Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live

MBOWE NA MBATIA WAWAFARIJI WANABUKOBA WALIOATHIRIWA NA TETEMEKO LA ARDHI.

$
0
0
Mhe. James Mbatia Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi ambae ni Mtaalamu wa Masuala ya Maafa na Mwenyekiti  wa Ukawa amewaunga mkono Wanabukoba leo akiambatana na Mwenyekiti mwenza Taifa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Mhe.Freeman Mbowe kwenye safari ya kuwatembelea wahanga. Katika Safari hiyo wametoa misaada ya dharura kwa wahanga ikiwemo chakula, sukari, fedha na n.k na kesho Jumatano wataendelea na safari hiyo kuwatembelea Wahanga hapa Mkoani  Kagera katika sehemu mbalimbali. Leo wametembelea sehemu ya Kibeta, Hamugembe, Kashozi, Nshambya katika shule ya Ihungo iliyoathiriwa zaidi na Tetemeko hilo kubwa la Ardhi na kuwafanya wanafunzi kusimamisha masomo yao kwa wiki mbili kwa kukosa sehemu ya kusomea/Madarasa na Mabweni.

Msafara kuelekea Kata ya Hamugembe





Pia walitembelea Kituo cha Watoto Yatima Hamugembe chenye watoto 36 ambacho kipo chini ya mwangalizi Bi. Saada ambacho kimepata matatizo kwa Nyumba zake kuanguka chini na kuwapa na kuwafariji 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Aikael Mbowe akisalimiana na Bi. Saada mwangalizi wa Watoto Yatima





Wakiteta na Wanakijiji wa Kibeta sehemu Mama anayotokea Mbunge wa Bukoba Mjini Wilfred Muganyizi Lwakatare.







Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia akipata Ndizi kwenye Soko la Nyakanyasi wakati wa kuwatembelea Wahanga wa Tetemeko la Ardhi Bukoba leo.






Sehemu ya Majengo katika Shule hiyo kwa sasa baada ya kutokea Tetemeko

Tetemeko likiwa limeharibu sana sehemu kubwa ya Kanisa katika Shule hiyo ya Ihungo iliyopo kilometa 8 kutoka Bukoba Mjini

Taswira ya sasa Wanafunzi wa Shule ya Ihungo wakijipanga kuondoka Majumbani mwao baada ya Tetemeko la jumamosi kuwaathiri kiasi kikubwa na kushinikizwa kufunga shule hiyo kwa wiki mbili kupisha kuangaliwa upya kwa Shule hiyo kutokana na kuathiriwa na tetemeko.


Wakiwa Kanisani ndani, Kanisa lililojengwa miaka mingi iliyopita

Akiwa Kanisani hapo alipata muda akafahamu Viongozi mbalimbali katika picha waliopitia katika kanisa Hilo linalotimiza miaka 125 hivi karibuni lililozinduliwa mwaka 1892 likiwa ni kanisa la kwanza likifahamika Kashozi Parish.


Mh. Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia pia alitembelea Kanisa la Kashozi

Kanisa la Kashozi kwenye Taswira ambalo pia limepata shida kwenye Tetemeko la Ardhi lililotokea hivi karibuni siku ya Jumamosi sept. 10, 2016.
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia alipata nafasi akapata picha na Mama mlezi kanisani hapo ambaye alitambulishwa kuwa ana umri mrefu.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Aikael Mbowe na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia leo jumanne septemba 13, 2016 wamewatembelea Waathiriwa wa Tetemeko na kuwafariji Bukoba. Pia waliambatana na Mbunge  wa Viti Maalum Bi.Savelina Mwijake na Viongozi mbalimbali wakiwemo wa Chadema.Mbunge wa Bukoba Mjini akiteta jambo na Wafabiashara mbalimbali walioathiriwa na Tetemeko hilo kubwa Hapa Bukoba na huku kilio chao kikubwa kikiwa ni malimbikizo ya madeni yao kwa serikali ambayo mpaka wanapata hasara kubwa na kwa ujio huu mbaya wa Tetemeko la Ardhi wakidai zaidi ya Milioni 600.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Aikael Mbowe na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi  James Mbatia(kulia) wakimsikiliza kwa makini mfanyabiashara huyo.
Janga la Tetemeko la Ardhi limewaathiri sehemu kubwa wafanyabiashara

WAKULIMA WA ZAO LA MAHINDI MKOANI RUVUMA WALALAMIKIA UTARATIBU WA KUNUNUA MAZAO HAYO.

$
0
0
Baadhi ya wakulima wa zao la Mahindi mkoani Ruvuma, wamelalamikia utaratibu wa Serikali wa kununua mahindi ya wakulima kiasi cha Tani Moja tu kwa kila Mkulima sawa na gunia Kumi na kwamba kiasi hicho ni kidogo mno ikilinganishwa na idadi kubwa ya mahindi waliyozalisha katika msimu huu.

PUMA ENERGY TANZANIA YAKABIDHI STIKA ZA WIKI YA USALAMA BARABARANI 2016 KWA JESHI LA POLISI JIJINI DAR LEO

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania,Phillipe Corsaletti akimkabidhi stika Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga ,zitakazotumika katika zoezi la ukaguzi wa magari katika juma la wiki ya usalama barabarani,inayotarajiwa kuanza hivi Karibuni.Bwa.Phillipe alisema kuwa hiyo ni sehemu ya uwekezaji wao katika masuala ya usalama barabarani ambao wanaamini ni wa muhimu sana kwa maendeleo ya Taifa."Tunaamini kuwa shughuli zetu zinaweza tu kuwa salama kama jamii inayotuzunguka ipo salama",alisisitiza Mkurugenzi huyo.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania,Phillipe Corsaletti pamoja na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,Kamanda Mohamed Mpinga wakionesha baadhi ya stika mbele ya mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo katika ofisi za makao makuu ya Trafiki,jijini Dar Es salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Puma Energy Tanzania,Phillipe Corsaletti akisoma taarifa yake kabla ya kukabidhi stika za Usalama Barabarani kwa Jeshi la Polisi Kitengo cha usalama Barabarani ,mbele ya mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika mapema leo jijini Dar.Bwa.Phillipe alieleza kuwa suala la usalama barabarani linaendelea kuwa na changamoto kubwa duniani kote,amesema kuwa kwa hapa Tanzania jamii inashuhudia ajali za barabarani karibu kila siku.

"Ajali hizi zinawagusa vijana na wazee,wanataaluma,wafanyabiashara,wakulima,wanasiasa,matokeo ya ajali hizi ni vifo,majeruhi,uharibifu wa mali,upotevu wa wataalamu na mwisho kabisa mzigo mkubwa ni kwa Taifa",alifafanua Bwa,Phillipe.

Hivyo Bwa,Phillipe ameziomba mamlaka zinazohusika kuyatazama mambo hayo kwa undani na kuweka mfumo ambao utasaidia kuondoa ama kupunguza kwa kiaisi kikubwa wimbi la ajali za barabarani.Mkurugenzi huyo amesema kuwa pamoja na kuwa na wadau wakubwa wa mambo ya usalama barabarani pia wamekuwa wakitoa elimu kwenye shule mbalimbali za msingi hapa nchini na kuwa mpaka sasa wamefanikiwa kuzikifia shulu 30,amesema na kuongeza kuwa lengo lao kubwa ni kuzifikia shule zote za msingi za serikali hapa nchini kupitia mpango huo wa kutoa elimu ya usalama barabarani kwa shule za msingi.

Bodi ya Filamu yaahidi ushirikiano uanzishwaji wa Mradi wa TYEEO Barazani Entertainment.

$
0
0
Na: Frank Shija, MAELEZO

SERIKALI imepongeza juhudi za wadau wa Tasnia ya Filamu nchini kutokana na jitihada zao katika kuhakikisha tasnia hiyo inakuwa na kuwaletea maendeleo endelevu ikiwemo Ajira za uhakika kwa vijana.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mktendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania (KBF) Bibi. Joyce Fissoo alipokutana na ujumbe kutoka Taasisi isiyo ya Kiserikali ya TYEOO walipomtembelea ofisini kwake jana kwa ajili ya kutambulisha rasmiMradi wa TYEEO Barazani entertainment jana Jini Dar es Salaam.

Fissoo alisema kuwa mradi huo ni muhimu kwa mustakabari wa kukuza tasni ya Filamu nchini kwani utarahisha kufikisha katika kuwafikia wadau wengi zaidi wa tasni hiyo walioko katika mikoa ya pembezoni.

“Niseme tu kwa dhati kabisa nawapongeza sana kwa ubunifu wenu mradi huu ni mzuri na utaongeza tija katika tsni yetu ya Filamu, name nina waahidi kuwapa ushirikiano pindi mtakapo kuwa mnahitaji”. Alisema Fissoo.

Aidha alitoa ushauri kwa Taasisi hiyo kutumia vibanda vya maonyesho ya Filamu vilivyopo katika maeneo mbalimbali nchini ili kutekeleza mradi huo kwa kuwa nia ya Serikali ni kuona dhana ya urathimishaji wa kazi za wasinii inafanikiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa TYEEO, John Kallaghe amesema kuwa pamoja na kuwa mradi huo ni binafsi lakini kutokana na imani kubwa waliyonayo juu ya Bodi ya Filamu wameona siyo busara kuendelea kutekeleza jambo kubwa kama hili bila ya kushirikisha mamlaka hiyo ambayo ndiyo msimamizi mkuu wa Tasnia ya Filamu nchini.

Aliongeza kuwa wazo la kuanzishwa kwa mradi huu ilikuwa ni kusaidia kuwawezesha vijana kujikomboa katika lindi la umaskini kupitia huduma itokanayo na mradi huu ambayo ni utayarishaji na usambazaji wa kazi za wasanii wa Filamu kwa njia ya kisasa zaidi.

Kallaghe alisema kuwa wao kama wadau tasni hiyo wako tayari kupokea ushauri na maelekezo ya namna ambavyo wanaweza kuboresha na kutekeleza mradi huo kwa ajili ya maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Mradi wa TYEEO Barazani ni miongoni mwa miradi kadhaa ambayo imeanzishwa na taasisi ya TYEEO, ulioasisiwa tangu mwaka 2013 na unakadiriwa kutoa fursa ya ajira za uhakika kwa vijana takribani 6000 katika kada zote za Filamu hadi kufikia mwaka 2017.

SERIKALI ITUME WATAALUMU KUFANYA UTAFITI DODOMA.

$
0
0
 
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Nchini(GST) Profesa Abdulkarim Mruma,
 
Na Sheila Simba,Maelezo.
14.9.2016
WAKALA wa Jiolojia Nchini (GST) imezitaka Taasisi za Umma, Wizara na Idara za Serikali kuwatumia Wataalamu wa jiolojia katika shughuli za ujenzi wa ofisi za Serikali Mkoani Dodoma ili kuweza kukabiliana na athari za matetemeko la ardhi yanayotokea mara kwa mara Mkoani humo. 

Wito huo umetolewa leo na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Jiolojia Nchini(GST) Profesa Abdulkarim Mruma, wakati wa mahojiano yake na MAELEZO kuhusiana na athari zitokanakazo na mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo matetemo ya ardhi hususani katika kipindi hiki ambacho Serikali imepanga kuhamishia shughuli zake mkoani Dodoma. 

“Nashauri Serikali kutuma wataalamu kufanya utafiti ili kuangalia ni maeneo gani yanafaa kujenga ofisi za Serikali na zinatakiwa zijengwe kwa mfumo upi ili ziweze kuhimili matetemeko ya ardhi pindi yanapotokea” alisema Profesa Mruma .Aliongeza kuwa hapo awali ujenzi wa magorofa mkoani humo ilikuwa mwisho ghorofa nne kutokana na mkoa huo kupitia na Bonde la Ufa la Afrika Mashariki ambalo kusababisha matetemeko ya mara kwa mara. 

Akizungumzia kuhusu ujenzi wa maghorofa Mkoani humo, Prof. alisema magorofa yanayotakiwa kujengwa yawe mapana na yenye kuzingatia ugumu wa nondo, aina saruji inayotumika katika ujenzi na uimara wa jengo husika. “Jengo likiwa nyembamba na refu ni rahisi kupata madhara pindi tetemeko linapotekea hivyo ni vyema watu wafuate ushauri wa wataalamu kabla kufanya ujenzi na pia kuangalia maeneo yanayofaa kwa ujenzi” alisema Prof Mruma .

Aidha ameongeza kuwa majengo yote yatakayojengwa yanatakiwa kuzingatia ubora wa majengo kwa kutumia wataalamu badala ya kujenga bila kushirikisha wataalamu.

TASWIRA MBALIMBALI KUTOKA BUNGENI MJINI DODOMA LEO

$
0
0


 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Mhe. Mwigulu Nchemba akiwaeleza jambo Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kushoto) na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakati wa kikao cha bunge kinachoendelea leo Mjini Dodoma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Kazi,Ajira na Walemavu Mhe. Anthony Mavunde akijibu swali wakati wa kikao cha bunge kinachoendelea leo Mjini Dodoma.


 Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia mijadala bungeni leo

 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akijibu swali wakati wa kikao cha bunge kinachoendelea leo Mjini Dodoma ambapo alisema kuwa serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni mbili (2) katika mfuko wa mazingira kwa ajili ya zoezi ya upandaji miti ili kutunza mazingira.

 Waziri Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage  akijibu swali wakati wa kikao cha bunge kinachoendelea leo Mjini Dodoma ambapo alisema kuwa agizo la Rais Dkt. Magufuli la kuhakikisha viwanda vinavyobinafsishwa vinafanya kazi linaendelea kutekelezwa tangu Novemba 2015

 Mwenyekiti wa Bunge Mhe. Azzan Musa Zungu akiendesha kikao cha bunge leo mjini Dodoma



Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Charles Tizeba akiwasilisha bungeni Muswada wa Sheria ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo wa mwaka 2016

 Baadhiya wabunge wakiingia katika ukumbi wa Bunge kuhudhuria vikao vya bunge vinavyoendeleo Mjini Dodoma.


PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

DC STAKI APONGEZA JAMII YA KIMASAI KUACHANA NA MILA POTOFU NA KUANZA KUMWABUDU MUNGU

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule akisikiliza kwa makini maelezo ya mmoja ya wazee wa kabila la Kimasai kuhusu umuhimu wa elimu katika maeneo hayo.
Mkuu wa Wilaya ya Same Rosemary Staki Senyamule, Viongozi wa dini na wananchi wakishuhudia sherehe ya vijana wa kimasai (Morani) kuingia stage ya uzeeni.
 Baadhi ya vijana wa Kimasai wakipandisha Mori kwa furaha ya kuingia stage ya uzee.
Dc Staki akisalimiana na viongozi wa dini walioendesha misa hiyo mara baada ya kuwasili katika viwanja hivyo
 Dc Staki akishuhudia vijana wakipandisha Mori
Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Rosemary Staki Senyamule akiwa kwenye sala wakati wa Misa
Dc Staki akifatilia kwa makini zoezi la kuingia hatua ya Uzee kwa waliokuwa vijana wa Kimasai
 
Na Mathias Canal, Kilimanjaro

Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Rosemary Staki Senyamule amewapongeza baadhi ya vijana wa kimasai kwa kuachana na imani potofu na hatimaye kuanza kumwabudu Mungu kwa kuhudhuria Misa mbalimbali katika makanisa.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu huyo wa Wilaya hiyo wakati wa sherehe maalumu kwa waliokuwa vijana wa Kimasai (Morani) kuingia hatua kubwa ya uzeeni na ya heshima katika kabila hilo.

 Sherehe hiyo ilifanyika katika uwanja wa Kitongoji cha Endevisi, Kijiji cha Emuguru na ibada hiyo kuongozwa na Mchungaji Joshua Laiser kutoka kanisa la Kiinjili la kilutheli Tanzania (KKKT) Wilaya ya Hai Dayosisi ya Moshi na Mchungaji Andrea Sangolo wa Usharika wa Bonde la Ruvu Same na baadaye kufuatiwa na shughuli za kutoa Baraka kwa vijana hao zoezi lililofanywa na viongozi wa dini, Serikali na Wazee wa Mila.

Sherehe hizo zimefanyika zikiwa na lengo la kufanya mageuzi kwa jamii ya kimasai na hatimaye kuachana na mila potofu kama vile kuabudu waganga wa jadi na kuanza kumuabudu Mungu wa kweli.

Pamoja na pongezi hizo za mkuu wa Wilaya ya Same kwa jamii ya kimasai kufanya mapinduzi hayo ya kuachana na mila potofu pia aliwataka kuwekeza zaidi kwenye swala la elimu na kuwataka kuwaruhusu watoto wote wa kiume na watoto wa kike kusoma kwa usawa.

Katika Jamii ya kimasai kumekuwepo na kadhia mbalimbali za mila Potofu za kuozesha watoto wadogo na kufanyiwa tohara kwa watoto wa kike, matukio ya ubabe ikiwemo wizi wa mifugo na mauaji kwa imani potofu jambo ambalo limezuiwa na Mkuu huyo wa Wilaya hiyo.

Dc Staki ametumia nafasi hiyo pia kuwataka wananchi wote wa jamii hiyo ya Kimasai kutumia rasilimali walizo nazo kwa kuuza kiasi ikiwemo Ng’ombe ili kujenga Hospitali zitakazo wasaidia kuimarisha afya zao na kujenga shule ambazo zitawaimarisha watoto wao kielimu.

Tukio hilo la Ibada kwa vijana hao ni kubwa katika historia ya kabila la Kimasai na limejumuisha jamii ya Kimasai kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo Tanzania na nchi jirani ya Kenya.

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUEPUKA MADHARA YANAYOWEZA KUSABABISHWA NA TETEMEKO LA ARDHI.


VODACOM YAENDELEA KUFANIKISHA WIKI YA USALAMA BARABARANI.

$
0
0

  Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Kamanda Mohammed Mpinga (wapili kulia)wakipongezana na wadhamini wa wiki ya Usalama barabarani itakayofanyika kitaifa mkoani Geita hivi karibuni wakati wa kukabidhiana stika maalum kwa ajili ya zoezi hilo jijini Dar eS Salaam leo,kutoka kushoto Mkurugenzi wa Mawasiliano na  Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia,Mkurugenzi mkuu wa Puma energy,Philippe Corsaletti na Mkurugenzi wa Selcom,Benjamin Mpamo.
  Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Kamanda Mohammed Mpinga (kulia) akikabidhiwa stika  na Mkurugenzi wa Mawasiliano na  Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia jijini Da res Salaam leo,zitakazotumika katika zoezi la wiki   ya Usalama barabarani inayodhaminiwa na Vodacom Tanzania itakayofanyika kitaifa mkoani Geita hivi karibuni.
 Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Kamanda Mohammed Mpinga (kulia)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)kuhusiana na wiki   ya Usalama barabarani itakayofanyika kitaifa mkoani Geita hivi karibuni,wakati wa kukabidhiwa stika zitakazotumika katika zoezi hilo zilizokabidhiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano na  Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia(wapili kulia).
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Nchini, Kamanda Mohammed Mpinga (kulia)akionesha stika zitakazotumika katika wiki ya Usalama barabarani itakayofanyika kitaifa mkoani Geita hivi karibuni wakati wa kukabidhiana stika hizo maalum kwa ajili ya zoezi hilo leo jijini Dar eS Salaam,wanaoshuhudia kutoka kushoto Mkurugenzi wa Mawasiliano na  Uhusiano wa Vodacom Tanzania Rosalynn Mworia,Mkurugenzi mkuu wa Puma energy,Philippe Corsaletti.

KAMPENI YA DECLUTTER AND DONATE YAZINDULIWA DAR ES SALAAM.

$
0
0
 Katikati - Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Kampeni ya Declutter and Donate Bi. Nasra Karl akiongea na waandishi wa habari katika mkutano jijini Dar es Salaam (kushoto) Hyacinta Ntuyeko - Mkurugenzi wa Glory Sanitary Pads (Kulia) Aunty Sadaka - Lifestyle Consultant na kushoto kabisa Bi Stella Malisha - Mkurugenzi wa IS Duke International.
 Aunty sadaka akitilia mkazo umuhimu wa kampeni ya declutter and donate kwa waTanzania wote. Kushoto kwake ni Bi. Stella Mashila Mkurugenzi wa IS Duke International.
 Bi Hyacinta Ntuyeko wa Glory Sanitary Pads akijibu swali kutoka mwandishi wa habari katika uzinduzi wa kampeni ya Declutter and Donate iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto kwa Bi Nasra karl Mwanzilishi na Mkurugenzi ya kampeni ya Declutter and Donate na pembeni yake Aunty Sadaka Lifestyle consultant.
Bi Nasra Karl, Mkurugenzi na Mwanzilishi ya kampeni wa Declutter and Donate akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam. 

KAMPUNI ya Elite Organizing Services Limited imezindua kampeni inayoitwa Declutter and Donate jijini Dar es Salaam. Hii ni mara ya kwanza kwa kampeni ya aina hii kuzinduliwa nchini Tanzania. Kampeni ya Declutter & Donate ni mpango wa kijamii unaohamasisha umma kugawa vitu ambavyo hawavihitaji.

Mwanzilishi na Mkurugenzi wa kampeni Bi Nasra Karl alisema “wazo la kuanzisha kampeni hii lilikuja hapo mheshimiwa Raisi John Pombe Magufuli alivyotamka kuwa siku ya Uhuru itasherekewa kwa kufanya usafi ila kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu.  Hapo basi tulikuja na wazo yakuanza kusaidia nyumba na biashara mbali mbali kuepukana na vitu wasiyo hitaji ambayo inasaidia kukuza mazingira safi na kusaidia kuzingatia ubora katika maisha yetu ya kila siku. 

Kuwa kampuni ya uandalizi inayotoa huduma kusaidia watu binafsi na biashara mbali mbali kuepuka kuishi na vitu wasiyo viihitaji na maisha ambayo yanampangilio, ELITE ORGANIZING SERVICES LIMITED iliona haja ya kuongeza uelewa kuelimisha umma maana ya kutoa vitu visivyo na umuhimu katika maisha yao ( declutter) na ni jinsi gani vinaweza kupunguzwa katika maisha ya watu na jinsi gani inaweza kutumika kwa manufaa ya wengine.  Kama msemo maarufu  ya kingereza inayosema ‘ Taka taka ya mwanaume moja ni dhahabu kwa mwanaume mwingine’ 
Kampeni ya Declutter & Donate Campaign itaanza mwezi wa tisa Septemba na kuisha mwezi wa kumi na mbili yaani miezi mitatu. 

Katika kipindi hiki tunawaomba watu binafsi, familia na biashara mbali mbali kugawa vitu vyao ambayo zimetumika na kuuuzwa katika yard sale, mwanzoni mwa Disemba tunategemea kuwa na tukio itakayo changisha kwa ajili ya kituo inayosaida watu. (charity).

Mwishoni mwa Disemba tutakuwa na tukio ambapo tutakuwa na wataalamu wa kudeclutter wakija kuongea na wa Tanzania na kuwaeleza jinsi ya kuepeukana na vitu visivyo na muhimu katika biashara zao, nyumba zao na maeneo yanayowazunguka.  

Mwaka huu kampeni ya Declutter & Donate watasaidia watoto yatima na wanawake wanaoishi katika mazingira magumu. Mwaka huu tunapenda kusaidia wanawake wanaopata shida katika usalama ya hedhi na  ‘Mtoto anayesoma atakuwa mtu anayeweza kufikiri’ kwa watoto wanao ishi katika mazingira magumu. 

Mara nyingi tukietembelea watoto yatima na kugawa chakula, nguo na vitu vingine vya kutumia kila siku tunasahau kwamba michezo na vitabu vina jukumu kubwa katika ukuaji bora wa motto na ndio maana tumeamua kuwapa michezo na vitabu.  


Tunapokea fenicha, vifaa vya nyumbani, vitabu vya watoto na michezo ya watoto. Hivi sasa tunaishughulikia mahala pakuacha hiv vitu na tutaweza kuwajulisha hivi karibuni kupitia vyombo vya habari.   

Tamasha la uhondo wa Zantel lakongo nyoyo za wakazi wa Tameke

$
0
0
 Meneja Habari na Uhusiano wa Kampuni ya simu ya Zantel, Winnes Lyaro
(kulia), akitoa maelezo kwa baadhi ya wakazi wa Temeke, Dar es Salaam
 kuhusu huduma na bidhaa  mpya zitolewazo na kampuni hiyo wakati
wa tamasha lililopewa jina la ‘uhondo wa Zantel’ lililodhaminiwa na
kampuni hiyo.
 Msanii wa muziki wa bongo flava, Seif Mwinjuma ‘sholo mwamba’ akiimba
katika tamasha la Uhondo wa Zantel lililofanyika katika viwanja vya
Temeke Mwisho, Dar es Salaam hivi karibuni ikiwa ni moja ya kampeni za kampuni ya simu ya mkononi ya Zantel kuwa karibu na wateja wake ikiwajulisha bidhaa na huduma mpya zilizopo sokoni.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ally Momba ‘Momba’ akionyesha umahiri
wake wa kuimba katika tamasha la Uhondo wa Zantel lililofanyika katika
viwanja vya Temeke Mwisho, Dar es Salaam ikiwa ni moja ya kampeni
za kampuni ya simu ya mkononi ya Zantel kuwa karibu na wateja wake
ikiwajulisha bidhaa na huduma mpya zilizopo sokoni.
Msanii maarufu anayetesa na wimbo wake wa ‘segere’ Siza Mazongela
akikonga nyoyo za mashabiki wake katika tamasha la Uhondo wa Zantel
lililofanyika katika viwanja vya Temeke Mwisho, Dar es Salaam
ikiwa ni moja ya kampeni za kampuni ya simu yamkononi ya Zantel kuwa
karibu na wateja wake ikiwajulisha bidhaa na huduma mpya zilizopo
sokoni.

MAJALIWA AZINDUA MIONGOZO YA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI MJINI DODOMA

$
0
0

 Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akizungumza wakati alipozindua  Miongozo ya Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi  Miongozo ya Mfumo wa Anwani  za Makazi na Postikodi  kwenye ukumbi wa Msekwa , bungeni mjini Dodoma Septemba 14, 2016.
 Msanii, Mrisho Mpoto akitumbuiza katika uzinduzi wa  Miongozo ya Mfumo wa Anwani  za Makazi na Postikodi uliofanywa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenye ukumbi wa Msekwa , bungeni mjini Dodoma Septemba 14, 2016. 
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea bango lenye anwani na Postikodi ya makazi yake ya Dodoma baada ya kuzindua  Miongozo ya Mfumo wa Anwani  za Makazi na Postikodi  kwenye ukumbi wa Msekwa , bungeni mjini Dodoma Septemba 14, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha nakakala ya kitabu cha Miongozo ya  ya Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi bada ya kuuzindua kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni mjini Dodoma Septemba 14, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

PROF. MBARAWA ATOA MIEZI SITA KUMALIZA UPANUZI WA UWANJA WA NDEGE WA MWANZA.

$
0
0
Mkandarasi wa kampuni ya Nyanza Road Construction inayojenga barabara ya Furahisha hadi Pasiansi akitoa maelezo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipokagua ujenzi wa barabara hiyo jijini Mwanza.
 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa mkandarasi Nyanza Road Construction inayojenga barabara ya Furahisha hadi Pasiansi KM 2.8 wakati alipokagua ujenzi wa barabara hiyo, jijini Mwanza.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amemtaka Mkandarasi wa kampuni ya Beijing Construction Engineering Group anayejenga uwanja wa ndege wa Mwanza kumaliza kazi ya upanuzi wa uwanja huo ifikapo mwezi Februari Mwakani.

Profesa Mbarawa ametoa kauli hiyo alipokuwa akikagua kazi ya ujenzi na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza pamoja na daraja la watembea kwa miguu lililopo maeneo ya furahisha, jijini Mwanza.

Profesa Mbarawa amesema kuwa kukamilika kwa ujenzi na upanuzi wa uwanja huo kutaimarisha hali ya usafiri wa anga kwa wakazi wa Mwanza na mikoa mingine na hivyo kukuza shughuli za kibiashara nchini.

“Hakikisheni upanuzi wa uwanja wa ndege huu unakamilika haraka ili kurahisisha na kuboresha huduma za usafirishaji kiwanjani hapa”, amesema Waziri Mbarawa.

Aidha, Profesa Mbarawa amemtaka mkandarasi wa kampuni ya Nyanza Road Construction kumaliza kwa wakati upanuzi wa barabara ya ‘Mwanza-Airport’ eneo linaloanzia Ghana Quarters hadi Uwanja wa Ndege wa Mwanza KM 9.15 pamoja na daraja la watembea kwa miguu la furahisha ili kukuza uchumi na kupunguza kero ya msongamano wa magari katika jiji la Mwanza.

Katika hatua nyingine Prof. Mbarawa amewataka wananchi wa Mwanza kutoharibu miundombinu ya barabara na madaraja ambayo Serikali inatumia gharama kubwa katika utengenezaji wake.

“Naomba muitunze na kuithamini miundombinu hii kwani Serikali inatumia gharama kubwa katika kutengeneza na kukarabati”, amesisitiza Prof. Mbarawa.

Ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza ni mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa uwanja huo unaboreshwa kuwa wa kisasa na wa kimataifa ili kuwezesha ndege kubwa kutua kwa wingi na kuwa kiungo muhimu kwa mikoa 10 ya kanda ya Ziwa na Kati.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

VISIMA 7 KUPUNGUZA TATIZO LA MAJI KISHAPU

$
0
0
Youth Climate Activist Network (YouthCAN) Tanzania Ni mtandao wa vijana wanaotoka kwenye taasisi za dini mbalimbali wanaofanya shuguli mbalimbali za mazingira na afya kwa ujumla kwa kujitolea chini ya Shirika la Norwegian Church Aid (NCA)

Kuanzia Tarehe 11/9 /2016 vijana hawa walianza masafara wa Kutembelea baadhi ya maeneo yaliyo athirika sana na mabadiliko ya tabia nchi. Ili kutoa elimu ya Utunzaji wa mazingira, vyanzo vya maji na usafi .baada ya kutoa elimu hiyo Halmashauri ya wiliya Kishapu Mkoani Shinyanga wanatarajia kwenda Kutoa elimu hiyo Mkoani Manyara kwenye baadhi ya vijiji vilivyopo Hanang.Hydom na Mbulu.

Licha ya kutoa elimu juu mazingira,Maji ana afya vijana hawa watapata nafasi ya kuzindua baadhi ya Visima vya maji vilivyo jengwa na Shirika la Norwegian Church Aid (NCA) kwa kushirikiana na Washirika wake.

Ambapo kwa kuanza wamepata fursa ya kushiriki uzinduzi wa visima 7 vilivyojengwa kwa msaada wa watu wa Norway visima hivyo vitasaidia kutatua tatizo la maji safi na salama katika vijiji vi 3 wiliyani Kishapu .ambavyo ni IKONDA A,UBATA na MWAWEJI.

Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya Kishapu Bwana.Stephen M Magoiga akizindua moja kati ya Visima saba.

Afisa Mradi Mwandamizi Mama Tina Mosha Akimtwisha maji Moja ya wanakiji wa IKONDA.
Nizar Selemani Mratibu wa shuguli za vijana katika shirika la NCA na Baraka Chedego ambae ni Mratibu wa Youth CAN wakizungumza jambo wakati wa mkutano na wanakijiji cha Ikonda.
Moja visima vilivyokuwa vikitumiwa na wanachi kabla ya ujenzi wa visima vya kisasa.
Vijana wa YouthCAN wakitoa elimu ya Mazingira,Maji na Afya kwa njia ya Nyimbo Kijijini Ikonda.
ikundi Mvalimbali vya sanaa kutoka Kishapu vikitoa burudani wakati wa Mkutano.
Wananchi wa Kishapu wakifatilia mkutano kwa Umakini Mkubwa.



SERIKALI ITAHAKIKISHA WALIOTEKWA NYARA KONGO WANAPATIKANA WAKIWA SALAMA

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga

Na. Immaculate Makilika- MAELEZO.

Serikali imesema kuwa inashirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuhakikisha kuwa madereva wanaoendesha magari aina ya malori ambao wametekwa nyara jana na waasi wa kikundi cha Maimai katika eneo la Namoyo jimbo la Kivu kusini katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanapatikana wakiwa salama.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Mindi Kasiga leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuwakoa watanzania waliotekwa nyara.

“Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Kongo inaendelea kufanya kila jitihada kuhakikisha madereva hao wanaachiwa huru haraka iwezekanavyo na kurudishwa nchini wakiwa salama”

“ Waasi hao wa Maimai wametoa masaa 24 hadi kufikia leo wawe wamelipwa kiasi cha Dola 4,000 kwa kila dereva ili waweze kuwaachia huru na kutishia kuwadhuru endapo hawatapata fedha hizo, hivyo basi Serikali imeendelea kuwa na mazungumzo na Serikali ya Kongo ili kupata ufumbuzi wa suala hili” alisema Kasiga.

Aliongeza kuwa malori yaliyotekwa nyara ni 12 kati ya hayo nane ni mali ya mfanyabiashara wa kitanzania Bw. Azim Dewji na mengine ni mali za wafanyabiashara kutoka nchini Kenya.Aidha, Serikali imewataka watanzania kufahamu hali ya usalama wa nchi wanazokwenda ili kujikinga na matatizo mbalimbali yanayoweza kuwapata wakiwa katika nchi hizo.

SERIKALI IMEJIPANGA KUJENGA KIWANDA CHA KUSINDIKA MAHINDI MKOANI RUVUMA

$
0
0
Katika kuhakikisha wakulima wananufaika na zao la mahindi mkoani ruvuma serikali imejipanga kujenga viwanda vya kusaga mahindi mkoani humu,pia inawakaribisha wa wekezaji kujitokeza kujenga viwanda vya kusaga mahindi.
Na hii inatokana na mkoa wa ruvuma kuzalisha kwa wingi mahindi zaidi ya tani laki nane  kwa kila mwaka ambapo mahindi mengi huaribika huku na wakati mwingine wakulima huyauza mahindi hayo kwa bei ya hasara.

FORUM CC YAWAKUTANISHA WADAU MBALIMBALI KUJADILI MWONGOZO WA KUFANYA USHAWISHI NA UTETEZI KUHUSU MABADILIKO YA TABIANCHI

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Shakwaanande Natai akifungua kongamano la mabadiliko ya Tabianchi lenye lengo la kujadili mwongozo wa ushawishi na utetezi katika mipango ya Maendeleo ya Serikali iliyandaliwa na ForumCC na kuwakutanisha wadau mbalimbali kutoka serikarini na sekta binafsi iliyofanyika katika ukumbi wa Sayansi jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa bodi ya ForumCC, Euster Kibona akizungumza jambo wakati wa kongamano lililowakutanisha wadau mbalimbali kujadili mabadiliko ya Tabia ya nchi yaliyofanyika leo katika ukumbi wa Sayansi jijini Dar es Salaam.
Afisa Miradi kutoka ForumCC, Fazal Issa akitoa mada kuhusu mwongozo wa ushawishi na utetezi wa kuingiza mabadiliko ya Tabianchi katika mipango ya maendeleo ya Serikali pamoja na kupangiwa bajeti kuliko kusubilia majanga yakitokea.
Mratibu wa ForumCC, Rebecca Muna akichangia mada wakati wa kongamano lililowakutanisha wadau mbalilimbali wa mazingira kujadili mabadiliko ya Tabianchi.
 Mchumi kutoka Tume ya Mipango, Jordan Matonya akichangia mada wakati wa kongamano lililowakutanisha wadau mbalimbali wa mazingira
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari za MazingiraTanzania(JET), John Chikomo akichangia mada kuhusu jinsi ya kuripoti habari zinazohusu mabadiliko ya Tabianchi na kuwafunda waandishi wanaoripoti habari za Tabianchi.
Afisa Mifugo kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Theresia Massoy akichangia mada.
Afisa Msaidizi wa Miradi wa ForumCC, Jonathan Sawaga akichangia mada wakati wa kongamano lilowakutanisha wadau mbalimbali wa mazingira kujadili mabadiliko ya Tabianchi.
Wadau mbalimbali wa Mazingira wakifuatilia mada
Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA

RC MOROGORO MH. STEPHEN KEBWE ATAMBELEA UPIMAJI NA UMIRIKISHAJI WA ARDHI KIJIJI CHA DIHOMBO NA HEMBETI, MVOMERO.

$
0
0

Dr. Stephen Nindi(katikati) Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango na Matumizi ya Ardhi Tanzania akimuelezea jambo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe walipotembelea eneo la upimaji.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe akipongeza hatua ya upimaji wa ardhi na kuahidi kuendelea kutembelea kuona maendeleo
Bw. Ally Amri(kushoto) ambaye ni Land Surveyor akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe namna zoezi la upimaji linavyofanyika

Christian Thomas(aliyevaa shati la blue) ambaye ni mwenyekiti wa kijiji akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe namna zoezi la upimaji wa Ardhi lilivyo wasaidia
Viongozi wa Serikali na wadau mbalimbali wakiwa katika eneo la moja ya kijiji kuona jinsi shughuli za upimaji zinavyokwenda
Hiki ni kifaa kiitwacho Real Time Kinematic (RTK) ni moja ya kifaa cha kisasa kinachotumika katika upimaji wa ardhi.
Bw. Charles Charokiwa Msumari(katikati) Afisa Mifugo Msaidizi Mkuu wa Tume ya Mipango na Matumizi ya Ardhi akitoa ufafanuzi kwa Mkuu wa mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe alipotembelea kituo chao ambacho wanakitumia kukusanyia taarifa mbalimbali na shughuli zao

Baadhi ya wadau mbalimbali wakiendelea kufuatilia kwa makini maelezo
Mtaalam wa GIS Theonest Mlolewe akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mh. Stephen Kebwe (hayupo pichani) namna wanavyofanya kazi.


Picha zote na Fredy Njeje/ Blogs za Mikoa


MKUU wa Mkoa wa Morogoro Dkt.Stephen Kebwe amesema kazi ya upangaji wa matumizi bora ya ardhi kwa kiasi kikubwa itapunguza na kuondoa migogoro mbalimbali ya ardhi inayotokea katika kijiji kwa kijiji,kata kwa kata au kitongoji kwa kitongoji na kusisitiza kuwa Serikali haitashindwa kumchukulia hatua za kisheria mtu yeyote atakaekwamisha kazi ya upimaji wa ardhi yenye lengo la upangaji wa matumizi bora ya ardhi.

Akizungumza na wanakijiji wa kijiji cha Dihombo,Dkt.Kebwe alisema kazi hiyo itasimamiwa kikamilifu na kamati husika za ulinzi na usalama kutoka Wilayani,Kata hadi Mkoa kuhakikisha inafanikiwa. Alisema kazi hiyo inayofanywa ya upimaji wa ardhi itakuwa ndio muarobaini wa kuondoa migogoro inayojitokeza mara kwa mara ikiwemo ya Wakulima na Wafugaji katika mkoa huo.

Alisema kwa sasa wapimaji wa ardhi wanatumia vipimo vya kisasa zaidi ambavyo kwa kiasi kikubwa vipimo hivyo vitaweza kupima ardhi kwa kipindi kifupi na kila mtu kumiliki kipande cha eneo lake.

"Nakumbuka wakati wa kampeni mwaka jana,Rais Dkt.John Magufuli alihaidi wazi kuwa kipindi cha miaka 10 kutakuwa na upimaji katika maeneo yote ya nchi kwa utaratibu wa mpango mzuri na wa kisasa,kwa miaka mitano hii vijiji takribani 7500 vitapimwa kwa kupangwa kila halmashauri 25 ambapo kwa kila mwaka vitapimwa vijiji 1500,"alisema. Alisema kuwa zoezi la upimaji linaloendelea hivi sasa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM)kwa wananchi katika kuondoa migogoro inayojitokeza.

"Kazi hii ya upimaji wa maeneo katika kuhakikisha kunampango bora wa matumizi ya ardhi ni mpango wa nchi,ambapo serikali imechangua Mkoa wa Morogoro kuwa wa Mfano katika upimaji wa ardhi ambapo utahusisha nchi nzima,"alisema Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango na Matumizi ya Ardhi(NLUPC),Dkt.Stephen Nindi alisema ofisi yake inafanya kazi na wadau mbalimbali wa masuala ya ardhi zikiwepo wizara pamoja na mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali ikiwemo Shirika la Kimataifa la Care,Shirika la Oxfam,Chama cha Wafugaji Tanzania,Chuo kikuu cha Ardhi pamoja na Tamisemi.

Dkt.Nindi alisema kwa sasa kazi ya ya upimaji inafanywa na vifaa maalum vya kisasa vijulikanavyo kwa jina la Real Time Kinematic ambavyo vinafanya kazi kwa urahisi zaidi,licha ya vifaa hivyo kwa sasa vipo viwili nanvyakukodisha. "Tunahitaji kuwa na vifaa hivi walau vitano ambavyo vitatuwezesha kupima kwa wakati na kukaimilisha zoezi hili kwa haraka na kifaa kimoja kinagharimu kiasi cha sh.milioni 80,"alisema Dkt Nindi

Naye Mratibu wa Programu ya Ufugaji Asili kutoka Shirika la Kimataifa la Care,Marcely Madubi alisema suala la ardhi ni moja ya masuala muhimu yanayozingatiwa na shirika lao katika mikakati yao ya kimataifa. Alisema wadau mbalimbali nchini wanatakiwa kujitokeza kwa wingi katika kuchangia suala hili la kuhakikisha upimaji wa ardhi unafanikiwa hususani katika kuchangia ununuzi wa vifaa vya teknolojia mpya ya upimaji(Real Time Kinematic)ili kuwezesha upimaji wa ardhi kwenda kwa haraka zaidi na kupunguza migogoro inayoendelea kujitokeza.

DODOMA: MATUKIO BUNGENI.

$
0
0
 Spika wa Bunge la Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiingia katika ukumbi wa Bunge kuongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja ambapo pia alisema kiasi cha shilingi milioni themanini na tano na laki tano zimechangwa kutokana na makato ya posho ya siku moja yawabunge kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
 Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akimueleza jambo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira, Vijana na watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (MB) picha juu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo (MB) akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali itaendelea kupeleka fedha katika serikali za mitaa kwa kuzingatia hali ya makusanyo ya kila mwezi.
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akijibu swali bungeni ambapo alitoa wito kwa wabunge kuisaidia kutoa elimu kwa wananchi waliovamia maeneo ya jeshi kuondoka ili kusaidia kupunguza migogoro ya ardhi baina ya jeshi na wananchi, wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akijibu swali bungeni ambapo alisisitiza kuwa Serikali inatekeleza program ya maendeleo ya Sekta ya maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo, wakati wa kikao cha saba cha Bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Jumanne Maghembe (MB) akimueleza jambo Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angelina Mabula (MB), wakati wa kikao cha saba cha Bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Joseph Haule akiuliza swali bungeni kutaka kujua mikakati ya serikali katika kutatua migogoro baina ya wakulima na wafugaji inayopelekea mauaji ya raia ambapo Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi alisema Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanaohusika na mauaji ya raia nchini hasa ikiwemo wanaohusika kwenye migogoro hii.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.

Jokate awaomba Watanzania kuchangia wahanga wa tetemeko Kagera

$
0
0
Mrembo, msanii wa filamu na mwanamuziki, Jokate Mwegelo ametoa wito kwa jamii, mashirika na watu binfasi kujitolea kusaidia wahanga wa tetemeko la Ardhi lililoikumba mkoa wa Kagera na kusababisha vifo na baadhi ya watu kukosa makazi ya kuishi.

Jokate alitoa wito huo jana wakati wa kutangaza mikakati yake ya kusaidia wahanga wa tetemeko hilo kwa kushirikiana na Taasisi ya GSM Foundation. Alisema kuwa tikio hilo ni kubwa na lemeleta majonzi kwa baadhi ya familia na kuwaomba wadau kuungana kusaidia kuondoa changamoto zinazowakumba wahanga.

Alisema kuwa wakati anajipanga chini ya msaada wa GSM Foundation, ameamua kutoa rai kwa watanzania ikiwa pamoja na wanamichezo, wasanii, wanamuziki na wadau wengine mbalimbali kuchangia ili kuondoa changamoto hizo.

“Kwa kweli hali si nzuri kabisa, mimi kama msanii na ni Mtanzania, nimeguswa na kuamua kuingia mtaani kuhamasisha watu binafsi, makampuni na asasi mbalimbali kuunga mkono juhudi za serikali kusaidia wahanga wa tetemeko hilo,” alisema Jokate.

Alisema kuwa ni jukumu la kila Mtanzania kuungana katika tatizo hilo ambalo pia limeharibu baadhi ya shule na kusababisha wanafunzi kukosa sehemu ya kupata elimu. “Kwa wasanii, warembo na wanamuziki, ni wakati muafaka sasa kusaidia na kufanya mrejesho wa mapato yetu kwa jamii kwa kusaidia wahanga,” alisema.

Alifafanua kuwa suala hili si kwa watu wenye uwezo,tu, bali hata watu wenye kipato kidogo linawahusu kwani chochote walichonacho kama nguo, vyombo vya nyumbani, vitanda, magodoro, chakula, sabuni, mafuta na vitu vingine vinahitajika kwa wahanga wa tetemeko hilo.
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live




Latest Images