Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

MAJIBU YA ZITTO KABWE KWA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA

$
0
0

*Ni baada ya Ofisi ya Msajili kutoa barua ya kusudio la kukifuta Chama hicho
*ACT Wazalendo wajitetea kwa kukiri kupeleka hesabu kwa CAG,wagusia udini

Na Said Mwishehe,Globu ya jmii

CHAMA cha ACT Wazalendo kupitia Kiongozi wake Zitto Kabwe kimefafanua na kuweka wazi kuhusu tishio la Msajili wa Vyama vya Siasa kutaka kukifuta chama hicho ambapo pamoja na mambo mengine wamejibu hoja moja baada ya nyingine.

Kauli ya Zitto inakuja baada ya jana Machi 25,2019,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuwaandikia barua ACT-Wazalendo ambayo kwa sehemu kubwa ilijikita katika mambo matatu na kisha kutoa kusudio la kutaka kukifuta.

Kwa mujibu wa barua hiyo ya Msajili wa Vyama vya Siasa jambo la kwanza ni hoja zinazohusu ukaguzi wa hesabu ,pili ni vitendo vya kuchomwa hadharani kwa bendera na kadi za chama cha CUF na tatu ni matumizi ya neno Takbiri kama yalivyoonekana katika baadhi ya video zilizosambaa katika mitandao ya kijamii.

Akizungumza leo Machi 26,2019 akiwa katika Makao Makuu ya ACT-Wazalendo Zitto amesema kuhusu ukaguzi ni kwamba barua ya Msajili wa vyama vya siasa inadai ACT imekiuka sheria ya vyama vya siasa kwa kutopeleka kwake hesabu zilizokaguliwa kwa mwaka wa fedha wa 2013/2014 kama sheria inavyotoka.

Amesema tuhama hizo hazina ukweli wowote kwasababu wajibu wa Chama cha siasa ni kuwasilisha hesabu zake kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG) na kwamba hesabu za mwaka 2013/2014 ziliwasilishwa kwa CAG na kufafanua Chama hicho kilianzishwa kwa kupata usajili wa kudumu Mei 5 ,2014 miezi miwil kabla ya mwaka wa fedha wa Juni 30,2014. 

"Kwa kutumia kanuni za kimataifa za kihesabu na kwa ushauri wa CAG ,Chama chetu kilielekezwa kinaweza kuunganisha hesabu za mwaka 2013/2014 na 2014/2015 katika ripoti moja.Na hili ni jambo la kawaida kabisa katika kanuni za uhasibu kwani inaruhusu kuunganishwa hadi miezi 18 .ACT ilikuwa na miezi 14 tu.

" Kabla ya kuchukua uamuzi huu wa kuunganishwa hesabu,Chama chetu kilimwandikia Msajili wa vyama vya siasa kwa barua mbili zenye kumbukumbu namba AC/HQ/ MSJ/ 2015/006 na AC/ HQ/ MSJ/ 2015/008 za tarehe 22 na 29 Januari 2015.Naye alijibu na kuridhia hesabu za miezi miwili za mwaka 2013/2014 kuunganishwa kwenye mwaka wa fedha 2014/2015,"amesema.

Zitto ameongeza taarifa zote hizo ziko wazi kwa CAG na kama Msajili wa vyama vya siasa angekuwa na nia njema angeweza tu kuuliza na angepewa taarifa sahihi.Kazi ya Chama cha siasa ni kuwasilisha hesabu zake kwa CAG na sio kwa kukagua hesabu zake chenyewe.

"Tulitimiza wajibu wetu huo, CAG naye alitimiza wajibu wake kwa kutukagua ,hivyo basi Chama chetu kwa sasa hakuna mwaka ambao hakijawasilisha hesabu zake.Kwa mwaka 2015/2016 na 2016/2017 chama kina hati safi na mezani kwake.

" Mambo haya ya ukaguzi yako nje ya wigo wa uelewa wa Msajili na ndio maana sheria za nchi zinampa CAG wajibu wa kufanya mambo haya na ukaguzi wa msajili kuwa mlezi wa vyama vya siasa.Msajili afanye mambo anayoyajua,asiyoyajua aachane nayo,"amesema Zitto.

Kuhusu kuchoma bendera na kadi, Zitto amesema barua yenyewe ya Msajili iliyowafikia inasema kuwa hana uhakika kama kweli wahusika ni wanachama wa ACT Wazalendo wakichoma bendera na kadi za chama cha CUF.

"Katika hili Msajili mwenyewe anaonesha hana uhakika kama kweli wahusika ni wanachama wa ACT.Inashangaza anafika uamuzi wa kuandika barua ya kutishia kutufuta kama chama cha siasa kwa tuhuma ambazo hata yeye mwenywe hana uhakika nazo," amefafanua.

Kuhusu Takbir ,Zitto amesema barua ya Msajili wa vyama vya siasa inaeleza chama chao kimevunja sheria ya vyama vya kwasababu wanaodaiwa kuwa wanachama wao wametumia maneno ya takbiri kwenye shughuli za kichama na kwamba maneno hayo ni udini.

"Jambo hili limetushangaza na kutuudhi kwa wakati mmoja.ACT ni chama cha watu wa dini zote na hata wale wasio a dini.Katiba yetu ya Chama tumeonesha wazi hatufungamani na dini yoyote na ndio sababu tumeruhusiwa kufanya shughuli za kisiasa.Hata hivyo tunafahamu watanzania wana dini zao na wana maneno yao ambayo ni ya kawaida kutumia na hayana uduni wowote.

"ACT haitaki kuamini kusema Takbir kwa muumini wa dini ya Kiislam au hata kwa Mkristo ni udini .Jambo hili tunaachia wanazuoni na waumini wa dini ya Kiislamu walieleze vizuri na kumfahamisha Msajili kwamba hakuna udini wowote katika neno hilo la kuitiana hamasa kwa wahusika,"amesema Zitto.

Amefafanua barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa haina nia njema kwa ACT Wazalendo na wapenda demokrasia wote hapa nchini huku akiitumia nafasi hiyo kuomba Msajili kuangalia na kutafakari kwa upana kuhusu hiyo barua yake na ikiwezekana aifute mara moja kwani inaonesha namna ambavyo nia yake sio nzuri kwa Chama hicho. Hata hivyo amesema barua ya Msajili haiwatishi na wala hawatatishika na kusisitiza kuwa ACT inafanya shughuli zake za kisiasa kwa misingi ya kuheshimu na kuifuata Katiba ya nchini na kwamba wanachama wao kokote waliko wahakikishe wanaheshimu Katiba.
 Waandishi wa habari wakifautilia mkutano wa CHAMA cha ACT Wazalendo kupitia Kiongozi wake Zitto Kabwe alipokuwa akifanunua mambo mbalimbali kuhusiana na tishio la Msajili wa Vyama vya Siasa kutaka kukifuta chama hicho ambapo pamoja na mambo mengine wamejibu hoja moja baada ya nyingine.
 

NHIF TANGA YAJIPANGA KUTOA ELIMU YA KUTOSHA KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA ILIYOBORESHWA

$
0
0
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Tanga NHIF umejipanga kuhakikisha inatoa elimu ya kutosha kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima ya afya iliyoboreshwa .

Kauli hiyo imetolewa na Meneja wa Mfuko huo  Mkoani Tanga, Ally Mwakababu wakati akizungumza na MTANDAO huu kuhusu walivyojipanga kuhakikisha wanaongeza wananchi na kuboresha huduma zao.

Alisema kuwa iwapo wananchi wataweza kupata uwelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa kuwa na kinga ya matibabu kabla ya kuugua wataweza kuwakomboa wananchi wengi.

“Hakuna mtu au kiongozi ambaye atakuwa tayari kuongoza wananchi ambao ni goigoi wa maradhi hivyo Bima ya afya tumejipanga kuhakikisha kwanza tunaongeza idadi ya wanachama lakini kupitia wao  tutaweza kuboresha huduma katika vituo vya afya”alisema Mwakababu.

Hata hivyo Mwakababu alisema kuwa licha ya mkoa wa Tanga kuwa wapili kwa uandikishaji wa bima ya afya ya jamii CHF  lakini bado eneo hilo hawakuweza kufanya vizuri zaidi hivyo kwa mwaka huu wamejikita katika kuongeza uhamasishaji zaidi.

Alisema kuwa wamejipanga kufanya hamasa kuanzia ngazi ya mkoa hadi vijiji kwa kushirikisha viongozi wa kiserikali na kisiasa kwa lengo la kuhakikisha kila mwananchi ndani ya Tanga anaona umuhimu wa kuwa na kadi ya Bima.

Vile vile akiongelea kadi ya Bima ya Toto afya Mwakababu alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2017/18 waliweka lengo la kuandikisha watoto waliochini ya umri wa miaka 18 ,3000 badala yake waliandikisha 913.

Huku kwa walioko katika ngazi ya sekondari na vyuo ambao wanatumia huduma ya Toto afya kadi waliweza kuandikisha 1435 kati ya malengo waliyojiwekea ya kuandikisha wanachama 3000.

“Tatizo kubwa ni mwamko mdogo wa wananchi kuona umuhimu wa kuwa na bima ya afya  wao wanasubiri mpaka ugonjwa uwe mkubwa  na kushindwa gharama za matibabu lakini kumbe kama wangeweza kujiunga mapema wasiweza kupata huduma bora”alisema Meneja huyo.

KAMATI YA USHINDI YATOA SHUKRANI KWA WATANZANIA WOTE...MAKONDA AWEKA WAZI

$
0
0



*Asema ushindi wa Taifa Stars ni wa Watanzania wote

*Asisitiza sasa timu yoyote itakayokuja nchini itapigwa tu



Na Said Mwishehe,Globu ya jamii



KAMATI ya Saidia Taifa Stars ishinde yenye wajumbe 14 wakiongozwa na Mwenyekiti wao Paul Makonda imetoa shukrani kwa Watanzania wote kwa kufanikisha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kushinda mechi yake dhidi ya Timu ya Taifa ya Uganda.




Taifa Stars waliifunga Uganda mabao 3-0 na hivyo kufanikiwa kuipeleka Tanzania nchini Misri kwenye michuano ya AFCON mwaka 2019.Ushidni wa Taifa Stars umeifanya nchi yetu kuandika historia ya aina yake baada ya miaka 39.



Akizungumza leo Machi 26,2019 jijini Dar es Salaam Makonda amesema  Kamati ya Saidia Taifa Stars ishinde inatoa shukrani kwa makundi mbalimbali kwa kufanikisha ushindi huo ambao ni Watanzania wote.



"Nitoe shukrani kwa  wapenzi ,wakereketwa na wadau wote wa michezo. Walihakikisha Taifa Stars inashinda kwa kushiriki kwenye dua na sala.Kamati yetu ilikuwa na kazi kubwa mbili , kwanza ni kuhakikisha Taifa Stars inashinda na mbili kufuatilia mchezo mwingine wa Lethoto na Cape Verde.



"Baada ya Rais wa TFF kuteua kamati hii tulihakikisha  hatukuangushi na tunafahamu tulipoteza mechi yetu dhidi ya Lethoto ambako kwa sehemu fulani kulikatisha tamaa.Tuliwepa kazi ngumu,"amesema Makonda.



Amefafanua ili kuhakikisha kamati inatimiza majukumu yake ilichukua jukumu la kuunda makundi mbalimbali yakiwamo ya watu mashuhuri, mastaa katika tasnia ya sanaa nchini, wanamichezo wa zamani, wenye mahoteli, wenye baa,vyombo vya habari na wenye vyombo vya usafiri.



Amefafanua katika nchi yetu klabu za Simba na Yanga ndivyo vyenye mashabiki wengi wa soka, hivyo aliona haja ya kuwachukua Haji Manara na Jerry Muro ambao nao aliwaita kwenye kamati hiyo na hakika wametoa mchango mkubwa katika kusaidia kuunganisha mashabiki wa vilabu hivyo.



Makonda ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema pamoja na kazi hiyo Kamati yao ilihakikisha inairudisha timu ya Taifa Stars kwa Watanzania na kazi hiyo imefanikiwa kwani hapo awali ilionekana kama vile haina mwenyewe na baada ya hapo ndipo likaja wazo la kutafuta watu mashuhuri.



"Kazi ya pili ilikuwa kuzungumza na vyombo vya habari kusaidia kuhamasisha. Jambo la tatu ni kuhamasisha kwenye maeneo yenye watu wengi kama baa, hoteli na vyombo vya usafiri ili nao wato ruhusa ya kujadili kwa mchezo wa Uganda na Tanzania kama sehemu ya kuhamasisha.Kazi ambayo imefanikiwa na wote tumeona,"amesema Makonda.



Amefafanua ushiriki wa makundi hayo ya kufanya kazi ya kuhamasisha, Uwanja wa Taifa ulizidiwa kwa idadi ya watu ambapo ametumia nafasi hiyo kuomba radhi kwa wote waliokuwa na tiketi zao lakini hawakuingia uwanjani na kwamba wamejifunza , hivyo watajipanga isitokee tena.



"Kwa namna ambavyo walijitokeza kwa wingi uwanjani maana yake Watanzania wanapenda mpira na michezo mingine yote. Tutaendelea kushauri ikiwemo ya tiketi kukatwa mapema na pale ambapo uwanja utakuwa umejaa basi watu wambiwe mapema,"amesema Makonda.



Pia amempongeza Kocha wa Taifa Stars kwa kupanga kikosi kizuri cha ushindi na kufafanua zawadi ya viwanja ambayo imetolewa na Rais Dk.John Magufuli wataweka uratatibu utakaosaidia hata wale wachezaji ambao walikuwemo kwenye ile michezo ya awali nao wanapewa.



"Kwa namna ambavyo Watanzania wamehamasisha na timu yetu ya Taifa, nina uhakika timu yoyote itakayokuja Uwanja wa Mkapa lazima itapigwa tu.Mashabiki ni mchezaji wa 12 na sasa tunao , hatuna wasiwasi na timu yetu,"amesema Makonda.


KAMATI ya Saidia Taifa Stars ishinde yenye wajumbe 14 wakiongozwa na Mwenyekiti wao Paul Makonda ikitoa shukrani kwa Watanzania wote kwa kufanikisha timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kushinda mechi yake dhidi ya Timu ya Taifa ya Uganda.


TUNAELEKEZA NGUVU KWA TIMU YA VIJANA KUELEKEA AFCON UNDER 17 , MECHI YA TWIGA STARS -MAKONDA

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda @baba_keagan amemkabidhi Kijana Ikuzi Kicheko muhamasishani Mzalendo Kitita cha Shilingi Milioni 1 Baada ya Kujitolea Kutembea Kwa Mguu Kutoka MANYARA Mpaka DAR Kuja Kuhamasisha Ushindi Kwa Taifa Stars,Lakini Pia Viongozi wa TFF Wameahidi Kumpatia Zawadi zaidi na Kwa Kuanzia Wamempa Nguo Zikiwemo Jezi Original za Taifa Stars na Mpira Ili akirudi Mkoani Manyara Watu Wasimshangae na Kumkataa Tena Njiani.
 
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KAMATI ya Saidia Taifa Stars ishinde imesema baada ya kufanikisha ushindi wa Taifa Stars sasa inaelekeza nguvu zake kuweke mikakati ya ushindi kwa Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 17 ya Serengeti Boys inayojiandaa kushiriki kushiriki mashindano ya AFCON Under 17.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda amesema kuna mashindano makubwa yanakuja ya AFCON Under 17 ambayo yatafanyika nchini Tanzania.

"Tunawaomba Watanzania tuendelee kushikamana na kuonesha umoja wetu kwa kuhakikisha timu yetu ya vijana inashinda michuano ya AFCON na kupata tiketi ya kwenda kushiriki kombe la Dunia la vijana linalotarajia kufanyika nchini Brazil.

"Tuna uhakika kwa umoja wetu na kwa mapenzi ya Mungu tutakwenda Brazil.Kikubwa ni kuwapa hamasa wachezaji wetu wa Seregeti Boys watafanya vema, katika mashindano ya AFCOM under 17 tunahitaji kushinda mechi mbili tu , tuna uhakika tutashinda na Kamati yetu imejipanga na tutaendelea kupeana taarifa kila kinachoendelea,"amesema Makonda.

Pia amesema kuwa Aprili 5, mwaka huu timu ya Taifa ya Wanawake 'Twiga Stars' nayo inacheza na ni jukumu la Watanzania kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri kwa kuinga mkono. "Tuna uhakika Taifa Stars itashinda katika mchezo wa Aprili 5, 2019 kwani katika Uwanja wa Mkapa yoyote atakayekuja atapigwa tu,'amesema Makonda.

Bodi ya Bonde la Wami/Ruvu:Vyanzo maji visimamiwe kwa vizazi vya sasa na vijavyo

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.

Bodi ya Bonde la Wami/Ruvu imesema kuwa vyanzo vya maji ni lazima visimamiwe kuhakikisha rasilimali hiyo ya maji inapatikana ya kutosha na inakuwa endelevu kwa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Huduma ya upatikanaji wa maji ambayo kupitia watoa huduma hiyo hususani mamlaka za maji, yanatokana na uhifadhi unaofanywa na Bodi za Maji za Mabonde (ambayo ni 9) yaliyopo nchini ambapo yanayotekeleza Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji Na. 11 ya Mwaka 2009.

Hayo yamezungumzwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Maji ya Bonde Wami/Ruvu Hamza Sadiki wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Warsha Maalumu kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa Usimamizi na Utunzaji wa Rasilimali za Maji iliyoandaliwa na Bodi.

Amesema Bodi hiyo ndio wasimamizi wa vyanzo vyote vya maji vilivyopo kwenye Bonde la Wami/Ruvu ambalo linapita kwenye mikoa 7 ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Dodoma, Manyara, Tanga na…hivyo ni lazima wasambazaji wote wa maji hayo wapate kibali kutoka bonde hilo.

Akisisitiza kuwa wananchi wengi wana uelewa mdogo kuhusiana na uhifadhi wa maji na kusababisha vyanzo hivyo kuingiliwa na shughuli mbalimbali za kibidamu zikiwemo uvuvi, kilimo pamoja na ufugaji.

“Vyanzo vya maji nchini chanzo kikuu ni mvua, hivyo kila mmoja akivuna maji ya mvua. Mwisho wa siku maji hayo yanayohifadhiwa chini ya ardhi na kutumika kama vyanzo vya chini na juu ya ardhi yatakosekana”, amesema Mwenyekiti.
Mwakilishi wa Afisa wa Maji wa Bonde la Wami\Ruvu Mshuda Wilson amesema kuwa visima vinavyochimbwa vinatakiwa kuwa na kibali kuendelea kumiliki kisima hicho ni kosa la kisheria.

Sheria inakataa uchafuzi wa mazingira na inapotokea mtu anachafua maji ikiwemo utiririshaji maji maji katika vyanzo vya maji yatakiwa kuipimwa na ndipo yaweze kurudishwa katika vyanzo hivyo. Amesema shughuli za kibidamu katika ndani ya mita 60 ya vyanzo ya maji zinazuiliwa kufanyika na kuwepo shughuli hizo ni kinyume cha sheria ya maji ya usimamizi wa rasilimali za maji. 

Amesema kuwa maji ya mvua nayo uvunaji wake unaangaliwa kwa kiwango endapo kiwango kitazidi zaidi lita 20,000 lazima uvunaji wa maji hayo yapate kibali.
Mwenyekiti wa Bodi ya Bonde la Wami/Ruvu Hamza Sadiki. Akizungumza na waandishi wa Habari wa akifungua warsha ya Bonde la Wami/Ruvu

 Mwakilishi wa Bodi ya Bonde la Wami/Ruvu Mshuda Wilson akitoa taarifa Bonde la wami/Ruvu katika warsha ya waandishi habari kuhusiana na uhifadhi wa vyanzo vya maji

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KUTOKA MKOA WA MBEYA

$
0
0
 Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia watu ishirini na moja [21] kwa tuhuma mbalimbali ikiwa ni pamoja na kufanya shughuli za uganga bila kibali.

KUPATIKANA NA MALI IDHANIWAYO YA WIZI.

Mnamo tarehe 23.03.2019 saa 14:39 mchana huko eneo na Kata ya Ilomba, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walimkamata JOSEPH MGAYA [27] Mkazi wa Ilomba akiwa na Pikipiki MC 395 BYN aina ya Kinglion ambayo mtuhumiwa amekiri kuiiba Pikipiki hiyo huko Kijiji cha Lupatingatinga Wilaya ya Chunya. Upelelezi wa shauri hili unaendelea na mara baada ya kukamilika mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.

KUFANYA SHUGHULI ZA UGANGA BILA KIBALI.

Mnamo tarehe 25.03.2019 saa 00:10 usiku huko katika Kitongoji cha Mapinduzi 'B' kilichopo katika Kijiji cha Idunda, Kata ya Itewe, Tarafa ya Tembela, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walimkamata PASCHAL PATRICE [30] Mkazi wa Kijiji cha Idunda na wenzake 19 wakifanya shughuli ya uganga bila kibali.

Watuhumiwa wote wakiwemo wanawake 03 walikutwa wakiwa kwenye nyumba ya mtu aliyefahamika kwa jina moja la MWARABU mkazi wa Dar es salaam. Pia katika nyumba hiyo wamekutwa watu watatu wote wanaume waliokuwa wamekwenda kutibiwa hapo. 

Upekuzi umefanywa ndani ya nyumba hiyo na kufanikiwa kupata begi ambalo ndani yake likiwa na kibuyu kimoja, chupa mbili za plastiki zenye unga unaodhaniwa kuwa ni dawa za kienyeji, kikopo cha plastiki cha njano chenye unga unaodhaniwa kuwa dawa za kienyeji zinazotumiwa na waganga kutolea tiba pamoja na ngoma moja. Upelelezi unaendelea.

  
KUSAFIRISHA BIDHAA NJE YA NCHI BILA KIBALI.

Mnamo tarehe 24.03.2019 saa 12:15 mchana huko Kitongoji cha Mwambuluko, Kijiji cha Isaki, Kata ya Katumbasongwe, Tarafa ya Unyakyusa, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa mbeya. Askari Polisi walikamata gari moja lenye namba T. 268 BNH aina ya Mitsubishi Fuso truck likiwa limebeba magunia yenye nafaka mahindi makavu yapatao magunia 88 mali ya mtu mmoja aitwaye DORIN KAONGA [35] Mmalawi, Mfanyabiashara na Mkazi wa Kalonga - Malawi na GLORY KAFWILA [32] Mmalawi, Mfanyabiashara na Mkazi wa Kalonga - Malawi.

Dereva wa gari hilo alikimbia kusikojulikana na msako mkali wa kumtafuta unaendelea. Gari hilo lilikua likielekea kivuko haramu cha Nyasa katika mto Songwe mpakani mwa nchi ya Tanzania na Malawi kwa ajili ya kuyavusha magunia hayo ya mahindi kwa mitumbwi kuelekea nchi hiyo jirani ya Malawi.

Gari hilo lililotumika kubeba magunia hayo ya mahindi ni mali ya mtu mmoja aitwaye SHABAN ADIL KAJUNI wa huko Wilaya ya Rungwe. Vielelezo gari hilo na magunia hayo ya mahindi vimekabidhiwa mamlaka ya mapato idara ya forodha Kasumulu na hatua zaidi za kisheria. Upelelezi unaendelea.

Imetolewa na:
 [ULRICH O. MATEI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA 
Vifaa vya Uganga vilivyokamatwa 
Kivuko haramu kinacjotumiwa na wafanyabiashara wasiokuwa waaminifu kupitisha bidhaa kwenda nje ya nchi. 
 Magunia ya Mahindi yaliyokamatwa yakisafirishwa kwenda nchi jirani ya Malawi bila kufuata utaratibu.
 Kibuyu na vifaa vingine vilivyokamatwa. 
 Gari aina ya FUSO lililokuwa likisafirisha magunia ya Mahindi kwenda nchini Malawi kwa njia ya magendo.

Wanakamati wa Afya kutunukiwa cheti cha Uzalendo Kijiji cha Kirando

$
0
0








Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (mwenye kapolo) akimsalimia mmoja wa mama waliojifungua katika kituo cha afya Kirando ambacho kimekamila upanuzi wake na kuanza kutumika (kushoto) Daktari mfawidhi wa Kituo hicho Dkt. hashim Mvogogo.

…………………………..

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi kuhakikisha anawapatia wanakamati ya upanuzi wa ujenzi wa kituo cha afya Kirando cheti cha uzalendo pamoja na kifuta jasho baada ya wanakamati hao kuonesha uvumilivu na kushirikiana na serikali katika upanuzi wa kituo hicho bila ya kudai posho ya aina yeyote.

Amesema kuwa pamoja na wanakamati wengine kukimbia kutokana na kukosa malipo ya aina yeyote wakati wakiendelea na usimamizi wa upanuzi wa kituo hicho cha Afya wao waliendelea kusimama imara ili kuhakikisha wanafanikisha zoezi hilo na hatimae wananchi wa Kijiji, Kata na Tarafa ya Kirando waweze kufaidika na juhudi za serikali ya awamu ya tano katika kuboresha sekta ya afya katika Mkoa wa Rukwa.

“Na mtayarishe Mkurugenzi cheti cha Uvumilivu, na mkono mtupu haurambwi mtayarishe na hata senti Fulani mle ndani iwe posho yao kwasababu hawajapata posho hata sumuni, kwahiyo muangalie mtajibana wapi ili cheti kiambatane na kifuta jasho tutakuwa tumewatendea haki na wengine wataiga,”Alisema.

Wakati akielezea siri ya kusimama imara Mwenyekiti wa kamati kituo cha afya Kirando ambae alikuwa mjumbe katika kamati ya ujenzi kwaajili ya upanuzi wa kituo hicho Seetbert Kapalata alisema kuwa anamshukuru mheshimiwa Rais kwa kuwafikiria watu wa Kijiji cha kirando na kuwapelekea mradi huo.

“Kweli tunamsukuru mheshimiwa Rais kwani ni jambo la kipekee sana ilikuwa sio rahisi kufikiria kwamba tunaweza kuapata kitu kama hiki miaka imepita mingi lakini hatujapata jambo kama hili kwahiyo ilikuwa ni lazi sisi tuunge mkono jitihada hizo, inawezekana akaja mwingine asifikieriea vituo vya afya akafikiria mambo mengine lakini bila ya afya hakuna kingine katika maisha,” Alisema.

Kwa upande wake Mganga mfawidhi wa Kituo hicho ambae nae alikuwa katibu wa Kamati Dkt. Hashim Mvogogo wakati akitoa taarifa ya Kituo hicho cha afya alisema kuwa upanuzi huo umesaidia kuboresha huduma za upasuaji na maabara, jengo la wodi ya wajawazito pamoja na nyumba ya daktarin.

“Wodi ya akinamama imeboreshwa na hadi sasa jengo hilo lina uwezo wa kulaza kina mama 25 kwa wakati mmoja, vilevile chumba cha kujifungulia kina uwezo wa kubeba wajawazito wanne kwa wakati mmoja, hivyo tunaishukuru serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Wetu Dkt. John Pombe Magufuli kwa namna alivyoweza kutuboreshea huduma katika kituo chetu,” Alimaliza.

Ujenzi wa Upanuzi wa Kituo cha Afya cha Kirando ulianza mwezi Februari mwaka 2018 na kumalizika mwezo Oktoba mwaka 2018 na kugharimu shilingi milioni 412 kwaajili ya ujenzi wa jengo la maabara, wodi ya wajawazito, jengo la upasuaji na nyumba ya daktari.

RAIS MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA (TAA)


IFM KUJENGA TAWI JIPYA SIMIYU

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kulia) akizungumza na baadhi ya viongozi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), walipomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi, kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (kushoto) akizungumza Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta alipomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi, kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne A. Sagini (wa pili kushoto) akifurahia jambo na Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta( wa tatu kushoto) na watumishi wengine wa chuo hicho walimpomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi, kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati), baadhi ya watumishi wa Mkoa wa Simiyu (watatu wa mwanzo kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta( wa tano kulia) na watumishi wengine wa chuo hicho walimpomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi, kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.

Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta(kulia) akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka walimpomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi , kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (wa pili kushoto), akizungumza na Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta( wa tatu kushoto) na watumishi wengine wa chuo hicho walimpomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea na kuona eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi, kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.
Mwenyekiti wa RAAWU Taifa, Dkt. Micahel Mawondo akizungumza jambo wakati Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta( wa tatu kushoto) na watumishi wengine wa chuo hicho walimpomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(kushoto) ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea na kuona eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi , kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne A. Sagini (katikati), baadhi ya watumishi wa Mkoa wa Simiyu (watatu wa mwanzo kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Satta( wa tatu kulia mbele) na watumishi wengine wa chuo hicho walimpomtembelea ofisini kwake Machi 26, 2019 mara baada ya kutembelea na kuona eneo lililotolewa bure na Mkoa wa Simiyu katika Kata ya Sapiwi wilayani Bariadi, kwa ajili ya ujenzi wa Tawi la Chuo hicho mkoani hapa.
.

Na Stella Kalinga, Simiyu

Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kinatarajia kujenga Tawi jipya katika Kata ya Sapiwi Tarafa ya Dutwa wilayani Bariadi Mkoani Simiyu.

Viongozi wa chuo hicho wakiongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Tadeo Andrew Satta wametembelea eneo hilo Machi 26, 2019 na baadaye kufanya mazungumzo na viongozi wakuu wa Mkoa wa Simiyu ambapo wamekubaliana kushirikiana katika hatua zote kuanzia upimaji wa eneo mpaka ujenzi wa majengo ya chuo.

Akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Makamu Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Prof. Tadeo Andrew Satta amewashukuru viongozi hao kwa kutoa eneo la ekari ishirini bure akaahidi kushirikiana na Serikali mkoani hapa kuhakikisha tawi hilo linajengwa mkoani Simiyu ili kusogeza karibu huduma kwa wananchi wa Simiyu.

Awali akizungumza na viongozi hao Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Serikali mkoani humo iko tayari kushirikiana na viongozi wa Chuo hicho kwa kutoa wataalam watakaosaidia katika Usimamizi wa upimaji na akashauri ujenzi wa majengo ya chuo hicho ufanyike kwa kutumia mfumo wa ‘Force Account’ ili kupunguza gharama.

Amesema mfumo huu utapunguza gharama kwa kuwa hautumii wakandarasi badala yake ujenzi utafanywa na mafundi wa kawaida wakisimamiwa na wahandisi wa ujenzi Mkoa na Halmashauri mkoani Simiyu huku vifaa vyote vya ujenzi vikinunuliwa kwa pamoja na chuo hicho.

Aidha, amemhakikishia upatikanaji wa wanafunzi kwa kuwa hadi sasa Mkoa wa Simiyu bado una Vyuo vichache vya elimu ya juu, huku akibainisha kuwa tayari Serikali mkoani hapa imeshatoa ardhi bure kwa ajili ujenzi wa Matawi ya Vyuo mbalimbali vya elimu ya juu ikiwemo Chuo cha Mipango, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania na Chuo cha Mahakama.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema wanaendelea kushawishi Taasisi nyingi za Elimu ya Juu kujenga matawi yake Mkoani hapa, ili kutoa nafasi kwa Wanasimiyu kupata elimu ya juu itakayochangia kuleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi na kijamii

Dkt. Kalemani akagua REA III wilayani Kasulu, Buhigwe na Kigoma Vijijini

$
0
0
Na Teresia Mhagama, Kigoma
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Kasulu, Kigoma Vijijini na Buhigwe mkoani Kigoma kwa lengo la kukagua mradi wa usambazaji umeme vijijini wa Awamu ya Tatu (REA III) ambapo pia aliwasha umeme katika baadhi ya Vijiji.

Akiwa wilayani Kasulu, Dkt Kalemani alikagua kazi zinazofanywa na mkandarasi katika Kijiji cha Ruhita ambapo alikuta Kijiji hicho bado hakijaunganishwa umeme na kumuagiza Mkandarasi, kampuni ya CCCE Etern kufikisha umeme kijijini hapo baada ya siku 15.

Aidha, alimtaka Meneja wa TANESCO, Wilaya ya Kasulu kuhakikisha kuwa, anasimamia suala ya uchoraji wa ramani za kuingiza umeme ndani ya nyumba za wananchi kwani kuna baadhi ya watu binafsi wanaofanya kazi hizo wamekuwa wakiwatoza wananchi gharama kubwa bila kujali tofauti ya ukubwa au udogo wa kazi.

Vilevile, Dkt Kalemani alimtaka Meneja huyo kuhakikisha kuwa watu wanaofanya kazi za kufunga nyaya za umeme ndani ya nyumba za wananchi wanatambulika na TANESCO ili kuepusha utapeli na kufanya kazi chini ya viwango vinavyotakiwa.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Simon Anange alimweleza Dkt Kalemani kuwa, wananchi wa Kijiji hicho wamesubiri umeme kwa muda mrefu baada ya kupata ahadi ya kupelekewa nishati hiyo, hivyo wanaomba Mkandarasi akamilishe kazi hiyo mapema ili waweze kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo za kiuchumi.

Akizungumzia suala hilo, Dkt Kalemani alisema kuwa, Mkandarasi ambaye ni kampuni ya CCCE Etern ameanza kazi mwezi Januari mwaka huu tofauti na wanandarasi wa umeme katika maeneo mengine nchini ambao walianza kazi mwaka jana, hii ni kwa sababu ya masuala ya kisheria yaliyojitokeza hapo awali lakini sasa Mkandarasi huyo anaendelea na kazi.

Akiwa wilayani Buhigwe, Dkt Kalemani alikagua miundombinu ya umeme katika Kijiji cha Bulimanyi ambacho tayari kimeshafikishiwa umeme na kaya zaidi ya Kumi zimeshaunganishwa na nishati hiyo na kumuagiza Mkandarasi kupeleka umeme katika Vijiji vyote vya Wilaya hiyo.

Dkt. Kalemani pia alikagua miundombinu ya umeme katika Kijiji cha Mkigo wilayani Kigoma Vijijini, ambapo pamoja na kuzungumza na wananchi, aliwasha umeme katika Kijiji hicho.
 Moja Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Mpigo wilayani Kigoma Vijijini mkoa wa Kigoma kabla ya kuwasha umeme katika Kijiji hicho.
Wananchi katika Kijiji cha Bulimanyi wilayani Buhigwe, Mkoa wa Kigoma wakimsikiliza Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani (hayupo pichani) wakati alipofika kijijini hapo kukagua miundombinu ya usambazaji umeme.

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MKURUGENZI MTENDAJI WA BENKI YA NBC

$
0
0

1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi (kushoto) ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam
6
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi, Afisa  Masoko wa NBC Bi. Neenarose Singo pamoja na Meneja wa Mahusiano na Serikali Ndugu William Kallaghe (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam.
8
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja  na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi (kushoto) mara baada ya mazungumzo ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

………………………….

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 26, Machi 2019 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Ndugu Theobald Maingu Sabi ofisini kwake Ikulu, jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo amefika ofisini kwa Makamu wa Rais kwa lengo la kujitambulisha akiwa ameongozana na Meneja mahusiano na Serikali Bw. William Kalaghe pamoja na Afisa Masoko wa NBC Bi. Neemarose Singo.

SERIKALI YA MAREKANI KUFADHILI MAFUNZO YA KILIMO KINACHOENDANA NA HALI YA HEWA KWA WATUMISHI WA SERIKALI ZA MITAA NCHINI TANZANIA

$
0
0

Morogoro.

Viongozi na wadau kutoka baadhi ya mikoa na wilaya nchini Tanzania wamekutana Morogoro, Machi 25-29, kwa mafunzo ya Serikali yaliyofadhiliwa na Serikali ya Marekani kuhusu namna ya kupanga mikakati na kusaidia wakulima wadogo ili waweze kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kutekeleza kilimo kinachoendana na hali ya hewa. Mafunzo kama haya yatafanyika Unguja, Zanzibar, Aprili 1-5.

Programu ya mafunzo, “Landscape Climate-Smart Agriculture Pilot Course,” inafanywa na timu ya wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha California, Davis; Idara ya Kilimo ya Marekani (USDA); Chuo kikuu cha Cornell; kampuni ya EcoAgriculture; na Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo (IITA) na fedha kutoka Serikali ya Marekani kupitia Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID).

Mafunzo haya ni sehemu ya Mradi wa kujenga uwezo wa upatikanaji wa Chakula, ambao ni mpango wa Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na USDA na USAID. Mradi huu unaainisha mapungufu ya uwezo wa kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabia nchi yanayoathiri kilimo. Mradi huu unatekelezwa na IITA, FAO, na World Agroforestry Center.

Kilimo kinachoendana na hali ya hewa kinafafanuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) kama kilimo ambacho huongeza uzalishaji wa chakula na mapato ya wakulima, hupunguza uzalishaji wa gesi zinazochangia ongezeko la joto, na hukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi. Mbinu hii inasaidia sekta ya kilimo kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na athari zake kwenye hali ya hewa kama ukame, mvua finyu na mafuriko, pamoja na kukidhi ongezeko la mahitaji ya chakula.

Ili kuomba taarifa zaidi, tafadhali piga simu Ofisi ya Habari ya Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam kupitia: +255 22 229-4000 au barua pepe: DPO@state.gov.

BITEKO AFANYA MAZUNGUMZO NA KAMPUNI KUTOKA MAREKANI

$
0
0

Waziri wa Madini Doto Biteko akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya PRNG Minerals Ltd kutoka Marekani Rocky Smith kushoto kwa Waziri. Smith alimtembelea Waziri ofisini kwake jijini Dodoma kwa mazungumzo akiwa ameambatana na Mkurungenzi wa Maendeleo wa Kampuni hiyo Lucas Stanfield wa kwanza kulia, na wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa huduma za sheria Wizara ya Madini Edwin Igenge.
Waziri wa Madini Doto Biteko akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya PRNG Minerals Ltd kutoka Marekani Rocky Smith kushoto kwa Waziri. Smith alimtembelea Waziri ofisini kwake jijini Dodoma kwa mazungumzo, wa kwanza kushoto ni Ali Ali, Kamishna Msaidizi Uendelezaji Migodi na Madini Wizara ya Madini, anaefuatia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria Wizara ya Madini Edwin Igenge.

……………………..

Waziri wa Madini Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya PRNG Minerals Ltd, ya Marekani, Rocky Smith na Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni hiyo Lucas Stanfield ofisini kwake Jijini Dodoma.

Watendaji hao wapo nchini kwa ziara ya kawaida ya kikazi ya siku tano ambapo waliomba kukutana na Waziri wa Madini.

Pamoja na mambo mengine, kampuni hiyo inakusudia kuwasilisha taarifa juu ya hali na Maendeleo ya soko la dunia kwa Madini ya Rare Earth Elements na kuzungumzia hatua iliyofikiwa kwa ombi la leseni ya uchimbaji Mkubwa wa madini hayo.

Akizungumza katika kikao hicho, Waziri Biteko amesema wizara iko tayari kuipokea kampuni husika nchini baada ya kukamilika kwa taratibu kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu Rocky Smith, amesema kuwa, amefurahishwa na ushirikiano unaooneshwa na wizara na kuahidi kuanza shughuli za uchimbaji mara baada ya kukamilika kwa taratibu.

SPIKA JOB NDUGAI ATEMBELEA OFISI YA CCM MKOA WA KASKAZINI UNGUJA MJINI ZANZIBAR

$
0
0

Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe. Job Ndugai (kulia) akigawa kadi kwa mwanachama mpya wa Umoja wa Vijana CCM wakati wa zoezi la kugawa kadi kwa wanachama wapya wa CCM tukio lililofanyika jana Machi 26, 2019 Jimbo la Kiwengwa Muembe Majogoo Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar. (PICHA NA OFISI YA BUNGE)
Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe. Job Ndugai akiweka jiwe la msingi Tawi la CCM Muembe Majogoo kabla ya kuzungumza na viongozi wa Matawi, Wadi na Jimbo jana Machi  26 , 2019 katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar.
Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Job Ndugai (kulia)akisalimiana na Mwakilishi wa Jimbo la Chaani, Ndg. Nadir Abdulatif wakati alipowasili na kuzungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja na Wajumbe wa Baraza Kuu ya Jumuiya za Chama Mkoa na Wilaya zake katika kikao kilichofanyika jana Machi  26 , 2019  katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar. 
Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe. Job Ndugai akicheza Ngoma za Utamaduni wa Watu wa Mkoa wa Unguja wakati akikagua Ngoma hizo katika Ofisi ya CCM Mkoa wa kaskazini Unguja tukio lililotokea jana Machi  26 , 2019  katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar. 
Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe. Job Ndugai akizungumza na Viongozi wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja na Wajumbe wa Baraza Kuu ya Jumuiya za Chama Mkoa na Wilaya zake alipowatembelea jana Machi  26 , 2019 katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar. 
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kaskazini na Kusini Unguja, Wajumbe wa Baraza Kuu ya Jumuiya za Chama Mkoa na Wilaya zake wakimsikiliza Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe. Job Ndugai (hayupo kwenye picha) katika kikao kilichofanyika jana Machi  26 , 2019  katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar. 
Spika wa Bunge, Mlezi wa CCM Mkoa wa Kusini na Kaskazini Unguja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Mhe. Job Ndugai (kulia)akimsikiliza Mwakilishi wa Jimbo la Chaani, Ndg. Nadir Abdulatif akielezea changamoto mbali mbali ambazo wanakumbana nazo Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja na Wajumbe wa Baraza Kuu ya Jumuiya za Chama Mkoa na Wilaya zake katika kikao kilichofanyika jana Machi  26 , 2019  katika Ofisi za CCM Mkoa wa Kaskazini Unguja Mjini Zanzibar.

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YAPITISHA BAJETI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI, YAPONGEZA VYOMBO VYOTE VYA ULINZI NA USALAMA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola wa kwanza kushoto akitoa maelekezo kwa Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kabla Watendaji hao hawajaingia kwenye Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kilichoketi leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma leo, ili kupitia utekelezaji wa Mpango wa Bajeti kwa mwaka 2018/2019 na Makadirio ya Mapato, Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. Katikati ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Jacob Kingu, akifuatiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo Wanja Mtawazo. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Katibu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje , Ulinzi na Usalama, Ramadhani Abdallah wa kwanza kulia akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola wa kwanza kushoto pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Jacob Kingu katikati, muda mfupi baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kupitisha Makadirio ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola wa kwanza kushoto akizungumza na watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pichani baada ya kumalizika kwa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kilichoketi leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mjini Dodoma, ili kupitia Utekelezaji wa Mpango wa Bajeti kwa mwaka 2018/2019 na Makadirio ya Mapato, Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2019/2020. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, wa pili kulia, akifuatiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, wa kwanza kulia, pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo wakimsikiliza kwa makini, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola wa kwanza kushoto wakati akiwapa maelekezo mbalimbali baada ya kumalizika kwa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kilichoketi leo katika ukumbi wa Mikutano wa Bunge la Mjini Dodoma na kupitisha Makadirio ya Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2019/2020. (Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola, wa pili kushoto akiwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Hamadi Masauni, wa kwanza kushoto, Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, Faustine Kasike wa pili kulia na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Makakala wa kwanza kulia, wakielekea katika Ofisi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma, kwa lengo la kushiriki katika Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kilichoketi leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mjini Dodoma ili kupitia utekelezaji wa Mpango wa Bajeti kwa mwaka 2018/2019 na Makadirio ya Mapato, Matumizi ya kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ya Wizara hiyo. (Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi).

BARAZA LA KILIMO LAKUTANA KUJADILI MPANGO MKAKATI WA ACT KWA MWAKA 2019/2013.

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi (mwenye gauni la kitenge)  kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la kilimo Bi Janet Bitegeko wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wengine  baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili mpango mkakati wa ACT kwa mwaka 2019 hadi 2023, kikao hicho kilifanyika Machi 26,2019 Jijini Dar es salaam.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akiongoza kikao cha bodi hiyo kilichofanyika katika Ofisi za Baraza la Kilimo Machi 27,2019  Jiji Dar es Salaam.
 Sehemu ya wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania wakifuatilia kwa umakini agenda za kikao hicho cha kawaida cha siku moja kilichofanyika katika Ofisi za Baraza la kilimo, Machi 27, 2019  Jiji Dar es Salaam.
 Mratibu Taifa wa Ubia wa Kilimo Tanzania Bw Mark Magila, Bw. Omary Mwaimu Mjumbe wa bodi ya wakurugenzi na wajumbe wengine wakifuatilia kikao hicho cha Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akiongoza kikao cha bodi hiyo, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Bi Janet Bitegeko, kikao hicho cha siku moja kimefanyika  katika Ofisi za Baraza la Kilimo Machi 27,2019  Jiji Dar es Salaam.

BI JACQUELINE MKINDI AONGOZA KIKAO CHA BODI YA WAKURUGENZI WA BARAZA LA KILIMO

$
0
0
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akiongoza kikao cha bodi hiyo kilichofanyika katika Ofisi za Baraza la Kilimo Machi 27,2019  Jiji Dar es Salaam.
 Sehemu ya wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania wakifuatilia kwa umakini agenda za kikao hicho cha kawaida cha siku moja kilichofanyika katika Ofisi za Baraza la kilimo, Machi 27, 2019  Jiji Dar es Salaam.
 Mratibu Taifa wa Ubia wa Kilimo Tanzania Bw Mark Magila, Bw. Omary Mwaimu Mjumbe wa bodi ya wakurugenzi na wajumbe wengine wakifuatilia kikao hicho cha Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akiongoza kikao cha bodi hiyo, kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Bi Janet Bitegeko, kikao hicho cha siku moja kimefanyika  katika Ofisi za Baraza la Kilimo Machi 27,2019  Jiji Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi (mwenye gauni la kitenge)  kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la kilimo Bi Janet Bitegeko wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wengine  baada ya kumalizika kwa kikao cha kujadili mpango mkakati wa ACT kwa mwaka 2019 hadi 2023, kikao hicho kilifanyika Machi 26,2019 Jijini Dar es salaam..

Vodacom yazindua huduma mpya ya kurahisisha biashara inayoendana na mabadiliko ya kidijitali

$
0
0

 Hisham Hendi, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Vodacom, akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitengo maalum kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya wateja wanaofanya biashara kuanzia makampuni  madogo-ofisi ndogo za nyumbani(Soho), wafanyabiashara wa kati (SMEs) na makampuni makubwa jana jijini Dar es salaam. 
Hisham Hendi, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Vodacom, na Arjun Dhillon, Mkurugenzi wa Kitengo maalum cha Biashara wakizungumza wakati wa uzinduzi wa kitengo hicho maalum kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya wateja wanaofanya biashara kuanzia makampuni madogo-ofisi ndogo za nyumbani(Soho), wafanyabiashara wa kati (SMEs) na makampuni makubwa jana jijini Dar es salaam. 
Farid Seif (wa pili kushoto) na timu ya kitengo cha biashara wakimsikiliza moja kati ya wateja wao aliehudhuria uzinduzi wa kitengo hicho maalum kwa ajili ya kushughulikia mahitaji ya wateja wanaofanya biashara kuanzia makampuni madogo-ofisi ndogo za nyumbani(Soho), wafanyabiashara wa kati (SMEs) na makampuni makubwa jana jijini Dar es salaam.

 Katika jitihada za kuhakikisha biashara zinaenda sambamba na mabadiliko ya masoko ya kisasa, kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania PLC, leo imezindua kitengo kwa ajili ya kushughulikia huduma zinazoenda sambamba na mahitaji ya wateja wake wanaofanya biashara kuanzia makampuni madogo-Ofisi ndogo za nyumbani (Soho's), Wafanyabiashara wa kati (SMEs) na Makampuni makubwa. 

Lengo kuu la huduma hii ni kuwawezesha kufanya biashara kwa ufanisi zaidi, kuhimili ushindani, kujenga mtandao wa kibiashara na kuwawezesha kupata huduma zote za kurahisha biashara zao bila kuhangaika na masuala yaliyo nje ya biashara zao za msingi.

“Ulimwenguni kote kumetokea mabadiliko ya njia za kufanya biashara kutoka njia za zamani kwenda njia za kidijitali, kutumia mitandao na teknolojia za kisasa kama cloud ,tunatarajia wateja wetu kwenda sambamba na mabadiliko haya ili kufanya biashara zao kwa ufanisi na kuhimili ushindani katika masoko nasi tunaamini ni wabia wao muhimu katika kuleta ufumbuzi wa kufanikisha biashara zao”, alisema Hisham Hendi, Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania PLC.

Makampuni makubwa kama mabenki na sekta ya umma yanatafuta ufumbuzi wa ubunifu ambao utarahisisha shughuli za uendeshaji, kuhimili ushindani na kuhakikisha mali zake ziko salama. Vodacom Tanzania PLC kampuni kinara inayoongoza kutoa huduma za ubunifu wa kidijitali inawezesha kupata huduma za utambuzi wa maeneo, huduma za kompyuta kutumia teknolojia ya kisasa ya Cloud, data MPLS, huduma za simu ambazo mpigaji hatotozwa gharama za kupiga simu na biashara kutumia M-Pesa ili kuwezesha makampuni makubwa kufanya kazi kwa tija na ufanisi.

Msukumo wa kuifanya Tanzania kuwa nchi ya Viwanda umepelekea kuanzishwa kwa biashara ndogo na za kati ambazo uendeshaji wake kwa ufanisi unahitaji huduma za ubunifu wa kiteknolojia za kisasa ili kuzipunguzia gharama za uendeshaji

"Vodacom inayo dhamira ya kufanikisha ukuaji wa biashara nchini Tanzania kupitia ubunifu wake wa huduma za teknolojia ya kidijitali za kuwarahisishia wafanyabiashara kufanikisha malengo yao na kujiandaa kwa siku zijazo na ndio maana tumewaletea huduma hizi” alisema Bw, Hendi.

Biashara zenye ukubwa wa kati kama asasi zisizo za Kiserikali (NGO’s) ambazo zimejipanga kuendesha shughuli zake kwa njia za kisasa na ambazo zinatoa kipaumbele kutumia teknolojia za kisasa yatafaidika na huduma kama IoT (Internet of Things) , SIM Manager na utumaji wa ujumbe wa maneno kwa watu wengi kwa wakati mmoja (bulk SMS).

Kwa upande wa biashara ndogo na Ofisi ndogo za nyumbani (Soho's) zitanufaika kwa kubana matumizi na kujenga mtandao wa biashara kupitia huduma ya M-Pesa, huduma za kurahisisha biashara na utumaji wa ujumbe wa maneno kwa watu wengi kwa pamoja wataweza kubadilisha biashara zao na kuzifanya kukua zaidi.

Kupitia ubunifu huu mkubwa ambao unabadilisha mbinu za kufanya biashara, Vodacom Business imeonyesha dhamira kuwa ni mbia katika kuleta teknolojia zinazorahisisha biashara na kuwezesha kuhimili ushindani, huku wakiongeza ufanisi na kuwezesha kujenga mtandao katika uendeshaji.

“Sisi ni kampuni ya huduma za simu inayotoa huduma kupitia ubunifu wa kiteknolojia zinazoweza kurahisisha biashara, shughuli za viwanda na kuleta mabadiliko “alimazia kusema Bw. Hendi.

MAKAMU WA RAIS AZINDUA KONGAMANO LA 7 LA AFYA NA SAYANSI AFRIKA MASHARIKI

$
0
0

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasha mwenge kama ishara ya ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

6
Sehemu ya Wataalamu waliohudhuria ufunguzi wa  Kongamano la 7 la Afya na Sayansi la Afrika Mashariki lililofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).



=====  ===============  ===============


SPEECH BY H.E. SAMIA SULUHU HASSAN, VICE PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA  AT THE OFFICIAL OPENING OF THE  7TH EAST AFRICAN HEALTH AND SCIENTIFIC CONFERENCE, HELD AT JULIUS NYERERE INTERNATIONAL CONVENTION CENTER (JNICC)
DAR ES SALAAM, THE 27TH MARCH 2019

·       Hon. Chairperson of the EAC Council of Ministers and Minister of Foreign Affairs and International Cooperation, Republic of Rwanda;
·       Hon. Chairperson of the EAC Sectoral Council of Ministers of Health and Minister of Health, Republic of Rwanda;
·       Honourable Ministers of Health from the EAC Partner States;
·       Honorable Ministers;
·       Amb. Liberat Mfumukeko, Secretary-General of the East African Community;
·       Honourable Members of Parliament from the East African Legislative Assembly and National Assemblies of the EAC Partner States;
·       Permanent Secretaries of EAC Partner States;
·       Members of the Diplomatic Community;
·       Professor Gibson Kibiki, Executive Secretary of the East African Health Research Commission;
·       Representatives of Development Partners;
·       Researchers, Scientists and Practitioners;
·       Conference Participants;
·       Members of the Press;
·       Distinguished Guests;
·       Ladies and Gentlemen;
A very goodmorning to you all.

At the outset, allow me to express my profound gratitude and appreciation to the organizers for inviting me to such an auspicious occasion of the 7thEast African Health and Scientific Conference. We are all aware that no country/region can achieve meaningful and sustained economic growth without advancement in Digital technologies especially in the critical health sector.
In this regard I wish to commend the organizers for holding this biennial conferences successfully and consistently over the past years. The interest of the region’s health researchers and scientists in discussing the gains and setbacks in Health Sector and the role of Science and Technologies in developing the sector is clearly reflected in the extensive preparatory work that has gone into the conference, and at the range of expertise gathered here today.
I am witnessing firsthand the enthusiasm of this community to drive efforts to promoterapid technological and digital transformation to support the implementation of health sector interventions and programmes. This is surely a step in the right direction towards the attainment of SDG 3 and universal health coverage and am in full support of this.
We are grateful that you chose Tanzania as the venue.  Indeed we are extremely privileged to host you. Let me take this opportunity to welcome you all, I trust that the organizers have  done  everything  within  their means to make you feel at home KARIBUNI SANA TANZANIA.

Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates;
Investing in Health Sector and relevant digital technologies is key for our development that we need to pursue more aggressively as a region.  I am pleased with the region’s continued efforts towards operationalizing the EAC Treaty, particularly Article 118 that calls for collaboration in Health Sector as well as other relevant provisions of the EAC Common Market Protocol.

I am delighted to see that this conference is not only graced by Scientists coming from EAC but also brings together participants and delegates from all over Africa and beyond the Continent.I have no doubt thatyou will find the selected topics interesting and enriching. I believe this conference will provide you with yet another opportunity to exchange information on current development and deployment of potential approaches to scaling up innovative technologies that will accelerate the attainment  of the SDGs

Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates;
Science and technology is an important and vital tool in addressing fundamental gaps in the health sector. I wish to commend the organizers for the timely and relevant selection of the theme, “Technology for health systems transformation and attainment of the UN-Sustainable Development Goals”. This theme comes atan opportune moment as the world is in its fourth industrial revolution where science and technology is taking the lead in all aspects.
You will all agree with me that sustainable development is elusive if we do not invest in fit-for-purpose technologies in order to help our countries to generate answers and solutions to many public health problems and challenges.
I wish to underscore that the need to invest in Digital Health Technology cannot be understated if we are to fully implement the Sustainable Development Goals and address all aspects of poverty.We can no longer ignore the direct correlation of poverty and social vulnerability in aggravating poor health. Therefore, in order to address these vulnerabilities we need to invest inDigital Health Technology as a way of strengthening regional healthcare services.


We in Tanzania have been able to identify that and we have already embarked in digitizing our healthcare system through our Ministry of Health and the several agencies under them such as the MSD ( whereby the digitized technology helps us in tracking the consignement from purchase point to delivery point), the NHIF (management of the client membership, claim and contribution) and the TFDA (online reporting of import and exports under TFDA and online reporting of the adverse effects of the use of medicine and cosmetics) . In addition to what is happening at our Agencies level we have installed Hospital Management System in all Government Hospitals. This system gives real time data and you can track the movement of the patient and the medicine stock.

We have recorded positive impact of our healthcare sector since we embarked on digitizing our sytems. A number of gains have be made which among other things include;
         i.          Improved quality of healthcare services – For instance; having EMR in place, improved availability of patient history (medical records), enhance continuity of care, Today No Record Loss, Appointments are made by the Doctors right away, improved medication etc.
       ii.          Improved efficiency and time saving
     iii.          Availability of real- time data for better decision making
     iv.          Improved resource (health commodities, HRH) tracking and allocation based on the demand
      v.          Improved accountability (internally and externally)
     vi.          Improved data security, privacy, confidentiality, transparency and internal controls.
One of the gains that is dear to me is the  Reduced post-natal mortality rate through telemedicine e.g. Digital Village located in Ngorongoro – Ololosokwan.

Our challenges still remain in having adequate manpower to support these ICT initiatives and funds to train  new manpower and come up with new initiatives. I believe the discussions you will have today will share on your best practises and how you can cooperate with each other in scaling up digitized transformation in the region’s healthcare sector




Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates
Am made  aware that today, in addition to the East African Health and Scientific Conference, the East African Health Research Commission Commission has established new platforms meant to share research findings in the region, to build research capacity and to create a better environment for research on health matters. Allow me to mention a few of them:
1.     The Commission has developed a new concept note of the conference, approved by the 15th Sectoral Council of Ministers of Health, which makes the conference a biennial event instead of being an annual one as it was before. This gives time to implement the recommendations of the conference and to prepare for the next one.
2.     The Commission has established an official comprehensive compendium of health information in East Africa, which is a One-Stop Center for Health Information. It is operational through a web portal (www.eahealth.org), which will be launched during this ceremony.
3.     The Commission operationalized two (2) scientific Journals that are contributing to share with the global scientific community the scientific work part of the EAC region;
4.     The Commission established the Young East African Health Research Scientists’ (YEARS’) Forum which is an initiative aiming to empower East African Community (EAC) young researchers to be able to shape the future of research for health in the region; this initiative was approved by the 15th EAC Council of Ministers; YEARS’ Forum will also launched during this ceremony.
5.     The Commission initiated a number of other regional programs and projects that are running.

I therefore, take this opportunity to congratulate all members of the Commission from Partner States and the East African Health Research Commission Secretariat for these tremendous achievements and encourage them to keep up the speed and the commitment.
Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates;
The approval of the Digital Regional East African Community Health (Digital REACH) 10 years strategic plan by the Sectoral Council of Ministers of Health held in Kigali on 26thOctober 2018 is an important step  towards achieving transformation in the sector.  

I expect that Digital REACH will support the development and implementation of regional health programme, within existing EAC Regional policies and legal frameworks as provided by the Treaty Establishing the East African Community and as desired by each of the EAC Partner States.

I am informed that this initiative will build infrastructure and other digital health assets that can be used directly, by each country, for their own national programme implementations. It has been developed based on collaboration and inputs from representatives of the EAC Partners and is supported by respective Organs of the EAC.

However,  effective implementation of this regional initiative depends not only on  good coordination from the East African Health Research Commission but also on strong commitments of EAC partners States, Development Partners and every Health Sector Stakeholder in Partner States. I take this opportunity therefore to call upon our Development Partnersto continue their support to the East African Health Research Commission, and Partner States to implement and coordinate this initiative.

Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates;
As we discuss the above mentioned revolutionary and innovative initiative we must strive to put up  mechanisms that support and accelerate its implementation in the Health Sector. I am informed that all EAC Partner States are now implementing digital health initiatives that need to be supported. We should not forget however, that for effective integration of the EAC partner states they need to be regionally interoperable.

Digital health is proved as one of the enablers of Sustainable Development Goals in developed countries and a lot of pilot projects all over the world are confirming the same to be the case in low- and middle-income country settings.Digital solutions are used to strengthen all the core building blocks of health systems which are: service delivery; health workforce; health information systems; access to essential medicines;financing; and leadership/governance.

I therefore encourage Partner States to support the new development in EAC partner states and call upon them to work together through Digital Health Technology and I reiterate the commitment of the United Republic of Tanzania to take advantage of Digital Health technology to improve implementation of health sector interventions, with the aim of accelerating attainment of the Universal Health Coverage and SDGs.

Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates;
We realize however that, digital healthcare initiatives to achieve the SDGs have inherent challenges that go beyond the implementation of technology.These  challenges include among others the need for a trained workforce skilled in using digital health solutions and the need for proper governance and funding, among others.

To overcome these barriers, we need to take an interdisciplinary and inter-sectoral approach, bringing together all the main actors in the digital health ecosystem such as international organizations, health service institutions, academia, research centers, and public and private industry.

We need to align our digital health approaches and solutions with the specific needs of the country’s health system and the region. We need to define and implement digital health strategic plans which consider governance mechanisms in digital health.  Our national strategies and policies need to be developed and aligned together to ensure inter-sectoral cooperation.

Therefore, our Academia and research centers and institutions are expected to continuously develop and produce primary evidence that helps decision makers identify the best, most cost-effective solutions from the wide range of options available in digital health.

The public and private industry, which is revolutionizing the digital health sector, should consider national and regional health realities and priorities, and offer sustainable needs-oriented solutions in specific sociocultural and social health realities in line with resources available in the context.

This underlines the urgency of supporting the Digital REACH Initiative which is designed to complement, improve, and strengthen EAC Partner States specific work in digital health. Let us not lose this opportunity to boost the attainment of SDGs for our Community.

As for our experts gathered here today, the Community expects from you concrete, simple and cost effective actions, with high impact that EAC Partner States can undertake at national level or collectively at regional level.

Chairperson, Hon. Ministers, Distinguished Delegates;
Before I conclude my Remarks, let me once again welcome you all to Tanzania and thank Hon Ministers of Health from our Region and Your Country delegations for having decided to stay and attend this Conference after you concluded the Meeting of the EAC Sectoral Council on Health, which just ended on 26th of March 2019 in Dar es salaam. This is a testimony of how you value East African Cooperation in Health, Research and Science.

My appreciation would not be replete if do not thank all Members of the Diplomatic Community, Development Partners Members of The East African Legislative Assembly, Presenters of various scientific papers invited to the Conference and all those who have put in time and effort to ensure the success of this Conference.

I wish to conclude my remarks by thanking you all for attending, for those who are coming outside Tanzania and will get few days to rest, hope you will enjoy exploring the beauty of our country. I particularly recommend our sandy beaches in Zanzibar; our picturesque Kilimanjaro Mountain not forgetting our renowned Serengeti National Park.
I wish you fruitful deliberations.

IT IS NOW MY SINGULAR HONOR AND PLEASURE TO DECLARE THE 7THEAST AFRICAN HEALTH AND SCIENTIFIC CONFERENCE, OFFICIALLY OPENED.

I THANK YOU FOR YOUR KIND ATTENTION.

 

MEYA WA CUF MANISPAA YA MTWARA MIKINDANI AJIUNGA NA CCM.

$
0
0
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Godfrey Mwanchisye (CUF) na Diwani wa kata ya Chikongola Mussa Ismaili ‘Fashion’ (CUF) wamejiuzulu nafasi zao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi CCM.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images