Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

Google Waja na Miwani Inayopiga na Kurekodi Picha kwa Maelekezo

$
0
0
Miwani ya google
TEKNOLOJIA waliyotumia Google kutengeneza miwani ambayo ina uwezo wa kumpiga picha mtu au kurekodi bila muhusika kujua (google glass) sio mpya ila Kampuni ya Google ndio wakwanza kuja na teknoloji hiyo, ili kila mtu aweze kutumia na inakadiriwa huwenda bidhaa hii ikafanya vizuri sana katika mauzo. 

 Google glass ni rahisi sana kutumia, kama unataka kupiga picha unachotakiwa kusema ni “OK Glass, take a picture.” upo kwenye foleni unaona fujo unataka kuchukua video, mwambie Google Glass naye atakusaidia kuchukua video. 

Hii ndio kali, unataka kuwaonyesha ndugu na marafiki kitu unachokiona wakati huo huo? Google glass inafanya yote hayo, inakuja na kitu kama "Skype-style video chat". Umesafiri kwenda kuchukua mzigo China? Google glass itakusaidia kuchukua kutafsiri lugha. Umeenda Zanzibar kutembelea majengo ya kitalii na unabaki kushangaa shangaa, uliza Google glass na itakupa tour guide. 

Google glass ni kifaa ambacho unaweza kutumia kurekodi video, kupiga picha, kutafuta habari katika Google, kutafsiri lugha, na unaweza fanya yote haya bila kutumia mikono yako (hands free). Tatizo ni kwamba, ukishavaa hiki kifaa kama miwani, watu hawajui kama unawarekodi kwenye video au vipi, na kwa wabongo walivyo wanavyojua kujihami kupigwa picha au kurekodiwa kwenye video, ukivaa Google glass unaweza tolewa baa. 

Kwa nchini Tanzania kifaa hiki ambacho kitakuwa na wastani wa bei ya sh. mil 2. 2 ($1500). Hata hivyo kifaa hicho kinachovaliwa kama miwani, sijui kama utaweza kutembea nacho hata hatua kumi kabla ya vibaka kukuvaa baada ya kujua thamani yake. 

Tusubiri Google wakiwezeshe kifaa hiki kiweze elewa kiswahili ndio na sisi tutakifaidi zaidi kwani hapa hamna kubonyeza bonyesha ni kuongea tu. Je ukipata Google glass utatumia kifaa hiki cha kisasa kufanyia nini? Acha maoni yako.

TAHADHARI KUHUSU WATU WANAO FANYA UTAPELI MTANDAONI KWA JINA LA TAASISI YA RAFIKI ELIMU.

$
0
0

Uongozi  wa  Taasisi  Ya  RafikiElimu  Foundation  unapenda  kuwatahadharisha  wananchi wote  juu  ya  kuibuka  kwa  kundi  la watu  wanao  fanya  utapeli  mitandaoni  kwa  kutumia  jina  la  Taasisi  ya  RafikiElimu   Foundation.  Siku  ya  Ijumaa  ya  leo  tarehe  28  FEBRUARI  2013  mnamo  majira  ya  saa  5  kamili asubuhi, ofisi  yetu  ilitembelewa  na  mwanadada  aliye  jitambulisha  kwa  jina  la HAWA  MUSSA. Mwanadada  huyu  baada  ya  kujitambulisha, aliomba  kuonana  na  HUMAN  RESOURCES  MANAGER  wa  Taasisi  ya  RafikiElimu , baada  ya  kumuona, ali  onyesha  fomu  aliyopewa  kupitia  mtandaoni  na  watu  walio  jitambulisha  kwake  kama RafikiElimu  Foundation

Watu  hao  walitoa  tangazo  kupitia  mtandao  wa  ZOOM TANZANIA  wakidai  kuwa  wana wa  link, wahitimu  mbalimbali  wa  vyuo  vikuu    na  taasisi  mbalimbali  zisizo  kuwa  za  kiserikali  kwa  ajili ya  kufanya  kazi  katika  taasisi  hizo  kama volunteers.  Mwanadada  huyu  akaendelea  kueleza  ya  kwamba, baada  ya  kuona  tangazo  hilo  alivutiwa  na  kutuma  maombi  ambapo  walimjibu  kwa  kumpatia  fomu  aliyo  takiwa  kuijaza  na  kuirejesha  kwao.  

Baada  ya  kujaza  fomu  hiyo, walimtumia  barua  pepe  nyingine  na  kumwambia  kwamba  maombi  yake  yamekubaliwa, kisha  wakamtumia  fomu  na  kumwambia  aijaze, aimbatanishe  na   CV  yake, na  kuwatumia  pesa  kiasi  cha  shilingi  Elfu  Tano  ( TSH. 5,000/=)  kwa  njia  ya  MPESA   kwenda  namba  0763906931  ( AMBAYO  MBAYA  ZAIDI,  WAMEISAJILI  KWA  JINA  LA  RAFIKIELIMU  ). Baada  ya  kuwatumia  pesa  hiyo, wakamwambia    aripoti  na  fomu  yake  iliyojazwa, na  kuambatanishwa  na  CV kwa  HUMAN  RESOURCES  MANAGER   wa  Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, ( ( Ambaye  kwenye  barua  hiyo  walimtaja  kama  Mr. ALBERT  EMMANUEL  )  siku  ya  tarehe  28  FEBRUARI  2013  saa  5  kamili  asubuhi.

Sisi  kama  taasisi,   tulishangazwa  sana  na  taarifa  hii, kwa  sababu  kwanza,  hatukutoa  tangazo  la  aina  hiyo, lakini  pili  huwa  hatuwatozi  watu  pesa  ili  kuwatafutia   nafasi  za  kujitolea. Tulifadhaishwa  sana, na    tukabaini  kuwepo  kwa   utapeli unaofanywa  na  watu  kwa  jina  letu,   hivyo  moja  kwa  moja  tukaenda  kuripoti  tukio  hili  la  uhalifu  katika  kituo  kidogo  cha  polisi  kilichopo  katika  kituo  kidogo  cha  polisi   cha  Chuo  Kikuu  Cha  Dar  Es  salaam, sehemu  ya  Mlimani  na  kupewa  RB  namba    UD/RB/849/2013  WIZI  KWA  NJIA  YA  MTANDAO.

Baada  ya  hapo,  tukaenda  kulitazama  tangazo  hilo  katika  mtandao  wa  Zoom Tanzania.  Tangazo  hili lililo  wekwa  mtandaoni  mnamo siku  ya  tarehe   05 FEBRUARI  2013  lilisomeka  kama  ifuatavyo :

Volunteer program
Rafiki Foundation

Date Listed: Feb 5, 2013
Email Address: Click to Email
Areas: Mbeya, Morogoro
Application Deadline: Feb 28, 2013

Position Description:
We are looking for Highly motivated individuals to volunteer in different private Organisation at the following places
1. Iringa (5) posts
2. Njombe (6) posts
3. Dar es salaam  (7) posts
4. Mbeya (4) posts
5. Ruvuma (8) posts
6. Morogoro (3) posts

Application Instructions:
Candidates who are interested in such program must write the letter for inquire to the Email Link above   then he/she will receive the NGO application form depending to his/her area of interest.
Note: the organisation will provide to you only field allowance when you are out of the office (Field areas), Transport, Tea and Lunch.
Late submission will not be considered.


UDHAIFU  WA  TANGAZO  HILI:
i.  Namba  waliyo  weka  haipo (  IT  DOES NOT  EXIST  )
ii.   Wanasema  " We are looking for Highly motivated individuals to volunteer in different private Organisation ........

(   RafikiElimu  Foundation, huwa  hatu  'deal' na  private  organizations. Tuna  deal  na  NON-GOVERNMENTAL  ORGANIZATIONS  ).

iii.  Namba  za  simu  walizo  weka, hazipo  kwenye  blogu  yetu.

iv.   Katika  tangazo  lao,  hakuna  link  inayo  onyesha   anuani  ya  blogu  yetu.

v.   Wametoa  tangazo  lao  kwa  lugha  ya  kiingereza, sisi  kama  RafikiElimu  Foundation  hatujawahi  kutoa  tangazo  kwa  lugha  ya  kiingereza.

vi.  Kiingereza  walicho  tumia  ni  kibovu  sana.  

vii.  Anuani  ya  barua  pepe  waliyo  tumia  ni  batili  na  wala  haipo  kwenye  taarifa zetu  za  kwenye  blogu  yetu.   Anwani  ya  barua  pepe  waliyo   tumia  ni  :  graduatevolunteer@gmail.com    wakati   anuani  ya  barua  pepe  ya  taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation  ni   :  rafikielimutanzania@gmail.com


HATUA  TULIYO  CHUKUA  BAADA  YA  KULIONA  TANGAZO  HILI  NI  KUUFAHAMISHA  UONGOZI  WA  MTANDAO  WA  ZOOM    TANZANIA, KUHUSU  TANGAZO  HILO  LA  KITAPELI  ILI  KUWANUSURU   WANANCHI  WENGINE  ZAIDI   NA  TUNASHUKURU  ZOOM  TANZANIA  WAMEPOKEA  TAARIFA  YETU  NA  KUAHIDI  KULISHUGHULIKIA  TATIZO  HILO  KWA  KULIONDOA  KATIKA  TOVUTI  YAO .







                                 MAELEZO   YA  KWENYE   FOMU   YA  MATAPELI  HAWA


























 UDHAIFU   WA   FOMU   HII  :

1.  Namba  zao  walizo  zitoa  kwenye  fomu  hizi  za  kitapeli, hazipatikani  muda  wote, wakati  namba  zetu  zinapatikana  muda  wote.

2.   Katika  fomu  yao  ya  kitapeli, hawajaandika  location  ya  ofisi  zilipo, hawajaweka  sanduku  la  barua,  blog  adress   wala  namba  za  simu  zinazo  patikana.

3.   Hakuna  logo.

4.  Hakuna  sahihi.
5. Hakuna  jina
6. Hakuna  muhuri.









Tulipo  jaribu  kuwapigia  kwa  namba  walizo  ziweka  kwenye  mtandao  ambazo  ni  +255 22 524 3785  tukajibiwa  ya  kwamba  namba  hizo  hazipo  (  the  number  your  dialing  are  not existing  ).

Na  tulipo  jaribu  kuwapigia  kwa  namba   0763906931  nazo  zikawa  hazipatikani  muda  wote.




Taasisi  yangu  kwa  kushirikiana  na  jeshi  la  polisi,  tunafanya  msako  mkali  dhidi  ya  mtu  ama  watu  hawa  na  tunaahidi  ya  kwamba  tutawakamata  ndani  ya  muda  ambao  si  mrefu  sana  na  kuwafikisha  kwenye  vyombo  vya  dola.


OMBI  :  Kama   na  wewe  ni  miongoni  mwa  walio  tapeliwa  na  watu  hawa, tafadhali  wasiliana  nasi  kwa simu   0782405936  ili  tushirikiane  katika  kuhakikisha  wahalifu  hawa  wanatiwa  mbaroni  na  kufikishwa  katika  vyombo   vya  sheria. 


TAMKO  LETU  :  Tunalaani  vikali  kitendo  kilicho  fanywa  na  ama  kinacho  fanywa  na  wahalifu  hawa, kwani  mbali  na  kuiba  pesa  za  watanzania  masikini  kama  wao,  kitendo  hiki  kinachafua  jina  la  taasisi  yetu  ambayo  inafanya  kazi  zake  kwa  kushirikiana  na  wananchi.


                ANGALIZO  KWA  WANAO  TAFUTA  KAZI : 
  

i. Unapo  tuma  maombi  ya  kazi  katika  sehemu  yoyote  ile  halafu  ukaambiwa  utume  pesa  ili  kupatiwa  kazi  hiyo, jua  kwamba    huo  ni  utapeli  na  kazi  hiyo  haipo.

ii.  Hakikisha  unazifahamu  ofisi  za     taasisi  hiyo  zilipo  kabla  ya  kuchukua  maamuzi  yoyote  yanayo  husisha  pesa.  

iiii.  Ni  vyema  kufanya  uchunguzi  ili  kujiridhisha  kama  taasisi  hiyo  kweli  ipo.

iv.  Unapoona  tangazo  la kazi, na  kuvutiwa  nalo, jitaidi  kuwapigia  simu  walioweka  tangazo  na  kuwauliza   maswali mawili  matatu kuhusu  kazi  hiyo.  

HATA  HIVYO  :  Ninashukuru, mpaka sasa  ni  mtu  mmoja  tu  ndie  aliyeripoti  kutapeliwa  na  watu  hao  kwa  jina  la  taasisi  yetu.  Hii  ina  maana  kuwa  watanzania  wengi  wameelimika  kwa  sasa, inawezekana   watu  wengine  wali  lishtukia  tangazo  hili  na  kuachana  nalo.



ZINGATIA  :  Taarifa  yoyote  inayo  husu  taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, lazima  iripotiwe  kwenye  blogu  yetu  ambayo  ni  :
http://www.rafikielimu.blogspot.com//   taarifa  yoyote  ile  ambayo   haijaripotiwa  kwenye   blogu  yetu  hii, haihusiani  na  taasisi  yetu  wala  taasisi  yetu  haitawajibika  kwa  vyovyote  vile  na  taarifa  yetu.

Imetolewa  na    
UONGOZI,
RAFIKIELIMU  FOUNDATION,
DAR  ES  SALAAM.

0782405936

ushabiki wa mpira unataka moyo kweli kweli..!

mzoga unaondolowa..!

kujituma na kufanya kazi kwa bidiii ndio inafanya life isongeshe..!

sijaielewa akili ya mkulima huyu..!

mamlaka ya hali ya hewa wametangaza kutakuwepo na uhaba wa mvua.

waleee waaaa.......!


kitu kinapigwa sop sop...!

Neno La Leo: " Inuka Twende Ni Kwa Walioagana!"

$
0
0


Ndugu zangu,

Hakuna wawili watembeao pamoja pasi na maelewano. 
Ukiwaona wanadamu wawili wanatembea pamoja, basi, wana makubaliano. Ni watu waliopatana.

Kwenye kundi la watu wa mataifa tofauti ukimsikia Mtanzania anamtamkia Mtanzania mwenzake, tena kwa Kiswahili; " E bwana inuka twende zetu!", na Mtanzania huyo mwingine akabaki amekaa bila kushtuka, basi, utilie mashaka UTanzania wake.

Ndio, " Inuka twende ni kwa waliogana". Ni watu wenye kufahamiana. Ni ndugu. Nimeanza kuingiwa na hofu kuwa Watanzania tumeanza kupoteana kama ndugu. " Inuka twende' yetu imeanza kuangaliwa kwa sura ya udini, ukabila na itikadi. 

Hatujafika pabaya sana, lakini, tunakoelekea ni kubaya. Tumeshaziona ishara. Miongoni mwetu Watanzania tumeanza kuzisikia kaauli za ; " Umewasikia jamaa zetu Wakrito? Umewasikia jamaa zetu Waislamu? Umewasikia jamaa zetu WaZanzibar? Umewasikia jamaa zetu wa Bara?......"

Hizi ni ishara za undugu unaosambaratika. Zamani sisi sote tulikuwa ni ndugu. Tulitembea pamoja, ishara ya watu tuliopatana.  Leo kuna Watanzania wanaoambiwa; " E bwana wee, siku hizi nakuona unatembea na kuongea na wale jamaa zetu wa upande mwingine!"

Ndio, Watanzania tumeacha kuwa ndugu. Tunagawanyika kwenye mapande. Ni kwa kuzitazama tofauti za dini, kabila na itikadi.  Hatujafikia pabaya, lakini, tunakoelekea ni kubaya. Tukumbuke; " Inuka twende ni kwa waliogana". Watanzania tulishaagana. Tulishakubaliana. Tulijua tunakokwenda kama Taifa. Kama ndugu. Tumeanza sasa kusambaratika. 

Tuinuke sasa twende kupambana na yote yenye kutugawa kama ndugu wa taifa moja. Tuna kila sababu, nia na uwezo wa kushinda mapambano haya dhidi ya ubaguzi wa aina zote.

Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0788 111 765

KUMEKUCHA CCM KATA YA JANGWANI

$
0
0

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir (kulia) akipiga makofi  ya furaha wakati wa kumkaribisha Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa, Rameshi Patel  kufungua mkutano wao wa kwanza wa Halmashauri kuu ya kata hiyo Dar es salaam  tangia wachaguliwe kushoto ni Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Ilala Said Side.


Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa, Ramesh Patel katikati na kulia ni Mwenyekiti wa CCM Kata ya Jangwani Mohamed Bawazir pamoja na Diwani Bi Eshe Sururu na kushoto ni Katibu wa CCM kata hiyo Majala Balawa .


Baadhi ya wajumbe wa Halmashauri kuu ya CCM kata ya Jangwani wakipiga vigeregere na kumpongeza Mwenyekiti wao Mohamed Bawazir, Dar es salaam jana  wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kwanza tangia wachaguliwe viongozi wa kata hiyo.

MICHUANO YA MPINGA CUP YAANZA RASMI LEO

$
0
0
Kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es Saalam Suleiman Kova akijiandaa kudaka mpira ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa michuano ya Mpinga Cup inayowahusisha waendesha pikipiki maarufu kama Bodabado inayoanza rasmi leo kwa muda wa wiki moja. Mpinga cup imedhaminiwa na  Airtel , Rotary Club, Mr price na Shoprite  ikiwa na lengo la kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki na kupunguza ajali barabarani . akishuhudia kushoto ni  Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani  SACP. Mohamed Mpinga
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Seleman Kovaakidaka mpira ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa michuano ya Mpinga Cup inayowahusisha waendesha pikipiki maarufu kama Bodabado inayoanza rasmi leo kwa muda wa wiki moja. Mpinga cup imedhaminiwa na  Airtel , Rotary Club, Mr price na Shoprite  ikiwa na lengo la kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki na kupunguza ajali barabarani . akishuhudia kushoto ni  Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani  SACP. Mohamed Mpinga. 
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Seleman Kovaakikagua timu wakati wa uzinduzi wa  michuano ya Mpinga Cup inayowahusisha waendesha pikipiki maarufu kama Bodabado inayoanza rasmi leo kwa muda wa wiki moja. Michuano hii imeanza rasmi kwa mechi kati ya Kawe Tiptop na Manzese anayefata pichani ni Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani  SACP. Mohamed Mpinga. 
Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani  SACP. Mohamed Mpinga akikagua timu kabla ya mechi kati ya  Kawe Tiptop na Manzese leo wakati wa uzinduzi wa michuano ya Mpinga Cup, anayefata pichani ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando. 
kikosi cha timu ya Kawe Tiptop katika picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa mashindano ya mpinga Cup yaliyofanyika leo katika viwanja vya polisi oyesterbay , katikati pichani ni Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Seleman Kovaakifatiwa na Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani  SACP. Mohamed Mpinga.
kikosi cha timu ya Manzese  katika picha ya pamoja wakati wa uzinduzi wa mashindano ya mpinga Cup yaliyofanyika leo katika viwanja vya polisi oyesterbay , katikati pichani ni Kanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es Saalam Suleiman Kova akifatiwa na Mkuu wa kikosi cha Usalama barabarani  SACP. Mohamed Mpinga

Rais Kikwete apokea ujumbe Maalum Kutoka Kwa Rais Omar El Bashir wa Sudan

$
0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea ujumbe maalumu kutoka kwa Rais Omar El Bashir wa Sudan ulioletwa na Mhe.Dkt.Nafie Ali Nafie ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.(picha na Freddy Maro)
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mhe.Dkt.Nafie Ali Nafie ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi.(picha na Freddy Maro).

WAZIRI WA HABARI SAID ALI MBAROUK AZINDUA DIGITAL ZANZIBAR.

$
0
0
 Waziri wa Habari,Utalii Utamaduni na Michezo Said Ali Mbarouk akizungumza na wandishi wa habari jinsi ya utaratibu wa Digital utavyoanza na upatikanaji wa Vingamuzi huko ktk ukumbi wa salama holl Bwawani Mjini Zanzibar. PICHA NA YUSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.
Waandi wa habari wa vyombo mbali mbali wakimsikiliza Waziri wa Habari,Utalii Utamaduni na Michezo Said Ali Mbarouk hayupo pichani akizungumzia jinsi ya utaratibu wa Digital utavyoanza na upatikanaji wa Ving'amuzi huko ktk ukumbi wa salama holl Bwawani Mjini Zanzibar.

Kamanda kova autaja mtandao wa matapeli,azushiwa yu hoi kitandani..!


tatizo la maji jijini dar litakwisha lini..?

$
0
0
Mmoja wa wakazi wa eneo la Kimara,jijini Dar akisukuma mkokoteni wake uliobeba madumu ya maji mapema leo mara baada ya kunaswa na camaera ya Jiachie.Aidha eneo hilo la Kimara na maeneo mengine kadhaa ya jiji la Dar yamekuwa yakikumbwa na ukosefu mkubwa wa maji safi na salama.

kumekucha mwanamakuka awards 2013

WOMENCELEBRATIONS 2 DAYS TO GO

$
0
0

HAYA WANAWAKE WENZANGU.....WENGI MNA TICKET ZENU MKONONI
NGUO ZENU ZA #AFRICANPRINT.... Mmezihang wenyewe lakini ;)

NAOMBA NIWASISITIZIE PLZZZZZZZZZZZZZ PLZZZZZZZZZZZZZZZ TAFADHALIIIIINI SAANA.

TUZINGATIE MUDA ILI PROGRAM ZETU ZIENDE SAWA TUPATE

 MUDA WA KUCHEZE KWA RAHA ZETU

MAMBO YA KIKE KIKENI SHOST!!

MANGULA AKUTANA NA MSAIDIZI WA RAIS WA SUDAN LEO

$
0
0

Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara, Philip Mangula (kushoto) akiagana na mgeni wake, Nafie Ali Nafie, Msaidizi wa Rais wa Sudan, baada ya mazungumzo yao leo Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.Picha na Richar Mwaikenda wa Matukio Blog.

Balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania Mhe.Dianna Melrose awasilisha hati zake za utambulisho ikulu

$
0
0
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania Mhe.Dianna Melrose ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi(picha na Freddy Maro)
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images