protea Cortyard jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kuwasili kwa ajili ya mazungumzo na Kinana, leo Juni 6, 2013.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wapili kulia) akizungumza na Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam (CVP), Hoang Quan (wapili kulia), katika hoteli ya Protea Cortyard jijini Dar es Salaam. leo Juni 6, 2013. Kushoto ni Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro na Watatu kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.
Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Phili Mangula akizungumza wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa kwa ajili ya ujumbe wa Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan (wapili kushoto) katika Mgahawa wa Akemi jijini Dar es Salaam. leo
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimshukuru Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, baada ya mazungumzo yao katika hoteli ya Protea Courtyard, Dar es salaam, leo. Kushoto ni Dk. Asha Rose Migiro na watatu kushoto ni Nape Nnauye.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkaribisha katika hoteli ya Protea Cortyard jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kuwasili kwa ajili ya mazungumzo na Kinana, leo Juni 6, 2013.
Katibu wa NEC ya CCM, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akimpokea Mjumbe wa Kamati Kuu na Mwenyekiti wa Mambo ya Nje wa Chama Cha Kikomunisti cha Vietnam Hoang Quan, kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, leo, Juni 6, 2013.
↧
BARCLAYS TANZANIA - MATEMBEZI YAJULIKANAYO KAMA Step Ahead Walk 2013 kufanyika tarehe 08 June, 2013
Kila mwaka Benki ya Barclays inaandaa matembezi ya kuchangisha fedha yaliyobatizwa kwa jina la Step Ahead Walk. Mchakato huu umekuwa ukiendelea toka mwaka 2006 na Tanzania walifanya Step Ahead yao ya kwanza mwaka 2008 ambapo fedha zilichangishwa na zilitumika kusaidia matibabu ya kansa kwa watoto kwenye kituo cha kansa cha Ocean Road.
Tunu Kavishe, Meneja Mawasiliano na Huduma kwa jamii wa Benki ya Barclays Tanzania amesema tukio hili rasmi itafanyika tarehe 8 juni, 2013 katika hoteli ya Golden Tulip kuanzia saa kumi na mbili ya asubuhi na litahusisha matemebzi ya hisani ya kilomita tano (5) na kila mtu katika jamii anakaribishwa kushiriki.
Pia mtu yeyote anaweza kuchangia pesa kwa kutumia namba ya Mpesa au tigo pesa 133133. Mgeni wetu rasmi atakuwa Mheshimiwa Dr Asha Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu mstaafu wa Umoja wa Mataifa.
Naye Erwin Telemans, Mkurugenzi Mtendaji wa CCBRT amesema “msaada huu ambao CCBRT wanaupokea kutoka Benki ya Barclays ni wa thamani sana ambapo tunafanya kazi ili kufikia malengo ya Tanzania ambapo jamii itajiwezesha kupaha huduma bora na salama hasa kwa walemavu wa viungo na pia itawafikia wakinamama wote na kuhakikishia usalama wao kwenye huduma ya afya ya uzazi na watoto wachanga inafanikiwa.
Mkakati huu wa benki ya Barclays Step Ahead utasaidia pia katika kukinga mapungufu ya mtindio wa ubongo na fistula hapa Tanzania, na vile vile kuhakikisha kwamba wale waliopata mapungufu wakati wa kuzaliwa wanapata matibabu katika sehemu za viungo vyao haraka iwezekanavyo.
Naye Dr, Festus Ilako Mkurugenzi wa AMREF Tanzania amesema “Msaada na mkakati huu wa benki ya Barclays Tanzania kwa AMREF ni wa kila wakati, na kwa pamoja tunaweza tukaibadilisha jamii kutoka ilipo katika masuala ya afya kwa wakina mama na watoto, hivyo kuitengenezea jamii uelewa na ustadi katika kusimamia afya njema na kuvunja marudio rudio ya ufukara katika afya na umaskini.
Kampeni hii kutoka benki ya Barclays ijulikanayo kama Step Ahead itasaidia kuelimisha wakunga na wazalishaji katika wilaya ya Kilindi mkoani Tanga na kuwawezesha wakina mama wajawazito kujifungua katika mikono ya salama ya wafanyakazi waliofuzu katika Nyanja ya afya hivyo kupunguza uchangiaji wa vifo visivyo lazima na ulemavu wa viungo kwa mama na watoto chini ya miaka mitano. Ushirika huu baina ya Barclays na AMREF ni mfumo mpya ambayo utawezesha jamii kupata ubora na unafuu katika masuala ya kiafya.
Mwaka 2011, Benki ya Barclays na washiriki wake walifanikiwa kuchangisha shilingi za kitanzania milioni 150 kutokana na mauzo ya tiketi na matoleo mengine kutoka kwa wafadhili. Mwaka huu lengo ni kuchangisha zaidi ya marambili ya shilingi milioni 150 kutoka kwenye matoleo ya washirika muhimu na washiriki wengine katika jamii.
Fedha zitakazochangishwa mwaka huu zitakwenda kusaidia katika masuala ya uzazi na afya ya watoto kama ifuatavyo:-
1. Mafunzo kwa wakunga wa uzazi
2. Matibabu ya Fistula
3.Upasuaji kwa watoto waliozaliwa na ulemavu unaosababishwa na uzazi
Step Ahead Walk 2013 itaweza kufanikiwa tu kama itawezeshwa na kila mshiriki na jamii nzima ya kitanzania kwa ujumla. Kwa sababu hiyo basi tujiunge wote ili tuweze kufanya badiliko katika masuala ya afya kwa ujumla hapa Tanzania hususani masuala ya uzazi na afya ya watoto.
Matembezi haya yamedhaminiwa na Montage Ltd, ITV/Radio One Ltd, Clouds Media group, Mwananchi Communications, Cocacola, NSSF, African Medical Investments, Home Shopping Centre, Golden Tulip Hotels, Grand Malt na Serena Hotels
For more information contact:
Tunu Kavishe
Head of Communication and Citizenship
Barclays Bank Tanzania
+255 228 2018
↧
RAIS KIKWETE AHITIMISHA ZIARA YAKE NCHINI SINGAPORE KWA KUTEMBELEA MAENEO MBALIMBALI
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji Upya wa Miji Upya ya Singapore leo Juni 6, 2013 ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembelea Taasisi ya Elimu ya ufundi (Institute of Technical education) iliyo sawa na VETA kwa Tanzania leo Juni 6, 2013.ambapo pamoja na mambo mengine walijionea jinsi wanafunzi wake wanavyofundishwa kuunda vipuli vya aina mbalimbali ikiwa ni pamoja na vya ndege.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake wakitembezwa kwenye makao makuu ya Mamlaka ya Ustawishaji mijini ya Singapore leo Juni 6, 2013.ambapo wanajionea mfano wa jiji hilo ukiwa umetengenezwa mahususi kwa kuhakikisha mji unapangwa na kusimamiwa kisayansi kwa mipango miji ya muda mfupi na muda mrefu.
Baadhi ya wafanyabiashara walioongozana na Rais Jakaya Kikwete katika ziara ya kikazi nchini Singapore wakiwa katika picha ya kumbukumbu na mawaziri walio katika msafara huoleo Juni 6, 2013. . Wa pili kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe Bernard Membe akifuatiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda na Waziri wa Uchukuzi Dkt Harrison Mwakyembe (wa tatu) kulia.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Upya ya Miji ya Singapore leo Juni 6, 2013.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe wake katika picha ya pamoja na viongozi wa Taasisi ya Elimu ya Ufundi ya Singapore baada ya kutembelea kampasi yao jijini Singapore leo Juni 6, 2013. PICHA NA IKULU
↧
More Pages to Explore .....