Waziri wa Nchi Ofis ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. Kapteni Msaafu George Mkuchika akimkabidhi Tuzo, Bw.Vita Kawawa aliyeambatana na mwanafamilia mwenzake Bibi. Zamaradi Kawawa kwa niaba ya Waziri Mkuu wa zamani Hayati Rashid Mfaume Kawawa ikiwa ni kuthamini mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili kupitia sanaa ya maonesha na michezo ya kuigiza wakati wa hafla ya kilele cha Kamapeni ya Uzalendo na Utaifa leo jijini Dodoma. Kutoka kushoto ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi akimkabidhi Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe kwa niaba ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli zawadi ya Kamusi Kuu ya Kiswahili iliyotolewa na Baraza la Kiswahili Tanzania (Bakita) wakati wa Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”. Anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa CD za makala ya uzalendo wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akiwa pamoja na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza (kulia) na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi wakionyesha CD za makala ya uzalendo mara baada ya kuzinduliwa rasmi wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi Kitabu cha Uzalendo wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza akimkabidhi Tuzo mmoja ya wasanii wakongwe kwa kutambua mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili kupitia sanaa ya muziki wakati wa hafla ya kilele cha Kamapeni ya Uzalendo na Utaifa leo jijini Dodoma.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Masuala ya Ulemavu na Bunge, Stella Ikupa akimkabidhi cheti Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita), Dkt. Selemani Sewangi kwa kutambua mchango wake katika kukuza lugha ya Kiswahili wakati wa hafla ya kilele cha Kamapeni ya Uzalendo na Utaifa leo jijini Dodoma. Kutoka kulia ni Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe. (Picha zote na: Frank Shija – MAELEZO)
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bibi Susan Mlawi akizungumza wakati wa Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza akitoa neno la shukrani wakati wa hafla za Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
Msanii Mrisho Mpoto akitumbuiza mbele ya washiriki wa hafla ya Kilele cha Kampeni ya Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo katika ukumbi wa DCC jijini Dodoma. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Dkt. Ayoub Ryoba akielezea jambo wakati wa mdahalo kuhusu Uzalendo na Utaifa wakati wa Kilele cha Kampeni ya Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 leo jijini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Tanzania (Bakita), Dkt. Seleman Sewangi.
Baadhi ya washiriki wa hafla ya Kilele cha Kampeni za Uzalendo na Utaifa mwaka 2018 wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa hafla hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa DCC jijini Dodoma leo. Kauli mbiu ya Kampeni hizo kwa mwaka huu ni ” Kiswali Utashi Wetu, Uhai Wetu”.