Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

Watalaam wa Radiolojia kutoka Marekani wawasili Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila

$
0
0
Wataalam wa Radiolojia wakijengewa uwezo wa namna ya kutoa sampuli kwa kuongozwa na mashine ya Utrasound.
Radiolojia jpeg 03
Waalam wa Radilojia kutoka Marekani pamoja na wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila wakisoma kipimo cha Mamografia ili kubaini uvimbe uliopo kwenye matiti.
Radiolojia jpeg 04
 Dkt. Mwajuma Jumbe akitumia mashine ya Utrasound kupima uvimbe kwenye titi ili kubaini sehemu ambayo uvimbe upo.
Radiolojia 05
Dkt. Tim Rooney (kulia) pamoja na Madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila wakitoa sampuli ya uvimbe kwenye titi bila kufanya upasuaji (Core Biopsy) kwa kuongozwa na mashine ya Utrasound leo hospitalini hapo.
Radiolojia jpeg 01
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Prof. Lawrence Museru akipokea maelezo mara baada ya kuwasili kwa timu ya watalaam wa Radiolojia kutoka nchini Marekani.

                                                       
Timu ya watalaam wa Radiolojia kutoka nchini Marekani wamewasili katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila kwa ajili ya kuwajengea uwezo watalaam wa hospitali hiyo wa kutoa sampuli kwenye vivimbe vya kwenye matiti kupitia njia ya kitaalam (Core Biopsy).

Watalaam hao kwa kushirikiana na wataalam wa Hospitali ya Mloganzila watatoa sampuli kwa watu zaidi ya 50 ambao wana vivimbe kwenye matiti ambapo watashirikiana kutoa huduma hiyo kwa zaidi ya wiki mbili.

Februari 02 hadi Februari 03 mwaka huu Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mloganzila kwa kushirikiana na Madaktari kutoka Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania-MEWATA- walitoa huduma bure ya uchunguzi awali wa kuangalia uvimbe kwenye matiti.Katika zoezi hilo watu zaidi ya 130 walifanyiwa uchunguzi, kati ya hao 36 wamekutwa na vivimbe.

MWENYEKITI WA CCM RAIS DKT. MAGUFULI AIPATIA CHANNEL TEN MILIONI 200 KAMA ALIVYOAHIDI JANA

$
0
0
 Katibu wa NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akimsikiliza mmoja wa wafanyakazi wa Channel Ten Bi. Siri Pambe akisoma hundi ya Shilingi Milioni 200 kabla hajaikabidhi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya African Media Group Limited (AMBL)  Jaffari Haniu kama ilivyoahidiwa jana na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kununua vifaa kuimarisha utendaji wa televisheni hivyo. Akishuhudia kulia ni Katibu wa Mwenyekiti wa CCM Ndg. Ngusa Samike
 Katibu wa NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akimkabidhi  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya African Media Group Limited (AMBL)  Jaffari Haniu hundi ya shilingi Milioni 200 aliyoahidiwa jana na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kununua vifaa kuimarisha utendaji wa televisheni hivyo. Akishuhudia kulia ni Katibu wa Mwenyekiti wa CCM Ndg. Ngusa Samike
  Katibu wa NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akiongea machache baada ya kumkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya African Media Group Limited (AMBL)  Jaffari Haniu hundi ya shilingi Milioni 200 aliyoahidiwa jana na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kununua vifaa kuimarisha utendaji wa televisheni hivyo. Akishuhudia kulia ni Katibu wa Mwenyekiti wa CCM Ndg. Ngusa Samike
 Katibu wa NEC Idara ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya African Media Group Limited (AMBL)  Jaffari Haniu akitoa shukurani  baada ya kukabidhiwa hundi ya shilingi Milioni 200 aliyoahidiwa jana na Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ili kununua vifaa kuimarisha utendaji wa televisheni hivyo. Akishuhudia kulia ni Katibu wa Mwenyekiti wa CCM Ndg. Ngusa Samike. PICHA NA IKULU

RAIS DKT. MAGUFULI ASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA NCHINI, AZINDUA MAHAKAMA INAYOTEMBEA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kuzindua rasmi gari maalumu litakalotumika kama Mahakama inayotembea  akiwa na  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, , Mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Sophia Mjema wakati wa   maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ndani ya gari maalumu litakalotumika kama Mahakama inayotembea  baada ya kuizindua rasmi akiwa na  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Jaji Kiongozi Dkt. Eliezer Fereshi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Mbarouk Salum Mbarouk, Mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia nchini Bi. Bella Bird, wakati wa   maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019. Anayetoa maelekezo ni Mkuu wa Kitengo cha TEHEMA wa Mahakama ya Tanzania Bw. Enock Kalege na Kulia kabisa ni Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mashauri Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitelemka kutoka kwenye gari maalumu litakalotumika kama Mahakama inayotembea baada ya kulizindua rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongozana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mhe. Job Ndugai na Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma wakati alipowasili kuhudhuria  maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia  kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza  Mkuu wa Kitengo cha TEHEMA wa Mahakama ya Tanzania Bw. Enock Kalegebaada ya kuzindua rasmi Mfumo wa Kielektroniki wa Kuratibu Mashauri (DSDS ll)  wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Majaji Wakuu Wastaafu Mhe. Augustino Ramadhani na Mhe. Mohamed Chande Othmana kabla ya kupiga nao picha ya kumbukumbu kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Spika Job Ndugai, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma, Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi, Jaji Kiongozi Dkt. Eliezer Fereshi na Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Mbarouk Salum Mbarouk  baada ya kuhudhuria   kwenye maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Februari 6, 2019.
PICHA NA IKULU

AGPAHI YAKABIDHI MAGARI KUKABILIANA NA UKIMWI SHINYANGA, RC APONGEZA

$
0
0

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack ameipongeza Asasi ya kitaifa inayolenga kutokomeza UKIMWI kwa watoto na familia, Ariel Glaser Pediatric AIDS Health Initiative (AGPAHI) kwa jitihada inazozifanya katika kuboresha utoaji wa huduma za Virusi Vya UKIMWI (VVU) na UKIMWI mkoani Shinyanga.

Mhe. Telack ametoa pongezi hizo leo Jumatano Februari 6,2019 wakati akipokea magari mawili aina ya Nissan Patrol yenye thamani ya shilingi milioni 186.5 yaliyotolewa na AGPAHI kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI katika halmashauri za wilaya za Kahama Mji na Ushetu.

Alisema AGPAHI wamekuwa wadau bora katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI na kuwaomba kuendelea kushirikiana na serikali katika kuwahudumia wananchi.

Alisema kutokana na juhudi zinazofanywa na wadau wakiwemo AGPAHI kwa kushirikiana na serikali takwimu za maambukizi ya UKIMWI mkoani Shinyanga zimepungua kutoka asilimia 7.4 mwaka 2011/2012 hadi kufikia asilimia 5.9 mwaka 2016/2017. “Kazi mnayofanya ni ya kujenga familia za Watanzania,niwashukuru sana kwa ushirikiano mkubwa mnaotupatia,naomba tuendelee kushirikiana”,alisema Mhe. Telack. 

“Leo nimepokea magari haya mawili na sasa idadi ya magari yaliyotolewa na AGPAHI mkoani hapa tangu ilipoanza kazi zake,yanakuwa manne,naomba mtupatie pia magari kwa ajili ya Halmashauri ya wilaya ya Shinyanga na Manispaa ya Shinyanga kwani napo bado wananchi wanahitaji elimu ya VVU na UKIMWI”,aliongeza Mkuu huyo wa mkoa. 

Aidha aliahidi kuwa, magari hayo yatatumika kwa malengo yaliyokusudiwa huku akiwataka Wataalamu wa afya kutumia magari kuwafikia wananchi wengi zaidi yakiwemo maeneo ya wachimbaji madini na kuwaelimisha kuhusu masuala ya VVU na UKIMWI. 

Akikabidhi magari kwa mkuu wa mkoa, Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa alisema magari hayo yatasaidia katika kuboresha utoaji wa huduma na kuongeza tija katika kuboresha huduma za VVU na UKIMWI. 

“Tunatambua kuwa wilaya ya Kahama ina kiwango kikubwa cha maambukizi ya VVU, ndiyo maana tumeona vyema tutoe magari Kahama Mji na Ushetu kwani uhitaji ni mkubwa ili kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI tukishirikiana na serikali”,alisema Dk. Sekela. 

“Mbali na kutoa magari pia tulishatoa pikipiki na baiskeli. Aidha tumekarabati vituo vya kutolea huduma na tumewezesha ajira na mafunzo mbalimbali ya utoaji huduma za VVU na UKIMWI”,alisema. 

Aidha alieleza kuwa, katika kipindi cha kuanzia Januari 2017 hadi Disemba 2018, AGPAHI imefanikiwa kupima VVU watu 905,724 mkoani Shinyanga ambapo watu 27,724 wanaoishi na VVU walianzishiwa dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs) katika vituo 107 vya kutolea huduma. 

“Katika kipindi hicho pia akina mama wajawazito 140,173 walipimwa VVU ambapo 6,555 walionekana kuambukizwa.WAVIU wamama 6,481 (98.9%) walianzishiwa dawa na watoto 4,877 (96%) walizaliwa bila maambukizi”,alifafanua Dk. Sekela. 

Magari hayo yamekabidhiwa na AGPAHI kwa ufadhili wa Watu wa Marekani kupitia Mfuko wa Dharura wa Rais wa Marekani wa Kupambana na UKIMWI (PEPFAR) chini ya Vituo vya Kudhibiti Magonjwa na Kinga (CDC). 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack akizungumza wakati Asasi ya AGPAHI ikikabidhi magari mawili yenye thamani ya shilingi milioni 186.5 kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI katika halmashauri za wilaya za Kahama Mji na Ushetu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa, kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, Albert Msovela. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog 
Muonekano wa magari yaliyo magari mawili yaliyotolewa na AGPAHI kusaidia utoaji wa huduma za VVU na UKIMWI katika halmashauri za wilaya za Kahama Mji na Ushetu. 
Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa akimweleza jambo Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mheshimiwa Zainab Telack wakati akimkabidhi funguo za moja ya magari hayo ili akague. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack akijiandaa kuingia ndani ya gari wakati Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga, Albert Msovela akikagua gari. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack akiwasha gari ikiwa ni sehemu ya ukaguzi.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack akikabidhi ufunguo wa gari kwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Ushetu, Michael Augustino Matomora (wa kwanza kushoto mwenye suti nyeusi) na Mwenyekiti wa halmashauri ya Ushetu, Juma Kimisha (katikati).
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack akimkabidhi ufunguo wa gari Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Kahama Mji, Anderson Msumba (kushoto).
Kushoto ni Mwenyekiti wa halmashauri ya Ushetu, Juma Kimisha akipokea kadi ya gari. 
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack na Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa wakibadilishana hati za makabidhiano ya magari.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mheshimiwa Zainab Telack (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa wakisaini hati za makabidhiano ya magari mawili aina ya Nissan Patrol yenye thamani ya shilingi milioni 186.5.
Mratibu wa Mradi AGPAHI mkoa wa Shinyanga, Dk. Gastor Njau (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Ushetu, Michael Augustino Matomora nao wakisaini hati za makabidhiano ya magari.
Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa akimkabidhi Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack nakala ya Mpango Mkakati wa AGPAHI 2018-2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa (kulia) akieleza mafanikio ya AGPAHI hadi kufikia Septemba 2018 ambapo alisema watu 395,777 wanapatiwa huduma za VVU na UKIMWI katika vituo vya kutolea huduma katika mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara. Watu 248,000 wakiwemo watoto 13,600 wanatumia dawa za kupunguza makali ya VVU.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Dk. Rashid Mfaume akiishukuru AGPAHI kwa kuendelea kushirikiana na serikali katika kutoa huduma za VVU na UKIMWI. 
Mkurugenzi Mtendaji wa AGPAHI, Dk. Sekela Mwakyusa (kushoto) akiagana na Mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack baada ya kukabidhiana magari. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Jafo aonyesha mfano wa matumizi bora ya Force Account

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akiwaonyesha jengo la TAMISEMI (halipo pichani) wakati wa ziara yake na Makatibu Tawala, Wenyeviti wa halmashauri na Wakurugenzi kuwaonyesha mfano bora wa matumizi ya Force Account
Muonekano wa Jengo la Ofisi ya Rais TAMISEMI linaloendelea kujengwa katika Mji wa Serikali Ihumwa.
1. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akiwasili katika jengo la TAMISEMI linaloendelea kujengwa katika Mji wa Serikali Ihumwa kuwaonyesha Makatibu Tawala, Wenyeviti wa halmashauri na Wakurugenzi mfano bora wa matumizi ya Force Account.
1. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akielezea namna jengo la TAMISEMI litakavyokuwa wakati wa ziara yake na Makatibu Tawala, Wenyeviti wa halmashauri na Wakurugenzi kuwaonyesha mfano bora wa matumizi ya Force Account.

Majid Abdulkarim 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo ameonyesha matumizi bora ya utekelezaji wa miradi bila kutumia mkandarasi maarufu kama ‘Force Account ‘ kwa Makatibu Tawala wa Mikoa ,Wenye viti wa Halmashauri, Wakurungezi na Maafisa mipango wa Halmashauri kwa kuwapeleka kwenye mradi wa Ofisi za Jengo la Ofisi ya Rais TAMISEMI linaloendelea kujengwa katika mji wa Serikali Ihumwa Jijini Dodoma. 

Jafo amefanya ziara hiyo baada ya kikao chake cha maelekezo kwa viongozi hao ambao halmashauri zao zilifaulu vigezo na kusaini fedha za kutekeleza miradi ya kimkakati awamu ya Pili. 

Akizungumzia Force Account Jafo alisema kuwa nimeamua kutekeleza kwa vitendo yale ninayowaagizaga wakati wote wa maelekezo yangu kuhusu kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika maeneo yenu. 

Katika ujenzi wa Jengo hili la Ofisi za Wizara tuliamua na kukubaliana kwa pamoja kutumia mfumo ule ule ambao unatumika katika halmashauri zetu sio sisi tunatoa tu maagizo lakin hatutendi na sasa kupitia mradi huu tumeamua kuwa mfano halisi wa yale tunayoyazungumza alisema Jafo. 

Aliongeza kuwa katika mfumo huu wa force Account tumeweza kusimamia jengo hili kupitia kamati nne ambazo ni Kamati ya manunuzi, Kamati ya Vifaa, Kamati ya ujenzi na ile ya usimamizi na ufuatiliaji. 

“Mradi huu umekuwa na tija pia kwa jamii kwani umetengeneza ajira kwa vijana wetu kwani wao ndo wamekua nguvu katika kufanya shughuli zote za ujenzi kuendelea kwa mujibu wa maelekzo ya wahandishi ambao wanatokea Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na msimamizi wa mradi huu”Amesema Jafo 

Wakati huo huo Jafo aliongeza kuwa ujenzi wa Jengo hili la kisasa zaidi linagharimu shilingi billion moja tu Fedha zilizo tolewa na Rais Magufuli kwa kila Wizara kwa ajili ya kujenga Ofisi katika Mji wa Serikali Ihumwa. 

“Nataka niwahakikishie kuwa ujenzi wa jengo hilo umeratibiwa na mimi mwenyewe Waziri wa TAMISEMI ambapo niliwaunganisha viongozi wote wakuu wa Wizara pamoja na watendaji wa Wizara ili kuleta matokeo makubwa na ya haraka” 

Sasa kama mimi nimeweza wewe kwanini ushindwe na jengo hili limeanza kujengwa mwezi Disemba 2018 na kama mnavyoona sasa hivi jengo limeshafikia hatua ya mtamba wa panya kwahiyo kasi ya ujenzi iko vizuri sana na tutamaliza ujenzi huu ndani ya muda mfupi ujao; Nataka na nyie mkafanye hivi kwenye maeneo yenu alimalizia Jafo. 

Kwa kuongezea Jafo amazitaka halmashauri zilizo pata fedha ya kutekeleza miradi ya Kimkakati kuanza mipango ya utekelezaji wa miradi hiyo mapema iwezekanavyo ili fedha hizo zitakapo wasili katika halmashauri hizo miradi ianze mara moja na ili iweze kumalizika kwa wakati ulopangwa. 

Aidha naye Katibu Tawala Mkoa wa Tanga Eng.. Zenah Saidi ametoa shukrani za dhati kwa Mhe.Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa fedha hizo na kuhaidi kusimamia kwa umakini na kuhakikisha zinatekeleza miradi huska kwa ufasa na ubora wa miradi hiyo kuendana na thamani ya fedha hiyo. 

“Ni toe wito kwa viongozi wa halmashauri kuwa sasa ni wakati wa kutekeleza miradi hii kwa kutumia mfumo wa Force Account kwani kila mmoja wetu kapata kushuhudia kwa macho yake namna ya mfumo huu unavyo tumika na faida zake kazieleza Bi.Zenah 

Kwa kuhitimisha Bi.Zena amewataka viongozi wenzake kuwa makini wakati wa kutafuta wakandarasi wa kutekeleza miradi kwa wengi wao katika makaratasi wanakuwa vizuri lakini katika utekelezaji hakuna kitu. 

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI FEBRUARI 7,2019

WAZIRI MPINA ATOA MAAGIZO MAZITO

$
0
0
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina 



Na John Mapepele, Mpwapwa

WAZIRI waMifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amemuagiza Mkurugenzi waUtafiti, Mafunzo na Ugani kuandaa haraka kanuni na mwongozo utakaosimamia kuanzia uvunaji wa mbegu, uuzaji, usambazaji na uhimilishaji na uhamilisha mifugo kabla ya mwezi Machi mwaka huu ili kuwadhibiti madalali wote wanaokwenda kuwaumiza wananchi kwakutumia kivuli cha Serikali. 

Akizungumza mara baada ya kutembelea Mradi wa uzalishaji kwa kutumia teknolojia ya viinitete na uhawilishaji (MOET) unaotekelezwa na TaasisiyaUtafitiwaMifugo (TALIRI) Kituo cha Mpwampwa mkoani Dodoma, Waziri Mpina alisema watanzania wajivunie mradi huo ambao niwa kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati. 

Alisema kupatikana kwa teknolojiaya MOET kumeiwezesha Tanzania kuwa na njia tatu za kuboresha Koosafu ya mifugoa mbapo ni njia ya asili ya kutumia madume bora, uhimilishaji (AI) na Uhamilishaji (MOET) ambapo itachochea mageuzi makubwa ya uboreshaji wakoosafu ya mifugo ambayo itaongeza uzalishaji wa maziwa, nyama, ngozi na mazao mengine ya mifugo. 

Aidha aliagiza kuwa kila ifikapo mwezi Machi ya kila mwaka idara yake iwe imepeleka ajenda za kufanyiwa utafiti kwenye Taasisi ya Utafiti wa Mifugo ili kupata matokeo ya tafiti ambazo watanzania wanaumiza vichwa kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayowakabili na kuweka utaratibu wakupokea tafiti kutoka nje ya nchi.

Pia amemwagiza Mkurugenzi huyo waUtafiti, Mafunzo na Ugani kukutana na wazalishajiwamayai, vifaranga, ng’ombe, kuku, mbuzi, kondoo, punda, nguruwe, viwanda vya nyama, ngozi na maziwa ili kujua mahitaji yao kwasasa ni yepi kwani waondio wataotengeneza ajenda za utafiti zenye uhitaji kwasasa. 

Amekosoa mfumo wa uendeshaji wa tafiti za mifugo nchini kwakutokuwa na ajenda mahususi zinazohitajika kufanyiwa tafiti badala yake watafiti wengi wamekuwa wakiendesha tafiti za biashara kwa mataifa mengine ambazo hazina msaada kwa watanzania. 

Amesema mfumo wakuibua ajenda za utafiti haufahamiki huku kukiwa na ushirikishwaji dhaifu wa wadau hali inayosababisha tafiti nyingi kushindwa kutoa majawabu ya matatizo katika sekta ya mifugo nchini huku matokeo na mazao yatafiti hizo yakiwafikia watu wachache kinyume na malengoyaSerikali. 

Waziri Mpina alisema pamoja na kuwepo kwa njia zote hizo za uboreshaji Koosafu za mifugo bado kuna kasoro nyingi katika utaratibu unaotumika kuzalisha, kununua, kusambaza na kupandisha mifugo halii nayopelekea zoezi kuwa la kusuasua. 

Alisema pamoja na mbegu hizo kuzalishwa na Serikali na kuuzwamrijammojakwash 3,000 lakini kutokana na kutokuwepo mfumo madhubuti wa usimamizi na kuachiwa wafanyabiashara binafsi kwenda kuwauzia wafugaji katiyash 20,000 hadish 60,000 kwa mrija jambo linawakatisha tamaa wafugaji na kutofikiwa malengo ya Serikali. 

Hivyo Waziri Mpina alisema juhudi zote zinazofanywa na Serikali za kuzalisha mbegu bora katika vituo vyake vya NAIC Arusha na Taliri Mpwapwa haitakuwa na maana kama kasoro zilizopo sasa hazitaondolewa. 

Kwa upande wake MkurungeziwaUtafiti, Mafunzo na UganiwaWizarayaMifugo na Uvuvi, Dk. Angello Mwila waalimhakikishia Waziri Mpina kuwa atasimamia kikamilifu utekelezaji wa maagizo yake ili kuhakikisha wafugaji wananufaika na jitihadahizozinazofanywa na Serikali ya awamu ya tano katika mkakati wake wauboreshaji wa koosafu ya mifugo nchini. 

Naye Mkurungezi Mkuu wa TARILI, Dk. Eligy Shirima alisema mradi huo wa MOET unafadhili na COSTECH kwa gharama ya sh milioni 400 kwa ajili ya kununua vifaa vitakavyowezesha kukamua mbegu za dume na kuziweka kwenye jike maalum lililoandaliwa. 

Dk Shirima alisema jike hilo baada ya kuwekewa hormones husaidia mayai mengi kuiva kwa maramoja na kurutubishwa ambapo mbegu zilizorutubishwa hunyonywa na kuhifadhiwa na kisha kusambazwa kwa wafugaji kwaajili ya uhamilishaji hatua ambayo itawezesha kupatika namifugo bora.

KKKT MERU YAWEKA BARAKA UJENZI WA MADARASA

$
0
0
Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Meru Baba Elias Kitoi Nassari amepongeza kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa inayofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Cornel Muro ambapo amesema kanisa mbali na kupongeza linaunga mkono jitihada hizo.

Askofu Nassari amezungumza hayo jana Februari 6/2019 alipomtembelea Mkuu wa wilaya ya Arumeru ofisini kwake kwa lengo la kumpongeza kwa kazi Kubwa anayoifanya katika sekta ya Elimu na Afya huku akiwa ameambatana na Uongozi Mkuu wa kanisa Dayosisi ya Meru akiwepo Mchungaji Ndelekwa Kuvavanael Pallangyo Msaidizi wa Askofu, Ndugu Lazaro Andrew Katibu Mkuu wa Dayosisi na Ndugu Elisate Manyaeli Maturo Mtunza Hazina Wote ni kutoka KKKT Dayosisi ya Meru

Katika kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Mkuu wa wilaya ya Arumeru Baba Askofu Nassari amemkabidhi Lori lililoleta shehena ya mifuko ya saruji Kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika halmashauri ya Meru.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Arumeru Ndugu Jerry Muro mbali na kupokea pongezi na salamu za Kanisa, ameshukuru msaada wa shehena ya mifuko ya saruji iliyotolewa na kanisa, ambapo amemuhakikisha Baba Askofu Nassari kuwa Serikali ya wilaya ya Arumeru itaendelea kushirikiana na kanisa katika sekta zote za utoaji wa huduma Kwa wananchi.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mh.Jerry Cornel akimshukuru Askofu Nassari kwa mchango alioutoa katika kuunga mkono kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa aliyekuwa sambamba na Uongozi Mkuu wa kanisa Dayosisi ya Meru akiwepo Mchungaji Ndelekwa Kuvavanael Pallangyo Msaidizi wa Askofu, Ndugu Lazaro Andrew Katibu Mkuu wa Dayosisi na Ndugu Elisate Manyaeli Maturo Mtunza Hazina Wote ni kutoka KKKT Dayosisi ya Meru

Askofu Nassari akimpongeza Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mh.Jerry Cornel Muro ofisini kwake kwa kazi Kubwa anayoifanya katika sekta ya Elimu na Afya huku akiwa ameambatana na Uongozi Mkuu wa kanisa Dayosisi ya Meru akiwepo Mchungaji Ndelekwa Kuvavanael Pallangyo Msaidizi wa Askofu, Ndugu Lazaro Andrew Katibu Mkuu wa Dayosisi na Ndugu Elisate Manyaeli Maturo Mtunza Hazina Wote ni kutoka KKKT Dayosisi ya Meru
Mkuu wa wilaya ya Arumeru,Mh.Jerry Cornel akimshukuru Askofu Nassari kwa mchango alioutoa katika kuunga mkono kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa

Vodacom, CCBRT waungana kutokomeza fistula.

$
0
0
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Tanzania, Bi Rosalynn Mworia (wa pili kushoto) akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwatambua wanawake wenye Fistula na kuwawezesha kufika hospitali kupata matibabu kwa kutumia mfumo wa Vodacom M-Pesa kwa mabalozi wapya 50. Mafunzo hayo yamedhaminiwa na Vodacom Foundation Tanzania kwa kushirikiana na hospitali ya CCBRT. M-Pesa inatumika kuwatumia waathirika pesa ambazo zinakidhi mahitaji yao na usafiri mpaka kufika CCBRT au hospitali washirika kupata matibabu. Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT, Brenda Msangi. 
Mkurugenzi wa Vodacom Foundation Tanzania, Bi Rosalynn Mworia (kushoto) akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwatambua wanawake wenye Fistula na kuwawezesha kufika hospitali kupata matibabu kwa kutumia mfumo wa Vodacom M-Pesa kwa mabalozi wapya 50. Mafunzo hayo yamedhaminiwa na Vodacom Foundation Tanzania kwa kushirikiana na hospitali ya CCBRT. M-Pesa inatumika kuwatumia waathirika pesa ambazo zinakidhi mahitaji yao na usafiri mpaka kufika CCBRT au hospitali washirika kupata matibabu. Wa kwanza kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT, Brenda Msangi. 
Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation Bi Rosalynn Mworia (kulia) akisalimiana na baadhi ya wagonjwa wanaopata matibabu ya Fistula mara baada ya kuwasili kwenye Hospitali ya CCBRT wakati wa mafunzo ya kuwatambua wanawake wenye Fistula na kuwawezesha kufika hospitali kupata matibabu kwa kutumia mfumo wa Vodacom M-Pesa kwa mabalozi wapya 50. Mafunzo hayo yamedhaminiwa na Taasisi ya Vodacom Foundation Tanzania kwa kushirikiana na hospitali ya CCBRT. M-Pesa inatumika kuwatumia waathirika pesa ambazo zinakidhi mahitaji yao na usafiri mpaka kufika CCBRT au hospitali washirika kupata matibabu. 



Katika kuunga mkono na kuongeza nguvu juhudi za kutokomeza fistula nchini, Taasisi ya Vodacom Tanzania Faundation kwa kushirikiana na hospitali ya CCBRT wametoa mafunzo ya kuwatambua wanawake wenye Fistula na kuwawezesha kufika hospitali kupata matibabu kwa kutumia mfumo wa Vodacom M-Pesa kwa mabalozi wapya 50. M-Pesa inatumika kuwatumia waathirika pesa ambazo zinakidhi mahitaji yao na usafiri mpaka kufika CCBRT au hospitali washirika kupata matibabu. 

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wafanyakazi wa vituo vya afya na wadau mbalimbali kutoka ofisi za serikali. Programu hii ya “Fistula inatibika” ilianza mwaka 2012 na imelenga kuwasaidia wanawake wanaoishi na hali ya fistula kupata matibabu ya kiafya na kisaikolojia kwa sababu wengi wao hutengwa na jamii zinazowazunguka kutokana na ugonjwa huo, pamoja na kuwawezesha kurejea katika hali zao za kawaida na kujumuika kwenye jamii zao. 

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Foundation Bi Rosalynn Mworia alisema, “Mabalozi hawa wanaungana na mabalozi wengine zaidi ya 3000 wa fistula waliopo sehemu mbalimbali nchini, wenye uwezo wa kutambua na kuwawezesha waathirika wa Fistula kufika hospitali ya CCBRT au vituo vingine vya afya vinavyotoa matibabu hayo kama; Bugando (Mwanza), KCMC (Kilimanjaro), Nkinga (Tabora), Peramiho Mission Hospital (Ruvuma), Kabanga Mission Hospital (Kigoma), Songea Regional Hospital (Ruvuma) na Selian (Arusha) kwa kutumia mfumo wa M-Pesa. Nawasihi mabalozi hawa kutoa mafunzo kwa jamii zao kuhusu fistula kwa kuandaa semina ambazo zitaambatana na majadiliano ya changamoto mbali mbali zinazotokana na fistula”. 

Shirika la Afya duniani (WHO) linakadiria kwamba wanawake 3000 hupata tatizo la fistula kila mwaka nchini Tanzania. Hivyo mpango huu ulianzishwa na Vodacom Tanzania Foundation kama sehemu ya kuisaidia serikali kuboresha huduma za afya nchini na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. 

“Fistula ni hali inayozuilika na kutibika hivyo inabidi tuidhibiti kabisa. Katika karne hii hakuna mwanamke anayestahili kutengwa au kunyanyapaliwa na jamii yake kwa sababu ya fistula. Ninapongeza juhudi za taasisi ya Vodacom Tanzania Foundation katika kukabiliana na matatizo ya kiafya yatokanayo na uzazi nchini. Tunahitaji kukabiliana na mzigo huu wa akina mama wenye matatizo haya katika jamii zetu,” alisema Afisa Mtendaji mkuu wa hospitali ya CCBRT bi Brenda Msangi. 

Wanawake wenye fistula wana changamoto kubwa ya kutengwa katika jamii zao na wengi wao hawatambui kama hali hii inatibika kutokana na ukosefu wa elimu na taarifa. Utumiaji wa mabalozi wa Fistula ni hatua muhimu zaidi maana wao hutumika katika kuwatambua na kuwapa rufaa wanawake wanoishi na hali ya Fistula 

“Mwaka wa kwanza baada ya kuanza kutumia M-pesa kutoka Vodacom katika mfumo wetu wa rufaa tulishuhudia ongezeko la asilima 65 ya wanawake waliotibiwa ugonjwa wa fistula, kufikia mwaka 2016, asilimia 87 ya wagonjwa wa fistula walipata rufaa kupitia mfumo wa M-Pesa ambao tunashirikiana na Vodacom Tanzania Foundation, wakafanikiwa kufika CCBRT ambapo tulifanya upasuaji wa wagonjwa 1,012”, aliongeza Bi Msangi.

WAZIRI MKUU ATOA MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU UWEKEZAJI NCHINI

$
0
0

Na Said Mwishehe, Blog ya jamii

WAZIRI Mkuu Kassim Majali ametoa msimamo wa Serikali ya Awamu ya Tano kuwa mkakati wake ni kuendelea kuhamsisha uwekezaji nchini huku akitoa mwito kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika maeneo mbalimbali kwani mazingira ya uwekezaji ni salama.

Ametoa kauli hiyo leo Februari 7 , 2019 Bungeni Mjini Dodoma wakati anajibu maswali ya papo kwa papo ambapo moja ya swali aliloulizwa ilikuwa ni kufahamu msimamo wa Serikali kuhusu wawekezaji nchini ambapo alianza kujibu kwa kueleza kuwa msimamo wa Serikali ni kuendelea kuhamasisha wawakezaji kuwekeza nchini.

"Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli imeendelea kuwahamasisha wawakezaji wakiwamo wa nje kuja kuwekeza nchini na ndio maana mazingira mazuri ya uwekezaji yamekuwa yakiandaliwa nchini kwetu.Hivyo msimamo wa Serikali ni kuendelea kuwahamasisha wawakezaji waje kuwekeza.

"Mazingira ya kuwekeza katika nchi yetu ni mazuri na yako salama salama sana.Tutanaahidi tutaendelea kulinda wawekezaji mbalimbali ambao wamewekeza nchini wakiwamo waliwekeza kwa kujenga viwanda ndani ya nchi yetu,"amesema .

Waziri Mkuu huku akisisitiza jukumu la Serikali ni kuendelea kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji.Wakati huo huo Waziri Mkuu aliulizwa ni hatua gani ambazo Serikali inachukua katika kuboresha mazingira ya biashara nchini, ambapo amejibu kuwa zipo hatua mbalimbali zinaendelea kuchukuliwa kuhakikisha mazingira ya ufanyaji biashara unakuwa rafikia.

Amefafanua hata uamuzi wa Rais Dk.John Magufuli kugawa vitambulisho kwa ajili ya wafayabiashara wadogowadogo ni mkakati wa kuendelea kuweka mazingira mazuri ya wananchi kufanya biashara bila kusumbuliwa."Kama nilivyojibu kuhusu mazingira ya uwekezaji yaliyopo nchini, ndivyo ambavyo Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji wa biashara.Kuna mambo mengi yamekuwa yakifanyika kuboresha mazingira ya biashara nchini kwetu,"amesema Waziri Mkuu.

ACB WAJIZATITI KUWAINUA KIUCHUMI WAJASILIAMALI WADOGO NA WA KATI KWA MWAKA 2019

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

BENKI ya Akiba Commercial (ACB)   imejizatiti katika kuwainua wajasiliamali wadogo na wa kati (MSMEs) kwa kuwapatia mikopo nafuu na ya muda mrefu.

Hayo yalisemwa wakati benki hiyo wakitangaza matokeo mazuri ya fedha ya nusu ya pili ya mwaka 2018 kwa kupata faida ghafi yaani Pre-tax ya Bilion 1.2 ikwia ni katika ukuaji wa asilimia 600 ikilinganishwa na kipindi cha mwaka 2017.

Akizumgumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa ACB Augustine Akowuah amesema anafarijika na matokeo hayo ya nusu ya pili ya mwaka 2018 kwani mizania ya malengo yao kuanzia mwaka yamesababisha kuwa na muelekeo mzuri wakati wakifungua mwaka.

Amesema kuwa, wamefurahi hatua hiyo kwa kuwa mikakati mingi waliyojiwekea imeleta mabadiliko kwenye benki yao kwa muda mrefu japokuwa hali haikuwa nzuri mwanzoni mwa mwaka.

"Katika kipindi cha mwaka 2018, ilitelekeza mikakati ya kupunguza mikopo chechefu, kuimarisha makusanyo ya madeni sugu na utoaji wa mikopo mipya kwa kuzingatia ubora, hatua tulizochukua ikiwemo kunadilisha na kupitia majukumu ya kazi zililenga zaidi kwenye kuimarisha hatari zinazotokana na ukopeshaji,"amesema Akowuah. 

Afisa Biashara wa ACB, Felician Girambo amesema kuwa benki hiyo kwa mwaka huu 2019 wamejizatiti kuendelea na matokeo chanya kwani wamelenga kujena maendeleo chanya yaliyopatikana kwa mwaka 2018 ikiwemo jukumu pelee la kusaidia wajasiriamali wadogo na waka kati (MSMEs) nchini Tanzania kwa kutumia huduma bora za kifedha.

Girambo amesema mjasiriamali yoyote mwenye leseni ya biashara ana uwezo wa kupata mkopo hata kama hatakuwa na akaunti katika benki yao ila itamlazimu afungue kwa wakati huo, pia amesema mjasiriamali itamtaka awe na msingi utakaokuwa mara ya mbili ya mkopo anaohuitaji kwa wakati huo.

Ameongezea kuwa, kwa mwaka 2019 wamedhamiria kufikia lengo la kuwapatia mikopo wajasiriamali  12,000 kwa mwaka mzima na mikopo yao inarejeshwa kulingana na aina ya mkopo uliochukua.

Benki hiyo inajumla ya miaka 20 toka kuanzishwa kwake na ina matawi 18 katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Dodoma, Mbeya, Moshi na Mwanza.
Mkurugenzi Mtendaji Benki  ya Akiba Commercial (ACB) Augustine Akowuah akizungumzia matokeo mazuri ya fedha ya nusu ya pili ya mwaka 2018 kwa kupata faida ghafi yaani Pre-tax ya Bilion 1.2 ikwia ni katika ukuaji wa asilimia 600 ikilinganishwa na kipindi cha mwaka 2017.
Afisa Biashara wa Benki ya Akiba Commercial (ACB)
, Felician Girambo akizungumzia mikopo kwa 
 wajasiriamali wadogo na waka kati (MSMEs) nchini Tanzania kwa kutumia huduma bora za kifedha.
Meneja Mkuu Kitengo cha Fedha wa Benki ya Akiba Commercial (ACB) Bertha Simon akielezea mikakati waliyojiwekea katika mwaka 2019 ya kuhakikishia wanafikia malengo yao.

ZAIDI YA SH. BIL. 500 ZIMELIPWA KWA WAKULIMA WA KOROSHO-MAJALIWA

$
0
0
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema zaidi ya sh. bilioni 500 zimelipwa kwa wakulima wa korosho kati ya sh. bilioni 700 zinazotarajiwa na kwamba malipo hayo bado yanaendelea kulipwa kwa wakulima wengine waliosalia.

Amesema tamko la Rais Dkt. John Magufuli la kwamba Serikali itanunua korosho kwa bei ya sh. 3,300 ni kwa ajili ya korosho za daraja la kwanza  na bei ya korosho za daraja la pili ni asilimia 80 ya zile za daraja la kwanza.

Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Alhamisi, Februari 7, 2019) Bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu wakati akijibu swali la Mbunge wa Liwale, Zuberi Kuchauka.

Mbunge huyo alitaka kupata kauli ya Serikali kuhusu malipo kwa wakulima wa korosho ambao walikuwa wakilipwa sh. 2,600 kwa kilo wakati Rais Dkt.  Magufuli alisema Serikali itanunua kilo moja ya korosho kwa sh. 3,300.

“Malipo yanaendelea na sehemu kubwa ni kwa wakulima wenye kilo zaidi ya 1,500, Serikali itanunua korosho zote kama ilivyoelezwa. Taratibu zinazofanyika ni kuhakikisha anayelipwa ni muhusika. Wananchi endeleeni kuiamini Serikali yenu.”

Waziri Mkuu amesema ilikuwa ni lazima kwa Serikali ifanye uhakiki kwa wakulima hususani wale wenye kilo zaidi ya 1,500 ili kujiridhisha kama ni wakulima, hivyo baada ya kuhakikiwa wakulima wote watalipwa fedha zao.

Amesema Januari 27, 2019 alitoa maagizo kwa Wizara ya Kilimo pamoja na Bodi ya Mazao Mchanganyiko wahakikishe hadi Februari 15 mwaka huu wawe wamekamilisha zoezi la uhakiki na kuwalipa wakulima wote wa zao la korosho.

Waziri Mkuu alitoa agizo hilo wakati akizungumza na wadau wa zao la korosho kwenye kikao kilichofanyika mkoani Mtwara, lengo la kikao hicho ilikuwa ni kupata taarifa juu ya mwenendo mzima wa bidhaa hiyo kwa msimu wa mwaka 2018/2019.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu amesema Serikali haijakiuka sheria kuhusu suala la watumishi kupandishwa mishahara na kwamba ina nia njema ya kuhakikisha wanalipwa mishahara na posho nzuri.

Ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbozi, Pascal Haonga aliyedai Serikali imekiuka sheria ya utumishi kwa kutopandisha mishahara, ambapo Waziri Mkuu amesema  Serikali haikukiuka sheria, bali iliamua kushughulikia suala hilo kwa kuanza na uhakiki wa watumishi.

Waziri Mkuu amesema baada ya kufanya uhakiki na kubaini uwepo kwa watumishi hewa pamoja na waliokuwa wakitumia vyeti vya kugushi, iliwaondoa na sasa Bodi ya Mishahara na Maslahi ya Watumishi wa Umma inafanya mapitio ya mishahara baada ya kubaini tofauti, hivyo watumishi waendelee kuwa watulivu.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
ALHAMISI, FEBRUARI 7, 2019.






Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisikiliza swali kutoka Mbunge wa Mchinga, Hamidu Hassan Bobali ambaye aliuliza swali katika kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, Bungeni jijini Dodoma, Februari 7, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijibu maswali, Bungeni jijini Dodoma, Februari 7, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipongezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji , Angela Kairuki baada ya kujibu vizuri sana maswali ya papo kwa papo, Bungeni jijini Dodoma, Februari 7, 2019. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

LEMUTUZ AWAJIA JUU WANAOICHAFUA EQUITY BANK

$
0
0
The Art of FACTS mimi ni mteja wa Equity Bank I was shocked last week kuona habari za kuichafua my Bank ambayo kabla ya kufungua my account tayari nilishafanya utafiti wa kutosha na kuijua vizuri bank hii ambayo wala sio siri kwa maoni yangu ndiyo THE BEST BANK nchini so far ambayo ilianzishwa Mwaka 2012 na kwa sasa ina Branches 15 Tanzania nzima pamoja na Zanzibar na tayari wanazo ATM’s 21 wakiwa na nia ya kubadilisha maisha ya Wananchi wa kawaida kiuchumi kwa kuwapatia huduma bora na fursa. 

 Equity Bank Limited Tanzania ni part of Equity Group Holdings Plc iliyoanzishwa Mwaka 1984 kutokea Kenya na Mkurugenzi wake wa kwanza akiwa Dr. James Mwangi na leo Equity ipo Africa nzima na inaongoza masoko ya nchi za Kenya, Uganda na Rwanda, Congo-DRC, South Sudan. Bank hii ina wateja Millioni 21.8 na mtaji wa jumla ya Dola za Kimarekani USD 5.7 Billioni, kwa ujumla wake ni Bank ambayo inashika nafasi ya 11 Duniani kwa Matokeo na Mali ilizonazo. 

 Mwaka uliopita ilishinda zawadi ya “African Bank of the Year” na Mkurugenzi wake Mkuu Dr. James Mwangi ameshinda pia zawadi ya “African Banker of the Year 2018”. Sasa kwahayo machache naomba kuwakumbusha wale wote wanaohangaika kuichafua Bank hii kwamba mmepotea sana ushindani wa bank ufanyike kwa kazi na sio kuchafuana mitandaoni cause binafsi siwezi kunyamaza kuona Bank yangu inachafuliwa kwa sababu za kiushindani wa kibiashara …

I salute you Equity Bank endeleeni kusaidia Wajasiriamali wanyonge nchini kwa mikopo yenye riba nafuu na pia endeleeni kutusaidia hata sisi wajasiriamali wadogo wadogo kwa mikopo nafuu ..haya makelele ya Social Media niachieni mimi hahahahaha U know …MUNGU AIBARIKI TANZANIA! AMEN! – @ lemutuz_superbrand

DUDE AWAGEUZIA KIBAO WANAOBEZA JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI

$
0
0
Na Khadija Seif ,Globu ya jamii

MSANII wa Bongomovie Kulwa Kikumba a.k.a Dude awaonya watanzania wanaobeza uhudi za Serikali ya awamu ya tano.

Dude ameyasema hayo leo Februari 7,2019 wakati wa kutembelea mradi wa reli wa kisasa (SGR) ambapo amesisitiza ni wakati wa kupongeza na kuonesha ushirikiano kwa maendeleo yanayoletwa nchini chini ya Rais Dk. John Magufuli kwani Tanzania kwa sasa ni madhubuti na imara kwa kila sekta hasa ya uchukuzi.

"Hivi karibuni tulishuhudia ndege mbili zikikabidhiwa hiyo ni wazi kuwa Rais Magufuli lengo lake ni kuhakikisha Watanzania hatuko nyuma katika suala la
maendeleoe,"amesema Dude.

Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa wasanii kuwa mabolozi kwa kueleza mambo mambo mazuri yanayofanywa na Serikali na kwamba treni ya kisasa itakapoaza kutoa huduma ya kusafirisha abiria watoe hamasa ili wananchi wengi waitumie treni hiyo katika safari zao mbalimbali.

Wakati huo huo Dude ametumia nafasi hiyo kuwataka wasanii kuwa na umoja ambao utaleta tija kwa maslahi yao pamoja na kuboresha tasnia na kusiwepo kwa matabaka yatakayofanya tasnia kushuka kiwango.
MSANII wa Bongomovie Kulwa Kikumba a.k.a Dude 

Wabunge wa EALA walivyotoa Elimu ya Mtangamano wa EAC

$
0
0
Mkurugenzi Mkazi wa Trade Mark East Africa (TMEA), Bw. John Ulanga akitoa mada kwa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kuhusu shghuli za taasisi hiyo. Alisema taasisi yake inashirikiana na Serikali kuboresha miundombinu mbalimbali kwa madhumuni ya kuhakikisha kuwa biashara katika nchi za EAC inafanyika bila vikwazo. 
Waheshimiwa Wabunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakijadili kwa pamoja na Mkurugenzi wa TMEA kuhusu mchango wa taasisi hiyo katika kuboresha mwenendo wa biashara baina ya Tanzania na nchi nyingine za EAC. 
Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakijadili mada iliyowasilishwa na Mkurugenzi Mkazi wa TMEA. 



Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam
Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la EALA, Mhe. Dkt. Abdallah Makame (kulia) akijadili jambo na Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar Es Salaam mara baada ya kuwasili katika chuo hicho kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu EAC. 
Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika Bunge la EALA, Mhe. Dkt. Abdallah Makame (kulia) akipata chakula cha mchana na wanafunzi wa UDSM katika Cafteria Namba moja ya Chuo hicho. Mwenye nguo za bluu ni Mbunge mwenzake wa EALA, Mhe. Pamela Maasay. 
Wanafunzi wa UDSM wakipata chakula cha mchana ambapo Wabunge wa EALA walijumuika nao katika chakula hicho. 
Mbunge wa EALA, Mwalimu Josephine Sabastian (kushoto) akibadilishana mawazo na wanafunzi wa UDSM wakati wakipata kwa pamoja chakula cha mchana Cafteria. 
Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakiwa katika meza kuu kwenye Ukumbi wa Nkurumah kwa ajili ya kuongea na wanafunzi kuhusu fursa za EAC. 
Mbunge wa EALA, Mhe. Dkt. Ngwaru Maghembe akiwasilisha mada kuhusu EAC kwa wanafunzi wa UDSM. 
Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakiongea na wanafunzi wa UDSM kuhusu fursa za Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Wanafunzi walioshiriki kwenye mazungumzo na Wabunge wa EALA. Mwenye suti ya bluu ni Rais wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam. 
Washiriki wengine katika mazungumzo hayo. 
Wanafunzi wakiuliza maswali na kutoa maoni namna Watanzania watakavyofaidika na Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki 
Waheshimiwa Wabunge wa EALA wakikabidhi bendera ya EAC kwa viongozi wa UDSM ili iwe inapeperushwa chuoni hapo. Walitoa wito kwa taasisi nyingine, hususan za Serikali kupeperusha bendera hiyo.

Mkutano na Asasi za Kiraia
Mbunge wa EALA, Mwalimu Josephine Sabastian akitoa elimu kuhusu EAC kwa wawakilishi wa Asasi za Kiraia zilizopo hapa nchini. 
Majadiliano baina ya Wabunge wa EALA na wawakilishi wa Asasi za Kiraia kuhusu ushiriki wa asasi hizo katika masuala ya EAC. 
Wabunge wa EALA na wawakilishi wa Asasi za Kiraia wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wabunge walisisitiza umuhimu wa wimbo huo kupigwa katika shughuli rasmi za Serikali. 
Mdau akifanya tafrisi ya lugha ya ishara kwa watu wenye ulemavu wa kusikia.

BOTI ILIOTENGENEZWA KWA PLASTIKI NCHINI KENYA YAWASILI ZANZIBAR.

$
0
0
Boti ya Beach Clianup iliotengenezwa kwa Plastiki iliowasili Zanzibar ikitokea Nchini Kenya ambayo imebeba Ujumbe wa Kuhifadhi mazingira ikiwa katika Bandari ya Malindi mjini Zanzibar.
Nahodha Muundaji wa Boti ya Plastiki Ali Abdalla Ali(SKANDA)akisalimiana na Wananchi wa Zanzibar na kuwapa ujumbe wa kuhifadhi mazingira katika hafla iliofanyika Bustani ya Forodhani ya kuipokea Boti iliotengenezwa kwa Plastiki iliobeba ujumbe wa kuhifadhi mazingira iliowasili Zanzibar ikitokea nchini Kenya.
Rais wa Baraza la Mazingira Duniani Siim Kiisler akitoa hotuba kuhusiana na Mazingira katika hafla iliofanyika Bustani ya Forodhani ya kuipokea Boti iliotengenezwa kwa Plastiki iliobeba ujumbe wa kuhifadhi mazingira iliowasili Zanzibar ikitokea nchini Kenya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed akitoa hotuba kuhusiana na kuhifadhi mazingira mara baada ya kuipokea Boti iliotengenezwa kwa Plastiki iliobeba ujumbe wa kuhifadhi mazingira iliowasili Zanzibar ikitokea nchini Kenya.PICHA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Marina Joel Thomas katikati akiwapamoja na viongozi mbalimbali wakifanya usafi wa mazingira kuondosha Chupa na Mifuko ya Plastiki na uchafu mwengine katika ufukwe wa Bahari ya Forodhani katika hafla ya kuipokea Boti iliotengenezwa kwa Plastiki iliobeba ujumbe wa kuhifadhi mazingira iliowasili Zanzibar ikitokea nchini Kenya.
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Marina Joel Thomas akizungumza na Wananchi na Vikundi mbalimbali vilivyoshiriki Usafi wa Mazingira katika ufukwe wa Bahari ya Forodhani katika hafla ya kuipokea Boti iliotengenezwa kwa Plastiki iliobeba ujumbe wa kuhifadhi mazingira iliowasili Zanzibar ikitokea nchini Kenya.

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KAIMU BALOZI WA EU NCHINI, MJUMBE MAALUMU WA RAIS WA ZIMBABWE IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Charles Stuart aliyemtembelea na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi February 7, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifanya  mazungumzo na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Charles Stuart aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi February 7, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza na kuagana na Kaimu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Charles Stuart aliyemtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi February 7, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Waziri wa Ardhi, Kilimo, Maji, Mazingira na Makazi vijijini wa Zimbabwe na Mjumbe Maalumu wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Pretence Shiri alipokutana nan a kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi February 7, 2019.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo  na Waziri wa Ardhi, Kilimo, Maji, Mazingira na Makazi vijijini wa Zimbabwe na Mjumbe Maalumu wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Pretence Shiri akiwa pamoja na Kaimu Balozi wa Zimbabwe nchini Mhe. Martin Tavenyika alipokutana na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi February 7, 2019.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza na kuamuaga baada ya mazungumzo  Waziri wa Ardhi, Kilimo, Maji, Mazingira na Makazi vijijini wa Zimbabwe na Mjumbe Maalumu wa Rais wa nchi hiyo Mhe. Pretence Shiri Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi February 7, 2019. PICHA NA IKULU

TOP 10 AFRICAN COUNTRIES TO INVEST IN 2019

BALOZI SEIF: UJIO WA MASHUA YA MAZINGIRA NI DARASA KWA WANANCHI WALIOWENGI NCHINI

$
0
0
Rais wa Taasisi inayosimamia mazingira ya Umoja wa Mataifa Bwana Siim Valmar Kiislar amesema wakati umefika kwa Mataifa yote Ulimwenguni kuwa na mfumo Mmoja unaoeleweka wa utunzaji wa Mazingira utakaosaidia kuifanya Dunia iendelee kubakia salama.

Bwana Siim Valmar Kiislar alisema hayo wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi katika Ofisi yake iliyomo ndani ya Jengo la Baraza la Wawakilishi liliopo Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amesema Zanzibar bado inaendelea kuathirika na mabadiliko ya Tabia Nchi akatolea mfano ufukwe wa Bahari ya Msuka uliopo kaskazini mwa Kisiwa cha Pemba ambao tayari umeshaliwa na mawimbi ya Bahari kwa sehemu kubwa.

Balozi Seif aliueleza Ujumbe huo ujio wa mashua ya Mazingira katika Visiwa vya Unguja na Pemba utasaidia mfano wa Darasa kwa Wananchi waliowengi kuwa na muelekeo wa jitihada za mapambano dhidi ya mabadiliko ya Tabia Nchi yanayoikumba Dunia hivi sasa na kuleta athari kubwa ya Kimazingira.

Imetolewa na kitengo cha Habari (OMPR)
Fubuari 07, 2019.





PETER MSECHU AWATOLEA UVUVI WATANZANIA WENYE MOYO WA CHOYO

$
0
0
*Asema wasipofurahia treni ya umeme,mnataka wafurahie ya dizeli?

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MSANII maarufu nchini Peter Msechu amesema anashangazwa na moyo wa choyo walionao baadhi ya Watanzania ambao kwao ni ngumu kupongeza juhudi za Serikali na badala yake kazi yao ni kutukana wale wanaoamua kutembelea miradi mikubwa ya maendeleo nchini.

Msechu ametoa kauli hiyo akiwa njiani kuelekea mkoani Morogoro akitokea Dar es Salaam kwa usafiri wa treni yeye pamoja na wasanii wengine wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.

Wasanii wa fani mbalimbali nchini leo Februari 7,2019 wamepata fursa ya kutembelea ujenzi wa reli ya treni ya kisasa ambayo itatumia umeme ambapo Msechu amepongeza juhudi za Serikali katika kuhakikisha ujenzi huo unatekelezwa kwa fedha za ndani.

"Tumefurahi kuwa sehemu ya Watanzania ambao tuliobahatika kuutembelea ujenzi huu wa reli ya kisasa.Ila inasikitisha sana tunapoonekana kwenye miradi mikubwa kama hii ambayo ina tija kwa Taifa letu baadhi ya watu wanatutukana na kusema tumenunuliwa," amesema Msechu.

Ameongeza kuwa ingekuwa leo Makonda angeamua kuwachukua wasanii wa Kenya na Uganda anaamini Watanzania wangelalamika kwanini wamechukuliwa wasanii wa Tanzania hawakuchukuliwa kwenda kuona utekelezaji wa ujenzi wa reli hiyo ya kisasa.

"Leo Mkuu wa Mkoa kaamua kutuchukua sisi tuambatane naye msema....mnataka mtuone wapi?Mara ooh mmelipwa sasa sisi kazi yetu nini.Kwani tukilipwa na sisi tukalika kodi Serikalini kuna tatizo gani?

" Mnataka kutuambia huu mradi wa reli ya kisasa hauna manufaa kwa Watanzania wakati kwa muda mrefu tumekuwa tukilalamika Serikali haiboreshi reli ya kati,leo hii inaboreshwa mnataka tubeze,"amesema Msechu.

Ameongeza msanii huyo kuwa "Serikali hii ni yangu,Rais Magufuli huyu ni wangu ,kodi nalipa kwa fedha yangu,mazuri nitayasema kwa nguvu zangu zote.Niache kufurahia treni ya umeme nifurahie treni ya dizel?Hata mwehu atanicheka."

MSANII maarufu nchini Peter Msechu akiwa na Mkuu wa Mkoa Mh Paul Makonda
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images