Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

PROFESA MARK MWANDOSYA AENDELEA KUSAKA WADHAMINI MKOANI KILIMANJARO

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama akisalimiana na Waziri wa nchi,Ofisi ya Rais(Kazi Maalum) Prof,Mark Mwandosya mara baada ya kufika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Kilimanjaro wakati akiwa njiani kutafuta wadhamini.
Prof,Mwandosya akiteta jambo na RC Gama mara baada ya kukutana.
Prof,Mark Mwandosya akisalimiana na Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Makazi ,Angela Kairuki walipokutana katika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Kilimanjaro.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro akimpatia kipaza sauti Prof Mwandosya asalimie wajumbe waliokuwa katika ukumbi huo.
Profesa Mwandosya akizungumza katika ukumbi huo.
Prof Mwandosya akitoka katika ukumbi wa mikutano wa mkoa wa Kilimanjaromara bada ya kusalimia.
Prof,Mwandosya akiagana na mkuu wamkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama mara baada ya kusalimia .
Prof,Mark Mwandosya akiondoka ukumbini hapo kuendelea na safari ya kusaka wadhamini mkoani Arusha. Na Dixo Busagaga wa Globu ya Jamii kanda ya Kaskazini.

RAIS KIKWETE: SERA YA NJE ITABAKIA ILE ILE

$
0
0
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Rais wa Visiwa vya Comoro baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Waziri wa Nchi (OR) Ikulu na utawala bora DrMwinyihaji Makame Mwadini Zanzibar akisalimiana na katibu Mtendaji wa SADC Dkt.Stergomena Tax wakati wakisubiri Rais Jakaya Mrisho Kikwete ahutubie na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Mamia ya wanahabari wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015  kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Brigedia Jenerali Sara Thomas Rwambali, Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Afrika katika Sudan ya Kusini akiwa kwenye kwenye Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015  kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
Shehemu ya wajumbe wa  Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015  kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
 Wajumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa Jumapili June 14, 2015  kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mwenyekiti wa AU Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na rais Yoweri Museveni wa Uganda baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais wa Somalia  Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wajumbe mbalimbali baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Waziri Mkuu wa Misri Mhe Ibrahim Mahlab baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mfalme Mswati wa Swaziland baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mjumbe maalumu wa Marekani katika Mazia Makuu  baada ya kuhutubia  na  kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika Jumapili June 14, 2015 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 


Rais Kikwete: Sera ya Nje itabakia ile ile
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa siasa ya nchi za nje na misingi mikuu ya kuongoza mahusiano ya Tanzania na nchi za kigeni hayatabadilika hata baada ya yeye kuondoka madarakani mwanzoni mwa Novemba, mwaka huu, 2015.

Aidha, Rais Kikwete amewahakikishia viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kuwa yeye anaondoka madarakani lakini Tanzania waliyoizoea na kuijua itabakia pale pale na kuwaomba viongozi hao kumpa ushirikiano mkubwa mrithi wake kama walimpa yeye.

Rais Kikwete ametoa uhakikisho huo mara mbili leo, Jumapili, Juni 14, 2015, wakati alipohutubia kuwaaga wakuu wenzake wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) wakati wa Mkutano wa 25 wa Kawaida wa Umoja wa Afrika uliofunguliwa leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Sandton Convention mjini Johannesburg, Afrika Kusini. 

Wakati wa mkutano ujao wa kawaida wa AU mjini Addis Ababa, Ethiopia, Januari, mwakani, Tanzania itakuwa na Rais mpya, Rais wa Tano.

Aidha, Rais Kikwete amerudia kauli na msimamo huo wa Tanzania wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Somalia, Mheshimiwa Hassan Sheikh Mahmoud ambako kiongozi huyo wa Somalia amemjulisha Rais Kikwete kuwa angependa kutembelea Tanzania baadaye mwaka huu.

Alisema Rais Kikwete kuwa misingi ya siasa za nchi za nje za Tanzania na misingi mikuu ya kuongoza mahusiano yake na nchi za nje yaliwekwa tokea Uhuru na hasa tangu kutungwa wa Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania mwaka 1972 na tokea wakati huo hajapata kubadilika kama kama wamebadilika viongozi mara nne sasa.

“Hatujapata kubadilisha misingi hiyo inayoelekeza kuwa mahusiano yatajengwa kuanzia nchi za jirani, zikifuatiwa na nchi za Afrika, nchi marafiki duniani na nchi nyinginezo.”

“Sina shaka kabisa kuwa misingi ya siasa za nje na misingi  mikuu ya uongozi wan chi yetu itabakia ile ile isipokuwa kama Rais ajaye atatoka chama kingine. Kitakachobadilika ni staili ya uongozi tu lakini misingi ya uongozi itabadilia pale pale kwa sababu ni misingi mizuri, ni misingi ya busara ambayo imeongoza nchi yetu vizuri kwa miaka mingi.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Ni matumaini yangu kuwa Watanzania tutachagua kiongozi mzuri atakayeendela kutoa kipaumbele cha juu kwa masuala ya Afrika pamoja na uanachama na ushiriki wetu katika Umoja wa Afrika. Haya ni miongoni mwa misingi mikuu ya Sera ya Mambo ya Nje ya Tanzania tangu uhuru mpaka sasa. Nawaomba mumpe ushirikiano mkubwa kama mliopnipatia mimi na hata kuzidi.”

MASHINDANO YA MTEMVU CUP YAFIKIA TAMATI, KATA YA 14 YAIBUKA KIDEDEA

$
0
0
Nahodha wa Timu ya Kata 14,Uhuru Selemani akiwa ameinua kombe baada ya kukabidhiwa na mgeni rasmi Waziri wa Habari  Vijana Utamaduni na Michezo, Dk.Fenellah Mukangala baada ya kuibuka washindi.
Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akiwa na Waziri wa Habari  Vijana Utamaduni na Michezo, Dk.Fenellah Mukangala (kulia) aliyekuwa mgeni rasmi katika fainali za mashindano ya Mtemvu CUP yaliyofikia tamati viwanja vya Mwembe Yanga Dar es Salaam jana. Timu zilizoingia ingia fainali hiyo ni Miburani Kata ya 15 na Kata ya 14 ambayo iliibuka kidedea kwa ushindi wa bao 1-0.
Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akiwa na Waziri wa Habari  Vijana Utamaduni na Michezo, Dk.Fenellah Mukangala (kulia), wakati akizungumza na wananchi baada ya kumalizi kwa fainali hizo.
Mashabiki wakiwa kwenye fainali hizo.


Mchuano ukiendelea.
Hapa ni kazi tu kwa kwenda mbele.

Vikombe na mipira vilivyotolewa kwa washindi.
Waratibu wa mashindano hayo yaliyohusisha kata zote za wilaya hiyo wakiwa kwenye fainali hizo.

Na Mwandishi wetu

BAADHI ya wadau wa mpira wa miguu nchini wameiomba serikali kumpa ushirikiano  Mbunge wa Jimbo la Temeke Abbas Mtemvu kufuatia kuanzisha michuano ya soka kwakuwa anatambua umuhimu wa vijana kuendelezwa.

Hayo yalisemwa jana na wadau hao mada baada ya mchezo wa fainali ya ya kombe la Mbunge wa Temeke, Mtemvu Cup ikiwa ni muda mfupi baada ya    Waziri wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Dk. Fenellah Mukangala   alipokuwa akikabidhi zawadi za washindi wa kombe hilo la Mbunge wa jimbo la Temeke  ambapo timu ya Temeke Kata ya 14 ilifanikiwa kuibuka mshindi wa kombe hilo na kupatiwa kikombe na pesa tasilimu sh. mil 1.5 huku Miburani Kata 15 wakiambuliwa sh mil 1 na kikombe kama washindi wa pili na nafasi ya tatu ilichukuliwa na timu ya Kilakala ambayo ilipatiwa sh 750,000 na kikombe kama mshindi wa tatu.


Mukangala aliwaomba madiwani wa Manispaa ya Temeke kufanya jitihada za kuujenga Uwanja wa Mwembe Yanga kuwa wakisasa zaidi ili utumike kwa ajili ya kupata vipaji vya michezo vya vijana wa manispaa hiyo pia kuwaingizia kipato kutokana na viingilio.


Wakizungumza Dar es salaam jana wadau  huyo alisema kuwa Mtemvu ni  kiongozi anayeendeleza michezo nchini hivyo vijana watumie fursa hiyo.


Walisema kuwa michezo ni moja ya sera ya kutoa ajira kwa vijana ambao wameamua kujiajiri kupitia michezo hivyo kuna haja ya vijana kutambua jitihada hizo.


Hata hivyo wadau hao wamekiri kuwa serikali ya awamu ya nne ndiyo serikali iliyochangia kukuza michezo nchini.


Mbunge wa Jimbo hilo, Abbas Mtemvu ameahidi kuendelea kuwekeza nguvu zake zote katika michezo ili kupata vipaji ambayo vitaitangaza nchini kimataifa.



"N ahidi kuendelea kukuza vipaji vya vijana,kwakuamua kuendeleza na kukuza soka ili tanzania iwe kujulikana zaidi nje na "alisema.

Alisema ataendeleza mashindano hayo hata kama hatachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo. 

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI, PAUL MAKONDA, AONGOZA MAMIA MAZISHI YA BABA YAKE MSANII STEVE MENGERE

$
0
0
 Marehemu Francis Festus Mengele, enzi za uhai wake.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu Francis Festus Mengele.
 Shangazi wa Msanii, Steve Nyerere, Grace Mengele (katikati), akiwa na wadogo zake Steve Nyerere wakati akiwasili makaburi ya Kinondoni kwa mazishi ya mpendwa wao, Francis Mengele.
 Watoto wa marehemu na dada zake wakiwa kwenye ibada ya maziko makaburi ya Kinondoni.
 Ibada ya maziko ikiendelea.
 Hali ilivyokuwa wakati wa mazishi.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Francis Mengele 
likishushwa kaburini.
  Jeneza lenye mwili wa marehemu Francis Mengele 
likishushwa kaburini.
 Wasanii mbalimbali wakiwa kwenye mazishi hayo.
 Ni huzuni tupu.
 DC Makonda akiwa udongo kwenye kaburi la Francis Mengele wakati wa mazishi.
 Kaburi likijengwe baada ya kuwekwa mwili wa marehemu kaburini.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa marehemu Francis Mengele.
 Waombolezaji wakiwasili makaburi ya Kinondoni tayari 
kwa mazishi.
 Hali ilivyokuwa makaburini.
 Hali ilivyokuwa makaburini.

Wasanii  mbalimbali wakiwa kwenye maziko hayo.

Na Dotto Mwaibale
WASANII mbalimbali wa filamu na bongo fleva  wamejitokeza kwa wingi katika mazishi ya baba ya msanii mwenzao Steve Mengele 'Steve Nyerere, aliyofanyika juzi makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Msanii Jacob Stephen JB ni miongoni mwa wasanii waliohudhuria mazishi ya marehemu Francis Mengele baba yake na msanii huyo aliyefariki wiki iliyopita kutokana na maradhi ya mapafu.


Wasanii wengine waliohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Micky, Vicent Kigosi 'Ray' Elizabeth Michael 'Lulu' Chuchu Hans, Kajala Masanja 'Kajala' , Mtunzi na muongozaji wa filamu Myovela Mswaisa na wengine wengi.


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda aliyeongoza mazishi hayo alisema kifo cha Mengele ni pigo kubwa katika wilaya hiyo ya Kinondoni na familia kwa ujumla.


"Mengele alikuwa na mchango mkubwa katika wilaya yetu ya Kinondoni katika kulipa kodi kutokana na biashara zake alizokuwa akizifanya na wingi huu wa watu waliojitokeza katika mazishi yake inaonesha jinsi alivyokuwa akishirikiana na wenzake hasa waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Kimara alikokuwa akisali" alisema Makonda.


Makonda alitumia fursa hiyo kuiomba Manispaa ya Kinondoni ndani ya miezi mitatu kuhakikisha inajenga choo katika makaburi hayo ya Kinondoni kwani ni aibu kwa eneo hilo kukosa choo hivyo kuwafanya wananchi wanaofika kwa ajili ya maziko kukosa huduma ya choo.

MWILI WA MUFTI KUSAFIRISHWA KESHO MKOANI SHINYANGA.

$
0
0
Mufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba enzi za uhai wake.
 Sehemu ya wanawake waliofika nyumbani kwa Marehemu  Mufti Alhaj Sheikh Shabaan Issa Bin Simba Mikocheni B jijini Dar es Salaam leo.
Sheikh  Mkoa wa Dar es Salaam,Alhaj Sheikh Alhad Mussa Salum akibadilishana na mawazo na Sheikh wa Mkoa wa Kigoma Hassan Kiburwa walipofika nyumbani kwa Marehemu Mufti ,Mikocheni B leo jijini Dar es Salaam .

Kulia ni Sheikh wa Mkowa Dar es Salaam,Alhaj Sheikh Alhad Mussa Salum akiwa na baadhi ya Masheikh waliofika Nyumbani kwa Marehen Mufti,Shabaan Issa Bin Simba Mikocheni B Jijini Dar es Salaam.(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA.)

Na Chalila Kibuda.
MWILI wa  Mufti ,Alhaj Sheikh Shaban Issa Bin Simba unatarajiwa kusafirishwa kesho mkoani Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata),Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam,Alhaj Mussa Salum amesema mwili wa marehemu utaswaliwa kesho katika Msikiti wa Msilimu ,viongozi mbalimbali wa dini na serikali watakuwepo.

Amesema marehemU alikuwa akisumbuliwa na sukari,Shinikizo la Damu (BP)  pamoja na Figo.

Hata hivyo amesema kuwa jana (Jumapili) Mufti alifanyiwa oparesheni ya figo katika Hospitali ya TM Jijini Dar es Salaam na Mauti ya Mufti yamekuta majira ya saa moja leo.

Salum amesema marehem anatarajiwa kuzikwa Alhamis mkoani Shinyanga.

PAMOJA NA KUKOSA TUNZO YA KILI KI MIZENGWE CHRISTIAN BELA APAGAWISHA TABORA!

$
0
0
Christian Bella akijimwaga jukwaani.
Masaa machache baada ya kukosa kitatanishi tunzo ya wimbo bora wa mwaka katika Kili Music Awards Christian Bela (King of melodies) alipagawisha wapenzi wa muziki mjini Tabora alipoporomosha bonge la show akiwa na kundi zima la Malaika Band. 

Christian Bela alitarajiwa na  wadau wa muziki nchini kuwa angebeba tunzo hiyo bila ushindani mkubwa kutokana na wimbo wake wa Nani kama mama ambao aliomshirikisha Ommy Dimpoz kutamba sana katika vituo vyote vya redio na Runinga hapa nchini, lakini kama kawaida ya tunzo hizo zinazosimamiwa na BASATA na kudhaminiwa na kampuni ya utengenezaji bia ya Tanzania TBL zimekuwa zikilalamikiwa kila mwaka huku waanadaaji wakioneka kuweka pamba mbichi masikioni.

 Tunzo hiyo ya wimbo bora wa mwaka ilienda kwa wimbo wa Mwana wa msanii Ali Kiba. Onesho hilo lilifanyika katika viwanja vya Bwalo la Polisi Tabora.
Bella akifanya yake jukwaani.
Mashabiki wa Malaika Band wakpozi.
Hapo sasa!
Baadhi ya mashabiki wakijmwaga!
Music Producer Dula K kulia na msanii Masha Kay kushoto wakiwa na mdau.

Wacha wee Benny Ngwasuma akijiachia
Picha na habari na Mkala Fundikira TBN CENTRAL ZONE

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE AMETUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA WAISLAMU WOTE NA BAKWATA KUFUATIA KIFO CHA SHEIKH MKUU WA TANZANIA MUFTI SHEIKH ISSA BIN SHAABAN SIMBA

$
0
0

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Waislamu wote nchini na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania  (BAKWATA)) kufuatia kifo cha Sheikh Mkuu wa Tanzania  Mufti Sheikh  Issa Bin Shaaban Simba.

Marehemu Mufti amefariki  leo 15/6/2015 asubuhi katika hospitali ya TMJ – DSM alipokuwa amelazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa sukari na shinikizo la damu (pressure).

"Kifo kinaleta huzuni, hata hivyo Kifo hakizuiliki, hatuna budi kukikubali na ni wajibu wetu kumuombea Sheikh Mkuu kwa Mola wetu ampe mapumziko ya milele". Rais Kikwete ametuma salamu hizo za rambirambi kupitia kwa Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salum.

"Nawaombea subra wana familia, ndugu, jamaa, waislamu wote na wana jamii kwani Mufti alikua kiongozi katika Jamii yetu'Rais amesema na kueleza kuwa "Kamwe mchango wake hautasahaulika katika jamii yote kwa Ujumla na hakika sote tutamkumbuka" ameongeza.

Marehemu alijiunga na BAKWATA mwaka 1968 na amekuwa mwalimu wa chuo katika mikoa mbalimbali ya Mwanza, Bukoba na Mwaka 1970 alikuwa Shekhe wa Mkoa wa Shinyanga.

Rais amemuelezea Marehemu Mufti kama mwalimu katika jamii ambaye alikua na uzoefu wa hali ya juu na mwenye kupenda dini yake na kuitumia kwa manufaa ya jamii iliyomzunguka

"Amekua mwalimu imara na mtu wa kutumainiwa na kutegemewa katika uislamu na jamii kwa ujumla, hakika tutamkumbuka siku zote' Rais Kikwete ameongeza.

Shekhe Issa Bin Shaaban Simba alikuwa na uzoefu  mkubwa ndani ya BAKWATA na  aliwahi kukaimu nafasi ya mufti kwa siku 90, baada ya kifo cha Mufti Hemed mwaka 2002.

Baada ya hapo akasimamia mchakato wa uchaguzi wa Mufti Mkuu na baadaye 2003 akachaguliwa kuwa Mufti Mkuu wa Tanzania.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake pahali pema Peponi, Amina.

Imetolewa na :
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu-DSM

15 Juni, 2015

WAZIRI LUKUVI NA BALOZI WA IRELAND FIONNUAL GILSENAN WASAINI MKATABA WA ARDHI

$
0
0
Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan akisaini kitabu cha wageni alipomtembelea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (kushoto) ofisini kwake leo jijini Dar es salam. 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiongea na mgeni wake Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan (kulia) leo jijini Dar es salam. Kushoto ni Kamishna wa Ardhi nchini Dkt. Moses Kusiluka. 
Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan akisisitiza jambo wakati alipomtembelea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (kushoto) ofisini kwake leo jijini Dar es salam. 
Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan akiwaonesha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (katikati) na Kamishna wa Ardhi nchini Dkt. Moses Kusiluka (wa kwanza kushoto) baadhi ya picha na michoro inayoonesha namna bora ya matumizi ya ardhi kulingana na matumizi husika ikiwemo mipango miji na vijiji.(picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)

Na EleuteriMangi-MAELEZO
Serikali inadhamira yadhati kuboresha huduma ya ardhi nakuipeleka karibu na wananchi kwa wakati ili iwe na tija kwa maendeleo endelevu.


Hayo yamebainishwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alipokuwa akiongea na Balozi wa Ireland nchini  Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan leo jijini Dra es salam.


Akifafanua kuhusu namna huduma hiyo itakavyopelekwa karibu na wananchi, Waziri Lukuvi amesemakuwa wizara yake imeanzisha kanda nane ili kusogeza huduma za ardhi karibu na wananchi badala ya hali ilivyokuwa zamani ambapo huduma hizi zilitolewa makao makuu ya wizara hiyo tu yaliyopo jijini Dar es salaam.


“Ili kutoa huduma ya ardhi kwa wakati kwa wananchi, huduma ya utoaji wa Hatimiliki za ardhi sasa ni kwenye kanda ambazo zinasimamiwa na Makamishna wa Ardhi Wasaidizi.” Alisema Lukuvi.


Kanda hizo ni kanda ya Dar es salaam inayojumuisha Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni, kanda ya Mashariki ambapo makao makuu yake yapo Morogoro, kanda ya Magharibi makao yake makuu yapo Tabora,  kanda ya Ziwa makao yake makuu yapo Mwanza na kanda ya Kaskazini makao yake makuu yapo Moshi mkoani Kilimanjaro.


Kanda nyingine ni pamoja na kanda ya kusini ambayo makao yake makuu yapo Mtwara,  kanda ya Kusini Magharibi makao yake makuu yapo Mbeya na Kanda ya Kati ambayo makao yake makuu yapo mkoani Dodoma.


Katika kutoa huduma yenye ubora kwa wananchi kwa wakati, Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri wataongeza watumishi wakada za wapimaardhi, wapangaji wa miji na vijiji pamoja na wathaminia mbao watafanyakazi kwa pamoja kwenye kanda husika ambapo huduma ya ardhi itakuwa karibu zaidi na wananchi.


Naye Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan amempongeza Waziri Lukuvi na watendaji wote wa wizara hiyo kwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma haraka na kwa wepesi zaidi kwa jamii hatua ambayo ni yakupongezwa na kila mpenda maendeleo.


Balozi Bi Gilsenan alisema kuwa ardhi nibidhaa muhimu inayoweza kutumika kwa kutoa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu, maji, barabara, ujenzi wa viwanda na miundo mbinu mingine ili kumfanya mwananchi kupata huduma yenye tija kwa wakati.


Aidha, kwa upande wake Kamishna wa Ardhi nchini Dkt. Moses Kusiluka alisema kuwa utoaji wa huduma ya usimamizi wa ardhi umeanza kuboreshwa kwa kubadili mfumo wa utoaji wa huduma kuwa wa kielekroniki kutoka mfumo wa kawaida, yaani‘manual’.


Dkt. Kusiluka amesisitiza kuwa mfumo wa kielektroniki utaboresha sana utoaji wa huduma za ardhi, ikiwa ni pamoja nak uondoa tatizo la milkipandikizi (double allocation), kuondoa udanganyifu, kuongeza ufanisi wa watendaji na kuongeza mapato ya Serikali.

EWURA YAPATA TUZO MDHIBITI BORA WA NISHATI 2015

$
0
0
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari juu ya tuzo waliopata Dubai katika udhibiti wa Nishati iliofanyika Ofisi za EWURA,  leo  jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mhandisi wa Umeme EWURA, Anastas Mbawalla.
 Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Felix Ngamlagosi akionyesha kitabu cha kinachofafanua masuala ya mikataba katika sekta ya Nishati ambacho Mtaalam wa Mhandisi wa Umeme, Anastas Mbawalla (kushoto)alishiriki katika kuandika kitabu hicho.
Mhandisi wa Umeme wa EWURA, Anastas Mbawalla akizungumza na waandishi wa habari juu alivyoshiriki katika kuandika kitabu cha masuala ya mikataba ya nishati iliofanyika leo katika ofisi za EWURA jijini Dar es Salaam, Kulia ni Mkurugenzi Mkuu EWURA, Felix Ngamlagosi.(PICHA NA EMMANUEL MASSAKA.GLOBU YA JAMII)

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA),imeibuka mshindi wa mashindano ya Tuzo  ya Mdhibiti Bora wa mwaka wa Nishati 2015.


Akizungumza na waandishi wa habari leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,Felix Ngamlagosi amesema kuwa tuzo hiyo imetolewa Juni 8 mwaka huu kwenye uzinduzi wa sherehe za 17 za Mkutano Mkuu wa Kila mwaka wa Nishati wa Afrika  uliofanyika Dubai.


Ngamlagosi amesema kuibuka kwa  EWURA  katika Tuzo za Nishati inalenga kuwatambua wale wote ambao wametoa mchango kwa maendeleo ya soko la nishati barani Afrika.


“Ushindi wa Tuzo ya Udhibiti Bora wa mwaka wa nishati 2015 imetambua mchango wetu wa udhibiti kutokana na huduma tunayotoa kwenye malengo  ya kuboresha mazingira ya uwekezaji  katika sekta ya nishati kutokana na mahitaji”amesema Ngamlagosi.


Amesema tuzo hiyo inaifanya Tanzania sasa itambulike Kimataifa kwa kuwa na taasisi thabiti ya uhakika ya udhibiti wa sekta nishati na maji ,ambalo ni jambo la muhimu kwa nchi kuendelea kuimarisha imani ya wawekezaji ambayo inatakiwa sana katika kuvutia mitaji binafsi kwenye sekta ya nishati.

Wananchi walivyotembelea mradi wa viwanja Vikuruti

$
0
0
Baadhi ya wananchi wakiangalia ramani katika mradi wa viwanja unaoendeshwa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, katika eneo la Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani mwishoni mwa wiki na kusimamiwa na Meneja Mauzo wa Taasisi hiyo Nasra Sudi. Picha zote na Mpigapicha Wetu.
Wananchi waliokwenda kuonyeshwa viwanja hivyo wakipata somo la mradi huo wa vianja vya Vikuruti unaoendeshwa na Taasisi ya Bayport Financial Services.
Wananchi hawa wakiangalia kwa makini ramani ya viwanja vya Vikuruti, vinavyoratibiwa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, mwishoni mwa wiki. Zoezi la viwanja hivyo kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni binafsi na wajasiriamali linaendelea hadi Juni 30 mwaka huu, ambapo kila Mtanzania anaweza kupata kiwanja hicho kwa fedha taslimu au kwa mkopo. Thamani ya viwanja hivyo inaanzia Sh 1,400,000 na kuendelea.
Afisa Mauzo wa Bayport Financial Services, Catherine Tesha, akitoa maelekezo kwa baadhi ya wananchi waliokwenda Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani kujipatia fursa ya viwanja vinavyoratibiwa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, mwishoni mwa wiki. Zoezi la viwanja hivyo kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni binafsi na wajasiriamali linaendelea hadi Juni 30 mwaka huu, ambapo kila Mtanzania anaweza kupata kiwanja hicho kwa fedha taslimu au kwa mkopo. Thamani ya viwanja hivyo inaanzia Sh 1,400,000 na kuendelea.

CHADEMA WATOA SALAAM ZA POLE NA RAMBIRAMBI MSIBA WA MUFTI MKUU SHEIKH SIMBA

$
0
0

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
(CHADEMA).

SALAAM ZA POLE NA RAMBIRAMBI MSIBA WA MUFTI MKUU SHEIKH SIMBA.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa masikitiko na majonzi makubwa taarifa za msiba wa Mufti Mkuu wa Tanzania Tanzania, Sheikh Issa Shaaban bin Simba, Kiongozi Mkuu wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kilichotokea asubuhi ya leo kwa maradhi ya sukari na shinikizo la moyo.

Akitoa salaam za pole na rambirambi kwa waumini wa madhehebu ya Kiislamu na Watanzania wote kwa ujumla baada ya kupata taarifa za msiba huo, Mwenyekiti wa CHADEMA (T), Freeman Mbowe amesema kuwa Mufti Mkuu Simba atakumbukwa kwa namna aliyosimama kama kiongozi wa dini kupitia kauli zake mara kwa mara akisisitiza ushirikiano ndani ya jamii ya Watanzania bila kujali tofauti zao katika itikadi za dini.

“Mara kwa mara Mufti Mkuu Simba amesikika akiwaambia Watanzania, si Waislam pekee aliokuwa akiwaongoza kiroho, hata wale wanaoamini katika madhehebu tofauti, umuhimu wa kudumisha ushirikiano miongoni mwa dini mbalimbali na makundi mengine katika jamii ikiwa ni mojawapo ya misingi ya kuimarisha umoja wa taifa letu.”

“Naungana na Waislam wote nchini katika wakati huu wa kuomboleza kifo cha kiongozi huyu wa kiroho. Kwa niaba ya niaba ya uongozi wa CHADEMA, wanachama, wapenzi na wafuasi, natoa salaam za pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki, BAKWATA, viongozi wa kiroho nchini na Watanzania wote ndani na nje ya nchi walioguswa na msiba huu mzito.”

“Mwenyezi Mungu awatie nguvu wote na kuwafanyia wepesi katika wakati huu mgumu wa majonzi ya msiba wa Mufti Mkuu Simba,” amesema Mbowe
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji’un.

Imetolewa leo Jumatatu, Juni 15, 2015 na;
Idara ya Habari na Mawasiliano- CHADEMA.

MGOMBEA URAIS, DKT. MOHAMMED GHARIB BILAL, ARUDISHA FOMU ZA URAIS MJINI DODOMA.

$
0
0
 Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi  CCM, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Fomu zake za kuwania urais, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, Rajab Luhwavi, wakati alipowasili kwenye Ofisi za Makao Makuu wa CCM mjini Dodoma leo kwa ajili ya kurejesha Fomu za kuwania urais katika uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Mwezi Oktoba mwaka huu. Kulia ni Mke wa Makamu wa Rais Mama Zakia Bilal.
 Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi  CCM, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwasalimia  wanachama wa CCM, wakati akitoka kwe ye Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma leo, wakati alipotoka kurejesha Fomu za kuwania urais katika uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Mwezi Oktoba mwaka huu. Nyumba yake  ni Mke wa Makamu wa Rais Mama Zakia Bilal.
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi  CCM, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipunga mkono kuwasalimia  wanachama wa CCM, wakati akitoka kwe ye Ukumbi wa CCM Makao Makuu mjini Dodoma leo, wakati alipotoka kurejesha Fomu za kuwania urais katika uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Mwezi Oktoba mwaka huu. Nyumba yake  ni Mke wa Makamu wa Rais Mama Zakia Bilal. Picha na OMR

SERIKALI YA ZANZIBAR HAIJAFANYA UBAGUZI WA UTOAJI WA VIBALI VYA UCHUMBAJI WA MCHANGA/UDONGO KATIKA MAENEO YA UNGUJA NA PEMBA.

$
0
0
Takdir Ali-Maelezo Zanzibar.
Serikali kupitia Idara ya Mazingira na Maliasili zisizorejesheka haijawahi wala haina sababu za kufanya ubaguzi wa kutoa ruhusa ya mtu yeyote kuchimba mchanga katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais Fatma Abdul-habiib Fereji wakati akijibu swali la Mwakilishi wa Jimbo la Wawi Saleh Nassor Juma katika Baraza la Wawakilishi linaloendelea Chukwani nje kidogo ya Mji wa  Zanzibar.

Amesema Serikali kupitia Idara ya Maliasili zisizorejesheka ambayo ni Taasisi yenye dhamana ya kutoa vibali vya Mchanga/Udongo kwa baadhi ya Maeneo kwa miradi maalum ya maendeleo ambayo hutowa vibali hivyo bila ubaguzi wa aina yeyote kitu cha muhimu ni kufuata Taratibu na Sheria za nchi.

Amesema Maeneo hayo hutolewa baada ya kufuata Taratibu zote za nchi ikiwa ni pamoja na kufanya Ukaguzi Shirikishi wa Wadau na kwa kuzingatia mahitaji maalum ya aina ya Mchanga inayohitajika kwa ajili ya Shughuli za Mradi husika.

Aidha amesema uchunguzi wa Kimaabara wa kuangalia aina ya Mchanga/Udongo hufanywa ili kubaini eneo linalofaa kuchimbwa Mchanga.

Amefafanua kuwa kwa ujumla uchimbaji wa Mchanga/Udongo na wanaohusika kuchukua Mchanga/Udongo kwenye Maeneo hayo ni wale tu wanaohusika na shughuli za  Mradi husika.

Akielezea kuhusu eneo linalohusika  kwa kazi maalum ya Ujenzi wa nyumba za JWTZ ambazo zinajengwa katika eneo la Ngerengere kwenye kambi ya Jeshi la Wawi Fereji amesema Mkandarasi wa Ujenzi wa nyumba hizo alihitaji kupata Mchanga maalum ili kufikia Masharti ya Ujenzi wa nyumba hizo.

Ameendelea kusema kuwa kutokana na hali hiyo na baada ya kufanya uchunguzi wa kimaabara wa mchanga (soil test) katika maeneo mbali mbali ndio mchanga wa eneo hilo unaonekana kuwa unafaa kwa mahitaji ya ujenzi wa nyumba hizo.

Mbali na hayo amesema baada ya uchunguzi huo kuthibitika hali hiyo,ndipo taratibu ziliopo za maombi zikafuatwa na baada ya taratibu hizo kukamilika ndipo Idara ya Misitu na Maliasili zisizorejesheka ikatoa kibali cha uchimbaji.

 IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR.

MAPOKEZI YA MH. LOWASSA MJINI BUKOBA LEO,AENDELEA KUJIZOLEA WADHAMINI

$
0
0
 Umati wa wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera ukiwa umemzunguka Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa, wakati alipowasili kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Kagera, leo Juni 15, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akipokea fomu kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya ya Bukoba mjini, Acheni Mwinshehe, zenye majina ya wanaCCM wa Mkoa wa Kagera waliomdhani ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. 
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akizungumza na umati wa wanaCCM pamoja na wananchi wa Mji wa Bukoba mkoani Kagera leo Juni 15, 2015, Wakati akitoa shukrani zake kwa kumdhamini ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. Zaidi ya wanaCCM 6000 wamdhamini mkoani Kagera.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mh. Edward Lowassa akipongezwa na Bibi huyu (ambaye jina lake halikuweza patikana kwa haraka) mara baada ya kupokea fomu za wanaCCM zaidi ya 6000 waliomdhamini ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. 

KATIBU MKUU CCM NDUGU KINANA NA MSAFARA WAKE WAWASILI LEO MKOANI GEITA NA KUANZA ZIARA YA SIKU SITA

$
0
0
Katibu Mkuu wa CCM,Ndg Kinana akisisitiza jambo.
Umati wa wakazi wa Chato mjini wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa akihutubia kwenye uwanja wa stendi ya Zamani.Katibu Mkuu wa CCM aliwaambia wananchi hao kuwa Serikali inabidi ifute kodi kandamizi zinazowazuia wananchi kurahisisha maisha yao.
 Umati wa wakazi wa Chato mjini wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipokuwa akihutubia kwenye uwanja wa stendi ya Zamani.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndg Kinana akisisitiza jambo
Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana ukipokelewa katika kijiji cha Kasenga,ukitokea mkoani Kagera,tayari kwa kuanza ziara ya siku 6 mkoani Geita.
Ndugu Kinana akisalimiana na wananchi wa Kasenga,wilayani Chato mkoani Geita ikiwe ni sehemu ya mapokezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akiweka jiwe la msingi ofis mpya ya CCM katika kata ya Kasenga,wilaya ya Chato mkoani Geita.
Muonekano wa ofisi hiyo ya CCM
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo mafupi mara baada ya kuwasha mtambo wa maji uliojengwa Chato Mlimani kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji utakaohudumia wakazi wa mji huo leo, wakati wa ziara yake katika mkoa wa Geita .

Kinana anaendelea na ziara hiyo ya kikazi mkoani humo baada ya kumaliza ziara kama hiyo mkoani Kagera jana, Kinana anaendelea  na ziara hiyo yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kuhimiza uhai wa chama, kukosoa na kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili wananchi kwa maisha na maendeleo yao kwa ujumla akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana pichani kushoo na Katibu wa NEC itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakisoma bango lenye maanidishi lililobebwa na baadhi ya vijana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji Paulina Sabinati mara baada ya uzinduzi wa mradi huo.
Katibu Mkuu wa CCM akizungumza na Wanachama wa Mshikamano Saccos wapatao zaidi ya 400,ampapo pia alikabidhi mikopo kwa wanachama wa saccos hiyo wapatao 20,kiasi cha shilingi milioni 78
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na  Mkuu wa wilaya ya Chato Ndugu Rodrick Mpogole, viongozi wa CCM wilaya ya Chato pamoja na mafundi wa Tanesco akishiriki kutandaza waya za umeme katika mradi wa umeme vijijini REA katika kijiji cha Mkungo,wilayani Chato mkoani Geita.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akizungumza na Wananchi wa kijiji cha Makurugusi kuhusiana na mpango wa kupata umeme katika kijiji chicho,ambapo kijiji chao kimerukwa na kuachwa bila kuweka umeme,hiuvyo Wananchi hao wamemuomba Ndgugu Kinana kuhakikisha anawasaidia na wao wanapata umeme katika kijiji chao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipeana tano na wananchi hao mara baada ya kuwaahidi kuongea na Waziri wa Nishati na Madini ili kijiji hicho kiwekewe umeme vijijini  REA, ambapo wanakijiji hao walijawa na furaha mara baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kwa kiongozi huyo wa juu wa CCM.
Umati wa wananchi wa Chato mjini wakishangilia mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliyeanza ziara ya siku sita mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika ujenzi wa nyumba ya daktari katika kijiji cha Ihanga wilayani Chato.
 Wananchi wakinyanyua mikono yao juu juu kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati akihutubia wakazi wa Chato mjini ikiwa siku ya kwanza ya ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mkoani Geita.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Chato ikiwa siku yake ya kwanza ya ziara mkoani Geita baada ya kumaliza ziara ya siku 10 mkoa wa Kagera.Katibu Mkuu wa CCM anazunguka nchi nzima kukagua,kuhimiza na kusukuma utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM akiwa ameambatana Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nnape Nnauye..
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Diwani wa kata ya Biziku Bw. Magomamoto Zanzibar akijinadi na kueleza namna alivyotekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM katika kata yake.

BILIONEA DANGOTE ALIDHIA UJENZI WA BANDARI YAKE MTWARA KWA KUSHIRIKIANA NA TPA

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaji Aliko Dangote, akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Hawa Ghasia alipowasili kwenye uwanja wa Ndege mjini Mtwara jana kwa ajili ya kutembelea kiwanda chake cha Cementi kilichoko Msijute, mkoani Mtwara.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Hawa Ghasia akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaji Aliko Dangote, alipowasili kwenye uwanja wa ndege wa Mtwara leo kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kiwanda cha Cementi cha Dangote. Katikati ni Balozi wa Nigeria Nchini Tanzania, Ishaya Manjanbu.
 Mkurugenzi wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kulia), akijadiliana jambo na Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka, walipokutana mjini Mtwara jana kuangalia uwezekano wa kujenga kituo cha kusafirisha saruji katika eneo la Bandari ya Mtwara.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaji Aliko Dangote, akizungumza na waandishi wa habari baada kuwasili mjini Mtwara jana na kutembelea kiwanda chake cha Cementi, kilichoko Msijute, mkoani Mtwara.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote akisaini kitabu cha wageni, baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege mjini Mtwara jana, kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa kiwanda chake cha saruji. Kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka.

 Mkurugenzi wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote akiwafuatana na wenyeji wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Hawa Ghasia (wa pili kushoto), Balozi wa Nigeria, Ishaya Manjanbu (wa pili kulia) na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Bi. Fatma Salum Ali (kushoto), alipowasili kwenye uwanja wa ndege, mjini Mtwara jana.






Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote, akiteta jambo na Mwakilishi mkazi wa Dangote nchini Tanzania, Bi. Esther, mjini Mtwara , baada ya Mkurugenzi huyo kutembelea kiwanda chake cha saruji kinachojengwa mkoni Mtwara.


ZITTO KABWE AWAHUTUBIA WAKAZI WA MKOA WA KAGERA KWA MARA YA KWANZA LEO

$
0
0

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe, Akifurahia mara baada ya kutua Bukoba na tayari kuwahutubia wakazi wa mji wa Bukoba leo wakati wa mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Mashujaa/Uhuru Platform Bukoba leo Jumatatu tarehe 15 june, 2015. Kiongozi huyu ambaye amefuatana na viongozi wenzake wa juu wa chama hicho, yuko kwenye ziara ya kukitangaza chama na sera mpya ya azimio la arusha lenye usasa. 
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe akiongea na wakazi wa Mji wa Bukoba leo Jioni jumatatu ya juni 15, 2015. 
Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghira, akiwahutubia wakazi wa mji wa Bukoba leo wakati wa mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Uhuru Platform leo Jumatatu juni 15, 2015.

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

MAMA SALMA AHUTUBIA MKUTANO WA WAKE WA MARAIS NA WAKUU WA NCHI ZA AFRIKA (OAFLA) NCHINI AFRIKA KUSINI

$
0
0
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akielekea kwenye ukumbi wa mkutano wa Sandton Internationa Center unakofanyika mkutano wa wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika huko Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 15.6.2015. Aliyefuatana na Mama Salma ni Mwenyekiti wa OAFLA anayemaliza muda wake Mama Hinda Derby Itno.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiangalia moja ya machapisho mbalimbali yanayohusiana na Mkutano wa Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika (OAFLA) unaofanyika nchini Afrika Kusini.
  Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mkutano wao wa mwaka unaozungumzia uwezeshaji kwa wanawake na Maendeleo katika Bara hili.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa hotuba yake ya mwisho kwenye kikao cha Wake wa Marais na Wakuu wa Nchi za Afrika kinachofanyika kwenye Ukumbi wa Sandton jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini tarehe 15.6.2015.




VYAMA VYA WAONGOZA WATALII NA WAPAGAZI TANZANIA WATOA SIKU 30 KWA SERIKALI KUSHUGHULIKIA MADAI YAO

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha waongoza watalii mkoa wa Kilimanjaro (KGA) Respicius Baitwa akizungumza katika mkutano wa vyama vinayofanya shughuli za Utalii katika hifadhi za taifa juu ya kusudio la kutaka kusitisha kutoa huduma katika hifadhi kutokana na malalamiko yao kutofanyiwa kazi hadi sasa.
Baadhi ya wajumbe walioshiriki mkutano huo uliofanyika katika Hotel ya Uhuru mjini Moshi.
Katibu wa KGA ,James Mong'ateko akizungumza katika mkutano huo.
Wajumbe wengine wa vyama vinayofanya shughuli za utalii katika hifadhi za taifa ikiwemo mlima Kiliamanjaro.
Mwanasheria wa Chama cha waongoza watalii mkoa wa Kilimanjaro (KGA) Elikunda Kipoko akitoa ufafanuzi wa kisheria katika mkutano huo.
Mmoja wa wajumbe katika mkutano huo akichangia hoja juu ya kusudio la kutaka kuhitisha mgomo kwa lengo la kudai maslahi yao.
Mkutano huo ulitoa siku 30 kwa serikali kutekeleza mambo mawili moja likiwa ni kutoa taarifa juu ya kikosi kazi kilichoundwa na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama kufuatilia kero mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutaka kuonana na waziri wa maliasili na utalii,Lazaro Nyalandu. Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI,NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI,ANGELA KAIRUKI AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA MKOA WA KILIMANJARO JUU YA TUHUMA MBALIMBALI ZA ARDHI ZILIZOIBULIWA BUNGENI HII KARIBUNI.

$
0
0

Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Angela Kairuki akizungumza katika mkutano huo uliowashirikisha wakuu wa wilaya,kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa,maafisa ardhi ,madiwani pamoja na wananchi wa kawaida.
Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na maendeleo ya Makazi,Angela Kairuki akiteta jambo na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama katika mkutano huo. 
Baadhi ya viongozi pamoja na watumishi wengine walioshiriki mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Leonidss Gama akizungumza katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo,Anthony Tesha akitoa taarifa juu ya kiwanja kilichotolewa kwa waweezaji na halmashauri hiyo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha saruji.
Mkurugenzi wa Halamshauri ya wilaya ya Moshi,Fulgence Mponji akitoa ufafanuz juu ya mgogoro wa kiwanja kinachomilikiwa naaliyekuwa mbunge wa jimbo la Vunjo ,Aloyce Kimaro.
Baadhi ya Madiwani wa Halamshauri ya manispaa ya Moshi wakiongozwa na Naibu Meya ,Dkt Mbando,PeterKimaro pamoja na Raymond Mboya.
Mkuu wa wilaya ya Siha,Dk Charles Mlingwa (kushoto) akiwa na mkuu wa wilaya ya Mwanga Shahibu Ndemanga (katikati) pamoja na Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Koka Moita wakiwa katika mkutano huo.
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Kilimanjaro wakifuatilia mkutano huo.
Naibu waziri a Ardhi ,Nyumbana Maendeleo na Makazi,Angela Kairuki akiongozana na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Leonidas Gama wakati  alipowasili Kilimanaro kwa ajili ya tuhuma dhidi ya mkuu huyo wa mkoa pamoja na migogoro ya ardhi.
Na Dixon Buagaga wa Globu ya Jamii Knada ya Kaskazini.
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images

<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596344.js" async> </script>