Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46396 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli amteua Prof. Humphrey Mushi kuwa Mwenyekiti wa FCC


KAMPUNI YA KILUWA GROUP YAWATAMBULISHA WADAU WAKE WA UWEKEZAJI WA VIWANDA KWA MKUU WA MKOA WA PWANI

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Pwani,Mhandisi Evarist Ndikilo akimsikiliza Mwenyekiti wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa alipokuwa akiwatambulisha Wadau wake wa uwekezaji kutoka nchini china,waliofika Oktoba 29,2018  kumtembelea na kujitamulisha ofisini kwake ,kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong akiwa ameambatana na Wenzake Wane.Kampuni hiyo inajishughulisha na uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za ngozi nchini China. 
Meneja wa Kampuni ya Kiluwa Group Ndugu Madoweka pichani kulia akifafanua zaidi kwa lugha ya Kichina, kilichokuwa kikizungumzwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani,Mhandisi Evarist Ndikilo kwa Wawekezaji hao waliofika nchini kwa mwaliko wa Kampuni ya Kiluwa Group,kutafuta fursa za uwekezaji wa viwanda katika bidhaa mbalimbali za ngozi
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong akiwa ameambatana na Wenzake Wane (hawapo pichani),akiushukuru uongozi wa Mkoa wa Pwani pamoja na Kampuni ya Kiluwa Group kwa mapokezi mazuri kufuatia ujio wao wa kutafuta fursa za uwekezaji kupitia kampuni yao inajishughulisha na uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za ngozi nchini China,pichani kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group Bi.Naima Kiluwa.
Mkuu wa mkoa wa Pwani,Mhandisi Evarist Ndikilo akizungumza na ugeni wake uliomtembelea Ofisini kwake Oktoba 29,2018 na kuzungumza nae mambo kadhaa katika suala zima la uwekezaji katika mkoa wa Pwani,wakiwa na mwenyeji wao Mwenyekiti wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa .
Mkuu wa mkoa wa Pwani,Mhandisi Evarist Ndikilo akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong inayojishughulisha na uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za ngozi nchini China.
Wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya utambulisho

ROCK CITY MARATHON 2018 ILIVYONOGA: Watanzania, Wakenya wang’ara Rock City Marathon

$
0
0
 Mwanariadha Mourice Masima Kutoka Kenya  akimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza mwishoni  mwa wiki baada ya kutumia  muda wa saa 2:19:14. Kivutio katika mbio hizo ilikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella ambae licha ya kuzindua mbio hizo, alikimbia kikamilifu mbio za km 42 akiambatana na baadhi ya viongozi  waandamizi  wa serikali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Magu  Dk. Philemon Sengati .
 Mwanariadha Emmanuel Giniki  kutoka Tanzania akimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 21 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza leo baada ya kutumia  muda wa 1:04:09 akifuatiwa na Mkenya Daniel Kayioki alietumia muda wa saa 1:04:47.
 Mshindi wa kwanza  mbio za km 42 kwa upande wa wanawake Naomi Jepngetich kutoka Kenya  aliyetumia muda wa saa 02:44:19 kukamilisha mbio hizo.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akishiriki katika mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akishiriki katika mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Baadhi ya washiriki wa mbio za Rock City Marathon wakiwa kazini!
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  akimaliza mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza.
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akikabidhi zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mwanariadha Mourice Masima Kutoka Kenya  aliemaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza mwishoni  mwa wiki baada ya kutumia  muda wa saa 2:19:14.
 Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya TIPER, Bw Emmanuel Kondi akikabidhi  zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 4 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 42 kwa wanawake mwanariadha Naomi Jepngetich kutoka Kenya  aliyetumia muda wa saa 02:44:19 kukamilisha mbio hizo. Kulia  ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bw John Mongella. TIPER ni moja ya wadhamini wakubwa wa mbio hizo.
 Mwakilishi kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Bi. Flora Ndutta akikabidhi  zawadi ya cheti,medali na pesa taslimu kiasi cha sh mil. 3 kwa mshindi wa kwanza mbio za km 21 mwanariadha Failuna Matanga kutoka Tanzania.
 Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MWAA) Bw Silas Lucas (kulia) akikabidhi zawadi  kwa mshindi wa kwanza mbio za KM 21 Emmanuel Giniki kutoka Tanzania alietumia saa 1:04:09 akifuatiwa na Mkenya Daniel Kayioki alietumia muda wa saa 1:04:47.
 Baadhi ya washiriki wa mbio za km 5 wakimalizia mbio hizo zilizohitimishwa kwenye viunga vya jengo la Rock City Marathon.
 Mmoja wa washiriki wa mbio za KM 3 mahususi kwa ajili ya wazee akiwa kazini
 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , John Mongella  (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa mbio za km 42 Rock City Marathon kwa upande wa wanawake. Wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa mbio hizo Bw Zenno Ngowi  (wa tatu kulia), Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Kuhifadhi Mafuta ya TIPER, Bw Emmanuel Kondi (Kulia kwa Mkuu wa Mkoa) pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Riadha Mkoa wa Mwanza (MWAA) Bw Silas Lucas.
Mkuu wa Wilaya ya Magu  Dk. Philemon Sengati (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa mbio za km 5 kwa upande wa watu wenye ualibino.


Katika mashindano hayo ilishuhudiwa washiriki ambao pia ni wadhamini wa mbio hizo kutoka  makampuni ya Puma Energy Tanzania, Tiper,Rock City Mall,  NSSF, Gold Crest, New Mwanza Hotel,  CF Hospital, Coca Cola, Metro Fm, EF Outdoor,  KK Security, Belmont Fairmount Hotel , Bigie Customs na Global Education Link wakishiriki kikamilifu katika mbio za KM 5 sambamba na watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino.

Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein, Atembelea Mradi wa Ujenzi wa Jengo Jipya ya Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimskiliza Kaimu Mkurugenzi Tiba Dr. Fadhil Abdallah, akitowa maelezo ya Ujenzi wa Jengo Jipya la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati alipotembelea Mradi huo wa ujenzi wake katika eneo la Hospitali ya Kivunge Zanzibar, kulia Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed na kushoto Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe Vuai Mwinyi.

Jengo Jipya la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja likiwa katika Ujenzi wake katika eneo la hospitali hiyo. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Eng. wa Kampuni ya World Class Engineering Contractars Ndg. Joshua Christopher Nyari, akitowa maelezo ya michoro ya ujenzi wa Hospitali hiyo inayojengwa katika maeneo ya Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Daktari Dhamani wa Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja Dr. Tamim Hamad Said, akitowa maelezo ya michoro ya jengo jipya la Hospitali ya Kivunge kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, wakati alipotembelea Mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali hiyo katika eneo la Hospitali ya Kivunge.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Afya Zanzibar, wakati alipotembelea Mradi wa Jengo la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja. kulia Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed na kushoto Daktari Dhamana wa Hospitali ya Kivunge Dr. Tamim Hamad Said na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bi. Asha Abdallah.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja, kushoto Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed, wakitembelea Mradi huo wa ujenzi wa jengo hilo katika viwanja vya Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.   
Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed akitowa maelezo ya Mradi huo wa ujenzi wa jengo la Hospital ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Mradi huo, akiwa katika ziara yake.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akielekezwa  na kuonesha moja ya sehemu ya jengo hilo na Kaimu Mkurugenzi Tiba Wizara ya Afya Zanzibar na Dr. Fadhil Abdallah wakati akitembelea Mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali Mpya ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.wakati wa ziara yake Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu)  

POLISI,TRA KILIMANJARO WANASA KIWANDA FEKI CHA KUTENGENEZA POMBE KALI.

$
0
0
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamisi Issah (anayeongea na Simu ) akiongozana na Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoa wa Kilimanjaro ,Godfrey Kitundu walifika kwenye nyumba inayoaminika kuwa kiwanda cha kutengeneza Pombe kali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Hamisi Issah akitizama baadhi ya chupa ambazo zimendaliwa kwa ajili ya kujaza kimiminika cha Pombe kali.
Sehemu ya Mitambo iliyopo ndani ya kiwanda hicho kilichopo katika wilaya ya Himo ambacho kinaaminika kuhusika katika kutengeneza Pombe kali bila ya kufuata taratibu.
Anayedaiwa kuwa mmoja wa wafanyakazi wa kiwanda hicho akitoa maelezo kwa kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Hamisi Issah pamoja na Meneja Msaidizi wa TRA Kilimanjaro anayeshughulikia masuala ya forodha ,Godfrey Kitundu ndani ya kiwanda hicho.
Sehemu ya Mitambo iliyopo ndani ya kiwanda hicho.
Baadhi ya Chupa zilizokutwa ndani ya kiwanda hicho zikiwa hazina stika ya TRA.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Hamisi Issah akijadili jambo na Meneja Msaidizi wa TRA -Kilimanjaro ,Godfrey Kitundu mara baada ya kukagua kiwanda hicho.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

JESHI la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamefanikiwa kukamata kiwanda  cha kutengeneza Pombe kali ambacho kimekuwa kikizalisha bidhaa hiyo bila ya usajili.
Moja ya dira za serikali ya awamu ya tano ni kufikia uchumi wa kati kupitia Viwanda ,hata hivyo baadhi ya wafanyabiahara watafsiri Dira hii tofauti kwa kuamua kuanzisha Viwanda bila ya kufuata matakwa ya Sheria na taratibu za nchi.

Hali hii imejidhihirisha mkoani Kilimanjaro katika mji mdogo wa Himo baada ya Polisi,TRA na TFDA kubaini uwepo wa kiwanda bandia kinachozalisha Pombe kali .
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamisi Issah amesema jeshi la Polisi litaendelea kushirikiana na idara nyingine za serikali kuhakikisha kodi ya serikali inapatikana pamoja na kuhakiki ubora wa bidhaa kwa ajili ya afya ya watumiaji.
Zoezi la kubaini uwepo wa viwanda bandia katka mkoa wa Kilimanjaro ambapo katika siku za karibuni viwanda vilivyogundulika ni vile vinavyotengeneza Pombe za kienyeji na Pombe kali ,baadhi  vikiwa katika wilaya ya Rombo.

NIMERIDHISHWA NA HATUA ZA AWALI ZA UWEKEZAJI MKINGA-MAJALIWA

$
0
0
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tanga, Henry Shekifu wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Tanga kuanza ziara  ya kazi mkoani humo, Oktoba 30, 2018. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela wakati alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Tanga kuanza  ziara ya  kazi mkoani humo Oktoba 30, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea eneo la mradi wa ujenzi wa viwanda 11 katika kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga, ambapo amesema ameridhishwa na hatua za awali za uwekezaji huo.

Katika eneo hilo vinatarajiwa kujengwa viwanda mbalimbali kikiwemo cha saruji cha Hengya, kiwanda cha vioo, kiwanda cha vifaa vya kisasa vya ujenzi, uzalishaji wa umeme kwa kutumia makaa ya mawe.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Oktoba 30, 2018) wakati akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mtimbwani wilayani Mkinga akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya kikazi ya siku tatu mkoani Tanga.

Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kulinufaisha Taifa na wananchi wakazi wa wilaya ya Mkinga kwa kuwa kinatarajiwa kuajiri zaidi ya watu 8,000, hivyo amewaomba wananchi hao waendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji hao.

Kuhusu wananchi ambao eneo lao limechukuliwa na wawekezaji na bado hawajalipwa fidia Waziri Mkuu amewataka wawe na subira kwa kuwa wote watalipwa. “Muwekezaji amenihakikishia kwamba atawalipa wananchi wote wanaodai fidia.”

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuuamewataka watumishi wa umma kutenga siku tatu katika wiki na kuwafuata wananchi waishio maeneo ya vijijini kwa ajili ya kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi.

Amesema Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuwatumikia wananchi bila ya ubaguzi wa kidini, kisiasa, rangi  na kimapato, hivyo amewataka watumishi hao wafanye kazi kwa bidii.

Awali, Mbunge wa jimbo la Mkinga, Dastan Kitandula ameishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi wa Mkinga baada ya Serikali kufuta hati ya shamba la moa na kuirudisha ardhi hiyo kwa wananchi, pia ameomba ifute hayi za mashamba mengine yaliyotekelezwa katika Tarafa ya Maramba.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMANNE, OKTOBA 30, 2018.

Rais Dk. Shein Atembelea Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja leo

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimskiliza Kaimu Mkurugenzi Tiba Dr. Fadhil Abdallah, akitowa maelezo ya Ujenzi wa Jengo Jipya la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati alipotembelea Mradi huo wa ujenzi wake katika eneo la Hospitali ya Kivunge Zanzibar, kulia Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed na kushoto Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Mhe Vuai Mwinyi.
Jengo Jipya la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja likiwa katika Ujenzi wake katika eneo la hospitali hiyo. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Eng. wa Kampuni ya World Class Engineering Contractars Ndg. Joshua Christopher Nyari, akitowa maelezo ya michoro ya ujenzi wa Hospitali hiyo inayojengwa katika maeneo ya Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Daktari Dhamani wa Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja Dr. Tamim Hamad Said, akitowa maelezo ya michoro ya jengo jipya la Hospitali ya Kivunge kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, wakati alipotembelea Mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali hiyo katika eneo la Hospitali ya Kivunge.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akisisitiza jambo wakati akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Afya Zanzibar, wakati alipotembelea Mradi wa Jengo la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja. kulia Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed na kushoto Daktari Dhamana wa Hospitali ya Kivunge Dr. Tamim Hamad Said na Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bi. Asha Abdallah.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Mradi wa Ujenzi wa Jengo la Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja, kushoto Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed, wakitembelea Mradi huo wa ujenzi wa jengo hilo katika viwanja vya Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.   
Waziri wa Afya Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohammed akitowa maelezo ya Mradi huo wa ujenzi wa jengo la Hospital ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Mradi huo, akiwa katika ziara yake.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akielekezwa  na kuonesha moja ya sehemu ya jengo hilo na Kaimu Mkurugenzi Tiba Wizara ya Afya Zanzibar na Dr. Fadhil Abdallah wakati akitembelea Mradi huo wa Ujenzi wa Hospitali Mpya ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akitembelea Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Kivunge Mkoa wa Kaskazini Unguja.wakati wa ziara yake Mkoa wa Kaskazini Unguja.(Picha na Ikulu) 

IGP SIRRO AKUTANA NA IGP WA RWANDA

$
0
0
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro (kushoto) akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Rwanda DCG Dan Munyuza, leo 30/10/2018 walipokutana katika eneo la Kirehe karibu na mpaka unaotenganisha nchi hizo mbili Tanzania na Rwanda ambapo baadae watafanya kikao cha Ujirani mwema kitakachojadili masuala mbalimbali ya kiusalama baina ya nchi hizo mbili. Picha na Jeshi la Polisi Tanzania.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro (kushoto) akiwa amefuatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Rwanda DCG Dan Munyuza, leo 30/10/2018 wakivuka mpaka unaotenganisha nchi hizo mbili Tanzania na Rwanda na kuingia eneo la Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera kwa ajili ya kikao cha ujirani mwema kitakachojadili masuala mbalimbali ya kiusalama baina ya nchi hizo mbili. Picha na Jeshi la Polisi Tanzania.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, akimsikiliza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Rwanda DCG Dan Munyuza, wakati wa kikao cha ujirani mwema kinachofanyika Rusumo wilayani Ngara mpakani mwa Tanzania na Rwanda leo 30/10/2018. Picha na Jeshi la Polisi Tanzania.
Kikao kikiendelea

Makamu wa Rais atembelea Banda la IPP TOUCHMATE wiki ya maonyesho ya Viwanda Kibaha

$
0
0
Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan jana amezindua wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’ yanayofanyika katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani.
Kabla ya kutoa hotuba yake katika uzinduzi huo, Makamu wa Rais alitembelea banda la kampuni ya IPP TOUCHMATE na kupata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti Mtendaji wa Makapuni ya IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi.
Dk. Mengi alimweleza Makamu wa Rais kuhusu ushirikiano wa kampuni hizo mbili wa kuanzisha kiwanda cha kutengeneza vifaa mbalimbali vya Kielekroniki nchini vitakavyouzwa kwa bei nafuu na kutumika katika utoaji wa elimu, ili kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu wa tano ya kuboresha  elimu.
Dk. Mengi alimweleza Makamu wa Rais kuwa kampuni ya Touchmate ipo Dubai na ina uzoefu wa miaka 30 wa kutengeneza vifaa vya kielektroniki kama simu za kisasa (smart phones, tablets, kompyuta na vifaa vya nyumbani).
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi akisalimiana na mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan alipowasili katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani kwa ajili ya kufungua wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’. 
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi akiteta jambo na mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan alipowasili katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani kwa ajili ya kufungua wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’. 
 Mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani alipowasili katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani kwa ajili ya kufungua wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’.  
 Mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (kulia), alipotembelea banda la IPP TOUCHMATE katika maonyesho ya wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’. Kushoto ni Mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani.
 Mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan akikagua vifaa vya kielektroniki kama simu za kisasa (smart phones, tablets, kompyuta na vifaa vya nyumbani) huku akipata maelezo kutoka kwa mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani (kushoto) alipotembelea banda la IPP TOUCHMATE katika maonyesho ya wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’. Kushoto ni Mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha na wa pili kulia ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi.
 Mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan akisoma maelezo yaliyomo kwenye moja ya bidhaa za kielektoniki alipotembelea banda la IPP TOUCHMATE katika maonyesho ya wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’. Kushoto ni mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani.
Baadhi ya wananchi waliotembelea banda la IPP Ltd lililopo katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani  wakiangalia vifaa vya kielektroniki kama simu za kisasa (smart phones, tablets, kompyuta na vifaa vya nyumbani) wakati wa ufunguzi wa wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’, yaliyofunguliwa rasmi jana na Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan mkoani humo.
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Nishati, Mh. Subira Mgalu wakati wakisubiri kuwasili kwa mgeni rasmi Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani kwa ajili ya kufungua wiki ya maonyesho ya viwanda ambapo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’. Katikati ni Mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (kushoto) na Mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani wakiwa kwenye picha ya pamoja ndani ya banda la IPP Ltd lililopo katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani wakati wa ufunguzi wa wiki ya maonyesho ya viwanda ambayo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’, yaliyofunguliwa rasmi jana na Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan mkoani humo.
 Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Ltd, Dk. Reginald Mengi (wa pili kulia), Mwasisi na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Touchmate, Bw. Vasant Menghani (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha (wa pili kushoto) katika picha ya pamoja nje ya ya banda la IPP Ltd lililopo katika viwanja vya Sabasaba, Kibaha picha ya Ndege, Mkoani Pwani wakati wa ufunguzi wa wiki ya maonyesho ya viwanda ambayo taasisi 25 zinashiriki kuonyesha  bidhaa zake huku yakibeba kauli mbiu ya ‘Viwanda Vyetu, Uchumi Wetu’, yaliyofunguliwa rasmi jana na Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu Hassan mkoani humo.

DC CHONGOLO ASITISHA UCHIMBAJI WA KOKOTO KWA MUDA BOKO,JIJINI DAR

$
0
0


Mkuu wa Wliaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo amekiri kuwepo kwa migogoro mingi ya ardhi kwenye Wilaya hiyo, ambapo amesema migogoro hiyo inaibuka kutokana na kutengenezwa na watu.

DC Chongolo ametoa kauli hiyo wakati alipotembelea eneo la Uchimbaji Kokoto katika eneo la Boko jijini Dar es Salaam, eneo lililokumbwa na migogoro baina ya Wawekezaji na Wachimbaji hao.

Akizunguma na Globu ya Jamii na Michuzi TV, Mhe. Chongolo amesitisha shughuli za uchimbaji kokoto katika eneo hilo mpaka watakapokaa kwa pamoja Novemba Mosi 2018, kati ya Wachimbaji wa Kokoto,wamiliki wa eneo na Serikali ili kusuluhisha mgogoro huo ikiwa sambamba na kuangalia namna ya kuendelea au kuacha shughuli hizo.

Chongolo amesema katika maeneo hayo ya uchimbaji watahakikisha yanakuwa na Leseni ya Manispaa, Leseni ya Madini, Cheti cha TRA, Mazingira, Mikataba kwa Waajiriwa, Malipo ya ushuru wa Madini kwa Manispaa na usajili katika uzalishaji Madini. "Kwenye haya maeneo ya uchimbaji Kokoto wanachimba kiholela, uharibufu ni mkubwa sana, magari yanapita juu chini wamechimba mashimo, mvua ikinyesha wanakimbilia wanajificha kwenye haya mashimo, ikileta madhara kwa watu malalamiko yote yanakuja kwa Serikali’’, amesema DC Chongolo.

Kwa upande wake mmoja wa Wawekezaji katika eneo la Boko, Mwakilishi wa Kampuni ya Usafirishaji na Uchimbaji wa Kokoto ya Al-Hushoom Evestment, Badi Lema amedai wao ni wamiliki halali wa eneo hilo, amesema kuna Watu wamevamia eneo hilo hivyo waliiomba Serikali ifike kwenye eneo hilo kujionea uvamizi huo.

Badi amesema licha ya kulinda eneo hilo, Wavamizi hao wameendelea kuingia kwenye eneo hilo kwa ajili ya kufanya shughuli za uchimbaji wa kokoto. Hata hivyo moja ya Wananchi wanaofanya shughuli hizo za Uchimbaji amedai kuwa eneo hilo wamepewa na Wazo, wamedai eneo hilo walipewa kama Wananchi wa Boko. Pia baadhi ya Wachimbaji hao wamedai kuwa ruhusa ya Uchimbaji Kokoto katika eneo hilo la Boko wamepewa na Serikali ya Mtaa.
Baadhi ya Wachimbaji wa Kokoto wakiendelea na shughuli zao katika eneo linalodaiwa kuvamiwa na watu hao,ikiwemo uvunjwaji wa sheria za utunzaji mazingira,na utaraibu wa kuchimba kokoto hizo

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni akizungumza mbele ya Wachimbaji Kokoto katika eneo la Boko,ambalo linadaiwa kuvamiwa na wananchi huku wakiendeleza shughuli za uchimbaji bila kufuata utaratibu/sheria.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Daniel Chongolo akiwa na watalaamu wake wakiondoka kwenye eneo hilo la wachimbaji Kokoto eneo la Boko,mara baada ya kujionea hali halisi na kuamuru uchimbaji kokoto katika eneo hilo usitishwe mara moja,mpaka hapo watakapokutana siku ya Alhamisi na kuamua nini kifanyike.

Mmoja wa wachimbaji Kokoto katika eneo hilo akieleza jambo kwa mkuu wa Wilaya Mh.Daniel Chongolo (hayupo pichani),aliyefika kujionea halisi ya eneo hilo

DIRA YA KITAA MPAMBANAJI NA MTAFUTAJI

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 31,2018

KAMISHNA JENERALI WA MAGEREZA PHAUSTINE KASIKE AFUNGA MKUTANO MKUU WA SITA WA MAGEREZA SACCOS, LEO JIJINI DODOMA

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike ambaye pia ni Mlezi wa Magereza SACCOS nchini akitoa hutuba ya ufungaji wa Mkutano Mkuu wa sita wa Mwaka wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara. Mkutano huo unaofanyika kwa siku mbili leo Oktoba 30, 2018 jijini Dodoma.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa sita wa Mwaka wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(hayupo pichani) ambaye pia ni Mlezi wa Magereza SACCOS nchini .
Wanachama mbalimbali wa Saccoss ya Magereza wakiwa mbele ya wajumbe wakati wa uchaguzi wa Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara katika Mkutano huo.
Wajumbe wa Sekretarieti ya Mkutano Mkuu wa sita wa Mwaka wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Watumishi wa Jeshi la Magereza Tanzania Bara wakifuatilia ufungaji wa Mkutano huo.
Kamishna Jenerali wa Magereza, Phaustine Kasike(katikati) ambaye pia ni Mlezi wa Magereza SACCOS nchini akiondoka ukumbini mara baada ya ufungaji wa Mkutano, aliyeambatanaye ni Mwenyeketi wa Bodi ya Magereza Saccos, SACP. Mbaraka Semwanza(kushoto). Kulia ni Kamishna wa Utawala na Rasilimali watu, Gaston Sanga(Picha zote na Jeshi la Magereza).

MZEE ALIYEKAA HOSPITALI YA KIOMBOI IRAMBA MIAKA 10 AOKOLEWA NA ZIARA YA DKT. NDUGULILE

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amemuagiza Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi kuhakikisha Bibi. Aisha Hamisi aliyeishi zaidi ya miaka kumi katika Hospitali ya Kiomboi iliyopo Wilaya ya Iramba Mkoani Singida anapelekwa katika Makao ya kuhudumia Wazee na Wasiojiweza.

Hatua hiyo imekuja baada ya Naibu Waziri huyo kuongea na Mzee huyo na kupata taarifa kuwa hana ndugu wala Jamaa wa kumlea hivyo anakosa huduma muhimu za kibinadamu wakati wa ziara yake katika Hospitali ya Kiomboi iliyopo Wilaya ya Iramba Mkoani Singida.

Kwa mujibu wa Taarifa ya Afisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Iramba amemueleza Naibu Waziri Ndugulile kuwa Bibi Aisha Hamisi amekaa zaidi ya miaka kumi katika Hospitali ya Kiomboi alikuwa akitibiwa na kuendelea kukaa hapo kwa kukosa ndugu wa kumchukua na kumtunza.

Aidha Dkt. Ndugulile ameagiza Mzee huyo apelekwe katika Makao ya kuwahudumia Wazee na Wasiojiweza ya Sukamahela yaliyopo Wilaya ya Manyoni ili kupata huduma muhimu. Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa Serikali ina jukumu la kuwatunza Wazee na Wasiojiweza kwa wale ambao hawana ndugu wala jamaa wa kuwatunza.

Akipokea maelekezo hayo Kamishna Msaidizi wa Ustawi wa Jamii Bw. Rabikira Mushi amesema kuwa suala la kumuhamishia Bibi Aisha kwenye Makao ya Wazee litafanyika mara moja na hatahamishiwa katika Makao ya Wazee ya Sukamahela.

Kwa upande wake Bibi Aisha Hamisi amemshukuru Naibu Waziri kwa kuja kutembelea Hospitali ya Kiomboi na kumwomba kutatua changamoto za matibabu zinazowapata Wazee.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akisaliana na Bibi Aisha Hamisi wakati alipofanya ziara katika Hospitali ya Kiomboi Wilayani Iramba Mkoani Singida kuangalia hali ya utoaji wa huduma za Afya, Ustawi na Maendeleo ya Jamii. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW 

MSICHAGUE VIONGOZI MAZEZETA NA MANANGA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2019-SAMIA

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Samia Suluhu amewataka wananchi wa Kibaha Mjini Mkoani Pwani ,wajipange kuchagua viongozi wepesi kufuatilia maendeleo na kwenda mbio badala ya kuchagua mazezeta na mananga ,katika uchaguzi unaokuja wa serikali za mitaa- 2019.

Akihitimisha ziara yake ya siku sita mkoani hapo katika mkutano wa hadhara ,Mailmoja Samia aliwasihi wasichague watu wazito,wezi na mafisadi bali waweke viongozi watakaojenga Kibaha .

"Wanasema mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe ,mimi nikija ninaona kasoro zilizopo nitakwambieni kuna kasoro lakini warekebishaji ni nyinyi na viongozi mtakaowachagua ""Mkichagua wazuri wataondosha kasoro zilizopo haraka lakini mkichagua wazito na mananga hapa yatazama tuu chini kunyanyuka hayanyanyuki ,kutembea hayatembei "alisisitiza Samia .

Akizungumzia suala la ardhi anasema",Wakati napita ,mheshimiwa mkuu wa mkoa alinionyesha eneo kubwa halina kitu chochote nikamwambia mnataka manispaa ,lakini mbona eneo hili mwitu mtupu hakuna kuendelezwa akaniambia linamilikiwa na taasisi fulani "

Aidha ,ameitaka wilaya na halmashauri ya Mji huo kukaa chini na taasisi ambazo zimehodhi maeneo bila kuyaendeleza katika kipindi kirefu ili ziweze kuingia ubia .Awali Mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini ,Silvestry Koka aliomba mji huo upandishwe hadhi na kuwa manispaa kama vigezo vinaruhusu.Alitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni ,usambazaji wa maji kwenda kwa wananchi unasuasua kasi iongezwe kwani mji unakua ila maji hayajawafikia .

" Eneo la Tamco-Mapinga zaidi ya miaka mitano wapo wananchi walifanyiwa tathmini lakini hawajalipwa fidia zao ,tunaomba utusaidie wananchi hawa waweze kufaidika na fidia hizo"alielezea Koka.Koka alitaja tatizo jingine ni ucheleweshaji wa nishati ya umeme , kasi ni ndogo kufika kwa baadhi ya maeneo na wawekezaji ,ameomba uwafikie maeneo yaliyo katika miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.

Akijibu changamoto hiyo, Naibu waziri wa nishati ,Subira Mgalu alisema , kupitia serikali ipo sheria iliyoanzisha wakala wa nishati ya umeme vijijini lakini maeneo ya miji sheria ile ilikuwa huwezi kufanya miradi ya umeme mijini."Serikali ya awamu ya tano kwa makusudi mazima iliona miji ifaidike na raslimali zinazopatikana kwenye mfuko wa umeme vijijini na kwa maelekezo yenu tulibuni mradi wa Peri Urban";alifafanua Subira.

Subira alisema ,kiasi cha sh. bilioni 82 zimetengwa kwa ajili ya mradi huo na sasa hatua iliyopo ni kumpata mkandarasi ili mradi uanze kazi .Aliwahakikishia wananchi ambao hawana umeme katika kata ya Mailmoja ,Viziwaziwa,Pichandege ,Pangani, Misugusugu ,Sofu watanufaika na mradi huo .

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ramadhani Maneno, alisema Pwani ipo salama na ushindi ni lazima ,iwe jua iwe mvua uchaguzi ujao wa serikali za mitaa atahakikisha wanashinda .
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan

MAJALIWA AWEKA JIWE LA MSINGI LA KIWANDA CHA CHOKAA CHA NEELKANTH CHEMICALS LIMITED CHA JIJINI TANGA

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka jiwe la msingi la kiwanda cha chokaa cha Neelkanth Chemical Limited kilichopo jijini Tanga, Oktoba 30, 2018. Wapili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela, watatu kushoto ni mmiliki wa kiwanda hicho, Rashidi Liemba na kulia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Tanga, Henry Shekifu. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

DKT KALEMANI: AWATAKA MAMENEJA WA TANESCO NCHINI KUWAKATIA UMEME WADAIWA SUGU KWENYE MAENEO YAO.

$
0
0
 WAZIRI wa Nishati Dkt Medard Kalemani kulia akizundua mradi wa umeme wa gharama nafuu (REA awamu ya tatu) kwenye Kijiji cha Katurukila wilayani Kilombero mkoani Morogoro wakati wa ziara yake kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Kilombero James Ihunyo akishuhudia 
 WAZIRI wa Nishati Dkt Medard Kalemani kulia akizundua mradi wa umeme wa gharama nafuu (REA awamu ya tatu) kwenye Kijiji cha Katurukila wilayani Kilombero mkoani Morogoro wakati wa ziara yake
 WAZIRI wa Nishati Dkt Medard Kalemani akizungumza na wananchi wa kwenye Kijiji cha Katurukila wilayani Kilombero mkoani Morogoro mara baada ya kuzindua Rea awamu ya tatu
  WAZIRI wa Nishati Dkt Medard Kalemani akizungumza na wananchi wa kwenye Kijiji cha Katurukila wilayani Kilombero mkoani Morogoro mara baada ya kuzindua Rea awamu ya tatu
 MKUU wa wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro James Ihuny'o akizungumza katika uzinduzi huo
 Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Shirika la Tanesco Mhandisi Theodory Bayona ambaye pia ni Meneja Mwandamizi wa Usambazaji na huduma kwa wateja akizungumza katika uzinduzi huo
 Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco Kanda ya Kati akizungumza wakati wa ziara hiyo
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani kulia akimsikiliza kwa umakini Meneja wa Shirika la Tanesco mkoani Morogoro Mhandisi Hassan Saidi wakati wa ziara yake 
 Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani katikati akielekea kufanya uzinduzi huo
 Sehemu ya wananchi wakifurahia hotuba ya Waziri wa Nishati Dkt Kalemani 
Sehemu ya wananchi wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Waziri wa Nishati Dkt Kalemani




WAZIRI wa Nishati Dkt Medard Kalemani amewaagiza Mameneja wa shirika la Umeme (Tanesco) kote nchini kuhakikisha wanakata huduma ya umeme kwa wadaiwa sugu ikiwemo sekta binafasi na serikalini. 

Dkt Kalemani aliyasema hayo wakati wa ziara yake wilayani Morogoro iliyokuwa na lengo la kutembelea maeneo yanayozalisha umeme ikiwemo Kidatu ambako uzalishaji wa umeme ni 204 mw. 

Licha ya kutembelea eneo hilo lakini pia alizindua mradi wa umeme wa gharama nafuu (REA awamu ya tatu) kwenye Kijiji cha Katurukila wilayani Kilombero mkoani Morogoro. Alisema kwamba hatua hiyo inaweza kuwa mwarobaini wa kuweza kusaidia kukusanya madeni hayo ambayo yamekuwa kwa muda mrefu na hivyo kupelekea kukwamisha malengo yao waliojiwekea. 

Aidha alisema kwamba haiwezekani shirika hilo likawa linawadai watu fedha nyingi ambazo zingeweza kutumika kwenye kutekeleza shughuli za kimaendeleo na kuweza kuwafikia wananchi wengi huku wakiacha kuwachukulia hatua ambazo zinaweza kusaidia kupata ufumbuzi wake. 

“Ndugu zangu mameneja wa mikoa hakikisheni mnawakatia umeme wadaiwa wote sugu kwenye maeneo yenu wakiwemo wale wa sekta binafasi na serikali kwani hii ndio njia inayoweza kuwasaidia kukusanya madeni hayo “Alisema Dkt Kalemani. Akizungumzia kitengo cha huduma kwa wateja ndani ya shirika hilo Dkt Kalemani alisema ni muhimu watumishi wa kada hiyo wakabadilikana kitabia kwa sababu imedodira sana na kwenye maeneo mengi hazifanyi kazi zao ipasavyo. 

“Ukatakuta wateja wanapiga simu haipokelewi wakati watu wanaohusika nacho wapo hivyo kuanza sasa sipendi kusikia simu ikipigwa haipokelewi mameneja hakikisheni watu wa namna hiyo mnawachukuliwa hatua”Alisema. 

“Lakini pia ikibidi mtoeni yupo ndani ya uwezo wenu lakini kama anamajibu mabaya wachukulieni hatua…. Haiwezekani mtu anapiga simu unamwambia huu sio masaa ya kazi juzi manyara nilipiga simu nikaambiwa kwamba haya sio masaa ya kazi huyu mtu bado namtafuta kwani huwezi kuwa na biashara nzuri kama mtu anayekutana na wateja wao hatekelezi wajibu wake”Alisema Waziri Dkt Kalemani 

Awali akizungumza katika ziara hiyo Meneja wa Shirika la Tanesco Kanda ya Kati Mhandisi Atanausus Nangali alisema mradi huo wa gharama nafuu ni mradi wa ubunifu wa miundombinu ya gharama nafuu wa majaribio uliojengwa kupitia Rea na kugharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano. 

Alisema kwa Tanzania mradi huo umefanyika kwa wilaya mbili ambazo ni wilaya ya Mbozi wilayani Mbeya na Kilombero mkoani Morogoro kwa mkoa wa Morogoro mradi wa LCD ambao ulitekelezwa na mkandarasi NAMIS Corparate Limited chini ya usimamizi wa Tanesco uliandaliwa kujenga njia za umeme zenye urefu wa kilomita 137.7 na msongo wa kati. 

Alisema pia kilomita 55.4 za umeme mdogo na kuweka mashine umba 320 na kuunganisha wateja 5731 kati ya hao wateja 5637 wa njia moja na wateja 94 wa njia tatu katika kutekeleza mradi huu mkandarasi alipewa jukumu la kujenga mifumo ya kusambaza umeme kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 2.4 huku zifaa vyote vikiletwa na kampuni ya Rea.

TAARIFA KWA UMMA

Advocating for nationwide connectivity/Connecting the unconnected Tanzanians – One region at a time.

$
0
0

No matter what part of the world you live in, communication is a vital aspect of everyday life facilitating connection between people. The use of phones has evolved from interactions with friends and family to tools that enable commercial transactions for businesses. In Tanzania, the highest rate of mobile phone penetration is in urban areas however 67.6% of the population resides in rural areas where connectivity remains a challenge.

A Deloitte study of 40 African economies reveals that the introduction of mobile networks has the potential to influence socio-economic development for individuals and villages in remote areas. Additionally, the study shows that 1% increase in market penetration leads to an increase of 0.28 percentage points in GDP and 1% increase in internet penetration increases the GDP growth rate by 0.077 percentage points in the economy.

We live in a world where a person in the southern highlands of Tanzania needs to be able to access breaking news as it happens from his mobile phone and also have the ability to use the same phone to source commercial opportunities in other parts of Tanzania. Without enabling rural access it would take a long time for information to reach people in rural areas thus hindering their progress.

According to FinScope Tanzania 2017, 78% of Tanzanian adults in rural areas have a financial access point within a 5km radius. Due to the limited footprint of traditional bank branches, the majority of financial service providers found within a 5km radius are mobile money agents whose presence facilitate transactions that allow for residents to participate in economic activities that improve their livelihoods. Rural connectivity empowers the lives of those that reside great distances from urban centers.

Vodacom Tanzania PLC, the leading telecommunications company in the country, has been at the forefront of advancing rural connectivity and has demonstrated its commitment by supporting the government in its objectives to bridge the digital divide by progressing connectivity to over 60% of the population that resides in the rural areas in order to unlock the economic potential that lies in the rural areas. The Telco has been at the forefront ensuring that all Tanzanians have access to communication. The company currently covers over 75 % of the connected population with a bouquet of technologies ranging from GSM 900/1800, 3G and WiMAX 803.16d.

The future is promising for rural connectivity in Tanzania - Vodacom recently entered into a long term contract with The National ICT Broadband Backbone (NICTBB) that allows the former to use government-owned fiber optic cable infrastructure to enhance connectivity in rural Tanzania. With increasing demand for information services, Vodacom will use the government infrastructure to meet customer needs as fiber optics cables can carry larger amounts of information over a longer distance helping bridge the technological disparities of rural areas.

Additionally, through an agreement with Universal Communication Service Access Fund (UCSAF), Vodacom has set out to improve basic telecom services to the most rural villages and underserved urban areas in Tanzania. Under this agreement, 194 new sites have been added reaching 187 wards in Tanzania providing access to communication and internet services to improve the socio-economic standing of 654 new villages in Tanzania.

Schools in those remote villages can now connect to the internet and share ideas with others far away, farmers can quickly check prices of produce and make informed decisions on trading. Mwanahamisi, a woman trader in Mtwara remarks, ‘it is now so easy for me to talk to the company in Mozambique that buys my rosella products. I don’t have to keep crossing the border.’

Connectivity also enables the transfer of critical health data and life-saving information by text messages to clinics to support rapid diagnoses for patients in remote villages.Although the socio-economic benefits are vast, the deployment of rural access services remains a challenge due to the required investment to ensure that broadband services are not only deployed but also remain sustainable.

In order for rural connectivity to be realized, key conditions have to be met: partnerships between the private and public sector, roll out of projects that provide high-speed network access, and the provision of friendly regulatory frameworks. These strategies lie at the heart of providing an enhanced and holistic service to potential customers in the rural areas of Tanzania.

Vodacom Tanzania named the Best Employer in Africa 3rd year in a row

$
0
0
Tanzania’s leading telecommunication service provider Vodacom has been named as the best employer in Africa and Tanzania for the 3rd time in a row by global company Top employer Institute. Top Employer Institute is a global certification company recognizing excellence in the conditions that employers create for their people.

The Global Top employer institute, now in its 25th year conducts in-depth assessment to identify top employers in the world who meet set criteria which include best HR practices. Vodacom Tanzania PLC has been certified as a 2019 Top Employer after leading the way in outstanding ‘people-first’ HR practices and qualified as one of the successful organisations.

A statement from the company signed by Human Resources Director Perece Kirigiti detailed that the exciting achievement was officially announced last week as a result of global research and subsequent certification of only the very best employers worldwide.

She hinted that as a proud Top Employer 2019, Vodacom’s practices were assessed through the analysis of 100 questions which covered 600 people practices across 10 Human Resources topics including but not limited to Talent Strategy, On-boarding, Learning & Development and Compensation & Benefits. The Top Employers Institute Programme provides organisations with the ability to leverage employer branding, benchmark practices against other top performers and globally align policies.

Kirigiti concluded that the award means a lot to Vodacom saying “As a certified Top Employer 2019, we have the honour of showcasing our Certification seal with pride for the upcoming year. This seal serves as a reminder that we are a part of a global community of forward-thinking organisations that continue to strive for only the best people practices, and this seal further cements our commitment to optimizing and improving our business performance.”
Viewing all 46396 articles
Browse latest View live




Latest Images