Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

Mtendaji Mkuu TTCL Azinduwa Bonanza la SHIMMUTA Dar

$
0
0
 Ofisa Mkuu wa Biashara utoka TTCL, Kanda ya Dar es Salaam, Karim Bablia akizungumza kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura katika hafla ya uzinduzi wa Bonanza la Shirikisho la Michezo la mashirika ya.Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) jana viwanja vya Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam.
 Kikosi cha UDSM mpira wa miguu kilichoshiriki Bonanza la Shirikisho la Michezo la mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) jana viwanja vya Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam.
Kikosi cha kampuni ya TTCL mpira wa miguu kilichoshiriki Bonanza la Shirikisho la Michezo la mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) jana viwanja vya Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam.
========  =======  =========
OFISA Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura Oktoba 11, 2014 amezinduwa Bonanza la Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania (SHIMMUTA) lililofanyika viwanja vya Chuo Kikuu (UDSM) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hotuba yake, iliyosomwa kwa niaba na Ofisa Mkuu wa Biashara wa TTCL, Kanda ya Dar es Salaam, Karim Bablia aliwataka washiriki wa bonanza kutumia nafasi hiyo ya kuwa pamoja ili kufahamiana zaidi, kubadilishana mawazo na kushirikiana.

“…Bonanza hili limetuwezesha sisi Wanamichezo Wafanyakazi kuweza kufahamiana miongoni mwetu, kubadilishana mawazo ya nini kinafanyika kwenye kampuni, mashirika au taasisi zetu ikiwa ni pamoja na kupeana taarifa za huduma na bidhaa tunazotoa kwa wateja wetu na wananchi kwa ujumla,” alisema Dk. Kazaura.

Aidha aliipongeza Kamati ya maandalizi ya bonanza hilo kwa kitendo cha kuwakutanisha pamoja wanamichezo hao, kwani mbali na kushindana kimichezo na kufahamiana wanapata fursa ya kujenga afya za wafanyakazi, umoja na undugu.

Alizishauri taasisi hizo kutenge muda maalum wa kufanya mazoezi kwenye taasisi zao kila siku kwa lengo la kuimarisha afya na kuiwezesha miili kuwa na nguvu ili kuzalisha tija zaidi kwenye sehemu zao za kazi, kwani taasisi kuwa na mfanyakazi lege lege haiwezi kuzalisha tija zaidi mahali pa kazi. 

“…Napenda nitumie nafasi hii kuwapongezeni Kamati nzima ya Utendaji ya SHIMMUTA kwa jambo hili kubwa mlilofanya ambalo kusema kweli limetukutanisha sisi wanamichezo wafanyakazi mahala pamoja na kuweza kufanya michezo mbalimbali ambayo kwa hakika, naona imewawezesha 
Wanamichezo Wafanyakazi wa rika zote kucheza kila mmoja na mchezo aliouzoea.

Hata hivyo alizipongeza taasisi na mashirika yaliyoshiriki katika bonanza hilo ikiwemo kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Chuo cha Tiba Muhimbili,(MUHAS) Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam (DIT) Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Taasisi ya Mifupa (MOI) Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT). 

Taasisi nyingine zilizoshiriki bonanza hilo ni pamoja na Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE).

Pamoja na hayo, Ofisa Mtendaji Mkuu huyo wa Kampuni ya TTCL aliishauri SHIMMUTA kufikiria kuanzisha mabonanza kama hayo mikoa mingine ili kuhamasisha michezo kwenye mikoa hiyo na kujenga mahusiano mema miongoni mwa Wafanyakazi wa nchi hii. Mashindano yenyewe ya SHIMMUTA kwa mwaka 2014 yanatarajia kufanyika Mkoa wa Tanga kuanzia Novemba 20, 2014, ambapo itashirikisha michezo mbalimbali.

RAIS KIKWETE AONGOZA MAZISHI YA MEJA JENERALI MSTAAFU MUHIDDIN MFAUME KIMARIO MJINI MOSHI

$
0
0
 
 Ma-Meja wakiwa wamebeba Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Meja Jenerali mstaafu wa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) huku wakisindikizwa Ma-Kanalki wakiwasili katika makaburi ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro Jumamosi Oktoba 11, 2o14.
  Rais kikwete akiwa na Jenerali Mstaafu Mirisho Sarakikya (kushoto kwa Rais) na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Ibrahim Msengi (kulia) na Meja Jenerali  Ezekiel  Kyunga, mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange (kulia kwa Rais) wakati mwili wa marehemu Meja Jenerali Mstaafu Muhiddin Mfaume Kimario ukiwasili katika makaburi ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro Jumamosi Oktoba 11, 2o14
 Mwili wa marehemu ukiwasili katika makaburi ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro Jumamosi Oktoba 11, 2o14
 Rais Jakaya  Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la Meja Jenerali Mstaafu Muhiddin Mfaume Kimario wakati wa mazishi katika makaburi ya Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro Jumamosi Oktoba 11, 2o14
 Rais Kikwete akimfariji mjane wa marehemu alipokwenda kutoa pole baada ya mazishi
  Rais Kikwete akiwafariji familia  wa marehemu alipokwenda kutoa pole baada ya mazishi
 Rais Kikwete akiendelea kuwafariji familia  wa marehemu alipokwenda kutoa pole baada ya mazishi
 Rais Kikwete akiweka sahihi kwenye kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu Meja Jenerali Mstaafu Muhiddin Mfaume Kimario mjini Moshi Jumamosi Oktoba 11, 2014
 Waombolezaji wakiwa wamebeba Jeneza lenye mwili wa Marehemu Meja Jenerali mstaafu wa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) Marehemu Muhiddini Kimario katika  makaburi ya manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro kwa mazishi Jumamosi Oktoka 11, 2014.
 Waombolezaji wakiwa wamebeba Jeneza lenye mwili wa Marehemu Meja Jenerali mstaafu wa jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ) Marehemu Muhiddini Kimario katika  makaburi ya manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro kwa mazishi Jumamosi Oktoka 11, 2014. PICHA NA IKULU

WAFANYAKAZI WA BENKI YA CRDB TAWI LA MOSHI WAFURAHIA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA.

$
0
0
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Moshi wakiwa katika picha ya pamoja ,aliyekaa ni meneja wa tawi hilo Francis Mollel.
Baadhi ya afanyakazi wa kike wa Benki ya CRDB tawi la Moshi wakiweka pozi la picha pembeni ya Keki.
Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Moshi akikata keki kwa ajili ya wateja.
Keki maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wa Benki ya CRDB tawi la Moshi wakati wa week ya huduma kwa wateja. 
Na Dixon Busagaga wa Globu ya jamii kanda ya kaskazini.

Sitti Abbas Mtemvu aibuka mshindi Redd's Miss Tanzania 2014,kujinyakulia milioni 18,mabango na vipeperushi vya ushindi vyatawala.!

$
0
0
Baada ya kuibuka Mlimbwende kutoka kwa washiriki 30, Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014,Sitti Abbas Mtemvu akishuka jukwaani kwa ulinzi mkali wa mabaunsa.Sitti Mtemvu alianza kwa kunyakua Redds Miss Chang'ombe na baadaye Redds Miss Temeke. Sitti ni binti wa Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbas Mtemvu.
 Baadhi ya washabiki na wapambe wa wakiwa na vipeperushi vilivyotengenezwa maalum kumshangilia  Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014,Sitti Abbas Mtemvu mara baada ya kutangazwa

Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014,Sitti Abbas Mtemvu akiwa katika picha ya pamoja na Mshindi wa pili,Lillian Kamazima (kulia) na Mshindi wa Tatu,Jihhan Dimachk mara baada ya kutawazwa rasmi usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam.Sitti Mtemvu alianza kwa kunyakua Redds Miss Chang'ombe na baadaye Redds Miss Temeke. Sitti ni binti wa Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbas Mtemvu.

  Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbas Mtemvu akizungumza jambo mbele ya wanahabari mara baada ya mtoto wake kutangazwa kuwa
Redd's Miss Tanzania 2014
Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014,Sitti Abbas akivalishwa taji.
 Pichani ni Washiriki waliochaguliwa kuingia kwenye hatua ya tano bora katika shindano la Redds Miss Tanzania 2014 linaloendelea hivi sasa ndani ya ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar.Picha zote na Othman Michuzi.
 Mmoja wa Washiriki waliongia katika nafasi ya tanno bora shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakijibu maswali mbalimbali
 Mmoja wa wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya pichani kulia Ommy Dimpoz akitumbuiza jukwaani akiwa sambamba na msanii Vanessa Mdee mbele ya wageni waalikwa (hawapo pichani),waliofika kushuhudia shindano hilo.
Washiriki wa Redds Miss Tanzania 2014 wapatao 15 mara baada ya kuchujwa. 
 Sehemu ya baadahi ya Wageni waalikwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye shindano hilo la kumsaka Kinara wa Redds Miss Tanzania 2014 
Baadhi ya Washiriki wa Shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakicheza moja ya onesho lao la ufunguzi wa shindano hilo,ambapo mshindi atatangazwa usiku huu na kujinyakulia kiasi cha shilingi miloni 18 taslim.
 Baadhi ya Washiriki wa shindano la Redds Miss Tanzania 2014,wakiwa jukwaani na mavazi ya ufukweni. 
 Msaniii wa Muziki wa kizazi kipya Vanessa Mdee a.k.a V-Money akitumbuiza kwenye shindano la kumsaka mshindi wa Redds Miss Tanzania 2014,yanayofanyika usiku huu ndani ya moja ya ukumbi wa Mlimani,jijini Dar. 
 Washiriki wa shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakikatiza jukwaani na mavazi yao ya ubunifu
 Baadhi ya Majaji wakifuatilia kwa makini 
Pichani ni Washiriki wa Redds Miss Tanzania 2014 wapatao 30 wakiwa jukwaani tayari kwa kuanza kuchujwa kupata washiriki 15 bora. Picha zote na Othman Michuzi.

WILAYA YA SAME NA MWANGA YAPATA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 56.10 KUTOKA MFUKO WA MAENDELEO YA UCHUMI WA KUWAIT.

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuuwa SerikaliDr.    Servacius Likwelile akitia saini makubaliano ya mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Aliye kulia kwake Bw. Abdulwahab A. Al- Bader  ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa maendeleo ya uchumi wa Kuwait. Waliosimama nyuma ni  Bi. Suzan Mkapa, Mkurugenzi wa sheria kutoka Wizara ya Fedha na wengine ni wataalam kutoka Kuwait.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuuwa SerikaliDr.    Servacius  Likwelile na  Bw. Abdulwahab A. Al- Bader  ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa maendeleo ya uchumi wa Kuwait wakibadilishana mikataba hiyo baada ya kutiliana saini.
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa serikali  Dr. Servacius Likwelile akiwa na ujumbe kutoka mfuko wa maendeleo ya uchumi wa Kuwait wakisubiri kutiliana saini mkataba wa  makubaliano ya kuanzisha mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Aliye kulia  kwake ni Bw. Abdulwahab A. Al- Bader  ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko huo.
Wajumbe kutoka Tanzania na Kuwait wakishangilia kwa furaha baada kusainiwa kwa mkataba wa kuanzisha mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga.  Picha zote na Ingiahedi Mduma-Wizara ya Fedha  tukiwa Washington DC.
 
====== =======  ========

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA FEDHA

 

 


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WILAYA YA SAME NA MWANGA YAPATA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 56.10 KUTOKA MFUKO WA MAENDELEO YA UCHUMI WA KUWAIT.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa serikali  Dr. Servacius Likwelile, mchana wa leo ametiliana saini makubaliano ya mkataba wa kuanzisha Mradi wa Maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Dr. Likwelile alisaini Mkataba huo kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mfuko wa maendeleo ya uchumi wa Kuwait . Aliye wakilisha Mfuko huo ni Bw. Abdulwahab A. Al- Bader  ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko.
Aidha katika kutiliana saini Mkataba huo Dr. Likwelile alimueleza Bw. Abdulwahab A. Al- Bader kuwa, Serikali ya Tanzania inatambua kuwa mfuko umetoa Dola za Kimarekani milioni 34.0 sawa na shilingi Bilioni 56.10 za Kitanzania kwa ajili ya kusaidia mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Hivyo inatoa shukrani zake za dhati kwa nchi ya Kuwait na hasa kwa mfuko huu wa maendeleo ya kiuchumi.
“Msaada huu tulioupata leo utaisaidia Serikali kutatua tatizo la maji katika wilaya ya Same na Mwanga, hii inaonyesha  ni jinsi gani mfuko huu wa Kuwait unavounga mkono na kutekeleza jukumu zima la kushiriki katika masuala ya kijamii na ya kiuchumi kwa nchi yetu ya Tanzania, hivyo tunaomba muendelee kutusaidia”. Alisema Dr. Likwelile.
Dr. Likwelile alimueleza Bw. Abdulwahab A. Al- Bader kuwa, kama anavyofahamu  gharama za mapendekezo ya mradi mzima ni Dola za Kimarekani  million 110.43 na hii inahitaji uchangiaji kutoka katika mifuko mingine kama BADEA, mfuko wa maendeleo wa Saudia , Mfuko wa Kimataifa wa OPEC  na Serikali kuchangia fedha kusaidia mradi huu. Kwa hili sina wasiwasi nalo kwani ninafuraha kujua kwamba umeshakubaliana na ninaujasiri kuwa jitihada zako zitafanikiwa.
“Mradi huu wa  maji wq wilaya ya Same na Mwanga unalenga kusaidia kuwepo kwa maji kwenye jamii mbalimbali zilizopo kwenye mradi huo.” Aliongeza Dr.Likwelile.
Aliendelea kusema kuwa,mradi huo utakapo kamilika :
(i)                 utaongeza kiwango cha watu wengi kuweza kupata maji safi na salama ya  kunywa.
(ii)               Uchumi wa Same na Mwanga utaimarika pamoja na hali ya afya kwa jamii nayo itakuwa imara hasa kwa maeneo yale yanayoguswa na mradi.
(iii)              Hali ya maisha ya watu wa Same na Mwanga itainuka.
“Mafanikio ya ukamilishaji wa mradi huu ni muhimu sana kwa uchumi wa jamii na maisha bora kwa watu wa wilaya ya Same na Mwanga”. Alisema Likwelile.

Dr. Likwelilie alimalizia kwa kusema kuwa“Tanzania na Kuwait ni marafiki wa muda mrefu sana, hivyo tutazidi kushirikiana na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa”.
Hali ya hewa ya mjini Washington Dc. ni mvua za vipindi na baridi kiasi.


Imetolewa na:
Ingiahedi Mduma
Msemaji
Wizara ya Fedha
Washington D.C
11/10/2014

 


Waziri Mkuu Pinda mgeni rasmi mechi ya viongozi wa dini jijini dar leo.

$
0
0
 Waziri Mkuu Mizengo Pinda akikabidhi Kombe kwa kiongozi wa timu ya Mshikamano,ambapo timu hiyo imenyukwa goli moja dhidi ya timu ya Amani,mchezo huo wenye lengo la kuimarisha na kudumuisha amani na mshikamano tulionao umefanyika katika Uwanja wa Taifa,jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini na serikali
Waziri Mkuu Mh.Mizengo Pinda akikabidhi Kombe kwa kiongozi wa timu ya Amani,ambayo imeibuka kinara katika mashindano hayo kwa kuichapa timu ya Mshikamano goli moja.Mchezo huo wenye lengo la kuimarisha na kudumisha amani na mshikamano tulionao umefanyika katika Uwanja wa Taifa,jijini Dar  ukijumuisha viongozi mbalimbali wa dini ya Kikristo na Kiislamu,ambapo pia viongozi wa ngazi mbalimbali wa dini na serikali walihudhuria.
 Waziri Mkuu Pinda akiwa katika picha ya pamoja na timu ya Amani
 Waziri Mkuu Pinda akiwa katika picha ya pamoja na timu ya Mshikamano
 Sehemu ya umati wa watu waliokuwepo kushuhudia mechi ya Amani na Mshikamano,iliyofayika jioni ya leo ndani ya uwanja wa Taifa.
 Waziri Mkuu Mh.Mizengo Pinda akizungumza jambo mbele ya wachezaji wa timu ya Amani na Mshikamano,zilizoundwa mahsusi katika kuadhimisha siku ya amani duniani,ambapo  viongozi wa dini uliojumuisha Masheikh, Maimamu, Maaskofu, Wachungaji na Mapadre.Mgeni rasmi katika mchezo huo alikuwa ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,Shoto kwake ni Mkuu wa  Mkoa wa Jiji la Dar,Mh.Said Meck Sadick na Rais wa TFF,Bwana Jamal Malinzi.

Katika mchezo huo wa kujenga amani na mshikamano uliopo nchini,Mwamuzi msaidizi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa jiji la Dar,Mh. Said Meck Sadick na mwamuzi aliyeshika kipyenga alikuwa ni Kamishna wa Kanda Maalumu, Seleman Kova 
Mkuu wa Mkoa wa jiji la  Dar, Mh.Said Meck Sadick  ambaye alizungumza machache na kumkaribisha Mgeni Rasmi wa mchezo huo wa Viongozi wa Dini kati ya Amani na Mshikamano,Waziri Mkuu,Mh Mizengo Pinda pichani kulia. 
 Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhaj Mussa ambaye ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya mchezo huo,akizungumza machache. 
 Rais wa TFF,Bwan, Jamal Malinzi akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa jiji la Dar, Mh.Said Meck Sadick  ambaye alizungumza macheche na kumkaribisha Mgeni Rasmi wa mchezo huo wa Viongozi wa Dini kati ya Amani na Mshikamano,Waziri Mkuu,Mh Mizengo Pinda.

AJALI MBAYA YA BASI LA HAPPY NATION NA GARI NDOGO,WATU KADHAA WADAIWA KUPOTEZA MAISHA HEDARU.

$
0
0
 Pichani juu ni baadhi ya Watu wakitazama ajali iliyotokea maeneo ya Hedaru Wilayani Same mkoani Kilimanjaro jioni ya leo,ambapo ajali hiyo ilihusisha gari ndogo yenye namba za usajili T653 BZR kuingia chini ya uvungu wa basi la abairia lijulikanalo kwa jina la Happy Nation,kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari kilieleza kuwa abiria wote waliokuwemo ndani ya gari ndogo (ambao idadi yao haikujulikana) walipoteza maisha papo hapo.Aidha bado haikufahamika mapema chanzo cha ajali hiyo ni nini.

RAIS KIKWETE AONGOZA SHUGHULI YA KUAGA MWILI WA DKT SHIJA VIWANJA VYA KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwa mwili wa Marehemu Dkt William Shija alipoongoza shughuli za kuaga leo Jumapili Oktoba 12, 2014 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole Mama Getrude Shija, Mjane wa  Marehemu Dkt William Shija alipoongoza shughuli za kuaga leo Jumapili Oktoba 12, 2014 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka sahihi kitabu cha maombolezo cha msiba wa  Marehemu Dkt William Shija alipoongoza shughuli za kuaga leo Jumapili Oktoba 12, 2014 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

KILA KATA INAPASWA IWE NA KITUO CHA AFYA – WAZIRI MKUU

$
0
0
1aWaziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua wodi ya   ya wanawake wajawazito wanaosubiri kujifungua katika hospitali ya wilaya ya Urambo, Oktoba 12, 2014. Kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum, Margareth Sitta ,,watatu kulia ni Mbunge wa Urambo Mashariki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta na  wapili kulia ni  Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatuma Mwansa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu  M izengo Pinda na Mbunge wa Urambo Mashariki, ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Samuel Sitta (mwenye miwani ya jua nyuma ya Waziri Mkuu) wakikagua  wodi ya wanawake wajawazito wanaosubiri kujifungua katiakhospitali ya wilaya ya Urambo, Oktoba 12, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)3aWaziri  Mkuu, Mizengo Pinda akipokea zawadi kutoka kwa Wabunge Samuel Sitta na mkewe Margareth  baada ya kuzindua wodi ya   wanawake wajawazito wanaosubiri kujifungua katiak hospitali ya wilaya ya Urambo, Oktoba 12, 2014.   Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatuma Mwasa.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)4aWaziri Mkuu, Mizengo Pinda akipokea kwa niaba ya Halmashauri ya Wilaya ya Urambo, msaada wa vyandarua 100 na blanketi 300 kutoka kwa  Mbunge wa Urambo Mashariki na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Samuel Sitta katika mkutano wa hadhara aliohutubia mjini  Urambo, Oktoba 12, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) .
 
…………………………………………………………………………………….
*Azindua jengo la kisasa la Mama Ngojea wilayani Urambo
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka viongozi wa mkoa wa Tabora wajipange vizuri na kuhakikisha kuwa wanajenga vituo vya afya katika kila kata za wilaya ya Urambo kwa sababu bado iko nyuma.
“Hatua hii itasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali ya wilaya ya Urambo kwa sababu yenyewe imekuwa ndiyo kimbilio la kila mgonjwa kwa sasa,” amesema.
Ametoa agizo hilo leo mchana (Jumapili, Oktoba 12, 2014) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mji wa Urambo mara baada ya kuzindua jengo la Mama Ngojea linaloitwa Mayu Lindila lililopo kwenye hospitali ya wilaya hiyo.
“Wilaya yenu ina kata 16, ina vijiji 57 na zahanati 22 lakini ina kituo kimoja tu cha afya. Na hii maana yake ni kwamba kuna vijiji havina zahanati kabisa. Huu ni mtihani mkubwa na ndiyo maana kila mtu akiumwa anakimbilia kwenye hospitali ya wilaya,” alisema Waziri Mkuu.
“Kisera kila kata ni lazima iwe na kituo cha afya, kwa hiyo viongozi wa mkoa na wilaya ni lazima mjipange kuona ni kwa namna gani mtaitekeleza sera hii, na pia jengeni zahanati kwenye vijiji ambavyo havina zahanati,” alisisitiza.
Akizungumzia kuhusu umuhimu wa huduma ya Mama Ngojea, Waziri Mkuu alisema unasaidia kuokoa maisha ya mama mjamzito anayetoka kata ya mbali ambaye anakabiliwa na tishio lakini siku zake za kujifungua zinakuwa hazijafika.
Alisema kutokuwepo kwa majengo ya Mama Ngojea katika maeneo mengi ni changamoto kubwa na hatari kwa akinamama wengi hasa waishio mbali na huduma za tiba. “Hivi kama kata moja iko mbali na makao makuu ya wilaya, na mama mjamzito mwenye tatizo hawezi kufika hospitali unadhani ataenda wapi? Si ataenda kwa wakunga wa jadi au waganga wa kienyeji tu?”
Aliwasihi akinamama wa wilaya hiyo wajitahidi kutumia huduma za hospitali kwa sababu kwa wakunga wa jadi na waganga wa kienyeji hakuna wataalamu kama waliopo hospitalini.
Alimtaka Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Bibi Fatma Mwassa afanye utaratibu ili kila wilaya pawe na Mama Ngojea. “Hata kama hakuna hospitali ya wilaya lakini pana kituo cha afya, ni vema pawe na jengo la Mama Ngojea ili kuokoa maisha ya akinamama.
Akitoa taarifa ya ujenzi wa jengo hilo, Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dk. Kheri Kagya alisema jengo hilo lenye uwezo wa kulaza wagonjwa 24 kwa wakati mmoja, lilianza kujengwa Agosti 25, 2012 na lilikamilika Novemba 10, 2013 kwa gharama ya sh. milioni 198/-. Lina jiko, sehemu ya kulia, mabafu, vyoo, eneo la kufulia na kupumzikia.
Lengo la kujenga kituo hiki ni kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 228 kwa kila vizazi hai 100,000 na kufikia vifo 90 kwa kila vizazi hai 100,000 au chini ya hapo ifikapo mwaka 2015. “Mwaka 2012 tulikuwa na vifo 253 kwa kila vizazi hai 100,000 na mwaka jana tulikuwa na vifo 228 kwa kila vizazi hai 100,000. Nia yetu ni kupunguza kabisa vifo vya akinamama kabla na wakati wa kujifungua,” alisema.
Aliwashukuru Mbunge wa jimbo la Urambo ambaye pia ni Waziri wa Afrika Mashariki, Bw. Samuel Sitta na mkewe Mama Margareth Sitta (ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa huo) kwa kubuni wazo hilo na kutafuta fedha za kujenga Mama Ngojea kwenye hospitali ya wilaya hiyo
Wakati huohuo, Bwana na Bibi Sitta wamechangia mablanketi 300 na vyandarua 100 kwa ajili ya Mama Ngojea pamoja na hospitali ya wilaya hiyo.
Waziri Mkuu amerejea jijini Dar es Salaam mchana huu.

BENKI YA KIARABU YA MAENDELEO YA UCHUMI YA AFRIKA ( BADEA)YATOA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 12.0 (SHILINGI BILIONI 20.1) KUSAIDIA MAENDELEO KATIKA WILAYA YA SAME NA MWANGA

$
0
0
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa serikali  Dr. Servacius Likwelile akiwa na ujumbe kutoka Tanzania wakiwa tayari kutiliana saini mkataba wa makubaliano ya mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Aliye kushoto kwake ni Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti  na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia.Fedha hizo zimetoka BADEA.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr.    Servacius Likwelile akitia saini makubaliano ya mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. Aliye kushoto kwake ni Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti  na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia. Aliyeko kulia ni Bi. Suzan Mkapa, Mkurugenzi wa sheria kutoka Wizara ya Fedha.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr.    Servacius Likwelile  na Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti  na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia, wakibadilishana mikataba hiyo baada ya kutiliana saini.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr.    Servacius Likwelile  na Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti  na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia, wakiionyesha mikataba hiyo kwa waliohudhuria sherehe hiyo  baada ya kutiliana saini.
======== =======   ========
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa serikali Dr. Servacius Likwelile, mchana wa leo ametiliana saini makubaliano ya mkataba wa kuanzisha Mradi wa Maji katika Wilaya ya Same na Mwanga mkoani Kilimanjaro.
 Dr. Likwelile alisaini Mkataba huo kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Benki ya Kiarabu ya Maendeleo ya uchumi ya Afrika. Aliye wakilisha Benki hiyo ni Eng. Yousef I. Al-Bassam ambaye ni Makamu wa Mwenyekiti na Mkurugenzi Msimamizi wa mfuko wa maendeleo wa Saudia. 
 Aidha katika kutiliana saini Mkataba huo Dr. Likwelile alimueleza Eng. Yousef I. Al-Bassam kuwa Serikali ya Tanzania inatambua kuwa BADEA imetoa Dola za Kimarekani milioni 12.0 sawa na shilingi Bilioni 20.1 za Kitanzania kwa ajili ya kusaidia mradi wa maji katika Wilaya ya Same na Mwanga. 
Hivyo inatoa shukrani zake za dhati kwa BADEA kwa kusaidia kuchochea maendeleo ya Tanzania. “Msaada huu tulioupata leo utaisaidia Serikali kutatua tatizo la maji katika wilaya ya Same na Mwanga, hii inaonyesha ni jinsi BADEA unaunga mkono na kutekeleza jukumu zima la kushiriki katika masuala ya kijamii na ya kiuchumi kwa nchi yetu ya Tanzania, hivyo tunaomba muendelee kutusaidia”. Alisema Dr. Likwelile.
 Dr. Likwelile alimueleza Eng. Yousef I. Al-Bassam kuwa, kama anavyofahamu gharama za mapendekezo ya mradi mzima ni Dola za Kimarekani million 110.43 na hii inahitaji uchangiaji kutoka katika mifuko mingine kama mfuko wa maendeleo wa Saudia , Mfuko wa Kimataifa wa OPEC na Serikali kuchangia fedha kusaidia mradi huu. 
"Kwa hili sina wasiwasi nalo kwani ninafuraha kujua kwamba umeshakubaliana na ninaujasiri kuwa jitihada zako zitafanikiwa. Mradi huu wa maji wq wilaya ya Same na Mwanga unalenga kusaidia kuwepo kwa maji kwenye jamii mbalimbali zilizopo kwenye mradi huo.” Aliongeza Dr.Likwelile. Aliendelea kusema kuwa,mradi huo utakapo kamilika: 
(i) utaongeza kiwango cha watu wengi kuweza kupata maji safi na salama ya kunywa. 
(ii) Uchumi wa Same na Mwanga utaimarika pamoja na hali ya afya kwa jamii nayo itakuwa imara hasa kwa maeneo yale yanayoguswa na mradi. 
(iii) Hali ya maisha ya watu wa Same na Mwanga itainuka. 
“Mafanikio ya ukamilishaji wa mradi huu ni muhimu sana kwa uchumi wa jamii na maisha bora kwa watu wa wilaya ya Same na Mwanga”. Alisema Likwelile. Dr. Likwelilie alimalizia kwa kusema kuwa“Tanzania na Saudia ni marafiki wa muda mrefu sana, hivyo tutazidi kushirikiana na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa”. 
  Imetolewa na: Ingiahedi Mduma 
Msemaji - Wizara ya Fedha 
Washington D.C

CCM YAISAFISHA CHADEMA MUFINDI

WAZIRI MKUU PINDA AMPA DED UYUI SIKU 60 KUHAMA NA TIMU YAKE,AFUNGUA KITUO CHA POLISI WILAYA HUMO

$
0
0


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifungua kituo cha polisi cha wilaya ya Uyui akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Tabora, Oktoba 11, 2014. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe Fatuma Mwasa na Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Uyui, Mhe. Lucy Mayenga.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, ACP Suzan Kaganda (kulia) baada ya kufungua kituo cha polisi cha wilaya ya Uyui akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Tabora, Oktoba 11, 2014.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, ACP Suzan Kaganda (kulia) baada ya kufungua kituo cha polisi cha wilaya ya Uyui akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Tabora, Oktoba 11, 2014. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.

 ===========  ========  =======
WAZIRI MKUU AMPA DED UYUI SIKU 60 KUHAMA NA TIMU YAKE
*Asema lazima wajali matatizo ya wananchi, wasijifanye wakubwa mno

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amempa miezi miwili Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui, mkoani Tabora, Bi Khadija Makuani kuhakikisha kuwa watumishi wote wa wilaya hiyo wanahamia Isikizya yalipo makao makuu ya wilaya hiyo.

Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumamosi, Oktoba 11, 2014) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Isikizya waliofika kushuhudia uzinduzi wa makao makuu ya polisi ya wilaya hiyo.

“DED nimekagua nyumba ya mkuu wa Wilaya na kuzindua nyumba zile nane, miundombinu iliyopo inatosha, hamia wewe na watu wako. Ninataka ifikapo Desemba 31, mwaka huu wote muwe Isikizya. Atakayegoma, RC niletee jina lake,” amesema Waziri Mkuu.

“Shauku ya wananchi kuwasubiri mhamie hapa imetosha. Mtumishi ambaye atagoma ni ishara kuwa hataki kuwahudumia wananchi, na sisi tutasema hatukutaki. Tatizo la watumishi wengi ni kujifanya wakubwa mno kuliko wananchi mnaowahudumia,” alisema huku akishangiliwa na wakazi wa Isikizya.

Waziri Mkuu ambaye aliwasili mjini Tabora jana mchana, alitembelea makao makuu ya wilaya hiyo ili kukagua mradi wa ujenzi wa makazi ya watumishi wa wilaya hiyo. Mara baada ya kuwasili wilayani humo, Waziri Mkuu alizindua nyumba nane za watumishi zilizojengwa kwa gharama ya sh. milioni 555 ambazo kati yake, sh. milioni 400 ni ruzuku kutoka Serikalini.

Pia alikagua ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Uyui ambayo iko katika hatua za mwisho za ujenzi. Kabla ya kuzungumza na wananchi hao, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa jengo la ghorofa moja la ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ambalo awamu ya kwanza ya ujenzi itagharimu sh. bilioni 1.1/- na awamu ya pili itagharimu sh. bilioni 1.4/-.

Alisema wakati wakisubiri ujenziwa ofisi yao ikamilike, watafute nafasi kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ili waweze kuwa karibu na wananchi na kuwahudumia kutatua changamoto zinazowakabili.

“Mnakaa Tabora mjini halafu mnadai mnawatumikia wnanchi wa Uyui. Haiwezekani kabisa. Hayo mafuta mnayotumia kwenda na kurudi mjini si mngetembelea wananchi wa vijijini na kuhimiza shughuli za maendeleo?” alihoji.

“Hamieni hapa muweze kutatua changamoto za wananchi. Kama mngehamia mapema hata tatizo la maji lingekwishatatuliwa na ujenzi wa nyumba za watumishi wote ungeshakamilika.”

Kuhusu changamoto ya uhaba wa maji, Waziri Mkuu aliahidi kuwatafutia sh. milioni 200/- kutoka wizara husika ili ziwezeshe kuvuta maji kutoka chanzo cha Igombe kilichopo km. 35 kutoka Isikizya.

Aliwapongeza askari ambao wameamua kuhamia katika wilaya hiyo na kuishi Isikizya licha ya mazingira magumu waliyoyakuta. Alisema atawasiliana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) ili waone namba ya kuwasaidia kuapata walau nyumba pacha mbili au tatu (two in one) zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa wilayani humo.

Alimtaka pia Mkuu wa Mkoa huo, Bibi Fatma Mwassa aangalie uwezekano wa kuwatumia vijana waliojiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ili kupata utaalamu wao na kuuhamishia kwa wananchi. “RC tafuteni namna ya kutumia utaalamu wa hawa vijana wa JKT ili wawafundishe wananchi mbinu za kilimo bora, ufugaji bora ama ujenzi wa nyumba bora. Siyo mnawatumia kwa kuimba tu,” alifafanua.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, OKTOBA 12, 2014.

Wiki ya Vijana yaendele kuwa Chachu ya Uzalendo

$
0
0
TBR1Waziriwa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akiangalia Jarida katika banda la Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Dunia (UNFPA – Tanzania) alipotembelea katika Maonyesho ya  Wiki ya Vijana leo mjini Tabora. Kutoka kushoto ni Mchambuzi wa Miradi ya Vijana na Maendeleo wa  UNFPA – Tanzania Bi. Tausi Hassan na Mshauri wa Vijana wa Shirika hiloBw. John Kalimbwabo.
TBR2
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwezeshaji Vijana, Jinsia, Wanawake na Watoto ya Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar Bw. Ally Hamisa konyesha nyaraka za vibali na sahihi za Wakuu wa Mikoa alipopita Kijana mzalendo Bw.Abiudi Denis aliyetembea nchi nzima kwa Siku 65 kwa lengo la kuhamasisha uzalendo ikiwemo kupinga Muundo wa Serikali Tatu, Kumpongeza Rais Jakaya Kikwete na Kupinga watu wanaombeza Hayati  Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere leo mjini Tabora wakati alipokea Bendera ya Taifa kutoka kwa kijana huyo kwenye Viwanja vya Maonyesho ya Wiki ya Vijana.
TBR3
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel  akitembelea mabanda wakati wa Maonesho ya  Wiki ya Vijana yanayoendelea katika Viwanja vya Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.
Pichana Frank Shija, WHVUM

Mhariri Gazeti la MTANZANIA akabidhi vyeti Shule ya Salma Kikwete

$
0
0



 Mhariri Msanifu wa Gazeti la Mtanzania, Khamis Mkotya, akizungumza jambo wakati wa kukabidhi cheti kwa mwanafunzi Ahmed Adamu katika mahafali ya tano ya wahitimu wa Kidato cha nne katika  Shule ya Sekondari ya Salma Kikwete iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam juzi. Kulia ni  Mwenyekiti wa walimu wa maarifa ya Uislamu Dar es Salaam, Suleiman Gombe.
Mhariri Msanifu wa Gazeti la Mtanzania, Khamis Mkotya, akikabidhi cheti kwa mwanafunzi Ahmed Adamu katika mahafali ya tano ya wahitimu wa Kidato cha nne katika  Shule ya Sekondari ya Salma Kikwete iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam juzi. Kulia ni  Mwenyekiti wa walimu wa maarifa ya Uislamu Dar es Salaam, Suleiman Gombe.
========  ========  ========
WAZAZI na walezi nchini wametakiwa kutambua wajibu kwa kuhakikisha wanawekeza kwenye elimu kwa watoto wao. Wito huo ulitolewa Dar es Salam na Mhariri Msanifu wa gazeti la MTANZANIA, Khamis Mkotya alipokuwa akizungumza katika mahafali ya tano ya Jumuiya ya wanafunzi wa Kiislamu wa Shule ya Sekondari ya Salma Kikwete.

Mkotya ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafali hayo ambapo alisema ni lazima jamii ikubali kuondokana na kulalamika na badala yake iandae mazingira mazuri ya watoto wao kuhakikisha wanasoma kwa bidii.

“Bado siku chache wanafunzi wa kidato cha nne nchini, mtafanya mitihani ya kuhitimu lakini tambueni kumaliza elimu hii kwa ngazi yetu ni chachu ya kutafuta zaidi ya elimu.

“Na mkiwa hamtafanya hivi mtakuwa mmekwenda ninyume na mafundisho ya Mtume wetu Muhammad (S.A.W) ambaye amatutaka tutafute elimu hadi uchina. Na hata leo ukimaliza mtihani wa kidato cha nne na kuona umemaliza tambueni elimu mlionayo sasa ni sawa na elimu ya msingi,” alisema Mkotya. Alisema ili maendeleo chanya yaweze kupatikana nchini ni lazima jamii ijiandae vema kuyapokea kwa kuwa na mkakati hasa kwa wanafunzi kujifunza kwa bidii kwenye masomo yao.

Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya mtoto wa kike yaliyo ratibiwa na WiLDAF yafana jijini Dar es salaam

$
0
0
Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya mtoto wa kike yaliyo ratibiwa na Women in Law and Development in Africa - WiLDAF yafana jijini Dar es salaam.

Octoba 11 ya kila mwaka ni siku iliyopitishwa na Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kuwa Siku ya Kimataifa ya Mtoto wa Kike duniani kote. Maadhimisho haya yalifanyika katika Hoteli ya Double Tree, Dar es Salaam.
Washiriki wa maadhimisho hayo wakiwa katika picha ya pamoja.
Mmoja wa washiriki waliofika kwenye hafla hiyo ya maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Mtoto es Kike yaliyoratibiwa na WiLDAF akichangia mada.

VISIT BY THE CHINA NATIONAL DEVELOPMENT AND REFORM COMMISSION

KONGAMANO NA MAONESHO YA TATU YA MAFUTA NA GESI ASILIA TANZANIA

JUKATA WATEMA CHECHE, WASEMA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA HAIKATI KIU YA WATANZANIA

$
0
0
Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA), Deusi Kibamba (katikati) akiongea mbele ya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Akionyesha tofauti ya Katiba mpya na ile ya zamani. Picha na Cathbert Kajuna wa Kajunason Blog.
Siku chache baada ya Mjumbe wa bunge Maalum la katiba ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti kupitia chama cha NCCR Mageuzi - Zanzibar, Haji Ambar Hamis kutoa tuhuma za kupigishwa kura ya kupitisha Katiba inayopendekezwa bila ridhaa yake. Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) nalo limetoa tuhuma kwa kitendo cha udanganyifu kwa upande wa Zanzibar ambapo Mheshimiwa Zakia Megji amewekwa kama mjumbe kutokea Zanzibar na wakati yupo upande wa Tanzania bara. Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa JUKATA, bwana Deus Kibamba jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wahabari. Aidha Kibamba amesema kwamba katiba inayopendekezwa imeshindwa kukata kiu ya Watanzania walio wengi kuhusu namna ya kutatua tatizo la kushuka kwa maadili ya viongozi na watumishi wa umma katika Taifa.

BALOZI WA FINLAND NCHINI BI. SINIKKA ANTILA AMTEMBELEA WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROFESA SOSPETER MUHONGO

$
0
0
 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akimkaribisha   Balozi wa Finland Nchini Bi.  Sinikka Antila (kushoto) kabla ya kuanza kikao  kilichojadili  utekelezaji wa mradi mkubwa wa kuboresha umeme katikati ya jiji la  Dar es Salaam. Pia kikao hicho kilihusisha ujumbe wa balozi wa Finland na  wataalamu kutoka Wizara  ya Nishati na Madini.
 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza na Balozi wa Finland Nchini Bi.  Sinikka Antila na ujumbe wake pamoja na wataalamu kutoka Wizara  ya Nishati na Madini.
 Balozi wa Finland Nchini Bi.  Sinikka Antila akisisitiza jambo wakati wa kikao hicho.
 Balozi wa Finland Nchini Bi.  Sinikka Antila (kushoto) akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya  Waziri wa Nishati na Madini. Kulia ni  Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Finland Nchini Bi.  Sinikka Antila (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa mazungumzo.

VITABU VYA AIRTEL VYAIBUA ARI YA WANAFUNZI GUNGU SEKONDARI KIGOMA

$
0
0
Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi na Afisa Elimu vifaa na Takwimu wa Manispaa ya Kigoma Ujiji Bwana Yalagwila Gwimo makabidhiano ya vitabu
Wanafunzi wa shule ya sekondari Gungu akifurahia kupokea vitabu vya masomo ya sayansi kutoka kwa kamouni ya simu za mkononi ya Airtel.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images