Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA YAWAFUNDA WAKUU WA IDARA NA VITENGO JUU YA HAKI ZA BINADAMU.

$
0
0

 Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan akisoma hotuba wakati wa
kufungua mafunzo kwa Wakuu wa Idara na vitengo kutoka Mkoa wa Dodoma na
Singida ya Mpango kazi wa Haki za Binadamu.
 Washiriki wa mafunzo kutoka Mkoa wa Singida wakiwa katika picha ya
Pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan.
 Washiriki wa mafunzo kutoka Mkoa wa Dodoma wakiwa katika picha ya
Pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan.
Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan (katikati)akiwa katika
picha ya pamoja na Mratibu wa Mpango kazi wa Haki za Binadamu Bw. Laurenti  
Buliro (mwenye suti nyeusi)na mtumishi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na ASA
Utawala bora Bw Vicent Mbombo (kulia).

"Suala la uwajibikaji kwa watumishi wa umma wakiwemo wa Halmashauri ni
changamoto kubwa kutokana na  baadhi yao kutozingatia maadili ya kazi zao,  
kuendekeza rushwa, kutoa huduma zisizokidhi matarajio ya wananchi na hivyo  
kusababisha malalamiko ya wananchi dhidi ya serikali".

Katibu Tawala Mkoa wa Singida Liana Hassan ameyasema hayo leo asubuhi
katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wakati akifungua mafunzo ya Mpango   
kazi wa Kitaifa wa haki za Binadamu kwa wakuu wa idara na vitengo 60  
kutoka Mikoa ya Dodoma na Singida.

Liana  amesema ipo haja kubwa ya kueneneza elimu ya haki za binadamu na 
misingi ya utawala bora katika jamii ili haki hizo ambazo zimeaninishwa
katika Katiba ya nchi, sheria na mikataba ya haki za binadamu itambuliwe
na kuheshimiwa na watu wote.

Ameongeza kuwa hivi karibuni vyombo vya habari vimekuwa vikitoa taarifa za  
uvunjifu wa haki za binadamu hali inayoonesha kuwa bado kuna uelewa mdogo 
wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora katika jamii.

Liana amesisitiza kwa kutoa mifano ya taarifa za ukatili dhidi ya watoto,
matukio mbalimbali ya wananchi kujichukulia sheria mikononi dhidi ya
watuhumiwa wa uhalifu, ukatili dhidi ya wanawake na utumikishwaji wa
watoto kuwa yamekuwa yakijitokeza kwa wingi.

Tume ya haki za Binadamu inatoa mafunzo ya siku nne kwa wakuu wa Idara na 
Vitengo 60 kutoka Mikoa ya Dodoma na Singida juu ya Mpango kazi wa Kitaifa 
wa Haki za binadamu.

Mafunzo hayo yatajikita katika kutambua makundi mbalimbali ya haki za
binadamu ambayo ni haki ya kiraia na kisiasa, haki za kiuchumi, kijamii na
kiutamaduni, haki za makundi na misingi ya utwala bora.

KAMPUNI YA MAFUTA NA GESI YA SWALA (TANZANIA) PLC INATANGAZA UZINDUZI WA IPO.

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Swala (Tanzania) PLC, David Mestres Ridge (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu ufunguzi wa ofa ya awali kwa umma ijulikanayo kwa kifupi (IPO) ambayo itakuwa na hisa za kawaida,9,600,000. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa ARCH Financial $ Investment Adivisory Limited,Iyen Nsemwa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Swala (Tanzania) PLC, Abdullah Mwinyi (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu ufunguzi wa ofa ya awali kwa umma ijulikanayo kwa kifupi (IPO) ambayo itakuwa na hisa za kawaida,9,600,000. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Swala, David Mestres Ridge na Mkurugenzi Mkuu wa ARCH Financial $ Investment Adivisory Limited,Iyen Nsemwa. 

=====  =======  =========

 Kampuni ya Mafuta na Gesi ya Swala (Tanzania) Plc leo imetangaza ufunguzi wa ofa yake ya awali kwa umma ijulikanavyo kwa kifupi kama ("IPO") yenye hisa za kawaida 9,600,000. Kampuni itakuwa ikiuza kila hisa  kwa bei ya shilingi za Kitanzania 500 kuanzia tarehe 9 juni 2014 mpaka tarehe 4 Julai 2014. 

Tangazo hili limekuja wiki moja baada ya kampuni  kupokea idhini yake rasmi kutoka Mamlaka ya masoko ya Mitaji na Dhamana Tanzania ("CMSA"), na kuifanya kuwa ni ofa ya kwanza kufanyika kwenye sekta ya mafuta na gesi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Mkurugenzi Mtendaji wa Swala Bwana David Mestres Ridge alisema, "Tunafuraha kuwa, leo Kampuni ya mafuta na gesi ya Swala (Tanzania) Plc imezindua rasmi mpango wake wa ofa ya awali kwa umma ijulikanayo kama IPO. Hii ni hatua kubwa si tu kwa ajili ya Swala lakini pia kwa Tanzania na watu wake kwa ujumla. . Kuwekeza hisa katika mafuta na gesi ni moja ya njia za kupanua wigo wa kiuchumi kwa mtu yeyote na inaruhusu mtu yeyote kumiliki hisa katika biashara hii inayokua kwa kasi ".


Bwana Ridge alizidi kusema, "Tunaishukuru sana Serikali ya Tanzania, Shirika la mafuta na gesi Tanzania (TPDC), Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) kwa kuturuhusu kuwa kampuni ya kwanza ya Mafuta na gesi katika Afrika Mashariki inayomilikiwa na umma. Kwa niaba ya wakurugenzi wote wa Swala napenda kuukaribisha rasmi umma kuwekeza katika Kampuni ya  mafuta na gesi ya Swala (Tanzania) Plc ".


                      Mhe. Abdullah Mwinyi, ambaye ni Mkurugenzi wa Swala Tanzania Plc aliongeza, "Kumekuwa na mjadala mkubwa kwa wazawa katika sekta hii ya uchimbaji wa mafuta na gesi; Tumefurahia kwamba leo kampuni ya mafuta na gesi ya Swala imekuwa ya kwanza kuanza utekelezaji wa haja za wazawa katika sekta hii ya mafuta na gesi. Tunaamini kwa dhati kabisa kwamba Watanzania wapewe nafasi ya kushiriki katika biashara ya mafuta na gesi; ufunguzi huu wa IPO unaruhusu wao kufanya hivyo."


Fomu za maombi na nakala ya Waraka wa matarajio zitakuwa zinapatikana katika ofisi zote za Mawakala wenye leseni kutoka soko la hisa la Dar Es Salaam (DSE) walioko karibu yako, matawi ya Benki ya CRDB Plc na ofisi za Arch Financial & Investment Advisory Ltd. Ofa iko wazi kuanzia tarehe 9 Juni 2014 mpaka 4 Julai 2014. 

Kwa sasa hakuna ukomo wa kiwango cha juu cha hisa, lakini kiwango cha chini cha kununua ni hisa 100 kwa mtu. Waraka wa Matarajio wa kielektronikia unapatikana kwenye tovuti ya kampuni www.swala-energy.co.tz au www.nihisa.com

BALOZI MPYA WA MAREKANI AJITAMBULISHA KWA MHESHIMIWA MAKAMU WA RAIS

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib, akimkaribisha Balozi mpya wa Marekani nchini Tanzani, Mark Childres, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 9, 2014 kwa mazungumzo na utambulisho wa balozi huyo. Picha na OMR.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika mazungumzo na Balozi mpya wa Marekani nchini Tanzania, Mark Childres, wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Juni 9, 2014 kwa mazungumzo na utambulisho wa balozi huyo. Picha na OMR

======= ========
BALOZI MPYA WA MAREKANI AJITAMBULISHA KWA MHESHIMIWA MAKAMU WA RAIS
Ikulu, Dar es Salaam: 2014-06-09

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal leo amekutana na Balozi mpya wa Marekani, Mheshimiwa Balozi Mark Childress ambaye amefika ofisini kwa mheshimiwa Makamu wa Rais kwa ajili ya kujitambulisha.

Balozi Childress alimueleza Mheshimiwa Mkamu wa Rais kuwa, Tanzania ni nchi yenye uhusiano maridhawa na Marekani na kwamba katika kipindi chake kama Balozi atahakikisha uhusiano huu mzuri uliojengwa unadumishwa na kwamba, nchi hizi mbili zinazidi kuwa na maeneo ya kushirikiana hasa yanayolenga kuboresha maisha ya watu na kuwapatia maendeleo.

Balozi Childress pia alisema kuwa Tanzania imekuwa ikitumia kama mfano kufuatia kuonesha mabadiliko ya haraka katika miradi mbalimbali inayoendeshwa hapa nchini kwa ushirikiano na watu wa Marekani na akafafanua kuwa, kazi iliyoko mbele ni kuhakikisha kuwa Tanzania inapiga hatua zaidi na sio kurudi nyuma.

“Mheshimiwa Makamu wa Rais, kila nikipata fursa ya kukutana na wenzangu tumekuwa tukizungumzia suala la Tanzania kupiga hatua kwa haraka. Mna mambo mengi yaliyofanyika na kazi iliyopo ni kuendelea kupiga hatua pasipo kurudi nyuma,” alisema.

Kwa upande wake Mheshimiwa Makamu wa Rais alimueleza Balozi Childress kuwa, Tanzania ipo katika kipindi ambacho kinaonesha mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kwamba kazi ya serikali ya Tanzania ni kuhakikisha kuwa uchumi unakuwa na unasaidia vizazi vya sasa na vijavyo.

“Mtazamo wetu katika serikali ni kuwa Tanzania itapiga hatua kubwa katika miaka michache ijayo. Lengo letu ni kutazama kuwa ukuaji wa uchumi hauwi wa muda mfupi, tunatazama pia maendeleo kwa vizazi vijavyo.

Kuhusu suala la utunzaji mazingira, Balozi Childress alisifu hatua za Mheshimiwa Makamu wa Rais hasa katika kazi ya uhamasishaji upandaji miti na akasema, utunzaji wa mazingira ni jambo la muhimu ili kuifanya nchi yetu iweze kuendelea na isikabiliane na matatizo yanayotokana na mazingira kuharibiwa.

“Nakupongeza Mheshimiwa Makamu kwa kazi yako ya uhamasishaji utunzaji wa Mazingira. Usichoke kufanya hivyo maana unasaidia dunia,” Balozi Childress alisema.

Imetolewa na : Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es Salaam

Tamko la wabunge tanzania katika bunge la afrika mashariki

$
0
0
Mwenyekiti wa wabunge wa Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki(EALA) Mh. Adam Kimbisa akitoa tamko la wabunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki kwa waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu sakata la kumvua madaraka spika wa bunge hilo wakati wa Mkutano uliofanyika katikamukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO).Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Bw. Assah Mwambene.

 Katibu wa wabunge wa Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki(EALA) Mh. Shy-rose Bhanji akieleza kwa waandishi wa habari juu ya uamuzi wake wa kutoiunga mkono hoja kwa kutoa sahihi zao kama inavyoelezwa katika kanuni ya 9(2) ya kanuni na utaratibu wa uendeshaji wa bunge.Kulia ni Mbunge wa Bunge hilo Mh. Twaha Taslima
 Mbunge wa Tanzania katika bunge la Afrika Mashariki(EALA) Mh. Twaha Taslima akieleza jambo kwa waandishi wa Habari(Hawapo pichani)wakati wa Mkutano uliofanyika katikamukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO). Kushoto ni Katibu wa wabunge wa Tanzania katika bunge hilo Mh. Shy-rose Bhanji.Picha na Hassan Silayo-MAELEZO.
=======  ======  =========

BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI KANDA YA TANZANIA (EALA-TZ)

_____________________________________________________




TAMKO LA PAMOJA LA WABUNGE WA TANZANIA WANAOWAKILISHA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI (EALA) JUU YA SAKATA LA KUTAKA KUMVUA MADARAKA SPIKA WA BUNGE HILO 0/06/2014


Sisi, Wabunge saba wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania (EALA-TZ), tunapenda kusisitiza msimamo wetu wa kutounga mkono jaribio la kutaka kumuondoa madarakani Spika wa EALA, Mh. Margaret Nantongo Zziwa.


Baada ya kutafakari kwa uangalifu na kwa umakini mkubwa kuhusu chanzo halisi cha hoja yenyewe ya kutaka kumuondoa Spika wa EALA madarakani, tuligundua mambo yafuatavyo:


1. Hoja hii haina maslahi ya Tanzania na iko kinyume na malengo ya ushirikiano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Tumebaini kuwa hoja yenyewe ni sehemu ya "mchezo mchafu" wa ajenda ya siri ya kujaribu kuweka mbele maslahi ya baadhi ya wanachama wachache wa jumuiya badala ya kuzingatia maslahi mapana ya EAC.


2. Tuhuma mbalimbali zilizotajwa dhidi ya Spika wa EALA kuhusu yeye kuonesha upendeleaji, ujeuri na mapungufu mengine ya uongozi zimegundulika kuwa hazina mashiko na wala mantiki .


3. Kitendo ambacho kimetushtua ni kuwa kumekuwa na majaribio kadhaa ya baadhi ya Wabunge wa EALA kutoka nje ya Tanzania na viongozi wa Sekretarieti ya EAC kutaka kulazimisha sahihi za baadhi ya Wabunge wa Tanzania zitumike kinyume na utaratibu kuunga mkongo Azimio tajwa (kitu ambacho tunakipinga kwa nguvu zote). Hii inadhihirisha kuwepo kwa ajenda ya siri katika sakata hilo dhidi ya maslahi ya Tanzania na jumuiya kwa ujumla.



4.                         Kufuatia malumbano yaliyoibuka katika kikao cha Bunge cha mwezi Machi huko Arusha, sisi Wabunge wa Tanzania tulipokea maoni na masikitiko mengi kutoka kwa wana Afrika Mashariki na viongozi kwa ujumla wakitusihi kumaliza tatizo hili kwa njia ya amani na utulivu, lakini jitihada zetu ziligonga ukuta. Hatua hii ilizidi kutudhihirisha kuwepo kwa ajenda ya siri.

 

Ikumbukwe kuwa azimio la kutaka kumuondoa Spika madarakani awali lilipangiwa kuwasilishwa katika kikao cha Bunge la EALA cha mwezi Machi 2014 huko Arusha lakini liligonga mwamba baada ya kuibuka mabishano ya kisheria, hali iliyopelekea kuahirishwa kwa kikao hicho.


Hoja hii ililetwa tena kwenye vikao vingine vya EALA, lakini baada ya kutafakari kwa makini kuhusu chanzo halisi cha mzozo huu, idadi kubwa ya Wabunge kutoka Tanzania (7 kati ya 9) waliamua kwa pamoja kuipinga hoja hii kwani imekosa mashiko na haizingatii maslahi ya Tanzania na maslahi mapana ya jumuiya kwa ujumla.


Aidha, wabunge watatu wa EALA kutoka Tanzania ambao awali waliunga mkono hoja hii waliamua baadae kuipinga kwa kutoa sahihi zao kwa hiari yao wenyewe na walimwandikia barua Katibu wa Bunge wa EALA kumueleza maamuzi yao kwa mujibu wa utaratibu mnamo tarehe 29 Mei 2014. Barua hizo za Wabunge wa Tanzania wa EALA kutoa sahihi zao kwenye hoja hiyo zilipokelewa rasmi na Katibu wa Bunge.


Wabunge hao wa EALA kutoka Tanzania walitumia haki zao za kikanuni kuondoa sahihi zao kama inavyoeleza katika kanuni ya 9 (2) ya Kanuni na Utaratibu wa Uendeshaji wa Bunge (Rules of Procedure of the Assembly) inayosema: "Azimio la kumuondoa Spika madarakani halina budi kuambatana na sahihi zisizopungua nne kutoka kila nchi mwanachama."


Hoja yenyewe ya kumuengua Spika wa EALA ni batili kisheria kwa kuwa haikuwasilishwa Bungeni ndani ya siku 7 tangu ilipopelekwa kwa Katibu wa Bunge na pia imekosa sahihi za kuungwa mkono na wabunge wanne kutoka kila nchi mwanachama wa EAC kama kanuni zinavyotamka.


Uamuzi wa Wabunge wa EALA kutoka Tanzania kuondoa sahihi zao kwenye hoja hiyo ni lazima uheshimiwe na kila mtu kwa kuwa wanatekeleza haki yao ya kidemokrasia.


Tunaomba uongozi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ngazi zote ikiwemo Sekretarieti ya jumuiya kuheshimu maamuzi ya Wabunge wa EALA kutoka Tanzania. Ikumbukwe kuwa hapo awali, wabunge wa 5 wa EALA kutoka Tanzania kati ya jumla ya wabunge wote 9 wa Tanzania walionesha kuunga mkono hoja hii. Baada ya kubaini kuwepo kwa “mchezo mchafu” na ajenda ya siri, Wabunge watatu wa EALA kutoka Tanzania waliondoa sahihi zao na hivyo basi kufanya idadi kubwa ya Wabunge kutoka Tanzania (7 kati ya 9) kuipinga hoja hii batili.


Wabunge wa EALA wameshapoteza muda mwingi, fedha na rasilimali nyingine mpaka sasa kwenye hoja hii isiyo na tija ya kujaribu kumng'oa madarakani Spika wa EALA. Sasa hatuna budi kuweka jitihada zetu kwenye kazi muhimu ya kutetea maslahi ya raia wapatao milioni 140 wa Afrika Mashariki.


Hatuwezi kuwahudumia raia wa Afrika Mashariki kwa kuweka mbele ajenda za siri na kujishughulisha kwenye siasa za malumbano. Wananchi wa Afrika Mashariki wanataka kuona faida halisi kutoka kwenye jumuiya yao. Tuna imani na Spika wa sasa wa Bunge la EALA kuwa ni kiongozi sahihi wa kuongoza Bunge hilo.


Tunaamini kuwa hakuna tija yoyote kwa Wabunge wa EALA kuendelea kupoteza fedha za walipa kodi wa Afrika Mashariki kwa kujadili hoja hii batili. Badala yake, Wabunge wa EALA wana kazi ngumu ya kusimamia maslahi ya wananchi wa jumuiya wanaotaka kupata elimu bora, maji safi na salama ya kunywa, uhakika wa chakula, afya bora, miundombinu ya kisasa na maendeleo ya kiuchumi -- siyo siasa za ulaghai.


Tunatoa wito pia kwa Wabunge wenzetu wa EALA kutoka nchi nyingine wanachama na kwa viongozi wa Sekreterieti ya EAC kutojihusisha na ajenda zozote za siri za kujaribu kumng'oa Spika wa sasa wa EALA aliyepo madarakani kisheria. Wananchi wa Afrika Mashariki wanastahili zaidi ya hayo.


Njia pekee ya kufikia maslahi yetu ya pamoja ni kwa kutumia ushirikiano, badala ya kuendekeza malumbano na siasa za chuki na kututenganisha.  Sisi Wabunge saba bado tunasisitizia AMANI NA UTULIVU kwani bila ya hivyo hakuna maendeleo na ustawi wa jamii.




Tamko hili limetolewa Dar es Salaam tarehe 9 Juni 2014 na Wabunge wafuatao:



Mhe. Adam Kimbisa, Mwenyekiti wa Wabunge wa EALA wa Tanzania


Mhe. Shy-rose Bhanji, Katibu wa Wabunge wa EALA wa Tanzania


Mhe. Charles Makongoro Nyerere, Mbunge wa EALA


Mhe. Maryam Ussi, Mbunge wa EALA


Mhe. Bernard Murunya, Mbunge wa EALA


Mhe. Twaha Taslima, Mbunge wa EALA


Mhe. Angellah Kizigha, Mbunge wa EALA




________________________                                                       

Mwenyekiti, Wabunge wa EALA wa Tanzania 


                     


________________________                                                        

Katibu, Wabunge wa EALA wa Tanzania    




________________________                                                       

Mwanasheria, Wabunge wa EALA wa Tanzania      

RAIS KIKWETE AHANI MSIBA WA KANALI MSTAAFU ALI MWANAKATWE JIJINI DAR LEO

$
0
0
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya Marehemu Kanali mstaafu Ali Hassan Mwanakatwe wakati wa hafla ya kuaga mwili wa marehemu katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo, jijini Dar es Salaam leo Juni 9, 2014.
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt Hussein Mwinyi, Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Samuel Albert Ndomba na maafisa waandamizi wa jeshi na waombolezaji  wakiwa katika shughuli ya kuaga mwili wa Marehemu Kanali mstaafu Ali Hassan Mwanakatwe katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo, jijini Dar es Salaam leo Juni 8, 2014.
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima zake za mwisho kwenya shughuli ya kuaga mwili wa  Marehemu Kanali mstaafu Ali Hassan Mwanakatwe aliyefariki  dunia Jumamosi  asubuhi katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo, jijini Dar es Salaam.
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akifariji wafiwa  kwenya shughuli ya kuaga mwili wa  Marehemu Kanali mstaafu Ali Hassan Mwanakatwe aliyefariki  dunia Jumamosi  asubuhi katika Hospitali Kuu ya Jeshi (GMH) Lugalo, jijini Dar es Salaam.

MKURUGENZI WA KIWANDA CHA MONABAN CHA JIJINI ARUSHA ASIMIKWA RASMI KUWA KAMANDA WA VIJANA UVCCM MKOA

$
0
0
003Makamu mwenyekiti UVCCM Taifa Mboni Mhita akimuapisha Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel kuwa kamanda wa vijana UVCCM Mkoa sherehe zilizofanyika juzi jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho
002Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel akiapa kuwa kamanda wa vijana UVCCM Mkoa sherehe zilizofanyika juzi jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho
001Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel akiwa ameshililia ngao mkuki ishara ya kusimikwa rasmi kuwa kamanda wa vijana UVCCM Mkoa sherehe zilizofanyika juzi jijini Arusha na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho
004Hapa akiwa anavalishwa taji
005Makamu mwenyekiti UVCCM Taifa Mboni Mhita akiwa anaongea katika sherehe hizo za kusimikwa rasmi Mkurugenzi wa kiwanda cha kuzalisha unga kilichopo jijini Arusha Bw.Philemon Mollel kuwa kamanda wa vijana Mkoa.Picha na Pamela Mollel wa Jamiiblog

WAKUU WA IDARA, MANISPAA NA HALMASHAURI ZA UNGUJA WAPATIWA MAFUNZO JUU YA HAKI ZA BINADAM.

$
0
0
 Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya siku nne ya Wakuu wa Idara, Manispaa na Halmashauri za Unguja kuhusu mpango kazi wa kitaifa wa haki za binadam, yalioandaliwa na Tume ya Haki za Binadam na Utawala Bora. katika ukumbi wa Eacrotanal Mjini Zanzibar. 
 Kamishna Tume ya Haki za Binadam na Utawala Bora Zanzibar Zahor Juma Khamis akifungua mafunzo ya siku nne ya Wakuu wa Idara, Manispaa na Halmashauri za Unguja kuhusu mpango kazi wa kitaifa wa haki za binadam, (kulia) Mkurugenzi wa Haki za Binadam na Utawala Bora Francis Nzuki na (kushoto) Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serekali Ofisi ya Dar es Salaam Bi. Alesia Mbuya
 Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serekali  Bi. Alesia Mbuya akiteta kitu na Kamishna wa Tume ya Haki za Binadam na Utawala Bora Zanzibar Zahor Juma.
Kamishna Tume ya Haki za Binadam na Utawala Bora Zanzibar, Zahor Juma (alievaa koti) katika picha na washiriki wa mafunzo ya siku nne ya Wakuu wa Idara, Manispaa na Halmashauri za Unguja yanayofanyika Eacrotanal Mjini Zanzibar. (Picha na Makame Mshenga wa Maelezo Zanzibar).

RAIS KIKWETE AHANI MCHEKESHAJI SAIDI NGAMBA "MZEE SMALL" JIJINI DAR LEO

$
0
0
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika dua  wakati alipokwenda kuhani msiba wa msanii  maarufu wa filamu vichekesho Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small” nyumbani kwa  marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014  
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati alipokwenda kuhani msiba wa msanii  maarufu wa filamu vichekesho Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small” nyumbani kwa  marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014  Kulia ni Bw. Mahmoud Saidi, Mtoto wa Marehemu “Mzee Small”.
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete wakifariji wafiwa   wakati walipokwenda kuhani msiba wa msanii  maarufu wa filamu vichekesho Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small” nyumbani kwa  marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014  
 Mama Salma  Kikwete akimpa pole mjane wa  Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Smal”l  wakati alipokwenda kuhani msiba wa msanii huyo  maarufu wa filamu za vichekesho nyumbani kwa  marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014  
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimpa pole mjane wa  Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small  wakati alipokwenda kuhani msiba wa msanii huyo  maarufu wa filamu za vichekesho nyumbani kwa  marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014 .PICHA NA IKULU
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Bw. Mahmoud Saidi, Mtoto wa Marehemu Saidi Ngamba “Mzee Small” wakati alipokwenda kuhani msiba wa msanii huyo maarufu wa filamu vichekesho nyumbani kwa  marehemu Tabata Kimanga jijini Dar es salaam leo Juni 9, 2014


 Msafara wa magari na waendesha Bodaboda wakiwa katika barabara ya Segerea Kinyerezi wakati wakielekea Makaburi ya Segerea kwaajili ya Kumpumzisha Kwa Amani Mkongwe wa Sanaa ya Vichekesho Nchini Said Ngamba almaarufu Mzee Small
 Gari lililobeba Mwili wa Marehemu Said Ngamba aka Mzee Small (la kwanza) likiwa limesimama kwaajili ya Vijana kuubeba Mwili wake hadi kwenye Makaburi ya Segerea jioni Hii
 Vijana wakishusha jeneza lenye mwili wa Marehemu Mzee Small kwaajili ya kuelekea kwenye Makaburi ya Segerea
 
Vijana wakiwa wamepanga mstari kuanzia Barabara ya Segerea Kinyerezi hadi makaburini kwaajili ya kupokea jeneza lenye Mwili wa Marehemu Mzee Small.
 Vijana wakiwa wamebeba jeneza lenye Mwili wa Marehemu Mzee Small wakielekea kwenye Makaburi ya Segerea Jioni Hii.
 Watu mbalimbali wakisubiri Mwili wa Marehemu kuwasili katika makaburi ya Segerea
 Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifamba akiwasilika katika eneo la Makaburi ya Segerea jioni hii kwaajili ya kumzika Mzee Small
 Mwili wa Marehemu Mzee Small ukitolewa kwenye jeneza tayari kupumzishwa katika Nyumba yake ya Milele katika makaburi ya Segerea.
 Watu mbalimbali wakiwasili kwenye makaburi ya Segerea kwaajili ya kumzika Mzee Small. 
 Umati wa watu wakielekea Kupokea Jeneza lenye mwili wa Marehemu Mzee Small wakati ulipowasili kwenye eneo la Makaburi ya Segerea.
 Wanahabari wakitafuta taswira katika mazishi ya Mzee Small katika Makaburi ya Segerea
Picha Zote na Josephat Lukaza - Lukaza Blog

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AFUNGUA MAONYESHO YA SIDO NA TAHA

$
0
0
 Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mh Magessa Mulongo akiwa anaangalia bidhaa zinazotengenezwa na kabila la wahabeshi katika uzinduzi wa maonyesho ya  sido.
 Mkurugenzi wa Sido Taifa Omary Bakari akiwa anasoma risala kwa mgeni rasmi katika maonyesho hayo.
 Meneja wa Sido  Isidori kayenze Arusha akiendelea kunogesha maonyesho hayo.
baadhi ya bidhaa za shanga zilizopo katika maonyesho ya sido
 Mkurugenzi wa TAHA, Jacqueline Mkindi akiwa anaangalia na kufurahia bidhaa zinazotengenezwaa na shanga zilizopo katika viwanja vya makumbusho katika maonyesho ya wajasiriamali toka  viwanda vidogo vidogo
 wahadzabe wakiendelea kutengeneza mikuki yao.

KINANA AKUTANA NA BALOZI WA UINGEREZA

$
0
0
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akimkaribisha kwa furaha, Balozi wa Uingereza hapa nchini, Dianna Melrose, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam,  leo June 9, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, na Balozi  huyo wa Uingereza hapa nchini, Dianna Melrose, wakipena mikono kabla ya kuanza mazungumzo yao, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, June 9, 2014.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungumza na Balozi wa Uingereza hapa nchini, Dianna Melrose, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, leo, June 9, 2014. Picha zote na Bashir Nkoromo-CCM Blog.

BONDIA IBRAHIMU CLASS 'KING CLASS MAWE' AIWEKA PAZURI TANZANIA KIMATAIFA

$
0
0
-----------------------------
Bondia Mtanzania anaeshika rekodi  namba moja nchini Ibrahimu Class 'King Class Mawe' amerudi na ubingwa wa WPBF  nchini akitokeza Zambia ambapo alifanikiwa kumpiga kwa K,O mbaya sana bondia Mwansa Kabinga wa Zambia mchezo uliochezwa Arthur Davis Stadium, Kitwe, Zambia
Akizungumzia safari yake ya kuelekea kunyakuwa ubingwa huo alisema amepata tabu sana wakiwa njiani ambapo wame ondoka alhamisi usiku sana na kufika Jumamosi asubuhi nchini Kenya ambapo alizuiwa kutokana na kuwa na passport ndogo hivyo hakufanikiwa kwenda Zambia. Hapo Nairobi wakasaidiwa na  Balozi wa Tanzania nchini Kenya, hat hivyo ndege waliyokuwa wapande ilikuwa imeshaondoka zamani

Baada ya hapo kuna pesa  walitakiwa waongeze,  wakaongeza kiasi kwa kudunduliza ndipo wakasafiri mpaka Zambia.

Huo ulikuwa ni mchezo wake wa kwanza kucheza nje ya nchi tangia ajiunge na ngumi za kulipwa na kufanikiwa kunyakuwa ubingwa huo ambao umemuweka katika ramani nyingine kabisa ya kimataifa. 
Mkuu huyo wa Wilaya alisema "Watu wengi wanapenda mchezo wa ngumi hivyo kwa niaba ya serikali nitafanya jitiada nikupatie mchezo mmoja kwa ajili ya kutetea mkanda wako hata burundi ili uzidi kufahamika na kukuza kipaji chako"

Bondia Ibrahimu Class 'King Class Mawe' hajawa nyuma kuwashukuru makocha wake ambao wamemwezesha kufika hapo ambao ni pamoja na Habibu Kinyogoli 'Masta',  Kondo Nassoro, Sako  Mtulya na kocha wa kimataifa wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ambaye anamtafutia mapambano mbalimbali na humpa ushauri.

SMART CODES goes to the next level with award nomination

$
0
0
Smartcodes, a tech startup from Dar-es-Salaam has been nominated in the 2014 Awwwards from awwwards.com as one of the best websites. As the #1 pick from Tanzania, Smartcodes has been nominated on an international platform going against web development and tech companies from around the world.

About the nomination for best website


The Awwwards are judged by a jury and users from the site who also get a say in which nominees have the chance of winning. Smartcodes will be judged on criteria such as design, user interface, content and creativity. As the #1 pick from Tanzania to be nominated, CEO Edwin Bruno said: “We were thrilled to hear that we have been nominated for this award. As the top choice from Tanzania to be nominated, we hope to represent our country well in this award competition. To be put amongst the best in the world for nominations, we couldn’t be happier.”

  
As an IT company, Bruno says that Smartcodes is defined by its mission to bring technology to everyone. The company achieves this thanks to products and services such as website design, mobile application, domain hosting and software development. Edwin Bruno continued to say: “We think our nomination for the Awwwards for website design is a sign that people appreciate beautifully-designed websites because design is the centre of what makes a website special. We look forward to sharing our philosophy on website design with everyone in Tanzania.”

  
You can read more about the Awwwards here(http://www.awwwards.com/about-us) and you can vote for Smartcodes by clicking VOTE herehttp://www.awwwards.com/best-websites/smart-codes



NSSF YAPIMA AFYA BURE KWA WAKAZI WA MKOA GEITA

$
0
0
Kaimu Meneja wa Mafao ya Matibabu Dk. Lucy Simbila akizungumza kabla ya Kumkaribisha Mgeni Rasmi Kaimu Mganga Mkuu Mkoa wa Geita Dk. Ndinisyu Daniel (kushoto) kufungua zoezi hilo. Wengine ni Dr. Ali Mzige (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Bw.Shaban Mpendu, Meneja wa NSSF Mkoa wa Geita na Mwisho ni Regional Aids Control Cordinator (RACC), Elisande Shumbi.
wakazi wa Geita wakiwa wamejitokeza kwa wingi kupima Afya zao.

Meneja wa NSSF GEITA, Bw. Shaban Mpendu akimsikiliza kwa makini  Dr. All MZIGE akimuelezea  mgeni rasmi kaimu mganga mkuu wa Geita   DR.Ndinsyu Daniel zoezi la upimaji sukari kwenye moja ya banda la upimaji afya.
Meneja NSSF Geita bwana Shaban Mpendu akimuongoza mgeni Rasmi Kaimu Mganga Mkuu wa Geita  DR. Ndinisyu Daniel kutembelea mabanda ya upimaji afya.

Afisa Mwandamizi  Uendeshaji   Bi.Siaeli akiandikisha wanachama wapya waliojitokeza kujiandikisha kwenye kambi ya upimaji Afya.

Mmoja ya watu waliojitolea kutoa damu kwa hiyari baada ya kupima Afya kwenye kambi hiyo ya upimaji Afya
Mmoja wa Madaktari akimpima mkazi wa Geita Urefu na Uzito ili kutambua uwiano wa urefu kwa uzito na kujua hali ya kiafya (BMI).
Shirika la Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), linaendesha  kambi za upimaji wa Afya bure kwa wakazi wa kanda ya ziwa kwa kipindi cha mwezi mmoja.

Lengo la kambi hizi ni kuweza kutoa elimu na  kuwahamasisha wanachama wa NSSF na wananchi kwa ujumla waweze kujenga  tabia ya kupima afya zao mara kwa mara na kujiwekea mfumo bora wa maisha ili kuepukana na magonjwa sugu yasiyoambukiza.



Zoezi ambalo lilianzia mkoa wa Mara na kupata mwitiko mkubwa wa wakazi wa Mara kwa kupima watu 1582 na kufuatiwa na mkoa wa Shinyanga hususani wilaya ya Kahama ambako walijitokeza watu 700 linaendelea mkoa wa Geita , kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi ya Kalangalala, kuanzia tarehe 09/06/2014,  kwa siku mbili mfululizo, kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja Jioni.  Kambi hizi zinatarajia kuishia  katika  Mkoa wa Kagera.



HUDUMA ZITAKAZOTOLEWA

Huduma mbalimbali zitatolewa  kwenye kambi hizi zikiwemo;

·         Upimaji wa Shinikizo la damu

·         Upimaji wa sukari kwenye damu- Kisukari

·         Upimaji wa hali ya lishe (Uwiano wa Urefu kwa Unene)

·         Utoaji wa dawa za Minyoo

·         Ushauri wa kitaalam kwa watakaokutwa na Matatizo

·         Ushauri nasaha  na upimaji hiari wa VVU (UKIMWI)

·         Kutoa vipeperushi vya Maelezo ya uboreshaji wa Afya.


Huduma  zote hizi zitatolewa na NSSF, BURE.


Pia kulikuwa na zoezi la uchangiaji wa damu kwa hiyari kwenye Benki ya Damu ya Mkoa ambapo Uniti za Ujazo 50 Ziliweza kukusanywa.



NSSF inaendelea kuwasii na kuwahimiza wakazi wa kanda ya ziwa kuwa waendelee kujiandikisha kwenye NSSF HIARI Scheme. NSSF HIARI Scheme ni kwa ajili ya wajasiriamali wadogo, wachimbaji wadogo, Ushirika wa Bodaboda , Ushirika wa Wakulima pamoja na wanachama wa Mifuko mingine ya hifadhi ya jamii.



Jiunge na NSSF HIARI Scheme ili uweze kujipatia mafao bora ya NSSF yakiwemo Bima ya Afya BURE kwa familia nzima (SHIB), mikopo nafuu ya SACCOS,  pamoja na Mafao bora mengineyo.



Wananchi wa kanda ya ziwa wanakumbushwa na kuhimizwa kujitokeza kwa wingi ili kupimwa na kupewa ushauri wa afya zao Bure.


NSSF INAJENGA MAISHA YAKO YA SASA NA YA BAADAE.

VIKUNDI 6 VYAKABIDHIWA MASHINE ZA KUKAMUA ASALI

$
0
0
 Katibu wa  Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Kanda ya Kitapilimwa (MJUMIKK), Samson Fuko akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi Jesca Msambatavangu wakati wa hafla ya kukabidhiana mashine za kukamua asali na mizinga ya nyuki pamoja na mavazi maalum ya uvunaji asali   iliyofanyika katika kijiji cha Kinywang'anga hivi karibuni.
 Mgeni rasmi Jesca Msambatavangu mwenye kashda ya Tanzania shingoni akiwa na baadhi wa wavunaji wa asali kabla ya kwenda kuvuna asali na baadaye katika hafla ya kukabidhiana mashine za kukamua asali na mizinga ya nyuki pamoja na mavazi maalum ya uvunaji asali iliyofanyika katika kijiji cha Kinywang'anga hivi karibuni.

 Mgeni rasmi Jesca Msambatavangu na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa akikabidhi mmoja wa wenyeviti wa vikundi mashine ya kukamua asali hafla ya kukabidhiana mashine za kukamua asali na mizinga ya nyuki pamoja na mavazi maalum ya uvunaji asali.
 Afisa misitu mstaafu Teresphory Kahatano akitoa maelekezo kwa walinaji wa asali kabla ya kwenda katika mizinga ya nyuki.
 Baadhi ya mashine za kukamua asali na mavazi rasmi yaliyokabidhiwa kwa vikundi 6 vya ujasiliamali.

Mgeni rasmi Jesca Msambatavangu na mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa akikabidhi mmoja wa wenyeviti wa vikundi moja ya mizinga iliyotolewa na TaFF kwa kushirikiana na MJIMUKK. (Picha zote na Denis Mlowe)


Na Denis Mlowe,Ismani


MFUKO wa Hifadhi ya Misitu Tanzania (TaFF) kwa kushirikiana na Mtandao wa Jamii wa Usimamizi wa Misitu Kanda ya Kitapilimwa (MJUMIKK) umewakabidhi mashine sita  za kukamua asali na mizinga ishirini kwa  vikundi vya ujasiriamali vinavyojishughulisha na ulinaji wa asali katika kata za Kitapilimwa na Kiwele katika jimbo la Ismani mkoani Iringa


Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika kijiji cha Kinywang’anga hivi karibuni, katibu wa mtandano wa MJUMIKK, Samson Fuko alisema lengo la msaada huo ni kuleta ufanisi wa kulinda, kutunza na kutumia kwa njia endelevu rasilimali za misitu na kuongeza kipato cha mwananchi mjasiriamali.


Alisema mashine hizo zitakuwa shamba darasa la ufugaji wa nyuki na upandaji miti utakaotumika kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanachama wake na kutoa elimu kwa jamii juu ya uhifadhi wa mazingira.


Fuko alisema mtandao huo umefanikiwa kuongeza idadi ya wanachama kutoka 50 waliokuwa mwanzao hadi wanachama 200 walioko sasa ambao unajihusisha na ufugaji wa nyuki unaotekelezwa katika vijiji sita kati ya vijiji 11.

 Alivitaja vikundi vilifaidika na msaada huo kuwa ni Kinywang’anga, Faraja group, Twiga group, Mshikamano. Jitegemee na kikundi cha Umoja vyote vikipatiwa  mizinga mashine na za kukamulia asali pamoja na mavazi maalumu ya kuvaa wakati wa kulina asali vyote vikiwa na thamani ya sh. milioni 4.5

Aidha aliwataka wadau kuvisaidia vikundi vya ufugaji nyuki mizinga ya nyuki na mbegu za miti kwa lengo la kuanzisha shamba darasa la ufugaji wa nyuki na shamba darasa la upandaji miti na mavazi ya kuvunia asali kwa vikundi hivyo.


Kwa upande wake mgeni rasmi Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu aliyekuwa mgeni rasmi katika makabidhiano ya mashine hizo amewaasa wazazi na walezi kuwahamasisha vijana kujiunga katika shughuli za maendeleo  wasiwaache  wakilegalega kwani vijana hao ndio nguvu kazi ya taifa.


 Alisema maendeleo ya mtu hayaletwi kwa kukaa bila kujishughulisha na kukaa vijiweni na kuwataka wajasiliamali hao kutumia  fursa waliyoipata kuitumia katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla.
 Aidha Msambatavangu aliwahidi wafugaji nyuki kuwatafutia soko la bidhaa zao kuweza kuwafikia watu wengi zaidi katika jamii ya mkoa wa Iringa na nje ya nchi.

Msambataangu ambae pia ni mlezi wa vikundi hvyo amewaeleza  wananchi kuwa kiongozi bora ni yule anaetekeleza majukumu  aliyopewa na wananchi na sio kuwadharau wale waliompa dhamana ya kuwa kiongozi

 Msambatavangu  amewataka viongozi wote waliopewa dhamana na wananchi kuwatumikia na kuwatatulia matatizo yao mda wowote wanapowahitaji na kuwajibika  sio kukaa na kutoa lawama

Aidha amempongeza   Mkurugenzi wa Halmashauri  ya wilaya ya Iringa  Pudensiana  Kisaka kwa kazi anayofanya  ikiwa  ni moja  ya utekelezaji wa majukukumu aliyopewa na serikali  na amesema kuwa kiongozi huyo anapaswa kuigwa na viongozi wa halimashauri nyingine kwani amekuwa akisikiliza matatizo ya wananchi katika halimashauri  yake na kuyafanyia  kazi.


TBL YATOA SOMO LA UKULIMA BORA WA ZAO LA SHAYIRI MKOANI ARUSHA

$
0
0
 Joel Msechu mtaalamu wa zao la shayiri kutoka Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) akiwaonesha wakulima magonjwa wa shayiri na namna ya kuzuia magonjwa hayo katika katika mashamba yaliyopo Kijiji cha Emairete Monduli juu, mkoani Arusha. Wakulima hao huwezeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika uzalishaji wa zao hilo ambalo ni malighafi ya kutengenezea bia zinzozalishwa na kampuni hiyo.
 Meneja wa Zao la Shayiri Dk. Bennie Basson akiwaonesha wakulima kijitabu cha muongozo wa kilimo cha shayiri katika Kijiji cha Emairete Monduli juu, mkoani Arusha juzi. Wakulima hao huwezeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika uzalishaji wa zao hilo ambalo ni malighafi ya kutengenezea bia zinzozalishwa na kampuni hiyo.

 Meneja wa Shayiri wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) D.. Bennie Basson akizungumza na wakulima wa shayiri ktk kijiji cha Emairete Monduli juu, mkoani Arusha. Wakulima hao huwezeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika uzalishaji wa zao hilo ambalo ni malighafi ya kutengenezea bia zinazozalishwa na kampuni hiyo.
 Meneja wa Zao la Shayiri Dk. Bennie Basson akiwaonesha wakulima wa shayiri chati ya matumizi ya mbolea na viuatilifu vinavyoweza kuongeza mavuno ya shayiri katika Kijiji cha Emairete Monduli juu, mkoani Arusha. Wakulima hao huwezeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika uzalishaji wa zao hilo ambalo ni malighafi ya kutengenezea bia zinazozalishwa na kampuni hiyo.
 Mtafiti wa zao la shayiri Geremia Mremi kutoka Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) akitoa elimu juu ya mbegu bora zilizothibitishwa kutoka TBL alipowatembelea wakulima wa zao hilo katika Kijiji cha Emairete Monduli juu, mkoani Arusha juzi. Wakulima hao huwezeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika uzalishaji wa zao hilo ambalo ni malighafi ya kutengenezea bia zinazozalishwa na kampuni hiyo.

 Meneja wa Zao la Shayiri Dk. Bennie Basson, akiwaonesha magugu ambayo ni hatari kwa zao la shayiri  alipowatembelea wakulima wa zao hilo Kijiji cha Emairete Monduli juu, mkoani Arusha juzi. Wakulima hao huwezeshwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) katika uzalishaji wa zao hilo ambalo ni malighafi ya kutengenezea bia zinazozalishwa na kampuni hiyo.

Washauri kuundwa sheria kusimamia utekelezaji wa bajeti

$
0
0
Mmoja wa washiriki wa mjadala wa wazi akichangia mada. Mmoja wa washiriki wa mjadala wa wazi akichangia mada.Mmoja wa washiriki akichangia mada kwenye mjadala wa wazi. Mmoja wa washiriki akichangia mada kwenye mjadala wa wazi.Baadhi ya washiriki wa mjadala kutoka asasi anuai wakifuatilia mada. Baadhi ya washiriki wa mjadala kutoka asasi anuai wakifuatilia madaBaadhi ya washiriki wa mjadala kutoka asasi anuai wakifuatilia mada. Baadhi ya washiriki wa mjadala kutoka asasi anuai wakifuatilia mada..Washiriki wa mjadala. Washiriki wa mjadala.Mwakilishi wa asasi ya Network for Vulnerables Rescue Foundation (NVRF), Ezekiel William akichangia hoja. Mwakilishi wa asasi ya Network for Vulnerables Rescue Foundation (NVRF), Ezekiel William akichangia hoja.[/caption] BAADHI ya wanaharakati wamevitaka vyombo vinavyotunga sheria nchini kwa pamoja kwa kushirikiana na wanaharakati kuhakikisha wanashinikiza kutungwa kwa sheria itakayo simamia bajeti za kila mwaka na pale ambapo Serikali na idara fulani zinaonekana kukwamisha utekelezaji sheria ichukue mkondo wake. 

Kauli hiyo ilitolewa juzi jijini Dar es Salaam na baadhi ya wawakilishi kutoka asasi anuai za kiraia ambao walishiriki katika mjadala wa wazi wa kudai uwajibikaji kwa watunga sera kwa kuzingatia mgawanyo wa rasilimali kijinsia ulioandaliwa na TGNP Mtandao. Akizungumza katika majadiliano mwakilishi wa wa asasi ya Network for Vulnerables Rescue Foundation (NVRF), Ezekiel William alisema anakerwa na kitendo cha serikali kupanga bajeti kila mwaka lakini asilimia kubwa ya fedha za bajeti hasa zile za maendeleo hazipelekwi katika wizara na idara kama ilivyopangwa.

 “…Mimi ni miongoni mwa watu wanaokerwa na kitendo cha Serikali kupanga bajeti na bunge kuidhinisha lakini baadaye unasikia idara na wizara zikilalamika kuwa asilimia 45 ya bajeti ya bajeti zao haikupelekwa hivyo haikutekelezwa hadi muda unaisha…mwaka mwingine inatengwa nyingine na mambo ni yaleyale,” alisema William. “...Kuna haja ya kutungwa sheria ya kusimamia bajeti, yaani endapo bajeti haijatekelezwa sheria ichukuwe mkondo wake…washtakiwe wale waliokwamisha utekelezaji wa bajeti hiyo hii itakuwa ni fundisho na itachochea maendeleo,” alisisitiza William. 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa SIKIKA, Irenei Kiria akiwasilisha mada juu ya huduma zinazotolewa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na changamoto zake, alisema bado sekta hiyo inachangamoto nyingi kwani uhaha wa vitendea kazi wataalamu katika maeneo mbalimbali ya wizara ni takribani asilimia 50 licha ya bajeti ndogo inayopangwa kila mwaka. 

Naye Ofisa Miradi wa Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA), Bi. Asha Komba akiwasilisha mada yake juu ya rushwa ya ngono nchini‘Sextortion’ alisema matokeo ya rushwa hiyo yamekuwa na madhara makubwa kiutendaji jambo ambalo alishauri asasi mbalimbali kuungana kukabiliana nayo kwa kuhamasisha utoaji taarifa. Alisema rushwa ya ngono imekwamisha utendaji kazi na usimamizi maeneo mbalimbali ndani ya Serikali na nje katika asasi na taasisi anuai jambo ambalo linakwamisha maendeleo nchini na unyanyasaji wa kijinsia. 

Aidha alisema kuongezeka kwa rushwa za ngono zimeongeza migogoro katika familia na kuathiri maendeleo ya elimu katika ngazi zote za elimu, pia alitolea mfano kwamba kuongezeka kwa idadi ya wasichana wanaofeli kunachangiwa na rushwa za ngono. “…Rushwa za ngono zimeongeza mimba utotoni, zimechangia kushuka kwa viwango vya elimu na sasa ni kikwazo katika elimu ya vyuo,” alisema Bi. Komba. 

Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu Mallya ambaye aliongoza mjadala huo ulioshirikisha asasi anuai kutoka Dar es Salaam na mikoa ya jirani ikiwemo Pwani na Morogoro, aliwataka washiriki kuhakikisha wanaunganisha nguvu zao na kupaza sauti kusimamia hoja za msingi wanazo ziibua kwa manufaa ya jamii kwa kuzingatia makundi yote. *Imeandaliwa na www.thehabari.com

WANAFUNZI WAGONJWA WAPELEKWA HOSPITALI KUWA KUTUMIA TOLORI KATAVI

$
0
0
??????????????????????????????? 
Mmoja wa walimu katika shule ya sekondari karema akipokea msaada wa vifaa vya umeme kutoka kwa mbunge wa jimbo la mpanda Vijijini Moshi Kakoso ili visaidie katika kuwapatia mwanga na kuongeza wigo wa kujisomea wakati wa usiku na huduma nyingine za kijamii shuleni hapo.
……………………………………………………………………
Na Kibada Kibada –Katavi. 

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Karema Wilayani Mpanda  Mwambao wa ziwa Tanganyika   Mkoa wa Katavi  wanakabiliwa na changamoto ya usafiri shuleni hapo hali inayowafanya wakiugua ghafla usiku kupelekwa hospitali   kwa kulaza  godoro  juu ya tolori    na  kupelekwa  Hospitali ili kupatiwa  matibabu.

 Hayo yamebainishwa na walimu katika shule hiyo wakati wakiwasilisha chanagamoto zao na  kilio chao kwa Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini Moshi Kakoso aliyefanya ziara ya kutembelea shule hiyo ili  kukagua  shughuli za maendeleo pamoja na kupokea baadhi ya changamoto zinazo wakabili na kuzipatia ufumbuzi .

 Awali Mkuu wa shule Osward Kalula alitoa taarifa ya shule kuhusu maendeleo yaliyopo na changamoto zinazowakabiri  katika eneo lao kwenye taasisi hiyo na kueleza kuwa baadhi yake ni  ukosefu wa umeme, maji, vitabu,  na usafiri, ambapo changamoto ya umeme iliyopatiwa ufumbuzi hapo hapo na mbunge  kwa kukabidhi nyaya za umeme zenye mita miambili ili kusambazwa umeme katika nyumba za walimu na mabweni, na  madarasani kwa kutumia jenerata ndogo ya shule iliyopo shuleni hapo.

Mbali ya kutoa nyaya hizo na vifaa vingine  vinavyohusiana na umeme ili vifungwe na umeme uanze kufanya kazi na  kuondoa kero ya ukosefu wa umeme pia Mkuu wa shule alipata nafasi ya kushukuru kwa msaada huo ulotolewa na mbunge kwa kuonesha jinsi anavyowajali wananchi wake na kujali elimukatika jimbo lake,pia  akawapa nafasi walimu kutoa changamoto nyingine zilizopo katika shule hiyo kwa mwakilishi wao mbunge Kakoso.

Mmoja wa walimu katika shule hiyo Donatha Chamoto alieleza kuwa kwa kutolea mifano kuwa mwanafunzi mmoja aliugua usiku ikalazimika kubwebwa kwenye tololi kupelekwa hospitali usiku hali ambayo ni hatari kwa kuwa eneo shule ilipo na kituo cha Afya kilipo ni mbali kidogo.

Kutokana na tatizo hilo wanaomba kupatiwa usafiri japo hata bajaji itakayosaidia hata kuwa wanawapeleka hospitali pindi linapotokea tatizo la kuugua ghafla usiku kwa kuwa huwezi kujua lolote lawaza kutokea na hali ya hapo jinsi ilivyo ni tatizo kubwa walieleza.
  Naye Diwani Kata ya Karema Maiko Kapata akashauri kuwa iwapo usafiri wa gari ukikosekana wanaomba wapatiwe japo pikipiki za miguu mitatu ili iwe inasaidia iwapo litajitokeza tatizo kama hilo kuliko kuacha kama ilivyo sasa.

Akaongeza kuwa kwa kuwa sasa shule imepewa hadi ya kuwa na kidato cha tano na sita ni vyema serikali iakaangaliza namna gani ya kusaidia hata usafiri wa gari ili shughuli za kiutendaji ziweze kwenda vizuri kwani kutakuwa namajukumu ya kufuatilia makao makuu ya wilaya na pengine mkoani na upo umbali mkubwa  zaidi ya kilometa 100 hadi kufika mpanda kutokea Karema ni mbali bila kuwa na usafiri wa uhakika inakuwa tatizo kwa kusubiria magari ya kudadia ni vyema Shule ikawa na usafiri wake wenye uhakika kulingana na majukumu yatakayokuwa yapo shuleni hapo.


Kwa upande Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini Moshi Kakoso alishauri waangalie namna ya kuweza kupatiwa usafiri kwa kutumia mfuko wa jimbo wakae katika vikao waone namna ya kutumia fedha hizo

MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAZAZI ABDALLAH BULEMBO AWAAPISHA WANACHAMA 367 WAPYA WA CCM WILAYA YA NYASA MKOANI RUVUMA

$
0
0
 Mwenyekiti  wa Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha mapinduzi CCM (Taifa) Bw. Abdallah  Bulembo akiwaapisha wanachama wapya wa  CCM.
Wananchama wapya wa CCM wakiwa wamenyoosha kadi za Chama Cha Mapinduzi juu wakati wakiapa.
Mwenyekiti  wa Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha mapinduzi CCM (Taifa) Bw. Abdallah  Bulembo akizungumza katika mkutano wa hadhara baada ya kuwaapisha wanachama wapya kijiji cha KINGIRIKITI kata ya LUMEME wilayani NYASA .
 Mwenyekiti  wa Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha mapinduzi CCM (Taifa) Bw. Abdallah  Bulembo aliyevaa taji shingoni akicheza ngoma ya asili katika kijiji cha Kingirikiti Wilaya ya Nyasa wakati wa Ziara yake 

 Kikundi cha akina mama  kikitoa burudani

 Mwenyekiti  wa Jumuiya ya wazazi ya Chama Cha mapinduzi CCM (Taifa) Bw. Abdallah  Bulembo akitoa kadi kwa mwanachama mpya wa CCM kata ya LUMEME kijiji cha KINGIRIKITI wilaya ya Nyasa, kwa wanachama 367 waliojiunga na chama hicho cha CCM.Picha na kikosi cha Demashonews

Rais Kikwete azindua Chapisho la Tatu la Taarifa za Sensa

$
0
0
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi chapisho la tatu la taarifa za msingi za kidemografia,kijamii na kiuchumi pamoja na tovuti katika kupata taarifa za Sensa na Makazi katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwl.Julius Nyerere jijini Dar es Salaam leo.

Viongozi wengine walioshiriki katika hafla ya uzinduzi huo kutoka kushoto ni Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi, Bibi Mariam Khan Mwakilishi wa UNFPA,Waziri Mkuu Mizengo Pinda,Waziri wa Fedha Bi.Saada Mkuya na kulia ni Kamishna wa Sensa na Makazi Hajjat Amina Mrisho Said.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia wageni waliohudhuria hafla ya uzinduzi  wa Chapisho la tatu la taarifa za msingi za kidemografia,kijamii na kiuchumi pamoja na tovuti itakayowezesha kupatikana kwa taarifa mbalimbali za sensa ya watu na Makazi katika hafla iliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es salaam 

Benki ya Exim kupiga jeki huduma za afya ya uzazi na mtoto

$
0
0
 Baadhi ya kina mama nje ya hospitali ya Bombo mkoani Tanga wakiwa na miamvuli waliyosaidiwa na Benki ya Exim Tanzania ikiwa ni sehemu ya mpango wa Benki hiyo wa kugawa miamvuli bure kwa kina mama wazazi katika kuunga mkono jitihada za serikali kuboresha afya nchini. Benki ya Exim imejikita katika mpango huo ili kuwasaidia kina mama kujikinga na adha ya jua kali na mvua pale wanapohudhuria kliniki na watoto wao. 
Afisa Masoko wa Benki ya Exim Fatma Kilinda (mwenye fulana nyeupe) akigawa miamvuli kwa kina mama nje ya hospitali ya Bombo mkoani Tanga iliyotolewa na Benki hiyo ikiwa ni sehemu ya mpango wa Benki hiyo wa kugawa miamvuli bure kwa kina mama wazazi katika kuunga mkono jitihada za serikali kuboresha afya nchini. Benki ya Exim imejikita katika mpango huo ili kuwasaidia kina mama kujikinga na adha ya jua kali na mvua pale wanapohudhuria kliniki na watoto wao.

============   =======  ==========
Benki ya Exim kupiga jeki huduma za afya ya uzazi na mtoto


Na Mwandishi Wetu, Tanga

KATIKA jitihada za kusaidia mpango wa serikali wa kuboresha afya ya uzazi na mtoto nchini Tanzania, Benki ya Exim Tanzania imebainisha kuendelea kutoa misaada katika sekta hiyo kwenye maeneo ambayo yanaonekana kutoingia kwenye mpango wa uboreshaji wa sekta hiyo ya afya ya uzazi na mtoto.


Benki hiyo ikiwa inaamini katika kauli mbiu yake kuwa "Ugunduzi ni maisha",  imejikita katika mpango wa kusambaza miavuli bure kwa akina mama wanaohudhuria kliniki katika hospitali mbalimbali ya nchini.


Akizungumza muda mfupi baada ya kutoa miavuli kadhaa kwa kina mama mbali mbali nje ya hospitali ya Bombo katika mkoani Tanga, Meneja wa Benki ya Exim Tawi la Tanga, Bw. Deogratius Makwaia alisema kuwa benki ya Exim imeamua kuelekeza sehemu ya fedha zake zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za kijamii kununua miavuli kwa kina mama na watoto wao ambao baadhi yao hawana uwezo wa kununua miamvuli hiyo.

"Ni kweli kwamba Serikali, mashirika ya maendeleo na wadau wengine wanapiga jeki sekta ya afya ya uzazi na mtoto ikiwa ni eneo lenye kipaumbele katika sekta ya afya. Hata hivyo, wakati wa kupanga, tuligundua kwamba fedha nyingi uelekezwa kwenye ujenzi wa vituo vya afya, kununua vifaa na dawa, lakini kusahau kusaidia vitu vingine muhimu  ambavyo mama na mtoto uvihitaji baada ya kuondoka katika kituo cha afya.


"Baada ya utafiti wetu katika hospitali kadhaa nchini kote, tuligundua kwamba akina mama wengi wanaohudhuria kliniki za wajawazito ukumbana na wakati mgumu pindi mvua zinaponyesha au wakikumbana na jua kali wakitokea sehemu mbali kuhudhuria kiliniki na watoto wao.


"Ukosefu wa makazi kwa akina mama hawa na watoto wao, inaweza kuwa ndiyo sababu inayochangia kwa baadhi yao hasa katika maeneo ya vijijini – kutohudhuria huduma za kiafya mara kwa mara ambayo utolewa bure.

"Mpango wa Benki ya Exim wa kutoa miamvuli kwa kina mama na watoto, umeanzishwa ili kusaidia wale kina mama ambao hawana uwezo wa kumudu gharama za miamvuli kujikinga dhidi ya mvua na jua kali ambalo linaweza kuwa na madhara kwa afya zao," alisema Makwaia.

Aidha, alisema kuwa Benki ya Exim itaendelea kuiunga mkono serikali katika utekelezaji wa miradi mingine ya maendeleo nchini.


"Utamaduni wa kurejesha sehemu ya pato letu kwa jamii umekuwa ni kipaumbele chetu kikubwa. Hilo linatokana na Benki ya Exim kuendelea kukua na kwa mwaka jana ilipata faida ya shilingi bilioni 20. Nina hakika kwamba uongozi wetu umekuwa ukifanya bidii za kutosha kurejesha pato hili kwa jamii kama njia ya kuboresha hali ya maisha ya wananchi pale ambapo Benki inafanya shughuli zake, kama vile kusaidia ukuaji wa kiuchumi," aliongeza Makwaia.


Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images