MWANAMITINDO AFANYAYE KAZI ZAKE ZA UANAMITINDO ALOJIKITA MAREKANI FLAVIANA MATATA AMEKUWA AKIFANYA KAZI MBALI MBALI ZA KUONESHA MAVAZI JUKWAANI SAMBAMBA NA HIZI ZA MATANGAZO YA KIBIASHARA YA MATANGAZO YA MAVAZI NA SAFARI HII AMEFANYA NA KAMPUNI YA NEWYORK AND COMPANY KWA AJILI YA MAVAZI YA MAJIRA YA JOTO
FLAVIANA MATATA FOR NYANDCOMPANY
↧
↧
DC MBONI AWAHAMASISHA WANAWAKE MUFINDI KUGOMBEA NAFASI ZA UDIWANI,UBUNGE NA URASI
Mkuu wa wilaya ya Mufindi Bi Mboni Mhita akifungua kongamano la Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Mufindi leo |
Washiriki wa kongamano la UWT wilaya ya Mufindi wakimshangilia mkuu wa wilaya ya Mufindi hayupo pichani |
Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mosha akimkaribisha mgeni rasmi |
Washiriki wa kongamano hilo wakifuatilia mafunzo ya afya na uzazi na yale ya ujasiliamali |
Katibu wa UWT Mufindi |
Viongozi wa UWT mkoa na wilaya pamoja na DC mufindi wakifuatilia mafunzo |
Mtaaluam wa afya akitoa semina ya afya kwa washiriki |
Mtaalam wa afya akitoa elimu ya matumizi sahihi ya kondom |
Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Iringa vijijini Bi Shakra kiwanga akitoa salam zake |
Na FgBlog Mufindi
MKUU wa wilaya ya Mufindi mkoani Iringa Bi Mboni Mhita amewataka wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbali mbali za uongozi ikiwemo nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Octoba mwaka huu
Alisema ushindi wa wanawake katika nafasi mbali mbali ikiwemo ya udiwani ,ubunge na urais ni kubwa zaidi iwapo wanawake wenyewe watajiamini na kuepuka na maneno ya watu ambayo kimsingi wengi wao wanatamani kuona wanawake wakiwa nyuma .
Bi Mboni ambae ni mjumbe wa NEC Taifa alitoa rai hiyo leo katika ukumbi wa CCM wilaya ya Mufindi wakati akifungua kongamano la umoja wa wanawake Tanzania (UWT) alisema kuwa muda ukifika wanawake hawana sababu ya kuogopa kuingia katika nafasi mbali mbali za uongozi na kuwa wale wenye uwezo wa kugombea udiwani ,ubunge na Urais wajitokeze bila katika mapambano kuogopa .
Alisema kikubwa si wanawake kuwatazama wenzao wanapoingia katika mapambano ila ni kuona wanawake wanatengezeza jeshi moja la mapambano ya kumsaidia kwa nguvu zote mwanamke mwenzao anayesimama katika kuwania nafasi za uongozi.
Bi Mboni alisema vijana pia hawana sababu ya kuchangamkia nafasi za uongozi mbali mbali katika uchaguzi ujao badala ya kuwa nyuma na kuwa kwa upande wake anajivunia kuwa mkuu wa wilaya ya Mufindi nafasi ambae pia ni mkuu wa wilaya mwenye umuri mdogo zaidi kuliko wote nafasi aliyeteuliwa na Rais Dr Jakaya Kikwete jambo ambalo anampongeza Rais kwa uteuzi huo japo kabla ya uteuzi huo alikuwa ni makamu mwenyekiti wa UVCCM Taifa .
Pia alisema kuwa yeye pia ni miongoni mwa wajumbe wa NEC Taifa wadogo zaidi ila pia alipata kuchaguliwa kuwa kiongozi wa vijana barani Afrika na kuwa nafasi zote hizo amekuwa akizipata kutokana na kuthubutu na kutojinyanyapaa kama mwanamke.
Hivyo alisema wakati umefika wa vijana na wanawake nchini kutumia nafasi ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu kujitokeza kuwania nafasi mbali mbali bila kuogopa .
Awali akimkaribisha mkuu huyo wa wilaya kufungua kongamano hilo mwenyekiti UWT wilaya ya Mufindi Bi Marcelina Mkini mbali ya kumpongeza mkuu huyo wa wilaya ya Mufindi kwa utendaji wake mzuri bado alisema kuwa wanawake katika wilaya ya Mufindi kwa mwaka huu wamejipanga kugombea nafasi zote tatu ya udiwani ,ubunge na Urais
Kuwa ushindi wa wanawake katika nafasi mbali mbali za uongozi utatokana na ushirikiano mzuri wa wanawake wenyewe katika kuwaunga mkono wale wote wanaogombea nafasi mbali mbali na kuwa falisafa ya UWT Mufindi ni wanawake Kwanza .
Bi Mkini ambae ni mjumbe wa NEC Taifa akiwakilisha wilaya hiyo ya Mufindi alisema kuwa wanawake wa wilaya hiyo ya Mufindi wamehamasishwa vya kutosha kuweza kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali za uongozi na kuwa mwitikio wa wanawake kuanza kuamka kugombea nafasi za uongozi ulianza kuonekana katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika mapema hivi karibuni kwa wanawake kuonyesha ushiriki mzuri katika mchakato huo.
Bila kutaja kutaja idadi ya wanawake walioshinda katika uchaguzi huo bado alisema matokeo mazuri ya uchaguzi wa serikali za mitaa ambayo yaliiwezesha wilaya ya Mufindi kuongoza kwa mkoa wa Iringa kwa CCM kushinda kwa zaidi ya aslimia 90 katika uchaguzi huo wa serikali za mitaa ni moja kazi nzuri ya wanawake katika ushiriki wao katika uchaguzi huo.
Kwani alisema nguvu kubwa iliyoonyeshwa na wanawake wa wilaya hiyo ni chachu ya kubadili mtazamo uliokuwepo wa wanawake kuendelea kuwa madaraja ya kuvusha wanaume wanaogombea hivyo mtazamo huo kwa sasa umeanza kupotea baada ya wanawake kuonyesha ushiriki wao katika kugombea nafasi mbali mbali za uongozi .
Bi Mkini alisema ushahidi wa nguvu ya wanawake katika kampeni upo wazi katika wilaya hiyo ya Mufindi ambayo mkuu wa wilaya ni mwanamke ,mkurugenzi ni Mwanamke na mjumbe wa NEC Taifa ambae ni yeye mwenyewe na kuwa nafasi hiyo aliipata baada ya kupambana na wanaume
↧
UJUMBE WA MAOFISA WA UMOJA WA BENKI ZA AKIBA DUNIANI KANDA YA AFRIKA WATEMBELEA ZANZIBAR
Meneja wa Tawi la Benki ya Posta Zanzibar Ndg Justin S.Nandonde akisalimiana na kumkaribisha wageni wake walipotembelea Tawi hilo Zanzibar kujionea utendaji wa Benki ya Posta Tawi la Zanzibar wakiwa katika ziara yao Zenj.
MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg. Sabasaba Moshingi, akitowa maelezo ya Ujumbe wa Maofisa wa Benki wa Umija wa Mabenki Duniani Kanda ya Afrika, walipotembelea Benki ya Posta tawi la Zanzibar.
Wajumbe wa Mkutano wa Wanachama wa Umoja wa Mabenki Duniani na Kanda ya Afrika wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania wakati walipofika Tawi la Benki ya Posta Zanzibar,
MKURUGENZI Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg. Sabasaba Moshingi, akitowa maelezo ya Ujumbe wa Maofisa wa Benki wa Umija wa Mabenki Duniani Kanda ya Afrika, walipotembelea Benki ya Posta tawi la Zanzibar.
Mkurugenzi wa Tekohama na Uendeshaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg Jema Msuya akitowa maelezo ya kiufundi kwa ujumbe huo.walipotembelea Benki ya Posta Tawi la Zanzibar Mchangani
Meneja wa Benki ya Posta Tawi la Zanzibar Ndg. Justin SNdandonde akitowa maelezo kwa ujumbe huo ulipotembelea Tawi hilo na kuagalia ufanisi wa huduma za Benki hiyo kwa wateja wao
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania Ndg Sabasaba Moshingi akiwa na wakeni wake wakitoka katika moja ya sehemu ya historia ya Kanisa la Mkunazi Zanzibar.
Mtembeza Watalii katika Mji Mkongwe seif Ali akitowa maelezo kwa Ujumbe huwa sehemu za historia za Mji Mkongwe wa Zanzibar.
Maofisa wa Umoja wa Benki za Akiba Duniani Kanda ya Afrika wakiwa katika ziara yao katika mji mkongwe na kupata kuonja Ubuyu wa Kwaissa sokomuhugo Zenj wakiwa katika ziara ya siku mbili Zanzibar baada ya kumaliza Mkutano wao Dar.
Mtembeza Watalii Zenj akitowa maelezo kwa Ujumbe huo wa Maofisa wa Mabenki ya Akiba wakiwa katika ziara yao kutembelea sehemu za historia za mji Mkongwe Zanzibar wakipata maelezo ya Mlango wa Zanzibar
↧
JAMBO LEO YAICHABANGA BODABODA FC TAMASHA LA BODABODA UKONGA
Mlinda mlango Maganga Benjamin wa timu ya Bodaboda Wilaya ya Ilala, akiudaka mpira katikati ya wachezaji wa timu ya Jambo Leo 'Wagumu Stars' Zahoro Mlanzi (kushoto) na Ali Salum wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa. Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
Mchezaji wa timu ya Jambo Leo, Frank Balile (kushoto) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya Bodaboda, Sharif Mohamed
Moja ya kizazaa langoni mwa Bodaboda FC iliyosababishwa na washambuliaji wa Jambo Leo
Mshambuliaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, Ali Salum (katikati) akifunga bao la kwanza dhidi ya Bodaboda FC,wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
Slaa akiwasalimia wachezaji wa timu hizo mbili
Wachezaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, wakifanya mazoezi ya kupasha mwili muda mfupi kabla ya kuvaana na timu ya Bodaboda FC ya Wilaya ya Ilala, wakati wa Tamasha la Bodaboda kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Katika mechi hiyo, Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
Kikosi cha timu ya Gazeti la Jambo Leo kilichopambana na Bodaboda FC
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (wa pili kulia), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, muda mfupi kabla ya timu hiyo kukipiga na timu ya Bodaboda FC ya Wilaya ya Ilala, wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam jana.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa (kushoto), akisalimiana na wachezaji wa timu ya Bodaboda FC , muda mfupi kabla ya timu hiyo kukipiga na timu ya Gazeti la Jambo Leo, wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam
Silaa akitoa mawaidha kwa timu hizo kabla ya mechi kuanza
↧
Tangazo la Msiba wa Ndg Sebastian Lukas Mgimba wa Sinza Kumekucha
Familia ya bwana Sebastian Lukas Mgimba ya sinza kumekucha inasikitika kutangaza kifo cha baba Yao mpendwa ndugu Sebastian Lukas Mgimba kilichotokea alhamis 28/5/2015 katika hospital ya kairuki mikocheni Dar es salaam. Mipango ya mazishi Inafanyikia nyumbani kwa marehemu sinza kumekucha. Mwili unatarajia kusafirishwa kwenda Lugarawa Ludewa Njombe jumatatu 1/6/2015.
Habari ziwafikie Familia ya Malyatabu Mgimba iliyopo Lugarawa Ludewa familia ya Philipo Mshengeli Msuya ya shighatini Mwanga pamoja na ndugu jamaa na marafiki popote pale walipo.
Misa takatifu pamoja na Kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu zitafanyikannyumbani kwa marehemu Sinza Kumekucha tarehe 1-06-2015 kuanzia saa Sita Mchana.
Bwana ametoa na bwana ametwaa jina la Bwana lihimidiwe
↧
↧
MCHUMI WA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA KUGOMBEA UBUNGE JIMBONI KWA WAZIRI MGIMWA
Bw Exaud Kigahe mgombea ubunge jimbo la Mufindi kaskazini |
Wanahabari wakimsikiliza Bw Kigahe wakati akitangaza nia ya kugombea ubunge |
MDAU mkubwa wa maendeleo ya elimu katika wilaya ya Mufindi mkoani Iringa na mzaliwa wa kijiji cha Nungwe, wilayani Mufindi Mkoani Iringa Bw Exaud Kigahe ambae ni mchumi mkuu wa wizara ya viwanda na biashara amepania kuwakomboa kimaendeleo wakazi wa jimbo la Mufindi Kaskazini linaloongozwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mahamudu Mgimwa iwapo watamchagua kuwa mbunge wa jimbo hilo.
Akizungumza na wanahabari juzi wakati akitangaza nia hiyo, Kigahe ambaye ni Mtaalamu wa Takwimu anayefanya kazi katika Wizara ya Viwanda na Biashara jijini Dar es Salaam alisema; “ni haki yangu kikatiba katika mchakato mzima wa demokrasia ya kweli, nilifanya hivyo mwaka 2010 lakini kura hazikutosha nataka kuingia tena mwaka huu.”
Katika kura za maoni za CCM za mwaka 201, Mgimwa alipata kura 6,386 huku Mungai akipata kura 3,430 na yeye (Kigahe) akiwa mshindi wa tatu kwa kupata kura 1,208. Alisema anataka kugombea ubunge katika jimbo hilo huku akifahamu kwamba wananchi wake wengi ni masikini pamoja na wana rasilimali za kutosha.
“Tuna ardhi nzuri inayofaa kwa kilimo cha mazao mbalimabli ya chakula na biashara kama chai, pareto na miti,” alisema. Alisema wakati wilaya hiyo ikiwa na shamba kubwa kuliko mengine yote ya miti nchini, bado baadhi ya shule zake hazina madawati, milango na madirisha.
Alisema anataka kuingia katika kinyang’anyiro hicho huku kipaumbele chake kikiwa ni elimu kwani hazina hiyo ndio pekee inayoweza kusaidia kubadili maisha, uchumi na maendeleo ya ujumla ya wilaya ya Mufindi.
“Watoto wetu wakiwezeshwa, wakapata elimu bora wanaweza kushiriki kupambana na umasikini kwa kutumia rasilimali zilizopo,” alisema.
Alisema kwa muda mrefu jimbo la Mufindi Kaskazini limeendelea kupata viongozi wasio na mbinu za kuibadili hali hiyo.
Aliyataja maeneo mengine atakayoyapa kipaumbele endapo atashinda kura za maoni na kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo kuwa ni pamoja na kuwashirikisha wananchi na serikali kuboresha sekta ya afya, kilimo, maji, biashara, mawasiliano na miundombinu ya barabara.
Katika Uchaguzi Mkuu wa 2010, Mgimwa aliwania ubunge wa jimbo hilo baada ya kumuangusha katika kura za maoni, Joseph Mungai; kigogo aliyebahatika kushika uwaziri wa wizara mbalimbali katika awamu za serikali zote ikiwemo ya serikali ya Mwalimu Julius Nyerere na Jakaya Kikwete.
Katika awamu ya kwanza ya Rais Jakaya Kikwete, Mungai alipata kuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika kabla hajahamishiwa katika wizara ya Mambo ya Ndani.
↧
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AZINDUA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA MARIAN BAGAMOYO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Pengo, kwa pamoja wakikata utepe kuzindua Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Pengo, kwa pamoja wakifunua kitambaa kama ishara ya kuweka Jiwe la Msingi la uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na baadhi ya waumini wa dini ya Kikristu, katika Ibada maalum ya uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian, baada ya uzinduzi wa Chuo hicho uliofanyika leo Mei 31, 2015 mjini Bagamoyo. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Pengo, baada ya uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Pengo, baada ya uzinduzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongozana na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Pengo na baadhi ya viongozi na waumuini baada ya kuzindua rasmi Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian mjini Bagamoyo,leo Mei 31, 2015. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akisikiliza maelezo kutoka kwa mkandarasi wa majengo ya Chuo Kikuu Kishiriki cha Marian wakati akitembelea kujionea ramani ya Chuo hicho baada ya uzinduzi wa Chuo hicho uliofanyika leo mjini Bagamoyo. Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na baadhi ya waumini wa Dini ya Kikristu, baada ya uzinduzi wa Chuo hicho uliofanyika leo chuoni hapo mjini Bagamoyo. Picha na OMR
↧
RAIS KIKWETE AKUTANA NA MAALIM SEIF IKULU DAR ES SALAAM
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad ikulu jijini Dar es Salaam
(picha na Freddy Maro)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa kwenye picha ya pamoja na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad ikulu jijini Dar es Salaam.
↧
VIJANA WA KAWE WASHIRIKI JOGGING
- Jogging zawaweka wananchi wa Kawe pamoja
- Watumia mazoezi kama njia ya kupinga matumizi ya madawa ya kulevya
- Kuhamasisha vijana wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura Makundi zaidi ya 20 yashiriki.
Vijana wa Kawe wakishiriki Jogging.
Gabriel Munasa (mwenye kaptura ya pink) akishiriki jogging pamoja na vijana wa Kawe,kushoto kwake ni Elias Nawera.
Gabriel Munasa akiongea na vyombo vya habari ambapo alielezea lengo na madhumuni ya kuwasaidia vijana kupitia vikundi vya jogging na pia alitumia fursa hiyo kuwaeleza nia yake ya kugombea ubunge kwa jimbo la Kawe na kama litagawanywa atagombea jimbo la Bunju.
Bendera ya Taifa ikiwa juu kuashiria kuhitimisha kwa mchakamchaka huo ambao mgeni rasmi alikuwa Gabriel Munasa.
Gabriel Munasa akishiriki mazoezi ya viungo kwenye viwanja vya michezo vya Kawe.
Burudani baada ya mazoezi.
↧
↧
RAIS KIKWETE AKUTANA NA MKURUGENZI MKUU WA KAMPUNI YA UNILEVER DUNIANI
↧
NYALANDU KUCHUKUA FOMU ZA URAIS JUNI 7 MJINI DODOMA
Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu na waumini mbalimbali baada ya Ibada ya jumapili Jijini Arusha katika Kanisa la KKKT Diyoyosis ya Mjini Kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi .
Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu akibadilishana mawazo na Kada wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA James Olemilia baada ya ibada ya jumapili iliyofanyika katika Kanisa la KKKT Diyosisi ya mjini kati Arusha ambapo Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutaja rasmi kuwa tarehe 6 mwezi ujao atachukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kuwania urais .
Mpiga picha wa Chanell ten Arusha Aristrides Dotto na Elia Mbonea mwandishi wa gazeti la Mtanzania wakifanya mahojiano na Waziri wa mali asili na utalii Lazaro Nyarandu mara baada ya ibada ya jumapili katika Kanisa la KKKT Diyoyosis ya Mjini kati ambapo Waziri Nyarandu alitumia nafasi hiyo kutangaza rasmi siku atakayochukua fomu ya kuwania nafasi ya kuteuliwa kupeperusha bendera ya kuwania Urais kupitia chama cha Mpindunzi.
**************
WAZIRI wa Mali Asili na Utalii, Lazoro Nyalandu ambaye alishatangaza nia ya kukiomba chama Chake cha Mapinduzi (CCM) kumteua kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, anataraji kuchukua fomu ya kutimiza adhma yake hiyo Juni 7 mwaka huu mjini Dodoma.
ametangaza rasmi kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo baada ya kutangaza nia yake miezi saba iliyopita mkoani Singida.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana, Nyalandu ambaye ni Mbunge wa Singida Magharibi, baada ya kushiriki ibada ya jumapili katika kanisa la KKKT Usharika wa mjini Kati Arusha.
Nyalandu anaungana na makada wengine wa CCM kuingia katika kinyang’anyiro hicho ambapo anasema mpango na dhamira yake ya kuwania kuteuliwa na chama chake uko palepale huku akijinasibu kuwa dunia itaandika historia pale atakapo ibuka kidedea kwa kupeperusha bendera ya ccm katika kinyang’anyiro hicho.
“Mpango na dhamira yangu ya kuomba ridhaa ya Chama change kuniteua kugombea urais mwaka huu upo palepale na dunia itaandika historia pale nitakapo ibuka kidedea na kuipeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa mwaka huu,” alisema Nyalandu.
Waziri Nyalandu atakungana na makada na Mawaziri wakongwe katika siasa za Tanzania katika kuwania nafasi hiyo ndani ya CCM kama akina Edward Lowassa, Steven Wasira, Bernard Membe, Samuel Sitta, na wengineo wengi ambao tayari wameshatangaza nia na dhamira yao ya kuutaka urais.
↧
HIVI NDIVYO HALI ILIVYOKUWA WAKATI MH. LOWASSA ALIPOKUWA AKIELEKEA KWENYE UWANJA WA SHEIKH AMRI ABEID KUTANGAZA NIA YA URAIS
Sehemu ya Waendesha Bodaboda wa Jijini Arusha wakiusubiria msafara wa Mh. Lowassa, maeneo ya Uwanja wa Ndege wa Arusha.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI
Wadau wakichukua taswira ya Mh. Lowassa wakati alipotika eneo hilo.
Abiria kwenye basi pia hawakua nyuma kuchua Taswira zako pale walipomuona Mh. Lowassa akiwa kwenye gari lake.
Kila mmoja alikuwa na shauku ya kumuona na kumsabahi kama hivi.
Sehemu ya wakazi wa Arusha wakimshangilia Mh. Lowassa alipokuwa akipita katika barabara ya Sokoine, Jijini Arusha wakati alielekea kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kutangaza nia.
WanaArusha wakiwa wamejipanga Barabarani.
Ilikuwa ni shangwe tupu kwa kila aliemuona.
Wapiliza Matarumbeta wakawasahau mpaka maharusi waliowapa kazi, ili tu waweze kumuaona Mh. Lowassa akipita.
↧
Mh.Mwigulu alivyotangaza nia ya kuwania urais mkoani Dodoma jioni ya leo.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akiwapungia mkono baadhi ya wafuasi wake waliojitokeza kwa wingi,kumsikiliza wakati akitamka kutangania nia ya kugombea kiti cha uraui kupitia CCM.
Baadhi ya wakazi wa Dodoma wakimsikiliza kwa makini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alipokuwa akitangaza nia yake ya kugombea kiti cha Urais kupitia chama cha CCM
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba akizungumza mbele ya umati wa wakazi wa mji wa Dodom mapema jioni ya leo katika moja ya ukumbi wa chuo cha Mipango
Baadhi ya wakazi wa Dodoma wakimsikiliza kwa makini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alipokuwa akitangaza nia yake ya kugombea kiti cha Urais kupitia chama cha CCM
↧
↧
WAZIRI MEMBE AWASIHI WATANZANIA KUTOCHAGUA VIONGOZI WANAOSAKA UONGOZI KWA KUTOA RUSHWA
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatifa, Bernard Membe akimkabidhi Bi. Shamim Khan tuzo ya heshima ya kujishughulisha na kazi za kijamii hapa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akipokea tuzo maalumu kutoka kwa Sheikh Ismail Mohamed wakati wa tamasha la kwanza la Kaswida lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa na kudhaminiwa na Kampuni ya Dira ya Mtanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumza katika tamasha hilo la kwanza Qaswida, lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamini Mkapa,Mh Membe amewataka Watanzania kusubiri kwa hamu siku ya kutangaza nia ya kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu,
Alisema siku hiyo ya Juni 6, wananchi wasikilize nini anataka kuifanya nchi iweze kuondoka ilipo ikiwemo kuendelea kudumisha amani na utulivu uliopo. “Mkae tayari siku hiyo, naamini uongozi mzuri wa nchi ni ule wa kudumisha amani na utulivu na ili nchi iweze kusonga mbele, maadili kwa viongozi ni muhimu,” alisema Waziri Membe.
Membe alitumia nafasi hiyo kuwasihi Watanzania kuacha kuchagua viongozi ambao kwa nje, wanajinadi wana dini, lakini matendo hayaendani na maadili ya dini zao. Alisema ili mtu aweze kuaminika kuwa ana dini, jamii ifuatilie katika madhehebu yao, hivyo amewasihi wasichague viongozi wanaosaka uongozi kwa kutoa rushwa.
“Msikubali kuwa na viongozi ambao kwa nje, wanaojinadi kuwa na dini kinyume na matendo yao, lazima mchague wenye hofu ya Mungu ambayo husisitizwa na dini zote,” Alisema uongozi wa heshima ni ule unaochukia rushwa ambayo ni adui wa haki, hivyo amewataka wananchi kuwaogopa wapenda rushwa kama ukoma.
Baadhi ya Washiriki waliohudhuria tamasha hilo.
Baadhi ya Washiriki waliofika kwenye tamasha hilo la kwanza la Qaswida.
Baadhi ya Washiriki waliofika kwenye tamasha hilo la kwanza la Qaswida.
Mmoja wa washiriki wa tamasha la Qaswida kutoka Madrasa ya Nur-Pugu,Samiu Mussa akighani Qaswida mbele ya wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani) waliofika kwenye tamasha hilo,lililodhaminiwa na kampuni ya Dira ya Mtanzania
Kikundhi cha Qaswida kiitwacho Iqhyau wakighani Qaswida ya maadili
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatifa, Mh.Bernard Membe akipokelewa na wenyeji wake alipokuwa akiwasili katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa,kwa ajili ya kushiriki tamasha la kwanza la Qaswida
Mkurugenzi wa Kampuni ya Ulamaa Qaswida Promotions ambao ndio waandaji wa tamasha la kwanza la Qaswida,Ustaadh Jumanne Ligopora akimkaribisha mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimatifa, Mh.Bernard Membe
Sheikh Ismail Mohamed akizungumza jambo na Waziri Membe wakati wa tamasha la kwanza la Qaswida lililofanyika jijini Dar es Salaam na kudhaminiwa na Kampuni ya Dira ya Mtanzania.
Waimbaji wa Qaswida kutoka kikundi cha Muumini cha Buguruni jijini Dar es Salaam wakiimba kwenye tamasha la kwanza la Kaswida lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa. Tamasha hilo lilidhaminiwa na Kampuni ya Dira ya Mtanzania.
↧
Heri ya Kuzaliwa mwanakijiji Josephat Lukaza
Mwanakijiji Josephat Lukaza.
Tunapenda Kuchukua nafasi hii kukupongeza kwa kufikisha Miaka kadhaa ya kuzaliwa kwako na ukiwa sehemu ya wanakijiji wa digitali hapa duniani.
Tunachukua nafasi hii kumuomba Mwenyezi Mungu aendelee kukulinda na kukubariki kwa kukuongezea maisha marefu na yenye heri hapa duniani ili vizazi vingine viweze kufaidi baraka na neema za mwenyezi Mungu kupitia Wewe.
Leo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa Kwako iwe chachu na siku ya kufikiria ulipotoka, Ulipo na uendapo ili kuweza kutimiza Malengo yako huku Jamii inayokuzunguka Ikitegemea Mazuri mengi kutoka Kwako.
Ni ngumu kuyatimiza pekee yako lakini tunakuombea kwa Mungu akujalie wepesi katika kutimiza yaliyo mema mbele zake na Jamii inayokuzunguka Umekuwa Mtu ambae ni wa kipekee sana na mwenye kupenda kushirikiana na watu wote pale ambapo unaombwa msaada bila kujali huyu ni nani Mungu Akujalie uendelee na moyo huo huo na mazuri hayo hayo .
Tunakuombea Kwa Mwenyezi Mungu azidi kukupa maisha marefu na yenye Baraka na fanaka tele hapa duniani. Ukiwa kama Mwanakijiji Mwenzetu tunapenda kukutakia Heri ya Kumbukumbu ya Siku yako ya Kuzaliwa kwa kihispania wanasema
"Feliz cumpleaños Josephat Lukaza"
↧
TAMASHA LA KOMAA CONCERT LILIVYOFANA NDANI YA KIOTA CHA MARAHA CHA DAR LIVE JIJINI DAR.
Uongozi pamoja na Wafanyakazi wa kituo cha radio ya EFM 93.7 kwa pamoja wakikata keki kusherehekea kutimiza mwaka mmoja wa kituo hicho ambacho kwa sasa kinakuja kwa kasi jijini Dar na kwingineko,hafla hiyo ilikwenda sambamba na kuadhimisha miaka 16 ya msanii Mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature,katika tamasha lililoitwa KOMAA CONCERT,ambalo lilifanyika ndani ya kiota cha maraha cha Dar Live,Mbagala jijini Dar mwishoni mwa wiki na kuhudhuriwa na maelfu ya mashabiki na wapenzi wa muziki .
Lengo la kuwaburudisha Mashabiki wa Juma Nature na wasikiliazaji wa 93.7 EFM ilikuwa pia ni sehemu ya kuwashukuru mashabiki kwa ushirikiano wao kwa miaka kumi na sita ya muziki tangu kuanza msanii huyo Juma Nature aingie kwenye game ya Muziki nchini Tanzania.
Baadhi ya Wasanii walioshiriki kulinogesha tamasha hilo ni pamoja na Profesa Jay, Shetta, Snura, Makomando, Msagasumu na wengine wengi. Katika tamasha hilo lililowavutia wakazi wa Mbagala na vitongoji vyake,kiingilio kilipangwa kuwa ni shilingi 7,000 tu.
Meneja Mwasiliano na mambo ya Sheria wa EFM 93.7 Deniss ssebo alisema kuwa wanaamini Msanii Juma nature ni msanii mwenye kipaji kikubwa na aliyewahamasisha wasanii kibao kuingia katika muziki huu wa kizazi kipya hivyo anastahili kupewa heshima kubwa kwa mchango wake mkubwa katika kukuza muziki wa kizazi kipya,alisema na kuongeza kuwa lakini kwa Efm huyo ni msanii wa Kwanza tu na itaendelea kufanya hivyo kwa wasanii wengine kwa kuwa wanaaamini Muziki unaongea.
Mkurugenzi wa Efm Dj Majay akiongoza jopo la wafanyakazi wenzake kukata keki
Pichani kulia ni Meneja Mwasiliano na mambo ya Sheria wa EFM 93.7 Deniss Ssebo akizungumza jambo mbele ya mwashabiki na wapenzi wa muziki na pia wasikilizaji wakubwa wa kituo hicho kuhusiana na utaratibu mzima wa sherehe hiyo,kulia ni Mkurugenzi wa Efm Dj Majay akigawa keki kwa mashabiki waliofika kushuhudia tukio hilo ndani ya Dar Live.
Msanii Mkongwe wa muziki wa kizazi kipya Juma Nature akitumbuiza jukwaani mbele ya mashabiki wake,pia akiwashukuru kumpa sapoti ya kutosha tangu ameanza muziki na sasa anatimiza miaka 16 katika tasnia hiyo adhimu.
Wakongwe pamoja Juma Nature na Prof.Jay wakishoo love kwa mashabiki wao.
Msanii Snura na Madansa wake wakilishambulia jukwaa la KOMAA CONCERT
Msanii wa muziki wa kizazi kipya atambulikae kwa jina la kisanii Shetta akitumbuiza mbele ya mashabiki kibao waliofika kwenye tamasha la KOMAA CONCERT.
Makamuzi yalikuwa yakiendelea jukwaani.
Mashabiki walikuwa kibao.
Deejay Spar akionesha uwezo wake kwa mashabiki.
Shabiki wa ukweli kwa Juma Nature
Burudani ilipangwa sawa bin sawia huku Ma -Mc wakinogesha shughuli
Dar Live palinoga usiku huo wa KOMAA CONCERT
Mtangazaji mahiri wa EFM Capt.Gadn G Habash akizungumza jambo mbele ya mshabiki
Kila alieweza kuchukua kumbukumbu kwa aina yake,ilikuwa ruksaa.
Dj Majay akihakikisha mambo yanakwenda sawa
↧
Article 13
↧
↧
TAARIFA YA MAKUSANYO UJENZI YA MSIKITI
Kwa Jina la M/Mungu nina anza Andika , Nawashukuru Ndugu zangu WA TANZANIA ,KENYA na wasio kuwa hao kwa Upamoja wao wa Michango yao ya hali na Mali katika Kuimarisha UJENZI WA MSIKITI UNAONA KATIKA PICHA .
Nakushukuru BLOGS ZOTE ZA TANZANIA shukran za Pekee kwa Brother Mroki Mroki wa Father Kidevu Blog kwa kuwa Balozi Mzuri wa kulitangaza Jambo hili kwa Jamii pamoja na Blogs nyingi Marafiki wa Father Kidevu Blog. Leo Tarehe 30/5/2015 NAOMBA NIULETE MREJESHO HUU KWENU WA MAKUSANYO TOKA TAREHE 19/5 mpaka Tarehe 29/5/2015.
Na niwaombe Wadau kurudi tena kuleta mrejesho kama huu M/Mungu akipenda Tarehe 15/6/2015 .
UFUATAO NI MREJESHO WA MICHANGO YA UJENZI WA MSIKITI ULIOPO MKOA WA PWANI , WILAYA YA MKURANGA , KIJIJI CHA MLAMLENI , KITONGOJI CHA KIMBANGULILE .
Naomba Nianze Ijumaa , Tarehe 29/5/2015 . TUMEPATA KIASI CHA TSHS 238,700/=
Nakushukuru BLOGS ZOTE ZA TANZANIA shukran za Pekee kwa Brother Mroki Mroki wa Father Kidevu Blog kwa kuwa Balozi Mzuri wa kulitangaza Jambo hili kwa Jamii pamoja na Blogs nyingi Marafiki wa Father Kidevu Blog. Leo Tarehe 30/5/2015 NAOMBA NIULETE MREJESHO HUU KWENU WA MAKUSANYO TOKA TAREHE 19/5 mpaka Tarehe 29/5/2015.
Na niwaombe Wadau kurudi tena kuleta mrejesho kama huu M/Mungu akipenda Tarehe 15/6/2015 .
UFUATAO NI MREJESHO WA MICHANGO YA UJENZI WA MSIKITI ULIOPO MKOA WA PWANI , WILAYA YA MKURANGA , KIJIJI CHA MLAMLENI , KITONGOJI CHA KIMBANGULILE .
Naomba Nianze Ijumaa , Tarehe 29/5/2015 . TUMEPATA KIASI CHA TSHS 238,700/=
- CASH :- Tshs 96,700/= Nimezipokea Western Union.
- Tigo -Pesa Tshs 142,000/= Jumla ya Pesa zote unapata Tshs 238,700.
- TULIZOKUSANYA TSHS 1,373,500/= tukijumlisha na Siku ya Ijumaa Tarehe 29/5 tunapata TSHS 1,612,200/=
- Katika hiZo Pesa Taslimu ni Tshs 1,470,200/= na Tigo -Pesa 142,200/=
JUMLA YA MAKUSANYO YOTE Tshs 1,612,200/=
Balozi wetu wa KENYA Ali Bajiy Nasor update zake zitawajia atakapo kusanya Ahadi alizopewa Mpaka sasa amekusanya KSHS 4300/= ambae anakusanya kupitia M-PESA NAMBA +254725113783. ( Usajili ALI HAMIS ) .
Balozi wetu kwa waliopo Uingereza Tafadhali wawasiliane kwa Namba hii muwasilishe Michango yenu +447460340624.
Tanzania CHANGIA KUPITIA TIGO PESA 0715800772 (Brother ALI )
Mawasiliano zaidi Tuwasiliane Whatsapp : +255689604780 au Tembelea Facebook ID yetu :- Kijana Wa Kiislam DsmNAWASHUKURU WOTE MLIO CHANGIA NA MTAKAO ENDELEA KUCHANGIA KWA HALI NA MALI , kwa Pamoja TUIJENGE NYUMBA YA IBADA MALIPO YAKE AKHERA NI MAKUBWA ZAIDI NA DUNIANI PIA UNAPATA .
Daima Jamii ya watu huwa Nzuri zaidi na ikishikamana na IBADA na KUMTAMBUA MUUMBA kama Ni hivyo basi kwa PAMOJA TUUJENGE MSIKITI HUU tupate kuwa na Jamii Njema.
Wabillahi Taufiqh.
Wako katika Usimamizi wa hili .
GHALIB NASSOR MONERO.
↧
KAMPENI YA UELEWA KUHUSU TATIZO LA USONJI YAZINDULIWA JIJINI DAR
Mkurugenzi Mtendaji wa Lotus Clinic, Dialla Kassam (katikati), akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya kueneza uelewa kuhusu tatizo la usonji ‘Autism’ nchini Tanzania iliyondaliwa na Lotus Medical Clinic kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na taasisi ya Autism Education Trust ya Uingereza. Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia watu wenye Usonji Tanzania, Dk. Stella Rwezaula na Daktari wa kufundisha kuongea, Nazreem Sumar.
Mkurugenzi Mtendaji wa Lotus Clinic, Dialla Kassam (katikati), akitoa utambulisho kwa meza kuu mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana katika uzinduzi huo. Kushoto ni Mtaalam wa Afya kutoka taasisi ya Autism Education Trust ya Uingereza, Kevin Baskerville, Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia watu wenye Usonji Tanzania, Dk. Stella Rwezaula (wa pili kushoto), Daktari wa kufundisha kuongea wa Lotus, Nazreem Sumar (wa pili kulia) na Daktari Fathema Hasham.
Mkurugenzi Mtendaji wa Lotus Clinic, Dialla Kassam.
Mtaalam wa Afya kutoka taasisi ya Autism Education Trust ya Uingereza, Kevin Baskerville (kushoto) akipongezana na Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia watu wenye Usonji Tanzania, Dk. Stella Rwezaula,baada ya kumaliza mkutano na waandishi wa habari.
Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia watu wenye Usonji Tanzania, Dk. Stella Rwezaula (kushoto), akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Lotus Clinic, Dialla Kassam, baada ya kumaliza mkutano na waandishi wa habari.
---
Kampenii dhidi ya ugonjwa wa usonji yazinduliwa • Familia nyingi Tanzania hazina ufahamu wa hali hii Na Mwandishi wetu
Kliniki ya Lotus kwa kushirikiana na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, zimeanzisha kampeni mpya inayolenga kuelimisha uma kuhusu ugonjwa wa usonji (autism), ambao watanzania wengi hawaufahamu.
Ugomjwa huu sasa unatishia familia nyingi kwani dalili zake huanza utotoni na zinaweza kuendelea hadi ukubwani.
Akizugumza wakati wa uzinduzi huo Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama cha Kuhudumia watu wenye Usonji Tanzania, Dk. Stella Rwezaula ambaye pia ni mtaalamu wa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na pia ana mtoto mwenye ugonjwa huo, aliishukuru Kliniki ya Lotus kwa
kuwa katika mstari wa mbele kuanzisha kampeni hiyo ili kuwaelimisha watanzania kuhusu ugonjwa huo.
“Ni vyema ugonjwa huu ukigundulika mapema na kutibiwa ili aliyeathirika aweze kupona na kuishi maisha ya kawaida hapo baadaye kulingana na athari aliyoipata. Mtoto kuanzia miaka 0-6 anaweza
kutibiwa vizuri na kusaidia kubadilisha maisha yake,” alisema.
Alisema watoto wenye hali hii wana shida katika kuwasiliana na tabia zao ni kurudia rudia mambo anayofanya mara kwa mara na pia watuwengi wenye ugonjwa huu wananamna yao ya kujifunza, kusikiliza na kuitika.
“Mfano wa hali hii ni kwamba katikahali ya kawaida, mtoto wa mwaka mmoja hutabasamu au kuwa na furaha kila wakati, huiga mambo mbalimbali anayoona na kufuatilia vitu anavyoviona vikisogea, lakini mtoto mwenye ugonjwa huu hafanyi vitu hivi,”alisema.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kliniki ya Lotus, Dialla Kassam alisemamuelewa bado ni mdogo nchini Tanzania na watoto wengi huathiriwa na kuja kujukilana wakati hali imeshakuwa mbaya zaidi.
“Kukosa uelewa wa hali hii ya watoto wenye mahitaji huwafanya walimu na wazazi kudhani watoto ni watundu, wavivu au wanakera na wakati mwingine huadhibiwa kwa sababu hiyo wakati kwamba watoto hawa wanahitaji uangalizi wa karibu, kupendwa na kupata msaada kutoka kwa
walimu na wenzao,” alisema.
Alisisitiza umuhimu wa kuwafundisha walimu na wazazi kuhusu watoto hawa wenye mahitaji maalumu ili waweze kuwasaidia kuishi na kukubalika katika jamii.
Alisema kliniki yake inahudumia watoto wenye mahitaji ya aina hii jijini Dar es Salaam na kuwa timu yake ina wataalamu mbalimbali wanaofanya kazi pamoja ili kutoa elimu kuhusu watoto wenye matatizo haya.
“Hii inafanyika kwa kushirikiana na mashirika ya kimataifa kwa kutoa elimu kwa wadau mbalimbali wakiwemo walimu na wazazi kupitia warsha,mafunzo mbalimbali, kutafuta wafanyakazi wa kujitolea na kutoa rasilimali kwa taasisi mbalimbali kama Shule ya Mbuyuni ya watu wenye ugonjwa huu,” alisema.
Alisema kliniki mbalimbali kuhusu ugonjwa huo hufanyika katika Hospitall ya Taifa ya Muhimbili kila Alhamisi na kwamba Chama Cha Watu Wenye Usonji-Tanzania (NAPA-T) kimekuwa kikisaidia.
↧
DUNIA YATAZAMA WAKIMBIZI NYARUGUSU, WA MTABILA WAREJEA TENA
Baadhi ya Waomba hifadhi katika kambi ya Wakimbizi Nyarugusu wakiwa wamempumzika huku wengine wakipata chakula cha mchana kama walivyokutwa na kamera ya modewjiblog.
Kinababa nao hushiriki kuandaa chakula cha mchana kwa familia zao kama huyu aliyekutwa na kamera ya modewjiblog.
Mkuu wa Kambi ya Wakimbizi Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma, Sospeter Christopher Boyo (aliyesimama mwenye shati la kitenge) akisoma taarifa fupi ya Kambi ya Nyarugusu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe (aliyeketi mwenye suti ya kijivu) aliyeambatana na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez mara baada ya kuwasili kwenye kambi hiyo kujionea hali halisi ya mazingira na changamoto zinazowakabili Waomba hifadhi wa Burundi na Kongo. (Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).
Mkurugenzi wa Idara ya huduma za Wakimbizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke (wa pili kushoto) akizungumza jambo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) huku Mkuu wa kambi mpya inayotarajiwa kuanzishwa ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile (wa nne kulia) akitoa maelezo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe (wa tatu kushoto) mara tu baada ya kuwasili na kusomewa taarifa kwenye kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Wengine pichani ni baadhi ya viongozi wa ulinzi na usalama wa wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.
Mkuu wa kambi mpya inayotarajiwa kuanzishwa ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile akifafanua jambo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe wakati akitembelea na kukagua maeneo mbalimbali ya Kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole wakikagua sehemu wanayolala Waomba hifadhi wanaoendelea kuwasili katika kambi ya Nyarugusu ambayo inaelemewa kutokana na wingi wa Waomba hifadhi hao wanaoendelea kumiminika mjini Kigoma.
Muonekano wa moja ya chumba cha kulala familia za waomba hifadhi katika kambi ya Nyarugusu ambapo kifika muda wa kulala wanatandika mkeka chini katika vumbi hilo jekundu na kupata usingizi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe (mwenye suti ya kijivu), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) pamoja na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole (kushoto) wakisikiliza hoja mbalimbali kutoka kwa Waomba hifadhi wanaohifadhiwa kwenye kambi ya Wakimbizi Nyarugusu iliyopo wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma walipotembelea kambi hiyo kukagua kambi hiyo na kuangalia changamoto mbalimbali zinazowakabili na namna ya kuzitatua.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe (mwenye suti ya kijivu) akiteta jambo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakati walipotembelea kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma mwishoni mwa juma lililopita.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe akigawa vifaa vya matumizi ya nyumbani ambavyo ni Blangeti, Mkeka, Kontena la kuhifadhi chakula na dumu la maji la lita 10 kwa mmoja wa Waomba hifadhi waliowasili siku ya ziara ya kutembelea kambi ya Nyarugusu mwishoni mwa juma wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Anayeshuhudia tukio hilo ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (mwenye shati jeupe).Kulia ni Mkuu wa kambi mpya inayotarajiwa kuanzishwa ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile.
Waomba hifadhi na familia zoa wakiwa katika foleni ya kupokea vifaa hivyo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe akizungumza na Waomba hifadhi katika kambi ya Nyarugusu wakati alipofanya ziara ya kutembelea eneo hilo akiwa ameambatana na Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa pamoja na Mwakilishi wa shirika la kuhudumia Wakimbizi nchini (UNHCR).
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akizungumza na mmoja wa wakinamama anayeishi kwenye kambi ya Wakimbizi Nyarugusu wakati wa ziara maalum ya kutembelea maeneo hayo iliyohusisha Serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu wakibadilishana mawazo na mmoja wa wafanyakazi wa Shirika la Kimataifa Ia Uhamiaji (I.O.M) (katikati) ambaye jina lake halikuweza kupatikana kiurahisi katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Mkurugenzi wa Idara ya huduma za Wakimbizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke (mwenye suti ya kijivu) akifafanua jambo kwa Mh. Mathias Chikawe alipotembela katika chumba maalum kichotumika kufanya usajili kwa Waomba hifadhi na familia zao kwa ajili ya kupewa hati ya kuwa Wakimbizi kamili kama watatimiza vigezo vinavyohitajika. Aliyeketi kulia ni Msajili wa Waomba hifadhi, Ndalo Charles Bogohe.
Zoezi la usajili likiendelea kwa familia za waomba hifadhi katika kambi ya Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Wakinamama wakiandaa chakula cha mchana kwa familia zao kama walivyokutwa na kamera ya modewjiblog.
Sehemu ya familia za Waomba hifadhi katika kambi ya Wakimbizi Nyarugusu, wilayani Kasulu, mkoani Geita wakiendelea kujipanga baada ya kuwasili kwenye eneo hilo.
Moja ya familia za waomba hifadhi ikiwa imejipumzisha mara baada ya chakula cha mchana huku nyuso zao zikionekana kuwa na furaha na matumaini mapya.
Hili ni eneo ambalo Waomba hifadhi kutoka nchini Burundi wa kambi ya Nyarugusu wakiteka maji safi kwa matumizi yao.
Mkurugenzi wa Idara ya huduma za Wakimbizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Harrison Mseke (kushoto) akizungumza jambo na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) wakati wakielekea kukagua vyumba vya madarasa katika shule ya msingi Mapendo ambayo yamegeuzwa kuwa nyumba za kulala Waomba hifadhi, kutokana na uhaba wa makazi ya kuishi kwenye maeneo ya kambi ya Nyarugusu, wilayani Kasulu mkoani Kigoma. Wengine pichani ni baadhi ya viongozi wa ulinzi na usalama wa wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma katika msafara huo.
Eneo la shule ya msingi Mapendo katika kambi ya Wakimbizi Nyarugusu ambalo kwa sasa linatumika kuhifadhi Waomba hifadhi wanaoendelea kuwasili nchini wakitokea Burundi kupitia mji wa Kigoma.
Madawati ya wanafunzi katika shule ya msingi Mapendo yakiwa nje ya madarasa yakitumika kuanikiwa nguo na huku wakati wa msimu wa mvua yakinyeshewa.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakibadilishana mawazo na wasimizi wa kambi hizo za Nyarugusu wakati wa ziara ya siku moja wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) akiwa ameambatana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Mathias Chikawe wakikagua eneo jipya litakaloitwa Nyarugusu B lililotolewa na serikali kwa ajili ya Waomba hifadhi wanaoendelea kumiminika mjini Kigoma ambalo liko mbioni kutengenezwa na kukamilika ndani ya miezi 3 ijayo.
Eneo jipya la kambi ya Nyarugusu B ambalo limetengwa na serikali ya Jamhuri ya Tanzania kwa ajili ya makazi ya Waomba hifadhi wanataotenganishwa Burundi na Congo mara tu baada ya kukamilika.
Muonekano wa eneo jingine la makazi ya Waombahifadhi ndani ya kambi ya Wakimbizi Nyarugusu iliyopo wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Amani na upendo itawale kati yetu......ndivyo wanavyosema kwa pamoja baadhi ya watoto waomba hifadhi wakifurahia picha pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez.
Na Modewjiblog team, Kigoma
WAKATI dunia kupitia Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanahangika kutanzua changamoto za wakimbizi Nyarugusu, mkoani Kigoma imeelezwa kuwa idadi kubwa ya Wakimbizi waliorejeshwa nchini Burundi kutoka kambi ya Mtabila iliyoko Kigoma iliyofungwa rasmi Desemba, 2012 wameingia tena nchini na kujazana katika makazi ya muda ya Nyarugusu wakiomba hifadhi.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu Sospter Christopher wakati akizungumza na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi aliyekwenda kuangalia hali halisi ya kambi ya Nyarugusu na Wakimbizi akiambatana na Maofisa wa Umoja wa Mataifa akiwemo Mratibu wa Mashirika hayo nchini Alvaro Rodriguez. Kurejea kwa wingi kwa Wakimbizi hao ni pigo kisaikolojia kwa watu ambao walirejeshwa nyumbani kwa kuonekana kwamba hali ni shwari na walikuwa wameanza kuishi maisha ya kawaida.
Mkuu huyo wa kambi alisema idadi hiyo ikichanganyika na wengine imafanya kambi kuhemewa na kuonekana haja ya kutafuta eneo jingine la kupiga kambi kwa ajili ya Wakimbizi hao ambao mpaka mwishoni mwa wiki iliyopita walikuwa zaidi ya elfu 51.
“ Kwa sababu tunapokea idadi kubwa ya waomba hifadhi toka Burundi, tumekuwa tukiongeza idadi ya vituo vya mapokezi ili kukidhi mahitaji ya kuwapokea wakati tukisubiri maelekezo toka ngazi za juu za kuwahamishia Migunga Hills eneo linalopendekezwa kufunguliwa kambi ya Nyarugusu B” alisema Christopher mbele ya Waziri Chikawe.
Alisema walianza kupokea waomba hifadhi hapo kambini kuanzia Aprili 29, 2015 kwa idadi ndogo kabisa ya watu 36, lakini idadi hiyo ilianza kuongezeka siku hadi siku na kufikia Mei 27 mwaka huu idadi yao ilifikia 48,333, idadi kubwa ikiwa wanawake na watoto. Wakimbizi hao walikuwa wakipitia vituo vya Kigoma (27,638), Manyovu (4,439), Kilelema (1,603) na Kigadye (1,291).
Kambi hiyo yenye uwezo wa kubeba watu 50,000 imeelemewa kwa sababu ya ujio mpya uliosababisha kuwepo kwa Wakimbizi zaidi ya 106,410.
Kuna matatizo zaidi ya milipuko ya wagonjwa kambi hii imechanganywa na Wakimbizi wa Kongo watu ambao hawana utamaduni wa pamoja na kuonekana hatari ya kukabiliana kwa kutosikilizana. Aidha kambi hiyo pamoja na kuwahifadhi waburundi wapo pia Wakimbizi kutoka Kongo wapatao 54,706; Burundi,3261 ; Rwanda 72; Uganda 17; Sudan Kusini wanane; Kenya 7; Somalia 3; Ethiopia 1; Zimbabwe 1; na Ivory coast 1.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari walioambatana naye katika ziara hiyo kuhusu hali ya baadae ya Wakimbizi wa Kongo ambao wapo nchini kwa takribani miaka 19 sasa, Waziri Chikawe alisema kwamba serikali haina mpango wa kuwapa uraia kwa sasa ingawa Marekani imesema itawachukua Wakimbizi elfu 30 kuwapeleka kwao na kwingine duniani.
“hatuna mpango wa kuwapa uraia kwa sasa…” alisema Chikawe na kusema kwamba kwa kuondolewa kwa hao wengine kutasaidia kupunguza idadi yao katika kambi hiyo. Alisema kwamba ni lengo la serikali kuhakikisha kwamba kambi hiyo inapunguzwa ili kuweza kuchangia ipasavyo kwa hali bora ya Wakimbizi na kwamba mchakato wa kuwaangalia waomba hifadhi kama wanafaa kuwa Wakimbizi unaendelea.
Akizungumzia malalamiko ya upatikanaji wa chakula, Waziri Chikawe alisema kwamba si kweli kuwa kuna watu hawajapata chakula kwa siku saba la sivyo wangelikufa. Alisema wengi wa Wakimbizi ni watoto na kwamba wanapoingia nchini wanapewa vyakula vikavu (kama biskuti) lakini wakishafika kambini wanapewa chakula kilichopikwa na resheni ya siku 14 .
Alisisitiza kuwa kama kungelikuwa hakuna chakula watoto hao wasingeishi, labda kama wanataka kuongezewa chakula zaidi. Kuhusu ujenzi wa kambi mpya Migunga alisema kwamba wataalamu wanaangalia barabara mbadala kwani iliyopo sasa pamoja na kuhitajika milioni 300 kuitengeneza lakini bado kila mvua itakapokuwa inanyesha itahitaji kutengenezwa.
Naye Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mtaifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Joyce Mends-Cole katika mahojiano na waandishi wa habari aliishukuru serikali ya Tanzania kwa kufungua mipaka ili Wakimbizi waweze kuingia na kutoa eneo kwa ajili ya kambi mpya kutokana na ya sasa kujaa sana.
Aidha aliishukuru serikali ya Uingereza kwa kuwa ya kwanza kutoa misaada kwa ajili ya Wakimbizi hao na kutarajia nchi nyingine kama Marekani itafanya hivyo mapema ili kuisaidia serikali ya Tanzania katika kuhudumia waomba hifadhi. Naye Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Alvaro Rodriguez amesema wanafanya kila linalowezekana ili kupunguza idadi ya Wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu kwa kuwapatia eneo jingine la kujihifadhi.
Alisema kwa kuwatoa hapo watasaidia shule zilizofungwa ambazo zinasomesha watoto kutoka kwa Wakimbizi wa Kongo kurejea madarasani kukamilisha mtaala wao.
↧
More Pages to Explore .....