Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU ATEMBELEA PIRAMIDS MISRI

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akipeana mkono na Mkurugenzi wa Piramidi Ashraf Mohy, wakati alipotembelea Piramidi mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. Tokea kushoto ni Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga, Waziri wa Kilimo na Uhaulishaji wa Ardhi Dkt. Azzeldin Abosteit (katikati) Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akishika jiwe lililotumika kujengea Piramidi, wakati alipotembelea Piramidi hizo, mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa amepanda juu ya Piramidi, akionesha jambo wakati alipotembelea Piramidi hizo, mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa ndani ya Piramidi, wakati alipotembelea Piramidi hizo, mjini Cairo Misri, Julai 9.2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwa anashuka kwenye Piramidi, wakati alipotembelea Piramidi hizo, mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akifurahia jambo, baada ya kutembelea Piramidi, mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiangalia bidhaa za wajasiriamali, baada ya kutembelea Piramidi, mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akitembea nje ya Piramidi, wakati alipotembelea Piramidi hizo mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. kulia ni mwenyeji wake, Waziri wa Kilimo na Uhaulishaji wa Ardhi Dkt. Azzeldin Abosteit. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Mkurugenzi wa Piramidi Ashraf Mohy, wakati alipotembelea Piramidi hizo mjini Cairo Misri, Julai 9.2019. Kulia ni Waziri wa Kilimo na Uhaulishaji wa Ardhi Dkt. Azzeldin Abosteit. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Tanzania Kuendelea Kunufaika Kiuchumi na SADC

$
0
0
Katibu Mkuu mstaafu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Mussa Uledi akiwasilisha mada wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi katika kuandika na kuripoti habari zinazohusu Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) yanayoendelea mjini Morogoro leo Julai 9, 2019 ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo yaliyofunguliwa Julai 8, 2019 na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza. 
Sehemu ya washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi katika kuandika na kuripoti habari zinazohusu Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika yanayoendelea mjini Morogoro leo Julai 9, 2019 ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo yaliyofunguliwa Julai 8, 2019 na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza. 
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari- MAELEZO Bi Zamaradi Kawawa akisisitiza jambo wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi katika kuandika na kuripoti habari zinazohusu Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) yanayoendelea mjini Morogoro leo Julai 9, 2019 ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo yaliyofunguliwa Julai 8, 2019 na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza. 

Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa weledi katika kuandika na kuripoti habari zinazohusu Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) yanayoendelea mjini Morogoro leo Julai 9, 2019 ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo hayo Bi Nelly Mtema akisisitiza jambo wakati wa mafunzo hayo yaliyofunguliwa Julai 8, 2019 na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza..(Picha zote na Abubakari Kafumba, MAELEZO- Morogoro) 
………………… 

Na Frank Mvungi- MAELEZO- Morogoro 
Katibu Mkuu Mstaafu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Mussa Uledi amesema kuwa Tanzania inanufaika kiuchumi kama mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) pamoja na jumuiya nyingine ambazo Tanzania ni mwanachama. 

Akizungumza wakati akiwasilisha mada leo mjini Morogoro ikiwa ni siku ya pili ya mafunzo kwa waandishi wa habari ya kuwajengea uwezo wa kuandika na kuripoti habari za SADC, Bw. Uledi amesema kuwa nchi yetu imenufaika na utekelezaji wa miradi ya miundomnbinu, biashara, uwekezaji na viwanda. 

“ Mkakati wa maendeleo wa SADC unafafanana kwa kiwango kikubwa na ule wa Tanzania ambao pia unazingatia haja ya utekelezaji wa viwanda na miundombinu hapa nchini hali itakayochangia katika kuimarisha maendeleo na kukuza uchuni na ustawi wa wananchi” Alisisitiza Bw. Uledi 
Akifafanua amesema kuwa vipaumbele vya Tanzania vimejikita katika upanuzi wa Mauzo nje na uongezaji wa michepuo yake lengo likiwa ni kukuza na kuendeleza biashara hali inayowezesha uendelezaji wa viwanda vya kuongeza thamani katika malighafi za ndani hususan mazao ya kilimo na madini. 

Aliongeza kuwa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli katika baadhi ya nchi wanachama wa SADC imeonesha kuwa Tanzania imejipanga vizuri kimkakati inaweza kuwa ghala la Chakula kwa kukuza zaidi uzalishaji kuendana na mahitaji katika soko la jumuiya hiyo na hata nje ya jumuiya. 

Alitaja vipaumbele vingine kuwa ni pamoja na uendelezaji miundombinu kama barabara, reli, usafiri wa anga, uzalishaji na usambazaji huduma za umeme ambayo ni nyenzo muhimu sana katika kuyaunganisha masoko ya nchi wanachama wa SADC. 

Aliongeza kuwa vipaumbele vingine ni utafutaji wa rasilimali na utekelezaji wa miradi ya Kikanda kwa kuundwa kwa kikosi kazi cha Mawaziri wenye dhamana ya Fedha na uendelezaji miundombinu, Amani na Usalama umeendelea kuimarika ndani ya SADC. 

Tanzania inatarajiwa kuleta msukumo mpya kwa nchi wanachama wa SADC katika utekelezaji wa miradi na program za maendeleo za Jumuiya hiyo kwa kuwa itakuwa na dhamana kubwa ya kukidhi matarajio makubwa ya nchi wanachama wakati wote wa uenyekiti wake. 

Kwa upande wake Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, Brigedi ya Magharibi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanali Wilbert Ibuge akiwasilisha mada katika mafunzo hayo amesema kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa Barani Afrika zilizotoa mchango mkubwa na kuratibu kuanzishwa kwa mtangamano wa SADC. 

“Hadi sasa hali ya amani na usalama imeendelea kuimarika katika SADC kama inavyojidhihirisha kwa takribani nchi zote za SADC ambapo nchi wanachama ziliazimia kusimamia maendeleo ya kiuchumi ya Kanda kwa kuzingatia malengo ikiwemo kukuza uchumi, kuondoa umasikini, kuboresha hali ya maisha ya wananchi. 

Msingi wa SADC ni kusimamia malengo yake ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii sambamba na yale ya ulinzi na usalama unabainishwa katika Ibara ya 2 ya mkataba wa SADC ( Article 2 of SADC Treaty).

MAFUNZO YA MSASA UWEZESHAJI MASHAMBA DARASA KWA MAAFISA VIUNGO NA MRADI YAENDELEA MJINI MOROGORO

$
0
0
Mafunzo ya Msasa ya Uwezeshaji kuhusu Mashamba darasa kwa Maafisa Viungo wa Mradi kutoka Wizara na timu za uwezeshaji za wilaya wa mradi wa kurejesha ardhi iliyoharibika na kuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini (ldfs) yameendelea leo katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo mkoani Morogoro ikiwa ni siku ya pili.
Pichani washiriki wa mafunzo hayo wakijadili masuala ya mabadiliko ya tabia nchi katika makundi. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI CHATO MKOANI GEITA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia sanamu ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yenye ujumbe maalum kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira ya wanyama pori.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla mara baada ya kumkabidhi Sanamu hiyo ya Baba wa Taifa. Rais Dkt. Magufuli ametoa maelekezo kuwa Sanamu hiyo aliyokabidhhiwa ijengewe eneo zuri katika hifadhi hiyo ya Burigi Chato ili watalii wakija waweze kumjua zaidi Muasisi wa Taifa letu Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. PICHA NA IKULU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla pamoja na viongozi wengine wakivuta  utepe kuashiria uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali, Wakuu wa mikoa, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Dini pamoja na Mabalozi mara baada ya kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Chato kabla ya kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mara baada ya kumkabidhi Hundi ya Shilingi milioni kumi , kama shukrani katika mchango wake alioutoa katika utunzaji wa wa hifadhi mbalimbali ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wafanyakazi wa TANAPA wakati akielekea kwenda kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka mara baada ya kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
 Wakuu wa Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu wakijadiliana jambo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa kabla ya kuanza kwa  sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Kikosi cha Jeshi Usu la kukabiliana na vitendo vya Ujangili pamoja na kulinda hifadhi za taifa kabla ya kuanza kwa  sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi  -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
 Kikosi cha Jeshi Usu cha kukabiliana na Vitendo vya Ujangili pamoja na kulinda hifadhi za Taifa kikipita mbele ya  Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya ukaguzi katika sherehe hizo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Tuzo ya Hifadhi bora ya Serengeti ambayo imekuwa ya kwanza katika Bara la Afrika kwa mwaka 2019 kutoka kwa Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla.

SERIKALI YAPOKEA GAWIO LA SH. BILIONI MOJA KUTOKA TPB BANK

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb) akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi bilioni moja kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB, Dkt. Edmund Mdolwa katika hafla ya kupokea gawio hilo jijini Dodoma. Benki ya Posta imetoa gawio hilo ikiwa ni faida iliyopatikamna mwaka 2018.
Mkurugenzi wa Benki ya Posta Nchini (TPB) Bw. Sabasaba Moshingi akizungumza wakati wa kukabidhi gawio kwa Serikali. Benki hiyo imetoa gawio la Sh. Bilioni moja kwa Serikali ikiwa ni gawio kutokana na faida ya mwaka 2018. Anayefuatia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo Dkt. Edmund Mdolwa. Hafla hiyo imefanyika Jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB, Dkt. Edmund Mdolwa akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi mfano wa hundi ya Sh. Bilioni moja kwa Serikali, hafla hiyo imefanyika Jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb) (kushoto), akiteta jambo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya TPB, Dkt. Edmund Mdolwa (katikati) na Mkurugenzi wa Benki ya Posta Nchini (TPB) Bw. Sabasaba Moshingi baada ya hafla ya kupokea gawio la Sh. Bilioni moja lililotolewa na Benki ya TPB, jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Mb) (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Baadhi ya watendaji wa Benki ya TPB na Wizara ya Fedha na Mipango mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kupokea Gawio toka Benki hiyo jijini Dodoma. Benki ya TPB imetoa Gawio kwa Serikali kiasi cha shilingi bilioni moja ikiwa ni gawio kutokana na faida ya mwaka 2018.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM).



Na Saidina Msangi na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma

Serikali imepokea gawio la Shilingi Bilioni 1 kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB) linalotokana na faida ya uwekezaji wake wa asilimia 83 ya hisa katika Benki hiyo katika mwaka wa fedha 2018/19.

Hafla ya makabidhiano ya Hundi kifani ya gawio hilo imefanyika jijini Dodoma, kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) ambaye alipokea kwa niaba ya Serikali, naMwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo Dkt. Edmund Mndolwa.

Akizungumza katika hafla hiyo Dkt. Mpango aliipongeza Benki hiyo kwa kutoa gawio kwa Serikali, na kuahidi kuwa fedha hizo zitatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

“Utoaji huu wa gawio ni kiashiria tosha kwa Serikali kuwa Benki inazidi kukua na kuwapa moyo watanzania na wawekezaji kuwa TPB inatoa huduma bora katika jamii”, alisema Dkt. Mpango.

Aliitaka Benki hiyo kuongeza wigo wa utoaji huduma ili kuwafikia wananchi hususani waishio vijijini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi hao kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, kukopa sambamba na kurejesha mikopo kwa wakati.

“Riba katika benki zetu bado ni kubwa taasisi za fedha zione namna ya kuzipunguza sambamba na kutoa mikopo kwa kuzingatia kanzidata ya wakopaji ili kuepuka mikopo chechefu.”, alisisitiza Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango ameiagiza Benki hiyo kuendelea kuwapa wanawake kipaumbele katika upatikanaji wa huduma za fedha na mikopo ili waweze kuendesha shughuli za maendeleo.

Pia Dkt. Mpango aliiagiza TPB kusimamia uadilifu kwa watumishi wake na kuwa makini na kutoa taarifa za miamala yenye mashaka ili kuzuia utakasishaji wa fedha haramu.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB Dkt. Edmund Mndolwa alisema kuwa gawio hilo ni sehemu ya faida ya Sh. Bilioni 17.2 kabla ya kodi ambayo Benki yake imeipata katika mwaka wa fedha 2018/19. Pia ameeleza kuwa Benki hiyo itaendelea kutoa huduma bora ili kukidhi mahitaji ya wanahisa wake na wananchi kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Mndolwa aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa utendaji mzuri ambao umeiwezesha Benki hiyo kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kuahidi kuendelea kushirikiana nayo ili kukuza uchumi wa nchi.

KATIBU MKUU JUMUIYA YA MADOLA AKUTANA NA PROF. KABUDI LONDON,UINGEREZA

$
0
0
Jumuiya ya Madola imeonesha kuridhishwa na namna Tanzania inavyotekeleza mageuzi ya kiuchumi,uwajibikaji na uawala bora kwa wananchi wake jambo ambalo jumuiya hiyo inalihimiza na kulisimamia kwa Nchi wanachama wake.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za sekretarieti ya jumuiya hiyo zilizopo London Nchini Uingereza.

Katika mazungumzo hayo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola Bi Patricia Scotland ameeleza kuridhishwa na maelezo yaliyotolewa na Prof. Palamagamba John Kabudi kuhusu utekelezaji wa masuala ya demokrasia,utawala bora na utawala wa sheria pamoja na Haki za binadamu nchini Tanzania na kwamba Jumuiya hiyo inatambua juhudi hizo na inaunga mkono hatua hiyo.

Katibu Mkuu huyo ameongeza kuwa mbali na kuhimiza utekelezaji wa utawala bora,haki za binadamu na utawala wa sheria pia Jumuiya ya Madola imelenga kukuza na kuwezesha biashara miongoni mwa nchi wanachama ikiwa ni pamoja na fursa zilizopo kupitia shirika la biashara la kimataifa (WTO) na mashirikiano ya biashara ya kikanda. 

Amesema ni jukumu la nchi za Jumuiya ya Madola kuhakikisha uwepo wa amani na utulivu katika jumuiya hiyo ili kuiwezesha kupiga hatua za haraka za kimaendeleo na kuifanya Jumuiya nzima kuendelea bila ya kuacha nchi nyingine nyuma kutokana na uwepo wa migogoro ama machafuko ya wenyewe kwa wenyewe miongoni mwa wanachama wa Jumuiya. Katika hili ameisifia Tanzania kwa kuwa na Amani na utulivu muda wote na pia kushiriki katika juhudi za kutatua migogoro kwa nchi zingine wanachama na wasio wanachama wa Jumuiya.

Kuhusu suala la mabadiliko ya tabia nchi,Katibu Mkuu huyo wa jumuia ya madola amesisitiza umuhimu wa ushirikiano miongoni mwa nchi wanachama wa Jumuiya hiyo ili kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi. Ameeleza kuwa Jumuiya hiyo itaendelea kushirikiana na Tanzania katika program mbalimbali zinazolenga kukabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabia nchi na masuala ya mazingira kwa ujumla.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagamba John Kabudi amemhakikishia Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola kuwa Tanzania inaipa umuhimu mkubwa jumuiya hiyo na itaendelea kushirikiana nayo katika masuala ya ukuzaji wa uchumi, utawala bora hususani wakati huu ambapo Tanzania inafanya mageuzi ya kiuchumi katika kuelekea kuwa nchi ya uchumi wa kati.

Ameipongeza jumuiya ya madola kwa mpango maalum inayoandaa kwa ajili ya kukuza na kuongeza biashara baina ya Tanzania na nchi nyingine wanachama wa jumuiya hiyo kwa ujumla jambo ambalo litafungua fursa biashara na masoko kwa bidhaa na mazao ya Tanzania. Amemuahidi Katibu Mkuu huyo kuwa Tanzania itashiriki ipasavyo katika mpango huo.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Kabudi pia amekubaliana na Bi Scotland kuangalia namna ya kuwasaidia vijana kuongeza ubunifu ili waweze kujiajiri na kuimarisha uchumi ili kukabiliana na tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana huku akimpongeza Katibu Mkuu huyo kwa mageuzi makubwa anayoyafanya ndani ya jumuiya hiyo ili iweze kuwahudumia wanachama wake kwa ufanisi zaidi.

Profesa Palamagamba John Kabudi yuko London Nchini Uingereza kwa ziara ya siku nne kuhudhuria mkutano wa Mawaziri wa mambo ya Nje wa Jumuiya ya madola pamoja na mkutano wa Kimataifa kuhusu uhuru wa vyombo vya habari.
 Katibu Mkuu wa jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) alipomtembelea katika ofisi za Sekretarieti za jumuiya hiyo zilizopo London,Uingereza. Kulia ni Balozi wa Tanzania Nchini Uingereza Dkt. Asha-Rose Migiro. July 9, 2019.
 Katibu Mkuu wa jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland akisalimiana na waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika ofisi za Sekretarieti za jumuiya hiyo zilizopo London,Uingereza. July 9, 2019. 
  Katibu Mkuu wa jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika ofisi za Sekretarieti za jumuiya hiyo zilizopo London,Uingereza. July 9, 2019
 Katibu Mkuu wa jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) katika ofisi za Sekretarieti za jumuiya hiyo zilizopo London,Uingereza. July 9, 2019. 
 Katibu Mkuu wa jumuiya ya Madola Bi. Patricia Scotland akimsindikiza mgeni wake ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) alipomtembelea katika ofisi za Sekretarieti za jumuiya hiyo zilizopo London,Uingereza.July 9, 2019.

Wananchi Wajitokeza Kufungua Akaunti Banda la Benki ya Mkombozi Maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es Salaam.

$
0
0
 Meneja wa Huduma za Benki za Kidijitali wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Boniface Thomas (kushoto), akimkabidhi kadi ya akaunti ya akiba mteja mpya Bi. Lusia Benson alipotembelea banda la benki hiyo katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’Jijini Dar es Salaam.
PICHA ZOTE NAPHILEMON SOLOMON

 Meneja wa Huduma za Benki za Kidijitali wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Boniface Thomas (kushoto), akimkabidhi zawadi ya tisheti Bi. Vitoria Silayo  baada ya kufungua akaunti ya akiba  alipotembelea banda la benki hiyo katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’Jijini Dar es Salaam (katika) Meneja Mikopo wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Andrew Chimazi. 
 Afisa Masoko wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Antony Munyambo (kushoto), akimkabidhi kadi ya akaunti ya akiba mteja mpya Bi. Lucy Peter alipotembelea banda la benki hiyo katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’Jijini Dar es Salaam.
 Meneja wa Huduma za Benki za Kidijitali wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Boniface Thomas (kushoto), akimkabidhi kadi ya akaunti ya akiba mteja mpya Bi. Jesinta  Benson alipotembelea banda la benki hiyo katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’Jijini Dar es Salaam.
 Meneja Mikopo wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Andrew Chimazi (kulia), akimuonesha  Bi. Victoria Silayo kipeperushi chenye maelezo ya huduma za kibenki alipotembelea banda hilo kwaajili ya kufungua akaunti maalumu ya akiba .katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Uendeshaji wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Erick Musiba (kulia),akiwaonesha wananchi kipeperushi chenye maelezo ya MWANA ACCOUNT kwa ajili ya watoto walio na umri chini ya miaka kumi na nane, inayomuwezesha mzazi kuweka akiba kwa ajili ya watoto ili kuwajengea tabia ya kujiwekea akiba wanapofikia umri wa kujitegemea.
 Meneja Mikopo wa Benki ya Biashara Mkombozi Bw. Andrew Chimazi (kushoto), akimuelezea mwananchi kuhusina na akaunti ya bima alipotembelea banda hilo katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ‘Sabasaba’Jijini Dar es Salaam.
 Picha ya pamoja.

Vodacom yazindua huduma m pya inayowawezesha wateja wa M-Pesa kutumia pesa zaidi ya kiasi walichonacho kwenye akaunti

$
0
0

Mkurugenzi wa 'M-Commerce' Vodacom Tanzania (Wapili kushoto), Epimarck Mbeteni , Mkuu wa kitengo cha huduma kwa wateja Bi.Herieth Lwakatare (watatu kulia) na Mkurugenzi wa Wateja wa Mikataba (Business Enterprise Unit), Arjun Dhillon (wa kwanza kulia) wakishikana mikono na Mkurugenzi wa Usimamizi wa Hatari na Utekelezaji, Moses Manyatta (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi wa Masoko na Maendeleo ya Biashara, Deogratius Kwiyukwa (watatu kushoto) na Mkuu wa matawi, Bonaventura Paul (wapili kulia) kutoka Tanzania Postal Bank (TPB) , kuashiria uzinduzi wa huduma mpya ya kifedha iitwayo 'M-Pesa songesha' amabayo inawawezesha wateja wa Vodacom Tanzania kutumia fedha zaidi ya kiwango walichonacho kwenye akaunti zao, Dar es Salaam, Jana. Kampuni ya Vodacom imedhamiria kubadili Tanzania kuwa jamii inayofanya malipo kidigitali zaidi.Mkurugenzi wa 'M-Commerce' Vodacom Tanzania, Epimarck Mbeteni akizungumza katika sherehe ya uzinduzi wa huduma mpya ya kifedha itwayo 'M-Pesa songesha' amabayo inawawezesha wateja wa Vodacom Tanzania kutumia fedha zaidi ya kiwango walichonacho kwenye akaunti zao, Dar es Salaam, jana. Kampuni ya Vodacom imedhamiria kubadili Tanzania kuwa jamii inayofanya malipo kidigitali zaidi.


Kampuni inayoongoza nchini kwa huduma za kifedha kwa njia ya mtandao wa simu, Vodacom, leo imezindua huduma ya kwanza na ya kipekee nchini ambayo inaruhusu wateja wa M-PESA kukamilisha miamala wakati hawana fedha za kutosha katika akaunti zao za M-PESA. Uvumbuzi huu wa kibunifu uitwao M-Pesa Songesha umezinduliwa leo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya kampuni hiyo.

Kwa kutumia huduma hii, wateja wa M-Pesa sasa wataweza kutumia huduma hii kwa urahisi zaidi wakiwa na uhakika wa upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kukamilisha miamala yao kama vile kulipia bili, kutuma pesa kwa ndugu jamaa na marafiki au hata kununua bidhaa pasipo kuwa na fedha za kutosha katika akaunti zao.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Mkurugenzi wa M-Commerce, Epimack Mbeteni alisema, "dhamira yetu ya kuleta mifumo bunifu ya kifedha kwa kutumia simu za mkononi ilitupelekea kutazama kwa makini vikwazo vya mara kwa mara vinavyowazuia wateja wetu kukamilisha miamala yao kwa sababu ya upungufu wa fedha katika akaunti zao. Uchunguzi huo umepelekea kuja na ufumbuzi wa kibunifu wa wateja wetu kuweza kukamilisha miamala ya M-Pesa ambayo ingeshindikana kukamilika kwa sababu ya upungufu wa fedha".

Songesha ni moja kati ya huduma nyingi za M-Commerce zilizozinduliwa mwaka huu. Huduma hizi ambazo nyingi zinaendana na maisha ya kidijitali zimewezesha Vodacom kuendelea kuongoza katika huduma za simu na fedha nchini kupitia miamala ya simu, umiliki wa soko na wateja. Katika mwaka wa fedha uliomalizika mwezi Machi mwaka huu, M-Pesa iliongeza umiliki wa soko hadi kufikia asilimia 40 na kuingiza watumiaji zaidi ya milioni 9 katika mifumo rasmi ya kifedha ambao wanafanya miamala ya zaidi ya trilioni 4.1 kwa mwezi.

Watumiaji wa M-Pesa wanaweza kufikia Songesha kwa kupiga namba za huduma ya M-Pesa, *150*00#, kisha kuchagua huduma za kifedha na kujiunga na huduma hiyo ya M-Pesa Songesha. Mara tu baada ya mteja kujiunga na Songesha, atapata ujumbe wa kiwango ambacho anastahili na ataweza kutumia kiwango hicho kukamilisha miamala yake. Kiasi hicho kitarejeshwa pale ambapo mteja atapokea fedha katika akaunti yake ya M-Pesa.

"kiwango hicho kina riba ya asilimia 1 kwa siku 18 na wateja wetu wanaweza kufanya miamala kwa kutumia huduma hii kadri watakavyo ikiwa ni ndani ya kikomo cha kiwango chao. Tumeungana na benki ya TPB kuwezesha huduma hii na ili kuamua kiwango mteja anachostahili, benki itatumia taratibu zilizowekwa kulingana na miamala ya mteja husika katika matumizi yake ya M-Pesa" alisema Epimack.

Akiongea kuhusu huduma hii mpya, kaimu Afisa mtendaji mkuu wa TPB Bank Moses Manyatta alisema, “lengo letu kama benki ni kuhamasisha huduma jumuishi za kifedha huku tukiwahamasisha Watanzania kujenga tabia ya kujiwekea akiba na kujipatia mikopo kwa urahisi, Songesha ni kila kitu na inapatikana masaa 24 kwa siku saba kupitia simu yako ya mkononi! Tunajivunia kuwa na uhusiano huu na tuna Imani kwamba mapinduzi haya yatasaidia katika huduma jumuishi za kifedha,” alisema.

"Tunaendeleza nia ya kubadili Tanzania kuwa jamii inayofanya malipo kidijitali, tunawekeza katika teknolojia ya simu ambayo itaingiza watu wengi zaidi katika mifumo ya kifedha na hatimaye, kufikia malengo ya kijamii na kiuchumi ya nchi." alielezea Mbeteni.

Wafanyabiashara waaswa kutumia Fursa kutoka NMB kuendeleza biashara zao

$
0
0
Mbunge wa jimbo la Babati Mjini,Pauline Gekul amewataka wafanyabiashara kutumia fursa ya kuendeleza biashara zao baada ya serikali kuondoa mlolongo wa tozo mbalimbali zilizokua zikitozwa na Mamlaka ya Mapato(TRA) kabla ya kufungua biashara.

Akizungumza katika mkutano uliondaliwa na benki ya NMB kwa wafanyabiashara mkoani Manyara(NMB Business Club) mjini Babati alisema waache kulalamikia mazingira ya biashara kwani katika bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020 serikali imesikiliza kilio chao.

“Nawapongeza NMB kuwa na utaratibu wa kukutana na wafanyabiashara na kuwapa maarifa ya mikopo na kukuza biashara zenu,naamini mtaendelea kutoa mikpo zaidi kwa wananchi wangu ili waweze kujiletea maendeleo kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi,”alisema Gekul

Meneja Mwandamizi wa NMB Wogofya Mfalamagoha alisema NMB ipo tayari kuwahudumia wafanyabiashara wa ngazi zote kutokana na mtandao uliosambaa nchini nzima ikiwa na matawi zaidi ya 228 na mawakala 6,800.

“NMB ina wafanyabiashara zaidi ya 200,000 nchi nzima ambao wamechukua mikopo yenye thamani ya Sh 600 bilioni,mtakubaliana name kuwa mikutano ya wafanyabiashara ambayo tunaifanya kuwaelimisha mambo ya biashara imekua na tija kwetu sote,”alisema Mfalamagoha

Aliwataka wafanyabiashara kutokutanguliza dhamana zao wanapotaka kuchukua mikopo bali wazo la biashara ambalo linaweza kuwaletea faida kwani benki haipendi kuuza dhamana za wateja baada ya kushindwa kurejesha mikopo waliyochukua.

Alisema shughuli za wafanyabiashara wadogo na kati ni muhimu sana katika kukuza uchumi wa nchi ikizingatiwa kuwa uchumi kwa ujumla wake unategemea mafanikio ya shughuli za kibiashara zinazofanywa na wafanyabiashara wadogo na kati nchini na duniani.

“Lengo la kukutana nanyi ni kuhakikisha mnakuza mitaji yenu, kutoa ajira kwa watanzania wengi zaidi na kuchangia uchumi kupitia ulipaji wa kodi na kwamba NMB imejipanga kuhakikisha inatoa huduma bora kwa jamii ya wafanyabiashara katika makundi yao,”alisema Mfalamagoha

Mwenyekiti wa wafanyabiashara(NMB Business Club) Mkoa wa Manyara, Ally Msuya alisema wamekua na mahusiano mazuri na NMB hiyo kupitia umoja wao ambao wameutumia kutatua changamoto za wafanyabiashara wanaochipukia na wenye uzoefu wa muda mrefu.

Mfanyabiashara Ophii Urasa akizungumza wakati wa mkutano wa NMB(NMB Business Club) na wafanyabiashara wanaonufaika na mikopo ya benki hiyo kwa wilaya za Babati, Hanang na Mbulu mkoani Manyara.
 Meneja Mwandamizi Uhusiano Kitengo cha Biashara Benki ya NMB, Wogofya Mfalamagoha akizungumza wakati wa mkutano wa NMB na Wafanyabiashara (NMB Business Club) mjini Babati Mkoani wa Manyara. 
 

TANTRADE KUENDELEA KUJENGA MAZINGIRA WEZESHI KWA WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI WADOGO NCHINI.

$
0
0


MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) imesema itaendelea kuimarisha mitandao ya wadau na makampuni mbalimbali wafanyabiashara ili kuhakikisha kuwa wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo nchini wanapatiwa fursa za masoko ili kuweza kukuza sekta ya biashara nchini. 

Hayo yamesemwa leo Alhamisi (Julai 11, 2019) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TANTRADE Zanzibar, Latifa Khamis wakati wa mkutano wa ana kwa ana baina ya wafanyabiashara, wazalishaji na wanunuzi wa bidhaa za ngozi na shule katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika Viwanja vya Julius Nyerere. 

Latifa alisema kuwa Serikali kupitia TANTRADE itaendelea kutumia majukwaa na fursa mbalimbali za kibiashara kwa ajili ya kuwawezesha wajasirimali na wafanyabiashara kuweza kutumia fursa zilizopo ikiwemo kupata masoko ya uhakika ya biashara zao kupitia kwa wadau mbalimbali waliopo ndani na nje ya nchi. 

“TANTRADE imeandaa mkutano huu maalum kwa ajili ya kuwasaidia wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo kuweza kupata fursa za masoko ya kuuzia masoko yao ambapo utaratibu huu utakuwa endelevu, hivyo kampuni ya DHL kupitia Market Plaze Africa wametoa fursa kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wa hapa nchini kutangaza biashara zao” alisema Latifa. 

Aidha Latifa alisema mara baada ya kuisha kwa maonyesho ya 43 ya DITF, TANTRADE imeandaa mkakati maalum wa kuwaunganisha wajasiriamali wadogo na wafanyabiashara kupitia maonesho ya bidhaa za wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo nchi nzima ambapo wataanzia katika Mkoa wa Ruvuma na baadae Zanzibar. 

Aidha Latifa alisema katika mkutano huo pia TANTRADE imewakutanisha wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo na taasisi mbalimbali za kifedha ikiwemo Benki ya NMB ambayo imekuwa na utaratibu wa kutoa mikopo kwa wajasiriamali kuanzia kiwango cha Tsh 500,000 hadi Milioni 50,000,0000. 

Kwa upande wake Meneja Mkazi wa Kampuni ya DHL Tanzania, Paul Makolosi aliwataka wajasirimali na wafanyabiashara wadogo kutangaza bidhaa zao katika taasisi hiyo kwa kuwa masoko ya bidhaa zao yapo kwani nchi nyingi za mabara ya Ulaya na Amerika yamekuwa wakivutiwa na bidhaa zinazozalishwa katika nchi za Bara la Afrika ikiwemo Tanzania. 

Aliongeza kuwa taasisi hiyo ina uzoefu wa miaka 30 ya kufanya biashara duniani, ambapo katika utendaji kazi wake imekuwa ikiwasaidia zaidi wajasiriamali wadogo waliopo katika Bara la Afrika, hivyo ujio wa taasisi hiyo hapa nchini ni fursa kwa wajasiriamali na wafanyabiashara hao. 

“Katika Nchi za Bara la Ulaya na Amerika, bidhaa za ngozi hususani viatu vimekuwa na soko kubwa sana, na kwa kuwa wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo wa hapa Tanzania wamekuwa wakizalisha bidhaa hiyo, sisi DHL kupitia Market Place Africa tupo tayari kuwasaidia ili kupata masoko ya uhakika” alisema Makolosi.

RAIS DKT. MAGUFULI AZUNGUMZA NA WANANCHI WA KYAKA, RWAMISHENYE, KEMONDO NA MULEBA WAKATI AKITOKEA KARAGWE MKOANI KAGERA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Muleba wakati akitoka nyumbani kwa marehemu Mhandisi Leopard Mjungi ambaye alikuwa Mkurugenzi wa barabara Kuu wa Wizara ya Ujenzi. PICHA NA IKULU
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Rwamishenye wakati akitokea Karagwe mkoani Kagera
 . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiandika kero mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na wananchi wa Muleba mkoani Kagera wakati akielekea Chato mkoani Geita.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza wananchi wa Muleba Mjini mkoani Kagera wakati walipokuwa wakielezea changamoto  mbalimbali zinazowakabili.
 Mtume Venon Fernandes wa Kanisa la Agape akiwa pamoja na wananchi wa Rwamishenye wakifurahia wakati wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli wakati aliposimama katika eneo hilo na kuwasalimu.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mtume Venon Fernandes wa Kanisa la Agape katika eneo hilo la Rwamishenye wakati akielekea Chato mkoani Geita.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiombewa na Mtume Venon Fernandes wa Kanisa la Agape pamoja na wananchi wa Rwamishenye Bukoba mkoani Kagera mara baada ya kuzungumza nao wakati akitokea Karagwe.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Kemondo nje kidogo ya Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka katika eneo la Muleba mjini mara baada ya kuzungumza na wananchi wa eneo hilo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisali mbele ya Kaburi la Marehemu Mhandisi Leopard Mjungi ambaye alikuwa Mkurugenzi wa barabara Kuu kutoka Wizara ya Ujenzi.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza nyumbani kwa marehemu Mhandisi Leopard Mjungi ambaye alikuwa Mkurugenzi wa barabara Kuu kutoka Wizara ya Ujenzi mara baada ya kuwasili kijijini hapo Muleba mkoani Kagera. Marehemu Mhandisi Mjungi alifariki mwaka 2007. 

BALOZI SEIF ALI IDDI AITAKA TANTRADE KUIMARISHA MITANDAO YA KUWASAIDIA WAFANYABIASHARA

$
0
0
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akimkabidhi cheti cha ushindi mmoja wa washiriki wa makampuni kutoka nchini Rwanda, wakati wa hafla kufunga Manoesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11, 2019)yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi, Balozi Seif Alli Idd akimkabidhi cheti cha ushindi mmoja wa washiriki wa makampuni yaliyoshiriki katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam wakati hafla kufunga maonesho hay oleo Alhamisi (Julai 11, 2019) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Alli Idd akimkabidhi cheti cha ushindi Afisa Habari Mwandamizi wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi Dorina Kaaya wakati wakati wa hafla kufunga Manoesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11, 2019)yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Alli Idd akimkabidhi cheti cha ushindi mmoja wa washiriki kutoka Kampuni ya uzalishaji maziwa ya Asasi Diaries wakati wakati wa hafla kufunga Manoesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11, 2019)yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.

Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa akizungumza wakati wa hafla ya kufunga Manoesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere leo Alhamisi (Julai 11, 2019). 
(PICHA NA PASCHAL DOTTO-MAELEZO) 

………………………… 
Na Mwandishi Wetu,MAELEZO 
DAR ES SALAAM 

MAKAMU wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Iddi ameitaka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) kuendelea kuimaisha mitandao na mifumo ya biashara nchini ili kuwawezesha wafanyabiashara wa Tanzania kuweza kuwa na uhakika wa masoko bora ya bidhaa za ndani na nje ya nchi. 

Akifunga Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) leo Alhamisi (Julai 11, 2019) Balozi Idd alisema Maonesho hayo ya mwaka huu yameonesha dhamira na mwelekeo wa Serikali katika kutumia fursa biashara na viwanda katika kujenga uchumi imara pamoja na kutengeneza ajira kwa wananchi. 

Balozi Idd alisema ni wajibu wa TANTRADE kutumia fursa za uwepo wa makampuni ya wazalishaji, wauzaji na wafanyabiashara kutoka nje wanaoshiriki katika maonesho hayo kuweza kujenga mitandao imara ya mahusiano na ushirikiano kwa wafanyabiashara wa ndani ili kuweza kuwatafutia masoko ya bidhaa zao ambazo kwa sasa zimeanza kuzalishwa katika viwango bora nchini. 

“Nawapongeza TANTRADE kwa juhudi zenu za kuanzia klinilki za biashara, na hili limewezesha wafanyabiashara wetu kuweza kukutana na wanunuzi mbalimbali ambao huweza kuwapa uzoefu wa namna bora zaidi ya kuzalisha bidhaa zenye kukithi viwango na ubora unaotakiwa” alisema Balozi Idd. 

Aidha Balozi Idd alisema Serikali kwa sasa inatekeleza Mpango Kazi wa Kuboresha Mfumo Udhibiti wa Biashara Nchini (Blue Print), ambao umekusudia kuondoa changamoto mbalimbali za wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi, hivyo aliitaka TANTRADE kushirikiana na wadau na wazalishaji wa sekta binafsi ili kuiwezesha sekta ya biashara kuvutia wawekezaji wengi zaidi. 

Kwa mujibu wa Balozi Iddi pia aliitaka TANTRADE kuweka utaratibu wa kufuatilia oda za maombi mbalimbali zinazotolewa na wafanyabiashara kutoka nje ya nchi ili kuendelea kupanua wigo wa soko la bidhaa za Tanzania nje ya nchi ambalo kwa sasa limeendelea kupanuka kutokana na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali. 

Balozi alisema ni wajibu wa Watanzania kujenga utamaduni wa kuthamini bidhaa za ndani ili kuziwesha kupata masoko ya uhakika kwa kuwa kwa kufanya hivyo kutatoa fursa ya kuweza kutambulika kwa haraka pamoja na kumudu changamoto ya ushindani wa masoko ya bidhaa zinazozalishwa nje ya nchi. 

Alisema kuwa maonesho hayo ya 43 yamethibitisha uwezo wa wafanyabiashara wa Tanzania katika kutengeneza na kuzalisha bidhaa mbalimbali kwani idadi ya washirki wa maonesho kutoka nje ya nchi imeweza kuongezeka kutoka makampuni kutoka nje 2956 mwaka 2018 hadi kufikia 3250 mwaka 2019, hivyo kudhibitisha uwezo wa serikali katika kusimamia sekta ya biashara nchini. 

Balozi Idd anasema kuwa Makampuni ya wafanyabiashara ya Tanzania yaliyoshiriki maonesho hayo yanapaswa kupata uzoefu na uelewa mkubwa katika namna bora zaidi ya kusimamia na kuratibu sekta ya biashara nchini katika viwango bora ili kuweza kutengeneza masoko ya uhakika katika nchi za nje. 

Kwa upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa alisema Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya biashara nchini ikiwemo kuanza kufanya mapitio ya sera na sheria mbalimbali ambazo awali zilikuwa zikileta changamoto mbalimbali kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi. 

Aliongeza kuwa katika kuhakikisha kuwa sekta ya viwanda na biashara inaleta tija katika ukuaji uchumi nchini, Serikali imekusudia kuweka msisitizo katika kujenga uchumi jumuishi kwa kuziweka sekta ya uvuvi, kilimo na mifugo kuwa kipaumbele muhimu katika kuzitumia rasilimali mbalimbali zilizopo katika sekta hizo katika kutengeneza ajira kwa wananchi walio wengi.

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ZANZIBAR ATEMBELEA BANDA LA NMB SABASABA

$
0
0

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Zanzibar, Mheshiwa Hamis Hafidh Hassan akisaini kitabu cha wageni ndani ya Banda la Benki ya NMB kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Zanzibar, Mheshiwa Hamis Hafidh Hassan (kushoto) akiwa ndani ya Banda la Benki ya NMB alipotembelea banda hilo kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea viwanja vya Sabasaba. Kulia ni Kaimu Meneja wa Banda la Benki ya NMB kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa, Bi. Saumu Mohamed Mollel akiwa na mgeni wake.
Kaimu Meneja wa Banda la Benki ya NMB kwenye Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa, Bi. Saumu Mohamed Mollel (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Zanzibar, Mheshiwa Hamis Hafidh Hassan alipotembelea Banda la NMB Sabasaba.
Wateja mbalimbali wa Benki ya NMB wakipata huduma ndani ya Banda la Benki hiyo walipotembelea Maonesho ya 43 ya Biashara Kimataifa yanayoendelea viwanja vya Sabasaba.

WIZARA YA MADINI KUFUTA LESENI ZOTE AMBAZO HAZIFANYI KAZI NA KUWAPA WACHIMBAJI WADOGO

$
0
0

Afisa Mkuu wa Wateja Wadogo na Kati wa NMB Filbert Mponzi (kushoto) akimpa mkono Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo baada ya kuzungumza na wachimbaji wadogo wa madini wa mkoa wa Geita, kwenye jukwaa la mtaji wa Maendeleo, katikati ni Mkuu Mkoa wa Geita- Robert Gabriel.


Meneja wa NMB kanda ya Ziwa - Abraham Augustino akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini.
 
Geita. Wizara ya madini nchini imesema itaendelea kuzifuta leseni zote za utafiti ambazo hazifanyiwi kazi na zile ambazo hazilipiwi na kuwapatia wachimbaji wadogo hili waendelee kuzifanyia kazi ambazo zitasaidia kuinua uchumi wa nchi na kuzalisha ajira kwa vijana na watu ambao wanazunguka maeneo hayo.



Hayo yamesemwa Jana na Naibu waziri wa Madini Staslaus Nyongo wakati wa ufungaji wa Kongamano la Jukwaa la mitaji na maendeleo Mkoani Geita lililodhaminiwa na Benki ya NMB ambalo limefanyika kwa siku tatu kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mji wa Geita.

Amesema Wizara imejidhatiti kuendelea kutoa maeneo ambayo yataongeza uzalishaji kwa wachimbaji wadogo na kwamba wanataka kuona wachimbaji wadogo wanainuka kiuchumi ili waweze kulipa mrabahaa wa serikali pamoja na kodi.

“Sisi kama wizara hatutakaa kimya kuona namna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakipatiwa maeneo kwa ajili ya kufanya utafiti wanakaa nayo bila ya kuyashughulikia tutaendelea kuyataifisha maeneo hayo na kuwapa wachimbaji wadogo hili waweze kuinua vipato vyao”Alisema Naibu waziri Nyongo.

Aidha Waziri Nyongo aliishukuru Benki ya NMB kwa namna ambavyo imeendelea kuwa mstari wa mbele kuwasaidia wachimbaji wadogo ikiwa ni pamoja na kufadhili Kongamano hilo ambalo limedumu kwa siku tatu na kwamba anaamini elimu ambayo wameipata itawasaidia kuweka akiba na kujulikana shughuli ambazo wanazifanya ili iwe Rahisi kupatiwa Mikopo.

Mkuu wa Mkoa huo,Robert Gabriel alisema mkoa huo bado unakabiliwa na changamoto kubwa ya uhaba wa maeneo ya uchimbaji na kwamba ni vyema sasa kwa wizara kutuma wataalamu ambao wataweza kuja na kuona namna ambavyo watawasaidia kupata maeneo mengine ya uchimbaji.

Filbert Mponzi, ambaye ni afisa mkuu wa wateja wadogo na wakati NMB alisema Benki hiyo inatambua mchango wake mkubwa kwa jamii wakiwemo wachimbaji wadogo na ndio sababu ambayo imepelekea kufadhili semina hiyo ya siku tatu.

“Imani yetu ni kwamba maelekezo na elimu ambayo tumeitoa naamini wachimbaji wadogo wakiifanyia kazi sisi tupo tayari kuwakopesha tulikuwa tunashindwa kutokana na namna ambavyo walikuwa wakihama hama lakini naamini maelekezo tuliyowapa watayatekeleza”Alisema Filbert

Baadhi ya wachimbaji wadogo Mkoani humo,wameishukuru Benki ya NMB kuwa tayari kuwakopesha kwenye shughuli zao na kwamba kupitia mikopo ambayo watapatiwa itawasaidia kwa kiasi kuboresha shughuli zao za uchimbaji ambazo wamekuwa wakizifanya kila siku.

Vodacom donated 300 desks in Bariadi District benefiting more than 400 students

$
0
0
Bariadi-Simiyu: Vodacom Tanzania has donated 300 desks worth TZS 61,360,000 to Salunda and Somanda primary schools in Bariadi, Shinyanga, at a handover ceremony held at Sengerema Primary School that was witnessed by Bariadi District Commissioner, Festo Kiswaga. The move is in support of the government’s effort to curb the existing shortage of desks in primary schools and increase availability of basic school infrastructure countrywide.

Speaking during the ceremony, DC Festo Kiswaga said the 300 desks will greatly improve access of learning facilities as well as the learning condition for children in Bariadi, and called upon other well-wishers to come forward and join the effort to offset the remaining shortage of desks in the District.

“As we all know, education is an instrumental vehicle of development. We sincerely want to thank Vodacom for supporting us in our effort to improve access of learning facilities and offset the existing shortage of desks in schools here. We believe these 300 desks will go a long way in enabling hundreds of children with a conducive environment needed for effective learning.” Kiswaga said.

Vodacom Tanzania Lake Zone, Head of Consumer Business Department, Dominician Mkama, said the donation is in line with the company’s vision of being a purpose led brand and the new Vodacom Tanzania Foundation’s strategy of contributing towards fostering Tanzania human development through inclusive and quality education.

“Education is a fundamental human right and a key aspect of achieving the Sustainable Development Goals. The donation is part of Vodacom’s investment in human development projects that have high impact to the community. Through this donation, Vodacom is playing a key role in shaping the future leaders, doctors, engineers and other experts of this country” Mkama said.

He added that the company has been actively engaging with communities and collaborating with social partners to tackle national challenges including education and last year, they were able to reach 60,023 students through Instant schools’ platform. Vodacom continues to support government’s effort to make education accessible and conducive for every child in Tanzania under the country’s Development Vision 2025.



Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Festo Kiswaga (Kushoto) akipeana mkono na Meneja mauzo mwandamizi wa Vodacom Tanzania kanda ya ziwa, Ahmed Akberali (Kulia) katika hafla ya kukabidhi madawati 300 yenye thamani ya TZS millioni 61 yaliyotolewa na taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation kwa ajili ya shule ya msingi ya Salunda na Somanda jana, Dutwa wilayani humo. Taasisi hiyo imetoa msaada wa madawati ikiwa ni njia mojawapo ya kuisaidia serikali kupunguza uhaba wa madawati katika shule za msingi nchini.
Wanafunzi wa shule ya Msingi ya Salunda na Somanda wakiwa wamekalia madawati yaliyokabidhiwa na Taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation, jana wilayani Bariadi mkoani Simiyu. Taasisi hiyo imetoa madawati 300 yenye thamani ya TZS milioni 61 kwa shule hizo ikiwa ni njia mojawapo ya kuisaidia serikali kupunguza uhaba wa madawati katika shule za msingi nchini.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA VIET NAM,AWAKARIBISHA KUWEKEZA BANDARI,USAFIRI WA ANGA NA KILIMO.

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung, katika mazungumzo ya faragha yaliyofanyika ofisini kwa Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 12, 2019 
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung (wa pili kulia) katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 12, 2019. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung (kulia) katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 12, 2019. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi zawadi ya picha ya Mlima Kilimanjaro, Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung, baada ya mazungumzo yao, ofisini kwa Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam, Julai 12, 2019. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam, Trinh Dinh Dung wakitoka ofisini kwa Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es salaam baada ya mazungumzo yao, Julai 12, 2019. 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu wa Vietnam,Trinh Dinh Dung wakigonganisha glass katika chakula cha mchana alichoandaa Waziri Mkuu wa Tanzania kwa heshima ya mgeni huyo kwenye hoteli ya Hyatt Regency- Kilimanjaro jijini Dar es salaam, Julai 12, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
)
*Awakaribisha Waviet Nam waje kuwekeza katika bandari, usafiri wa anga na kilimo 


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekuna na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu wa Viet Nam, Trinh Dinh Dung na amewakaribisha wawekezaji kutoka Viet Nam waje kuwekeza kwenye maeneo mbalimbali yakiwemo ya mipango miji, madini, bandari, usafiri wa anga, ufundi stadi, kilimo pamoja na uvuvi. 

Amesema kuwa anatambua kwamba nchi ya Viet Nam inafanya vema katika suala la mazao ya kilimo kwa kuongeza tija kwenye mazao hayo na kukifanya kilimo kuwa cha biashara, hivyo amezialika kampuni za Viet Nam zenye teknolojia mahsusi katika maeneo tajwa ili kushirikiana na Tanzania katika mikakati yake ya kuendeleza kilimo. 

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Julai 12, 2019) wakati wa mkutano wake na Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Viet Nam , ambapo ametumia fursa hiyo kumuhakikishia kwamba Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano wake na Viet Nam kwa manufaa ya watu wa nchi mbili hizo. 

Amesema uwepo wa kampuni ya Viettel PLC (Halotel) ya kutoka nchini Viet Nam ni ishara tosha ya imani ya uwekezaji iliyopo kwa wawakilishi wa Viet Nam. “Nawakaribisha sana wawekezaji kutoka Viet Nam kuja kuwekeza Tanzania kwani kwa kufanya hivyo hawatojutia uamuzi wao wa kuwekeza Tanzania.” 

Waziri Mkuu amesema Viet Nam imeendelea kuwa mshirika muhimu wa kiuchumi kwa Tanzania, hivyo ametumia fursa hiyo kuishukuru Serikali ya Viet Nam kwa kuendelea kuunga mkono Serikali ya Tanzania katika jitihada za kuwaletea wananchi wake maendeleo. 

“Kwa mfano, kampuni ya mawasiliano ya Viettel PLC (maarufu kama Halotel) ambayo imewekeza nchini tangu mwaka 2014 inafanya vizuri katika sekta ya mawasiliano. Kampuni hiyo, imewezesha mawasiliano ya simu kuwafikia Watanzania wengi hususan wale waishio vijijini.” 

Waziri Mkuu amesema kampuni hiyo ya Halotel imeweza kuzalisha ajira takriban 1,600 za moja kwa moja kwa wazawa na ajira takriban 100,000 zisizokuwa za moja kwa moja hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2018; 

Amesema lengo la Serikali ya Tanzania ni kuendelea kushirikiana na Serikali ya Viet Nam katika masuala ya mawasiliano na masuala mengine ikiwemo biashara na uendelezaji na masoko ya mazao ya kilimo hususan korosho, kahawa, kilimo mseto cha mpunga na uvuvi wa samaki ambako Viet Nam inafanya vizuri zaidi. 

Akizungumzia kuhusu sekta ya utalii, Waziri Mkuu amesema Tanzania ni nchi nzuri, watu wake ni wakarimu na pia imebarikiwa vivutio vingi vya utalii. Hivyo, amezikaribisha kampuni za Viet Nam kuja kuwekeza katika sekta ya utalii na utamaduni nchini. 

“Halikadhalika, sina shaka kwamba wengi wenu mmewahi kusikia kuhusu Visiwa vya Zanzibar, Mlima Kilimanjaro, pamoja na Mbuga za Serengeti na Ngorongoro. Hivyo ni baadhi tu ya vivutio vingi vya utalii tulivyojaliwa kuwa navyo nchini mwetu.” 

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Viet Nam, Trinh Dinh Dung ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushgirikiano na kwamba ameomba ushirikiano huo uimarishwe kupitia ziara za viongozi wa wakuu wa nchi mbili hizo. 

Naibu Waziri Mkuu huyo wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Viet Nam, amemuhakikishia Waziri Mkuu kwamba Serikali ya Viet Nam itazidi kuimarisha ushirikiano wake na Serikali ya Tanzania hususani katika sekta za kilimo, biasdhara na uvuvi. 

Kadhalika kiongozi huyo amesema kuwa nchi ya Viet Nam iko tayari kununua mazao mbalimbali ya kutoka nchini Tanzania yakiwemo ya korosho na pamba. Amesema lengo la Serikali yao ni kuhakikisha kwamba biashara kati ya Tanzania na Viet Nam inafikia dola bilioni moja ifikapo 2020.

UINGEREZA YAAHIDI KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA TANZANIA

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje wa Uingereza, Mhe. Harriett Baldwin,London Uingereza. July 12, 2019 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje wa Uingereza, Mhe. Harriett Baldwin mara baada ya kumaliza kufanya mazungumzo baina yao kuhusu masuala mbalimbali kati ya Tanzania na Uingereza. Mazungumzo hayo yamefanyika London Uingereza. July 12, 2019. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje wa Uingereza, Mhe. Harriett Baldwin mara baada ya kumaliza kufanya mazungumzo baina yao kuhusu masuala mbalimbali kati ya Tanzania na Uingereza. Mazungumzo hayo yamefanyika London Uingereza. Pembeni kushoto ni Balozi wa Tanzania Nchini Uingereza Dr. Asha -Rose Migizro. July 12, 2019. 

************** 

Uingereza imeihakikishia Tanzania kuwa itaendelea kuwa mshirika wake katika masuala mbalimbali ya ubia wa maendeleo ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wawekezaji wengi kutoka Uingereza kuwekeza Tanzania kama moja ya hatua za kuiunga mkono Serikali ya Awamu ya Tano ili iweze kufikia azma yake ya kuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda ifikapo 2025. 

Waziri wa Masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza katika Idara ya Ushirikiano wa Maendeleo, Mhe. Harriett Baldwin ameyasema hayo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi, Jijini London, Uingereza kwa nia ya kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo na ushirikiano baina ya Tanzania na Uingereza. 

Katika mazungumzo hayo Waziri Harriett na Prof. Kabudi wamezungumzia kuhusu hali ya ushirikiano wa ubia wa maendeleo uliopo hivi sasa na kuonesha kuridhishwa na Serikali ya Tanzania inavyosimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofadhiliwa na Serikali ya Uingereza katika sekta za elimu,afya, maji, kilimo pamoja na miundombinu ya barabara hususani vijijini ikiwemo maboresho ya mifumo ya fedha,utumishi wa umma, serikali za mitaa miongoni mwa miradi mingine mingi. 

Pia, Waziri Harriett ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika kupambana na rushwa,kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma katika sekta ya umma, kuongeza uwajibikaji na utawala bora mambo aliyoyataja kama hatua muhimu ya kufikia malengo ya haraka na kuondoa umasikini. 

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba John Kabudi ameishukuru Serikali ya Uingereza kwa kuwa mbia mkubwa wa maendeleo na kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa uwekezaji,biashara na utalii nchini Tanzania. 

Aidha, Prof Kabudi amemhakikishia Waziri Harriett nia thabiti ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kufanya mageuzi muhimu ya kiuchumi na kiutawala yanayolenga kuifikisha Tanzania katika mojawapo ya nchi za uchumi wa kati. 

Miongoni mwa maboresho hayo, Waziri Kabudi ameyataja kuwa ni pamoja na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na biashara,maboresho katika usimamizi wa utendaji wa Serikali katika kuwahudumia wananchi na utoaji huduma za kijamii hususani sekta zinazowagusa wananchi wengi hususani wa kipato cha chini. 

Akihitimisha mazungumzo hayo Waziri wa masuala ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza, Mhe. Harriett Baldwin amemhakikishia Waziri Kabudi kuwa Uingereza inafuatilia kwa ukaribu mageuzi na maboresho ya kiutendaji yanayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli yakiwemo, kuimarisha mazingira ya uwekezaji na biashara,kukuza demokrasia na utawala bora na hivyo Tanzania itegemee ongezeko la wawekezaji kutoka Uingereza.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 13,2019

RAIS WA UGANDA YOWERI KAGUTA MUSEVENI AREJEA NCHINI KWAKE MARA BAADA YA ZIARA YAKE YA SIKU MOJA CHATO MKOANI GEITA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku moja Chato mkoani Geita
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati akiagana na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku moja Chato mkoani Geita.
 Rais wa Uganda Yoweri Museveni akizungumza na wananchi wa Nyabilezi kabla ya kuondoka na kurejea nchini kwake Uganda. Rais Museveni ameahidi kujenga madarasa saba kwa ajili ya Shule ya Msingi Nyabilezi Chato mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakati akielekea kupanda ndege mara baada ya kumaliza ziara yake ya siku moja Chato mkoani Geita.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Chato mkoani Geita. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia kwaya ya watoto wa Shule ya Msingi Kalembo Umitashunta mara baada ya kumsindikiza mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia kwaya pamoja na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakati akimsindikiza . PICHA NA IKULU
 


MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 14,2019

Viewing all 46343 articles
Browse latest View live


Latest Images