Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

BENKI YA EXIM YAPATA ONGEZEKO LA ASILIMIA 80 LA FAIDA KABLA YA KODI

$
0
0
 Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha na Meneja Mwandamizi wa Fedha  wa Benki ya Exim Tanzania, Bw. Issa Hamisi (katikati) akizungumza juu ya utendaji wa benki yake katika robo ya pili ya mwaka 2014 jijini Dar es Salaam jana. Pamoja naye ni Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu wa Benki hiyo George Binde (kushoto) na Meneja Utafiti na Uchambuzi Biashara Bw. Joseph Mrawa.

FAIDA ya kabla ya kodi ya robo ya pili mwaka 2014 ya Benki ya Exim imeongezeka kwa asilimia 80 mpaka shilingi bilioni 9.6 kutoka kipindi kama hicho mwaka jana.  “Tunayofuraha kuripoti matokeo mazuri ya robo ya pili ya mwaka,” alisema Bw.  Issa Hamisi, Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya Exim jijini Dar es Salaam jana.

“Ukuaji huu wa mapato unaashiria mafanikio yatokanayo na vyanzo vya benki tofauti vya mapato. Tunaendelea kuboresha ufanisi katika uendeshaji ili kuweza kufikia matakwa ya wateja wetu. Benki yetu ipo katika muelekeo nzuri. Tupo katika hatua nzuri ya kufikia malengo yetu. Matokeo yetu ya robo ya mbili yanaonyesha kuwa tumeendelea kufanya vizuri mwaka huu,” alisema.  

Faida ghafi ya riba, limekuwa kwa asilimia 36 katika kipindi sawa na hicho mwaka 2013 mpaka shilingi bilioni 14.3. Biashara ya fedha za kigeni imekuwa katika robo hii ambapo asilimia 33 imeongezeka kwenye robo ya pili ikilinganishwa na mwaka jana. Gawio lililopokelewa katika robo ya pili toka katika vyanzo vyetu vya uwekezaji kwa Benki ya NMB na tawi letu la Comoro kwa mwaka 2013 limeonyesha kuwa chanya katika matokeo yetu mazuri. 

Pato la tozo na kamisheni limeongezeka kwa asilimia 19 toka katika robo ya mwaka uliopita, hadi shilingi bilioni 6.2, lililotokana na kukua kwa biashara ya fedha za kigeni na bidhaa za kifedha za biashara baada ya utekelezaji wa mpango mkakati wa miaka mitatu. Pato toka katika vyanzo vya uwekezaji limekuwa kwa asilimia 184 ikilinganishwa na kipindi hicho mwaka jana, hadi shilingi bilioni 4, litokanalo na ongezeko la pato la gawio lililopokelewa.  

“Gharama za jumla za uendeshaji zilidhibitiwa na kukua kwa asilimia 21 tu mpaka shilingi bilioni 16.7 kutokana na gharama za uanzishwaji wa matawi mapya na motisha za wafanyakazi katika jitihada za kuongeza upatikanaji wa huduma za Benki kijeografia na kuiimarisha Benki kwa ujumla. Kwa matokeo hayo, gharama za uwiano wa pato (cost to income ratio) zimeweza kushuka toka asilimia 64 iliyopatikana katika robo ya mwaka uliopita mpaka asilimia 57,” aliongeza. 

Amana za wateja zimeripotiwa kuwa shilingi bilioni 776 ikilinganishwa na robo ya mwaka uliopita zikiwa na ongezeko la amana zitokanazo na CASA (Current & Savings Accounts) katika robo hiyo la shilingi bilioni 36 ikilinganishwa na matokeo ya robo ya kwanza ya mwaka 2014. Mikopo iliyotolewa imerekodi ongezeko la asilimia 16 ikilinganishwa na robo kama hiyo mwaka jana mpaka shilingi bilioni 558 na vivyo hivyo mizania ya benki imekua kwa asilimia 9 mpaka shilingi tilioni 1.15. 

“Kipaumbele kikubwa bado kipo katika jitihada zetu za kuimarisha nafasi yetu katika soko na kuboresha utosherezaji wa mahitaji ya mteja kupitia ufanisi wa kiuendeshaji.  Mwenendo thabiti katika kufikia matakwa ya mteja ni ishara tosha ya kwamba tunaweza kufanikisha malengo yetu kwa mwaka huu, "alisema kaimu Afisa Mkuu wa Fedha na Meneja Mwandamizi wa Fedha wa Benki hiyo.

Katika jitihada za kuimarisha nafasi yake ya kiushindani benki imejikita katika muundo wa kibunifu wa biashara ndogo (innovative retail model) ambao umeboresha mawasiliano na wateja na uendeshaji wa karibu zaidi wa matawi yote. Muundo huo mpya wa menejimenti katika matawi umeanzishwa mwaka 2014.  

“Katika hatua ya kuboresha uendeshaji kwa ajili ya utoaji wa huduma bora kwa wateja, baadhi ya shughuli zetu kama vile za ufunguaji wa akaunti na nyinginezo vimewekwa katika mfumo mmoja. Uanzishwaji wa ‘mfumo wa uendeshaji mmoja’ umelenga katika uboreshaji wa huduma za benki pamoja na kuongeza ufanisi katika uendeshaji wa benki kwa ujumla,” alisema Bw. Issa Hamisi. 

Benki pia imeendelea na jitihada zake dhidi ya shughuli mbali mbali za kijamii katika robo hiyo kwa kushiriki katika matukio ya kijamii na kutoa misaada. Hii ni pamoja na kuchangia magodoro katika hospitali ya Mwananyamala, kompyuta katika shule ya msingi ya Kilakala na kutoa malazi kwa wazee kupitia taasisi ya Tushikamane Pamoja Foundation (TPF). 

Kutokana na utendaji huo nzuri wa robo ya pili na fursa zilizopo kwenye uchumi, Benki inategemea utendaji mzuri zaidi katika robo zifuatazo, kampeni za mauzo zikitiliwa mkazo na kuimarisha ufanisi wa kiuendeshaji. 


Radio 5 yapongezwa kwa mchango wake wa kukuza sanaa za vichekesho vya majukwaani.

$
0
0
Wasanii wa fani ya Uchekeshaji mahiri kutoka nchini Uganda,Kenya na Tanzania wakitoa burudani kwa washabiki na wapenzi wa fani hiyo ,iliofanyika kwenye moja ya ukumbi wa hotel ya Golden Tulip Jijini Dar,pichani shoto ni Fred Omondi kutoka Kenya,mwanadada Anne Kansiime kutoka nchini Uganda na Mc Pilipili wa Tanzania.

 Sehemu ya washabiki na wapenzi wa fani hiyo wakivunjika mbavu kwa kucheka.
 mwanadada Anne Kansiime kutoka nchini Uganda akitoa burudani ya vichekesho kwa watazamaji (hawapo pichani),ndani ya moja ya ukumbi wa hotel ya Golden Tulip jijini Dar hivi karibuni

Kituo cha Radio 5, kimepongezwa na wadau wa sanaa kwa mchango wake wa kukuza sanaa za vichekesho vya majukwaani hapa nchini.

Wadau hao wa sanaa za vichekesho vya majukwaani waliipongeza Radio 5, wakati wa burudani ya wachekeshaji wa majukwaani iliyofanyika mwishoni mwa wiki hii katika ukumbi wa Golden Tulip. Burudani hiyo ambayo ilifana sana iliwajumuisha mchekeshaji kutoka Uganda, mwanadada Anne Kansiime, Fred Omondi kutoka Kenya na Pilipili wa Tanzania.

Akizungumzia onyesho hilo, mmoja ya mashabiki waliohudhuria onyesho hilo, amesema sanaa ya vichekesho vya majukwaani nchini haijapewa kipaumbele kama aina nyingine za sanaa. ‘Watu wengi bado wanaamini sanaa za kuchekesha majukwaani sio kazi rasmi kama kazi nyinginezo, lakini hii imeanza kubadilika hapa nchini, na tutarajie mabadiliko zaidi kama wadau wengine kama radio 5 wakijitokeza kusaidia’ alisema Farida Akida.

Akijibu swali aliloulizwa na waandishi wa habari kuhusiana na anavyoiona tasnia ya vichekesho vya majukwaani Afrika Mashariki, mchekeshaji Anne Kansiime anasema anaamini sanaa ya vichekesho vya majukwaani inaanza kujijengea heshima kubwa miongoni mwa wananchi.  ‘Mimi sio mbunge au mwanasiasa, lakini nimepata mapokezi makubwa, kwa kazi hii tu ya kuchekesha watu, hivyo naona hii tu pekee ni dalili ya kukua kwa tasnia hii hapa Afrika Mashariki’ alisema Anne.

Ikiwa ni mara ya kwanza kwa mwanadada Kansiime kuja Tanzania kutoa burudani, hasa baada ya kujijengea umaarufu mkubwa kupitia vipande vyake vya vichekesho vilivyo mtandaoni, tiketi za burudani yake ziliisha wiki moja kabla hajawasili.  Katika usiku huo wa burudani ulioitwa, Cheka Kwa Nguvu, mchekeshaji toka Tanzania, Pilipili aliwatoa kimasomaso mashabiki waliofurika kwa vichekesho vyake vilivyoonekana kuwagusa mashabiki moja kwa moja.

Huku mashabiki wengi wakiwa hawamfahamu vyema, Pilipili ambaye kitaaluma ni mwalimu, anasema aliacha kazi ya ualimu ili awe mchekeshaji, hivyo kwake yeye, kuchekesha ni kazi kama kazi nyingine. ‘Kwangu mimi hii ni kazi ambayo najivunia, na naamini nitaweza kuwawakilisha watanzania vyema kimataifa kupitia uchekeshaji, na naishukuru Radio 5 kwa kunipa fursa ya kuonyesha kwamba ninaweza’ alisema Pilipili.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Radio 5, Robert Francis amesema huu ni mwanzo tu wa kuwaandalia watanzania burudani za kipekee na watarajie mengi zaidi kutoka Radio 5. ‘Sanaa ya uchekeshaji jukwaani bado haijapewa nafasi kubwa hapa nchini, lakini kama mlivyoona, mashabiki wamejitokeza kwa wingi sana kwenye burudani yetu, hivyo watu watarajie burudani za aina hii nyingi zaidi kutoka kwetu’ alimaliza Francis.

PSPF YASHIRIKI MAONESHO YA WAKULIMA NANENANE MKOANI LINDI KWA MAFANIKIO

$
0
0
MKUU WA WILAYA YA LINDI MJINI DOKTA HAMID NASSORO (KATIKATI)  AKISAINI KITABU CHA WAGENI ALIPOTEMBELEA BANDA LA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF KWENYE MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE MKOANI LINDI, (WAPILI KULIA) NI AFISA MAKOSO WA PSPF RAHMA NGASSA. (KUSHOTO) NI OMARI KALILO AFISA MFAWIDHI WA PSPF MKOA WA LINDI.MENEJA MIRADI MFUKO WA PENSHENI WA PSPF, MASOUD AKITOA MAELEZO KWA WATU MBALIMBALI WALIOTEMBELEA BANDA LA PSPF KWENYE MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE MKOANI LINDI.
 AFISA UENDESHAJI WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF DOLPHIN RICHARD AKIMWELEKEZA MARTHA HONGERA (KATIKATI) NAMNA YA KUJAZA FOMU YA UCHANGIAJI WA HIARI WALIOTEMBELEA BANDA LA PSPF KWENYE MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE MKOANI LINDI.
BALOZI WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF, MRISHO MPOTO “MJOMBA” AKIFURAHIA JAMBO NA MENEJA MASOKO WA PSPF, RAHMA NGASSA WAKATI AKITOA BURUDANI KWENYE MAONYESHO YA WAKULIMA NANENANE MKOANI LINDI.

Nakumatt inches closer to golden milestone as second Dar es Salaam store opens its doors

$
0
0
Nakumatt holdings MD Atul Shah (left) guides Tanzania's Deputy Minister Hon. Janet Mbene (centre) on a tour of the new Nakumatt Mlimani as the retailer's Regional Director Mr Thiagarajan Ramamurthy looks on.

Regional retailer, Nakumatt Holdings, has officially opened its second, Dar Es Salaam, Tanzania, store as it inches closer to the opening of its 50thbranch in coming days.

The opening of the 49thNakumatt store this morning, is a major milestone for the retailer which had earlier set a corporate target to open 50 branches by February 2015.

Following its recent acquisition of three retail stores formerly owned by South African retailer Shoprite, Nakumatt, has now opened its 49th branch to be known as Nakumatt Pugu Road and is on course to open its 50thbranch in Arusha, Tanzania in the next two weeks.

Speaking during the official opening ceremony, Nakumatt Holdings, Managing Director, Atul Shah, said the opening of the store, will further enhance the retailer’s footprint in Dar es Salaam.

“The opening of Nakumatt Pugu Road Supermarket is a major milestone for us, particularly because we are essentially racing against time to complete the progressive launch of the three new Tanzania branches by mid-August,” Shah explained.

And added: “The new Nakumatt Pugu Road will essentially enhance our footprint in Dar Es Salaam city where we are already enjoying overwhelming support following our recent opening of Nakumatt Mlimani also in Dar.”

Located along the busy Nyerere road in Dar Es Salaam, Nakumatt Pugu Road, historically holds the pride of place as the first Shoprite store ever opened in Tanzania by the South African retailer way back in 2001. With the recent acquisition, the Nakumatt Pugu Road Complex will also host the retailer’s (Nakumatt) Tanzania’s Headquarters; acting as the hub for its Moshi, Arusha and Dar Es Salaam stores.

As part of a phased out opening plan, the store has been outfitted to the signature Nakumatt corporate colours and layout.

With the opening of Nakumatt Mlimani and Pugu road, Shah, pointed it out that Nakumatt now has three running stores in Tanzania. Nakumatt Pugu road and Mlimani are the latest additions to the existing Nakumatt Moshi store which opened its doors in 2011 in the bustling town at the foot of Mt Kilimanjaro.

In Kenya, Nakumatt is also gearing up for the opening of three new stores in Kenya by the end of the year.

Bendera atilia mkazo soka la vijana wakati wa uzinduzi wa mashindano ya Airtel Rising Stars mkoani morogoro

$
0
0
Mkuu wa Morogoro Joel Bendera akipiga mpira kuashiria uzinduzi wa Airtel Rising Stars mkoani Morogoro.
  

 Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera akikagua timu wakati wa uzinduzi wa Airtel Rising Stars mkoani Morogoro.

Bendera atilia mkazo soka la vijana.
Mkuu wa mkoa wa Morogoro Joel Bendera, atilia mkazo soka la vijana na kuwataka viongozi wa mpira wa miguu mkoa wa Morogoro na chama cha mpira wa miguu Tanzania kutilia mkazo program za vijana.

Kocha wa zamani wa timu ya Taifa – Taifa Stars atoa changamoto wakati akifungua mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Morogoro siku ya jumanne. Alisema kuwa hakuna njia ya mkato katika maendeleo ya mpira wa miguu zaidi ya kuwekeza katika shule za soka na programu za vijana kama Airtel Rising Stars. Awapongeza  Airtel kwa mchango wao.

Zaidi ya majuma mawili kumekua na maoni ya kutoka kwa wakuu wa mikoa na wadau wengine wakisisitiza viongozi wa mpira wa miguu nchini kutilia mkazo programu za vijana kuiwezesha Tanzania kufanya vizuri.

Wakifungua mashindano ya Airtel Rising Stars katika mikoa yao hivi karibuni, Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Said Meck Sadiki na Mkuu wa mkoa Mbeya Abbas Kandoro nao walitilia mkazo kuwekeza katika mpira wa vijana. Wengine waliotoa maoni hayo ni meya wa Mwanza Stanslaus Mabula na Mbunge wa Ukonga Eugen Mwaiposa.

Mashindano ya Airtel Rising Stars yanaitimishwa leo (August 7) na timu zinatarajiwa kuwasili jijini Dar-es-Salaam siku ya jumamosi August 9 katika fainali za taifa ambazo zinaanza kutimua vumbi jumapili katika kiwanja cha kumbukumbu ya Karume. Fainali za Taifa zitamalizika tarehe 17 August na wachezaji wakiume na wa kike watakao chaguliwa wataweka kambi jijini Dar-es-Salaam wakijiandaa na mashindano ya kimataifa Airtel Rising Stars yatakayofanyika nchini Gabon.

Mwaka jana mashindano hayo yalifanyika nchini Nigeria na timu ya wasichana ya Tanzania walinyakua ubingwa na kuzawadiwa dollar za marekani 10,000.  

NABAKI AFRIKA MABINGWA VIFAA VYA UJENZI

$
0
0
20140806_050949Meneja wa kampuni ya Nabaki Afrika tawi la Arusha Jesse S. Madauda akiongea na wateja waliotembelea katika  banda lao viwanja vya nane nane jijini Arusha
20140806_051800 
Hii ni moja ya vifaa vinavyopatikana katika banda lao maarufu kwa jina la Gutter System,kazi yake kubwa ni kuvuna maji ya mvua ,uv resistance,hazikakamai wala kuvunjika na guarantee yake miaka 10
20140806_051639
Hii ni Plumbing System ni kwaajili ya mfumo wa maji taka na safi na sifa yake kuu nikwamba huwezi kuona chemba zile za nje na haizibi.

 
20140806_050615Vigae vya kuezeka (Decra Roofing Tiles )sifa yake kuu ni havipauki ,havipati kutu na havipukutiki na guarantee yake miaka 50
20140806_051321Floor Tiles za  mbao, ambazo zinatafutwa sana sokoni
20140806_051551Muonekano banda la Nabaki Afrika katika viwanja vya nane nane jijini Arusha,katika banda hilo utaweza kujipatia vifaa bora vya ujenzi wa nyumba yako pamoja na ushauri
20140806_051448Pump za maji za visima na matumizi ya nyumbani
20140806_051224Water Filter, kazi yake kubwa ni kuchuja maji,kutoa chumvi kwenye maji na kufanya yawe salama kwa kunywa
20140806_051429
Heater za maji kwaajili ya kupasha maji moto ikijulikana kwa jina la Ariston, Pia wanahita za umeme na za solar yaani  mionzi ya jua
20140806_053955Vigae vya kuezeka ( Fortiza Roofing Tiles )sifa yake kuu ni havipauki ,havipati kutu na havipukutiki na guarantee yake miaka 25
20140806_050843Conmix Decorative plaster SP3 ni plasta bora zilizo na rangi hazihitaji kupaka rangi(zikiwekwa dawa hazipitishi maji)

Kampuni ya Nabaki Afrika ni kampuni pekee isiyo na mshindani katika ubora wa vifaa mbalimbali vya ujenzi.Kampuni hiyo inahusika katika maeneo makuu matatu,yaani uezekaji,ujenzi (Construction) na maji.

Kwa mawasiliano  wasiliana nao kupitia info@nabaki.com au tembelea tovuti yao www.nabaki.com au piga simu namba 0766 827417 au 0786 966114.Nabaki Afrika imejaribiwa,Imepimwa na Imeaminiwa zaidi ya miaka 20 Tanzania.(Habari picha na Pamela Mollel wa jamiiblog)

Benki ya Posta yaipiga tafu Taswa SC

$
0
0
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Moses Manyata (wa kwanza kushoto)akikabidhi mfano w hundi kwa mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary (wa kwanza kulia)ikiwa sehemu ya benki hiyo kusaidia michezo nchini. Katikati ni Afisa Mawasiliano wa wa benki hiyo, Chichi Hilda Banda.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Moses Manyata (wa kwanza kushoto)akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusiana na hatua ya benki hiyo kuisaidia timu ya waandishi wa habari za michezo nchini Taswa SC. Benki hiyo ilikabidhi hundi ya Sh milioni 2 na pia itasaidia jezi kwa timu ya mpira wa miguu na netiboli.kulia ni Mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary.

Benki ya Posta Tanzania (TPB) imeidhamini klabu ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa SC), kufuatia juhudi zake za kuhamasisha na kuendeleza michezo nchini.

Benki hiyo imeisaidia klabu hiyo fedha taslims sh. Milioni 2 na inatarajia kuwapa jezi seti moja moja kwa timu ya mpira wa miguu na mpira wa pete (netiboli) ikiwa ni kuthamini mchango wao Taswa SC katika sekta ya michezo nchini.

Kaimu Afisa Mteandaji Mkuu wa TPB, Moses Manyatta alisema kuwa wanafuraha kubwa kusikia kuwa waandishi wa habari za michezo wameamua kufanyakazi kwa vitendo kwa kuanzisha timu ya mpira wa miguu ambayo kwa sasa ina miaka zaidi ya 20 na timu ya mpira wa pete (netiboli) ambayo ina mwaka mmoja na nusu.

“Tumefarijika kutokana na ukweli kuwa mbali ya kuandika, mmeamua kufanya michezo kwa vitendo na kuwa mfano wa kuigwa, TPB ipo bega kwa bega nanyi na tutaendelea kushirikiana katika sekta mbali mbali tofauti na michezo,” alisema Manyatta.

Alisema kuwa TPB ni benki halisi ya Kitanzania yenye kutoa huduma bora kwa wateja wake na kwa sasa imeingia katika sekta ya michezo ambapo kwa sasa inashirikiana na timu kongwe nchini, Yanga na Simba katika zoezi la kuandikisha upya wanachama na mashabiki wa timu hizo.

Mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary aliipongeza TPB kwa kutoa msaada huo na kuahidi kuwa wadau wakubwa wa benki hiyo katika shughuli zake mbalimabli. Majuto alisema kuwa wameomba udhamini kwa makampuni mengi kutokana na ukweli kuwa timu yao inachangamoto nyingi pamoja na kuwa na mafanikio makubwa.

“Tunawapa pongezi kubwa sana TPB, mmeonyesha kuwa ni benki halisi ya Kitanzania yenye kutoa huduma bora hapa nchini, Taswa SC ipo bega kwa bega nanyi katika kuendeleza gurudumu la maendeleo la nchi hii,” alisema Majuto.

Majuto pia aliwaomba wanachama wa timu ya Taswa SC kuwa mstari wambele katika shughuli za TPB kwani wameonyesha kuwajali katika shughuli za kila siku.

WATANZANIA WAENDELEA KUMIMINIKA KATIKA BANDA LA NHC NANENANE KUJIPATIA HUDUMA MBALIMBALI

$
0
0
IMG-20140806-WA0003
Afisa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi. Edith Nguruwe (katikati) akimuelekeza mwananchi aliyetembelea banda la NHC, kujaza dodoso la kufahamu uwezo na mahitaji ya nyumba kwa wananchi. (Picha zote kwa Hisani ya Shirika la Nyumba la Taifa).
IMG-20140806-WA0001
Banda la maonyesho la Shirika la Nyumba la Taifa lililopo katika viwanja vya Ngongo, vilivyopo nje kidogo ya mji wa Lindi mkoani Lindi.
IMG-20140806-WA0002
Wageni mbalimbali wakipata maelezo kutoka kwa maafisa wa shirika la nyumba la taifa
IMG-20140806-WA0000
Afisa Mauzo, Deogratius Batakanwa na Afisa Masoko Chediel Msuya wa NHC wakiwaelimisha Maafisa wa TFDA juu ya utaratibu wa kumiliki nyumba za NHC. Maafisa hao walifika katika banda la maonyesho la NHC kufahamu shughuli za Shirika la Nyumba na utaratibu wa manunuzi ya nyumba.

JUHUDI ZA UONGOZI WA MKOA WA RUKWA KUENDELEZA UTALII WA MAPOROMOKO YA KALAMBO (KALAMBO FALLS) ZAENDELEA, MKUU WA MKOA HUO ENG. STELLA MANYANYA AKABIDHIWA RAMANI YA ENEO LILILOPIMWA TAYARI KUENDELEZWA

$
0
0
Kaimu Afisa Ardhi na Maliasili Wilaya ya Kalambo Ndugu Makwasa Biswalo (katikati) akimuonyesha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya eneo lililopimwa katika kijiji cha Kapozwa kwa ajili ya kuendeleza Utalii katika Kijiji hicho ambacho kina maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls), maporomoko ambayo ni ya pili kwa urefu barani Afrika yakiwa na urefu wa mita 235. 

Zipo jitihada kadhaa zilizokwishafanywa na uongozi wa Mkoa wa Rukwa ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Eng. Stella Manyanya katika kuhakikisha eneo la maporomoko hayo linaimarishwa na kuwa kivutio kikubwa cha utalii na chanzo cha mapato kwa halmashauri husika na taifa kwa ujumla. 

Jitihada hizo ni pamoja kuwahamasisha wananchi wa kijiji cha Kapozwa na wadau wengine katika kutambua umuhimu wa maporomoko hayo ambapo mpaka hivi sasa wananchi hao wameshashiriki kufyatua matofali kwa ajili ya kujenga kituo cha utalii katika eneo hilo.

 Jitihada zingine ni zile za kupima viwanja na kuandaa michoro katika eneo hilo ambapo ramani imeshaidhinishwa na tathmini ya kuwafidia wananchi maeneo yao imeshafanyika. 

Aidha zimekuwepo jitihada za kutafuta fedha kutoka Serikalini na kwa wahisani mbalimbali katika kusaidia kujenga na kuimarisha utalii katika maporomoko hayo (Kalambo Falls). Wakala wa Misitu Taznania (TFS) wamesaidia upatikanaji wa kiasi cha fedha (Tsh. Mil. 10) ambazo zitasaidia kufungua baadhi ya mitaa katika eneo liliopimwa na shughuli zingine zitakazohitajika katika eneo hilo.  

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya anawaomba wadau wote wa utalii nchini ikiwemo Serikali, Mashirika binafsi, Wawekezaji na Wahisani mbalimbali kuwa na jicho la pamoja katika kuona Maporomoko ya Mto Kalambo (Kalambo Falls) yanachukuliwa umuhimu wa pekee wa kuendelezwa na kutangazwa kwa nguvu kwani ni miongoni mwa kivutio kikubwa cha utalii nchini na barani Afrika kwa ujumla. 

Maporomoko ya Mto Kalambo (Kalambo Falls) yenye urefu wa mita 235 yapo Mkoani Rukwa katika Wilaya ya Kalambo na ni sehemu ya mpaka kati ya Nchi ya Tanzania na Zambia. Nchi ya Zambia imekuwa ikitumia fursa ya mpaka huo kuendeleza eneo lao la mpakani na kuitangaza Kalambo Falls jambo ambalo likiachwa kwa muda mrefu bila Tanzania kuchukua hatua kama hiyo itapelekea dunia kubaki na picha isiyo sahihi kuwa maporomoko hayo yapo nchini Zambia wakati sehemu kubwa ipo Tanzania na hata muonekano mzuri unapatikana kutokea Tanzania na maji ya mto huo yanatokea Tanzania. 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya akiangalia ramani ya viwanja vilivyopimwa katika kijiji cha Kapozwa kwa ajili ya kuendeleza utalii katika kijiji hicho cha mpakani na nchi ya Zambia yalipo maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls). Mkuu huyo wa Mkoa alikabidhiwa ramani hiyo na Kaimu Afisa Ardhi na Maliasili Wilaya ya Kalambo Ndugu Makwasa Biswalo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya na Meneja wa Misitu Wilaya ya Sumbwanga na Kalambo Ndugu Martin Hamis wakipanda mti wa kumbukumbu katika eneo lililopimwa la kijiji cha kapozwa kwa ajili ya kuendeleza utalii wa maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls). 
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella Manyanya na wapimaji wa ardhi kutoka chuo cha Ardhi Morogoro waliokuwa wakishirikiana na wataalamu wa ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kupima ardhi ya kijiji cha Kapozwa kwa ajili ya kuiendeleza kiutalii wakiangalia Maporomoko ya Moto Kalambo (Kalambo Falls).  
Sehemu ambayo ni nusu ya maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls). 

 
Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Smythies Pangisa akiangalia bonde la maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls).
Sehemu ya jitihada za wananchi wa kijiji cha Kapozwa ambao wamefyatua matofali kwa ajili kujenga kituo cha utalii kwa ajili ya maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls).
Sehemu ya mchoro kwa ajili ya kujenga kituo na geti la utalii katika maporomoko ya mto Kalambo (Kalambo Falls). Jitihada hizi zimefanywa na uongozi wa Mkoa wa Rukwa ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Eng. Stella Manyanya.
Vijana wa nchi jirani ya Zambia wakiwa wanapunga upepo kandokando ya maporomoko ya mto Kalambo. Upande wa nyuma zinaonekana ngazi maalum ambazo ni sehemu ya miundombinu iliyojengwa na Serikali ya Zambia kuwavutia watalii katika eneo hilo. Serikali ya Tanzania ina changamoto kubwa ya kuhakikisha eneo hilo muhimu la utalii linaendelezwa ili kulijengea umiliki halali tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo inaonekana limetelekezwa kwa muda mrefu.
Sehemu ya bonde ambalo ni maangukio ya maji ya mto Kalambo yanapotengenezwa maporomoko (Kalambo Falls).(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa).

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA KIMATAIFA LA SAYANSI KWA NCHI ZA AFRIKA NA KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA, JIJINI ARUSHA

$
0
0
Makamu wa Rais Dkt. Bilal katika picha ya pamoja na washiriki wa kongamano hilo, baada ya ufunguzi.Picha na OMR
Kongamano hilo la siku tatu limefanyika katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) Jijini Arusha jana Agosti 5, 2014, na kushirikisha mabingwa mbalimbali wa tafiti ndani ya Afrika na nchi za ukanda wa Jangwa la Sahara.

Kongamano hilo ambalo limedhaminiwa na Shirika la misaada la Kimataifa la Marekani (USAID) linalenga kukuza tafiti za kisayansi na kutanua maendeleo ya tafiti hizo ili yasaidie wananchi wa nchi za ukanda huu hasa vijana ambao wanaelezwa kuwa na idadi kubwa kulinganisha na wazee na akina mama.

Katika Hotuba ya mgeni rasmi Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, alisema kuwa, dhana ya umuhimu katika uwekezaji na utanuaji wa sayansi katika Afrika, inahitaji kutazama kundi la vijana na kulihamasisha kushiriki katika masomo ya sayansi ili kuharakisha maendeleo kwa Bara la Afrika.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Chuo cha Nelson Mandela cha jijini Arusha wakati alipowasili kwa ajili ya kufungua Kongamano la Kimataifa la siku tatu kuhusu ukuzaji na uendelezaji wa Tafiti za Kisayansi kwa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la sahara.
Makamu wa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo cha Nelson Mandela, Bernard Mussa, aliyetafiti kuhusu kuongeza joto katika Majiko kwa kutumia mwanga wa jua, wakati Dkt. Bilal alipofika chuoni hapo kwa ajili ya kufungua Kongamano la Kimataifa la siku tatu lenye lengo la kujenga nguvu ya pamoja katika ukuzaji na uendelezaji wa Tafiti za Kisayansi kwa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la sahara.
Makamu wa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa mradi wa Masai Stove’s & Solar, Kisioki Moitiko aliyetafiti kuhusu mzunguko wau meme wa Jua kutumika katika nyumba za kabila la kimasai (Maboma) wakati Dkt. Bilal alipofika chuoni hapo kwa ajili ya kufungua Kongamano la Kimataifa la siku tatu lenye lengo la kujenga nguvu ya pamoja katika ukuzaji na uendelezaji wa Tafiti za Kisayansi kwa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la sahara.
Makamu wa Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Hassna Founoune, kutoka Taasisi ya Tafiti ya Kilimo ya Senegal, wakati Dkt. Bilal alipofika chuoni hapo kwa ajili ya kufungua Kongamano la Kimataifa la siku tatu lenye lengo la kujenga nguvu ya pamoja katika ukuzaji na uendelezaji wa Tafiti za Kisayansi kwa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la sahara.
Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa jambo katika Screen na Makamu Mkuu wa Chuo cha Nelson Mandela, Prof. Bulton Mwamila, wakati wakiangalia mjadala uliokuwa ukiendelea kupitia ‘Video Conference’ kati ya Marekani na Tanzania, kwenye ufunguzi wa Kongamano la Kimataifa la siku tatu kuhusu ukuzaji na uendelezaji wa Tafiti za Kisayansi kwa nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la sahara.

LAPF YATOA MIKOPO YA ELIMU KWA WANACHAMA WAKE

$
0
0
 Kaimu meneja Masoko wa LAPFBi Rehema Mkamba akitoa maelezo kwa wananchi na wanachama waliotembelea banda la lapf Nane Nane Mjini Dodoma.
 Afisa matekelezo wa LAPF  Bi Christina Mbaga akitoa maelezo juu ya Mkopo wa Elimu unaotolewa kwa wanachama wa LAPF. Mkopo huu umekuwa kivutio kikubwa kwa wanachama na wasio wanachama. 
 Afisa Mifumo ya Computer Bi. hilda Kato akifafanua jambo kwa wanachama waliotembelea bandani hapo. 
Maafisa wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF walioshiriki katika maonyesho ya Nane Nane Nzuguni Mjini Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja

MfukowaPensheniwa LAPF  umeanza kutoa Mikopo ya Elimu ya Juu kwa wanachama wake kwalengo la kuwasaidia wanachama wanaotaka kujiendeleza kielimu kwa kuwalipia ada ya masomo. LAPF inajua kuna baadhi ya wanachama walitamani kujiendeleza kielimu lakini kwa namna moja au nyingine wameshindwa kutokana na gharama za masomo hayo hivyo LAPF itawawezesha kutimiza malengo yao.  LAPF ndio Mfuko Pekee wa Pensheni nchini unaotoa mkopo wa Elimu kwa wanachama wake. 
LAPF, MCHANGO ULE ULE MAFAO ZAIDI.

RAIS KIKWETE AJIUNGA NA VIONGOZI WENGINE WA AFRIKA KATIKA MKUTANO WA VIONGOZI WA AFRIKA NA MAREKANI JIJINI WASHINGTON DC LEO

$
0
0
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakiwasili katika Ikulu ya Marekani (White House) jijini Washington DC kwa dhifa ya Kitaifa waliyoandaliwa viongozi wa Afrika na mwenyeji wao Rais Barak Obama Julai 5, 2014.
 Rais Jakaya Kikwete na viongozi wenzake wa Afrika katika mkutano wa Viongozi wa Afrika na Marekani  ambao umefunguliwa na Rais Barak Obama katika ukumbi wa State Department jijini Washington DC  leo Julai 6, 2014.
 


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry anaelekeza namna ya kutumia kipaza sauti baada ya Rais Obama kufungua mkutano huo, wakati  mwenyekiti wa Umoja wa Afrika  Rais  Mohamed Ould Abdel Aziz alipoongea kwa niaba ya Viongozi wa Afrika.PICHA NA IKULU.

SSRA YAZINDUA KANUNI MPYA ZA KUHUISHA MAFAO YA PENSHENI

$
0
0
Waziri wa Kazi na Ajira, Dk.Gaudensia Kabaka akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma juzi kuhusu mabadiliko ya Kanuni za Kuhuisha Mafao ya Pensheni kwa Mifuko ya  Hifadhi ya Jamii ya kuwa na aina moja kwa wastaafu.Katikati ni Mwenyekiti wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA),Juma Muhimbi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka hiyo, Irene Isaka.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa  Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) Irene Isaka akifurahia jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari mjini Dodomajuzi.
 Wakurugenzi Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii wakimsikiliza Waziri wa Kazi na Ajira Dk Gaudensia Kabaka,kuhusumabadiliko ya Kanuni za Kuhuisha Mafao ya Pensheni kwa Mifuko ya  Hifadhi ya Jamii ya kuwa na aina moja kwa wastaafu kupitia Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA).
Wakurugenzi Wakuu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii wakiwa katika picha ya pamoja na  Waziri wa Kazi na Ajira Dk Gaudensia Kabaka na Naibu wake Makongoro Mahanga.

MAZISHI YA ANDREA DUMA BABA WA MWANDISHI WA HABARI WA MOblog SINGIDA

$
0
0
DSC00331
Jeneza lililobeba mwili wa mchungaji mstaafu wa kanisa la Free Pentekoste (FPCT) Ihanja wilaya ya Ikungi, Andrew Duma (92).
DSC00343
Katibu mkuu wa makanisa ya Free Pentekoste nchini,Elias Shija, akihubiri kwenye ibada ya mazishi ya mchungaji mstaafu wa Free Pentekoste Ihanja wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida, Andrea Duma.
DSC00357
Mjumbe wa halmashauri kuu CCM (NEC) Singida mjini, Hassan Mazala, akitoa nasaha zake kwenye ibada ya mazishi ya mchungaji mstaafu wa kanisa la Free Pentekoste Ihanja wilaya ya Ikungi, Andrea Duma.Mazishi hayo yamefanyika jumamosi katika kijiji cha Ihanja.
DSC00355
Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali waliohudhuria mazishi ya mchungaji mstaafu wa kanisa la Free Pentekoste Ihanja wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida.Andrea Duma.Mazishi hayo yamefanyika katika kijiji cha Ihanja Jumamosi iliyopita.
DSC00337
Baadhi ya waombelezaji waliohudhuria mazishi ya mchungaji mstaafu kanisa la Free Pentekoste Ihanja Andrea Duma yaliyofanyika katika kijiji cha Ihanja.
DSC00347
DSC00363
Jeneza lillobeba mwili wa mchungaji mstaafu wa kanisa la Free Pentekoste (FPCT) Ihanja wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida Andrea Duma (92), likiingizwa kaburini, kuhitimisha safari yake hapa duniani.Mazishi hayo yamefanyika Jumamosi iliyopita katika kijiji cha Ihanja.(Picha zote na Nathaniel Limu).

TAHA WASHIRIKI MAONYESHO YA NANE NANE MBEYA

$
0
0
Afisa kilimo Mkoa wa Mbeya (Aliyevaa tai) akipokea maelezo ya kilimo cha mboga ndani ya hema maalumu ya kuoteshea nyanya iliyowekwa na Barton Tanzania kwa ushirikiano na TAHAAfisa kilimo Mkoa wa Mbeya (Aliyevaa tai) akipokea maelezo ya kilimo cha mboga ndani ya hema maalumu ya kuoteshea nyanya iliyowekwa na Barton Tanzania kwa ushirikiano na TAHA katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya
Afisa Kilimo na Msimamizi wa ofisi ya TAHA ukanda wa Nyanda za Juu Kusini Bw. Ringo (Mwenye Jaketi jekundu) akifafanua juu ya matumizi bora ya teknoloji za kisasa kwenye kilimo cha mboga ili kuongeza tija kwa MkulimaAfisa Kilimo na Msimamizi wa ofisi ya TAHA ukanda wa Nyanda za Juu Kusini Bw. Ringo (Mwenye Jaketi jekundu) akifafanua juu ya matumizi bora ya teknoloji za kisasa kwenye kilimo cha mboga ili kuongeza tija kwa Mkulima katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya
Mtaalamu wa Kilimo wa TAHA Bw. Anania Bansimbile akiwaonyesha wananchi namna bora ya kuotesha mimea ya mboga kabla ya kupandwa shambaniMtaalamu wa Kilimo wa TAHA Bw. Anania Bansimbile akiwaonyesha wananchi namna bora ya kuotesha mimea ya mboga kabla ya kupandwa shambani katika viwanja vya John Mwakangale jijini Mbeya
Chainizi iliyopandwa kwa ustadi wa hali ya juuChainizi iliyopandwa kwa ustadi wa hali ya juu.
 
Hema maalumu(greenhouse) la kuoteshea mazao yanayohitaji joto ili yaweze kustawi vizuriHema maalumu(greenhouse) la kuoteshea mazao yanayohitaji joto ili yaweze kustawi vizuri
Plot ya TAHA na mshirika wake Barton kama inavyoonekana katika pichaPlot ya TAHA na mshirika wake Barton kama inavyoonekana katika picha
Mazao ya mboga yaliyopandwa kwa utaalamu wa hali ya juu kwenye vitalu vya mboga vya TAHAPlot ya TAHA na mshirika wake Barton kama inavyoonekana katika picha
Karoti iliyovunwa kutoka katika vitalu vya TAHA kwa ajili ya maonesho ya wakulima katika viwanja vya Nanenane MbeyaKaroti iliyovunwa kutoka katika vitalu vya TAHA kwa ajili ya maonesho ya wakulima katika viwanja vya Nanenane Mbeya
Wananchi wakipokea elimu kutoka kwa mtaalamu wa TAHA namna ya kuotesha nyanya kwenye hema maalumu ya kuoteshea mazao ya mbogaWananchi wakipewa elimu lishe kuhusu umuhimu wa matumizi ya mboga kutoka kwa mtaalamu wa masuala ya lishe wa TAHA Bi. Lawrencia wakati wa maonyesho ya Nanenane Mbeya
Mtaalamu akimuelekeza jambo Mkulima aliyetembelea Banda la TAHAMtaalamu akimuelekeza jambo Mkulima aliyetembelea Banda la TAHA

Mahojiano na mgombea urais wa jumuia DMV, Liberatus Mwang'ombe

$
0
0
Karibu katika mahojiano kati ya Kwanza Production na Liberatus Mwang'ombe. Mgombea uRais wa Jumuiya ya waTanzania waishio Washington DC, Maryland na Virginia Uchaguzi unategemewa kufanyika Agosti 9, 2014

MO awashtaki CCM Singida kwa Kinana

$
0
0
kapambala
Katibu wa CCM Mkoa wa Singida Naomi Kapambala akizungumza na waanndishi wa habari juu ya ufafanuzi wa maendeleo ya ujenzi wa uwanja huo.

Na Hillary Shoo, Singida.
Mbunge wa Jimbo la Singida mjini (CCM), Mohammed Dewji ameulalamikia uongozi wa Chama chake Mkoa wa Singida kwa kitendo cha kuchelewesha mchakato wa kumalizia ujenzi wa Uwanja wa michezo Namfua ikiwa ni moja ya ahadi zake alizotoa kwa wananchi wakati wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

Kuchelewa huko kuanza kwa mchakato wa ukarabati na uwekaji wa nyasi za bandia kwenye uwanja huo imeelezwa ni kutokana na urasimu na maslahi binafsi miongozi mwa viongozi wa CCM Mkoa wa Singida.

Katika barua yake ya Julai 31 mwaka huu kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Dewji amedai kuwa kwa kiasi kikubwa ameweza kutekeleza Ilani ya Uchaguzi kwa vipindi vyote viwili pamoja na ahadi zake binafsi, isipokuwa ahadi ya kumalizia ujenzi wa michezo Namfua.

Katika barua hiyo, ambayo pia ameinakili kwa Rais Jakaya Kikwete, Katibu Baraza la wadhamini CCM Taifa, Katibu wa Uchumi na Fedha na Katibu wa CCM mkoa wa Singida, Dewji amedai kuwa kila alipotaka kufanya hivyo alipata vikwazo kutoka kwa viongozi wa CCM mkoa wa Singida.
sehemu ya uwanja
Katikati ya kiwanja chenyewe.
Amesema kuwa matayarisho yote muhimu kuhusiana na ujenzi huo yapo tayari, ikiwa ni pamoja na kuwepo dola za kimarekani 880,000 (sawa na sh bilioni 1.46) ambazo kwa kushirikiana na Rais Kikwete aliweza kuzipata kutoka Makampuni ya Airtel Tanzania na Mohammed Ent (T) Ltd.
Dewji amesema wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 yeye pamoja na Raisi Jakaya Kikwete walitoa ahadi ya kukarabati na kuweka nyasi za bandia kwenye uwanja huo unaomilikiwa na chama cha mapinduzi CCM.

 
uwanja
Hili ni jukwaa kuu la uwanja wa Namfua unaomilikiwa na CCM Mkoa wa Singida.

“Baada ya uchaguzi sote wawili tulishinda na sasa tunatumikia wananchi, na kwa kiasi kikubwa tumefanikiwa kutekeleza ilani ya uchaguzi kwa vipindi vyote viwili, pamoja na ahadi zetu binafsi, lakini ahadi tuliyotoa ya ukarabati wa uwanja mpaka sasa hatujafanikiwa kuitekeleza. Alisem MO na kuongeza Dewji amesema anasikitishwa na uongozi wa CCM Mkoa wa Singida bila sababu za msingi wanachelewesha kuanza kwa mchakato wa ukarabati wa uwanja huo.

Aidha amesema kuna vikao vingi viimefanyika na makampuni hayo bila mafanikio na hivyo anaomba CCM Makao makuu kuingilia kati ili kama kuna jambo linasababisha kusuasua kwa mchakato huo liweze kupatiwa ifumbuzi na ukarabati ufanyike haraka iwezekanavyo.
wakicheza
Vijana wakicheza mpira uwanjani humo.
Amesema suala la uchakavu wa uwanja wa Namfua imekuwa ni kero kubwa inayowakabili wananchi wa jimbo la singida mjini kwa sasa na hivyo kuwanyima vijana fursa za kutumia uwanja huo ili kupata ajira na kukuza vipaji kwa vijana. Kutokana na ukweli kwamba muda wa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015 unayoyoma, Dewji maarufu kwa jina la "MO" amemwomba Katibu Mkuu wa CCM kuingilia kati urasimu huo usio wa lazima ili ujenzi uweze kufanyika mapema.

Akizungumzia madai hayo ya Mbunge Dewji, Katibu wa CCM Mkoa wa Singida, Naomi Kapambala alikiri kupata nakala ya barua hiyo na kusema kuwa wamefanya matayarisho yote muhimu ikiwa ni pamoja na kufuatilia Airtel makao makuu juu ya suala hilo.
Aidha Kapambala amesema kuwa kamati ya siasa imemaliza kazi na kupeleka baraza la wadhamini, na kinachosubiriwa na baraza kukaa ili kutoka majibu.

“Mi namshangaa ni kwa nini yeye mwenyewe Dewji hajafika hapa ofisini na kupata ufafanuzi juu ya hili matokeo yake analeta nakala ya barua kwetu, akamwulize katibu Mkuu ambaye amemwandikia hii barua.” Alisema Kapambala Hata wakati katibu mkuu alipokuja hapa tulimweleza juu ya hilo , yeye kama anaonaje ni vyema akafika ofisini ili kujua inachoendelea.
jukwaa
Sehemu ya jukwaa la uwanja wa Namfua linalotumiwa na washabiki likiwa linaonekana kuchakaa.
Aidha Kapambala amesema Katibu mkuu msaidizi yuko jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamemwagiza kupitia baraza la wadhamini wa CCM ili kujua hatma ya suala hilo. Pia Kapambala amesema pia ofisi yake imekwishatoa notisi kwa wafanyabiashara mbalimbali kuondoka kwenye eneo la uwanja ili kupisha ukarabati huo.

Mwenyekiti wa SIREFA Baltazari Kimario alisema anasikitishwa kuona maendeleo ya uwanja huo bado haujakamilika na hivyo kuathiri maendeleo ya soka katika mkoa wa singida.
Aidha wadau mbalimbali nao wametoa masikitiko yao kwa uongozi wa CCM Mkoa wa singida kuchelewesha mchakato huo kwa maslahi binafsi, huku Mbunge akiwa tayari kushughulikia kero hiyo. Uwanja huo hivi sasa umebaki kuwa kama eneo maarufu la vijana kuvuta bangi na wengine kujisaidia hovyo kwenye vyoo na hivyo kutapakaa kwa vinyesi kila mahali ndani ya uwanja huo.

Ujenzi wa Uwanja wa Namfua,ambao ulikuwa ukienda sambamba na Jengo la CCM mkoa, ulisimama miaka ya 1990 na tangu wakati huo uwanja huo umebakia gofu na kugeuka maficho ya wahalifu mbalimbali na eneo la choo cha jumuiya.
waandishi
Baadhi ya Waandishi wa habari wa Mkoa wa Singida wakipiga picha jengo la makao makuu ya CCM Mkoa wa Singida.
bangi
Vijana hawa walikutwa wakivuta bangi kwenye majukwaa ya uwanja wa Namfua.
jengo la ccm
Hapa ndio makao makuu ya CCM Mkoa wa Singida.(Picha zote na Hillary Shoo).

Hotuba ya Mhe Rais Uhuru Kenyatta kwa waKenya Washington DC. Aug 6, 2014

$
0
0
Mhe. Rais Uhuru Kenyatta akihutubia waKenya jijini Washington Aug 6, 2014
Karibu kusikiliza hotuba ya Mhe. Uhuru Kenyatta alipozungumza na waKenya usiku wa Agosti 6, 2014 kwenye hotel ya Marriott Wardman Park Hotel, jijini Washington DC nchini Marekani.

WEZI WA KAZI ZA WASANII KUKIONA,KAMATA KAMATA YAANZA RASMI

$
0
0
 Kampuni ya Msama Promotions Ltd,kwa kushirikiana na Wizara ya habari vijana,utamaduni na michezo  imetangaza neema kwa wasanii kuanza zoezi la kuwakamata watu wanaouza nakala feki  za wasanii hapa nchini.

Mkurugenzi wa kampuni hiyo,Bwana  Alex Msama  amesema hayo jijini dar ,kuwa zoezi hilo limekwishaanza, na mpaka  sasa wamekamatwa vijana wane katika mkoa wa Dodoma na watatu jijini Mwanza.

‘’Kuna kazi mbalimbali ambazo zinaibiwa kila kukicha huku wamiliki wa kazi hizo wakiendelea  kushuka kiuchumi  na kutoona faida  yoyote ya kazi hizo,huu ni wakati kwa wasanii kuneemeka na kazi zao.Hivyo tutahakikisha tunafika kila mahali hata sehemu zisizofikika kirahisi na yote hii ni kuonyesha kuwa tunajali na tunathamini kazi za wasanii wetu’’,alisema Msama kwa msisitizo.

Alisema, nakala zote zitakuwa na stika za TRA  kuhakikisha hakuna wizi wowote unaofanyika  na unaotokea katika kazi mbalimbali za wasanii.Stika hizo zimewekwa ili kuwabaini wale wote wenye hulka hiyo ya kuiba kazi za wasanii .Operesheni  hiyo itafanyika  bila kujali wadhifa wake ama cheo chake,akaongeza kusema kuwa zoezi hilo ni salamu kwa wale wote wanoatumia kazi za wasanii bila kufuata  utaratibu wa sheria zilizopo.

Pia amelipongeza Jeshi la Polisi nchini kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha katika changamoto,na pia wamekuwa wakishirikiana  nao kuhakikisha  zoezi hilo linakuwa endelevu na kuzunguka kila mkoa kuhakikisha  kazi za wasanii zinaheshimiwa na zinalindwa kwa kila namna.

HITIMISHO LA SHINDANO LA ELIMU YA UWEKEZAJI KWA WANAZUONI (DSE SCHOLAR INVESTMENT CHALLENGE) KUFANYIKA AGOSTI 13 2014

$
0
0
Soko la Hisa Dar es Salaam (Dar es Salaam Stock Exchange), kwa udhamini wa benki ya NMB, Selcom na FSDT, linapenda kuwajulisha wanafunzi wa elimu ya juu nchini walioshiriki katika shindano la elimu ya uwekezaji kwa mwaka 2014 (DSE Scholar Investment Challenge 2014) kuwa maandalizi yote ya kuhitimisha shindano hili kwa sasa yamekamilika.

Mchakato wa kutambua nafasi ya kila mshiriki wa shindano umemalizika. Majina ya wanafunzi 50 wanaoongoza katika shindano hilo yamebandikwa katika mtandao wa DSE (www.dse.co.tz) kwenye kipengele cha Investment Challenge.

Sherehe za kuwatambua washindi na kuwapatia vyeti na zawadi zitafanyika tarehe 13 August 2014 jijini Dar es Salaam. Mialiko ya kuhudhuria sherehe hizo inaendelea kutumwa kwa njia ya simu.
 (sehemu ya umati wa wanafunzi walioshiriki katika elimu ya uwekezaji kwenye hisa na masoko ya mitaji nchini iliyoendeshwa na DSE kwa wanazuoni).

Shindano la elimu ya uwekezaji kwa wanazuoni (DSE Scholar Investment Challenge) lilianza tarehe 01/04/2014 na kumalizika tarehe 30/06/2014. Wanafunzi washiriki walipewa nafasi ya kutumia simu zao za mkononi ili kununua na kuuza hisa zinazouzwa katika soko la hisa (DSE) la Dar es Salaam. Kila mshiriki alipewa mtaji (virtual capital) wa shilingi milioni moja. Ushiriki kwa shindano hili ulikuwa ni bure na huru kwa yeyote aliyependa.

Nia kubwa ya shindano hili ni kuwapatia vijana walio katika vyuo vya elimu ya juu nchini fursa ya kuwekeza katika soko la hisa kwa majaribio na kuangalia mitaji yao ikikua. Elimu hii pia ni muhimu katika kujenga utamaduni wa utunzaji fedha na uwekezaji miongoni mwa vijana walio vyuoni (ambao ni viongozi, wawekezaji, wahasibu, wachumi, na washauri watarajiwa).

Washiriki walitegemewa kushindana kukuza mitaji waliyopewa kwa kipindi cha miezi mitatu. Mafanikio ya shindano na elimu hii ni makubwa sana. Mwanafunzi anayeongoza amekuza mtaji wake kutoka shilingi milioni moja aliyopewa na kufikisha shilingi milioni nne (kwa kipindi cha miezi mitatu tu).
DSE inawapongeza zaidi ya wanafunzi 5,000 walioshiriki katika shindano na elimu hii muhimu kwao na taifa kwa ujumla.

Shindano na elimu hii imepangwa kufanyika tena mwakani na kuwahusisha wanafunzi wengi zaidi ya elfu tano walioshiriki mwaka huu. DSE imepanga kuwawezesha wanafunzi na vijana nchini kutumia simu pamoja na intaneti mwakani ili kuwapa uwanja mpana zaidi wa kushiriki. Mipango ya baadaye ni kuwashirikisha wanafunzi walioko kwenye shule za sekondari pia.
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live


Latest Images