Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

KATIBU TAWALA ATUMIA WAANDISHI WA HABARI WA KASKAZINI KUTUMA SALAM KWA WAFANYABIASHARA

$
0
0
Na Woinde Shizza, Michuzi TV Kilimanjaro.

KATIBU Tawala wa Mkoa Kilimanjaro Mhandisi Aisha Amour amewataka wafanyabiashara kutoka mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kuitumia Bandari ya Tanga katika kusafirisha mizigo yao kwani hivi sasa imeboreshwa kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza katika kikao kati yake na waandishi wa waandishi wa habari wa mikoa ya Arusha na Kilimanjaro ambapo amesema wafanyabiashara wengi kutoka mikoa hiyo wamekuwa wakitumia kusafirisha mizigo kupitia bandari ya Mombasa nchini Kenya kutokana na changamoto ambazo zilikuwepo hapo nyuma lakini kwa sasa Bandari ya Tanga imeboreshwa.

Ametumia nafasi hiyo kuipongeza Mamalaka ya Bandari ya Tanzania chini ya uongozi wa Mhandishi Deusdedit Kakoko kwa jitihada kubwa za kuboresha miundombinu na utoaji wa huduma katika kiwango cha hali ya juu katika bandari ya Tanga na kuwa mkakati huo utaifanya bandari hiyo kuwa kimbilio la wafanyabiashara na wawekezaji. "Tunawaomba wafanyabiashara watumie hii Bandari ya Tanga kwani sasa hivi imeboreshwa zaidi ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa mitambo mikubwa ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kurahisisha utoaji huduma,"amesema Mhandishi Aisha. 

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Tanga, Percival Salama amesema kuwa bandari hiyo imeweza kuhudumia tani 506,000 Kwa kipindi cha mwaka 2017/2018 ambapo hadi kufika Juni mwaka huu watakuwa wamehudumia tani 700,000.Amesema bandari hiyo ina jumla ya mitambo 42 kwa sasa, ambapo kwa mwaka 2018/2019 imeagiza mitambo 20 kati ya hiyo mitambo 16 imeshawasili sawa na asilimia 80 .

Ameongeza hivi sasa changamoto ya suala la mitambo katika bandari hiyo limepatiwa ufumbuzi wa kudumu, hivyo kuwataka wafanyabiashara wa Arusha na Kilimanjaro kujitokeza Kwa wingi kuitumia bandari hiyo.

"Bandari ya Tanga ya sasa hivi si ile tuliyoizoea zamani, sasa hivi bandari imeboreshwa sana ikiwa ni jitihada za Mkurugenzi Mkuu wa bandari Tanzania, Mhandisi Deusdedit Kakoko lengo likiwa ni kuhakikisha wafanyabiashara wote waliokuwa wakitumia bandari zingine wanarudi nyumbani kwani sasa kumenoga,"amesema Salama. 

Amefafanua bandari ya Tanga ndio bandari pekee Afrika yenye uwezo wa kuhudumia nchi saba kwa kutumia mpaka mmoja, ambapo nchi hizo ni Malawi, Zambia, DRC Congo, Rwanda, Burundi, Uganda na Kenya.
 Katibu Tawala  wa mkoa wa  Kilimanjaro muhandisi Aisha Amour akiongea na waandishi Wa habari  katika mkutano  Wa waandishi Wa  habari   ulioandaliwa na mamlaka ya bandari ya Tanga  uliofanyika Leo katika ukumbi Wa mikutano Wa mkuu Wa mkoa Wa Kilimanjaro.

 Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye mkutano huo


WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUFANYA KAZI ZAO KWA WELEDI

$
0
0
WAANDISHI wa habari wametakiwa kufanya kazi zao kwa weledi na kusaka vyanzo tofauti katika habari zao badala ya kuegemea chanzo kimoja.

Hayo yalielezwa jana katika uzinduzi wa machapisho ya matatu ya Baraza la Habari Tanzania (MCT), ambayo ni ripoiti ya hali ya tasnia ya habari nchini ya mwaka 2017/2018 iliyoandikwa na Dr. Joyce Bazira, Muhadhiri wa Chuo Kikuu cha Zanzibar Dr Ali Uki na Henry Muhanika, chapisho la pili ni ukiukwaji wa maadili kwenye tasnia ya uandishi wa habari kilichoandikwa na Mhariri wa Gazeti la Daily News Pudenciana Temba na Attilio Tagalile, wakati chapisho la tatu ni fani ya uwandishi katika habari za kiuchunguzi zinavyoathirika ikitolea mfano kesi ya waandishi wa habari Ruvuma , ambapo kimeandikwa na Hamis Mzee, Lucas Liganga na Florence Majani.

Katika utafiti huo wa MCT unaonyesha kuwa vyombo vingi vya habari nchini vinakabiliwa na ugonjwa wa chanzo kimoja cha habari (SSS).

Akisoma ripoti hiyo, Mwenyekiti mstaafu wa Jukwaa la Wahariri Absalom Kibanda alisema kinachosikitisha zaidi kuhusu chanzo kimoja cha habari ni kwamba hutawaliwa na sauti za wanaume.

“Utafiti mmoja mahususi uliofanywa na MCT umeonyesha gazeti la Mwananchi lilikuwa na habari 99 za chanzo kimoja, ya vyanzo viwili zilikuwa 63 na habari za vyanzo vingi zilikuwa 158, habari zenye sauti za wanaume 1,913 sawa na asilimia 95 wakati zenye sauti za wanawake ni 93 sawa na asilimia tano.

Alisema utafiti huo pia umeonyesha gazeti la Nipashe lilikuwa na habari za chanzo kimoja ni 184, zenye vyanzo viwili ni 133 na habari za vyanzo vingi ni 103, habari zenye sauti za wanaume 1,307 sawa na asilimia 94 na zenye sauti za wanawake zilikuwa 88 sawa na asilimia sita wakati gazeti la Uhuru lilikuwa na habari za chanzo viwili zilikuwa 155 na habari za vyanzo vingi zilikuwa 204, huku zenye sauti za wanaume 3,111 sawa na asilimia 95 wakati sauti za wanawake zilikuwa 237 sawa na asilimia nane.

“Takwimu hizo zinaonyesha ukubwa wa tatizo ambalo lazima lishugulikiwe haraka na vyombo vya habari vya ndani, mfano kuna wakati Zito Kabwe anageuzwa yeye ndio waziri wa fedha, ndio profesa wa uchumi, ndio CAG, mchambuzi wa mambo ya uchumi, habari ukiikuta ni Zito alisema, aliongeza, alifafanua, waandishi toeni haki ya kujibu, hii itasaidia kukwepa vitanzi vya kisheria.”alisema Kibanda na kuongeza

“The Citizen walifungiwa wiki mbili, mimi namuunga mkono Dr Abbas kwa vile waliegemea upande mmoja walipaswa kupata upande wa pili lakini walikuwa na haraka, juzi kuna vyombi vya habaru vimeandikiwa barua baada ya kuandika ripoti aliyotoa Zito, ni sahihi kwa vile hawakutoa haki kwa mamlaka nyingine kujibu, hii ingesaidia, wasingepata kitanzi cha kisheria.”alisema Kibanda

Alisema changamoto kubwa kwa sasa hali ya uandishi wa habari ina wasomi lakini kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa kimaadili, msingi ya kitaaluma leo hii kuliko miaka ya nyuma ambapo wasomi walikuwa wachache.

“Waandishi wanatakiwa kujitazama na kujitathmini kama wanatimiza wajibu wao kitaaluma, mnapaswa kuwa makini kuliko wakati mwingine wowote.”alisema na kutolea mfano waandishi wa mitandao ya kijamii hususani you tube ambayo wamekuwa wakitoa kipande kidogo kwa makusudi na kuharibu maana nzima ya habari.

Akitolea mfano online tv alisema misingi ya kitaaluma inabidi ielekezwe huko kwani wamekuwa wakipotosha zaidi, bila kujali usahihi ulivyo na kusababisha mkanganyiko kwa jamii.

“Usahihi ni msingi namba moja hasa kwenye mitandao ya kijamii ambayo inafatiliwa kwa haraka, Uhuru uliopo usipitilize, misingi, maadili na miiko ya taaaluma inabidi itimizwe, la sivyo tusipotimiza hili, tutakwisha.”alisema

Alisema waandishi wa mitandao ya kijamii wanapaswa kufuata msingi wa kutoegemea upande wowote, na kuzingatia misingi ya kutoa haki na wajibu.

Kwa upande wa gwiji la habari, Pili Mtambalike ambaye alifanya rejea ya chapisho la Ukiukwaji wa Maadili kwenye Tasnia ya Uandishi wa Habari alisema ripoti hiyo imechukua miaka miwili ambayo ni 2017 na 2018 ambayo imepitia masuala ya sheria, sera, kanuni na changamoto mbali mbali zinazotokana na sheria za vyombo vya habari, kanuni na athari zitokanazo na sheria mpya ya vyombo vya habari.

Naye Atilio Tagalile akizungumzia ripoti ya Ruvuma ambayo waandishi wameenda kinyume na maadili ya vyombo vya habari alisema waandishi wanapaswa kushikamana na sio kuumizana na wasikubali kutumika.

“Waandishi wengi wa sasa ni wasomi, lakini inasikitisha baadhi yao hawana weledi kwenye kazi yao, nawakumbusha kwa nyakati hizi mnapaswa kufanya kazi zenu kwa umakini na weledi wa hali ya juu, la sivyo kuna anguko zaidi katika tasnia ya uandishi iwapo hatua hazitachukuliwa haraka.”alisema

Naye Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga alisema hali ya uhuru wa vyombo vya habari nchini imeporomoka kwa nafasi 47 katika nchi ndani ya miaka mitatu kuanzia mwaka 2016 hadi mwaka 2018, ambapo mwaka 2016 iliporomoka nafasi 12, mwaka 2017 ikaporomoka nafasi 10 na mwaka 2018 imeporomoka nafasi 25.

Kongamano la Kimataifa la QNET Lawaleta Pamoja wajasiriamali 13,000 Penang

$
0
0
Afisa Mtendaji Mkuu wa QNET na Wageni  wa heshima wakiwa wamepozi pamoja mara baada ya kukata utepe wa uzinduzi wa kongamano la siku tano la QNET
Wageni waheshima wa QNET, Maofisa wa Malaysia na wageni wa heshima waalikwa wakiwa kwenye sherehe za ufunguzi wa kongamano la siku tano la QNET lililofanyika jijini  nchini Malaysia  . Zaidi ya wajasiriamali 13,000 waliudhuria kwenye maonyesho hayo.


Kampuni maarufu ya kimataifa yenye asili ya Asia ya mauzo ya moja kwa moja, QNET inaendesha kongamano la siku tano la kimataifa ambalo linaleta pamoja takribani wajasiriamali 13,000 kutoka maeneo mbalimbali duniani katika kisiwa cha Penang 

Kongamano lenye hamasa litashuhudiwa na wasambazaji wa QNET kutoka katika zaidi ya nchi 30 watakao kutana pamoja katika ukumbi wa mikutano ya kimataifa na maonyesho wa Subterranean Penang International Conference & Exhibition Centre (SPICE) katika mji wa Bayan Baru, Penang, Malaysia 

Shughuli za ufunguzi wa sherehe zilifanywa na Yang Berhormat Profesa Dr. P. Ramasamy, Naibu Waziri Kiongozi II wa Penang, Mwenyekiti Mtendaji wa QI Group, Dato Sri Vijay Eswaran na Kaimu Naibu Mwenyekiti Joseph Bismark. Vile vile walikuwepo Mh. Cissé Ibrahim Sory, Meneja Mkuu wa Guinea Microfinance Agency ANAMIF, na washirika wengine wa biashara za kimataifa wa QNET kutoka Afrika, na sehemu mbalimbali duniani. 

Kongamano hili ambalo linajulikana kama V-Malaysia 2019 limefanyika Penang kwa miaka sita mfululizo. Wateja na wasambazaji kutoka katika masoko makubwa ya kikanda ya QNET katika Mashariki ya Kati, Katikati ya Asia, Afrika, Bara Hindi, Indonesia na Malaysia wanahudhuria kongamano la mwaka huu. Kongamano la siku tano litajumuisha mfululizo wa programu za mafunzo, hotuba za uhamasishaji, kutambulisha bidhaa mpya za mtindo wa maisha wa QNET na burudani. Kivutio kikubwa mwaka huu ni QNET Carnival ambayo itaonyesha zaidi ya nembo au lebo 50 za bidhaa za QNET katika moja ya maonyesho makubwa kuwahi kufanywa na kampuni hiyo. 

Katika hotuba yake, Naibu Waziri Kiongozi II wa Penang Profesa Dr. P. Ramasamy alitoa shukurani zake kwa QNET kwa kuja Penang kwa miaka sita mfululizo na kufanya kongamano kubwa la siku tano. 

"Ningependa kusisitiza kwamba Penang inajulikana vyema kwa ari yake ya ujasiriamali na kwa kutengeneza wajasiriamali kwa miaka mingi nchini. Ninahakika kwamba QNET itasaidia kuhamasisha wajasiriamali wa leo kuwa chombo cha mabadiliko ya kesho," alisema Dr. P. Ramasamy na kufuatia na shangwe za nguvu na makofi kutoka kwa wasambazaji wa QNET kutoka sehemu mbalimbaloi duniani. 

Mkurugenzi Mkuu wa QNET Bwana, Malou Caluza alisema: "Matukio kama haya ya Kongamano - V (V-Convention) linatupa fursa ya kuwahudumia wasambazaji wetu na kuwaruhusu kuwa na sisi kwa karibu. Tumewaleta takribani wafanyakazi 250 kutoka katika maeneo mbalimbali duniani kutusaidia katika kongamano hili na kuwapa washiriki wa kongamano hili uzoefu wa hali ya juu. Vile vile ni jukwaa bora la kusherehekea ari ya ujasiriamali ambayo kampuni ya mauzo ya moja kwa moja kama QNET inachochea kwa mamilioni ya watu duniani kote, kuwasaidia kuboresha maisha yao na kuchangia katika jamii." 

Akiongeza katika hilo, Meneja Mkuu wa QNET wa eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara bwana M. Biram Fall alisema: "V - Malaysia inafuatilia kongamano lenye mafanikio 2019 la msimu wa QNET Expo lililokuwa linajulikana kama Absolute Living, sambamba na misingi ya kampuni ya mauzo ya moja kwa moja na falsafa ya RYTHM - Raise Yourself to Help Mankind – inayofanyika kila mwaka katika nchi mbalimbali duniani kote ikiwa na lengo la kuonyesha bidhaa na huduma zake zilizoko sokoni ambalo lilianza mwaka 2019 jijini Dar es salaam, Tanzania mwezi uliopita, kisha kuhamia jijini Kumasi, Ghana na baadae katika nchi nyingine za Afrika. 

QNET, Kampuni tanzu inayoongoza ya kundi la makampuni la QI (QI Group of Companies), inauza reja reja bidhaa mbalimbali za Afya na ustawi, huduma binafsi na urembo, sikukuu, utunzaji wa nyumba na kozi kwa njia ya mtandao miongoni mwa nyingi zingine ambazo zinaboresha maisha ya kila siku ya wateja wake duniani kote. QNET iliwekwa katika moja kati ya makampuni 100 makubwa na imara ya MLM (Solid Top MLM Companies) kwa mwaka 2018 na Portal ya habari za mauzo ya moja kwa moja ya Business for Home.

TIC YAMSHUKURU RAIS MAGUFULI,YAKASIRIKA KUFUNGWA KWA BIASHARA, VIWANDA KWASABABU YA MADENI KATIKA KODI

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KITUO cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kimemshukuru Rais Dk.John Magufuli kwa namna anavyokipigania kituo hicho kufanikisha majukumu yake huku kikitoa rai kwa taasisi nyingine nchini kuacha kufungia viwanda na biashara kwani madhara yake ni makubwa.

Akizungumza leo Aprili 25,2019 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) Geoffrey Mwambe amesema wanamshukuru Rais kwani anawapigania sana akiwa katika ziara yake ya Lindi,Mtwara,Ruvuma na Njombe ametoa maagizo na maelekezo kwa TIC na taasisi nyingine zinazohusika na uwekezaji.

"Huu ni wakati wa kuacha kufikiria misaada na badala yake ni kuweka mipango kufanya uwekezaji, Rais anataka rasilimali zetu zitumike kuleta maendeleo. Kwa rasilimali ambazo nchi yetu inazo ni matajiri,nchi nyingine wanamiliki milima na barafu tu.  

"Kwetu sisi TIC Rais anatusaidia sana na imefika mahali akasema iwapo TIC haipewi nguvu kama yeye anavyotaka yupo tayari kituo cha uwekezaji kihamie katika ofisi yake lakini Waziri Mkuu naye amesema hayuko tayari kuona inaondoka kwake,"amesema.

Amefafanua pamoja na mafanikio ambayo yamepatikana TIC bado shida iko katika upatikaji huduma kwa wawekezaji na hiyo haiko kwao na tayari Waziri Mkuu amesema yupo tayari kukaa na wadau wengine kuweka mikakati itakayofaniksha wote kuzungumza lugha moja ya uwekezaji.

Mwambe amesema kila taasisi ijitoe kwa ajili ya maendeleo ya nchi na hivyo wanatoa ahadi kwa Rais kuwa wataendelea kupambana na kutekeleza majukumu yao kikamilifu ili dhamira njema ya Serikali ya Awamu ya Tano iweze kutimia katika kufanikisha uwekezaji nchini.

Kuhusu kufungiwa kwa wafanyabiashara na viwanda kwasababu ya kudaiwa kodi au vibali vingine kwa wawekezaji, Mwambe ametoa ushauri badala ya kufungia ni vema hiyo ikawa hatua ya mwisho kabisa kwani madhara yake ni mengi kuliko faida.

 " Ni vema taasisi nyingine zifahamu kufunga biashara za watu na kufunga kiwanda ni kuongeza hasara na iwapo kuna ulazima wa kufunga basi iwe hatua ya mwisho. Hivyo hakuna saabu ya kufunga biashara zipo njia nyingi za kufanya na biashara zikaendelea Unapofunga biashara kwa sababu ya kudai kodi , ukweli hutapata hiyo kodi na hakutakuwa na biashara,"amesema.

Amefafanua yeye ni mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) na katika vikao vya bodi  wamekuwa wakijadili kuhusu namna bora ya kudai kodi na wamekuwa wakikataa kufungia biashara na akaunti za wafanyabiashara.

"Mkurugenzi Mkuu wa TRA mara kadhaa amekuwa akieleza kufunga akaunti ni mchakato mgumu na sio kazi rahisi  na pale ambapo kutakuwa na kesi maalum kuna taratibu za kuafuatwa,"amesema Mwambe.

Amesisitiza "Kuna wimbi la watumishi wa TRA kwenda kufunga biashara za watu jambo ambalo si sawa. Kuna biashara ambazo kodi wanalipa kila siku,hivyo kufunga biashara maana yake TRA haitapata kodi na deni halitalipwa.Ninaumia sana ninapoona yale ambayo tunayazungumza kwenye bodi hayapo kwa watumishi wengine".

Wakati huo huo amesema ni wakati muafaka kwa kila taasisi kuhakikisha inafanya kazi kwa bidii ili kuondoa malalamiko yanayotolewa na wawekezaji nchini na iwe mwisho kuendelea kusikia malalamiko yakitolewa.

Pia Mwambe amesema Rais Magufuli amekuwa akishangazwa na idadi ndogo ya walipaji kado ambayo ni milioni mbili wakati kuna Watanzania zaidi ya milioni 50, hivyo ni wajibu wao kuhamasisha uwekezaji na hatimaye kuongeza idadi ya walipa kodi.

Mwambe pia amesema wanamshukuru Rais kwa kuwapa Jengo jipya lililopo pembeni mwa Jengo la ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kuwa makao makuu ya TIC na hivyo watahamia katika ofisi hizo siku za karibuni.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Geoffrey Mwambe akizungumza leo jijini Dar es Salaam kuhusu jitihada za kituo hicho katika kuhamasisha uwekezaji nchini 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)Geoffrey Mwambe akifafanua jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumzia namna ambavyo Rais Dk.John Magufuli ambavyo amekuwa karibu na kituo hicho ili kitekeleze vema majukumu yake.
 Mkurugenzi Mtendaji was Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC)Geoffrey Mwambe (wa kwanza kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam leo Aprili 25,2019

RAIS DKT. MAGUFULI NA RAIS PROF.MUTHARIKA WAZINDUA MSIMU WA SOKO LA TUMBAKU KANENGO - LILONGWE NCHINI MALAWI.

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Tumbaku ambayo ipo tayari kwa kuuzwa alipotembelea pamoja na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe kabla ya kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.
 Tumbaku ambayo ipo tayari kwa kuuzwa katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe 
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akikagua Tumbaku ambayo ipo tayari kwa kuuzwa alipotembelea katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe kabla ya Rais Dkt.John Pombe Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishangiliwa na Wanawake wa Lilongwe waliojitokeza katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe kumlaki  mara baada ya kukagua Tumbaku ambayo ipo tayari kwa kuuzwa alipotembelea pamoja na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika kabla ya kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  nchini Malawi.Aprili 25, 2019.

 Watanzania wanaoishi nchini Malawi wakimshangilia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kukagua Tumbaku alipotembelea katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe pamoja na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika kabla ya kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  nchini Malawi.Aprili 25, 2019.



 Sehemu ya Wananchi wa Malawi wakimshangilia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli huku mmoja akionyesha Picha yake wakati wa Sherehe ya Uzinduzi wa msimu wa Soko la biashara ya Tumbaku katika shehere zilizofanyika  Kanengo Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mwenyeji wake Rais wa Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika,Mama Janeth Magufuli, Prof.Gertrude Mutharika Mke wa Rais wa Malawi huku wimbo wa Taifa wa Malawi Ukipigwa wakati wa Sherehe za Uzinduzi wa Msimu mpya wa Soko la Tumbaku zilizofanyika katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe Lilongwe Malawi.Aprili 24, 2019.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika sherehe ya Uzinduzi wa Soko la Msimu mpya wa biashara ya Tumbaku katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe nchini Malawi.Aprili 25, 2019.

 Sehemu ya Wananchi wa Malawi wakimshangilia kwa nyimbo  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe wa Sherehe ya Uzinduzi wa msimu wa Soko la biashara ya Tumbaku katika shehere zilizofanyika  Kanengo Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikabidhiwa zawadi na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe kabla ya kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika mara baada ya kumkabidhi zawadi katika sherehe zilizofanyika Kanengo Jijini Lilongwe kabla ya kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mbele ya Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika na wananchi wa Malawi  katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe kabla ya kuzindua rasmi msimu wa Soko la biashara  Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.
 Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli akicheza ngoma pamoja na Mke wa Rais wa Malawi Prof.Grtrude Mutharika na Wanawake wa Malawi  katika eneo la Kanengo Jijini Lilongwe wakati wa sherehe za Uzinduzi wa msimu wa Soko la biashara  Jijini Lilongwe Malawi.Aprili 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mwenyeji wake na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika wakati wimbo wa Taifa wa Tanzania unapigwa katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kamuzu kabla ya kuanza safari ya kurejea Nchini Tanzania.Aprili 25, 2019.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua gwaride Lililoandaliwa na Jeshi la Malawi  kwaajili ya kumuuga katika  Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kamuzu kabla ya kuanza safari ya kurejea Nchini Tanzania.Aprili 25, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mwenyeji wake na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kamuzu kabla ya kuanza safari ya kurejea Nchini Tanzania. Aprili 25, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kumuaga Mwenyeji wake na Rais wa Jamhuri ya Malawi Prof. Arthur Peter Mutharika  na Wananchi wa Malawi katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kamuzu kabla ya kuanza safari ya kurejea Nchini Tanzania.Aprili 25, 2019.

Picha na Ikulu

Maadhimisho ya Miaka 55 ya Uhusiano wa Tanzania na China

$
0
0

Wasanii kutoka China wakitoa burudani katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Kikundi cha ngoma za asili kutoka Mwananyamala Jijini Dar es Salaam, kikitoa Burudani katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019. (Picha na Paschal Dotto-MAELEZO).



Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako Akizungmza katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China, iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke, akizungumza katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako akisalimiana na Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke mara baada ya kumaliza kuhutubia katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China, iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako, akiteta jambo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.Damas Ndumbaro na Katibu Mkuu CCM, Dkt. Bashiru Ally katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda na mkewe Tunu Pinda, wakifuatilia hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Faraji Mnyepe(kushoto), akifuatilia hotuba ya Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako, katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke (wa pili kushoto) akifuatilia burudani katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019, kushoto kwake ni Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako, Katibu Mkuu CCM, Dkt. Bashiru Ally, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.Damas Ndumbaro na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt.Agustine Mahiga.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, zimeadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia ulioasisiwa na Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mao Ze Dong, Rais wa kwanza wa China.

Akiongea katika maadhimisho hayo Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, amesema kuwa uhusiano huo umejenga urafiki mkubwa kwa Tanzania na China katika Nyanja zote za maendeleo.

“Napenda kuanza na Nukuu ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere ambaye alisema kuwa “sisi tunataka kuwa rafiki wa kila mtu na hatuwezi kuwa na rafiki ambaye anatuchagulia adui yetu”, China ilionyesha dhamira ya kuwa rafiki wa Tanzania, rafiki ambaye tulizuiwa kuwa rafiki yetu kipindi cha ukoloni, maneno haya ya Baba wa Taifa yalionyesha namna gani alivyokuwa anathamini urafiki wa Tanzania na China, kwa hiyo China ni rafiki yetu mkubwa”. Amesema Prof. Ndalichako.

Prof. Ndalichako ameeleza kuwa miaka 55 ya uhusiano huo umechochea kuwa na urafiki mkubwa ambao umeleta faida kwa kila nchi kwa sababu ya kujenga historia kubwa, kuthaminiana, kuheshimiana, kwa hiyo huo ni urafiki ambao kila mtu anamuheshimu mwenzie.

Prof.Ndalichako amesema kuwa katika maadhimisho ya miaka 55 kumekuwa na mafanikio makubwa katika Nyanja ya kiuchumi kwa kuwepo na miradi mbalimbali inayotokana na uhusiano China na Tanzania, miradi ambayo imetekelezwa ni Reli ya TAZARA, Kiwanda cha Urafiki, Kiwanda cha UFI, Kiwanda cha dawa keko, Kiwanda cha sukari Mahonda Zanzibar na Shamba la mpunga Mbarali.

Miradi mingine iliyotekelezwa kwenye urafiki huo ni Uwanja cha mpira wa Taifa, Uwanja wa mpira Amani Zanzibar, Bwawa la maji Chalinze, Kituo cha Mikutano Julius Nyerere, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Maktaba ya Chuo Kikuu Dar es Salaam ambayo ni maktaba kubwa kuliko zote ukanda wa Afrika pamoja na jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Prof. Ndalichako amesema kuwa China imekuwa ikiifadhili Tanzania nafasi 100 za wanafunzi kusoma China katika fani mbalimbali zikiwemo za uhandisi na udaktari “Kila mwaka China imekuwa ikitoa nafasi 100 kwa wanafunzi wetu kusoma nchini China, lakini pia katika maeneo muhimu kama udaktari kuna nafasi 20 za madaktari bingwa kwenye fani ya upandikizaji uboho na nafasi 30 kwa madaktari kwenda kusoma mafunzo mafupi, hakika huu ni urafiki mzuri na umekuwa na mafanikio makubwa”, amesema Prof.Ndalichako.

Kwa upande wa Miradi ya uwekezaji Prof.Ndalichako amesema kuwa tokea mwaka 1990 hadi Desemba mwaka jana tayari China ina miradi 723 ambayo imefanywa na wawekezaji kutoka China ambayo imetengeneza ajira 87,126, pia kwenye utalii Tanzania na China zimekuwa zikishirikiana kwa muda mrefu sasa.

“Tanzania na China zimekuwa na ushirikiano mkubwa pia katika sekta ya utalii na sekta ya utamaduni, ikiwemo kwa Chuo chetu cha Dar es Salaam na Dodoma kuwa na taasisi za kufundisha utamaduni wa China, lakini pia tumeanza kufundisha lugha ya kichina na mpaka sasa shule 15 zinafundisha lugha hiyo, kwenye utalii uzinduzi wa safari ya ndege yetu ya Dreamliner 787 itaanza safari zake moja kwa moja mpaka China na kuleta watalii wengi kutoka china kuja kutalii nchini”.

Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke alisema kuwa uhusiano huo ulioasisiwa na Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, Rais wa kwanza wa Tanzania na Mao Ze Dong Rais wa kwanza wa China, umeleta urafiki mkubwa kwa watu wa Tanzania na China.

“Hatuna budi kuulinda urafiki huu kwani ni urafiki wa faida, tumekuwa tukishirikiana katika miradi mbalimabli ikiwemo ujenzi wa reli ya TAZARA na miradi mingine ya maendeleo ambayo inaleta faida na manufaa kwa watu wetu”, alisema Wang Ke. Urafiki wa Tanzania na China ulianza mwaka 1964 mara baada ya Tanganyika na Zanzibar kuungana na kuunda Serikali ya Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MABALOZI WA KENYA, KUWAIT

$
0
0
*Asisitiza uwekezaji kwenye ujenzi wa viwanda

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefanya mazungumzo na mabalozi wa Kenya na Kuwait na kuwasisitizia kwamba Tanzania inakaribisha wawekezaji kutoka kwenye nchi zao na hasa eneo la ujenzi wa viwanda.

Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Aprili 25, 2019) alipokutana kwa nyakati tofauti na Balozi wa Kenya nchini, Bw. Dan Kazungu na Balozi wa Kuwait nchini, Bw. Mubarak Alsehaijan ofisini kwake bungeni jijini Dodoma.

“Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kujenga uchumi wa viwanda, tutafurahi tukipata wawekezaji kutoka Kenya ili waje wawekeze kwenye viwanda kwani tunajua Kenya ilianza mapema kujihusisha na ujenzi wa viwanda wakati sisi tukiwa bado na mfumo wa ujamaa,” amesema.

Waziri Mkuu alimweleza Balozi Kazungu kuwa anatambua kwamba miongoni mwa nchi za Afrika, Kenya inaongoza kwa uwekezaji hapa nchini lakini kwa fursa ambazo Tanzania inazo, bado wanayo nafasi ya kuja kuwekeza.

“Kwa kuzingatia kuwa Mheshimiwa Rais ameleta Waziri, Katibu Mkuu na TIC kwenye ofisi yangu, hii maana yake ninapaswa nisimamie suala la uwekezaji kwa karibu zaidi. Tumetengeneza blueprint, tumeweka taasisi 11 pale TIC za kurahisisha usajili na hivi sasa mwekezaji siyo lazima aje Tanzania, anaweza kujisajili mtandaoni hukohuko aliko,” amesema.

Pia alisisitiiza suala la kulinda amani katika nchi hizo mbili na hasa ulinzi wa mipakani. “Wenzetu mmepata mitisikiko ya ugaidi hivi karibuni, lakini ulinzi wa uhakika wa pamoja ni jambo linalojadilika na linalowezekana. Sisi tuko tayari kuwaunga mkono katika vita dhidi ya ugaidi, uharamia, na usafirishaji wa dawa za kulevya,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Balozi Kazungu amemshukuru Waziri Mkuu kwa ushirikiano ambao Serikali ya Kenya imekuwa ikiupata kutoka Tanzania na kuahidi kudumisha udugu ambao umekuwepo kwa miaka mingi.

“Sisi ni ndugu, tena ni majirani na mtu huwezi kuchagua jirani yako awe nani. Tunahitaji tuwe karibukaribu na kama ni biashara, basi watu wetu wawe wanafanya biashara kama majirani,” alisema Balozi Kazungu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemshukuru Balozi wa Kuwait kwa misaada ambayo nchi hiyo imekuwa ikiipatia Tanzania kupitia taasisi zake za kijamii.

Mbali na hayo, Waziri Mkuu amesema Serikali ya nchi hiyo kupitia Kuwait Fund, imesaidia ujenzi wa barabara ya Chaya-Nyahua (Tabora), mradi wa maji wa Same - Mwanga - Korogwe na ukarabati wa hospitali ya Mnazi Mmoja huko Zanzibar.

Amesisitiza kuwa bado Tanzania na Kuwait zinahitaji kuimarisha mahusiano yao katika maeneo mengine ya kiuchumi.

Naye Balozi Alsehaijan wa Kuwait amemshukuru Waziri Mkuu na kuahidi kuwa nchi yake iko tayari kuendelea kutoa misaada na huduma za kijamii.

Alisema kupitia taasisi za kujitolea, kuna mashirika manne (charity groups) ambayo yamejenga vituo vya watoto yatima Singida na Mwanza lakini kwa Mwanza, pia wameanza kuwahudumia na watu wenye ulemavu. “Pia wanajenga hospitali huko Zanzibar,” alisema.


 Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Balozi wa Kenya nchini, Dan Kazungu, ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma, Aprili 25, 2019. (Picha na  Ofisi ya Waziri Mkuu).
  Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Balozi wa Kenya nchini, Dan Kazungu, ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma, Aprili 25, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa, akisalimiana na Balozi wa Kuwait nchini, Mubarak Alsehaijan, ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma, Aprili 25, 2019.
Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa, akizungumza na Balozi wa Kuwait nchini, Mubarak Alsehaijan, ofisini kwake Bungeni jijini Dodoma, Aprili 25, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri  Mkuu Kassim Majaliwa, akijibu swali, katika kipindi cha maswali na  majibu, Bungeni jijini Dodoma, Aprili 25, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

RAIS DKT. MAGUFULI AWASILI MKOANI MBEYA NA KUWASALIMIA WAKAZI WA MBALIZI, NZOVWE, IYUNGA NA MAFIATI JIJINI MBEYA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwasili katika uwanja wa ndege wa Songwe mkoani Mbeya mara baada ya kuwasili akitokea nchini Malawi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Mbeya waliofika katika uwanja wa ndege wa Songwe kumpokea.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) aliyefika katika uwanja wa ndege wa Songwe kumpokea.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Mbalizi wakati akielekea Mbeya mjini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza wananchi wa Mbalizi mara baada ya kuwasili katika eneo hilo.
Wananchi wa Mafiati jijini Mbeya wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alipowasili katika eneo hilo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi (Sugu) katika eneo la Mafiati mara baada ya kuhutubia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Nzovwe mara baada ya kuwasili katika eneo hilo. PICHA NA IKULU.




RAIS DKT MAGUFULI ATEUA MWENYEKITI,WAJUMBE WA TASAF

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA JENGO LA NHIF NA KUHUTUBIA MAMIA YA WANANCHI WA JIJI LA MBEYA

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akivuta utepe pamoja na Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kuashiria ufunguzi wa Jengo la Ofisi za NHIF lililopo jijini Mbeya leo tarehe 26/04/2019.
2
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Afya Ummy Mwalimu mara baada ya kufungua Jengo la Ofisi za NHIF lililopo jijini Mbeya leo tarehe 26/04/2019.
3
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, Mwenyekiti wa Bodi ya  Mfuko huo wa Bima ya Afya Anna Makinda akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Jengo hilo.
4
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoka kwenye jengo hilo la NHIF mara baada ya kulifungua.
5
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia na kuwashukuru wananchi wa Mbeya waliokusanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya mara baada ya kuwasili.
67
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia na kuwashukuru wananchi wa Mbeya waliokusanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya mara baada ya kuwasili.
8910
Sehemu ya Wananchi wa Mbeya waliohudhuria Mkutano wa hadhara katika viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya.
11
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Mbeya katika viwanja vya Ruanda Nzovwe.
12
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa Mbeya katika viwanja vya Ruanda Nzovwe.
131415
Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi akiwa na wananchi wengine akifatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika Viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya. PICHA NA IKULU

DK.MABODI AMWAGA NEEMA KIJIJI CHA KIKOBWENI

$
0
0


 NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi akizungumza katika Mkutano wa Jimbo wa Jimbo la Chaani wa  kuelezea Utekelezaji wa Ilani ya CCM.
IMG_3592A
NAIBU Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Dk.Abdulla Juma Saadalla Mabodi(kulia) akimsikiliza Mkaazi wa Kijiji cha Kikobweni Ndugu Hassan Nganja(kushoto) aliyetoa maoni yake juu ya kuwepo na upungufu wa huduma za Maji Safi katika Kijiji hicho.
IMG_3545A
BAADHI ya Wananchi wa Jimbo la Chaani wakisikiliza kwa makini taarifa mbali mbali za Utekelezaji wa Ilani katika Jimbo hilo.
IMG_3578A
MWAKILISHI wa Jimbo la Chaani Unguja Mhe.Nadir Abdul-Tif Yussuf akizungumza na Wananchi katika Mkutano wa Jimbo hilo katika uwanja wa Mpira wa Kijiji cha Kikobweni Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja.
…………………….

NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.
NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Zanzibar Dk.Abudlla Juma  Saadalla Mabodi amesema CCM itachimba Kisima cha Maji Safi na Salama kwa  muda wa Wiki mbili ili kuondosha changamoto ya ukosefu wa huduma hiyo  kwa Wananchi wa Kijiji cha Kikobweni Jimbo la Chaani Wilaya ya Kaskazini  ‘A’ Unguja.

Ahadi hiyo ameitoa katika Mkutano wa Jimbo la Chaani wa kueleza  utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa Chama na Serikali,ambapo baadhi ya  Wananchi wa kijiji hicho wamedai  kukabiliwa na upungufu wa huduma za maji safi na kwa sasa wanatumia maji ya kisima cha zamani cha kuvuta kwa kamba  kisichokidhi mahitaji yao.

Dk.Mabodi alisema kwa hatua ya awali anatoa kiasi cha shilingi milioni  1.5 kwa ajili ya maandalizi ya uchimbaji wa kisima hicho ili wananchi wa  kijiji hicho na vijiji jirani wapate huduma hiyo kwa wakati hasa katika  mwezi Mtukufu wa Ramadhani unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Alisema wananchi wana haki ya kueleza changamoto zinazowakabili kwa  viongozi wao waliowapa ridhaa ya kuwaongoza katika ngazi mbali mbali za kiuongozi katika Chama na Serikali.

Alisema CCM ni Taasisi ya Kisiasa inayoahidi na ikatekeleza kwa vitendo na kwa wakati mwafaka na haitoi ahadi za kuwalaghai wananchi kama vinavyofanya baadhi ya vyama vya upinzani kuwa wataijenga Zanzibar kwa  Siku 100 iwe kama Nchi ya Singapore.

Alisema maendeleo hayana itikadi wala misimamo ya kisiasa kwani inapotekelezwa Ilani ya CCM kwa kuwafikishia wananchi huduma za maji,Umeme,Bababara na Vituo vya Afya fursa hizo hazitumiwi na Wanachama wa CCM pekee yao bali wananufaika wananchi wote.

Alieleza kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa sasa inatekeleza Ilani ya CCM kwa kujenga Barabara yenye kiwango cha Lami katika Mkoa wa Kaskazini Unguja ili kurahisisha huduma za Usafiri kwa wananchi wa Mkoa huo.

Katika maelezo yake Dk.Mabodi aliwambia wananchi wa Jimbo la Chaani kwamba Serikali ipo katika hatua za kutekeleza Mradi mkubwa wa Maji Safi na Salama ambapo ukikamilika utamaliza changamoto ya upungufu wa huduma za maji Mkoani humo.

Kupitia Mkutano huo Dk.Mabodi alielezea kuridhishwa kwake na Utekelezaji wa Ilani ya CCM katika Jimbo hilo, licha ya kuwepo kwa changamoto ndogo ndogo zinazotafutiwa ufumbuzi wa kudumu na viongozi wa jimbo hilo.
Aliwataka Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo hilo watatue changamoto zilizopo katika maeneo mbali mbali ya jimbo hilo ili Chama kishinde bila vikwazo  katika uchaguzi mkuu ujao.

Alisema CCM inapozungumzia ushindi wake wa Kihistoria katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2020, ni kutokana na utekelezaji mzuri wa ahadi zilizotolewa kupitia Uchaguzi Mkuu uliopita.

Pamoja na hayo aliwasihi wananchi wa Jimbo hilo kuthamini miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwani kuna baadhi yao wamekuwa wakihujumu miradi hiyo kwa makusudi hali inayokwamisha baadhi ya fursa za kimaendeleo.
” Nimeshuhudia katika Mkoa huu inahujumiwa miondombinu ya Maji Safi na Salama kwa kuiba vifaa vya umeme,kuharibiwa kwa Gari ya wagonjwa na matukio mengine ya kukatisha tamaa na yote hayo yanatekelezwa na watu wachache wapinga maendeleo.

Kupitia Mkutano huu nawambia waache Tabia hizo mara moja vinginevyo mtu yeyote atakayebainika anatekeleza uhalifu huo litakalomkuta litakuwa ni fundisho kwa watu wengine, kwani haiwezekani mtu kuharibu miundombinu inayotegemewa na makundi mbali mbali ya wananchi wakiwemo Wenye Mahitaji Maalum. “,alifafanua Dk.Mabodi.

Aliwaonya baadhi ya Watendaji na Viongozi wa Ngazi za Majimbo katika Wilaya ya Kaskazini ‘A’ Unguja, wanaojihusisha na mipango ya kuwaandaa wagombea wa ngazi mbali mbali za uongozi kabla ya muda wa kufanya hivyo kufika kwani kufanya hivyo ni kukiuka Katiba ya CCM ya mwaka 1977 na miongozo yake. 
Pamoja na hayo alisema kwamba CCM itaendelea kulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa gharama yeyote na atakayejaribu kubeza atakuwa ni msaliti na adui wa Taifa.

 Akitoa Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe.Nadir Abdul-Tif Yussuf alisema kwa kipindi cha mwaka 2016-2017 alitekeleza masuala mbali mbali yakiwemo kuvipatia fedha za mitaji vikundi vya ujasiriamali,alinunua Gari maalum la Wagonjwa,kuweka Taa za umeme za kuwasha usiku Viwanja Vitatu,kujenga visima vya Maji Safi na Salama pamoja na kununua mashine za Kilimo za Power Tiller kwa ajili ya shughuli za Kilimo.

Miradi mingine iliyotekelezwa ni pamoja na matengenezo ya Ofisi mbali mbali za CCM,ununuzi wa Dawa za Binadamu katika Vituo vya Afya mbali mbali mbali pamoja na ununuzi wa Vyarahani 10 kwa ajili ya vikundi vya Jimbo.

Mhe.Nadir alitoa alitoa tahadhari kwa baadhi ya Watu wanaotengeneza makundi ya kuwagawa na kuwafitinisha viongozi wa Jimbo hilo uku wakipanga wagombea kinyume na utaratibu na kuongeza kwamba watu hao hawakitakii mema Chama Cha Mapinduzi.

Wakizungumza kwa wakati tofauti Wananchi wa Jimbo hilo mara baada ya Mkutano huo,walieleza kwamba wamenufaika sana na miradi inayotekelezwa na fedha za Mfuko wa Jimbo wa Mwakilishi.

RAIS MAGUFULI ATOA MAAGIZO KWA TCRA KUTOZIFUNGA LAINI ZA SIMU AMBAZO HAZIJASAJILIWA

$
0
0

Na Said Mwishehe, Globu ya jamii

RAIS Dk.John Magufuli amesema mchakato wa kusajili laini za simu kwa kuunganisha na Kitambulisho cha Taifa(NIDA) usogezwe mbele hadi Desemba mwaka huu huku akiagiza Watanzania wasiokuwa na vitambulisho vya NIDA wasihukumiwe kwa laini zao kufungiwa.

Kabla ya kauli hiyo ya Rais Magufuli ambayo ameitoa leo Aprili 26,2019 akiwa mkoani Mbeya ,Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA) walitangaza kuwa watazima laini za simu ambazo hazitakuwa zimesajiliwa na kuunganishwa na NIDA kwa kuweka alama ya kidole kigumba ambapo pia walitangaza kuanza kwa usajili wa laini za simu kuanzia tarehe moja ya mwezi ujao.

Akizungumza leo akiwa ziarani mkoani Mbeya pamoja na mambo mengine Rais Magufuli amezungumzia usajili wa laini za simu uliotangazwa na TCRA ambapo amesema hakuna sababu ya kuwahukumu Watanzania kwa kuzima laini zao za simu kwa kigezo kwamba hawajasajili laini za simu.

Amesema ifahamike si kwamba anazuia usajili wa laini kwani ni muhimu na usajili huo una faida zake na ni nyingi lakini amefafanua Tanzania kuna Watanzania zaidi ya milioni 50 na wenye vitambulisho vya NIDA hawafiki milioni 15.

Hivyo amesema ni vema TCRA waongeze muda wa kusajili laini za simu kwa kwenda sambamba na utoaji wa vitambulisho vya Taifa. "Watu wasihukumiwe kwa kutosajili simu kwasababu ya NIDA.Mchakato uende pamoja ili watazania wasiopata wasihukumiwe," amesema Rais Magufuli .
 
Amesisitiza kadri NIDA wanavyotoa vitambulisho ndivyo kasi yake iendane na usajili wa laini za simu,hivyo wasifungue laini kwa kipindi hiki kwani kufanya ni sawa na kuwahukumu Watanzania.

Wakati huo huo Rais Magufuli ameagiza Jeshi la Polisi mkoani Songwe kuanza kuchunguza upya madai ya mtoto wa miaka minne wa kiume kulawitiwa.Rais ametoa maagizo hayo baada ya mmoja aliyekuwa katika mkutano wa Rais kupata nafasi ya kuzungumza mbele take ambapo alitoa malalamiko ya mtoto wake kulawitia.

Mama huyo baada ya kupewa nafasi ya kuzungumza amemwambia Rais Magufuli kuwa mtoto wake wa kiume amelawitiwa na sasa anajisaidia muda wote na baada ya kitendo hicho aliamua kwenda kwenye vyombo vya ulinzi na usalama lakini hadi sasa haana msaada wowote zaidi ya kuzungushwa.

Amesema kuwa amekwenda kuonana na Kamanda wa Polis Mbeya,Mkuu wa Jeshi la Polisi ncbini IGP pamoja na Jaji Mkuu lakini anaona anazungushwa tu,hivyo matumaini yake yamebaki kwa Rais Magufuli ambaye ni Rais wa wanyonge.

"Rais wangu naomba msaada wako,nimekwenda kila mahali hadi kwa Jaji Mkuu,nisaidie mheshimiwa Rais ,nyaraka za note ambako nimekwenda ninazo.Mtoto aliyelawitiwa ni mwanaume na picha yake ninayo,lakini kwenye makaratasi wanasema ni mwanamke," amesema mama huyo wakati anamuleza Rais.

Hata hivyo Rais alimuuliza kama amekwenda na mtoto huyo mkutano hapo lakini mama huyo akajibu ameshindwa kwenda naye kwani anajisaidia Mara kwa mara,hivyo hakuweza kufika naye

Kutokana na maelezo hayo Rais Magufuli alimhakikishia mama huyo kuwa uchunguzi utafanyika na haki itatendeka ambapo ameomba nyaraka akabidhiwe mwanasheria ili kuanza ufuatiliaji.

Pia Rais Magufuli alitoa maagizo kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha mama huyo hasumbuliwi huku akimpa fedha kwa ajili ya kujikimu na mtoto wake.

POLISI ARUSHA WAJENGA NYUMBA ZAO SIKU YA MUUNGANO

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akishiriki kubeba matofali wakati wa ujenzi wa nyumba za askari polisi eneo la Njiro mjini Arusha ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Sherehe za Muungano.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha (RPC), Jonathani Shana akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kushiriki ujenzi wa nyumba Sita za Polisi eneo la Njiro mjiani Arusha jana ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Muungano.
 Askari na baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani Arusha wakishiriki usaombaji wa matofauri wakati wa ujenzi wa nyumba za makazi kwa askari hao eneo la Njiro mjini Arusha ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya sherehe za Muungano. 
 Askari Polisi wakiwa chini ya msingi kwa ajili ya kumwaga zege wakati wa ujenzi wa nyumba za askari eneo la Njiro mjini Arusha ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za Muungano.
 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo mwenye jacket akiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha (RPC), Jonathan Shana wakishiriki kubeba zege wakati wa ujenzi wa nyumba za polisi eneo la Njiro mjini Arusha ikiwa ni sehemu ya sherehe za Muungano.
  Askari na baadhi ya Maofisa wa Jeshi la Polisi mkoani Arusha wakishiriki usaombaji wa matofauri wakati wa ujenzi wa nyumba za makazi kwa askari hao eneo la Njiro mjini Arusha ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya sherehe za Muungano. 
 
 

'TUNATAKA WATOTO WAZALIWE BILA VVU' - AGPAHI

$
0
0

Afisa Miradi Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Mwanza, Cecilia Yona akizungumza wakati wa kufunga warsha ya MAMA RIKA mkoa wa Mwanza Aprili 25,2019.



Tunataka Taifa la Tanzania liwe na watoto wanaozaliwa bila kuwa na Maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI (VVU)!

Haya ni maneno ya Cecilia Yona ambaye ni Afisa Miradi Huduma Unganishi kwa Jamii wa asasi ya Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) inayojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi Vya UKIMWI na UKIMWI, wakati akifunga warsha kwa MAMA RIKA mkoa wa Mwanza iliyolenga kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI.

MAMA RIKA ni Waelimishaji wa akina mama wajawazito na wanaonyonyesha wanaoishi na VVU ambao wanapata huduma za tiba na matunzo katika kliniki ya mama,baba na mtoto (RCH) ili kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto. Warsha hiyo ya siku mbili imemalizika Alhamis Aprili 25,2019 jijini Mwanza na kuhudhuriwa na MAMA RIKA 70,wauguzi, waratibu wa huduma ya afya ya uzazi,waratibu wa huduma za VVU na UKIMWI katika jamii mkoa wa Mwanza.

Afisa Miradi huyo wa Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Mwanza, Cecilia Yona alisema ili kuwa na watoto wanaozaliwa bila maambukizi ya VVU katika taifa la Tanzania ni lazima akina mama wanaoishi na VVU wapewe elimu ya kutosha kuhusu namna ya kuzuia maambukizi wakati wa ujauzito, kujifungua na wakati wa kunyonyesha.

“Hatuwezi kupata watoto ambao ni Free From HIV (watoto wasio na HIV),bila akina mama kuwa na elimu,ndiyo maana AGPAHI tumewakutanisha MAMA RIKA ili tuwajengee uwezo juu ya masuala ya VVU na UKIMWI na namna ya kusaidiana kupitia uzoefu kutoka ujauzito mpaka watoto wanapopata kipimo cha mwisho cha uhakiki”,alieleza Yona.

“Lengo la kuwa na MAMA RIKA kwenye vikundi ni kusaidia kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto,hivyo tunaamini mama akielewa vizuri,akipata elimu ya kutosha na akafuatilia yale aliyoelekezwa mtoto hatapata maambukizi ya VVU”,alisema.

“AGPAHI iko bega kwa bega kufanya kazi na MAMA RIKA,tunaamini kwamba huyu mama akijengewa uwezo vizuri kwa njia ya wataalamu na kufundishana wao kwa wao,wanapata nafasi kubwa ya kujifunza wenyewe kwa wenyewe kwa kutumia uzoefu walionao,yule ambaye ameshajifungua atamfundisha mjamzito, yule amemaliza kunyonyesha atamfundisha anayeanza kunyonyesha, kwa hiyo wanafundishana kwa njia ya uzoefu na elimu hiyo inakuwa sehemu ya maisha yao na kuwasaidia akina mama wengine”,aliongeza Yona.

Yona alitoa wito kwa washiriki wa warsha hiyo kuwa mabalozi na wasimamizi kwa akina mama wengine ili watakaporudi wakawasaidie akina mama waliopo katika kitengo cha kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Hata hivyo MAMA RIKA walioshiriki warsha hiyo walisema hivi sasa suala la ubaguzi na unyanyapaa limepungua kutokana na watu wengi kupata elimu kuhusu VVU na UKIMWI na wengi kujiweka wazi wakibainisha kuwa kupata maambukizi siyo mwisho wa maisha.

Aidha walishauri elimu iendelee kutolewa zaidi kwa akina mama wajawazito wahudhurie kwenye vituo vya afya wafundishwe mambo muhimu badala ya kufuata maneno mtaani na kujinyanyapaa matokeo yake wanajifungua watoto wenye maambukizi.
Afisa Miradi huyo wa Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Mwanza, Cecilia Yona akifunga warsha ya siku mbili ya MAMA RIKA mkoa wa Mwanza iliyofanyika katika ukumbi wa Gold Crest Hotel jijini Mwanza -Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog.

Cecilia Yona akiwasisitiza washiriki wa warsha hiyo kuwa mabalozi kwa akina mama wengine wawape elimu ya kutosha kuhusu masuala ya VVU na UKIMWI ili wazaliwe watoto wasio na maambukizi ya VVU.

Washiriki wa warsha wakiwa ukumbini.
Cecilia Yona akionesha kitabu cha mwongozo wa kuendesha vikundi vya akina mama wanaoishi na VVU wenye ujauzito na wanaonyonyesha kutoka kitengo cha kuzuia maambukizi ya toka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT).
MAMA RIKA,wauguzi, waratibu wa huduma ya afya ya uzazi na waratibu wa huduma za VVU na UKIMWI katika jamii wakionesha vitabu vya mwongozo wa kuendesha vikundi vya akina mama (PMTCT) baada ya kugawiwa wakati wa warsha hiyo. Kushoto ni Mwezeshaji wa kitaifa wa masuala ya Vijana,VVU na UKIMWI, Dkt. Happiness Wimile Mbeyela.
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini.

Awali,Mwezeshaji wa kitaifa wa masuala ya Vijana,VVU na UKIMWI, Dkt. Happiness Wimile Mbeyela akitoa mada kuhusu unyanyapaa na ubaguzi kwa watu wanaoishi na maambukizi ya VVU. Dkt. Happiness Wimile Mbeyela akisikiliza swali kutoka mmoja wa washiriki wa warsha hiyo.
Mwezeshaji katika warsha hiyo, Edwiga Zumba akitoa mada ukumbini.

Mwezeshaji katika warsha hiyo,Yahaya Isangula akiwasisitiza akina mama wajawazito na wanaonyonyesha wenye maambukizi ya VVU kuendelea kuwa wafuasi wazuri wa dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs).
Mmoja wa washiriki wa warsha hiyo akiuliza swali.
Mratibu wa huduma ya afya ya uzazi halmashauri ya wilaya ya Ilemela,Grace Kusaya akiwahamasisha MAMA RIKA kuwapa elimu akina wajawazito na wanaonyesha ili watoto wasipate maambukizi ya VVU.
Mratibu wa huduma ya afya ya uzazi halmashauri ya wilaya ya Misungwi, Flora Kuzenza akichangia hoja.

Kaimu mratibu wa huduma ya afya ya uzazi halmashauri ya wilaya ya Ukerewe, Laurencia Damas akizungumza ukumbini.
Picha ya pamoja washiriki wa warsha.


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog Soma pia : AGPAHI YAENDESHA WARSHA KWA MAMA RIKA MKOA WA MWANZA

DC MSHAMA AWAASA MADEREVA BODA KULIPIA VITAMBULISHO VYA UJASIRIAMALI

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA

MKUU wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama ,amewaasa madereva wa pikipiki maarufu kama bodaboda ,kulipia vitambulisho vya wajasiriamali na endapo watashindwa kufanya hivyo hawataruhusiwa kufanya biashara ya kubeba abiria.

Aliyasema hayo mjini Kibaha alipokuwa akizungumza na madereva hao na kusema ,wao ni moja ya kundi ambalo linapaswa kuwa na vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo ambapo wanatakiwa kulipia shilingi 20,000.

Mshama alisema kuwa agizo la watu wanaofanyabiashara ambayo mtaji wake hauzidi kiasi cha sh.milioni nne wanapaswa kuwa na vitambulisho hivyo .

“Mnapaswa kununua vitambulisho hivyo na kwa wale ambao hawatakuwa na vitambulisho hivyo hawataruhusiwa kufanya biashara hiyo hivyo hakuna budi kila mmoja wetu kuhakikisha analipia kiasi hicho ili waweze kufanya kazi bila ya usumbufu,” alisema Mshama.

Aliwataka wafanyabiashara wengine nao kulipa ili wapatiwe vitambulisho ambavyo Rais ametaka wajasiriamali wadogo wawe navyo kwani nao wanachangia uchumi wa taifa.

“Tunaendelea kuwahamasisha wajasiriamali wadogo wachangamkie fursa hiyo kwani ushuru waliokuwa wakilipa kwa sasa utakuwa haupo na kitambulisho hicho ndicho kitakuwa kimefidia na haitaruhusiwa kufanya bishara kama hawana vitambulisho hivyo,” alisema Mshama.

Kwa upande wake Bakari Kapera wa kitengo cha elimu ya mlipa kodi kutoka mamlaka ya mapato (TRA) mkoa wa Pwani alisema kuwa fedha wanazolipia leseni siyo kodi bali ni ada ili mtu kutambulika kuwa ni dereva.

Stanley Ndunguru kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Anga na Majini (SUMATRA) alisema kuwa malipo hayo yanalipwa na mmiliki wa chombo na siyo wao kama madereva kwani hawaruhusiwi kulipa ikiwa ni pamoja na bima. 

Awali mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha Jenifa Omolo alisema kuwa waendesha boda boda nao wametajwa kuwa nao ni mwiongoni mwa wanaotakiwa kulipia vitambulisho hivyo.

Katibu wa Chama cha Wamiliki na Waendesha Pikipiki wilaya ya Kibaha (CHAWAMAPIKI) Shaban Kambi alisema kuwa kilichosababisha wakashindwa kuchukua vitambulisho hivyo ni kutopatiwa elimu juu ya wanaopaswa kulipia.
MKUU wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama

WAZIRI MHAGAMA AWAPA HAMASA TUCTA KUANZISHA VIWANDA

$
0
0


 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza wakati wa Mkutano wake na Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) walipokutana kujadili masuala ya Wafanyakazi nchini leo Aprili 26, 2019, katika ukumbi wa PSSSF Jijini Dodoma. (Kushoto) ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Phillip Mpango, (wa tatu kutoka kushoto) ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jaffo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika na rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya.
????????????????????????????????????
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Phillip Mpango akielezea jambo wakati wa mkutano huo, Kulia ni  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama
????????????????????????????????????
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika (wa pili kutoka kulia) akisisitiza jambo kwa Viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) walipokutana kujadili masuala ya Wafanyakazi nchini leo Aprili 26, 2019, Jijini Dodoma. (Kushoto) ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Phillip Mpango na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama na (wa tatu kutoka kushoto) ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jaffo.
????????????????????????????????????
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde(wa kwanza kushoto) pamoja na  Katibu mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Andrew Massawe (katikati) na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) wakifuatilia mada wakati wa Mkutano huo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya Viongozi wa Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi (TUCTA) wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa Mkutano huo.
????????????????????????????????????
Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya akieleza jambo kuhusu masuala ya Wafanyakazi nchini walipokutana Aprili 26, 2019 Jijini Dodoma.
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akichangia mada wakati wa Mkutano huo walipokutana kujadili masuala ya wafanyakazi nchini wakati wa kikao hiko kilichofanyika Jijini Dodoma. 
????????????????????????????????????
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro akielezea jambo wakati wa Mkutano huo
????????????????????????????????????
Mwenyekiti Kamati ya Wanawake, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Bi. Rehema Ludanga akichangia jambo wakati wa mkutano huo.
????????????????????????????????????
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa Pili kutoka Kushoto) wakiimba kwa pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Phillip Mpango (Kushoto), (wa tatu kutoka kushoto) ni  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika na rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya.
????????????????????????????????????
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (wa Pili kutoka Kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Shrikisho la Vyama vya Wafanyakazi mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo. (Kushoto) ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Phillip Mpango, (wa tatu kutoka kushoto) ni Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamghokya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika na Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Anthony Mavunde.PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU
(KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
………………………..


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewataka viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi kuanzisha viwanda ili kuinua uchumi na kuchangia adhma ya Serikali ya kuwa na uchumi wa viwanda.

Ametoa kauli hiyo hii leo Aprili 26, 2019 Jijini Dodoma wakati wa mkutano wake na viongozi hao uliohudhuriwa na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Mkuchika, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo pamoja na Naibu Waziri anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana Mhe. Anthony Mavunde ili kujadili masuala yanayohusu wafanyakazi nchini.

Waziri mhagama aliwataka viongozi hao kuwa wabunifu kwa kuanziasha viwanda vitakavyowezesha kujikwamua kiuchumi pamoja na kuwajengea uwezo wa kujitegemea na kukuza mapato ya vyama vyao.

“Niwaombe sana muwe na mitazamo chanya katika kuchangia adhma ya Serikali kuwa na uchumi wa viwanda kwa kuanzisha viwanda vitakavyowawezesha kukuza uchumi mfano viwanda vya chaki, mbao na vingine vingi”, alieleza waziri Mhagama

Aidha aliwaeleza umuhimu wa kuanzisha viwanda hivyo ikiwa ni pamoja na kuchangia ukuaji wa uchumi nchini, kusaidia kuboresha maslahi ya wafanyakazi na kuongeza motisha na kutoa fursa za ajira kwa wananchi kwa ujumla.

“Hii leo nimeona niwape changamoto ya kuona umuhimu wa kuwa na viwanda vyenu kwa kuangalia mchango wenu katika jamii na kuendelea kuwa na tija kwa kuzingatia umuhimu wa kuwa na viwanda nchini,” alisisitiza Mhagama

Kwa upande wake rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini Bw. Tumaini Nyamhokya alishukuru mchango wa serikali na maoni yao kwa kuwapa chachu ya kuona umuhimu wa kuwa na viwanda na kuahidi kulifanyika kazi suala hilo.

“Kipekee nimefurahishwa na maoni na mawazo ya serikali hivyo hatuna budi kuanza kulifanyia kazi suala hilo ili kuendelea kuwa na mchango katika ukuaji wa uchumi wa nchi yetu”, alisema Nyamhokya

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Wanawake Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bi. Rehema Ludanga alieleza alivyopokea ushauri huo wa serikali na kuona ni namna bora ya kujishirikihsha katika uchumi wa viwanda na kuonesha utayari wa kufanyia kazi suala hilo.

“Binafsi nikiwa kama mwenyekiti Kamati ya Wanawake nimelichukua kwa dhati kabisa na nitajitahidi kulifanyia kazi mapema iwezekanavyo ili wanawake nao waweze kunufaika na fursa hii hasa upande wa sekta ya kilimo,” alieleza Bi. Rehema.

DKT MSONDE ATOA ONYO KWA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA

$
0
0


Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde akizungumza na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu walio katika kambi ya Kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, wakati alipotembelea kambi hiyo Aprili 25,2019.
PICHA B
Baadhi ya Wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu wakimsikiliza Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde (hayupo pichani) wakati alipowatembelea katika kambi ya Kitaaluma inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019.
PICHA C
Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju akizungumza kabla ya kumkaribisha Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde azungumze na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, walio katika kambi ya Kitaaluma  Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa  Aprili 25, 2019.
PICHA E
Mwanafunzi wa Kidato cha Sita Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa,  Julieth John akitoa shukrani kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde alipowatembelea Wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, Aprili 25, 2019  katika kambi ya Kitaaluma Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa
PICHA F
Mwanafunzi wa Kidato Cha Sita Shule ya Sekondari Simba wa Yuda,  Innocent Leonard  akitoa shukrani kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taiga(NECTA), Dkt. Charles Msonde alipowatembelea Wanafunzi wa Kidato Cha Sita Mkoani Simiyu, Aprili 25, 2019  katika kambi ya Kitaaluma Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
PICHA G
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Mwl. Kuyunga Jackson akizungumza kwa niaba ya walimu wakati wa ziara ya Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde katika kambi ya Kitaaluma kwa Wanafunzi wa KIDATO Cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, Aprili 25, 2019.
PICHA I
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa(NECTA), Dkt. Charles Msonde(katikati walioketi) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa wa Idara ya Elimu Mkoa wa Simiyu, walimu na wanafunzi wa Kidato Cha Sita mkoani Simiyu, Mara baada ya kuhitimisha ziara yake katika kambi ya Kitaaluma ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita inayoendelea katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa.
 …………………..


Na Stella Kalinga, Simiyu

Katibu MTENDAJI wa Baraza la Taifa la Mitihani nchini (NECTA) amewataka wanafunzi wa kidato cha sita nchini wanaotarajia kufanya mtihani wao wa mwisho mapema mwezi Mei, 2019 kuepuka aina yoyote ya udanganyifu kwenye mtihani huo.

Dkt. Msonde ameyasema hayo wakati akiongea na wanafunzi wa kidato cha sita mkoani Simiyu waliopo kwenye kambi ya kitaaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa, ambayo inayohusisha wanafunzi 1166 kutoka shule 12 zikiwemo 10 za umma na mbili za binafsi zenye kidato cha sita.

“Niwatake msifanye asilani habari yoyote ya udanganyifu kwenye mtihani wenu, mkifanya hayo tu kwanza yatawafanya mshindwe lakini pili tutakaponusa tu harufu yoyote ya udanganyifu tutawafutia matokeo”alisema Dkt. Msonde.

Wakati huo huo Dot. msonde amewataka wanafunzi hao kuondokana na dhana kwamba mtihani wa Taifa ni mgumu hali inayopelekea kuwa na homa ya mtihani(hofu), badala yake wajiamini na wajiandae vema kwa kuzingatia waliyofundishwa na walimu wao.

Pamoja na hayo amewapongeza viongozi wa mkoa wa Simiyu kwa ubunifu wao wa kuanzisha kambi za kitaaluma hatua inayopelekea mkoa huo kupiga hatua ya katika ufaulu wa mitihani ya kidato cha sita na kidato cha nne.

Awali akimkaribisha Katibu Mtendaji wa NECTA, Afisa Elimu mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema kuwa awali mkoa ulikuwa na ufaulu mbaya lakini kupitia kambi ufaulu umepanda kuanzia matokeo ya kidato cha sita kutoka nafasi ya 26 mwaka 2017 hadi nafasi ya 10 mwaka 2018 na kidato cha nne kutoka nafasi ya 12 mwaka 2017 hadi nafasi ya 9 mwaka 2018.

Akiongea kwa niaba ya walimu mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana Maswa Mwl. Kuyunga Jackson amesema kuwa vijana wa kidato cha sita Simiyu wamepikwa vizuri kitaaluma hivyo matarajio yao ni kuingia tatu bora kitaifa.

Katika hatua nyingine wanafunzi waliopo kambini hapo wamesema kuwa ujio wa katibu mtendaji NECTA umekuwa chachu ya ufaulu wao na kuahidi kuyafanyia kazi yale yote aliyoyaeleza ikiwemo kuepuka udanganyifu pamoja na kuondoa homa ya mtihani.

“Tunakushukuru Sana kwa ujio wako umetujenga na kutuondolea hofu ya mtihani, tutafanyia kazi uliyotueleza, tunakuhakikishia hatutajihusisha na udanganyifu wowote kwa sababu walimu wametuandaa vizuri na tunajua udanganyifu unaweza kusababisha tusifikie ndoto zetu; tutazingatia yote tuliyofundishwa na walimu wetu” alisema Julieth John.

Taasisi ya APHFTA yashiriki Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani 2019

$
0
0
Kila mwaka Aprili 25 huwa ni maadhimisho ya siku ya Malaria duniani ambapo kwa mwaka huu 2019, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya imekuja na mkakati wa “Zero Malaria” unaolenga kutokomeza Malaria hadi kufikia mwaka 2030. Kitaifa maadhimisho ya siku ya Malaria 2019 yamefanyika mkoani Lindi yakiwa na kaulimbiu isemayo “ZeroMalaria inaanza na mimi” huku mikoa mingine nayo ikipata fursa ya kuandaa maadhimisho yake.

Katika Mkoa wa Geita, Chama cha Watoa Huduma Binafsi za Afya Tanzania (APHFTA) kwa kushirikiana na Serikali pamoja na wadau wengine wa afya, kimeandaa maadhimisho haya kimkoa katika shule ya msingi Mkapa iliyopo Mji Mdogo Katoro ambapo huduma mbalimbali ikiwemo upimaji wa Malari bure kutolewa kwa wananchi.

Chama cha APHFTA kimekuwa ikitekeleza mradi wa kupambana na Malaria mkoani Geita kuanzia mwezi Januari mwaka 2017 unaotarajiwa kufikia tamati mwezi Disemba mwaka huu ambapo mradi huo na mikakati mingine, umesaidia kupunguza kiwango cha maambukizi kutoka asilimia 38.1 mwaka 2015/16 hadi asilimia 17.3 mwaka 2017/18.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Kaimu Mganga Mkuu Mkoa Geita, Frank Moshi akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Geita kwenye Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani 2019 mkoani humo yaliyofanyika kwenye viunga vya Shule ya Msingi Mkapa iliyopo katika Mji Mdogo wa Katoro.
Mgeni rasmi, Kaimu Mganga Mkuu Mkoa Geita, Frank Moshi akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Geita kwenye Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani 2019 mkoani humo.
Mratibu wa Udhibiti Malaria Mkoa Geita, Dkt. Moses Simon akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Tanzania inazidi kupiga hatua kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ambao vimelea vyake huenezwa na mbu jike aina ya “Anopheles” ikielezwa kwamba maambukizi yameshuka kwa  asilimia 50. Malaria ni hatari kwa sababu mtu mmoja hupoteza maisha duniani kila baada ya dakika moja kutokana na ugonjwa huo.

Mgeni rasmi, Kaimu Mganga Mkuu Mkoa Geita, Frank Moshi (katikati) akiwa ameshika bango la "Ziro Malaria, Inaanza na Mimi" ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa mkakati wa Serikali kutokomeza Malaria ifikapo mwaka 2030.
Wakati chanjo mpya ya Malaria inayotambulishwa na Shirika la Duniani (WHO) ikitarajiwa kufanyiwa majaribio katika nchi za Kenya, Malawi na Ghana, Serikali ya Tanzania imetenga shilingi Bilioni 12.5 ili kutekeleza program mbalimbali za kupambana na Malaria hususani katika wilaya 10 nchi zenye kiwango kikubwa cha maambukizi.

Wilaya zenye kiwango kikubwa cha maambukizi ya Malaria Tanzania ni Kakonko yenye asilia 30.8, Kasulu asilimia 27.6, Kibondo asilimia 25.8, Uvinza asilimia 25.4, Kigoma asilimia 25.1, Buhigwe asilimia 24, Geita asilimia 22.4, Nanyamba asilimia 19.5, Muleba asilimia 19.4 na Mtwara asilimia 19.1.

Juhudi za kupambana na Malaria ni pamoja na kutokomeza mazalia ya mbu, kugawa bure na kuhamasisha matumizi ya vyandarua vyenye dawa, kunyunyizia dawa za kuua mbu majumbani, kutoa elimu kwa wananchi ili kuweka mazingira yao safi, kuwahi hospitalini wanapohisi viashiria vya Malaria ikiwemo joto kali na kutapika.

Sehemu ya wananchi waliohudhuria Maadhimisho ya Siku ya Malaria Duniani 2019 kwa Mkoa Geita yaliyofanyika katika Mji Mdogo wa Katoro.
Mgeni rasmi, Kaimu Mganga Mkuu Mkoa Geita, Frank Moshi akikagua zoezi la upimaji Malaria kwenye maadhimisho hayo.
Tanzania inazidi kupiga hatua kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa wa Malaria ambao vimelea vyake huenezwa na mbu jike aina ya “Anopheles” ikielezwa kwamba maambukizi yameshuka kwa  asilimia 50. Malaria ni hatari kwa sababu mtu mmoja hupoteza maisha duniani kila baada ya dakika moja kutokana na ugonjwa huo.

Mwaka 2015 Tanzania ilikuwa na asilimia 14.4 ya maambukizi ya Malaria ambapo juhudi za serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali zimesaidia kiwango hicho kitaifa kupungua hadi asilimia 7.3 mwaka huu. Hata hivyo juhudi zaidi zinahitajika kwani kwa mujibu wa ripoti ya mwaka jana kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), Tanzania ina asilimia 80 ya vifo vitokanavyo na Malaria.

Idadi kubwa ya wananchi ilijitokeza kupima Malaria bure.
Mmoja wa wakati wa Katoro mkoani Geita (katikati) akiwa kwenye bango la "Ziro Malaria, Inaanza na Mimi" ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono mkakati huo wa kutokomeza Malaria Tanzania ifikapo mwaka 2030. Kushoto ni Mratibu wa Udhibiti Malaria Mkoa Geita, Dkt. Moses Simon na kulia ni Bigeso Makenge ambaye ni Mratibu wa Mradi wa kupambana na Malaria mkoani Geita unaotekelezwa na APHFTA kuanzia Januari 2017 hadi Disemba 2019.
Mwaka 2015 Tanzania ilikuwa na asilimia 14.4 ya maambukizi ya Malaria ambapo juhudi za serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali zimesaidia kiwango hicho kitaifa kupungua hadi asilimia 7.3 mwaka huu. Hata hivyo juhudi zaidi zinahitajika kwani kwa mujibu wa ripoti ya mwaka jana kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), Tanzania ina asilimia 80 ya vifo vitokanavyo na Malaria.

Aidha matokeo ya utafiti wa viashiria vya Malaria Tanzania mwaka 2017 yanaonyesha Mkoa wa Kigoma unaoongoza kwa kiwango kikubwa cha ugonjwa huo ukiwa na asilimia 24 ukifuatiwa na Geita asilimia 17, Kagera na Mtwara asilimia 15, Tabora, Ruvuma na Lindi asilimia 12 hii ikiwa ni mikoa yenye kiwango cha juu cha maambukizi.

Taasisi ya APHFTA iligawa vipeperushi vyenye elimu kuhusu Malaria kwenye maadhimisho.
 Mikoa inayofuatia ni Mara yenye asilimia 11, Morogoro asilimia 10, Mwanza asilimia nane, Katavi asilimia saba, Simiyu na Shinyanga asilimia sita, Pwani asilimia tano, Mbeya asilimia nne, Tanga asilimia tatu, Singida, Rukwa na Iringia asilimia mbili, Dar es salaam, Dodoma na Mjini Magharibi Zanzibar asilimia moja.

Tazama BMG Online TV hapa chini

Halmashauri Zakusanya Bil 449 Mapato Ya Ndani

$
0
0
Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI 

IKIWA imepita robo tatu ya mwaka wa fedha 2018/2019, halmashauri zote zimekusanya Sh bilioni 449.8 ambayo ni asilimia 61 kati ya Sh bilioni 735.6 kutoka kwenye vyanzo vya ndani huku Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mkoa wa Dar es Salaam zikiongoza kwa mapato ghafi. 

Hayo yabamebainishwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa alipokuwa akitoa taarifa za makusanya kwa halmashauri kuanzia Juni mwaka jana hadi Machi mwaka huu na kusisitiza kuwa vyanzo vya mapato vinavyokuswanywa na serikali kuu havijumuishi katika makusanyo hayo. 

Akifafanua zaidi Jafo alisema halmashauri tano zilizoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani kuwa ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi(asilimia 113), Geita (asilimia 109), Wanging’ombe(asilimia 105), Kilolo (asilimia 103) na Sumbawanga (asilimia 92) huku zile zilizofanya vibaya kuwa ni Newala na Tandahimba (asilimia 15), Momba na Masasi (asilimia 13) na Nanyamba (asilimia 12) 

Kwa kigezo cha pato ghafi, Jafo alisema halmashauri zinazongoza kwa wingi wa mapato kuwa ni Halmashauri ya Jiji la Dodoma 9 (Sh bilioni 49.9), Ilala (Sh bilioni 44.8), Kinondoni(Sh bilioni 23.5) Temeke Sh bilioni 20.6) na Jiji la Arusha (Sh bilioni 12.5) wakati halmashauri tano zilizofanya vibaya katika kundi hili ni Madaba(Sh milioni 293.7), Newala (Sh milioni 268.3) Kakonko (Sh milioni 238.6) Buhigwe (Sh milioni 177.3) na Momba(Sh milioni 170.4). 

Aidha, katika kundi la mikoa kwa kigezo cha asilimia, Jafo alisema mikoa inayoongoza kwa kigezo cha asilimia ya mapato ya ndani ni Mkoa wa Iringa (asilimia 77), Geita (asilimia 73), Dar es salaam (asilimia 72), Dodoma na Songwe (asilimia 68) wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Shinyanga (asilimia 46), Katavi (asilimia 43), Kigoma na Lindi (asilimia 42) na Mtwara (asilimia 26). 

Kwa upande wa mikoa kwa kigezo cha pato ghafi, Jafo alitaja mikoa inayoongoza kuwa ni Dar es Salaam (Sh bilioni118.4) Dodoma (Sh bilioni 57.30), Mwanza (Sh bilioni 22.9) Arusha (Sh bilioni 22.8) na Mbeya (Sh bilioni 19.8) wakati mikoa iliyofanya vibaya katika kundi hili ni Manyara (Sh bilioni 6.5) Lindi (Sh bilioni 6.1), Rukwa (Sh bilioni 5.8) Kigoma (Sh bilioni 4.5) na Katavi Sh bilioni 3.8). 

Aidha, Jafo alisema Jiji la Dar es Salaam linaongoza katika kundi la halmashauri za majiji kwa asilimia kwa kukusanya asilimia 87 ya makisio huku jiji la Tanga likiwa la mwisho katikakundi hilo baada ya kukusanya asilimia 57 ya makisio. 

Alisema Halmashauri ya Dodoma inaongeza kwa kigezo cha patoghafi ambapo imekusanya Sh bilioni 50 na halmashauri ya jiji la Tanga imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya Sh bilioni 8.7. 

Aidha, Jafo alisema halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga imeongoza kundi la halmashauri za Manispaa kwa kukusanya asilimia 92 ya makisio huku Lindi ikishika nafasi ya mwisho kwa kukusanya asilimi 23 ya makisio. 

Jafo alisema kwa upande wa halmashauri ya Manispaa ya Ilala imeoongoza katika kundi la halmashauri za Manispaa kwa kigezo cha mapato ghafi baada ya kukusanyw Sh bilioni 50 huku Tanga ikiwa ya mwisho kwa kukusanya Sh bilioni 8.7. 

Aidha, JAfo alisema halmashauri ya Mji wa Kondoa imeongoeza kundi la halmashauri za miji kwa kigezo cha asilimia ambapo wamekusanya kwa asilimia 92 ya makisio huku halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho baada ya kukusanya asilimi 12 ya makisio. 

“ Katika kigezo ya pato ghafi kwa halmashauri za mji, Geita inaongeza baada ya kukusanya Sh bilioni 5.9 na halmashauri ya mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho ikiwa imekusanya Shilingi milioni 293.9. 

Kwa upande wa halmashauri za wilaya, Jafo alisema Mbozi inaongoza kwa kukusanya kwa asilimia 113 ya kamkisio nay a mwisho ni Masasi iliyokusanya asilimia 13 ya makisio wakati kwa upadne wa pato ghafi, Chalinze inaoongoza kwa kukusanya Sh bilioni 4.6 na ya mwisho katika kundi hili ni Momba iliyokusanya Sh milioni 170.4. 

Aidha, Jafo aliwataka wakurugenzi ambao makusanyao yao hayajafika asilimia 50 kuaza kujitathimini huku asikisisitiza kuwapo taarifa za baadhi ya watumishi kuhujumu ukusanyaji wa mapato. 

“ Mkurugenzi usikubali kurudishwa nyuma na watendaji wasio waamini, maana kuna baadhi ya maeneo watu wamekuwa wahatumii mifumo ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kieletroniki na wengine hawatumii kabisa,” 

Aidha, Jafo ameendelea kusisitiza wakurugenzi kuhakikisha fedha za mapato ya ndani asilimia 40 au 60 kuelekezwe kwenye miradi ya maendeleo eneo husika sambamba na utoaji wa asilimia 10 za fedha za ndani kwa walemavu, vijana na wanawake na kusisitiza kuwa mwisho wa mwaka mambo hayao yatakuwa ni tathimini ya utendaji wa wakurugenzi hao. 



CCM MANISPAA YA IRINGA NA NAIBU MEYA WAMVAA TENA MBUNGE PETER MSINGWA SWALA BARABARA

$
0
0
Naibu meya wa halmashauri ya manispaa ya Iringa Joseph Lyata kupitia chama cha mapinduzi akikagua utekelezaji wa ahadi waliyoitoa kwa wananchi wa kata ya Mkimbizi mtaa wa Ugele manispaa ya Iringa
Naibu meya wa halmashauri ya manispaa ya Iringa Joseph Lyata akiwa sambamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Manispaa ya Iringa Edwin Bashir pamoja na mwenyekiti wa vijana kata ya Mkimbizi wakikagua utekelezaji wa ahadi yao
Naibu meya wa halmashauri ya manispaa ya Iringa Joseph Lyata akiwa sambamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Manispaa ya Iringa Edwin Bashir pamoja na diwani wa kata ya Mwangata Nguvu Chengula wakifurahi jambo na wananchi wa mtaa wa Ugele mara baada ya kutekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara
Naibu meya wa halmashauri ya manispaa ya Iringa Joseph Lyata akiwa sambamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Manispaa ya Iringa Edwin Bashir pamoja na diwani wa kata ya Mwangata Nguvu Chengula wakifurahi jambo na wananchi wa mtaa wa Ugele mara baada ya kutekeleza ahadi ya ujenzi wa barabara


NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

NAIBU meya wa manispaa ya Iringa amewataka wananchi wa manispaa ya Iringa kumkataa mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa kwa kushindwa kutekeleza wajibu wa kuleta maendeleo kwa wananchi waliompa kura.

Akizungumza na wananchi wa kata ya Mkimbizi mtaa wa Ugele,Naibu meya Joseph Lyata alisema kuwa mfuko wa mbunge unapesa nyingi za kusaidia kuleta maendeleo kwa wananchi lakini hali imekuwa tofauti kwa mbunge huyo kushindwa kutatua changamoto za wananchi.

“Mbunge anauwezo wa kuwatembelea wananchi wa Ugele na kuja kutatua changamoto mlizonazo kwa kuwa anapesa za mfuko wa mbunge ambao anauwezo wa kutoa pesa kwa ajili ya kukarabati barabara hii ambayo imekuwa kikwazo kikubwa katika kuleta maendeleo ya eneo hili” alisema Lyata

Lyata alisema kuwa wananchi wa mtaa wa Ugele wanakabiliwa na tatizo la kukosa huduma bora za afya kwa kuwa mbunge wa jimbo hilo hayupo tayari kuwasaidia kutatua changamoto hizo.

“Mlifanya kosa kubwa sana kumchagua mbunge huyo kwa kuwa hajawai kuja kuwasikiliza kero zeo na kuzitatua ndio maana maumivu hayo mnayapa hii leo kwa kuwa hakuna maendeleo ambayo mmefanyiwa na mbunge huyo” alisema Lyata

Lyata amewataka wananchi wa mtaa wa Ugele kutomchagua tena mbunge huyo kuwa kuwa hana faida ya kimaendeleo kwa wananchi kwa kuwa ameshindwa kuleta maendeleo kwa kushindwa kuboresha sekta ya afya,elimu na miundombinu.

“Mmemchagua kiongozi ambaye hawasikilizi na anashindwa kutatua kero za wananchi ndio maana hadi hii leo mnateseka kwa kushindwa kutatuliwa kero zenu huyo sio kiongozi na hafai tena kuwa kiongozi” alisema Lyata

Aidha Lyata alisema kuwa chama cha mapinduzi manispaa ya Iringa kimeamua kutatua kero zenu kwa kuwa hamna kiongozi ambaye anaweza kuwatatulia kero kwa kuwa mbunge mliyemchagua ameshindwa kutatua kero hizo.Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Manispaa ya Iringa Edwin Bashir aliwataka wananchi wa mtaa huo kuendelea kuwa na imani na chama cha mapinduzi kwa kuwa kinafanya kazi ya kuleta maendeleo kwa vitendo.

“Tulikuja hapa kukiwa hakuna barabara lakini tulifanya mkutano wa hadhara na kuwasikiliza kero zetu hatimaye mkatupa kero ya barabara na zahanati hivyo sasa tumeanza kutengeza barabara kwa kiwango bora kinachosaidia kuleta maendeleo kwa wananchi” alisema Bashir

Bashir alisema kwa sasa hakuna chama kinachoweza kutekeleza ahadi zake kwa umakini kama chama cha mapinduzi hivyo wananchi mnatakiwa kuendelea kuwa na imani na chama hicho.“Jamani mnatakiwa kuendelea kukienzi na kukitunza chama hiki bora ambacho ndio chama bora kwa kuleta maendeleo ya kweli kwa wananchi wake na sio vyama vingine” alisema Bashir

Kwa upande wake diwani wa kata ya Mwangata Nguvu Chengula alisema kuwa chama cha mapinduzi na naibu meya wa manispaa ya Iringa walikuwa hawalali kwa ajili ya kutatua tatizo la barabara ya Ugele kwa kuwa wananchi hao wanahitaji kufanya kazi za kimaendeleo

“Wananchi wa kata ya Ugele wanahitaji kufanya maendeleo kwa kuwa wamekuwa wachapa kazi wakubwa lakini mbunge wao amekuwa hawasaidie kwa lolote hivyo ndio chama na Naibu Meya walipobebe jukumu la kutatua changamoto hiyo” alisema Chegula

Chegula alisema kuwa kipaumbele kilikuwa kutatua changamoto ya barabara ndipo wanatafuta njia nyingine ya kutatua changamoto nyingine zilizopo katika mtaa wa Ugele ili wananchi wafanye kazi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anavyotaka.

Nao wananchi wa Mtaa wa Ugele Manyigi Uliopo Kata ya Mkimbizi Manispaa ya Iringa wameishukuru serikali Chini ya Naibu Meya Manispaa ya Iringa kwa kuwakarabatia barabara ambayo ilikuwa awali ilikuwa kero kwao.

“Baadhi ya wananchi wa Mtaa huo wamesema kuwa awali kabla ya ukarabati wa barabara hiyo, wajawazito walikuwa wanapata shida pindi wanapoelekea mjini kupata huduma za afya” walisema wananchi

Mwenyekiti wa Mtaa wa Ugele Manyigi Aloyce Laurent amemshukuru Naibu Meya Joseph Lyata kwa kupeleka Greda katika Mataa wake na kurekebisha barabara ambayo ilikuwa kero kwa wananchi wake.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images