Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

TAARIFA KWA WANAOSAJILI LINE ZA SIMU HOLELA,BILA IDHINI


TANZANIA YAPEWA JUKUMU KURATIBU MRADI WA KUWAUNGANISHA WANAWAKE WAJASIRIAMALI KATIKA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0
Pichani kulia ni Naibu Katibu Mkuu (EAC),Christopher Bazivamo akizungumza kwenye Warsha ya siku moja mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) hivi karibuni kuhusu mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,unaotarajiwa kuratibiwa nchini Tanzania ili kuwaunganisha wanawake Wajasiriamali katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki,Kushoto ni
Mkurugenzi wa Idara ya Jamii (EAC),Mary Makoffu.Picha na Michuzi JR.
Warsha hiyo ya Wanahabari ikendelea
 Naibu Katibu Mkuu (EAC),Christopher Bazivamo akifafanua zaidi kwenye Warsha ya siku moja mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) hivi karibuni kuhusu mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,unaotarajiwa kuratibiwa nchini Tanzania ili kuwaunganisha wanawake ,pia katika nchi za Ecowas na Commesa  na lengo lake kubwa ni kuwawezesha wanawake kiuchumi na hususani wanawake wajasiriamali,Pichani kulia ni  Mkurugenzi wa Fedha (EAC) Juvenari Ndimurirwo na  kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Jamii (EAC),Mary Makoffu
Mkurugenzi wa Idara ya Jamii (EAC),Mary Makoffu(katikati) akizungumza mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani),kwenye Warsha hiyo ya siku moja iliofanyika jijini Dar,kushoto ni Ofisa Maendeleo Mwandamizi wa Wizara hiyo kutoka Idara ya Jinsia Mapunda John
Mratibu wa Mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,Bw. Wilson Muyenzi akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari katika semina hiyo.
Mkurugenzi wa Fedha (EAC) Juvenari Ndimurirwo akifafanua namna ya umuhimu wa kupanga na matumizi ya fedha katika mambo mbalimbali ikiwemo mradi wa Mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking,hasa kwa watakaosiriki kwa namna moja ama nyingine.

Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii.
 
WIZARA ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto imeeleza faida za upatikanaji wa taarifa muhimu zikiwemo za fedha kwa Wanawake wajasriamali kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki na nchi nyingine Barani Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Ofisa Maendeleo Mwandamizi wa Wizara hiyo kutoka Idara ya Jinsia Mapunda John amesema wajasiriamali hao wanaunganishwa kupitia mradi wa 50 Milioni African Women Speak Networking.

Amesema ni mradi ambao unatekelezwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki,pia katika nchi za Ecowas na Commesa  na lengo lake kubwa ni kuwawezesha wanawake kiuchumi na hususani wanawake wajasiriamali.

"Kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mradi unatekelezwa kwenye nchi sita. Na sio jumuiya ya Afrika Mashariki tu bali hata katika nchi nyingine nje. Kuhusu kuwawezesha wanawake kiuchumi ni katika suala zima la kuwapatia taarifa muhimu ikiwa pamoja na taarifa za fedha na taarifa ambazo sio za fedha.

"Sasa kwa maana ya taarifa za fedha tunamaanisha taarifa kwa mfano za wapi mikopo inapatikana ,wapi grants zinapatikana lakini ili waweze kutumia kama mitaji kuendesha biashara zao lakini tunavyosema taarifa ambazo sio za fedha kuna taarifa mbalimbali ambazo ni muhimu kwa wajasiriamali kuzipata," amesema John.

Pia amesema taarifa zinazohusu masoko na mambo mengine ya kutambua thaman na wapi kwenye uhitaji na hata usalama wa biashara kwani kuna baadhi ya nchi nyakati za uchaguzi hahuko salama ,hivyo lazima wajasiriamali hao wawe na taarifa.

Amesisitiza kwamba lengo kubwa la mradi huo ni kuhakikisha ni namna gani taarifa hizo zitawafikia wanawake wajasiriamali na ndio maana matarajio ni kuandaliwa kwa Website ambayo ndani yake kutakuwa kunawekwa taarifa zote muhimu.

"Na kwamba si tu bali wanafikiria kwa kuwa na eneo moja la wajasiriamali kukutana watakuwa na mijadala mbalimbali kati ya wafanyabiashara wakubwa na wakati ikiwa pamoja na kubadilishana uzoefu," amesema John.

Amefafanua kuwa wameona kuwa wanaweza kutengeneza Website nzuri na kuwekwa taarifa zote lakini kama wanawake wajasiriamali hawajui haitakuwa na maana yoyote.

Hivyo amesemani fursa muhimu kwao kukutana na vyombo vya habari kwani kwa kutumia njia zao za kufikisha taarifa watawafikishia wanawake wajasiriamali taarifa za nchiradi huo  na wanafanya hivyo kwa kuamini kuna takribani ya wanawake milioni 500 na malengo ni kuwafikia wanawake asilimia 10 ambayo ukiiigiwa unapata wajasiriamali milioni 50 kwa jumuiya tatu ambazo kuna nchi 38.

"Wanawake wapo wengi,wapo ambao wamefanikiwa na wapo ambao hawajafanikiwa.Kwa kutumia Poto hii au Website tunaamini itakuww chachu ya maendeleo yao na nchi husika kwa ujumla," amesema John.

LUGOLA ASEMA POLISI WANAOSHIRIKIANA NA MAFISADI KUDHULUMU ARDHI YA WANANCHI MASKINI, DAWA YAO IMEIVA

$
0
0
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Haruzale, Kata ya Nyamihyolo, Mwibara, Wilayani Bunda, leo. Lugola alisema tabia ya baadhi ya polisi nchini wanaoshirikiana na mafisadi kudhulumu ardhi ya wananchi maskini, dawa yao imeiva, hatamuonea mtu huruma. 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akiwaelekeza wananchi wa Kijiji cha Kabainja Kata ya Kasuguti, Mwibara, Wilayani Bunda, jinsi ya kujenga darasa lililoimara katika shule ya msingi Kabainja kijijini hapo, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
……………………… 
Na Felix Mwagara, Mwibara (MOHA) 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amesema baadhi ya polisi wasiokuwa waaminifu nchini wanaoshirikiana na mafisadi kudhulumu ardhi ya wananchi maskini, sasa dawa yao imeiva. 
Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Haruzale, Kata ya Nyamihyolo, Jimbo la Mwibara, Bunda akiwa katika ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo jimboni mwake, Lugola amesema amepokea malalamiko mengi ya ardhi katika jimbo lake na sehemu mbalimbali nchini. 

Amesema mafisadi wa ardhi hukimbilia kufungua kesi vituoni wakilazimisha kwa kutumia fedha ardhi iwe mali yao wakiwatumia polisi wasiokuwa waaminifu ili kufanikisha matwaka yao. 

“Haiwezekani tabia hii ikachekewachekewa na kuonekana ni kawaida, nimekemea sana katika mikutano yangu hapa Mwibara na sehemu zinginezo hapa nchini, nitahakikisha napambana na mafisadi pamoja na polisi hao wasiokuwa waaminifu,” alisema Lugola. 

Waziri Lugola alisema kila kukicha anapata malalamiko mengi kutoka sehemu mbalimbali nchini kuwa mafisadi wanaendelea kuwaonea wananchi maskini kwa kupora ardhi wakidai wao ndio wamiliki halali. Aliongeza kuwa, utumia polisi wasiokua waaminifu kuwakandamiza wananchi ambao hawana nguvu ya kifedha na kufanikiwa kudhulumu ardhi zao. 

“Dawa yao ilikuwa jikoni, sasa imeiva, siwezi mwangusha Mheshimwa Rais Dkt. John Magufuli, Serikali hii haichezewi hata siku moja, sasa nitawashughulikia ipasavyo,” alisema Lugola. 

Aidha, Lugola aliwataka wananchi wa Mwibara kuhifadhi vyakula vizuri ili kuepusha janga la njaa kwa hapo baadaye na kusababisha wananchi kuja kuteseka kwa ukosefu wa vyakula na kusababisha mateso katika familia. 
“Tutunzeni vyakula vyetu, msitumie hovyo, kuweni makini na matumizi ya vyakula, sitaki nije kuona mnateseka na njaa, hakikisheni mnatunza vyakula kwa ajili ya matumizi ya baadaye, ogopeni njaa kama ukoma,” alisema Lugola. 
Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo hilo, alifanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo akikagua madarasa ya shule ya msingi pamoja na zahanati.

RAIS WA KENYA UHURU KENYATTA AMALIZA ZIARA YAKE BINAFSI YA SIKU MBILI CHATO MKOANI GEITA NAKUREJEA NCHINI KWAKE

$
0
0

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta katika uwanja wa ndege wa Chato mara baada ya kumaliza ziara yake binafsi ya siku mbili Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta wakati wakipita kwenye Gadi ya Heshma iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ katika uwanja wa Ndege wa Chato mkoani Geita.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni  wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta wakati wakisikiliza nyimbo iliyokuwa ikiimbwa na wanakwaya wa Mwagazege ya Chato kabla ya Rais Kenyatta kuondoka na kurejea nchini Kenya.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya mazungumzo yake na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta Chato mkoani Geita.

 Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akimsalimia Mama mzazi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Bibi Suzana Magufuli ambaye anapatiwa matibabu kijijini kwake Mlimani Chato mkoani Geita kabla ya kuondoka kurejea Kenya mara baada ya kumaliza ziara yake binafsi ya siku mbili.
 Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akizungumza na wanahabari mara baada ya mazungumzo yake na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.
  Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta akiweka shada la maua katika moja ya makaburi ya Familia ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli yaliyopo katika kijiji cha Mlimani Chato wakati akiwa katika ziara yake binafsi ya siku mbili.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na  mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta kabla ya kuanza mazungumzo yao Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na  mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta mara baada ya mazungumzo yao Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na  mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta  ambaye aliambatana na ujumbe wake kutoka Kenya katika ziara yake binafsi ya siku mbili katika kijiji cha Mlimani Chato Mkoani Geita.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Kenya Mheshimiwa Uhuru Kenyatta kabla ya kuondoka katika kijiji cha Mlimani Chato na kurejea nchini kwake Kenya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpungia mkono mgeni wake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wakati akipanda ndege kurejea nchini Kenya. PICHA NA IKULU



BRELA YAWAPIGA MSASA WAFANYABIASHARA MKOA WA PWANI JINSI YA KUJISAJILI KWA MFUMO WA MTANDAO

$
0
0
Afisa Mfawidhi kutoka Brela kanda ya kusini ambaye ni mtaalamu wa mfumo wa usajili Francis Mwakalebela aliyesimama akitoa maelekezo kwa kwa njia ya vitendo washiriki wa mafunzo hayo kuhusina na namna ya kuweza kusajili makampuni ya na majina ya biashara kwa njia ya mtandao.
Baadhi ya wafanyabiashara wa Mkoa wa Pwani wakiwa katika zoezi la kujifunza jinsi ya kufanya usajili kwa kutumia mfumo wa mtandao
Washiriki wa mafunzo hayo kutoka maeneo mbali mbali ya Mkoa wa Pwani wakiwa wanaelekezana jinsi ya kuweza namna na kujisajili makampuni na majina ya biashra kwa kwa kutumia njia ya mtandao.
Wafanyabishara wa Mkoa wa Pwani wakiwa katika mafunzo ya kujifunza namna ya kusajili makampuni na majina ya biashara kwa njia ya mtandao.
Afisa maendeleo ya jamii katika halmashauri ya mji Kibaha Lea Lwanji kushoto akiwa na mshiriki mwenzake wakiwa wanafuatilia kwa umakini mafunzo ya usajili kwa kutumia mfumo wa njia ya mtandao
Washiriki wa mafunzo hayo wakiwa wanaangalia jinsi ya mfumo wa kujisajili kwa njia ya mtandao unavyofanya kazi
Moja ya bango la Brela ambalo linaonyesha maelezo kuhusiana na mfumo wa kufanya usajili kwa kutumia mfumo wa mtandao.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
……………………
VICTOR MASANGU, PWANI 
BAADHI ya wafanyabiashara Mkoani Pwani ambao kwa kipindi cha muda mrefu waliokuwa wanakabiliwa na changamoto sugu ya kufanyiwa vitendo vya utapeli pindi wanapotaka kupatiwa usajili wa makampuni yao pamoja na majina ya biashara hatimaye wamepata ufumbuzi baada ya kupatiwa mafunzo maalumu kutoka Wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA) kwa lengo la kujifunza sheria na taratibu za usajili.

Wakizungumza katika ufunguzi rasmi wa mafunzo maalumu yaliyoandaliwa kwa umma juu ya kujifunza jinsi ya kutumia mfumo wa usajili wa makampuni na majina ya biashara baadhi ya wafanyabiashara hao akiwemo Abdala Ndauka na Elina Mgonja wamesema kwa miaka mingi wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya upateli hivyo kujikuta wanaingia hasara kubwa katika zoezi zima la upatikanaji wa leseni.

Aidha wafanyabiashara hao wametoa pongezi kwa Brela kwa kuwapatia mafunzo hayo ambayo yataweza kuwasaidia kwa kiasi kikubwa changamoto mbali mbali ambao ilikuwa zikiwakabili katika siku za nyuma katika kutekeleza majukumu yao hususan kuweza kutumia mfumo wa usajili wa kampuni na majina ya biashara zao.

“Kwa kweli sisi kama wafanyabiashara wa Mkoa wa Pwani tunatoa pongezi zetu za dhati kwa mamlaka husika ya Brela kwa kuona umuhimu ya kutupatia mafunzo hayo ya kujisajili kwa kutumia njia ya mtandao, maana hapo awali tulikuwa tunapata usiumbufu mkubwa na wakati mwingine kutapeliwa na baadhi ya watu hivyo kwa sasa tunaweza kutimiza majukumu yetu kwa weledi wa hali ya juu,”walisema wafanyabiashara hao.


Kwa upande wake mkurugenzi wa utawala na fedha kutoka Wakala wa usajili wa biashara na leseni (BRELA)Bakari Mketo alibainisha kwamba lengo la kuandaa mafunzo hayo kwa wafanyabiashara pamoja na umma kuhusina na kupata huduma za usajili kwa njia ya mtandao ikiwemo kuwajengea uwezo katika suala zima la ulipaji wa madeni kwa wateja wao ili kuondokana na usumbufu waliokuwa waliokuwa wanaupata.

“Lengo letu kubwa kwa sasa tunazunguka katika mikoa mbali mbali na kwa sasa tumeamua kuwakutanisha wafanyabiashara wa Mkoa wa Pwani ili tuweze kuwapa mafunzo maalumu ambayo yatawawezesha kuweza kujisajili kwa kutumia njia ya mtandao pamoja na kujifunza mambo mbali mbali ambayo yanahusiama ma utoaji wa leseni za viwanda,”alisema Mketo.

Pia alibainisha kwamba lengo lao kubwa ni kuweka mikakati kabambe ambayo iytaweza kuwasaidia wafanyabiashara kuondokana na changamoto mbali mbali ambazo zimekuwa zikiwakabili katika utekelezaji wa majukumu yao,ili waweze kufanya usajili wa makampuni yao pamoja na majina ya biashara zao bila ya kuwepo na usumbufu wowote.

Naye Afisa biashara mkuu kutoka Wizara ya viwanda na bishara Jane Lyatuu aliwataka wafanyabishara wote nchini kuhakikisha wanazisajili biashara zao zote pamoja na makampuni,taasisi, viwanda kwa lengo la kuweza kuhimili ushindani uliopo katika soka la bara la afrika kwa kuzingatia ubora wa bidhaa zinazotengezwa nchini.

KATIKA mafunzo hayo yaliyokuwa ya siku mbili yalitolewa kwa umma juu ya kutumia mfumo wa usajili wa kampuni na majina ya biashra , pamoja na alma za bishara na utoaji wa leseni za viwanda yamewashirikisha wadau mbali mbali wa maendeleo, maafisa biashara, wafanyabiashara wadogo na wakubwa, maafisa maendeleo, mkaguzi wa ndani pamoja na wanasheria.

RAIS MSTAAFU JAKAYA KIKWETE ASIFU MAONESHO YA 43 YA SABABSABA JIJINI DAR

$
0
0
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa
Maafisa wa Kampuni ya uzalishaji wa mbegu bora za mazao ya Kilimo ya Seed Co.wakati wa ziara yake aliyoifanya leo Jumamosi (Julai 6, 2019) kutembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Maafisa wa Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) wakati wa ziara yake aliyoifanya leo Jumamosi (Julai 6, 2019) kutembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa
Wakufunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakati wa ziara yake aliyoifanya leo Jumamosi (Julai 6, 2019) kutembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati wa ziara yake aliyoifanya leo Jumamosi (Julai 6, 2019) kutembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete akipata maelezo kutoka kwa Mmoja wa Maafisa wa Idara ya Sera na Machapisho wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakati wa ziara aliyoifanya leo Jumamosi (Julai 6, 2019) kutembelea mabanda mbalimbali ya washiriki wa maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. 


RAIS Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete amezipongeza Wizara ya Viwanda na Biashara na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kwa maandalizi mazuri ya Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere. 

Akizungumza leo Jumamosi (Julai 6, 2019) mara baada ya kutembelea na kukagua mabanda mbalimbali ya washiriki wa Maonesho hayo, Rais Mstaafu Kikwete alisema hizo ni dalili njema kwa maonesho hayo kwa kuwa yamekuwa bora zaidi ya maonesho yaliyofanyika mwaka jana. 

Aidha aliongeza kuwa maonesho ya mwaka huu, yameonesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kujenga uchumi wake kupitia viwanda, kwa kuwa katika maonesho ya mwaka huu malighafi nyingi za kilimo zimepewa kipaumbele na wazalishaji wa bidhaa mbalimbali. 

“Maonesho ya mwaka huu yamekuwa bora zaidi, kwani tumeshuhudia malighafi nyingi za kilimo zikipewa kipaumbele na hii imekuwa ni dalili njema na point (alama) tunayotakiwa kuifikia kwa sasa” alisema Kikwete. 

Awali akitembelea Banda la Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Rais Mstafu Kikwete alilitaka jeshi hilo kuwa wabunifu kwa kuzalisha bidhaa bora zitakazoweza kutumika nje ya Tanzania hususani bidhaa za ngozi ikiwemo viatu vinavyozalishwa na Jeshi hilo.

MAOFISA MAMLAKA YA MAABARA YA MKEMIA MKUU WA SERIKALI WAFAFANUA NAMNA MAMLAKA INAVYOFANYA KAZI

$
0
0
Na Said Mwishehe,Michuzi TV

MAOFISA wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali waliopo kwenye Maonesho ya Biashara ya 43 ya Kimataifa yanayoendelea viwanja vya Mwalim Nyerere maarufu Sabasaba jijini Dar es Salaam wameendelea kutoa maelezo ya kina kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo.

Idadi ya wananchi wanaofika kwenye maonesho hayo wamekuwa wakienda katika banda la Mamlaka hiyo ambapo wengi wao wamekuwa wakitaka kufahamu zaidi kuhusu namna mtambo wa DNA unavyofanya kazi na wengine wakitaka kufahamu wanawezaje kutumia mamlaka hiyo katika shughuli zao za kila.

Akizunguza kwenye maonesho hayo ya biashara yanayoendelea katika viwanja hivyo Mkurugenzi wa Usimamizi, Udhibiti na Ubora wa Bidhaa Sabanitho Mtega ametumia nafasi hiyo kuelezea majukumu ya msingi yanayofanywa na mamlaka hiyo.

Ametaja baadhi ya majukumu hayo ni kufanya uchunguzi wa bidhaa mbalimbali kama vile vyakula, kufanya uchunguzi kwa ajili ya kusaidia vyombo vya ulinzi kufanya uchunguzi wa sampuli ambazo ni za makosa ya jinai kama vile dawa za kulevya, sampuli za sumu na aina nyingine za sampuli zote.

Pia Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali inadhamana ya kusimamia sheria namba tatu ya mwaka 2003 ambapo sheria hiyo pamoja na mambo mengine inasimamia utoaji wa vibali vya katika maeneo yote nchini ikiwemo kwenye viwanja vya ndege, mipakani na bandarini.

"Kwa kufanya hivyo inatuhakikishia kuwa Kemikali zote zinazoingizwa nchini hazileti madhara kwa mazingira na wakati huo huo kwa usalama wa nchi. Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali ndio iliyopewa dhamana kupitia sheria namba 8 ya mwaka 2016 kuwa matokeo yanayotolewa na mamlaka hiyo ndio ya mwisho na hayabishaniwi.

Pia ni chombo cha serikali ambacho kazi yake ni kuhakikisha vyombo vya maamuzi vinatapa matokeo ya uchunguzi ili kufanya maamuzi sahihi. "Tunawakaribisha wananchi kwenye banda la mamlaka yetu ili wapate maelezo ya kina kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo.Pia kupata maelezo yatakayowasaidia kwenye maisha yao ya kila siku,"amesema.

Kuhusu uelewa , amesema kwa sasa wananchi wengi wanailewa mamlaka hiyo na wao wamekuwa wakitumia maonesho mbalimbali kutoa elimu kwa umma.Akizungumzia mtambo wa DNA amesema unafanya kazi nyingi zaidi ya kupima vinasaba vya kutambua uhalali wa mtoto na kwamba mtambo huo unatumika hata kupima sampuli za makosa ya jina, majanga ya moto, ndege, kubaini askari walipoata majanga.Pia kupima wanaohitaji kuwekewa figo ili kujua kama damu zao zinaendana.

Kwa upande wake Ofisa Masoko na Mawasiliano wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Cletus Reuben Mnzava amesema wananchi wengi wanaofika kwenye banda lao kna mambo mengi wanapenda kufahamu.Baadhi ya mambo hayo ni kufahamu namna ambavyo maabara ya mkemia mkuu wa serikali inafanya kazi.Wengine wanataka kujua kuhusu mtambo wa DNA unatumika kupima sampuli za aina gani hasa ukiondoa kujua uhalali wa mtoto.

"Wapo baadhi ya wananchi ambao wanataka kufahamu kuhusu ubora wa bidhaa, pia wanaotaka kufahamu kuhusu usalama wa chakula na dawa ambazo wanazitumia."Wengine wanapenda kufahamu kuhusu uchunguzi wa sampuli ambazo zinafanywa na maabara ya mkemia mkuu.Kuna wajasiriamali ambao wao wakifika hapo wanataka kufahamu ni kwa namna gani maabara hiyo inaweza kutumika katika kuwafanya kuzalisha bidhaa zilizo bora.Wote wenye maswali tunawajibu na wanaridhika,"amesema Mnzava.
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Ubora wa Bidhaa Sabanitho Mtega pichani kushoto akizungumza na mmoja wa wadau waliofika kwenye banda la Mkemia Mkuu kuusu majukumu ya msingi yanayofanywa na mamlaka hiyo.Ametaja baadhi ya majukumu hayo ni kufanya uchunguzi wa bidhaa mbalimbali kama vile vyakula, kufanya uchunguzi kwa ajili ya kusaidia vyombo vya ulinzi kufanya uchunguzi wa sampuli ambazo ni za makosa ya jinai kama vile dawa za kulevya, sampuli za sumu na aina nyingine za sampuli zote.Picha na Michuzi Jr.
 Ofisa Masoko na Mawasiliano wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Cletus Reuben Mnzava akizungumza na na baaadhi ya Wananchi waliofika kwenye banda hilo kufahamu mambo mbalimbali kuhusu mamlaka hiyo
  MAOFISA wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali waliopo kwenye Maonesho ya Biashara ya 43 ya Kimataifa yanayoendelea viwanja vya Mwalim Nyerere maarufu Sabasaba jijini Dar es Salaam wameendelea kutoa maelezo ya kina kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo. 
 Baadhi ya Wananchi wakiendelea kupata elimu na kufahamu mambo mbalimbali yahusuyo Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kutoka kwa Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Ubora wa Bidhaa Sabanitho Mtega 
Ofisa Masoko na Mawasiliano wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Cletus Reuben Mnzava akizungumza na na baaadhi ya Wananchi waliofika kwenye banda hilo kufahamu mambo mbalimbali kuhusu mamlaka hiyo.
 MAOFISA wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali waliopo kwenye Maonesho ya Biashara ya 43 ya Kimataifa yanayoendelea viwanja vya Mwalim Nyerere maarufu Sabasaba jijini Dar es Salaam wameendelea kutoa maelezo ya kina kuhusu majukumu ya mamlaka hiyo.

NMB YAWASHAURI WAZAZI KUWAFUNGULIA WATOTO WAO AKAUNTI ZA WATOTO SABASABA

$
0
0
Bi. Lilian Kisamba akifafanua jambo alipozungumzia umuhimu wa kuwaandaa watoto kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha na kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba kwa malengo, akiwa ndani ya Banda la Benki ya NMB kwenye maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea Sabasaba Dar es Salaam.
Sehemu ya watoto wanaotembelea Banda la NMB wakichorwa nyuso zao baada ya kupata huduma.

Meneja Mradi wa Uwajibikaji kwa Jamii, Bi. Lilian Kisamba akizungumza juu ya umuhimu wa kuwaandaa watoto kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha na kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba kwa malengo, akiwa ndani ya Banda la Benki ya NMB kwenye maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea Sabasaba Dar es Salaam.

Sehemu ya watoto wanaotembelea Banda la NMB wakichorwa nyuso zao baada ya kupata huduma na elimu ya masuala ya fedha.

BENKI ya NMB imewashauri wazazi na walezi kuwafungulia watoto wao akaunti za watoto pamoja na Chipukizi akaunti kwa ajili ya kuwawekea akiba na kuwajengea utamaduni wa kujifunza usimamizi wa fedha zao kwa maisha bora ya baadaye.

Kauli hiyo imetolewa leo katika viwanja vya Sabasaba ndani ya Banda la Benki ya NMB kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam. Akizungumza Meneja Mradi wa Uwajibikaji kwa Jamii, Bi. Lilian Kisamba alisema akaunti hizo zinasaidia kuwaandaa watoto kuwa na nidhamu katika matumizi ya fedha na kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba kwa malengo.

Alisema elimu hiyo ikitolewa vizuri na mapema kwa watoto na jamii nzima inasaidia kupunguza umasikini kwani tutakuwa nafamilia zenye uelewa na matumizi sahihi ya fedha kimalengo.

"Hizi akaunti za wajibu mzazi au mlezi anaweza kuweka kiwango chochote kwenye akaunti ya mtoto hata shilingi 1000 kwa akiba ya mtoto wake...pia hazina gharama zozote za uendeshaji kama akaunti zingine.

Aidha aliongeza kuwa jamiii kwa ujumla ina kila sababu ya kuona umuhimu wa elimu ya masuala ya fedha kuenea kwa kiasi kikubwa na hata ikiwezekana Serikali kuifanya sehemu ya mtaala ili iwe ikimfikia kila mmoja na kujifunza kwa undani wajibu na mahitaji.

WAZIRI LUGOLA APIGA MARUFUKU MAKAMANDA WA POLISI KUYAKAMATA MABASI USIKU, ASEMA NCHI INA AMANI, ATAKA YASAFIRI SAA 24 BILA KUBUGUDHIWA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Namibu, Kata ya Neruma, Jimbo la Mwibara,Wilayani Bunda Mkoa wa Mara, leo. Lugola amepiga marufuku Makamandawa Polisi wa Mikoa nchini kuyazuia mabasi yanayotoka Mikoa ya Kanda yaZiwa kwenda Dar es a Salaam au kurudi Kanda ya Ziwa muda wa usiku kwa kisingizio cha kuofia kuvamiwa na majambazi. Picha na Wizara yaMambo ya Ndani ya Nchi. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, (wapili kushoto),akimsalimia Mkazi wa Kijiji cha Namibu, Kata ya Neruma, Jimbo laMwibara, Wilayani Bunda Mkoa wa Mara, leo, wakati alipofanya ziara kijijinihapo. Lugola amepiga marufuku Makamanda wa Polisi wa Mikoa nchinikuyazuia mabasi yanayotoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa kwenda Dar es aSalaam au kurudi Kanda ya Ziwa muda wa usiku kwa kisingizio cha kuofia
kuvamiwa na majambazi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi. 

********************* 

Na Felix Mwagara, Mwibara (MOHA) 

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amepiga marufuku
Makamanda wa Polisi wa Mikoa nchini kuyazuia mabasi yanayotoka Mikoa
ya Kanda ya Ziwa kwenda Dar es a Salaam au kurudi Kanda ya Ziwa
kusafiri muda wa usiku kwa kisingizio cha kuofia kuvamiwa na majambazi. 

Lugola amesema Jeshi la Polisi lipo imara na kamwe haliwezi kucheka na
majambazi wala kuwaonea huruma majambazi na kuanza kutupangia
majambazi muda gani mabasi yasafiri na yasisafiri, mabasi hayo
yanapaswa kusafiri saa 24. 

Akizungumza na katika mkutano wa hadhara Kijiji cha Namibu Kata ya
Neruma, Jimbo la Mwibara, Wilayani Bunda, Lugola amesema mabasi
yanayosafiri kutoka Kanda ya Ziwa kwenda Dar es Salaam yasizuiwe
Morogoro na yanayotoka Dar es Salaam kwenda kanda ya ziwa yasizuiwe
Shinyanga kwasababu zinazodaiwa za kiusalama. 

“Mimi ndiyo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, hatuwezi kupangiwa
ratiba ya kusafiri na majambazi, Serikali ya Rais Magufuli ipo imara, na
Polisi ipo imara, hivyo agizo hili ambalo pia niliwahi kulitoa lizingatiwe
ipasavyo, niliagiza majambazi wote wasambaratishwe, asakwe mpaka
jambazi wa mwisho, akamatwe kama kuku”.Alisema Lugola na kuongeza. 

“Taarifa ya uhalifu zinaonyesha Jeshi la Polisi limefanya kazi kubwa ya
kupambana na uhalifu na hasa uhalifu wa majambazi, na niliwahi kuagiza
kipindi hiki si cha kuwa na huruma na majambazi ni kipindi cha
kuwashughulikia ili wananchi waishi kwa amani”. 

Lugola alifafanua kuwa, nchi haiwezi kupangiwa na majambazi muda wa
kusafiri, kufanya biashara, hivyo maelekezo aliyoyatoa kwa Jeshi la Polisi
liendelee kupambana na majambazi popote walipo nchini. 

“Nimeelekeza magari yanayosafiri yasizuiwe Morogoro yanpopita muda wa
usiku saa nne usiku na kuendelea, yasizuiwe Shinyanga, ili majambzi wajue
popote walipo wapo imara wamejipanga vizuri na mimi Waziri wao nipo
imara kuhakikisha Jeshi la Polisi linawashughulikia makambazi mmoja
baada ya mwingine ili kuwafanya wananchi katika nchi yao waendelee
kushughulika na masuala ya kujijengea uchumi ili Serikali ya Rais Magufuli,
iweze kuwa na uchumi wa kati na majambazi wote wakamatwe kama
kuku,” alisema Lugola.

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE AWATAKA WANANCHI KUTUNZA VYANZO VYA MAJI,ARIDHISHWA NA UHIFADHI WA MAZINGIRA NA VYANZO VYA MAJI MUHEZA

$
0
0

MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Mkinga Mark Yona
 KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally akivishwa skafu na vijana wa skauti mara baada ya kuwasili wilayani Muheza.
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo katikati akiwa na viongozi mbalimbali mara baada ya mwenge kuwasili kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Muheza Like Gugu na Mbunge wa Jimbo la Muheza( CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto ni  KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akihamasisha kushiriki kuimba kwa pamoja nyingi mbalimbali za mwenge wakati wakiiusubiri
 MMOJA kati ya wakimbiza Mwenge Kitaifa akiweka mwenge mara baada ya kukimbizwa kwenye miradi mbalimbali
 Mwenge wa Uhuru 2019 ukikimbizwa wilayani Muheza
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kulia akiteta jambo na Mwenyekiti wa Halmashauri Bakari Mhando
 KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally katikati akionyeshwa namna ya utunzaji wa mazingira unavyoifanyika wakati alipotembelea na kukagua mradi wa shughuli za uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji Kijiji cha Shembekeza.
 KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally kushoto akimkabidhi cheki ya Sh.Milioni moja Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbaramo Mussa Salimu ikiwa ni mchango uliotoka Halmashauri kuunga mkono ujenzi wa Hosteli kwenye shule ya Msingi Mbaramo kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalumu anayeshuhudia katikati ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo
 MKUU wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo kulia akiwakabidhi zawadi mbalimbali wakimbiza Mwenge wa Uhuru 2019

KIONGOZI wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 Mzee Ally amewataka wananchi wanaoishi karibu na vyanzo vya maji wilayani Muheza mkoani Tanga kuhakikisha wanavitunza ili viweze kuwa endelevu.

Alitoa kauli hiyo mara baada ya Mwenge wa Uhuru kukagua mradi wa shughuli za uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji ikiwemo kukagua mabanda ya wadau wa mazingira na kupanda miti eneo maalumu lillotengwa Kijiji cha Shembekeza.

Akiwa kwenye eneo hilo kiongozi huyo alionyeshwa kuridhishwa na namna mradi wa uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji ambao umesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uharibifu wa vyanzo vya maji.

Alisema kwani Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kutekeleza miradi hiyo kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji hivyo ni muhimu kulindwa na kuendelezwa kwa ajili ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kiongozi huyo alisema suala la upatikanaji wa maji limekubwa na changamoto nyingi ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za serikali huku baadhi ya waka ndarasi wamekuwa wakichukua muda mrefu kukamilika miradi hiyo na hata wengine kukamilisha chini ya kiwango.

“Lakini pia niwaambie kwamba sio jambo jema kufanya shughuli za kibinadamu karibu na vyanzo vya maji ikiwemo ukulima, ufugaji na kujenga karibu na vyanzo hivyo tushirikiane kuhakikiha tunatunza vyanzo vya maji ili vielendee kumudu kwqa vizazi vya sasa na vijazo”Alisema Kiongozi huyo.

Awali amkizungumza wakati akisoma taarifa ya miradi itakayozinduliwa na mwenge ikiwemo kukaguliwa Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo alisema kwamba miradi yenye thamani ya Bilioni 29.471.7 huku akieleza kwamba mwenge huo umekimbizwa kwenye miradi na shughuli mbalimbali.

Alisema wakati wa mkesha wa mwenge huo huduma mbalimbali zilitolewa ikiwemo upimaji vvu ambapo walipimwa watu 448 ambapo kati yao wanaume 307 na wanawake 141 na waliokutwa na maambukizi ni wanaume wawili na wanawake wawili

Wakati huo huo Mpiga picha wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga Muka Sabuni amepongeza na viongozi wa mbio hizo kutokana na namna aliyoweza kutengeneza mabango yenye picha zao wakati ulipoongia wilayani Muheza.

Hatua ya mmoja ya wakimbiza Mwenge ni kushangazwa na ubinfu uliotumiwa na mpiga picha huyo kwa kuweka picha zao kwenye mabango yaliyokuwa yamebeba ujumbe wa mwenge wilayani humo.

Kutokana na hali hiyo mmoja wa wakimbiza Mwenge hao Kenon alitumia muda wa makabidhiano baina ya Muheza na Pangani ndipo aliposimama na kumtambulisha huku akionyeshwa kufurahishwa na utendaji wake na kuiwataka viongozi wa wilaya hiyo kuendelea kumtumia kwenye shughuli mbalimbali.

KAMPUNI YA UUZAJI MAGARI KWA NJIA YA MTANDAO YA NIKKYO YATUA RASMI TANZANIA

$
0
0
Mkurungezi Mkuu wa Kampuni ya Nikkyo Japanese Leon Sera(kulia) inayojihusisha na uuzaji wa magari kwa njia ya mtandao akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kampuni hiyo nchini Tanzania.Lengo ni kurahisisha watanzania kuagiza magari kupitia kampuni hiyo kwa gharama nafuu kwa magari yenye ubora.Katikati ni Meneja mkazi nchini Tanzania wa kampuni hiyo Abbas Mussa na kushoto ni mmoja wa maofisa wa Nikkyo barani Afrika KentaroIkezawa.. Meneja Usafirishaji wa NIkkyo nchini Tanzania Aaliyah Abdulrhman akifafanua kwa kina kwa wageni waalikwa kuhusu ambavyo wamejipanga kuhakikisha wateja wao wanapata magari yaliyo bora.Ametoa ombi kwa Watanzania kuitumia Nikkyo kuagiza magari pindi. Mkurugenzi Mkaazi wa kampuni ya Nikkyo nchini Tanzania Pili Mkufunzi akizungumza ujio wa kampuni hiyo ambayo ilishaingia nchini mwaka mmoja uliopita na sasa imetangazwa rasmi na kuomba Watanzania kuitumia katika kuagiza magari ya aina mbalimbali kutoka Japan. 
Viongozi wa kampuni ya Nikkyo wa nchini Tanzania na Japan wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuizindua rasmi kampuni hiyo ambayo inajihusisha na uuzaji wa magari kwa njia ya mtandao.Utambulisho umefanyika jijini Dar es Sala na kuhudhuriwa na wageni waalikwa mbalimbali. Meneja Masoko mkaazi wa kampuni ya Nikkyo nchini Tanzania Abbas Muusa akizungumza wakati wa sherehe za kuitambulisha kampuni hiyo kwa Watanzania ambayo ina uzoefu katika biashara hiyo kwa miaka 24 na kwa Tanzania imeingia mwaka jana. 

KAMPUNI ya uagizaji, usafirishaji na uuzaji magari ya nchini Japan ‘Nikkyo’ imeingia na kuwekeza katika biashara hiyo nchini huku ikiahidi kutekeleza kwa vitendo adhma ya Serikali katika kukuza uchumi kupitia mpango wake wa maendeleo ya viwanda. 

Aidha katika kutekeleza adhma hiyo, Kampuni hiyo iliyoanzishwa Mwaka 1995 na kufanya uwekezaji katika nchi mbalimbali zikiwemo za Uganda na Kenya imewahikikishia wananchi kuwapa huduma bora na zinazokidhi viwango ili kuendana na malengo iliyoyakusudia. 

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa shughuli za kampuni hiyo hapa nchini Mkurugenzi Mtendaji wa Nikkyo Leon Sera alisema kuzinduliwa kwa kampuni hiyo hapa nchini ni mkakati unaolenga kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwaletea maendeleo wananchi kupitia sekta ya usafirishaji. 
Alisema katika kutekeleza mkakati huo Nikkyo ambayo ina ubobezi wa zaidi ya miaka 20 katika sekta ya uuzaji magari, imejipanga kuwafikia wananchi wenye mahitaji ya ununuzi wa magari ya aina mbalimbali kutoka nchini Japan na kuwafikishia pasipo usumbufu wowote. 

“Tumeingia kuwekeza hapa nchini kutokana na uwepo wa mazingira mazuri na kuvutia uwekezaji, kwetu ni fahari kubwa kuja kuwekeza katika Taifa hili ambalo kwa sasa limejielekeza katika kukuza uchumi wake kupitia viwanda, tuna ahidi kuwa tutafanya shughuli zetu kwa uaminifu mkubwa” alisema Sera 
Alisema kampuni hiyo ambayo inauza magari hayo kupitia mtandao kwa mteja kuchagua aina ya gari anayoihitaji, inampa uhahika mteja wa kupata gari analolihitaji likiwa salama na lenye ubora kwa lengo la kutimiza matakwa ya mteja huyo. 

Kwa upande wake Meneja wa Kampuni hiyo tawi la Tanzania Abbas Ally, alisema ujio wa kampuni hiyo hapa nchini kutawawezesha watu wenye mahitaji kuondokana na usumbufu waliokuwa wakiupata katika uagizaji magari. 

Alisema ukitifautisha na kampuni nyingine zinazojishughulisha na uuzaji wa magari, Nikko imejiwekea utaratibu mzuri wa kutuma mtu kwenda hadi nchini Japan kulikagua gari linalopendekezwa na mteja kabla ya kumletea hapa nchini hatua iliyolenga kumpatia gari iliyo na ubora. 

Wakati huo huo Meneja Usafirishaji wa Nikkyo nchini Tanzania Aaliyah Abdulrhman alisema wao wanachoangalia zaidi ni kuhakikisha mteja anayehitaji kuagiza gari kupitiakwao anapata gari yenye uhakika na iliyobora kwani kabla ya kuagiza gari wanatuma maofisa wao kwa ajili ya kufanya uchunguzi na baada ya kuridhika ndipo sasa wanamletea mteja wao. 

“Hatuangalii fedha bali kwetu cha kwanza ni ubora wa gari, tunataka kuhakikisha gari inayoagizwa kupitia kampuni yetu inakuwa katika mazingira mazuri na iwapo tutaona kuna tatizo tunamshauri mteja na sio tu kuchukua fedha yake.Tunaomba Watanzania wote wanapotaka kuagiza magari watuitumie Nikkyo kwani inayo uzoefu wa kutosha na kwa Tanzania ndio imeingia lakini katika nchi nyingine barani Afrika na Ulaya imekuwa ikifahamika na maarufu kwa uagizaji magari kutoka Japan,”amesema.

Waziri Kabudi atembelea maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa (Sabasaba).

$
0
0
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Wizara hiyo kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (wa kwanza kutoka kushoto) akisikiliza maelezo kutoka kwa Bi. Tagie Daisy Mwakawago Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 
Bw. Hassan Mnondwa akielezea picha za Mawaziri waliowahi kuiongoza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa wanafunzi waliojitokeza kwenye banda hilo. 
Bw. Joseph Mwasoto akifanunua jambo kwa wateja waliyotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba 
Bi. Praxida Gasper akifanunua jambo kwa wateja waliyotembelea banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, kwenye maonesho ya sabasaba 
Huduma zikiendelea kutolewa kwa Wananchi mbalimbali wanaoendelea kutembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya Sabasaba 
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Chuo cha Diplomasia kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akitizama Ramani ya Majengo mapya ya Chuo hicho yanayoyengwa sasa hivi, Kurasini jijini Dar Es Salaam 
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akisaini kitabu cha wageni, alipotembelea banda la Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa (AICC) kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akijionea ufanisi wa utengezaji wa bidhaa mbalimbali za Nyumbani zilizotengenezwa na Jeshi la Magereza, alipotembelea banda la Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa (AICC) kwenye maonesho ya 43 ya biashara ya kimataifa yanayoendea katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam. 
Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Wizara alipotembelea banda la Wizara kwenye maonesho ya sabasaba 
Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika mahojiano na wanahabari kwenye maonesho ya biashara kimataifa maarufa sabasaba yanayofanyika jijini Dar es Salaam

BENKI YA NMB YAKABIDHI VYETI VYA MFANO KWA WAFANYABIASHARA,YAAHIDI KUKUZA MITAJI YAO KWA NGAZI ZOTE

$
0
0
Afisa mkuu wa fedha benki ya NMB, Ruth Zaipuna (wa kwanza kushoto) akimkabidhi mfanyabiashara cheti kilichotolewa na benki hiyo kwa baadhi ya wafanyabiashara wa kupigiwa mfano. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya NMB, Donatus Richard akishuhudia. NMB imewakutanisha wafanyabiashara mbali mbali kwenye Kongamano la Klabu ya Biashara ya NMB mkoa wa Singida kutoa elimu ya biashara.
 
Afisa mkuu wa fedha benki ya NMB, Ruth Zaipuna (wa kwanza kushoto) akimkabidhi mfanyabiashara cheti kilichotolewa na benki hiyo kwa baadhi ya wafanyabiashara wa kupigiwa mfano. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya NMB, Donatus Richard akishuhudia. NMB imewakutanisha wafanyabiashara mbali mbali kwenye Kongamano la Klabu ya Biashara ya NMB mkoa wa Singida kutoa elimu ya biashara.

Benki ya NMB imejipanga kuhakikisha wafanyabiashara wa ngazi zote wanakuza mitaji yao, itakayowawezesha kuajiri Watanzania wengi na hivyo kupunguza makali ya uhaba wa ajira nchini.

Pia waajiriwa hao kupitia kodi watakazolipa, zitachangia kukuza uchumi wa Taifa .

Hayo yamesemwa juzi na Afisa mkuu wa fedha benki ya NMB, Ruth Zaipuna, wakati akizungumza kwenye kongamano iliyohudhuriwa na wanachama wa NMB Business Club mkoa wa Singida. Warsha hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Katala Beach Hotel mjini hapa.

Akifafanua, alisema NMB ina business Clubs 36 nchi nzima, na kila moja ina wanachama kati ya 150 na 300.

“Kundi hilo kubwa la wanachama limekuwa likifaindika na mafunzo mbalimbali tunayotoa. Mafunzo hayo yanajumuisha na bidhaa zinazotolewa kwao na Benki yetu,ikiwemo jinsi ya kutunza vitabu vya mahesabu. Vile vile elimu ya masoko na elimu ya mlipa kodi, ambayo tumekuwa tukifanya kwa kushirikiana na TRA”,amesema Ruth.

Akifafanua zaidi, afisa huyo amesema lengo ni kuhakikisha wafanyabiashara wote wanakuza mitaji yao.Aidha, amesema shughuli za wafanyabiashara wadogo na wa kati (MSMEs) ni muhimu mno kwa uchumi wa Taifa letu.

“Uchumi kwa ujumla wake, unategemea mafanikio ya hizi MSME. Nasi tunajivunia sana kuona kada hii ya biashara imeendelea kukua kadri siku zinavyokwenda. Hayo ni mafanikio makubwa sana, na ya kujivunia”,alisema.

Kwa mujibu wa Afisa Zaipuna, jumla ya wafanyabiashara 200,00 wadogo na wa kati (MSMEs) nchi nzima,mikopo yao inafikia thamani ya shilingi bilioni 600.

Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha biashara NMB,Donatus Richard,amesema lengo la kuwaunganisha au kuwakutanisha wafanyabiashara hao zaidi ya 200 kwenye warsha hiyo,ni wao kufahamaiana na kupeana uzoefu wa biashara za aina mbalimbali.

“Lengo mahususi kuwa na klabu hizi,ni kuendeleza mahusiano na wateja wetu.Mahusiano haya yamesaqidia mno benki kukua.NMB ikiendelea kukua,biashara nazo zinakua kwa kiwango kikubwa”,amesema Richard kwa kujiamini.

Wakati huo huo,mfanyabishara wa mabasi (Dubai express) Evans Makundi,ametumia fursa hiyo kuipongeza tawi la NMB mkoa wa Singida,kwa madai halina urasimu katika kupata mikopo.

NIC yakabidhi hundi kwa wateja wa bima za maisha zilizoiva

$
0
0
 Ofisa mwandamizi wa Bima Washirika la Bima la Taifa NIC, Catherine Nangali,kulia akimkabidhi Elisa Moses Mjema,kushoto mfano wa hundi ya Bima ya maisha iliyoboreshwa. wa pili kushoto ni Ivonne Elisa, Mtoto wake na wapili kulia ni Ofisa Bima wa NIC Vicent Rogath. Makabidhiano hayoyalifanyikaka katika banda la maonyesho ya  43 ya  sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam viwanja vya Mwalimu Nyerere.
 Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Elisante Maleko (Kulia) akimkabidhi Hamadi Rugambwa Ndibalema,mfano wa hundi ya Bima ya maisha iliyoboreshwa.makabidhiano hayoyalifanyikaka katika banda la maonyesho ya  43 ya  sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam viwanja vya Mwalimu Nyerere 
 Baadhi ya wakazi wa jijini Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa Hundi zao za Bima ya maisha iliyoboreshwa katika banda la maonyesho ya  43 ya  sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam viwanja vya Mwalimu Nyerere 
 Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Elisante Maleko (Kulia) akimkabidhi Hamadi Rugambwa Ndibalema,mfano wa hundi ya Bima ya maishailiyoboreshwa.makabidhiano hayoyalifanyikaka katika banda la maonyesho ya  43 ya  sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam viwanja vya Mwalimu Nyerere 
Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Sam Kamanga akiwa mbele ya banda la NIC wakati wa maonyesho ya  43 ya  Sabasaba yanayoendelea Jijini Dar es Salaam viwanja vya Mwalimu Nyerere.Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko na Huduma kwa Wateja NIC Elisante Maleko

SERIKALI YAISHUKURU BENKI YA NMB KUENDELEA KUSAIDIA SEKTA YA ELIMU NA AFYA

$
0
0
SERIKALI Imeishukuru Benki ya NMB kuendelea kusaidia katika Sekta ya Elimu kwa kuchangia madawati baadhi ya Shule zilizo na upungufu na uhitaji mkubwa wa madawati ili wanafunzi waweze kufanya vizuri katika masomo yao.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kupokea madawati 50 yenye thamani ya Sh, milioni 5 kutoka Benki ya NMB, mgeni rasmi Ofisa Habari na Uhusiano wa Manispaa ya Ilala, Tabu Shaibu, aliyemwakilisha Mkurugnezi, aliipongeza benki hiyo kwa kuendelea kuchangia madawati kwa shule zilizo na upungufu.

Aidha alisema kuwa Serikali inatambua mchango mkubwa unaotolewa na Benki hiyo ikiwa ni jitihada za kumuunga mkono juhudi za serikali inayotilia mkazo suala zima la masomo ili kila mtoto aweze kupata elimu.

''Pamoja na Serikali kutangaza kuwa elimu ni bure ili watoto wetu wote waweze kwenda shule, lakini bado inahitahi kushirikiana na wadau wa Elimu kama Benki hii ya NMB ii iweze kufikia lengo la kila mtoto kwenda shule,

Mwaka jana 2018 watoto wa darasa la kwanza walioandikishwa walikuwa ni 22, 000 lakini kwa mwaka huu wameongezeka na kufikia 38,000 hii inaonyesha kuwa hata wazazi wameamka ka kuelewa lengo la Serikali kutoa elimu bure, na idadi hii namini itazidi kuongezeka kila mwaka kutokana na mwamko wa wazazi''. Alisema Tabu

Naye Meneja wa NMB Tawi la Gongolamboto, Rehema Mwibura, alisema kuwa katika kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika Sekta ya Elimu na Afya, NMB itaendelea kuwa karibu na Jamii kwa kutoa sehemu ya faida yao kusaidia Sekta hizo zenye uhitaji.

''Pamoja na kwamba tumeshatoa misaada ya aina hiio kwa shule mbalimbali nchini na vituo vya afya lakini bado tutaendelea kurudisha faida tunayoiapata kwa jamii kwa kuchangia katika masuala ya kijamii. NMB imekuwa ikichangia sekta za Elimu na Afya kwa kutoa vifaa mbalimbali kama vitanda vya Hospitali na vifaa tiba na Madawati pamoja na viti vyake kwa shule za Msingi na Sekondari.

Ofisa Habari na Uhusiano wa Manispaa ya Ilala, Tabu Shaibu (wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria kupokea msaada wa Madawati 50 yenye thamani ya Sh. milioni 5 kutoka kwa Meneja wa Tawi la Gongolamboto, Rehema Mwibura (kushoto) na Meneja Mahusiano Biashara za Serikali wa NMB, Faraja Kaziulaya (kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano ya madawati hayo kwa ajili ya Shule ya Msingi Yangeyange iliyopo Msongola Manispaa ya Ilala, jana.


BALOZI SOKOINE AFUNGUA MAFUNZO YA WAWEZESHAJI WA MASHAMBA DARASA

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine leo amefungua Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nch (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Msasa ya kuhusu Uwezeshaji Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (ldfs),wakiwa kwenye makundi kufanya uchambuzi yakinifu wa mimea na ikolojia shambani katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine akizungumza na Profesa Henry Mahoo wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (katikati) na Dkt. Moses Temi Mkufunzi Mkuu wa Shamba Darasa katika kituo cha Mafunzo ya Kilimo Nkindo wilaya ya Mvomero mara baada ya kufunguaMafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro 

……………………………………………. 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine leo amefungua Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini (ldfs), katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro.

“Ni matumaini yangu kuwa elimu na ufahamu mtakauopata kupitia mafunzo haya, mtaitumia katika kufanikisha uanzishaji wa mashamba darasa katika maeneo ya mradi” alisema Balozi Sokoine.Mafunzo hayo ya siku 5 yanalenga kujenga uwezo kwa washiriki katika uanzishaji wa mashamba darasa katika vijiji na shehia ambako mradi wa LDFS unatekelezwa.

Tanzania kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wamekuwa wakitekeleza miradi inayolenga kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mifugo kwa kusogeza karibu teknolojia kwa wakulima. Lengo likiwa ni kuongeza usalama wa chakula na kuongeza kipato cha jamii. Mradi wa LDFS ambao umeandaa mafunzo haya ni mfano wa juhudi hizo za Serikali. Juhudi hizi zinahusisha uingizaji na matumizi ya teknolojia mpya ikiwemo matumizi sahihi ya mbolea, mbegu zenye ubora; uboreshaji wa nyanda za malisho; utoaji wa huduma za ugani na mafunzo kupitia shamba darasa. Juhudi hizi zote zina lengo la urejesha ardhi iliyoharibika ili iweze kuendelea kuzalisha mazao ya kilimo, mifugo na misitu.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi huo wa LDFS Bw. Joseph Kihaule amesema mradi huo utajumuisha na uanzishwaji wa mashamba darasa 100.
Wawezeshaji wa mradi huo ni Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO), Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Wakala wa Taifa wa Mbegu za Miti Tanzania (TTSA) ambapo washiriki wa mafunzo hayo wametoka Wizara za Kilimo, Maliasili na Utalii, Maji, Mifugo na Uvuvi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Idara ya Mazingira, Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Zanzibar. Aidha, washiriki wengine ni kutoka katika Halmashauri zinazotekeleza Mradi za Mkalama, Micheweni, Magu, Nzega na Kondoa, pamoja waalikwa rasmi Daktari Moses Temi na Bwana Charles Mjema. 
Sehemu ya Wajumbe walioshiriki Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Balozi Joseph Sokoine (katikati)akihutubia wakati wa ufunguzi Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchini (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro, wengine pichani ni Mratibu wa Mradi huo Bw. Joseph Kihaule (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Mazingira Bw. Faraja Ngerageza. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Sehemu ya Wajumbe walioshiriki Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (LDFS), yanayofanyika katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Morogoro . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Msasa ya kuhusu Uwezeshaji Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (ldfs),wakiwa kwenye uchambuzi yakinifu wa mimea na ikolojia shambani katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Msasa ya kuhusu Uwezeshaji Mashamba darasa kwa Maafisa viungo wa mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame ya nchi (ldfs),wakiwa kwenye makundi kufanya uchambuzi yakinifu wa mimea na ikolojia shambani katika Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) mkoani Morogoro. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 

NMB Yakabidhi Gawio la Shilingi Bilioni 10.48 kwa Serikali

$
0
0

Waziri wa Fedha na Mipango – Dr. Philip Mpango, akipokea gawio la shilingi  Bilioni 10.48 kwa Serikali, ikiwa ni sehemu ya faida ya benki ya NMB kwa mwaka 2018 kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi Joseph Semboja (pili kutoka kushoto), Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Albert Jonkergouw na Afisa Mkuu wa Fedha Ruth Zaipuna. 



Benki ya NMB jana ilikabidhi gawio la shilingi Bilioni 10.48 kwa Serikali ikiwa ni sehemu ya faida ya Benki hiyo ya mwaka 2018. 

Akikabidhi hundi kwa Waziri wa Fedha na Mipango – Dr Philip Mpango, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa NMB Albert Jonkergouw alisema fedha hizo ni sehemu ya hisa ambazo ni asilimia 31.8 zinazomilikiwa na serikali ndani ya benki ya NMB. 
Pamoja na gawio hilo, pia NMB imelipa serikalini jumla ya kiasi cha shilingi bilioni 168.8 ikiwa ni kodi tofauti tofauti kama kodi ya mishahara ya wafanyakazi, kodi ya bidhaa, kodi uendelezaji ufundi stadi (SDL) na kodi ya ongezeko la thamani (VAT). 

“Tupo imara sana kama Benki ambayo vitabu vyetu vya hesabu vinaonyesha mwelekeo chanya unaosababishwa na utoaji huduma bora za kifedha,” alisema Bw Jonkergouw, na kuongeza kuwa mazingira ya kufanya biashara nchini bado yana fursa mbalimbali na NMB kama Benki yenye mtandao mkubwa ipo katika nafasi nzuri zaidi ya kuiunga mkono jumuiya ya wafanyabiashara nchini ili kufikia malengo yao. 

Akipokea gawio la serikali, Dr. Mpango alifurahi kupokea gawio hili kutoka NMB na kutoa changamoto kwa makampuni na taasisi nyingine za serikali kuiga mfano. “NMB ni mfano wetu mzuri wa mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika ubinafsishaji nchini, wamekuwa wakifanya vizuri sana wakati wengine wamekuwa wakilalamika tu bila na kuacha kuzitumia fursa nyingi zilizopo nchini kama wanavyofanya NMB katika kupanua zaidi biashara zao,” aliongeza. 

Katika mkutano mkuu wa wanahisa uliofanyika mwezi uliopita jijini Dar es Salaam, wanahisa walipitisha kiasi cha shilingi bilioni 33 kama gawio ambalo limegawanywa kwa wanahisa ikiwa ni sawa na shilingi 66 kwa hisa moja. Katika kipindi cha mwaka uliopita, NMB iliweza kupata faida kabla ya kodi ya shilingi bilioni 142 ikiwa ni ongezeko la asilimia 3 kutoka shilingi bilioni 138 katika mwaka uliotangulia. 

Bw Jonkergouw alisema Benki inaendelea kuweka uwiano mzuri katika kutoa gawio kwa wanahisa na pia kuwekeza ili kuimarisha biashara ya benki na kuifanya ichangie zaidi katika uchumi. NMB ni moja ya makampuni  yaliyobinafsishwa na serikali na kuweza kupata mafanikio makubwa ambapo katika kipindi cha miaka kumi imeweza kutoa kiasi cha shilingi bilioni 118 kwa serikali kama gawio. 


“NMB imekuwa ikifanya vizuri sana katika biashara na itaendelea kujizatiti ili kuwa imara na kutoa huduma bora zaidi. Ili kutekeleza hili, NMB itaendelea kujiimarisha kiuwekezaji katika mifumo yake ya malipo ili kuwawezesha wateja kupata huduma bora zaidi na kuchangia ukuaji wa uchumi ,alisema

WIZARA YA FEDHA WAASWA KUZINGATIA SHERIA ZA UTUMISHI WA UMMA

$
0
0
Na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Watumishi wa Wizara ya Fedha ya Mipango wametakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma katika kutekeleza majukumu yao. Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Bw. Doto James wakati wa kikao cha watumishi wa Wizara hiyo.

Bw. James alisema kuwa watumishi wote wanawajibu wa kufanya kazi kwa ufanisi na weledi na kwa kuzingatia nidhamu, maadili, sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa Umma.

“Ni wajibu wa kila mtumishi kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi  wote wanaohitaji huduma katika Wizara yetu” Alisema Bw. James.

Aidha Bw. James aliwapongeza Watumishi wa Wizara hiyo kwa kazi wanazozifanya hususan kazi ya uandaaji wa Bajeti Kuu ya Serikali iliyopishwa na Bunge hivi karibuni na kuwataka waendelee kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa Bajeti hiyo.

Kwa upande wa Watumishi wa Wizara hiyo waliupongeza uongozi wa Wizara hiyo kwa kutenga muda wa kuzungumza nao na kusikiliza changamoto mbalimbali zinazo wakabili pamoja na kuzitolea ufafanuzi.

Waliahidi kutatekeleza maelekezo yote aliyotolewa kwa uadilifu ili kuongeza ufanisi wa kazi kwa maendeleo ya nchi.
 Katibu Mkuu wa Wizara  ya Fedha na Mipango  Bw. Doto James, akifungua kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la maadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma, Jijini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara  hiyo  Bw. Doto James (hayupo pichani), wakati wa kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Adolf Ndunguru akifafanua jambo wakati wa kikao Kati ya Viongozi na Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika Jijini Dodoma, ambapo Watumishi waliaswa  kufanya kazi kwa bidii na weledi.
 Mhasibu Mkuu wa Serikali, Bw. Francis Mwakapalila akijibu hoja katika kikao kati ya viongozi na Watumishi wa Wizara  ya Fedha na Mipango kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Kamisha wa Sera wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Mgonya Benedicto akichangia hoja wakati wa kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo kilichofanyika Jijini Dodoma.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Alfred Dede akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja zilizoibuliwa wakati wa kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo ambacho kiliongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara  hiyo  Bw. Doto James (hayupo pichani), Jijini Dodoma.
 Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Sekta ya Umma (TUGHE) wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Jenjel James akichangia mada katika kikao cha viongozi na Watumishi wa Wizara hiyo ambapo Watumishi walitakiwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utumishi wa Umma.
 Katibu Mkuu wa Wizara  ya Fedha na Mipango  Bw. Doto James, akisisitiza jambo wakati wa kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo, Jijini Dodoma.
 Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia kwa karibu kikao cha viongozi na Watumishi wa Wizara hiyo, kiliongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara  hiyo  Bw. Doto James (hayupo pichani), Jijini Dodoma.
 Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango wakisikiliza hoja mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika kikao cha Watumishi wa Wizara hiyo Jijini Dodoma.
Mtumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Hilder Rugemalira akitoa hoja wakati wa kikao kati ya viongozi na Watumishi wa Wizara hiyo Jijini Dodoma.

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA KUIPANDISHA DARAJA TANZANIA

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru alipomtembelea ofisini kwake Jijini Dodoma.
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru (kulia) akielezea jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb), Jijini Dodoma. 
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru akielezea jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Isdor Mpango (Mb) (hayupo pichani), Jijini Dodoma. 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Adolf Ndunguru (kushoto), na Kaimu Kamishna wa Fedha za Nje Bw. Adrian Njau wakisikiliza kwa makini mazungumzo kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru (hawapo pichani), kilichofanyika Jijini Dodoma. 
Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru akielezea jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb), Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akiwa na mgeni wake Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru aliomtembelea na kufanya naye mazungumzo katika Ofisi Ndogo ya Hazina-Treasury Squire, Jijini Dodoma. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb), akiteta jambo na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Jijini Dodoma. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb) (aliyeketi mbele kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao jijini Dodoma. Waliosimama wa pili kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Bw. Adolf Ndunguru wa Wizara ya Fedha na Mipango na Maafisa wengine waandamizi kutoka Wizara hiyo. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb) (kushoto), akiagana na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Jijini Dodoma. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini- Wizara ya Fedha na MIpango) 

……………………….. 

Na Saidina Msangi na Josephine Majura, WFM, Dodoma 
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inatarajia kuipandisha daraja Tanzania kutoka katika hadhi ya kunufaika na Mfuko wa Maendeleo wa Benki (ADF) hadi kuwa na hadhi itakayoiwezesha Tanzania kuweza kupata rasilimali fedha zaidi kupitia dirisha la African Development Bank (ADB) la Benki ya Maendeleo ya Afrika. 

Endapo Tanzania itafanikiwa kupandishwa hadhi, nchi itaweza kunufaika na ongezeko la fedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika kutoka Dola za Marekani milioni 350 kwa mwaka hadi Dola za Marekani milioni 812 kwa mwaka. 

Hayo yamesemwa Jijini Dodoma na Mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo Dr. Alex Mubiru alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha na Mipango-Treasury Square. 

Katika mazungumzo hayo, Dr. Alex ameeleza kuwa hatua hiyo ya kupandishwa hadhi ama kupandishwa daraja inatokana na uchumi wa nchi kufanya vizuri hususani katika maeneo ya kasi ya ukuaji wa uchumi na kuwa na deni himilivu. 

“Hatua hiyo itaiwezesha Tanzania kupata fedha zaidi kutoka katika Benki hiyo na kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na vipaumble kwa Serikali” Alisisitiza Bw. Mubiru. 

Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru, amesema kuwa benki hiyo inajivunia kufanya kazi na Tanzania ambayo ni miongoni mwa nchi Waasisi wa Benki hiyo. 

Katika mazungumzo yao, Dkt. Mpango ameeleza kuwa Serikali inajivunia kufanya kazi pamoja na Benki ya AfDB kwa kuwa benki hiyo imekuwa na masharti rafiki katika upatikanaji wa mikopo. 

Dkt. Mpango amesema kuwa Benki hiyo ina mtazamo chanya katika maendeleo ya watu na kuwa dira katika mipango ya maendeleo na kuahidi kushirikiana nao vyema katika kukuza uchumi wa nchi. 

Aidha, Waziri Mpango ameipongeza benki hiyo kwa kukubali kutekeleza miradi ya Ujenzi wa Barabara ya Mzunguko Dodoma (km110.2) kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma (Msalato) na kubainisha kuwa uamuzi huo ni mzuri kwani licha ya Dodoma kuwa ni Makao Makuu ya nchi lakini pia miundombinu hii itaunganisha na kuchochea ukuaji wa uchumi na biashara katika mikoa mingi nchini pamoja na nchi jirani.

Airtel yatoa msaada wa kitanda cha oparesheni Hospitali ya Mkuranga

$
0
0
Airtel yatoa msaada wa kitanda cha oparesheni Hospitali ya Mkuranga
Ni muendelezo wa kampeini ya Airtel Tunakujali ambapo wafanyakazi wa kampuni huchangia kipato chao kusaidia vikundi mbali mbali katika Jamii wenye uhitaji maalum

MKURANGA, KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kupitia kitengo chake cha Huduma kwa wateja wakubwa wameshiriki kampeni maalum yakusaidi jamii inayojulikana kama Aitel Tunakujali kwa kutoa msaada wa kitanda cha kufanyia upasuaji (oparesheni) kwa kwa akinamama wanojifungua kwenye thamnai ya Sh. Milioni tano kwa hospitali ya wilaya ya Mkuranga mkonini Pwani.

Airtel Tunakujali ni programu maalum ambapo wafanyakazi wa kampuni hiyo huchangia sehemu ya kipato chao kwa ajili ya huduma za kijamii zikiwemo afya na elimu.

Akizungumza jijini wilayani Mkurranga wakati wa hafla fupi ya kukabidhi msaada huo wa kitanda mwishoni mwa wiki, Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando alisema kuwa kitengo cha kuhudumia wateja wakubwa Airtel kiliandaa hafla kwa ajili ya kuchangia fedha kwa ajili ya kulipia bima ya afya ya watoto ambao wazazi wao hawana uwezo wa kulipia matibabu na tayari watoto hao washalipiwa bima kwa mwaka mzima.

‘Hapa leo tufanya muendelezo wa kuendelea kusaidia huduma ya afya. Kwa leo tunakabidhi hiki kitanda cha upasuaji kwa akinamama wanaojifungua. Hii inatokana na kuelewa ya kwamba hospitali hii ina changamoto nyingi na upungufu wa vifaa vya hospitali huku hiki kitanda kikiwa ni moja wapo. Sisi Airtel tuna uhakika ya kwamba kitasaidia wale akina mama waliokuwa na utahitaji wa upusuaji lakini wanakosa huduma kama hii. Tunaomba uongozi wa hospitali ukitunze vizuri na sisi Airtel tunahidi kuendelea kusaidia kwenye huduma za afya na zingine zenye kugusa jamii yetu moja kwa moja, Mmbando alisema.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Dkt Stephen Mwandambo mbali na kutoa pongezi kwa Airtel alisema kuwa hospitali ya wilaya ya Mkuranga inakabiliwa na changamoto kadhaa huku akitoa mfano kuwa hospitali hiyo ina uwezo wa kuhudumia wakinamama waokuja kujifungua kwa wastani wa 70 kwa mwezi lakini kwa hali halisi imekuwa ikihudumia 270 mpaka 400.

‘Kulingana na idadi hiyo kubwa ya wakinamama ambao wanapata huduma ya kufingulia kwenye hospitali yetu ya wilaya tumekuwa tukipata changamoto nyingi huku tukiwa na kitanda kimoja tu kwa ajili ya upasuaji. Kwa msaada huu kutoka Airtel itasaidia sana sisi pamoja na kupunguza wa vifo vinavyotokana na kukosa kitanda hiki, alisema Dkt Mwandambo huku akiongeza kuwa hospitali hiyo imekuwa ikitoa huduma ya matibabu kwa wakazi wa wilaya ya Mkurunga asilimia 80 na asilimia 20 wanatoka wilaya za Kibiti na Temeke.

Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Mkurunga Injinia Mshanu Munde akipokea msaada huo kwa niaba ya serikali ya wilaya alitoa pongezi kwa Airtel na hasa wanafanyakazi ambao waliweza kutoa sehemu ya kipato chao na kufanikisha upatikanaji wa kitanda hicho.

Sisi zote tunajua kampuni ya Airtel ni ya kizalendo kwa inamilikiwa na wananchi kupitia serikali yao kwa asilimia 49. Lakini naomba niwapongezi wanafanya kazi kitengo cha kuhudumia wateja wakubwa na uzalendo wao wa kuona umuhimu wa kuimarisha sekta ya afya na kuamua kwa hiari yao kutoa sehemu ya mapato yao na kuweza kufanikisha jambo hilo. Na wakaribisha kwenye wilaya yetu lakini tuna changamoto nyingi kwenye sekta hizi mbili za afya na elimu nawaomba mkipata nafasi siku nyingi kuja na kuendelea kutuunga mkono alisem Injinia Munde.

Meneja wa Kitengo cha kuhudumia wateja wakubwa Airtel Tanzania Alice Maziku akimkabidhi kitanda cha upasuaji Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Mkuranga Injinia Mshanu Munde mwishoni mwa wiki. Kampuni ya Airtel Tanzania kupitia mradi wa AIRTEL TUNAKUJALI ilitoa kitanda cha upasuaji kwa wakinamama wanaojifungua kwa hospitali ya Mkurunga ikiwa ni juhudi za kusaidia jamii iiliyo kwenye mahitaji maalum. Wengine ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Dkt Stephen Mwandambo (kati kati), Meneja Uhusiano Airtel Tanzana Jackson Mmbando (wa kwanza kulia) na katibu wa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Omari Kisali (wa kwanza kulia).
Meneja Uhusiano Airtel Tanzania Jackson Mmbando (kulia) akisalimiana na Injinia Mshanu Munde baada ya Airtel kukabidhi kitanda cha upasuaji kwa hospitali ya wilaya ya Mkuranga mwisho mwa wiki. Airtel ilitoa kitanda hicho kwenye thamani ya Milioni tano ikiwa ni juhudi za kusaidia jamii kupitia mradi wa AIRTEL TUNAKUJALI. Wengine ni Wengine ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Dkt Stephen Mwandambo (kati kati) na katibu wa Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Omari Kisali (wa kwanza kulia).
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images