Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

WAZIRI ENG. KAMWELWE AZUNGUMZA NA TATOA

$
0
0


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe akimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa malori nchini (TATOA) Bw, Elius Lukumay hayuko pichani katika kikao kazi cha kujadiliana namna bora ya kufuata sheria ya kudhibiti uzito wa magari ili kulinda barabara nchini kilichofanyika mjini Dodoma leo. 
2-min
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe akisisitiza jambo katika kikao cha wataalam wa Wizara yake na viongozi wa TATOA kilichofanyika mjini Dodoma, (kulia) ni Naibu Waziri wa Ujenzi Mh. Elias Kwandikwa na (kushoto) ni Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Atashasta Nditie.
3-min
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Isack Kamwelwe akijadiliana jambo na Makamu Mwenyekiti wa TATOA  Bw, Elius Lukumay katika kikao cha viongozi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na TATOA cha kujadiliana namna bora ya kufuata sheria ya kudhibiti uzito wa magari ili kulinda barabara na madaraja hapa nchini. 

PWANI YAPOKEA BILIONI 4.5 KWA AJILI YA UJENZI WA HOSPITAL TATU ZA WILAYA -RC NDIKILO

$
0
0

NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA .

KATIKA kukabiliana na changamoto ya utoaji wa huduma ya afya kwa wananchi, serikali ya awamu ya tano inajenga hospitali za wilaya tatu za kisasa , halmashauri ya Kibaha Mjini, Kibaha Vijijini na Kibiti mkoani Pwani ambazo zitagharimu kiasi cha sh. bilioni 4.5. 

Akizungumza wakati alipotembelea ujenzi wa hospital ya halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Lulanzi kata ya Pichandege, kwenye ziara yake inayoendelea kukagua miradi ya maendeleo, mkuu wa mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo alisema kukamilika kwa hospital hizo, kutaondoa kero ya kutembea umbali mrefu kufuata matibabu. 

“Kila hospital inatarajiwa kugharimu bilioni 1.5 ,matarajio yetu ni kuona ujenzi unakamilika na sio kuanza mradi na kisha kusuasua “alieleza Ndikilo.
Aidha ameelezea, fedha zote zinazoelekezwa katika miradi hiyo muhimu zitumike kwa wakati na kwa matumizi lengwa bila kuziacha kubaki viporo. 

Hata hivyo Ndikilo, aliwaasa wahandisi wa halmashauri ya Kibaha Mji na wa serikali ya mkoa huo kujiwekea utaratibu wa kutoka maofisi kwenda kutembelea miradi pasipo kusubiria ziara ama kiongozi kutembelea ndipo nao watoke maofisini. 

Nae mkuu wa wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama alitoa rai kwa jamii kushirikiana na serikali katika kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya elimu na kujitolea kwenye miradi ya kimaendeleo. 

Diwani wa kata ya Picha ya ndege Robert Machumbe alieleza, nia ya serikali ni kuwaletea wananchi mabadiliko chanya ya kimaendeleo ambapo amefafanua kwamba, eneo hilo linalojengwa hospital lina ukubwa wa hekari 25 lipo eneo linalojengwa shule ya sekondari Lulanzi lenye ukubwa wa hekari 11.7

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AZUNGUMZA NA VIONGOZI WA UWT ZANZIBAR

$
0
0



RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).Bi. Thuwaiba Kisasi , akiwa na Ujumbe wa Viongozi wa (UWT) Afisi Kuu ya Zanzibar,walipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo leo.7-2-2019
IMG_2386-minIMG_2384-min
RAIS wa Zanzibar na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) walipofika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo leo 7-2-2019.ukiongozwa na Makamu Mwenyekiti wa (UWT.)Bi. Thuwaiba Editon Kisasi.(Picha na Ikulu)

OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAFANYA UFUATILIAJI WA UTEKELEZAJI WA WARAKA WA MAVAZI KWA WATUMISHI WAKE

$
0
0
Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ukuzaji Maadili, Sehemu ya Ufuatiliaji Uzingatiaji wa Maadili, Bibi Janeth Mishinga akihimiza uzingatiaji wa Waraka wa Mavazi Na. 3 wa Mwaka 2007 kwa watumishi wa Umma nchini mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ukaguzi na ufuatiliaji wa Waraka huo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Baadhi ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa sehemu ya mapokezi kusaini kitabu cha mahudhurio wakati wa zoezi la ukaguzi na ufuatiliaji wa Waraka wa Mavazi Na. 3 wa Mwaka 2007 lililofanywa na Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora kwa kushirikiana na Kamati ya Uadilifu ya ofisi hiyo kwa lengo la kuhimiza uzingatiaji wa waraka huo na kuwahi kazini.
Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ukuzaji Maadili, Sehemu ya Ufuatiliaji Uzingatiaji wa Maadili, Bibi Janeth Mishinga akiwa na baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Uadilifu wa ofisi hiyo wakati wa zoezi la ukaguzi na ufuatiliaji wa Waraka wa Mavazi Na. 3 wa Mwaka 2007 lililofanyika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa lengo la kuhimiza uzingatiaji wa waraka huo kwa watumishi wa umma nchini.
Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Uadilifu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Constantino L. Kinawiro (mwenye suti) akipongezwa na mtumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora mara baada ya kamati hiyo kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa Waraka wa Mavazi Na. 3 wa Mwaka 2007 kwa watumishi wa ofisi hiyo.

…………………………..

Idara ya Ukuzaji Maadili, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kwa kushirikiana na Kamati ya Uadilifu ya ofisi hiyo, imefanya ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Waraka wa Mavazi Na. 3 wa Mwaka 2007 kwa watumishi wa ofisi hiyo kwa lengo la kujiridhisha na kiwango cha utekelezaji wake, ikiwa ni pamoja na kuhimiza watumishi wa umma nchini kuzingatia waraka huo mahala pa kazi.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Ukuzaji Maadili, Sehemu ya Ufuatiliaji Uzingatiaji wa Maadili, Bibi Janeth Mishinga mara baada ya kukamilika kwa zoezi la ufuatiliaji wa Utekelezaji wa Waraka huo kwa watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ambao unawaelekeza watumishi wa umma aina ya mavazi wanayostahili kuyavaa mahala pa kazi.

Bibi Mishinga amesema, Ofisi ya Rais-Utumishi ni msimamizi wa miongozo mbalimbali ya kiutumishi ikiwemo Kanuni za Maadili ya Utendaji katika Utumishi wa Umma ambapo kanuni ya kwanza inaelekeza utoaji wa huduma bora na kuongeza kuwa moja ya kigezo cha watumishi wa umma kutoa huduma bora ni pamoja na kuvaa mavazi yenye staha.

Bibi Mishinga amefafanua kuwa, zoezi hilo la ukaguzi katika ofisi ya Rais-Utumishi limebaini kuwa asilimia 95 ya watumishi wameonekana kutekeleza vema waraka huo wa mavazi ikiwemo kuwahi kazini na asilimia tano ya watumishi waliobainika kutotekeleza waraka huo wamekumbushwa kuuzingatia.

Aidha, Bibi Mishinga ametoa wito kwa wasimamizi wa taasisi zote za umma nchini kufanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa waraka huo na kuwahimiza watumishi walio chini yao kuwahi kazini kwa ili kutoa huduma bora na kwa wakati kama ambavyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anavyohimiza.

Bibi Mishinga amesisitiza kuwa, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikiwa ndio msimamizi wa waraka huo wa mavazi itaendelea kufanya ukaguzi na ufuatiliaji katika taasisi zote za umma nchini na haitosita kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wote wa umma watakaobainika kuukiuka.

Serikali imejiandaa Vyema Kunufaika na Ujio wa Mashindano ya AFCON

$
0
0

Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza akijibu swali la Mbunge wa Konde Mhe.Khatib Haji (CUF) kuhusu mgao wa fedha za FIFA zinazopelekwa TFF na utaratibu unaotumiwa na TFF kuwapatia fedha hizo Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) leo Bungeni jijini Dodoma

……………………..

Na Anitha Jonas – WHUSM,Dodoma.

Serikali kwa kushirikiana na taasisi zote muhimu imejiandaa kupokea wageni wote watakao shiriki mashindano ya AFCON yanayotarajia kufanyika nchini hivi karibuni .

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni jijini Dodoma na Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Kilolo Venance Mwamoto (CCM) wakati wa maswali ya papo kwa papo ya wabunge.

“Serikali inatambua maandalizi yanayofanyika na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) pamoja na wadau mbalimbali na tunatambua kuwa tutapokea wageni wengi akiwemo Rais wa Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA)”,alisema Mhe.Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha,Mheshimiwa Waziri Mkuu aliendelea kusema kuwa kupitia mashindano hayo serikali imehamasisha Mikoa ya jirani kujipanga kunufaika na mashindano hayo na jumla ya viwanja vitatu vitatumika na nijukumu la watanzania wote kushirikiana ili kuhakikisha tunanufaika kwa ujio huu mkubwa.

Pamoja na hayo Mheshimiwa Majaliwa aliendelea kuwasisitiza TFF kuimarisha maandalizi ya timu hiyo itayoshiriki ili taifa liweze kuibuka kidedea,vilevile aliwasihi watanzania wote kuonyesha uzalendo kwa timu yao ili kuweza kuwatia moyo kwa kuwa na imani kuwa timu hiyo itaweza kushinda.

Nae Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana Shonza ametoa majibu ya swali la Mbunge wa Konde Mhe.Khatibu Haji (CUF) lilihoji kuhusu mgao wa fedha zinazotolewa na FIFA kwa TFF kuwa ni kiasi gani zimekwisha pelekwa kwa Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kwa kusema kuwa kuwa kufuatia changamoto TFF kutokukidhi vigezo vya utawala bora na uwazi katika matumizi ya fedha kwa zaidi ya miaka mitatu wamekuwa hawapati mgao na FIFA ila kwa kuanzia mapema mwaka huu wanatarajia kuanza kupata mgao huo baada ya kutatua changamoto hizo.

Halikadhalika katika swali la nyongeza Mhe.Naibu Waziri Shonza alijibu kuwa si kweli kuwa ZFA haijawahi kupatiwa msaada wa TFF kwani wameshawahi kupatiwa msaada wa miradi moja wapo ni ujenzi wa ukarabati wa uwanja wa Gombani Pemba na kufafanua kuwa ZFA ni sehemu ya TFF hivyo fedha zinazoletwa na FIFA kwa TFF hugawiwa kwa mashirikisho yote na ZFA hawaletewi fungu lao peke yao kwani ZFA siyo mwanachama FIFA wala CAF.

Fundi magari Tabata akabidhiwa bodaboda yake kutoka biko

$
0
0
Fundi magari mwenye maskani yake Tabata jijini Dar es Salaam, Saimon Mushi, amekabidhiwa bodaboda yake aliyoshinda jana kwenye droo kubwa ya Jumatamu Jenga, huku akishinda sambamba na wenzake watano kutoka kwenye bahati nasibu hiyo, ambapo washindi wawili waliibuka na bodaboda na sh milioni moja huku wengine wanne wakishinda mamilioni ya wapendanao.

Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mratibu Msaidizi wa Matukio wa Biko Hassan Ahmed.Akizungumza katika makabidhiano hayo, fundi huyo aliishukuru Biko kwa kumkabidhi bodaboda yake akisema kuwa itamsaidia kwa kiasi kikubwa katika maisha yake kwa namna moja aka nyingine.

Kucheza Biko sasa ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500 wakati watakaocheza kwa sh 1000 na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.

Bahati nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi kubwa katika droo ya Jumatano na Jumapili.
 Mshindi wa bodaboda na sh milioni moja kutoka bahati nasibu ya Biko wa droo ya 179, Saimon Mushi wa Tabata jijini Dar es Salaam, akipokea bodaboda yake aliyoshinda kwenye droo kubwa iliyofanyika Jumatano, maarufu kama Jumatano Jenga ambapo washindi sita walipatikana wakiwamo wa mamilioni na wawili wa bodaboda. Makabidhiano hayo yameongozwa na Mratibu Msaidizi wa matukio wa biko Hassan Ahmed. Picha na Mpigapicha Wetu.
 

Watumishi wa Umma Kuweni na Subira Ongezeko la Mishahara - Waziri Mkuu Majaliwa

$
0
0

Na Jacquiline Mrisho - MAELEZO

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Kassim Majaliwa, amewataka watumishi wa umma kuwa na subira kwa sababu Serikali inaendelea na mchakato wa kuwatambua watumishi wa umma halali na kufanya ulinganifu wa mishahara katika kada mbalimbali ili watumishi hao waanze kulipwa mishahara stahiki. 

Waziri Mkuu Majaliwa ameyazungumza hayo leo Jijini Dodoma wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Mhe Pascal Haonga, lililohoji juu ya ongezeko la mishahara kwa watumishi wa umma chini ya Sheria ya Utumishi wa Umma.

Mhe. Majaliwa amefafanua kuwa mwanzoni nchi ilikuwa na idadi kubwa ya wafanyakazi hewa ambapo wote kwa pamoja walikuwa wakilipwa mishahara na posho mbalimbali hivyo, ili kuwatambua watumishi halali Serikali iliamua kufanya uchunguzi na kuwagundua watumishi hao hewa.

Pia, Serikali ilifanya uchunguzi mwingine wa kuwatambua watumishi wenye vyeti stahiki vya kufanya kazi mbalimbali Serikalini kwa mujibu wa Kanuni za Utumishi wa Umma.

Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa baada ya kumaliza utambuzi wa watumishi halali, Rais Dkt. Magufuli aliunda Tume ya Mishahara na Motisha kwa ajili ya kufanya mapitio ya kada zote za Utumishi wa Umma na viwango vya mishahara ili kutambua ulinganifu kati ya stahiki ya mshahara na kada husika.

"Lengo la Rais Magufuli kuunda tume hiyo ni kufanya tathmini nzuri ili kutambua weledi wa kazi, uwajibikaji na tija inayopatikana mahala pa kazi, hivyo baada ya kukamilika Serikali itatoa taarifa," alisema Mhe. Majaliwa.

Aidha, Mhe. Majaliwa ametoa rai kwa Watumishi wa Umma kuendelea kuiamini serikali kwani ina nia ya dhati kuhakikisha watumishi wote wanapata haki zao stahiki vile vile mpaka sasa mjadala kati ya Serikali na Vyama vya Wafanyakazi unaendelea vizuri.

TAARIFA KWA UMMA: UBADILISHAJI PESA ZA KIGENI


CCM YAWAONYA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA WASIO WAJIBIKA,YAAHIDI KUTOWARUDISHA KATIKA UCHAGUZI WA 2019

$
0
0
Akiwa katika ziara ya Kata kwa kata ya uhuishaji wa hai wa Chama na ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya CCM ya Mwaka 2015 – 2020 Mkoa wa Arusha, Wilaya ya Arusha Mjini katika Kata za Engutoto, Lemara, Muriet, Terrat, Olasiti na Osunyai Ndg. Humphrey Polepole Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi amesema CCM inawaonya viongozi wake wote wa Serikali za Mitaa wasiowajibika kusoma mapato na matumizi na chama kimeahidi kutowarudisha katika uchaguzi wa serikali za mitaa Mwaka huu 2019.

Akifafanua suala hilo Ndg. Polepole amesema kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa viongozi wote wasiowajibika, wasio soma mapato na matumizi kwa mujibu wa sheria, wenye tabia za kupokea au kutoa rushwa Chama hakitawavumilia na hawatapewa fursa ya kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2019.

"Tunaposimamisha wagombea wa CCM kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa wa 2019 tunahitaji watu mwenye tabia nzuri, waaminifu, wanyenyekevu, wachapakazi, wapole lakini wakali kwenye mambo ya hovyo na wanaokubalika kwa watu” amesisitiza Ndg. Polepole

Aidha akiwa katika ziara hiyo Ndg. Polepole amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa jengo la cha Wagonjwa wa Nje (OPD) la hospitali ya Wilaya ya Arusha Jiji lililopo katika Kata Engutoto, Ujenzi wa barabara kuu ya mchepuko (kilometa 42. 4 kwa kiwango cha lami) yenye madaraja 7, ujenzi wa maabara  katika shule ya Sekondari Terrati katika Kata ya Muriet, Ujenzi wa madarasa manne katika shule ya msingi muriet Darajani na ujenzi wa barabara ya Sombetini FFU yenye urefu wa kilometa 2.1 kwa kiwango cha lami.

Huu ni muendelezo wa Ziara za ujenzi wa Chama na ukaguzi wa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi Mkuu ya Mwaka 2015 – 2020.

Imetolewa na,
IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARI 8,2019

TANGA UWASA YAKABIDHI VIFAA VYA UJENZI VYENYE THAMANI YA MILIONI 10 SHULE YA SEKONDARI MIKANJUNI

$
0
0
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa katikati akipokea vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya sh.milioni 10 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule ya Sekondari Mikanjuni kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Rahma Msofe kulia jana ambao walikabidhi vifaa hivyo ili viweze kutumika kwenye ujenzi huo ili kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim 
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa katikati akipokea vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya sh.milioni 10 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule ya Sekondari Mikanjuni kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Rahma Msofe kulia jana ambao walikabidhi vifaa hivyo ili viweze kutumika kwenye ujenzi huo ili kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa shuleni hapo wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly wa pili kutoka kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim 
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano 
Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Rahma Msofe akizungumza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa 
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly akizungumza katika halfa hiyo 
Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga (DAS) Faidha Salimu akizungumza katika halfa hiyo 
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo akizungumza katika halfa hiyo 
Afisa Elimu Taaluma Jiji la Tanga akizungumza katima hafla hiyo 
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mikanjuni Kaana Erasto akitoa taarifa ya shule hiyo 
Sehemu ya wanafunzi wa shule hiyo 
Sehemu ya walimu wa shule hiyo wakifuatilia halfa hiyo ya makabidhiano
Sehemu ya walimu wa shule hiyo wakifuatilia halfa hiyo ya makabidhiano
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Dorrah Killo kulia akiamkaribisha Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Mikanjuni
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya kamabidhiano hayo 
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly akiwaongoza viongozi mbalimbali wakati walipotembelea ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule ya Sekondari Mikanjuni 
Sehemu ya watumishi wa Tanga Uwasa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mkuu wa wilaya ya Tanga
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akiagana na watumishi wa mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) mara baada ya kumalizika kwa halfa hiyo kulia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim
Sehemu ya Kokoto zilizokabidhiwa

MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa kushoto akitokea nondo 60 kwa ajili ya ujenzi kutoka kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) Rahma Msofe kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga Uwasa Mhandisi Geofrey Hilly 



MAMLAKA ya Maji Safi na Usafiri wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) imekabidhiwa vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya milioni 10 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa madarasa kwenye shule ya sekondari Mikanjuni ikiwa ni mkakati wa kuunga mkono juhudi za Serikali kuondosha changamoto zinazoikabili sekta hiyo. 

Halfa ya makabidhiano hayo ilifanyika kwenye shule hapa baina ya Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Rahma Msofe na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa wakiwemo Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Mhandisi Geofrey Hilly na Katibu Tawala wa wilaya ya Tanga Faidha Salim. 

Vifaa vilivyokabidhiwa shuleni hapo kwa ajili ya kumalizia madarasa matatu ni pamoja na saruji mifuko 100, nondo 60, shehena za kokoto, mchanga, mbao, waya na vifaa vingine vyot ambavyo vitasaidia ujenzi huo ili kutoa fursa wanafunzi kupata fursa ya kusoma bila kuwepo kwa vikwazo vyovyote. 

Akizungumza mara baada ya kutokea msaada huo wa vifaa hivyo vya ujenzi Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa alipongeza juhudi ambazo zimefanywa na mamlaka hiyo kwa kusaidia kuondosha changamoto za elimu kwenye shule hiyo. 

Mwilapwa alisema juhudi ambazo zimefanywa na mamlaka hiyo zinapaswa kuungwa mkono na mashirika ya Umma na makampuni binafsi kuhakikisha yanachangia masuala ya elimu ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kukabiliana na uhaba wa madarasa.

Mkuu huyo wa wilaya alisema serikali inakabiliwa na changamoto kubwa hasa katika sera yake ya elimu bure kutokana na idadi ya wanafunzi wanaofaulu toka darasa la saba kwenda kidato cha kwanza kuongezeka siku hadi siku na kupelekea uhaba wa vyumba vya madarasa.

Alisema mamlaka hiyo mbali na jitihada za kuimarisha huduma ya maji nam usafi wa mazingira Jijini Tanga pia imechukua dhamana ya kuimarisha miundombinu ya shule hiyo ambayo inauhitaji wa madarasa kutokana na ongezeko la wananfunzi.

Awali akizungumza katika halfa hiyo ya makabidhiano Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo Rahma Msofe alisema kilichofanywa na Mamlaka hiyo ni sehemu ya kuchangiaji wa huduma za kijamii ili kumuunga mkono Rais Magufuli katika harakati zake za kuiboresha elimu.

Msofe alisema vifaa vilivyotolewa shuleni hapo kwa ajili ya kumaliziamadarasa matatu ni pamoja na saruji mifuko 100, nondo 60, shehena za kokoto, mchanga, mbao,waya na vifaa vingine vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 10.

“Malengo yetu si kuhudumia sekta ya maji tu bali tutaendelea kujikita katika kusaidia huduma za kijamii pale tutakapoona upo ulazima wa kufanya hivyo bila ya kuathiri utendaji wa kazi zetu”Alisema Msofe.

Awali akisoma taariafa fupi mbele ya mgeni rasmi Mkuu wa Shule hiyo Kaana Erasto alisema shule hiyo iliyo na wanafunzi 1319 inauhitaji wa madarasa 33 huku yaliyopo 24 ambapo kunaupungufu wa vyumba 9 ili kutoa fursa kwa wananfunzi kupata sehemu ya kujisomea.Alisema jitihada za wadau zimeanza na tayari ujenzi wa vyumba vitatu kati ya tisa umekwisha anza na majengo yapo katika hatua za mwisho ili kuweza kukabiliana na uhaba huo na kutoa fursa kwa wanafunzi ambao wamekosa mahala pa kujisomea.

Erasto alisema wanafunzi waliopata nafasi ya kujiunga na shule hiyo kidato cha kwanza mwaka 2019 ni 405 huku 150 ndio waliopo madarasani ambapo wanafunzi 255 wakikosa mahala ma kujisomea na kupelekea wahisani kujitolea katika ujenzi wa madarasa.

Mkazi wa Arusha akabidhiwa mamilioni ya biko akiwa na mkewe

$
0
0

Mstaafu kutoka Wizara ya Kilimo, Daniel Shigela na mkewe wamekabidhiwa sh milioni tano kutoka kwenye bahati nasibu ya biko inayoendesha bahati nasibu nchini, huku ikitoa fursa za Watanzania kuibuka mamilionea kwa kushinda kwenye mchezo huo.

Makabidhiano hayo yamefanyika mkoani Arusha, akiwa sambamba na mkewe Edith Shigela ikiwa ni siku moja tu baada ya kushinda.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Shigela aliishukuru Biko kwa kumpatia fedha zake hizo akisema kuwa fedha hizo zitawanufaisha yeye na mkewe kwenye familia yao hiyo.

Kucheza Biko sasa ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500 wakati  watakaocheza kwa sh 1000 na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.

Bahati nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi kubwa katika droo ya Jumatano na Jumapili

 Mstaafu kutoka Wizara ya Kilimo, Daniel Shigela, mwenye maskani yake Sombetini jijini Arusha, akiwa na nyuso ya furaha na mke wake Edith Shigela baada ya kukabidhiwa fedha zao sh milioni tano alizoshinda kutoka kwenye bahati nasibu ya Biko inayondelea kumwaga mamilioni kwa Watanzania wanaocheza Biko mchezo huo ambapo sasa droo ya wapendanao ikichezeshwa na watu kuvuna fedha pamoja na bodaboda. Picha na Mpigapicha Wetu.

NHC YAKABIDHI MIFUKO 200 YA SIMENTI KWA MKUU WA WILAYA NA KINONDONI

$
0
0

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) imekabidhi jumla ya mifuko ya simenti 200 kwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Daniel  Chongolo ikiwa ni mchango wake kwa jamii katika kuhakikisha sekta ya elimu inaboreshwa.

Akiongea wakati wa kupokea msaada huo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Chongolo, pamoja na kulishukuru Shirika la Nyumba la Taifa ameuelekeza msaada huo katika ujenzi wa madarasa katika shule za Sekondari ili kupunguza pengo la madarasa 100 yanayohitajika kwa ajili ya wanafunzi waliochaguliwa kijuninga na elimu ya sekondari Januari Mwaka huu.

Alisema kuwa Wilaya ya Kinondoni ilipata baraka ya kusajili watoto wengi kwaajili ya kujiunga na elimu ya kidato cha kwanza na kwamba elimu bila malipo imehamaisha watoto wengi kujiunga na elimu hiyo na hivyo kusababisha kuwa na upungufu wa vyumba vya kujifunzia.

Alisema uongozi wa wilaya kwa maana ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri pamoja na watendaji wote kwa ujumla walichukua jukumu la kuendesha harambee itakayowezesha kujenga angalau madarasa 100 ili kukabili upungufu wa madarasa na yakamilike kabla ya Machi mwaka huu.

“Napenda kuwahakikishia wadau na watoto wetu waliobahatika kujiunga na elimu ya sekondari mwaka huu kwa wilaya ya Kinondoni kwamba, madarasa tunayoyapigia kampeni ya kuyajenga yatakamilika Machi na watoto kuingia, pamoja na changamoto ndogo ndogo tulizo nazo ambazo tutawaomba wadau waendelee kutuunga mkono kuzimaliza,” alisema Chongolo.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Yahya Charahani alisema kuwa Shirika limetoa vifaa hivyo ili kuhakikisha wanafunzi hawakosi masomo na wanasomea katika mazingira mazuri.
Alisema Shirika la Nyumba la Taifa liayo sera iliyojikita katika kusaidia vijana na kwamba sera hiyo imeshasaidia vijana takribani 6,000 nchi nzima kwa kuwapatia mashine za kufyatulia tofali za kufungamana kwa ajili ya kujengea nyumba na hivyo kujiongezea kipato.

“Pamoja na sera hii ya Shirika kujikita kuwasaidia vijana kujiajiri, pia shirika linasaidia katika sekta za afya na majanga mbalimbali yanayojitokeza ili kuwaokoa wanaokutikana na majanga,” alisema.

Alisema hii ni sehemu tu ta jitihada zao katika kuhakikisha sekta za elimu na afya, hasa kwa kizazi kijacho zinahudumia wananchi katika hali ya ubora.

Alisema kuwa sekta ya elimu ina changamoto nyingi lakini Shirika kwa kushirikiana na wananchi watahakikisha wanazikabili kwa kutoa misaada mbalimbali iliyomo ndani ya uwezo wao ili kuboresha mazingira ya usomaji.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo (kulia) akipokea mifuko 200 ya Saruji kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Yahya Charahani wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Turiani, Kinondoni.
Shehena ya mifuko 200 ya Saruji kutoka Shirika la Nyumba la Taifa, iliyokabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya katika Shule ya Sekondari Turiani, Kinondoni.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Turiani, Kinondoni. Kutoka kushoto ni Dereva wa Shirika la Nyumba la Taifa, Jackson Bagera, Afisa Manunuzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Paskalina Monko, Afisa elimu Sekondari wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Msigwa, Yahya Charahani na Kushoto kwa Mkuu wa Wilaya ni Afisa Huduma kwa Jamii, Yamlihery Ndullah na wa kwanza kulia ni Abeld Ngassa Joram Afisa wa NHC.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo (kulia) akisalimiana na Afisa elimu Sekondari wa Wilaya ya Kinondoni Bw. Msigwa wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa, Yahya Charahani.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo akisalimiana na Afisa Manunuzi wa Shirika la Nyumba la Taifa, Paskalina Monko.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo akisalimiana na Dereva wa Shirika la Nyumba la Taifa, Jackson Bagera.
Shehena ya mifuko 200 iliyokabidhiwa kwa Mkuu wa Wilaya katika Shule ya Sekondari Turiani, Kinondoni ikiingizwa ndani ya ghala la kuhifadhia.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete aongoza Kikao kazi cha Shirikisho za Kiuchumi za Afrika.

$
0
0
Addis Ababa, 7 February 2019.

Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika nafasi yake ya mjumbe wa taasisi ya kutokomeza malaria (End Malaria Council) jana aliendesha kikao cha kikazi na wakuu mbalimbali wa Shirikisho za Kikanda za Kiuchumi za Africa. Katika Kikao hicho Mhe. Kikwete alielezea umuhimu wa kuwekeza nguvu za pamoja katika kuutokomeza ugonjwa wa malaria katika bara letu la Afrika. 

Katika Mwaka 2017. Malaria iliua watu 435,000 duniani, wengi wao wakiwa ni watoto. Asilimia tisini ya vifo hivyo vilitokea Africa. Pamoja na kuwa kumekuwa na juhudi kubwa za kutokomeza malaria, Ugonjwa huo umeendelea kuwa tishio kubwa katika juhudi za maendeleo. Ni katika kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa huo, Mhe. Kikwete na taasisi ya kutokomeza malaria imeonelea ishirikiane na shirikisho hizo za kikanda kuwa na mikakati ya pamoja katika kutokomeza malaria.

Mhe. Kikwete aliitambulisha rasmi taasisi hiyo ya kutokomeza malaria kwa wajumbe. Taasisi hiyo iliyoanzishwa na Bill Gates pamoja na Ray Chambers kwa kushirikiana na taasisi ya wadau wa malaria inayojulikana kama Roll Back Malaria Partnership to end Malaria inajumuisha viongozi wenye nguvu za ushawishi na pia watu wenye uwezo wa kifedha ambao huziwekesha kwenye shughuli za maendeleo. 

 Wajumbe kwenye taasisi hiyo ni Bill Gates, Ray Chambers .Peter Chernin, Aliko Dangote, Mhe.Jakaya Kikwete, Graça Machel, Luis Alberto Moreno, Mhe. Ellen Johnson Sirleaf, na mwenyekiti wa ALMA ambaye kwa kipindi hiki ni Mfalme Mswati III wa Ufalme wa Eswatini.

Ikumbukwe kuwa Mhe. Kikwete ni mkereketwa mkubwa katika masuala ya Afya. Katika kipindi chake cha urais aliweza kushirikisha maraisi wa Afrika kupambana na malaria kupitia chombo alichokianzisha kinachojulikana kama African Leaders Malaria Alliance (ALMA). Katika kikao hicho Katibu Mkuu wa secretariat ya chombo hicho alimshukuru Mhe. Kikwete kwa kuanzisha chombo hicho ambacho kilianza na marais nane na sasa kinajumuisha marais wote wa Africa. 

 Naye Katibu Mkuu wa SADC Dr. Stergomena Tax, alisema taasisi yake ipo tayari kufanya kazi na Mhe. Kikwete na taasisi ya kutokomeza malaria, kwani kwa SADC suala la malaria limepewa kipaumbele kikubwa. Wajumbe wote waliokuwapo katika kikao hicho wakiwemo wawakilishi wa umoja wa Afrika na RBM walimpongeza mhe. 

Kikwete kwa uongozi wake katika masuala ya malaria na kuelezea utayari wao wa kufanya kazi pamoja naye na na taasisi ya kutokomeza malaria. 
 Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika nafasi yake ya mjumbe wa taasisi ya kutokomeza malaria (End Malaria Council) (wa pili kulia)  jana akiendesha kikao kazi cha wakuu mbalimbali wa Shirikisho za Kikanda za Kiuchumi za Africa. Katika Kikao hicho Mhe. Kikwete alielezea umuhimu wa kuwekeza nguvu za pamoja katika kuutokomeza ugonjwa wa malaria katika bara letu la Afrika. 
 Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika nafasi yake ya mjumbe wa taasisi ya kutokomeza malaria (End Malaria Council) jana akiendesha kikao kazi cha wakuu mbalimbali wa Shirikisho za Kikanda za Kiuchumi za Africa. Katika Kikao hicho Mhe. Kikwete alielezea umuhimu wa kuwekeza nguvu za pamoja katika kuutokomeza ugonjwa wa malaria katika bara letu la Afrika. 

 Picha ya pamoja 

Naibu Mawaziri watembelea Kituo cha kutoa huduma kwa pamoja cha Mtukula.

$
0
0

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) amekutana na Naibu Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Uganda, Mhe. Julius Wandera Maganda katika Kituo cha kutoa huduma kwa pamoja mpakani cha Mutukula mpakani mwa Tanzania na Uganda Tarehe 7 Februari 2019. Mara baada ya kukutana walipata fursa ya kutembelea na kujionea namna kituo cha kutolea huduma kwa pamoja mpakani cha Mtukula (OSBP) kinavyofanya kazi na kufanya Mkutano wa pamoja uliowashirikisha wadau mbalimbali kutoka Tanzania na Uganda. Mkutano huo umefanyia Mpakani mwa Tanzania na Uganda eneo la Mtukula.
Dkt. Ndumbaro akizungumza na Mhe. Waganda kabla ya kufanya mkutano wa pamoja na wadau mbalimbali. Wengine katika picha ni wajumbe walioongozana na Naibu Mawaziri hao. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt.Ndumbaro (Mb.) akizungumza kwenye Mkutano na wadau mbalimbali pamoja na jumuiya ya wafanya biashara walio hudhuria mkutano huo. 
Naibu Waziri wa Masuala ya Afrika Mashariki wa Uganda, Mhe. Maganda naye akizungumza na wadau pamoja na jumuiya ya wafanya biashara walio hudhuria mkutano huo 
Wadau kutoka upande wa Tanzania wakisikiliza kwa makini wakati Naibu Mawaziri, Mhe. Dkt. Ndumbaro na Mhe. Maganda walipokuwa wakizungumza kwenye mkutano uliyofanyika mpakani wa Tanzania na Uganda-Mtukula 
Mhe. Dkt. Ndumbaro akiwa na Mhe. Maganda wakisikiliza kwa makini michango mbalimbali ya wadau iliyokuwa ikiwasilishwa kwenye mkutano. 
Mwakilishi wa jumuiya ya wafanya biashara akichangia mada kwenye mkutano
Mmbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Uganda naye akichangia mada wakati wa mkutano huo ukiendelea.
Ujumbe wa Uganda nao wakifuatilia mazungumzo hayo kwa makini. 
Viongozi wa pande zote mbili walipata fursa ya kuzungumza na waandishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari waliohudhuria mkutano huo na kuwaelezea yaliyojiri kwenye mkutano. 
Dkt. Ndumbaro pamoja na Mhe. Maganda wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mkutano. 
Viongozi hao wakifanya ziara kwenye maeneo mbalimbali ya kituo hicho cha pamoja na kujione namana watendaji wanavyo fanya kazi kwa umakini kwa kutumia vifaa vya kisasa katika kupambana na mambo mbalimbali ikiwemo namna ya udhibiti wa magonjwa ya mlipuko. 
Dkt. Ndumbaro pamoja na Mhe. Maganda wakimsikiliza Afisa wa ukusanyaji mapato kutoka Tanzania Bw. Mohamed Shamte alipokuwa akielezea namna kituo hicho cha pamoja kinavyo fanya kazi. Naibu Mawaziri hao walijione namna watendaji wanavyofanya kazi kwa umakini kwa kutumia vifaa vya kisasa katika kupambana na mambo mbalimbali, ikiwemo udhibiti wa magonjwa ya mlipuko kama vile Ebola.. 
Dkt. Ndumbaro pamoja na Mhe. Julius wakiendelea na kukagua Kituo ili kujionea namna watendaji wake wanavyotoa huduma kwa wananchi wa pande zote mbili. 
Katika picha ni jengo la Kituo cha kutolea hudmua kwa pamoja Mtukula mpakani mwa Tanzania na Uganda. 



Akizungumza kwenye mkutano huo, Mhe. Dkt. Ndumbaro alisema lengo la ziara yao katika kituo hicho cha kutolea huduma kwa pamoja Mtukula ni pamoja na kujionea mafanikio na kubaini changamoto zinazokabili utendaji wa kazi na kuzipatia ufumbuzi. 

Akiainisha mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kituo hicho , Dkt. Ndumbaro alieleza namna mizigo mbalimbali ikipita kwa wakati kwa kuzingatia taratibu zote zilizopo pamoja na wafanyabiashara kati ya nchi hizi mbili wakifanya biashara zao bila vikwazo vyovyote vile.

Pamoja na mambo mengine Dkt. Ndumbaro alitumia fursa hiyo kuwajulisha wadau mbalimali waliohudhuria mkutano huo, kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeanzisha safari za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), kutoka Dar es Salaam, Arusha mpaka Enttebe, Uganda. Mafanikio hayo yametokana na mahusiano mazuri ya kidiplomasia yaliyopo baina ya Tanzania na Uganda na pia kupitia Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Kwa upande wake Mhe Maganda, alifurahishwa na hali ya kituo hicho namna huduma zinavyotolewa. Aidha, aliahidi kuwa Serikali ya Uganda itaongeza watendaji kazi kwenye kituo hicho ili kuwezesha upande wa Uganda kufanya kazi masaa 24 kama ilivyo kwa upande Tanzania. Pia alisisitiza nchi yake kuendelea kushirikiana na Tanzania katika masuala mbalimbali ya Ushirikiano.

Pia katika Mkutano huo wadau walitoa pongezi kwa viongozi wa Serikali za pande zote mbili kwa kuanzisha kituo hicho cha kutolea huduma kwa pamoja mpakani Mtukula, ambapo walisema kuanzishwa kituo hicho kumeongeza chachu ya maendeleo kwa wafanyabiashara wa pande zote mbili ambapo wamekuwa wakisafirisha bidhaa zao kwa wingi bila kupata changamoto kulinganisha na hapo awali kabla ya kuanzishwa kwa kituo hicho.

Kadhalika wadau walitoa pongezi kwa watendeji waliopo kituoni hapo kwa upande wa Tanzania, kwa kutoa huduma nzuri kwa masaa 24 kwenye kituo hicho ambapo, imepelekea wafanyabiashara kutokupoteza muda mwingi wafikapo mpakani hapo. 


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.

WASANII WAFURAHISHWA NA KUSIFU KASI YA UJENZI WA RELI YA KISASA YA UMEME (SGR)

$
0
0
Mataruma yakiwa tayari kwa ajili ya kupangwa kwenye tuta ili kutandika reli.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza na wasanii mbalimbali, Wachezaji wa zamani na waandishi wa habari mara baada ya kufika katika kambi kubwa ya Soga mkoani Pwani wakati wa ziara ya kutembelea na kujionea jinsi shughuli za ujenzi wa reli ya kisasa ya umeme Starndard Gauge Railway (SGR) kutoka Dar es salaam kwenda Morogoro unavyoendelea.

Wakiongeza katika ziara hiyo wasanii mbalimbali wamesifu juhudi za sreikali ya awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa utekelezaji mzuri wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2015-2020 kwa jinsi inavyotekelezwa na serikali kwa kasi kubwa na kuleta matumaini kwa watanzania.

Mradi huo unajengwa na kampuni ya Yapi Merkezi kutoka nchini Uturuki na kwa sasa ujenzi huo umefikia asilimia 42 ambapo kazi mbalimbali zinaendelea kama vile kujenga madaraja, kupasua miamba ya milima kuunganisha tuta katika vipande mbalimbali, kutandika mataruma na reli na kusimika pia nguzo za umeme katika maeneo ambayo tayari yameshatandikwa reli.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakati akitoa maelezo mbalimbali kwa wasanii mbalimbali waliotembelea mradi huo.PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-SOGA PWANI
Baadhi ya wasanii wakiwa katika eneo la Soga.
 
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakizungumza na waandishi wa habari mbalimbali ndani ya treni.
Irene Uwoya pamoja na mwenzake wakiwa wameketi kwenye reli ya kisasa ya umeme SGR baada ya kufika eneo la Soga mkoani Pwani.
Ujenzi wa madaraja ukiendelea.
Mratibu wa ziara hiyo mchekeshaji Steve Nyerere akizungumza jambo na mwigizaji Irene Uwoya.
Mitambo mbalimbali inayotumika katika ujenzi huo.
 
Baadhi ya maeneo yakiwa yamesimikwa nguzo za umeme.
 
Hii ndiyo treni ya Delux ya TRC iliyowachukuwa wasanii mbalimbali pamoja na waandishi wa habari kwa ajili ya kutembelea mradi huo.
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakimsikiliza Babu Tale Meneja wa WCB wakati akizungumza katika kambi ya Soga mkoani Pwani.
Wasanii mbalimbali wakiwa katika kambi ya Soga.
Wasanii Mchizi Mox kushoto na Mtunis ambaye ni muigizaji wa filamu wakipozi kwa picha,
Waigizaji Welu kushoto na Maya wakipozi kwa picha.
Meneja Msoko wa shirika la bima la taifa NIC Elisante Maleko akionyesha reli ya kisasa ya umeme SGR kipande kilichokamilika Shirika la bima la NIC ndilo limeikatia bima kampuni ya Yapi Merkezi inayojenga mradi huo.
Meneja Msoko wa shirika la bima la taifa NIC Elisante Maleko akiwa pamoja na wafanyakazi wenzake kutoka NIC.
 
MKuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC)Bw. Masanja Kadogosa wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasanii katika kambi kubwa ya Soga mkoani Pwani.

Mfumuko wa Bei Waendelea Kushuka hadi asilimia 3.0 Mwezi Januari 2019

$
0
0
Na; Frank Mvungi- MAELEZO

Mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Januari, 2019 umeshuka hadi asilimia 3.0 kutoka asilimia 3.3 ya mwezi Desemba mwaka 2018.

Akizungumza wakati akiwasilisha hali ya mfumuko wa bei leo Jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Sensa ya Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo, amesema kuwa kasi ya mabadiliko ya bei za bidhaa na huduma kwa mwezi Januari, 2019 umepungua ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo mwezi Desemba, 2018.

“Kupungua kwa mfumuko wa bei wa Taifa kwa mwezi Januari 2019 kunatokana kupungua kwa bei za bidhaa za vyakula katika mwezi huo ikilinganishwa na bei za mwezi Januari 2018.” alisisitiza Kwesigabo

Akifafanua, Kwesigabo amesema kuwa mfumuko wa bei wa bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa mwezi Januari umeendelea kupungua hadi kufikia asilimia 0.7 kutoka asilimia 1.0 iliyokuwa mwezi Desemba, 2018.

Aliongeza kuwa baadhi ya bidhaa zilizochangia kupungua kwa mfumuko wa bei wa mwezi Januari 2019 ni pamoja na mchele asilimia 3.9, mahindi13.9, unga wa mahindi 8.9, mtama 5.1, unga wa muhogo 6.8, maharage 4.2, choroko 10.5, mihogo mibichi 5.6, viazi vitamu kwa asilimia 3.3, magimbi 18.6 na ndizi za kupika 13.3

Kwa upande wa nchi za Afrika Mashariki, mfumuko wa bei nchini Kenya umepungua hadi asilimia 4.70 kutoka asilimia 5.71 kwa mwezi Desemba 2018, nchini Uganda mfumuko wa bei kwa mwezi Januari umeongezeka hadi asilimia 2.7 kutoka asilimia 2.2 kwa ya mwezi Desemba 2018.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ni Taasisi ya Serikali iliyoanzishwa kwa sheria ya Takwimu ya mwaka 2015 na kupewa majukumu ya kutoa, kusimamia, na kuratibu upatikanaji wa Takwimu rasmi nchini ikiwa ni pamoja na takwimu za mfumuko wa bei kwa ajili ya matumizi ya Serikali na wadau wa takwimu.
Mkurugenzi wa Sensa na Takwimu za Jamii kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo akisisitiza kuhusu kushuka kwa mfumuko wa Bei hadi asilimia 3.0 kwa mwezi Januari 2019 ikilinganishwa na asilimia 3.3 kwa mwezi Desemba 2018.

WIZARA YAKUTANA NA WATAALAM WA MAENDELEO YA JAMII, USTAWI WA JAMII NA ELIMU MKOANI NJOMBE WAWEKA MIKAKATI YA KUTOA ELIMU KWA JAMII

$
0
0

Kiongozi wa Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bi. Hanifa Selengu (kulia) akifafanua jambo kwa Wataalam kutoka Halmashauri ya Mji wa Njombe na halmashauri ya Wilaya ya Njombe katika ujio wa timu hiyo kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Maendeleo ya jamii wa Mkoa wa Njombe Bw. Cassian Nkunga akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw.Abraham Kaaya akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Mji wa Njombe Bi. Enembora Lema akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw. Averino Chaula akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Mji wa Njombe Bw. Hosea Yusto akichangia hoja katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Mwanasheria kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bw. Denis Bashaka akifafanua jambo katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Afisa Ustawi waJamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) (wa pili kushoto) Bi. Mwanaisha Moyo akifafanua jambo katika kikao kazi kilichowakutanisha Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe na Timu kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati Timu kutoka kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.
Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

……………………….

Na Mwandishi Wetu Njombe

Timu ya Wataalam kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) wamekutana na Wataalam kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Njombe na Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa lengo la kuunganisha nguvu na Serikali ya Mkoa katika kupata namna bora ya kukomesha na mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani Njombe.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Timu hiyo Bi. Hanifa Selengu amesema kuwa Wizara imeuunda Timu hiyo kwa lengo la kuunga mkono juhudi za Mkoa wa Njombe katika kutafuta namna bora ya kukomeshana mauaji ya watoto yaliyotokea mkoani humo na kuwezesha wataalam wa mkoa kwa kushirikiana na wadau kwenda kwa jamii kutoa elimu juu ya kuachana na mila zisizofaa hasa zinazoangamiza watoto.

Ameongeza kuwa lengo la kukutana na Wataalam hao ni kuandaa jumbe maalum zitakazotumika katika jamii ili kutoa hamasha kwao kuzingatia umuhimu wa malezi kwa watoto na kuachana na mila zisizofaa katika jamii elimu itakayowasaidia kutimiza majukumu yao ya kupambana na vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Akizungumza katika kikao hicho Afisa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Njombe Bw. Cassian Nkunga amewataka Maafisa hao kutoka Idara za Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu kutoa maoni yao ili yawezeshe kutengeneza jumbe maalum zitakazotumika katika jamii ili kutoa hamasha kwao kuachana na mila zisizofaa katika jamii hasa zinazoangamiza watoto.

Akitoa Taarifa ya utendaji kazi ya Idara ya Ustawi wa Jamii kwa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Afisa Ustawi wa Jamii Bw. Averino Chaula amesema kuwa Idara ya Ustawi wa Jamii ya Wilaya imeshirikiana na wadau wa watoto katika kutoa elimu kwa jamii kila mara na waliongeza nguvu kubwa mara baada ya kutokea kwa mauji ya watoto mkoani Njombe.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Bw. Abraham Kaaya ameshauri elimu kutolewa kwa jamii kwa kuwataka wanajamii kuvunja ukimya kwa kutoa taarifa ya vitendo vyote vya ukatili dhidi ya watoto.

Kwa upande wake Mwanasheria kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii) Bw. Denis Bashaka amesisitiza suala la kujikita katika kufichua tatizo linalosababisha kutokea kwa mauaji hayo na kuangalia namna bora ya kuzifikia jamii kutoa elimu na kuzingatia Sheria, Sera na Miongozo katika kuandaa jumbe hizo.

Wizara imekutana na Wataalam wao kutoka Idara ya Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Elimu mkoani Njombe kutengeneza jumbe maalaum zitakozotumika katika Jamii, Vyombo vya Habari katika kutoa elimu juu ya kuzingatia malezi bora kwa watoto na kuachana na mila zisizofaa hasa zinazoangamiza watoto.

WATUMISHI OFISI YA MWANASHERIA MKUU WATAKIWA KUTUNZA MITI WALIYOIPANDA

$
0
0
Kila jambo jemba huanza ni dua au sala, kabla ya kuaza kwa zoezi la upandaji miti, watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali mafanya maombi mafupi kumwomba Mungu aikuze miti hiyo. Pichani watumishi wakiwa wameinamisha vichwa kumwomba Mungu ashushe baraka zake katika kazi yao.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dr. Evaristo Longopa akipanda mti aina ya Ashok wakati zoezi la upandaji miti kwa watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Jumla ya miti 75 ilipandwa katika eneo linalozunguka kiwanja inapojengwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, katika Mji wa Serikali huko Ihumwa nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Dr. Longopa alitoa wito kwa watumishi hao kuwa wasiishie kupanda tu bali pia kuitunza ili ikue na kupendezesha mandhari ya Ofisi na kuhifadhi mazingira.
Watumishi wakiwa wametawanyika wakiendelea na zoezi la kupanda miti aina ya Ashok na Miti Dodoma katika kwanja panapojengwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali zaidi ya miti 600 ikiwamo ya matunda inatarajiwa kupandwa katika eneo hilo.
Baada ya kupanda miti Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliwaongoza watumishi katika kuangalia kazi ya ujenzi wa Ofisi yao ilivyokuwa ikiendelea. Pichani Naibu Mwanasheria Mkuu akiongozwa na Injinia Suma Atupele kukagua kazi ya ujenzi inavyoendelea.
Naibu Mwanasheria Mkuu akiangalia mabati yatakayotumika kuenzekea Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali huku Injia Suma Atupele akitoka maelezo


Na Mwandishi Maalum, Dodoma 

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dr. Evaristo Longopa amewataka watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhakisha kwamba, miti waliyoipanda leo inatunzwa ipasavyo na kukua ili ipendezeshe mandhari ya Ofisi na kuhifadhi mazingira. 

Dr.Longopa ametoa wito huo leo, Ijumaa, wakati alipowaongoza watumishi wa Ofisi yake katika zoezi la upandaji miti, katika kiwanja inapojengwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika Mji wa Serikali huko Ihumwa nje kidogo ya Jiji la Dodoma. 

Miti ambayo imepandwa katika zoezi hilo ni 75 kati ya 640 inayotarajiwa kupandwa katika eneo hilo. Miti hiyo 75 ni aina ya Ashoki na Miti Maji au maarufu kama miti Dodoma imepandwa kama sehemu ya mpaka wa kiwanja cha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. 

“Watumishi wenzangu, leo tunazindua zoezi la kupanda miti 75 kati ya 640 ikiwamo ya matunda ambayo tutapanda katika eneo letu. Upandaji huu wa miti unayo malengo tuseme mawili, kwanza kupendezesha mandhari ya eneo la Ofisi yetu ili yawe ya kuvutia na pili ni kuhifadhi mazingira. Niwatake basi tusiishie kupanda tu bali kila mmoja wetu ahakikishe anatunza miti hii ili iweze kukua na kustawi”. Akasema Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. 

Pamoja na Naibu Mwanasheria Mkuu kuongoza na kushiriki zoezi hilo, wangine walioshiriki ni pamoja na Mkurugenzi wa Mipango Bi. Nkuvililwa Simkanga na Bw. Jackson Nyamihula ambaye n Mkurugenzi wa Utawala na Raslimali watu. 

Kwa upande wao watumishi hao wakionesha kufurahia zoezi hilo la upandaji  miti, baadhi walipendekeza kwamba kila aliyepanda mtu aweke alama yake ili kuhakikisha kwamba kila mmoja anautunza mti wake. 

Baada ya zoezi la upandaji miti, Naibu Mwanasheria Mkuu alikwenda kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi ambapo mmoja wa ma – Injinia anayesimamia ujenzi huo Injinia Suma Atupele alimweleza Naibu Mwanasheria Mkuu kwamba kazi inaendelea vizuri ambapo kazi mbalimbali zikwamo za uchapiaji na upakaji rangi na nyinginezo nyingi zimekuwa zikiendelea kwa kasi ya kuridhisha. 

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini 
Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali 
Dodoma

Viwanda 3,504 Vimeanzishwa Nchini

$
0
0
Na: Lilian Lundo - MAELEZO, Dodoma.

Jumla ya viwanda 3,504 vimeanzishwa nchini kutokana na juhudi za kujenga uchumi wa viwanda zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano tangu iingie madarakani hadi kufikia Desemba, 2018.

Hayo yameelezwa leo Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya alipokuwa akijibu swali la mbunge wa Chumbageni, Mhe. Ussi Salum Pondeza juu ya viwanda vingapi vimeanzishwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano ianze utekelezaji wa mpango wa kuimarisha uchumi wa kati wa viwanda.

"Kati ya viwanda hivyo 3,504 vilivyoanzishwa, vinajumuisha viwanda vidogo sana 2,500, viwanda vidogo 943, viwanda vya kati 51 na viwanda vikubwa 10," amesema Mhandisi Manyanya.

Amesema wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa ikifanya tathmini ya viwanda 156 vilivyobinafsishwa na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa kwa viwanda 68 ambavyo havijaendelezwa.

Aidha amesema, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilijiridhisha na mapendekezo yaliyotolewa na kuiwezeshsa Ofisi ya Msajili wa Hazina kuchukuwa hatua.

Mhandisi Manyanya amesema hatua iliyochukuliwa na Ofisi ya Msajili ni kuvirejesha viwanda 14 Serikalini na juhudi za kuvitafutia wawekezaji wengine walio tayari kuviendeleza zinaendelea.

Ameeleza kuwa, kwa mujibu wa hali ya uchumi ya mwaka 2017, mchango wa sekta ya viwanda katika Pato la Taifa ni asilimia 5.5 ikilinganishwa na asilimia 4.9 mwaka 2016, sawa na ongezeko la asilimia 0.6.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Mhandisi Stella Manyanya
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images