Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

Mji wa Serikali Ukamilike Ifikapo Aprili 15-Majaliwa


AGAPE YAENDESHA WARSHA KWA WASIMAMIZI WA SHERIA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA KWENYE MASOKO

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape,John Myola.

Shirika la Agape AIDS Control Program la mkoani Shinyanga limeendesha warsha kwa Wasimamizi wa Sheria ili kutambua haki za binadamu kwa lengo la kuondoa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye masoko ya Manispaa ya Shinyanga. 

Warsha hiyo ya siku mbili imeanza leo Machi 27,2019 katika ukumbi wa Katemi Hotel Mjini Shinyanga na kukutanisha pamoja wasimamizi wa sheria wakiwemo polisi,migambo,maafisa masoko,maafisa maendeleo ya jamii,wenyeviti wa kamati za masoko na wafanyabiashara sokoni. 

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo,Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape,John Myola alisema warsha hiyo ni sehemu ya kutekelezaji wa Mradi wa “Mpe Riziki Si Matusi” unaofadhiliwa na shirika la UN WOMEN kupitia Shirika la kitaifa la Equality for Growth (EfG). 

“Agape tunatekeleza huu katika Manispaa ya Shinyanga,katika warsha hii tumekutana na wasimamizi wa sheria na wafanyabiashara kutoka masoko kwenye masoko sita tunakotekeleza mradi ambayo ni Soko Kuu Mjini Shinyanga,Kambarage,Nguzo Nane,Ibinzamata,Ngokolo Mitumbani na Majengo Mapya”,alisema Myola. 

Kwa upande wake,Meneja Miradi wa shirika la Agape, Mustapha Isabuda alisema lengo la warsha hiyo ni kuwajengea uwezo wasimamizi wa sheria ili waende wakasaidie kutokomeza ukatili wa kijinsa unaotokea kwenye masoko yaliyopo katika Manispaa ya Shinyanga. 

“Tafiti mbalimbali zimekuwa zikionesha kushamiri kwa matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na wasichana wafanyabiashara sokoni,mfano wanatolewa lugha chafu,wanadhulumiwa,wanabaguliwa katika nyadhifa za uongozi sokoni lakini pia kufanyia mashambulio ya aibu ikiwemo kushikwa shikwa bila idhini yao”,alieleza Isabuda. 

“Baada ya kutoa elimu kwa wasaidizi wa sheria pia tutatoa elimu kwa wasaidizi wa sheria sokoni ambao watakuwa na kazi ya kutoa elimu kwa wafanyabiashara,kutoa taarifa ya vitendo vya ukatili sokoni na kutoa rufaa kwa wahanga wa ukatili na usuluhishi”,aliongeza. 

Kwa upande wao wafanyabiashara sokoni walikiri kufanyiwa vitendo vya kikatili kama vile kudhulumiwa malipo,kubaguliwa katika uongozi kwenye masoko,kutukanwa na wateja,wasichana kutongozwa kwa lazima na kushikwashikwa ovyo. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape,John Myola akifungua Warsha ya siku mbili kwa Wasimamizi wa Sheria ili kutambua haki za binadamu kwa lengo la kuondoa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye masoko ya Manispaa ya Shinyanga. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde - Malunde1 blog. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape,John Myola akiwasisitiza wasimamizi wa sheria kuhakikisha vitendo vya ukatili wa kijinsia kwenye masoko unatokomezwa. 
Wasimamizi wa sheria wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Agape,John Myola. 
Meneja Miradi wa shirika la Agape, Mustapha Isabuda akielezea lengo la Mradi wa “Mpe Riziki Si Matusi” unaolenga kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na wasichana wafanyabiashara kwenye masoko. 
Meneja Miradi wa shirika la Agape, Mustapha Isabda akizungumza wakati wa warsha hiyo. 
Washiriki wa warsha hiyo wakiwa ukumbini. 
Mwanasheria Martha Masalu kutoka ofisi ya Masalu Law Attoneys akitoa mada ya 'Uelewa wa Jumla wa Kisheria kuhusu haki za wanawake na wasichana'. 
Warsha inaendelea. 
Mwanasheria Martha Masalu akiendelea kutoa elimu kuhusu sheria mbalimbali. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AKAGUA OFISI ZA WIZARA KATIKA MJI MPYA WA SERIKALI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kukagua ofisi mpya za wizara ambazo zimejengwa katika mji mpya wa Serikali jijini Dodoma Machi 27.2019 (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ofisi za wizara zilizojengwa katika mji mpya wa Serikali jijini Dodoma Machi 27.2019
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Mhandisi Valentino Chaffu,wakati alipo kagua jengo la Ofisi ya Rais (TAMISEMI) katika mji mpya wa Serikali jijini Dodoma Machi 27.2019
Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora, katika mji mpya wa Serikali jijini Dodoma Machi 27.2019 kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Dkt. Francis Michael, katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Marry Mwanjelwa.

UJENZI WA MJI WA SERIKALI WAKAMILIKA KWA 99%-MAJALIWA

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema nia ya dhati ya Rais Dkt. John Magufuli ya kujenga upya mji wa Serikali imetekelezwa baada ya mji huo kukamilika kwa asilimia 99.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Machi 27,2019) alipotembelea mji mpya wa Serikali unaojengwa katika eneo la Mtumba, Jijini Dodoma. Majengo ya wizara 20 yamekamilika.

Katika ziara yake hiyo, Waziri Mkuu ametembelea na kukagua majengo ya Wizara 13, ambapo amesema ameridhishwa na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika maeneo mengi.Hata hivyo katika maengo hayo ya wizara 13 aliyoyatembelea, Waziri Mkuu, alibaini kasoro kwenye mlango wa kuingilia katika Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira.

Kufuatia hali hiyo, Waziri Mkuu amemuagiza mkandarasi anayejenga jengo hilo auondoe na aweke mwingine kwa kuwa mbao zilizotumika zipo chini ya kiwango na haupendezi.Kadhalika, kuhusu ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ambayo bado haikamilika, Waziri Mkuu amemuongezea siku 10 mkandarasi na kumtaka akamilishe.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amewaagiza Mawaziri na Makatibu Wakuu wahakikishe kazi iliyosalia ambayo ni ya kuboresha mazingira ya nje ya ofisi hizo iwe imekamilika ifikapo Apriri 15, mwaka huu. Mji huo unatarajiwa kuzinduliwa na Rais Dkt. Magufuli.

Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama alisema ujenzi wa mji huo ulianza Desemba mwaka jana na ulitarajiwa ukamilike Februari mwaka huu lakini utakamilika Mei mwaka huu.

Waziri Jenista alisema ujenzi wa majengo ya wizara tatu ambayo hayajakamilika ikiwa ni pamoja na OR-TAMISEMI na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi na Wenye Ulemavu yatakamilika Mei mwaka huu.

MATUKIO KATIKA PICHA KIKAO CHA WABUNIFU WA MITINDO NA USHONAJI NA NAIBU WAZIRI WA MICHEZO, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO

$
0
0


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akizungumza na wabunifu wa mitindo na ushonaji (hawapo pichani), baada ya kufungua kikao kusikiliza changamoto zao, kikao hicho kilifanyika katika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam, kulia ni Rais wa TAFCA, Adrian Nyangamalle na Kaimu Mkurugenzi wa Sanaa, Bi. Leah Kahimbi.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akitoa afafanuzi wa jambo kwa wabunifu wa mitindo na ushonaji ( hawapo pichani ), baada ya kufungua kikao kusikiliza changamoto zao, kikao kilifanyika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam, kulia ni Rais wa TAFCA, Adrian Nyangamalle na Kaimu Mkurugenzi wa Sanaa, Bi. Leah Kahimbi.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akijibu swali la mmoja ya washiriki katika kikao cha Wabinifu wa mitindo na ushonaji, kilichofanyika katika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam, kulia ni Rais wa TAFCA, Adrian Nyangamalle na Kaimu Mkurugenzi wa Sanaa, Bi. Leah Kahimbi na kushoto ni katibu mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) Godfery Mngereza.
Kaimu Mkurugenzi wa Sanaa, Bi. Leah Kahimbi (aaa na Michezo, Juliana Shonza (kushoto) kuhusu changamoto zilizotolewa na Wabunifu wa Mitindo katika kikao kilichofanyika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam, kulia ni Rais wa TAFCA.
Mbunifu wa Mitindo Airinda Sawe (Afrika sana), akichangia hoja mbele ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza katika kikao cha Wabinifu wa mitindo na ushonaji kilichofanyika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam.
Mbunifu wa Mitindo na Mshonaji kutoka Chuo cha Ufundi(VETA) Athanasia Kisyeli akitoa mawazo yake kuhusu sanaa ya mitindo na ushonaji mbele ya Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza(hayupo pichani) aliyeitisha kikao cha kuwasikiliza Wabunifu wa mitindo na ushonaji, kilichofanyika katika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam.
Mwenyeketi wa Chama cha fashion Association Tanzania (FAA) ambaye pia ni Mbunifu wa mitindo, Mustafa Hassanali akieleza changamoto ambazo wanakumbana nazo katika kazi zao.
Mbunifu wa mitindo na Mshonaji kutoka Speshoz, Jeff akitoa mchango wa mawazo wa kuinua tasnia ya ubunifu na ushonaji katika kikao cha Wabunifu na Washonaji kilichofanyika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam.
Washiriki wa kikao cha Wabunifu na washonaji wakimsikiliza Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Juliana Shonza (hayupo pichani) wakati wa kikao, kilichofanyika Uwanja wa Mpira wa Taifa (National Stadium ) Jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA KONGAMANO LA AFYA NA SAYANSI KISHA AFANYA MAZUNGUMZO NA BINTI WA MFALME WA JORDAN

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema teknolojia ni zana muhimu katika kushughulikia mapungufu ya msingi katika sekta ya afya.

Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.“tunahitaji kuwekeza katika teknolojia ya afya ya kidijitali kama njia ya kuboresha na kuimarisha huduma ya afya za kikanda” alisema Makamu wa Rais.

Makamu wa Rais ametanabaisha kuwa Tanzania imeweza kutambua na kuanza kujenga mfumo wetu wa huduma za afya kupitia Wizara ya Afya na mashirika kadhaa kama vile MSD (ambayo teknolojia ya kidijitali inasaidia kufuatilia usambazaji kutoka hatua ya ununuzi hadi utoaji kwa uhakika), NHIF (usimamizi wa uanachama wa mteja, kudai na mchango) na TFDA (taarifa ya mtandaoni ya kuagiza na kuuza nje chini ya TFDA na taarifa ya mtandaoni ya madhara mabaya ya matumizi ya dawa na vipodozi) pia kuna Mfumo wa Usimamizi wa Hospitali haswa katika Hospitali zote za Serikali. Mfumo huu hutoa taarifa halisi ya muda na unaweza kufuatilia harakati za mgonjwa na za dawa.

Mkutano huo unaofanyika kila baada ya miaka miwili unawakusanyisha wadau wa sekta za afya kutoka Afrika Mashariki na Wataalamu kutoka sehemu mbalimbali duniani ambao una lengo la kuangalia namna ya kutumia utaalamu wa kisasa katika huduma ya afya kwa kutumia mfumo wa kidijitali.

Kwa upande wake Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu amesema Kongamano hili linafanyika wakati ambapo kanda hii, na Afrika nzima, inahitaji mabadiliko ya teknolojia ya haraka hasa katika teknolojia ya kidijitali ili kusaidia utekelezaji wa hatua za sekta za afya na mipango na kuongeza kasi ya kufikia Ufikiaji wa Afya wa Ulimwengu (UHC) ili kufikia kufikia Lengo la Maendeleo Endelevu (SDG) 3 kwa ujumla.

Wakati huohuo Makamu wa Rais amekutana na kufanya mazungumzo na Binti wa Mfalme wa Jordan Sarah Zeid ambapo walizungumzia masuala mbali mbali ya kuboresha lishe na afya kwa Mama na Mtoto.

Binti huyo wa Mfalme aliambata na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani Bw. Michael Dunford.

BILIONI 50 ZAWANUFAISHA WANANCHI KATIKA UJENZI WA MJI WA SERIKALI-IHUMWA- DODOMA

$
0
0
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akieleza kuhusu Sh.  bilioni 50 ambazo zimetumika na wakandarasi katika shughuli mbalimbali na kuwanufaisha wananchi waliopata ajira katika ujenzi wa Mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma. Kulia ni  Waziri  Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.
 Muonekano wa  Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma ambazo zinajengwa na  Mkandarasi, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na zimekamilika kwa asilimia 99.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akipata maelezo kuhusu uwekaji wa Transfoma ili kupata umeme wa uhakika kutoka kwa Mhandisi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Elisante Ulomi, wakati Waziri huyo alipotembelea  na kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma.

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Khatibu Kazungu, akimsikiliza kwa makini Mhandisi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Elisante Ulomi alipokua anatoa maelezo kuhusu miundombinu ya Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali Ihumwa, Jijini Dodoma.
Waziri  Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (wa tatu kushoto),  Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) pamoja na viongozi wengine wakisikiliza maelezo ya jumla ya ujenzi wa ofisi katika Mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma.(Picha na Peter Haule, Wizara ya Fedha na Mipango).
 Waziri  Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (kulia) akipeana mkono na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), alipotembelea na kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali, Ihumwa Jijini Dodoma.
 Waziri  Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kulia) akikagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma. Watatu kulia ni Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb).

 Waziri  Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa (kushoto), akipongeza kazi nzuri ya ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma ambazo zimekamilika kwa asilimia 99 na kuagiza Mkandarasi ambaye ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuhakikisha anamalizia kasoro ndogondogo zilizoonekana kabla ya Ofisi hizo kuzinduliwa rasmi.

Na Peter Haule, WFM, Dodoma
Serikali imeeleza kuwa takribani Sh. bilioni 50 zimewanufaisha wakandarasi na wananchi wa hali ya chini wakati wa  ujenzi wa ofisi za wizara mbalimbali katika Mji wa Serikali katika eneo la Ihumwa, Jijini Dodoma.
Hayo yameelezwa Jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango, wakati Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, alipotembelea na kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango katika Mji wa Serikali uliopo eneo la Ihumwa.
Dkt. Mpango alisema kuwa katika eneo la ujenzi kulikuwa na mafundi kutoka kila pembe ya nchi, wafanyabiashara wadogo wa chakula (mama lishe) na wakandarasi ambao wamenufaika na uwekezaji mkubwa wa majengo ya ofisi za Serikali katika eneo hilo la Ihumwa.
Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa jengo la Wizara ya Fedha na Mipango, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, amepongeza maendeleo ya ujenzi wa Ofisi hizo ambao umekamilika kwa asilimia 99.
Waziri Mkuu Majaliwa alimeagiza Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha inatengeneza  Bustani nzuri, kusawazisha eneo hilo na kuweka samani katika ofisi hizo ili ziweze kutumika.
Aidha, alimtaka mkandarasi ambaye ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kurekebisha kasoro alizozibaini wakati akikagua jengo hilo hususan mlango mkuu wa kuingia ofisi hizo kabla ya kuzinduliwa rasmi na Mhe. Rais hivi Karibuni.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhe. Dkt. Khatib Kazungu, alisema kuwa Wizara imepokea maelekezo ya Waziri Mkuu na kuahidi kuyatekeleza kwa haraka ili watumishi waanze kutumia ofisi hizo.
Mhandisi kutoka NHC, anayesimamia ujenzi huo Bw. Elisante Ulomi ameishukuru Wizara ya Fedha na Mipango kwa ushirikiano waliompa katika kufanikisha ujenzi huo ulioanza Desemba 29, 2018 na kuahidi kurekebisha kasoro zilizobainishwa wakati wa ukaguzi huo.

WAZIRI MHAGAMA AWAHIMIZA VIJANA KUWA WAZALENDO KWA NCHI YAO

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akikabidhi Bendera ya Taifa kwa vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro ikiwa ni kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akifurahia jambo wakati wa kuwaaga vijana kabla ya kuanza zoezi la kupanda Mlima Kilimanjaro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali, Uongozi wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro na Vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akivishwa skafu na vijana wa skauti mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Mhe. John Palingo mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, Mkoani Kilimanjaro.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na Viongozi na wakazi wa Marangu wakati wa hafla ya kuwaaga vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro ikiwa ni kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba akieleza jambo kwa vijana watakaopanda Mlima Kilimanjaro ikiwa ni kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya Kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi akufafanua jambo kuhusu ushiriki wa vijana hao watakaopanda Mlima Kilimanjaro, Machi 26, 2019.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkuu wa Hifadhi ya Kilimanjaro Betrita Loibooki (aliyesimama kulia) alipokuwa akiwasilisha taarifa fupi kuhusu Hifadhi hiyo. (Kushoto aliyekaa) ni Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba.
Baadhi ya watumishi wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama alipofanya ziara ya kuwaaga vijana hao.
Vijana wanaotarajiwa kupanda Mlima Kilimanjaro wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulika Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama kabla ya kuanza safari ya kupanda mlima huo.PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)


……………………..


Na; OWM – KVAU, Kilimanjaro


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amewahimiza vijana kuwa wazalendo na kuithamini nchi yao.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga vijana waliopanda Mlima Kilimanjaro jana tarehe 26 Machi, 2019 Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni kuaadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere.

Waziri Mhagama alisema kuwa, Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere alikuwa kiongozi mzalendo kwa nchi yake na alijali utu na usawa, hivyo ni vyema vijana na vizazi vijavyo wakarithishwa falsafa za Baba wa Taifa.

“Vijana mna kila sababu kuyaenzi matendo ya Baba wa Taifa Mwl. Julius K. Nyerere na Mhasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, Abeid Amani Karume kwa vitendo kwa kuwa ninyi ndio nguzo ya Taifa na mnaelewa vema tulipotoka, tulipo na tunapoenda,” alisema Mhagama.Aliongeza kuwa, Viongozi hawa hawakuwa wabinafsi kwa kujilimbikizia mali na hawakubagua mtu kwa rangi wala kabila bali walijenga Taifa na kudumisha amani na moja.

Aliendele kwa kuwapongeza vijana kwa azma yao ya kuenzi historia na mazuri yaliyofanywa na viongozi hao kwa kupanda mlima Kilimanjaro na kuwatakia baraka waende na kurudi salama.“Kitendo hiki ni cha kishujaa na uzalendo wa hali ya juu kwa Taifa ikiwa ishara ya kumuenzi Baba wa Taifa,” alieleza Mhagama

Aidha Waziri Mhagama alitoa rai kwa vijana kuwa wazalendo na kuwasihi wafanye kazi kwa bidii ili kujenga Taifa kupitia uchumi wa viwanda utakao ifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.Alifafanua kuwa uzalendo lazima ujengwe sambamba na ujenzi wa uchumi wa Taifa, ulinzi na usalama wa Taifa na utunzaji wa tunu za Taifa.

Pamoja na hayo, aliwapongeza na kuwashukuru Viongozi wa Mkoa wa Songwe na Lindi pamoja na uongozi wa Hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) kwa ushirikiano mkubwa na Ofisi yake katika kuwashirikisha vijana kwenye suala hilo.Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Mhe. Kippi Warioba alisema kuwa tukio hili ni muhimu kwa vijana kutambua historia na mchango wa Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere katika Taifa.

“Tumieni fursa hii kupitia vitabu mbalimbali vya kihistoria ili mjifunze mipango, mwenendo na malengo ya Baba wa Taifa itawasaidia na kuwajengea nafasi nzuri ya kujitambua na kuelewa historia ya Taifa,” alisema Warioba.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Bw. James Kajugusi alieleza kuwa Baba wa Taifa alianza harakati za kulikomboa Taifa akiwa kijana na aliendelea kufanya hivyo kwa kuwa hamasisha vijana kujenga Taifa lao baada ya kupata uhuru.

BABA MZAZI WA JOHN BUKUKU AZIKWA KIJIJI CHA IWEZI,MBOZI MKOANI SONGWE

$
0
0
3
Baadhi ya wanakijiji pamoja na viongozi mbalimbali wakiwa wamebeba jeneza la Marehemu Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku(101) tayari wakiupeleka kwenye makazi ya milele
4
John Bukuku ambaye ni Mmiliki wa Blogu ya Fullshangwe ,Baba mzazi wake Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku(101), aliyefariki usiku wa kuamkia , Machi 24, 2019.
2
Jana alihifadhiwa katika nyumba ya milele katika kijiji cha Iwezi,wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria mazishi hayo wakiwemo viongozi wa CCM mkoa wa Songwe pamoja na mkoa wa Mbeya.
1
index
John Bukuku ambaye ni Mmiliki wa Blogu ya Fullshangwe akiwa na baadhi ya ndugu zake baada ya kumaliza shughuri za kumzika ,Baba yake mzazi Marehemu Angolwisye Mwambande Bukuku(101), aliyefariki , Machi 24, 2019. na kuzikwa jana Machi 26 katika kijiji cha Iwezi,wilayani Mbozi Mkoa wa Songwe ambapo viongozi mbalimbali walihudhuria mazishi hayo wakiwemo viongozi wa CCM mkoa wa Songwe pamoja na mkoa wa Mbeya.
Bwana alitoa na sasa ametwaa, jina lake lihimidiwe.
Ameen.

VIJANA TUKILINDA AMANI TUKAWA WAMOJA MAENDELEO YATAKUJA - RC GAGUTI

$
0
0

Anaandika Abdullatif Yunus - Kagera.

Katika kuhakikisha Amani na Usalama Wa Taifa la Tanzania iliyoasisiwa na Viongozi waliotangulia inazidi kudumishwa, Vijana Mkoani Kagera wametakiwa kuwa wazalendo, wamoja, wabunifu, na wajasiliamali ili kuondokana na Umaskini.

Akizungumza na Mamia ya Waendesha pikipiki Mkoani hapa wakati Wa Droo ya Kupanga Timu za Vijana hao ambao Jumamosi ijayo wanatarajia kuanza mashindano ya Ligi ya mpira Wa Miguu maarufu kama JPM BODABODA CUP, Mkuu Wa Mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti mnamo 26, Machi 2019 amesema.

Vijana wana dhima na jukumu kubwa la kulinda Amani ya Nchi yetu kupitia shughuli wanazozifanya kikubwa ikiwa ni matumizi bora ya Vyombo vya Moto, na kupitia mashindano hayo ya JPM BODABODA CUP Vijana wataelimishwa zaidi masuala ya Usalama barabarani.

Kwa upande Mwingine Mh. Gaguti amekaririwa akisema kuwa Tayari Serikali Mkoani Kagera imekwishatenga Zaidi ya Milioni 20 kwa ajili ya Vijana kujiendeleza katika shughuli za Ujasiliamali, ambapo anetumia fursa hiyo kuwataka Vijana Wa bodaboda kuimarisha Vikundi vyao kwa ajili ya kupatiwa fedha ambazo zitawasidia kufanya shughuli nyingine za uzalishaji.

Mashindano ya JPM CUP yanayoratibiwa na Ofisi ya Mkuu Wa Mkoa Kagera kwa Kushirikiana na Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama barabarani yanaanza kutimua vumbi rasmi Jumamosi ya Tarehe 30, Machi kwa kuzishirikisha Timu 16 za Waendesha Bodaboda Manispaa ya Bukoba, huku zawadi zikitajwa kuwa ni pamoja na Kombe kwa Washindi Tatu Bora, pamoja na pesa Taslimu Sh. Milioni 6.
Picha ni RC Gaguti akionesha uwezo wake wa kumiliki mpira wakati wa kuelekea kuanza kwa mashindano ya JPM BODABODA CUP 2019 KAGERA, yanayoratibiwa Chini ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Jeshi la Polisi Kitengo Cha Usalama Barabarani.

 Sehemu ya Vijana wa Bodaboda walohudhuria Uwanjani Kaitaba katika Shughuli ya Kupanga makundi ya Timu zitakazoshiriki Ligi ya Kombe la JPM 2019 KAGERA.
 Mmoja kati ya Viongozi wa Timu za Waendesha pikipiki akiokota karatasi ya Droo ya Upangaji Timu na Makundi katika Mashindano ya JPM BODABODA CUP 2019 KAGERA.
 Pichani ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akizungumza na Vijana Waendesha Bodaboda Uwanjani Kaitaba, katika kuelekea Kuanza kwa Mashindano ya JPM BODABODA CUP Jumamosi ya wiki hii.

JPM amteua Dkt. Richard Faustine Sambaiga kuwa Mwenyekiti wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

HESLB yaweka mikakati ya utoaji elimu kwa wanafunzi wa kidato cha sita.

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) iko katika mkakati wa utoaji wa elimu kwa wanafunzi wa kidato cha sita ili kuweza wanafunzi hao waelewe namna ya kujaza fomu kwa usahihi wakati wa kuomba mikopo katoka bodi hiyo.

Wakizungumza na wanafunzi katika shule za Sekondari za St.Anthony, Kisutu na Zanaki wamesema kuwa wakati wa kuomba mikopo wanafunzi wamekuwa wanafanya makosa ambapo Bodi imeona kuna umhimu wa kuwapa elimu wanafunzi.

Afisa wa Bodi hiyo Daud Elisha amesema elimu wanayoitoa kwa wanafunzi ni kutokana na kuwepo kwa makosa baadhi ya wanafunzi wakati wa uombaji wa mikopo.

Elisha amesema lengo la bodi kuona wanafunzi wa kidato cha sita wanapata uelewa mapema namna ya kuomba mikopo ya bodi kwa vigezo vilivyowekwa.

Aidha amesema elimu wanayoitoa ni mwendelezo kwa nchi nzima katika kuhakikisha kila mwanafunzi anajua kinagaubaga kuhusiana na bodi inavyofanya kazi katika utoaji mikopo kwa wanafunzi wahitaji wa kitanzania.

"Tumedhamiria kutoa elimu kwa wanafunzi wa kidato cha sita pindi wanapohitimu na kujiunga na elimu ya juu wakiomba mkopo wa wasiwe na changamoto ya kufanya ashindwe kuomba mkopo huo"amesema Elisha.

Nae Afisa Mikopo wa Bodi Christina Chacha amesema kuwa licha ya kuwapa elimu ya wanafunzi kuhusiana na uombaji mkopo pia wanatoa elimu ya namna ya kurejesha mkopo huo kwa wale watakaonufaika.

Amesema mkopo wanayotoa kwa wanafunzi kwa ajili ya elimu ya juu lazima ilipwe kwa ajili wengine kukopeshwa.

Aidha maswali ya wanafunzi wengi yalijikita endapo mwanafunzi atapohitimu shahada yake na akawa hajaajiriwa ataulipaje mkopo ambapo bodi hiyo imesema kukosa kazi sio kigezo cha kutolipa mkopo kwani elimu hiyo anaweza kufanya kazi nyingine na kuweza kulipa mkopo huo.
 Afisa wa HESLB Daud Elisha akizungumza na wanafunzi wa kidato cha sita shule ya sekondari kisutu kuhusiana na vigezo vya uombaji mikopo katika bodi hiyo.
 Wanafunzi wa kidato cha sita  Shule ya Sekondari Zanaki wakisikiliza maelezo ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) .
 Afisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Daud Elisha akizungumza na wanafunzi wa kidato cha Sita Shule ya Sekondari Kisutu wakati Bodi hiyo ilipokwenda kutoa elimu ya masuala mbalimbali ya namna wanafunzi wanavyoweza kuomba mkopo katika Bodi hiyo.
 Afisa wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Christina Chacha akitoa maelezo kwa wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya Sekondari Kisutu kuhusu vigezo vya uombaji mikopo na masharti ya mkopo.
 Mkuu wa Shule ya Sekondari Zanaki Julieth Matowo akitoa maelezo wakati Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ilipokwenda kutoa elimu katika shule hiyo.
Wanafunzi wa Kidato cha Sita  Shule ya Sekondari Kisutu wakisikiliza mada kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB)

MAGAZETI YA LEO AL HAMISI MACHI 28,2019

EMIRATES YATANGAZA OFA KWA WATANZANIA ZA KWENDA DUBAI

$
0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

SHIRIKA la Ndege la Emirates limeamua kutoa ofa kwa Watanzania kutembelea Dubai ambapo ofa itapatikana katika daraja la biashara na uchumi ikiwa ni pamoja na mzigo wa tatu kuwa bure.

Taarifa ya Emirates iliyoitoa leo Machi 28,2019 kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam imesema kuwa ofa hiyo ni kwa tiketi ya daraja la uchumi kutoka Dar es Salam hadi Dubai inaanza $ 489 na daraja la biashara ya kuanzia $ 1,499 na kwamba ofa hizo zitatolewa kwa muda maalum na tiketi zinatakiwa kukatwa kuanzia Machi 26, 2019 na Aprili 9, 2019, safari zitaanza kati ya kati ya 26 Machi 26,  2019 na Septemba 30, 2019. Gharama ya tiketi ni pamoja na kodi ya uwanja wa ndege.

Pia Emirates inatoa ofa ya mzigo wa tatu bure mpaka kilo 23 kwa daraja la uchumi na kilo 32 kwa daraja la biashara huku ikifafanua watakaopata ofa hiyo watapata nafasi ya kuitembelea Dubai  ambapo kuna jua mwaka mzima, kuna maduka makubwa ya kutembelea, fukwe nzuri na majengo ya kipekee kwa familia nzima. 

"Wageni wa Dubai wanaweza kufurahia maeneo mengine ya jiji kwa kuona na kutembelea Hifadhi ya Kijiji cha Kimataifa - tamaduni mbalimbali na maeneo ya shopping - pamoja na viwanja vya mandhari kama Wild Wadi Waterpark na IMG World of Adventures,"imesema taarifa hiyo.

Emirates imesema kuwa katika Mji wa Dubai watatoa aina mbalimbali za malazi kukidhi bajeti zote na katika ndege zote za Emirates, wateja wanaweza kufurahia muda wa burudani kwenye mfumo wa burudani unaoweza kushinda tuzo inayoitwa ICE, ambayo inaonesha zaidi ya  vituo 4,000 vya burudani na ya kusikiliza na ya kuona, kutoka kwenye filamu za hivi karibuni na mziki.

Pia vitabu vya sauti na michezo, pamoja na bidhaa zinazopendwa na wanafamilia na huduma kwa watoto, ikiwepo ni pamoja na michezo ya kupendezwa, chakula cha watoto na sinema,familia zitapewa kipaumbele katika kutumia gari ya kumsukumia mtoto akifika uwanja wa Ndege wa Dubai.

Imesisitiza pamoja na huduma nzuri za kuingia na bidhaa, wateja wataweza kupokelewa vizuri na wafanyakazi wa kimataifa wa Emirates ambao hutokana na zaidi ya mataifa135 na ambao wanazugumza lugha zaidi ya 60, huku wakifurahia vyakula vya kikanda na kimataifa, kwa kutumia viungo vingi, ikifuatana na aina mbalimbali za mvinyo na vinywaji vingine.

"Tunawaomba Watanzania kuchangamkia ofa hii ambayo imekuja wakati muafaka , kikubwa ni kuhakikisha wananunua tiketi za Emirates kulingana na muda ambao umetolewa wa kipindi cha ofa.Kwa anayehitaji mawasiliano tafadhali anaweza kutembelea tovuti yetu ya www.emirates.com/tz au tembelea ofisi za Emirates au wakala wa usafiri,"imesema taarifa hiyo.

BancABC yatoa msaada wa mabati 200 kwa wilaya ya Kilindi.

$
0
0
BancABC kupitia Huduma yetu ya Mkopo Rahisi imejidhatiti kuweza kuhakikisha kwamba tunainua kuendeleza mazingira ya elimu katika wilaya ambazo benki hii inafanya shughuli zake kupitia miradi yetu ya kusaidia jamii inayotuzunguka. 

Sisi BancABC tunaamini kwenye umuhimu wa elimu bora katika jamii zetu hapa Tanzania na kwa hivyo tunaunga mkono Serikali ya Awamu ya 5 na hususani Rais wetu Mhe. John Pombe Mafuguli Katika miradi mbali mbali ya elimu kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu na kuweza kuwafikia kila jamii na hasa maeneo ya vijijini kwa wale ambao wako kwenye hali duni. 

Akizungumza katika hafla hiyo fupi Bw. Emmanuel Nzutu ambaye ni mkuu wa kitengo cha mauzo rahisi alisema; “Kwa kuunga mkono juhudi za serikali za kutoa elimu bure kwa kila Mtanzania kuanzia chekechekea hadi kidato cha nne, Leo Bancabc tunatoa msaada wa mabati 200 kwa wilaya ya Kilindi, na msaada huu tunaukabidhi hapa kwa Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Sauda Salum Mtondoo.” 

Napenda kuchukua fursa hii kuwakaribisha Bancabc na pia kuwajulisha kuwa benki yetu tunatoa huduma ya Mkopo ambao ni mahususi kwa wafanyakazi wa serikali, Easy loans ambapo inakupa nafasi ya kulipa Mkopo kwa muda wa miaka sita na vile vile una uwezo wa kuweza kuongeza Mkopo hata kabla ya kumaliza kulipa ule wa awali. 

Uzuri wa mkopo huu tofauti na mikopo mingine ni kwamba, mwenye kuomba Mkopo anaweza kuchagua ni mradi gani wa kuwekeza fedha zake kwa mfano kulipa karo ya shule, kununua gari, kufanya marekebisho ya nyumba, kulipa kodi ya nyumba au kumalizia ujenzi. 

Vile vile tunaweza kununua Mkopo wako wa awali ukabaki na Mkopo mpya. 

‘Mkopo huu utakuwa na bima ya maisha pale ambapo mwenye Mkopo anapofariki, familia yake inapewa pesa taslimu Tzs500, 000 kwa ajili ya kugharamia mazishi.’ 

Tunatoa wito kwa wateja wetu na wale ambao pia sio wateja wetu kujiunga na Bancabc na kuchangamkia Mkopo huu kwani sisi tunakuweka karibu na ndoto zako.
Mwakilishi wa benki ABC Bw. Emmanuel Nzutu (Mkuu wa kitengo cha mauzo rahisi) akikabidhi msaada wa mabati kwa mkuu wa wilaya ya Kilindi Mh. Sauda Mtondoo
Mwakilishi wa benki ABC Bw. Emmanuel Nzutu (Mkuu wa kitengo cha mauzo rahisi) akiwa pamoja na Asmah Abubakar(kushoto) kutoka kitengo cha masoko wa BancABC wakikabidhi msaada wa mabati kwa mkuu wa wilaya ya Kilindi Mh. Sauda Mtondoo (kulia)
Mwakilishi wa benki ABC Bw. Emmanuel Nzutu (Mkuu wa kitengo cha mauzo rahisi) akiwa pamoja na Asmah Abubakar(kushoto) kutoka kitengo cha masoko wa BancABC wakikabidhi msaada wa mabati kwa mkuu wa wilaya ya Kilindi Mh. Sauda Mtondoo (kulia)
. Mheshimiwa Sauda Salum Mtondoo, mkuu wa Wilaya ya Kilindi akikabidhi mabati yaliyotolewa na BancAbc kwa walimu wa shule ambazo zimenufaika na msaada huo.
Mwakilishi wa benki ABC Bw. Emmanuel Nzutu (Mkuu wa kitengo cha mauzo rahisi) akiwa pamoja na Asmah Abubakar kutoka kitengo cha masoko wa BancABC wakikabidhi msaada wa mabati kwa mkuu wa wilaya ya Kilindi Mh. Sauda Mtondoo
Mwakilishi wa benki ABC Bw. Emmanuel Nzutu (Mkuu wa kitengo cha mauzo rahisi) akipeana mkono na mkuu wa wilaya ya Kilindi Mh. Sauda Mtondoo baada ya kukabidhi msaada wa mabati 200. Wengine katika picha ni Asmah Abubakar na Raphael Kalinga wa BancAbc.

MISS TANZANIA QUEEN ELIZABETH ASAINI MKATABA NA TTB KUTANGAZA UTALII

$
0
0
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.

Miss Tanzania 2018/2019 Queen Elizabeth Mukune amesaini mkataba 
wa kuwa Balozi wa Bodi ya Utalii Tanzania leo March28 2019 kwa kutangaza Utalii wa ndani na kutoa hamasa kwa watanzania. 

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam  wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba huo wa mwaka mmoja Queen Elizabeth anasema kuwa yeye anaona fahari kubwa kupata nafasi ya kuwa balozi wa kutangaza vivutio vyetu hivyo amefurahi kupata nafasi hiyo.

"nimefurahi kupata nafasi ya kutangaza vivutio vyetu ndani na nje ya nchi na naahidi kuitumia nafasi hii vizuri kabisa  kwa kutumia nafasi na umaharufu wangu nilionao kwa sasa kwa kuwa mfano wa Mrembo ambaye nitafanya ziara ya utalii wa ndani kama taji langu linavyojieleza kwani nitatoa hamasa kupitia mitandao yangu ya kijamii na makundi yote yanayoniunga mkono hili waweze kutembelea vivutio vyetu vilivyopo hapa nchini"anasema 

Naye Mkurugenzi Mwendeshaji wa bodi ya Utalii nchini Devotha Mdachi anasema katika kuendelea kutangaza utalii wa nchi wamehamua kutumia vijana wenye ushawishi ili kuzidi kuitangaza  utalii wetu kwa watanzania na wageni wanaotuzunguka. 

"Tumeamua kumtumia Miss Tanzania kwanza ni kijana pia anaushawishi mkubwa kwa jamii kwa watu wengi kwani ameweza kutuwakilisha kimataifa hivyo kupitia yeye tutaweza kutangaza vivutio vyetu vikafika mbali na kuwafikia vijana wengi hapa nchini ambao wamekuwa wakifatilia masuala ya burudani na urembo"anasema.

anasema wataendelea kuwatumia vijana maarufu kuzidi kutangaza utalii wa nchi na wameshaanza mazungumzo na baadhi yao. 
 Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii nchini,Devotha Mdachi akizungumza na Waandishi wa habari Kabla ya kutiliana Saini na Miss Tanzania 2018/2019, Queen Elizabeth Mukune katika Ofisi za TTB Zilizopo Jijini Dar es Salaam.
 Miss Tanzania 2018/2019, Queen Elizabeth Mukune akizungumza na Waandishi wa habari kabla ya kutiliana Saini Mkataba wa kuwa Balozi wa Bodi ya Utalii Nchini.
 Miss Tanzania 2018/2019, Queen Elizabeth Mukune pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii nchini,Devotha Mdachi wakitiliana saini Mkataba wa mrebo huyo kuwa balozi wa utalii nchini
  Miss Tanzania 2018/2019, Queen Elizabeth Mukune pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii nchini,Devotha Mdachi, Wakibadilishana Mkataba mara baada ya kuliana Saini
Sehemu ya Waandishi wa habari waliofika kushuhudia utiliaji saini Mkataba wa  Miss Tanzania 2018/2019, Queen Elizabeth Mukune pamoja na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Bodi ya Utalii nchini,Devotha Mdachi

Dkt. Ussi atembelea Shamba Asilia nchini Cuba

$
0
0
Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Ufugaji na Uvuvi Zanzibar, Mhe. Dkt. Makame Ali Ussi, ametembelea shamba la mimea asilia ( organic farm ) nchini Cuba, ambapo alipata maelezo juu ya uzalishaji wa mazao mbalimbali bila kutumia kemikali ambapo mradi huo umeweza kuajiri wafanyakazi takribani 200 wakiwemo wazee na vijana. Wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Shamba hilo, wa pili kutoka kulia ni mkalimani Bi. Beatriz Soto na wa kwanza kushoto ni Afisa kilimo, Bw. Jose Antonio. 
Mhe. Dkt. Ussi akiendelea kupata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa shamba hilo, Bw.Miguel Angel Lopez, wa kwanza kulia ni Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Mohamed Kamal Mohamed, akisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa. 

Mhe. Dkt. Ussi akiendelea kupata maelezo juu ya kilimo cha miwa. 
Juu na chini Mhe. Dkt. Ussi akipata maelezo namna ya utengenezaji wa mbolea isiyokuwa na kemikali yeyote. 
Bw. Lopezi akimwonyesha Mhe.Dkt. Ussi teknolojia ya kifaa cha kupandia mazao. 
Mhe. Dkt. Ussi akizungumza na mmoja wa wakulima kwenye shamba hilo, aliyeonekana kufurahishwa na ujio wa Watanzania.
Sehemu ya mazao yanayopatikana kwenye shamba hilo. 


TFS YATAJA HATUA ZA KUCHUKUA KUKABILI ATHARI ZA UHARIBIFU WA MAZINGIRA NCHINI

$
0
0


*Yazungumzia Maadhimisho ya Siku ya upandaji miti itakayofanyika Aprili Mosi

*Kitafaifa kufanyika Wilaya ya Same mkoani Kimanjaro.... yatoa mwito kwa jamii



Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) umesema ili kukabiliana na athari za uharibifu wa misitu ipo haja ya kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana na hali hiyo ikiwemo ya kila familia kuanzisha bustani ndogo yenye miche inayoweza kutoa kivuli na matunda ambayo inayolingana na idadi ya wanafamilia.

Ambapo hiyo itakuwa rahisi kuitunza miche hiyo kwa kutumia maji yanayopatikana nyumbani au kutumia umwagiliaji wa matone ya maji kwa kutumia chupa (drip irrigation).

Hayo yamesemwa kwenye taarifa ya TFS iliyotolewa leo Machi 28,2019, kuelea Maadhimisho ya Siku ya Upandaji Miti ambayo ni Aprili 1 na kitaifa maadhimisho ya siku hiyo yatafanyika wilayani Same mkoani Kilimanjaro ambayo yatakwenda ambamba kwa ngazi ya mikoa yote Tanzania Bara kupanda miti.

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Tulizo Kilaga amesema kuwa maadhimisho ya mwaka huu ni ya kipekee kwa kuwa ni mwaka ambao utaratibu wa kuadhimisha siku hiyo utafanyika kwa kupanda miti zaidi badala ya kutumia fedha nyingi katika sherehe ya maazimisho ya siku hiyo. Kaulimbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni 'Tanzania ya Viwanda inawezekana, panda miti kwa maendeleo ya Viwanda'.

Akifafanua zaidi kuhusu hatua nyingine za kuchukua kukabiliana na athari za uharibifu wa misitu ni kuongeza kiwango cha upandaji miti kwa kupanda mbegu moja kwa moja ardhini kwa baadhi ya miti hasa katika mikoa iliyo na maeneo yenye mvua nyingi ikiwqepo Mikoa ya Tanga, Iringa, Mbeya na Njombe.


Pia kustawisha miti kwa kutumia miche inayojiotea yenyewe ardhini kama maotea. Miche hiyo inapandwa katika sehemu zilizokusudiwa ikiwa bado midogo. Njia hii inatumika hasa kwenye sehemu zenye mvua nyingi na udongo tifutifu.

Kilaga amesema ni vema kustawisha misitu ya asili kwa kutenga na kulinda eneo kutokana na uharibifu wa kimazingira ili mbegu ziote zenyewe (natural regeneration).Njia hiyo imefanikisha shughuli za kustawisha misitu na malisho ya mifugo mkoani Shinyanga na kwamba wananchi wa Shinyanga wanatumia utaalam wao wa jadi unaojulikana kwa jina la Ngitili wa kutenga maeneo na kuyapumzisha ili mbegu zijiotee zenyewe, matokeo yake mkoa huo umeongeza zaidi ya hekta 500,000 za ardhi ambayo ilikuwa imeharibika kabisa hapo awali lakini sasa ina miti.

Pia kuanzisha mashamba makubwa ya miti kwa lengo la kutunza mazingira na kujiongezea kipato na kwmaba katika kuadhimisha siku hiyo TFS itapanda miti katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa kushirikiana na wadau ambapo katika jiji la Dar es Salaam upandaji huo utafanyika eneo la Kilongawima Mbezi Beach kwa kupanda mikoko na mivinje.

"Wadau na wananchi wote mnakaribishwa kushiriki zoezi hili muhimu kwa mstakabari wa nchi yetu. Maadhimisho ya Siku ya Taifa ya kupanda miti yalifanyika kwa mara ya kwanza Januari Mosi mwaka 2001 kutokana na Waraka wa Waziri Mkuu namba 1 wa mwaka 2000 na kuhuhishwa mwaka 2009 na kuifanya siku hiyo kufanyika Aprili Mosi kila mwaka ukimtaka kila mwananchi kupanda miti kwa manufaa yake.

"Mwaka jana Siku ya Taifa ya Kupanda Miti iliadhimishwa kitaifa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Aprili 3 hadi 5, 2018.Ni wajibu wa kila mmoja wetu kutathimini athari atakazopata kutokana na ufyekaji na uharibifu wa misitu ili aamue kwa dhati kuihifadhi misitu kwa ajili ya kuwanufaisha watu wa kizazi hiki na vizazi vijavyo,"amesema.

Kuhusu maadhimisho ya siku hiyo ya upandaji miti ,Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unatoa mwito kwa kila Mtanzania kutathmini tulikotoka, tulipo na tunapokwenda kuhusiana na hali ya misitu.

KWA TANESCO HII MSEMA KWELI MPENZI WA MUNGU...

$
0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MACHO yangu yanashuhudia kazi kubwa na nzuri inayofanywa na Shirika la Umeme  Tanzania(TANESCO) chini ya Wizara ya Nishati kwa niaba ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dk.John Magufuli.

Kubwa zaidi masikio yangu kwa miaka miwili sasa yamekuwa yakisikia sifa zikitolewa kwa TANESCO kwasababu tu yale mambo ya kukatika katika kwa umeme yamepungua .Tulizoea kuita mgao.Mara umeme unatika...mara huooooo umerudi.Leo hii umeme ukikatika basi ni kwasababu maalumu na umma utakuwa umeshapata taarifa mapema.Mbona raha jamani.

Kwangu mimi najaribu kuiangalia TANESCO ya sasa na ile ya zamani.Kuna tofauti kubwa ya kiutendaji.TANESCO ya sasa chini ya Mkurugenzi Mtendaji wake Dk. Tito Mwinuka inajua umuhimu wa nishati ya umeme.Inajua kabisa uchumi wetu unahitaji uwepo wa umeme wa uhakika katika kufanya shughuli zao za kila siku.

TANESCO inayoongozwa na Dk.Mwinuka inajua umuhimu wa kutoa taarifa kwa wananchi hasa pale ambapo kutakuwa na matenengezo katika eneo fulani.TANESCO ya sasa inajua kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inataka kuelekea uchumi wa kati ambao utachagwiza na umeme wa uhakika.

Pia inatambua fika kama kuna eneo ambalo lilikuwa linalalamikiwa ni kukatika kwa umeme.Mgao wa umeme ulikuwa kero kwa watu wengi.Tena kero haswaa na najua sio kwangu tu hata kwako.Ndio mgao ilikuwa kero.Unabisha?

Serikali ya Awamu ya Tano kwa kutambua nchi yoyote ili iendelee inahitahaji kuwa na nishati ya umeme wa kutosha na uhakika.Ndio maana leo hii TANESCO inaendelea na ujenzi wa miradi mikubwa na midogo ya umeme ambayo ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji wake.

Kutekelezwa kwa miradi hiyo na hasa kwenye maeneo ambayo awali yalikuwa na tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara leo hii hakuna tena mgao.Wananchi wanafurahia nishati hiyo ya umeme wa uhakika.Ukitaka kuamini hili inaloeleza hapa nenda mikoa ya Kaskazini ikiwemo ya Arusha na Kilimanjaro.Hawana tena tatizo la kukatika kwa umeme kama zamani.

Sote tunafahamu kabla ya Awamu ya Tano kuingia madarakani kulikuwa na changamoto kubwa ya umeme.Leo hii imebaki historia.Umeme unaozalishwa Mkoa wa Arusha umekidhi mahitaji na kufanya kuwepo na umeme wa akiba.Hivyo ninaposema TANESCO inastahili pongezi sio kwamba natoa sifa sehemu ambayo haistahili.

Hongereni TANESCO kazi ambayo mnaifanya kwa niaba ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kubwa na tunaiona. Pamoja na mambo mengine , TANESCO kwa sasa wanaendelea na majukumu ya kuendelea kutatua changamoto zilizopo kwenye sekta ya nishati ya umeme.

Na si tu kuondoa changamoto,pia imeendelea na wajibu wake mkubwa kusambaza umeme kwa wananchi.Nafahamu jitihada za kupeleka umeme kwa kila kijiji ndani ya nchi yetu kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA).

Naomba niwe mkweli na msema kweli ni mpenzi wa Mungu.Hakika Wizara ya Nishati na TANECSO wanafanya kazi kubwa ya kuhakikisha umeme unafika kwa kila Mtanzania anayeuhitaji.Kwa siku mbili hizi nimekuwa nikishuhudia baadhi ya nyumba tena za matembe zikiwa zimewekwa umeme.

Kwa muda mrefu tumekuwa tukisikia tu, umeme unawekwa vijijini ila kwa bahati mbaya tupo baadhi yetu ni kama Tomaso.Bila kuona hakuna kuamini.Sasa tunaamini kumbe kweli.Hivyo uwepo wa picha hizo ambazo zinaonesha nyumba za udongo zikiwa zimewekwa umeme inaleta maana halisi ya kile ambacho Wizara ya Nishati inafanya kwa wananchi wake.

Tunafahamu kauli mbiu ya TANESCO imekuwa ikisema "Tunaangaza maisha" .Nimeamini hata uwe kijijini bado utaangaziwa maisha.Hili ni jambo jema na la kupongezwa.Umeme wa uhakika vijijini ni jambo la msingi sana, na tunafahamu kwa muda mrefu vijiji vyetu vilikosa maendeleo kwasababu ya kutokuwa na umeme.Leo wanao.

Kwa waliobahatika kuishi maeneo ya vijijini wanafahamu mazingira ya kutokuwa na umeme.Wana vijiji wanalazimika kutembea umbali mrefu kutafuta nishati ya umeme.Ameaniaka mahindi au mpunga wake lakini linapofika suala la kusaga au kukoboa anawaza umbali wa kwenda mashineni.Leo hii hakutakuwa na kuwaza tena.

Umeme unapatikana kila mahali.Shida iko wapi? Hata hivyo, kuna baadhi ya watu kwenye mitandao nimeona wakijadiliana na wengine kuhoji kwanini umeme unawekwa kwenye nyumba za tembe ambazo kuta zake zinatengenishwa na udongo.Kwangu naona wanaohiji hayo ni kama vile wamekosa hoja.

Watalaam wamejiridhisha na wanajua hakuna madhara yoyote kwani kuna vifaa maalum vinavyotumika katika kuunganisha umeme kwenye nyumba hizo.Nitoe rai kwa Wizara ya Nishati pamoja na TANESCO endeleeni na majukumu yenu ya kuweka umeme vijijini.Kwa maisha ya sasa nishati ya umeme ambayo ni ya uhakika inahitajika sana kuliko nyakati nyingine zozote.Huo ndio ukweli.

Kwanini bibi na baba yangu waendelee kuteseka? Eti washindwe kuwa na luninga pale sebuluni kisa tu wapo kijijini.Eti waendelee tu kutumia vibatari .Hapana bwana lazima ifike mwisho.Walioko vijijini ni Watanzania na wana haki ya kupata umeme kama wengine wanaoishi maeneo ya mijini.

Tunafahamu kuna baadhi ya familia ambazo ziko mjini na zilishindwa kutembelea ndugu , jamaa na marafiki walioko vijijini na sababu tu ni kwamba eti wakienda huko hakuna umeme na wanasema hawawezi kutumia vibari.Kufungwa kwa umeme katika nyumba zetu za vijijini ambako wengi ndiko tunatokea, kunakwenda kufanya mabadiliko makubwa.

Mjini umeme upo na kijiji nako upo.Ukiishi kwenye ghorofa utakuwa na umeme na ukiishi kwenye nyumba ya tembe utakuwa na umeme.Hongereni TANESCO. Kufungwa umeme kwenye nyumba za vijijini kunakwenda kuifanya Tanzania kuwa yenye maendeleo.Kokote Mtanzania alipo na anahitaji umeme kwa ajili ya ujenzi wa maendeleo ya nchi yetu.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ameizindua nyumba ya Rose Kagoma iliyounganishiwa umeme wa REA katika Kijiji cha Ruganga Wilayani Kibondo.Katika hafla hiyo iliyofanyika Machi 24 mwaka huu, Waziri Kalemani amewataka Wandarasi kutokubagua Wananchi kwenye mradi huoKijiji cha Rugunga kimeunganishiwa umeme kupitia mradi wa umeme Vijijini wamu ya tatu sehemu ya kwanza(REA)

SELOU MARATHON KUFANYIKA KWA MARA YA KWANZA MKOANI MOROGORO AGOSTI 25 MWAKA HUU

$
0
0

Na Agness Francis, blogu ya jamii.

UZINDUZI wa maandalizi ya mbio za riadha Selou marathon umefanyika leo ambapo itakuwa ni mara ya kwanza kufanyika mkoani Morogoro agosti 25 mwaka huu, lengo likiwa ni kukuza utalii wetu wa ndani na nje ya nchi pamoja na kujenga afya.

Mgeni rasmi ambaye ni muaakilishi wa mkurugenzi wa baraza la michezo Taifa Neema Msitu, akizungumza na vyombo vya habari wakati wa uzinduzi huo leo Jijini Dar es Salaam ambapo ametoa wito kwa watanzania kujitokeza kushiriki mbio hizo za Selou marathon itakayofanyika mkoani Morogoro pamoja na kushiriki michezo yote kwa ujumla.

"Michezo inajenga mwili na afya na kutupa uhai hivyo basi watanzania tuweke utamaduni wa kufanya mazoezi,pia tukijumuika kwa pamoja kushiriki mbio hizo tutakuza utalii wetu na uchumi pia"amesema Neema Msitu.

Aidha mratibu wa Mratibu wa Selou Marathon Rehema Jonas amesema kuwa uzinduzi wa mbio hizo inahazina kubwa ya watu wanaopenda michezo na kwa kutambua hilo wameamua kuchukua jukumu la kuandaa mbio za riadha mwaka huu mkoani morogoro.

"Morogoro ni Mkoa unaofikika kiurahisi zaidi nataraji watu wengi kutoka sehemu mbali mbali watajitokeza kuja kujumuika nasi mbio ambazo zitaanzia kilimota 21,kilomita 10,kilomita 5 ambazo ni za furaha pamoja na mbiao za kilomita 2 na nusu kwa ajili ya watoto." amesema Mratibu huyo.

Hata hivyo mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya Selou marathon Emmanuel Kajula pia ameongezea kuwa lengo la kuandaa mbio hizo ni kutaka kuchochea na kukuza maendeleo ya mbio za riadha nchini Tanzania, ambapo ameeleza kuwa maendeleo ya mchezo huo hautafika mbali kama hakutakuwepo na waandaaji wa uhakika.

Nao mabalozi wa Selou marathon Msanii wa kizazi kipya Barnaba boy pamoja na mchekeshaji Tabu mtindiga wametoa wito kwa wasanii na vijana wenzao kuunga mkono mandalizi ya mbio hizo mpaka zitakapofikia kilele chake agosti 25 mwaka huu.
Mgeni rasmi  ambaye ni  muaakilishi wa mkurugenzi wa baraza la michezo Taifa Neema Msitu,akikata utepe akiashiria maandalizi ya uzinduzi wa Selou Marathon yamezinduliwa rasmi leo Jijini Dar es Salaam
 Mgeni rasmi  ambaye ni  muakilishi wa mkurugenzi wa baraza la michezo Taifa Neema Msitu akizungumza wakati wa uzinduzi wa Selou Marathon leo Jijini Dar es Salaam ambapo mbizo hizo zitafanyika Mkoani Morogoro agosti 25  mwaka huu.
 msanii wa kizazi kipya Barnaba boy, ambaye pia mi balozi wa mbio za Selou marathon  akizungumza na vyombo vya habari  wakati wa uzinduzi huo leo Jijini  Dar es Salaam.
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images