Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live

RC Wangabo atoa maamuzi mazito baada ya makusanyo ya bilioni 1.34 kuwa mikononi mwa watendaji

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo

……………………………………………………

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku saba kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, kuhakikisha anaunda timu ya uchunguzi ili kuwabaini wadaiwa wa shilingi bilioni 1.34 za makusanyo ya mapato ya ndani ya halmashauri na kuwachukulia hatua wahusika wote ili kuleta ustawi katika utekelezaji wa majukumu ya kiserikali.

Amesema hayo baada ya kupitia taarifa za makusanyo na kubaini tatizo la kutowasilishwa kwa makusanyo ya mapato ya ndani kwa kutumia mfumo wa Local Governent Revenue Collection Information System (LGRCIS) na kueleza kuwa kumekuwa na watendaji ambao sio waaminifu wanaokabidhiwa makusanyo hayo na kuyaingiza kwenye matumizi binafsi wakitegemea kurudisha na matokeo yake Bili za wakusanyaji hazikubali kutoka kwenye mfumo hadi fedha zote alizokusanya zitimie.

Akitolea mfano halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mh. Wangabo alisema kuwa “hadi kufikia mwezi Februari mwaka 2019, jumla ya Shilingi Milioni 98 zimetumika kama sehemu ya gharama za wakusanyaji baada ya kuzikata na kutumia. Matokeo yake fedha zinapelekwa Halmashauri zikiwa pungufu na kuongeza kuwa jumla ya shilingi 241 za halmashauri hiyo zilitumika kabla ya kupelekwa benki jambo hilo ni kinyume na kifungu cha 32 cha Memoranda ya Fedha za Serikali za Mitaa.”

Alitoa agizo hilo wakati wa ufunguzi wa semina ya mafunzo elekezi kwa waheshimiwa madiwani kutoka katika halmashauri zote nne za Mkoa wa Rukwa iliyofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Sumbawanga ambapo Mh. Wangabo alikuwa mgeni rasmi wa semina hiyo.

Akitoa neno la Shukurani kwa mgeni rasmi mstahiki Meya wa manispaa ya Sumbawanga alipongeza juhudi za mkuu wa mkoa wa Rukwa kuhakikisha anasimamia vyema maendeleo ya mkoa huo, na kumuhakikishia kuwa hawatamuangusha katika kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unaongezeka

“ Sisi kama ALAT mkoa na nipende kuwaarifu madiwani wa halmashauri zote na itakuja kwenye vikao vyenu, tuliona kuliko kulalamika kwa kusema hatuna vyanzo vya mapato, halmashauri za mkoa wa Rukwa zina migogoro mingi ya ardhi kwa kutopanga matumizi ya ardhi, hivyo tumeamua ardhi zote ndani ya mkoa zipimwe na tumeshanunua mashine ya Alat K yenye thamani ya Shilingi Milioni 37 ili tuongeze mapato kwa kupima ardhi,” Alisema.

Hadi kufikia tarehe 12 mwezi Machi mwaka 2019 Manispaa ya Sumbawanga in wadaiwa wa makusanyo ya mapato ya ndani shilingi milioni 45.97, Sumbawanga Vijiji Shilingi Milioni 756.17, Wilaya ya Kalambo Shilingi Milioni 252.64 na Wilaya ya Nkasi Shilingi Milioni 290.95

MKOA WA KATAVI WAZINDUA MPANGO WA KUTANGAZA UTALII WAKE

$
0
0


Mkuu wa mkoa wa Katavi Amos Makala katikati akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mlele Rachel Kasanda, Dk Theresia Olemako kutoka taasisi ya Jane Godall, , akifuatiwa na Mkuu wa hifadhi ya Katavi Stephano Msumi na kaimu katibu tawala mkoa wa Katavi Awaryiwa Nnko pamoja na watendajiwengine wa mkoa huo.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Amos Makala akisoma moja ya bango linaloielezea mbuga ya wanyama ya Katavi.

Baadhi ya picha zikionyesha baadhi ya wanyama wanaopatikana katika mbuga ya wanyama wa Katavi mkoani Katavi.
Mkoa Wa Katavi Umezindua Rasimu Ya Mpango Mkakati Wa Miaka Kumi Ya Kukuza Sekta Ya Utalii Mkoani Katavi Kwa Lengo La Kuongeza Watalii Kutoka Wastani Wa Watalii 3340 Waliotembelea Hifadhi Hiyo Mwaka 2018 Hadi Kufikia Watalii 6012 Mwaka 2029

Akizungumza Mara Baada Ya Kuzindua Rasimu Hiyo Bwana Makalla Amesema Mpango Huo Utawezesha Kukuza Uchumi Wa Mkoa Wa Katavi

Aidha Mkuu Huyo Wa Mkoa Wa Katavi Amewataka Wananchi Kuacha Tabia Ya Kuharibu Mazingira Ili Kuwa Na Maeneo Ya Wanyama Pori Sanjari Na Kuwataka Waandishi Wa Habari Kutumia Taaluma Yao Katika Kuutangaza Utalii Katika Mkoa Wa Katavi Kwani Ni Mkoa Wenye Vivutio Vya Kipekee

Awali Akitoa Taarifa Ya Hifadhi Ya Taifa Ya Katavi Mkuu Wa Hifadhi Hiyo Bwana Stephano Msumi Amesema Wamefanikiwa Kudhibiti Ujangili Wa Tembo Kwa Asilimia Mia Moja Ambapo Kwa Mwaka Uliopita Hakuna Tembo Hata Mmoja Aliyeuwawa

Katika Uzinduzi Huo Kaimu Mtendaji Mkuu Wa Taasisi Ya Jane Goodall Dk. Theresia Olemako Alipata Nafasi Ya Kuwasilisha Mada Juu Ya Wanyama Aina Ya Sokwe Mtu Na Kusema Mwaka 1900 Kulikuwa Na Sokwe Mtu Zaidi Ya Milioni Mbili Lakini Sasa Wamebaki Sokwe Laki Tatu Tu

Mkuu Huyo Wa Mkoa Aliambatana Na Baadhi Ya Wajumbe Wa Kamati Ya Ulinzi Na Usalama Pamoja Na Watendaji Mbalimbali Ambao Walipata Fursa Ya Kutembelea Hifadhi Ya Katavi; Ambapo Walipata Nafasi Ya Kujifunza Namna Mzimu Wa Katabi Unavyoaminiwa Na Watu Wa Jamii Ya Wabende Na Wapimbwe

LUGOLA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA KITUO CHA TRAFIKI BUIGIRI MKOANI DODOMA, BAADA YA KUPATA MALALAMIKO YA MADEREVA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akizungumza na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma, SSP Nuru Selemani (katikati) katika kituo cha Trafiki Buigiri kilichopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Waziri huyo alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho leo, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa madereva kuonewa mara kwa mara na askari katika kituo hicho. Hata hivyo, askari hao walimweleza Waziri huyo utendaji kazi wao pamoja na changamoto wanazozipata kituoni hapo. Kulia ni Askari wa Usalama Barabarani wa kituo hicho, CP Amina.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimfafanulia jambo na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma, SSP Nuru Selemani katika kituo cha Trafiki Buigiri kilichopo nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Waziri huyo alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo hicho leo, baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa madereva kuonewa mara kwa mara na askari katika kituo hicho. Hata hivyo, askari hao walimweleza Waziri huyo utendaji kazi wao pamoja na changamoto wanazozipata kituoni hapo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.



Na Mwandishi Wetu, MOHA

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amefanya ziara ya kushtukiza kituo cha Askari wa Usalama Bararani (Trafiki) Buigiri Mkoani Dodoma, baada ya kupokea malalamiko mara kwa mara kutoka kwa madereva wanaoitumia barabara hiyo.

Lugola alifika katika kituo hicho kilichopo barabara kuu ya Dodoma-Morogoro, nje kidogo ya Jiji la Dodoma, saa kumi alasiri akiwa ameambatana na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani humo, SSP Nuru Selemani, na kuanza kutaka kujua utendaji kazi wa askari hao katika kituo hicho.

Akizungumza na askari hao, Lugola aliwataka wafanye kazi kiweledi bila kuwaonea madereva kwa kuwaomba rushwa au kuwapiga faini kwa uonevu.

“Licha ya kuwapongeza kwa kazi nzuri kwa kuyaongoza magari lakini mnapaswa kufuata sheria na si kufanya kazi kwa uonevu, nimekua napokea malalamiko mara kwa mara kutoka kwa madereva kuhusu kituo hiki, fanyeni kazi kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani zinavyoelekeza,” alisema Lugola.

Kwa upande wake SSP Selemeni, alimweleza Waziri huyo kuwa, wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika utendaji wa kazi zao, lakini maelekezo ya utendaji kazi wa weledi waliopewa wameyapokea na kuahidi kuyafanyia kazi.

Lugola alisema yeye ni Waziri ambaye anafuatilia maagizo yake kila anapoyatoa, hivyo askari ambao wanachafua Jeshi la Polisi hatawavumilia, na ataendelea kufanya ziara za kushtukiza kama hizo mara kwa mara sehemu mbalimbali nchini.

Waziri huyo yupo njiani kuelekea Mjini Morogoro kwa ajili ziara ya kikazi atakayoifanya Kesho Machi 15, Tarafa ya Kimamba, Wilayani Kilosa, Mkoani humo.

MWAKYEMBE AKEMEA UHARIBIFU WA MAENEO YA KIHISTORIA KWA LENGO LA KUTAFUTA MADINI

$
0
0



Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (katikati) akisoma maelezo leo kwenye sanamu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mjini Tabora wakati wa ziara yake katika Manispaa ya Tabora ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.


Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (katikati) akizungumza na wananchi leo kwenye sanamu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mjini Tabora wakati wa ziara yake katika Manispaa ya Tabora ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.
Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na watumishi na viongozi mbalimbali leo wakati wa ziara yake katika Manispaa ya Tabora ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.



Baadhi ya watumishi na viongozi wa Manispaa ya Tabora wakimsikiliza Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (hayupo katika picha ) wakati wa ziara yake katika Manispaa ya Tabora ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.



Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe (kulia) akisalimiana na watumishi leo wakati wa ziara yake katika Manispaa ya Tabora ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.
Picha na Tiganya Vincent

……………..

NA TIGANYA VINCENT

SERIKALI imewataka wananchi kuacha tabia ya kuharibu maeneo ya kihistoria ikiwemo majengo ya kale kwa madai potofu kuwa kwenye maeneo hayo wakoloni walificha madini ndani yake.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe wakati wa ziara yake katika Manispaa ya Tabora ya kutembelea maeneo ya urithi wa ukombozi wa bara la Afrika.

Alisema vitendo vya aina hiyo vinasababisha Serikali kutumia gharama kubwa pindi wanapotaka kukarabati na kurudisha historia ya maeneo hayo.

“Hakuna ambaye ni mjinga aweke ndani ya nyumba dhahabu halafu asiifuate…hata wangekuwa wameweka mali ndani ya majengo yao wamekuja na njia nyingine ya kutaka kuendeleza maeneo hayo kwa kuweka miradi ya kuchimba visima ili wachukue madini kama yangekuwepo” alisema.

Mwakyembe alisema maeneo hayo ni muhimu sana katika Historia ya Tanzania na pia katika ukuzaji wa utalii kwa ajili ya kulipatia Taifa fedha za kigeni. Aliongeza kuwa maeneo hayo ni muhimu katika kutoa elimu kwa vijana wa kitaifa kufahamu historia ya nchi yao kwa ajili ya kuwa wazalendo wazuri wa Tanzania. Mwakyembe alisema Wizara yake inaewndelea na utaratibu wa kuyaorodhesha maeneo yote ya kihistoria kwa ajili ya kuyahifadhi na kuyakarabati kwa ajili faida ya kizazi cha sasa na kijacho.

Aidha Waziri huyo alisema Serikali iko mbioni kupeleka Bungeni Muswada wa Sheria ambayo utafanya maeneo ya kihistoria yasiguswe na kuzuia uharibifu. Alisema baada ya muswada huo kupitishwa na hatimaye kuwa Sheria utasaidia kulinda utajiri wa urithi wa Kihistoria ulipo hapa nchini usiweze kuharibiwa na kupotea. Katika hatua nyingine Mwakyembe alisema Serikali itahakikisha inarudisha nchini Fuvu la Kichwa cha Mama Shujaa mpiga ukoloni wa Kijerumani kutoka Singida Bibi Liti.

Alisema Shujaa huyo aliweze kupambana na Wajerumani kwa kutumia nyuki hadi hapo aliposalitiwa na wenzake na hatimaye Wajerumani wakata kichwa chake na kuondoka nacho.

Mwakyembe alisema lazima fuvu la kichwa lirudishwe nchini na kuhifadhiwa katika jumba maalumu kwa ajili ya historia ya Tanzania

Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini Atoa Ufafanuzi Mwananchi Aliyebambikiziwa Kesi na Polisi

SERIKALI YAOKOA BILION 3.4 KWENYE MATIBABU YA UGONJWA WA FIGO

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongea na Waandishi wa Habari (Hawapo kwenye picha) wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma. Wakwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Tiba Wizara ya Afya Dkt. Grace Maghembe na wamwisho ni Mwenyekiti wa Chama cha Magonjwa ya Figo nchini Dkt. Kisanga
Waandishi wa Habari waliojitokeza kumsikiliza Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati akitoa tamko la Siku ya Figo Duniani, lililotolewa leo katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma.


Na WAMJW-DOM.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali imefanukiwa kuokoa kiasi cha Shilingi Bilion 3.4 ambacho kingetumika katika matibabu kwa Wagonjwa wa Figo nje ya Nchi.

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo leo Machi 14 wakati akiongea na Waandishi wa Habari katika Ofisi za Wizara ya Afya Jijini Dodoma ikiwa ni Siku ya Figo Duniani ambayo inaongozwa na kauli mbiu ya Afya ya figo kwa kila mmoja kila.Dkt. Ndugulile amesema kuwa Serikali imeokoa kiasi cha shilingi bilioni 4.2 ambacho kingetumika katika matibabu ya wagonjwa 80 mpaka 100 ambao wangepelekwa nje ya nchi kwaajili ya matibabu.

“Wagonjwa waliokwishapandikizwa figo hapa nchini ni 42, kama tungewapeleka wagonjwa nje ya nchi ingegharimu serikali kiasi cha shilingi bilioni 4.2 kwa idadi hiyo ya wagonjwa. 80 mpaka 100, wakati huduma hii hapa nchini inagharimu kiasi cha shilingingi milioni 21 kwa kila mgonjwa.” Alisema Dkt. Ndugulile

Aidha, Dkt, Ndugulile amesema kuwa miongoni mwa sababu zinazochangia magonjwa ya figo ni pamoja na uzito wa kupindukia (obesity), matumizi makubwa ya sigara, unywaji wa pombe, uvutaji wa sigara,kutokufanya mazoezi na kunywa madawa kiholela hasa dawa za kupunguza maumivu.Aliendelea kusema kuwa, magonjwa ya kisukari na shinikizo la damu ni magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha matatizo ya figo, magonjwa haya yakitambuliwa mapema yanaweza kudhibitiwa kwa matibabu na kuepusha madhara kwenye figo.

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile amesema kuwa Kufikia Desemba mwaka 2018, jumla ya vituo 28 vyenye jumla ya wagonjwa 1050 vilikuwa vikitoa huduma ya usafishaji damu katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha, Kilimanjaro na Dodoma.Mbali na hayo, Dkt. Ndugulile amesema Serikali imepiga hatua kubwa ya kuanzisha huduma za kupandikiza figo hapa nchini katika hospitali ya Taifa Muhimbili na Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari wa Figo nchini Dkt. Onesmo Kisanga amesema kuwa Ugonjwa wa Figo ni tatizo kubwa nchini huku wananchi wengi wakiwa na uelewa mdogo juu ya athari na visababishi vya ugonjwa huo.

Aidha Dkt. Onesmo amewataka wananchi kuacha tabia ya kunywa dawa bila kupata ushauri wa kitaalamu hivyo kuepuka kuzalisha sumu mwilini na kupelekea ugonjwa wa figo.Hata hivyo Dkt. Onesmo Kisanga ameishukuru Serikali kwa kuwaendeleza kimasomo wataalam kwenye upande wa matibabu ya figo ambao sasa wamesambazwa sehemu mbali mbali ndani ya nchi kutoa huduma za matibabu.

Naye Dkt. Grace Maghembe Kaimu Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara ya Afya amesema ungojwa huu umekuwa ukiwaathiri zaidi wakazi wa mijini kuliko vijijini kutoka na mfumo wa maisha uliopo sasa ambapo watu wengi wamekuwa hawazingatii mtindo bora wa maisha kwa kutofanya mazoezi pamoja na kula chakula bora.Dkt. Maghembe amesema bado ipo changamoto kwenye matumizi ya dawa za mitishamba ambazo bado hazijatambuliwa na kuthibitishwa huku akiwataka wananchi kuwa waangalifu pia kwenye matumizi ya dawa hizo.

“Serikali inatambua umuhimu wa tiba mbadala pamoja na matibabu ya tiba za asili na ndio maana zipo taasisi za serikali zinazohusika kuzitambua dawa hizo ni zipi na zina vitu gani na unatakiwa kutumia kwa kiwango gani” amesema Dkt Maghembe nakuwataka watengenezaji wa dawa hizo kufuata taratibu zilizopo ili kuthibitisha na kusajili dawa zao.

RC ARUSHA AZURU KAYA ZILIZODHANIWA KUATHIRIKA KWA MAJI SAFI KUCHANGANYIKA NA MAJI TAKA

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo akizungumza na waandishi wa habari katika mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya kuwatembelea wananchi ili kuwasikiliza na kujua ukweli kuhusiana na sakata la maji mkoani hapo. Picha na Vero Ignatus.
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira,Mhandisi Ruthy Koya akiongea na waandishi wa habari ambapo amesema wataalam wamechunguza maji hayo na kubaini kuwa hayana tatizo na kusisisitiza wananchi kuendelea kuyatumia kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Ghambo, kushoto kwake ni Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Hospitali ya Mkoa ,Dk,Omary Chande
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akimsikiliza mmoja wa wazee katika baadhi ya mitaa aliyoitembelea.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrosho Gambo akinywa maji kwenye moja ya kaya aliyoitembelea ambapo maji hayo wananchi wamekuwa akiyashuku kuwa siyo salama,na kuwahakikishia kuwa ni salama na hayana tatizo.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira,(AUWSA) Mhandisi Ruth Koya akinywa maji ambayo wananchi wameyatilia shaka kwamba siyo safi na salamaamewahakikishia kuwa maji hayo hayana tatizo na kusisisitiza wananchi kuendelea kuyatumia, huku akisisitiza wayachemshe na kuyachuja vizuri
Mtaalamu wa vipimo katika kutoka wizara ya maji mahabara ya kituo Arusha ambapo ndipo maji yapimwa. na kujiridhisha kuwa maji ni safi na salama na yana dawa ya kutosha, mkuu wa Mkoa akipewa maelekezo namna inavyofanya kazi


Na. Vero Ignatus, Arusha.


Ile sintofahamu ya wakazi wa Jiji la Arusha kuendelea kupata homa ya matumbo kutokana kudaiwa kunywa maji yaliyochanganyikana na maji taka limechukua sura Mpya Mara baada ya Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kutembelea kaya zilizoathirika huku akinywa maji hayo kwa lengo la kujiridhisha na kubaini maji hayo hayana madhara

Akiongea na wananchi katika Kata ya Themi Gambo alikiri kuwa baadhi ya wananchi wamekumbwa na tatizo la kuumwa matumbo na kuhara ndiyo maana wao kama serikali wameamua kuwatembelea na ili kujiridhisha kuwasikiliza

Katika ziara hiyo Mhe. Gambo aliambatana na wataalamu wa Afya Mkoa wa Arusha Mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira ,kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa

Mitaa ambayo wameitembelea ni pamoja na mitaa ya Naura Kata ya kati ,Mtaa wa Ndarvoi kata ya Daraja mbili na Kata ya Themi ambapo wananchi walimweleza ambapo wananchi waliweza kumueleza wa mkoa jinsi walivyoathirika na kunywa maji hayo waliodai yamekuwa na harufu kali ya kinyesi.

Wananchi hao ,Boniface Chacha,Jesta John na Hawa Hasan wamesema maji ya bomba wanayokunywa ni changamoto kubwa kwao na kuitaka serikali iwasaidie kuhakikisha afya zao hazidhuriki kutokana na matumizi ya maji safi wanayotumia."Nimetembelea eneo moja baada ya nyingine kujionea tatizo la maji na nikiri kweli kunabaadhi ya watu wanaumwa matumbo na bado wataalam wanachunguza suala hili lakini nasisitiza hakuna uchafuzi wa maji safi kuingiliana na maji taka"

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Hospitali ya Mkoa ,Dk,Omary Chande amesema madaktari wamechukua sampuli za maji na wanaendelea kuzipima kwenye maabara na hakuna mgonjwa yoyote aliyelazwa hospitali ya mkoa bali Jiji kwa maana ya vituo vya afya wamepokea wagonjwa 310

Dkt. Chande amesema sampuli mbalimbali zinaendelea kuchunguzwa ili kubaini ni kitu gani kimesababisha watu kuumwa matumbo

Naye Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira,Mhandisi Ruthy Koya amesema wataalam wamechunguza maji hayo na kubaini kuwa hayana tatizo na kusisisitiza wananchi kuendelea kuyatumia na wale wasiyotumia maji hayo wachemshe maji


Amesema baada ya kuoana taarifa Mamlaka waliweza kutembelea sehemu husika zinazolalamikiwa na kuchukua sampuli na kuwashirikisha wenzao wizara ya maji mahabara Arusha na kujiridhisha kuwa maji ni safi na salama na yana dawa ya kutosha

Amesema AUWSA hawajaweza kukidhi uhitaji wa maji katika jiji la Arusha kwa 100%kwani,upatikanaji wa maji ni 40%kwahiyo ile 60%inakuwa inajazilushiwa na watu binafsi kwa vyanzo vyao tofauti

Natoa shukrani nyingi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli pamoja na serikali yake shukrani kwani ametoa fedha nyingi kwaajili ya kuondoa tatizo la maji Jijini Arusha

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Shana ametoa onyo kwa mtu yeyote yule ambae atasambaza habari za uchochezi au mtu yotote atakayeeneza uvumi wa maji safi kuchanganyika na maji taka atachukuliwa hatua za kisheria kwani tayari ufafanuzi wa kina umeshatolewa na mamlaka husika

BI.GAUDENSIA ATUA MKOA WA MJINI ZANZIBAR,ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO

$
0
0



NA IS-HAKA OMAR, ZANZIBAR.

MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Ndugu Gaudensia Kabaka amewataka Wanawake kuitumia vyema fursa ya Ujasiriamali ili wajiongezee kipato na kujiajiri wenyewe.

Rai hiyo ameitoa katika ziara yake katika Mkoa wa Mjini Kichama wakati akizungumza na Wana CCM huko katika ukumbi wa Kwa Waazee Sebleni Unguja.

Alisema ujasiriamali ni nyenzo pekee ya kuwakomboa wanawake kiuchumi na wakaweza kuwa na uwezo na nguvu za kujiajiri wenyewe.

Ameeleza kwamba CCM kwa sasa ipo katika Sera na Mkakakati wa Siasa na Uchumi hatua inayotakiwa kuchangamkiwa na Akina Mama Nchini, kwa kuanzisha vikundi vya ushirika.

Kupitia ziara hiyo aliipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwalea wazee katika mazingira bora yanayowawezesha kupata huduma zote za msingi za kijamii.

Alimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapibduzi Dk. Ali Mohamed Shein kwa busara zake za kuendeleza mambo mbali mbali yaliyoasisiwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar marehemu Mzee Abeid Amani Karume hasa kuendeleza Vituo vya ustawi wa jamii vya kuwatunza wazee.

Aliongeza kuwa wazee ndio chimbuko la maendeleo ya Zanzibar kwani wao ndio waliotoa nguvu zao kujenga nchi katika nyanja za kiuchumi, kimaendeleo na kijamii.

Akizungumzia ziara yake katika Wilaya ya Amani aliwapongeza viongozi wa UWT kwa juhudi zao za kubuni masuala mbali mbali ya kuimarisha jumuiya hiyo na CCM kwa ujumla.

Wakati huo huo akizungumza na Akina Mama wa Wilaya ya Mjini aliwapongeza kwa ubunifu wao wa kuanzisha Kituo cha mafunzo ya Amali ya kuwajengea uwezo wa fani mbali mbali Vijana wa CCM ili wapate ujuzi na kujiajiri wenyewe.

Alielezea kufurajishwa kwake na hatua hiyo ya kuwapatia vijana wafunzo ya Ushoni, Uuguzi, Uandishi wa Habari na mafunzo ya Komputer kwani fani hizo alizitaja kuwa zinaendana na wakati wa sasa kiajira.

Sambamba na hayo alitembelea Shule ya Maandalizi iliyopo katika Jengo la UWT Mkele na kuwataka Wazazi na Walezi kuwarithisha Watoto Elimu ili iwasaidie katika maisha yao ya sasa na baadae.

Aidha alitembelea Kanisa la Angilicana la Mkunazini Zanzibar na kujionea kumbukumbu za historia ya Watu ambazo ni miongoni mwa vielelezo vya historia ya Nchi.

Aliwasihi Wanawake Zanzibar bila kujali tofauti za Kisiasa wajitokeze kwa Wingi kushiriki Kongamano la Kitaifa la UWT la kupongeza Serikali ya Awamu ya Saba inayoongozwa na Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein, litakalofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Kimataifa ya Verde Machi 16,mwaka 2019 kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 9:00 Mchana ambapo Mawaziri na Manaibu Waziri watazungumzia kwa upana namna Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walivyotekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2015/2020 kwa ufanisi mkubwa.

Katika ziara hiyo alipokea Taarifa za Utekelezaji wa shughuli za UWT Wilaya ya Mjini, Wilaya ya Amani pamoja na Taarifa ya Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Mjini.

Bi. Gaudensia ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa aliambatana na Viongozi mbali mbali wa Umoja huo akiwemo Makamu Mwenyekiti wa UWT Taifa Ndugu Thuwaiba Kisasi, Katibu Mkuu wa UWT Taifa Mwl. Queen Mlozi,Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar Ndugu Tunu Juma Kondo, Naibu Katibu Mkuu wa UWT Tanzania Bara Ndugu Jesca Mbogo ‘Jasmini’ pamoja na Wajumbe wa Kamati Tekekelezaji wa UWT Taifa

TIMU ZA UENDESHAJI WA HUDUMA ZA AFYA MKOA NA WILAYA ZATAKIWA KUWA WABUNIFU

$
0
0

Naibu Katibu Mkuu Afya, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Dkt.Dorothy Gwajima akiwaonyesha moja ya taarfa ya utekelezaji majukumu kwa Timu za huduma za afya Mkoa (RHMT) na Wilaya(CHMT),(hawapo pichani) katika kikao cha Mrejesho wa Utekelezaji wa yatokanayo na ziara za usimamizi shirikishi za utendaji kwa watoa huduma za afya katika Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Chamwino leo jijini Dodoma katika ukumbi wa Reforms uliopo katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
Mwonekano wa kwa Timu za huduma za afya Mkoa (RHMT) na Wilaya(CHMT)wakiwa katika katika kikao cha Mrejesho wa Utekelezaji wa yatokanayo na ziara za usimamizi shirikishi za utendaji kwa watoa huduma za afya katika Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Chamwino leo jijini Dodoma katika ukumbi wa Reforms uliopo katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI.
Baadhi ya wajumbe katika kikao cha Mrejesho wa Utekelezaji wa yatokanayo na ziara za usimamizi shirikishi za utendaji kwa watoa huduma za afya katika Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Chamwino leo jijini Dodoma katika ukumbi wa Reforms uliopo katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI wakimsikiliza kwa umakiniDkt.Gwajima .

…………………………………..

Na. Majid Abdulkarim

Kamati za huduma za afya Mkoa (RHMT) na Wilaya(CHMT) nchini zimetakiwa kuwa wabunifu katika kutekeleza shughuli zake na kuhakikisha wanaboresha huduma za afya kuanzia ngazi ya msingi hadi mkoa kwa ujumla ili kuleta matokeo bora kwa watanzania.

Hayo yamebainishwa na Naibu Katibu Mkuu Afya, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Dkt.Dorothy Gwajima katika kikao cha Mrejesho wa Utekelezaji wa yatokanayo na ziara za usimamizi shirikishi za utendaji kwa watoa huduma za afya katika Manispaa ya Dodoma na Halmashauri ya Chamwino leo jijini Dodoma katika ukumbi wa Reforms uliopo katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

Dkt. Gwajima amesema kuwa ubunifu unaotakiwa ni kujenga mahusiano mazuri baina ya mteja na mtoa huduma za afya ili mteja awezekuwa uhuru na kujisikia faraja katika kupata huduma kutoka kituoni hapo.

“Mahusiano mazuri yanajengwa na ukarimu, lugha nzuri kwa mteja na utendaji kazi wenu kwa ujumla mnavyo hudumia wateja wenu kwa kuwa mawakili wazuri katika jamii yao kulingana na mlivyo wahudumia” Ameseama Dkt.Gwajima

Lakini pia Dkt.Gwajima amewataka watoa huduma za afya kuwa na mpango kazi utakao weza kuwaongoza vyema katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ili kufikia kiwango bora cha utoaji huduma za afya nchini.

Dkt.Gwajima ameeleza kuwa mpango kazi kwa mtumishi utasaidia kuweza kupata tathimini ya utekelezaji wa amjukumu ya mtoa huduma za afya na kujua matokeo yapi yamefanyikiwa , kubaini changamoto zilizojitokeza na kuzitafutia suluhisho ili kufikia malengo ya mtoa huduma aliyojiwekea katika mpango kazi wake.

“Ili kupata tathimini ya utendaji kazi wa watoa huduma za afya amesisitiza kuhakikisha kila mmoja kuwa na taarfa ya uwajibikaji wake ukiwa na takwimu sahihi ili kuweza kupata matokeo bora katika sekta ya faya”.Ameongezea Dkt.Gwajima

Aidha Dkt.Gwajima amehitimisha kwa kuwataka watoa huduma za afya kutekeleza mipango kazi yao kwa vitendo ili kuweza kupata matokeo chanya yatakayo onyesha mabadili katika sekta ya afya na hapo tutakuwa tumetimiza azma ya serikali ya kumuhudumia mwananchi.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt.Samwel Seseja amesema kuwa atasimamia vyema maelekezo yalotolewa na Dkt.Gwajima ili kuhakikisha utendaji kazi na uboreshaji wa huduma za afya kuanzia ngazi ya msingi hadi mkoa zina boreka na kuimarishwa vizuri kwa faida ya watanzania.



MKUU WA IDARA YA ARDHI KYERWA APEWA WIKI MOJA VINGINEVYO KUTUMBULIWA

$
0
0

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera baada ya kutoa hati za ardhi katika halmashauri hiyo katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia sekta ya ardhi jana.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akitoka katika Masijala ya Ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera alipokwenda kukagua majalada ya ardhi akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia sekta ya ardhi jana.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika Masijala ya Ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera alipokwenda kukagua majalada ya ardhi akiwa katika ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia sekta ya ardhi jana. Wa pili kulia ni Mkuu wa Idara ya Ardhi halmashauri ya Karagwe ambaye pia ni Afisa Ardhi Mteule katika halmashauri hiyo na ile ya Misenyi Benard Esau.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akivalishwa Scalf na Skauti baada ya kuwasili katika wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kuanza ziara ya kuhamasisha ukusanyaji maduguli ya serikali kupitia sekta ya ardhi jana



………………………………

Na Munir Shemweta, KYERWA

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amempa wiki moja Mkuu wa Idara ya Ardhi katika Halmashauri ya wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kuhakikisha anaingiza viwanja 516 katika Mfumo wa Malipo ya Serikali kwa njia ya Kielektroniki vinginevyo ataondolewe katika wadhifa huo.

Agizo hilo limafuatia Dkt Mabula kuelezwa na Mkuu huyo wa Idara kuwa katika halmashauri hiyo jumla ya viwanja 348 pekee ndvyo vilivyoingizwa katika Mfumo wa Kielektroniki huku viwanja 516 vikiwa havijaingizwa kwenye mfumo huo.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitoa agizo hilo jana tarehe 15 Machi 2019 wakati akiwa katika mfululizo wa ziara yake ya kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia sekta ya ardhi katika wilaya za mkoa wa Kagera.

Dkt Mabula alisema kuna uzembe mkubwa kwa Mkuu huyo wa Idara ya Ardhi ambaye pia ni Afisa Ardhi Mteule wa halmashauri ya wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera kusimamia uingizaji viwanja kwenye mfumo ambao ndiyo unaosaidia kuongeza mapato ya serikali.

Naibu Waziri alishangazwa na Mkuu huyo wa Idara kushindwa kuingiza idadi hiyo ya viwanja kwenyea mfumo wa kielektroniki katika kipindi cha mwaka mzima wakati alieleza kuwa kwa siku moja anao uwezo wa kuingiza viwanja ishirini.

‘’Kuna uzembe katika kusimamia idara hii ya ardhi na kama mzigo ni mkubwa kwako kusimamia idara hii basi chagua kuachia nafasi moja katia ya Ukuu wa idara ya ardhi au Afisa Ardhi Mteule ili uweze kuifanyia nafasi moja kwa ufanisi’’ alisema Mabula.

Akigeukia suala la utoaji hati katika halmashauri hiyo ya Kyerwa, Dkt Mabula aliiagiza halmashauri ya Kyerwa kuhakikisha maeneo yote yaliyochukuliwa kwa ajili ya matumizi ya umma yanapatiwa hati ili kuepuka migogoro ya ardhi.

Alisema, migogoro mingi kwenye taasisi za umma inasababishwa na taasisi hizo kutokuwa na hati kwenye maeneo yake na kutolea mfano moja ya maeneo yanayovamiwa sana ni yale ya wazi na kuzitaka idara husika kusimamia suala hilo kwa makini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Rashid Mwaimu alisema viwanja vingi katika wilaya yake havina hati jambo alilolieleza kuwa wakati mwingine linawapa ugumu wa kuchukua hatua kwa wamiliki wake ambao aliwaeleza kuwa wengi wameacha maeneo yao kuwa mapori.

Kwa mujibu wa Mwaimu wilaya hiyo imetoa miezi sita kwa wamiliki wote wa viwanja ambao hawajaviendeleza na kuviacha mapori kuviendeleza vinginevyo watafutiwa umiliki wake.

Katika hatua nyingine Dkt Mabula ametaka halamashauri ya wilaya ya Karagwe mkoa wa Kagera kulitumia Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kujenga nyumba kwa ajili ya watumishi wake ili kuondoa uhaba wa makazi kwa watumishi wa halmashauri hiyo.

Alibainisha kuwa, hata kama halmashauri hiyo haihitaji nyumba kwa ajili ya watumishi wake basi inaweza kujengewa nyumba na shirika hilo kwa ajili ya kuutengeneza mji wa Karagwe na wakati huo kuzitumia nyumba hizo kama rasilimali ambapo nyumba hizo zinaweza kupangishwa na kuiwezesha halmashauri kujipatia kipato.

‘’Halmashauri badala ya kutegemea kuingiza mapato katika baadhi ya vyanzo kama vile kituo cha mabasi wanaweza kulitumia shirika la nyumba kuongeza hadhi ya mji na mapato kwa halmashauri’’ alisema mabula.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MACI 15,2019

ASILIMIA 80 YA WANANCHI SIMIYU KUTUMIA BIMA YA AFYA

$
0
0
Na Stella Kalinga, Simiyu

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mkoa huo umejiwekea malengo ya kuhakikisha zaidi ya asilimia 80 ya wananchi wake kuwa na kadi za bima ya afya ili kujihakikishia upatikanaji wa huduma za matibabu katika vituo vya kutolea huduma za afya hapa nchini.

Mtaka ameyasema hayo wakati ufunguzi wa Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS)wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.

Amesema yeye kama Mkuu wa Mkoa atafanya vikao na wanachama wa AMCOS na makundi mbalimbali ya wananchi katika wilaya zote mkoani hapa na kuzungumza nao kuwaelimisha juu ya umuhimu wa kila mwananchi kuwa na Bima ya Afya kwa ajili ya matibabu.

Aidha, amesema atawaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwa katika Vyama vya Ushirika Vya Msingi ambavyo vinawapa nafasi ya kupata Bima ya afya na kupata matibabu makubwa katika vituo vya kutolea huduma za afya vya binafsi na vya umma kwa gharama nafuu ya shilingi 76,800/= kwa mtu mmoja(mwanachama wa ushirika).

“Nitafanya vikao na wanachama wa AMCOS zote, wakulima, wafugaji, wajasiriamali, makundi yote ya wananchi kwenye mkoa wetu wa Simiyu, tuweze kuwaelimisha faida ya mwananchi wa mkoa wa Simiyu kuwa na bima ya afya, kubwa zaidi umuhimu wa kuwa kwenye ushirika ambao utamwezesha kupata matibabu makubwa kwa bei nafuu” alisema

Katika hatua nyingine Mtaka amesema katika kipindi cha msimu wa pamba kila kituo cha kununulia pamba NHIF itaweka Afisa wake kwa ajili ya kusajili wakulima na wanachama wa vyama vya ushirika walio tayari, hivyo akatoa wito kwa viongozi walioshiriki jukwaa la ushirika afya kutoa taarifa na elimu kwa wenzao juu ya umuhimu wa suala hilo.

Mtaka pia ametoa wito kwa wakulima wote wa pamba kulipa kipaumbele suala la afya kwa kuchukua hatua ya kuwa na bima za afya ili waweze kuona manufaa ya Serikali kuboresha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kujenga Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Hospitali za wilaya kwa kila wilaya na Vituo vingine vya kutolea huduma za afya.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bernad Konga amesema NHIF ni wadau wakubwa mkoani Simiyu, hivyo wako tayari kutoa huduma bora na watawafikia wananchi wa makundi yote mkoani hapa na watahakikisha wanatoa kadi za bima ya afya kwa wakati kwa wanachama wote watakaojiunga.

Katika jukwaa hili washiriki wamepata nafasi ya kuchangia michango mbalimbali huku wanachama wa AMCOS wakiunga mkono mpango huo wa kupata bima ya afya kwa gharama ya shilingi 76,800/= ili waweze kumudu gharama za matibabu.

“Mpango huu nimeupokea vizuri ila ninashauri elimu iendelee kutolewa zaidi na zaidi ili wanachama wote wajue umuhimu wa kuwa na kadi za bima ya afya na namna zitakavyowasaidia” Lucas Ephraim mshiriki kutoka AMCOS ya Dutwa Bariadi.

“ Binafsi niko tayari kujiunga na mfuko wa bima ya afya ili nipate hiyo kadi itakayonifanya niweze kutibiwa popote hapa Tanzania, lakini naomba tutakapolipia hiyo 76,800/= kadi zetu tuzipate mapema” Mmoja wa Wanachama wa Vyama vya Ushirika vya msingi, Bw. Magwashi Gandila

Mkoa wa Simiyu una vyama vya Ushirika Vya Msingi(AMCOS) zaidi ya 379 vyenye wanachama zaidi ya 300,000 na Jukwaa hili limeazimia wanachama wa AMCOS wakawe mabalozi wazuri kuwahamasisha wananchi kujiunga na Bima ya Afya.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akizungumza na viongozi wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS)mkoani humo katika Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi. 
Mkurugenzi mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Benard Konga akizungumza na viongozi wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS)mkoani humo, katika Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka(katikati) aizungumza na Meneja wa Wanachama kutoka NHIF(kushoto) na Mkurugenzi mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF), Benard Konga, mara baada ya kumalizika kwa Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa Serikali na viongozi wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS)mkoani Simiyu, wakifuatilia masuala mbalimbali yakiwasilishwa katika Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.
Baadhi ya viongozi wa dini, viongozi na watumishi wa Serikali na viongozi wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS)mkoani Simiyu, wakifuatilia masuala mbalimbali yakiwasilishwa katika Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.
Mwanachama wa Chama cha Ushirika cha Msingi cha Dutwa wilayani Bariadi, Bw. Lucas Ephraim akichangia hoja katika Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini akitoa taarifa ya utangulizi katika Jukwaa la Ushirika Afya Mkoa wa Simiyu lililofanyika kwa lengo la kujadili namna wanachama wa Vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) wanavyoweza kujiunga na Bima ya afya na kupewa kadi kupitia vyama vyao na kama familia, ambalo limefanyika Machi 14, mjini Bariadi.

QNET inaleta bidhaa zake za kuboresha maisha nchini Tanzania

$
0
0
· Dar es salaam inakuwa mwenyeji wa siku 2 za maonyesho ya Absolute Living (Kuishi kikamilifu) ya bidhaa QNET 

· Watu wote wanakaribishwa kuhudhuria na kuelewa bidaa za QNET, huduma na mtindo wake wa biashara. 

Tarehe 13 Machi 2019, Dar es salaam: Kampuni yenye asili ya Asia ya mauzo ya moja kwa moja QNET itaendesha maonyesho ya bidhaa na huduma zake jijini Dar es salaam siku ya tarehe 16 na 17 Machi 2019 katika ukumbi wa Mlimani City kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 1 Jioni. 

Maonyesho yenye jina la Absolute Living, (Kuishi Kikamilifu) sambamba na falsafa ya bidhaa za kampuni ya mauzo ya moja kwa moja, huwa yanafanyika kila mwaka katika nchi mbalimbali duniani kote ikiwa na lengo la kuonyesha bidhaa zake na huduma kwenye masoko mapya. Onyesho hilo pia linakuwa kama jukwaa kwa wateja na wadau wengine wanaotaka kufahamu kuhusu QNET na mtindo wake wa biashara. 

Nadharia ya Absolute Living (Kuishi Kikamilifu) inaakisi juhudi za QNET za kukuza mwenendo wa kujali afya, mtindo wa maisha wenye uwiano sahihi, ikiwa inatilia mkazo katika Afya, Ustawi na Elimu. 

Akizungumza kwenye mkutano na vyombo vya habari Meneja Mkuu wa Kanda wa QNET kwa Kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara Afrika, Biram Fall alisema kwamba, "Tunatoa aina mbalimbali za bidhaa za kiwango cha juu na huduma kwa wateja wetu kuwasaidia waweze kuishi maisha yenye uwiano sahihi, na pia kutatua tatizo la msingi kama vile elimu, ufahamu, na maendeleo binafsi kupitia program za mafunzo yetu, ambayo yanawasaidia katika safari yao ya kujiajiri mwenyewe. 

 Kutoka katika kozi za elimu kwa njia ya mtandao kama vile SELI/qLearn, mpaka katika vifurushi vya sikukuu kama vile Tripsavr, mpaka bidhaa za kuongeza nguvu kama vile Bio Disc3, virutubisho kama EDGE, na saa za mkononi kama Bernhard H. Mayer, QNET ina aina mbalimbali za kukidhi mahitaji mbalimbali ya watu. Katika kitovu cha yote haya, ni hamu yetu ya kutoa fursa ya Kuishi Kikamilifu "Absolute Living” 

Zaidi ya watu elfu mbili wanatarajiwa kuhudhuria maonyesho ya siku 2 ambayo yatakuwa na bidhaa za mfano katika onyesho, na kuonyesha namna ya matumizi ya bidhaa na faida zake kwa wateja na watumizji wa mwisho. Kwa kuongezea, wataalamu wa bidhaa na biashara watakuwepo kwa ajili ya kujibu swali lolote kutoka kwa wageni ili kuelewa vizuri ulimwengu wa QNET. 

QNET inaalika watu wote kuhudhuria onyesho hili jijini Dar es salaam na kujifunza kwanza kuhusu bidhaa, huduma na fursa za biashara. 

Maonyesho ya Dar es salaam yanafuata mfululizo wa maonyesho kama hayo yaliyofanikiwa nchini Togo, Guinea, Ivory Coast, Senegali, Burkina Faso na Cameroon mwaka jana. 

Msafara wa maonyesho utasisimama katika mji wa Kumasi, Ghana, baada ya Dar es salaam kuanzia tarehe 23 mpaka 24 Machi mwaka 2019.

NFRA KUJA NA MKAKATI WA KUWA NA MFUMO WA KIELEKTONIKI WA KUFUATILIA NA KUHIFADHI TAARIFA (COMMODITY TRACKING SYSTEM)

$
0
0
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia Zikankuba akizungumza kwa niaba ya watumishi wenzake Kwenye hafla ya kukabidhi mtambo wa kusafisha nafaka uliotolewa na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na kuzinduliwa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) Tarehe 15 Machi 2019.


Na Mathias Canal, NFRA-Dodoma

Kutokana na kukua kwa Technolojia kila siku, na matumizi ya techolojia yanaongeza ufanisi, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) umeanza na unaendelea na mkakati wa kuhakikisha kunakuwa na mfumo wa kielektroniki wa kufuatilia na kuhifadhi taarifa za Hifadhi ya Taifa ya Chakula (Commodity Tracking System). 

Lengo la kuwepo kwa mkakati huo ni kuongeza ufanisi kwa kupunguza mianya ya udanyanyifu na wizi na ili kufikia lengo hilo ifikapo mwishini mwa mwaka 2020, Mpango wa Chakula Duniani (WFP) umekubali kusaidia kupata ufadhili wa fedha na utaalamu ili kufanikisha lengo hilo. 

Hayo yamebainishwa na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bi Vumilia Zikankuba wakati akizungumza kwa niaba ya watumishi wenzake Kwenye hafla ya kukabidhi mtambo wa kusafisha nafaka uliotolewa na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na kuzinduliwa na Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb).

Alisema kuwa WFP ni mdau muhimu wa NFRA katika kuzungusha akiba ya chakula huku Utekelezaji wa mauzo ya tani 36,000 ukiwa unaendelea. 

Zikankuba alisema kuwa mpaka sasa Tani zote zimekwisha andaliwa na WFP wamekwisha kuchukua Tani 20,400 huku Tani 15,600 zikiwa zimekwisha andaliwa na zimehifadhiwa vizuri kwa ajili ya WFP kuchukua.

“Mauzo haya moja kwa maana yake ni kwamba Mkulima hasa mdogo anapata fursa ya soko la kimataifa moja kwa moja kwa kuwa NFRA hununua mazao yake moja kwa moja kutoka kwa wakulima” Alikaririwa

Bi Zikankuba alitumia mkutano huo kuujulisha ujumbe wa WFP kuwa NFRA ipo tayari na ina uwezo wa kuuza tani nyingine zaidi baada ya mkataba unaoendelea wa Tani 36,000 kukamilika. 

“Pia tupo tayari kufanya mazungumzo na WFP ili kukusanya na kuwauzia mazao mengine ya nafakai mtama kuanzia msimu ujao wa mavuno” Alisema

Aliongeza kuwa Mikakati na programu mbalimbali zinazoendeshwa na WFP zinasaidia NFRA kupata mazao yenye vigezo kupitia vikundi vya wakulima. Mfano: Katika msimu huu, kati ya vikundi vya wakulima 216 vilivyouza mahindi yao NFRA takribani vikundi 62 vilipata mafunzo ya kutunza na huhifadhi mazao ya nafaka kupitia programu ya Farm to Market Alliance ya WFP.

Shabiki wa Simba ashinda Sh123.6million za M-Bet

$
0
0
Dar es Salaam. Shabiki wa Simba na mkazi wa mkoa wa Songwe, Willy Mwakapembe Wadson ameshinda Sh 123,614,160 baada ya kubashiriki kwa usahihi jumla ya mechi 12 katika za  mchezo wa kubahatisha wa Perfect 12 unaondeshwa na kampuni ya M-Bet Tanzania.
Mwakapembe ambaye ni mfanyabiashara ndogondogo na mkulima wa Tunduma anakuwa mshindi wa tatu tokea kuanza  mwaka huu  kushinda kiasi kikubwa cha fedha ambacho amesema kitabadili maisha yake.
Washindi wengine ni Frank Kayombo  ambaye alishinda kiasi cha Sh milioni 188.4 wakati mshindi wa pili alikuwa Simon Muray aliyeshinda Sh milioni  81.
Meneja Masoko wa M-Bet, Allen  Mushi pia alisema kuwa kuna washindi wengi waliojishindia mamilioni kupitia Jackpot Bonus ya kampuni yao.
Mushi amesema kampuni yao inazidi kupata washindi na mpaka sasa jumla ya Sh milioni 500 zimetumika kuwazawadia washindi mbalimbali.
Alisema kuwa kampuni yao inazidi kuwabadili maisha Watanzania huku wakichangia pato la serikali kiasi cha Sh milioni 24.7. Alisema ili kuweza kucheza bahati nafasi hiyo unaweza kutembelea http://bit.ly/2VZCB38 ili kuanza kuanza kubet.
“M-Bet inazidi kuchanja mbuga na kuinua vipato vya Watanzania na kuchangia maendeleo ya nchi chini ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dk John Pombe Joseph Magufuli. Nawaomba Watanzania kucheza  ili kushinda zawadi za fedha,” alisema Mushi.
Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Wadson alisema kuwa alianza kubeti muda mrefu kabla ya kupata ushindi huo mnono.
Alisema kuwa hakukata tamaa pamoja na kutaniwa na marafiki zake wengi kuwa hataweza kushinda fedha nyingi zaidi ya kupoteza muda wake.
“Sikukata tamaa na kuendelea kubeti, niliamini kuwa siku moja nitapata bahati ya kushinda, nashukuru Mungu kupata kiasi hiki cha fedha na nitakaa mke wangu kupanga jinsi gani ya kuwekeza na kujiongezea kipato,” alisema Mwakapembe.
Meneja Masoko wa Kampuni ya M-Bet Tanzania, Allen Mushi (Kulia) akikabidhi mfano wa hundi, Willy Mwakapemba  (katikati) kutoka mkoa wa Songwe aliyeshinda Sh Milioni 123.7 za mchezo wa Perfect 12 wa kampuni ya M-Bet Tanzania. Anayeshuhudia ni  Kaimu Msimamizi wa Kitengo cha Michezo ya Kubahatisha, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kikodi, Ilala Philipo Haule.

TTCL YAZINDUA ENEO LAKE LA MAPOKEZI LIKIWA NA SEHEMU MAALUM YA MAONESHO YA KIHISTORIA YA MAWASILIANO NCHINI

$
0
0
Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (wa pili kulia) akikata utepe leo kuashiria uzinduzi wa eneo la mapokezi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) lililopo Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba akishiriki uzinduzi huo.

Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (wa kwanza kulia) akizungumza na wageni mara baada ya kuzinduwa eneo la mapokezi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) lililopo Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam. Anayefuata ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba akizungumza na wageni waalikwa kwenye hafla ya uzinduzi wa eneo la mapokezi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) lililopo Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu akifuatilia.
Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (wa pili kulia) akikata utepe leo kuashiria uzinduzi wa eneo la mapokezi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) lililopo Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba (kulia) akimuonesha Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu eneo maalumu la historia ya mawasiliano lililopo eneo la mapokezi mpya ya Shirika la Mawasiliano Tanzania Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam mara baada ya kuzinduliwa leo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (wa kwanza kulia) akizungumza na wageni waalikwa (hawapo pichani) mara baada ya kuzinduwa eneo la mapokezi ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) lililopo Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba.

Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (wa kwanza kulia) akisisitiza jambo kwenye uzinduzi huo.
Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (kulia) akiwamiminia shampeni baadhi ya wageni waalikwa katika uzinduzi huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba (kushoto) akimmiminia shampeni kuashiria uzinduzi wa eneo la mapokezi lililozinduliwa leo Makao Makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam leo.
Meneja Uhusiano wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Nicodemas Mushi (wa kwanza kulia) akitoa maelekezo mbalimbali katika hafla ya uzinduzi wa mapokezi hiyo ya kisasa.


SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania (TTCL) leo limezinduwa eneo la mapokezi ya shirika hilo lililopo Makao Makuu ya Shirika, jijini Dar es Salaam. Eneo hilo lililoboreshwa kwa ukarabati wa kisasa limeongezewa sehemu maalum ya maonesho na historia ya mawasiliano nchini ikiwa ni kutoa elimu zaidi kwa jamii.

Akizinduwa eneo hilo, Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu amewataka wafanyakazi wa shirika hilo kuendelea kutoa huduma bora kwa wateja ili kwenda sambamba na maboresho makubwa yanayofanywa ndani ya shirika la TTCL.

Alisema muonekano mpya wa eneo la mapokezi katika Jengo la Makao Makuu ya Shirika hilo ni kielelezo muhimu cha jinsi gani TTCL mpya inavyo wathamini wateja wake kwa kuwapa kipaombele." Tunatambua kuwa bila wao, huduma na bidhaa zetu hazitakuwa na maana yoyote wala hatuta weza kutimiza wajibu wetu kwa Umma na Taifa letu. Hii ndio sababu ya msingi inayotufanya siku zote tuwape Wateja wetu nafasi ya kwanza katika kila mipango tunayoipanga na kuitekeleza," alisema Mhandisi Nundu.

Aliwataka menejimenti na Wafanyakazi wote wa TTCL, kuongeza ubora wa Huduma zinazotolewa na Shirika na hasa Kipengele cha Huduma kwa Wateja ili kukidhi matarajio na mahitaji ya Wateja wake.Aidha aliongeza kwa mwaka 2019, TTCL Corporation imejipanga vyema kuhakikisha kuwa Huduma za shirika hilo inasambaa zaidi kote nchini huku ikisimamia ubora na unafuu wa gharama ambazo Wananchi wote wata zimudu.

"Tunakusudia kuendelea kufanya mageuzi makubwa ndani ya Shirika ili kuliwezesha kushindana kikamilifu katika Soko la Huduma za Mawasiliano nchini sambamba na kutimiza wajibu wa kimsingi wa kuwa mchangiaji muhimu katika Pato la Taifa."Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Waziri Kindamba awali akizungumza, alisema; "Tunafanya maboresho makubwa katika majengo ya Ofisi za watumishi, Majengo ya kuhifadhia Mitambo na Teknolojia pamoja na Maduka na Vituo vyetu vya Huduma kwa Wateja Nchi nzima."

"Hadi kufikia sasa, Majengo ya TTCL katika Mikoa kumi tayari yamefanyiwa ukarabati mkubwa huku Maduka na Vituo vya huduma kwa Wateja 15," aliongeza kiongozi huyo.Pamoja na hayo Bw. Kindamba alisema kukamilika kwa ukarabati katika eneo hilo la mapokezi lililofanyiwa maboresho kunaongeza uwezo wa kuwahudumia Wateja sambamba na kukabiliana na ushindani kutoka kwa Watoa huduma wengine.
Tupo tayari kuwahudumia wateja; Sehemu ya wahudumu katika eneo la mapokezi  wakiwa katika picha ya pamoja.

Sehemu ya wahudumu katika eneo la mapokezi hiyo wakionesha baadhi ya simu za zamani zilizotumiwa kipindi cha nyuma.

Picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL, Mhandisi Omari Rashid Nundu (mwenye koti) kwa baadhi ya viongozi walioshiriki uzinduzi huo.

RC MONGELA ARIDHISHWA NA MAANDALIZI KIKAO KAZI CHA MAAFISA MAWASILIANO

$
0
0
Na Ndimmyake Mwakapiso
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mwanza ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. John Mongela, imefanya ziara rasmi katika ukumbi wa BOT kukagua maandalizi ya kikao kazi cha Maofisa Mawasilino Serikali kinachotarajiwa kufungulia na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kasimu Majaliwa, Jijini humo.

Akitoa tathmini yake mara baada ya ukaguzi wa ukumbi wa mkutano huo, Mkuu wa Mkoa ameridhishwa na mandalizi yanayoratibiwa kwa pamoja na Idara ya Habari MAELEZO kwa kushirikiana na Uongozi wa Chama cha Maofisa Mawasiliano Serikalini TAGCO.

“Mnakwenda vizuri, naona kila kitu kipo vizuri na kwa maandalizi haya ni imani yangu kuwa mkutano huu utaenda vizuri na msisite kutufahamisha endapo kutakuwa na mabadiliko yoyote”.

Mapokezi ya kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, yaliongozwa na Mkurugenzi wa idara ya Habari Maelezo ambaye pia ndiye msemaji mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abasi na viongozi wa chama cha Maofisa Mawasiliano Serikalini TAGCO.

Kikao hicho ni cha siku tano kinachotarajiwa kuanza siku ya Jumatatu, Machi 18 hadi Ijumaa 22, mwaka huu kinachotarajiwa kuwakutanisha zaidi ya Maofisa Mawasiliano 300 kutoka Wizara, Mashirika ya Umma, Taasisi za Serikali, Tawala za mikoa na Serikali za mitaa.
Mkuu wa Mkoa huo Mhe. John Mongela,

KAMATI YA BUNGE YAKABIDHI HATI ZA KWA WAKILMA-LINDI

$
0
0
JOSEPH MPANGALA , NACHINGWEA LINDI

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za mitaa imekabidhi hati za Kimila za Umiliki ardhi Mia Moja{100} kwa wakazi wa kijiji cha Mbondo kilichopo Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi 

Ugawaji wa Hati hizo unakuja baada ya kujengewa Uwezo na Mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania{MKURABITA} kwa kutoa mafunzo jinsi ya kupima ardhi kwa Halmashauri ya Nachingwea kwa lengo la kuongeza thamani ardhi hizo pamoja na kuondokana na Migogoro Mbalimbali inayotokana na Mipaka.

Menyekiti wa kamati hiyo Jason Rweikiza amesema ugawaji wa Hati utawezesha wakulima kuweza kukopa katika taasisi mbalimbali za kifedha kwa lengo la kuendeleza ardhi hizo kwa kulima kilimo kitakacholeta tija na mafanikio na hivyo kujiletea maendeleo.

“Tayari taasisi za kifedha zimeanza kukubali kupokea Hati hizi hivyo wakulima wananafasi kubwa ya kuweza kuendeleza mashamba yao kwa kulima kisasa zaidi na kujiletea maendeleo”amesema Rweikiza mwenyekiti wa kamati.

Naye Mratibu wa Mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania{Mkurabita}Dkt.Seraphia Mgembe amesema kuwa Wananchii waliopokea hati wanauwezo mkubwa wa Kuondokana na Umasikini kwa Kutumia hati zao kwa kushirikiana na wawekezaji mbalimbali watakaotaka kuwekeza hasa katika zao la korosho.

“Hii hati ni htai ambayo Vyombo vya fedha na Wawekezaji wanaamini kuwa wewe ndio mmiliki halali wa Shamba hilo kama kuna mtu anataka kuwekeza kwenye shamba lako na ili ajue kuwa wewe ndio mwenye shamba lazima umuoneshe Hati hiyo na katka wakati huu wa kilimo cha kisasa cha zao la Korosho,Wanaweza wakatokea watu wengi wakitaka kulima korosho Nachingwea na ili aweze kuingia ubia na wewe lazima umuoneshe Hati’’

Koini Mwanjisi ni Mkulima wa mazao ya Korosho na mahindi katika kijijji cha Mbondo Wilayani nachingwea tayari amepima Ardhi ya Heka saba na Kupatiwa hati anasema kwa sasa ameweza kufahamu jinsi ya kupata mikopo katika taasisi za kifedha ili kweza kulima kisasa zaidi.

“Sasa nimeoneshwa milango wapi nitaingilia kuweza kupata mkopo sababu nilikuwa nalima bila ya kuwa na nguvu za ziada lakini sasa hivi nimeshaoneshwa na Mkurabita nafikiri katika mika mingine inayokuja nitakuwa juu tofauti na hatua niliyonayo sasa hivi”alisema Mwanjisi.
mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa  Jason Reikiza akimkabidhi Hatimiliki za ardhi kwa Koini Mwanjisi katika hafla ya kukabidhi Hatimiliki za kimila miamoja {100} kwa wakulima wa kijiji cha Mbodo Wilaya ya Nachingewa mkoa wa Lindi.
Kutoka Kushoto Mratibu wa Mpango wa kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania{Mkurabita}Dkt.Seraphia Mgembe wakifurahi jambo na Mbunge wa iramba Mashariki Mwigulu Nchemba mara baada ya kupokea taarifa ya Mkoa Kuhusu Urasimishaji wa Ardhi katika Mkoa wa Lindi.
Naibu waziri Ofisi ya Rais menejimenti ya Utumishi wa uma na Utawala Bora Marry Mwanjelwa wakijadili jambo na Mratibu wa Mkurabita Dkt.Seraphia Mgembe mara baada ya kumaliza kukagua Masjala ya Kijiji cha Mbondo kwa ajili ya kuhifadhi Hati za kimila za wananchi.
Naibu waziri Ofisi ya Rais menejimenti ya Utumishi wa uma na Utawala Bora Marry Mwanjelwa akijadili jambo na wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa mara baada ya kumaliza kugawa hati miliki za kimila za Mashamba kwa wakulima wa Kijiji cha Mbondo kilichopo Wilaya ya Nachingwea Mkoani Lindi.

RC Kigoma: Bodi ya Mikopo mnafanya kazi kubwa

$
0
0
*Aagiza taasisi zinazodaiwa malimbikizo kulipa mara moja 

Na Eline Maronga – HESLB, Kigoma

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali (mstaafu) Emmanuel Maganga amewaagiza waajiri wote mkoani Kigoma ambao wanadaiwa malimbikizo ya makato ya mikopo ya elimu ya juu kuhakikisha wanawasilisha fedha hizo kwa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) mara moja.

Mkuu huyo wa mkoa ametoa maagizo hayo Jumanne, Machi 12, jioni wakati akikabidhi tuzo zilizotolewa na HESLB kwa waajiri watano bora mkoani Kigoma ambao wanatekeleza matakwa ya sheria ya HESLB kwa ufanisi.

“Nawapongezeni sana Bodi ya Mikopo, mnafanya kazi kubwa sana kwa taifa letu. Lakini nimeambiwa kuna baadhi ya taasisi hapa mkoani kwangu zinawakata wafanyakazi lakini hazileti kwenu fedha za makato, nimeshaelekeza wahakikishe fedha hizo zinalipwa mara moja,” alisema Brigedia Jenerali Maganga.

Kiongozi huyo, ambaye alikua mgeni rasmi katika hafla hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya Lake Tanganyika, aliihimiza Bodi ya Mikopo kuhakikisha kila mnufaika wa mkopo ambaye hajajitokeza anasakwa na kuaSnza kurejesha.

“Akipatikana, wewe kata tu,” alisema na kuwapongeza wawakilishi wa waajiri kutoka taasisi tano ambazo ni Danish Refugee Council inayowasilisha Tshs 10.8 milioni kila mwezi kutoka kwa wanufaika 54.

Nyingine ni Norwegian Refugee Council inayowasilisha Tshs 7.3 milioni kwa mwezi kutoka kwa wanufaika 28; Diocese of Kigoma (CARITAS) yenye wanufaika tisa na inawasilisha Tshs 1.7 milioni kwa mwezi.

Nyingine ni Baba Watoto Centre for Youth and Children yenye wanufaika wanne na inayowasilisha Tshs 1.1 milioni kwa mwezi na taasisi ya Relief to Development Society (REDESO) yenye wanufaika 13 na inawasilisha Tshs 0.9 milioni kwa mwezi. 

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru alimweleza kiongozi huyo kuwa katika mwaka wa fedha 2017/2018, HESLB ilikusanya Tshs 181.4 bilioni na kuwa kutoka mkoa wa Kigoma pekee, zilikusanywa Tshs 2.66 bilioni (asilimia 1.4).

“Tunadhani tunaweza kukusanya zaidi kwa sababu tuna waajiri, wengine ni taasisi za Serikali, wanakata wanufaika lakini fedha hizo hazifiki kwetu … tumekuja kutoa tuzo lakini pia kuwahimiza waajiri sugu watimize matakwa ya sheria,” alisema Badru.

Akiwa mkoani Kigoma, Bw. Badru pia alipata fursa ya kuwasilisha mada kuhusu ‘Wajibu wa Waajiri katika Urejeshaji wa Mikopo’ kwa wajumbe wa Baraza la Ushauri la Mkoa wa Kigoma linalowajumuisha viongozi wote wakuu wa mkoa na wilaya.

Katika mada hiyo, Bw. Badru aliwakumbusha viongozi hao kuhusu wajibu wa waajiri kuhakikisha kuwa wanawasilisha kwa HESLB orodha ya waajiriwa wapya ndani ya siku 28 tangu wawaajiri kama sheria inavyoelekeza. 

“Wajibu mwingine ni kukata asilimia 15 ya mshahara ghafi wa mnufaika wa mkopo, na si chini ya hapo. Baada ya kukata, kila mwajiri anapaswa kuhakikisha anawasilisha makato hayo kwa Bodi ya Mikopo ndani ya siku 15 baada ya tarehe ya mwisho wa mwezi wa makato,” alifafanua Bw. Badru na kujibu maswali mbalimbali yaliyojitokeza.

HESLB ilianzishwa mwaka 2004 na kuanza kazi rasmi mwaka 2005 ikiwa na majukumu kadhaa, lakini makuu mawili – kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji wa kitanzania waliopata nafasi za kujiunga na taasisi za elimu ya juu; na kukusanya mikopo iliyoiva iliyotolewa na Serikali tangu mwaka 1994/1995.
 Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Bregadia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga akipokea tuzo ya Bodi ya kutambua mchango wake kwa waajiri wa Mkoa huo kutekeleza sheria ya Bodi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Abdul-Razaq Badiri akizungumza na waajiri waliotekeleza sheria ya Bodi katika kulipa mikopo ya wanufaika mkoani Kigoma
Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Bregadia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga akiwa katika picha ya pamoja Waajiri wa Mkoa huo na Watendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu

OLE SENDEKA AAGIZA UTEKELEZAJI KAMPENI YA JIONGEZE TUWAVUSHE SALAMA MKOANI NJOMBE

$
0
0
 Mary Sapali, Mratibu Wa Damu Salama Kanda ya Nyanda za Juu Kusini akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama mkoani Njombe.
Dionisia Simime, Mratibu Wa Damu Salama Halmashauri ya wilaya ya Njombe akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama mkoani Njombe.
  Dkt.Bumi Mwamasage, Mganga mkuu Wa mkoa Wa Njombe akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama mkoani Njombe.
 Mhe. Christopher Ole Sendeka, Mkuu Wa mkoa wa Njombe, wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama.
Na. Vero Ignatus.

Kampeni ya 'Jiongeze Tuwavushe Salama' imezinduliwa mkoani Njombe, ambapo Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Christopher Ole Sendeka amewataka watendaji kufanya kila wawezalo kuhakikisha kampeni hiyo inaleta tija kwa kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga pindi wanapozaliwa.

Kuzinduliwa kwa kampeni hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Serikali kwa wakuu wote wa mikoa nchini katika kuhakikisha vifo vya wajawazito na watoto wachanga vinapungua.

Kampeni hiyo ilizinduliwa Kitaifa mwaka jana mkoani Dodoma na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, kuhudhuriwa na wakuu wote wa mikoa, akiwemo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu.

Mhe. Ole Sendeka amesema kampeni ya 'Jiongeze Tuwavushe Salama' ni ya kitaifa, ikiwa chini ya Raisi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, hivyo watendaji wajipange kuhakikisha malengo yanafikiwa.

"Naagiza Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Njombe, Makatibu Tawala na Wakurugenzi kuhakikisha hatua za kuzuia vifo, ikiwemo kutoa huduma za kitaalamu kwa wakati na kuhakikisha vifaa tiba vinapatikana katika vituo vya Afya," alisema Ole Sendeka.

Amesema serikali inafanya kila iwezalo kuhakikisha mama wajawazito wanapatiwa ushauri, dawa, kuanzia kliniki hadi pale kujifungua salama

"Mhe Dkt. Magufuli, kwa kuwajali wananchi wake, ametupatia zaidi ya bilioni 3 ili tujenge vituo vya afya katika mkoa wetu, Wakuu wa Wilaya katembelea maeneo ya ujenzi kila mara ili kuhakikisha ujenzi sahihi, kwa matumizi sahihi ya fedha unafanyika," alisema Ole Sendeka. 

Dkt. Bumi Mwamasage ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Dkt. Bumi amesema uwajibikaji wa kuhakikisha mama wajawazito wanajifungua salama unapaswa kuanzia katika ngazi ya familia.

"Baba na wana familia wanalazimika kuhakikisha mama anahudhuria kliniki ili apate elimu ya ujauzito wake na umuhimu wa chanjo kwa ajili ya kujilinda yeye na mtoto atakayemzaa.

Dkt. Bumi amesema Kampeni hiyo ni ya mwaka mmoja katika mpango wa 'Life Plan' wenye lengo la kuhakikisha hakuna tena vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga, hivyo inabidi jamii yote ishiriki elimu ya kutosha itolewe katika kulikabili tatizo hilo.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa iliahidi kuchangia shilingi 500,000 Mkuu wa Wilaya 100,000 kila Mkurugenzi, Wenyeviti wa halmashauri Waganga Wakuu wakiahidi kutoa 50,000 ikiwa sehemu ya kuchangia upatikanaji wa Damu Salama wakati wa mama anapojifungua na kutokwa damu nyingi ambao miongoni mwao hupoteza maisha

Kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama  inatekelezwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Mashirika yasiyo ya kiserikali ikiwemo UNICEF.

Mwisho

Matukio mbalimbali wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama mkoani Njombe.




Viewing all 46397 articles
Browse latest View live




Latest Images