Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

MFUKO WA BIMA YA TAIFA ULIVYOSHIRIKI KUTOA HUDUMA KWA WANA MICHEZO KUMBUKUMBU YA SOKOINE

$
0
0
Wanamichezo wakipewa huduma ya vipimo katika banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha. 
Wanamichezo wakipewa huduma ya vipimo katika banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha. 
Mmoja wa wanamichezo akipimwa urefu na huduma nyingine za huduma ya afya katika banda la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha. 
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ukitoa huduma za vipimo vya afya wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha. 
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ukitoa huduma za vipimo vya afya wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha.
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ukitoa huduma za vipimo vya afya wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha. 

Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF),mkoa wa Arusha,Isaya Shekifu akifurahia baada ya kumalizia mbio za kilometa tano wakati mashindano ya kumbukumbu ya Sokoine jijini Arusha.

Mwenge wa Uhuru Kung’arisha miradi ya Shilingi Bilioni 45.4 Rukwa.

$
0
0
Mwenge wa Uhuru wa Mwaka 2019 utakaokimbizwa katika wilaya tatu na Halmashauri Nne za Mkoa wa Rukwa unategemewa kuweka Mawe ya Msingi, kukagua na kuzindua miradi 35 ya maendeleo pamoja na vikundi 11 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambapo miradi hiyo ina thamani ya Shilingi Bilioni 45,404,104,489.59.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo baada ya kukabidhiwa mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia. Jenerali. Mstaafu Nicodemus Mwangela mara tu baada ya kuvuka daraja la mto Momba mbao ndio mpaka wa Mkoa wa Rukwa na Songwe katika Kijiji cha Kilyamatundu, Wilayani Sumbawanga.

Mkuu wa Mkoa amesema kuwa Mwenge wa uhuru ukiwa katika Mkoa wa Rukwa utakimbizwa umbali wa jumla ya Kilomita 832.5 kuanzia tarehe 7 hadi 11, April, 2019 nahatimae kuwakabisdi majirani Mkoa wa Katavi, ambao utakuwa mkoa wa tatu tangu kuwashwa kwake katika mkoa wa Songwe mapema mwezi huu.

Wakati akifafanua michanganuo ya uchangiaji wa miradi hiyo Mh. Wangangabo alisema “Wananchi Shilingi 244,524,500.00 sawa na asilimia 0.5 ya gharama zote.Halmashauri Shilingi 619,611,106.00 sawa na asilimia 1.4, Serikali Kuu Shilingi 16,426,480,402.00 sawa na asilimia 36.2, Wadau wa maendeleo Shilingi 759,489,800 sawa na asilimia 1.7 Aidha, kuna mradi wa uchimbaji makaa ya mawe ambao unathamani ya Shilingi 27,353,998,681.59 mradi huu utakaguliwa, ambao una wastani wa asilimia 60.2 ya gharama zote.”

Kwa upande wake Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2019 aliupongeza uongozi wa mkoa wa Rukwa kwa mapokezi mazuri aliyoyapata na kuwaahidi kutowaangusha wananchi katika ukaguzi wake wa miradi ambayo Mwenge wa Uhuru utaipitia.

Kauli mbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru 2019 ni “Maji ni haki ya kila Mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa”
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia) akikiri kuupokea Mwenge wa Uhuru wa mwaka 2019 baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brigedia. Jenerali. Mstaafu Nicodemus Mwangela (kushoto).

Masauni lauds efforts by Meadows Academy

$
0
0

The Deputy Minister for Home affairs Hon Hamaad Masauni addressing participants at Uhuru Walk 5

Speaking at the just-ended Uhuru Walk 5, the Deputy Minister of Home Affairs Hon Hamaad Masauni, lauded the efforts pitched in by Upanga-based Meadows Academy in using the Uhuru Walk event to raise the spirit of community service while engaging in capacity building activities at Tumaini la Maisha (Muhimbili) as well as the House of Blue Hope.

"What particularly strikes me as a unique concept about Uhuru Walk is that it is an effort by a small kindergarten to mobilise community support and invest in human resource at the very beginning of life.  We see several efforts around us in which organisations build structures and buildings, which are of course very necessary, but what we usually forget is that the most important building blocks of growth in any nation, are the people.  And this is something, that you as all know, our Hon President H E Dr John Pombe Magufuli, regularly reminds us that we must not forget those around us who are less privileged, that we must remain fair to the idea of collective development."

He ended his speech as follows: I would like to end by quoting what the Almighty says in the Holy Qur’an "Hal jaza-ul Ihsan Illal Ihsan" Is there any reward for Good other than Good ? - Surah Ar-Rahmaan

Hon Masauni, flanked by Upanga West Ward Councillor Hon Adnan Kondo and Fire Rd Chairperson Bi Jokha, then proceeded to lead 800 odd walkers in the 6.3km walk, which brought several schools including Azania Secondary School
Tambaza Secondary School
Zanaki Secondary School
Aga Khan Mzizima Secondary School
Dar es Salaam International Academy
Academic International Secondary School

 Owners of Meadows Academy Mohamedarif Suleman and Mohamed Suleman pose for a group photograph with the leadership of Upanga West Bi Jokha Lamki - mwenyekiti Fire Rd and Hon Adnan Kondo, Diwani Upanga West
A section of the 800 participants at the start of the event
 Kinders of the Meadows Academy helping the chief guest in cutting the ribbon as Mohamedarif Suleman, Event Team Leader (left) and Hon Adnan Kondo (Right) look on
 Hon Hamaad masauni, Deputy Minister of Home Affairs (extreme left) walking the 6.3km route flanked by Hon Adnan Kitwana Kondo, Diwani Upanga West and Mwenyekiti Fire Rd, Bi Jokha Lamki

BENKI YA NMB YAZINDUA KLABU YA WAFANYABIASHARA PEMBA,SERIKALI YAUNGA MKONO JUHUDI ZA KUWAUNGANISHA WAFANYABIASHARA KISIWANI HUMO

$
0
0
MWENYEKITI wa Klabu ya Wafanyabiashara wa NMB Kisiwani Pemba Abdalla Ali Said, akimkabidhi cheti cha shukurani mmoja wa wafanyabiashara na mteja wa benk ya NMB Pemba, Mwanakhamis Khamis, wakati wa hafla ya uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara hafla iliyofanyika mjini Chake Chake.
MWENYEKITI wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB Kisiwani Pemba Abdalla Ali Said, akimkabidhi cheti meneja wa NMB Tawi la Pemba Ahmed Nassor, kwa niaba ya mfanyabiashara Abdalla Nassor Abdalla, wakati wa hafla ya uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara hafla iliyofanyika mjini Chake Chake.
MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Rashid Hadid Rashid (kushoto), akisalimiana na mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB Kisiwani Pemba, Abdalla Ali Said (Ngonda) baada ya kuchaguliwa kwake na wafanyabiashara wakati wa uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)
MWENYEKITI Mteuliwa wa klabu ya wafanyabiashara ya NMB Kisiwani Pemba Abdalla Ali Said (Ngonda), akizungumza na wafanyabiashara katika mkutano wa uzinduzi wa klabu hiyo, mkutano uliofanyika mjini Chake Chake.
MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Rashid Hadid Rashid, akizungumza na wafanyabiashara wa Pemba, wakati wa uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB Pemba, uzinduzi huo uliofanyika mjini chake chake.
MENEJA wa NMB kanda ya Dar es Salam na Zanzibar, Badru Iddi akizungumzia malengo ya Benk ya NMB kanda yake kwa mwaka 2019, wakati wa uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB Pemba, hafla ya uzinduzi huo uliofanyika mjini Chake Chake.
MWAKILISHI kutoka NMB Loelia Kibasa, akiwasilisha mada kuhusu NMB na Idara ya biashara, wakati wa ufunguzi wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB kisiwani Pemba, halfa iliyofanyika mjini Chake Chake.
MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Rashid Hadid Rashid (kushoto), akisalimiana na mwenyekiti wa klabu ya wafanyabiashara wa NMB Kisiwani Pemba, Abdalla Ali Said (Ngonda) baada ya kuchaguliwa kwake na wafanyabiashara wakati wa uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara Pemba.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MKUU wa Wilaya ya Chake Chake Rashid Hadid Rashid, amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inaunga mkono juhudi mbali mbali zinazochukuliwa na benki ya NMB, katika kuwaunganisha wafanyabiashara wa Kisiwa cha Pemba, jambo linaloweza kupelekea kuongezeka kwa mapato ya nchi. 

Alisema wafanyabiashara ni watu muhimu katika maendeleo ya uchumi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla, katika suala zima la kukusanya mapato. 

Alisema malengo ya Serikali ya awamu ya saba ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kuhakikisha, inaboresha mapato ya serikali kupitia kodi na kuziba mianya yote ya ukwepaji wa kodi, ambayo husababisha upotevu wa mapato ya serikali hali inayopelekea kuzoretesha maendeleo ya nchi. 

Mkuu huyo wa Wilaya ya aliyaeleza hayo, mjini chake chake wakati wa uzinduzi wa klabu ya wafanyabiashara wa Pemba, ikiwa ni klabu ya kwanza kisiwani hapa kuanzishwa na NMB. 

“Muunganiko huu pia utaweza kutoa mafunzo kwa wafanyabiashara, katika suala la kodi na jinsi ya kutunza fedha, jambo hili ni muhimu litaweza kusaidia malengo ya wafanyabiashra, ili kuweza kujengewea uwelewa katika suala zima la ulipaji wa kodi”alisema. 

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya alisema, kuanzishwa kwa klabu hiyo itaweza kutoa mwangaza kwa wafanyabiashara, kupata mafunzo mbali mbali ya biashra, pamoja na kuelimishwa juu ya utunzaji wa kumbukumbu za biashara, masoko, huduma nzuri kwa wateja, upangaji wa bei, sheria za biashara na mahesabu ya fedha. 

Aidha aliwataka wafanyabiashara kufanya utafiti kwa kina wa biashara wanayotaka kuifanya, kabla ya kuomba mkopo ili fedha wanazopatiwa waweze kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa, pamoja na benki kufuatilia wafanyabiashara waliowapatia mikopo na kujuwa biashara zao ipasavyo.

Meneja wa NMB kanda ya Dar es Salam Badru Iddi, alisema NMB imeamua kuwafikia wananchi wote wa kipato cha chini Tanzania nzima, kwani mwaka 2018 walifungua klabu za wafanyabiashara 50 Tanzania na mwaka 2019 mikakati yao ni kufungua klabu 36 Tanzania ikiwemo ya Kisiwani Pemba.

WAZIRI LUKUVI ATOA NENO KWA MABENKI MAONESHO YA NMB NYUMBA DAY JIJINI ARUSHA

$
0
0
WAZIRI wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi ,William Lukuvi,amezitaka Taasisi za Kifedha hapa nchini ikiwemo Benki kuwawezesha wananchi wa hali ya chini kupata mikopo ya nyumba kwa riba nafuu.

Aidha amezitaka taasisi hizo za kifedha kushirikiana na kampuni za ujenzi ili kuwasaidia wananchi wanaochukua mikopo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba,kumiliki nyumba kwa gharama nafuu.

Waziri Lukuvi aliyasema hayo jijini Arusha katika maonyesho ya NMB Nyumba Day,yaliyofanyika jijini hapa na kukutanisha wateja na watoa huduma katika ujenzi na uuzaji wa nyumba ambapo Benki ya NMB inatoa huduma ya mikopo kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kumiliki nyumba.

Amesema kuwa taasisi za fedha zinazotoa mikopo ya nyumba zinatakiwa kutafuta namna ya kuwasaidia wananchi ili kuweza kumudu na kupata nyumba kwa gharama nafuu.

"Ili gharama za ujenzi wa nyumba za Tanzania zisiwe za ghali taasisi za kifedha kuweni na mpango mahsusi,endelevu na ulio rahisi wa kumkopesha mtu nyumba,ili wananchi wa hali ya chini kupata mikopo kwa riba nafuu na mshirikiane na kampuni za ujenzi ili kuwasaidia wananchi wanaochukua mikopo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba,kumiliki nyumba kwa gharama nafuu," alisema

Waziri Lukuvi aliipongeza Benki ya NMB kwa kuanzisha mikopo hiyo ambapo ni miongoni mwa Benki zilizopo hapa nchini ambazo zinashirikiana na wadau wengine kuhakikisha wananchi wanapata mikopo kwa riba nafuu na kuwawezesha kumiliki nyumba za makazi.

Awali Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo na wa Kati kutoka Benki ya NMB,Salie Mlay,anasema benki hiyo imekuwa baina ya wananchi na serikali katika kuwawezesha wananchi ili wapate makazi bora.

Waziri wa Ardhi,Nyumba Maendeleo na Makazi William Lukuvi,akizungumza na wananchi jijini Arusha leo,katika hafla ya maonyesho ya nne ya NMB Nyumba Day,yaliyofanyika katika eneo la Baracuda,jijini Arusha,maonyesho yaliyolenga kuwakutanisha wateja na watoa huduma za ujenzi na uuzaji wa nyumba ambapo benki ya NMB inatoa huduma ya mikopo kwa ajili ya kuwawezesha wateja wake kumiliki nyumba

WAZIRI wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi ,William Lukuvi,maonesho ya NMB Nyumba Day,yaliyofanyika jijini Arusha akimsikiliza mmoja wa Wadau wa Maonesho hayo wakati wa maonesho hayi yaliyowakutanisha wateja na watoa huduma katika ujenzi na uuzaji wa nyumba ambapo Benki ya NMB inatoa huduma ya mikopo kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kumiliki nyumba.Pichani kulia ni Kaimu Mkuu wa Wateja Wadogo na wa Kati kutoka Benki ya NMB,Salie Mlay

UHAMASISHAJI WA UTAFITI UTAWEZESHA UHIFADHI NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

$
0
0
Na Ismail Ngayonga,MAELEZO

TATHMINI za uwekezaji katika kutunza mazingira katika nchi ni moja ya kazi muhimu za Ofisi ya tathmini ya Baraza la Kituo cha Kimazingira Duniani (GEF) linalotoa taarifa na matokeo ya jumla ya miradi na utendaji katika ngazi ya kitaifa.

Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA) ambao ni mwongozo muhimu katika kuleta maendeleo endelevu, unatambua kuwa mazingira bora ni msingi wa maendeleo endelevu na kupunguza umaskini.

Mkakati huu umeainisha malengo 15 yanayohusu mazingira na utekelezaji wa MKUKUTA unahusisha wadau mbalimbali, ambapo Ofisi ya Makamu wa Rais (OMR) inalo jukumu la kuratibu ujumuishaji wa masuala ya mazingira katika mipango na bajeti za kisekta za kupunguza umaskini.

Katika kutekeleza jukumu hili, OMR imefanikisha na inaendelea kutekeleza mipango na programu kadhaa ikiwemo ile ya utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Mazingira, Sheria ya Mazingira na Kanuni zake.

Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 imeeleza wazi wajibu na majukumu ya wadau mbalimbali kuanzia serikali za mitaa hadi taifa ikisisitiza mipango na usimamizi wa matumizi endelevu ya mazingira: kudhibiti uchafuzi wa mazingira; utunzaji wa taarifa na takwimu za mazingira; utafiti na ushiriki wa jamii na utekelezaji wa majukumu yatokanayo na mikataba ya kimataifa.

Akiwasilisha Makadirio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2018/19, Waziri wa Nchi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Januari Makamba anasema Serikali kupitia Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limeendelea kutekeleza Ajenda ya Taifa ya Utafiti katika Mazingira (NERA 2017-2022).

Waziri Makamba anasema katika mwaka wa fedha 2017/18, NEMC kwa kushirikiana na wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kamisheni ya Matumizi ya Ardhi, Taasisi ya Huduma za Misitu na Halmashauri ya Wilaya ya Same imefanya tathmini ya hali ya mazingira kwenye maporomoko ya ardhi katika milima ya Mamba Miamba iliyopo Wilayani Same.

Anaongeza kuwa katika tathmini ya utafiti huo ilibaini chanzo cha maporomoko hayo ni aina ya udongo wa mfinyanzi uliopo katika eneo hilo pamoja na shughuli za kibinadamu zinazofanyika huko ikiwa ni pamoja na ukataji holela wa miti na uchomaji moto hovyo katika maeneo hayo.

Aidha anasema NEMC limepeleka mapendekezo ya kuzuia uharibifu wa mazingira katika eneo hili kwa wadau ili hatua thabiti za uhifadhi zichukuliwe, ikiwa ni pamoja na kuangalia uwezekano wa kulitangaza eneo hilo kuwa ni eneo tete la mazingira na kulitengenezea mpango wa kudhibiti uharibifu wa mazingira.

“Katika mwaka 2017/18, Baraza limefanya utafiti wa uharibifu wa mazingira wa Bwawa la Mindu lililopo katika Manispaa ya Morogoro na mmonyonyoko wa ardhi katika fukwe za Ziwa Viktoria. Matokeo ya tafiti hizo yalibainisha vyanzo mbalimbali vya uharibifu na kupendekeza hatua za kuchukuliwa” anasema Waziri Makamba.

Kwa mujibu wa Waziri Makamba anasema NEMC imefanya utafiti wa namna ya kuboresha mazingira ya mji wa Dodoma ili uwe ‘mji wa kijani’ kwa kutumia dhana za green city, eco-buildings nasustainable construction.

Akifafanua zaidi anasema katika mwaka 2017/18, Baraza limeendelea kuratibu shughuli za Hifadhi Hai kwa kuwasilisha taarifa za awali katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kwa ajili ya kuingiza Hifadhi ya Gombe Ugalla -Masito kwenye mtandao wa Hifadhi Hai za Dunia.

Waziri Makamba anasema NEMC pia imeandaa Mpango wa Usimamizi wa Mazingira (Environmental Management Plan-EMP) kwa maeneo mawili ambayo ni Dakio la Bonde la Kihansi na eneo la Ziwa Chala–Jipe. Aidha, Baraza limekamilisha zoezi la uwekaji mipaka katika eneo la Kihansi ambalo linatarajiwa kutangazwa kuwa eneo lindwa la kimazingira.

Anasema katika mwaka 2018/19, Baraza litaendelea kukusanya takwimu na na kuandaa taarifa za hali ya mazingira ya milima nchini, taarifa ya mazingira ya pwani (State of the Coastal Environment Report – SOCR, 2018); utafiti wa mifumo ya ikolojia ya hali ya mabonde ya mito mikubwa, maeneo ya malisho ya mifugo na wanyamapori.

Tanzania ni nchi yenye uwezo mkubwa wa kuweza kutoa manufaa kimazingira duniani, kwa kuzingatia changamoto za kimazingira za kitaifa na kimataifa zinazoikumba nchi ni wajibu wa wadau wa kitaifa na kimataifa kuwekeza rasilimali ili kukuza, kuchangia na kuthibiti maliasili ili kuboresha na kuongeza mchango wa Tanzania katika mazingira Duniani.

Airtel, DTBi yatoa mafunzo kwa wajasiriamali wanawake

$
0
0
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) imemaliza kutoa mafunzo ya Tehama kwa wanawake wajasiriamali yenye lengo la kuwapa ujuzi wa kutumia kompyuta ili kurahisha kufanya biashara zao kwa njia ya mtandao.

Mafunzo hayo yalikuwa yakifanyika kwenye maabara ya Tehama iliyopo katika shule ya msingi kijitonyama Manispaa ya Kinondoni na yamefikia tamati mwishoni mwa wiki chini ya udhamini wa Airtel kwa kushirikiana na DTBi

Akiongea jijini Dar es Salaam mara baada ya kukamilika kwa mafunzo hayo, Meneja maabara ya Airtel Fursa na ambaye pia alikuwa ni mratibu wa mafunzo hayo Michael Thomas alisema kuwa teknolojia inaweza kuwafanya wajasiriamali kupata na kutumia ujuzi wa mtandao na kupata taarifa au habari ambazo zina umuhimu na tija kubwa kwao. ‘Ni furaha sana kuona wajasiriamali wetu na hasa wanawake wamejitokeza kwa wingi kuja kupata mafunzo ya Tehama ambayo yatawasaidia kuendesha biashara zao kwa njia ya kisasa ya mtandao’, alisema Thomas.

‘Mafunzo haya ya Tehama yamewapa ujuzi wajasiriamali jinsi ya kutumia vitabu vya biashara kwa ajili ya kuhifadhi rekodi zao. Vile vile, yamewapa ujuzi wa kutumia kompyuta na hasa kwenye kufanya mahesabu ya mauzo na manunuzi, alisema Thomas huku akiongeza kuwa hii itakuwa ni fursa ya kipekee ya kukuza biashara zao kwa kutumia njia ya mtandao.

”Natoa rai kwa kwa wale wajasiriamali wanaonza au waliopo kwenye biashara kupata mafunzo ya Tehama kwani itasaidia kuwapunguzia kazi zao na vile vile kukuza biashara kwa njia bora ya kisasa ya mtandao, alisema Thomas.

Thomas alisema kuwa wajasiriamali wanawake wako na hamasa kubwa ya kujifunzi kozi mbali mbali zinazotolewa hapa. Tulikuwa na wajasiriamali wanawake 26 hapa na wote wameonyesha nia ya kweli ya kupata mafunzo, aliongeza Thomas.

Thomas aliongeza kuwa mpaka kufikia mwisho wa mafunzo hayo wajasiriamali hao wameweza kujifunza maana na historia ya kompyuta, kutumia applikesheni na programu tofauti za kompyuta, kutumia teknolojia kutangaza biashara na hasa kwenye face book na instragrams, kutumia kompyuta kuweka rekodi ya biashara zao, kutumia kompyuta kufanya hesabu ili kujua faida na hasara na pia kuweza kuzijua baadhi ya mambo ndani ya kompyuta.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema Airtel pamoja na DTBi zimeweza kuvuta wanafunzi wengi kujifunza Tehama tangu kuzinduliwa kwa maabara hiyo. Tumeweza kutoa mafunzo mengi kwa vikundi mbali mbali ikiwemo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, waalimu na kwa sasa wanawake wajasiriamali. Naomba nitoe rai kwa yeyote ambaye anataka kujifunza Tehama kujitokeza kwani tuna waalimu wanzuri na waliobobea, alisema Singano.

Wakati huo huo, DTBi imetangaza mafunzo ya Tehama kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wakati wa likizo inayokuja na kuwaomba Wazazi na walezi kuwasajili kwa kupitia www.teknohama.or.tz or www.airtelfursa.com au kwa kutembelea maabara ya Airtel Fursa ambayo ipo kwenye shule ya msingi ya Kijitonyama.
 Meneja wa maabara ya Airtel Fursa, Michael Thomas akitoa maelekeo ya mafunzo ya kutumia kompyuta kwa moja ya wajasiriamali wanawake Joyce Mmasi kwenye mafunzo ya Tehama kwa wajasiriamali wanawake yenye lengo la kuwapa ujuzi wa kutumia kompyuta ili kurahisha kufanya biashara zao kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yaliendesha na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Meneja wa maabara ya Airtel Fursa, Michael Thomas akitoa maelekeo ya mafunzo ya kutumia kompyuta kwa moja ya wajasiriamali wanawake Elizabeth Joshua kwenye mafunzo ya Tehama kwa wajasiriamali wanawake yenye lengo la kuwapa ujuzi wa kutumia kompyuta ili kurahisha kufanya biashara zao kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yaliendesha na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Mkurugenzi wa Fedha kutoka Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) Makange Mramba (kushoto) akimkabidhi cheti moja ya wajasiriamali wanawake Martha Aloyce baada ya kuhitimu mafunzo ya Tehama kwa wajasiriamali wanawake yenye lengo la kuwapa ujuzi wa kutumia kompyuta ili kurahisha kufanya biashara zao kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yaliendesha na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Mkurugenzi wa Fedha kutoka Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) Makange Mramba (kushoto) akimkabidhi cheti moja ya wajasiriamali wanawake Devotha Michael baada ya kuhitimu mafunzo ya Tehama kwa wajasiriamali wanawake yenye lengo la kuwapa ujuzi wa kutumia kompyuta ili kurahisha kufanya biashara zao kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yaliendesha na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
 Mkurugenzi wa Fedha kutoka Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) Makange Mramba (kushoto) akimkabidhi cheti Ali Mohammed baada ya kuhitimu mafunzo ya Tehama kwa wajasiriamali yenye lengo la kuwapa ujuzi wa kutumia kompyuta ili kurahisha kufanya biashara zao kwa njia ya mtandao. Mafunzo hayo yaliendesha na kampuni ya simu za mkononi ya Airtel kwa kushirikiana na Atamizi ya Teknohama ya Dar es Salaam (DTBi) jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Meneja Matukio Airtel Tanzania Dangio Kaniki.


WANARIADHA MASHUHURI KUSHIRIKI NGORONGORO MARATHONI APRIL 20

$
0
0
Na woinde shizza globu ya jamii Arusha

Wanariadha nyota wa Tanzania  Alfonce Simbu na Josephy Panga ni miongoni mwa wakimbiaji mashuhuri ambao watashiriki katika mashindano ya Ngorongoro marathon  yanayotarajiwa kufanyika April 20 mwaka huu.
 
Wakimbiaji wengine nyota waliothibitisha kushiriki mashindano ni pamoja na Failuna Matanga,Anjelina Tsere ,Magdalena Shauri ,Fabian Joseph ,Faraja Damas pamoja na Natalia Elsante.

Akizungumza na Globbu ya Jamii leo muandaaji wa mbio hizo Meta Petro alisema kuwa mbio hizi ambazo zinafanyika kwa miaka 12 mfululizo zitashirikisha wakimbiaji zaidi ya 1000 kutoka ndani na nje ya nchi  wakiwemo wakimbiaji mashuhuri kutoka nchini Kenya.

Alisema mbio hizo zitakuwa za kilometa 21 ,kilometa tano pamoja na kilometa mbili na nusu kwa ajili ya watoto ambapo alitaja zawadi kuwa mshindi wa kwanza  wa kilometa 21 atapata milioni moja ,mshindi wa pili atapata laki tano ,na mshindi wa tatu atapewa laki tatu.

Alitaja malengo ya mbio hizo ni kupiga vita ujangili pamoja na kuhamasisha utalii wa ndani.

"Unajua wananchi wengi na maanisha wa Tanzania wengi wamekuwa na tabia ya kutotembelea hifadhi zetu za taifa hivyo mbio hizi zitasaidia kuhamasisha wa Tanzania kuwa na tabia ya kutembelea hifadhi zetu" alisema Meta
  
Alisema  kuwa kwa washindi wa mita zote ambao watashika kuanzia Namba tano hadi kumi wao watapata fursa ya kutembelea mbuga ya wanyama  ya Ngorongoro  kwa ajili ya kujionea vivutio vilivyopo katika hifadhi hiyo.

Alitoa wito kwa wa Tanzania kujitokeza kushiriki mbio hizo .
Picha muandaaji wa Ngorongoro marathon akiongea na mwandishi wa habari hizi hii leo

WANAHISA WASHAURIWA KUENDANA NA SERA YA SERIKALI.

$
0
0
Benki ya CRDB mkoa wa Morogoro imeamua kushirikiana na serikali katika kuhamasisha wananchi kuchangamkia fursa mbali mbali  kujitokeza  kwenye uwekezaji wa viwanda ili kuendana na matakwa ya sera ya nchi katika mpango uliopo wa miaka mitano .

Akizungumza mara baada ya semina ya wanahisa wa bank ya CRDB mkoa wa Morogoro iliyolenga kuwa elimisha wanahisa na wananchi wengine fursa mbalimbali za kiuchumi na mambo yanayohusu Benki hiyo .
 
Mkurugenzi wa wateja wakubwa Bank ya CRDB Goodluck Nkim amesema wametoa nafasi kwa wanahisa kuelewa Zaidi uwekezaji wa viwanda na kuwaeleza kitu gani wanaweza kufanya ili kufaidika na myororo wa uchumi hii ikiwa ni njia Mojawapo ya CRDB kuonesha mchango wake katika ujenzi wa viwanda huku Mkurugenzi wa benki ya CRDB mkoa wa Morogoro Lusingi Sitta amewataka wananchi kujisajili katika ununuzi wa hisa kwenye bank hiyo kwani umilikiwa hisa unafaida mbali mbali ikiwemo kukuza kipato cha mtu binafsi na makampuni.

Aidha washiriki wamepongeza utoaji wa mafunzo hayo yaliyoweza kuongeza uwelewa wa wanahisa na kuiomba bank iweze kujitanua Zaidi katika kukopesha wanahisa walioko katika vyama mbalimbali vya wakulima ,kuelimisha Zaidi maana ya viwanda na kutengeneza jambo endelevu kwa ajili ya wastafu ambao sasa hivi ni wanahisa wa bank ya CRDB baadala ya kufikilia kuwakopesha .
 Wanahisa wa benki ya CRDB mkoa wa Morogoro wakisajiliwa na wafanyakazi wa bank hiyo  ili kupokea makablasha ya mkutano kabla ya kuanza mafunzo yaliyolenga kuwa elimisha namna ya  kuchangamukia fursa mbali mbali zinazo wezakujitokeza kwenye uwekezaji wa viwanda.
 Mkurugenzi wa benki ya CRDB mkoa wa Morogoro Lusing Sitta akiteta jambo na Meneja wa CRDB tawi la Mandela mkoa wa Morogoro Stephen Mapunda wakati wa mkutano baina ya benki na wanahisa wa benki hiyo.
 Wafanayakazi wa CRDB wakiwasikiliza  kwa makini wanahisa waliohitaji kujisajili na kupewa kablasha zao zinazoonesha vipengele vya mafunzo ya wanahisa na vyeti vya kuthibibisha kuwa ni wanahisa.
 Mkurugenzi wa mikopo kwa wateja wakubwa Goodluck Nkim akiwaelezea wanahisa faida za  kununua hisa katika benki ya CRDB na namna ambavyo wametoa nafasi kwa wanahisa kuelewa Zaidi uwekezaji wa viwanda  na kuwaeleza kitu gani wanaweza kufanya ili kufaidika na myororo wa uchumi.
 Wanahisa wakijisomea  kilichoandikwa  kwenye makablasha waliopewa mara baada ya kujisajili kushiriki mafunzo ya wanahisa na Benki ya CRDB mkoa wa Morogoro .
 Wafanyakazi wa benki ya CRDB mkoa wa Morogoro wakifatilia kwa makini  mada zinazotolewa na wawezeshaji katika mafunzo ya wanahisa mkoani Morogoro.
 Meneje wa bank ya CRDB tawi la Mzumbe mkoani Morogoro Jane Maganga akiteta jambo na Meneja wa mikopo CRDB Denis Kayanda  nje ya mkutano .

RAIS DKT. MAGUFULI AKAGUA MASHAMBA YA MAHINDI YA GEREZA LA KILIMO NA MIFUGO LA KITAI MBINGA MKOANI RUVUMA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Mashamba ya mahindi ya Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitai lililopo Mbinga mkoani Ruvuma huku akitoa maelekezo kwa viongozi hao wa Jeshi la Magereza nchini.
 Sehemu ya Mashamba hayo ya Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitai lililopo Mbinga mkoani Ruvuma ambayo yamelimwa ekari 650 za mahindi katika mwaka huu.
  Baadhi ya Maafisa mbalimbali wa Jeshi la Magereza wakisikiliza hotuba ya . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyokuwa akiitoa katika eneo hilo la Kitai Mbinga mkoani Ruvuma.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Maafisa mbalimbali wa Jeshi la Magereza katika eneo la Gereza la Kitai mara baada ya kukagua mashamba ya mahindi ya Gereza hilo lililopo Mbinga mkoani Ruvuma.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza huku akiwa na mwanafunzi wa darasa la saba Cristian Josephat Komba ambaye alizungumza kuhusu uchakavu wa vyoo katika  Shule ya Msingi ya Kitai. Rais Dkt. Magufuli alichangia kiasi cha Shilingi milioni tano kwa ajili ya ujenzi wa vyoo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza huku akiwa na mwanafunzi wa darasa la saba Cristian Josephat Komba ambaye alizungumza kuhusu uchakavu wa vyoo katika  Shule ya Msingi ya Kitai. Wapili kutoka kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Onesmo Luwena 
 . Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wanafunzi wa katika  Shule ya Msingi ya Kitai mara baada ya kuwachangia kiasi cha Shilingi milioni tano
. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike mara baada ya kuwahutubia. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Phaustine Kasike mara baada ya kuwasili katika eneo la Mashamba ya Mahindi ya Gereza la Kilimo na Mifugo la Kitai lililopo Mbinga mkoani Ruvuma.

PICHA NA IKULU

KATIBU MKUU WA CCM DKT.BASHIRU AUNGURUMA ZANZIBAR

$
0
0
NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR.

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM),Dk.Bashiru Ali Kakurwa amewataka vijana nchini kuwa mstari wa mbele kulinda kwa vitendo urithi wa fikra za kimaendeleo zilizoasisiwa na Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Alisema kundi hilo la vijana linatakiwa kujengewa mazingira rafiki ya kuelezwa na kurithishwa maadili,historia na itikadi yakinifu zinazotokana na harakati za miongozo ya ASP na TANU ili kupata viongozi bora na makini wa sasa kama akina hayati Karume,Nyerere na Aboud Jumbe.

Wito huo ameutoa katika Mahojiano Maalum na Kituo cha Radio ya Bahari FM kilichopo Migombani Zanzibar, wakati akizungumzia siku ya Mashujaa ya kumbukizi ya miaka 47 toka kuuawa kwa Rais wa Kwanza wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Karume.

Alisema bila Waasisi wa Mapinduzi ya Januari 12,mwaka 1964 wakiongozwa na Hayati Karume pasingekuwepo na Muungano pamoja na uhuru wa Waafrika wa Zanzibar.

Alieleza kuwa ukweli ni kwamba Mapinduzi hayo ndio chimbuko la uhuru wa kimwili na kifikra,utu,haki za binadamu,ustawi wa kijamii na kimaendeleo pamoja na ukuaji wa Demokrasia.

Alisema miaka 47 ni umri ni mingi lakini ni muhimu kukumbushana kuwa bila jasho na damu za wanamapinduzi bado Zanzibar mpaka leo ingendelea kuwa chini ya Utawala wa Kisultani.

" Lazima tukumbushane japo kwa muda mdogo kwani miaka 47 ni mingi kwa umri lakini kwa nchi ambayo ni tegemezi na ipo katika nchi zinazoendelea ni michache sana kwani Watu waliopinduliwa bado wapo na wanatamani kurudi tena, jambo ambalo haliwezekani.",alisema Dkt.Bashiru.

Pamoja na hayo alisisitiza mambo matatu ya msingi yanayotakiwa kuzingatiwa na Vijana pamoja na makada wa CCM kuwa kwanza kutambua historia halisi ya Taifa lao, pili kusimamia misingi ya waasisi wa Taifa lao na tatu kuwa wabunifu ili waendeleze mapambano katika Mazingira Mapya ya zama za sasa za Sayansi na Teknolojia.

Dkt.Bashiru aliweka wazi kuwa ukombozi haupatikani bila ya mapambano baina ya pande mbili, hivyo CCM katika suala la Mapinduzi na Muungano ni lazima iwe imara katika kulinda upande wa kulinda historia isipotoshwe na waliopinduliwa.

Alisema CCM ambayo imeshinda kwa awamu ya kwanza ya ukombozi wa kisiasa ni lazima Jeshi lake ambalo ni Wanachama, Viongozi na Watendaji wasibweteke bali waendelee kuongeza nguvu za kumiliki umma na kuhakikisha upinzani unakosa sifa za kubaki katika ushindani wa kisiasa.

"Tusipojiimarisha vizuri hata haya Mapinduzi tunayoyazungumzia leo yatatuponyoka kwani mifano ipo mingi Nchi kama Somalia, na Sudan yaliwahi kuwa Mataifa huru yakawa shwari lakini leo hii katika mataifa hayo kunawaka moto.",alifafanua Katibu Mkuu huyo.

Aliongeza kuwa uwepo wa Muungano ni kwa sababu unalindwa hivyo ni muhimu kuambizana ukweli kuwa waliopinduliwa bado wapo na hawautaki muungano na wanaendelea kujenga hoja dhaifu ili muungano huo uvunjike.

Akizungumzia dhana ya Umoja uliossisitizwa na Waasisi wa Mapinduzi Dkt.Bashiru alieleza kuwa dhana hiyo ya umoja inatakiwa kurutubishwa hasa katika kusimamia misingi ya ukweli,haki,usawa na utu.

Katika maelezo yake Dkt.Bashiru alifafanua kuwa pindi wananchi wanapoanza kudharau yale yaliyopatikana kwa jasho na damu basi panavunjwa msingi mkuu wa maendeleo.

Alisema watu wanatakiwa kupewa haki mbali mbali kama haki ya kufikri, haki ya elimu, haki ya Afya pamoja na haki ya elimu pamoja na haki ya kujitawala kama Taifa mambo ambayo toka enzi ya Katiba za ASP na TANU mpaka hivi sasa zimeanishwa vizuri katika Katiba ya CCM ya mwaka 1977 iliyoeleza namna ya haki kuzilinda na kuzisimamia haki hizo.

Alisema CCM na Serikali zake inapambana vikali na vitendo vya rushwa ambayo ndio chimbuko la kuwakosesha haki mbali mbali wananchi.

Dkt.Bashiru akizungumzia mfumo wa Vyama vingi kuwa upo Kikatiba na Kisheria na kueleza kuwa miongoni mwa faida za mfumo huo ni vyama hivyo kuchangia uwepo wa amani na utulivu.

Alisema Chama Cha Mapinduzi hakikukurupuka kukubali mfumo huo bali kiliamini kuwa vyama hivyo vitakuwa na imani ya kisiasa,kushindanisha imani hizo na mikakati ili kupata Taifa bora na imara kwa nyanja zote hatua ambayo bado haijafikiwa.

Pamoja na hayo alipongeza kasi ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa upande wa Zanzibar kwa kueleza kuwa ameridhishwa na kazi hiyo ambayo ndio sehemu muhimu ya Chama Cha Mapinduzi kujijenga kisiasa kwa kuvuna wanachama wengi.

Aidha alitoa wito kwa Wanachama wa CCM kwa Zanzibar na Tanzania bara kuwa wahakikishe CCM inashinda kwa kura nyingi katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2019 pamoja na uchaguzi Mkuu wa Dola wa mwaka 2020,ili kuendelea kulinda Tunu za Taifa za Muungano na Mapinduzi ya Zanzibar.

Katika mahojiano yake hayo aliahidi kuwa CCM itaimarisha Vyombo vyake vyoye vya Habari vilivyopo Zanzibar na Tanzania bara ili Watendaji wake wafanye kazi katika mazingira rafiki na kupata maslahi yanayoendana na hadhi ya Taasisi wanayoifanyia kazi.

Pamoja na hayo alizipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na CCM kwa ujumla kwa kuandaa utaratibu mzuri wa kuwaenzi na kuwaombea Dua ya Kitaifaa Waasisi mbali mbali walioshiriki katika harakati za Ukombozi wa Zanzibar wakiongozwa na Hayati Karume.

Mapema Katibu Mkuu huyo aliwatembelea Viongozi wastaafu mbali mbali wa CCM na Serikali zake akiwemo Naibu Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Waziri wa Zamani wa Mambo ya Ndani wa Serikali ya awamu ya Tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ali Ameir Mohamed, Rais mstaafu wa awamu ya Sita Dkt. Amani Abeid Karume na Mke wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume.
 KATIBU Mkuu wa CCM Dkt.Bashiru Ally Kakurwa akizungumza katika Kipindi Maalum kinachozungumzia Kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa Zanzibar huko katika Kituo cha Radio ya Bahari FM Migombani Zanzibar.
RAIS mstaafu wa Zanzibar wa awamu ya Sita Dkt.Amani Abeid Karume(kushoto), Katibu Mkuu wa CCM Dkt.Bashiru Ally Kakurwa(katikati) na Naibu Katibu Mkuu wa CCM zanzibar Dk.Abdulla Juma mabodi(kulia).
  KATIBU Mkuu wa CCM Dkt.Bashiru Ally Kakurwa(kushoto),Mke wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Mama Fatma Karume(katikati),Naibu Katibu Mkuu wa CCM zanzibar Dk.Abdulla Juma mabodi(kulia)wakiwa na Mama Fatma Karume nyumbani kwake Maisara.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM zanzibar Dk.Abdulla Juma mabodi(kushoto) akibadilishana mawazo na Katibu Mkuu wa CCM Dkt.Bashiru Ally Kakurwa(kulia) wakiwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hayati Abeid Karume Zanzibar mara baada ya Katibu Mkuu kuhitimisha ziara yake fupi iliyoambatana na shughuli ya Hitma ya Siku ya Mashujaa.(PICHA NA IS-HAKA OMAR-AFISI KUU CCM Z'BAR).

MAGAZETI YA LEO JUMANNE,APRIL 2019

MWENYEKITI WA TUME ASIKITISHWA NA UKOSEFU WA UANDILIFU KWA WATUMISHI WA TUME YA MADINI

$
0
0

Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula akiongea na wafanyakazi wa Tume ya Madini kwenye ukumbi wa mikutano katika ofisi za Tume hiyo mkoani Morogoro. Kulia kwake ni Kamishna wa Tume hiyo Dkt. Athanas Macheyeki. Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula akitolea ufafanuzi masuala mbalimbali yaliyo wasilishwa na Kaimu Afisa Madini Mkazi Morogoro wakati wa kikao chake na wafanyakazi wa Tume ya Madini alipotembelea kwa ziara ya kikazi. Kulia kwake ni Kamishna wa Tume hiyo Dkt. Athanas Macheyeki na kushoto ni Mhandisi Emmanuel Shija Kaimu Afisa Madini Mkazi Morogoro.


Athanas Macheyeki Kamishna wa Tume ya Madini mwenye vitabu mkononi akimsikiliza jambo Mwenyekiti wa Tume Prof. Kikula wakati wakikagua maeneo mbalimbali yanayo zunguka ofisi za Tume ya Madini Mkoa wa Morogoro
…………….

Na Issa Mtuwa- Morogoro

Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula amekerwa na kukasirishwa na ukosefu wa uadilifu kwa wafanyakazi wa Tume ya Madini katika baadhi ya Ofisi na kueleza kuwa, suala hilo halitavumilika kwa wanaokwenda kinyume na maadili ya kazi.

Akizungumza na wafanyakazi wa Tume ya Madini Mkoa wa Morogoro katika siku ya kwanza ya ziara yake aliyoianza Aprili 8, 2019, Prof. Kikula amewaeleza wafanyakazi wa ofisi hiyo kuwa, yeye na viongozi wenzake wa tume wamekerwa na kusononeshwa na vitendo vya ukosefu wa uadilifu vinavyofanywa na baadhi ya wafanyakazi wa Tume ya Madini.

Ametolea mfano wa kitendo kilichofanywa na wanafanyakazi wa Tume hiyo wilayani Chunya ambapo watumishi wote wa kituo hicho wamesimamishwa kazi na Waziri wa Madini Doto Biteko kutokana na kukosa uadilifu na kutoa taarifa isiyo sahihi kwenye takwimu za madini.

“Kuna udanganyifu mkubwa unaofanywa na wachenjuaji madini, na udanganyifu huo unachochewa na watumishi wa Tume. Angalia mfano pale Chunya, wale wachenjuaji wamedanganya lakini ukifuatilia utagundua wafanyakazi wa tume wanahusika na huo udanganyifu, na ndio maana hata Waziri wa Madini aliamua kuchukua hatua ya kuwasimamisha kazi wafanyakazi wote wa kituo kile,” amesema Prof. Kikula.

Kufuatia hali hiyo, Prof. amekemea vitendo hivyo na kueleza kuwa, suala la uadilifu ni muhimu katika kazi za watumishi wa tume na kueleza kuwa, pamoja na kuwepo vishawishi vingi katika sekta ya madini, lakini wanapaswa kukumbuka kuwa kazi ni muhimu kwao na familia zao.

“Mimi na wenzangu tunaumizwa moyoni tunapoona wafanyakazi wa Tume wanakutwa na hatia ya ukosefu wa uadilifu inatusikitisha sana, sana”, amesisitiza Prof. Kikula.

Akitolea ufafanuzi kuhusu masuala mbalimbali yaliyowasilishwa na Kaimu Afisa Madini Mkazi, Prof. Kikula amewapongeza watumishi wote wa kituo cha madini Morogoro kwa kazi nzuri ya kusimamia ukusanyaji wa maduhuli na kuwaomba kuongeza bidii ili wafikie malengo waliyojiwekea.

Kuhusu masuala ya leseni, Prof. Kikula amemuagiza Kaimu Afisa Madini Mkazi kufuatilia leseni zote zilizopo na kubainisha leseni ambazo sio hai na kuzifuta kwa mujibu wa sheria. Aidha, amekumbusha kuhusu kufuata utaratibu halali uliowekwa kwa mujibu wa sheria katika hatua za ufutaji wa leseni hizo na kusema “asimuogope mtu lakini pia asimuonee mtu katika hatua hiyo ya ufutaji wa lesini zisizo hai”.

Aidha, Prof. Kikula amekiri kuwepo kwa changamoto na kuwataka watumishi hao kuwa na subira na kuongeza kuwa, Tume imepanga kununua magari 34 ambayo yatasambazwa katika mikoa yote ili kuongeza tija. Prof. Kikula amezungumza hayo baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya ofisi hiyo ambayo ilieleza kuwepo kwa changamoto kadhaa.

Kwa upande wake, Kaimu Afisa Madini Mkazi Morogoro Mhandisi Emmanuel Shija akisoma taarifa ya ofisi hiyo, pamoja na mambo mengine, amemweleza Mwenyekiti wa Tume masuala kadhaa yanayosimamiwa na ofisi hiyo ikiwemo uanzishwaji wa soko la Madini, ufutaji wa lesseni za uchimbaji kwa wamiliki wanaoshindwa kutimiza vigezo vya leseni zao, ukusanyaji wa maduhuli na changa moto zinazo wakabili katika kutekeleza majukumu yao.

Mhandisi Shija amesema, pamoja na changamoto zilipo, ofisi hiyo inafanya jitihada za kusimamia ukusanyaji wa maduhuli ambapo mpaka sasa imefikia asilimia 53 ya lengo na kwamba, inategemea kufikia malengo ya ukusanyaji waliyojiwekea.

Naye, Kamishna wa Tume ya Madini Dkt. Athanas Macheyeki ambaye amembatana na Mwenyekiti wa Tume, amewapongeza kwa ukusanyaji mzuri wa maduhuli na kuwataka kujiwekea muda wa utekelezaji wa malengo ili waweze kujipima vizuri.

“Unapojiwekea muda wa utekelezaji unakufanya uongeze bidii pindi unapoona uko nyuma ya muda ya utekelezaji wa lengo hivyo ni muhimu wa kulizingatia hilo,”amesema Dkt. Macheyeki.

Prof. Kikula na Dkt. Macheyeki wako mkoani Morogoro kwa ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa shuguli za Tume katika Wilaya mbalimbali zinazofanya shuguli za madini sambamba na kutatua kero za wachimbaji na wadau wa madini, mkoani humo.

MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA

$
0
0

Mkurugenzi wa Sensa ya Takwimu za Kijamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa taarifa ya hali ya mfumuko wa bei wa kipindi cha Mwezi Machi mwaka huu.
…………………….
 
Na.Alex Sonna,Dodoma 

Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS) imesema kuwa mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia Machi mwaka huu umeongezeka kidogo hadi asilimia 3.1 kutoka 3.0 sawa na ongezeko la asilimia 0.1.

Hayo yamesemwa leo jijini hapa na Mkurugenzi wa Sensa ya Takwimu za Kijamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Ephraim Kwesigabo, wakati akitoa taarifa ya hali ya mfumuko wa bei wa kipindi hicho.

Bw.Kwesigabo ameeleza kuwa kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioshia Machi mwaka huu kumechangiwa hasa na kuongezeka kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula zikilinganishwa na bei za mwaka ulioishia Machi mwaka jana.

“Hiyo inamaanisha kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia Machi mwaka huu imeongezeka kidogo ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioishia Februari,” amesema Kwesigabo

Aidha amefafanua kuwa kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioshia Machi mwaka huu kumechangiwa hasa na kuongezeka kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula zikilinganishwa na bei za mwaka ulioishia Machi mwaka jana.

Kwisegabo alitaja baadhi ya bidhaa hizo kuwa ni pamoja na mavazi na viatu(4.4%), kodi ya pango(4.7%), mafuta ya taa(1.8%), dizeli(8.3%), chakula na vinywaji kwenye migahawa(4.6%) na malazi kwenye mahoteli(5.7).

Hata hivyo amefafanua kuwa mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa machi mwaka huu umepungua hadi asilimia 0.1 kutoka asilimia 0.5 kwa mwaka ulioishia Februari mwaka huu. Kuhusu hali ya mfumko wa bei kwa nchi za Afrika Mashariki alisema nchini Uganda kwa mwezi ulioishia Februari mwaka huu umebaki asilimia 3.0 kama ilivyokuwa ulioishia Februari.

Pia Kwesigabo ameongeza kuwa kwa upande wa Kenya mfumuko kwa mwaka ulioishia Machi mwaka huu umeongezeka hadi asilimia 4.35 kutoka 4.14 kwa mwaka ulioishia Februari mwaka huu.

DAWA MUHIMU ZAIDI YA 300 ZINAPATIKA KATIKA VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA.

$
0
0
Na WAMJW - NJOMBE

Serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kuvuka kiwango cha upatikanaji wa dawa muhimu kwa binadamu kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) katika ngazi ya Hospitali ya Wilaya kwa kuwa na idadi kubwa ya dawa muhimu zinazopatikana kwenye vituo vya kutolea huduma za afya.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu alipotembelea Hospitali Teule ya Rufaa ya Mkoa wa Njombe kujioinea hali ya utoaji wa huduma.

Waziri Ummy Mwalimu aliyeongozana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula pamoja na watendaji walio chini ya Wizara yake, amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano imeendelea kuboresha upatikanaji wa dawa kwa wananchi huku ikipitiliza kiwango kilichowekwa na WHO kwa kuwa na dawa muhimu 312 huku kigezo kilichowekwa na Shirika la Afya Duniani kikiwa ni dawa 30.

“Tuna mfumo wa ukusanyaji wa taarifa kuanzia ngazi ya zahanati, kituo cha afya mpaka hospitali unaotuwezesha Serikali kutambua mahitaji na matumizi ya dawa katika vituo vya kutolea huduma” amesema Waziri Ummy wakati akifafanua namna ya Serikali ilivyojipanga kupata takwimu sahihi za dawa.

Waziri Ummy amesema kuwa zipo propaganda zinazoendeshwa na watu wenye ushawishi ambao wamekuwa wakiwahadaa wananchi kwa kusema kuwa dawa hakuna ili hali dawa zipo na zinapatikana katika vituo vya kutolea huduma.

“Ni lazima tumtendee haki Rais wetu DKt. John Pombe Magufuli, amefanya makubwa kwenye Sekta ya Afya kwa kuboresha upatikanaji wa Dawa, tunaposema tumeongeza upatikanaji wa dawa maana yake dawa zinapatikana kwa urahisi hata kwenye vituo binafsi” amesema Waziri Ummy,

Waziri Ummy amezitaja dawa zenye kipaumbele kikubwa zikiwemo Dawa za kudhibiti maambukizi ya bakteria (Antibiotics), Dawa za kudhibiti Malaria, Dawa za magonjwa yasiyo ya kuambukiza, Dawa za uzazi salama pamoja na Dawa za maumivu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa Ofisi yake kupitia Waziri wa Afya wako mbioni kuwasilisha muswada wa Bima ya Afya ambao utawawezesha wananchi wote sasa kuwa na bima ya afya.

Aidha, Dkt. Chaula amewataka watumishi katika Hospitali hiyo kuwahamasisha zaidi wagonjwa kujiunga na huduma za bima ya afya ili kuwa na uhakika wa matibabu pindi wanapougua.

“Niwaombe watendaji wote hapa kuwasisiza wagonjwa wanaofika hapa kupata matibabu kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya” Alisema Dkt. Chaula.

Naye Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt. Winfred Kyambile amesema kuwa hali ya upatikanaji wa huduma imeimarika kutokana na mapato kuongezeka hivyo kuiwezesha Hospitali kutoa huduma bora kwa wananchi.

Dkt. Kyambile amesema kuwa kuongezeka kwa upatikanaji wa dawa  imesaidia kuongezeka kwa mapato hospitalini hapo, amesema kuwa hapo awali mapato ya hospitali hiyo kwa mwezi yalikuwa Shilingi Milioni 12 huku sasa mapato hufikia Shilingi milioni 90 mpaka 100, fedha ambazo amesema wanazitumia kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo.

Easter Holiday Packages from Tanga Beach Resort

UCHAGUZI MDOGO WA KATA SITA KUFANYIKA MEI 19 MWAKA HUU

$
0
0
Na. Idara ya Habari-NEC

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetangaza uchaguzi mdogo wa madiwani kwenye kata sita (6) zilizopo kwenye halmashauri sita (6) katika mikoa sita (6) ya Tanzania Bara.

Mwenyekiti wa Tume Jaji (Rufaa) Semistocles Kaijage amesema Jijini Dar es Salaam leo (Jumanne 09.04.2019) kwamba uchaguzi huo utafanyika tarehe 19 Mei mwaka huu.

Akisoma taarifa kwa umma iliyotolewa na Tume, Jaji Kaijage amesema kwamba fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kati ya tarehe 15 hadi tarehe 19, Aprili mwaka huu.

Aidha Mwenyekiti huyo wa Tume amesema kwamba uteuzi wa wagombea pia utafanyika tarehe 19, Aprili mwaka huu na kampeni za uchaguzi zitafanyika kuanzia tarehe 20, Aprili hadi tarehe 18 Mei mwaka huu.

Alifafanua kwamba uchaguzi katika kata hizo, utafanyika sambamba na Uchaguzi Mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Arumeru Mashariki

“Tume inapenda kuvikumbusha Vyama vya Siasa na wadau wote wa Uchaguzi kuzingatia Sheria, Kanuni, Maadili ya Uchaguzi, Taratibu, Miongozo na Maelekezo yanayotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi wakati wa kipindi chote cha Uchaguzi huu mdogo,” alisema Jaji Kaijage.

Awali Jaji Kaijage alisema kwamba maamuzi ya kutangaza uchaguzi kwenye kata hizo yamefanyika baada ya Tume kupokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa ambaye kwa kutumia mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 13(1) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 aliitaarifu Tume juu ya uwepo wazi wa nafasi hizo.

Alisema kwamba nafasi hizo wazi zimetokana na vifo vya Madiwani watano (5) na mmoja (1) kujiuzulu.

Kata hizo ni pamoja na Uwanja wa Ndege iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi, Kitobo iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi Mkoani Kagera, Kyela iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya, Mikocheni iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mkoani Dar es Salaam, Mvuleni iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Lindi Mkoani Lindi na Manda iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Mwenyekiti wa Tume Jaji (Rufaa) Semistocles Kaijage

BINGWA WA HIP HOP TUPAC SHAKUR ALIVYOUAWA

$
0
0
Na Moshy Kiyungi,Dar es Salaam.

Tupac Shakur alikuwa mwanamuziki maarufu wa muziki wa hip hop kutoka nchini Marekani.

Alifahamika zaidi kwa jina lake la kisanii la 2Pac.

Shakur aliuawa kwa kupigwa risasi Septemba 13,1996 wakati akiwa anaendesha gari mjini Las Vegas, Nevada nchini Marekani.

Alikuwa mmoja kati ya wasanii wa muziki wa Hip hop, waliouza rekodi nyingi za muziki duniani.2Pac alikuwa mtoto wa Afeni Shakur, ambaye alikuwa mwanachama wa Black Panther Party. Mama yake alitolewa jela mwezi mmoja kabla ya kujifungua mtoto wake Tupac.

Shakur alikuwa na vipaji vingi vilivyo vilivyomuongezea umaarufu akiwa na umri mdogo.Vipaji hivyo vya Shakur ni kwamba alikuwa rappa, mwigizaji, mtayarishaji wa rekodi, mshairi, mwanaharakati na mtunzi wa nyimbo. 

Majina yake halisi alikuwa akiitwa ‘Tupac Amaru Shakur’. Maana halisi ya jina Tupac ni Nyoka inayong’ara. Majina ya ‘TuPac Amaru Shakur’ ni makubwa yaliyoweka historia kubwa katika dunia hasa kwenye suala zima la mziki wa Hip-Hop.

Alizaliwa mnamo mwaka Juni 16, 1971 katika jiji la New York, nchini Marekani.Mara nyingi aliitwa 2Pac, Pac, Makaveli na pia mwenyewe akajiita The Don Kiluminati.Tupac, pia alishawahi kushikilia rekodi ya Guinness ya ulimwengu (Guinnes World Record), kwa kuwa na mauzo ya juu sana kwa msanii wa muziki wa rap ya hip hop.

Shakur aliwahi kupata mauzo takriban milioni 74 kwa hesabu ya dunia nzima na milioni 44 kwa mauzo ya Marekani pekee.Alishirikiana na baadhi ya vikundi na wanamuziki wakubwa nchini mwake kama Outlawz, Thug Life, Danny Boy, Digital Underground, Dr. Dre, Johnny "J",Ice Cube, Nate Dogg, The Notorious B.I.G. na Snoop Dogg.

Chanzo cha kifo chake kilielezwa kwamba mnamo Septemba 07, 1996 Tupac alikwenda katika jiji la Las Vegas, kwa ajili ya kuhudhuria pambano la ngumi kati ya bondia Mike Tyson alipokuwa akinyukana na mpinzani wake Bruce Seldon.

Kwa mujibu wa taarifa zilieleza kwamba 2pac alifikia katika hoteli moja ya kifahari jijini Las Vegas iliyokuwa inaitwa Luxor Hotel - Casino.Mpambano huo wa ngumi ulikuwa unafanyiika katika ukumbi maarufu ujulikanao kama MGM Grand Hotel.

Ilielezwa kwamba siku ya mpambano huo, Tupac alihudhuria sambamba na Goons (kampani) yake akiongozwa na Marion ‘Suge’ Knight, ambaye alikuwa mwanzilishi na mmiliki wa record label ya Death Row.Kampuni hiyo ilikuwa ikisimamia kazi za muziki za Tupac ikiwemo kurekodi nyimbo na kadhalika.

Katika mpambano huo, Tupac aliketi kiti kimoja na mlinzi wake aliyekuwa akiitwa Frank Alexander na rafiki wa Suge knight, sambamba na mcheza filamu maarufu wa Hollywood Louis Gossett Jnr.

Wengine waliokuwa karibu naye walikuwa Mchungaji Jesse Jackson, Charlie Sheen pamoja na mchezaji wa baseball aliyevuma wakati huo Reggie Jackson katika eneo la wageni maalumu (V.I.P).

Kwenye pambano hilo kiti kimoja cha V.I.P, kilitozwa kiasi cha dola za kimarekani 1,000, hiyo ilitokana na ukubwa wa pambano hilo.Hivyo watu walioweza kuketi viti vya V.I.P.walikuwa ni mashuhuri na wenye ‘mkwanja’ wa nguvu.

Wimbo alioingia nao Mike Tyson kabla ya pambano lake kuanza, uliandikwa na Tupac Shakur uliokuwa unaitwa ‘Wrote The Glory’.Katika pambano hilo Mike Tyson aliweza kuibuka kidedea baada ya kumchakaza mpinzani wake Bruce Seldon katika raundi ya pili ya pambano hilo.

Baada ya Pambano hilo kuisha, kundi ambalo lilikuwa linaongozwa na Tupac Shakur, liliingia katika mzozo katika sebure ya ukumbi wa MMG baada ya kurushiana maneno dhidi kundi lingine.Chanzo ugomvi huo hakikuweza kujulikana mara moja licha ya kwamba askari wa usalama ukumbini hapo waliweza kuingilia kati ili kuweka hali ya amani.

Ilielezwa kwamba Tupac na kundi lake waliondoka katika eneo hilo la tukio na kuelekea katika Hotel waliyofikia.Kifo hicho kiliacha maswali mengi na simanzi miongoni mwa wapenzi na mashabiki wa muziki kutoka katika kila pembe za dunia.

2Pac Shakur wakati wa uhai wake alikuwa mmoja kati ya marapa waliojizolea umaarufu mkubwa na mafanikio kupitia kazi ya muziki kwenye miaka ya 1990.

Hata hivyo alikuwa na kipaji kingine cha uigizaji.

Septemba 13, 2019, ‘TuPac Amaru Shakur’ atatimiza miaka 23 tangu kutokea kifo chake baada ya kupigwa risasi mnamo Septemba 13,1996 wakati akiwa anaendesha gari mjini Las Vegas, Nevada.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa DED Nyasa na amteua Jimson Mhagama kuwa DED Nyasa

NHIF YAWAFIKIA WANANCHI WA MAFIA NA HUDUMA ZA MKOBA ZA MADAKTARI BINGWA

$
0
0
 Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) umezindua rasmi huduma za Mkoba za Madaktari Bingwa wilayani Mafia mkoani Pwani ambazo zitaendelea kwa wiki nzima katika hospitali ya Wilaya ya Mafia.

Akizungunza leo katika uzinduzi huo, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya  Bernard Konga amesema mpango huu ni mwendelezo wa mkakati wa Mfuko huu kufikia wananchi  na huduma za madaktari bingwa katika maeneo ambayo yana uhaba wa madaktari hao.

Amesema Mfuko kwa nyakati tofauti umeshafikia mikoa 17 na huduma hizo za mkoba za madaktari bingwa ambayo ni Rukwa, Lindi, Kigoma, Pwani, Mara, Tabora, Manyara, Mtwara, Shinyanga, Simiyu, Kagera, Singida, Ruvuma, Iringa, Njombe, Geita na Katavi. Kati ya hiyo mikoa 6 imeshafikiwa na mara mbili.

"Tumeona hitaji la huduma hizi huku Mafia na kwa kushirikiana na Hospitali ya Wilaya hapa Mafia zoezi hili litaendelea kwa wiki nzima kwa kila mwananchi mwenye hitaji la huduma za madaktari hawa ambao wametoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili" alisema Konga

Akifungua huduma hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani aliyewakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mafia  Shaibu Nunduma ameipongeza NHIF kwa kuleta huduma hii Mafia.

"Asilimia kubwa ya wagonjwa wetu hawana uwezo wa kuzifuata huduma za madaktari bingwa huko walipo na kwa idadi ya wataalam waliopo hapa Mafia tusingeweza kuhudumia wananchi wa mafia ambao wako 53,083 hivyo naishukuru sana NHIF kwa kutuletea huduma hizi," amesema Shaibu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF Anne Makinda amesema
Serikali yetu imeweka mkazo mkubwa katika afya na bajeti ya dawa kwa sasa imeongezeka hadi kufikia takriban bilion 300. Amesema lengo la Serikali yetu ni kila mtu kuwa na bima ya afya na katika kutimiza azma hii, Mfuko huu unalengo la kufikia asilimia 50 ya wananchi mwakani 2020.

"Lengo letu ni kuwa na watu wenye bima ya afya wakiwa wazima maana itakuja siku ambayo ugonjwa unakujia ghafla na huna fedha. Mfuko huu unamwezesha hata mtoto wako kuwa na uhakika wa matibabu kwa mwaka kwa Sh. 50,400 wakati kwa wakulima Sh. 76,800 kwa  kwa mwaka" amesema Makinda

Wakati huo huo wananchi wa Mafia ambao walifika kwa wingi kupata huduma za Madaktari Bingwa hao kutoka Hospitali ya Muhimbili wameushukuru  Mfuko kwa huduma hizo na wameonesha kuhamasika kuitumia fursa hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa NHIF Bw. Bernard Konga akitoa maelezo ya awali wakati wa uzinduzi wa mpango huo katika Hospitali ya Wilaya vs Mafia
 Wananchi Wilayani Mafia wakifuatilia uzinduzi wa huduma za Madaktari Bingwa ambazo zimewezeshwa na Mfuko wa  Taifa wa Bima ya Afya..
Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF Mama Anne Makinda akitoa salaam za Bodi wakati wa uzinduzi wa huduma hizo.
 Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Shaibu Nundulu akifungua rasmi huduma za Madaktari Bingwa Mafia  kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images