Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 49516 articles
Browse latest View live

NAIBU Waziri wa Sheria na Katiba, Angellah Kairuki akitaka kikundi cha habari group kujikomboa kiuchumi.

$
0
0

Habari group walipokutana na mama mlezi, Mhe.Angellah Kairuki na
kujadili maendeleo ya kikundi hicho cha waandishi wa habari wanaofanya
mambo ya ujasiriamali muda wa ziada. Jokate Mwegelo (pichani kulia) naye alikuwepo na alitawazwa rasmi kuwa dada mlezi wa kikundi.
========  =======  =======
NAIBU Waziri wa Sheria na Katiba, Angellah Kairuki amewataka
wanachama wa kikundi cha waandishi wa habari cha kujikomboa
kiuchumi (Habari Group) kupendana na kuaminiana ili kukifikisha
kikundi hicho mbali.

Kairuki ambaye pia ni mlezi wa Habari Group, alikitaka kikundi hicho
kutokuwa wachoyo wa kusaidia waandishi wa habari wengine wenye nia ya kuungana na kufanikiwa kimaisha.

Akizungumza na kikundi hicho Dar es Salaam juzi, alisema ili mtu
afanikiwe ni lazima awe mwenye upendo na kusaidia wengine pale
penye mwanya wa kufanya hivyo na kuwataka wanachama wote kuwa na moyo wa kujitolea kwa ajili ya kikundi.

"Sitopenda kusikia kikundi hiki kimekufa kwa sababu ya mifarakano na chuki miongoni mwenu kwani kwa kufanya hivyo hamtofikia malengo mliyokusudia," alisema Kairuki.

 Aliongeza kuwa wakati anaingia madarakani aliweka vipaumbele kwa wafanyakazi wa majumbani, madereva wa aina zote, wafanyakazi wa mashambani, wahudumu wa baa na nyumba za wageni, walinzi na waandishi wa habari.

 Na kwamba ameanza kushughulikia haki mbalimbali za makundi hayo, ambapo kwa sasa wapo kwenye mchakato wa kuishinikiza serikali kusaini mkataba wa kuridhia haki za wasichana wa majumbani.

Aliwapongeza waandishi wa habari kwamba pamoja na changamoto
nyingi wanazokutana nazo, lakini hawakati tamaa na wamekuwa
wakifanya kazi yao kwa moyo mmoja na kwa bidii.

Kama mkakati wake wa kuwasaidia waandishi wa habari, alisema
atasimamia Habari Group ili wawe mabalozi wazuri kwenye mambo
mbalimbali kwa jamii, ikiwemo kuwapatia mafunzo ya ujasiriamali,
kuwapa elimu ya umuhimu wa cheti cha kuzaliwa, sambamba na
kushirikiana nao bega kwa bega kwenye mambo muhimu ya kijamii.

"Kuwasidia kwenu ni miongoni mwa malengo yangu niliyojiwekea ya
kupigania haki ya baadhi ya makundi ambyo nimeona haki zao kama wafanyakazi hazitekelezwi,"aliongeza.

Tigo yadhamini Ngorongoro Marathoni

$
0
0

Kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Tigo imedhamini Mbio za Sita za Ngorongoro Marathon zenye lengo la kupambana na ugonjwa wa malaria zinazotarajiwa ‘kutimua vumbi’jumamosi ya Aprili 6, mwaka huu  katika mji mdogo wa Karatu, mkoani Arusha. Ufunguzi wa mbio hizo utafanywa na Naibu waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Lazaro Nyalandu.

Meneja Chapa wa Tigo Bw. William Mpinga alisema kuwa, kwa mwaka huu kampuni hiyo imetoa  fedha taslimu, simu za kisasa kabisa za mkonaoni pamoja na muda wa hewani kwa mshindi wa kwanza wa kundi la wanaume na mshindi wa kwanza kwa kundi la wanawake.

“Tigo kwa kuwajali Watanzania, tumeona umuhimu mkubwa sana wa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na serikali katika mapambapo dhidi ya malaria ambayo imekuwa ikipoteza maisha ya watu wengi wa rika mbalimbali kupitia mbio hizi…” alifafnua Mpinga. Kwa upande wake Mratibu wa ZARA Charity ambao ndio waandaji wa mbio hizo Bw, Datus Joseph alifafanua kuwa, pamoja na kusaidia mapambano dhidi ya malaria, mbio za Ngorongoro Marathon pia zinasaidia kukuza utalii wa ndani na nje ya nchi.

“Mbio hizi ni za Sita tangu kuanzishwa kwake na Tigo wameendeea kutupa ‘support’ na tunawashukuru sana kwa kuendelea kuwa wadhamini wetu…” alifafanua Joseph. Aliendelea kufafanua kuwa, ZARA Charity inawashukuru wadhamini mbalimbali wa mbio hizo ambazo zimekuwa za mafaniko makubwa.

CRDB YAPATA FAIDA YA BILION 81

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakati akitoa ripoti ya faida ya mapato katika utendaji kazi wa benki hiyo kwa mwaka 2012 jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi, Ally Laay na Mchambuzi Masuala ya Fedha, Mohammed Warsame. (Picha na Habari Mseto Blog)
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya CRDB, Dk. Chales Kimei (katikati) akiwa na Mchambuzi wa masuala ya Fedha, Prof. Mohammed Warsame, Mjumbe wa Bodi, Ally Laay, Joyce Nyanza na Mkurugenzi Rasirimali Watu, Dorah Ngaliga.
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo.
Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Uudumu kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akifafanua jambo wakati wa mkutano huo.

DAR ES SALAAM, Tanzania

IMEELEZWA kwamba mfumuko wa bei umechangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa uchumi hali inayosababisha mazingira magumu ya utendaji kazi katika taasisi za kibenki hapa nchini.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakati akitoa ripoti ya faida ya mapato katika utendaji kazi ya mwaka 2012 ambapo alisema kuwa pamoja na kushuka kwa uchumi benki yake imepata faida ya shs.bilioni 81 sawa na asilimia 113 ambayo ni kubwa kuliko miiaka ya nyuma.

Alisema faida hiyo imepanda kwa asilimia kubwa tofauti na mwaka 2011 ambapo walikuwa na faida ya shs. Bilioni 38 na kuongeza kuwa faida ya mapato kibenki imepungua kwasababau ya hali ya uchumi na ongezeko la bei.

Kimei alisema kuwa, hali hiyo pia husababishwa na ushindani wa kibenki ambao umekuwa mkubwa ambapo hadi sasa kuna benki 50 ingawa kabla ya hapo kulikuwepo na benki 27 nchi nzima.

Aidha, benki hiyo kwa mara ya kwanza katika historia  imefanikiwa kufungua tawi nchini Burundi mwishoni mwa mwaka jana ambako  kuna makao Makuu ya benki ya  CRDB pamoja na matawi madogo madogo  na kwamba ndani ya mwezi mmoja walifanikiwa kupata faida ya shs.bilioni 1.2 

Kamanda Ras Makunja wa FFU Ughaibuni ! na kikosi kazi Ngoma Africa Band

$
0
0


Kamanda Ras Makunja aka Field-Marshal(FFU), wa Ngoma Africa Band aka FFU, katika gwanda za gwaride !

Inasemekana Kikosi kazi cha  Ngoma Africa band aka FFU Ughaibuni ,aka wazee wa bongo tambarare ukipenda "Watoto wa mbwa " chini ya kamanda Ras Makunja aka field-marshal, aka King of Anunnaki Empire (pichani), wameshatoka kambini,na wapo tayari tayari kwa gwaride katika majukwaa ya kimataifa,pia inasemekana kamanda wao kapandishwa cheo kama anavyoonekana !
Katika kambi yao FFU Camp at www.ngoma-africa.com pia kumepigwa soup soup na virungu vya muziki kama kazi vinasikika at www.ngoma-africa.com

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL, ASHIRIKI SHUGHULI ZA KUAGA MWILI WA MAREHEMU JAJI MSTAAFU JUSTICE ERNEST MWIPOPO KARIMJEE DAR LEO

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa marehemu Jaji Mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, aliyefariki kwa ajali ya gari April 3, huko maeneo ya Morogoro. Shughuli hizo za kuaga mwili huo zimefanyika leo April 5, 2013 kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya shughuli hizo mwili ulisafirishwa kuelekea Mkoani Iringa kwa maziko kesho.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji ndugu wa marehemu baada ya kutoa heshima za mwisho, wakati wa shughuli za kuaga mwili wa marehemu Jaji Mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, aliyefariki kwa ajali ya gari April 3, huko maeneo ya Morogoro. Shughuli hizo za kuaga mwili huo zimefanyika leo April 5, 2013 kwenye Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam, ambapo baada ya shughuli hizo mwili ulisafirishwa kuelekea Mkoani Iringa kwa maziko kesho.

  Mmoja wa majaji akibeba picha ya marehemu wakati majaji hao wakishuha jeneza hilo lenye mwili wa marehemu, ili kuanza shughuli za kuaga katika viwanja vya Karimjee leo.
 Majaji wakibeba jeneza lenye mwili wa Marehemu Jaji Mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, wakishusha katika gari kwa ajili ya kuanza shughuli za kuaga katika viwanja vya Karimjee, leo 
  Mmoja wa wanafamilia akibugujikwa machozi wakati wa shughuli hiyo ya kuaga.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Jaji Mkuu Kiongozi na Jaji Mkuu wakati akiwasili kwenye Viwanja vya Karimjee leo kushiriki kwenye shughuli za kuaga mwili wa marehemu Jaji Mstaafu, Justice Ernest Mwipopo, aliyefariki kwa ajali ya gari April 3, huko maeneo ya Morogoro
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanaznia, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Spika wa Bunge, Anne Makinda, Jaji Mkuu Kiongozi na Jaji Mkuu wakiwa katika shughuli hiyo ya kuaga mwili.Picha na OMR

Media Day sasa kufanyika Leaders Klabu badala ya TCC Chang'ombe

$
0
0
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) kinasikitika kuwajulisha wadau wake kuwa bonanza la wanahabari lililopangwa kufanyika kesho viwanja vya Sigara (TCC) Chang’ombe sasa litafanyika viwanja vya Leaders Klabu, Kinondoni Dar es Salaam siku hiyo hiyo ya Aprili 6,2013.

Uamuzi huo wa kushtukiza umefikiwa kwenye kikao cha dharura kilichofanyika jana usiku kati ya TASWA ambao ni waandaaji na wadhamini wa bonanza hilo Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kutokana na kushindwa kuafikiana baadhi ya mambo na menejimenti ya viwanja hivyo.

Tunawaomba sana radhi wanahabari kwa usumbufu mkubwa ambao wataupata kutokana na mabadiliko haya, lakini tunaamini yamefanyika kwa dhamira nzuri yenye nia ya kuboresha bonanza letu na kwa kiasi kikubwa litafana kwa asimilia 100.

Dhamira ya TASWA ni kuona inakuwa na bonanza zuri lisilokuwa na aina yoyote ya kwikwi, hivyo tayari tumeshamalizana na menejimenti ya viwanja vya Leaders Klabu na kila kitu kitakuwa safi kuliko maelezo.

Pia tunaishukuru menejimenti ya viwanja vya Sigara kwa ushirikiano iliotupa kwa nia ya kufanya bonanza hilo eneo lao, ingawa ndoto zetu hazikutumia, lakini tunaamini siku za usoni tunaweza kufanya nao kazi.

Tunasisitiza lengo la bonanza letu ambalo mgeni rasmi atakuwa Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe ni kuwaweka pamoja waandishi wote wa habari bila kujali ni wa siasa, michezo, uchumi, afya na mambo mengine pamoja na wafanyakazi wa vyombo mbalimbali vya habari, ili kubadilishana mawazo na kufurahi pamoja.

Awali bonanza letu ilikuwa lifanyike Leaders Klabu, lakini tulilihamishia viwanja vya Sigara kutokana na wadau wengi kuomba wapate nafasi ya kwenda kutazama mechi ya Kombe la Shirikisho kati ya Azam ya Tanzania na Barrack Young Controllers ya Liberia kesho. Hata hivyo tunaamini wahariri wa habari za michezo watajipanga vizuri kulingana na mabadiliko hayo na hakuna litakaloharibika.

Pia katika kuboresha bonanza hilo litakalotumbuizwa na bendi ya Extra Bongo na kundi la taarabu la Jahazi Modern, kutafanyika mchezo wa soka kati ya wanahabari ambao wameoa na wale ambao hawajaoa utakaofanyika baada ya michezo ya kawaida baina ya vyombo vya habari kumalizika.

Bonanza litaanza saa tatu asubuhi kwa washiriki kucheza michezo mbalimbali ikiwemo soka, netiboli, wavu, kuruka kichura, aina mbalimbali za riadha, kuvuta kamba na kucheza muziki. Bonanza litamalizika saa moja usiku.

Ahsanteni.

Amir Mhando 
Katibu Mkuu TASWA 
05/04/2013

milima ya uluguru ikipiga chafya.

KIKOSI CHA BLOGERS FC CHAKABIDHIWA JEZI NA SAPPHIRE COURT HOTEL YA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Mkurugenzi wa Hoteli ya Sapphire Court ya Jijini Dar es Salaam, Abdulfatah Salim (kulia) akimkabidhi sehemu ya vifaa vya michezo, Nahodha wa timu ya wamiliki wa Magazeti 'Tando' Blogers Fc, Muhidin Sufiani, ambaye ni mmiliki wa mtanda wa www.sufianimafoto.com, kwa ajili ya kushiriki katika Bonanza maalum la waandishi Medi Day linalofanyika kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni kesho. Katikati ni Meneja wa muda wa timu hiyo, Mroki Mroki. Timu hiyo ambayo inashiriki kwa mara ya kwanza katika michezo na bonanza kama hilo, inatarajia kushiriki katika michezo yote itakayo chezwa hiyo kesho, ikiwa ni pamoja na Soka, Netiboli, Kukimbiza Kuku, Kukimbia na Magunia, Kuvuta Kamba, Kucheza Pool, Kuimba na Kudansi 'Sebene' na mingineyo.
 Makabidhiano yakiendelea, hii ni Jezi ya Kipa.
Nahodha wa timu hiyo Sufianimafoto (kushoto) akiwa na Meneja wa muda wa timu hiyo, Mroki Mroki, wakiwa na Vifaa vilivyokabidhiwa.
*************************************** 
HOTELI ya Sapphire Court iliyopo makutano ya mitaa ya Swahili na Lindi, Dar es Salaam leo imekabidhi vifaa vya michezo kwa timu ya wamiliki wa magazeti tando (Blogers FC) kwa ajili ya Bonanza la Media Day, linalotarajiwa kufanyika kesho kwenye viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar es Salaam.

Akikabidhi vifaa hivyo, Mkurugenzi wa Sapphire, hoteli iliyojizolea umaarufu mkubwa kwa sasa nchini, Abdulfatah Salim Saleh amesema ameamua kukabidhi vifaa hivyo ili kuunga mkono timu hiyo mpya inayoanzishwa katika tasniya ya michezo nchini.

“Nilipopata ombi lenu, sikutaka hata kujifikiria, nilisema nitawasadia, na huu ni mwanzo tu. Naahidi kushirikiana nanyi zaidi na zaidi na ninawakaribisheni wakati wowote, mimi ni shabiki wa timu yenu kuanzia sasa,”alisema. Kwa upande wake, Meneja wa Muda wa Blogers FC, Mroky Mroky alisema kwamba wanashukuru kwa msaada huo na wanaahidi kudumisha uhusiano mzuri na Sapphire.

“Wazo hili la kuanzisha timu ni la muda mrefu, lakini lilikuwa likisuasua, ila tukaamua kwa vyovyote lazima tutokee kwenye Media Day ya mwaka huu. Tulipofikiria suala la wapi tutapata vifaa vya michezo, vichwa vilituuma kidogo, lakini tunashukuru Sapphier wametuliza maumivu hayo,”alisema Mroky.

Naye Nahodha wa Blogers FC, Muhiddin Sufiani amesema kwamba baada ya kupata vifaa hicyo kesho wanatarajia kuanza kuonyesha cheche zao kesho katika Bonanza la Media Day, lengo likiwa ni kubeba ubingwa upande wa soka na kutwaa pia mataji mengine madogo madogo. 
     
Miongoni mwa wachezaji nyota wanaotarajiwa kuichezea Blogers FC kesho ni Issa Michuzi, Majjid Mjengwa, Sufiani mwenyewe, Majuto Omary, Joseph Lukaza, Shaffi Dauda, Saleh Ally, Mahmoud Zubeiry, Millard Ayo na John Bukuku.

Bonanza la wanahabari linaloandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), litafanyika kesho kwenye viwanja vya Leaders, chini ya udhamini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL). Pamoja na wanahabari kuchuana katika michezo mbalimbali, lakini Bonanza hilo pia litapambwa na burudani ya bendi ya Extra Bongo na kundi la taarabu la Jahazi Modern.

Kutakuwa pia na mechi maalum baina ya wanahabari ambao wameoa na wale ambao hawajaoa utakaofanyika baada ya michezo ya kawaida baina ya vyombo vya habari kumalizika.

Bonanza litaanza saa tatu asubuhi kwa washiriki kucheza michezo mbalimbali ikiwemo soka, netiboli, wavu, kuruka kichura, aina mbalimbali za riadha, kuvuta kamba na kucheza muziki. Bonanza litamalizika saa moja usiku.   

ZAIDI ya shilingi bilioni 14 zahitajika kukamilisha ujenzi wa chuo cha Taasisi ya Sayansi za Bahari.

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo kwa Mhadhiri Mwandamizi wa Taasisi ya Sayansi ya Bahari Dkt Narriman Jiddawi juu ya Utunzaji wa Samaki Aquarium wakati wa Ziara ya waziri huko Zanzibar
Kaimu Mkurugemzi waTaasisi ya Sayansi ya Bahari ya chuo kikuu cha Dar es Salaam Dkt Christopher Muhando akimtembeza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Jengo la Taasisi ya Sayansi ya Bahari huko Chukwani Mjini Unguja wakati wa Ziara yakutembelea taasisi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mhadhiri Mwandamizi wa Tasisi ya Sayansi ya Bahari ya Chua Kikuu cha Dar es Salaam Dkt NarrimanJiddawi akimuonyesha Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan aina ya Kasa katika chumba cha Kutunzia samaki[AQUARIUM}wakati wa Ziara ya Kutembelea Tasisi za jamhuri ya Muungano wa Tanzania zilizopo Unguja.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo juu ya Ujenzi wa Kituo cha tasisi ya Sayansi za Bahari kilichopo Chukwani Unguja kwa Kaimu Mkurugenzi Dkt Christophet Muhando wakati waziri alipofanya Ziara ya Kutembelea Tasisi za Jamhuri za Muungano wa Tanzania zilizopo Unguja.PIcha na Ali Meja.
=====  ========  =======

Na Ali Issa Maelezo, Zanzíbar.
ZAIDI ya shilingi bilioni 14 zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa chuo cha Taasisi ya  Sayansi za Bahari kilichopo Buyu wilaya ya Magharibi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Hayo yamesemwa leo huko Forodhani mjini Zanzibar na Muhadhiri Dkt. Ntahondi Nyandwi wakati alipokuwa akisoma ripoti ya chuo hicho na rasilimali zake mbele ya Waziri anae shughulikia masuala ya Muungano Samia Suluhu Hassan aliyekuwa katika mfulilizo wa ziara yake kuzitembelea Taasisi za muungano hapa Zanzibar.

Amesema fedha hizo zitahitajika ili kukamilisha ujenzi wa  jengo lote na miundombinu  ikiwemo vifaa vya maabara, sehemu za wanafunzi wa uzamili,  uzamivu, kumbi za mikutano, ofisi za programu za kimataifa, ofisi za wageni wa kimataifa na mengineyo.

Dk. Nyandwi amesema kupatikana kwa fedha  hizo kutakamilisha mahitaji hayo na mengine ambapo kwa sasa ujenzi huo umefikia  hatua nzuri  na wameshatumia zaidi ya bilioni nne  kwa kujenga miundo mbinu mbalimbali ikiwemo  ofisi za viongozi na madarasa.

“Kwa vile pesa za kumlipa mkandarasi hazikupatikana kwa wakati na hakukuwa na uhakika kuzipata, ujenzi ulisimama Agosti 2008 na mkandarasi aliondoka lakini kwa sasa ujenzi unaendeleo taratibu”alisema Nyandwi .

Aidha alifahamisha kuwa ujenzi huo unaendelea kidogo kidogo  kadri fedha zinavyo patikana baada ya kumuomba mkanda rasi awapunguzie gharama na kuweza kumaliza mipango ya awamu ya kwanza na ya pili.  

Nae Waziri wa  Nchi Afisi ya Makamu wa Rais,  Muungano  Samia Suluhu Hassan  amesema kuwa atamuagiza Mkuu wake wa kazi kuja Zanzíbar  kujionea na yeye   Jengo hilo hatua ilio fikiwa. Aidha alisema kua ujenzi huo utaendelea kidogokidogo mpaka utapomalizika.

Maendeleo ya ujenzi wa Taasisi ya sayansi Baharini ni moja ya Taasisi za Chuo  Kikuu cha Dar-es Salaam kampasi  ya Mwalimu Nyerere ambapo umuhimu wa Taasisi hiyo ulianza kujitokeza Mwaka 1978 chini ya sheria Na. 12 ya 1970 ya chuo kikuu cha Dar-slamu kwa tamko la Serikali Na. 34 lililo pitishwa tarehe 16 march 1979.

Chuo hicho kumalizika kwake kufanya kazi za kutafiti nyanja zote za Sayansi za Baharini, kutoa mafunzo ya uzamivu, uzamili katika sayansi ya Bahari ,kutoa ushauri wa kitalamu ,kutoa mafunzo ya Shahada ya kwaza  kwa kulingsana na mahitaji ya  Taifa la Tanzania   kama sehemu ya Taluma kwa vitendo.

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR LEO 5/4/2013

ujio wa jamvi jipya la reuben mchome wa ITV na RAdio One.

$
0
0

Habari Wadau,

Napenda kuwafahamisha juu ya Blog mpya ya Habari za michezo na burudani kwa ujumla wake. Humu utapata updates za mambo mbalimbali kitaifa ikiwa ni habari kutoka karibu mikoa yote ya Tanzania na kimataifa.



KARIBUNI WOTE


Reuben Mchome,

Presenter - ITV/RADIO ONE.

Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba AFUNGUA BARAZA LA WAFANYAKAZI TMA.

$
0
0
 Naibu Waziri wa Uchukuzi , Dk Charles Tizeba ( watano kutoka kulia) aakiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa TMA na wafanyakazi ambao ni wajumbe wa Baraza la wafanyakazi.
 Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dk Agnes Kijazi akitoa ufafanuzi wa jambo kabla ya kukaribishwa mgeni rasmi , Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba ( hayupo pichani) wakati wa mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa TMA

Naibu  Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba ( kati kati) akifafanua jambo mbele ya wajumbe ( hawapo pichani) jana ( Aprili 5) wakati wa hotuba yake ya kufungua mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ( TMA), ( kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Amanzi  na ( kushoto) ni Mkurugenzi Mkuu na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Dk Agnes Kijazi.

Naibu  Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tizeba ( kulia)akimpongeza Mtabiri Mwandamizi na Msimamizi mkuu wa shughuli za utabiri , Wilberforce Kikwasi, ambaye amechanguliwa na Uongozi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  kuwa ni mfanyakazi bora mwaka huu kutokana na ubunifu katika matumizi ya teknolojia ya kisasa na utafiti kwa kubuni mfuno wa ICT ‘ Software’ ( Digital Meteorological Observatory) inayosaidia kurahisisha mawasiliano na uhifadhi wa taarifa za hali ya hewa, Naibu Waziri huyo jana ( Aprili 5) alikuwa ni mgeni rasmi ufunguzi wa mkutano wa Baraza la wafanyakazi wa TMA.( Picha zote na John Nditi).

muendelezo wa tamasha la pasaka ndani ya Iringa.

$
0
0
 Rose Muhando akienda sawa katika Tamasha la Pasaka 2013 mjini Iringa.

Solomon Mukubwa akikonga nyoyo za wakazi wa Iringa kwenye uwanja wa Samora wakati wa Tamasha la Pasaka 2013 lilipofanyika mkoani Iringa.

Rose Muhando akienda sambamba na Upendo Kilahiro.
 Faraja Ntaboba kutoka DRC Congo akiwafurahisha wakazi wa Mbeya katika Tamasha la Pasaka jijini mbeya
 Solomon Mukubwa na Annastazia Mukabwa wote kutoka Kenya wakiwa Iringa,Tamasha la pasaka 2013
Upendo Nkone akikonga nyoyo za wakazi wa Mbeya waliojitokeza katika Tamasha la Pasaka

Manguli wa muziki wa Injili, solomon Mukubwa, Upendo Kilahiro, Faraja Ntaboba,na Bonny Mwaitege wakiwa jukwaani mjini Iringa

picha mbalimbali za hafla ya tuzo za Ejat 2012

$
0
0

 Katibu Mkuu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga akizungumza katika hafla hiyo.
 Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara akizungumza katika hafla hiyo.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi.
 Brass Band ya JKT iktoa burudani katika hafla hiyo.
 Mpiga Picha Bora 2012, Joseph Senga kutoka Kampuni ya Free Media, wachapishaji wa Magazeti ya Tanzania Daima na Sayari, kabla ya kukabidhiwa tuzo yake.
 Baadhi ya washiriki walioingia katika dfainali za tuzo hizo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio akimkabidhi tuzo ya Mpiga Picha Bora 2012, Joseph Senga kutojka Kampuni ya Free Media inayochapisha magazeti ya Tanzania Daima na Sayari. SDEnga amepata tuzo hiyo baada picha aliyopiga ikimuonesha askarti Polisi akimsurubu Mwandishi wa Habari, Marehemu Daudi Mwangosi wa Kituo cha Televisheni cha Chanel Ten.
 Hongera, ulistahili
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akimkabidhi mfano wa hundi mshindi wa jumla wa tuzo za EJAT 2012, Lucas Liganga.
  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad akimkabidhi mfano wa hundi mwandishi mkongwe aliyepata mafanikio. 
Mpiga Picha Bora 2012, Joseph Senga (kulia) akiwa na mpiga picha wa magazeti ya Uhuru na Mazalendo, Emmanuel Ndege ambaye aliingia katika fainali za kinyang'anyilo cha kumtafuta mpiga picha bora.
 Mwandishi wa Habari wa Mwananchi Communications, Anthony Mayunga akipokea tuzo yake.
Jaji Mstaafu Thomas Mihayo akimkabidhi tuzo ya mwandishi bora wa habari za watoto, Shadrack Sagati kutoka TSN.
 Mpiga Picha Bora 2012, Joseph Senga akiwa na tuzio yake.
Mwandishi mkongwe Hamza Kasongo akiwa na mmoja wa majaji wa tuzo hizo, Mwanzo Milinga
 Picha ya pamoja.
 Picha ya pamoja.

Bonanza la Media Day lilivyofana leo ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar

BOTSWANA YAAHIDI KUFANYA KAZI NA IBF/AFRICA

$
0
0

Serikali ya Botswana imeahidi kushirikiana na Shirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) katika program yake ya “Utalii wa Michezo” na kuifanya nchi hiyo kuwa moja ya mataifa yanayong’ara kwenye medani ya masumbwi katika bara la Afrika. Ahadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Michezo la Botswana bwana Persy Raditladi alipofanya mazungumzo na Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati Mtanzania Onesmo Ngowi katika ofisi za BNSC leo.

Rais Ngowi yuko nchini Botswana kuutangaza mkanda wa ubingwa wa ngumi wa kimataifa ambao utashindaniwa tarehe 5 July nchini Namibia kati ya  bondia  wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia kutoka Namibia Immanuel Naidjala. Wawili hao walitoka sare katika mpambano wa kukata na shoka wa kugombania mkanda huo tarehe 20 Machi mwaka huu katika jiji la Windhoek, nchini Namibia.

Serikali ya Botswana imeahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha kuwa programu ya “Utalii wa Micheazo ya IBF” inanufaisha nchi hii yenye vivutio kadhaa vya kitalii likiwamo bonde la maarufu la “Okavango Delta”

Katika mazungumzo yao Rais Ngowi alieleza jinsi IBF inavyozinufaisha nchi ambazo zimeingia katika programu hii na namna mabondia wanaotoka katika nchi hizi wanavyonufaika na viwango vya kimataifa vya IBF. Ngowi aliielezea Botswana kama nchi yenye neema ya vipaji vya mabondia wazuri wa ridhaa na kuwashauri kuwa waweke mikakati ya mabondia wa ridhaa wanavyoweza kujiunga na ngumni za kulipwa ili waweze kufaika na vipaji vyao.


Nchi ya Botswana ni moja kati ya nchi zenye mabondia wazuri katika ngumi za ridhaa lakini kumekuweko na pengo la kuwaendeleza wanapofikia kustaafu na kutokuwa na uwazi wa namna ya kujiunga na ngumi za kulipwa. Ujio wa Rais wa IBF Afrika nchini Botswana umefanyika wakati nchi hii inapokabiliwa na sintofahamu juu ya kuwaendeleza mabondia wake wanapostaafu ngumi za ridhaa.

Mazungumzo ya Rais Ngowi na serikali ya Botswana yalitanguliwa na mkutano wa waandishi wa habari pamoja na wadau kadhaa wa ngumi za kulipwa uliofanyika katika ukumbi wa BNSC jijini Gaborone Botswana leo. Katika mkutano huo Rasi Ngowi aliuonyesha mkanda wa IBF wa kimataifa katika uzito wa bantam utakaoshindaniwa kati ya bondia wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia kutoka Namibia Immanuel Naidjala tarehe 5 July mwaka huu jijini Windhoek, Namibia.
Rais Ngowi aliwahakikishia wadau wa ngumi wa Botswana kuwa IBF itafanya kila liwezalo kuhakikisha kuwa Botswana imejenga msingi mzuri wa ngumi za kulipwa na kutumia vipaji vilivyonavyo katika ngumi za ridhaa. Rais Ngowi aliondoka leo kwenda nchini Afrika ya Kusini ambako atakutana na wadau wa ngumi na kutangaza mapambano kadhaa ya IBF yanayotarajiwa kufanyika nchini humo kuanzia mwezi ujao!
Picha Na. 1: rais Ngowi akihutubia katika miytano wa waandishi wa  habari katika ukumbi wa BNSC
Picha Na. 2: Rais Ngowi akiwa amesimama na Mkurugenzi Mtendaji wa BNSC bwana Persy  Raditladi
 
INTERNATIONAL BOXING FEDERATION AFRICA (IBF/AFRICA)
DAR-ES-SALAAM, TANZANIA
Benjamin William Mkapa Pension Towers

Tower B, Mezzanine Floor, Azikiwe Street
Dar-Es-Salaam - Tanzania

KONGAMANO LA KUMUENZI MUASISI WA MAPINDUZI-MAREHEMU ABEID AMANI KARUME

$
0
0
 Mgeni Rasmi katika kongamano la Kumuenzi Muasisi wa Mapinduzi-Marehemu Mzee Abeid Aman Karume, Ndugu Ally Vuai akiwasili katika Kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha karume, Mbweni Zanzibar.
 wajumbe mbalimbali waliohudhuria katika kongamano la kumuenzi muasisi wa mapinduzi-marehemu mzee abeid amani karume lililofanyika katika ukumbi wa chuo cha karume, mbweni zanzibar leo tarehe 06 April 2013.
 Katibu Mkuu wa jumuiya ya umoja wa vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) akisalimiana na wajumbe mbalimbali waliohudhuria kongamano la kumuenzi marehemu karume
 Meza Kuu kutoka kulia Katibu Mkuu wa UVCCM Martine Shigela, M/kiti wa UVCCM Taifa Sadifah Juma, Naibu Katibu Mkuu Znz Ally Vuai na M/kiti wa Mkoa wa Magharib Yusuph M. yusuph.
 wajumbe mbalimbali waliohudhuria katika kongamano la kumuenzi muasisi wa mapinduzi-marehemu mzee abeid amani karume lililofanyika katika ukumbi wa chuo cha karume, mbweni zanzibar leo tarehe 06 April 2013.


 Msomaji wa Dua ya kumuombea Marehemu Mzee Karume akisoma Dua hiyo mbele ya wahudhuriaji wa kongamano la kumuenzi Muasisi wa Mapinduzi-Marehemu Mzee Karume yaliyofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Karume, Mbweni Zanzibar,leo Jumamosi tarehe 06th April  2013
M/kiti wa UVCCM Taifa akizungumza katika kongamano la Kumuenzi Muasisi wa Mapinduzi-Marehemu Mzee Abeid Aman Karume,

uchaguzi wa Rais wa Chuo cha maendeleo na utalii Zanzibar wafanyika.

$
0
0

Na Miza Othmani Maelezo Zanzibar  6/4/2013 .

TUME  ya Chuo cha maendeleo na utalii Zanzibar kimemtangaza rasmi mwanafunzi Mussa Mohd Rashid kuwa Rais wa chuo hicho . Tume hiyo imetangaza Rais Mussa Moh’d  baada ya uchaguzi uliyofanyika Maruhubi mjini Zanzibar

Katika  kinyanganyiro cha Uchaguzi huo waligombania  ni Juma Ali Abdalla na Mussa Moh’d Rashid waliopiga kura ni jumla  wanafunzi 200 kura  zilizoharibika   02, kura halali zilizopigwa ni 198, kwa upande wa matokeo,  Juma  Ali Abdalla amepata kura 97- 48.5% na mgombea mweza Mussa Moh’d  Rashid alipata kura 101 -50%.

Hata hivyo kwa upande wa Rais Mussa Moh’d  alisema kuwa kudumisha umoja na  mashirikiano kutaondosha kugawanyika makundi na matabaka na kutaleta maendeleo chuoni hapo .

Aidha alisema  kuwa katika madaraka aliyopewa atatekeleza ahadi zote alizoahidi na kuifanya serikali kuwa imara na yenye nguvu na kuepukana na migogoro ambayo yatakwamisha utekelezaji wa kazi.

“kuondoa makundi na kuondoa matabaka nitatekeleza ahadi zote nilizoahidi ”,Alisema Rais . Alisisitiza kuwa wanafunzi atakuwa pamoja  nao bega kwa bega katika matatizo mbali mbali yatakayojitokeza na  kuwa imara katika kukabiliana na majukumu ya chuoni hapo .

Nae Omar Moh’d  Khamis kwa niaba ya wanafunzi wenzake amesema kuwa kudumisha mashirikiano ya pamoja na uongozi wa chuo ndio njia pekee ya kuleta maendeleo na ufanisi mkubwa .
“tujenge mashirikiaano tuepukane na ubaguzi na kuleta maendeleo endelevu chuoni”Alisema Omar.

Uchaguzi huwo umefanyika baada ya Rais aliyokuwepo Bakar Haji Kheir kumaliza muda wake wa uongozi . 

MKUTANO WA CUF MKWAJUNI KASKAZI (A) UNGUJA

$
0
0

  Katibu Mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamadi akiwahutubia wananchi wa Mkwajuni katika mkuto wa hadhara wa chama hicho uliofanyaka  katika viwanja vya mpira Mkwajuni,leo April 06/2013.
 - Wanachama wa CUF wakisikiliza kwa makini  Maalim Seif Sharif Hamadi hayupo pichani alipokuwa akiwahutubi katika mkutano wa hazara uliofanyika katika viwanja vya mpira Mkwajuni.

 Katibu Mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamadi akisikiza utenzi kwa makini,kulia ni Naibu katibu Mkuu wa CUF Hamad Masud Hamad na kushoto Mwenyekiti wa Wilaya ya Kaskazini (A). huko Mkwajuni Kaskazini A Unguja.
  Katibu Mkuu wa chama cha wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamadi akiwahutubia wananchi wa Mkwajuni katika mkuto wa hadhara wa chama hicho uliofanyaka  katika viwanja vya mpira Mkwajuni,leo April 06/2013.


Wanachama wa CUF wakiburudika kwa rusha roho kabla yakuwasili kwa mkeni wa heshma katika mkutano wahazara uliofanyika huko Mkwajuni Kaskazini A Unguja.

=========  ========  ===========
Na Miza Kona  Maelezo Zanzibar .

KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Maalim Seif Sharif Hamad amesema Zanzibar ni nchi ya biashara hivyo inataka kujitegemea iweze kupunguza ushuru ili wananchi wapate kununua bidhaa kwa bei nafuu.

Kauli hiyo ameitoa huko katika viwanja vya Skuli ya Mkwajuni Wilaya ya kaskazini “A” wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Mkoa huo.

Amesema iwapo Zanzibar itapata mamlaka yake kamili itaweza kuwa na bandari huru, ushuru na bei za bidha vitapungua. “Zanzibar ni nchi ya biashara tunataka tuwe na bandari huru ili tupate kuweka kodi ndogo na ushuru ukipungua bei za bidhaa zitapungua”alieleza Maalim.

Aidha amesema kuwa wananchi wanataka kuwepo kwa bandari na kupungua ushuru ili wapate kuweka bei wanazotaka wenyewe na sio kuamuliwa na mtu mwengine.

Akizungumzia Muungano Maalim Seif amesema wazanzibar waliowengi wanataka serikali ya mkataba iwe na mamlaka kamili na isiingiliwe katika maamuzi yake.

“Haya ni matakwa ya wananchi wenyewe na sio matakwa ya CUF hili ni la wazanzibar wenyewe” alieleza Katibu huyo. “Zanzibar ni nchi matakwa ya wazanzibari yaheshimiwe yasiingiliwe na wengine kwani mamlaka na madaraka hayo ndiyo yanayoweza kuyatatua matatizo ya wazanzibar” alifafanua Maalim Seif.

Hata hivyo Katibu huyo ameitaka Tume ya kukusanya maoni ya Katiba kuhakikisha kwamba wajumbe waliochaguliwa kuwakilisha kutoa maoni katika Katiba hiyo wamechaguliwa kihalali na sio kupandikizwa.  
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

BLOG MPYA YA EDDYMOBLAZE TOKA MAKETE

$
0
0

Habari za leo wadau, Napenda kuchukua fursa hii kuitambulisha kwenu blog yangu mpya ambayo ina lengo la kutoa habari mbalimbali kutoka Makete na sehemu za jirani ili kuendelea kuwajuza wasomaji waliopo kila pembe ya Dunia hii kwa muda wote bila kuchoka. Jina la blog hiyo ni EDDYMOBLAZE BLOG unaweza kuipitia kwa kubonyeza link ifuatayo:-  


asante kwa ushirikiano wenu

Edwin Moshi
Mmiliki wa Blog
Eddymoblaze Blog 

PPF YATOA VIFAA KUMALIZIA UJENZI KITUO CHA POLISI NYAKOTO MWANZA

$
0
0
Meneja wa PPF Kanda ya ziwa Meshack Bandawe akimkabidhi mifuko ya simenti Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ernest Mangu, mchango wenye thamani zaidi ya shilingi milioni 2, kwaajili ya kuchangia uharakishwaji wa ujenzi wa kituo cha polisi Nyakato jijini Mwanza. 


Mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa kituo cha polisi Nyakato Bw. Alfred Wambura, amesema kuwa kamati yake imenuia kuhakikisha ujenzi wa kituo hicho unakamilika mwishoni mwa mwezi wa 5 na kukabidhiwa kwa jeshi la polisi.

Mikakati mingine iliyowekwa na kamati hiyo ni kukamilisha ujenzi wa nyumba ya makazi ya OSS wa Nyakato pamoja na watendaji wengine watatu wanaomfuata kwa cheo, ili kurahisisha utendaji wa kila siku wa shughuli za usalama wa jeshi hilo. 


Meneja wa PPF Kanda ya ziwa Mesharck Bandawe amesema kuwa ulinzi kwa maisha ya baadaye ya mwananchi uko ndani ya  mfuko wa uwekezaji wa PPF,  na ulinzi wa wananchi na mali zao uko chini ya jeshi la polisi hivyo amewataka wadau wengine wa mashirika mbalimbali kujitokeza kulisaidia jeshi hilo kukamilisha shughuli za utendaji kwa manufaa ya ustawi wa jamii.


Wadau wa PPF wakisikiliza kwa makini yanayojiri kwenye makabidhiano hayo.


Diwani wa kata ya Mahina, Mhe. Chinchibela ametoa rai kwa mashirika mengine kusaidia jeshi la polisi kama sehemu ya ulinzi shirikishi, kwani msaada huu wa PPF umekuwa wa tatu kutoka kwa mashirika mbalimbali mkoani Mwanza ambayo yamethubutu kukisaidia kituo hicho. 




Mhe. Manyerere ambaye ni diwani wa kata ya Nyakato ameishukuru asasi ya PPF kusaidia kuchangia ujenzi wa kituo cha polisi Nyakato ambacho ni moja kati ya vituo muhimu kwani kinahudumia usalama wa maeneo ya kata takribani 4 za jiji la Mwanza. 


Mifuko ya simenti iliyotolewa na PPF ikishushwa kutoka kwenye roli. 


Meneja wa PPF Kanda ya ziwa Meshack Bandawe akiteta jambo na Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza Ernest Mangu mara baada ya makabidhiano kukamilika.


Kamanda akifanya ukaguzi kwa shughuli za ujenzi zinazoendelea kituoni hapo. 


Hiki ni chumba cha mahabusu ambacho kwa mujibu wa kamati ya ujenzi kitakuwa na choo kukidhi usumbufu na changamoto zilizojitokeza katika vituo vingine.


Ukaguzi ukiendelea...


Maelekezo toka kamati ya ujenzi.


Ujenzi ukiendelea na mchango wa PPF kama unavyoonekana. PICHA/HABARI NA G. SENGO

Viewing all 49516 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>