Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live

RAIS DKT. MAGUFULI MGENI RASMI KWENYE MASHINDANO MAALUMU YA 20 YA QUR-AAN AFRIKA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM MEI 19, 2019

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa kaongozana na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry bin Ally akiwasili kuwa mgeni rasmi kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi mara baada ya kuwasili kuwa mgeni rasmi kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa na Raisi wa Taasisi ya Al Hikma Foundation Sheikh Shariff Abdulqadir (kushoto) na Waziri wa TAMISEMI wa Saudi Arabia Sheikh Dkt. Swaleh al Sheikh mara alipowasili kuwa mgeni rasmi kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili kuwa mgeni rasmi kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Mohamed Ghalib Bilali mara baada ya kuwasili kuwa mgeni rasmi kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa meza kuu wa viongozi wengine wakati wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry bin Ally  wakati wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
 Sehemu ya maelfu ya waumini waliohudhuria kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
 Sehemu ya wadau wakati wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Maelfu ya waumini waliohudhuria kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akwa meza kuu na  Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa,  Rais MStaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete pamoja na Raisi wa Taasisi ya Al Hikma Foundation (kushoto kwake) na Waziri wa TAMISEMI wa Saudi Arabia Sheikh Dkt. Swaleh al Sheikh (wa tatu kulia) akifuatilia  mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiteta jambo na Rais wa Taasisi ya Al Hikma Foundation (kushoto)wakati wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  na meza kuu wakimsikiliza  Sheikh Nurdeen Kishk, Mratibu Mkuu wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
 Sehemu ya Wafadhili wakuu wa Mshindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Taasisi ya Al Hikma Foundation Sheikh Shariff Abdulqadir akihutubuia kwenye mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Wafadhili wakuu wa wakitambulishwa baada ya kufanikisha mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akifuatilia mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akifuatilia mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akihutubia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine wakati akihitimisha mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akielekea sehemu ya kutolea zawadi  baada ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akipungia maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine baada ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiislamu ya Amana Dr. Muhsin Salim Masoud ambapo Benki hiyo ndiyo ilikuwa wadhamini wakuu wa mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Mwakilizshi wa Kituo cha Televisheni cha ZBC Bw. Mehbooud Al Haddad kwa kuwa mmoja wa wadhamini  mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia  Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Ali Hassan Mwinyi kwa kuwa mlezi wa mashindano hayo ya Qur’aan Tukufu Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa kwa kuwa mdau mkubwa wa mashindano hayo ya Qur’aan Tukufu Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeiry bin Ally  wakati wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Bi. Sumayyah Juma Abdallah wa Tanzania baada ya kupata alama 98.66 na kuibuka mshindi wa tano wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalum ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa baada ya kumzawadia Bi. Sumayyah Juma Abdallah wa Tanzania alitepata  alama 98.66 na kuibuka mshindi wa tano wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalum ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Bw. Idrissa Ousmane wa Niger   baada ya kupata Alama 98.67 na kunyakua ushindi wa nne wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Bw. Shamshuddin Hussein Ali wa Zanzibar baada ya kuzoa Alama  98.83 na kuibuka mshindi wa tatu wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimzawadia Bw. Faruq Kabiru Yakubu wa Nigeria  baada ya kuzoa Alama  98.91 na kuibuka mshindi wa Pili wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaidiana na    Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Kiislamu ya Amana Dr. Muhsin Salim Masoud  (kulia) akimzawadia Bw. Mohamed El Moujabba Diallo wa Senegal  (wa pili kushoto) zawadi ya shilingi milioni 20 baada ya kuzoa Alama  99.88 na kuibuka mshindi wa Kwanza wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalumuya 2o ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akimpatia pesa taslimu shilingi milioni moja Bi Sumayyah Juma Abdallah wa Tanzania ikiwa ni zawadi kutoka kwa Rais Dkt. Magufuli baada ya kupata alama 98.66 na kuibuka mshindi wa tano wa Washindi wa Kuhifadhi Juzuu 30 katika mashindano maalum ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na viongozi wengine wakiwa katika dua baada ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na viongozi wengine pamoja na washiriki pamoja na wajumbe wa kamati kuu ya maandalizi ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na viongozi wengine pamoja na kamati kuu ya maandalizi ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiagana na Sheikh Nurdeen Kishk, Mratibu Mkuu wa mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiaga maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine baada ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiaga maelfu ya waumini wa Kiislamu na wadau wengine baada ya mashindano maalumu ya 20 ya Qur’aan Tukufu yaliyofanyika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo Jumapili Mei 19, 2019. 
PICHA ZOTE NA IKULU

Tigo yaendesha zoezi la usajili wa laini Wizara ya Mambo ya Ndani

$
0
0
 Afisa huduma kwa wateja kutoka Kampuni ya Tigo Obrien Kinunda, akimsajilia  laini ya simu Mkuu wa Nidhamu wa Jeshi la Polisi Oscar Mushi kwa kutumia mfumo mpya wa usajili unatumia alama za vidole katika makao makuu ya Wizara ya Mambo ya Ndani jijini Dar es Salaam jana.

Afisa huduma kwa wateja wa kampuni ya Tigo Nimzihirwa Elias, akimsajilia laini ya simu mmoja wa wateja wa kampuni hiyo ambaye ni mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa kutumia utaratibu mpya wa usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole zoezi lililofanyika makao makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es Salaam jana.
 Afisa huduma kwa wateja wa kampuni ya Tigo Nimzihirwa Elias, akimsajilia laini ya simu mmoja wa wateja wa kampuni hiyo ambaye ni mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa kutumia utaratibu mpya wa usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole zoezi lililofanyika makao makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es Salaam jana.

Afisa huduma kwa wateja wa kampuni ya Tigo Pendo Stephen, akimsajilia laini ya simu mmoja wa wateja wa kampuni hiyo ambaye ni mtumishi wa Wizara ya Mambo ya Ndani kwa kutumia utaratibu mpya wa usajili wa laini za simu kwa kutumia alama za vidole zoezi lililofanyika makao makuu yan Wizara hiyio jijini Dar es Salaam jana.

WATATU WAPANDISHWA KIZIMBANI KWA SHITAKA LA UHUJUMU UCHUMI,WAKUTWA NA VIPANDE VINNE VYA MENO YA TEMBO

$
0
0

WATU watatu, wakazi wa jijini Dar es Salaam,  wamepandishwa katika kizimba cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu shitaka la uhujumu uchumi kwa kukutwa na nyara za serikali na utakatishaji wa vipande vinne vya meno ya tembo yenye thamani ya zaidi ya  Sh. Milioni 69.

Wakili wa serikali Candid Nasua amewataja washtakiwa hao kuwa ni, Godlisten Mtui, mfanyabiashara, Frank Lucas dereva wa pikipiki na Mhando Shomary, Mkulima

Mbele ya Hakimu Mkazi Maila Kasonde imedaiwa,  Mei 7 mwaka huu, huko katika eneo la Mbezi Luis jijini Dar es Salaam, washtakiwa, walikutwa na vipande vinne vya meno ya tembo vya USD 30000 ambazo ni sawa na Sh. 69,025,000 bila ya kuwa na kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori.

Aidha washtakiwa hao wanakabiliwa na shtaka la utakatishaji, ambapo wanadaiwa kumiliki vipande hivyo vya meno ya tembo huku wakijua wakielewa fika kuwa, vipande vivyo vya meno ya tembo vimetokana na kosa la uwindaji haramu.

Hata hivyo, washitakiwa hao hawakuruhusiwa kujibu kitu chochote mahakamani hapo kw kuwa, mahakama ya Kisutu  haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hadi Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), atakavyoelekeza vinginevyo.

Washitakiwa wote wamerudishwa rumande hadi Juni 4 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika.

VODACOM YASAJILI WANAFUNZI MFUMO MPYA WA ALAMA ZA VIDOLE JIJINI DODOMA

$
0
0
 Wafanyakazi wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc Michael Mhando na Emmanuel Medukenya wakisajili wanafunzi kwa kutumia mfumo mpya wa alama za vidole katika viwanja vya chuo kikuu cha Dodoma, jijini humo. Hivi karibuni kampuni hiyo imewezesha wafanyakazi wake na vifaa vya kusajilia kwa kutumia alama za vidole ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo kwa wateja wake popote nchini.

RAIS DKT. MAGUFULI APOKEA GAWIO LA SERIKALI KIASI CHA SHILINGI BILIONI MBILI TTCL

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL Waziri Kindamba wakati akiwasili katika Makao Makuu ya Ofisi za Shirika hilo katika Gorofa la Extelecom Posta jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wakuu wa Mikoa minne nchini kwa njia ya Simu ya Video Conference mara baada ya kuwasili katika   Makao Makuu ya Ofisi za Shirika hilo la TTCL lililopo katika Gorofa la Extelecom Posta jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Gawio la Serikali kiasi cha Shilingi Bilioni 2.1 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL Waziri Kindamba, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe pamoja na  Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL Omar Nundu katika hafla fupi iliyofanyika katika makao makuu ya Shirika hilo jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia vitendea kazi mbalimbali katika makumbusho iliyopo ndani ya Ofisi za Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wageni mbalimbali waliofika katika hafla ya upokeaji wa Gawio kwa Serikali kutoka kwa Shirika la Mawasiliano TTCL jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania TTCL Waziri Kindamba mara baada ya kuwasili katika eneo la utoaji wa Gawio katika ofisi za Shirika hilo jijini Dar es Salaam.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi mbalimbali katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa TTCL mara baada hafla ya upokeaji wa Gawio la Serikali katika Ofisi hizo za TTCL. PICHA NA IKULU

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 22,2019

MAMA JANETH MAGUFULI ATOA FUTARI KWA AJILI YA FAMILIA ZENYE UHITAJI JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, amewasihi Waislamu nchini kuendelea kuliombea Taifa muda wote, hususan katika kipindi hiki cha  Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, na kuendeleza mshikamano bila kujali dini ama kabila tabaka zao.

Mama Magufuli ametoa wito huo leo tarehe 22 Mei, 2019 Jijini Dar es Salaam wakati akitoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji.

Vyakula alivyotoa ni tani 5 za mchele, tani 3 za sukari na tende. Hafla hiyoimehudhuriwa na Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA Shekhe Haidary Kambwile na wawakilishi wa vikundi mbali mbali vya wenye uhitaji.

Mama Magufuli pia amemuomba Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, azikubali funga za Waislamu wote  na kuwalipa malipo stahiki wakati wakitekeleza moja ya nguzo muhimu za Dini ya Kiislamu.

“Kipindu cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni kipindi cha toba. Ni kipindi cha kutenda matendo mema na kujizuia na vitendo viovu” amesema Mama Magufuli.
Mama Magufuli amesema licha ya kwamba Tanzania ina watu wa imani za Dini tofauti lakini siku zote wananchi wake wamekuwa wakishirikiana nyakati za dhiki na za raha bila ubaguzi.

Ametoa mfano kuwa licha ya tofauti za kidini zipo baadhi ya familia ambazo Baba Muislamu na Mama ni Mkristo zinaishi kwa amani na kushirikiana katika masuala yote ya kifamilia na kwamba sifa hii ni moja nguzo muhimu za umoja wa Watanzania.

“Binafsi nakumbuka zamani nikiwa mdogo tulikuwa tunatafuta Mwislamu aje atuchinjie kuku ama mbuzi ama ng’ombe” , alisema na kuongezea: “Ni kutokana na utamaduni huo uliojengeka miongoni mwa Watanzania , leo nimeguswa kutoa sadaka yangu kwa ajili ya ndugu zangu wenye uhitaji…”
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiongea machache wakati wa hafla ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019.
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimsiliza Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe  Nuhu Muma akitoa shukurani wakati wa kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019.

 Wawakilishi waliohudhuria wakiitikia dua baada ya kupokea msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Wawakilishi waliohudhuria wakiitikia dua baada ya kupokea msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiitikia dua baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe  Nuhu Muma msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi Mkurugenzi wa Hija wa BAKWATA Shekhe Haidary Kambwile  msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi muwakilishi wa watototo msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi muwakilishi wa wazee msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akimkabidhi muwakilishi wa kinamama msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli katika picha ya kumbukumbu na   Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA Shekhe Haidary Kambwile pamoja na wawakilishi wa vikundi mbali mbali vya wenye uhitaji baada ya hafla ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa vikundi mbalimbali vyenye uhitaji.
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na wawakilishi baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mama Janeth Magufuli, akiagana na  Katibu Mkuu wa BAKWATA Shekhe Nuhu Mruma, Mkurugenzi wa Hijja wa BAKWATA Shekhe Haidary  baada ya kutoa msaada wa vyakula kwa ajili ya futari kwa niaba ya vikundi mbalimbali vyenye uhitaji jijini Dar es salaam leo Jumatano Mei 22, 2019

MUFTI MKUU TANZANIA AIPONGEZA BENKI YA NMB,AITABIRIA MAKUBWA

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Beni ya NMB, Albert Jonkergouw akizungumza na Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir (kushoto) , Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhaj Mussa Salum na Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam Id Badru.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Albert Jonkergouw (kulia) akimkaribisha Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubeir (kushoto) wakati wa Futari iliyoandaliwa na NMB katika Hotel ya Serena. Katikati ni Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salaam Id Badru
Mkuu wa Kitengo cha wateja binafsi wa Benki ya NMB, Omari Mtiga, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Steven Kabwe na Mkurugenzi wa ndni wa benki hiyo, Juma Kimori wakiwaongoza wageni kuchukua futari iliyoandaliwa na benki ya NMB iliyodanyika kwenye Hoteli ya Flomi Morogoro. 
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk. Steven Kebwe akizungumza wakati wa futari iliyoandaliwa na Benki ya NMB katika Hoteli ya Flomi mkoani Morogoro. 
Shekhe Mkuu Mkoa wa Mtwara, Nurdin Mangochi akiwa kwenye iftari iliyoandaliwa na Benki ya NMB jana. 
Mkurugenzi wa ndani wa Benki ya NMB Juma Kimori, akizungumza wakati futari iliyoandaliwa na Benki ya NMB katika Hoteli ya Flomi mkoani Morogoro. 


MUFTI Mkuu wa Tanzania, Sheikh Aboubakar Zubeir, ameitabiria makubwa Benki ya NMB, kutokana na utamaduni chanya walionao wa kuijali, kuithamini na kuipa kipaumbele jamii chini ya mwamvuli wa kaulimbiu yao ya Karibu Yako.

Mufti Zubeir alitoa mtazamo huo wakati akizungumza na waaalikwa wa hafla ya pili ya benki ya NMB kufuturisha waumini wa Dini ya Kiislamu tangu kuanza kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka huu 2019.

Ukiondoa Mufti Zubeir, hafla hiyo iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam, ikishirikisha waumini wa Kiislamu, wateja na waalikwa wengine, ilihudhuriwa pia na Sheikh Mkuu wa Mkoa, Alhad Mussa Salum na Meya wa Jiji, Issaya Mwita.

“Niwapongeze kwa uamuzi huu wa NMB kufuturisha waumini wa Kiislamu, hasa ukizingatia mnahudumia makundi mbalimbali wakiwemo Wakristo na wasio na dini. Hii inatoa tafsiri moja tu kuwa NMB inajali makundi na kada mbalimbali za jamii, jambo ambalo litawapa mafanikio.

Aliongeza ya kwamba walichofanya NMB ni jambo kubwa, linalojenga mahusiano makubwa baina ya Waislamu na wasio Waislamu, na kila mmoja kuitazama NMB kama taasisi inayojali makundi yote ya watu na kwa namna hiyo wanazivuta nyoyo za wengi kuona inafaya kazi kwa weledi.

“Mtu akiwa mwema kiasi hicho ama hata taasisi, Mwenyezi Mungu humlipa ama huilipa, hii maana yake ni kuwa kwa utamaduni huu, NMB itapata mafanikio makubwa kutokana na namna mnavyojali makundi mbalimbali ya jamii,” alisema Mufti Zubeir.

Aliitaka NMB kutoacha tamaduni ya kufungamanisha makundi kwa kufuturisha waumini wa Kiislamu na kuutaka uongozi kuufanya utamaduni huo kuwa wa kudumu ili pindi awamu moja ya uongozi inapomaliza muda wake, iache alama kwa jamii.

Awali akimkaribisha Mufti Zubeir, Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Albert Jonkergouw, alisema benki yake inajisikia furaha kuungana na Waislamu katika kutimiza moja ya nguzo muhimu za dini yao, huku akiahidi kuwa NMB itaendelea kusapoti na kushirikia na jamii.

Alisema tukio hilo ni la pili tangu kuanza kwa mfungo wa Ramadhani mwaka huu, baada ya kukutanisha, kufuturisha na kujadiliana kwa ufupi na Waislamu wa Jiji la Tanga na kwamba wamepanga kufuturisha katika miji kadhaa Tanzania Bara na Visiwani.

“Tukio kama hili leo linafanyika mjini Iringa, awali lilifanyika Tanga na sasa tunaelekea Zanzibar (Unguja na Pemba), na pia mikoa ya Mtwara, Mwanza na kwingineko kulingana na ratiba itakavyoturuhusu,” alisema Jonkergouw.

Akijibu wito wa Mufti Zubeir, aliyeomba muendelezo wa hafla za kufuturisha, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd, alisema NMB itaendelea na utaratibu wa kufuturisha waumini wa Kiislamu na kwamba wamefanya hivyo mara nyingi na wataendelea.

NMB YAWEZESHA MJADALA WA MAONI KUKUZA UKUSANYAJI MAPATO JIJI LA DAR

$
0
0

Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Abubakar Kunenge akizungumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) katika mkutano wa kupokea maoni toka kwa wadau anuai ili kuboresha sekta ya ukusanyaji mapato kwenye mkoa huo.
Ofisa Mwandamizi Wateja wa Serikali, Bi. Vicky Bishubo kutoka NMB Makao Makuu (kulia) akizungumza katika mkutano wa kupokea maoni toka kwa wadau mbalimbali ili kuboresha ukusanyaji mapato Mkoa wa Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja wa Benki ya NMB, Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd ambao ni wadhamini wa mkutano huo.
Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Abubakar Kunenge akizungumza na wadau mbalimbali (hawapo pichani) katika mkutano wa kupokea maoni toka kwa wadau anuai ili kuboresha sekta ya ukusanyaji mapato kwenye mkoa huo. Kushoto ni Meneja wa Benki ya NMB, Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd ambao walidhamini mkutano huo.
Mwakilishi kutoka Chuo cha Kodi TRA, Emmanuel Masalu akiratibu majadiliano katika mkutano wa kupokea maoni toka kwa wadau anuai ili kuboresha sekta ya ukusanyaji mapato ya jiji la Dar es Salaam. Kushoto ni Meneja wa Benki ya NMB, Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd ambao ni wadhamini wa mkutano huo.
Sehemu ya washiriki wa mkutano wa kupokea maoni toka kwa wadau mbalimbali jijini Dar es Salaam ili kuboresha ukusanyaji mapato kwenye mkoa huo.
Meneja wa Benki ya NMB, Kanda ya Dar es Salaam na Zanzibar, Badru Idd (kushoto) akizungumza jambo na Ofisa Mwandamizi Wateja wa Serikali, Bi. Vicky Bishubo kutoka NMB Makao Makuu kwenye mkutano huo.

SERIKALI YADHAMIRIA KUMLINDA MTEJA KUANGALIA GHARAMA ZA WAKANDARASI - NAIBU WAZIRI MGALU

$
0
0
NA SAMIA CHANDE, RUFIJI

NAIBU Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu amewasha umeme katika vijiji vya Muhoro Mashariki na Magharibi wilayani Rufiji Mkoani Pwani leo Mei 22, 2019 ikiwa ni muendelezo wa Serikali kuhakikisha watanzania wote wakiwemo wa vijijini wanapata umeme.

Akiwaelimisha wananchi kuhusu gharama za kuunganishiwa umeme wakati wa hafla hiyo iliyofanyika shule ya msingi Nyampapu iliyoko kijiji cha Muhoro Mashariki, Naibu Waziri alisema serikali inaowajibu wa kumlinda mlaji na mtumiaji wa huduma mbalimbali ndio maana katika swala la umeme vijijini imeshusha gharama za kuunganishiwa umeme hadi shilingi 27,000/= tu.

“Awali gharama za kuunganishiwa umeme zilikuwa ni shilingi 177,000, lakini Serikali kwa vile inawajali wananchi wake imelipa shilingi 150,000/= kwa kila anayeweka umeme, na kazi ya mwananchi ni kulipia kiasi kidogo tu cha shilingi 27,000/=, tofauti na hapo awali.” Alisema Mhe. Naibu Waziri Mgalu katika hafla hiyo ambapo takriban Kaya 26 zimefaidika na zoezi hilo.

Alisema anatambua wapo wananchi wapo karibu na miundombinu ya njia ya umeme na sio kwamba wanashindwa kulipa shilingi elfu 27,000/= bali wanashindwa na gharama ya kutandaza umeme ndani ya nyumba (wiring) inayofanywa na wakandarasi.(mafundi).

“Alisema gharama hizo za wiring zimeonekana kuwa ndio changamoto kwa wananchi na serikali imepokea changamoto hiyo na kwamba itafanyia kazi.” Alisema.

Alitoa wito kwa wakandarasi wanaofanya kazi ya wiring wazingatie vipato vya watanzania wenzao, watakapoweka bei kubwa watapata wateja wachache lakini wakiweka bei ya kawaida, wateja wengi ambao serikali imelenga kuwaunganishia umeme watawapata.Aidha Mhe. Naibu Waziri Subira Mgalu, aliwataka wananchi wa Wilaya ya Rufiji kuchangamkia fursa za kutoa huduma kwa wafanyakazi wanaojenga mradi wa umeme wa maji wa Mto Rufiji.

“Vijana nendeni Ngarambe, Mloka na Mwasemi, ajira ziko za kutosha, akina mama ntilie, wanatakiwa vibarua, lakini pia kunachangamoto ya nyumba za kulala wageni, kwa hivyo ziko fursa nyingi katika maeneo ya mradi.” Alisema.
Alisema kuna mahitaji mbalimbali ya vyakula kama vile mbogamboga, kitoweo, mahitaji ya bidhaa hizo yamekuwa makubwa na kutoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Rufiji kuhcngamkia fursa hiyo.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu (mwenye hijab mbele), akizunhgumza baada ya zoezi la kuwasha umeme kwenye vijiji vya Muhoro Mashariki na Magharibi wilayani Rufiji Mkoani Pwani leo Mei 22, 2019. Takriban Kata 26 zimefaidika na zoezi hilo.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu, (aliyesimama), akitoa hotuba yake wakati wa hafla ya kuwasha umeme katika vijiji vya Muhoro Masharki na Magharibi iliyofanyika shule ya msingi Nyampapu wilayani Rufiji Mkoani Pwani leo Mei 22, 2019. Mwenye shati la bluu ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Mhe. Juma Njwayo.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu, (wapili kulia), akiongozana na baadhi ya viongozi wa wilaya ya Rufiji baada ya hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu, (kushoto), akipokea zwadi kutoka kwa akina mama wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), baada ya kuhutubia wananchi katika hafla ya kuwasha umeme iliyofanyika shule ya msingi Nyampapu iliyopo Muhoro Mashariki wilayani Rufiji Mkoani Pwani leo Mei 22, 2019. (PICHA NA SAMIA CHANDE).

MAJAJI WASAJILI LAINI ZA SIMU KWA ALAMA ZA VIDOLE

$
0
0

Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe Ibrahim Juma(katikati) akisajili  laini  ya simu kwa alama za vidole katika kampuni za simu ya Smile,kushoto  ni Mackie Mdachi  na Arnold Ntiga, ambao ni wasajili kutoka kampuni hiyo.Usajili huo umefanyika leo kwenye ukumbi  namba moja wa Mahakama ya Rufaa Tanzania..
Majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Mhe. Winfrida Korosso,(kulia), Mhe. Rehema Mkuye(katikati) na Mhe. Barke Mbaraka Sehel(kushoto) wakisikiliza maelezo kuhusu usajili laini za simu kwa vidole wakati  wakijisajili zao  leo katika kampuni ya simu ya Halotel. Usajili huo umefanyika leo kwenye ukumbi namba moja wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe.           Dkt.Eliezer Feleshi akisajili laini  ya simu kwa alama za vidole katika Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) na kulia aliyevaa shati la kitenge  ni  Afisa Mauzo wa TTCL, Usajili huo umefanyika leo kwenye ukumbi namba moja  wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Jaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Mhe, Rehema Mkuye akisajili laini ya simu kwa alama za vidole  katika kampuni ya Halotel. Usajili huo umefanyika leo kwenye ukumbi  namba moja wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.
Jaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania, Mhe, Augustine Mwarija akisajili laini ya simu kwa alama za vidole  katika kampuni ya  Vodacom. Usajili huo umefanyika leo kwenye ukumbi namba moja  wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.Kushoto ni  anayemsajili ni Meneja Mauzo wa kampuni ya Vodacom Happiness Shuma.
Baadhi ya watumishi wa Mahakama ya Tanzania wakisajili laini za simu  kwa alama za vidole katika kampuni mbalimbali za simu, wakati wa usajili huo uliofanyika leo kwenye ukumbi namba moja  wa Mahakama ya Rufaa Tanzania.
(Picha na Magreth Kinabo.)

IFAD KUENDELEA KUISAIDIA TANZANIA KUENDELEZA SEKTA YA KILIMO

$
0
0
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akimkabidhi zawadi ya picha, Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bw. Gilbert Fossoun Houngbo, baada ya Mkutano ulioangazia maendeleo ya sekta ya kilimo nchini na namna ya kutatua changamoto zake, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dodoma. 
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) akipeana mkono na mgeni wake Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bw. Gilbert Fossoun Houngbo, katika Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dodoma. 
Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bw. Gilbert Fossoun Houngbo, akiipongeza Serikali ya Tanzania kwa ukuaji wa Sekta ya Kilimo kwa takribani asilimia 6, kiwango ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na nchi nyingi za Afrika, wakati wa Mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), kushoto ni Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. John Rubuga. 
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa sita kushoto) na Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD) Bw. Gilbert Fossoun Houngbo (wa sita kulia), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe kutoka Tanzania na IFAD, baada ya kumalizika kwa mkutano ulioangazia Maendeleo ya Sekta ya Kilimo kikiwemo kilimo cha umwagiliaji, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dodoma. 


Na Peter Haule, WFM, Dodoma 

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Gilbert Houngbo, na kuiomba Taasisi hiyo kusaidia kuendeleza zaidi Sekta ya Kilimo kupitia mpango wake mpya wa awamu ya 11 wa kuendeleza kilimo nchini. 

Dkt. Mpango ameyataja baadhi ya maeneo ya kipaumbele kuwa ni uzalishaji wa mbegu bora, kusaidia kilimo cha umwagiliaji, kutafuta masoko ya uhakika ya mazao ya wakulima, kusaidia upatikanaji wa mitaji kwa wakulima na kuanzisha taasisi za utafiti wa kilimo za kikanda. 

Aidha, Dkt. Mpango alimwomba kiongozi huyo kusaidia pia mbinu za kupunguza upotevu wa mazao wakati na baada ya mavuno ili kuchochea na kuongeza tija katika sekta ya kilimo ambayo amesema inaajiri zaidi ya asilimia 66 ya Watanzania. 

”Takiribani asilimia 66 ya watanzania wanategemea kilimo na kilimo ndio mwajiri mkuu hivyo kwa kuwa IFAD ina program mpya, tumeamua kushauriana ili wajue vipaumbele vya Serikali na fedha tutakazo zipata tuzielekeze katika maeneo hayo”, alieleza Dkt. Mpango. 

Dkt. Mpango alisema kuwa Serikali inaunda kikosi kazi kitakacho husisha Wizara ya Kilimo, Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ili kuweka nguvu ya pamoja kwa kuangalia maeneo ya vipaumbele ambavyo Mfuko wa IFAD utasaidia. 

Kwa upande wake Rais wa IFAD Bw. Gilbert Houngbo, alisema kuwa Taasisi yake itashirikiana na Tanzania katika jitihada zake za kupunguza umasikini wa wananchi kupitia kilimo kwa kuyapatia ufumbuzi masuala kadhaa ikiwemo changamoto ya upatikanaji wa mbolea na mbegu bora za kilimo na mifugo, masoko ya bidhaa, upatikanaji wa mitaji, kuongeza ujuzi wa wakulima, kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na kuwashawishi vijana wengi kujihusisha na kilimo. 

Alielezea kufurahishwa kwake na mwamko pamoja na mwitikio wa baadhi ya wakulima na wafugaji walionufaika na awamu zilizotangulia za uendelezaji sekta ya kilimo na mifugo kupitia taasisi yake aliowatembelea, ambao amesema wanamtazamo mzuri wa kilimo cha kibiashara kinachozingatia uongezaji wa mnyororo wa thamani, suala ambalo ni moja ya lengo la Mfuko huo katika kuendeleza Sekta hiyo. 

Mfuko wa IFAD ulianza kuisaidia Tanzania kutekeleza miradi ya maendeleo ya kilimo kuanzia mwaka 1978, ambapo hadi sasa imesaidia miradi 15 yenye thamani ya dola za Marekani milioni 385.80 na katika awamu mpya ya miaka mitatu kuanzia mwaka 2019/2021, IFAD imetenga zaidi ya dola za Marekani milioni 58.8 kwa ajili ya kuendeleza Sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini. 

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na kuwasaidia wakulima kutumia teknolojia ya kisasa ya kilimo na mifumo ya masoko, kuhamasisha Sekta binafsi katika uwekezaji na kuwasaidia wakulima wadogo na wavuvi kuongeza kipato na kupunguza umasikini kwa kuzingatiakuongeza mnyororo wa thamani ya mazao husika. 

Sekta ya Kilimo nchini inachangia asilimia 30.1 ya jumla ya pato la ndani (GDP), asilimia 26 ya mapato ya kigeni, ajira takribani asilimia 65.5, inachangia malighafi za viwandani kwa takribani asilimia 65 na inachangia kwenye mahitaji ya chakula kwa asilimia 100.

ISACA TANZANIA CHAPTER 2019 annual Conference

BENKI YA EXIM YAFUTURISHA WATEJA WAKE WA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo na kati wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Andrew Lyimo (kulia) sambamba na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo walioudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wa huduma za reja reja wa benki hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo na kati wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Andrew Lyimo (kulia) akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wa huduma za reja reja wa benki hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam jana.
Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo na kati wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Andrew Lyimo (kulia) akizungumza wateja wa benki hiyo waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wa huduma za reja reja wa benki hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam jana.
Mmoja wa wateja wa benki ya Exim Tanzania kutoka taasisi Ahmadiyya Muslim Jamaat Tanzania, Bw Abdulrahman Mohamed Ame akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wateja wa benki hiyo waliohudhuria hafla ya futari iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam jana.

Airtel yatangaza punguzo kabambe kwa wateja wake kupiga simu Mitandao Yote

$
0
0
 Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano na Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isaack Nchunda wakionyesha bango baada ya  ya Airtel kuzindua huduma mpya inayojulikana kama ‘TAMBA MITANDAO YOTE’, huduma hiyo ina lengo la kuwapa wateja wake suluhisho na uhuru wa kuchagua huduma ya mawasiliano ambayo ni nafuu zaidi wakati wowote hata kama mteja hajajiunga na bando. 
 Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam baada ya Airtel kuzindua huduma mpya inayojulikana kama ‘TAMBA MITANDAO YOTE’, huduma hiyo ina lengo la kuwapa wateja wake suluhisho na uhuru wa kuchagua huduma ya mawasiliano ambayo ni nafuu zaidi wakati wowote hata kama mteja hajajiunga na bando. Kushoto ni Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isaack Nchunda.



· Punguzo Pekee kutoka Airtel, uhuru wa kuongea

· Airtel sasa yawezesha wateja kupiga simu mitandao yote kwa 1TZS bila bando 

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania imeendelea kuwapa wateja wake huduma kabambe na za kipekee ikiwa ni jibu na itikio la mahitaji ya wateja wao kwa kuzindua huduma mpya inayojulikana kama ‘TAMBA MITANDAO YOTE’, huduma hiyo ina lengo la kuwapa wateja wake suluhisho na uhuru wa kuchagua huduma ya mawasiliano ambayo ni nafuu zaidi wakati wowote hata kama mteja hajajiunga na bando.

Huduma hii mpya ya TAMBA MITANDAO YOTE inakuja wakati muafaka na kuwapa wateja wa Airtel uhuru wa kupiga simu kwenda mtandao wowote nchini kwa punguzo la kiasi cha 1TZS tu kwa kila sekunde hata kama mteja hajajiunga na bando au kuishiwa bando.

Mkurugenzi wa Masoko Airtel Tanzania Isaack Nchunda akizungumza leo jijini Dar es Salaam kuthibitisha kuzinduliwa kwa huduma hiyo ya TAMBA MITANDAO YOTE kwa niamba ya Mkurugenzi Mkuu, alisema ‘Tunayo furaha kubwa kuzindua huduma hii ambayo inawapa wateja wa Airtel uhakika wa kupiga simu kwenda mtandao wowote hapa nchini kwa gharama nafuu ya 1TZS kwa sekunde, tunaamini kupitia Tamba Mitandao Yote mteja wetu ataona thamani ya pesa yake na kufurahia uhuru wa kuongea wakati wowote. 

 Nchunda aliongeza kuwa wateja wa Airtel watafurahia pia punguzo la vifurushi vya intaneti kutoka TZS172 kwa MB mpaka TZS40 kwa MB ikiwa hajajiunga na bando lolote, pia mteja atafurahia kutumia TZS10 tu kwa MB ikiwa mteja alikuwa na kifurushi cha bando ambacho hakijaisha muda wake huku punguzo la gharama za ujumbe mfupi zikishuka kutoka TZS 69 kwa kila ujumbe mpaka TZS 10 kwa kila ujumbe’.

”TAMBA MITANDAO YOTE” ni huduma ambayo inampa mteja wa Airtel huduma bora, huru na nafuu kwani hata kama mteja atakuwa hajajiunga na bando yoyote bado anaweza kupiga simu kwenda mtandao wowote nchini kwa gharama ndogo ya 1TZS kwa sekunde. Tunaamini hii ni hatua kubwa sana kwenye sekta ya mawasiliano ambapo vikwazo vyote vimeondolewa na kuwapa Watanzania unafuu wa kupiga simu bila kujali kipato chake,’ alisema Nchunda.

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema ‘Kulingana na taarifa kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), idadi ya wateja wanaotumia simu za mkononi kwa kupiga kati ya mwaka 2017 na 2018 imeongezeka kutoka milioni 40 mpaka 43. Idadi ya wateja wetu imeongezeka pia kwa kipindi cha robo mbili za mwaka uliopita na hii imetokana na hudumu zetu zenye ubunifu na unafuu wa hali ya juu. Tunaamini huduma yetu itawawezesha wateja wetu kupata uhuru wa kupiga na kuongea ,wakiokoa fedha zao na kuziweka kwenye maendeleo ya kiuchumi. 

Airtel imekuwa mstari wa mbele kwenye kuleta huduma nafuu na zenye ubunifu ambazo zinakidhi matakwa ya wateja wetu kama vile huduma za kifedha, SMS, kupiga simu na hata kwenye huduma za intaneti.

‘Airtel inaendelea kukuza wigo wa mtandao wake nchini ambapo kwa sasa tuna maduka ya Airtel Money Branches zaidi ya 650 ambapo mteja anaweza kupata bidhaa na huduma mbalimbali kama za kifedha, kuunganisha kwenye vifurushi vya intaneti pamoja na kusajili laini za simu kwa kutumia alama za vidole’, aliongeza Singano.

Benki ya NMB Tawi la Kisiwani Pemba Lafutarisha Wateja Wake na Wananchi.

$
0
0
MENEJA wa Bank ya NMB Kisiwani Pemba Ahmed Nassor, akitoa shukurani kwa wananchi na wateja wao waliohudhuria futari maalumu, iliyoandaliwa na Bank hiyo kwa wateja wao na kufanyika mjini Chake Chake
MENEJA wa NMB kanda ya Dar es Salam na Zanzibar Badru Iddi, akizungumzia juu ya mikakati ya NMB kwa wateja wake mara baada ya kumalizika kwa futari Maalumu iliyoandaliwa na benk hiyo na kufanyika mjini Chake Chake.
AFISA mdhamini Wizara ya Fedha na Mipango Pemba Ibrahim Saleh Juma, akizungumza na wananchi na wateja wa NMB kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, mara baada ya kumalizika kwa futari maalumu iliyoandaliw ana bank hiyo kwa wateja wao na kufanyka mjni Chake Chake.
WAFANYAKAZI wa Bank ya NMB Kisiwani Pemba, wananchi na wateja wao wakiwa katika sala ya pamoja, iliyofanyika Chake Chake kuelekea kwenye futari maalumu iliyoandaliwa na Banke ya NMB kwa wateja wake
AFISA Mdhamini Wizara ya Fedha na Mipango Ibrahim Saleh Juma (katikati) akipata uji wakati wa futari maalumu iliyoandaliwa na bank ya NMB kwa wateja wake, kulia ni meneja wa benk hiyo kanda ya Dar es Salam na Zanzibar Badru Iddi na kushoto ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Shekh Mahmoud Mussa Wadi, futari hiyo imefanyika Chake Chake Pemba 
MENEJA wa Bank ya NMB kanda ya Dar es Salam na Zanzibar Badru Iddi, akichukua futari maalumu iliyoandaliwa na benk hiyo kwa wateja wake Kisiwani Pemba na kufanyika mjini Chake Chake
BAADHI ya wateja wa Bank ya NMB na wananchi wa Kisiwa cha Pemba, wakichukua futari maalumu iliyoandaliwa na Bank hiyo kwa wateja wake na kufanyika mjini Chake Chake'
AFISA Mdhamini Wizara ya Fedha na Mipango Ibrahim Saleh Juma (katikati) akipata uji wakati wa futari maalumu iliyoandaliwa na bank ya NMB kwa wateja wake, kulia ni meneja wa benk hiyo kanda ya Dar es Salam na Zanzibar Badru Iddi na kushoto ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Shekh Mahmoud Mussa Wadi, futari hiyo imefanyika Chake Chake Pemba
VIONGOZI wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kusini Pemba, wakiongoza na Kamanda wa Polisi Mkoa huo Hassan Nassir Ali wa pili kutoka kulia, akifuatiwa na Kamanda wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania 14KJ Khamis, wakipata futari maalumu iliyoandaliwa na Bank ya NMB kwa wateja wao na kufanyika Mjini Chake Chake
BAADHI ya wafanyakazi wa NMB, wateja wao na wananchi wa Kisiwa cha Pemba, wakichukuwa futari maalumu iliyoandaliwa na benk hiyo kwa wateja wao Kisiwani hapa
BAADHI ya wateja wa Banki ya NMB na wananchi akipata futari maalumu, iliyoandaliwa na benk hiyo kwa wateja wao na kufanyika mjini Chake Chake
(Picha na Abdi Suleiman - Pemba).

BENKI YA NMB KUTOA ELIMU YA FEDHA KWA WANANCHI

$
0
0
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai akikata utepe baada ya kukabidhiwa viti na meza kwa ajili ya Shule ya Sekondari Mnyakongo zilizotolewa na Benki ya NMB tukio lililofanyika leo katika Shule ya Sekondari Mnyakongo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. Kuanzia Kushoto ni Meneja wa NMB Benki tawi la Kongwa, Ndg. Tuntufye Mwakatika, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa, Ndg. White Zuberi, Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Ndg. Margaret Ikongo, Afisa Mkuu wa Kitengo cha Digitali, Mifumo na Bidhaa kutoka NMB Benki, Ndg. Pete Novert na Meneja wa NMB Benki Kanda ya Kati, Ndg. Nsolo Mlozi
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai akikata utepe baada ya kukabidhiwa Mabati kwa ajili ya Shule ya Sekondari Chiwe yaliyotolewa na Benki ya NMB tukio lililofanyika leo katika Shule ya Sekondari Mnyakongo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. Kulia ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Ndg. Margaret Ikongo
Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimshukuru Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Ndg. Margaret Ikongo baada ya kukabidhiwa Mabati kwa ajili ya Shule ya Sekondari Chiwe yaliyotolewa na Benki hiyo tukio lililofanyika leo katika Shule ya Sekondari Mnyakongo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.Picha na Alex Sonna


Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akisalimiana na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Digitali, Mifumo na Bidhaa kutoka NMB Benki, Ndg. Pete Novert walipokutana leo katika Shule ya Sekondari Mnyakongo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma. Katikati ni Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Ndg. Margaret Ikongo na Meneja wa NMB Benki Kanda ya Kati, Ndg. Nsolo Mlozi

Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai (kulia) akiteta jambo na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya NMB, Ndg. Margaret Ikongo (katikati) na Afisa Mkuu wa Kitengo cha Digitali, Mifumo na Bidhaa kutoka NMB Benki, Ndg. Pete Novert walipokutana leo katika Shule ya Sekondari Mnyakongo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.

Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnyakongo alipowatembelea leo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.

Meneja wa NMB kanda ya kati Nsolo Mlozi,akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnyakongo baada ya kwenda kukabidhi Viti,Meza na Mabati wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.

Mkuu wa Shule ya Mnyakonga Mpokeeni Sanga,akitoa taarifa ya shule yake baada ya kupokea Viti,Meza kutoka benki ya NMB wilayani Kongwa Mkoani Dodpoma.


Diwani wa Kata ya Kongwa Mhe.White Zuber akitoa neno la shukrani kutoka kwa benki ya NMB mara baada ya kukabidhi Viti,Meza kwa shule ya Sekondari Mnyakongo pamoja mabati 250 kwa shule ya Chiwe zote za wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma

Mjumbe bodi ya wakurugenzi Benki ya NMB Margaret Ikongo akitoa semina kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari Mnyakongo na Chiwe baada ya kufanya ziara ya kukabidhi Viti,Meza na Mabati wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.

Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mnyakongo wamsikiliza Spika wa Bunge na Mbunge wa Kongwa, Mhe. Job Ndugai (hayupo kwenye picha) akizungumza baada ya kuitembelea Shule hiyo leo Wilayani Kongwa Mkoani Dodoma.

...........................

Na.Alex Sonna,Kongwa.

SPIKA wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai ameiomba Benki ya NMB kutoa elimu kwa wananchi ili wajue jinsi ya kutunza fedha za mikopo yao.

Ndugai ameyasema hayo wakati wa NMB ilipofanya ziara ya kukabidhi viti na meza 63 vyote vikiwa na idadi hiyo kwa Shule ya Mnyakongo pamoja na mabati 250 kwa Shule ya Chiwe zilizopo Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma.
Spika amesema kuwa NMB wanakila sababu ya kutoa elimu ya utunzaji fedha kwa wananchi kama wanavyofanya kwa wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari ili wawe na ujuzi zaidi.Aidha amesema kuwa watu wengi wanakopa fedha lakini hawajui wafanyie nini baada ya kuzichukua.

‘’Yaani unashangaa muda mchache ukikutana na watu hao hakuna cha maana walichofanyia badala yake wanarudi katika maisha ya chini badala ya kusonga mbele kimaisha’’amesema Ndugai

Spika Ndugai amesema kutokana na hilo kuna sababu ya elimu hiyo kutolewa kwa wananchi ili wakope fedha huku wakijua wanakwenda kuzifanyia nini.
Ndugai amefafanua kuwa ameshakutana na kesi hizo nyingi kwa ndugu jamaa na marafiki ambao wamekopa bila ya kupata mafanikio yoyote.

‘’Kwa kweli kwa hilo naomba mlifanyie kazi kwani limekuwa likiwaumiza wananchi na kupelekea kurudi nyumba kimaendeleo badala ya kwenda mbele katika maisha kupitia fedha walizokopa’’amesisitiza Ndugai.Kwa upande wake Meneja wa NMB kanda ya kati Nsolo Mlozi amesema kuwa wataendelea kuiunga mkono Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Pombe Magufuli hivyo wametenga maeneo manne kwa ajili ya kusaidia jamii.
Mlozi ameyataja amaeneo hayo ni Elimu,Afya,Kilimo na utunzaji Fedha kwa vijana mpaka watu wa rika la juu kwa lengo la kuwainua kiuchumi kwa kunufaika kwa kupitia NMB.

Hata hivyo amesema kuwa mpaka sasa tayari milioni 400 zimeshatolewa kwa ajili ya misaada katika shule na hospitli ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa.Mlozi amesema kuwa NMB iko pamoja na serikali kuhakikisha wanafikia malengo waliojiwekea.

Naye Mkuu wa Shule ya Mnyakonga Mpokeeni Sanga amesema kuwa walikua na upungufu wa madawati 70 na wanaishukuru NMB kuwapa viti 63 na meza 63 na ambavyo wanaamini vitasaidia kupunguza uhaba waliokuwa nao.Sanga amewahakikishia NMB kuwa vitu hivyo watavitunza ili hapo wanafunzi wengine waje kuvitumia hapo mbeleni na amewaomba waendelee na moyo huo wa kusaidia jamii kwani wamekuwa mfano wa kuigwa nchini.

Mkuu wa shule ya Chiwe Aron Mango amesema kuwa mabati hayo waliopewa yatawasaidia kuezeka mabweni ya wasichana ambayo yanajengwa shuleni hapo

Hakuna mipaka tena katika mawasiliano

$
0
0
Kampuni ya Halotel Tanzania imekuja na huduma mpya ya mawasiliano iitwayo ‘MPANGO MZIMA’ ambayo pamoja na faida zake nyingine inamuwezesha mtumiaji wa simu wa mtandao wa Halotel kupata unafuu katika huduma mbalimbali za simu.

Kuanzishwa kwa huduma ya Mpango Mzima ni muendelezo wa kampeni mbalimbali zinazoendelea kufanywa na Halotel katika kumrahisishia mteja wake kupata huduma bora za mawasiliano zikiwemo za kutumia Intaneti bila kikomo, kupiga simu matandao yote bila kikomo, kutuma ujumbe mfupi wa maneno(sms),

Akiziungumza kuhusu ‘Mpango Mzima’ Mkurugenzi wa Halotel, Nguyen Van Son alisema ujio wa huduma hiyo mpya na ‘Kijanja’ imelenga kumwezesha mtumiaji wa mtandao huo kutumia intaneti yenye kasi na ukubwa wa (GB 5) bila kikomo.

Pamoja na Intaneti hiyo mtumiaji wa mtandao huo pia ataweza kupiga simu kwenda mitandao yote bure kwa kila dakika 5 za kwanza pamoja kuzawadiwa sms 5000 atakazozitumia katika kipindi cha mwezi mzima.

“Huu ni muendelezo wa mpango wa mapinduzi ya kimawasiliano wa Halotel kuwa karibu na kuwajali wateja wetu kwa huduma bora. Kuanzishwa kwa Mpango Mzima kutamwezesha mteja wetu wa Halotel kutumia intaneti ya kasi kubwa , kupiga simu bila kikomo kwa mitandao yote bure kila dakika 5 za mwanzo na hivyo kumuondolea hofu ya simu kukatika kabla hajamaliza maongezi” amesema Son.

Amesema ili mteja aweze kufaidika na huduma hiyo mpya anapaswa kujiunga kwa kupiga *148*66# na kuchagua Mpango Mzima ambapo ataweza kujiunga na kuwa tayari kwa kuanza kufurahia unafuu huo mahususi kwa ajili ya watumiaji wa mtandao wa Halotel.

Mkurugenzi huyo Bw. Nguyen Van Son amesema huduma ya Mpango Mzima ni mpya kuwahi kutolewa na mtandao mwingine wowote wa simu hapa nchini na kuwaambia watumiaji wa Halotel kuwa hiyo ni zawadi kwao hivyo wanapaswa kuifurahia na kuitumia wakati wote.

Aidha Mkurugenzi huyo Bw. Nguyen Van Son wa alisema Halotel pia imeweza kuunganisha Optic Fiber zenye urefu wa zaidi ya Kilomita 20,000 katika maeneo yenye miundombinu yake kwa ajili ya kuwezesha upatikanaji wa data kwa maeneo mapya na hivyo kuiwezesha kuwa chaguo la kwanza kwa wateja pale linapokuja suala la huduma za Internet.

SHIRIKA LA NDEGE LA EMIRATES LAZINDUA APP YA KIARABU, JUMLA YA LUGHA 19 KUTUMIKA

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

SHIRIKA la Ndege la Emirates limesema kwama vipengele vyote vya App ya Emirates sasa vinapatikana kwa lugha ya kiarabu, ikileta jumla ya lugha 19.

Taarifa ya Shirika hilo ambayo imeitoa leo kwa vyombo vya habari imesema App ya Emirates sasa inapata wastani download 600,000 kila mwezi na inaruhusu watumiaji kutafuta, vitabu na kuweza kufanya booking.Pia kuangalia vitu ambazo vinaweza kuwasaidia kwenye safari yao ya ndege pamoja na akaunti zao za Emirates Skywards.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo inaeleza kuwa Emirates ni shirika la ndege pekee duniani kuwa na app yake ya simu inayopatikana katika lugha 19, ikiwa ni pamoja na Kiarabu, Kiingereza, kichina ya kizamani na Kichina Kilichorahisishwa , Kicheki, Kifaransa, kijerumani, Kigiriki, Kiitaliano, Kijapani, Kikorea, Kireno (Brazil na Ureno), Kipolishi, Kirusi , Kihispania, Thai na Kituruki

Imefafanua katika miaka ya hivi karibuni, shirika la Emirates imetumia ufahamu wa kuchambua wateja ili kuboresha njia zote za kidigital. Mwaka wa mwisho wa kifedha, robo ya mauzo yote ya tiketi yalitolewa kwenye mtandao na channeli za simu na wateja zaidi ya asilimia 40 waliweza kucheck kupitia app ya shirika hilo.

"Tumefanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha wateja wetu wanafurahia huduma za kipekee kutoka shirika la Emirate katika ulimwengu wa digitali kama wanavyofanya wakati wa kufurahia bidhaa na huduma za kushinda tuzo.

"App yetu imekuwa rafiki mzuri wakati wa kusafiri kwa zaidi ya wasafiri milioni 1.5 kwa mwezi na inahakikisha safari iliyo imara. Tutaendelea kuwekeza katika simu ili kuwapa wateja uzoefu na kendelea kuwafurahisha na kufanya safari za wateja wetu kuwa nzuri, "amesema Makamu wa Rais Mkuu Corporate Communications, Marketing na Brand (Digital) Alex Knigge.

Knigge amesema katika taarifa hiyo kuwa mapema mwaka huu, App ya Emirates iliimarishwa na teknolojia mpya ambapo iliwawezesha wateja kujenga mtiririko wa orodha wa burudani zao kabla ya safari na kuweza kuzicheza wakiwa kwenye viti vyao mara baada ya kuingia ndani ya ndege, ili kutoa uzoefu murua wa safari.

Kuhusu kutumia teknolojia katika digitali amesema Shirika la ndege imezingatia katika kuinua wateja wake kwenye uzoefu wa kidigitali kwa kuangalia teknolojia.

Imeelezwa kuwa mwaka jana, Emirates ilizindua mfumo mpya wa kiti cha kitekinolojia cha 3D,na kuifanya Emirates kuwa ndege ya kwanza kutumia mfumo huo mpya wa kidigitali wa kiti cha 3D.Kiti hicho cha 3D kinatumia mfumo wa injini ya kutazama ambayo inaonyesha mtazamo wa 3D na kuonyesha mambo ya ndani ya Emirates A380.

Pia inaonesha aina zote za ndege za Emirates B777, kuruhusu watumiaji kupitia madaraja ya Uchumi, Biashara na daraja la Kwanza, pamoja na sehemu ya mapumziko na pakuogea ndani ya A380.

"Shirika letu lilipata tuzo ya 'Best Digital Strategy' kwa uvumbuzi huu katika Tuzo za Wateja wa Ghuba ya mwaka huu. Teknolojia ya VR inatumika kwa kazi nyingine za shirika la emirates.com hivi karibuni itashughulika na mifano halisi ya lounge za uwanja wa ndege duniani kote.

"Njia za digitali za Emirates zinaendelea kushinikiza mipaka kama inachunguza teknolojia inayojitokeza zaidi na kuandaa kuunganisha Intelligence Artificial (AI) ili kuboresha uzoefu kwa wateja baadaye mwaka huu,"amesema Knigge katika taarifa hiyo na kuongeza App ya Emirates ni bure na inaweza kupakuliwa kwenye iOS or Android devices.

KILUWA GROUP LTD WASAINI MKATABA NA KAMPUNI YA KUTOKA CHINA INAYOTAKA KUJENGA KIWANDA CHA SUKARI ,KILIMO

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii 

KITUO cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kimewakaribisha Watanzania wazalendo kutembelea katika ofisi za kituo hicho kwa lengo la kujua taarifa mbalimbali na fursa za uwekezaji zilizopo kwenye maeneo tofauti. 

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi Idara ya Uhamasishaji TIC John Mathew kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe katika hafla ya kutia saini mikataba ya makubaliano ya uwekezaji kati ya kampuni za Tanzania na China ambapo amesema huu ndio wakati wa vijana kuwa karibu na kituo hicho ili kupata taarifa za kila siku juu ya uwezekaji. 

Amefafanua kuwa Kampuni ya Kiluwa Group inafanya kazi kubwa ya kuzungumza na wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali hasa China ambapo leo wanashuhudia utiwaji saini mkataba wa mwakubaliano ili kuanzisha kiwanda cha sukari nchini. 

"Wachina hawa baada ya kuvutiwa na mikataba hii watavutia wawekezaji wengine ndani na nje ya nchi, Kampuni ya Kiisu Minyuan International Trading Ltd inataka kuwekeza katika kiwanda cha kutengeneza sukari, hii itasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza idadi ya uzalishaji wa bidhaa hii muhimu kwa maendeleo ya nchi,,"amesema Mathew. 

Ameongeza wadau wengine wajitokeze ili wasaidiwe namna bora ya kuunganisha kampuni kutoka nje na kampuni za ndani ili kuhakikisha kunapatikana urahisi katika baadhi ya masuala. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kiluwa Group, Mohammed Kiluwa amesema mara nyingi anapokuwa katika mikutano ya kimataifa inayohusu uwekezaji amekuwa akijitahidi kuhakikisha anavuta wawekezaji wakubwa kuja kuwekeza nyumbani Tanzania. 

"Hivi karibuni nilikuwa katika mkutano wa One Belt One Road, nikauza fursa za uwekezaji, wengi walipenda na baadhi yao ni hawa tuliotiliana nao saini. Sisi ndio wajenga nchi na hasa katika kipindi hiki ambapo Rais Dk. John Magufuli ameamua kwa dhati kuifanya nchi kuwa na uchumi wa kati kwa kutegemea viwanda. 

"Hivyo, viwanda vingi iwezekanavyo vinahitajika. Kwa mfano kwa uwekezaji huu sisi tutahitaji eneo lenye ukubwa wa hekta 30,000 na hili si eneo moja bali tutaweza kuwa na uwekezaji katika mikoa mbalimbali. 

"Kama mnavyofahamu kiwanda cha sukari uzalishaji wake una mambo mengi, muwa unapoingizwa kiwandani unakuwa na vitu vingi hivyo tutakuwa na Industrial Park za kutosha,"amesema Kiluwa. 

Pia amewataka Watanzania kushirikiana katika kutangaza fursa zilizokuwepo nchini kwenye uwekezaji, anadai anajiona yuko peke yake wengi hawachangamkia nafasi za kutangaza maeneo ya nchi kwenye uanzishwaji viwanda kwa faida ya taifa. 

Wakati huo huo Rais wa kampuni ya Kiisu Minyuan International Trading Ltd, Yu Liang amesema amevutiwa na namna Tanzania inavyothamini wageni hasa wawekezaji. Anaamini watakuwa na muda mzuri wakiwa nchini kwenye shughuli za kukuza uchumi wa Afrika na China. 

"Udugu kati ya China na Tanzania ni wa kupigiwa mfano, tumezunguka maeneo mengi ambayo bwana Kiluwa alitueleza tukiwa China na sasa tumeamini hakika Tanzania inayo nafasi kubwa ya kukua katika sekta ya viwanda,,"amesema Liang.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group, Mohammed Kiluwa akitiliana saini na Rais wa kampuni ya Kiisu Minyuan International Trading Ltd, Yu Liang kuhusu mkataba wa makubaliano ya uwekezaji wa kujenga kiwanda cha sukari na kilimo. Makubaliano hayo yamefanyika leo katika ofisi za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group, Mohammed Kiluwa akipeana mkono mara baada ya kutiliana saini na Rais wa kampuni ya Kiisu Minyuan International Trading Ltd, Yu Liang kuhusu mkataba wa makubaliano ya uwekezaji wa kujenga kiwanda cha sukari na kilimo. Makubaliano hayo yaliyoshuhudiwa na Mkurugenzi Idara ya Uhamasishaji TIC John Mathew kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe, yamefanyika leo katika ofisi za Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya mashahidi Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group Naima Kiluwa na Mwakilishi wa kampuni ya Kiisu Minyuan International Trading Ltd, wakitia saini makubaliano kama sehemu ya Mashahidi wa tukio hilo 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group, Mohammed Kiluwa akizungumza jambo mbele ya Wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wawekezaji kutoka nchini China,mara baada ya kutiliana saini kuhusu mkataba wa makubaliano ya uwekezaji wa kujenga kiwanda cha sukari na kilimo.
Mkurugenzi Idara ya Uhamasishaji TIC John Mathew kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe, (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wawekezaji wa nchini Tanzania na China mara baada ya kumaliza kusaini makubaliano yao,leo katika ofisi hizo jijini Dar
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group, Mohammed Kiluwa akipeana mikono na Wabia wake mara baada ya kusaini makubaliano yao leo jijini Dar
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live




Latest Images