Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

WANACHAMA WA CUF KUPIGA HODI KWA IGP MANGU ENDAPO ATAENDELEA KUKIFUATILIA CHAMA HICHO

$
0
0


Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul (wa nne kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf. Wengine ni maofisa mbalimbali wa chama hicho.
Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, Shaweji Mketo, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam , wakati wa kutoa msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Ulinzi Taifa, Mustafa Wandu na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul.


Na Dotto Mwaibale

MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Chama cha Wananchi (CUF) Shaweji Mketo amesema iwapo Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu ataendelea kukifuatilia chama hicho wanachama wa chama hicho watekwenda ofisini kwake kumsalimia.

Mketo ameyasema hayo Makao Makuu ya Chama hicho Buguruni leo Dar es Salaam leo wakati Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul alipo kuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf.

“Tunasema sisi Cuf hatumuogopi IGP na kama ataendelea kutufuatafuata haita pita wiki mbili tutamfuata kwenda kumsalimia ofisi kwake” alisema Mketo. Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul

alisema chama hicho kimesikitishwa na kauli ya IGP aliyoitoa hivi karibuni wakati akihojiwa Tido Mhando wa Kituo cha Televisheni cha Azzam kuwa jeshi hilo wakati wowote litamkamata Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad kwa kuwachochea wafuasi wake ili waichukie serikali iliyopo madarakani.

Alisema baada ya kuitafakari kauli hiyo ya IGP wamebaini kwamba hivi sasa IGP Mangu ameamua kuwathibitishia watanzania kuwa jeshi la polisi ni idara maalumu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mazrul alisema kwa muda mrefu IGP Mangu amekuwa akilitumia jeshi la polisi kushiriki katika matukio mbalimbali ya kuhujumu demokrasia na kukiuka haki za binadamu kwa lengo la kukinusuru Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana na anguko kubwa la kukataliwa na wananchi kama ilivyothibitika kabnla na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana.

Alisema jeshi la polisi limekuwa na utaratibu wa kukamata raia, kuwapiga kuwabambikia kesi, kuwashikilia na kuwatesa katika vituo vya polisi bila ya kuwafikisha mahakamani.

Mazrul alisema hadi sasa zaidi ya wananchi 400 wameathiriwa kutokana na hujuma za jeshi la polisi kwa kuwabambikia kesi.

Programu za vyuo vikuu ambazo hazijasajiliwa na TCU na NACTE kufutwa

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Bi. Maimuna Tarishi ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) kufuta programu zinazotolewa na vyuo vikuu hapa nchini ambazo hazijafanyiwa tathmini wala kusajilwa.Katibu Mkuu huyo ameyasema hayo leo alipokuwa akifunga maonyesho ya kumi na moja ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia yaliyoanza Julai 20 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

“Wakati mwingine najiuliza inakuwaje chuo kinafundisha programu ambayo haijatathminiwa wala kusajiliwa na TCU au NACTE, ni lazima tuwe makini kwani tunahitaji elimu bora katika vyuo vyote nchini bila kuangalia kama ni cha Serikali au ni Binafsi,” alifafanua Bi. Tarishi.

Aliendelea kwa kusema kuwa, TCU na NACTE wanajukumu ya kuzifuta programu hizo na kuanzisha programu zenye uhitaji mkubwa kama vile shahada ya mafuta na gesi, Kompyuta na Ualimu wa Sayansi ambapo wataalamu katika maeneo hayo wamekuwa wakihitajika zaidi katika kipindi hiki ambacho Serikali ya Awamu ya Tano inajikita zaidi katika uanzishwaji wa viwanda.

Aidha Bi. Tarishi amewataka TCU na NACTE kudahili wanafunzi wenye vigezo vinavyohitajika na kusisitiza kuwa ni bora kuwa na wanafunzi wachache katika vyuo vikuu kuliko kuwa na wanafunzi wengi ambao hawana sifa.Wakati huo huo Mkuu wa Kitivo cha Biashara Chuo Kikuu cha Zanzibar Salehe Mwinyi amesema kuwa wanafunzi wengi wamejitokeza kutembelea banda la Chuo hicho kutaka kujua pogramu zinazotolewa na wengi wao wameonyesha nia ya kujiunga katika Chuo hiko.

Vile vile Mwinyi amesema kuwa mwaka huu idadi ya wanafunzi waliotembelea maonyesho hayo ni wengi zaidi kutokana na eneo lililochaguliwa kufikika kwa urahisi kutoka pande zote za jiji la Dar es Salaam ukilinganisha na mwaka jana ambapo yalifanyika viwanja vya Saba Saba na kutembelewa na idadi ndogo ya wanafunzi na wazazi.Kwa upande wake, Fadia Suleiman mwanafunzi anayetegemea kujiunga na Chuo Kikuu mwaka huu, amesema kuwa maonyesho hayo yamemsaidia kwa kiasi kikubwa kujua ni programu gani asome kutokana na ufaulu wake wa kidato sita.

Maonyesho ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia ambayo huandaliwa na TCU hufanyika kila mwaka yakitoa fursa kwa Vyuo Vikuu vya ndani na nje ya nchi kutoa elimu kwa wazazi na wanafunzi wanaotegemea kujiunga na vyuo vikuu kwa mwaka husika juu ya programu zinazotolewa na vyuo hivyo pamoja na kutoa ushauri ni programu gani mwanafunzi asome kwa kuangalia ufaulu wake.

Mh.Jenista Mhagama na Mh.Jordan Rugimbana waongelea maandalizi kuelekea Maadhimisho ya siku ya Mashujaa Mjini Dodoma

JK KUKABIDHI KIJIKI LEO KWA DKT JOHN POMBE MAGUFULI

$
0
0
 Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete,akifafanua jambo wakati akisoma hotuba yake ya Mwisho katika kiti hicho.PICHA NA MICHUZI JR -DODOMA.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma hotuba yake fupi mbele ya Wajumbe na kumkaribisha Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa ratiba na miongozo mbalimbali kwa Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao tayari wako ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.
Sehemu ya Meza kuu kama ionekanavyo pichani tayari wamekwisha ingia ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.Pichani kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete,Makamu Mwenyekiti Zanzibar Rais Dkt Shein pamoja na Mwenyekiiti mtarajiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
 Baadhi ya Viongozi wakuu wa Wastaafu wa chama cha CCM na Serikali kwa ujumla wakifuatilia yanayojili ukumbini .
 Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikisomwa na Mwenyekiti ambaye leo anaachia kiti hicho na kukabidhi kwa Mwenyekiti mpya Dkt John Pombe Magufuli,katika mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaofanyika ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC),mkoani Dodoma.
Mwanana mahiri wa nyimbo za Taarab kutoka kundi la Tot Plus Khadija Kopa akiimba mbele ya Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao tayari wako ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.
Baadhi ya wageni waalikwa kutoka vyama mbalimbali vya upinzani pia wanahudhuria mkutano huu Maalum wa CCM.Ambapo vyama vya siasa vipatavyo 12 vilialikwa na vyote vimefika katika mkutano huo isipokuwa chama cha CHADEMA.
Baadhi ya Wageni waalikwa wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa ndani ya ukumbi ambapo leo mkutano Mkuu Maalum wa CCM unafanyika kwa ajili ya kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka kumi,Rais John Pombe Magufuli anatarajiwa kukabidhiwa kijiti hicho kutoka kwa Mwenyekiti ambaye anamaliza muda wake leo, Rais Mstaafu wa awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete,mkutano huo unafanyika ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) ulioko nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Baadhi ya Wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali wakiwa ndani ya ukumbi ambapo leo mkutano Mkuu Maalum wa CCM unafanyika kwa ajili ya kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka kumi,Rais John Pombe Magufuli anatarajiwa kukabidhiwa kijiti hicho kutoka kwa Mwenyekiti ambaye anamaliza muda wake leo, Rais Mstaafu wa awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete,mkutano huo unafanyika ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) ulioko nje kidogo ya mji wa Dodoma.

Angalia Kipindi Chote Cha ' Nyumbani Na Diaspora' TBC1

Serikali yasisitiza matumizi ya bidhaa za ndani.

$
0
0



Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Uledi Mussa akiongea na wadau mbalimbali wa uchumi nchini hawapo pichani wakati wa kufunga mkutano wa mwaka wa mashauriano ya ushiriki wa watanzania Katika uwekezaji uliofayika jijini Dar es salaam.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la uwezeshaji Wananchi Kiuchumi(NEEC) Bi. Beng’i Issa akiongea na wadau mbalimbali wa uchumi nchini hawapo pichani wakati wa kufunga mkutano wa mwaka wa mashauriano ya ushiriki wa watanzania Katika uwekezaji uliofayika jijini Dar es salaam.
Mdau wa Uchumi nchini na Mkurugenzi wa taasisi binafsi inayojihusisha na biashara Namaingo Business Agency Bi. Biubwa Ibrahim akichangia hoja wakati wa kufunga mkutano wa mwaka wa mashauriano ya ushiriki wa watanzania Katika uwekezaji uliofayika jijini Dar es salaam.
Mdau wa Uchumi nchini na Mkurugenzi wa Mfuko wa Bima (NIC) Bw. Sam Kamanga akichangia hoja wakati wa kufunga mkutano wa mwaka wa mashauriano ya ushiriki wa watanzania Katika uwekezaji uliofayika jijini Dar es salaam.
wadau mbalimbali wa uchumi nchini wakifuatilia kwa makini majadiliano ya wachngiaji mada wakati wa kufunga mkutano wa mwaka wa mashauriano ya ushiriki wa watanzania Katika uwekezaji uliofayika jijini Dar es salaam.


Na Ally Daud-Maelezo

Serikali imesisitiza matumizi ya bidhaa za ndani ya nchi zinazotengenezwa na watanzania ili kukuza uchumi wa nchi na kupanua ukubwa wa masoko ili kuleta maendeleo.

Akizungumza hayo wakati wa kufunga mkutano wa mwaka wa mashauriano ya ushiriki wa watanzania Katika uwekezaji Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Uledi Mussa amesema kuwa watanzania wajifunze kupenda na kutumia bidhaa za ndani ili kuweza kuinua nchi kiuchumi kwa maendeleo ya Taifa letu.

“Ni lazima watanzania tujifunze kubadilika kifikra na kimtazamo katika kutumia bidhaa zilizopo nchini kuchangia Katika kukuza uchumi wa nchi yetu ili kupiga hatua Katika maendeleo ya Tanzania”alisisitiza Bw.Uledi.

Aidha Bw. Uledi amesema kuwa mwekezaji yeyote awe wa ndani au wa kigeni anapaswa kutumia wafanyakazi wa nchini kama kama anataka kuwekeza Katika Taifa letu ili kutoa fursa kwa watanzania kushiriki Katika kuinua uchumi.

“Mwekezaji wa kigeni au wa ndani inampasa atumie wataalamu na wafanyakazi wa Tanzania kama anataka kuwekeza nchini mwetu ili vijana wetu wa kitanzania wapate fursa ya kuchangia Katika kuinua uchumi wa nchi”.aliongza Bw. Uledi.

Mbali na hayo Bw. Uledi Mussa amesema kuwa kiwanda chochote kinachowekeza nchini wanapaswa kutumia malighafi kutoka Tanzania ili kuweza kupiga hatua kimaendeleo Katika Taifa letu kwa ujumla.

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la uwezeshaji Wananchi Kiuchumi(NEEC) Bi. Beng’i Issa amesema kuwa Katika mkutano huo wenye kauli mbiu ya “Ongeza Ushiriki Inua Uchumi” umetoka na mkakati wa kuhakikisha makampuni yote ya uwekezaji kutoka nje yajiandikishe Katika soko la Hisa (DSE) ili kuongeza ushirikina umiliki wa watanzania Katika makampuni husika.

Aidha bi. Issa ameongeza kuwa mkutano huo umelenga kuwa wakandarasi wote ambao wa ndani wanapewa malipo yao kwa wakati kama walivyokubaliana ili kumsaidia mtanzania kushiriki Katika kukuza uchumi wa nchi.

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII, ENG. RAMO MAKANI ATEKELEZA AHADI YA SERIKALI ALIYOITOA BUNGENI YA KUTEMBELEA ENEO LA MGOGORO WA HIFADHI YA MSITU WA SAYAKA MKOANI MWANZA

$
0
0
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (wa pili kulia) akikagua eneo la mpaka katika Msitu wa Hifadhi wa Sayaka katika Kijiji cha Bugatu, Wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza hivi karibuni. Anayeongoza utambuzi wa mpaka huo ni Afisa Misitu na Nyuki TFS Wilaya ya Magu, Ayoub Mikae (wa tatu kulia). Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Magu, Boniventure Kiswaga.  Eng. Makani aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini kwa ajili ya kutafutiwa suluhu ya kudumu. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (wa sita kushoto) akiwa na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Magu na baadhi ya Wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Msitu wa Sayaka wakikagua mpaka wa hifadhi hiyo hivi karibuni. Kinachoonekana mbele yao ni Kigingi cha mpaka kinachodaiwa kusogezwa mbele na wananchi wa maeneo hayo kwa ajili ya kumega eneo la Hifadhi. 
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia) akizungumza na wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Msitu wa Sayaka katika Kijiji cha Bugatu Wilayani Magu Mkoani Mwanza hivi karibuni. Aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini na kutafutiwa suluhu ya kudumu. 
Naibu Waziri Maliasili , Eng. Ramo Makani (kulia) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Bugatu, Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza hivi karibuni wakati akikagua ramani ya Hifadhi ya Msitu wa Sayaka kubaini maeneo ya mpaka yenye mgogoro. Eng. Makani aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini kwa ajili ya kutafutiwa suluhu ya kudumu
Mbunge wa Jimbo la Magu, Boniventure Kiswaga (kulia) akizungumza na wananchi wa Jimbo lake katika Kijiji cha Bugatu Wilayani Magu hivi karibuni.
Mwananchi wa Kijiji cha Salama kilichopo kandokando ya Hifadhi ya Msitu wa Sayaka Wilayani Magu, Charles Kassandiga (kushoto) akitoa ombi kwa niaba ya wananchi wa kijiji hicho la kupatiwa maeneo ya kulima na kufuga kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia). Eng. Makani aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini na kutafutiwa suluhu ya kudumu. 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kushoto) akiongoza kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama cha Wilaya ya Magu alipotembelea Wilayani humo hivi karibuni kuona eneo la mgogoro katika Hifadhi ya Msitu wa Sayaka ambapo aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini na kutafutiwa suluhu ya kudumu.

NA HAMZA TEMBA - WMU
_____________________________________
Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imeahidi kupitia upya maeneo yote ya Hifadhi nchini yenye migogoro ya ardhi kwa ajili ya kuyatafutia suluhu ya kudumu kwa kutumia mbinu shirikishi.


Hayo yamesemwa jana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Eng. Ramo Makani wakati akizungumza na Wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Msitu wa Sayaka katika Kijiji cha Busega Wilayani Magu Mkoani Mwanza.


Eng. Makani alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano imekusudia kubadilisha mfumo wa utendaji Serikali ambapo kwenye utatuzi wa migogoro iliyopo kwenye maeneo ya hifadhi nchini itatatuliwa kwa kuwashirikisha wananchi wa maeneo husika na kuweka kumbukumbu sahihi za makubaliano kufikia suluhu ya kudumu.


“Maeneo yote yenye migogoro tunaenda kuyapitia upya, tukija kwenye utatuzi tutawashirikisha wananchi kupitia Serikali zao za Vijiji ambazo wajumbe wake watahusika kwenye makubaliano kwa kuzingatia umuhimu na faida za Uhifadhi lakini huku tukihakikisha tunajibu kero zinazowakabili” Aliesema Eng. Makani.


Aliongeza kuwa wakati wa kutatua migogoro hiyo yataainishwa maeneo kwa ajili ya shughuli za ufugaji na kilimo kuepusha muingiliano kati ya wakulima na wafugaji pamoja na kuepusha uvamizi kwenye maeneo ya Hifadhi yaliyoainishwa, utaratibu huo utazingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali ya Serikali.


Awali akizungumzia mgogoro wa Hifadhi ya Msitu wa Sayaka, Eng. Makani alisema kuwa, uamuzi wa kufika katika eneo hilo la mgogoro ni kuona uhalisia kabla ya kuchukuliwa hatua za kumaliza mgogoro huo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Serikali aliyoitoa bungeni hivi karibuni kwa Mbunge wa Jimbo la Magu, Boniventure Kiswaga.


Katika mgogoro huo wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi hiyo walitoa malalamiko yao kwa Naibu Waziri Makani kuwa maofisa wa TFS wamekuwa wakisogeza vigingi vya mpaka wa eneo hilo kumega maeneo ya vijiji bila kuwashirikisha. “Sio kwamba tunapinga Uhifadhi, lakini tunauliza kwanini vigingi vinahama kila mwaka kusogelea maeneo yetu” Alihoji Mwanyekiti wa Kijiji cha Bugatu, Charles Kusenza.


Akijibu malalamiko hayo Afisa Misitu na Nyuki wa TFS Wilaya ya Magu, Ayoub Mikae alisema kuwa, kilichokuwa kinafanyika sio kusogeza vigingi bali na kuimarisha vigingi vilivyokuwepo ambapo utambuzi wake ulifanyika kitaalam kwa kutumia GPS. Aliongeza kuwa baadhi ya wananchi wasio waadilifu walidaiwa kusogeza vigingi vya mpaka wa Hifadhi hiyo ili wapate eneo la kulima jambo lililoleta taswira tofauti wakati wa kufanya marekebisho sahihi kwa kutumia mtambo wa GPS uliosaidia kubaini mpaka asilia.


Ayoub alisema kuwa sababu ya kuanzishwa kwa Hifadhi ya Msitu Sayaka ilikuwa ni kuhifadhi uoto wa asili, kutunza vyanzo vya maji na kuhifadhi samaki wa Ziwa Victoria kwa kuwa mto uliopo katika hifadhi hiyo unapeleka maji Ziwa Victoria.


Baada ya kusikiliza hoja mbalimbali za wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi hiyo katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Bugatu, Eng. Makani alisema kuwa tatizo kubwa aliloliona katika mgogoro huo ni changamoto za Uhifadhi ikiwemo uelewa hafifu wa baadhi ya wananchi juu ya umuhimu wa uhifadhi, ushirikishwaji hafifu wa wananchi kwenye uwekaji wa vigingi na baadhi ya wananchi kuchanganya vigingi vya hifadhi ya maji na hifadhi ya Msitu, changamoto ambazo alisema zitazingatiwa kwa kina wakati wa utatuzi wa mgogoro huo.


Alisema kuwa “Tunahitaji uhifadhi endelevu, peke yetu bila wananchi hatuwezi, tunahitaji uhifadhi rafiki, tukiwa na uelewa wa pamoja juu ya umuhimu wa uhifadhi na tukajibu kero zenu mtatusaidia kulinda na kuhifadhi Maliasili zetu”. 

Kwa upande wa Wananchi wa vijiji vinavyozunguka hifadhi hiyo waliopewa fursa ya kuchangia na kuuliza maswali kwenye mkutano huo walipaza sauti zao kuiomba Serikali kupitia Naibu Waziri huyo kuwasaidia maeneo ya kufuga na kulima kutokana na ufinyu wa maeneo uliosababishwa na ongezeko kubwa la watu. Naibu Waziri Makani Aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi nchini yenye migogoro na kuyatafutiwa suluhu ya kudumu kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo mbalimbali ya Serikali.

JK AKABIDHI RASMI KIJITI CHA UENYEKITI KWA DKT JOHN POMBE MAGUFULI JIONI YA LEO MJINI DODOMA

$
0
0
 Mwenyekiti aliyemaliza Muda wake Dkt Jakaya Kikwete pamoja na Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt John Pombe Magufuli wakiwapungia mkono Wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum mara baada ya matokeo kutangazwa rasmi na Dkt John Pombe Magufuli kuibuka kwa kura zote za ndio ziapatazo 2398 na hakuna kura zilizokuwa zimeharika.
Mwenyekiti Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete akimkumbatia Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli mara baada ya kutangazwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka kumi.
  Mwenyekiti aliyemaliza muda wake leo,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete akimkabidhi vitendea kazi mbalimbali vya chama cha Mapinduzi (CCM),Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli aliyepigiwa kura na Wajumbe wa Mkutano Mkuu maalum na kuibuka na kura zote za ndio kutoka kwa Wajumbe 2398 na hakuna kura zilizokuwa zimeharika
 Makamu Mwenyekiti-Zanzibar Dkt Shein akimpongeza Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka 10,pichani katia anaeshuhudia ni Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Jakaya Kikwete 
  Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrhamani Kinana akimpongeza Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka 10.

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu,Mh William Mkapa akimpongeza Mwenyekiti Mpya,Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho kwa miaka 10.
 Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi CCM Dkt John Pombe Magufuli akihutubia mbele ya Wajumbe wa Mkutano mkuu Maalum wa chama cha CCM mara baada ya kutangazwa rasmi kuwa Mwenyekiti wa chama hicho .


makabidhiano ya halmashauri kwa wakurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

$
0
0
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa (Kulia) Ndg Twalib A. Mbasha akitoa  hati ya makabidhiano ya Wilaya kwa Mkurugenzi wa sasa wa Halmashauri hiyo Ndg Zabron I. Bugingo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg Zabron I. Bugingo (Kushoto) akipata Picha ya pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hio Ndg Twalib A. Mbasha. Katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri Bwana Abubakar Mussa Mjaka.
Picha ya pamoja ya aliyekuwa Mkurugenzi na Mkurugenzi wa sasa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Pamoja nawakuu wa Idara/Wataalamu wa Halmashauri. Nyuma waliosimama wa katikati ni Mwenyekiti wa Halmashauri mwenye T-shirt. Picha na Bernad Mpangala.(Mchambuzi wa Mifumo Kilwa (W).

MGANA MSINDAI ALIYEKUWA CHADEMA AMWAGA YAKE YA MOYONI MKUTANO MKUU WA CCM LEO MJINI DODOMA

BENKI YA CRDB YAKABIDHI TIKETI ZA NDEGE KWA WASHINDI WA KAMPENI YA 'SHINDA NA TEMBOCARD

$
0
0
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kulia), akimkabidhi tiketi ya ndege ya kwenda Dubai mshindi wa kampeni ya ‘Shinda na TemboCard’, Juliana Utamwa katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaa.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto), akimkabidhi tiketi ya ndege ya kwenda Dubai, Dorisia Nanage ambaye ataambatana na mshindi wa kwanza, Juliana Utamwa.

Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (katikati), akifafanua jambo wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi ya tiketi ya ndege ya kwenda Dubai kwa mshindi wa kampeni ya ‘Shinda na TemboCard’, Juliana Utamwa (kushoto) katika hafla iliyofanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaama, mwishoni mwa wiki. Kulia ni Dorisia Nanage ambaye ni ndugu yake atakayeambatana naye.

Baadhi ya maofisa wa Benki ya CRDB wakiwa katika hafla hiyo iliyofanyika makao makuu ya benki ya CRDB.
Wafanyakazi wa benki ya CRDB wakishuhudia tukio hilo.
Mshindi wa Kampeni ya 'Shinda na TemboCard', Juliana Utamwa akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tiketi ya ndege ya kwenda Dubai na Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (kushoto), katika hafla ya makabidhiano ya zawadi kwa washindi wa kampeni hiyo iliyofanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
Maofisa wa benki ya CRDB wakishuhudia tukio la kukabidhi tiketi kwa washindi wa Kampeni ya 'Shinda na TemboCard'
Maofisa wa benki ya CRDB wakiwa katika hafla hiyo.

Ntahakikisha Serikali inahamia Dodoma :Rais Magufuli

$
0
0
Na. Immaculate Makilika- Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amesema katika kipindi cha uongozi wake atahakikisha Serikali inahamishia makazi yake mjini Dodoma.

Amesema hayo leo, wakati alipokuwa akihutubia wajumbe wa Chama cha Mapinduzi(CCM) katika Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama hicho uliofanyika mjini Dodoma mara baada ya kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti.

“Nitahakikisha katika awamu ya uongozi wangu, Serikali inahamia Dodoma, najua viongozi wengine wote nao watanifata, kwa kuwa sasa miundombinu ya Dodoma inaweza kukidhi mahitaji yote” alisema Rais Magufuli.Rais Magufuli aliendelea kusema kuwa katika kipindi cha miezi nane ya uongozi wake chini ya Serikali ya Awamu ya Tano ameweza kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuanza kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Akiongelea maeneo ya utekelezaji katika kipindi chake Dkt. Magufuli alisema kuwa mpaka sasa Serikali imefanikiwa kusimamia suala la utoaji wa elimu bure kwa shule za Msingi na Sekondari nchini na kuwezesha udahili kuongezeka zaidi tofauti na miaka iliyopita.

Aidha Dkt. Magufuli alisema kuwa Serikali yake pia imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika ukusanyaji wa mapato ya serikali hali itakayosaidia kuimarisha utoaji wa huduma muhimu za jamii.Aidha, Serikali ya Awamu ya Tano imeagiza ndege mbili mpya zinazotarajiwa kuwasili nchini Septemba mwaka huu,

Rais Dkt. Magufuli aliongeza kuwa Serikali yake kwa kushirikiana na Serikali ya Uganda wamefanikiwa kujenga bomba la kusafirisha mafuta kutoka Hoima katika ziwa Alberti nchini Uganda kwenda bandari ya Tanga ambapo mafuta hayo yatasafirishwa sehemu mbalimbali duniani na bombahilo litazalisha zaidi ya ajira 20,000.

Vile vile, Rais Magufuli alisema kuwa Serikali yake imeweza kurudisha nidhamu ya kazi kwa watumishi wa umma na kuweza kuondoa watumishi hewa waliokuwa na waliokuwa wamefikia 12,500,na kuongeza kuwa kwa mwaka huu Serikali imetenga fedha za matumizi jumla ya shilingi trilioni 29.5, ambapo asilimia 40 ya fedha hizo zitapelekwa katika kutekeleza shughuli za maendeleo.

Mkutano Mkuu Maalum wa CCM ulihudhuriwa na wajumbe zaidi 2,000 ulimpitisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa mshindi na Mwenyekiti wa Chama hicho kwa kura 2398 kati ya kura 2398 zilizopigwa ikiwa ni sawa na asilimia 100.

Rais Magufuli anakuwa Mwenyekiti wa awamu ya Tano baada ya kupokea uongozi huo kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama hicho anayemaliza muda wake Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka 10.

WANARIADHA JWTZ WAMUAHIDI MKUU WA MAJESHI MEDALIJI

$
0
0

Wanariadha wa Timu Teule ya JWTZ wakifanya mazoezi katika Kambi iliyoko Mbulu Mkoani Manyara ikiwa ni Sehemu ya Maandalizi mashindano ya Afrika mashariki yanayotarajiwa kufanyika Kigali Nchini Rwanda mapema Agosti Mwaka huu (Picha na Selemani Semunyu).
Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa JWTZ Brigedia Jenerali Martin Busungu akizungumza na Wanariadha wanaojiandaa na mashindano ya Afrika Mashariki alipowatembelea katika kambi ya Timu Teule ya Riadha iliyoko Mbulu Mkoani Manyara (Picha na Selemani Semunyu).
Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa JWTZ Brigedia Jenerali Martin Busungu akisalimiana na Mwanariadha Jackline Sakilo mara baada ya kutembelea katika kambi ya Timu Teule ya Riadha inayojiandaa na mashindano ya Afrika mashariki iliyoko Mbulu Mkoani Manyara (Picha na Selemani Semunyu).
Wanariadha wa Timu Teule ya JWTZ wakifanya mazoezi ya Viungo katika Kambi iliyoko Mbulu Mkoani Manyara ikiwa ni Sehemu ya Maandalizi mashindano ya Afrika mashariki yanayotarajiwa kufanyika Kigali Nchini Rwanda mapema Agosti Mwaka huu (Picha na Selemani Semunyu).

 
Na Selemani Semunyu JWTZ .

Wanariadha wa Timu Teule ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania JWTZ imemuahidi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange kurejesha heshima katika Michezo kwa kuleta medali nyingi kutoka Rwanda. 

Hayo yamesemwa Mwishoni mwa Wiki na Wanariadha hao wakati walipotembelewa na Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili wa JWTZ Brigedia Jenerali Martin Busungu katika kambi yiliyowekwa Katika eneo la Sanu Baray Wilayani Mbulu Mkoani Manyara. 

Walisema Maandalizi ya Safari hii kuelekea mashindano ya Afrika Mashariki yanayotarajia kufanyika Agosti Mwaka huu Nchini Rwanda ni Maandalizi ya kina ukizingatia Jeshi likiwa limewawezesha ipasavyo hivyo hawana sababu ya kukosa ushindi. 

Mmoja wa Wanariadha hao ni Jackline Sakilo ambaye ni mmoja wa wanariadha tishio alisema kambi imewekwa katika eneo ambalo lina hali ya hewa inaruhusu ambayo ni Futi 1980 kutoka usawa wa bahari hivyo Mkuu wa majeshi ajiande kupokea medali kutoka kwa Vijana wake . 

“ Mkuu wa majeshi ya Ulinzi lakini pia Rais na Amiri Jeshi Mkuu Afande Dk Magufuli wajiandae tu kupokea Medali kwa Niaba ya Watanzania kwani ndio tunakwenda kuwawakilisha watuombee ili ndoto zetu zitimie” Alisema Jackline. Kwa upande wake Mkurugenzi wa Michezo na Utimamu wa Mwili Brigedia Jenerali Busungu amewataka Wanariadha hao kutunza Morali yao na mabadiliko ya Umbali isiwe kigezo cha Kufanya Vibaya kwani yametokea dakika za Mwisho na ni Kwa Nchi zote. 

“Sasa Wanariadha wote watakimbia Kilometa 10 badala ya Kilometa Nane kwa wanawake na kilometa 12 kwa Wanaume kama ilivyozoeleka na kutangazwa Awali lakini kwa maandalizi haya ni matumaini yangu tutafanya vyema tu” Alisema Brigedia Jenerali Busungu. 

Aliongeza kuwa Jeshi linamategemeo kwa Wachezaji wote wa Timu teule za Jeshi lakini pia Wananchi kwa ujumla wanategemea Timu yao itafanya vyema hivyo wanapaswa kupigana vilivyo kuibuka na ushindi kwa kila Mchezo. Brigedia Jenerali Busungu aliongeza kuwa amesikia ahadi ya wachezaji ya kupata ushindi na kuleta medali nyingi na kuwapongeza kwa ahadi hiyo na kutaka sasa ikafanyike kwa vitendo. 

Mashindano ya Majeshi kwa Nchi za Afrika Mashariki yanatarajiwa kufanyika Kigali Nchini Rwanda kuanzia Agosti Saba hadi Agosti 17 Mwaka huu Nchini Rwanda huku Tanzania katika Riadha itapeleka Wanariadha 12 Wanawake Sita na Wanaume Sita.

Wanafunzi watarajiwa chuo cha UDSM wafundwa juu ya maisha ya chuo

$
0
0
Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Amina Abdul ambaye pia ni Mratibu wa Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na wanahabari. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Amina Abdul ambaye pia ni Mratibu wa Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo akifafanua jambo alipokuwa akizungumza na wanahabari.Bi. Sadaka Gandi (mbele) mmoja wa wawasilishaji mada katika semina hiyo akizungumza jambo kwa baadhi ya wanahabari. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Bi. Sadaka Gandi (mbele) mmoja wa wawasilishaji mada katika semina hiyo akizungumza jambo kwa baadhi ya wanahabari. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.
Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo. Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo.

Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani. Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani. IMG_0336 Bi. Sadaka Gandi (mbele) mmoja wa wawasilishaji mada katika semina hiyo akizungumza jambo kwa baadhi ya wanahabari. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite (kushoto) akimkabidhi zawadi mmoja wa wanafunzi baada ya kujibu swali kiufasaha. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite (kushoto) akimkabidhi zawadi mmoja wa wanafunzi baada ya kujibu swali kiufasaha.Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuani. Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM wakifuatilia mada anuaniMeneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite (kulia mbele) akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washirikiMeneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Meneja wa Mafunzo na Maendeleo wa Benki ya NMB, Edith Mwiyombela (kulia) akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo wakiwa kwenye banda la mdhamini mkuu wa semina hiyo kujifunza shughuli mbalimbali wanazofanya. Baadhi ya washiriki wa Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo wakiwa kwenye banda la mdhamini mkuu wa semina hiyo kujifunza shughuli mbalimbali wanazofanyaMsanii nyota Nick Wa Pili akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM. Msanii nyota Nick Wa Pili akiwasilisha mada kwenye Semina kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB, pamoja na wadhamini wengine wakiwemo PSPF, Crown Cartilage, ACCA na Clouds FM.Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo. Mmoja wa wasilishaji mada kutoka Kampuni ya Bridge Tanzania Limited akiwaelekeza wanasemina namna nzuri ya kutumia baadhi ya vifaa vya 'printer' na matumizi mazuri ya wino wa mashine hizo.
Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki. Meneja Mwandamizi wa Benki ya NMB Kitengo cha Wateja Wadogo, Ally Ngingite akiwasilisha mada juu ya Matumizi Mazuri ya Fedha kwa washiriki.Mmoja wa waratibu wa semina hiyo akitoa mwongozo kwa washiriki. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB. Mmoja wa waratibu wa semina hiyo akitoa mwongozo kwa washiriki. Semina hiyo kwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na baadhi ya wanachuo iliandaliwa na Kampuni ya Bridge Tanzania Limited kwa kushirikiana na DUFA chini ya udhamini Mkuu wa Banki ya NMB.

Kwaheri JK, Karibu Magufuli: Uchambuzi wa kina kuhusu uchaguzi wa m/kiti wa CCM (T)

$
0
0
Jana Julai 23, 2016 Rais Dokta John Magufuli alichaguliwa kwa asilimia 100 kuwa Mwenyekiti mpya wa Taifa wa chama tawala CCM, na mtangulizi wake, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, kung'atuka rasmi. Ufuatao ni uchambuzi wa kina kuhusu mabadiliko hayo ya uongozi wa juu kabisa wa chama hicho kikongwe, hasa fursa na changamoto kwa Mwenyekiti mpya Magufuli. Karibuni
Check this out on Chirbit

Waliokuwa wanafunzi wa Bwawani Sekondari waikumbuka shule yao kwa kuitembelea

$
0
0

Baadhi ya wanafunzi tuliosoma Shule ya Sekondari Bwawani tukiwa katika picha ya pamoja wakati wa kuelekea kuitembelea shule yetu hiyo..
Mwalimu Leornad Chintowa akiwakaribisha baadhi ya wanafunzi waliopata kusoma katika shule ya Sekondari ya Bwawani inayomilikiwa na jeshi la Magereza nchini mara baada ya kuwasili kwa waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo mapema leo.
Baadhi ya waliokuwa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Bwawani iliyopo mkoa wa Pwani wakipata maelekezo kutoka Kwa viongozi wa wanafunzi kuhusiana na Maabara mpya iliyojengwa shule hapo kipindi ambacho waliokuwa wanafunzi katika shule hiyo hawakuiacha.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Bwawani wakipiga picha na aliyewahi kuwa mwanafunzi wa shule hiyo na kuhitimu mwaka 2004, Christopher Mwansasu mara baada ya waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo kutembelea shule yao kwaajili ya kuwatia moyo na amasa ya kusoma vijana wanaoendelea na masomo shule hapo
Baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma Shule ya Bwawani na kuishi katika Bweni la Nguvu Kazi wakiwa mbele ya bweni walilowahi kuishi miaka hiyo wakiwa shuleni hapo. Kutoka kulia ni Amosi Kilindo ambaye alihitimu kidato cha nne shuleni hao mwaka 2004 na anayefuata ni Peter Mloka ambaye alihitimu kidato cha Nne mwaka 2005.
Aliyewahi kuwa mchezaji wa netball wa timu ya shule ya Bwawani kuanzia mwaka 2003 hadi mwaka 2006, Maria Plantana akimkabidhi mchazaji wa netball wa timu ya shule ya bwawani Kwa sasa mpira wa Netball ikiwa kama zawadi ya kuwatembelea wanafunzi hao shuleni hapo.
Maelekezo yakiendelea kwa waliokuwa wanafunzi wa shule ya Bwawani iliyopo Mkoa wa Pwani.
Aliyekuwa Mwanafunzi wa Shule ya Bwawani, Salome Mathew akipanda Mti kama ishara ya kumbukumbu shule hapo mara baada ya kuwasili shuleni hapo kwaajili ya kuwatia moyo wanafunzi wanaoendelea na masomo
Kaka Mkuu msaidizi (Mwenye sare) akibadilishana mawazo na waliokuwa wanafunzi katika shule hiyo wakati walipotembelea shule hiyo kwaajili ya kuwatia moyo na amasa wanafunzi wanaoendelea na Masomo katika shule hiyo ya Bwawani inayomilikiwa na Jeshi la Magereza nchini Tanzania wanaoshuhudia Pembeni ni walimu wa shule hiyo
Baadhi ya wanafunzi wanaoendelea na masomo shule hapo wakiwa katika Picha ya Pamoja na walimu na baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika Shule hiyo ya Bwawani miaka kadhaa iliyopita.
Baadhi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza mpaka cha sita wakiwa katika bwalo la shule kwaajili ya kuwasikiliza waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo miaka kadhaa iliyopita ambao waliwatembelea na kuongea nao machache ikiwemo kuwapa moyo na kuwafanya waone umuhimu wa shule pindi wanapokuwa shuleni.
Baadhi ya wanafunzi waliowahi kusoma katika shule ya Bwawani iliyopo Mkoa wa Pwani wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kutembea sehemu mbalimbali za shule hiyo kujionea tofauti
Mmoja wa wanafunzi aliyehitimu mwaka 2006, Frank Mushi akipanda Mti mara baada ya kuwasilini shule hapo wakati wa ziara iliyofanya na wanafunzi waliohitimu katika shule ya bwawani huku baadhi ya wanafunzi hao waliowahi kusoma hapo wakitoa zawadi ya mipira kama vile mpira wa miguu, wavu na mpira wa pete, huku wakitoa Miche 30 ya miti ambayo imepandwa shule hapo kama ishara ya kumbukumbu kwa wanafunzi hao
Baadhi ya wanafunzi waliosoma na kuhitimu katika shule ya Sekondari Bwawani iliyopo Mkoani Wa Pwani wakiepelekwa kujionea ujenzi wa majengo mbalimbali yanayoendelea kujengwa shule hapo yakiwemo mabweni ya wanafunzi.Picha zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog


Na Josephat Lukaza - Bwawani

Hatimaye waliowahi kusoma na kuhitimu katika Shule ya Sekondari ya Bwawani iliyopo Mkoa wa Pwani wamefanikisha adhma yao ya kuitembelea iliyokuwa shule yao kwaajili ya Kuwatia moyo na amasa vijana wanaoendelea na masomo katika shule hiyo huku wengi wao wakiwa ni vijana wa kidato cha Kwanza hadi cha Nne.

Waliowahi kuwa wanafunzi hao waliwasili majira ya saa sita mchana na kupokelewa na waliokuwa walimu wao kipindi hiko wakiwa wanasoma shule hapo na kupata nafasi ya kuonyeshwa sehemu mbalimbali za shule hiyo huku waliokuwa wanafunzi katika shule wakipata nafasi pia ya Kuzungumza machache na wanafunzi wanaoendelea na masomo katika shule hiyo na kuweza kuwasaidia vifaa vya michezo kama mipira huku wakipanda miti kwaajili ya kumbukumbu.

Waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Magereza nchini waliweza kutoa miche 30 ya miti kwaajili ya kupandwa shule hapo huku wanafunzi wakishukuru kwa kupokea mipira kama zawadi kutoka kwa kaka na dada zao waliotangulia shuleni hapo.

Akizungumza na waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo Kaka Mkuu msaidizi alisema "Kwa niaba ya wanafunzi wenzangu napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru kaka na dada zetu ambao mliweza kusoma hapa na kuamua kuja kutusalimia na kututia moyo, Kiukweli tumefarijika sana na tunaomba muendelea kuja shule hapa muda wowote ule kwa maana tumejisikia faraja sana kuwaona na vilevile tunapenda kushukuru kwa kutuletea Zawadi ya Mipira hii, tunasema asanteni sana"

Mara baada ya waliokuwa wanafunzi wa shule hiyo kutembelea sehemu mbalimbali za shule na kuzungumza na wanafunzi wa shuleni hapo waliweza kupata chakula cha mchana na waliokuwa walimu wao kipindi wanasoma na kuweza kubadilishana mawazo huku walimu wakishukuru sana na kusema wamefurahi sana kuwaona wanafunzi hao kwa maana ni miaka mingi sana imepita tokea wengi wao wahitimu masomo yao hapo shule.

Shule ya sekondari ya Bwawani ilikua ikiitwa Ubena kabla ya kubadilishwa jina na Kuitwa Bwawani kutokana na mantiki ya kuwa shule ya kufundisha raia peke yao ambapo awali ilikuwa ni shule kwaajili ya kuendeleza elimu kwa askari wake wa jeshi la magereza, Mnamo mwaka 2002 jina lilibadilika kutoka Shule ya Sekondari Ubena na kuitwa Bwawani ambapo sasa ilianza kupokea wanafunzi raia ambao kwa mara ya kwanza usajili wa wanafunzi raia ulianza mwaka 2001. Katika kipindi hiko shule ya Bwawani ilikuwa ni shule yenye Kidato cha Kwanza mpaka Cha nne ambapo sasa shule hiyo ina kidato cha Tano na cha sita.

BANCABC YAIWEZESHA BoT KUNUNUA NYUMBA ZA NHC MTWARA

$
0
0

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akimkabidhi ufunguo
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania- B0T Prof. Benno Ndulu

Gavana wa Benki kuu ya Tanzania- BoT Prof. Benno Ndulu akimsikiliza mkurugenzi wa masoko kitengo cha makampuni makubwa wa Bancabc Khilifa Zidadu wakati wa uzinduzi wa nyumba za BoT Mtwara na kushoto kwa gavana ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu.
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania- BoT Prof. Benno Ndulu akifafanua jambo kuhusina na ununuzi wa nyumba kwa ajili ya wafanyakazi wa benki hiyo mkoani mtwara, kulia kwa gavana ni mkurugenzi wa masoko kitengo cha makumpuni makubwa wa Bancabc Khalifa Zidadu na kushoto kwa gavana ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu. Gavana wa Benki kuu ya Tanzania- BoT Prof. Benno Ndulu akibadilishana mawazo na mkurugenzi wa masoko kitengo cha makampuni makubwa wa Bancabc Khalifa Zidadu wa pili kushoto na Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu. aliyevaa fulana.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu akitoa maelezo ya kukamilika kwa mradi wa nyumba kwa ajili ya wafanyakazi wa benki kuu ya tanzania mkoani mtwa kwa gavana wa benki hiyo Prof  Benno ndulu na Mkurugenzi wa masoko kitengo cha makampuni makubwa wa Bancabc Khalifa Zidadu.
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania- BoT Prof. Benno Ndulu akimshukuru Mkurugenzi wa masoko kitengo cha makampuni makubwa wa Bancabc Khalifa Zidadu kwa kuwezesha BoT kununua nyumba hizo mkoani Mtwara, kushoto  ni Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw. Nehemia Mchechu.


Shirika la nyumba la Taifa (NHC)limekabidhi nyumba za makazi kumi kwa banki kuu ya Tanzania (BoT) ikiwa ni sehemu ya nyumba walizozinunua katika mradi wa eneo la Shangani ambao katika utekelezaji wa ujenzi huo wameingia mkataba na Bancabc katika ununuzi wa nyumba hizo.

Mkurugenzi mkuu wa NHC,Nehemia Mchechu alisema hadi kukamilika kwa mradi huo utagharimu kiasi cha Sh 4.8 bilioni ambapo una majengo matatu yenye ghorofa tano kila moja ambapo kwa ghorofa zote zina nyumba za kuishi 30 zenye vyumba vitatu kila moja huku banki kuu wakiwa tayari wamenunua jengo mojalenye nyumba kumi.

“Nyumba hizi zinauzwa kwa wananchi, hadi hivi sasa benki kuu imenunua ghorofa moja yenye nyumba kumi za makazi ambapo kila moja ina vyumba vitatu vya kulala viwili vikijitegemea,jiko la kisasa lenye stoo,sebule ,sehemu ya chakula na stoo ya ziada na sehemu na kuogea na mita za maji na umeme,”alisema Mchechu

Aidha alisema shirika hilo lina mradi mwingine eneo la Raha Leo ambao pia wameingia mkataba na Bancabc ambayo imetoa fedha kwa ajili ya kufanikisha mradi huo ambao utagharimu kiasi cha 22.5 bilioni hadi kukamilika ambapo Benki kuu tayari imenunua majengo mawili yenye nyumba 40 kwaajili ya wafanyakazi watakaokuwa Mtwara.

Mkurugenzi wa masoko kitengo cha makampuni makubwa kutoka Bancabc,Khalifa Zidadu alisema NHC ni moja ya wateja wao ambao hushiriki kuwasapoti katika miradi yao ikiwa ni moja sehemu ya utendaji kazi wao.

“NHC ni moja ya wateja wetu ambao tumeshiriki katika kuwasapoti kwenye miradi miwili wa Shangani ambao tumewaunga mkono kwa asilimia 30 na mradi wa Raha Leo tumewapatia kiasi cha 11 bilioni ili kuufanikisha na hii ni sehemu ya utendaji kazi wetu,”alisema Zidadu

Aidha alisema benki hiyo kwa miaka miwili iliyopita wamekuwa wakishirikiana na makampuni makubwa na kuwaunga mkono na kuyataka makampuni na mashirika mengine kujitokeza ili kupata ushirikiano kutoka katika Benki hiyo.

“Niwaombe tu wananchi ambao wanahitaji kuwa sehemu ya miradi ya shirika la nyumba na miradi ya makampuni mengine watuone kwasababu tunaangalia pande zote na kuwaunga mkonoa,”alisema Zidadu

Akizungumza gavana wa benki kuu,Prof Benno Ndulu alisema ujenzi wa tawi la benki hiyo tayari umekamilika kwa asilimia 98 ambapo hadi kufikia mwezi Septemba wanatarajia watumishi waanze kuingia kwenye nyumba hizo na kuanza shughuli Novemba mwaka huu.

“Nyumba ni moja ya sekta zinazoongoza maendeleo,sisi tunataka kufungua milango ya shughuli zetu ifikapo Oktoba,nitoe rai hizi nyumba 40 zilizosalia zifanyike kila jitihada ifikapo mwezi Septemba mwishoni tuweze kukabidhiwa majengo yote mawili ili wale wanaotakiwa kufika huku wakute mazingira tayari waanze kazi,”alisema Prof Ndulu

Aidha alisema Tawi la Mtwara litakuwa likitoa huduma kwa serikali,mabenki,na shughuli mbalimbali za kiuchumi, katika kanda ya kusini na sehemu ya Pwani.

WATANZANIA WAASWA KUWA WAZALENDO NA NCHI YAO

$
0
0


Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mh. Christina Mndeme akiwasha Mwenge wa uhuru katika mnara wa mashujaa kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mshujaa, hafla iliyofanyika Saa Sita Kamili usiku ya tarehe 25 julai 2016 Mkoani Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Jordan Rugimbana akiongea na baadhi wa viongozi wa serikali waliohudhuria tukio hilo la uwashwaji wa Mwenge na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuupa heshima Mkoa wa Dodoma wa kuadhimisha siku ya mashujaa.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiongea na baadhi wa viongozi wa serikali waliohudhuria tukio hilo la uwashwaji wa Mwenge na kutoa rai kwa watanzania kuwa wazalendo na nchi yao bila kujali itikadi ya mtu kama walivyofanya wazee wetu waliopigania uhuru wa nchi.

Wanajeshi wa Kikosi cha Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakiimba wimbo wa Taifa mara baada ya kuwashwa kwa Mwenge kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Mshujaa yatakayofanyika tarehe 25 julai 2016 Mkoani Dodoma.

Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa Serikali wakishuhudia uwashwaji wa Mwenge.

Mwenge wa uhuru mara baada ya kuwashwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mh. Christina Mndeme, Tarehe 25 julai 2016 Saa Sita Kamili usiku Mkoani Dodoma. PICHA NA HASSAN SILAYO


Na. Immaculate Makilika Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama amesema kuwa kufanyika kwa maombolezo ya kumbukumbu za Mashujaa inawakumbusha watanzania kuwa wazalendo.

Akizungumza wakati wa maombolezo ya kumbukumbu za Mashujaa sambamba na kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru katika mnara wa kumbukumbu za Mashujaa, leo usiku katika viwanja wa Mashujaa vilivyopo mjini Dodoma, Waziri Mhagama alisema kuwa kufanyika kwa maombolezo ya Mashujaa mkoani Dodoma ni heshima kwa wananchi wa Dodoma na watanzania wote kwa ujumla.

“Kufanyika kwa maombolezo haya inatukumbusha watanzania kuwa wazalendo na kupigania bila kuchoka, bila kujali makabila yetu na tujifunze kwa Mashujaa hawa waliopigania uhuru wetu” alisema Waziri Mhagama.

Waziri Mhagama aliwaomba watanzania kutumia siku ya kumbukumbu ya Mashujaa ambayo ni Julai 25, kwa namna mbalimbali ikiwemo kufanya maombi ya sala kwa Mashujaa wote walifariki katika harakati mbalimbali za kupigania uhuru wa Taifa la Tanzania.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mheshimwa Jordan Rugimbana aliishukuru Serikali kwa uwamuzi wa kuadhimisha kumbukumbu za mwaka huu za Mashujaa mkoani Dodoma, na kusema kuwa kufanyika kwa tukio hilo la kihistoria linakumbusha uwajibu wa watanzania na Mkoa wa Dodoma utaienzi heshima hiyo.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Mheshimiwa Christina Mndeme aliwasha Mwenge wa Uhuru katika kilele cha mnara wa mashujaa mnano saa 6 kamili usiku ikiwa ni sehemu ya maombolezo ya kumbukumbu ya Mashujaa.

Mnara wa Mashujaa uliopo mkoani Dodoma ni kati ya vituo 4 vilivyopo nchi nzima ambavyo vimekuwa na makaburi ya Mashujaa mbalimbali waliopigania uhuru wa nchi ya Tanzania. Vituo vingine vipo meneo ya Mtwara, Dar es Salaam na Kagera.

Maadhimisho ya kumbukumbu za Mashujaa kwa mwaka huu yanatarajiwa kufanyika kesho julai 25, mkoni Dodoma ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli atakuwa mgeni rasmi.

HABARI ZA MAGAZETINI LEO.

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,MHANDISI RAMO MAKANI ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA RUBONDO.

$
0
0
Mkuuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Missana Mwishawa akimkabidhi Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani taarifa ya Hifadhi hiyo.Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akipokelewa na Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku (Msukuma) mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ,Herman Kapufi mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha  Rubondo. 


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii katika Shirika la Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ,Missana Mwishawa muda mfupi baada ya kuwasili katika hifadhi hiyo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.
  Mkurugenzi wa Idara ya Utaliii wa Shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) Ibrahimu Musa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani kabla ya kuanza kikao na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Mkurugenzi wa Idara ya Utaliii wa Shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) Ibrahimu Musa akizungumza wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Baadhi ya Madiwani wa mkoa wa Geita wakiwa katika kikao hicho.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ,Missana Mwishawa akisoma taarifa ya hifadhi hiyo kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani.
Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ,Herman Kapufi akizungumza katika mkutano wa Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani (kulia kwake) alipotembelea Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utalii wa Shirika a Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.
Baadhi ya watumishi katika Hifadhi ya taifa ya kisiwa cha Rubondo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo alipofanya ziara ya siku moja katika Hifadhi hiyo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo pamoja na viongozi wengine wa serikali wa mkoa wa Geita mara baada ya kumalizika kwa kikao na watumishi wa hifadhi hiyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Geita mara baada ya kumaliza kikao na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo. 
Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog kanda ya Kaskazini.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images