Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 23, 2019


SERIKALI KUPITIA TANESCO YAANZA KUTEKELEZA MRADI WA UMEME WA KENYA-TANZANIA POWER INTERCONNECTION

$
0
0

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Monduli

MRADI wa umeme wa Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK tayari umeanza kutekelezwa ambapo kazi ya kutengeneza misingi ya kusimika minara (towers) imeanza, Mratibu wa Mradi huo kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Peter Kigadye amewaambia wahariri wa vyombo vya habari waliotembelea kambi ya wakandarasi iliyoko kijiji cha Nanja kilichoko barabara ya Bababti-Arusha wilayani Munduli leo Januari 22, 2019.

Mradi huo ni sehemu moja ya mradi mzima wa regional power connection ambao lengo lake ni kuunganisha mfumo wa umeme wa Tanzania na Afrika Mashariki (East Africa Power Pool) kwa upande wa Kaskazini, na baadaye utekelezaji wa sehemu nyingine ya tatu ambayo itakuwa inaunganisha mifumo ya nxchi Kusini mwa Afrika, kupitia chombo kinachoitwa Southern Africa Power Pool (SAPP)

“Tanzaania tumebarikiwa tutakuwa na sehemu tatu ya kwanza ni mradi wa Backborn ambao umejengwa katikati ya nchi yetu na ulikuwa na kilomita 670 inaanzia Shinyanga hadi Iringa, sehemu ya pili ni kuunga kutoka Singida hadi mpakani na Kenya kuna kituo kimoja kinaitwa Isinya, jumla hapo kuna kilomita 510.7 na hizo ndio kilomita za mradi tunazoanza kuutekeleza hivi sasa.” Alisema Mhandisi Kigadye.
 
“Baada ya hapo sehemu ya tatu ni kuanzia Iringa kwenda Kusini ambapo kuna mradi utakaoitwa Zambia Interconector ambako kuna kilomita nyingine 624 kwahiyo Tanzania tutakuwa tumekamilisha ule mkongo wa msongo wa kilovoti 400.” Alisema Mhandisi Kigadye.Akielezea zaidi kuhusu kuunganiushwa kwa umeme kwenye nchi za Ukanda wa Mashariki na Kusini Mhandisi Kigadye alisema, “ Lengo ni kuunganisha nchi yetu na ukanda nchi za Kikanda kuanzia Kaskazini kuungana na Kenya na Kusini kuungana na Zambia.”

Alisema mradi wa Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK, utakamilika Aprili 2020, wakati ule Zambia Connector utakamilika mwaka 2022 tutakuwa tumemaliza mikongo hii mitatu (3)na nchi yetu itakuwa tayari kushiriki kwenye biashara ya umeme Kikanda.Akifafanua zaidi kuhusu mradi huo wa Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK Mhandisi Kigadye alisema sehemu ya kwanza itahusu ujenzi wa njia za kusafirisha umeme (transmission lines) na ujenzi wa vituo vya kupozea umeme.

Mradi mzima una urefu wa kilomita 510 na umegawanyika kwenye sehemu nne, ambazo ni Isinya Kenya hadi Namanga Kilomita kilomita 96, sehemu ya pili unahusu Namanga-Arusha Kilomita 114, sehemu ya tatu Arusha-Babati kilomita 150, na Bababti-Singida kilomita 150.

Kwa upande wake, Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi Emmanuel G. Manirabona, alisema tayari vifaa vya kutekeleza ujenzi wa mradi huo vimewasili kwa kiasi kikubwa cha kazi kuanza.

Akieleza zaidi Mhandisi Manirabona alibainisha kuwa kila kitu kiko sawa na wananchi wote ambao wako kwenye sehemu mradi unakopita, tayari Serikali imeshawalipa fidia na ndiyo maana mkandarasi anaendelea na kazi.
Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi Emmanuel G. Manirabona, akifafanua mambo mbalimbali yahusuyo utekelezaji wa mradi huo leo Januari 22, 2019
Mratibu wa Mradi huo kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Peter Kigadye, akifafanua jambo kwa wahariri eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza umeme Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha leo Januari 22, 2019
Vifaa viko site tayari
Vifaa viko site tayari
Zege linamwaga kwenye msingi wa kusimika mnara wa kupitisha nyaya za umeme mkubwa
Eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza umeme Kisongo.






Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi Emmanuel G. Manirabona (kushoto), akimsikiliza Mhandisi Mshauri Mradi wa umeme wa Kenya-Tanzania Interconnection-Lot2(KTPIP-Lot2), Gilles Allard kutoka kampuni ya Intec, kwenye eneo la ujenzi wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme kinachojengwa eneo la Kisongo nje kidogo ya jiji la Arusha Januari 22, 2019.
Mhandisi Herini Mhina. Meneja wa TANESCO jijini Arusha.
Mhandisi Peter Kigadye
Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na Miradi, Mhandisi Emmanuel G. Manirabona (kushoto), akiwa na Meneja Mkazi, Mradi wa Kenya-Tanzania Interconnection Project-Lot2 SBU Power Bouygues ya Ufaransa, Christophe Batholome
Mhandisi Mshauri Mradi wa umeme wa Kenya-Tanzania Interconnection-Lot2(KTPIP-Lot2), Gilles Allard kutoka kampuni ya Intec
Mhariri wa gazeti la Majira, Bw. Imma Mbuguni akizungumza jambo.



Meneja Mkazi, Mradi wa Kenya-Tanzania Interconnection Project-Lot2 SBU Power Bouygues ya Ufaransa, Christophe Batholome(kulia), akibadilishana mawazo na Meneja wa TANESCO jijini Arusha, Mhandisi Herini Mhina, (katikati) na Msimamizi wa ujenzi kutoka Tanesco.


Mashimo manne ya nguzo nne za mnara (tower) moja. mafundi wanasubiri kumwaga zegu.

Mafundi wakiwa wamesimama mbele ya moja ya shimo litakalotumika kusimika mnara (tower). Kwa kawaida Mnara mmoja nashikiliwa na nguzo nne, hili shimo ni la kusimika nguzo moja kati ya hizo.
Mhandisi Kigadye akifafanua jambo eneo la uchimbaji na usimikazji minara ambapo kazi ya kumimina zege kwenye mashimo imeanza
Waandishi na wahariri wakinukuu taarifa muhimu eneo la utendaji huko wilayani Monduli.
Mafundi wakiwa kazini.

LTSP YATOA MAFUNZO KWA MABARAZA YA ARDHI YA KIJIJI KUPUNGUZA MLUNDIKANO KESI ZA ARDHI ULANGA

$
0
0
Wizara ya Ardhi nyumba na maendeleo ya makazi kupitia mpango wake wa kuwezesha umilikishaji Ardhi(TLSP) imetoa mafunzo kwa mabaraza ya ardhi ya Vijiji 56 vilivyopo katika wilaya za Ulanga ,Kilombero na Malinyi Mkoani Morogoro ili kukabiliana na migogoro ya ardhi na namna bora ya kuisuruhisha. 

Mratibu wa mafunzo hayo JAMES BALELE amesema utafiti uliofanywa na mradi huo umebaini migogoro mingi ya ardhi imekuwa haimaliziki kutokana na uelewa mdogo wa wasuluishi,ufinyu wa vitendea kazi pamoja na miongozo ya kisheria. 

Awali akifunga mafunzo hayo ,mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga, FADHILI FURAHA ameishukuru wizara ya Ardhi kupitia mpango wake wa uwezeshwaji na umilikishaji Ardhi TLSP kwa kutoa mafunzo hayo yatakayo punguza migogoro kwa wananchi huku mwanasheria wa halmashauri hiyo DEVOTA KISEMBO akaeleza changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo mabaraza hayo ya ardhi.
Mafunzo kwa Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji katika Wilaya ya Ulanga katika kijiji cha Mavimba yakiendelea ikiwa ni sehemu ya hafla ya kuhitimisha mafunzo haya kwa wajumbe wa mabaraza wilayani humo.
Mwezeshaji kutoka Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi (LTSP) ambaye ndie mratibu wa mafunzo hayo yanayoendeshwa na LTSP akitoa salamu za utangulizi kwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Manispaa Ulanga ambaye ndie alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo
Mgeni Rasmi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Manispaa Ulanga Fadhili Furaha akitoa salamu kwa washiriki wa warsha hiyo ya mafunzo.
Mmoja wa wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya kijiji akichangia hoja mara baada ya mgeni rasmi kuwasili katika hafla hiyo ya ufungaji wa mafunzo ya mabaraza ya ardhi ya kijiji Ulanga. 
Mgeni Rasmi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki pamoja na wawezeshaji wa mafunzo hayo.

MKANDARASI ANAYESIMAMIA MRADI WA MAJI BOGA WILAYANI KISARAWE AONDOLEWA

$
0
0
 Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii .

 Mkandarasi wa Kampuni ya Mazongela Bulding Limited aliyekuwa anasimamia mradi wa Maji katika Kata ya Boga Wilayani Kisarawe ameondolewa kuendelea kusimamia ujenzi wa mradi huo baada yakubainika kusuasua kwa muda. 
 Kampuni hiyo ya ujenzi iliyo chini ya Mkandarasi, Salum Suleiman Ally ameondolewa kuendelea na ujenzi wa mradi huo licha yakutengewa zaidi ya Shilingi Milioni 536/- ambazo angelipwa katika utekelezaji wake. 

 Akizungumza na Waandishi wa Habari pamoja na Wananchi wa Kata ya Boga wilayani humo wakati akitembelea miradi mbalimbali ya Maji, Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Jumaa Aweso amesema Mkandarasi huyo hafai kutokana na kuwaumiza Wananchi hao kwa muda mrefu, ambapo ameagiza asipewe kazi yoyote katika Halmashauri hiyo ya Kisarawe. 

 ‘’Changamoto kubwa katika Wilaya hii ya Kisarawe kuwaweka Wakandarasi wasio na uwezo kusimamia miradi mbalimbali ya Maji, wengi wanapatikana Kindugu hii haiwezekani’’, amesema Mhe. Aweso. 

Mhe. Aweso amewaasa Watendaji wa Wizara hiyo Wilayani humo, kukataa Wakandarasi wasio na uwezo, badala yake amewataka kuchukua Wandarasi wenye uwezo, hata hivyo Aweso amewataka Watendaji hao kuhakikisha Mkandarasi mwengine anapatikana kwa haraka ili kutekeleza mradi huo kwa haraka. Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwangelo ameiomba Serikali kupitia Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso kuwachukulia hatua kali Wakandarasi ambao watashindwa kutekeleza miradi yao ipasavyo kutokana na Wilaya hiyo kukumbwa na kero kubwa ya Maji. 

 ‘’Kuna Miji mikubwa kama Nairobi imeundwa mwaka mmoja na Wilaya yetu lakini wao wana maendeleo sisi bado tupo nyuma’’, amesema Jokate. 
Naye Diwani wa Kata ya Boga, Inadi Chachaka amekili kuwepo kwa changamoto ya upatikanaji wa Maji katika Kata hiyo, ambapo pia amemuomba Naibu Waziri kwa kushirikiana na Watendaji wake Wilayani Kisarawe kusimamia ipasavyo miradi hiyo ikiwemo Mradi wa Maji katika Kata ya Boga.
 Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwangelo akisisitiza jambo kwa Naibu wa Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso wataki walipotembelea mradi wa maji eneo la Mnarani, Kisarawe.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Jumaa Aweso pamoja na Watendaji wengine wa Wizara ya Maji wakiangalia mradi wa maji wa Kata ya Boga, Wilayani Kisarawe baada kuambiwa umesuasua kwa muda kutokana na Mkandarasi anayetekeleza mradi kushindwa kusimamia ipasavyo licha yakutengewa zaidi ya Shilingi Milioni 536/-
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Jumaa Aweso akishuhudia Shimo lililochimbwa kwa kile lilichoelezwa ni utekelezaji wa mradi wa maji, Kata ya Boga, Kisarawe.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Jumaa Aweso na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwangelo wakimsikiliza Mhandisi wa Wilaya ya Kisarawe, Majid Mtili katika kutembelea utekelezaji wa mradi wa maji, Kata ya Chole.

NAIBU WAZIRI DK MABULA ARIDHISHWA NA UJENZI WA NHC KATIKA MJI WA SERIKALI MTUMBA

$
0
0
Na Munir Shemweta, Dodoma
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angeline Mabula ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa ofisi za wizara katika mji wa serikali ya Mtumba mkoani Dodoma unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Dk Mabula alitoa kauli hiyo leo tarehe 22 Januari 2019 wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa ofisi za Serikali katika mji wa Mtumba mkoani Dodoma unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambalo liko chini ya Wizara yake.
Alisema kazi inayofanywa na shirika la Nyumba la Taifa kujenga ofisi za Serikali katika mji huo kwa sasa unaenda kwa kasi na unatia moyo jambo linalooonesha kuwa mradi wa ujenzi wa ofisi hizo utakamilika katika muda uliopangwa.
Katika mradi huo Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kupitia kampuni yake ya ujenzi inajenga ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Fedha na Uchumi, Wizara ya Nishati pamoja na Wizara ya Viwanda na Biashara.
Aidha, Dk Mabula amefurahishwa na ufuatialiaji wa ujenzi wa ofisi hizo unaofanywa na Wizara ya Fedha pamoja na Viwanda na Biashara na kueleza kuwa hatua hiyo inalifanya Shirika hilo kufanya kazi kulingana na mahitaji ya wateja wake.
Alibainisha kuwa, pamoja na changamoto ya kukatika umeme lakini NHC imejitahidi na kilichomfurahisha ni kuwepo vifaa vyote vya ujenzi kwenye eneo la ujenzi jambo linalompa faraja kuwa hakuna kitakachokwamisha ujenzi kukamilika kwa wakati
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amepongeza jitihada znazofanywa na Rais John Pombe Magufuli za kuhamishia Makao Makuu ya Serikali Dodoma na kubainisha kuwa hatua hiyo inatimiza ndoto ya baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Naye Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Emma Lyimo alilisifu Shirika la Nyumba la Taifa kwa kasi kubwa wanayoendelea nayo kwenye ujenzi wa ofisi ya Wizara yake na kubainisha kuwa pamoja na kuchelewa kuanza ujenzi lakini kasi wanayoenda nayo ana imani ujenzi utakamilika kwa wakati.
Naye Msimamizi wa ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo la Makazi Mhandisi Grace Musita alisema, ujenzi wa ofisi umefikia asilimia sabini na tano na anatarajia utakamilika katika tarehe iliyopangwa kwa kuwa wamefikia hatua nzuri ya kukamika.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akiangalia maendeleo ya Ujenzi ya Ofisi ya Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Mtumba, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Elisante Ulomi na katikati ni meneja mradi Haikameni Mlekio.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akioneshwa moja ya kifaa kitakachotumika katika Ujenzi ya Ofisi ya Wizara ya Nishati katika mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma, kulia ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Elisante Ulomi na kushoto ni meneja mradi Haikameni Mlekio.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akimsikiliza Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Viwanda na Bisahara Emma Lyimo (Kulia) wakati alipotembelea maendeleo ya Ujenzi wa Ofisi ya Wizara ya Viwanda na Biashara katika mji wa Serikali wa Mtumba mkoani Dodoma, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Hassan Mohamed.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akiongozwa na Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita kukagua ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali eneo la Mtumba Dodoma .
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula katikati akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali wa Mtumba kutoka kwa meneja mradi wa Shirika la Nyumba Haikameni Mlekio wakati alipofanya ziara, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita.
 Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk Angelina Mabula akipata maelezo ya maendeleo ya ujenzi wa ofisi ya Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi katika mji wa Serikali wa Mtumba kutoka kwa meneja mradi wa Shirika la Nyumba Haikameni Mlekio (kulia) wakati alipofanya ziara, kushoto ni Mhandisi wa ujenzi kutoka Shirika la Nyumba la Taifa Grace Musita. (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

DC JOKATE ALIA NA UKOSEFU WA MAJI KISARAWE

$
0
0
Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwangelo amemuomba Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Jumaa Aweso kuhakikisha Wilaya hiyo inapata Maji yakutosha kutokana nakuwepo changamoto kubwa ya upatikanaji wa Maji hayo.

Akizungumza na Watendaji wa Wilaya hiyo wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso - Jokate ameshukuru kuwepo mradi wa Maji unaotoka Ruvu Juu, amesema mradi huo umekaa kimkakati kutokana na Wilaya hiyo kuwa na Viwanda vingi.

Hata hivyo, Jokate amesema maendeleo ya Wilaya ya Kisarawe yamekwamishwa kwa ukosefu wa Maji Safi na Salama hivyo kuna nia yakuhakikisha Maji hayo yanapatikana. ‘’Haileti maana kama Kisarawe haina Miundombinu yakuwezesha Viwanda mbalimbali kustawi, hata uwepo wa Bandari na Kiwanja cha Ndege’’, amesisitiza Jokate.

‘’Watu wengi wamekuwa na imani Kisarawe kuwa sio eneo la Makazi, wengi wanaishi Gongo la Mboto, Chanika kutokana nakukosekana huduma ya maji’’, ameeleza Jokate.

Jokate ameshukuru kuwepo ziara ya Naibu Waziri wa Maji ambapo amemuomba kuangalia kwa umakini miradi hiyo, Je inatekelezwa ipasavyo?
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Mhe. Jumaa Aweso akisisitiza jambo wakati alipowasili katika Ofoisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya ziara yake yakutembelea miradi mbalimbali ya Maji Wilayani humo.Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwangelo akizungumza jambo mbele ya Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso wakati wa ziara yake yakutembelea miradi mbalimbali ya Maji Wirani Kisarawe Mkoa wa Pwani.

ULEGA AAGIZA AFISA MIFUGO KATIKA MANISPAA YA TABORA AUCHUNGUZWE

$
0
0
NA TIGANYA VINCENT

NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega ameagiza Afisa Mifugo wa Manispaa ya Tabora Cornelius Masawe achunguzwe na achukuliwe hatua baada ya kutuhimiwa na wafanyabiashara wa mifugo wa Mnada wa Ipuli kuwanyanyasa ikiwemo kuwatoza malipo zaidi bila kuwapa stakabadhi.

Alisema tuhuma hizo ni nzito kwa kuwa zinaweza kusababisha Serikali kukosa mapato yake ikiwa wafanyabaishara hao watakaa kupeleka mifugo mnadani.

Ulega alitoa kauli hiyo leo wakati wa mkutano na wafanyabiashara wa mifugo kuhusu kuondoa mvutano ulikouwa umezuka katika Mnada wa Ipuli uliopo Manispaa ya Tabora kuhusu utaratibu wa usafirishaji ng’ombe kutoka na kuingia.

Alisema kuwa ni vema vyombo vinavyohusika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) na vyombo vingine kuchunguza tuhuma zilizotolewa na wafanyabiashara hao wa mifugo dhidi ya Masawe za kutoza fedha za faini ya mifugo bila ya kukatia stakanadhi au kutoa ambayo halingani na malipo yaliyotolewa.

Kufuatia tuhuma hizo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri aliagiza Masawe akamatwe na Polisi kwa ajili ya mahojiano na TAKUKURU , kwa kushirikiana na Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kiusalama. Alisema wafugaji kama makundi mengine Mkoani Tabora wana haki sawa na haipaswi kunyanyaswa na ikitokea wamenyanyaswa ni vema wakatoa taarifa mapema ili hatua ziweze kuchukuliwa.

Mwanri alisema tuhuma zilizotolewa na wafanyabiashara hao ni nzito haiwezekani zikapuuziwa ni vema hatua zikachukuliwa ili kubaini ukweli na ikibidi na hatua za kulifilisha katika maamuzi zifanyike haraka. Baadhi ya wafanyabishara walisema Masawe wakati wa kuendesha operesheni amekuwa akiwakata na kuwapiga watu wanaokutwa na ng’ombe katika maeneo ambayo hayakatazwi kisheria. Walisema ameweka migambo katika kila pande ya kuelekea Mnadani ili kuwavizia na anawakamata anawatoza shilingi 50,000/- kila ng’ombe kwa madai kuwa wanapita njia zisizo rasmi.

Walisema Masawe alishawi kupokea shilingi 900,000/- lakini aliandika stakabadhi ya laki 5 tu. Walisema amekuwa akiendesha zoezi hilo wakati akijua njia za kupitishia mifugo kwenda Mnadani zimevamiwa na watu mbalimbali na kujenga.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo amsema kuwa utaratibu wa nyuma wa kupeleka mifugo katika Mnada wa Ipuli uendelee kutumika wakati suluhusho la kudumu kuhusu kuendelea au kuhamisha likifanyiwa kazi kutokana na eneo hilo kuwa katikati ya mji hivi sasa likitafutwa na pande zote.

Aliwataka wafugaji kuendelea kutii Sheria zilizopo za Manispaa wakati wanaendelea kulitafutia ufumbuzi wa kudumu suala lao la kupitisha ng’ombe kutoka kwao kwenda mnadani.

Ulega alisema tatizo kubwa lilisababisha mvutano huo ni makosa yaliyofanyika nyuma ya kushindwa kulinda njia ya kusafirisha ng’ombe kutoka maeneo mbalimbali na kwenda katika Mnada wa Ipulu na kusababisha watu kujenga.
 Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu akitoa maelezo mafupi jana kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akitoa maelezo mafupi jana wakati wa Mkutano wa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega na wafanyabiashara wa ng'ombe.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza na wafanyabiashara wa mifugo katika Mnada wa Ipuli mkoani Tabora jana

MRADI WA NJIA KUU YA UMEME KUIUNGANISHA TANZANIA NA KENYA WAANZA KUTEKELEZWA

$
0
0
*TANESCO yazungumzia faida zake ikiwamo ya kuiwezesha Tanzania kuuza au kununua umeme kwa nchi nyingine za Afrika
*Wananchi ambao mradi huo unapita washauriwa kutoa ushirikiano ili kuhakikisha kazi inakwenda kama ilivyokusudiwa

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

MRADI mkubwa wa umeme unaotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) ambao utaiwezesha nchi kununua au kuuza umeme katika nchini za Afrika umeanza kutekelezwa ambapo kwa sasa mradi wa kuunganisha umeme katika nchi za Kenya na Tanzania umeanza.

Mradi huo unafahamika kwa jina la Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP) ambapo kutakuwa na hatua mbalimbali za kuutekeleza mradi huo uliogawanywa katika hatua nne za utekelezaji wake huku TANESCO ikifafanua umuhimu na faida lukuki za mradi utakapokamilika na kwa sasa wakandarasi wapo kazini na kanzi imeanza kufanyika.

Kwa mujibu wa TANESCO awamu ya kwanza itakuwa ni kuzinganisha nchi za zilizopakana na Tanzania kuwa na umeme wa uhakika huku awamu ya pili ya mradi huo ukihusisha nchi za Tanzania na Zambia (ZTK) ambao nao tayari umeanza kutekelezwa ambapo kazi ya kutengeneza misingi ya kusimika minara imeanza.Akiuzungumzia mradi huo jana jijini Arusha, Mratibu na Msimamizi wa Mradi huo kutoka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Peter Kigadye, amefafanua mradi huo wanaamini utakamilika kwa wakati kama ambavyo wamekubaliana na wakandarasi ambao tayari kazini na vifaa vyote muhimu vimefika na kazi ya kusimika nguzo imeanza.

Ameongeza kuwa mradi huo ni sehemu moja ya mradi mzima wa Regional Power Connection ambao lengo lake ni kuunganisha mfumo wa umeme wa Tanzania na Afrika Mashariki (East Africa Power Pool) kwa upande wa Kaskazini na baada ya kukamilika utekelezaji wake itakuwa inaunganisha mifumo ya nchi Kusini mwa Afrika, kupitia mradi wa Southern Africa Power Pool (SAPP).

Amesema kuwa Tanzania imebarikiwa kwai itakuwa na sehemu tatu za mradi huo ambapo ya kwanza ni mradi wa Backborn ambao umejengwa katikati ya nchi yetu na ulikuwa na kilomita 670 inaanzia Shinyanga hadi Iringa wakati sehemu ya pili ni kuunga kutoka Singida hadi mpakani na Kenya ambapo kuna kituo kimoja kinachoitwa Isinya.

"Jumla ya mradi wote una umbali wa kilometa 510 lakini kwa upande wetu Tanzania tunazo kilometa 414 na upande wa Kenya nao wanakilometa 96.Kwa upande wetu tunakwenda vizuri kwani kila kipande cha ujenzi wa mradi kuna mkandarasi wake na kila mmoja yupo hatua mbalimbali za ujenzi.Kupitia watalaam wetu tumekuwa tukifuatilia hatua kwa hatua na wakati huo huo wapo watalaamu wengine ambao nao wanafanya kazi hiyo hiyo kuhakikisha kila kinachofanyika kimezingatia mahitaji na vigezo vya viwango vya ubora,"amesema Mhandisi Kigadye.

Amefafanua pia kutakuwa na sehemu ya tatu ambayo ni Iringa kwenda Kusini ambapo kuna mradi utakaoitwa Zambia Interconector ambako kuna kilomita nyingine 624, hivyo baada ya kukamilika kwa mradi Tanzania itakuwa imekamilisha ule mkongo wa msongo wa Kilovoti 400.Lengo kuu la kuunganisha nchi yetu na ukanda nchi za Kikanda kuanzia Kaskazini kuungana na Kenya na Kusini kuungana na Zambia maana yake ni kuifanya Tanzania kuingia kenye mfumo wa umeme ambao utahusisha nchi mbalimbali za Afrika.

"Tunafahamu mradi huu wa njia ya umeme ya Kenya-Tanzania Power Interconnection (KTIPIP)ZTK, unatarajiwa kukamilika Aprili 2020 na ule Zambia Connector utakamilika mwaka 2022.Hivyo maana yake ni kwamba hii itakuwa tumemaliza mikongo hii mitatu na nchi yetu.Kupitia huu mfumo nchi hizo zitakuwa zimeingia kwenye biashara ya umeme na hakutakuwa na tatizo la umeme tena,"amesisitiza.

Kuhusu mradi wa Kenya-Tanzania Power Interconnection kwa maelezo ya Mhandisi Kigadye amesema sehemu ya kwanza itahusu ujenzi wa njia za kusafirisha umeme na ujenzi wa vituo vya kupozea umeme.

"Kama ambavyo nimeeleza awali jumla ya kilometa za mradi huo ambapo utapita ni 510 na umegawanyika kwenye sehemu nne, ambazo ni Isinya Kenya hadi Namanga Kilomita kilomita 96, sehemu ya pili unahusu Namanga-Arusha Kilomita 114, sehemu ya tatu Arusha-Babati kilomita 150, na Bababti-Singida kilomita 150.Kiasi cha fedha ambacho kitatumika kwa ajili ya mradi huo ni dola za Marekani milioni 258,"amesema Mhandisi.

Wakati huo huo Meneja Mwandamizi wa TANESCO anayehusika na miradi Mhandisi Emmanuel Manirabona amesema katika kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati tayari vifaa vyote muhimu tayari vipo maeneo y mradi na wakandarasi wanaendelea na ujenziAmetumia nafasi hiyo kuzungumzia umuhimu wa wananchi ambapo mradi utapita kutoa ushirikiano ili kufanisha mradi na hasa kwa kuzingatia TANESCO imeshalipa fidia kwa watu wote ambao wanastahili na hivyo haitarajii kuona watu wengine wanajitokeza na kukwamisha ujenzi huo kwa kigezo cha kudai fidia.

Mhandisi Manirabona ameelezea matumaini ya TANESCO baada ya kukamilika kwa mradi huo ambao utatoa fursa ya nchi moja kununua umeme kwa nchi nyingine iwapo itahitajika kufanya hivyo lakini kwa Tanzania mradi huo umekuja wakati muafaka hasa kwa kuzingatia nchi inatekeleza ujenzi wa viwanda , na hivyo mwito wao ni kuhamasisha watu kuwekeza kwa kujenga viwanda maeneo mbalimbali nchini kwani hakuna tatizo la nishati ya umeme.
 Meneja Mwandamizi wa Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) anayehusika na miradi Mhandisi Emmanuel Manirabona akifafanua jambo kuhusu ujenzi wa mradi wa kuunganisha umeme unaendelea mkoani Arusha
 Shughuli za ufungaji vifaa ukiendelea
Baadhi ya vifaa ambavyo vipo kwenye eneo la ujenzi wa mradi wa umeme unaoendelea mkoani Arusha

TAnTrade,NEEC WAKUBALIANA KUFANYA KAZI PAMOJA KUWEZESHA WANANCHI SEKTA ZOTE ZA KIUCHUMI IKIWEMO MASOKO

$
0
0
 Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) na Baraza la Uwezeshaji Wananchi kiuchumi (NEEC) jana Januari 22 , 2019 wakubaliana kufanya kazi kwa pamoja katika maeneo ya kuwezesha wananchi wa Watanzania katika sekta zote za kiuchumi na kuwawezesha upatikanaji wa masoko. Kikao kazi cha mkakati kiliongozwa na Bw Edwin Rutageruka Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade na Bibi Beng'i Issa Katibu Mtendaji wa NEEC .Picha na TanTrade 

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI APIGA 'STOP' KAMATAKAMATA YA NG'OMBE WANAOZAGAA MTAANI MANISPAA YA TABORA

$
0
0
Na Amisa Mussa

NAIBU Waziri Wa Mifugo Na Uvuvi Abdallah Ulega ameiagiza Serikali ya Mkoa wa Tabora kuitaka Halmashauri ya Manispaa ya Tabora kusitisha mchakato wa ukamataji wa ng'ombe ambao wanadaiwa kuzagaa mitaani baada ya kuonekana kuna harufu ya rushwa.

Mbali ya rushwa katika kuutekeleza mchakato huo imedaiwa linawaumiza wafugaji na wafanyabiashara ya ng'ombe ambao wanafanyabiashara mnada wa Ipuli wilayani humo.

Kutokana na kuwepo kwa gogoro baina ya wafugaji na Halmashauri ya Manispaa Ya Tabora Naibu Waziri Ulega mmetembelea mkoani humo ili kujionea hali halisi ambapo baada ya kusikiliza malalamiko kutoka kwa wafugaji ameamua kutoa maagizo ya kukamatwa kwa watendaji wa halmashauri waliohusika kutekeleza mchakato huo kwani kuna harufu ya rushwa.

Pia ameagiza Ofisa Mifugo Msaidizi Cornelius Masawe akamatwe na hivyo alikamatwa huku akimtaka ofisa hiyo kufanyiwa uchunguzi kwani ndio amekuwa akitekeleza agizo hilo la kukamata ng'ombe ndani ya manispaa hiyo.

Baada ya uamuzi huo Naibu Waziri huyo alipata fursa ya kusikiliza malalamiko ya wafugaji na wafanyabiashara ya ng'ombe ambao hawakusita kpaza uauti zao."Kilichofanyika sasa hivi ni kushika mashavu basi, tunamshukuru Mungu kwa sababu mimi nilikuwa na ng’ombe 45 kwa kumatwa na Masawe zimebaki ng’ombe 13 Nyingine zimeshaliwa,”alisema Alon mmoja wa wafugaji

Wafugaji Emmanuel Cosmas na Jani Kasunzu wamemueleza Naibu Waziri kuwa imefika wakati suala la suala la ng’ombe limekuwa ni dili kwa baadhi ya watumishi.Akiwa katika mnada wa Ipuli Manispaa ya Tabora na kusikiliza kilio cha wafugaji hao Naibu Waziri Ulega ameonesha kuguswa na malalamiko hayo ambapo aliamua kutoa msimamo wa Wizara.

“Ni lazima Oparesheni hii isimame ili iratibiwe vyema na hatimaye baadae ndio iendelea lasivyo tutawadhuru watu ambao hawana hatia,” alisema Naibu Waziri Ulega.

Aidha mwishoni mwa Wiki iliyopita wafugaji na wafanyabiashara wa ng’ombe waliingia katika mgogoro na Halmashauri ya Manispaa Ya Tabora hatua ilyosababisha jamii hiyo ya wafugaji kugoma kutumia mnada wa Ipuli kuuza na kununua ngo’mbe wilayani humo kwa kile kinachodaiwa kamatakamata ambayo imekuwa ikifanywa na Manispaa ya Tabora.
 Baadhi ya Wafugaji walipokuwa wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza na wafanyabiashara wa mifugo katika Mnada wa Ipuli mkoani Tabora jana
 Baadhi ya Mifugo

Naibu Katibu Mkuu UWT Taifa ampongeza Rais Magufuli

$
0
0





BMG Habari .

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Bara kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Jesca Mbogo ametoa pongezi kwa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha za ujenzi wa Kituo cha Afya Mwera kilichopo Wilaya ya Pangani mkoani Tanga.


Mbogo alitoa pongezi hizo jana ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake mkoani Tanga, yenye lengo la kujionea utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2015/20 na namna inavyogusa maisha ya akina mama.


"Namshukuru sana Rais Magufuli kwa kuboreshea Kituo hiki kwani akinamama sasa watapata huduma za afya hapa na kuepuka adha ya kusafiri umbali mrefu kwa kivuko hadi Pangani kutafuta matibabu". Alisema Mbogo ambaye ameanza ziara yake ya kwanza mkoani Tanga tangu ateuliwe kuwa Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara.


Mbogo pia alipokea shukrani za akina mama wilayani Pangani waliomshukru Rais Magufuli kwa juhudi zake za kuboresha huduma za afya nchini ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Afya Mwera kitakachowarahisishia upatikanaji wa huduma za afya.

Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara, Jesca Mbogo akisaini kitabu cha wageni.

Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara, Jesca Mbogo.

Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara, Jesca Mbogo akizungumza na akina mama wilayani Pangani (hawako pichani).

Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara, Jesca Mbogo akizungumza na akina mama wilayani Pangani.

Akina mama wilayani Pangani wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara, Jesca Mbogo.

Zawadi

Naibu Katibu Mkuu UWT Tanzania Bara, Jesca Mbogo alipata fursa ya kupata mche maalumu kama ishara ya mwanzo moya wa maboresho ya huduma za afya kwa akina mama.

FEMINA YAWAKUTANISHA VIJANA KOTE NCHINI KUSHEREKEA MIAKA 20 YA SHIRIKA HILO

$
0
0
* Wanafunzi waiomba serikali kutambua na kuunga mkono jitihada za FEMINA nchini kote.

Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
SHIRIKA lisilo la kiserikali la FEMINA linaloshughulika na masuala ya vijana hasa kwa kutoa elimu ya afya ya uzazi na ujinsia pamoja na shughuli ya ujasiriamali limetimiza miaka 20 tangu kuanzishwa kwake kwa kuwakutanisha vijana kutoka klabu zote nchini na kutoa elimu kuhusiana masuala ya afya na fursa za kiuchumi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo Meneja wa idara ya uhamasishaji jamii kutoka FEMINA Nashivai Mollel amesema kuwa licha ya kusherekea miaka 20 ya FEMINA wamewakutanisha vijana hao kwa lengo la kutoa mafunzo kama vile elimu ya afya ya uzazi na fursa za kijasiriamali bila kutegemea kuajiriwa pekee.

Amesema kuwa  malengo ya mkutano huo ni kuleta mabadiliko chanya pamoja na kutatua changamoto hizo kwa vijana kwa kushirikiana na walimu walezi wa klabu hizo.

Pia ameishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli pamoja na viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa afya, maendeleo ya jamii, wazee, jinsia na watoto Ummy Mwalimu kwa jitihada wanazoonesha katika kuwasaidia vijana. Na amehaidi kuwa wataendelea kuwasaidia vijana katika nyanja mbalimbali kwa kuwasaidia vijana wengi zaidi.

Kuhusiana na mchango wa klabu za FEMA katika kuchangia ufaulu wa wanafunzi mashuleni, mlezi wa klabu ya Mnyuzi, Charles Mayombo amesema kuwa klabu hizo zimekuwa chachu kubwa kwa wanafunzi katika kufanya vizuri katika masomo yao, hiyo ikiwa ni pamoja na sifa mojawapo ya kuwa mwanaklabu ya FEMA lazima mwanafunzi afanye vizuri katika masomo yake na hiyo imedhihirika kwa matokeo ya kidato cha pili yaliyotoka hivi karibuni kwa walezi wote wa klabu za FEMA kuleta mrejesho mzuri kuhusiana na matokeo hayo ambapo wanafunzi wengi walionekana kufanya vizuri.

Baadhi ya wanafunzi walioshiriki mkutano huo wameeleza kuwa klabu hizo zinasaidia sana kwa kuwa wanapata elimu ya kujitambua, nidhamu pamoja na kupambana na changamoto wanazopitia katika masuala ya ukuaji na wameiomba Serikali kuzitambua na kuunga mkono jitihada zinazofanywa na FEMINA.
 Meneja idara ya uhamasishaji jamii Nashivai Mollel akizungumza na wanafunzi kutoka katika Mikoa mbalimbali nchini katika mkutano huo uliowakutanisha katika kusherekea miaka 20 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo, leo jijini Dar es Salaam.
 Walimu walezi wa klabu za FEMA, (Walioketi) wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa FEMINA mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao kwa kuonesha mchango chanya katika klabu hizo mashuleni.
 Mkurugenzi wa Habari wa FEMINA Amabilis Batamula (katikati) akizungumza katika mkutano huo wa kuadhimisha miaka 20 ya FEMINA uliofanyika leo jijini Dar es salaam, kushoto ni Meneja idara ya uhamasishaji jamii kutoka FEMINA, Nashivai Mollel.
 Walimu kutoka Mikoa mbalimbali nchini wakiwa na vyeti walivyotunukiwa katika mkutano wa kuadhimisha miaka 20 ya FEMINA uliofanyika leo jijini Dar es Salaam na hiyo ni kutokana  na  kuonesha juhudi za ziada katika kutekeleza majukumu ya kuwasaidia vijana.
Meneja idara ya uhamasishaji Jamii, Nashivai Mollel akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa shirika hilo leo jijini Dar es Salaam.

Balozi Possi awasilisha Hati za Utambulisho Bulgaria

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani ambaye anawakilisha pia nchini Bulgaria , Mhe. Dkt. Abdallah Posi akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Bulgaria, Mhe. Rumen Radev. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu ya nchi hiyo hivi karibuni. 
Mhe. Balozi Dkt. Posi akizungumza na Mhe. Rais Radev mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho 
Mhe. Balozi Dkt. Posi akiagana na Mhe. Rais Radev mara baada ya kuwasilisha hati za utambulisho 
Mhe. Balozi Dkt. Posi akiwa mbele ya gwaride la heshima alipowasili Ikulu ya Bulgaria kwa ajili ya kuwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa nchi hiyo.

POLISI KILIMANJARO YANASA DAWA ZA KULEVYA KILO 80.

$
0
0
Anaandika Dixon Busagaga,Moshi.

KIKOSI cha  Pikipiki cha jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kimefanikiwa kukamata kilogramu 80 za Dawa za Kulevya  aina ya Mirungi iliyokuwa ikisafirishwa kwa kutumia pikipiki kutoka nchi jirani ya Kenya kuelekea mkoa wa Arusha.

Majani hayo ya Miringi yaliyokuwa yamefungwa katika vifurushi vidogo vidogo zaidi ya 50 na kisha kuwekwa kwenye mfuko mmmoja  mkubwa maarufu kama Kiroba yalipatikana baada ya askari Polisi kujaribu kumkimbiza msafirishaji wa Mirungi ambaye alitekeleza pikipiki na mzigo huo.

Kamanda wa Polisi mkao wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa alithibitisha kukamatwa kwa Dawa hizo za kulevya katika eneo la Uchira ambapo msafirishaji huyo alifanikiwa kukimbia na kuiacha pikipiki aliyokuwa akitumia.

“Mkoa wa Kilimanjaro kumekuwa na tatizo kubwa sana, linalohusiana na usafirishaji wa Mirungi  na wasafirishaji  wamekuwa  wakitumia barabara kuu, sasa askari wa pikipiki  ambao wanafanya kazi hii ya kufukuzana na hawa watu wa mirungi wamefanikiwa kukamata kilogramu 80 za Mirungi”alisema Issah.

Alisema kundi la wasafirishaji wa Dawa hizo za kulevya ambao wamekuwa wakisafirisha kutoka nchi ya Kenya kupitia mpaka wa Holili pindi linapoingia barabarani limeonekana kuwa tishio na hatari kwa usalama wa watu wengine barabarani kwa namna wanavyoendesha pikipiki zao.

“Siku ya leo(Jana) imekamatwa pikipiki moja yenye namba MC 168 CAZ ambayo imetoka nchini Kenya lakini  ni ya Tanzania  na ikiwa na gunia moja kubwa lenye uzito wa kilo 80,nah ii inaonyesha ilikuwa bado  hawajagawana kabisa  lakini askari wetu kwa ushujaa wao wamewafukuza hawa watu  na matokeo yake wamekamata”alisema Issah .

Kamanda Issah alisema  baada ya kufungua mfuko huo walibaini uwepo wa vifurushi vingi vikiwa vimefungwa Majani ya Mirungi kwa njia tofauti tofauti huku ikiwa imepewa majina maalumu ya wahusika wa Dawa hizo.
 MIrungi hiyo naona ilivyohifadhiwa na watuhumiwa hao tayari kwa kusafirishwa. 
 Kamanda wa Polisi mkao wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa akionesha Dawa za kulevya aina ya Mirungi walioikamata eneo la Uchira,ambapo msafirishaji huyo alifanikiwa kukimbia na kuiacha pikipiki aliyokuwa akitumia.
 Mirungi iliyokamatwa ikikusanywa na kuwekwa vizuri

DAWASA YAMTUA NDOO YA MAJI MAMA MARIA NYERERE

$
0
0
 Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere (kulia) akiwakaribisha Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (katikati) na Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kulia) pamoja na wageni wengine waliokuwa wameambatana nao kukabidhi mradi wa tenki la maji lililokarabatiwa na DAWASA. Picha na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.  Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema akitoa maelezo machache kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili toka kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kushoto) na Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere pamoja wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.  Kaimu Mkurugenzi wa miradi DAWASA Lydia Ndibalema akitoa maelezo machache kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili toka kushoto), Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kushoto) na Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere pamoja wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.  Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja akitoa maelezo machache kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange na wageni waalikwa.  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano DAWASA Neli Msuya akitoa ufafanuzi wa mradi huo.  Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja akitoa maelezo juu ya mradi huo mbele ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (wa pili toka kushoto) na Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere pamoja wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa DAWASA, Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (Katikati), akizungumza mbele ya wanahabari juu ya mradi wa ukarabati wa tenki la maji alilokabidhiwa Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere (kushoto). Pembeni ni Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Cyprian Luhemeja (kwanza kulia).  Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere akitoa shukrani zake mbele ya wageni waliohudhuria hafla ya kukabidhi tenki la maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere lililokarabatiwa na DAWASA hivi karibuni.  Wafanyakazi wa DAWASA, Wanahabari na wageni waalikwa wakisikiliza kwa makini. 


Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA) mapema leo amekabidhi tenki la maji lenye ujazo wa lita 170,000 kwa mke wa hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Mama Maria Nyerere. Tenki ambalo lilikuwa halitumiki na sasa litatumika na litawawezesha kupata maji nyumbani kwa Hayati Mwalimu Nyerere, Msasani jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza na Wanahabari mara baada ya kumaliza kukabidhi tenki hilo Msasani, jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa Bodi ya DAWASA Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange amesema wameamua kukarabati tenki hilo lilokuwa halitumiki kwa muda mrefu kutokana na miundombinu ya tenki kuwa chakavu nakupelekea kuwa na ukosefu wa maji ya kutosha nyumbani kwa Mama Nyerere.

Amesema maji ni kila kitu katika maisha ya binadamu hivyo hatuna budi kuyalinda na kuyatunza ili yaweze kututunza pia. Nae Mtoto wa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Makongoro Nyerere ameishukuru DAWASA kuweza kulikarabati tenki hilo lililokuwa limekufa na halitumiki kwa muda mrefu. 

"Kiukweli sina cha kusema zaidi ya kutoa shukrani zangu za pekee kwenu kwa niaba ya mama yangu, hili tenki lilikuwa halitumiki kwa muda mrefu ila nyie mmelifufua na sasa tunapata maji ya kutosha," amesema Makongoro Nyerere. 

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema wao walijitoa kukarabati tenki hilo kwa kuondoa laini ndogo ya inchi moja ilikuwa inasababisha kutumia mota kuvuta maji ilikuwezesha kupata maji yakutosha hivyo kupelekea bili ya maji kuwa kubwa pamoja gharama za umeme.

NJOMBE MJI YAIPIGA MSASA SUMBAWANGA

$
0
0
 Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu kutoka katika Manispaa ya Sumbawanga wakiwa kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe mara baada ya kuwasili kwa lengo la kujifunza maswala ya usafi wa mazingira na ukusanyaji mapato. (Aliyesimama) ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Illuminata Mwenda
 Mweka Hazina wa Halmashauri ya Mji Njombe Bi. Dorcas Mkello akiwasilisha mada ya ukusanyaji mapato kwa Wahe. Madiwani na Wataalamu kutoka Manispaa ya Sumbawanga

 Afisa Mazingira Halmashauri ya Mji Njombe Lawi Bernard, akitoa mpango mkakati wa Halmashauri ya Mji Njombe wa utunzaji na uthibiti wa taka ngumu kwa Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu kutoka katika Manispaa ya Sumbawanga wakati wa ziara ya mafunzo ya timu hiyo katika Halmashauri ya Mji Njombe. 
 Afisa TEHAMA kutoka Halmashauri ya Mji Njombe Isack Mapunda akitoa ufafanuzi wa matumizi bora ya mashine za ukusanyaji mapato (POS) kwa Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu kutoka katika Manispaa ya Sumbawanga wakati wa ziara ya mafunzo ya timu hiyo katika Halmashauri ya Mji Njombe.
Mradi wa ujenzi wa kituo kipya cha mabasi unaofadhiliwa na benki ya dunia kupitia mradi wa uboreshaji na uimarishaji Miji (ULGSP) katika Halmashauri ya Mji Njombe  ni miongoni mwa mradi uliotembelewa na  Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu kutoka Manispaa ya Sumbawanga.




=========  ============   ================  ============

MARA BAADA YA KUZIBURUZA HALMASHAURI ZA MIJI KWENYE MASHINDANO YA USAFI, HALMASHAURI YA MJI NJOMBE YAIPIGA MSASA MANISPAA YA SUMBAWANGA.

Hyasinta Kissima-Njombe

Halmashauri ya Mji Njombe imepokea ugeni wa Waheshimiwa Madiwani wakiambatana na Wataalamu kutoka katika Manispaa ya Sumbawanga lengo ikiwa ni kujifunza na kuongeza maarifa kuhusiana na maswala ya mapato na usafi wa Mazingira.

Haya yamebainika wakati wa hafla fupi ya kuwakaribisha wageni hao iliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Njombe, ambapo ugeni huo ulikiri wazi kuwa wamevutiwa kufika Halmashauri ya Mji Njombe kujifunza kutokana na sifa ambazo Halmashauri imekuwa ikijizolea kila mara katika eneo la usafi wa Mazingira pamoja na ukusanyaji mapato.

“Halmashauri ya Mji Sumbawanga kwa mwaka wa fedha 2017/2018 tulikasimia kukusanya bilioni mbili na milioni mia tano, lakini hatukufanikiwa kukusanya asilimia 80 kwa mujibu wa maagizo ya Mhe. Waziri Mkuu tulikusanya asilimia 54 pekee. Kwa upande wa mashindano ya usafi na Mazingira tulishika nafasi ya pili kutoka mwisho kutokana na ukosefu wa vyoo bora na matumizi bora ya vyoo.”Alisema Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Mhe. Justin Emmanuel Malisawa.

Alifafanua kuwa changamoto kubwa ambayo imekuwa ikiwakabili ni kwenye utekelezaji wa sheria ndogo ndogo za Halmashauri na changamoto kutoka kwa wanasiasa ambao wamekuwa wakipinga na kutotekeleza ipasavyo baadhi ya maazimio waliyojiwekea kwenye ukusanyaji wa mapato na utunzaji Mazingira na ndio maana waliona umuhimu wa kuja kujifunza kutoka Njombe.

Akielezea mafanikio ya Halmashauri ya Mji Njombe ambayo imefikia kwa upande wa usafi wa Mazingira sambamba na ukusanyaji mapato, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe, Bi Illuminata Mwenda amesema kuwa mafanikio hayo yalitokana na utayari na kujitoa kwa Madiwani bila kujali itikadi za vyama vyao na ushirikiano wa Wataalamu.

“Madiwani ndio wanaotaka Halmashauri yao iweje, hivyo ndivyo ninavyofahamu. Mnaweza mkawa na mipango mizuri lakini Waheshimiwa Madiwani wakisema hapana inakuwa ndivyo. Madiwani wetu agenda zao kuu ni mapato na usafi. Na hata katika vikao vya wataalamu tumekuwa tukijadili na kuboresha mapungufu yanayojitokeza na kuweka mikakati thabiti kwenye ukusanyaji mapato na usafi wa Mazingira na tumekuwa tukifanikiwa kwa kiasi kikubwa.”Alisema Mwenda.

Dorcas Mkello ni Mweka Hazina wa Halmashauri ya Mji Njombe ambaye yeye amesema kuwa miongoni mwa mbinu ambazo wamekuwa wakizitumia kwenye ukusanyaji mapato ni sambamba na utoaji wa motisha ya pikipiki kwa watendaji wanaofanya vizuri kwenye ukusanyaji mapato na kutoa milioni 5 kwa kila Diwani kwa kila robo ya mwaka fedha ambazo hukabidhiwa kwa diwani wa Kata husika kwa ajili ya kuchochea maendeleo kwenye Kata yake. Hivyo kupitia fedha hizo, kila diwani amekuwa mlinzi kwenye usimamizi wa mapato kwani wasipofanya hivyo wanaelewa fika fedha hizo hazitapatikana bila kukusanywa kwa nguvu kubwa.

Afisa Mazingira Halmashauri ya Mji Njombe Lawi Bernard amesema kuwa licha ya kuwa na mwamko chanya wa wananchi kwenye uchangiaji wa tozo za taka, Halmashauri kupitia mapato ya ndani imekua ikiona umuhimu wa kuiwezesha idara hiyo na ndio maana kwa mwaka wa fedha 2018/2019 walifanikiwa kutenga fedha kupitia mapato ya ndani na kununua tractor kwa ajili ya kubeba taka na hivyo kuzuia mlundikano wa taka katika maeneo ya Mji kutokana na uwepo wa vitendea kazi vya kutosha.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe Edwin Mwanzinga alisema kuwa, siri ya mafanikio ni umoja baina ya Waheshimiwa Madiwani na wataalamu kwani wamekuwa wakipokea maelekezo ya wataalamu na panapokuwa na mapungufu wamekuwa wakishirikiana kuboresha kwa manufaa ya Halmashauri nzima.

“Wenzangu wa Sumbawanga niwaombe muwe na ushirikiano katika ukusanyaji mapato. Maendeleo ni ya wananchi wote na hayana vyama, naomba pia mfahamu kuwa katika swala la Usafi na Mazingira hamtaweza kufanya vizuri kwa kutegemea Halmashauri itaondoa taka yenyewe, lazima mzalisha taka awe na jukumu la kuondoa taka kwa kuchangia gharama.”Alisema Mwanzinga.

Aidha, Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu kutoka Manispaa ya Sumbawanga wameishukuru Halmashauri ya Mji Njombe kwa elimu waliyoipata na wamepongeza ujenzi wa kiwango cha hali ya juu unaoendelea katika kituo kipya cha Mabasi na wameahidi kutengeneza mtandao wa mawasiliano na Halmashauri ya Mji Njombe ili kuendelea kupata ujuzi na mbinu mpya katika maeneo mbalimbali.

Ikumbukwe kuwa Halmashauri ya Mji Njombe kwa miaka miwili mfululizo; 2017/2018 na 2018/2019 imepokea wageni kutoka Halmashauri nane za Mikoa ya Songwe, Singida, Shinyanga na Rukwa kwaajili ya kujifunza mbinu na siri ya ushindi inayotumia Halmashauri ya Mji Njombe katika kuimarisha hali ya usafi katika maeneo yake yote.

MFANYABIASHARA KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA KUCHAPISHA TAARIFA ZA UONGO DHIDI YA RAIS MAGUFULI

$
0
0

Na Karama Kenyunko, Globu ya jamii

MFANYABASHARA Henry  Munisi (30)mkazi wa mkoani Mbeya, Leo Januari 22,2019 amepandishwa katika kizimba  cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo dhidi ya Rais Magufuli.

Akisoma hati ya Mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi Patrick Mwita amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Salum Ally kuwa mshtakiwa ametenda kosa hilo Desemba 28, mwaka 2018 akiwa jijini Mbeya.

Imedaiwa kuwa,  siku ya tukio mshtakiwa Munisi kupitia ukurasa wake wa Facebook  alichapisha taarifa  za uongo zinazosema "Jinsi Magufuli alivyochota Sh.trilioni 1.5 za ATCL akitumia  ujanja wake wa kuleta ndege ili atuibie" huku akijua taarifa  hizo ni za uongo na zina lengo la kupotosha umma. 

Hata hivyo, mshtakiwa amekana kutenda kosa hilo na amerudishwa rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ambapo mahakama imemtaka mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye barua za utambulisho watakaosaini bond ya Sh. 500,000.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka,  upelelezi katika kesi hiyo bado haujakamilika na kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 6, 2019.
MFANYABASHARA Henry  Munisi (30)mkazi wa mkoani Mbeya, leo Januari 22,2019 akipandishwa katika kizimba  cha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kujibu tuhuma za kuchapisha taarifa za uongo dhidi ya Rais Magufuli.

KAMATI YA HUDUMA NA MAENDELEO YA JAMII YAPOKEA TAARIFA YA BODI YA MIKOPO

$
0
0
 Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Ndg. Abdul Razaq Badru  akiwasilisha Taarifa ya utekelezaji wa majukumu na bajeti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu kwa kipindi cha nusu mwaka 2018/2019 mbele ya  Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii katika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma hii leo.
 Mjumbe wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mheshimiwa Hawa Ghasia akichangia jambo mbele ya Kamati hiyo ilipokuwa ikipokea na kujadili Taarifa ya utekelezaji wa majukumu na bajeti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu kwa kipindi cha nusu mwaka 2018/2019 katika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma hii leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Selukamba akifafanua jambo mbele ya Kamati hiyo ilipokuwa ikipokea na kujadili Taarifa ya utekelezaji wa majukumu na bajeti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu kwa kipindi cha nusu mwaka 2018/2019 katika Ukumbi wa Msekwa Jijini Dodoma hii leo.

SHIRIKA LA BIMA ZANZIBAR LADHAMINI MASHINDANO YA RIADHA

$
0
0
Na Ahmed Mahmoud,Arusha.

Shirika la bima Zanzibar limedhamini mashindano ya riadha ya Mererani Tanzanite Half Marathon ambayo yatafanyika mwishoni mwa wiki na kujumuisha idadi kubwa ya wanariadha kutoka mikoa ya Arusha,Manyara na Kilimanjaro.

Mkurugenzi wa shirika la bima Zanzibar kanda ya Kaskazini Hamis Matumla alisema hayo Jana wakati akikabidhi kiasi cha shillingi milioni mbili ambazo ni udhamini was shirika hilo ikiwa ni njia mojawapo ya kuunga mkono michezo na kuhamasisha umuhimu wa afya kwa wachezaji.
Matumla alisema kuwa kuelekea Mashindano ya Riadha ya Mbio fupi yajulikanayo kama Mererani Tanzanite Half Marathon yatakayofanyika huko Mkoani Manyara ,Wadau wa Michezo wanapaswa kujitokeza kushiriki pamoja na kudhamni Mashindano hayo yenye lengo la kutangaza madini hayo yanayopatikana Tanzania Pekee.

"Jamii inatapaswa kujenga utamaduni wa kupenda kushiriki Michezo kwani michezo ni ajira na michezo ni afya pia" Alisema Matumala

Kwa upande wao waandaaji wa Mashindano hayo wakiongozwa na Mwenyekiti wao Charles Mnyalu wanasema uandikishaji unaendelea katika Vituo mbalimbali vilivyopo hapa nchini na Washiriki na Washindi watapata Zawadi Mbalimbali.

Alisema Mbio hizo zitakazofanyika mnamo tarehe 27 mwezi huu katika Viunga vya mji wa Mererrani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara zitashirikisha wanariadha wa kilometa tano ambao ni Watoto pamoja na Kilometa ishirini na Moja kwa Watu Wazima huku zaidi wanariadha elfu moja mia tano wakitarajia kushiriki.

Mjumbe Kamati ya Mashindano Alfredo Shahanga aliwataka Wakazi wa manyara ,Arusha na mikoa ya jirani kujitokeza kwa wingi katika mbio hizo.

BENKI YA NMB YASAIDIA ELIMU WILAYA ZA MOMBA NA ILEJE

$
0
0


Wanafunzi wa Shule ya sekondari Ileje wakionyesha furaha yao baada ya kupokea msaada wa viti (stuli) 184 vyenye thamani ya shilingi Milioni 5 ambavyo ni miongoni kwa msaada uliotolewa na NMB Bank kwaajili ya kuboresha masomo ya sayansi mashuleni wilayani Ileje na Momba za jijini Mbeya. Benki ya NMB juzi ilitoa bati 254 kwa Halmashauri ya Tunduma wilayani Momba, Madawati 50 kwa shule ya msingi Nyerere na Stuli 184 kwa shule za sekondari Ileje na Kafule vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 25.

Wanafunzi wa Shule ya sekondari Ileje wakiwa wamebeba madawati yaliyotolewa na benki ya NMB kwaajili ya shule ya Msingi Nyerere Wilayani Ileje Mkoani Songwe. Benki ya NMB juzi ilitoa bati 254 kwa Halmashauri ya Tunduma wilayani Momba, Madawati 50 kwa shule ya msingi Nyerere na Stuli 184 kwa shule za sekondari Ileje na Kafule vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 25.

Wanafunzi wa Shule ya sekondari Ileje wakiwa wamebeba madawati yaliyotolewa na benki ya NMB kwaajili ya shule ya Msingi Nyerere Wilayani Ileje Mkoani Songwe. Benki ya NMB juzi ilitoa bati 254 kwa Halmashauri ya Tunduma wilayani Momba, Madawati 50 kwa shule ya msingi Nyerere na Stuli 184 kwa shule za sekondari Ileje na Kafule vyote vikiwa na thamani ya shilingi Milioni 25.

 
WAKUU wa Wilaya za Ileje na Momba Mkoani Songwe wamewapigita magoti taasisi, makampuni na mashirika kujitokeza kusaidia miundombinu ya elimu ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitohaza za Serikali kuwahudumia wananchi.

Wakuu hao ni Jumaa Irando wa Momba na Joseph Mkude wa Ileje walitoa rai hiyo jana kwa nyakati tofauti wakati wakipokea msaada wa vifaa vya shule kutoka Benki ya NMB ambayo ilitoa bati 254 kwa Halmahauri ya Tunduma Wilaya ya Momba na madawati 50 kwa shule za Msingi Nyerere na sturi 184 za maabara shuleni kwa shule za Sekondari za Ileje na Kafule zote za Wilayani Ileje huku vyote vikigharimu Sh25 milioni.

Irando alisema Mji wa Tunduma ni miongoni mwa miji inayokuwa kwa kasi kutokana na ongezeko kubwa la watu hivyo wamekuwa na changamoto lukuki kwenye suala la miondombinu ya shule kwa Serikali pekee kulitimiza bali kwa kuungwa mkono na wadau mbalimbali kama walivyofanya NMB.“Kwa kweli tunachangamoto kubwa sana hapa Tunduma, kuna ongezeko kubwa la watoto wanaoanza darasa la kwanza kila mwaka tofauti na makisio au matarajio tunayokuwa tumejiwekea.

Jambo hili linafanya kuwa na msongamano mkubwa mashuleni kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa na madawati pia, hivyo NMB mmetuangalia kwa jicho la pekee kabisa kuona tunahitaji msaada wenu na wadau wengine waige hili jambo kwa ajili ya kuisadia jamii yetu,”

Alisema mahitaji ya huduma za kijamii ikiwemo afya na elimu yanahitaji kuungwa mkono na taasisi na mashirika mbalimbali ya kijamii kama inavyofanywa na Benki ya NMB.Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Joseph Mkude alisema imetekeleza wajibu wao na thamani yao kwa Watanzania hususani wananchi wa Ileje ambao kimsingi wapo pembezoni kabisa mwa nchi.

Alisema ‘Nawashukuru sana NMB kutukubalia ombi letu na leo hii kutuletea sturi na madawati kwetu sisi tunauthamini mno mchango wenu na katika hili tunazidi kuwaunga mkono kwa jitihada zenu, na tuwaahidi tutahakikisha vifaa hivi vinatunzwa ili vidumu kwa muda mrefu’.

Awali Meneja wa NMB Kanda ya Nyanda za Juu, Straton Chilongola alisema benki ya NMB inatambua umuhimu wa elimu na afya kwa Watanzania hivyo katika kipindi cha mwaka huu wa 2019, NMB imetenga Sh1 bilioni kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya jamii ikiwamo afya, elimu na majanga ya dharula kwa nchi nzima.

Hivyo benki hiyo itaendelea kusaidia katika sekta hiyo ikiwa ni sehemu ya kuunga juhudi za Serikali za kuwahudumia wananchi wake. Alisema NMB ni wadau muhimu kwa Serikali na Watanzania hivyo wanao wajibu wa kuunga mkono juhudi za maendeleo kwa sababu jamii wanayoisaidia ndiyo inayowawezesha kupata faida katika biashara yao.

“Tunambatua changamoto ya elimu na afya, sisi NMB tunazipa kipaumbele sana kwa sababu hizi sekta mbili ni muhimu mno katika ustawi wa jamii yetu,” alisema Chilongola.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images