Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MEI 25,2019


WAFANYABIASHARA NCHINI WATAKIWA KUBORESHA VIFUNGASHIO-BRELLA

$
0
0
 Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzana Senso akisisitiza jambo kwa Kaimu Afisa Forodha wa Kituo cha Horohoro Nsajigwa Mwambegele katikati ni Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo
Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo katikati akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani wakati wa ziara hiyo kushoto ni Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzana Senso kulia ni Kaimu Afisa Forodha wa Kituo cha Horohoro Nsajigwa Mwambegele
Kaimu Afisa Forodha wa Kituo cha Horohoro Nsajigwa Mwambegele katikati akiteta jambo kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo kulia ni Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzana Senso
Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzana Senso kushoto akitetaa jambo na Kaimu Afisa Forodha wa Kituo cha Horohoro Nsajigwa Mwambegele wakati wa ziara hiyo
Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzana Senso kulia akiwa na Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo
Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo katikati akiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ziara hiyo kushoto ni Afisa Mfawidhi wa Forodha wa Kituo cha Horohoro Bakari Athumani kulia ni Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzana Senso
Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo kulia akimkabidhi vipeperushi Afisa Mfawidhi wa Forodha wa Kituo cha Horohoro Bakari Athumani kushoto mara baada ya ziara hiyo
Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo akisaini kitabu cha Wageni mara baada ya kufika ofisi ya Forodha kituo cha Horohoro mpakani mwa Tanzania na Kenya wakati wa ziara yake wakati zoezi la Uhamasishaji wa utengenezaji wa bidhaa bora katika soko hilo ambapo alisema bidhaa bora ni lazima ziwe kwenye kifunganisho ambacho pia kitaonyesha taswira halisi ya thamani.
Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo kulia aakiteta jambo na Kaimu Afisa Forodha wa Kituo cha Horohoro Nsajigwa Mwambegele
Kaimu Afisa Forodha wa Kituo cha Horohoro Nsajigwa Mwambegele kushoto akiteta jambo na Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo wakati wa ziara yake wakati zoezi la Uhamasishaji wa utengenezaji wa bidhaa bora katika soko hilo ambapo alisema bidhaa bora ni lazima ziwe kwenye kifunganisho ambacho pia kitaonyesha taswira halisi ya thamani.



WAFANYABIASHARA wa Kati na Wakubwa nchini wametakiwa kuboresha vifungashio vya bidhaa zao katika soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuepuka kupoteza ubora na bidhaa wanazotengeneza kutokana na kukosekana kwa hali hiyo

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Utawala na fedha wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELLA) Bakari Mketo wakati alipofanya ziara ya kutembelea mpaka wa Horohoro unaotengenisha ya Tanzania na Kenya.

Ziara hiyo ilikuwa ni zoezi la Uhamasishaji wa utengenezaji wa bidhaa bora katika soko hilo ambapo alisema bidhaa bora ni lazima ziwe kwenye kifunganisho ambacho pia kitaonyesha taswira halisi ya thamani.

Aidha alisema kwamba lazima wafanyabiashara wahakikisha wanakuwa bora kwenye kuzipa thamani bidhaa zao kwani vifungashio sio kupaki tu bali hata ujumbe uliopo na nembo ya bidhaa anuani na eneo ambalo unapatikana ili kurahisisha upatikanaji wake.

“Isije kutokea watu wanakaa na vifungishio vya nchi jirani kuliko vya hapa nchini inafanya wakati mtu anaponunua bidhaa za ndani hajisikii kukaa na bidhaa hiyo kuliko ilivyokuwa vya nje kwenye soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki hivyo lazima tuingie kwenye ushindani tukiwa na ubora wa vifungashio”Alisema, 

Mkurugenzi huyo alisema walichokuwa wakiangalia kwenye ziara hiyo ni namna gani brella wanaweza kupata huduma ya boda linki kwa kuhusanisha na kituo hicho cha horohoro ili kuhakikisha wadau wao hawapati usumbufu kwenye urasimishaji wa biashara zao .

Naye kwa upande wake Msajili Msaidizi Kitengo cha Ubunifu (Brella) Suzan Senso alisema mpaka sasa wamekwisha kutembelea mikoa 17 ambapo sehemu kubwa ya wafanyabiashara wamehamasika na kuanza kusajili biashara zao ili kukuza thamani ya bidhaa wanazozalisha.

Alisema pamoja na mambo mengine watawaelimisha waafanyabiashara kuhusu mfumo wa usajili wa ORS hivyo wanaimani kubwa mwitikio wa wafanyabiashara kujisali utaongezekana kutokana na kupata uelewa wa masuala mbalimbali .

NYONGO ASHUHUDIA JIWE LA ALMASI LA UZITO WA “CT” 512.15 LIKIUZWA KWA BILION 3, 262, 149, 332

$
0
0
Naibu waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akionyesha jiwe la madini ya Almasi lenye uzito wa “ct” 512.15 leneye thamani Tsh. Bilion 3, 262, 149, 332.75 mali ya mchimbaji mdogo bwana Joseph mkazi wa Shinyanga. Kushoto kwake ni Kamishna wa Madini Prof. Mruma na kulia kwake ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko. 
Kamishna wa Tume ya Madini Prof. Mruma akimuonyesha jambo Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo jiwe la madini ya Almasi lenye uzito wa “ct” 512.15 leneye thamani Tsh. Bilion 3, 262, 149, 332.75 wakati wa mauzo yake yaliyofanyika katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga. 
Bi. Dorcas Moshi, Mchambuzi na Mthamini wa Madini ya Vito na Almasi kutoka tume ya Madini akiifunga rasmi Almasi ya Josephy Temela mara baada ya kukamilika kwa taratibu za uthaminishaji na kupata ghara halisi huku ikishuhudiwa na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo mwenye suti ya Blue. 
Bw. Joseph Temba mchimbaji mdogo ambae ameuza jiwe lake la madini ya Almasi lenye uzito wa “ct” 512.15 leneye thamani ya Tsh. Bilion 3, 262, 149, 332.75 wakati wa mauzo yake yaliyofanyika katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga. 


Na: Issa Mtuwa (Wizara ya Madini) – Shinyanga 

Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, ameshuhudia mchimbaji
mdogo wa madini ya almasi bwana Joseph akijizolea fedha, dola za
kimarekani (USD) milioni 1, 418,510.82 ambazo sawa na Tsh. bilioni 3,
262,149,332.75 kutokana na mauzo ya jiwe moja lenye uzito wa Kareti
(ct)512.15. Shuguli ya mauzo ya Almas hiyo imefanyika leo tarehe
25/05/2019 katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga na kushuhudiwa
pia na Kamishna wa Tume ya Madini Prof. Mruma na vyombo mbalimbali
vya usalama na wawakilishi wa benki ya CRDB Shinyangai. 

Akiongea wakati wa kushuhudia mauzo hayo , Naibu waziri Nyongo
amesema, kutokana na mauzo hayo serikali itapata USD 103,551.29 sawa
na Tsh. milioni 238,136,901.61. Ameongeza na kusisitiza kuwa, adhima ya
serikali ya awamu ya tano ni kuwezesha shuguli za wachimbaji wadogo na
wadau wote wa sekta ya madini kufanyika kwa utaratibu unao eleweka
kwa faida yao na ya serikali. 

“Nimpongeze bwana Joseph ambae anauza almasi yake hapa leo kwenye
soko hili la madini, kila kitu kinakuwa wazi mbele ya serikali, polisi, watu wa
usalama na wawakilishi wa Bank ya CRDB, bila usumbufu wowote, na hiki
ndicho tunachokitaka sisi kama serikali, wachimbaji wote kufuata utaratibu
tuliouweka.

Niwaombe wachimbaji kwa mara nyingine, acheni kuuza madini
mchochoroni haita wasaidia zaidi ni kuhatarisha usalama wenu, na pengine
hata kupunjwa kutokana na kuto kujua thamani halisi na bei ya madini yenu
igeni mfano wa bwana Joseph, na niwaambie ukweli ukikamatwa unauza
madini nje ya soko madini hayo yanataifishwa, hivyo utakuwa umekula
hasara na utachukuliwa hatua za kisheria.” amesema Nyongo. 

Kwa upande wake Afisa msaminishaji madini kutoka tume ya Madini Bi.
Dorcas Moshi, Mchambuzi na Mthamini wa Madini ya Vito na Almasi
kutoka tume ya Madini aliekuwa anafanya shuguli nzima ya uthaminishaji
wa Almasi hiyo, amefafanua kuwa fedha iliyopata serikali, Milioni
238,136,901.61 inajumuisha Mrabaha wa USD 85,110.65 sawa na Tsh.
Milioni 195,728,959.97, Ada ya ukaguzi ni USD 14,185.11 sawa na Tshs.
32, 621, 493, .33 na Mrabaha wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu ilikotokea Almasi hiyo (Service Levy) ni USD 4,255.53 sawa na Tsh. 9,
786,448. 

Kwa upande wake Kamishina wa Madini prof. Mruma amewasisitiza
wachimbaji wadogo kuzingatia sheria na taratibu hususani kuchimba
kihalali kwa kuhakikisha wanakuwa na leseni za uchimbaji na kulipa tozo
zote za serikali kwani serikali ipo kwa ajili yao hivyo hawana sababu ya
kuikwepa. 

Kwa upande wake bwana Joseph mmiliki wa almasi hiyo, ameishukuru
Wizara ya madini na Tume ya madini kwa utaratibu waliouweka katika
kutoa muongozo na usimamizi wa namna ya mauzo ya madini
unavyotakiwa kufanyika, ulinzi wa madini yao pindi wanapoyapata na
ametoa wito kwa wachimbaji wadogo wenzake kuwa hakuna sababu ya
kuyakimbia masoko yaliyoanzishwa na serikali kwani yanafaida nyingi
ikiwemo usalama, ulinzi, uwazi na utambuzi wa thamani halisi ya madini
kitu ambacho nadra sana kwenye masoko yasiyo rasmi.

Benki ya CRDB ni salama kutuma na kupokea mialmala ya kimataifa (International Transfers 2018)

$
0
0
Mkurugenzi wa benki ya (CRDB) Bw. Abdulmajid Nsekela amepokea tuzo ya Benki ya (CRDB) kuwa benki salama na ya uhakika katika huduma kutuma na kupokea mialmala ya kimataifa (Iternational Transfers 2018) kutoka kwa Makamu wa Rais wa Citi Bank Afrika Mashariki Mary Sabwa Kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa (CRDB) Dkt Joseph Witts. Mkurugenzi wa benki ya (CRDB) Bw. Abdulmajid Nsekela akijadiliana jambo na Makamu wa Rais wa Citi Bank Afrika Mashariki Mary Sabwa mara baada ya kupokea tuzo ya Benki ya (CRDB) kutoka kwa Makamu wa Rais huyo kuwa benki salama na ya uhakika katika huduma ya kutuma na kupokea mialmala ya kimataifa (International Transfers 2018)
Mkurugenzi wa benki ya (CRDB) Bw. Abdulmajid Nsekela akizungumza na Makamu wa Rais wa Citi Bank Afrika Mashariki Mary Sabwa kulia aliyesimama ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa (CRDB) Dkt Joseph Witts.

SHULE YA MSINGI HOLILI YAPEWA MIFUKO YA SARUJI 300 KUFANIKISHA UJENZI WA MADARASA 10, NYUMBA ZA WALIMU

$
0
0
Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Godwin Kamando (kushoto), akikabidhi msaada wa mifuko 300 ya saruji yenye thamani zaidi ya shs Milioni 3,388,488 kwa Ofisa Mtendaji wa kata ya Holili, Fadhili Buzebuze (Ward Executive Officer) (watatu kulia) na Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Holili, Paschal Ntomola kwa ajili ya ujenzi wa Vyumba 10 vya madarasa, Ofisi 2 na nyumba 2 za walimu wa Shule ya Msingi Holili iliyopo wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro. Hafla ya makabidhiano ilifanyika kiwandani hapo Pongwe, Tanga jana.Wengine ni Maofisa wa kampuni hiyo.
Meneja Afya, Usalama na Mazingira wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Emmanuel Ntoma (wa pili kushoto), akikabidhi msaada wa mifuko 300 ya saruji yenye thamani zaidi ya shs 3,388,488 kwa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Holili, Paschal Ntomola (kulia) kwa ajili ya ujenzi wa Vyumba 10 vya madarasa, Ofisi 2 na nyumba 2 za walimu wa Shule ya Msingi Holili iliyopo wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro. Hafla ya makabidhiano ilifanyika kiwandani hapo Pongwe, Tanga jana.Wapili kulia ni Ofisa Mtendaji wa kata ya Holili, Fadhili Buzebuze na Wengine ni maofisa wa kampuni hiyo.
Meneja Ugavi wa Kampuni ya Tanga Cement (TCPLC), Livin Masawe (wa pili kushoto), akikabidhi msaada wa mifuko 300 ya saruji yenye thamani zaidi ya shs Milioni 3,388,488 kwa Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Holili, Paschal Ntomola (wapili kulia) kwa ajili ya ujenzi wa Vyumba 10 vya madarasa, Ofisi 2 na nyumba 2 za walimu wa Shule ya Msingi Holili iliyopo wilaya ya Rombo Mkoani Kilimanjaro. Hafla ya makabidhiano ilifanyika kiwandani hapo Pongwe, Tanga jana.Watatu kulia ni Ofisa Mtendaji wa kata ya Holili, Fadhili Buzebuze na Wengine ni Maofisa wa kampuni hiyo.



Na Ripota Wetu,Michuzi TV

KAMPUNI ya Tanga Cement (TCPLC), imetoa msaada wa mifuko 300 ya saruji kwa Shule ya Msingi ya Holili yenye thamani ya Sh.3,388,488 ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali kuimarisha sekta ya elimu.

Makabidhiano ya msaada huo yamefanyika katika kampuni hiyo iliyopo eneo la Pongwe mkoani Tanga ambapo viongozi wa ngazi mbalimbali Kata ya Holili na maofisa wa kiwanda hicho wameshuhudia makabidhiano hayo.

Akizungumza leo wakati wa kukabidhi msaada huo, Meneja Uendeshaji wa Kampuni ya Tanga Cement Godwin Kamando amesema lengo lao ni kusaidia maendeleo ya Kata ya Holili na wameona haja ya kusaidia sekta elimu kwa kutoa mifuko hiyo ya saruji kwa ajili ya Shule ya Msingi Holili.

"Msaada huu wa mifuko ya saruji ambayo tumeitoa katika Kata ya Holili ni kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa Shule ya Msingi Holili na hasa kwa kuitumia kujenga nyumba mbili za walimu, ofisi mbili za shule na ujenzi wa vyumba 10 vya madarasa 10,"amesema Kamando.

Ameongeza moja ya mkakati wao ni kurudisha sehemu ya faida yake kwa jamii ya Watanzania kwa kusaidia shughuli za maendeleo na msaada huo ni maalumu kwa ajili ya eneo hilo la Holili ambalo wao wamekuwa wakipata sehemu ya malighafi kwa shughuli za uzalishaji wa saruji.

" Malighafi inayopatikana eneo la Holili ni madini aina ya Pozzolana ambayo ni muhimu sana katika kutengeneza moja ya aina ya saruji,"amesema na kuongeza wanaamini msaada huo utatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kamando amefafanua pamoja na kusaidia katika shule hiyo, wamekuwa wakisaidia katika shughuli nyingine za kimaendeleo na hasa ya ujenzi wa miundombinu katika afya, elimu na mazingira na hadi sasa ndani ya kata hiyo wameshatoa jumla ya mifuko ya saruji 1150. 

Kwa upande wake Ofisa Mtendaji Kata wa Holili Fadhili Buzebuze amesema wanashukuru kupata msaada huo wa mifuko ya saruji na kufafanua watahakikisha mifuko hiyo inatumika kwa ajili ya malengo yaliyokusudiwa.

MTAJI WA BENKI YA BIASHARA MKOMBOZI WAFIKIA SHILINGI BILIONI 20.62 MWAKA 2018

$
0
0

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, Beatus Kinyaiya, akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Kumi wa Wanahisa wa Benki ya Biashara Mkombozi uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Thomas Enock na Kaimu Mwenyekiti wa bodi, Profesa Marcellina Chijoriga.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara Mkombozi, Thomas Enock, akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Kumi wa Wanahisa wa Benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, Beatus Kinyaiya na Mwenyekiti wa bodi, Profesa Marcellina Chijoriga.
Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu.
Wanahisa wakiwa kwenye mkutano huo.
Wanahisa wakijisajil kabla ya kuanza kwa mkutano huo
Mmoja wa Wanahisa akiuliza swali kwenye mkutano huo
Mwanahisa akichangia jambo kwenye mkutano huo




Na Dotto Mwaibale


MTAJI wa Benki ya Biashara Mkombozi umeongezeka kutoka shilingi za kitanzania bilioni 6.01 mwaka 2009 na kufikia shilingi za kitanzania bilioni 20.62 mwaka 2018.

Hayo yalisemwa na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa benki hiyo, Profesa Marcellina Chijoriga wakati akitoa taarifa kwenye mkutano mkuu wa kumi wa wanahisa,wa benki hiyo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.

" Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita tangu kuanzishwa kwa benki yetu mwaka 2009 tumeshuhudia ukuaji wake kutoka hadhi ya benki ndogo mpaka kufikia benki ya hadhi ya kati kwa mantiki ya rasilimali, amana za wateja, shughuli za uendeshaji na faida" alisema Chijoriga.

Alisema mpaka sasa benki hiyo imeweza kufungua matawi 10, manne katika mkoa wa Dar es Salaam, moja katika mikoa ya Morogoro, Moshi, Mwanza, Kagera na hivi karibuni Iringa na Dodoma.

Aliongeza kuwa rasilimali za benki hiyo zimekua kutoka shilingi za kitanzania bilioni 8.69 mwaka 2009 na kufikia shilingi za kitanzania bilioni 178.82 mwaka 2018.

Alisema Amana za wateja nazo zimeongezeka kutoka shilingi za kitanzania bilioni 2.19 mwaka 2009 na kufikia shilingi za kitanzania bilioni 136.47 mwaka 2018 huku mikopo ikikua kutoka shilingi bilioni 37 mwaka 2009 na kufikia shilingi bilioni 99.04 mwaka 2018.

Alisema benki hiyo imefanikiwa kulipa gawio kwa wanahisa la thamani ya shilingi za kitanzania bilioni 0.41 mwaka 2016 na shilingi bilioni 0.52 mwaka 2017.

Akitaja mafanikio ya benki hiyo kwa mwaka 2018 alisema licha ya matatizo ya kiuchumi na mazingira ya soko benki hiyo iliweza kupata faida baada ya kulipa kodi ya shilingi za kitanzania milioni 806.04 na kuwa changamoto kubwa waliyokuwa nayo ilikuwa ni kuanza kwa matumizi ya Kanuni namba 9 ya Kanuni za Kimataifa za Uwasilishaji wa Taarifa za Fedha inayojulikana kitaalamu kama Internatipnal Reporting Standard (IFRS 9)

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dodoma, Beatus Kinyaiya ambaye ni mmoja wa Wakurugenzi wa benki hiyo aliwaomba wanahisa wa benki hiyo kwa kipindi hiki kutochukua hisa zao kwani hali ya soko duniani sio nzuri hivyo wasubiri hali itakapo kuwa nzuri ndipo wachukue kwa faida kubwa.

Masoko Mapya ya Madini Yaingiza Bilioni 34.3 Kwa Mwezi Mmoja

$
0
0
Na Frank Mvungi- MAELEZO 

Dhahabu ya Bilioni 34.3 imeuzwa katika Kipindi cha mwezi mmoja kupitia katika masoko 21 yaliyoanzishwa kwa ajili ya kuuza madini katika mikoa mbalimbali hapa nchini. 

Akizungumza katika mahojiano maalum na idara ya habari MAELEZO, Bungeni Jijini Dodoma Waziri wa Madini Mhe. Dotto Biteko amesema kuwa kuanzishwa kwa masoko hayo kumekuwa chachu ya kuongeza mchango wa sekta ya madini katika kukuza uchumi na pato la Taifa kwa ujumla. 

“ Katika kipindi cha mwezi mmoja tu yaani Machi 17 mpaka Aprili 17 mwaka huu,jumla ya kilo 409.3 za dhahabu pekee zenye thamani ya shiilingi bilioni 34.3 imeuzwa kupitia katika maduka yaliyoanzishwa katika mikoa mbalimbali” Alisisitiza Biteko. 

“katika kilo hizo,Mkoa wa Geita umeongoza kwa kufanya biashara ya jumla ya kilo 289,Kahama kilo 44,Mara kilo 13,lakini cha kufurahisha zaidi ni kwa Wilaya ya Chunya ambako jumla ya kilo 52 zimeuzwa katika soko hilo zikiwa nia siku chache toka kufunguliwa kwake ,”,aliongeza, mheshimiwa Biteko. 

Aidha mheshimiwa Biteko, katika mahojiano hayo maalum,ameeleza kuridhishwa na biashara inayofanyika katika maduka hayo ya madini kote nchini na kueleza kuwa licha ya mafanikio hayo yaliyofikiwa katika kipindi kifupi,serikali inashughulikia changamoto ndogondogo ikiwemo wafanyakazi,mashine za XRF na idadi ya watoa vibali. 

Akifafanua amesema kuwa dhamira ya Serikali ni kuona sekta hiyo inatoa mchango stahiki katika kujenga uchumi na kuchangia maendeleo hapa nchini ndio sababu mkazo umewekwa katika kusimamia sekta hii. 

Pia aliwataka wachimbaji wadogo na madalali wa madini kuhakikisha kuwa wanatumia masoko hayo kikamilifu na kujiepusha na vitendo vyovyote vinavyoweza kusababisha kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufutiwa leseni jambo alilosema serikali haipendi, 

Akizungumzia mikakati ya kusimamia sekta hiyo Mhe. Biteko amesema kuwa ni pamoja na kushirikisha wachimbaji wadogo katika kuhakikisha kuwa vitendo vya utoroshaji wa madini unakomeshwa ili kulinda mapato ya Serikali. 

Aliongeza kuwa hatua nyingine ni usimamizi wa karibu katika maeneo yote ya uzalishaji wa madini ya aina mbalimbali na kuchukua hatua za kutatua changamoto mbalimbali katika sekta hiyo. 

Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Waziri Biteko amebainisha kuwa masoko mengine 7 yanatarajiwa kufunguliwa. 

Baadhi ya Mikoa ambayo imeshafungua masoko ya kuuza madini ni pamoja na Geita, Dodoma, Mwanza, Tabora, Shinyanga, Morogoro, Mbeya, ambapo tayari mikoa 21 imeshafungua maduka hayo hadi sasa ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alilolitoa kwa wakuu wa mikoa wote hapa nchini.

BENKI YA EXIM YAFUTURISHA WATEJA WAKE WA DAR ES SALAAM NA ZANZIBAR

$
0
0
 Mkuu wa Kitengo cha wateja wakubwa (corporate) wa benki hiyo Bw Shrikant Ganduri akizungumza wateja wa benki hiyo waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wakubwa wa  benki hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki
 Mmoja wa wateja wakubwa wa benki ya Exim Tanzania akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wateja wa benki hiyo waliohudhuria hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Mmoja wa wateja  wa benki ya Exim Tanzania  akiongoza ibada wakati hafla hiyo.
 Baadhi ya wafanyakazi wa benki ya Exim wakitoa neno la shukrani pamoja na utambulisho mbele ya wateja wa benki hiyo waliohudhuria hafla ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wakubwa wa  benki hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 
 Kaimu Mkuu wa Idara ya Mikopo wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Issa Hamis (kushoto) sambamba na Mkuu wa Kitengo cha wateja wakubwa (corporate) wa benki hiyo Bw Shrikant Ganduri (katikati) wakizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo waliohudhuria  hafla ya futari iliyoandaliwa kwa ajili ya wateja wakubwa wa benki hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki

 Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo na kati wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Andrew Lyimo (kulia) akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo pamoja na wageni waalikwa wakiwemo Waziri wa Habari, Michezo, Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar  Bw Mahamoud Thabit Kombo pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Bw Issa Haji Ussi wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa mwishoni mwa wiki kwa ajili ya wateja wa benki hiyo Zanzibar.
 Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo na kati wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Andrew Lyimo (wa pili kulia) akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo pamoja na wageni waalikwa akiwemo Waziri wa Habari, Michezo, Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar  Bw Mahamoud Thabit Kombo (kulia kwake) wakati wa hafla ya futari iliyoandaliwa mwishoni mwa wiki kwa ajili ya wateja wa benki hiyo Zanzibar
 Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo Waziri wa Habari, Michezo, Utalii na Mambo ya Kale wa Zanzibar  Bw Mahamoud Thabit Kombo (katikati) pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Bw Issa Haji Ussi (Kulia) wakijadili jambo walipokutana kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya Exim kwa ajili ya wateja wa benki hiyo Zanzibar iliyofanyika visiwani humo mwishoni mwa wiki.
Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo na kati wa Benki ya Exim Tanzania, Bw Andrew Lyimo (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo kutoka Dar es Salaam na Zanzibar kwenye hafla ya futari iliyoandaliwa na Benki ya Exim kwa ajili ya wateja wa benki hiyo Zanzibar iliyofanyika visiwani humo mwishoni mwa wiki.

CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE TANZANIA (TAWLA) CHATIMIZA MIAKA 30 TANGU KUANZISHWA KWAKE

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA)Tike Mwambipile akikata keki pamoja na viongozi wengine wa Chama katika Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama ulifanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Chama hicho kinatimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA)Tike Mwambipile akikata vipande vya keki huku viongozi wengine wa Chama hicho wakishuhudia katika Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama ulifanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Chama hicho kinatimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.
Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) Bi. Athanasia Soka akizungumza katika mkutano wa mwaka wa Chama hicho ulioshirikisha wanachama wake ambao ni wanasheria wanawake, Mkutano huo umefanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
viongozi wengine wa Chama hicho wakiongoza Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama ulifanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, Chama hicho kinatimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.
Jaji Winfrida Koroso Mwanachama mwandamizi wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania TAWLA akizungumza katika mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama hicho uliofanyika jana kwenye hotel ya Serena jijini Dar es salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA)Tike Mwambipile akifafanua jambo katika mkutano huo.
Meneja wa Benki ya (TIB) tawi la Samora Bw. Philip Pilla akitoa mada katika mkutano huo.
Mmoja wa wanachama wa chama hicho akiuliza swali katika mkutano huo.
Picha zikionyesha baadhi ya maofisa wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA).
Baadhi ya wanachama wa Chama hicho wakiwa katika mkutano huo.

Jaji wa Mahakamani Kuu ambaye pia ni mwanzilishi wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) , Joaquine De Mello amesema anafurahi kushuhudia chama hicho kikitimiza miaka 30 kikiwa kimepiga hatua kubwa na kinajiuza, hakijawahi kuyumba wala kutoka nje ya lengo la kuanzishwa kwake.

Alisema kipindi chote (TAWLA) kimekua mstari wa mbele kutumia taaluma ya kisheria kusaidia wanawake wasio na uwezo kupata msaada wa kisheria na haki zao ikiwa ni pamoja na kushughulika na masuala mbalimbali ya usalama barabarani.

Wanasheria wana faida kubwa, wanajua sheria, wanajua mikataba mbali mbali ya kisheria, lakini je wanatumiaje hizo nafasi zinapokuja?, lazima kujiulizaa kutafakari.

Wanawake ambao hawakupata nafasi ya kusoma, na wale wa ngazi za chini tunasema mfumo dume na kutojua sheria inayowakandamiza, sasa sisi tunaoijua tunaitumiaje, tunaonyesha mfano gani, tunafanya nini kama wanasheria.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa (TAWLA), Tike Mwambipile alisema chama hicho ambacho kinatimiza miaka 30 tangu kuanzishwa kwake, kinaendelea kutoa misaada mbali mbali ya kisheria kwa wanawake na vijana kujua haki zao akitea mfano sheria ya ardhi ambayo wote wana haki sawa ya kumiliki.

"Miaka 30 ya (TAWLA) changamoto bado nyingi hasa kwa wanawake wanaokuja kutaka msaada wa kisheria, unamsaidia kwa nia njema lakini wengine wanamalizana kifamilia, mwisho tunaonekana wabaya, na kuonekana ndio tunamshawishi, kuchukua hatua." alisema Mwambipile.

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA AFRIKA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA IKULU YA PRETORIA NCHINI AFRIKA KUSINI SIKU MOJA MARA BAADA YA KUAPISHWA NA KABLA YA KUTEUA BARAZA LAKE LA MAWAZIRI

$
0
0
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Pretoria nchini Afrika Kusini leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Pretoria nchini Afrika Kusini leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpa zawadi ya picha ya wanyama Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa baada ya kuwasili katika Ikulu ya Pretoria nchini Afrika Kusini leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya Kamusi ya Kiswahili na Kingereza pamoja na Vitabu vya Kiswahili Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa kwa ajili ya kujifunza lugha hio ya Kiswahili leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa akisikiliza maelezo yaliokuwa yakitolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi kuhusu vitabu hivyo vya Kiswahili leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa mara baada ya mazungumzo yao katika Ikulu ya Pretoria nchini Afrika Kusini leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na mwenyeji wake Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa wakati akizungumza na wanahabari Pretoria nchini Afrika Kusini leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na mwenyeji wake Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa wakifurahia jambo katika mazungumzo yao Pretoria nchini Afrika Kusini leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Rais wa Afrika Kusini Mheshimiwa Cyril Ramaphosa mara baada ya kumaliza mazungumzo yao leo Mei 26, 2019 ikiwa ni siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Nchi hiyo na kabla hajateua Baraza lake la Mawaziri. PICHA NA IKULU


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Mei, 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Mhe. Cyril Ramaphosa, Ikulu Jijini Pretoria. 

Katika Mazungumzo hayo, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Mhe. Rais Ramaphosa kwa kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Afrika Kusini na amemhakikishia kuwa Tanzania itadumisha uhusiano na ushirikiano wa kidugu na kihistoria na nchi hiyo ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Hayati Nelson Mandela kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha ANC (African National Congress). 

Mhe. Rais Magufuli amemshukuru, Mhe. Rais Ramaphosa kwa kumkaribisha kufanya nae mazungumzo siku moja baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Afrika Kusini na amebainisha kuwa anatarajia uhusiano wa Tanzania na Afrika Kusini utaimarishwa zaidi katika masuala ya uchumi na kukuza lugha ya Kiswahili. 

Kwa upande wake, Mhe. Rais Ramaphosa amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwake, na amemhakikishia kuwa Afrika Kusini inatambua mchango mkubwa wa Tanzania katika ukombozi wa Taifa hilo na kwamba katika kipindi chake cha uongozi wake atauendeleza na kuuza zaidi uhusiano huo. 

Mhe. Rais Ramaphosa amesema kufuatia uamuzi wa Afrika Kusini kuanza kufundisha lugha ya Kiswahili, nchi yake itachukua walimu wa Kiswahili kutoka Tanzania ili watumike kufundisha somo hilo katika shule za msingi na sekondari. 

Aidha, Mhe. Rais Ramaphosa ameahidi kufanya Ziara Rasmi ya Kitaifa nchini Tanzania kabla ya Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) uliopangwa kufanyika mwezi Agosti 2019 nchini Tanzania. Na pia atahudhuria mkutano huo. 

Kabla ya mazungumzo hayo Mhe. Rais Magufuli ambaye ameongozana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amemkabidhi Mhe. Rais Ramaphosa zawadi ya vitabu vya kusoma na kufundishia lugha ya Kiswahili kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). 

Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Rais Ramaphosa wamefanya mazungumzo hayo ikiwa ni kabla Mhe. Rais Ramaphosa hajatangaza Baraza lake la Mawaziri. 

Mhe. Rais Magufuli kesho ataondoka nchini Afrika Kusini na kuelekea nchini Namibia ambako atafanya Ziara Rasmi ya Kitaifa kwa mwaliko wa Rais wa Namibia Mhe. Hage Geingob. 

Gerson Msigwa 
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU 
Pretoria 
26 Mei, 2019

Vodacom join hands with Amana bank to launch an Islamic mobile saving product- Halal Pesa

$
0
0
 Vodacom Tanzania Director of M-Commerce, Epimack Mbeteni (L) and Amana Bank Managing Director, Dr. Muhsin Masoud launching Halal Pesa, a new and innovative M-Pesa mobile service that adheres to Islamic laws on earning profits in Dar es Salaam, over the weekend. The product is the first-to-market innovative product that ensures all citizens have access to formal micro-savings and investment solutions which adheres to Islamic laws.
Vodacom Tanzania Director of M-Commerce, Epimack Mbeteni (C) and Amana Bank Managing Director, Dr. Muhsin Masoud (2nd R) launching Halal Pesa, a new and innovative M-Pesa mobile service that adheres to Islamic laws on earning profits in Dar es Salaam, over the weekend. \

 Vodacom Tanzania in partnership with Amana Bank has launched a new M-Pesa mobile service dubbed “Halal Pesa”.  ‘Halal’, which means ‘lawful’ is a fitting statement to this first-to- market innovative saving product that ensures all citizens and Muslims have access to a formal micro-savings and investment solution which adheres to Islamic laws on earning halal profits. The launch ceremony took place at Serena hotel, Dar es Salaam and was attended by Muslims and other Telco’s customers.

The launch of Halal Pesa plays a key role in Vodacom’s strategy to become a key contributor in the rapidly growing Islamic Finance sector, as the product targets to service more than three quarter of the total Muslim population in the country through M-Pesa, where they will be able to save money and gain profit with incurring interest.

Speaking during the launch ceremony, Vodacom Head of M-Pesa department, Tulisindo Rashid said “Our decision to launch Halal-Pesa is a direct response to feedback from our customers that they want their digital financial services needs met within Shariah principles. For a long time, the Muslim population has been in need of a mobile financial saving system which is tied to the pillars of Islamic faith, and hence this is a solution that will allow Muslim customers to achieve their financial goals while cementing their faith by abiding to sharia laws”.

Vodacom continues to create innovative financial solutions for all by using digital technology at an affordable cost.  “Halal Pesa is a user friendly and distinct service that is in line with Islamic principles. The service has diverse choices including saving money for Hajj, children or long-term savings ranging from 3 to 12 months. Also, customers can use halal-Pesa to offer their contributions to the Mosque and Zakat”, added Tulisindo.  

Speaking during an interview with the media, Vodacom’s customer Hajjat Hawa Hilal said; “This service comes at the right time as we are in the holy month of Ramadhan. I have been using M-Pesa for quite a long time, but these new services have motivated me to save money for Hajj, Zakat and other plans in harmony with our Islamic sharia”, 

The Managing Director of Amana Bank, Dr Muhsin Masoud, said that their partnership with Vodacom is expected to have a positive impact on Tanzania’s Islamic banking sector. “As an Islamic Bank, we have ventured into enabling believers in Islamic faith to deposit savings through formal means. It is our joy to collaborate with Vodacom because, now, we are bringing our bank services closer to our customer’s through Halal-Pesa on mobile money” added Dr Muhsin. 

These efforts are in hand with the government’s National Financial Inclusion Framework strategy (2018-2022) that focuses on enabling citizens to have access to formal financial services. “We are supporting the government by innovating and developing services that suit the needs of the population. Halal-Pesa is for all M-Pesa users - Muslims and non-Muslims - who would like to save their money while adhering to Islamic sharia, and we remain firm in our commitment - to be the right partner to our customers in fulfilling their evolving demands; and to the Government’s agenda in increasing accessibility to financial services”, Tulisindo concluded.

NMB BANK NI TAASISI INAYOPASWA KUIGWA KWA UBORA WA HUDUMA ZAKE NCHINI -Waziri Mkuu

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania – Kassim Majaliwa akihutubia wageni mbalimbali waliohudhuria Futari iliyoandaliwa na NMB.
Mkurugenzi wa NMB Bank – Albert Jonkergouw akimkaribisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania – Kassim Majaliwa kwenye futari maalumu iliyoandaliwa na NMB jijini Dodoma kwaajili ya wateja na wadau mbalimbali.Pembeni ni Spika wa Bunge – Job Ndugai
 

Picha ya pamoja.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaja benki ya NMB kuwa ni taasisi inayopaswa kuigwa kwa ubora wa huduma akisifia namna walivyoweka mizizi katika maeneo ya vijijini ambako wengi hawajafika.

Majaliwa alitoa kauli hiyo juzi katika hoteli ya New Dodoma wakati benki ya NMB ilipowakutanisha wadau kutoka mkoani hapa kwenye futari maalum kwaajili ya Mwezi Mtukufu.

Waziri Mkuu alisema benki hiyo inaisaidia serikali katika juhudi za maendeleo hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linaelekea katika uchumi wa kati hivyo anaomba Watanzania kwa Umoja wao kudumisha, amani, upendo na mshikamano ili kufikia malengo.

Alisema serikali ambayo ina hisa ndani ya benki hiyo, itaendelea kushirikiana nao pale wanapoona inafaa kufanya hivyo lakini akawataka waendelee kuboresha zaidi huduma zao katika maeneo ambayo hawajafika.

“Siyo dhambi nikisema mnaongoza kwa kutoa huduma bora, nawashukuru kwa kujikita katika taasisi kama mashule ambako mmesaidia kupeleka madawati na vitabu, lakini nafurahi kusikia mmeanza kufadhili hadi kwenye michezo, nawapeni hongera, tutaendelea kuwatia moyo na popote mlipo,” alisema Majaliwa.

Katika ukaribisho wake, Mkurugenzi wa benki ya NMB Albert Jonkergouw alisema benki hiyo inajishusha kwa kuwakumbuka waumini katika kipindi hiki ambacho wanahitaji kuwa karibu na muumba wao hivyo wanaungana katika tendo hilo jema.

Jonkergouw alisema wataendelea kufanya hivyo na kufuata taratibu za huduma za fedha nyingi ikiwemo kuwasogezea zaidi huduma watu ambao wamekuwa wakizitafuta kwa gharama lakini akasema katika futari watahitimisha Mei 31 mkoani Tabora lakini kila mkoa wanatumia nafasi hiyo kuwaalika na wawakilishi kutoka maeneo ya jirani.

MIFUKO YA FIDIA KWA WAFANYAKAZI YA ZAMBIA NA TANZANIA YASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

TANZANIA na Zambia kupitia Mifuko ya Fidia kwa Wafanyakazi, wamesaini mkataba wa ushirikiano utakaosaidia kubadilishana uzoefu kati ya mifuko hiyo.

Akizungumza mara baada ya kutiliana saini mkataba huo, kwenye ofisi za WCF jijini Dodoma Jumatatu Mei 27, 2019, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba alisema, Zambia inauzoefu wa zaidi ya miaka 40 katika sekta ya hifadhi ya jamii katika kulipa mafao ya Fidia kwa Wfanyakazi kwa hivyo makubaliano hayo yana manufaa makubwa.

Alisema makubaliano hayo ni ya kawaida kati ya mifuko na kwamba WCF na WCFCB watabadilishana uzoefu katika masuala ya namna ya ulipaji mafao, namna ya kuzuia ajali na magonjwa kazini kwa sababu mambo hayo ni muhimu sana katika mifuko ya fidia.

“Nguvu kazi ya taifa inapolindwa tija huongezeka makazini na jambo hili hudhihirika pale pato la taifa linaongezeka hususan kwetu sisi ambao tunajenga uchumi wa viwanda jambo hilo ni muhimu sana.”Alisema Bw. Mshomba.

Alisema kwa uzoefu ambao Zambia watakuwa wameupata kutoka kwao wataweza kuboresha huduma zao, na tayari Dkt. Nkumbula amethibitisha kuwa serikali ya Zambia inautegemea Mfuko huo katika kusaidia nguvu kazi ya taifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Zambia (WCFCB), Dkt. Elizabeth Lungu Nkumbula alisema, imekuwa ni siku njema kwao kwa kujenga ushirikiano wa pamoja katika eneo la hifadhi ya jamii.

“Zambai na Tanzania chini ya uongozi wa Dkt. Keneth Kaunda na Mwalimu Nyerere, waliweza kujenga reli ya TAZARA na bomba la mafuta TAZAMA kwa hivyo ushirikiano huu wa leo ni kumbukumbu ya ushirikiano uliojengwa kwa muda mrefu na viongozi hao wa mataifa hayo mawili.” Alifafanua.

Alsema ushirikiano huu utasaidia pande mbili kubadilishana uzoefu katika kutoa huduma za ulipaji fidia na mbinu za kuzuia majanga yatokanayo na kazi na hivyo kusaidia mataifa hayo kukuza uchumi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba (kulia) na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kutoka Zambia, (WCFCB) Dkt. Elizabeth Lungu Nkumbula, wakibadilishana hati baada ya kusaini makubaliano ya ushirikiano baina ya mifuko hiyo, huku maafisa wa juu kutoka pande hizo mbili wakishuhudia katika hafla iliyofanyika ofisi za WCF Dodoma Jumatatu Mei 27, 2019.Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba (waliokaa kulia) na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Mfuko wa Fidia kwa Wfanyakazi kutoka Zambia, Dkt. Elizabeth Lunhgu Nkumbula, wakitia saini makubaliano ya ushirikiano baina ya mifuko hiyo, huku maafisa kutoka pande hizo mbili wakishuhudia katika hafla iliuofanyika ofisi za WCF Dodoma Jumatatu Mei 27, 2019.
Bw. Masha Mshomba akisaini
Dkt. Elizabeth Lunhgu Nkumbula, akiweka saini yake.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba akizungumza kwenye hafla hiyo. Kulia ni mgeni wake, Dkt. Elizabeth Lungu Nkumbulu.
Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kutoka Zambia, (WCFCB), Dkt. Elizabeth Lungu Nkumbula akizungumza katika hafla hiyo. 
Bw. Mshomba akimkabidhi zawadi ya picha mgeni wake, Dkt. Elizabeth Lungu Nkumbula.

RAIS DKT.MAGUFULI AWASILI NCHINI NAMIBIA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEJI WAKE RAIS WA NAMIBIA HAGE GEINGOB KATIKA IKULU NCHINI NAMIBIA

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Gwaride la Heshma aliloandaliwa mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Namibia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Hage Geingob mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikaribishwa na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Hage Geingob mara baada ya kuwasili Namibia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo yake na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Hage Geingob mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza ujumbe wa Tanzania katika mazungumzo ya pamoja na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Hage Geingob ambaye alikuwa akiongoza ujumbe

wake mara baada ya mazungumzo yao katika Ikulu hiyo ya Namibia.

Rais Magufuli afanya Ziara Rasmi ya Kitaifa nchini Namibia,afungua mtaa mkubwa uliopewa jina la Mwl. Nyerere

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewaagiza Mawaziri wa Tanzania kuitisha kikao cha Kamati ya Pamoja ya Tanzania na Namibia (
Joint Permanent Commission – JPC) ndani ya kipindi cha miezi 2 ili kujadiliana juu ya fursa mbalimbali za ushirikiano wenye manufaa kwa nchi hizo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo tarehe 27 Mei, 2019 wakati wa mazungumzo rasmi kati yake na Rais wa Jamhuri ya Namibia, Mhe. Dkt. Hage Geingob yaliyofanyika katika Ikulu ya Windhoek nchini Namibia ambako ameanza Ziara Rasmi ya Kitaifa ya siku 2 nchini humo.

Mhe. Rais Magufuli ametoa maagizo hayo baada ya yeye na Mhe. Rais Geingob kupokea taarifa kuwa kikao cha JPC hakijafanyika tangu mwaka 1999 na kusababisha masuala mengi yakiwemo ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji kutopata msukumo wa kutosha.

Amebainisha kuwa licha ya uhusiano wa kihistoria na kidugu wa Tanzania na Namibia ulioasisiwa na Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Rais wa Kwanza wa Namibia Mhe. Sam Nujoma, nchi hizo zimekuwa na kiwango cha chini cha ushirikiano wa kibiashara baina yake ambapo katika mwaka uliopita biashara iliyofanyika ilikuwa na thamani ya shilingi Bilioni 59.556 tu na kwamba nchini Tanzania kuna kampuni 2 tu za Namibia zinazofanya biashara.

Pamoja na kutoa maagizo hayo Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Mhe. Rais Geingob kwa kumualika kufanya Ziara Rasmi ya Kitaifa nchini Namibia na amemhakikishia kuwa Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano wowote unaohitajika ikiwemo kushirikiana katika masuala ya kilimo, ufugaji, uvuvi, utalii, usafiri wa anga, biashara, uwekezaji, utamaduni na kufundisha lugha ya Kiswahili ambacho baadhi ya nchi za Afrika zimeridhia kianze kufundishwa katika shule zake.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amesema kwa kutambua uhusiano wa kihistoria na kidugu, Tanzania inakamilisha maandalizi ya kufungua Ubalozi wake Jijini Windhoek ili kurahisisha masuala mbalimbali ya uhusiano, hususani katika uchumi ambayo yapo nyuma.

Kwa upande wake Mhe. Rais Geingob amemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa kufanya ziara hiyo na amesema Namibia inatambua na kuenzi mchango mkubwa wa Baba wa Taifa Hayati Mwl. Nyerere na Watanzania katika juhudi za ukombozi wa Namibia.

Amefafanua kuwa wakati wa kupigania uhuru wa Namibia, wapigania uhuru wa Namibia walipata nafasi ya kuweka kambi yao huko Kongwa Mkoani Dodoma ambako licha ya kupiga kambi walisaidiwa kupata mafunzo ya kijeshi na waliishi vizuri na wananchi wa eneo hilo jambo ambalo hawatasahau.

Mhe. Geingob ameungana na Mhe. Rais Magufuli kusisitiza umuhimu wa kutekeleza makubaliano yatakayowekwa katika kikao cha JPC na kwamba Namibia ipo tayari kuyatekeleza kwa maslahi ya Wanamibia na Watanzania.
Kabla ya kufanya mazungumzo rasmi, Mhe. Rais Magufuli amefanyiwa mapokezi rasmi ambapo amepigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride rasmi liliandaliwa kwa heshima yake katika viwanja vya Ikulu Jijini Windhoek.
Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli ametoa zawadi ya vitabu vya kusoma na kufundishia lugha ya Kiswahili na amemhakikishia Mhe. Rais Geingob kuwa Tanzania ipo tayari kutoa walimu na vitabu vya kufundishia Kiswahili nchini Namibia.

Nyakati za jioni Mhe. Rais Magufuli na Mhe. Rais Geingob wamefungua rasmi mtaa mkubwa uliopo katikati ya Jiji la Windhoek ambao umebadilishwa jina na kupewa jina la Julius K. Nyerere ikiwa ni kuenzi mchango wake mkubwa katika ukombozi wa Namibia na Bara zima la Afrika.

Akizungumza katika hafla ya ufunguzi wa mtaa huo Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Rais wa Namibia Mhe. Dkt. Geingob na Wanamibia wote kwa heshima hiyo na ameeleza kuwa Watanzania wanajisikia faraja kuona Namibia inatambua mchango mkubwa wa Hayati Mwl. Nyerere na Watanzania katika ukombozi wa nchi yao.

Mhe. Rais Magufuli amebainisha kuwa Hayati Mwl. Nyerere alikuwa kiongozi shupavu, aliyepambana na ukoloni, ubaguzi wa rangi na kupigania usawa, na ametoa wito kwa viongozi wa Afrika kumuenzi Hayati Mwl. Nyerere na viongozi wengine wa Afrika waliotoa mchango mkubwa wakati wa ukombozi kwa vitendo.

Meya wa Jiji la Windhoek, Mhe. Muesee Kazapua amesema Namibia imeamua kulipanga upya Jiji hilo na kubadili majina yote ya mitaa na kuyapa majina ya viongozi wa Afrika waliotoa mchango mkubwa katika ukombozi na maendeleo, na kwamba mtaa uliopewa jina la Julius K. Nyerere unaungana na mitaa mitatu yenye majina ya viongozi waliotoa mchango mkubwa katika ukombozi ambao ni Robert Mugabe, Jan Jonkerweg na Mandume Ndemufayo.

Katika hafla hiyo, Mhe. Rais Magufuli ameongozana na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Philip Mangula na Mtoto wa Baba wa Taifa Ndg. Makongoro Nyerere ambaye katika salamu zake kwa niaba ya familia ameishukuru Namibia kwa kuendelea kumuenzi na kumpa heshima Hayati Mwl. Nyerere na kwamba wanafamilia wanapokea heshima hiyo kwa umuhimu mkubwa.

Jioni hii, Mhe. Rais Magufuli amehudhuria Dhifa ya Kitaifa iliyoandaliwa na mwenyeji wake Mhe. Rais Geingob kwa heshima yake. Hafla hiyo imehudhuriwa na Mke wa Rais wa Namibia Mhe. Mama Monica Geingos, Rais Mstaafu wa Kwanza wa Namibia Mhe. Sam Nujoma na Rais Mstaafu wa Pili wa Namibia Mhe. Hifikepunye Pohamba.

Kesho, Mhe. Rais Magufuli atamaliza Ziara Rasmi ya Kitaifa nchini Namibia ambapo atatembelea kiwanda cha Nyama kilichopo Jijini Windhoek na kisha ataondoka kwenda nchini Zimbabwe ambako atafanya Ziara Rasmi ya Kitaifa kwa mwaliko wa Rais wa Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa.
  
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Windhoek
27 Mei, 2019
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifunua kitambaa na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob kuashiria uzinduzi rasmi wa mtaa Julius K. Nyerere ulipo katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia.Mei 27, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob alipokuwa akimuonyesha Makongoro Nyerere mtoto wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere mtaa mpya unaoitwa JULIUS K. NYERERE uliopo katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia.Mei 27, 2019. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob mara baada ya kuzindua mtaa mpya wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere unaoitwa JULIUS K. NYERERE uliopo katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia.Mei 27, 2019

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob mara baada ya kuzindua mtaa mpya wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere unaoitwa JULIUS K. NYERERE uliopo katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia.Mei 27, 2019

 Mtaa mpya wenye jina Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere unaoitwa JULIUS K. NYERERE ukifunuliwa rasmi mara baada ya kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia. Mei 27, 2019
 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimweleza Mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob alichokiandika kwenye kitabu cha kumbukumbu kwa Lugha ya Kiswahili Katika kuhakikisha Kiswahili kinatangazwa kimataifa mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Jijini Windhoek Nchini Namibia.Mei 27, 2019.
 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahi na mwenyeji wake Rais wa Namibia Mheshimiwa Dkt. Hage Geingob wakati wa hafla ya kuzindua mtaa mpya wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere unaoitwa JULIUS K. NYERERE uliopo katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia. Mei 27, 2019 
Picha namba 9  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapongeza Watanzania wanaoishi Namibia mara baada ya kuzindua mtaa mpya wa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere unaoitwa JULIUS K. NYERERE uliopo katika Jiji la Windhoek Nchini Namibia.Mei 27, 2019.PICHA NA IKULU

Rais Magufuli awasili nchini zimbabwe kwa ziara rasmi ya kitaifa ya siku 2

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Zimbabwe mheshimiwa Emmerson Mnangagwa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Robert Mugabe nchini Zimbabwe.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Zimbabwe mheshimiwa Emmerson Mnangagwa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Robert Mugabe nchini Zimbabwe.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Zimbabwe mheshimiwa Emmerson Mnangagwa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Robert Mugabe nchini Zimbabwe.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono pamoja na mwenyeji wake Rais wa Zimbabwe mheshimiwa Emmerson Mnangagwa wakati wakiangalia vikundi vya ngoma za asili mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Robert Mugabe nchini Zimbabwe. PICHA NA IKULU

  

MUFTI WA TANZANIA ASHIRIKI FUTARI ILIYOANDALIWA NA KIBADA GARDENS KIGAMBONI,ATOA NENO KWA WAGENI WAALIKWA

$
0
0
   Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally na Mh. Ali Davutoglu, Balozi wa Uturuki nchini Tanzania pamoja na baadhi ya wageni wakibadilishana mawazo kabla ya kufuturu.
     Muda wa Kufuturu (Iftar)
Maulid Kitenge (MC) akifurahia jambo pamoja na Mufti, Sheikh Abubakar Zubeir.
Mufti akitoa mawaidha kwa watu mbalimbali waliofika Kibada Gardens kwa ajili ya Iftar maalum  iliyoandaliwa siku hiyo,Mufti amewataka Waislamu waendelee kumcha Mungu na kuendelea kufanya matendo mema yanayompendeza Mwenyezi Mungu,na kwa si kwa wakati huu tu wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani,lakini pia wakati wote.
Sheikh wa msikiti wa Kibada akikabidhiwa baadhi ya vitu kwa ajili ya Futari kwa wakazi wa Kibada.
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mr. Ali Davutoglu akipeana mkono na Sheikh wa wilaya ya Kigamboni, Mr. Sharrif Hassan wakati wa Iftar iliyoandaliwa na Kibada Gardens Dar es Salaam. Pili kushoto ni Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir bin Ally
    Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zubeir bin Ally akitoa maneno ya hekima kwa baadhi ya watu waliofika katika Iftar maalum iliyoandaliwa na Kibada Gardens, Kigamboni Dar es salaam.
    Mufti wa Tanzania pamoja na baadhi ya masheikh wa bakwata wakiwasili Kibada Gardens kwa ajili ya Iftar iliyoandaliwa maalum katika mfungo wa Ramadhan unaoendelea.
1.      Kibada Gardens imeandaa Iftar maalum ambayo ilihudhuriwa na Mh. Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally na Mh.  Ali Davutoglu, Balozi wa Uturuki nchini Tanzania.

PSSSF YALIPA MALIMBIKIZO YA MAFAO ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 880 KWA WASTAAFU ELFU KUMI

$
0
0
NA K-VIS BLOG, DODOMA

ZAIDI ya Shilingi bilioni 880 zimetumika kulipa malimbikizo ya mafao ya wastaafu takriban elfu kumi (10000), wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma (PSSSF), Meneja Kiongozi, Uhusiano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma, (PSSSF), Bi. Eunice Chiume amewaambia waandishi wa habari jijini Dodoma leo Mei 29, 2019.

“Dhamira ya Mfuko ni kuhakikisha kuwa wanachama wake wanalipwa mafao yao kwa wakati na kwa hakika tutaendelea kutoa huduma bora kwa wastaafu na wanachama wetu.” Alisema Meneja huyo.

Alisema, wastaafu wote wanapaswa kuhakikiwa taarifa zao kama ambavyo matangazo yamekuwa yakielekeza “Hadi kufikia Aprili 30, 2019 jumla ya wastaafu waliojitokeza kuhakikiwa ni 113,962, huku wastaafu wengine 10, 509 wakiwa bado hawajaripoti kwenye ofisi zetu ili kuhakikiwa taarifa zao,” Alifafanua Bi. Eunice Chiume na kuongeza 

“Nitoe wito kwa wastaafu wote ambao bado hawajahakikiwa kufika kwwenye ofisi zilizo karibu naye ili ahakikiwe taarifa zake.” Alisema. 

Meneja huyo Kiongozi, Uhusiano alibainisha kuwa had hivi sasa, Mfuko una jumla ya wastaafu 124,000 na wanachama 763,000 na kuwahakikishia kuwa Watumishi wa PSSSF wamejipanga kutoa huduma bora kwa wastaafu na wanachama wa Mfuko huo katika ofisi zote za Mfuko zilizo Tanzania bara na Visiwani.

“Niwatoe hofu wastaafu, zoezi hili la uhakiki ni endelevu na kwamba Wanachama wanaweza kuwasiliana na Mfuko kupitia namba 0800 110 055, 0800 780 060 na 0800 110 040 (namba hizi ni bure). Pia wanaweza tuma ujumbe mfupi kwa namba 0735 117 773 na 0736 117 773 “PSSSF inaendelea kuunga mkono ujenzi wa uchumi wa viwanda kwa kuwekeza kwenye viwanda kikiwemo kiwanda cha kuzalisha viatu cha Karanga kilichoko mjini Moshi mkoani Kilimanjaro kinachoendeshwa kwa ubia kati ya Mfuko na Jeshi la Magereza.

Meneja Kiongozi, Uhusiano, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Eunice Chiume akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Mei 29, 2019. Amesema takriban wastaafu 10,000 kote nchini wamelipwa malimbikizo ya mafao yao.
Meneja Kiongozi, Uhusiano, Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) Bi. Eunice Chiume (kushoto), akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Mei 29, 2019. Amesema takriban wastaafu 10,000 kote nchini wamelipwa malimbikizo ya mafao yao. Kulia kwake ni Afisa Uhusianio Mwandamizi wa Mfuko huo, Bw. Abdul Njaidi. (PICHA NA MAELEZO).

BRELA WATUMIA MAONYESHA YA SABA YA KIMATAIFA YA BIASHARA JIJINI TANGA KUFANYA USAJILI WA PAPO KWA PAPO

$
0
0
Msajili Msaidizi kutoka kitengo cha Ubunifu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) Suzana Senso akitoa elimu kwa wanafunzi wa shule ya Msingi Mwakidila ambao walitembelea Banda leo lililopo eneo la Mwahako Jijini Tanga kunakofanyika maonyesho ya saba ya Biashara ya Kimataifa
Msajili Msaidizi kutoka kitengo cha Ubunifu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) Suzana Senso kushoto akiwa na kikundi cha Strong Women Group cha watu sita wakiwa wamepata cheti chao cha usajili cha jina la Biashara kwenye maonyesho ya Tanga Trade Fair 2019 
Msajili Msaidizi kutoka kitengo cha Ubunifu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) Suzana Senso kushoto akiwa na kikundi cha Strong Women Group cha watu sita wakiwa wamepata cheti chao cha usajili cha jina la Biashara kwenye maonyesho ya Tanga Trade Fair 2019 

WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA) umesema kwamba wameamua kushiriki maonyesho ya saba ya Biashara ya Kimataifa mkoani Tanga ili waweze kufanya usajili wa papo kwa papo majina ya biashara. 

Hayo yalisemwa leo na Msajili Msaidizi kutoka kitengo cha Ubunifu wa Wakala huo Suzana Senso wakati akizungumza na vyombo vya habari mjini hapa kuhusu uwepo wao kwenye maonyesho hayo yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwahako Jijini Tanga. 

Alisema baada ya kupata mwaliko kutoka TCCIA na hivyo kushiriki kwenye maonyesha hayo watakuwa wakitoa huduma za usajili wa makapuni, majina ya biashara na nembo za biashara 

“Kwa kweli niwaambie wakazi wa mkoa huu wa Tanga na mikoa ya jirani wachangamkie fursa hii ya kuweza kutumia muda huu kuweza kusajili majina ya biashara zao, makampuni na nembo lakini pia leseni daraja A lililokuwa linasajiliwa Wizara limerudishwa kwetu na hivyo pia wanasajili iwapo walengwa watakidhi vigezo vilivyowekwa “Alisema 

Hata hivyo alitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye kusajili ili kuweza kusajili kampuni lakini lazima vigezo na masharti husika vinavyohitajika kwenye upatikanaji wa leseni hiyo lazima uzingatiwe.

KAMPUNI YA JATU KUFANYA MKUTANO MKUU WA WANAHISA WAKE JUMAMOSI,JUNI MOSI JIJINI DAR

$
0
0
MKUTANO mkuu wa Kampuni ya Umma ya Jenga Afya, Teketeza Umaskini (Jatu TLC) umepangwa kufanyika Jumamosi June Mosi, katika Ukumbi wa Mgulani jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, wanachama wa Kampuni hiyo watachagua viongozi wapya wa bodi ambao watakua na jukumu la kuingiza kampuni hiyo kwenye soko la hisa ( DSE)

Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare alisema kuwa kampuni hiyo itaingia rasmi kwenye soko la hisa mapema mwezi August kwa mtaji wa Shilingi Bilion 7.5

Akizungumzia kampuni hiyo alisema ilianzishwa na vijana 2015 kuhusiana na masuala ya afya na lishe na haki za binadamu, watu wengi wanapata changamoto kwenye masuala mbali mbali, "Wengi ni maskini wanashindwa kumudu gharama za maisha na kusababisha migogoro kwenye jamii,"alisema na kuongeza

"Tuwe na afya lakini tuweze kujitegemea na kuwa na afya nzuri, tumejikita kwenye kilimo, masoko na bima ya afya, watu wengi wanahitaji kuwekeza katika biashara na kuhitaji mikopo.

Alisema kampuni hiyo ya umma imesajiliwa mwaka 2016 na imefanikiwa katika Kilimo cha Mpunga Kilombero, Manyara kilimo cha Alizeti na Mahindi, Tanga kulimo cha Maharage.

"Tunawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao watawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

"Igima kiwanda cha kukoboa mchele, Kibaigwa kiwanda cha mahindi na alizeti, tunaunganisha kilimo na viwanda, na soko tumelitengeneza wenyewe."

Alisema Jatu unaponunua chochote kama chakula, ni rahisi kukuza faida Kwani kuna mfumo rasmi wa kugawa faida, mteja akinunua bidhaa anapata bonasi ambapo gawio analipata mwisho wa mwezi.

Alisema kampuni hiyo imekuwa inawawezesha wakulima kulima kilimo cha kisasa, na kuwapatia wataalamu ambao wanawapa elimu, na kilimo ni cha muda wote kisichotegemea hali ya hewa.

“Kilimo kinalipa ukikitilia manani, Jatu tuna watu zaidi ya 13,000 ambao wanafanya kilimo na biashara, kama kampuni tunanufaika pia na kupata mazao moja kwa moja kutoka kwa mkulima bila kupitia kwa madalali wa kati.” alisema 

Alisemaunaweza kujiunga kwa kuuza bidhaa upata mgao kila mwezi au ujiunge kwenye kilimo, au kununua hisa kupata gawiwo ukapata faida kutokana na faida ya kampuni.
Mkurugenzi  Mtendaji wa JATU  PLC  Peter Isare
Viewing all 46362 articles
Browse latest View live




Latest Images