Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEBRUARI 12,2019


DC MURO ANUSURU WANANCHI ZAIDI YA 260 ARUMERU

$
0
0
Mkuu wa Wilaya huyo Ndugu Jerry Muro akizsisikiliza changamoto za
Wananchi zaidi ya 260 katika kata ya bwawani Halmashauri ya Arusha , wilayani Arumeru Mkoani Arusha waliokuwa kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko kufuatia nyumba zao kuanza kutitia chini ya Ardhi .Mkuu wa Wilaya huyo Ndugu Jerry Muro akizsisikiliza changamoto za
Wananchi zaidi ya 260 katika kata ya bwawani Halmashauri ya Arusha , wilayani Arumeru Mkoani Arusha waliokuwa kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko kufuatia nyumba zao kuanza kutitia chini ya Ardhi .Wananchi zaidi ya 260 katika kata ya bwawani Halmashauri ya Arusha , wilayani Arumeru Mkoani Arusha waliokuwa kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko ambapo zaidi ya nyumba 100 zilianza kutitia chini ya ardhi wamesaidiwa na Mkuu wa Wilaya huyo Ndugu Jerry Muro kutolewa katika makazi yao ya awali ambayo yalikuwa hatarishi na kupelekwa katika maeneo mengine mazuri na Salama .

Wakizungumza katika ziara maalumu ya Mkuu wa wilaya Hiyo Ndugu Jerry Muro,wananchi hao wameeleza adha wanayokumbana nayo katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuishi kwenye nyumba ambazo kwasasa ni kama vibanda kutokana na kutitia kwa sababu ya mafuriko, wamesema kuwa wapo katika hatari kubwa na kuiomba serikali kuwatafutia namna ya kuwahamisha katika maeneo hayo

Kufuatia kilio cha wananchi hao ambao wanaishi katika shamba la mwekezaji Lusy Estate ambaye anaishi katika eneo hilo kwa ajili ya kilimo cha mkonge,Mwenyekiti wa ulinzi na usalama katika wilaya hiyo ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akatoa agizo la kuhama kwa wananchi hao ndani ya juma moja ili kuzinusuru familia zao.

"Familia hizi ambazo zinaishi katika eneo hili,ni waajiriwa katika shamba la Lus estate kwa ajili ya Kilimo cha Mkonge,ambapo wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya mafuriko huku wengine wakilazimika kuyakimbia makazi yao ,ambapo sasa huenda wakanusurika kutokana na agizo hilo la mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama.",alisema DC Muro.

 Mkuu wa Wilaya huyo Ndugu Jerry Muro akizsisikiliza changamoto za
Wananchi zaidi ya 260 katika kata ya bwawani Halmashauri ya Arusha , wilayani Arumeru Mkoani Arusha waliokuwa kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko kufuatia nyumba zao kuanza kutitia chini ya Ardhi .
  Mkuu wa Wilaya huyo Ndugu Jerry Muro akikagua baadhi nyumba  za
Wananchi zaidi ya 260 katika kata ya bwawani Halmashauri ya Arusha , wilayani Arumeru Mkoani Arusha zilizopo kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko kufuatia nyumba zao kuanza kutitia chini ya Ardhi .
 Mkuu wa Wilaya huyo Ndugu Jerry Muro akizungumza na baadhi ya Wananchi zaidi ya 260 katika kata ya bwawani Halmashauri ya Arusha , wilayani Arumeru Mkoani Arusha waliokuwa kwenye hatari ya kusombwa na mafuriko kufuatia nyumba zao kuanza kutitia chini ya Ardhi .

NAIBU WAZIRI AWESO AIPONGEZA IRUWASA KWA KAZI NZURI

$
0
0

Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Iringa (IRUWASA), Gilbert Kayange akiwaongoza Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela na Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso wakati wakikagua Chanzo cha Maji cha Ndyuka kinachohudumia wakazi wa Manispaa ya Mji wa Iringa, mkoani Iringa.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (kushoto) akiteta na Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (katikati) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Iringa (IRUWASA), Gilbert Kayange katika Chanzo na Mtambo wa Kutibu Maji, Ndyuka.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akipokea maelezo kutoka Mhaidrolojia wa Bodi ya Maji ya Bonde la Mto Rufiji, David Munkyala pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela (kushoto) katika sehemu ya kupima wingi wa maji cha Ndyuka katika Mkoa wa Iringa.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela wakati akikagua ujenzi wa ofisi za Bodi ya Bonde la Maji la Rufiji katika Manispaa ya Mji wa Iringa,mkoani Iringa.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akifungua maji kwenye mradi wa Ulonge alipofika kuukagua akiwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela mkoani Iringa.Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso ameipongeza Mamlaka ya Maji ya mjini Iringa (IRUWASA) kwa kazi nzuri inayofanya katika kutoa huduma ya majisafi kwa manispaa ya mji wa Iringa kwa asilimia 96.


Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso ameipongeza Mamlaka ya Maji ya mjini Iringa (IRUWASA) kwa kazi nzuri inayofanya katika kutoa huduma ya majisafi kwa manispaa ya mji wa Iringa kwa asilimia 96.

Naibu Waziri Aweso ametoa pongezi hizo wakati alipokua akizungumza na watumishi wa mamlaka hiyo mara baada ya kujionea miradi inayotekelezwa na mamlaka hiyo wakati alipokuwa katika ziara yake ya kikazi katika manispaa ya mji wa Iringa leo.

''IRUWASA ni moja ya mamlaka tunazojivunia kama wizara kutokana na kazi yenu nzuri na mimi binafsi nimejionea jambo hili kwa kufika hapa, hii inatokana na uongozi mzuri wa Mkuregenzi Mtendaji na Bodi yenu, pamoja na watumishi mlio nao'', amesema Aweso.

''Mmepiga hatua kubwa kiteknolojia kwa matumizi ya mita za kulipia kabla ya matumizi (prepaid meters, kukusanya madeni kutoka kwa wateja waliokuwa wadaiwa sugu, teknolojia ya ukusanyaji mapato na kuwaunganishia wateja wapya huduma miongoni kazi nzuri mnazozifanya'', amesema Aweso.

Aidha, Naibu Waziri Aweso ameitaka mamlaka hiyo kuongeza nguvu katika ujenzi wa mfumo wa majitaka ambao umefikia asilimia 40 na kufikisha huduma ya maji ya uhakika katika eneo la Nduli kwa kushirikiana na manispaa kwa kuwa bado huduma hiyo ni changamoto kwa wakazi wa eneo hilo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa IRUWASA, Gilbert Kayange amesema mpaka sasa wameweza kufunga prepaid meters 1857 tangu mwaka 2016 na kupunguza madeni kwa taasisi za Serikali kwa asilimia 30.

Kayange ameongeza kuwa wameweza kupunguza tatizo la upotevu wa maji mpaka kufikia asilimia 24.5 na wamejipanga kufanikisha zoezi la kupeleka maji katika eneo la Nduli kwa lengo la kufikisha asilimia 100 ya huduma ya maji kwa manispaa hiyo.

IRUWASA imekuwa ni mamlaka ya mfano kwa upande wa matumizi ya prepaid meters kwa mafanikio na immekuwa ni sehemu ya mamlaka nyingine za maji nchini katika kujifunza kuhusiana na matumizi ya mita hizo.

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Maji.


MAMILIONI YA WATAZANIA WALIOKOSA MATUMAINI YA KUPONA MAGONJWA MBALIMBALI,SASA KUPATA TUMAINI JIPYA

$
0
0

Picha ya pamoja.
Mwenyekiti wa IPP Dkt.Reginald Mengi akizungumza na wadau mbalimbali katika mkutano wa kimataifa wa wataalamu wa tiba za magonjwa ya binadamu uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza katika mkutano wa kimataifa wa wataalamu wa tiba za magonjwa ya binadamu uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (kushoto) akiteta jambo na Mwenyekiti wa IPP Dkt.Reginald Mengi jana jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akisalimiana na wadau mbalimbali  katika mkutano wa kimataifa wa wataalamu wa tiba za magonjwa ya binadamu uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)

 
 
MAMILIONI ya watu waliokosa matumaini ya kupona magonjwa mbalimbali hapa nchini, ambayo yaliaminika kuwa hayaponi kwa tiba ya kawaida sasa watapata tumaini jipya kufuatia ujio wa maabara ya kisasa ya tiba inayotumia teknolojia ya seli shina 'Stem Cell'.

Kwa teknolojia hiyo mpya, ambayo inatumia chembechembe za seli za mwanadamu kutibu kiungo chochote katika mwili husika, inatajwa kuwa na uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa mpaka yasiyoambukiza yakiwemo saratani zote, utindio wa ubongo, seli mundu, kisukari, ualbino na kupooza.

Akizungumza kwenye mkutano wa kwanza wa kimataifa wa wataalamu wa tiba za magonjwa ya binadamu jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa IPP, Dk. Reginald Mengi, alibainisha tiba hiyo ya seli shina ina uwezo mkubwa na tayari imethibitika duniani kumrudisha mtu aliyefika hatua ya uzee kuwa kijana mwenye afya njema.

Dk. Mengi kupitia kampuni yake ya IPP - Utafiti, Teknolojia na Ugunduzi, akishirikiana na wataalamu mbalimbali duniani, amesema ataanzisha maabara hiyo jijini Dar es Salaam, ambapo hatua iliyofikiwa mpaka sasa ni upatikanaji wa vibali kutoka serikalini.

Alisema kuanzishwa kwa maabara hiyo hakuna maana kwamba anapingana na uumbaji wa Mungu kuwa ni lazima binadamu afe, lakini lengo ni kuhakikisha wale wanaopitia maumivu na tabu kubwa kutokana na kukosa tiba ya magonjwa yanayowasumbua yakiwemo yanayotokana na umri mkubwa wanapata tiba hapa hapa nchini.

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, alisema serikali haina tatizo juu ya hilo, kwa sababu ni maendeleo makubwa kwenye sekta ya afya nchini na kumtoa hofu Dk. Mengi kuwa vibali hivyo vitapatikana haraka.

Lakini pia alisema kuwa serikali imetumia nguvu kubwa kuboresha sekta ya afya kwenye uboreshaji miundombinu na kuanzisha tiba mpya ambazo awali hazikuwepo hapa nchini ikiwemo upandikizi wa figo, uongezaji wa bajeti, upandikizi wa ini na ute wa mifupa 'Bone Marrow'.

Alisema tiba ya seli shina ni ya kisasa, ikiwa na uwezo mkubwa wa kutibu mtu kutokana na seli zake mwenyewe lakini alitahadharisha kuwa kwenye kila hatua ya tiba hiyo lazima maadili yazingatiwe na miiko ya kitabibu kama zinavyoelekeza kanuni za kada hiyo kote duniani.

Dk. Ndugulile alisema serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi kwenye uboreshaji wa sekta ya afya ili kuhakikisha kunakuwa na kasi kubwa ya maendeleo kwenye eneo hilo lililo uti wa mgongo wa maendeleo ya sekta zingine zinazotengemea nguvu kazi ya binadamu kwenye ukuaji wake.

Kwa upande wake Dk. Michael Magoti ambaye ni Mratibu mipango wa IPP Utafiti, Teknolojia na Uvumbuzi, alisema mkutano huo wa kwanza wa kimataifa umejumuisha wadau wa tiba kutokana nchi za Marekani, Australia, India, Thailand, Vietnam na Egypt.

Alisema pamoja na maabara ya utafiti, Dk. Mengi kupitia kampuni yake ya IPP Utafiti, Teknolojia na Uvumbuzi ana mpango wa kuanzisha kliniki ya tiba kwa watoto wenye utindio wa ubongo ambayo itasaidia sehemu kubwa ya watoto wanaozaliwa na matatizo ya kiakili kwa kutumia matibabu ya seli shina hapa nchini.

Naye Profesa Dk. Kampon Sriwatanakul, raia wa Thailand ambaye pia ni mtaalamu mshauri wa teknolojia hiyo ya tiba kutoka IPP, alisema amejitoa kuja Tanzania kumsaidia Dk. Mengi kufikia ndoto yake ya kuwafikia mamilioni ya watu wenye shida za kiafya ambazo tayari wamekata tamaa ya kupona.

Alisema kupitia teknolojia ya tiba ya seli shina, wana uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa mengi sugu ambayo kwa tiba za kawaida imeaminika kuwa hayawezekani kwenye hospitali nyingi kubwa zikiwemo zile za kimataifa zisizotumia teknolojia hiyo ya kisasa ya tiba.

Katika mkutano huo, jumla ya mada tisa zinazohusiana na tiba ya seli shina ziliwasilishwa na wataalamu waliobobea kwenye kada ya afya kutoka nchi kadhaa za Ulaya, Marekani na Asia.

RC GAMBO AITAKA KAMPUNI YA UWINDAJI YA GREEN MILES SAFARI KURIPOTI MBELE YA KAMATI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akizungumza wakati alipoagiza mmiliki wa Kitalu cha Kampuni ya Uwindaji ya Green Miles Safaris Ltd, kuripoti mbele ya kamati aliyoiunda ili kueleza sakata la kuuawa Twiga katika kitalu chake na kushindwa kuvilipa vijiji 23 kiasi cha sh 329 milioni ,wananchi wameipongeza serikali kuingia kati mgogoro huo.
Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido wakiwa katika mkutano huo wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Mkuu wa wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe akizungumza na kusema amekuwa akipokea vitisho kutoka sehemu mbalimbali kutokana na kuigusa kampuni hiyo lakini alisisitiza kusimamia sheria pamoja na maagizo aliyopewa na Rais John Magufuli katika kutetea wanyonge na maagizo ya Rc Gambo juu ya kutatua shida za wananchi wake hivyo atasimama kidete kuhakikisha haki inatendeka.


Mwandishi Wetu,Longido.

Wakati Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akiagiza mmiliki wa Kitalu cha Kampuni ya Uwindaji ya Green Miles Safaris Ltd, kuripoti mbele ya kamati aliyoiunda ili kueleza sakata la kuuawa Twiga katika kitalu chake na kushindwa kuvilipa vijiji 23 kiasi cha sh 329 milioni ,wananchi wameipongeza serikali kuingia kati mgogoro huo.

Mkuu huyo wa mkoa akizungumza katika wilaya ya Karatu, katika hafla yakabidhi vitambulisho 10,000 kwa wafanyabiashara wadogo, alisema kampuni hiyo imekuwa ikikaidi maagizo ya serikali wilaya ya Longido kulipa madai ya vijiji jambo ambalo halikubaliki.

Gambo aliagiza viongozi wa kampuni hiyo wajitokeze mahali popote walipo ili kwenda katika tume maalum aliyounda inayoongozwa na vyombo vya ulinzi na usalama kubaini kwanini mauaji ya Twiga yameshamiri zaidi katika eneo la kitalu hicho na kwanini hajalipa kodi za vijiji kwaajili ya maendeleo zaidi ya sh, milioni 329.

"Hii kampuni wanamaneno mengi sana nawaambia hivi serikali ya awamu hii haina maneno inasimamia sheria popote walipo wajitokeze katika kamati ili kubaini mambo ambayo tumegundua awali na waache kutisha watu taarifa zao tunazo na nakwambia DC Mwaisumbe nipo nyuma yako katika hili simamia sheria na kanuni zilizopo hakuna mtu yoyote kukatisha kwa jambo lolote lazima tuchukue hatua "

Naye Mkuu wa wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe alisema amepata matishio kutoka sehemu mbalimbali kutokana na kuigusa kampuni hiyo lakini alisisitiza kusimamia sheria pamoja na maagizo aliyopewa na Rais John Magufuli katika kutetea wanyonge na maagizo ya Rc Gambo juu ya kutatua shida za wananchi wake hivyo atasimama kidete kuhakikisha haki inatendeka. 

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Longido, Jumaa Mhina alisisitiza kampuni hiyo kulipa deni wanalodaiwa na vijiji hivyo sambamba na halmashauuri kulipwa malimbikizo ya madeni wanayoidai kampuni hiyo.
"Tumekwisha andika barua Wizara ya Maliasili na Utalii ili tulipwe lakini pia kuhakikisha vijiji vinalipwa" alisema


Wananchi Longido waipongeza Serikali.

Wakizungumzia maamuzi ya mkuu wa mkoa,baadhi ya wakazi wa Longido wamepongeza serikali kwa kuingilia kati mgogoro wao na mwekezaji huyo.
Julius Laizer mkazi wa Kutubeine alisema wanataka mwekezaji ambaye atatatua kero za wananchi katika wilaya hiyo na sio kuwa sehemu ya migogoro.

"Tunataka wanyamapori watusaidie kupata maendeleo hivyo tunaomba serikali kuingilia kati kudhibiti matukio ya ujangili" alisema
Peter Maleko kazi wa Mundarara alisema wanaomba serikali isaidie walipwe haki zao kutoka kwa mwekezaji kampuni ya Green Miles kwani wanadaia zaidi ya sh 11 milioni kila kijiji.


"Tunashukuru mkoa umefanyakazi lakini bado tunaomba tulipwe haki zetu" alisema.Hivi karibuni,Mkuu huyo wa mkoa, aliunda kamati maalum kwaajili ya kuchunguza mauaji ya Twiga katika wilaya ya Longido ambapo alibaini mambo mbalimbali ikiwemo Twiga 35 kuuawa kwakipindi cha mwaka miwili katika matukio mbalimbali ikiwemo Twiga 25 kuuliwa kutokana na ujangili.

T-Pesa kuanzisha mfumo wa malipo kwa kutumia card

$
0
0
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakisaini leo jijini Dar es Salaam makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakisaini makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakibadilishana nakala za makubaliano yao mara baada ya kusaini leo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakibadilishana nakala za makubaliano yao mara baada ya kusaini leo jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (wa pili kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (wa pili kushoto) wakionesha nakala za makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. Wanaoshuhudia kulia na kushoto ni wanasheria wa pande zote. 
Mkuu wa Huduma za T- PESA, Moses Alponce (kulia) pamoja na Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee (kushoto) wakifurahiya jambo mara baada ya kusaini leo jijini Dar es Salaam makubaliano ya mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card) utakaotumika kulipia huduma mbalimbali nchini Tanzania. 
Picha ya pamoja ya viongozi waandamizi wa kampuni zote mara baada ya hafla ya kusaini mkataba huo wa ushirikiano kibiashara. 



SHIRIKA la Mawasiliano Tanzania TTCL Corporation, kupitia mtandao wake wa huduma za kifedha wa T-PESA pamoja na wadau wa kibiashara, Kampuni tatu kutoka nchini Korea zimesaini mradi wa kutengeneza mfumo wa malipo kwa kutumia kadi (T Card).

Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Makao Makuu ya TTCL leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Huduma za T- PESA Ndugu Moses Alponce, alisema mfumo huo unaotumia teknolojia za kisasa ni matokeo ya utafiti uliofanywa na kuonesha mahitaji makubwa ya huduma za malipo yasiyotumia fedha tasilimu. 

Aidha aliongeza kuwa kukamilika kwa mfumo huo kutarahisisha shughuli za kibiashara na kuimarisha uwezo wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), katika kukusanya kikamilifu kodi za Serikali kutoka kila miamala itakayofanyika, sambamba na kuongeza ufanisi katika biashara na shughuli nyingine za kiuchumi.

Mfumo huo unaotekelezwa na T-Pesa kwa kushirikiana na wadau wake kibiashara kutoka Jamhuri ya watu wa Korea katika muunganiko wa Kampuni tatu, ambazo ni PayLink Korea, KEH Hana Card pamoja na ATECT & Company unakuwa wa kwanza kuletwa na huduma za fedha kwa kutumia simu za mikononi nchini Tanzania.

"..Kampuni hizi zitashirikiana na T PESA katika zoezi la kuandaa, kupanga na kutengeneza Mfumo wa kadi za NFC na POS Cashless Ecosystem," alisema Alponce.Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kampuni ya PayLink ya Korea, MoonKyu Lee akiwakilisha kampuni hizo alisema kuingia kwa ushirikiano katika mfumo huo utaongeza uwazi katika miamala ya kifedha jambo ambalo litaongeza mapato ya kodi kwenye mifumo ya malipo nchini na kuleta maendeleo.

Ikiwa sasa ni takribani miaka miwili tangu kuanzishwa kwake, T PESA imekuwa na mchango mkubwa katika huduma za Fedha mtandao Nchini, ambapo kwa mujibu wa ripoti ya TCRA toleo la mwaka 2019, T PESA ni moja ya huduma zinazokua kwa kasi kubwa ikiwa na Mawakala 10,000, wateja laki 320,000 wanaozungusha miamala ya takribani Tsh Bilioni 4.


DKT. NDUGULILE AKASIRISHWA NA KASI YA UJENZI WA MAABARA YA AFYA YA JAMII

$
0
0
Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akiongoza katika ziara ya kukagua ujenzi wa jengo la Maabara ngazi ya tatu yenye uwezo wa kuchukua vipimo vya magonjwa hatari Duniani kama Virusi vya Ebola, Mabag n.k, leo katika eneo la Mabibo jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akifanya ukaguzi wa chumba kwa chumba ili kujidhisha na maendeleo ya ujenzi wa jengo la Maabara ngazi ya tatu yenye uwezo wa kuchukua vipimo vya magonjwa hatari Duniani kama Virusi vya Ebola, Mabag n.k, unaojengwa katika eneo la Mabibo jijini Dar es salaam.
Muonekano wa jengo la Maabara ngazi ya tatu lenye uwezo wa kuchukua vipimo vya magonjwa hatari Duniani kama Virusi vya Ebola, Mabag n.k, jengo hilo lililokamilika kwa 90%, linajengwa katika eneo la Mabibo jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo, wakati akiongea na Mkandarasi pindi alipofanya ziara ya ukaguzi wa ujenzi wa jengo la Maabara ngazi ya tatu yenye uwezo wa kuchukua vipimo vya magonjwa hatari Duniani kama Virusi vya Ebola, Mabag n.k, unaojengwa katika eneo la Mabibo jijini Dar es salaam.
Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri Wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile baada ya ukaguzi wa ujenzi wa jengo la Maabara ngazi ya tatu yenye uwezo wa kuchukua vipimo vya magonjwa hatari Duniani kama Virusi vya Ebola, Mabag n.k, unaojengwa katika eneo la Mabibo jijini Dar es salaam.



Na WAMJW – DSM

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amekasirishwa na kasi ndogo ya ujenzi wa Maabara ya Afya ya Jamii ngazi ya tatu, inayoshughurikia magonjwa hatari ya mlipuko kama vile Ebola, Mabag, Kipindupindu hali inayopelekea kuchelewesha utoaji wa huduma hizo kwa Wananchi.

Hayo yamejiri leo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi wa jengo hilo lililo eneo la Mabibo jijini Dar es salaam ili kujidhihirishia thamani ya pesa zilizotumika na kiasi cha ujenzi wa jengo hilo ulipofika.Dkt. Ndugulile amesema kuwa haoni sababu ya msingi iliyopelekea kuchelewa kukamilika kwa ujenzi wa Maabara hiyo kwani fedha zote zipo, hivyo kukasirishwa kwa kasi ndogo ya ujenzi wa Maabara hiyo ulioanza tangu mwaka 2016.

” Nitoe asikitiko yangu kwamba, kazi hii imechukua muda mrefu sana, tangia 2016, wenzetu waliozipata fedha hizi wengi wamekwisha kamilisha kazi zao, sisi Tanzania bado tunasua sua, kibong’oto, Temeke, Mawenzi na hapa, najambo linalonisikitisha sana fedha tunazo” alisema Dkt. Ndugulile.pia, Dkt. Ndugulile amesema kuwa ujenzi wa Maabara hiyo utaisaidia Serikali kuokoa kiasi kikubwa cha fedha ambacho inakipeleka nje ya nchi kwaajili yakupima sampuli za magonjwa hayo, hivyo kukamilika kwa Maabara hiyo kutaifanya Tanzania kuwa moja kati ya nchi chache barani Afrika inayotoa huduma hizo.

Aidha, Dkt Ndugulile ameonekana kutoridhishwa na usimamizi wa ujenzi wa Maabara hiyo, hivyo kutoa onyo katika matumizi ya fedha za ujenzi wa Maabara hiyo, hii ni kutokana na kufanya marekebisho ya mara kwa mara wakati ramani ya jengo hilo ipo.“Fedha tunazo nyingi kupita maelezo, na ndiomaana mnaishia kuzitumia vibaya, matumizi ya hovyo yanapitishwa kwa haraka sana, lakini matumizi ya msingi yanasuasua, sasa niombe kwa niamba ya Kazi zote, hizi fedha tuliziomba kwa matumizi mahsusi kujenga hizi Maabara na isolation centers, naomba nitakaporudi haya tuliokubaliana mtimize” alisema Dkt Ndugulile

Kwa upande mwingie Dkt. Ndugulile amewata viongozi wa Wizara ya Afya kutokuwa kikwazo katika taratibu za ujenzi wa Maabara hiyo, ili kuepusha lawama kutoka kwa Wakandarasi, jambo litalosaidia katika kasi ya ujenzi wa Maabara hiyo.“Taratibu za ndani, sisi kama Wizara naomba zisiwe kikwazo kwakweli, kwasababu gharama za mradi mnazijua, uendeshaji tunaujua, na tulikuwa tunazifahamu, fedha tunazo zakutosha, mzipitishe katika taratibu zake zote ili hawa Wakandarasi wasije kutulalamikia” Alisema Dkt. Ndugulile

MAGAZETI YA LEO JUMATANO FERBRUARI 13,2019


Wagonjwa 12 wafanyiwa uchunguzi wa mishipa ya moyo kupitia mtambo wa Cathlab uliofungwa katika Hospitali ya Benjamini Mkapa jijini Dodoma

$
0
0
 
Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakimfanyia mgonjwa uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (Coronary Angiogram) kwa kutumia mtambo wa Cathlab. Jumla ya wagonjwa 12 wamefanyiwa uchunguzi katika mtambo huo ambapo watano kati yao wamekutwa na matatizo mmoja atatumia dawa na wengine wanne watazibuliwa mishipa ya moyo iliyoziba (Percutaneous Coronary Intervention – PCI).
Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakimfanyia mgonjwa uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (Coronary Angiogram) kwa kutumia mtambo wa Cathlab. Jumla ya wagonjwa 12 wamefanyiwa uchunguzi katika mtambo huo ambapo watano kati yao wamekutwa na matatizo mmoja atatumia dawa na wengine wanne watazibuliwa mishipa ya moyo iliyoziba (Percutaneous Coronary Intervention – PCI).

Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakimfanyia mgonjwa uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (Coronary Angiogram) kwa kutumia mtambo wa Cathlab. Jumla ya wagonjwa 12 wamefanyiwa uchunguzi katika mtambo huo ambapo watano kati yao wamekutwa na matatizo mmoja atatumia dawa na wengine wanne watazibuliwa mishipa ya moyo iliyoziba (Percutaneous Coronary Intervention – PCI).


Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kumaliza kumfanyia uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo (coronary angiogram) mgonjwa wa 12 kwa kutumia mtambo wa Cathlab ambao umezinduliwa leo katika Hospitali ya BMH.
Madaktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) ya jijini Dodoma wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzinduliwa kwa mtambo wa Cathlab ambao ni maabara ya uchunguzi na tiba ya mishipa ya damu ya moyo (coronary angiogram).

………………………………………………………………………………………………………

Na Mwandishi Maalum, Dodoma

Jumla ya wagonjwa 12 wamefanyiwa uchunguzi wa kuangalia jinsi mishipa ya damu ya moyo inavyofanya kazi kupitia mtambo wa Cathlab ambao ni maabara ya uchunguzi na tiba ya mishipa ya damu ya moyo.

Uchunguzi huo ambao umefanyika kwa siku mbili umefanywa na madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) iliyopo jijini Dodoma.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi alisema kati ya wagonjwa 12 waliofanyiwa uchunguzi watano wamekutwa na matatizo ya mishipa ya damu kutopitisha damu vizuri, wanne wanahitaji matibabu ya kuzibuliwa mishipa ya damu na mmoja atatumia dawa.

“Tumefanya uchunguzi kwa wagonjwa 12 , tisa wanamatatizo madogo ambayo hayahitaji matibabu makubwa na wanne wanahitaji matibabu makubwa ambayo ni kuzibuliwa kwa mishipa ya damu na mmoja atatumia dawa”, alisema Prof. Janabi .

Kwa upande wa wagonjwa waliofanyiwa uchunguzi waliishukuru Serikali kwa kusogeza huduma hiyo katika mkoa wa Dodoma ambapo wagonjwa wenye matatizo kama hayo wataweza kupata huduma hiyo katika Hospitali ya Benjamini Mkapa badala ya kusafiri kwenda mkoani Dar es Salaam kufuata huduma hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Mwalimu Mstaafu Simon Mesomapya ambaye ni mkazi wa kijiji cha Mtanana wilayani Kongwa alisema alianza kusumbuliwa na maradhi ya moyo mwaka 2016 na kutibiwa katika Hospitali mbalimbali ambapo mwaka huu alipewa rufaa ya kutibiwa BMH kwa uchunguzi zaidi.

“Kupatikana kwa huduma hii hapa BMH itapunguza gharama za kusafiri kwenda Dar es Salaam au nje ya nchi pia Dodoma ni kati kati ya nchi ni rahisi kwa wananchi wa mikoa jirani kupata huduma hiyo”, alisema Mwalimu Mesomapya.

Aliiomba Serikali iendelee kuboresha huduma hiyo ili wananchi wenye matatizo ya moyo waweze kufurahia huduma hiyo,

Mtambo huo wa kisasa wa Cathlab ambao ni maabara ya uchunguzi na matibabu ya mishipa ya moyo unauwezo pia wa kuchunguza mishipa ya damu ya mikono, miguu na kichwa.

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA

$
0
0


Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 23:45 usiku huko eneo la Soweto, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lilikamata gari lenye namba za usajili T.937 CKD aina Toyota Saloon likiwa na vipodozi vya aina mbalimbali vilivyopigwa marufuku nchini. Vipodozi vilivyokamatwa ni:-
  1. Extra Clair katoni nane [08].
  2. Perfect White katoni mbili [02].
  3. Epiderm Cream dazani arobaini na saba [47]
  4. Diproson dazani ishirini na moja [21]
  5. Coco Pulp katoni mbili [02]
  6. Carolight katoni sita [06]
  7. Citro Light katoni tatu [03]
  8. Teint Clair katoni mbili [02]
  9. Top Lemon katoni nne [04]
  10. Clair Men katoni mbili [02]
  11. Princes Clair katoni nne [04]
  12. Movet boksi mbili [02]
  13. Miki Clair katoni mbili [02]
  14. Top Clair Plus katoni moja [01]
  15. Collagen formula boksi mbili [02]
  16. Mont Clair boksi mbili [02]
  17. Movet tube pcs mbili [02]
  18. Movet boksi mbili [02]
  19. Cocoderm boksi moja [01]
KUPATIKANA NA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU NCHINI.
Mnamo tarehe 12.02.2019 majira ya saa 07:15 asubuhi huko eneo la Check Point Igurusi, Kata ya Igurusi, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali na Mkoa wa Mbeya, Polisi wakiwa doria walimkamata SAID IDDY @ MOHAMED [32] Dereva na Mkazi wa Mbadula Arusha akiendesha gari lenye namba za usajili T.298 DCH aina ya Scania Basi la abiria – HAJI’s akitokea Mbeya kuelekea Arusha akiwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku nchini aina mbalimbali.
Vipodozi vilivyokamatwa ni:-
  1. Diana Boksi mbili [02].
  2. White Max Boksi tatu [03].
  3. Secret White Location Boksi moja [01]
Upelelezi unaendelea na mara baada ya kukamilika, mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani.
KUPATIKANA NA SILAHA [GOBORE] BILA KIBALI.
Mnamo tarehe 11.02.2019 majira ya saa 14:35 mchana huko eneo la Makasini – Uyole, Kata ya Uyole, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya. Askari Polisi walimkamata PAUL ABRICK [66] Mkazi wa Mtaa wa Nyahoro – Uyole akiwa na silaha Gobore aina ya Tower yenye namba 1878 bila kibali. Upelelezi unaendelea.

DC NJOMBE AWAAGIZA WATENDAJI WA WILAYA KUBANDUA MABANGO YA WAGANGA WA KIENYEJI MITAANI

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Ruth Msafiri akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Mkoa Ulinzi kwa Mwanamke na Mtoto wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika mjini Njombe.
Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Dkt. Bumi Mwamasage akieleza lengo la Kamati ya Ulinzi kwa Mwanamke na Mtoto kukutana wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika mjini Njombe.
Kiongozi wa Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Hanifa Selengu akieleza lengo la timu hiyo kwenda mkoani Njombe wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika mjini Njombe.
Mwanasheria kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bw. Denis Bashaka akileza namna Sheri ya uchawi sura ya 18 ya Mwaka 2002 inavyozuia vitendo vya upigaji ramli na kazi za uganga wa kienyeji wakati wa kikao cha Kamati ya Ulinzi kwa Mwanamke na Mtoto kilichokutana Mjini Njombe

Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Mwanaisha Moyo akielezea umuhimu wa Kamati hiyo kutoa huduma kwa wahanga wa vitendo vya ukatili kwa haraka wakati wa kikao cha Kamati ya Ulinzi kwa Mwanamke na Mtoto kilichokutana Mjini Njombe.
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Mkoa wa Njombe ya Ulinzi kwa Mwanamke na Mtoto wakiongozwwa na Mkuu waWilaya ya Njombe kwa niaba ya Mkuu wa mkoa Ruth Msafiri (wa pili kulia) wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika mjini Njombe.

Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

………………………..

Na Mwandishi Wetu Njombe

Mkuu wa Wilaya ya Njombe Ruth Msafiri amemuagiza Katibu Tawala wa Wilaya hiyo na watendaji wote kuzunguka katika mitaa kubandua mabango yote yanayotangaza huduma za waganga wa kienyeji ambao wanafanya kazi kinyume cha Sheria.

Ameyasema hayo leo wakati akizungumza na Kamati ya Mkoa wa Njombe Ulinzi wa Mwanamke na Mtoto kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa na kusisitiza kuwa hatovumilia vitendo vya ukiukwaji Sheria ya Uchawi Sura ya 18 ya mwaka 2002 inayokataka upigaji ramli na kujihusisha na masuala ya kishirikina.

Ameongeza kuwa Serikali haitovumilia vitendo vyovyote vinavyojihusisha na masuala ya kishirikina kufanyika katika Wilaya ya Njombe kwani vimekuwa vikisababisha mifarakano na taharuki kubwa na kupelekea kutokea kwa utekaji na mauaji katika jamii.

Mkuu wa Wilaya huyo amesema kuwa baadhi ya watendaji wa Serikali za Mitaa na vijiji wamekuwa wakishiriana na waganga wa kienyeji kutekeleza masuala yanayohusishwa na imani za kishirikina.

“Nimemuagiza Katibu Tawala wa Wilaya kushusha agizo hili kwa watendaji wa vijiji na mitaa na sitaki kuyaona mabango hayo na nikiyaona tena nitachukua hatua kali za kisheria kwa watakaobainika kuyaweka” alisema

“Niseme tu sitosita kuwachukulia hatua watendaji watakaoendelea kushirikiana na waganga wa kienyeji na kuwakaribisha katika vijiji na mitaa yao na kuwasaidia kufanikisha kazi zao ambazo ziko kinyume cha Sheria” alisema

Mkuu huyo wa Wilaya ameomba ushirikiano kutoka kwa Kamati za Ulinzi wa Mwanamke na Mtoto kuanzia ngazi ya mkoa na Halmashauri ili kusaidiana katika mapambano ya kutokomeza vitendo vya ukatili kwa watoto.

Akizungumza katika kikao hicho kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe, Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Bumi Mwamasage amesema kuwa Kamati hiyo inatakiwa kuwajibika katika jamii kwa kutoa elimu na ishuke kwa jamii ili kuwawezesha wanajamii hao kuunga mkono mapambano ya vitendo vya kikatili dhidi ya Mwanamke na Mtoto.

Kwa upande wake Kiongozi wa Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Hanifa Selengu amesema kuwa Wizara imeamua kushirikiana na Mkoa wa Njombe kwa kuitisha Kamati ya Ulinzi wa Mwananmke na Mtoto ili kujadili kwa pamoja na kupata namna bora ya kupambana na kutokomeza vitendo vya kikatili kwa mwamake na Mtoto.

“Tumekuja kuongeza nguvu katika masuala haya yaliyojitokeza Mkoani hapa kwani wote tunadhamana ya kumlinda Mtoto dhidi ya vitendo vya kikatili” alisema. Naye Afisa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Mwanaisha Moyo amesema kuna umuhimu wa Kamati hiyo kutoa huduma kwa wahanga wa vitendo vya ukatili kwa haraka na kwa wakati.

Aidha Mwanasheria kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bw. Denis Bashaka namna Sheria ya Uchawi Sura ya 18 ya Mwaka 2002 inavyozuia vitendo vya upigaji ramli na kazi za uganga wa kienyeji ambavyo vinahusishwa na mauaji yaliyojitokeza mkoani Njombe.

Kamati ya Ulinzi kwa Mwanamke na Mtoto ya Mkoa wa Njombe imekutana Mjini Njombe kujadiliana na kupata namna bora ya kuondokana na vitendo vya kikatili hasa vitendo vya utekaji na mauaji ya watoto mkoani humo.

BREAKING NEWZZZ:MSANII MAARUFU WA BONGOFLEVA AFARIKI DUNIA

$
0
0
Hivi punde chumba cha habari Globu ya Jamii imepokea taarifa za kusikitisha/huzunisha  zinazohusu aliyekuwa Msanii mahiri katika miondoko ya kughani a.ka Rap almaarufu kwa jina la Godzilla amefariki Dunia.

Taarifa zinaeleza kuwa Msanii huyo maye kwa jina halisi anaitwa Golden Mbunda,aliyekuwa akitikisa anga ya bongofleva katika miondoko ya hip hop nchini ,amefariki Dunia ghafla  usiku wa kuamkia leo Jumatano Februari 13,2019 akiwa nyumbani kwao maeneo ya Salasala,jijini Dar.

Mwili wake umepelekwa kuhifadhiwa katika hospitali ya Lugalo,Mwenge.

Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi-AMIN.

TUTAENDELEA KUWAJUZA HABARI ZAIDI KADIRI ZITAKAVYOKUWA ZIKIINGIA.

UNITED BANK FOR AFRIC (UBA) BANK DONATES LITERATURE BOOKS TO SECONDARY SCHOOLS IN KISARAWE DISTRICT

$
0
0
In efforts to support the government in offering quality education in secondary schools, UBA Tanzania through UBA Foundation donated Literature textbooks worth TZS 6,400,000 to Kimani and Makurunge Secondary Schools of Kisarawe District, Coast Region.

The donation of the books was received by the Makurunge Secondary School Head Teacher Hassan Ruheye and Kimani Secondary School Mika Bareri on behalf of the school management.

Speaking after receiving the books, the Makurunge Secondary School Head Teacher Hassan Ruheye said that it was important to recognize the efforts which are being made by private institutions like UBA Tanzania in supporting education sector in the country. “We all understand that our government agenda is on industrialization, but we cannot have industries without good performance and adequate teaching materials in our schools. These books will increase the ability our students in performing good in literature and also in other subjects and in return will reach the government goal on industrialization”, Ruheye said.

Ruheye added “I call upon UBA Tanzania and other stakeholders to continue supporting us in other areas of our school so that we can create a good environment for our students”.

On his part, UBA Bank Tanzania Chief Operating Officer Flavia Kiyanga said that the bank believes in a society were learners get their education on a good environment and schools with learning equipment’s like textbooks. On that case, it’s good to invest on our children’s education and that has been fulfilled by donating these books to Kimani and Makurunge Secondary Schools.

UBA Tanzania has for a long time been supporting the education sector in our country. For that reason, the Bank was recognized by Tanzania Education Authority in 2018 among others as an institution that supports learning, UBA Foundation through its Read Africa Initiative has invested on the African youth to promote learning and a reading culture by donating various literature books to schools in Africa. To achieve this, we have been working with various institutions and I must thank the government for their support as UBA Foundation has been successful, said Kiyanga.

Kiyanga added that English language has been one of the barriers for students to perform well in their final exams. By donating these literature textbooks, we are creating an environment for our students to develop a culture of reading for themselves. We trust that these books will empower these students to perform well in their subjects and also increase the number of students taking who will be performing well in the final exams, said Kiyanga adding that UBA Tanzania will continue supporting schools in the country in various areas aiming at building students for a bright future.

Speaking on behalf Kimani and Makurunge Secondary Schools, the Kisarawe District Secondary School education officer Patrick Gwivaha said the UBA donation has come at the right time as the schools has been facing shortage of various textbooks something which has been affecting the academic performance. I take this opportunity to promise that we will take proper care of these books for the advantage of us and the coming generation.

He added ‘the shortage of textbooks in our schools has been affecting us very much considering that the geographical location of our district that makes it difficult for well-wishers like UBA to reach us. We really thank UBA Bank Tanzania for their support!
UBA Bank Tanzania Chief Operating Officer Flavia Kiyanga hands over literature textbooks to Kisarawe District Commissioner Jokate Mwegelo over the weekend. The UBA Bank Tanzania through UBA Foundation donated literature textbooks to Kimani and Makurunge Secondary Schools in Kisarawe District, Coast Region aimed at improving the school’s student’s performances.
Kimani Secondary School students take a reading of literature books donated by UBA Bank Tanzania to the school. The UBA Bank Tanzania through UBA Foundation donated literature textbooks to Kimani and Makurunge Secondary Schools in Kisarawe District, Coast Region aimed at improving the school’s student’s performances.

UBA Bank Tanzania Head of Marketing and Corporate Communications Brendansia Kileo distribute literature textbooks to Kimani Secondary School over the weekend. The UBA Bank Tanzania through UBA Foundation donated literature textbooks to Kimani and Makurunge Secondary Schools in Kisarawe District, Coast Region aimed at improving the school’s student’s performances.
UBA Bank Tanzania Chief Operating Officer Flavia Kiyanga speaks to students of Makurunge Secondary before handing over literature textbooks to the school. UBA Bank Tanzania through UBA Foundation donated literature textbooks to Kimani and Makurunge Secondary Schools in Kisarawe District Coast Region aimed improving academic performance to students.

Makurunge Secondary School students display literature textbooks donated by UBA Bank Tanzania. The UBA Bank Tanzania through UBA Foundation donated literature textbooks to Kimani and Makurunge Secondary Schools in Kisarawe District, Coast Region aimed at improving the school’s student’s performances

VICHEKESHO VYA MIZENGWE SI MCHEZO, WAWAVUNJA MBAVU WALIOHUDHURIA KONGAMANO LA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KUNDI la vichekesho la Mizengwe linaloundwa na watu limewavunja watu mbavu kutokana na vichekesho vyao walivyokuwa wanavitoa katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalim Nyerere jijini Dar es Salaam.

Wasanii hao wa vichekesho ambao wapo watano leo baada ya kupanda jukwaani walisema kuwa wamefika wanne kwani mwenzao mmoja amekwenda nchini India kwa ajili ya mazungumzo na Amitha Bachan.

Kitendo cha kueleza mwenzao yupo nchini India na anamazungumzo na Amitha Bachan watu waliokuwa ukumbini waliangua kucheka kwa sauti kubwa.

"Kundi la Mizengwe linaundwa na watu watano,ila leo mwenzetu mmoja anayefahamika kwa jina la Mzee Matata amekwenda India kuzungumza na Amitha Bachan.Hivyo tupo sisi tu," amesema  mmoja wa wasanii hao...watu kicheko.

Hata hivyo Mchekeshaji wa kundi hilo Rashid Coster a.k.a Mkongoman aliamua kutoa vichekesho vya aina yake na aliwavunja mbavu watu baada ya kusema kwao muhimu ni kuvaa kwani kula nani anakuona.

"Kwetu sisi Wasanii kula sio jambo muhimu sana kwani tumbo halina kioo lakini kuvaa ndio muhimu sana kwani nguo ndio zinaonekana," amesema Mkongaman.

Kwa upande wake Mwanadada pekee katika kundi hilo la Mizengwe Jesca alitumia nafasi hiyo kwa kutumia sanaa yake ya uigizaji kuzungumzia athari za dawa za kulevya.

Amesema wanaotumia dawa za kulevya hata ndoto za maisha yao zinatoweka na hivyo kuwaomba Watanzania na hasa wa wasanii kwa ujumla kuacha kutumia dawa za kulevya.

YALIYOJIRI KATIKA ZIARA YA KATIBU TAWALA MKOA WA SONGWE DAVID KAFULILA WILAYANI ILEJE

$
0
0

 Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila akitembea kukagua kaya zinazonufaika na Mpango wa TASAF katika Kijiji cha Ilulu Wilayani Ileje ili kujionea utekelezaji wa mpango huo.
 Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje ambapo amewasisitiza kutimiza majuku yao na kutii sheria na kanuni za utumishi wa umma.
2
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje wakimsikiliza Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila ambaye amewasisitiza kutimiza majuku yao na kutii sheria na kanuni za utumishi wa umma.
4
Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila akikagua baadhi ya nyaraka katika Ofisi ya Mtendaji wa Kijiji cha Ilulu Wilayani Ileje wakati akikagua utekelezaji Mpango wa TASAF katika Kijiji hicho.


……………….

Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila amefanya ziara Wilayani Ileje ambapo ameanza kwa kuzungumza na watumishi wa Halmashauri hiyo, amekagua Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Ileje na kutembelea kaya za Wanufaika wa Mpango wa TASAF ambapo haya ndiyo yaliyojiri;
Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila amekuja kuwakumbusha sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma kwakuwa yeye ndiye Mkuu wa Utumishi wa Umma Mkoa wa Songwe- Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Utumishi, Chele Ndaki
Napenda kuwakumbusha watumishi wote kuheshimu mamlaka zilizopo Kisheria na kuzingatia sheria zote za utumishi wa umma – Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Utumishi, Chele Ndaki

iii. Watumishi hakikisheni kuwa mnatimiza majukumu yenu wakati mnadai maslahi yenu yaani kama kuna mambo mnadai sio sababu ya kuweka uzembe katika utumishi wenu- Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila
Tulisaini Mkataba wa utumishi kwenye sekta za elimu na afya kwa kuwekeana vigezo ambavyo vitapimwa mwezi huu wa pili na mwezi wa tatu tutafanya tathmini, wale watakao shindwa kufikia vigezo hivyo tutawaondoa ili wawekwe wengine ambao watafanya vizuri – Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila

Kwa mujibu wa sheria za utumishi zinaruhusu mtumishi aliyeshindwa kutimiza wajibu wake kufukuzwa kazi au kunyang’anywa cheo, sio mpaka uibe – Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila
Kama taasisi wote tunatakiwa kuongeza ufanisi wa uendeshaji wa kazi zetu, kama Mkoa tumeanzisha mfumo wa kupima utendaji wa watumishi unaoitwa Songwe Task Information Management System, kwa mfumo huu tutakuwa wa kwanza kuutumia nchini na utawezesha kufahamu utendaji wa kila siku wa watumishi wote- Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila

vii. Mtendaji yeyote atakaye shindwa kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli la kuhakikisha kila mjasiriamali mdogo anapatiwa kitambulisho, hususani kwa kipindi kilichobaki cha wiki tatu, hilo ni kosa ambalo linatosha kumfukuzisha kazi- Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila

viii. Ujenzi katika Hospitali ya Wilaya ya Ileje Umesitishwa mpaka hapo kasoro zilizooneka zirekebishwe, awali ili ripotiwa kuwa kwenye beam kuna ufa na kusababisha mpasuko kwa ndani na Kupinda lakini tumekagua na kubaini sehemu ya juu imetitia kwa ndani, hili ni tatizo kubwa kuliko lilivyo ripotiwa awali- Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila .

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje ahakikishe waliohusika wote na ujenzi mbovu katika Hospitali ya Ileje popote pale walipo watafutwe na wachukuliwe hatua kali lakini pia Mkurugenzi ahakikishe ifikapo Juni 30, 2019 fedha zilizoletwa na serikali shilingi Bilioni 1.5 ziwe zimetumika kuendeleza ujenzi wa hospitali hiyo baada ya kurekebisha maeneo hayo yenye dosari -Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila.

Kuna umuhimu mkubwa wa kurekebisha makossa hayo yaliyojitokeza na kuendeleza ujenzi bila kufanya hivyo kunaweza kusababisha maafa yaani jengo hili kuanguka, Makosa yaliyofanyika ni ya design ndio maana eneo lililotitia limesababishwa na uzito wake wenyewe hivyo huwezi kuendelea na ujenzi wa ghorofa hili la hospitali- Meneja wa TARURA Wilaya ya Ileje Mhandisi Lugano Mwambingu.

Tunakiri hatukuona matatizo hayo mapema ila nia yetu ni kuhakikisha marekebisho hayo yanatekelezwa, jambo hili limetuathiri kwani nasi tulitarajia ghorofa hili likamilike ili wananchi wetu wanufaike na huduma katika hospitali hii- Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje Joseph Mchome

xii. Katika ziara hii pia nimebaini kuwa Kuna tatizo la serikali la vijiji kuendeshwa kwa kutofuata taratibu hasa kutofanya mikutano ya vijiji na kutotunza kumbumbuku za vijiji licha ya kuwa serikali imeajiri watendaji wenye diploma – Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila

xiii. Nawaagiza wakurugenzi wote Mkoa wa Songwe wafuatilie utendaji wa serikali ngazi ya vijiji, ili mapato na matumizi yabandikwe, vikao vya kisheria vifanyike na kuwepo file la mihtasari ya vikao vyote vya kijiji kwakuwa haya ni matakwa ya kisheria – Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila

xiv. Wajibu wa Halmashauri na waratibu wa TASAF ni kuhakikisha fedha zinawafikia walengwa na hakuna kaya hewa aidha wakaguzi wa ndani wakague fedha za TASAF kama mfuko maalumu tofauti na sasa wanavyofanya ukaguzi wa jumla ukizingatia hizi ni fedha nyingi kwani serikali kwa mkoa wa Songwe ni imetoa zaidi ya bilioni 14 kwa mpango huo- Katibu Tawala Mkoa wa Songwe David Kafulila 

Halmashauri itaendelea kusimamia watendaji wa vijiji na kata ili watimize majukumu yao kisheria, tumekuwa tukiwachukulia hatua watendaji ambao hawatimizi majukumu yao na tutaendelea kufanya hivyo – Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ileje Joseph Mchome

xvi. Tunashukuru mpango wa TASAF kwakuwa umetukomboa kimaisha, ijapokuwa mimi ni mjane nimeweza kupata mbolea na chakula kupitia fedha za TASAF, hivyo nawashukuru sana walio anzisha mpango huu-Hana Mtawa Mkaji wa Kijiji cha Ilulu, Ileje na Mnufaika wa TASAF

WAZIRI LUGOLA AANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI ARUSHA

$
0
0


 
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi,Kangi Lugola
 
Na. Vero Ignatus, Arusha

WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi,Kangi Lugola amelitaka Jeshi la Polisi nchini kushirikiana na mamlaka ya ya Mawasiliano nchini TCRA,ili kuweza kuwabaini wale wote wanaovunja Amani ya nchi,kwa kutumia njia ya Mtandao.

Ameyasema hayo Jijini Arusha Wakati akiwa katika ziara yake ya siku nane,lengo likiwa ni kufanya mikutano ya hadhara na kusikiliza maoni ya wananchi juu ya Usalama anaousimamia.Lugola amesema kuwa kwa sasa nchi ina Amani ya Kutosha na hivyo asitokee mtu wa kuvuruga Amani hiyo.

Aidha waziri Lugola ametoa wito kwa watanzania kuendelea kuliamini Jeshi la Polisi ,katika ufanisi wa kazi zao za kulinda raia na mali zake.Amesema mitandao ya kijamii inaweza kutumika kuleta maendeleo badala ya kuchochea Uvunjifu wa Amani.

Waziri Lugola yupo mmkoani Arusha ambapo anatarajiwa kufanya ziara yake ya kikazi ya kutembelea Wilaya zote Saba za Mkoa wa Arusha.

KAMPENI YA TBS YAWAFIKIA WANANCHI WA TARIME NA RORYA

$
0
0
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeendelea na Kampeni yake katika Wilaya ya Tarime na Rorya ya kutoa Elimu kwa umma juu ya umuhimu wa kununua bidhaa zilizothibitishwa ubora wake na TBS na jinsi gani wajasiriamali wanaweza kupata Leseni ya TBS bure bila gharama yoyote.

Kampeni hiyo ya Elimu kwa umma imefanyika Maeneo ya Soko jipya la REBU,Stendi ya Tarime Mjini,Mnada wa Mtana na maeneo mengine ya Halmashauri ya Mji na Wilaya.

wananchi walijitokeza kupata elimu sambamba na ufahamu wa masuala mbalimbali yahusuyo Ubora wa Bidhaa.Kwa upande wake Afisa Udhibiti ubora, Mhandisi Paul Ndege amezidi kuwakumbusha Wananchi wote kuwa vita ya bidhaa hafifu sio ya TBS pekee bali ya kwetu sote, Hivyo,wasisite kutoa taarifa kupitia mawasiliano waliyopewa pale wanapogundua uwepo wa bidhaa hafifu katika soko lao na kuhakikisha wananunua bidhaa zilizothibitishwa na TBS.

Vilevile Shirika lilipata fursa ya kutoa semina kwa wajasiriamali wanaojihusisha na bidhaa mbalimbali kama nafaka,sabuni, maziwa,asali na unga lishe,juu ya utaratibu wa kupata leseni ya kutumia alama ya ubora ya TBS na kuwa huduma hiyo inatolewa bure kwa wajasiriamali wadogo.

Wajasiriamali wengi walionyeshwa kufurahishwa na elimu waliyoipata na kushukuru TBS kwa kuja kutoa elimu hiyo ambayo itawapa matokeo yenye tija kwenye shughuli zao za uzalishaji.Semina hii ilifanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime

Kampeni hii inaendelea Wilaya ya Nyamagana .

 TBS ikiendelea na kampeni ya elimu kwa umma katika shule ya msingi Nyamisangura na Shule ya sekondari Sirari Wilayani Tarime.
 Afisa Udhibiti Ubora,Mhandisi Paul Ndege akiwaelekeza wajasiriamali  utaratibu  wa kupata leseni ya ubora ya TBS bila gharama yoyote,katika semina iliyofanyika ukumbi wa Halmashauri Wilayani Tarime.
 Pichani ni Mhandisi Paul Ndege, Afisa Uthibiti Ubora akitoa somo kwa mjasiliamali kuhusu umuhimu wa kuuza bidhaa zilizothibitishwa na TBS
Mhandisi Paul Ndege akiendelea na semina ya Elimu kwa Umma juu ya kutambua Bidhaa hafifu Mjini Mara.

SERIKALI YAZITAKA HOSPITALI BINAFSI KUCHANGIA GHARAMA ZA DAMU

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua idadi ya Wananchi waliofika kupata huduma wakati alipofanya ziara katika Mpango wa Taifa wa Damu salama jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikagua jokofu la kuhifadhia sampuli ya Damu pindi alipofanya ziara katika Mpango wa Taifa wa Damu salama jijini Dar es salaam. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipata maelezo kutoka kwa Afisa wa Mpango wa Taifa wa Damu salama, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kuangalia mashine mpya za kielektroniki za kupima sampuli ya Damu 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akipata maelezo kutoka kwa Mtaalamu wa Mashine yakupima Sampuli za Damu, Mpango wa Taifa wa Damu salama, wakati alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kuangalia mashine mpya za kielektroniki za kupima sampuli ya Damu. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo wakati akiongea na Watumishi wa Mpango wa Taifa wa Damu salama, alipofanya ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kuangalia mashine mpya za kielektroniki za kupima sampuli ya Damu katika taasisi hiyo. 
Meneja Mpango wa Taifa wa Damu salama Dkt. Magdalena Lyimo, akisikiliza maelekezo kutoka kwa Naibu Waziri wa Afya Dkt.Faustine Ndugulile (hayupo kwenye picha) wakati wa ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kuangalia mashine mpya za kielektroniki za kupima sampuli ya Damu. 
Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile baada ya kumaliza ziara ya kukagua hali ya utoaji huduma na kuangalia mashine mpya za kielektroniki za kupima sampuli ya Damu.
………………………. 


Na WAMJW – DSM 

Mpango wa Taifa wa Damu salama imetakiwa kuhakikisha Hospitali Binafsi zote zinaanza kuchangia gharama za huduma za afya ili kupata mgao wa damu. 

Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati alipofanya ziara ya kukagua mashine za kupima sampuli za damu na utendaji kazi wa Mpango wa Taifa wa Damu salama. 

Katika ziara hiyo Dkt. Ndugulile amesema kuwa ni lazima Mpango huyo uhakikishe unajiendesha wenyewe na kuhakikisha unapunguza gharama za utegemezi kwa Wafadhili na Serikali katika kutimiza majukumu yake. 

“Ni lazima kupunguza gharama za utegemezi kwa Wafadhili na Serikali kwa kuanzisha mfumo wa uchangiaji gharama za huduma za Afya wakati Sera inaelekea kukamilika, Mpango unapendekeza kurudisha gharama kutoka Hospitali binafsi kupitia njia ya Bima” Alisema Dkt. Ndugulile 

Dkt. Ndugulile alisema kuwa Idadi kubwa ya wanaokuja kuchukua Damu katika Taasisi hiyo ni Hospitali Binafsi ukilinganisha na Hospitali za Umma, ambapo mfumo wake ni wakutoza huduma kwa Wananchi (Biashara) 

“Wanaokuja kuchukua Damu nyingi hapa, wengi ni Hospitali Binafsi, kuliko hata za kwetu za umma, Damu nyingi tunawapa, lakini hawa tukiwapa Damu hizi, wao wanaenda wanatoza pesa, kwahiyo sisi tunawatengenezea bidhaa bure halafu wao wanaenda kutoza pesa, hata senti tano sisi hatupati, sio sahihi” alisema Dkt. Ndugulile. 

Aidha, Dkt. Ndugulile amewaagiza viongozi wa Mpango wa Taifa wa Damu salama kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kuangalia ni namna gani Damu iwe ni moja ya vitu vitakavyo gharamiwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya. 

“Muwahusishe Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, kuangalia jinsi gani damu itakuwa inagharamiwa na Bima ya Afya, mtuletee mapendekezo na sisi tutafanya maamuzi” Alisema Dkt. Ndugulile. 

Mbali na hayo Dkt. Ndugulile ameagiza kufanya maboresho ya mfumo wa Takwimu kuanzia kwenye ukusanyaji wa mapato mpaka hatua ambayo mgonjwa anapata damu hiyo jambo litakalosaidia kuboresha huduma kwa wananchi. 

Kwa upande mwingine Dkt. Ndugulile ameagiza kuweka mikakati ya kuhakikisha wanawabakishia wachangiaji Damu ambao wanakuja kuchangia, hii inatokana na takwimu kuonesha Wachangiaji wa Damu wa hiari wanapungua kutoka 67% mpaka 63% mwaka 2017-2018. 

“Taarifa yenu ya Mwaka 2017-2018 inaonesha kwamba, wachangiaji Damu wa hiari wanapungua kutoka 67% mpaka 63% , maana yake bado kuna changamoto, na kuna kazi tunatakiwa kufanya ikiwemo kuweka mikakati ya kuhakikisha kwamba tunaowapata Mara ya kwanza kuendelea kuwa nao” Alisema Dkt. Ndugulile 

Naye Meneja Mpango wa Taifa wa Damu salama Dkt. Magdalena Lyimo amesema kuwa Mpango una mkakati wa kuboresha mfumo wa ukusanyaji taarifa na Takwimu za kielektroniki unaunganishwa nchi nzima ili kuleta tija na ubora wa huduma za damu salama nchini. 

Kwa upande mwingine Dkt. Lyimo amesema kuwa Mpango umefanikiwa katika kipindi cha Mwaka 2018 kwa kushirikiana na timu za Mikoa na Halmashauri ulikusanya jumla ya chupa 307,835 ambayo ni sawa na Chupa 6 kwa kila watu 1000, huku Shirika la Afya Duniani linapendekeza kukusanya chupa 10 kwa kila watu 1000, makusanyo hayo ni sawa na ongezeko la chupa 73,882 sawa na 32% ikilinganishwa na Takwimu za 2017. 

Dkt. Magdalena Lyimo aliendelea kusema kuwa kwa Mwaka 2018, Wastani wa chupa 25,653 zilikusanywa kila mwezi na damu zote zilipimwa magonjwa ya HIV,Kaswende pamoja na makundi ya damu, huku matarajio ni kuongeza damu hadi kufikia chupa 375,000 kwa Mwaka 2019.

ZIARA YA PAMOJA YA NAIBU MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE NA FEDHA MPAKANI HOROHORO

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) kwa pamoja wamefanya ziara kwenye kijiji cha Jasini na Kituo cha kutolea huduma kwa pamoja Mpakani cha Horohoro kilichopo mpakani mwa Tanzania na Kenya Wilayani Mkinga, Mkoani Tanga. Pamoja na Mambo mengine Naibu Mawaziri hao waliweza kujionea changamoto mbalimbali ikiwamo ukusanyaji wa mapato kituoni hapo, pamoja na kuzungumza na wanakijiji cha Jasini na Watendaji wa Kituo hicho. 
Wadau walioshiriki ziara za Naibu mawaziri hao wakisikiliza wakati Dkt. Ndumbaro (hayupo pichani) akizungumza 
Sehemu nyingine ya wadau wakimsikiliza Dkt. Ndumbaro (hayupo pichani) 
Mkutano ukiendelea 
Wananchi wakipata huduma kwenye kituo hicho cha kutolea huduma kwa pamoja 
Dkt. Ndumbaro pamoja na Dkt. Kijaji wakimsikiliza Bw. Bilali Juma, Afisa Mkemia wa kituo cha kutolea huduma kwa pamoja mpakani Horohoro 
Dkt. Ndumbaro akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza mazungumzo na wadau mbalimbali 
Kituo cha kutolea huduma kwa pamoja cha Horohoro kilihopo Mpakani mwa Tanzania na Kenya kama kinavyoonekana pichani 
Dkt. Ndumbaro akisaini kitabu cha wageni cha kijiji cha Jasini kilichopo wilaya ya Mkinga, Mkoani Tanga, kabla ya kuanza ziara kwenye kijiji hicho
Naibu Mawaziri pamoja na wadau mbalimbali wakiwa wamesimama kwenye moja ya jiwe ambalo linaonyesha Mpaka wa Tanzania na Kenya. 
Mhe. Dkt. Ndumbaro na Mhe. Dkt. Kijaji wakiwa kwenye Nyumba iliyojengwa mpakani mwa Tanzania na Kenya. Horohoro. Mhe. Ndumbaro akiwa upande wa Kenya na Mhe. Kijaji akiwa upande wa Tanzania 
Mhe. Dkt. Ndumbaro na Mhe. Dkt. Kijaji wakiendelea na ziara na kujionea alama za mipaka zilizopo mpakani hapo 
Mhe. Dkt. Ndumbaro pamoja na Mhe. Dkt. Kijaji wakiwa kwenye moja ya alama za mpaka 
Mhe. Dkt. Ndumbaro akiwaeleza waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa ziara yao kwenye kituo cha kutoa huduma kwa pamoja cha Horohoro 
Mhe. Dkt. Kijaji akitizama kitambulisho cha mjasiriamali mdogo huku Dkt. Ndumbaro akishuhudia tukio hilo. Mjasiriamali huyo aliwavuti Naibu Mawaziri hao kwa mwitikio wake chanya katika kuhakikisha kila mjasiriamali nchini anapata kitambulisho cha kufanyia biashara 
Mmoja wa wanakijiji akielezea changamoto wanazokabiliana nazo kijijini hapo ikiwamo upatikanaji wa elimu kwa watoto wao ambao wanalazimika kwenda kusoma Kenya na jioni kurejea Tanzania.
Wanakijiji wakiwasikiliza kwa makini Naibu Mawaziri hawapo pichani
Naibu Mawaziri hao wakizungumza na baadhi ya wananchi wa Jasini mara baada ya kumaliza ziara kijijini hapo 
Waandishi wa habari wakiwa kazini 
Waheshimiwa Naibu Mawaziri wakimsikiliza Mohamed Ibrahim anayesoma Darasa la nne Shule ya Vumba Kuu iliyopo Kenya. Mohamed alikuwa amerudi nyumbani kupata chakula wakati wa mapumziko mafupi kabla ya kurudi darasani.









ZIARA YA PAMOJA YA NAIBU MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE NA FEDHA MPAKANI HOROHORO

Watendaji wa Kituo Cha Kutoa Huduma kwa Pamoja cha Horohoro kilichopo mkoani Tanga kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya wametakiwa kuhakikisha kuwa malengo yaliyowekwa ya kukusanya mapato kwenye kituo hicho yanafikiwa.

Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) walipotembelea kituo hicho tarehe 10 Februari 2019.

Dkt. Ndumbaro alishangazwa na mwenendo wa ukusanyaji wa mapato wa kituo hicho ambapo takwimu zimekuwa zikipungua badala ya kuongezeka kila mwaka. ‘Kwa miaka mitatu mfululizo takwimu za ukusanyaji wa mapato ya kodi katika Kituo hiki zimekuwa zikishuka badala ya kupanda, jambo ambalo si zuri kiuchumi na linakwenda kinyume kabisa na malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli’; Dkt. Ndumbaro alimwambia Meneja wa TRA kituoni hapo.

Kwa mujibu wa takwimu hizo mwaka wa fedha 2017/2018, makusanyo ya kodi kwenye kituo hicho ni asilimia 81 ya malengo na mwaka wa Fedha 2018/2019 inatarajiwa makusanyo yatafikia asilimia 76 ya malengo yaliyowekwa.

Mhe. Naibu Waziri aliwataka watendaji hao kuwa wabunifu kuhakikisha kuwa malengo ya Serikali yanafikiwa bila kumuonea mtu ikiwemo ubunifu wa kutatua changamoto zinazokikabili kituo hicho. Changamoto hizo ni pamoja na ukosefu wa maji ambapo yananunuliwa kwa gharama ya Shilingi milioni sita kwa mwezi. Naibu Waziri alishangazwa na uamuzi huo wa kutumia fedha nyingi kwa ajili ya maji wakati kuchimba kisima hakiwezi kugharimu zaidi ya milioni 10.

Dkt. Ndumbaro pia hakuridhishwa na ubora wa jengo la kituo hicho na kubainisha kuwa ndio sababu zinazofanya kituo hicho kutozinduliwa rasmi hadi leo.

Kwa upande wake, Dkt. Kijaji alisikitishwa na utendaji usiokuwa na kiwango wa mamlaka zote zilizopo kwenye kituo hicho na kusisitiza kuwa, kwa kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ipo chini ya himaya yake atachukua hatua zinazostahili. Moja ya maeneo yenye udhaifu katika kituo hicho ni uchukuaji wa takwimu zikiwemo za magari yanayoingia na kutoka ambapo kila mamlaka iliyopo hapo ina takwimu tofauti.

Aidha, Mhe. Kijaji alipiga marufuku kwa wafanyabiashara wa Wilaya ya Mkinga kwenda Wilaya ya Muheza kufuata huduma za kodi zikiwemo za kulipia kodi mbalimbali. Mhe. Naibu Waziri alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Mkinga kuwatangazia wafanyabiashara wa Mkinga marufuku hiyo na kuagiza watumishi wa TRA wa Mkoa kwenda Mkinga kutoa huduma za kikodi angalau mara tatu kwa wiki.

Kuhusu ubora wa jengo hilo, Dkt. Kijaji aliagiza apatiwe nyaraka za jengo hilo ifikapo tarehe 15 Februari 2019 ili aone majukumu ya kila mmoja katika ujenzi wa jengo hilo kwa madhumuni ya kuchukua hatua stahiki.

Mhe. Dkt. Ndumbaro na Mhe. Dkt. Kijaji walifanya ziara ya pamoja kwenye kituo hicho cha Horohoro kwa lengo la kujionea changamoto ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi.



Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
13 Februari 2019

MAKAMU WA RAIS AZUNGUMZA NA WASANII KWENYE KONGAMANO LA WASANII TANZANIA KUHUSU ATHARI ZA MATUMIZI NA BIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia kwa umakini Sanaa ya maigizo iliyokuwa ikionyeshwa na wasanii kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA) waliokuwa wakionyesha madhara ya dawa ya kulevya wakati wa Kongamano Kuhusu Tatizo la Dawa za Kulevya kwa Wasanii lililoandaliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo februari 13, 2019 .Kongamano hilo limefanyika katika  Kituo cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wasanii wa fani mbali mbali waliohudhuria  Kongamano Kuhusu Tatizo la Dawa za Kulevya kwa Wasanii lililoandaliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo februari 13, 2019 lililofanyika katika  Kituo cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais). 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza viongozi wa meza kuu na wasanii kusimama kwa dakika moja kama ishara ya kumkumbuka msanii wa hiphop Tanzania Golden Jacob Mbunda aliyefariki asubuhi ya leo kabla ya kuanza kuhutubia  Kongamano Kuhusu Tatizo la Dawa za Kulevya kwa Wasanii lililoandaliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo februari 13, 2019 lililofanyika katika  Kituo cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Heshima kwa Godzilla; Wasanii wa Filamu na Muziki wakiwa wamesimama kwa dakika moja kama ishara ya kumkumbuka msanii wa hiphop Tanzania Golden Jacob Mbunda aliyefariki asubuhi ya leo kabla ya kuanza kuhutubia  Kongamano Kuhusu Tatizo la Dawa za Kulevya kwa Wasanii lililoandaliwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya pamoja na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo leo februari 13, 2019 lililofanyika katika  Kituo cha Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Viewing all 46397 articles
Browse latest View live




Latest Images