Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live

BOT YAWATAHADHARISHA WANANCHI

$
0
0
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akimpatia vipeperushi Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, wakati alipotembelea banda la Wizara katika maonesho ya Wiki ya Utumishi, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akimpatia vipeperushi Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, wakati alipotembelea banda la wizara katika maonesho ya Wiki ya Utumishi, Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana.
Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu, kuhusu kazi ya Benki Kuu, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. 
 Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu, kuhusu sarafu ya sh. 500, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. 
Meneja Uhusiano wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Zalia Mbeo, akimpatia maelezo Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, HAB Mkwizu, kuhusu sarafu ya sh. 500, wakati wa ufunguzi wa maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam jana. (Picha zote na Kassim Mbarouk)



Na Salma Ngwilizi – Maelezo
BENKI  ya Tanzania(BOT) imewataadharisha wananchi kwamba  sarafu  ya sh. 500 haina  madini ya aina yoyote na wala haiuzwi haiuzwi  kama inavyoadaiwa na baadhi ya watu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Meneja  Uhusiano wa benki hiyo,  Zalia Mbeo wakati akitoa ufafanuzi kwa  Kaimu  Katibu Mkuu wa  Ofisi ya Rais Menejimenti ya  Utumishi wa Umma, HAB  Mwizu  ambaye aliuliza kwamba  kuna taarifa kuhusu sarafu  hiyo kuuzwa mitaani.

Kaimu Katibu Mkuu huyo ambaye alifungua maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma,  Mhe. Celina Kombani.

 “Watanzania wanatapeliwa sarafu hii haina thamani yoyote ni uzushi,” alisema Zalia.
 Aliongeza wananchi wadanganywa na watu kuwa sarafu hiyo ikiyeyushwa ina madini ambayo  yanaweza kuwapatia fedha nyingi  wakati si kweli.
Maonesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yamefunguliwa rasmi jana Juni 16, mwaka huu na yanatarajia kumalizika Juni 23, mwaka huu.

 Kauli mbiu ya mwaka huu “Utumishi wa Umma katika Bara la Afrika ni chachu ya kuwawezesha Wanawake kuongeza Ubunifu  na Kuboresha utoaji wa Huduma kwa Umma”.

WAZIRI WILLIAM LUKUVI ATATUA MIGOGORO MIKUBWA YA ARDHI MKOANI LINDI

$
0
0
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Vangimembe Lukuvi amemaliza ziara ya siku mbili Mkoani Lindi ambapo alikagua shughuli za Shirika la Nyumba la Taifa na kusikiliza migogoro ya ardhi inayowakabili wananchi wa Lindi eneo la Mitwero na kuitatua.

 Katika ziara hiyo, Waziri Lukuvi amewaonya na kuwaagiza Maafisa ardhi, wapima na maafisa mipango miji kuacha mara moja kujinufaisha kwa kuwadhulumu wananchi haki zao za ardhi.

 Aidha ameutaka Mkoa wa Lindi kuharakisha upimaji wa ardhi ya wananchi na utoaji wa hati ili kuwawezesha wananchi kumiliki ardhi na kupunguza migogoro ya ardhi.
New Picture (3)
Waziri William Vangimembe Lukuvi akisisitiza jambo baada ya Watendaji wa sekta ya ardhi ya Mkoa wa Lindi kushindwa kumudu maswali mbalimbali aliyowauliza na kuwataka watendaji hao kujipima kama bado wanastahili kuendelea kuwatumikia wananchi kwa nafasi zao wanazotumimkia.
New Picture (4)
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mh. Mwantumu Mahiza akimuomba Mheshimiwa William Lukuvi kuwaondoa watendaji wabovu wa sekta ya ardhi Mkoani Lindi akisema kuwa wapo watanzania wengi wenye uwezo wa kufanya kazi zao. Alisema kuwa hayuko tayari kuyumbisha kiti chake alichoaminiwa na Rais kwa kuwalea watendaji wazembe.
New Picture (6)
Sehemu ya umati wa wananchi waliofika eneo la Mitwero kuwasilisha kero zao kwa Waziri William Lukuvi. Malalamiko mengi ya wananchi yanatokana na kutokushirikishwa katika uthamini wa ardhi na mali yao hali ambayo imewafanya kupunjwa malipo ya fidia. Waziri Lukuvi ameagiza wanaothamini mali ya wananchi kote nchini kufanya kazi hiyo kwa uaminifu na kuwashirikisha wananchi hao katika hatua zote ili kuondoa malalamiko na kutenda haki.
New Picture (7)
Waziri Lukuvi akimhoji Mpima ardhi wa Manispaa ya  Lindi Bw. Mpoki baada ya kulalamikiwa na wananchi wengi kuwa anatabia ya kuomba rushwa ili kuwapa huduma wananchi. Waziri Lukuvi ameapa kutomsamehe Afisa yeyote wa sekta ya Ardhi atakayetajwa na wananchi na kubainika kula rushwa na kwamba uchambuzi wa malalamiko ya wananchi ukikamilika ataanza kuchukua hatua za kinidhamu kwa watendaji wabovu na wala rushwa.
New Picture (8)
Mwananchi aliyebahatika kutoa dukuduku zake kwa Waziri Lukuvi akimuonyesha Afisa anayelalamikiwa kwa rushwa katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi eneo la Mitwero lililopo nje kidogo ya Manispaa ya Lindi.
New Picture (1)
Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mh. Mwantumu Mahiza atiktoa taarifa ya migogoro ya Ardhi ya Mkoa wa Lindi kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Vangimembe Lukuvi alipowasili Ofisini kwake.
New Picture (2)
Sehemu ya Watendaji wa Mkoa wa Lindi wakiwemo Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya wakimsikiliza Waziri Lukuvi(hayupo pichani) alipozungumza nao katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kusisitiza uadilifu katika sekta ya ardhi ili kuhudumia wananchi kwa haki na kuondoa kero za ardhi.
New Picture
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mh. William Vangimembe Lukuvi akiongea jambo na Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC Bw. Muungano Saguya alipowasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa LindI tayari kuanza kikao cha Watendaji wote wa Mkoa huo.
New Picture (5)
Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi akishangazwa na uamuzi wa Manispaa ya Lindi wa kupimiwa ardhi na UTT kwa gharama kubwa jambo ambalo wangelifanya wao ili kujenga uzoefu, kupata faida kubwa na kupunguza gharama ya kupima na hatimaye kuuza viwanja hivyo kwa wananchi. Ameagiza kupitiwa upya makubaliano waliyofanya na UTT ili kupata fedha za kuwaongeza fidia wananchi wanaolalamikia kupunjwa fidia eneo la Mitwero, nje kidogo ya Manispaa ya Lindi.
New Picture (9)
Wananchi kadhaa wakimpongeza Waziri Lukuvi kwa kuweza kutatua migogoro yao ya ardhi iliyodumu kwa miongo miwili na zaidi alipomaliza mkutano wa kuwasikiliza na kuagiza mambo mbalimbali ya kuondoa kero za wananchi.

SHIRIKA LA OXFAM LAKABIDHI VITUO VYA KUSINDIKA NA KUHIFADHI MAZIWA KWA WANAWAKE WA VIJIJI VINNE VYA WILAYA YA NGORONGORO

$
0
0
Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro John Kulwa Mgalula akikata utepe kama ishara ya kuzindua  rasmi kituo cha kuhifadhia na kusindika maziwa.
Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro John Kulwa Mgalula akijalibisha Jokofu linalotumia umeme wa jua wakati wa uzinduzi huo.
  Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro John Kulwa Mgalula wa kwanza kushoto akioneshwa baadhi ya vifaa ambavyo walikabidhiwa vituo hivyo na Shirika la Oxfam Tanzania.
Baadhi ya Wanakikundi cha NOSOTWA kutoka kijiji cha Engaresero.
Stellah Julius kutoka Oxfam akizungumza  na wanakikundi cha NOSOTWA kutoka kijiji cha Engaresero.
 Mwenyekiti wa kikundi cha NAPONU akishukuru Oxfam kwakujengewa kituo cha kisasa cha kuhifadhi na kusindika Maziwa.
 Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro John Kulwa Mgalula Wanakikundi cha NOSOTWA kutoka kijiji cha Engaresero.
 Miriam Lembilika akishukuru kwa kuletewa vituo hivyo kijijini kwao.
Wanakikundi cha NYUWAT kutoka kijiji cha MALAMBO wakifurahia jambo.
  Afya imezingatiwa hiki ni moja ya vyoo ambavyo vipo katika vituo hivyo.
Wanakikundi cha NAPONU kutoka kijiji cha PINYINYI.
 Picha ya pamoja na wanakikundi wa NYUWAT kutoka kijiji cha MALAMBO.


Shirika lisilo la Kiserikali la Oxfam hapo jana lilikabidhi vituo vya kusindika maziwa kwa wanawake wa vikundi vinne kutoka vijiji vya Engaresero, Pinyinyi, Malambo na Piyaya vilivyoko katika wilaya ya Ngorongoro.

Akipokea vituo hivyo kwa niaba ya wanavikundi hao, Mkurugenzi wa Wilaya ya Ngorongoro John Kulwa Mgalula, alisema ana imani vituo hivi vitawasaidia wanawake kukua kiuchumi na kuepuka kuwa tegemezi kwani wanawake wengi wamekuwa na sifa ya uvumilivu, uangalifu wa hali ya juu na kwamba mara nyingi wao hufanya vitu kwa uaminifu.

Mkurugenzi aliyashukuru mashirika ya Oxfam waliofadhili ujenzi wa vituo hivi pamoja na PALISEP waliotekeleza mradi huu kwa jitihada mbalimbali ambazo yamekuwa yakifanya katika wilaya ya Ngorongoro ili kuwakuza wanawake kiuchumi huku akitaja miradi mingine iliyofadhiliwa na Oxfam kuwa ni pamoja na ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula, ujenzi wa majosho, pamoja na ujenzi wa vyanzo vya maji.

Akikabidhi vituo hivyo, Stellah Julius kutoka Oxfam alisema, “Baada ya kufanya utafiti uliowashirikisha wanawake wa vijiji hivi vinne walituambia kwamba wanahitaji vituo vya kusindika na kuhifadhia maziwa. Tumewajengea vituo hivi mvitumie kwa maendeleo yenu.” Stellah pia aliipongeza serikali na wadau mbalimbali kwa kutoa ushirikano mkubwa uliopelekea kufanikisha ujenzi wa vituo hivyo ikiwemo kutoa maeneo ya ardhi ya vijiji hivyo vinne.

Aidha Stellah aliwataka wanavikundi hao kuwa wabunifu wa namna ya kujiendeleza kibiashara na kuepuka kutegemea mashirika na taasisi ambazo zipo kwa muda tu.

Naye Mkurugenzi wa shirika la PALISEP Robert Kamakia alisema shirika lake limewajengea uwezo wana vikundi hao kwa kuwapa mafunzo ya ujasiriamali na mbinu mbalimbali za kibiashara pamoja na kuwafundisha namna za kutunza maziwa kwa usafi.

Kwa upande wake Thomas Nade, Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Ngorongoro aliwataka wanavikundi hao kusajili vikundi vyao mapema ili vitambulike kisheria na waweze kunufaika kwa namna mbalimbali ikiwemo kupatiwa mikopo na kufungua akaunti ya benki.


Wanawake kutoka vijiji hivi vinne wanatarajia kunufaika kwa kujipatia kipato kutokana na kuuza maziwa na siagi.

Akionyesha furaha yake, Mariam Lembilika kutoka kijiji cha Malambo alisema, “Mimi kama mwanamke ambaye nina watoto watano na sina mume natarajia kutumia kipato kutokana na biashara hii kusomesha watoto.”

Naye Mary Saigulan kutoka kijiji cha Engaresero alisema, “Tutauza maziwa na siagi na kujipatia fedha nyingi ambazo zitatusaidia kuanzisha miradi mingine na kutuwezesha kujitegemea“

Ujenzi wa vituo hivi vinne umegharimu takribani shilingi za kitanzania milioni 120 na kila kimoja kina jokofu linalotumia umeme wa jua, mashine za  kusindika maziwa, madumu ya kuhifadhia maziwa, vipima joto, vipimo vya kupimia ubora wa maziwa, tenki la maji pamoja na mashimo mawili ya vyoo na bafu.

Vikundi hivyo vya NOSOTWA (Engaresero), NAPONU (Pinyinyi), NYUWAT (Malambo) na NASERIYAN (Piyaya) vina wana kikundi wapatao 30 kila kimoja.

AIRTEL YAZINDUA MICHUANO YA ARS 2015

$
0
0
 Mkurugenzi wa Idara Michezo Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
michezo Leonard Thadeo akipiga mpira kuashiria uzinduzi rasmi wa
Airtel Rising Star msimu wa tano. Hafla ya uzinduzi ilifanyika jijini
Dar es Salaam leo 17th June,2015.
 Mkurugenzi wa Idara Michezo Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na 
michezo Leonard Thadeo akiwa alama ya uzinduzi wa kampeni ya " Its
Now" yenye kuwawezesha vijana  kutimiza ndoto zao katika Nyanja
mbalimbali kama technologia, michezo na muziki. Wakishuhudia ni Rais
wa TFF Jamali Malinzi( kushoto) Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Bi
Beatrice Singano Malya (kulia) akifatiwa na mwenyekiti wa soka la
vijana Bwana Ayoub Nyenzi.

 Wachezaji wa Airtel Rising Star 2013 ambao sasa wanachezea timu ya

wanawake ya Taifa Twiga Stars wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa
uzinduzi wa program ya Airtel Rising Stars ya msimu wa 5 iliyofanyika
katika makao makuu ya ofisi za Airtel Tanzania


Akiongea na waandishi wa habari kwenye hafla ya uzinduzi jijini Dar es

Salaam, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano amesema kampuni ya Airtel Tanzania  ina nia thabiti ya kusaidia maendeleo ya mchezo wa mpira wa miguu hapa nchini na kujivunia mafanikio yaliyotokana na michuano hiyo kwa miaka minne iliyopita.

"Tunaona fahari kwamba michuano ya Airtel Rising Stars imeweza kuibua

vipaji vya wachezaji ambao baadhi yao wamechaguliwa kujiunga na timu
za taifa za vijana chini ya umri wa miaka 20", alisema Singano.

Kumbukumbu za TFF zinaonyesha kwamba timu ya taifa ya wanawake
imeundwa na wachezaji wengi kutoka Airtel Rising Stars ambayo
madhumuni yake makubwa ni kuibua na kuendeleza vipaji vya soka kwa
vijana wenye umri chini ya miaka 17.

Singano pia ametangaza kampuni ya Airtel kuingia mkataba na nahodha wa 
Ivory Coast na kiungo wa Manchester City Yaya Toure katika kampeni
mpya iitwayo  "It's Now" yenye lengo la kulea na kukuza vipaji barani
Afrika kupitia Nyanja mbalimbali kama vile michezo, ikijumuisha
mashindano ya Airtel Rising Stars kwa vijana chini ya umri wa miaka
17.


MATUKIO KATIKA PICHA KWENYE HAFLA YA KUMUAGA RAS TANGA NA KUMKARIBISHA RAS RUKWA KATIKA UKUMBI WA KANYAU SUMBAWANGA MJINI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akisalimiana na Aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa sasa Mkoa wa Tanga Alhaj Salum Chima  muda mfupi kabla ya kuanza kwa hafla ya kumuaga Ndugu Chima na kumkaribisha Ndugu Smythies Pangisa (katikati) aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara sasa Mkoa wa Rukwa. Hafla hiyo ilifanyika tarehe 13 Juni 2015 katika ukumbi wa Kanyau Sumbawanga Mkoani Rukwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya hafla hiyo ambaye pia ni Meneja wa SIDO Mkoa wa Rukwa Ndugu Martin Chang'a akitoa salam za utangulizi katika hafla hiyo.
Meza Kuu.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akizungumza katika hafla hiyo. Aliwaasa watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na ubunifu mkubwa na kwamba  ndiyo siri pekee ya mafanikio katika utendaji wao wa kazi.  
Katika hali isiyotegemewa na wengi Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Alhaj Salum Chima "Muagwa" alitoa zawadi ya machungwa kutoka Tanga ambayo yaligawiwa kwa washiriki wote wa hafla hiyo kama inavyoonekana pichani.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa katika hafla hiyo.
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa akizungumza katika hafla hiyo. Kabla ya hapo alikua Katibu Tawala Mkoa wa Mtwara.
Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Alhaj Salum Chima wa pili kushoto akionyesha umahiri wake wa kucheza ngoma ya kinyaturu na baadhi ya wanakikundi wa ngoma hiyo.
Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Alhaj Chima na Mkoa wa Rukwa Ndugu Pangisa wakipokea zawadi kutoka kwa Watumishi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa.
Washiriki wote katika hafla hiyo walipata fursa ya kupeana mikono na Makatibu Tawala hao wa Mkoa wa Tanga na Rukwa.
Watumishi waliofanya kazi kwa karibu zaidi na Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Alhaj Salum Chima wakikabidhi zawadi zao.
Picha ya Pamoja kati ya wageni wa meza kuu na wakuu wa idara Sekretarieti ya Mkoa wa Rukwa.

UDHIBITI WA KUCHEPUSHA DAWA ZA SERIKALI WAANZA KUTEKELEZWA

$
0
0
 Ofisa Uhusiano Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD), Bi Etty Kusiluka (kushoto), akizungumza na mwananchi Juma Nyingi aliyetembelea banda la MSD katika maonyesho hayo.
 Ofisa Uhusiano wa MSD, Benjamin Massangya (kulia), akimueleza mkazi wa Utete kutoka wilaya ya Rufiji, Omary Abdallah shughuli mbalimbali zinazofanywa na MSD baada ya kutembelea banda la MSD leo mchana.
 Vitanda vya hospitali vilivyopo katika banda la MSD.



Na Dotto Mwaibale

IDADI ya vidonge vinavyosambazwa na Bohari ya Dawa (MSD) ambavyo vimewekewa nembo ya Serikali (GOT)  imefikia 42 hadi sasa huku wazabuni wanaoshinda tenda kwaajili ya dawa na vifaa tiba vya MSD wakiendelea kuelekezwa kukidhi utaratibu huo wa kuweka nembo ya GOT ili kuepusha uchepushaji wa dawa za serikali.

Bohari ya Dawa ilianza utekelezaji huo wa uwekaji wa nembo ya GOT kwenye vidonge katika mwaka wa fedha uliopita, ambapo awali walikuwa wakiweka nembo ya MSD kwenye vifungashio tu, na kusababisha dawa hizo kuishia kuchepushwa.

Akizungumza wakati wa maonyesho ya Utumishi wa Umma, yanayofanyika jijini Dar es Salaam Ofisa Uhusiano Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Bi. Etty Kusiluka ameeleza kuwa  zaidi  ya vifaa tiba na dawa 650 za serikali  ambazo zinasambazwa na Bohari ya Dawa zinapaswa zote kuwa na nembo ya 
MSD na GOT, na zoezi hili litakamilika kadri wazabuni wanavyoendelea kupokea maelekezo.

Baadhi ya dawa ambazo tayari zina nembo hiyo ni pamoja na Mgnesium, Amoxicillin, Pracetamol, Diclofenac, Ciprofloxacin na Cotrimoxazole.

Katika hatua nyingine, Bi Kusiluka ameeleza kuwa Bohari ya Dawa (MSD) inaendelea na mipango ya kusogeza huduma karibu zaidi na mwananchi kwa kuanzisha huduma ya uuzaji wa dawa katika maeneo ya hospitali na karibu na maeneo yenye uhitaji wa dawa, ambapo mauzo hayo yatafanyika kwa saa 24. Huduma hizi zitaanza katika miji mikubwa nchini ambayo ni pamoja na Mbeya, Dar Es Salaam, Mwanza na Arusha. Mkoa wa Mbeya ndio utakuwa wa  kwanza kutoa huduma hizi, ambapo hadi sasa maandalizi yako katika  hatua za mwisho.


Maduka haya yataiongezea Bohari ya Dawa wigo wa utendaji wa utoaji huduma kwa wananchi, ambapo hadi sasa huduma ya usambazaji wa dawa na Vifaa tiba na vitendanishi vya maabara inatolewa kupitia mali inayohifadhiwa kwenye maghala ya MSD ya kanda zake nane zilizopo mikoa ya Mwanza, Tabora, Mtwara, Mbeya, Iringa, Dar Es Salaam, Dodoma na Moshi pamoja na vituo vyake viwili vya mauzo vya Muleba na Tanga. 

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KWA KUSHIRIKIANA NA ASASI ZA KIMATAIFA WILDAID, AFRICAN WILDLIFE FOUNDATION WAZINDUA KAMPENI YA KUPAMBA NA NA UJADILI WA TEMBO

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa kampeni mpya ya kupambana na ujangilli wa Tembo uliofanyika katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam Juni 18, 2015.
Balozi wa Mpya wa Kampeni ya Kupambana na Ujangili wa Tembo, Msanii wa mziki wa kizazi kipya Ali kiba akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa kampeni mpya ya kupambana na ujangilli wa Tembo uliofanyika katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam Juni 18, 2015.
Afisa Mtendaji Mkuu wa African Wildlife Foundation, Dk. Patrick Bergin akizungumza katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni ya sifa ya wanyamapori katika hotel ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam Juni 18, 2015.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Mussa Salum akizungumza na waandishi wa habari leo katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam Juni 18, 2015.
Balozi wa Mpya wa Kampeni ya Kupambana na Ujangili wa Tembo, Msanii Jacqueline Mengi kuhusiana na uzinduzi wa kampeni mpya ya kupambana na ujangilli wa Tembo uliofanyika katika hoteli ya Sea Cliff jijini Dar es Salaam Juni 18, 2015.
Balozi wa Mpya wa Kampeni ya Kupambana na Ujangili wa Tembo, Msanii wa mziki wa kizazi kipya Ali kiba akizungumza na waandishi wa habari.
 Viongozi wa Dini waliofika katika uzinduzi huo wakifuatilia kwa makini...
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu akizungumza na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaji Mussa Salum.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wa kampeni hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyarandu akiwa pamoja na Viongozi wa dini na mabalozi wa kampeni hiyo.
---
Lengo la WildAid ni kukomesha biashara haramu ya wanyama pori kwa kupunguza mahitaji ya bidhaa zitokanazo na wanyamapori kupitia kampeni za uhamasishaji. 
 Pia lengo la WildAid ni kutoa hifadhi na ulinzi wa uhakika kwa viumbe wa baharini. Biashara haramu ya wanyama pori inakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola bilioni 10 kila mwaka na imesababisha kupungua sana kwa wanyama pori sehemu mbalimbali duniani. 
Kama ilivyo biashara ya madawa ya kulevya, uwepo wa sheria dhidi ya biashara hiyo na jitihada za kuhakikisha utekelezaji wa sheria havijaweza kuleta ufumbuzi wa tatizo hili. Kila mwaka, mamia ya mamilioni ya dola hutumika kuwalinda wanyamapori, lakini kiasi kidogo kukomesha mahitaji ya viungo vya wanyama pori na bidhaa zitokanazo na wanyama pori. 
WildAid ndio shirika pekee ambalo limelenga kupunguza mahitaji kupitia ujumbe rahisi usemao: UNUNUZI UKIISHA, MAUAJI NAYO YATAISHA. WildAid inafanya kazi na mamia ya watu mashuhuri katika bara la Asia na nchi za Magharibi hususani wanasiasa mashuhuri, watu maarufu na viongozi wa makampuni makubwa wakiwemo Mrithi wa Ufalme wa Uingereza Prince William, Yao Ming, Jackie Chan, Li Bingbing na Sir Richard Branson ili kuwashawishi watu waache kununua bidhaa zitokanazo na wanyama walioko katika hatari ya kutoweka. Hivi sasa ujumbe huu na jitihada kuelimisha watu zinawafikia mamia ya mamilioni ya watu nchini China kila wiki kupitia matangazo mbalimbali.

LOWASSA AENDELEA KUSAKA WADHAMINI MKOANI KILIMANJARO LEO

$
0
0
 Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akipokea fomu za wanachama 33,780 wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, waliomdhani ili aweze kupata ridhaa ya Chama chake katika kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.
 Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akizungumza na Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro leo Juni 18, 2015, wakati shukrani kwa udhamini wa kishindo alioupata kutoka wa WanaCCM hao, ili aweze kupata ridhaa ya Chama chake katika kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amepata udhamini wa wanaCCM 33,780.



Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akipokea fomu za wanachama 33,780 wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, waliomdhani ili aweze kupata ridhaa ya Chama chake katika kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Anaekabidhi fomu hizo ni Katibu wa CCM Wilaya ya Moshi Mjini, Loth Ole Nesele.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI


Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akizungumza na Umati wa WanaCCM pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro leo Juni 18, 2015, wakati shukrani kwa udhamini wa kishindo alioupata kutoka wa WanaCCM hao, ili aweze kupata ridhaa ya Chama chake katika kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Mh. Lowassa amepata udhamini wa wanaCCM 33,780.

Umati wa wanaCCM wa Mkoa wa Kilimanjaro, ukimshangilia kwa furaha, Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa (hayupo pichani) wakati alipopanda jukwaani kuwashukuru wa kumdhamini kwa kishindo. Mh. Lowassa amepata udhamini wa wanaCCM 33,780.

Sehemu ya WanaCCM na wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro wakiwa wamefurika katika eneo la uwanja wa Ofisi ya CCM Mkoa huo wakifatilia kwa majini maelezo ya Mh. Edward Lowassa (hayupo pichani) wakati alipokuwa akitoa shukrani kwa udhamini wa kishindo alioupata leo Juni 18, 2015.
Mh. Lowassa akisomewa Dua na Sheikh wa mji wa Moshi mara baada ya kupewa udhamini wa Kishindo katika Safari yake ya Matumaini.

Mchungaji akitoa maombi.




Wadau wakipata taswira ya Mh. Lowassa wakati akiondoka kwenye Uwanja wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro.

Vijana wa CCM wa Mji wa Muheza wakiuongoza Msafara wa Mh. Lowassa kwenye eneo hilo la Muheza kwa lengo la kuzumza nao.
Vijana wa CCM Mji wa Muheza wakimshangilia Mh. Lowassa wakati walipomzimamisha ili aongee nao, alipokuwa safarini kuelekea Mkoani Kilimanjaro.
Ujumbe wa Vijana wa Muheza.
Ni furaha tupu.
Mh. Lowassa akiwasalimia wananchi wa Mji wa Muheza sambamba na kuwatakia Heri ya Mfungo Mtukufu wa Mwezi wa Ramadhani, wakati akiwa safarini kuelekea Mkoani Kilimanjaro kusaka wadhamini watakamuwezesha kupata ridhaa ya CCM kuwania Urais wa Tanzania kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Juni 18, 2015.
Baada ya kuwasalimia wanaCCM wa Mji wa Muheza, Mh. Lowassa alipata wasaa wa kwenda kuhani msiba wa Baba Mzazi wa Balozi wa Tanzania Nchini Zimbabwe, Mh. Adadi Rajab, Marehemu Mzee Rajab nyumbani kwao Muheza, Mkoani Tanga. anaezungumza na Mh. Lowassa ni Mama Mzazi wa Mh. Adadi Rajab, Bi. Fatuma Omar.
Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mh. Steven Ngonyani "Prof. Maji Marefu" (katikati) pamoja na wananchi wa Korogwe wakiwa wamefunga barabara kuuzuia msafara wa Mh. Lowassa ili aweze kuzungumza nao, huku wakimuuga mkono katika safari ya Matumaini.
Mh. Lowassa alishuka garini na kuungana na wananchi hao.
Mh. Lowassa akiwasalimia wananchi wa Mji wa Korogwe wakati akiwa safarini kuenekea Mkoani Kilimanjaro.
Shangwe tupu kwa wananchi wa Korogwe.
Kwaherini wana Korogwe.

Alipofika Mombo
Mh. Lowassa akikata nyama ya mbuzi katika moja ya Majiko eneo hilo la Mombo.
Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini, Mh. Steven Ngonyani "Prof. Maji Marefu" akitoa neno.
Mh. Lowassa akitoa neno la shukrani kwa wakazi wa Mombo.
Mh. Lowassa akiwasalimia WanaCCM na Wananchi wa mji wa Hedaru.
Same.

Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mmoja wa Wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonard Minja wakati alipofika kumpongeza kwa udhamini anaoendele kuupata.


SHIRIKA LA MADINI LA TAIFA (STAMICO), LAELEZEA MAFANIKIO YA MIRADI YAKE MBALIMBALI

$
0
0
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO),  Zena Kongoi (kulia), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, kwenye maonyesho ya wiki ya utumishi wa umma yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuhusu mafanikio yaliyofikiwa na shirika hilo katika miradi mbalimbali. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa Stamico, Deusdedith Magala.
Madini mbali mbali yaliyopo katika banda la shirika hilo.
Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa STAMICO, Deusdedith Magala (katikati), akizungumza na wanahabari kuhusu mikakati ya maendeleo ya miradi mbalimbali inayofanywa na Stamico.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO),  Zena Kongoi (wa pili kushoto), akiwa na viongozi wenzake. Kutoka kulia ni Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma, Koleta Njelekela, Mhandisi Migodi Mwandamizi, Ibrahim Dauda, Mjiofizikia, Denis Silas na Kaimu Mkurugenzi Rasilimali Watu na Utawala wa STAMICO, Deusdedith Magala.



Na Dotto Mwaibale

SHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limeanzisha miradi mbalimbali ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini ili kuwaendeleza kutoka katika uchimbaji duni usiozingatia kanuni.

Kuanzishwa kwa miradi hiyo kunatokana na wachimbaji hao kutokuwa na maeneo maalum ambapo  itawasaidia wachimbaji hao kufikia kiwango cha uchimbaji wa kati chenye tija, ambapo ni muendelezo wa mradi wa kuratibu na kuwaendeleza.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo maonesho ya wiki ya utumishi wa umma yanafanyika jijini Dar es Salaam leo mchana, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Zena Kongoi alisema shirika hilo limepata mafanikio mbalimbali katika kipindi cha mwaka 2014 hadi mwaka huu wa 2015.

Alisema kupitia mradi huo, shirika limeweza kuwawezesha wachimbaji wadogo wa madini ya bati wa Wilaya ya  Kyerwa kupata soko la madini hayo, jambo ambalo limesaidia kupunguza utoroshaji wake kwenda nchi jirani na kuiongezea serikali mapato.

"Tumewawezesha kwa kuwapa ushauri wa kitaalamu na kiufundi kwa wachimbaji wadogo mbalimbali. Lakini pia tunaelekea kukamilisha mchakato wa mfumo mtandao wa uchimbaji mdogo utakaowawezesha kupata taarifa sahihi na kwa wakati kuhusu masoko, bei n aina bora za vifaa vya uchimbaji na uchenjuaji," alisema.

Kongowi alisema kwenye mradi wa dhahabu unaosimamiwa na kampuni tanzu ya Stamigold Biharamulo Gold Mine, mgodi huo umeweza kuingiza Dola za Marekani milioni 14.2 katika kipindi cha Agosti, mwaka jana na Mei, mwaka huu.

Aliongeza kuwa mgodi huo pia umeanza kulipia ushuru wa huduma wa asilimia 0.3 kwa halmashauri ya Biharamulo na kuchangia pato la taifa kwa kurejesha mrahaba wa asilimia 4, ambapo wanatarajia kupata Sh. milioni 609 kama ada ya usimamizi wa mgodi huo.

Mbali na mafanikio hayo alisema zipo baadhi ya changamoto ambazo wanaendelea kuzishughulikia ambapo miongoni mwake ni upungufu wa mtaji kutokana na kuwa shirika hilo kwa sasa linafufua upya  miradi yake mingi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu, Deusdedith Magala alisema, kulingana na kauli mbiu ya mwaka huu ya maonesho hayo, shirika hilo linahakikisha linawasaidia akinamama kwa kuwatengezea mazingira mazuri ya kufanya kazi ndani ya shirika hilo.

Aliongeza kutokana na shirika hilo kuanza kazi upya katika kipindi cha mwaka jana walilazimika kuajiri wafanyakazi  wapya 87 ambapo wanawake ni 25 na wanaume 62 lengo likiwa ni kuwezesha shirika hilo kusonga mbele. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com simu namba-0712-727062)

RAIS WA ZANZIBAR DK.ALI MOHAMED SHEIN ACHUKUA FOMU MGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR.

$
0
0
1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akionesha mkoba wa wenye fomu kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar baada ya kukabidhiwa Fomu hizo katiuka Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo Juni 18,2015. [Picha na Ikulu.]
6
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipozungumza na  Viongozi wa Chama cha Mapinduzi waliofika katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo alipofika  kuchukua fomu za kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar,(kushoto)Mama Mwanamwema Shein na Makamu wa Pili wa Rais wa zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,(kulia)Mwenyekiti wa CCM Mkoa Kaskazini Unguja Haji Juma na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar VuaiAli Vuai.
7
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein  akionesha Fomu za kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar kwa Viongozi wa Chama cha Mapinduzi waliofika katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo Juni 18, 2015 alipokuwa akizungumza nao baada ya kuchukua fomi hizo (kushoto) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,(kulia) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar VuaiAli Vuai.

4
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi waliofika katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja wakisherehekea wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokwenda kuchukua fomu kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwanndui Mjini Unguja leo.
5
Viongozi wa Chama cha Mapinduzi waliofika katika ukumbi wa Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja wakimsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipozungumza nao baada ya kuchukua fomu za kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwanndui Mjini Unguja leo,
2
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono Wanachama wa CCM waliofika Viwanja vya Jengo la Ofisi ya CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo  wakati alipofika kuchukua fomu kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar akifuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein (kushoto),
3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar pia Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Balozi Seif Ali Iddi  wakati alipofika kuchukua fomu kuomba ridhaa kwa Chama cha Mapinduzi kumteuwa kuwa mgombea Urais wa Zanzibar katika Ofisi ya CCM Kisiwanndui Mjini Unguja leo,akifuatana na Mkewe Mama Mwanamwema Shein (kushoto.

MAKAMU WARAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA SIKU YA TABIANCHI AFRIKA CHUO KIKUU CHA UDSM.

$
0
0
01
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi Kongamano la Siku ya Tabianchi Afrika, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya. Kuongamano hilo lilifanyika jana Juni 17, 2015 kwenye Ukumbi wa Nkhurumah Chuo Kikuu Dar es Salaam, jana. Picha zote na OMR
05
Baadhi ya wadau na wanafunzi waliohudhuria Kongamano hilo,wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia.
02
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa watafiti wa Kituo cha ‘Center For Climate Changes Styles’, Khalid Mwakobaa (kulia) na Rdith Benedict, wakati alipotembelea katika Mabanda ya maonesho kwenye Kongamano la Siku ya Tabianchi Afrika, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya, lililofanyika kwenye Ukumbi wa Nkhurumah Chuo Kikuu Dar es Salaam, jana.
03   06
Makamu wa Rasi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na wanafunzi  wa Chuo Kikuu UDSM, baada ya kufungua Kongamano la Siku ya Tabianchi Afrika, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kushirikiana na Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya. Kuongamano hilo lilifanyika jana Juni 17, 2015 kwenye Ukumbi wa Nkhurumah Chuo Kikuu Dar es Salaam, jana.
07
Picha ya pamoja kwa kumbukumbu, baada ya ufunguzi wa Kongamano hilo.

CHIEF SECRETARY AMBASSADOR OMBENI SEFUE MEETS 21 YOUTHS WHO WILL ATTEND THE 2015 MANDELA WASHINGTON FELLOWSHIP FOR YOUNG AFRICANS PROGRAM IN THE US

$
0
0
 2
The Chief Secretary Ambassador Ombeni Sefue talks to 21 Tanzanian youngsters who fly to the US tonight for a six-week  2015 Mandela Washington Fellowship for Young Africans Program when they paid him courtesy call the State House in Dar es salaam today June 18, 20151
The Chief Secretary Ambassador Ombeni Sefue and Charge D’Affaires at the US Embassy in Dar es salaam Ms Virginia Blaser pose with 21 Tanzanian youngsters who fly to the US tonightfor a six-week  2015 Mandela Washington Fellowship for Young Africans Program when they paid him courtesy call the State House in Dar es salaam today June 18, 2015.

CRDB TAWI LA MERU WATEMBELEA KITUO CHA YATIMA ST JOSEPH CHA MOSHONO ARUSHA

$
0
0


 Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Meru jijini Arusha  Leonce Matley akikabidhi  misaada kwa Mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha St.Joseph Christina Mnate juzi walipotembelea kituo hicho na kutoa misaada ya chakula na vifaa vya shule katika kituo hicho kilichopo kata ya Moshono jijini Arusha ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Mtoto Afrika .
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Meru jijini Arusha  Leonce Matley akikabidhi  misaada kwa Mkurugenzi wa kituo cha watoto yatima cha St.Joseph Christina Mnate juzi walipotembelea kituo hicho na kutoa misaada ya chakula na vifaa vya shule katika kituo hicho kilichopo kata ya Moshono jijini Arusha ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya Mtoto Afrika .
******************
JUKUMU la malezi ya watoto yatima na waishio katika mazingira magumu nchini linapaswa kutekelezwa na kila mtanzania pamoja na tasisi mbalimbali nchini ili kupunguza wimbi la wananchi tegemezi.

Hayo yalisema na Meneja wa Benki ya CRDb tawi la Meru, Leonce Matley, wakati wa kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali katika kituo cha watoto yatima na waishio katika mazingira magumu cha St.Joseph kilichopo Kata ya Moshono jijini Arusha. 

“Malezi ya watoto hawa yatima ni jukumu letu sote kama  watanzania  kuhakikisha kuwa tunawasaidia watoto yatima na wanaoishi mazingira magumu ili waweze kupata elimu bora itakayowakomboa kimaisha,” alisema Matley.

CRDB ilitembelea kituo hicho ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika iliyoadhimishwa dunai kote hivi karibuni ambapo wafanyakazi wa benki walipata wasaa wa kufurahi na watoto hao pamoja na kutoa misaada ya vyakula na vifaa vya shule katika kituo hicho ikiwa ni njia mojawapo kuwezesha upatikanaji wa mahitaji ya watoto yatima.

Aidha Matley amezitaka taasisi mbalimbali zilizopo nchini na asasi za kiraia kujaribu kujitoa kwa moyo kusaidia kundi hili la jamii ambalo likipata makuzi mazuri na salama litaweza kujiongoza lenyewe hapo baadae pasipo misaada zaidi hasa wakipatiwa mazingira mazuri ya kupata elimu.

Nae Mkurugenzi wa Kituo cha watoto yatima cha St.Joseph, Sister Mary Mushi  ametoa shukrani kwa uongozi wa benki hiyo kwa msaada walioupata na kutaka kuendelea kufanya hivyo kila wapatapo nafsi kwani huwapa faraja watoto hao.

“Nijambo la kumshukuru Mungu kwa moyo aliowapa wa kijitolea na kutukumbuka, na hili jamii isiyaachie tu makampuni kama CRDB bali hata mtu mmoja mmoja anaweza kuwasaidia yatima hawana kuwapa malezi bora badala ya kuwaachia wageni kutoka nchi za nje  ili kujenga taifa imara,”alisema Sister Mushi.

Siku ya Mtoto Afrika huadhimishwa kila mwaka June 16 katika nchi za Afrika huku Changamoto kubwa ya ongezeko la watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu ikiongezeka kutokana na mimba za utotoni.

ZIMBABWE TOURISM ON THE RIGHT TRACK

$
0
0
IMG_3864
Chief Executive of Zimbabwe Tourism Authority (ZTA), Karikoga Kaseke (Centre) briefing the International buyers who are attending the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo which is taking place in Harare International Conference Centre. Others from left is Mr. Wengayi Nhau the Representative from Zimbabwe Council for Tourism (ZCT ) , Executive Director Destination Marketing, Mr. Manjengwa Jefferies, Chief Operating Officer, Mr. Givemore Chidzidzi and Head of Africa & Middle East of Zimbabwe Tourism Authority, Ms. Praise Gurumani Mazhandu.(All photos by Zainul Mzige of modewjiblog)

By modewjiblog team, Harare
The Zimbabwe Tourism Authority (ZTA) has a mandate of marketing Zimbabwe as a tourism destination boasts its success in the tourism industry, by saying that last year the sector contributed 11 percent of the GDP.
On top of that the Authority has confidence that by the year 2020 they will be contributing 15 percent.

Speaking to Tanzanians journalists who are visiting Sanganai/ Hlanganani World tourism Expo, Chief Executive of Zimbabwe Tourism Authority, Karikoge Kaseke said Zimbabwe tourist industry employs 13 percent of the formal sector. He also said 86 percent of the tourists are coming from Africa and 14 outside Africa.

He said despite these successes, the nation believes regional integrations rather than each one going of their own.He said nothing could unite blacks rather than tourism industry hence there is a need to work together to bring tourism to another height. He said this expo will be a great way to advertise tourism and that his country for many years have been involved in many other expo taking place in Tanzania, Kenya and South Africa also as a part of strengthening cooperation in the sector.


The Chief Executive said he was happy to see Tanzanians especially journalists who have joined this initiative to promote tourism sector.
Tanzanian journalists featured in the expo include those from Daily News, The Africans, The Guardian, East African Business week and Modewjiblog.
IMG_3868
Above and below: International buyers who attended the briefing at the Harare International Conference Centre listening attentively.
The journalists are in Zimbabwe in response to invitation from Zimbabwe Tourism Authority, a trip which was sponsored by Fastjet Airline who are planning to extend their wings to Zimbabwe
The 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo was held from 18 – 20 June 2015 at the Harare International Conference Centre, with the target of meeting the ever-changing needs of the dynamic tourism sector.
According to the Authority there has been a big improvement for the 8th edition with 110 buyers and 27 media compared to 66 buyers and 10 international media hosted in 2014
“Despite the fact that the planning period was very limited due to the shift of dates to the first half of the year we have witnessed a great response” he said.
Speaking about the challenges they have encountered during the preparations he said inadequate of fund which remains a crippling factor for the growth of the event.
IMG_3869
IMG_3874
IMG_3884
IMG_3898
Tanzania based journalist who writes for the Guardian News paper, Frank Aman Interviewing Zimbabwe Tourism Authority Chief Executive Officer, Karikoga Kaseke (left) during the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo at the Harare International Conference Centre. At the centre is another Tanzanian Journalist working with East Africa Business Week, Timothy Kitundu.
IMG_3897
Zimbabwe Tourism Authority (ZTA), Chief Executive, Karikoga Kaseke exchanging ideas with participants at the 8th edition of the Sanganai/Hlanganani–World Tourism Expo which is taking place at the Harare International Conference Centre in Zimbabwe.

KIONGOZI WA CHAMA CHA ACT WAZALENDO ZITTO KABWE APATA MAPOKEZI MAKUBWA MJINI KIGOMA

$
0
0
1
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akiwapungia mkono wakazi wa mji wa Kigoma jana wakati akiwasili kabla ya kufanya mkutano wahadhara wa kutambulisha viongozi wa chama hicho.
5
Mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghwira, akiwapungia mkono wakazi wa mji wa Kigoma jana wakati akiwasili kabla ya kufanya mkutano wahadhara wa kutambulisha viongozi wa chama hicho.
6
7
Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, akicheza wimbo wa chama ulioimbwa na msanii, Baba Levo, wakati wa mkutano wahadhara mjini Kigoma jana.
2
Baadhi ya wakazi wa mji wa Kigoma wakifuatilia mkutano wa hadhara wa chama cha ACT Wazalendo mjini Kigoma jana.
34

KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA AWATAKA VIJANA WACHAPE KAZI NA SI KUKAA VIJIWENI.

$
0
0

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiswaga Ng'ombe kuingia kwenye josho katika kijiji cha Nyakwasi, Nyang'hwale mkoani Geita.Kinana aliwapongeza wana kikundi cha Songambele kwa kupambana na magonjwa ya mifugo kwa kujenga josho la kisasa,Pia Ndugu Kinana aliwaasa Vijana kufanya kazi kwa bidii n,a kuacha kukaa vijiweni kupiga sogakwani hakuna njia ya mkato ya maisha,badala yake ni kufanya kazi kwa bidii ikiwemo suala zima la kujiletea maendeleo kama vile kujishughulisha na ufugaji,ukulima ili kujikwamua na Maisha,Kinana akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  yupo mkoani Geita akitokea mkoani Kagera katika ziara ya Kuimarisha uhai wa chama,kukagua na kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2010-2015 pamoja na kusikiliza matatizo ya Wananchi na kuyatafutia ufumbuzi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakiangalia baadhi ya miradi ya akina mama wajasiliamali wa Nyang'hwale.
Katib Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwasha mashine ya kukoboa na kusaga,ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi huo wa akina mama Wajasiliamali,katika kijiji cha Nyamgogwa,wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kharuma ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa ili nchi isonge mbele inabidi matumizi yasiyo ya lazima yapunguzwe na vijana kuamini kuwa maisha ni kuchapa kazi na si kukaa vijiweni,aliwataka wananchi hao kuchagua viongozi wenye moyo na watu.
Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali akihutubia wakazi wa Kharumwa kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliokusanya wananchi wengi kuliko kawaida.
 Katibu wa Itikadi na Unezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kharumwa,wilaya ya Nyang'hwale na kuwaambia kuwa Kiongozi ni mtu mwenye moyo wa uvumilivu na usikivu, kiongozi wa siasa hapaswi kuwa na mashitaka ya kupiga watu.
 Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale akihutubia wananchi wa kaa ya Kharumwa waliojitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa michezo wa Kharumwa ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akifurahia jambo na Mwaandishi wa habari wa Magazeti ya Serikali (Daily News & Habari Leo),Bwa.Pius Lugonzibwa katika kijiji cha  Nyijundu,Wilayani Nyang'hwale mkoani Geita,alipokwenda kushiriki ujenzi wa vyumba vya madarasa vya shule ya sekondari ya Nyijundu.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa kata ya Nyijundu
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Nyijundu, wilaya ya Nywang'hwale mkoani Geita ambao kwa ushirikiano wa wananchi na Mbunge wao wameweza kujenga madarasa mengi ya shule ya sekondari ya kata ya Nyijundu.
Wananchi wa Kata ya Nyijundu wakinyoosha mikono juu kama ishara ya kukubali kazi inayofanywa na Chama cha Mapinduzi.
Diwani wa Kata ya Nyijundu Jacob Daniel Nyanda akizungumza na wakazi wa kata yake na kutoa shukrani kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa kutembelea na kujionea ujenzi wa shule ya sekondari.Nyijundu, wilaya ya Nyang'hwale ,Geita.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (katikati) akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali (kushoto) na M-NEC wa Nyang'hwale Mhe. James Musalika.
 Wananchi wa Kharumwa wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Kharuma,Wilayani  ya Nyang'hwale ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa ili nchi isonge mbele inabidi matumizi yasiyo ya lazima yapunguzwe,na pia vijana waamini kuwa maisha ni kuchapa kazi na si kukaa vijiweni,aliwataka wananchi hao kuchagua viongozi wenye moyo na watu.
 Wananchi wa kata ya Kharumwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali akiwatangazia wananchi wa kata ya kharumwa kuwa atagombea tena Ubunge wa jimbo hilo.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali wakati wa mapokezi katika kata ya Bukwimba wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishukuru kwa mapokezi mazuri kata ya Bukwimba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wakazi wa kata ya Bukwimba ikiwa sehemu ya ziara yake ya kujenga na kuimarisha Chama mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipaka rangi ukuta rangi jengo la ofisi ya chama kata ya Bukwimba,jengo hili lilijengwa mwaka 1966 na linatumika mpaka sasa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali(katikati) pamoja na Diwani kata ya Bukwimba na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale Mhe.Yavin Noah.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Nyakwasi wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.
 Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali akizungumza na Nyamgogwa kabla ya kuzindua mradi mashine za kukoboa mpunga na kusaga mahindi wa akina mama cha UWT ambacho kina wanachama 100 .


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali wakati wa mapokezi katika kata ya Bukwimba wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishukuru kwa mapokezi mazuri kata ya Bukwimba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wakazi wa kata ya Bukwimba ikiwa sehemu ya ziara yake ya kujenga na kuimarisha Chama mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipaka rangi ukuta rangi jengo la ofisi ya chama kata ya Bukwimba,jengo hili lilijengwa mwaka 1966 na linatumika mpaka sasa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali(katikati) pamoja na Diwani kata ya Bukwimba na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale Mhe.Yavin Noah.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Nyakwasi wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiswaga Ng'ombe kuingia kwenye josho katika kijiji cha Nyakwasi, Nyang'hwale mkoani Geita.Kinana aliwapongeza wana kikundi cha Songambele kwa kupambana na magonjwa ya mifugo kwa na josho la kisasa,Pia Ndugu Kinana aliwaasa Vijana kufanya kazi kwa bidii kwani hakuna njia ya mkato ya maisha,badala yake ni kufaanya kazi kwa bidii ikiwemo suala ziama la kujiletea maendeleo kama vile ufugaji,ukulima ili kujikwamua na Maisha,Lakini.Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwa ameambatana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye  yupo mkoani Geita akitokea mkoani Kagera katika ziara ya Kuimarisha uhai wa chama,kukagua na kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2010-2015 pamoja na kusikiliza matatizo ya Wananchi na kuyatafutia ufumbuzi
 Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali akizungumza na Nyamgogwa kabla ya kuzindua mradi mashine za kukoboa mpunga na kusaga mahindi wa akina mama cha UWT ambacho kina wanachama 100 .
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakiangalia baadhi ya miradi ya akina mama wajasiliamali wa Nyang'hwale.
Katib Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiwasha mashine ya kukoboa na kusaga,ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi huo wa akina mama Wajasiliamali,katika kijiji cha Nyamgogwa,wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akifurahia jambo na Mwaandishi wa habari wa Magazeti ya Serikali (Daily News & Habari Leo),Bwa.Pius Lugonzibwa katika kijiji cha  Nyijundu,Wilayani Nyang'hwale mkoani Geita,alipokwenda kushiriki ujenzi wa vyumba vya madarasa vya shule ya sekondari ya Nyijundu.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa kata ya Nyijundu
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Nyijundu, wilaya ya Nywang'hwale mkoani Geita ambao kwa ushirikiano wa wananchi na Mbunge wao wameweza kujenga madarasa mengi ya shule ya sekondari ya kata ya Nyijundu.
Wananchi wa Kata ya Nyijundu wakinyoosha mikono juu kama ishara ya kukubali kazi inayofanywa na Chama cha Mapinduzi.
Diwani wa Kata ya Nyijundu Jacob Daniel Nyanda akizungumza na wakazi wa kata yake na kutoa shukrani kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa kutembelea na kujionea ujenzi wa shule ya sekondari.Nyijundu, wilaya ya Nyang'hwale ,Geita.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (katikati) akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali (kushoto) na M-NEC wa Nyang'hwale Mhe. James Musalika.
 Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Nyang'hwale akihutubia wananchi wa kaa ya Kharumwa waliojitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa michezo wa Kharumwa ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Wananchi wa Kharumwa wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
 Katibu wa Itikadi na Unezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Kharumwa,wilaya ya Nyang'hwale na kuwaambia kuwa Kiongozi ni mtu mwenye moyo wa uvumilivu na usikivu, kiongozi wa siasa hapaswi kuwa na mashitaka ya kupiga watu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wakazi wa Kharuma,Wilayani  ya Nyang'hwale ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa ili nchi isonge mbele inabidi matumizi yasiyo ya lazima yapunguzwe na vijana kuami kuwa maisha ni kuchapa kazi na si kukaa vijiweni,aliwataka wananchi hao kuchagua viongozi wenye moyo na watu.
 Wananchi wa kata ya Kharumwa wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Kharuma ambapo aliwaambia wananchi hao kuwa ili nchi isonge mbele inabidi matumizi yasiyo ya lazima yapunguzwe na vijana kuamini kuwa maisha ni kuchapa kazi na si kukaa vijiweni,aliwataka wananchi hao kuchagua viongozi wenye moyo na watu.
Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amaliakihutubia wakazi wa Kharumwa kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliokusanya wananchi wengi kuliko kawaida.
Mbunge wa Jimbo la Nyang'hwale Mhe.Hussein Nassoro Amali akiwatangazia wananchi wa kata ya kharumwa kuwa atagombea tena Ubunge wa jimbo hilo.

Rais Kikwete akutana na Watanzania waishio India na Wawekezaji

$
0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa ubalozi wa Tanzania nchini India na familia zao jana muda mfupi baada ya kuzungumza nao katika hoteli ya Taj Mahal Palace jijini New Delhi India ambapo yuko kwa ziara ya kiserikali.Walioketi mbele kutoka kushoto ni baadhi ya mawaziri anaofuatana nao katika ziara hii.Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa mambo ya Nje Mahadhi Juma Maalim, watatu kushoto ni Waziri wa Maji Prof.Jumanne Maghembe,watatu kulia ni Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Zanzibar Haji Omar Kheri,Wanne kulia ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dr.Abdallah Kigoda, na wapili kulia ni Mbunge wa Nzega Said Nkumba.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na wafanyabiashara wa India wenye viwanda ambao wamewekeza nchini Tanzania muda mfupi baada ya kukutana nao leo. Picha na Freddy Maro

Article 24

MAMIA WAFURIKA BANDA LA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA (NHIF), KUPIMA AFYA ZAO KATIKA MAONYESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR

$
0
0
Ofisa Uratibu na Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Genoveva Vicent (kulia), akimuelekeza jambo mwananchi aliyetembelea banda la NHIF katika maonyesho ya wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea viwanja vya Manazi Mmoja Dar es Salaam jana. Wengine wa pili kushoto ni Ofisa wa NHIF, Ambrose Manyanda na Ofisa Mawasiliano wa NHIF, Luhende Singu.
Ofisa wa NHIF, Ambrose Manyanda (kulia), akimuelekeza jambo mwananchi aliyetembelea banda la NHIF.
Mtaalamu wa Maabara wa Hospitali ya Amana, Johnbosco Kishebuka (kushoto), akimpima urefu mwananchi aliyefika katika banda la NHIF kabla ya kufanyiwa vipimo vingine.
Mwanahabari Beatrice Mbwambo (kulia), ni miongoni mwa wananchi waliojitokeza kupima afya yake katika banda la NHIF ambapo huduma hiyo ya kupima ugonjwa wa kisukari, shinikizo la damu na , saratani ya matiti.
Ofisa wa NHIF (kushoto), akitoa maelekezo kwa wananchi waliofika kwenye banda la NHIF.
Ofisa Mawasiliano wa NHIF, Luhende Singu (katikati), akiwakaribisha wananchi waliotembelea banda la NHIF.
Wananchi waliotembelea banda la NHIF wakipata maelezo mbalimbali kutoka kwa maofisa wa NHIF.
Wananchi wakiwa wamefurika banda la NHIF kwa ajili ya kupata huduma za kupima afya zao.
Wadau mbalimbali wakisubiri kupata vipimo katika banda la NHIF. 

KAMPUNI YA SIMU YA TIGO YATOA DOLA ZA MAREKANI 150,000 KWA HOSPITALI YA CCBRT KUSAIDIA WATOTO WENYE MIGUU ILIYOPINDA

$
0
0
 Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez  (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana wakati wa hafla fupi ya kutiliana saini mkataba wa kusisaidia Hospitali hiyo. Kutoka kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans na Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute. 
 Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT, Erwin Telemans akizungumza katika hafla hiyo.
 Meneja  Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (wa pili kushoto), akibadilishana hati na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Hospitali ya CCBRT baada ya kutiliana saini mkataba wa kusaidi matibabu ya ulemavu wa miguu Dar es Salaam jana. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Mifupa wa Hospitali hiyo, Prosper Alute na Meneja Uwajibikaji kwa Jamii, Woinde Shisael.
 Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, John Wanyanja (kushoto), akizungumza katika hafla hiyo.

 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
 Picha mbalimbali zikionesha miguu iliyopinda.
 Wanahabari wakiwa kwenye hafla hiyo.
Joyce Moshi akiwa amembeba mtoto wake Gedion ambaye anatibiwa katika Hospitali hiyo kutokana na miguu yake kupinda ambapo sasa anaendelea vizuri.

Na Dotto Mwaibale
HOSPITALI ya CCBRT, imepokea dola 150,000 (zaidi ya sh. mil. 320) kutoka kwa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo kwa ajili ya kugharamia matibabu ya watototo wanaozaliwa na ulemavu wa nyayo zilizopinda kwa miaka mitatu ijayo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema hiyo si mara ya kwanza kwa kampuni hiyo kugharamia matibabu ya walewavu kwani miaka mitatu iliyopita pia waligharamia matibabu ya watoto wenye ulemavu wa midomo.

"Tuna amini watoto wenye ulemavu wa unyayo uliopinda watapatiwa matibabu mapema, hivyo tunaomba wazazi wenye watoto wao wanaozaliwa na ulemavu huo kujitokeza CCBRT kupatiwa matibabu kwani ni bure na kwa mwaka tunatoa dola 500," alisema Gutierrez.

Kwa upande wa Daktari wa Mifupa wa hospitali hiyo, Prosper Alute akizungumzia ugonjwa huo, alisema unasababishwa na kurithi kutoka kwa wazazi au ndugu na kunywa pombe kupindukia au kutumia dawa zenye viambata kali.

Alisema asilimia 50 ya watoto wanaozaliwa hupata ugonjwa huo kwa miguu yote ambapo tangu kuingia kwa mwaka huu hadi Aprili, watoto 117 wamegundulika kuwa na ugonjwa huo ambao ni sawa na wastani wa watoto 10 kwa wiki.

Alisema ugonjwa huo usipotibiwa kwa haraka unaweza kumsababishia mtoto kutembea kwa shida na wakati mwingine kutotembea kabisa.

Kwa upande wa Joyce Mosha, Mkazi wa Mwenge,  ni mmoja wa wazazi ambaye mtoto wake, Gidion ana miezi miwili alikutwa na tatizo hilo na kufanyiwa upasuaji, alisema mara baada ya kujifungua madaktari waligundua mtoto wake kuwa na tatizo hilo, hivyo waliamua aanze kupatiwa matibabu.

"Namshukuru Mungu alifanyiwa upasuaji mdogo na hivi sasa anaendelea vizuri, alipogunduliwa ana tatizo hilo kwanza walimfunga plasta ngumu (POP) kwa wiki tano na kisha kumfanyia upasuaji mdogo wa mfupa na kumpa viatu maalumu vya kuvaa na vingine huwa anavaa usiku tu wakati wa kulala," alitoa ushuhuda Joyce.
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>