Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46396 articles
Browse latest View live

SIJARIDHISHWA NA UTENDAJI WA OFISI YA MKURUGENZI KONDOA-DKT. KIJAJI

$
0
0
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza na wananchi wa wa Kijiji cha Kalamba wilayani Kondoa, ambapo wananchi hao walimuomba awahimize Watendaji wake ili jengo la Kituo cha Afya Kalamba likamilike na kuanza kutoa huduma kwa Wanakijiji hao. 
Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Kalamba wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani), alipokuwa akitoa maelekezo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa Bw. Mashauri Vicent (hayupo pichani) kuhusu umaliziaji wa Kituo cha Afya cha Kalamba ambacho kitakuwa kikihudumia zaidi ya Wanakijiji 13,000 wa Kalamba na Haubi.
Dkt. Alpha Kwilasa wa Kituo cha Afya cha Busi akimueleza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji huduma zinazotolewa katika kituo hicho cha afya wilayani Kondoa.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akikagua chumba cha kuhifadhia maiti alipotembelea miradi ya Ujenzi wa Vituo cha Afya Wilayani humo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akikagua chumba cha kuhifadhia maiti alipotembelea miradi ya Ujenzi wa Vituo cha Afya Wilayani humo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akitoa maagizo kwa uongozi wa kijiji hukakikisha wanafuatilia kila hatua ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa katika vijiji vyao ili viweze kumalizika kwa wakati alipotembelea wilayani humo.



Na Josephine Majura, Kondoa


Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametoa muda wa siku 37 kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa kuhakikisha kuwa ujenzi wa vituo vitatu vya afya vya Bereko, Thawi na Kalamba vinakamilika na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.

Dkt. Kijaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini, ametoa maagizo hayo alipofanya ziara ya kutembelea mradi ya ujenzi wa vituo vya afya vinavyojengwa kwa fedha za Serikali katika vijiji mbalimbali Wilayani Kondoa, mkoani Dodoma, ambapo alibaini kuna uzembe katika umaliziaji wa ujenzi wa baadhi ya vituo hivyo kikiwemo Kituo cha Afya Kalamba.

Alielezea kutoridhika na utendajikazi wa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo katika usimamizi wa miradi hiyo muhimu kwa wananchi wakati Serikali ilikwishatoa fedha zote za kukamilisha miradi hiyo na kuagiza hadi Oktoba 30 mwaka huu miradi hiyo iwe imekamilika.

“Dhamira njema ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli yakuleta milioni 400 kwenye kituo hichi cha Afya ni kupata huduma lakini hatujaanza kutoa huduma hiyo kwa zaidi ya mwaka sasa”, alisema Dkt. Kijaji. 

Aliiagiza Ofisi ya Mkoa na Wilaya hukakikisha wanafuatilia vizuri utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi inayofadhiliwa na Serikali ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati kwa sababu Serikali haianzishi mradi mpya bila kutoa fedha zote za miradi husika. 

Serikali ilitoa fedha kwa nyakati tofauti kwa ajili ya mradi wa Ujenzi wa vituo vya afya vitano wilayani Kondoa kati ya vituo hivyo, vituo viwili vya Mauno na Busi vimekamilika, huku vituo vitatu vya afya vya Bereko, Thawi na Kalamba havijakamilika. 

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Kondoa Bw. Mashauri Vicent alimuahidi Dkt. Kijaji kutekeleza magizo yote aliyoyatoa hasa ya kulipwa kwa watumishi waliofanya kazi mbalimbali kwenye vituo hivyo vya afya ndani ya siku 14. 

Naye Mwanakijiji wa Mauno Bw. Haji Selemani, ameishukuru Serikali kwa juhudi mbalimbali inayofanya katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo hasa huduma za jamii na kusifia huduma inayotolewa na Watumishi wa Kituo cha Afya Busi. 

Kwa upande wake Mwanakijiji cha Bereko Bw. Juma Saidi amempongeza Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambae pia ni Mbunge wa Kondoa Vijijini Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji kwa kazi kubwa anayoifanya jimboni huko na kumuombea afya njema ili awe na nguvu yakufanya kazi na zaidi. 

Dkt. Ashatu Kijaji alikuwa kwenye ziara ya siku mbili wilayani Kondoa, mkoani Dodoma ambapo ametembelea mradi wa Ujenzi wa vituo vitano vya afya wilayani huyo ambavyo vinajengwa kwa fedha za Serikali na kuahidi kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili Wakazi wa Wilaya ya Kondoa.

MAJALIWA AWEKA JIWE LA MSINGI LA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA GEITA NA KUFUNGUA NYUMBA ZA WATUMISHI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifungua Nyumba za Makazi za Wakuu wa Idara na Vitengo wa Secretarieti ya Mkoa wa Geita, Septemba 22, 2019. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj Said Kalidushi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri na kulia ni Mbunge wa Viti Maalum, Vicky Kamata, (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe wakati alipofungua Nyumba za Makazi za Wakuu wa Idara na Vitengo wa Secretarieti ya Mkoa wa Geita, Septemba 22, 2019. Wengine pichani kutoka kushoto ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Constantine Kanyasu, Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj Said Kalidushi, Mkuu wa mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani,Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, Mbunge wa Viti Maalum, Vicky Kamata na dulia ni Waziri wa Madini, Doto Biteko.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye pia ni Mjumbe wa kamati Kuu ya CCM, akizungumza baada ya kukagua ujenzi wa Ofisi ya CCM ya Mkoa wa Geita, Septemba 22, 2019. Wa tatu kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Geita, Alhaj Said Kalidushi, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel na wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na viongozi wa Mkoa wa Geita wakifurahia baada ya Waziri Mkuu kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita na kukagua ujenzi wa Hospitali hiyo, Septemba 22, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mkoa wa Geita baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita Septemba 22, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

WAZIRI MKUU MAJALIWA AFAFANUA UTEKELEZAJI WA MAAGIZO YA RAIS DKT. MAGUFULI KUHUSU MAPENDEKEZO YA KUPATA UFUMBUZI WA MIGOGORO YA MATUMIZI YA ARDHI NCHINI

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari juu ya utekelezaji wa Maagizo ya Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhusu Mapendekezo ya kupata ufumbuzi wa Migogoro ya Matumizi ya Ardhi Nchini,Mkutano uliofanyika Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2019.
 

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akiwa na Mawaziri nane wa Sekta zinazohusika na Matumizi ya Ardhi alipokuwa akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani) juu ya utekelezaji wa Maagizo ya Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhusu Mapendekezo ya kupata ufumbuzi wa Migogoro ya Matumizi ya Ardhi Nchini, Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2019.
 
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri nane wa Sekta zinazohusika na Matumizi ya Ardhi mara baada ya kuzungumza na Wanahabari juu ya utekelezaji wa Maagizo ya Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhusu Mapendekezo ya kupata ufumbuzi wa Migogoro ya Matumizi ya Ardhi Nchini. Mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2019.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa akizungmza na Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya pamoja ya Mawaziri nane wa Sekta zinazohusika na Matumizi ya Ardhi iliyoundwa na Mhe. Rais Dkt.John Pombe Magufuli kuhusu Mapendekezo ya kupata ufumbuzi wa Migogoro ya Matumizi ya Ardhi Nchini. Mkutano uliofanika katika Ofisi ya Waziri Mkuu Jijini Dar es salaam leo Septemba 23, 2019. Picha na Ikulu

RAIS MAGUFULI AMJULIA HALI ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU KATOLIKI LA DAR ES SALAAM MHASHAMU YUDA THADEUS RUWA’ICHI ANAYEPATIWA MATIBABU TAASISI YA MIFUPA MUHIMBILI (MOI)

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana kwa furaha na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye anapatiwa matibabu katika Taasisi hiyo ya Mifupa Muhimbili (MOI) mara baada ya kufanyiwa upasuaji wa Kichwa 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza sala ya kumuombea Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye anapatiwa matibabu katika Taasisi hiyo ya Mifupa Muhimbili (MOI)

 
Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ambaye alienda kumjulia hali katika Taasisi hiyo ya Mifupa Muhimbili (MOI). Wakwanza kulia ni Askofu Msaidizi Eusebius Nzigilwa wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, kushoto ni Padre Dkt. Alister Makubi Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es salaam 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Askofu Msaidizi Eusebius Nzigilwa wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam kulia, Padre Dkt. Alister Makubi kushoto, Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay jijini Dar es salaam wakifurahia jambo pamoja na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadeus Ruwa’ichi ambaye hali yake imezidi kuimarika mara baada ya kufanyiwa upasuaji katika taasisi hiyo ya MOI. PICHA NA IKULU.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 23 Septemba, 2019 amemjulia hali Askofu Mkuu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi anayepatiwa matibabu katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) Jijini Dar es Salaam. 

Mhe. Rais Magufuli amemkuta Baba Askofu Mkuu Ruwa’ichi akiwa anaendelea vizuri tofauti na hali ilivyokuwa alipomtembelea tarehe 10 Septemba, 2019 siku aliyoletwa MOI akitokea Hospitali ya KCMC Mkoani Kilimanjaro alikougua ghafla baada ya kupatwa na ugonjwa wa kiharusi. 

Akiwa MOI, Baba Askofu Mkuu Ruwa’ichi amefanyiwa upasuaji na timu ya Madaktari Bingwa wa ubongo na mishipa ya fahamu kwa mafanikio na sasa anaendelea vizuri. 

Mhe. Rais Magufuli ameeleza kufurahishwa kwake na kuimarika kwa hali ya Baba Askofu Mkuu Ruwa’ichi na amewapongeza Madaktari Bingwa wa MOI kwa kumtibu kwa mafanikio makubwa. 

Aidha, Mhe. Rais Magufuli, Baba Askofu Mkuu Ruwa’ichi, Baba Askofu Mkuu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mhashamu Eusebius Nzigilwa na Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro Padre Dkt. Alister Makubi wamesali sala ya pamoja ya kumshukuru Mungu kwa uponyaji na kuwaombea wagonjwa wote wapone haraka. 

Baada ya kutoka MOI, Mhe. Rais Magufuli amewajulia hali wagonjwa waliolazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) akiwemo Baba Mzazi wa Daktari wa Rais, Mzee Wilson Ngwale aliyelazwa hospitalini hapo. 

Kabla ya kutembelea wagonjwa, Mhe. Rais Magufuli amekwenda Msasani Jijini Dar es Salaam kumpa pole Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (JWTZ) Jen. Venance Salvatory Mabeyo ambaye amefiwa na mwanae Nelson Venance Mabeyo (aliyekuwa Rubani) ambaye amefariki dunia leo asubuhi baada ya ndege aliyokuwa akiiendesha kupata ajali muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja mdogo wa ndege wa Seronera Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara. 

Mapema leo asubuhi, Mhe. Rais Magufuli ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam. 


Gerson Msigwa 
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU 
Dar es Salaam 
23 Septemba, 2019

RAIS DKT. MAGUFULI AMPA POLE MKUU WA MAJESHI YA ULINZI YA WANANCHI WA TANZANIA JENERALI VENANCE MABEYO AMBAYE AMEFIWA NA MTOTO WAKE NELSON MABEYO

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha Ndugu Nelson Mabeyo mtoto wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo nyumbani kwao Msasani jijini Dar es Salaam. 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Mke wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo, Mama Mabeyo ambaye amefiwa na mtoto wake Nelson Mabeyo aliyepata ajali ya ndege Seronera Serengeti mkoani Mara.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpa pole Mke wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo, Mama Mabeyo ambaye amefiwa na mtoto wake Nelson Mabeyo aliyepata ajali ya ndege Seronera Serengeti mkoani Mara. 
 . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo msibani Msasani jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza sala pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo na familia yake wakimuombea marehemu   Nelson Mabeyo ambaye alifariki kwa ajali ya ndege Seronera Serengeti mkoani Mara.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Wananchi wa Tanzania Jenerali Venance Mabeyo msibani Msasani jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU


WAFANYAKAZI BENKI YA NMB WAFANYA USAFI NA KUKABIDHI VIFAA VYA USAFI HOSPITALI YA AMANA

$
0
0
WAFANYAKAZI wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam jana walijitolea kufanya usafi katika Hospitali ya Amana ya jijini Dar es Salaam pamoja na kukabidhi vifaa mbalimbali vya kufanyia usafi, ikiwa ni kuadhimisha siku ya usafi duniani zilizofanyika Septemba 21, 2019.

Akizungumza na wanahabari mara baada ya zoezi hilo katika Hospitali ya Amana, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Bw. Badru Idd alisema zoezi hilo ni utaratibu wa kawaida ambao NMB imejiwekea kuona ni jinsi gani inarudisha sehemu kidogo ya mapato yake katika jamii.

Alisema mbali na zoezi la kufanya usafi hospitalini hapo, wafanyakazi hao walikabidhi vifaa tofauti vya kufanyia usafi vikiwemo vifaa vya kuzolea na kuhifadhia taka, mifagio, vifaa vya kudekia, seti za vifaa vya kujikinga wakati wa kufanya usafi, buti za kufanyia usafi, makoleo maalum ya taka na dawa za usafi.

"...Leo tumekuja Hospitali ya Amana kwa ajili ya kujitolea kufanya usafi kuitikia maadhimisho ya usafi duniani, tumejipanga kufanya usafi maeneo mbalimbali ya nchi kwa kuwa tuna mtandao mpana vivyo hivyo wenzetu maeneo mbalimbali wanafanya usafi kama sisi. Na sisi kama kanda ya Dar es Salaam tumeamua kuja kufanya usafi Hospitali ya Amana."

Akifafanua zaidi alisema NMB pia imekuwa ikitumia fungu hilo katika kusaidia jamii kwenye elimu, afya pamoja na majanga pale yanapojitokeza kwa jamii yetu. "Hii yote ni kuleta ukaribu wa Benki yetu na jamii...hatuji tu kuomba biashara kwa jamii bali tunajitokeza kushiriki, na kusaidiana na jamii katika kufanya shughuli zao. Vifaa vyote tulivyokabidhi leo ni fedha zilizochangwa na wafanyakazi wetu kwa hiyari kujitolea kusaidia jamii," alisema Bw. Idd.

Aidha aliongeza kuwa NMB wakati wote imekuwa ikishirikiana na jamii katika shughuli mbalimbali, ikiwemo kutenga asilimia moja ya pato lake baada ya kuondoa gharama zote, na kwa mwaka huu imetenga zaidi ya bilioni moja kwa aajili ya shughuli za kijamii, huku hadi kufikia mwezi Julai, 2019 NMB imekwishatumia zaidi ya milioni 450 kwa shughuli kama hizo.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Bw. Badru Idd (kushoto) akitoa maelekezo kwa wafanyakazi wa benki hiyo kabla ya kuanza kufanya usafi katika Hospitali ya Amana walipojitolea. Mbali na kujitolea kufanya usafi wafanyakazi hao pia walikabidhi vifaa mbalimbali vya kufanyia usafi hospitalini hapo.
Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Bw. Badru Idd (kulia) akimkabidhi sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi Ofisa Muuguzi Kiongozi wa Hospitali ya Amana, Vicent Semkamba (kushoto) ikiwa ni msaada uliotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo walipojitolea kufanya usafi katika hospitali hiyo. Mbali na kujitolea kufanya usafi wafanyakazi hao pia walikabidhi vifaa mbalimbali vya kufanyia usafi hospitalini hapo.

Ofisa Muuguzi Kiongozi wa Hospitali ya Amana, Vicent Semkamba (kulia) akipokea sehemu ya vifaa vya kufanyia usafi kutoka kwa mmoja wa maofisa wa Benki ya NMB jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni msaada uliotolewa na wafanyakazi wa benki hiyo walipojitolea kufanya usafi katika hospitali hiyo.
Mmoja wa maofisa wa Benki ya NMB jijini Dar es Salaam akifyeka majani kwa kutumia mashine maalum Hospitali ya Amana walipojitolea kufanya usafi katika hospitali hiyo.
Sehemu ya wafanyakazi wa Benki ya NMB jijini Dar es Salaam wakifanya usafi maeneo mbalimbali ya Hospitali ya Amana leo ikiwa ni kujitoa kushiriki matendo ya kusaidia jamii.
Sehemu ya wafanyakazi wa Benki ya NMB jijini Dar es Salaam wakifanya usafi maeneo mbalimbali ya Hospitali ya Amana leo ikiwa ni kujitoa kushiriki matendo ya kusaidia jamii.
Ofisa Afya Hospitali ya Amana, Avit Maro (kulia) akiwashukuru wafanyakazi wa Benki ya NMB mara baada ya zoezi la kufanya usafi katika hospitali hiyo. Katikati ni Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Bw. Badru Idd.

BALOZI WA BURUNDI NCHINI TANZANIA AHUDHURIA TAMASHA LA JAMAFEST JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Balozi wa Burundi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Gervais Abayeho (kulia) akisalimiana na wacheza ngoma kutoka nchini Burundi waliokuja kushiriki katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Balozi wa Burundi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Gervais Abayeho (kulia) akisalimiana na wacheza ngoma kutoka nchini Burundi waliokuja kushiriki katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
 Balozi wa Burundi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Gervais Abayeho na viongozi alioambatana nao akisalimia wananchi waliofika katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Wacheza ngoma kutoka nchini Burundi wakitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Wacheza ngoma kutoka nchini Burundi wakitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Wacheza ngoma kutoka nchini Burundi wakitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Balozi wa Burundi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Gervais Abayeho (kulia) akiwa pamoja na wacheza ngoma kutoka nchini Burundi waliokuja kushiriki katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Biashara ya kakakuona yashika kasi nchi za Asia

$
0
0

Na BAKARI KIMWANGA-ALIYEKUWA THAILAND

TAASISI mbalimbali za kimataifa zimekuwa na mkakati madhubuti wa kulinda rasilimali hasa wanyama akiwamo kakakuona ambaye kwa sasa yupo hatarini kutoweka.

Hali hiyo inachangiwa kwa kiasi kikubwa na usafirishaji haramu wa wanyamapori kutokana nchi za Afrika hasa zile za Afrika Magharibi zikiwamo Ghana na Nigeria, na kwa upande wa Afrika Mashariki Kenya ikitajwa kama sehemu ya uchochoro wa ukusanyaji wa wanyama hao na kuwasafirisha kwenda nchi za Asia.

Timu ya wanahabari watano kutoka nchini ilitembela nchini Thailand na kuzunguka kwenye maeneo mbalimbali ikiwamo sehemu maalumu za wanyama waliokamatwa kutoka nchi za Afrika, Idara ya Forodha Uwanja wa Ndege wa Suvarnabhumi na soko la bidhaa ya wanyamapori.

Wanahabri hao waliungana na wenzao wa nchini Thailand, ambapo kila upande uliweza kutembelea kwenye nchi za wenzake kwa lengo la kubadilishana uzoefu na taarifa kuhusu usafirishaji haramu wa wanyamapori, chini ya ufadhili wa USAID Protect Tanzania na USAID Wildlife Asia, kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET).

Kutokana na hali hiyo, nchi ya Ghana imelazimika kuingia katika mkakati wa kuangalia upya sheria zake za wanyamapori kutokana na biashara ya kakakuona ambayo imekithiri kwa kasi kubwa.

Hali hii imesababishwa na hofu ya kwamba nchi hiyo inatumiwa kuendesha biashara haramu.Zaidi ya kilo 31,000 ya magamba ya kakakuona ilikamatwa duniani kote mwaka huu, hali hiyo inabainishwa na ripoti ya Shirika la Kimataifa la Ustawi wa Wanyama (IFAW).

Katika kipindi cha Mei na Juni mwaka huu, shehena mbili kubwa zilinaswa nchini Malaysia, ambapo pia kilo 700 zilipatikana zikiwa zimesafirishwa kupitia Ghana. Huku shehena nyingine kubwa zikikamatwa pia nchini Uganda, Cameron na Ivory Coast.

Mmoja wa maofisa wa juu wa IFAW, Mark Hofberg, anasema magamba mengi kutoka kwa mnyama huyo Afrika yameuzwa ili kufikia mahitaji yake katika Bara la Asia, ambako hutumiwa katika dawa za jadi.

Kakakuona anapatikana zaidi katika nchi za Afrika na Kusini Mashariki mwa Asia.Aina mbili kati ya nane ya mnyama huyo wameorodheshwa kuwa hatarini, wakiwekwa katika orodha nyekundu ya aina ya wanyama walio hatarini.

“Kuongezeka kwa kamatakamata ya mizigo hiyo kunaweza kuwa ishara kwamba mamlaka husika zinalichukulia suala hili kwa uzito, lakini nchi nyingi hazina sheria kali za kuadhibu wafanyabiashara haramu.

“Kwa biashara hii kupungua kwa kiasi kikubwa, kunahitajika adhabu na hukumu kali,” anasema Hofberg.Kakakuona ni mnyama aliyehifadhiwa nchini Ghana, ambapo Mwenyekiti wa Tume ya Wanyamapori wa Ghana, Nana Kofi Adu-Nsiah, anasema sheria kali inahitajika.

Sheria zilizopo za ulinzi wa wanyamapori zilipitishwa katika miaka ya 1960 na tume hiyo inataka ziangaliwe upya ili kufikia viwango vya kimataifa.Kutokana na ujangili huo mpya ambao sasa unashika kasi, watu watatu walikamatwa nchini Ghana kuhusiana na mizigo iliyonaswa Juni, mwaka huu, nchini Malaysia.

Viongozi wa Serikali wanaamini sheria mpya zitazuia nchi za Afrika Magharibi kutumiwa kuwa hatua ya usafiri kwa wanyama hao wanaosafirishwa lakini pia kuna wasiwasi pia juu ya uwindaji wa ndani wa kakakuona.

Wanyama hao ambao wana ukubwa wa sentimita 30 hadi 100 wanaweza kuuzwa kwa karibu dola za Marekani 45 au Euro 38. Na wale wanaowauza kwa kawaida huwa ni watu masikini.



UTAFITI

Watafiti wamegundua kuwa kakakuona anatumika kwa ajili ya chakula na magamba yake yanatumiwa kama viungo.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na USAID Wildlife Asia, uliainisha sababu za kuwapo kwa biashara haramu ya bidhaa za wanyamapori kama tembo, faru, kakakuona na tiger kunatokana na imani na tamaduni zao hasa kwa raia wa nchi za Thailand, China na Vietnam, ambapo pia inaelezwa kuwa asilimia 20 ya tembo wa Afrika wanadaiwa kuuawa na sehemu ya viungo vyao (pembe) husafirishwa kwa njia ya zisizo halali na kuingia kwenye nchi hizo.

“Mtu anatoa zawadi iliyotengenezwa kwa mazao ya wanyamapori kwa familia, marafiki, masuala ya kijamii na mitandao ya kibiashara kwa mazao ya wanyama wote wanne,” anaeleza mtaalamu wa mawasiliano na kubadilisha tabia wa USAID Wildlife Asia, Wenweena Tangsathianraphap.

Naye mfuatiliaji na mtaalamu wa uthamini na ufuatiliaji USAID Wildlife Asia, Pakprim Oranop, anaweka wazi suala hili na kusema kwamba bara hilo mtu kuvaa kidani au kitu chochote kilichotengenezwa kwa kiungo chochote cha mnyama ni ishara kwamba naye atakuwa jasiri kama mnyama aliyetokana na bidhaa hiyo au anajihakikishia ulinzi.

Hata hivyo, pia wapo wenye imani kwamba inaongeza nguvu za kiume au uwezo wa mwanamume kutambulika kuwa rijali, na wengine wakitumia kama dawa ya kuwafanya kuwa imara kama mnyama husika.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na USAID Wildlife Asia, ya kwanini watu wanatumia bidhaa za wanyamapori, walibaini kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya imani na utamaduni kwa wanaotumia bidhaa za wanyamapori.

“Wengi waliamini kuwa anapotumia kitu chochote kilichotengenezwa kwa jino la tembo, pembe ya faru au tiger (chui) basi naye atakuwa na matendo ya kishujaa kama huyo mnyama, ndiyo maana wengi wameendelea kutumia,” anaeleza.

Katika utafiti wa walaji wa mwaka 2018, kati ya watu 10 waliohojiwa ambao ni wanunuaji na watumiaji kwa miezi 12 iliyopita, ulibainisha kuwa nchini China watumiaji wa bidhaa za tembo asilimia 4.01 ni vya tofauti, asilimia 3.86 waliamini katika imani za kiroho na asilimia 3.79 waliamini katika urembo.

Kwa upande wa kakakuona, asilimia 4.14 waliamini inaponya maradhi mbalimbali, 3.72 inaleta afya njema na maisha mazuri na asilimia 2.74 inaongeza nguvu za kiume.



HALI ILIVYO THAILAND

Asilimia 94 ya waliohojiwa nchin Thailand, wanasema wanatumia bidhaa za meno ya tembo kwa kuwa ni kitu cha tofauti na thamani kubwa, asilimia 88 wanasema inaleta matumaini na bahati, wakati asilimia 79 wanasema inawalinda dhidi ya adui na majanga.

Kutokana na hali hiyo, Mwakilishi wa Shirika la Kudhibiti Usafirishaji wa Wanyamapori Asia (Traffic), Monica Zavagli, anasema biashara ya mazao ya wanyamapori inahusisha watu wenye mtandao mkubwa na wenye fedha nyingi ambazo huzitumia kununua nyara hizo.

“Hii biashara ni kubwa ambayo inatumia zaidi ya Dola za Marekani bilioni tisa hadi 30 kwa mwaka, mtandao huu unatumia taasisi za kifedha kuhamisha fedha na benki zina uwezo wa kuchunguza kwamba fedha hizo zinatokana na nini kama zinahusisha ujangili,” anasema.

“Hata hivyo, nchi kama Tanzania imefanya vizuri kuwa na sheria kali, lakini jitihada zaidi zinahitajika katika kushirikisha taasisi za fedha, kwa kufuatilia mali na mienendo yao kama fedha hizo zinahusisha biashara hiyo itasaidia kumaliza mtandao huo,” anasema Monica.

Mkuu wa USAID Asia, Craig Karkpatrick, anasema ripoti ya polisi wa kimataifa imeonyesha kuwa biashara haramu ya mazao ya wanyamapori ipo na inafanyika kwa kiasi kikubwa.



HALI ILIVYO TANZANIA

Kwa mujibu wa ripoti ya hali ya uchumi kwa Taifa ya mwaka 2017, inaonesha kwamba sekta ndogo ya wanyamapori ilikusanya zaidi ya Sh milioni 29 ikilinganishwa na zaidi ya Sh milioni 38 mwaka 2016, sawa na upungufu wa asilimia 22.7.

Kati ya mapato hayo, mapato kwa sarafu ya ndani yalikuwa Sh 2,904,631,101.82 na sarafu ya nje yalikuwa ni Dola za Marekani 11,940,029.80 ikilinganishwa na Sh 242,843,673,275 na Dola za Marekani 17,473,260 mwaka 2016.

Kwa mujibu wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamis Kingwangalla, Serikali inaendelea na jitihada za kulinda rasilimali za wanyamapori dhidi ya ujangili na uvunaji usio endelevu.

Katika kipindi hicho, anasema kulikuwa na siku za doria 262,770 zilizofanyika katika maeneo ya wazi na yaliyohifadhiwa ikilinganishwa na siku za doria 518,809 zilizofanyika mwaka 2016.



NYARA ZILIZOKAMATWA

Kutokana na doria hizo, nyara za Serikali za aina mbalimbali zilikamatwa ambazo ni pamoja na meno ya tembo 296 yenye jumla ya uzito wa kilo 929.8; nyamapori kilo 12,776; meno mawili ya simba, kakakuona 644; ngozi 10 za chui na ngozi moja ya simba.

Anasema pia jumla ya silaha 5,309 zilizohusika katika ujangili zilikamatwa zikiwamo SMG tisa, hunting rifles 14, shotgun 56, gobore 212, bastola mbili na nyaya za kutegea wanyama 5,016.

Huku watuhumiwa 3,889 wa makosa mbalimbali yakiwamo ujangili nao walikamatwa na kesi zao kuamuliwa na waliopatikana na hatia walilipa faini jumla ya Sh milioni 1.108 na wengine kufungwa jela miezi 12. Kesi 3,011 zilizobaki zilikuwa zinaendelea katika mahakama mbalimbali nchini.


MSIMAMO WA CITES

Katika mkutano wa wawakilishi wa nchi 183 wanachama wa mkataba wa kimataifa wa viumbe vilivyo hatarini kutoweka (CITES), uliofanyika hivi karibuni Geneva, Uswisi kwa lengo la kuimarisha mikakati ya kulinda viumbe hao, wanatoka na mapendekezo 56 yenye lengo la kuimarisha na kulinda viumbe vya porini.

Katibu Mkuu wa CITES, Ivonne Higuero, anasema tayari nchi hizo wanachama zimewasilisha mapendekezo 56 yenye lengo la kubadili na hatimaye kuimarisha kanuni za kulinda viumbe vya porini wakiwamo wanyama pamoja na maua, ambavyo vinauzwa kwenye soko la kimataifa.

“Mapendekezo mengi yanalenga kuhakikisha kuwa viumbe hivyo vilivyoko hatarini na ambavyo vinaendelea kuuzwa, vinasalia endelevu na hivyo mapendekezo yanataka vibali kutoka CITES ili kuruhusu biashara yao,” anasema Higuero.

Anasema mapendekezo mengine yanataka kupigwa marufuku kwa biashara za viumbe vilivyoko kwenye orodha I ilihali mengine yanataka kuwa viumbe ambavyo tayari idadi yao imekaa sawa vihamishwe kutoka orodha ya I kwenda orodha ya II ya mkataba wa CITES.

Anakumbusha kuwa kanuni zilizo wazi na zinazotekelezeka kwa kuzingatia sera thabiti ni muhimu katika kulinda utajiri wa asili na kufanikisha malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), ambayo yalipitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 2015.



Mwakilishi wa Shirika la Kudhibiti Usafirishaji wa Wanyamapori Asia (Traffic), Monica Zavagli
Mwandishi wa makala haya Bakari Kimwanga, akiuliza swali katika mafunzo nchini Thailand.

MAKAMU WA RAIS SAMIA AMUWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE MIAKA 25 YA CHUO KIKUU HURIA

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasssan, akiangalia Vitabu vya kumbukumbu ya Utafiti wa aina mbalimbali kwenye maonesho ya kilele cha Maadhimisho ya kutimia Miaka 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika leo Sept 24,2019 Kinondoni Jijini Dar es salaam, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye maadhimisho hayo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasssan, akihutubia kwenye kilele cha Maadhimisho ya kutimia Miaka 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika leo Sept 24,2019 Kinondoni Jijini Dar es salaam, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye maadhimisho hayo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasssan, akizungumza na Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Mhe. Mizengo Kayanda Peter Pinda Wakati wa kilele cha Maadhimisho ya kutimia Miaka 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika leo Sept 24,2019 Kinondoni Jijini Dar es salaam, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye maadhimisho hayo.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasssan, akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Kinondoni baada ya kuhutubia kilele cha Maadhimisho ya kutimia Miaka 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika leo Sept 24,2019 Kinondoni Jijini Dar es salaam, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye maadhimisho hayo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasssan, akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mafunzo katika Chuo Kikuu Huria Prof. Emmanuel Kigabe, kuhusu Vitabu vya kumbukumbu ya Utafiti wa aina mbalimbali kwenye maonesho ya kilele cha Maadhimisho ya kutimia Miaka 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika leo Sept 24,2019 Kinondoni Jijini Dar es salaam, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye maadhimisho hayo.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasssan, akipata maelezo kutoka kwa Sebastian Sambuo Mushi, kuhusu Utaalamu na Biashara ya Mchele kwenye maonesho ya kilele cha Maadhimisho ya kutimia Miaka 25 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika leo Sept 24,2019 Kinondoni Jijini Dar es salaam, Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais Dkt. John Magufuli kwenye maadhimisho hayo. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

BALOZI GETRUDE MONGELLA AFUNGUA TAMASHA LA 14 LA JINSIA 2019

$
0
0
Balozi Getrude Mongella ambaye ni Rais wa Kwanza wa Bunge la Afrika (PAP) na Katibu Mkuu wa Mkutano wa Nne wa wanawake duniani uliofanyika mwaka 1995 Beijing China amefungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 leo Jumanne Septemba 24,2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam.


Akizungumza wakati wa kufungua Tamasha hilo litakalodumu kwa muda wa siku nne (Septemba 24 hadi 27,2019),Balozi Mongella maarufu 'Mama Beijing' amesema ili kujenga Tanzania ya Viwanda ni lazima wanawake na wanaume washiriki.

Balozi Mongella pia amehamasisha umuhimu wa wanawake kushirikishwa katika utengezaji wa Ilani za uchaguzi za vyama vya siasa ili kuhakikisha masuala ya wanawake yanaingizwa kufikia usawa wa kijinsia.

"Huu msemo wa Wanawake wakiwezeshwa wanaweza mimi nasema hii ni dhambi...hatupaswi kuwa omba omba...Sisi wanawake tunaweza tunachotaka ni vikwazo vinavyotukwamisha viondolewe njiani,tunataka wanawake washiriki kwenye utengenezaji wa ilani za uchaguzi ili Rais atakayegombea apewe na kubeba ajenda zinazohusu wanawake",alisema Balozi Mongella.

"Tuone masuala yanayotuhusu wanawake ni sehemu ya ajenda na uchaguzi utakapopita iwe rahisi kwa tutakayemchagua kuwa Rais kumuomba akimbizane na ajenda za wanawake na asipofanya hivyo atakuwa hajatekeleza Ilani",

Hata hivyo aliipongeza serikali kwa kutekeleza ajenda za Mkutano wa Beijing mfano Sera ya elimu bure hali inayosababisha ongezeko la watoto wa kike kwenda shule na imeondoa kikwazo cha watoto kukosa elimu.Aidha Balozi Mongella amewataka wanasiasa kuepuka Rushwa huku akieleza kuwa Wanasiasa wanaohonga 'rushwa' ili wapate uongozi wanabaka siasa.

Naye Mgeni Maalumu kutoka serikalini,Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile alisema Ukatili wa Kijinsia ni janga jipya linaloitia doa nchi ya Tanzania hivyo kuwaomba wadau wote kuungana kutokomeza hali hiyo.

"Hatuwezi kufikia usawa wa kijinsia katika taifa kama tunaendelea kuwa na matukio ya ukatili ya kijinsia ambayo nyuma yake yana sura ya mila,desturi,umaskini na ukosefu wa elimu.Naomba tuvunje ukimya na tuepuke kumaliza kesi zinazohusu masuala ya ukatili kwa kuyamaliza kienyeje",alisema Dkt. Ndugulile.

Dkt. Ndugulile alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka 2020 na uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 24,2019.Akielezea kuhusu Tamasha la 14 la Jinsia 2019,Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi alisema linahudhuriwa na wadau mbalimbali wa haki za wanawake kutoka ndani na nje ya Tanzania likiongozwa na mada kuu 'Wanaharakati wa jinsia mbioni kubadili dunia'.

"Tamasha hili lina umuhimu wa kipekee kwani tunaendelea kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 ya TGNP tangu ianzishwe mwaka 1993 na kidunia tumeanza kusherehekea maadhimisho ya miaka 25 ya Azimio na Mpangokazi wa Beijing ambapo kilele chake ni mwaka 2020",alisema Liundi.
Balozi Getrude Mongella akifungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Balozi Getrude Mongella akifungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019.

Balozi Getrude Mongella akisalimiana na Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa kufungua Tamasha la 14 la Jinsia 2019 katika viwanja vya TGNP Mtandao Mabibo Jijini Dar es salaam leo Jumanne Septemba 24,2019. 
Naibu Waziri - Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019. 
Awali Balozi Getrude Mongella (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao,Asseny Muro wakifurahia jambo wakati akiwasili katika viwanja vya TGNP Mtandao kwa ajili ya kufungua Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019. 
Meza kuu wakiwa wamesimama baada ya Balozi Getrude Mongella kuwasili katika viwanja vya TGNP Mtandao jijini Dar es salaam. 
Washiriki wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 wakiendelea na burudani wakati Balozi Getrude Mongella akiwasili katika viwanja vya TGNP Mtandao kwa ajili ya kufungua tamasha hilo. 
Mwenyekiti wa Bodi ya TGNP Mtandao,Asseny Muro akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao,Lilian Liundi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
MC wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la Jinsia 2019 ambaye ni Mwanachama wa TGNP Mtandao Ulu Mallya akitoa maelekezo mbalimbali wakati wa sherehe hizo za ufunguzi wa tamasha.

Sehemu ya wageni waalikwa wakati wa tamasha hilo.
Spika Mstaafu wa Bunge la Tanzania,Anne Makinda akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Anders Sjoberg akizungumza wakati wa ufunguzi wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019.
Waziri Mkuu Mstaafu Tanzania,Joseph Sinde Warioba akizungumza wakati wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019. 
Washiriki wa Tamasha la 14 la jinsia mwaka 2019 wakicheza muziki. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

TIGO Yazindua promosheni ya Tigo Chemsha Bongo,KANDA YA ZIWA

$
0
0

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthmaan Madati(katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza, wakati wa ufunguzi wa msimu wa Tigo Fiesta Saizi Yako na bahati nasibu ya Tigo chemsha bongo, kushoto ni Meneja wa Tigo kanda ya Ziwa Daniel Mainoya na Afisa Huduma za Ziada wa Tigo Fabian Felician.


Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthmaan Madati,akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu gari atakalopewa mshindi wa Tigo chemsha bongo jijini Mwanza, wakati wa ufunguzi wa msimu wa Tigo Fiesta Saizi Yako na bahati nasibu ya Tigo chemsha bongo.

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthmaan Madati,akiwasha gari la mfano atakalopewa mshindi wa Tigo chemsha bongo jijini Mwanza, wakati wa ufunguzi wa msimu wa Tigo Fiesta Saizi Yako na bahati nasibu ya Tigo chemsha bongo.



Mteja wa Tigo kuzawadiwa gari aina ya Renault Kwid na wengine kujishindia mamilioni kama zawadi katika promosheni iliyozinduliwa leo Mwanza,iitwayo Tigo Chemsha Bongo katika msimu wa Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako.

Akizungumza na waandishi wa habari,(Septemba 24,2019), wakati wa uzinduzi wa shindano la Tigo Fiesta Chemsha Bongo, ambalo linatafanyia Tanzania nzima katika msimu wa Tigo, Mkurugenzi Tigo Kanda ya Ziwa, Uthmaan Madati, alisema kwa mara ya kwanza, mkoa huo umeweka historia ya kufungua shughuli zote za Tigo Fiesta Saizi Yako 2019

“Tunatambua umuhimu wa tamasha la Tigo Fiesta 2019 Saizi Yako, kwamba si tu linaleta burudani kwa taifa bali linaibua na kukuza vipaji vipya hususan kwa tasnia ya muziki nchini,” alisema Madati.

Alisema tamasha hilo pia linasaidia katika kutoa elimu ya ujasiriamali lakini pia kutoa fursa mbali mbali kwa vijana.

Aidha Mkurugenzi huyo alitumia nafasi hiyo kuishukuru serikali ya mkoa kwa ushirikiano wake wakati wote wa tamasha hilo na mengine mengi na kwamba hilo limesaidia kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi lakini pia kwa kujiamini. Katika hatua nyingine, Madata aliarifu kwamba kwenye shindano hilo, wanatoa zawadi za kila siku ikiwemo Sh 50,000 mpaka 100,000 na Sh 1 Milioni moja kila wiki.

“Katika kipindi cha miezi mitatu wakati kampeni hiyo ikiwa inaendelea, tutapata mshindi ambaye ataweza kujishindia gari lenye thamani ya Sh 23 milioni.,” alisema. Kwenye suala zima la usalama, Madata alisema wanashirikiana kwa ukaribu mkubwa na serikali huku akiwasihi wateja wa mtandao wa Tigo kujisajili kwa alama za vidole.

Katika hatua nyingine, Afisa Huduma za Ziada, Fabian Felician, alielezea kwamba msimu huu Tigo imeamua kushirikisha wateja wake wote kwa kuandaa maswali rahisi hususan yanayowahusu wasanii wa ndani. “Lengo la kufanya hivi ni kudhihirisha umuhimu na mchango wa wateja wetu na pia kutambua aina ya huduma tunazozitoa,” alisema Felician


Mathalan, Meneja wa Tigo, Kanda ya Ziwa, Daniel Mainoya alisema promosheni hiyo inaenda sambamba na msimu wenyewe ambao ni Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako, kwa maana ya wasanii na burudani. Tigo Fiesta itafungua pazia mkoa wa Mwanza, Septemba 28,2019 katika viwanja vya CCM Kirumba.

WAZIRI KANGI LUGOLA ATOA POLE KWA MKUU WA MAJESHI NCHINI

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akisaini kitabu cha maombolezo ya kmifo cha Nelson Mabeyo, mtoto wa Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo, nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi, Msasani jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2019.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akizungumza na Mkuu wa Majeshi Mstaafu, Jenerali Robert Mboma, nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Venance Mabeyo, Msasani jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2019, walipokwenda kuhani msiba wa mtoto wa Mkuu wa Majeshi, Nelson Mabeyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akizungumza na Mwanasiasa Mkongwe na aliyewahi kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Prof. Philemon Sarungi, wakati walipokwenda nyumbani kwa Mkuu wa Majeshi, Jenerali Venace Mabeyo, Msasani jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2019, walipokwenda kuhani msiba wa mtoto wa Mkuu wa Majeshi, Nelson Mabeyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimpa pole Mkuu wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo, wakati alipokwenda kuhani msiba wa mtoto wa Mkuu wa Majeshi, Nelson Mabeyo, Msasani jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2019. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Serikali yaipongeza kampuni ya usambazaji ya Route Pro kwa uwezeshaji vijana wa kuwapatia pikipiki 30

$
0
0

.Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Ajira na Vijana ,Anthony Mavunde (kushoto) akijaribu kuendesha moja ya pikipiki zilizotolewa kwa ajili ya kuwezesha vijana na Kampuni ya Route Pro Katika hafla iliyofanyika Dodoma,kushoto ni Meneja Uendeshaji wa Kampuni hiyo Jaja Mbazila ,Kulia  ni Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo,Duane Edward na nyuma ni baadhi ya vijana watakaonufaika na msaada huo 
 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Ajira na Vijana ,Anthony Mavunde akimkabidhi Augustine Dotto moja ya pikipiki iliyotolewa na Kampuni ya Route Pro. 

Meneja Mkuu wa Kampuni ya usambazaji Bidhaa ya Route Pro akikabidhi funguo za pikipiki zilizotolewa kwa ajili ya kuwawezesha vijana kibiashara kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Ajira na Vijana Anthony Mavunde wakati wa hafla hiyo iliyofanyika jijini Dodoma Katika viwanja vya Nyerere Square 

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Ajira na Vijana ,Anthony Mavunde (kushoto) akimkabidhi pikipiki, Peter Mushi mkazi wa Makole Jijini Dodoma moja ya kampuni iliyotolewa na kampuni ya usambazaji ya Route Pro kwa ajili ya uwezeshaji wa vijana kibiashara.


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi,Vijana na Ajira),Antony Mavunde, ameipongeza kampuni ya kitanzania ya usambazaji bidhaa ya Route Pro kwa ubunifu wake utakaowezesha vijana kupata ajira ambapo imetoa pikipiki 30 kwa vijana kutoka mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam, Arusha, Moshi na Singida ambapo pia itawapatia mafunzo ya biashara.

Mavunde, alitoa pongezi hizo katika hafla ya kampuni ya Route Pro, kukabidhi pikipiki 10 kwa vijana wa mkoani Dodoma iliyofanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini humo.

“Ukosefu wa ajira kwa vijana ni moja ya changamoto inayolikabili taifa letu, ili kukabiliana nalo Serikali imekuwa ikitoa kipaumbele kushirikiana na wadau wanaonyesha nia ya kusaidia kubuni mipango endelevu ya kuwezesha ajira kwa vijana , kama ilivyofanya kampuni ya Route Pro, kwa kutoa mafunzo ya biashara kwa vijana wetu,Tutaendelea kutoa ushirikiano mkubwa kufanikisha suala hili,” alisema Mavunde.

Kampuni ya Route Pro, itatoa pikipiki 30 kwa vijana sambamba na kuwapatia elimu ya biashara na usambazaji bidhaa pia itawapatia elimu ya kutumia vifaa vya teknolojia ya kisasa vya kusaidia kuratibu usambazaji na taarifa.Vijana hao pia itawaunganisha na wadau wake katika biashara na wazalishaji wengine na kushirikiana nao kusambaza bidhaa za wateja katika masoko mkakati ambao utawanufaisha vijana hao na kampuni kwa kugawana faida itakayopatikana nusu kwa nusu.

Akiongea katika zoezi la kuwachagua vijana hao, Meneja Uendeshaji wa kampuni ya Route Pro, Jaja Mbazila, alisema kampuni hiyo imepata walengwa wa kushirikiana nao katika mpango huu, kutokana na rekodi yake ya vijana ambao imewahi kufanya nao kazi katika miradi yake mbalimbali ya usambazaji bidhaa katika siku za nyuma na imewachagua waliokuwa wanafanya kazi kwa bidii na wenye malengo ya kukua kibiashara.

“Tumelenga kuwawezesha vijana wenye bidii ya kazi na kujituma kupata fursa kuwa na biashara zao,tumefanya nao kazi kwa karibu katika miaka iliyopita na wameonyesha kuwa na nia ya kufanya vizuri biashara ya usambazaji”,alisema Mbazila.

Aliongeza kuwa mbali na kuwapatia pikipiki,RoutePro itawapatia vijana hao kiasi cha shilingi 100,000/- kila mmoja ziwasaidie kuanzia kazi.

Baada ya miezi 24, pikipiki hizo zitakuwa mali yao kwa ajili ya kuwasaidia katika shughuli za usambazaji,ingawa watakaopenda kufanya kazi katika mpango huu wa Route Pro wa kuwezesha vijana watajiunga tena katika mpango wa miaka 2 na kupatiwa tena tena pikipiki mpya.

Route Pro ni kampuni ya Kitanzania yenye uzoefu mkubwa wa biashara ya usambazaji wa bidhaa,kwa hivi sasa inazo pikipiki zaidi ya 250 za usambazaji nchini kote,na inatumia teknolojia ya kisasa za kupata taarifa za mauzo kwa ajili ya kuzifanyia uchambuzi.

WASANII WA BONGOFLEVA WAWASHA MOTO KATIKA TAMASHA LA JAMAFEST JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Wasanii wa muziki wa Kizazi kipya wa kundi la TMK Wanaume Family wakiongozwa na Mhe. Temba akiogoza jahazi kutoa burudani ndani ya katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Country Boy akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Country Boy akitoa burudani.
Msanii Barnaba akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Nahreel wa kundi la Navy Kenzo akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Aika wa Navy Kenzo akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Nahreel na Aika wa kundi la Navy Kenzo wakitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Joh Makin akitoa burudani katika katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Dj D- Ommy kwenye mashine akiendelea kuwapagawisha wanajumuiya ya Afrika Mashariki waliofika katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Jux akitoa burudani katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Wasanii Jux (kushoto) na Joh Makin (kulia) wakitoa burudani. 
Aika, Nahreel na Jux wakitoa burudani kwa pamoja katika Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki linalojulikana kama JAMAFEST linalofanyika jijini Dar es Salaam, Tanzania. Tamasha hilo limeanza Septemba 21 na linatarajiwa kuisha 28, 2019.
Msanii Jux akimtambulisha mpenzi wake.
Mahaba niueee...

Stanbic Bank Tanzania commits TZS 177 billion to infrastructure projects in Tanzania

$
0
0



Stanbic Bank Tanzania today reaffirmed its commitment to the development of Tanzania and announced that in 2019 it provided TZS 177 billion in funding to various infrastructure development projects in the country. Providing finance and financial expertise to the private and public sector in Tanzania is a key focus for the bank.

Stanbic Chief Executive Mr. Ken Cockerill said, “Stanbic Bank is well positioned to play an important role in supporting Tanzania’s second Five Year Development Plan, which seeks to encourage industrialization and promote economic growth and social development.”

Mr Cockerill also mentioned that, “Infrastructure development is the cornerstone for sustainable long-term economic growth and competitiveness. With that in mind we are proud to be at the forefront of bridging the infrastructure funding gap to accelerate socioeconomic transformation in Tanzania.”

Unlocking private sector funding will create solutions to bridge Tanzania’s and the continent's infrastructure deficit and challenging business environment by developing and financing infrastructure, natural resources and industrial assets with a view to enhancing productivity and generating economic growth across Africa.

The Government of Tanzania has in 2019 dedicated over TZS 12.2 trillion (USD 5.3 billion) towards key development projects that include Africa’s longest Standard Gauge Railway (SGR), the Uganda-Tanzania Crude Oil Pipeline and Julius Nyerere International Airport Terminal 3.On his part, Stanbic’s Head of Corporate & Investment Banking, Mr. Manzi Rwegasira said, “Tanzania is well on its way to bridging the infrastructure gap which is critical to Tanzania becoming a middle-income country by 2025.”

Tanzania’s population is also growing at a rate of 1.6 million people per year and this is projected to reach 67 million people by 2025 and 77 million by 2030, hence the importance for modern infrastructure for an upcoming middle-income country.Mr. Rwegasira added that, “It is through collaboration between the private and public sector, spearheaded by corporates such as Stanbic Bank Tanzania, that will drive inclusive development in our economy.”

Official data from the Bank of Tanzania shows that the country’s economy grew at an average GDP growth rate of 6.6% in 2018 with the infrastructure sector significantly contributing to this growth. This year, the economy is projected to grow by 7.1 % with infrastructure projects such as roads, ports and rail expected to drive Tanzania’s GDP growth.

Since, 2018 Stanbic has raised over TZS 300 billion in financing for Tanzanian companies and institutions across the agricultural, consumer, industrial, natural resources and government sectors.

The bank is committed to working with the government and key stakeholders to improve the investment and resource mobilization climate in order to ensure that Tanzania realizes its socio-economic aspirations by 2025.



Naibu Waziri Ikupa Aipongeza JAMAFEST Kushirikisha Wenye Ulemavu

$
0
0
Naibu Waziri wa Nchi- Ofisi ya Waziri Mkuu (Anayeshughulikia Wenye
Ulemavu), Mhe. Stella Ikupa, akiangalia bidhaa za nguo katika moja ya banda la mjasiriamali anayeshiriki Maonesho ya Tamasha la Utamaduni la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki JAMAFEST linaloendelea katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam. (Picha na Idara ya Habari-Maelezo).

Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu (Anayeshughulikia Wenye Ulemavu),
Mhe. Stella Ikupa, Akikabidhi baiskeli ya watu wenye mahitaji maalum kwa Bw.
Martine Vicent Mkazi wa Wilaya ya Kigamboni mara baada ya kumaliza kutembelea
mabanda katika Maonesho ya Tamasha la Utamaduni la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki JAMAFEST linaloendelea katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam. (Picha na Idara ya Habari-Maelezo).

Naibu Waziri wa Nchi- Ofisi ya Waziri Mkuu (Anayeshughulikia Wenye
Ulemavu), Mhe. Stella Ikupa, akizungumza na Waandishi Wa Habari (hawapo pichani) Mara baada ya kutenmbelea mabanda katika Maonesho ya Tamasha la Utamaduni la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki JAMAFEST linaloendelea katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam. (Picha na Idara ya Habari-Maelezo).(Picha na Idara ya Habari-MAELEZO).

Eric Msuya – MAELEZO, Dar es Salaam


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshugulikia maswala ya Watu wenye Ulemavu, Mhe. Stella Ikupa amelipongeza Tamasha la Utamaduni wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST) kwa kuwazingatiaa watu wote wenye mahitaji Maalumu kwa kuwapa kipaumbele katika Tamasha hilo.

Ameseyasema hayo leo, mbele ya Waandishi wa Habari, mara ya baada ya kutembelea Mabanda na kujionea ubufunifu mbalimbali ya maonyesho ya Tamasha la JAMAFEST, linaloendelea kufanyika katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Amewapongeza Waandaji wa Tamasha la JAMAFEST kwa kuwapa kipaumbele watu wenye Ulemavu katika kuwapatia mabanda, kwa ajili ya kuuza na kuonyesha bidhaa zao katika Tamasha hilo na kuweza kutangaza biashara zao

“Nitoe Pongezi kwa Waandaji wa Tamasha hili la JAMAFEST, Muitikio wa watu umekuwa mkubwa hasa kwa kundi la watu wenye ulemavu, nimejionea vitu vingi vinavyotengenezwa na walemavu, bidhaa zao ni nzuri kabisa na zipo kwa viwango vya juu sana” Alisema Mhe. Stella Ikupa

Sambamba na hilo Mhe Ikupa Amewataka Watanzania kufika katika Viwanja vya Taifa kujionea bidhaa mbalimbali za kiutamaduni zinazo tengezwa na Watanzania ili waweze kujua Utamaduni wa Watanzania na Wanaafrika Masharikikwa ujumla.

Pia Mhe. Ikupa amewasisistiza Watanzania kutumia muda wao mwingi kujionea mambo mbalimbali ya Utamaduni yanayo fanyika katika Tamasha la Utamaduni la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki JAMAFEST

“Ukifika kwenye Tamasha hili la JAMAFEST hautajuta kupoteza huo muda wako, ila utakuwa umepata kitu kikubwa cha kujifunza juu ya Utamaduni wa Muafrika” Alisema Mhe. Stella Ikupa

Aidha katika Ziara hiyo Mhe. Ikupa amewakabidhi baiskeli za watu wenye mahitaji maalum ndugu Martini Vicente mkazi wa Kigamboni na Ndugu Rajabu Ismail mkazi wa Magomeni- Mwembe Chai ambao wote ni Walemavu wa Miguu.

BODI YA NYAMA:NI MARUFUKU MAGARI YENYE KUTU KUBEBA NYAMA.

$
0
0



Imani Sichalwe Kaimu Msajili wa Bodi ya nyama Tanzania akizungumza katika Maonyesho ya Teknolojia za Uchakataji wa nyama Jijini Arusha.


Na.Vero Ignatus Arusha.

Bodi ya Nyama nchini imepiga marufuku matumizi ya magari yenye kutu katika kubeba nyama kwani kutu ni hatari kwa afya ya binadamu hivyo amesema kuwa serikali haitasita kuchukua hatua kali kwa watakaokahidi agizo hilo.

Imani Sichalwe ni Kaimu Msajili wa Bodi ya nyama Tanzania akizungumza katika Maonyesho ya Teknolojia za Uchakataji wa nyama yaliyohudhuriwa na Wanachama wa Chama cha Wachinjaji na Wafanyabiashara wa nyama jijini Arusha ,amesema wamechukua hatua hiyo ili kulinda ubora wa nyama na kulinda afya za walaji kwa kihakikisha magari yenye kutu hayataruhusiwa kubeba nyama pamoja na ubebaji wa nyama mgongoni.

Alex Lasiki ni Mwenyekiti wa Chama cha Wachinjaji ameiomba serikali isogeze mbele katazo hilo la kutumia vigogo vya miti kukata nyama na kuweka mashine za kukata nyama kwani wachinjaji wengi wanakabiliwa na changamoto ya mitaji midogo ili waweze kujipanga kununua mashine za kisasa.


Ismail Kulanga ni Mkurugenzi wa Jiji la Arusha amesema kuwa jiji la Arusha litashirikiana na machinjio ya Arusha Meat ili kuboresha mazingira ya machinjio hayo na kuhakikisha huduma bora zinatolewa.

Wateja wa Tigo jijini Mwanza kufikiwa na huduma kwa urahisi baada ya ufunguzi wa duka jipya lililopo katika jengo la Rock City Mall.

$
0
0


Mkuu Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika, akikata utepe kuzindua duka la Tigo kwenye jengo la Rock City jijini Mwanza, kushoto ni Meneja Huduma kwa wateja kanda ya ziwa Beatrice Kinabo na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthmaan Madati wakishuhudia.
Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthman Madati akitoa hotuba kwa wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa duka la Tigo kwenye jengo la Rock City jijini Mwanza,

Mkuu Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika, akitoa hotuba wakati wa kuzindua duka la Tigo kwenye jengo la Rock City jijini Mwanza
wageni waalikwa wakifuatilia hotuba kwa makini uzinduzi wa duka la Tigo kwenye jengo la Rock City jijini Mwanza
Muonekano wa Duka jipya la Tigo Mwenye Jengo la Rock City Jijini Mwanza

Mkuu Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika(wa pili kulia) na Msimamizi wa duka la Tigo Rock city Neema Mossama, wakikata keki wakati wa uzinduzi duka la Tigo kwenye jengo la Rock City jijini Mwanza, kushoto ni Meneja Huduma kwa wateja kanda ya ziwa Beatrice Kinabo na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthmaan Madati(wa kwanza kulia) wakishuhudia.

Mkuu Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika(kulia) akizungumza na Meneja Huduma kwa wateja kanda ya ziwa Beatrice Kinabo(kushoto) Meneja wa Tigo kanda ya Ziwa Daniel Mainoya na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Ziwa Uthmaan Madati, baada ya kuzindua duka la Tigo kwenye jengo la Rock city.
Mkuu Wilaya ya Ilemela Dk Severine Lalika, akiangalia simu kwenye duka la Tigo kwenye jengo la Rock City jijini Mwanza baada ya kulizindua.



Kampuni inayoongoza katika maisha ya kidijitali Tanzania,Tigo, leo imefungua duka jipya jijini Mwanza.Duka hilo litawafanya wateja wa kampuni hiyo kupata huduma zote kwa urahisi zaidi ndani ya eneo moja la Rock City Mall.

Duka hilo litatoa huduma zote muhimu kuanzia usajili wa namba za simu kwa alama za vidole, huduma za kifedha ‘Tigo Pesa’ na mauzo ya data na vifaa vya mawasiliano kama simu janja, router na modem kwaajili ya huduma yetu tuliyo zindua hivi majuzi iitwayo ‘Tigo Home internet’.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa duka hilo, Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Uthmaan Madati amesema hatua ya kufungua duka hilo ni moja ya mkakati wa Tigo wa uboreshaji wa huduma na kuhakikisha zinawafikia wateja kwa wakati nchi nzima.

“Duka hili jipya litampa mteja wetu wasaa wa kutazama na kujaribu bidhaa mbalimbali kabla ya kuamua kufanya manunuzi.Hatua hii imekuja kufuatia maombi ya muda mrefu kutoka kwa wateja wetu waliokuwa wakihitaji uwepo wa duka letu kwenye jengo hili maarufu kibiashara hivyo tumekidhi mahitaji yao,”alisema Madati.

Awali akizindua duka hilo, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela,Mkoani Mwanza, Dkt.Severine Lalika alipongeza juhudi za Tigo katika kuwekeza rasilimali katika uboreshaji wa huduma na kuhakikisha zinakidhi viwango vya kimataifa.

“Huduma bora kwa wateja ni kitovu cha biashara na zaidi huwafanya wateja wajisikie wanathaminika na kuheshimiwa, Tigo wametekeleza jambo hili kwa vitendo kwa kufanya uwekezaji katika utoaji wa huduma zao jambo linalowapa utofauti wa kipekee sokoni,” alisema Lalika.

Kadhalika,duka hilo linakuwa la nne kufunguliwa mkoani humo huku likiwa na huduma mpya ikiwamo simu zinazotamba kwa sasa aina ya S3 na R7 pamoja na vifaa vya huduma za intaneti kwa makampuni maarufu kama ‘Tigo business’.

Maduka mengine matatu ambayo yanatoa huduma mkoani hapa ni pamoja na Mwanza kiosk-barabara ya Nyerere, Ukerewe shop-Wilaya ya Ukerewe, Sengerema shop-Wilayani Sengerema na Airport kiosk- Uwanja wa ndege wa Mwanza.

VIONGOZI WAELEZA HATUA AMBAZO ZINAZOCHUKULIWA NA SERIKALI, TIC KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI

$
0
0


Na Ripoti Wetu, Michuzi TV

KATIKA kutambua umuhimu wa biashara na uwekezaji nchini, viongozi wa ngazi mbalimbali wamezungumza hatua zinazochukuliwa na Serikali kuboresha huduma kwa wawekezaji na umuhimu wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) katika kufanikishwa uwekezaji wa wawekezaji watarajiwa nchini

Viongozi hao wamezungumza hayo hivi karibuni waliposhiriki mkutano wa kusikiliza changamoto za wafanyabiashara na wawekezaji katika Mkoa wa Ruvuma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angella Kairuki amesema kwa sasa wanafanya maboresho katika sera na sheria ya uwekezaji ili kuwa na mazingira mazuri kwa wafanyabiashara na wawekezaji.

Ameongeza kuwa mabadiliko ya sheria ya uwekezaji yanalenga kuvutia uwekezaji zaidi na itasaidia kupunguza kiwango kinachotakiwa ili kujisajili na TIC.Pia itasaidia au kuwezesha wawekezaji wa kada ya chini na kati pia kusajiliwa na TIC.

" Usajili utawasaidia kunufaika na faida zinazotokana na kujisajili ikiwamo vivutio vya kikodi na visivyo vya kikodi,"amesema Waziri Kairuki na kuongeza wanategemea mapendekezo hayo yawasilishwe Bungeni Novemba, mwaka 2019.

Aidha Kairuki ameshukuru juu ya matamko mabaya ya viongozi na vitisho kwa wawekezaji na wafanyabiashara kwamba kwa sasa yamepungua na wanaomba viongozi wenye tabia hiyo waache mara moja. Pia amesema Serikali ipo kwa ajili ya kuhudumia na kufanikisha malengo ya wafanyabiashara na wawekezaji maana ndio wanatoa fedha ya maendeleo ya nchi.

"Niwapongeze Mkoa wa Ruvuma, sijawahi kusikia wala sijapokea taarifa yakuwepo kwa matamko wala vitisho dhidi ya wawekezaji bali mmekuwa wakaribishaji na wasaidizi wa wawekezaji,"amesema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabulla amesema wawekezaji wote wanaohitaji ardhi lazima wapite TIC hasa wawekezaji wa kigeni.

Amesema lengo ni kutengenezewa hati pacha ya umiliki yaani 'Deriverrive Right' itakayompa uwezo wa kuimiliki. Ametoa mwito kwa kwa halmashauri zote kuhimiza wawekezaji wote hasa wa kigeni wanaohitaji ardhi ya uwekezaji kupitia TIC.

"Mnapopata ardhi kwa ajili ya uwekezaji msimpe mwekezaji moja kwa moja bali fuateni taratibu na sheria za kupitia TIC ili kujiepusha na migogoro inayoweza kujitokeza pasipo na sababu.Hili lizingatiwe,"amesema.

Hata hivyo amesema Novemba 19 mwaka huu Wizara itafungua ofisi kila mkoa ili kurahisisha upatiknaji wa ardhi ikiwamo ya uwekezaji, upimaji na upatikanaji wa hati ngazi ya kila mkoa. Amesema hiyo itapunguza usumbufu kwa wawekezaji na wafanyabiashara kufuatilia hati mikoa jirani (Kanda) au Dar es Salaam.

Wakati huo huo Naibu Waziri wa Fedha Dk.Ashatu Kijaji amesema hakuna nchi inayoendelea bila wafanyabiashara na wawekezaji. Na ili nchi iendelee tunahitaji kodi kwa maendeleo na kodi inatokana na wafanyabiashara na wawekezaji hivyo tushirikiane nao vizuri.

"Katika kuboresha na kuweka mazingira mazuri mwa wafanyabiashara na mwekezaji inashauriwa wapewe miezi sita(6) kabla ya kuanza kulipa kodi pale wanapoanza utekelezaji wa miradi yao,"amesema.

Ameongeza kuwa hiyo itawapa muda wa kujifunza, kujitathmini na kujipanga kwa ajili ya kulipa kodi na kuongeza malipo yafanyike kupitia mashine za EFD zinazotolewa na TRA na sio vinginevyo.

Pia amesisitiza kodi kulipwa kwa utaratibu wa sheria husika na si vinginevyo, hivyo maofisa wazingatie hilo na wafuate sheria wanapokusanya kodi.

Kwa upande wa Wizara ya Mazingira imeeleza kuna uhusiano mkubwa kati ya uwekezaji na mazingira na kwamba uwekezaji wowote unaofanyika lazima uwe endelevu kwa maana ya uzingatie sheria za kutunza uhifadhi mazingira kwa matumizi ya leo na hata vizazi vinavyokuja.

Wizara hiyo imetoa mwito kwa wawekezaji wote kuwasiliana na NEMC ili kupata miongozo ya mazingira wanapotarajia kutekeleza miradi yao nchini. Aidha NEMC pia inafanya maboresho ili kumwezesha mwekezaji kupata kibali cha kuendelelea na mradi wake. 
 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Angella Kairuki akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika Mkoani Ruvuma
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina  Mabula akifafanua jambo kuhusu uombaji wa ardhi kwa wanaohitaji ardhi kwa ajili ya uwekezaji
 Naibu Waziri wa Fedha Dk.Ashatu Kijaji akizungumza katika mkutano huo ambapo ametumia nafasi hiyo kuzungumzia umuhimu wa kukufanya kodi kwa mujibu wa sheria
 

RC BYAKANWA AZITAKA TAASISI ZA KIBENKI KUWAFIKIA WAKULIMA-MTWARA

$
0
0
Katika kuelekea Msimu wa Ununuzi wa Zao la Korosho 2019/2020 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa amezitaka taasisi za kibenki kuhakikisha zinawafiki na kuwafungulia akaunti wakulima wa zao la korosho kutokana na kuondokana na utaratibu wa kuwalipa wakulima mkononi.
Byakanwa ameyasema hayo mara baada ya kufungua Tawi la benki ya TPB lililopo Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara ambalo limeweza kutoa mikopo zaidi ya shilingi Bilion Nne mpaka sasa na kuwafikia wakulima wa korosho zaidi ya 2500 kwa mwaka huu pekee
Akiongea mbele ya wateja pamoja na wananchii waliohudhulia hafla hiyo Byakanwa ametumia nafasi hiyo kuzitaka taasisi za kibenki zilizopo katika mkoa wa Mtwara kuhakikisha zinawafikia wakulima wa korosho hasa  katika maeneo ya vijijini.
 “Ninazitaka benki zote kuhakikisha zinawafikia wakulima wote wa korosho kwa sababu hatutakuwa na utamaduni wa kumlipa mkulima mkononi lakini pia tumeondokana na utaratibu wa mkulima mmoja kupokea malipo ya wakulima zaidi ya watano wale ambao hawajafungua akaunti kwa hiyo niiombe TPB kuiona hiyo kama fursa”amesema Byakanwa
Aidha Byakanwa ameongeza kuwa anafarijika kuona huduma nzuri za benki hiyo kutokana na kutopata malalamiko yoyote kutoka kwa  wakulima hasa wa zao la Korosho.
“Ninafarijika na ubora mnazozitoa huduma mnazozitoa kwa wakulima wetu kwa mwaka wa pili huu sijapata malalamiko yoyote ya mkulima yoyote kuhusina na benki ya TPB sio masasi sio Mtwara”
Sabasaba Moshingi ni Mtendaji Mkuu wa benki hiyo anasema kuwa TPB tayari imeongeza idadi ya matawi hapa Nchini kutoka 32 na kufikisha 77 ambayo yameweza kuongeza idadai ajira pamoja na kutoa huduma za kifedha kwa Jamii husika.
“Benki imeendelea kutoa gawiwo kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo na mwaka huu kutokana na faida ya mwaka jana tumeweza kutoa gawiwo la shilingi Bilioni moja na million mia mbili kwa wanahisa wake ambao mwanahisa mkubwa ni serikali lakini tumeweza kuongeza idadi ya matawi na hili la masaSI ni miongoni ya matawi mapya ambayo tunafungua”Amesema Moshingi
5733.Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akifungua Tawi jipya la benki ya TPB lililopo wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara ambalo tayari limeweza kuwafiki wakulima wa zao la korosho zaidi ya 2500,kusoto kwake ni mtendaji mkuu wa benki hiyo Sabasaba Moshingi.
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akikata utepe kuashiria ufunguzi wa tawi la Benki ya TPB Wilaya ya Masasi Mkoa wa Mtwara ambalo Tayari limetoa mikopo ya zaidi ya shilingi billion Nne kwa wakulima wa zao la Korosho Wilayani hapo
 Mkuuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akiwa amebeba mtoto wa mmoja wa wananchi walioshiriki katika uzinduzi wa tawi la Benki ya TPB lililopo Masasi Mkoa wa Mtwara,kushoto ni Mtendaji Mkuu wa TPB Sabasaba Moshingi.
 Saidi Mbito kulia akiwa na Sulpis Likanda wakiwa na zawadi ya Ngao waliopewa na Benki ya TPB kama moja ya shukurani kwa kufanya kazi muda mrefu na benki hiyo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gelasius Byakanwa akiongozana na Mtendaji mkuu wa benki ya TPB Sabasaba Moshingi mara baada ya kutembelea na kukagua huduma mbalimbali zinazopatikana katika  tawi jipya la benki hiyo iliyopo Wilaya ya Masasi,Mtwara.
 Kikundi cha Ngoma Mchema Group kutoka wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara kikitumbuiza ngoma za kitamaduni za kabila la Wamakua katika uzinduzi wa Tawi la Benki ya TPB Masasi Mkoani Mtwara.
  Mkuu wa Mkoa wa mtwara Gelasius Byakanwa akiwa katika Picha ya Pamoja na Wafanyakazi wa benki ya TPB mara baada ya kufanya ufunguzi wa tawi la benki hilo wilya ya Masasi Mkoani Mtwara.


Viewing all 46396 articles
Browse latest View live




Latest Images