Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

Vodacom na Samsung wazindua S4.

$
0
0
Meneja wa kampuni ya simu za Samsung nchini Kishor Kumar akiwaonyesha simu aina ya Samsung Galax S4 iliyosheheni teknolojia mbalimbali za kisasa ,Meneja uendeshaji wa maduka ya Vodacom Tanzania Elihuruma Ngowi (kulia)  Meneja Mauzo na Usambazaji wa Samsung Sylvester Manyar na Meneja Masoko wa Vodacom Ibrahim Kingozi (kushoto) wakati wa uzinduzi wa  simu hizo mpya ambapo wateja watakaonunua aina ya simu hizo watapata  huduma ya bure ya Intaneti ya (5GB) kwa muda wa siku 30 ikiwa sambamba na waranti ya mwaka mmoja wa matengezo uzinduzi huo.ulifanyika katika duka la Vodacom lililopo eneo la Oysterbay jijini Dar es Salaam.

Samsung Tanzania Country Manager, Kishor Kumar, illustrates the features of the new Samsung Galaxy S4 to Vodacom Tanzania Manager for Franchise and Operations, Elihuruma Ngowi (right), Samsung Tanzania Manager for Sales and Distribution, Sylvester Manyar and Vodacom Tanzania Post Paid and Enterprise Acquisition Manager, Ibrahim Kiongozi (left) during the launch of the device in Oysterbay, Dar es Salaam. Upon purchase of the Samsung Galaxy S4, customers will get free 5GB internet for 30 days when activated with Vodacom SIM card. The device also comes with 24 months of warranty that will cover any device feature malfunctions. 
Meneja Mauzo na Usambazaji wa Samsung Sylvester Manyar (kushoto)akimuonesha mwandishi wa habari wa clouds media Bi.Esther Machangu moja ya teknologia iliyopo kwenye simu aina ya Samsung Galax S4 yenye teknolojia mbalimbali za kisasa ,wakati wa uzinduzi wa simu hizo  wateja watakaonunua  simu hizo watapata  huduma ya bure ya Intaneti ya (5GB) kwa muda wa siku 30 sambamba na waranti ya mwaka mmoja ya matengezo,uzinduzi huo ulifanyika Vodashop  Oysterbay jijini Dar es  Salaam,Wanaoshuhudia watatu toka kushoto ni Afisa Masoko wa Vodacom Ibrahim Kingozi,Elihuruma Ngowi, Meneja wa Samsung nchini Kishor Kumar.
Meneja  Uendeshaji wa Maduka ya Vodacom Tanzania,Bw.Elihuruma  Ngowi,akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa simu za mkononi za Samsung Galax S4 ambazo zitapatikana kwenye maduka ya Vodacom,wanaoshuhudia kulia ni Meneja wa kampuni ya simu za Samsung nchini Kishor Kumar na kushoto ni  Afisa Masoko wa Vodacom Ibrahim Kingozi. wateja watakaonunua aina ya simu hizo watapata  huduma ya bure ya Intaneti ya (5GB) kwa muda wa siku 30 ikiwa sambamba na waranti ya mwaka mmoja wa matengezo uzinduzi huo.ulifanyika katika duka la Vodacom lililopo eneo la Oysterbay jijini Dar es Salaam.

MKUTANO WA JUMUIYA ZA CCM NA WAANDISHI

$
0
0

 Baadhi ya Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali walioshiriki katika Mkutano wa Jumuiya za UVCC, UWT na Wazee. Mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya CCM Zanziba Kisiwandui. 
 Naibu Katibu mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania UWT Salma Abuod Talib akifafanua jambo katika Mkutano wa Jumuiya za UVCC, UWT na Wazee na Waandishi wa habari. Mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya CCM Zanziba Kisiwandui.
Mwandishi wa Gazeti la Habari Leo Khatib Burecha akiuliza swali katika Mkutano wa Waandishi wa habari na Jumuiya za UVCC, UWT na Wazee. Mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya CCM Zanziba Kisiwandui

========  =======  ======
Na Ali Issa-Maelezo Zanzibar 15/5/2013

Jumuiya za Chama cha Mapinduzi UVCCM, UWT na Wazazi zinakusudia kuwajengea uwezo Vijana ili kujinasua na hali ngumu ya kimaisha kwa kuwasomesha kupitia Skuli za Wazazi na Elimu ya Amali ili waweze kujiajiri wenyewe.

Zimesema Vijana watakapopata Elimu hiyo itawasaidia kuweza kujiajiri na kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira linaloendelea hapa Nchini. 

Naibu Katibu mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania UWT Salma Abuod Talib ameyamesa hayo huko Makao makuu ya CCM Zanzibar Kisiwa nduwi alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari kwa lengo la kupongeza mafanikio ya ziara ya kichama iliyofanywa na Dkt. Shein.

Amesema Mafunzo ya Amali yatawasaidia Vijana kuondokana na fikra za kutegemea Ajira kwa Serikali na kuwawezesha kujiajiri wenyewe badala ya kutegemea Serikali.

Akizungumzia ziara hiyo Bi Salma amesema ziara ya DKT Shein imekuwa na mafanikio makubwa kwani imeweza kuongeza Wanachama wapya  jambo ambalo ni ishara ya wazi ya uhai na matumaini ya ushindi wa Chama hicho katika Chaguzi za badae . 

Amesema katika hali hiyo kuna haja kubwa kumpongeza kiongozi hiyo kwani imetoa picha ya kufanikiwa kukiimarisha chama na kukiletea maendeleo hapa visiwani na Tanzania kwa ujumla. 

“Jumuiya za chama cha mapinuzi (UVCCM , UWT na Wazazi) Tuna mpongeza kwa dhati kabisa kuwa Mjasiri wa kutembea bila kuchoka na kuwa tayari kutumika kila ambapo alitakiwa ushiriki wake, inaonesha wazi kuwa Makamu Mweneyekiti wetu ni mtu wa watu na anapenda watu pamoja na maendeleo yao”amesema Bi Salma.

Aidha alisema katika ziara hiyo DKT Shein alikagua na kutembelea miradi ya CCM ambapo miradi 35 iliwekewa jiwe la msingi na kuziduliwa ikiwemo SACCOS mbali mbali na Vikundi vya Ushirika .

Akizungumzia sintofahamu iliyopo katika baadhi ya Majimbo Bi Salma alisema CCM imepanga kufanya vikao vitakavyojumuisha Viongozi wa Majimbo wakiwemo Wabunge na Wawakilishi pamoja na Wananchi wao ili kuimarisha uttendaji wao

Amesema Vikao hivyo vitatoa mustakabali nzuri kwa Viongozi hao na kuweza kuwatumikia Wananchi waliowachagua katika hali inayofaa.

Jumla ya Wanachama wapya 5,448 kutoka Vyama mbali mbali vya Siasa wamejiunga na Chama cha Mapinduzi kufuatilia Ziara ya Makamo Mwenyekiti wa  Chama hicho Dkt. Ali Mohammed Shein aliyoifanya karibuni kutembelea Mikoa mitano ya Unguja na Pemba kwa lengo la kuangalia na kukipa uhai chama cha Mapinduzi na jumuiya zake.

IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR 15/5/2013

Washindi wa droo ya Western Union wa kwea kuona fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya

$
0
0
 Kutoka kushoto katika picha ya pamoja ni Meneja Masoko wa Benki ya Posta (TPB) Bw. Andrew Chimazi, Quraish Shindo (mshindi), Flora Mbuya (mshindi), Mratibu wa promosheni hiyo kutoka 24D Brand Communications Bi. Farida Makame, Mkuu wa Huduma za Usafirishaji Fedha wa Benki ya Diamond Trust (DTB) Bi. Chandni Jiwa na Bw. Patropa Ndanshao (mshindi) wakiwa uwanjani JNIA.  

 Mmoja wa washindi wa tiketi kuona fainali ya ligi ya mabingwa iliyodhaminiwa na Western Union Bw. Quraish Shindo akihojiwa na waandishi wa habari kuhusu ushindi wake na safari ya kwenda kushuhudia fainali kati ya Chelsea FC na SL Benfica huko Amsterdam, Uholanzi leo. 

 Meneja Masoko wa Benki ya Posta (TPB) Bw. Andrew Chimazi akisisitiza jambo kwa waandishi wa  habari kuhusu huduma na promosheni za Western Union alipofika uwanja wa JNIA kuwatakia safari. 
Washindi wa Shinda Tiketi Kuona Fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA) Flora Mbuya (kulia) na mwenzake Quraish Shindo wakiwa katika wakati wa furaha kabla ya kukwea kuelekea jijini Amsterdam kushuhudia fainali ya Ligi ya Mabingwa kati ya Chelsea FC na SL Benfica itakayochezwa leo.


1.      Safari ndo imeiva: Mzee Patropa Ndanshao akielekea katika mstari wa kukaguliwa uwanjani JNIA tayari kwa safari ya Amsterdam. Mzee Patropa alitabiria ushindi wa Chelsea FC dhidi ya SL Benfica. 

CPwaa ateuliwa kuwa msimamizi mkuu na MC wa michuano ya Foosball

$
0
0
 Sharon Mariwa Meneja Muenezi Biashara Brainstormusic, Caroline Kakwezi, Meneja Masoko wa Heineken Tanzania na Uche Unigwe – Mkurugenzi Mkuu na Cpwaa msanii maarufu wakishikana mikono na Mkurugenzi wa Heineken Tanzania baada ya kusaini mkataba wa kuteuliwa kuwa msimamizi na MC wa michuano ya mpira wa mezani (Foosball) kulia ni Ronald Louis Meneja Opereshini wa Brainstormusic.
Cpwaa, msanii maarufu na wakimataifa wa Bongoflava akisaini mkataba wa kuteuliwa kuwa  msimamizi na MC wa michuano ya mpira wa mezani (Foosball) nchini Tanzania, pamoja naye ni Caroline Kakwezi meneja masoko wa Heineken Tanzania na Uche Unigwe Mkurugenzi wa Heineken Tanzania

WATAALAM WA KUKABILIANA NA MAJANGA KUTOKA TANZANIA NA MAREKANI WAKUTANA JIJINI DAR ES SAALAAM.

$
0
0
 
  Washiriki wa mkutano wa siku 2 unaojadili namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali na athari za Virusi vya mafua ya ndege wakiwa katika picha ya pamoja leo jijini Dar es salaam.
 Viongozi wa serikali ya Tanzania na Marekani, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha (kushoto) na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt (kulia) wakionyesha nyaraka mbili za Mpango wa kukabiliana na maradhi ya mafua ya ndege. Nyaraka hizo zinahusisha vikosi vya jeshi na raia nchini Tanzania na Kamandi ya Jeshi la Marekani la Kupambana na Majanga Barani Afrika (USAFRICOM). 
 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha akizungumza na viongozi mbalimbali wa vitengo vya kukabiliana na majanga kutoka Tanzania na Marekani leo jijini Dar es salaam.Pamoja na mambo mengine amesema Tanzania inaendelea kujenga uwezo wa ndani wa kukabiliana na majanga mbalimbali. 
 Balozi wa Marekani nchini Tanzania Alfonso Lenhardt akiongea na viongozi mbalimbali wa vitengo vya kukabiliana na majanga kutoka Tanzania na Marekani leo jijini Dar es salaam na kusisitiza kuwa serikali ya Marekani itaendelea kushirikiana na Tanzania na nchi nyingine katika kukabiliana na majanga yanayotokea.
  Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wa siku mbili kutoka Tanzania wakifuatilia masuala mbalimbali yaliyokuwa yakijadiliwa leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Shamsi Vuai Nahodha akitoa ufafanuzi kwa waandishi kuhusu utayari wa Tanzania katika kukabiliana na majanga mbalimbali yanayotokea kwa kuvishirikisha vikosi vya ulinzi na usalama, wataalam wa sekta nyingine, utoaji wa tahadhari mapema kwa wananchi na uimarishaji wa kitengo cha maafa nchini.
Washiriki wa vikosi vya kupambana na majanga kutoka Tanzania na Marekani wakiangalia moja ya filamu inayoonyesha athari za virusi vya mafua ya ndege kwa binadamu iliyowahi kutokea katika moja ya nchi na hatua zilizochukuliwa kudhibiti hali hiyo isilete maafa zaidi.  
Picha na Aron Msigwa - MAELEZO. 














Kitabu cha Mwakalebela hadharani mechi ya watani wa Jadi.

$
0
0

KITABU cha kwanza nchini kinachozungumzia soka la Tanzania kijulikanacho kwa jina la “Soka la Tanzania” kitaanza kuuzwa siku ya mechi ya watani wa Jadi, Yanga na Simba iliyopangwa kufanyika Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa.

Akizungumza na jijini jana, mtunzi wa kitabu hicho, Katibu Mkuu wa zamani wa Shirikisho la Kandanda nchini (TFF), Fredrick Mwakalebela alisema kuwa maandalizi ya zoezi hilo yamekamilika na yamedhaminiwa  na kampuni TSN Group kupitia kinywaji chake cha kuongeza nguvu Chilly Willy, Events World, Vannedrick Tanzania Limited na  Inbox Pub.

Wadhamini wengine ni Clouds FM, Times FM na Street Soul kwa mujibu wa Mwakalebela. Alisema kuwa kwa sasa ametoa nakala 10,000 kwa ajili ya kuuzwa Tanzania nzima. Alisema kuwa kitabu hicho kimezungumzia historia ya soka la Tanzania katika Nyanja za vijana, wanawake na wanaume, ligi kuu ya Tanzania Bara, Taifa Cup, Timu ya Taifa na Utawala Bora.

Mbali ya hayo, kitabu hicho kimezungumzia ujio wa kocha Marcio Maximo, mchango wa serikali katika kuinua mpira wa miguu, wadhamini, uhusiano kati ya waandishi wa habari na TFF na changamoto mbali mbali za mpira wa miguu Tanzania.

“Pia nimeelezea mambo niliyojifunza chini ya Rais Leodegar Tenga kwa kipindi cha miaka mine nikiwa TFF, matatizo niliyokutana nayo kutoka kwa makamandoo na kuniita mimi muimba kwaya wakati wa utambulisho wangu wa kwanza  Juni 15, 2006,” alisema Mwakalebela.

Alisema kuwa kitabu hichi ni muhimu sana kwa wana-habari, wachezaji, makocha, waamuzi na wadau wengine wa mchezo huo kwani kuna kumbukumbu zote za mechi za timu ya Taifa ikiwa mabao ya kufunga, wafungaji, vikosi tofauti vya timu za taifa na mambo mengine.

charity walk in support of maternal and child health

Msondo,Che Mundugwao,Majuto kuwasha moto Fainali za Taifa Miss Utalii Tanzania Mkwakwani Tanga mei 19.05.2013

$
0
0

Warembo wa Miss Utalii Tanzania 2013 wakiwa katika Picha ya Pamoja

Baada ya shamlashamla na mapokezi makubwa ya Miss Utalii Tanzania walipo ingia Mkoani Tanga na kupokelewa na umati mkubwa wa watu, warembo hao wapo kambini tayari kwa maandalizi ya Fainali hizo.

Fainali za Taifa Miss Utalii Tanzania zitafanyika Tarehe 19.05.2013 Mkoani Tanga ambapo warembo zaidi ya 30 watapanda Jukwaani kuwania Taji la Taifa la Miss Utalii Tanzania 2013 ndani ya Mkwakwani.

Sambamba na Fainali hizo za Miss Utalii , kutakuwa na Burudani ya Kukata na shoka ambayo itasindikizwa na Bendi kongwe ya Muziki Msondo Ngoma kutoka Dar es salaam, Mwanamuziki wa Kimataifa Che Mundugwao, Majuto Arts Group, Mdumange, vikundi vya ngoma na Sarakasi.

Fainali za Taifa zitaanza kuanzia saa 7 mchana hadi saa 12 jioni Ambapo viingilio kwa watoto itakuwa 2,000 na wakubwa 5,000 Baada ya hapo kuanzia saa 1 usiku hadi Majogoo viti Maalum itakuwa ni 20,000 na kawaida itakuwa 10,000 

Mpaka sasa Kambi ya Miss Utalii Tanzania 2013 ipo jijini Tanga Mwambani Hotel na inaendelea Vizuri, Warembo zaidi ya 30 kutoka mikoa yote nchini ,wanajiandaa vizuri  kwa ajili ya Fainali Hizo zitakazo fanyika wiki ijayo Tanga, Kanda Maalum ya Zanzibar na Vyuo vikuu Tanzania.

Washindi wa 1-5 wa Fainali za Taifa ,watawakilisha Tanzania katika mashindano mbalimbali ya Dunia na nchi yatakako fanyika katika mabano  International Miss Tourism World (Marekani), Miss Tourism United Nation (Mexico), Miss Heritage World (Tunasubiri Taarifa), Miss Tourism University World(Tanzania), Miss Globe International (Uturuki), Miss Tourism World ( Equatorial Guinea ), Miss Freedom Of The World ( Kosovo) , na Miss Tourism United Nation (Nigeria)  n.k

Wakati huohuo, katika kuhakikisha kuwa maandalizi ya Fainali za taifa, za mashindano hayo ambapo mkoa wa Tanga unakuwa wenyeji kwa mara ya kwanza yanafanyika kwa ubora na hayakwami, kamati ya maandalizi ya kimkoa umeundwa ambayo mwenyekiti wake ni Peter Semfuko Afisa Utamaduni wa Jiji la Tanga. Miss Utalii Tanzania ,hadi sasa tunashikilia Jumla ya mataji 5 ya Dunia na kimataifa, yakiwemo ya Miss Tourism World 2005-Africa,Miss Tourism World 2006-SADC,Miss Tourism World 2007-Africa, Miss Tourism.

Model Of The World 2008-Personality, Miss Africa 2006 – 1ST Runner Up n.k

watu wawili washikiliwa kwa kuiba bangi mahakamani Mkoani iringa

$
0
0

Katika hali isiyo ya kawaida watu wawili wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuiba bangi katika mahakama ya wilaya  ya Iringa yenye kilogram 371.2.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa wa Iringa MICHAEL  KAMUHANDA amewataja watu hao kuwa ni Lwitiko Lusekelo ambaye ni mlinzi katika mahakama hiyo pamoja na Juma Nzoa mkazi wa flerimo.


Kamanda Michael amesema kuwa tarehe 14 mwezi huu walimkamata Juma Nzoa akiwa na bangi hizo nyumbani kwake mtaa wa flerimo na alipohojiwa akasema  ameuziwa na lusekelo kutoka katika chumba cha mahakama cha kuhifadhia vitu vya kiharifu kitu ambacho ni kinyume na sheria.


Hata hivyo kamanda amesema kuwa watuhumiwa hao watafikishwa mahakamani wakati wowote huku jeshi la polis likiendelea kuwatafuta watuhumiwa wengine waliohusika katika tukio hilo.


Aidha ameongeza kwa kusema ni jambo la ajabu bangi kuweza kupatikana katika vyombo vya sheria kwani vitu kama hivyo havipaswi kuhifadhiwa pale vinapokamatwa vinapaswa kuteketezwa mara moja.

mtu mmoja akamatwa na jeshi la polisi mkoani iringa kwa kujifanya mtawa ili kutapeli watu.

$
0
0

Mwanamke mmoja aliyejulikana kwa jina la WANJIRU  KAMAU mwenye umri wa miaka 34 raia wa kijui nchini Kenya, anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kujifanya mtawa  ili kutapeli watu kwa njia ya kuomba msaada wa fedha.



Akizunngumza na Wanahabari,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa,Michael Kamuhanda,amesema kuwa tarehe 13 majira ya jioni katika eneo la ipogolo mwanamke huyo alienda katika nyumba ya masista na kujitambulisha kama ni mtawa lakin katika kukaa ma watawa hawa mienendo yake iliwafanya wagundue kuwa si mtawa kama alivyojitambulisha hivyo kuamua kutoa taarifa katika jeshi la polisi.

Kamanda amesema kuwa katika mahojiano waliyofanya na mwanamke huyo wamegundua kuwa si mtawa bali kazi yake ni ness huku akikutwa na paspot mbili za kusafiria ,ambapo paspoti ya kwanza ni EAS AFRICA PASPOT yenye namba  KE 020659 na paspoti ya pili ni REPULIC OF KENYA yenye namba A 1790366.


Hata hivyo kamanda amesema kuwa mwanamke huyo tarehe 22 mwezi huu ameweza kutembelea sehemu mbalimbali  ikiwemo Rwanda ,boda mifumo  na tarehe hiyohiyo alikwenda nchini Uganda na wiki mbili zilizopita alikuwa Tarime mkoani Mara.


Aidha kamanda ameongeza kwa kusema kuwa ilikuwa kazi ngumu kutambua vitu vyote hivyo kwani kila walipokuwa wakijaribu kumkagua alikuwa akidondoka kutokana na maradhi aliyonayo ya kisukari na jeshi la polisi bado linaendelea na mahojiano ili kubaini nini dhumuni la kutembea sehemu zote hizo na kujiita mtawa.


TIMU TANO KUTOKA AFRIKA MASHARIKI ZAINGIA NUSU FAINALI PAN-AFRICAN GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE

$
0
0
Timu zilizoshiriki robo fainali ya jana katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi cha Guinness Football Challenge mara tu baada ya kumalizika kwa kipindi hicho huku washindi wa dola 1,500 wakiwa wamebelea pesa zao.
Washindi war obo fainali ya 4 timu kutoka Kenya(wenye rangi nyekundu) na timu kutoka Ghana(wenye rangi nyeusi) wakjipongezana baada ya kipindi kuisha.
Washindi wa kwanza wa robo fainali ya mwisho ya Guinness Football Challenge Emmanuel Okraku Kofi(kushoto) na Isaac Aryee(kulia) katika picha ya pamoja na waendeshaji wa kipindi hicho Larry Asego na Mimi kalinda.

========  ========  ========= ======

* TIMU TANO KUTOKA AFRIKA MASHARIKI ZAINGIA NUSU FAINALI PAN-AFRICAN GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE*


15 Mai 2013, Dar es Salaam jana usiku kupitia televisheni za ITV na Clouds TV washindi kutoka Ghana katika GUINNESS® FOOTBALL CHALLENGE walisheherekea ushindi wao wa kufuzu nusu fainali kwa kucheza wimbo wa Azonto huku watangazaji Larry na Mimi nao wakijumuika nao.Emanuel Okarku(27) na Isaac aryee(25) hawakufanya vizuri katika hatua ya pesa ukutani na kupata dola za kimarekani 1,500 lakini waliufanya uwanja wote kucheza Azonto.


Emmanuel na Isaac waliwashinda wakenya katika hatua ya penati na kufikia hatua ya Ukuta  wa pesa wa Guinness, hata hivyo timu kutoka Kenya iliibuka mshindi wa pili na kufuzu kuingia nusu fainali.


Emmanuel, Isaac, Kenneth na Chris pamoja na washindi wengine wa robo fainali zilizopita wataendelea kucheza na kuziwakilisha nchi zao katika hatua ya nusu fainali na wana nafasi ya kupeperusha bendera za mataifa yao hadi mwisho. Pia wana nafasi ya kuwa washindi wa mashindano haya ya Pan African.

Nusu fainali hizi zitaoneshwa katika televisheni za ITV na Clouds TV kila siku za jumatano saa 3:15 usiku ITV na saa 2:15 usiku Clouds TV.Hakikisha haukosi  kuangalia mchezo  huu wa nusu fainali.


Mashabiki  na wapenzi wa soka wanaweza kupima maarifa yao kupitia simu zao za mkononi na kushiriki  GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kupitia GUINNESS® VIP™.  Jiunge bure sasa kupima maarifa yako,tembelea m.guinnessvip.com sasa.


Usikose kufuatilia ukurasa wetu wa facebook wa GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE kwa habari mbalimbali.

-www.facebook.com/guinnesstanzania



Tafadhali kunywa kistaarabu - Hairuhusiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18.


MSANII DIPO AJIUNGA KWENYE MASUMBWI

$
0
0

Kocha wa mchezo wa masumbwi Klabu ya Amana CCM ,Kondo Nassoro Kushoto  
akimwelekeza msanii wa michezo ya kuigiza kwenye Luninga, Haruna Mussa 
'dipo' Dar es salaam jana jinsi ya kutupa makonde alipokwenda kufanya
mazoezi ya ngumi kwa ajili ya kujiweka sawa sawa katika kuakikisha
anafanya vizuri kwenye fani yake.Picha na

Shughuli za mpakani zaathiri elimu ya sekondari Rombo

$
0
0

 Mpaka wa Tanz na Kenya Holili, Rombo - Geti la mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Holili, Wilaya ya Rombo.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Nduweni wakifanya mazungumzo na mwandishi wawww.thehabari.com (hayupo pichani) alippotembelea shule hiyo. Shule hii ni miongoni mwa sekondari zilizopo maeneo ya mpakani mwa Tanzania na Kenya wilayani Rombo

=======  ====== ========
Shughuli za mpakani zaathiri elimu ya sekondari Rombo

Na Thehabari.com, Rombo

SHUGHULI za biashara zinazoendeshwa maeneo kadhaa ya mpakani mwa Tanzania na Kenya katika Wilaya ya Rombo zimeathiri maendeleo ya elimu hasa kwa shule za sekondari zilizopo pembezoni mwa maeneo hayo kwa kile wanafunzi kujiingiza katika biashara hizo.

Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni wilayani hapa na mwandishi wa habari hizi umebaini baadhi ya wanafunzi katika shule za sekondari kutumika katika biashara za mipakani jambo ambalo linachangia wilaya hiyo kufanya vibaya kielimu katika matokeo hasa ya kidato cha nne.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya walimu wakuu wa shule za Sekondari za Urauri, Holili, Tanya, Nduweni pamoja na baadhi ya wadau wa elimu maeneo hayo wamesema wapo baadhi ya wanafunzi  wanajiingiza katika shughuli hizo ambazo huathiri maendeleo ya taaluma.


Akizungumzia shule yake, Mwalimu Mkuu wa Sekondari ya Urauli, iliyopo Tarakea wilayani Rombo, Sim Silayo alisema shughuli za biashara zinazofanyika mpakani mwa Tanzania na Kenya eneo hilo zinaathiri taaluma kwani wapo wanafunzi ambao hujiingiza katika shughuli hizo na kusahau masomo kwa vipindi tofauti.

Alisema baadhi ya wanafunzi wanafanya biashara ndogo ndogo na wengine kufanya vibarua mpakani jambo ambalo limekuwa likichangia taaluma kushuka katika shule hiyo, hasa nyakati za kilimo na mavuno maeneo ya vijiji vya mpakani Kenya na Tanzania.

"Kuna kipindi mahudhurio yanakuwa mabaya kabisa hasa kipindi cha mavuno, kilimo na palizi...wanafunzi wanakimbilia kufanya shughuli hizo kwa kulipwa, pia si wanafunzi tu wanaofanya kazi hizi hata baadhi ya wazazi nao hujumuika kufanya vibarua upande wa pili (Kenya) kwa madai kule malipo ni mazuri zaidi ya nchini kwetu," alisema Silayo.

Kwa mujibu wa matokeo ya kidato cha nne Shule ya Urauri mwaka jana, kati ya wanafunzi 92 waliofanya mtihani huo, ni wanafunzi sita tu ndiyo waliofanikiwa kufaulu huku wanafunzi 44 wakipata daraja la nne na wanafunzi 42 wakiambulia daraja sifuri.

Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Sekondari Holili, Benson Samizi alisema pamoja na sababu nyingine shughuli za mpakani zimekuwa zikichangia shule hiyo kufanya vibaya kwa kile wazazi kushindwa kuwadhibiti wanafunzi wanaporudi nyumbani na kuwa huru kufanya shughuli nyingine zinazowaathiri kitaaluma.

Alisema matokeo ya kidato cha nne mwaka jana shule hiyo ilifanya vibaya kwani kati ya wanafunzi 94 waliofanya mtihani huo, hakukuwa na ufaulu wa daraja la kwanza, daraja la pili na la tatu lilikuwa na mwanafunzi mmoja mmoja huku 39 wakipata daraja la nne na wengine 50 kupata sifuri.

Akizungumzia hali hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Rombo, Judethadeus Mboya alikiri shule nyingi kufanya vibaya hasa matokeo ya mwaka jana na kuongeza uongozi wake umeanza kuchukua hatua  kukabiliana na hali zote zinazoathiri maendeleo ya kitaaluma kwa shule zake.

Alisema kwa hatua ya kwanza halmashauri ilimgharamia mkaguzi wa shule ambaye alifanya ukaguzi katika shule mbalimbali zikiwemo zilizofanya vibaya na kutoa mapendekezo.

Aliongeza kuwa ili kukomesha utoro katika shule hizo viongozi wa serikali za vijiji waliagizwa kuwashughulikia wazazi wanaoshindwa kuwabana watoto wao katika kuhudhuria shuleni, ambapo baadhi walianza kutozwa faini mtoto anapokosa shule jambo ambalo alisema limeanza kuleta mabadiliko.

warembo 11 wajitokeza kushiriki shindano la kumsaka malkia wa kitongoji cha kigamboni.

$
0
0

WAREMBO 11 kutoka sehemu mbalimbali wamejitokeza kushiriki shindano la kumsaka malkia wa kitongoji cha Kigamboni mwaka huu "Redd's Miss Kigamboni 2013" linalotarajiwa kufanyika Ijumaa Juni 7 kwenye ukumbi wa Navy Beach kuanzia saa 2:00 usiku hapa jijini Dar es Salaam. 


Tayari warembo wameshaanza mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na shindano hilo ambapo wanajifua kwenye ukumbi wa Break Point (VIP) uliopo Posta hapa jijini.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mratibu wa shindano hilo, Somoe Ng'itu, alisema kuwa maandalizi ya shindano hilo yako katika hatua za mwisho na bado wanakaribisha warembo wenye sifa za kushiriki shindano hilo kufika mazoezini kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini. 


Aliwataja warembo ambao wameshaanza mazoezi kuwa ni pamoja na Rogathe Michael, Irene Rajab, Magdalena Olotu, Latifa Mohammed, Axsaritha Vedastus, Angella Lutataza, Sara Makembo, Amina Mussa,  Ellen Sulle, Julieth Mwanri na Rachel Reuben. "Tunatarajia kuwa na shindano lenye mvuto na litakalotoa washindani kwenye mashindano ya kanda na baadaye katika ngazi ya taifa, tumejipanga kufanya mapinduzi ndani ya sanaa hii ya urembo wa hapa nchini," alisema Somoe.

Aliongeza kwamba fomu kwa ajili ya kushiriki shindano hilo zinapatikana bure na warembo wanafanya mazoezi chini ya Blessing Ngowi, ambaye mwaka juzi alishiriki fainali za taifa za Redd's Miss Tanzania na alitwaa taji la Kanda ya Elimu ya Juu. Aliyataka makampuni na taasisi mbalimbali zinakaribishwa kudhamini shindano hilo ambalo mwaka jana lilitoa mshindi katika kinyang'anyiro cha Kanda ya Temeke ambaye ni Edda Sylivester.

Wadhamini ambao wamethibitisha kusaidia shindano hilo ni pamoja na kampuni ya bia Tanzania kupitia kinywaji cha Redd's Premium Original, Montage Limited, Clouds Media Group, Papa Z na Break Point.

Taji la Redd's Miss Tanzania linashikiliwa na Brigitte Alfred wakati Edda alishika alifanikiwa kushika nafasi ya tatu kwenye fainali hizo za taifa mwaka jana.

Rais Kikwete azindua kampeni ya lishe jijni dar jana

$
0
0

  Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kampeni ya uongezaji wa virutubishi  vya Vitamni A katika vyakula vinavyo zalishwa Viwandani,Uzinduzi huo ulifanyika katika kiwanda cha kuzalisha mafuta cha Bidco kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
 .Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimimina  mafuta ya virutubishi  katikia kinu cha kutengeneza mafuata ikiwa ni ishara ya uzinduzi rasmi wa Kampeni ya Uongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa  viwandani ,uzinduzi huo ulifanyika jana katika Kiwanda cha Bidco  kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, kushoto anayeshuhudia ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Kiwanda hicho Hemal Shah.
.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi zawadi ya ndoo ya mafuta yenye Virutubishi  yaliyozailishwa na nKiwanda cha Bidco Mkurugenzi Mkuu wa Chakula na Lishe Bw.Benedict Jeje wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya Uongezaji wa virutubishi katika Vyakaula vinavyo zalishwa Viwandani .Uzinduzi huo ulifanyika katika kiwanda cha Bidco kilichopo Mikocheni jijini Dar es Salaam. katikati ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Kiwanda hicho Hamal Shah.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiangalia baadhi ya mafuta yenye Virutubishi yanayozalishwa katika kiwanda cha Bidco  kilichopo Mikocheni jijini Dar es Da es Saloaam.kulia ni Afisa Mkuu Mtendaji wa Kiwanda hicho Hamal Shah ,wakati alipokwenda kufanya nuzinduzi rasmi  wa Kampeni mya Uongezaji wa nVirutubishi katika Vyakaula vinavyozalishwa Viwandani.
.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akioneshwa  na Afisa  Mkuu Mtendaji wa  Kiwanda cha Bidco Hamal Shah,moja ya ndoo za mafuta ya kupikia ambayo tayari yamewekwa virutubishi  wakati alipotembelea  kiwanda hicho kuzindua rasmi Kampeni ya Uongezaji waVirutubishi katika Vyakula vinavyozalishwa Viwandani .Uzinduzi huo ulifanyika katika kiwanda cha Bidco kilichopo jijini Dares Salaam.
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza kwa makini Afisa Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha  Kutegeneza Mafuta cha Bidco,Bw.Hemal Shah  alipokuwa akielezea jinsi wanavyotengeneza bidhaa zao za mafuata zenye kuchanganywa na  virutubisho vyenye Vitamnini A. Wakati Rais alitembelea kiwanda cha Bidco  kilichopo Mikocheni jijini Dar es nSalaam, kuzindua rasmi Kampeni ya uongezaji wa virutubishi katika Vyakula vinavyo zalishwa Viwandani .
Rais Dkt.Jakaya Kikwete akikaribishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kiwanda cha  Kutengeneza Mafuta cha Bidco Bw.Hemal Shah  wakati alipokwenda kufanya uzinduzi  rasmi wa kampeni ya uongezaji wa virutubishi  vya Vitamni A katika vyakula vinavyo zalishwa Viwandani katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Said Meck Sadick.

Taarifa Kwa Umma Kutoka Kamati Maalum Ya Katiba Mpya

UFAFANUZI ARV BANDIA

$
0
0

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII




UFAFANUZI WA TAARIFA MBALIMBALI ZILIZOTOLEWA KWENYE VYOMBO VYA HABARI DHIDI YA DAWA BANDIA YA KUPUNGUZA MAKALI YA UKIMWI YENYE JINA LA BIASHARA TT-VIR 30 TOLEO NAMBA 0C.01.85.

Tarehe 9 Mei, 2013, Mhe. Dkt. Hussein A. Mwinyi (Mb) Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, katika kuhitimisha hoja ya bajeti ya Wizara alitolea ufafanuzi suala la dawa bandia ya ARV kufuatia hoja zilizokuwa zimetolewa na Mhe. Zarina S. Madabida (Mb) kuhusu kuhusika kwa kiwanda cha dawa cha Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd (TPI) katika sakata la dawa bandia ya ARV.

Baada ya ufafanuzi huo wa Mhe. Waziri kutolewa, kumekuwa na taarifa mbalimbali kupitia vyombo vya habari zinazoleta mkanganyiko kwa wananchi kuhusu suala hili.

Ili kuondoa mkanganyiko ambao umeanza kujitokeza, Wizara inapenda kutoa ufafanuzi  kuhusu tamko lililotolewa na Mhe. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.  Aidha, kama ilivyoelezwa katika taarifa mbalimbali za umma zilizokwisha kutolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii pamoja na  TFDA  kuhusiana na suala hili, bado inasisitizwa kwamba kampuni ya TPI Ltd iliiuzia Bohari  ya Dawa (MSD) dawa bandia aina ya TT-VIR 30 toleo Na. 0C.01.85, kwa mujibu wa nyaraka zilizopo.

Tunapenda kusisitiza kwamba, Mhe. Waziri katika hotuba yake hakukanusha kuwa kampuni ya TPI Ltd iliiuzia MSD dawa bandia bali alieleza kwamba uchunguzi wa awali katika kiwanda cha kampuni hiyo haukuonesha dawa hiyo ilizalishwa na TPI Ltd  bali vifungashio ni vya TPI Ltd na nyaraka zinaonesha TPI Ltd kuiuzia MSD dawa hizo bandia. Aidha, alieleza kuwa vyombo vya usalama bado vinaendelea kulichunguza suala hilo ili kubaini chanzo na wahusika wakuu wa dawa hizo bandia.

Kwa kuzingatia unyeti wa suala hili, Wizara inatoa wito kwa vyombo vya habari kusubiri hatma ya uchunguzi unaofanywa na vyombo vya usalama na kuepuka kutoa taarifa ambazo zinaweza kupotosha umma na jitihada kubwa za Serikali katika kupambana na dawa bandia nchini.

N. Mwamwaja
MSEMAJI
16 Mei, 2013.

Mke wa waziri Mkuu pinda afungua kongamano la Makatibu Muhtasi Tanzania (TAPSEA) jijini Arusha leo.

$
0
0
Mgeni rasmi Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda (wa tano kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi viongozi wakuu wa TAPSEA pamoja na waratibu wa Kongamano hilo la Makatibu Muhtasi  Tanzania lililofanyika leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC.
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwezeshaji na Uwekezaji,ambaye pia ni mlezi wa TAPSEA.Dkt Mary Nagu akimkabidhi zawadi ya kinyago mgeni rasmi,Mke wa Waziri Mkuu,Mh.Mama Tunu Pinda ,shoto kwake ni Mwenyekiti wa TAPSEA,Bibi Pili Mpenda wakati wa Kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi Tanzania.
Mgeni rasmi,Mke wa Waziri Mkuu,Mh.Mama Tunu Pinda akifungua Kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi Tanzania,lililofanyika kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC ..
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwezeshaji na Uwekezaji,ambaye pia ni mlezi wa TAPSEA.Dkt Mary Nagu akizungumza jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye kongamano tatu la Makatibu Muhtasi Tanzania,lililofanyika kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC .
Waziri wa  Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto,Mh.Sofia Simba akizungumza jambo mbele ya wageni waalikwa mbalimbali kwenye
mkutano wa Kongamano  la  tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania,uliofanyika mapema leo  kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC .

Sehemu ya meza kuu ndani ya mkutano wa kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania lililofanyika leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC,kutoka kushoto ni  Waziri wa  Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto,Mh.Sofia Simba,Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Uwezeshaji na Uwekezaji,ambaye pia ni mlezi wa TAPSEA.Dkt Mary Nagu,Mgeni rasmi wa Kongamano hilo la TAPSEA,Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda,Mwenyekiti wa TAPSEA,Bibi Pili Mpenda pamoja na Naibu Waziri wa katiba na sheria ambaye pia ni Mshauri wa masuala ya sheria na kazi waTAPSEA,Bi.Angella Kairuki.
Pichani ni sehemu ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania lililofanyika leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC.
Pichani juu ni sehemu ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania lililofanyika leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC.
Baadhi ya wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali wakijiandikisha tayari kwa kushiriki kwenye kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania lililofanyika leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC.
Mwenyekiti wa TAPSEA,Bibi Pili Mpenda akimkaribisha mmoja wa wageni maalum wa kongamano hilo,Naibu Waziri wa katiba na sheria ambaye pia ni Mshauri wa masuala ya sheria na kazi waTAPSEA,Bi.Angella Kairuki alipokuwa akiwasili kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC .
Mwenyekiti wa TAPSEA,Bibi Pili Mpenda akimkaribisha Mgeni rasmi,Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda alipokuwa akiwasili  mapema leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC .
Wakielekea kwenye  ukumbi wa mikutano ambao Kongamano la  kwenye kituo cha mikutano cha kongamano la tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania (TAPSEA), lililofanyika leo kwenye kituo cha mikutano cha Kimataifa  jijini Arusha-AICC .
Mgeni rasmi,Mke wa Waziri Mkuu,Mama Tunu Pinda  (wa pili kushoto) pamoja na wageni waalikwa wengine wakitazama ngoma ya kimasai iliyokuwa ikitumbuiza nje ya jengo la mikutano la AICC kabla ya mkutano wa Kongamano  la  tatu la Makatibu Muhtasi  Tanzania kuanza.

JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN AKIWA ZIARANI MKOANI RUKWA AONANA NA UONGOZI WA MKOA HUO LEO

$
0
0
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohammed Chande Othman akizungumza na uongozi wa Mkoa wa Rukwa katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo mapema leo tarehe 16.05.2013 ambapo alizungumzia mambo kadhaa muhimu kuhusu sekta ya mahakama nchini na umuhimu wa kuboresha amani, ulinzi na usalama katika taifa unaokwenda sambamba na kuweka msukumo wa maendeleo nchini. 
Jaji Mkuu akifafanua jambo kwenye mkutano huo. Kushoto ni Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Alhaj Salum Mohammed Chima. 
Jaji Mkuu akiongoza kikao hicho kilichojumuisha msafara wake na viongozi wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa wa Rukwa.
Mkuu wa Wilaya ya Kalambo (aliyesimama) Moshi Chang'a akizungumza katika kikao hicho. (Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa - rukwareview.blogspot.com)
TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA JAJI MKUU LEO TAREHE 16 MEI, 2013

AJIRA KWA WATOTO MPAKA LINI; WATOTO MAKETE NA BIASHARA YA MKAA.

$
0
0
 Mkaa ukiwa sokoni makete amabo unauzwa sh. 2000 na watoto hao ambapo kwa mujibu wa maelezo yao wamesema wanatumwa na wazazi wao kufanya hivyo
Hapa wakijiandaa kuugawa mkaa huo kidogo kidogo ili wautembeze mitaani kusaka wateja 
 Waangalie wafanyabiashara hawa, ambao kwa mtazamo wangu wanatakiwa wafanye kazi moja kubwa ambayo ni kusoma
 Wakitafakari cha kufanya 
 Anazunguka mitaani kutafuta wateja
Akitafakari jambo, sijui kachoka ama vipi maana hii biashara duuuuuuh!
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images