Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live

BENKI YA KCB TANZANIA YATOA MSAADA WODI YA WANAWAKE KATIKA HOSPITALI YA RUFAA AMANA

$
0
0



Mkuu wa Masoko, Mawasililiano na Mahusiano wa Benki ya KCB, Christine Manyenye(kulia) akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye mkutano wa makabidhiano ya misaada mbalimbali ikiwemo vitanda 10 magodoro 10, mashuka 20, vyenye thamani ya shilling 6,017,000 katika wodi ya wananwake Hospitali ya Amana Ilala Jijini Dar Es Salaam. Kushoto ni Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dr. Amim Kilomoni.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali Ya Amana, Dr. Amim Kilomoni akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano wa makabidhiano ya misaada mbalimbali toka Benki ya KCB ikiwemo vitanda 10 magodoro 10, mashuka 20, vyenye thamani ya shilling 6,017,000 kwa wodi ya wanawake katika Hospitali hiyo leo jijini Dar Es Salaam.
Mkuu wa Masoko, Mawasililiano na Mahusiano wa Benki ya KCB, Christine Manyenye (kushoto) akimkabidhi Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dkt. Amim Kilomoni moja kati ya Vitanda na Vifaa vingine vyenye thamani ya Tsh 6,017,00/= kwa wodi ya wanawake Hospitali ya Amana, Dar Es Salaam
Wafanyakazi wa KCB na Wauguzi wa Hospitali ya Amana wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya Benki ya KCB kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vyenye thamani ya TSh . 6,017,000 kwa wodi ya wanawake leo kwenye Hospitali ya Amana Ilala, Dar Es Salaam.
Baadhi ya waandishi waliohudhuria mkutano wa makabidhiano.


 Benki ya KCB Tanzania imekabidhi msaada wenye thamani ya milioni 6 kwa wodi ya wanawake katika Hospitali ya Rufaa ya Amana, Ilala jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano Mkuu wa Masoko, Mawasililiano na Mahusiano wa benki hiyo, Christine Manyenye alisema kuwa mchango huo upo ndani ya vipaumbele vya benki katika uwekezaji jamii kwa ajili ya kusaidia jamii zilizo na uhitaji.

“Benki ya KCB Tanzania inadhamini uwajibikaji kwa jamii ambayo kwa kiwango kikubwa inalenga maeneo ya vipaumbele vya Afya, Elimu, Mazingira, Ujasiriamali na masuala ya ubinadamu”, Bi. Manyenye alisema na kubainisha kwamba tangu benki hiyo ilipofungua milango yake hapa Tanzania mwaka 1997, imekuwa ikijikita katika kuisadia jamii.

Benki ya KCB ilikabidhi misaada mbalimbali ikiwemo vitanda 10 magodoro 10, mashuka 20, vyenye thamani ya shilling 6,017,000 katika Hospitali hiyo. Mkurugenzi huyo alisema kuwa upungufu wa vitanda, magodoro na masuka katika hospitali nyingi nchini ni changamoto hasa katika wodi za akina mama na watoto Benki ya KCB iliamua kutoa msaada huo ilikupunguza changamoto hizo.

Akitolea mfano wa michango iliyotolewa na benki hiyo katika kupunguza viwango vya vifo vya kinamama na watoto nchini, Manyenye alisema: “Kupitia miradi hiyo Benki ya KCB Tanzania imeshazisaidia hospitali zaidi ya 15 kwa kuzipatia vifaa tiba mbalimbali.”

Alizitaja hospitali hizo kuwa ni Muhimbili, Mwananyamala, Ocean Road Cancer Institute, Buguruni, Sinza, Amana, Temeke na Kituo cha Afya cha Njia (Dar es Salaam); Mt. Meru na Ngarenaro (Arusha); KCMC, St. Thomas na Mawenzi (Moshi); SDA na Makongoro (Mwanza); Hospitali ya Morogoro (Morogoro); Kivunge Cottage na Kituo cha Huduma za Afya Kombeni (Zanzibar) na Hospitali ya Mkuranga (Pwani).

Kwa upande wake, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali Ya Amana, Dr. Amim Kilomoni aliishukuru KCB Bank kwa msaada waliotoa kwani utasaidia kupunguza changamoto zilizokuwa zinawakabili, ikiwamo uhaba wa vitanda, magodoro na mashuka.

MAKAMU WA RAIS AISHUKURU BENKI YA NMB KWA KUTOA MSAADA WA VIFAA VYA AFYA NCHINI

$
0
0
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Samia Suluhu Hassan, ameishukuru Benki ya NMB kwa kwa kutoa msaada wa mashuka 108, mashine za kupumulia wagonjwa mahututi, vitanda maalum vya kujifungulia, na vitanda vya wagonjwa vyote vikiwa na thamani ya Shilingi Milioni 15 kwenye kituo cha afya cha Maneromango wilayani Kisarawe mkoani Pwani.

Akipokea vifaa hivyo aliushukuru ongozi mzima wa Benki ya Nmb kwa kuendelea kusaidia jamii katika suala zima la afya katika wilaya ya Kisarawe na maeneo mengine hapa nchini.Mkuu wa Kitengo cha Biashara za Serikali cha NMB, Bi. Vicky Bishubo juzi alimkabidhi Makamu wa Rais Samia Suluhu msaada huo kwa ajili ya vituo vya afya vya Maneromango, Chole na Kirui vyote vya wilayani Kisarawe.

Makamu wa Rais Suluhu Hassan alipokea msada huo mara baada ya ziara yake ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara za lami Kisarawe mjini, ikiwa sehemu ya ziara yake ya siku sita ya kukagua na kuhamasisha shughuli za maendeleo katika Mkoa wa Pwani.

Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu akiangalia mashine ya Oxygen iliyokabidhiwa na Benki ya NMB kwa kituo cha afya Maneromango wilayani Kisarawe mkoani Pwani. Pia benki ilikabidhi jumla ya mashuka 108, vitanda vya kujifunguliwa, na vitanda vya wagonjwa vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 15. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Vicky Bishubo na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, NMB - Joseline Kamuhanda.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akipokea msaada wa vifaa vya hospitali kutoka kwa Mkuu wa kitengo cha Biashara za Serikali cha NMB – Vicky Bishubo kwaajili ya vituo vya afya vya Maneromango, Chole na Kirui vya wilayani Kisarawe. NMB ilikabidhi jumla ya mashuka 108, vitanda vya kujifunguliwa, na vitanda vya wagonjwa vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 15. Wa pili kutoka (kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo na wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano NMB, Joseline Kamuhanda.
Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan akiangalia moja ya kitanda cha kujifungulia kilichokabidhiwa na Benki ya NMB kwa kituo cha afya cha Maneromango wilayani Kisarawe mkoani Pwani. Pia benki ilikabidhi jumla ya mashuka 108, vitanda vya kujifunguliwa, na vitanda vya wagonjwa vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 15. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara ya Serikali wa Benki ya NMB, Vicky Bishubo na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa NMB - Joseline Kamuhanda.
 

NMB YADHAMINI SHINDANO LA KAMPUNI BORA 100 TANZANIA

$
0
0
KAMPUNI Bora 100 Tanzania (Top 100 Mid-sized Companies' Survey) ni shindano linaloendeshwa na Mwananchi Communications Limited kwa kushirikiana na KPMG. Shindano hili ambalo hufanyika kila mwaka tangu 2011, huku likiwa na lengo la kuzitambua na kuzizawadia kampuni za kati zinazofanya vizuri, kuchochea maendeleo ya Tanzania kiuchumi.

Benki ya NMB ni miongoni mwa wadhamini wa shindano hili, huku ikijikita katika kusaidia eneo la SME, kipengele ambacho ni muhimu katika maendeleo ya kiuchumi na kuchochea makampuni hayo kufanya vizuri zaidi. NMB ni kichocheo muhimu cha SME pia, lazima ijenge mazingira mazuri ili kuleta maendeleo zaidi. Utafiti huu kwa makampuni ni muhimu kwa sababu unatoa jukwaa la SMEs, kampuni ambazo wengi ni wateja wetu, kupata mafanikio katika maendeleo ya kiuchumi na taifa kwa ujumla.

Makampuni ambayo yanaingia katika ushindani ni yale ambayo mauzo yao yanaanzia shilingi 1 za kitanzania hadi bilioni 20, na kumbukumbu zake za kifedha kukaguliwa kwa miaka 3 iliyopita, na pia isiwe kwenye orodha ya soko la hisa wala kuwa kampuni ya benki / bima / SACCOS / Sheria / Uhasibu au kampuni ya ukaguzi mahesabu.

Makampuni za Juu 100 zilizopitishwa kati za makampuni yote yaliyoshiriki yatazingatiwa katika ukuzaji kimapato.Mbali na NMB, wengine wa kampuni bora Bora ya mwaka 2018/2019 ni pamoja na Soko La Hisa la Dar es Salaam na Azam Media na Hoteli ya Hyatt Regency.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker akizungumza kwenye hafla ya kutunuku kampuni Bora ya mwaka 2018/2019 (Top 100 Mid-sized Companies' Survey).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker akisalimiana na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harison Mwakyembe kwenye hafla hiyo.
Meza kuu katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker (kulia) katika mazungumzo na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Dk. Harison Mwakyembe (katikati) kwenye hafla hiyo. 

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KAMPUNI YA AIRTEL AFRICA KUUZA HISA KWENYE SOKO LA KIMATAIFA.

SERIKALI YA TANZANIA YAANZA MAZUNGUMZO NA UJERUMANI YA MGAO WA MAPATO YATOKANAYO NA MJUSI MKUBWA ‘DINOSAUR’ KUPITIA WATALII

$
0
0
 Serikali ya Tanzania kupitia Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Japhet Hasunga  imesema ipo kwenye hatua za awali za mazungumzo na Serikali ya Ujerumani kuona jinsi itakavyofaidika na mapato yatokanayo na utalii  kupitia mabaki ya Mjusi mkubwa ‘’Dinosaurs ambaye ni kivutio cha kikubwa cha  utalii  katika jumba la  Makumbusho nchini Ujerumani

Mjusi huyo kwa jina la kitaalamu anaitwa Dinosaur ambapo mabaki yake yalivumbuliwa  miaka  100 iliyopita katika eneo la Tendaguru  mkoani Lindi, yalikusanywa na kupelekwa  nchini Ujerumani ambako wataalamu waliyaunda na kisha kuyaweka kwenye Makumbusho hiyo.

Amesema lengo la mazungumzo hayo ni kutaka  kujua kiasi gani  cha mapato yanayokusanywa na  namna gani  wanavyoweza kugawana mapato hayo   yatokanayo na watalii kupitia mjusi huyo baina ya Serikali hizo mbili.

Amesema mwelekeo wa  mazungumzo hayo yaitapelekea Serikali ya Tanzania kufanya uamuzi   wa kumrudisha mjusi huyo  au kumuacha kule kule   lakini akiwa  analiingizia pato taifa  

Ameyabainisha hayo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na Waandishi wa habari kuhusiana na mIkakati ya  Serikali ya kuendeleza vivutio vya utalii kwa mikoa ya Kusini.
 Hata hivyo, Mhe.Hasunga amesema  uamuzi wa kumrudisha  mjusi huyo nchini utakuwa mgumu kwa vile sehemu kubwa ya mjusi huyo ameunganishwa unganishwa kwa kutumia vifaa maalumu.

Ameongeza kuwa kutokana na jinsi alivyounganishwa unganishwa na anakadiri wa kuwa na  urefu wa mita 13.7 kwenda juu  hivyo kumsafirisha itakuwa ngumu.

Katika hatau nyingine, Mhe Hasunga amesema hadi hivi sasa  Serikali ya Ujerumani haijaweza kuweka bayana kiasi cha mapato yanayokusanywa  kupitia Mjusi huyo licha ya kuwa Serikali hiyo  imekuwa ikifadhili miradi mingi ya uhifadhi nchini.

"Tunaamini kuwa pesa wanazofadhili miradi mingi ya Uhifadhi imekuwa inatokana na makusany okupitia Mjusi huyo Mkubwa" amesema Hasunga 

Hata hivyo,kuendelea kuwepo kwa masalia ya mjusi huyo katika Makumbusho hiyo kuna manufaa makubwa kwa vile anatambuliwa kuwa ni wa kutoka Tanzania,Hivyo ni Balozi wa Utalii na utafiti wa kisayansi anayeitangaza Tanzania sehemu mbalimbali duniani.

WAFANYAKAZI WATANO WA NEMC WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUGHUSHI SAINI YA WAZIRI JANUARI MAKAMBA

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii

WAFANYAKAZI watano wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka sita ya uhujumu uchumi likiwamo la kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais -Muungano na Mazingira Januari Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa mazingira.

Wakili wa Serikali Faraja Nguka amewasomea washtakiwa makosa yao leo Oktoba 31, 2018 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustina Mmbando.Wakili Nguka amedai washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, mawili ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuisababishia Serikali hasara ya Sh 160 milioni.

Aidha Mahakama imetoa hati ya kukamatwa kwa mshtakiwa Magori Wambura (38) mkazi wa Bombambili kwa sababu wakati washtakiwa hao wakisomewa mashtaka hayo yanayowakabili mshtakiwa huyo ambae ni Ofisa mazingira wa Nemc, hakuwepo mahakani.Wakili Nguka amewataja washtakiwa hao kuwa ni Ofisa wa Mazingira NEMC Deusdith Katwale, Msewe, Luciana Lawi, Edna Lutanjuka, Ofisia Mwaruka na Lilian Laizer.Imedaiwa kati ya Septemba 27, 2016 na April I mwaka huu wa 2018 washtakiwa walikula njama ya kutenda kosa la kughushi.

Katika shtaka la pili washtakiwa hao wanadaiwa, Oktoba 17,2017 kwa udanganyifu walighushi cheti cha tathmini ya uharibifu wa mazingira chenye namba ya usajili EC/EIA/3366 wakijaribu kuonesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati wakijua si kweli.Pia washtakiwa hao wanadaiwa kughushi saini ya Januari Makamba ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais -Muungano na Mazingira katika cheti cha tathmini ya uharibifu wa Mazingira chenye usajili namba EC/ EIA/3366 wakijaribu kuonesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati wakati wakijua si kweli.

Mshtakiwa Edna anadaiwa kuwa Oktoba 2017 katika ofisi za NEMC Makao Makuu Dar es Salaam kwa kujua alitoa cheti cha kughushi cha tathmini ya uharibifu wa mazingira chenye namba ya usajili EC/EIA/3366 cha oktoba 17,2017 kwa Deogratius Chacha, akijaribu kuonyesha kuwa cheti hicho ni halali na kwamba kimetolewa na NEMC wakati akijua si kweli.

Pia washtakiwa walijipatia kwa njia ya udangnyifu Sh.milioni 160 toka kwa PMM Estate (2001) Ltd kwa madai kuwa wangefanya tathimini ya uharibifu wa mazingira na kumpatia cheti ambacho kinatolewa na NEMC kitendo ambacho si kweli.Aidha washtakiwa wanadaiwa kati ya Septemba 27, 2016 na Aprili 6,2018 Dar es Salaam waliisababishia NEMC hasara ya Sh.milioni 160.

Washtakiwa hao hawakuruhusiwa kuongea chochote kwa sababu mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu,.Washtakiwa wamepelekwa rumande kesi imeahirishwa hadi Novemba 14, mwaka huu na upelelezi wake bado haujakamilika.
WAFANYAKAZI watano wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)  wakiwa wamefishwa katika chumba cha  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka sita ya uhujumu uchumi likiwamo la kughushi saini ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Rais -Muungano na Mazingira Januari Makamba katika vyeti vya tathmini ya uharibifu wa mazingira.

'TBL KUMENOGA, TUUTANE BAA' KUPATA MSHINDI WA GARI KUFANYIKA WIKI IJAYO

$
0
0






Meneja wa Udhamini na Mawasiliano ya Wateja wa TBL, David Tarimo na Meneja wa Biashara na ukuzaji wa Masoko wa TBL,wakionyesha magari ambayo washindi watajinyakulia kupitia promosheni hii. -Wateja wahimizwa kuichangamkia promosheni Mshindi wa kwanza wa gari mpya kupitia promosheni ya ‘TBL Kumenoga, tukutane baa’, kupatikana wiki ijayo kupitia droo ya kwanza itakayofanyika jijini Dar es Salaam. 
 
Meneja wa Udhamini na Mawasiliano ya Wateja wa TBL, David Tarimo, amesema tangu promosheni hiyo izinduliwe mapema mwezi huu wateja wengi nchini kote wameendelea kuichangamkia “Wateja wetu wanaendelea kuchangamkia ‘TBL Kumenoga, Tukutane Baa’ huku wakijishindia zawadi mbalimbali. Natoa wito kwa wateja wetu wazidi kujitokeza kushiriki, ili kujipatia nafasi ya kuchukua gari mpya. Tumejipanga vyema ili kuwafikia wote nchi nzima. Tumewaletea wateja wetu promosheni hii kwa lengo la kuwashukuru kwa kuendelea kutuunga mkono na kila mwezi tutakuwa na zawadi ya gari jipya katika kipindi cha miezi 3”, alisema Tarimo.

Aliongeza kusema kuwa promosheni hii inafanyika kwenye mabaa katika siku za mwisho wa wiki yaani Ijumaa, Jumamosi na Jumapili nchini kote kupitia chapa za bia za Safari Lager, Kilimanjaro Lager, Castle Lite na Balimi Extra Lager. Kwa upande wake, Meneja wa Biashara na ukuzaji wa Masoko wa TBL, Edith Bebwa, alisema mbali na zawadi kubwa ya magari mapya zipo zawadi nyingi za kujishindia papo hapo kwenye promosheni ikiwemo bia za bure. Promosheni inafanyika katika mabaa zaidi ya 5,000 nchini kote. 
 
“Wateja wetu wazidi kuitafuta bendera ya TBL Kumenoga na promosheni zetu zote kwani ndipo wateja wa TBL wanapokutana na kupata nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali na hatimaye kuingia kwenye ndoo kubwa ya magari mapya. 
 
Alisema ili kuingia kwenye droo ya magari mapya ya ‘TBL Kumenoga, Tukutane Baa’ wateja wanatakiwa kununua bia tatu kati ya Safari Lager, Kilimanjaro Lager, Castle Lite au Balimi Extra Lager kwenye promosheni kisha watapatiwa kuponi yenye namba, watatuma namba hiyo kwa meseji kwenda 15451, hii ni kwa wale wenye mitandao ya VODACOM, TIGO na AIRTEL. Kwa wateja wa mitandao mingine watatuma namba iliyo kwenye kuponi kupitia tovuti ya http://www.tblkumenoga.co.tz.

TAKUKURU MKOANI ARUSHA YAOKOA ZAIDI YA MILIONI 11

$
0
0

 Na. Vero Ignatus, Arusha

Imeelezwa kuwa Taasisi ya kupambana na Rushwa mkoa wa Arusha imepokea jumla ya malalamiko 108 kwa njia mbalimbali ikiwa ni jitihada za kupambana na rushwa mkoani hapo.

Akitoa ripoti ya miezi mitatu ya kiutendaji Naibu mkuu wa Takukuru mkoa wa Arusha Frida Wikesi amesema taarifa hizo zimehusu halmashauri mbalimbali katika mkoa, idara ya ardhi, Nida, afya, kilimo, elimu, serikali za vijiji na mahakama

Amesema jumla ya majalada 23 ya uchunguzi yalifunguliwa na yanaendelea kuchunguzwa ambapo chunguzi hizo zipo katika hatua mbalimbali, haswa zilizo katika muelekeo wa makosa ya rushwa. Aidha amesema sheria ya kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007 inashauri, ushauri yakinifu kutolewa kwa watoa taarifa kwa malalamiko yanayoonekana kutokuangukia kwenye sheria hiyo.

'' Malalamiko mengi yanayowasilishwa yanahusiana na rushwa, aidha kwa kipindi tajwa jumla ya makosa mapya mawili (02)yamefikishwa mahakamani '' alisema.Hata hivyo amesema kuwa ofisi ya takukuru mkoa wa Arusha wamefanya dhibiti moja la rushwa, na kuendesha zoezi la ufuatiliaji wa kuziba mianya ya rushwa.

'' Hadi kufikia mwezi septemba 2018 jumla ya mashauri 18 yaliendelea kusikilizwa mahakamani ambayo yalikuwa katika hatua mbalimbali za mahakama"alisema Wikesi.Katika kipindi tajwa TAKUKURU iliweza kuokoa jumla ya fedha kiasi cha 11,345,000 ambazo zililipwa kwa watumishi waliokua wakishughulikia maonyesho ya 88 kanda ya kaskazini mwaka 2017(10,055,00) fedha zilizokuwa za ujenzi wa mahabara sekondari ya Ilkiding'a Arumeru sh 1,290,000 ambazo zilirejeshwa serikalini. 



SPIKA NDUGAI AONGOZA KIKAO CHA TUME YA UTUMISHI WA BUNGE NA WATUMISHI WA OFISI YA BUNGE

$
0
0
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia) akizungumza na Watumishi wa ofisi ya Bunge katika kikao cha pamoja kati ya Tume ya Utumishi wa Bunge na Watumishi wa ofisi ya Bunge kilichofanyika leo tarehe 31 Oktoba 2018 katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Kuanzia kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Ndg. Alois Makoi
 Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai (aliesimama) akizungumza na Watumishi wa ofisi ya Bunge (hawapo kwenye picha) katika kikao cha pamoja kati ya Tume ya Utumishi wa Bunge na Watumishi wa ofisi ya Bunge kilichofanyika leo tarehe 31 Oktoba 2018 katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Wa pili kushoto ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai, Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Ndg. Alois Makoi (kulia), Mwenyekiti wa Bunge, Mhe. Mussa Zungu (wa pili nyuma) na Mhe. Mary Chatanda (wa pili kulia nyuma)
 Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu, Ndg. Alois Makoi akizungumza na Watumishi wa ofisi ya Bunge katika kikao cha pamoja kati ya Tume ya Utumishi wa Bunge na Watumishi wa ofisi ya Bunge kilichofanyika leo tarehe 31 Oktoba 2018 katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. Katikati mbele ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai, Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (Kushoto mbele) na Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai (mbele kulia), Mwenyekiti wa Bunge na Mbunge wa Ilala, Mhe. Mussa Zungu (wa pili nyuma kushoto), Mbunge wa korogwe Mjini Mhe. Mary Chatanda (wa pili kulia nyuma) na Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Fakharia khamis
Watumishi wa ofisi ya Bunge wakifuatilia kikao cha pamoja na Tume ya Utumishi wa Bunge kilichofanyika leo tarehe 31 Oktoba 2018 katika ukumbi wa Pius Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

MHANDISI NDIKILO APONGEZA JITIHADA ZA TIC KATIKA KUKUZA,KUVUTIA UWEKEZAJI NCHINI

$
0
0
Na Ripota Wetu,Kibaha

MKUU wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ametembelea banda la Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) katika Maonesho ya wiki ya

Viwanda Mkoa wa Pwani ambapo ameipongeza TIC kwa jitihada zake katika kukuza na kuvutia uwekezaji nchini na namna inavyowahudumia wawekezaji kupitia huduma za mahala pamoja zinazotolewa na taasisi mbalimbali zilizopo ndani ya ofis za kituo hicho.

Akizungumza leo akiwa kwenye banda la TIC, Mhandisi Ndikilo amesisitiza ni ukweli kwamba Mkoa wa Pwani ni miongoni mwa mikoa inayopokea wawekezaji wengi na hivyo nguvu ya

kuwahudumia lazima iimarishwe. Aidha ameshauri TIC kuhakikisha inapata taarifa zote muhimu zinazohusiana na uwekezaji ndani ya mkoa wa Pwani kwa kuwasilian na ofisi za Halmashauri zote za Mkoa wa Pwani kwani kwa kufanya hivyo kutarahisisha uratibu na

huduma kwa wawekezaji nchini.

Baadhi ya tarifa alizosisitiza TIC iwe nazo ni pamoja na maeneo ya uwekezaji yaliyotyengwa, takwimu za miradi ya uwekezaji. Katika kuhakikisha kwamba Mkoa wa Pwani unaendelea kuvutia uwekezaji Mkuu wa Mkoa atawasilisha TIC maeneo ambayo tayari yametengwa kwa ajili ya uwekezaji ili yaweze kutafutiwa wawekezaji.

Akizungumza na Waandishi wa habari katika banda la TIC kwenye maonesho ya Wiki ya Viwanda Mkoa wa Pwani yanayoendelea katika viwanja vya Sabasaba vilivyopo Picha ya Ndege wilayani Kibaha mkoani Pwani, Meneja wa Kanda ya Mashariki Venance Mashiba .Amesema kuwa katika kuharakisha utatuzi wa changamoto zinazowakabili wawekezaji, Kituo cha Uwekezaji Tanzania TIC kimeunda Kamati Maalum ya kiaifa inayojumuisha Wakuu wa Taasisi za Serikali ambazo ni wadau katika kuhudumia uwekezaji.

"Kamati hii hukutana chini ya Mwenyekiti wa muda ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa TIC na kujadili changamoto mbalimbali za uwekezaji na kuzitafutia ufumbuzi. Kamati hii inakaa kila baada ya miezi mitatu inajadili changamoto mbalimbali ikiwa ni sehemu yake ya mpango kazi wa kuhakikisha huduma za wawekezaji zinaboreshwa,"amesema.

Ameongeza kuwa kamati hiyo ilianza kufanya kazi mwishoni mwa mwaka jana ikiwa na wajumbe wanaounda kituo cha huduma za mahala pamoja inayoundwa na taasisi 11 zikijumuisha Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni BRELA, Uhamiaji, Shirika la Viwango Tanzania TBS, Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania TFDA, Wizara ya Ardhi, Kazi na Ajira, Wakala wa Usalama mahala pa Kazi OSHA, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa NIDA na Shirika la Umeme Tanzania TANESCO na NEMC.


“TIC tunataka kuhakikisha wawekezaji wanapata urahisi wa kuendesha miradi yao hapa nchini ndio maana tunahakikisha kila mara tunaboresha mazingira ya uwekezaji, hatutaki Mwekezaji akija hapa ahangaike kutafuta vibali au leseni zinazohitajika, au achelewe kutatua changamoto zinazomkabili, kwa hiyo kamati hii lengo lake ni kuhakikisha tunaondoa changamoto zote kwa wakati,"amesema Mashiba.

Aidha Kituo kinawakaribisha watu wote, jumuia ya wafanyabiashara na wawekezaji wote kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kwenye maonesho haya ili wajionee bidhaa zinazozalishwa mko wa Pwani na huduma nyingine zinazotolewa na taasisi mbalimbali zinazoshiriki

maonesho haya. Maonesho hayo yaliyoanza Otoba 29 yanatarajia kumalizika Novemba 4, 2018.
 Baadhi ya wadau wa masuala ya viwanda wakiwa kwenye banda la Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) wakipata maelezo leo baada ya kutembelea maonesho ya viwanda mkoani Pwani
 Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akisaini kitabu cha wageni leo baada ya kufika kwenye banda la Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC). Anayeshuhudia ni Meneja wa TIC Kanda ya Mashariki Venance Mashiba
Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) Kanda ya Pwani Venance Mashiba leo kwenye Maonesho ya viwanda mkoani humo

MSAFARA WA WAZIRI LUGOLA WANUSURIKA KUGONGWA NA BASI LILILOKUA MWENDOKASI LIKIOVATEKI KATIKA KONA GAIRO, DEREVA AKAMATWA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kushoto) akimsikiliza Dereva wa Basi la Hekima za Mungu, Isaac Vian, alipomkimbilia Waziri huyo huku akimuomba msamaha mara baada ya kusimamishwa kutokana na kuendesha kwa mwendo kasi pamoja na kuovateki katika kona katika eneo nje kidogo na mji wa Gairo Mkoani Morogoro. Dereva wa Basi hilo lenye namba za usajili T140 AZZ lililokua linatoka jijini Dar es Salaam kuelekea Kahama Mkoani Shinyanga alielekezwa akaripoti kituo cha polisi mkoani Dodoma ili aweze kufunguliwa mashtaka.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akiangalia namba za usajili T140 AZZ la Basi la abiria la Hekima za Mungu lililokua linatoka Jijini Dar es Salaam kuelekea Kahama ambalo Waziri alilisimamisha kutokana na kosa la mwendokasi pamoja na kuovateki katika kona nje kidogo wa Mji wa Gairo Mkoani Morogoro.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na abiria wa basi la Hekima za Mungu baada ya Dereva wa Basi hilo, Issac Vian kuendesha kwa mwendokasi na kuovateki katika kona kali ambapo angeweza kusababisha ajali kwa kugongana na gari la Waziri Lugola, uso kwa uso Kijijini, nje kidogo na Mji wa Gairo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akishuka katika Basi la Hekima za Mungu mara baada ya kuzungumza na abiria na kuwataka kukemea mwendokasi pamoja na kuovateki katika kona alivyofanya dereva wa basi hilo, Isaac Vian (kushoto), nje kidogo ya mji wa Gairo, mkoani Morogoro, leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akimuonya Dereva wa Basi la Hekima za Mungu, Isaac Vian (kushoto), kwa kosa la kuendesha basi hilo kwa mwendokasi pamoja na kuovateki katika kona nje kidogo ya mji wa Gairo, mkoani Morogoro, leo. Hata hivyo Dereva huyo Waziri huyo alielekeza akamatwe kutokana na kosa hilo ambalo lingesababisha ajali. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.


Na Felix Mwagara, MOHA-Gairo.

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amenusirika kupata ajali wilayani Gairo, Mkoani Morogoro baada ya basi la Hekima za Mungu kuovateki katika kona wakati gari la waziri huyo likiwa eneo sahihi.

Tukio hilo lilitokea saa 6:04 mchana wakati Waziri huyo alipokua anatokea Mjini Dodoma kuelekea Jijini Dar es Salaam, katika eneo la nje kidogo ya Mji wa Gairo, basi hilo likiwa mwendokasi likiovateki katika kona, ndipo dereva wa gari la Waziri Lugola alipunguza spidi ili kuiepuka ajali hiyo.

Hata hivyo Basi hilo lilipopita, Waziri huyo aliekeza gari hilo lifuate kwa nyuma mpaka walikamate, hata hivyo Basi hilo lilikamatwa na dereva wa basi hilo kukaguliwa kama alikua na sifa ya kua dereva. Bara baada ya kumkagua dereva huyo, Waziri Lugola alizungumza na abiria wa basi hilo lenye namba za usajili T140 AZZ ambalo lilikua linatoka Dar es Salaam kuelekea Mjini Kahama mkoani Shinyanga.

“Kwanini mnashindwa kukemea hii tabia ya huyu dereva, mnataka awaue?, alitaka kusababisha ajali mbaya sana hapa, nanyi mmekaa kimya, mnafanya makosa kutokuripoti hii tabia mbaya kabisa,” alisema Lugola. Aliongeza kua, yeye ni Waziri ambaye anakemea mwendokasi na kiuwataka madereva nchini waendeshe kwa umakini, lakini dereva huyo anashindwa kufuata sheria za usalama barabarani, hivyo anapaswa kuchukuliwa hatua na iwe fundisho kwa madereva wenye tabia kama hiyo.

Licha ya Dereva wa Basi hilo, Isaac Vian alikiri kosa hilo na kuomba msamaha lakini Waziri Lugola aliekeza akamatwe lakini atakapofika mwisho wa safari.

BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO KUHAMASISHA UZALISHAJI WA MAZIWA

$
0
0

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kulia) akimkaribisha Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Prof. Philemon Wambura (kushoto) alipomtembelea Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine akizungumza na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Prof. Philemon Wambura (hayupo pichani) wakati walipokutana kuzungumzia nafasi ya TADB na NARCO katika kusaidia tasnia ya maziwa nchini.
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Prof. Philemon Wambura akizungumza wakati wa kikao hicho.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kulia) akizungumza na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Prof. Philemon Wambura (kushoto) wakihimiza jambo wakati wa kikao cha kujadili nafasi ya taasisi zao katika kuchagiza uzalishaji wa tasnia ya maziwa nchini.

…………………….

Katika kuhakikisha tasnia ya maziwa inawanufaisha wazalishaji wadogo wadogo wa maziwa nchini Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) ipo kwenye mikakati ya kuanzisha Jukwaa la Ushirikiano wa Tasnia ya Maziwa.

Akizungumza na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine alisema Benki ya Maendeleo ya Kilimo imejipanga kuhakikisha uzalishaji wa maziwa unaongezeka nchini ili kutoa fursa kwa wazalishaji wadogo kuweza kuchangia ukuaji wa tasnia hiyo.

Bw. Justine alisema kuwa shughuli za usindikaji wa maziwa zipo chini ya kiwango kwa viwanda vyote vinavyosindika maziwa nchini kutokana na uzalishaji duni wa maziwa hali inayorudisha nyuma ukuaji wa tasnia hiyo. “Fursa za kimasoko na uendelezaji wa tasnia ya maziwa ni kubwa hivyo tumejipanga kuhakikisha tunachagiza tasnia hii ili kuongeza uzalishaji na kuwaongezea kipato wazalishaji hasa wale wadogo wadogo,” alisema.

Aliongeza kuwa TADB imejipanga kuwakutanisha wadau wa tasnia ya maziwa ili kujadili kwa kina mipango ya muda mfupi, wa kati na mrefu ili kuja na mpango mkakati wa kuongeza uzalishaji wa maziwa nchini. Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Kampuni ya NARCO, Prof. Philemon Wambura alisema NARCO imejipanga kuwezesha wazalishaji wa wadogo kote nchini kwa kuwapatia huduma za ugani ili waweze kuongeza uzalishaji wa maziwa.

Prof. Wambura aliongeza kuwa mchango wa Benki ya Kilimo katika kuhakikisha tasnia ya maziwa inachangia shughuli za uzalishaji ni jambo la kuungwa mkono. “Mchango huu wa TADB utasaidia kuongeza uzalishaji hali itakayowaongezea kipato wazalishaji wadogo nchini na hivyo kutasaidia kuwaongezea kipato wafugaji wetu,” alisema.

Kwa mujibu wa twakwimu za Bodi ya Maziwa Tanzania, tasnia ya maziwa inachangia asilimia 3.9 ya GDP huku ikikadiriwa kuwa na ng’ombe wa maziwa zaidi ya milioni 1.1 kati ya jumla ya ng’ombe milioni 30.5.

SERIKALI YAANDAA MPANGO MKAKATI KUWANOA WASAIDIZI WA KISHERIA NCHINI

$
0
0
Baadhi ya washiriki wa Mafunzo Maalum ya Wawezeshaji watakaotoa mafunzo maalum kwa wasaidizi wa kisheria ili waweze kupata usajiri rasmi na wa kisheria wa kutoa huduma za kisheria kwa wananchi. Mafunzo hayo yameandaliwa na Law School of Tanzania (LST) na kufadhiliwa na Shirika la Legal Services Facility (LSF) yaliofanyika Dodoma jana.


SERIKALI imeandaa mpango mkakati wa kutoa mafunzo maalum kwa wasaidizi wa kisheria ikiwa ni njia ya kuboresha huduma za msaada wa kisheria kwa watanzania maskini wanaokabiliwa na matatizo mbalimbali ya kisheria nchini.

Mpango wa mafunzo maalum kwa wasaidizi wa kisheria nchini unatarajiwa kuanza mapema Novemba mwaka huu na walengwa wakuu ni wasaidizi wote wa kisheria ambao wanaotoa huduma za msaada wa
kisheria katika maeneo mbalimbali nchi nzima.

Katika sehemu ya maandalizi ya mafunzo hayo, Serikali kupitia ofisi ya Msajili wa Watoa Huduma za Kisheria –Wizara ya Katika na Sheria, imeendesha mafunzo yaliyolenga kupika wataalum (wawezeshaji) wapatao 40 kutoka mashirika mbalimbali ya huduma za kisheria) watakaoendesha mafunzo hayo maalamu kwa wasaidizi wa kisheria.

Mafunzo ya kupika wawezeshaji yamefanyika Dodoma na yaliandaliwa na Law School of Tanzania (LST) kwa kushirikiana na Tanzania Law Society (TLS) na kufadhiliwa na Shirika la Legal Services Facility (LSF)—taasisi inayofadhiliwa miradi/shughuli mbalimbali ya wasaidizi wa kisheria Tanzania Bara na Zanzibar.

Akizungumzia mafunzo hayo Mratibu wa Mafunzo ya Wawezeshaji Suleiman Pingoni amesema mafunzo hayo yanalenga kupika wataalam mahiri wakaoendesha mafunzo maalum kwa wasaidizi wa kisheria, yanayotajiriwa kuanza rasmi mapema Mwezi Novemba, na kumalizika kabla ya Disemba 31, Mwaka huu.

Mafunzo kwa wawezeshaji, kwa mujibu wa Bw.Pingoni, yalilenga kuwawezesha kupata ufahamu wa kutosha kuhusu maswala ya msingi kuhusu sheria ya Msaada wa Sheria (Legal Aid Act ) ya Mwaka 2017 na Kanuni zake, matakwa ya sheria kuhusu usajiri na usaili wa wasaidizi wa kisheria. Sheria ya Msaada wa Kisheria inawataka wasaidizi wa kisheria kupata mafunzo maalum ili waweze kusajiliwa na kupewa leseni za kutoa huduma za kisheria kwa wahitaji.

“Kimsingi, sheria ya Msaada wa Kisheria imewatambua wasaidizi wa kisheria na kazi wanazofanya hivi sasa. Hata hiyo, sheria hiyo hiyo, inawataka wasaidizi hawa wa kisheria kupata mafunzo maalum ili waweze  kupatiwa liseni/vitambulisho ili waruhusiwa kutoa huduma za kisheria,” amesisitiza Bw. Pingoni.Kwa mantiki hiyo, Ofisi ya Msajili wa Watoa Huduma za Kisheria ameandaa mafunzo kwa wawezeshaji

watakaotoa mafunzo maalum kwa wasaidizi wa kisheria, ili waweze kukidhi matakwa ya sheria.Ameeleza wasaidizi wa kisheria watakapata mafunzo hayo maalum watapatiwa vyeti, ambavyo vinawazesha kutuma maomba ya kusajiliwa na kutambuliwa kama wasaidizi wa kisheria kwa mujibu wa Sheria, na baada kupatiwa vitambulisho maalum.

“Lengo kuu la michakato hii yote ni kupata wasaidizi wa kisheria mahiri na wenye uwezo, ambao wanafanya kazi zao kwa mujibu wa sheria, wakaoweza kutoa huduma bora na zenye viwango kwa wananchi, amesema Bw.Pingoni.Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mradi-LSF Scholastica Jullu ameelezea mafunzo maalum kwa wasaidizi wa kisheria kama “hatua kubwa katika jitiada za serikali na wadau wa huduma za kisheria zinazolenga kupanua wigo wa huduma za msaada wa kisheria na kuwezesha watu maskini, wanaodhulimiwa na kunyanyaswa kupigania na kupata haki zao.”



MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI YAPEWA SIKU 14 ZAIDI KUWASILISHA TAARIFA ZA MIRADI NA MATUMIZI YA FEDHA ZA MWAKA 2016 NA 2017

$
0
0
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto( Idara kuu ya Maendeleo ya jamii) Dkt. John Jingu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu nyongeza ya siku 14 zaidi zilizotolewa kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuhakikisha yanawasilisha taarifa za miradi na za fedha za mwaka 2016 na 2017 kwa Msajili wa Mashirika hayo kabla ya kufutiwa usajili wao. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW
Baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (Idara kuu ya Maendeleo ya jamii) wakifuatilia tamko la Katibu Mkuu Dkt. John Jingu la kuongeza siku 14 zaidi kwa Mashirika ya Yasiyo ya Kiserikali kuhakikisha yanawasilisha taarifa za miradi na za fedha zilizokaguliwa za mwaka 2016 na 2017 kwa Msajili wa Mashirika hayo kabla ya kufutiwa usajili wao. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.
Katibu Mkuu wa Braza la NGOs nchini Bw. Ismail A. Suleiman akieleza kuridhishwa kwake na kanuni mpya za NGOs (2018) ambazo zimezingatia matakwa ya kanuni za maadili katika kuboresha utendaji wa NGOs wakati wa kikao cha Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii kilichoeleza kuongeza siku 14 zaidi kwa Mashirika hayo kuwasilisha taarifa za miradi na fedha kwa Msajili wa NGOs. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW.


Na Mwandishi Wetu Dodoma.

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa siku kumi nne zaidi (14) kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuhakikisha yanawasilisha taarifa za miradi na za fedha za mwaka 2016 na 2017 zilizokaguliwa kwa Msajili wa Mashirika hayo kabla ya kufutiwa usajili wao.

Tamko hilo limetolewa leo jijini Dodoma na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto- Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii Dkt. John Jingu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa agizo la Serikali lililotolewa kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.
Ufafanuzi ulitolewa kuwa, “Siku ya tarehe 28 Septemba, 2018, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile alikutana na wawakilishi wa vyombo vya habari na kutoa maagizo yakuyataka Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kuwasilisha taalifa zao kwa Mashirika hayo ikiwa ni pamoja na taarifa za miradi na taarifa za fedha zilizo kaguliwa kwa mwaka 2017 na 2018”, alibainisha DKT. Jingu.

Dkt Jingu amefafanua kuwa, maagizo hayo yalipaswa kutekelezwa ndani ya siku thelathini (30) kuanzia tarehe 28.9.2018 ya agizo lilipotolewa na Serikali. Hata hivyo imeelezwa kuwa mwitikio wa utekelezaji umekuwa wa kuridhisha kutokana na ukweli kuwa Mashirika mengi yamezingatia maelekezo ya Serikali.

Aidha, Wizara imepokea maombi kutoka Ofisi ya Baraza la Taifa la NGOs na baadhi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wakiomba kuongezwa muda kidogo ili waweze kukamilisha maandalizi ya taarifa zao na kuziwasilisha haraka. Kutokana na kutambua nafasi ya NGOs katika maendeleo ya Taifa, Serikali imeridhia kuongeza siku kumi na nne (14) kuanzia leo (31/10/2018) ili kuwapa fursa wale ambao walikuwa bado hawajatimiza maelekezo hayo kutokana na sababu mbalimbali kufanya hivyo. “Nasisitiza kuwa hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza kwa wale ambao hawatakuwa wamewasilisha taarifa hizo ndani ya muda wa nyongeza. Shirika ambalo litakuwa halijawasilisha taarifa Wizara itachukua hatua stahiki kwa mujibu wa Sheria”. alisisitiza Dkt. Jingu.

Katibu Mkuu huyo amerudia kuhakikishia umma kuwa, Serikali inatambua na kuthamini mchango wa NGOs kwa maendeleo ya nchi. Msisitizo wa Serikali wa uwazi na uwajibikaji unalenga kuwezesha Serikali, wananchi na wadau wa maendeleo kutambua vizuri zaidi mchango wa NGOs katika shughuli za maendeleo. Pia kama ilivyo kwenye sekta nyingine, uwazi na uwajibikaji utasaidia kuzuia matumizi mabaya ya rasilimali zinazotolewa na wadau wa maendeleo kupitia Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ili kuwa kichocheo katika kufikia azma ya maendeleo jumuishi.

Akizungumza katika Mkutano huo, katibu Mkuu wa Braza la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Ismail A. Suleiman ameishukuru Serikali kwa kuridhia ombi nyenyekevu la kuongeza muda wa kuwasilisha taarifa za fedha na miradi ili kuwezesha NGOs kutimiza takwa la agizo hio. Bw. Ismail amebainisha kuwa kanuni mpya za NGOs (2018) zilizotangazwa tarehe 19/10/2018 kwa kiasi kikubwa zimezingatia utekelezaji wa kanunni za maadili; hivyo Braza la NGOs litaunda kikosi kazi kuzipitia na kutoa maoni kwa lengo la kuboresha utendaji wa NGOs kwa mujibu wa matakwa ya kisheria, kanuni na taratibu.

Baraza la NGOs limewataka wanachama wake wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kuhakikisha kuwa wanatekeleza kazi zao kwa mujibu wa katiba za mashirka yao ili kushirikiana na Serikali katika kuchochea ustawi na maendeleo ya watu hususan kunufaisha makundi yote ya kijamii.

Maagizo haya kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yanakuja mwezi mmoja baada ya AGIZO LA Serikali kutolewa likizitaka NGOs zote nchini pamoja na mambo mengine kuwasilisha taarifa zao za kazi na matumizi ya fedha ya miradi wanayoitekeleza. Imeelezwa kuwa hadi taarifa hii inatolewa zaidi ya Mashirika 2000 yamewasilisha taarifa zao na wengi wanaendelea kuitiki maelekezo hayo.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI NOVEMBA 1,2018


DC MURO ASHIRIKI UJENZI WA SHULE MPYA YA SEKONDARI YA LOSIKO PAMOJA NA WANANCHI KIJIJI CHA LOSIKITO

$
0
0

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe Jerry Muro jana ameungana na wananchi wa kijiji cha LOSIKITO kata ya Mwandeti Halmashauri ya Arusha katika ujenzi wa shule Mpya ya sekondari ya losiko ambayo inajengwa Kwa nguvu za wananchi.
 
Dc Muro ameamua kuungana na wananchi katika kuhakikisha shule hiyo inaanza kutumika Mwaka 2019 Kwa lengo la kupunguza uhaba wa shule na vyumba vya madarasa Kutokana na ongezeko Kubwa la wananchi waliofaulu Elimu ya Msingi ambao wanapaswa kuingia Kidato Cha kwanza Mwaka 2019.
Dc Muro anaendelea na ziara yake katika kata ya mwandeti iliyo halmashauri ya Wilaya ya ARUSHA
2
Dc Muro akiungana na Wananchi kushiriki ujenzi kuhakikisha shule hiyo inaanza kutumika Mwaka 2019 Kwa lengo la kupunguza uhaba wa shule na vyumba vya madarasa Kutokana na ongezeko Kubwa la wananchi waliofaulu Elimu ya Msingi ambao wanapaswa kuingia Kidato Cha kwanza Mwaka 2019.
index
Dc Muro akishiriki ujenzi wa shule  mpya ya sekondari ya Losiko katika kijiji ch Losiko,wilayani Arumeru,ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa ziara yake iliyoanza jana katika kata ya mwandeti,katika halmashauri ya Wilaya ya Arusha ambapo Mkuu huyo wa Wilaya anatarajiwa kutembelea Kata zote 53 za Wilaya ya Arumeru.
1
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro akifafanua jambo mbele ya baadhi wa viongozi aliombatana nao alipokwenda kuungana na wananchi wa kijiji cha LOSIKITO kata ya Mwandeti Halmashauri ya Arusha katika ujenzi wa shule Mpya ya sekondari ya losiko ambayo inajengwa Kwa nguvu za wananchi.
3

TCRA YAWATIA KIBANONI WANANE WANAODAIWA KUKIUKA SHERIA ZA MTANDAO KUANZIA JULY -SEPT

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imeshawachukulia hatua za kisheria watu nane wanaodaiwa kukiuka sheria za mtandao, ikiwemo kusambaza picha za nusu uchi, video za ngono na kutupia matusi katika kipindi cha July -Septemba mwaka huu. 

Aidha jamii imekemea matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na video za ngono kwani kwa kufanya hivyo hawatamuangalia mtu kwa sura ama umaarufu bali sheria itachukua mkondo wake. Ofisa mkuu wa mawasiliano kwa umma (TCRA) Semu Mwakyanjala aliwatahadharisha ,watu wasisambaze picha ama video za ngono na kuanzisha tovuti hizo kwani ni kukiuka sheria .

Alieleza kuna faida unapotumia mtandao inarahisisha mawasiliano ,unapunguza gharama ,inaokoa muda ,inatoa elimu na kukuza biashara badala ya kutumia masuala yasiyo na tija.“Kwasasa hatuna masihala, tunashirikiana na jeshi la polisi kubaini wale wanaokaidi kufuata sheria zilizopo “alieleza Mwakyanjala. Aliiomba jamii kutunza vifaa vya kielektronik ili watu waeiibe na kutymia vibaya .

Nae mkuu wa kanda ya Mashariki (TCRA) Lawi Odiero alisema, sheria ya kielektroniki iliyopo inakataza kusambaza ngono na baadhi ya watu wanachukuliwa hatua ya kulipa faini sh. mil tano ama miaka mitatu jela.

Aliwaasa wananchi kwenda kutembelea banda lao kujifunza ili kuelewa sheria zinazowabana ili kuepukana na adhabu. Odiero alieleza wazingatie wasiweke namba za siri kwenye simu ama internet miaka ya kuzaliwa bali watumie maneno mengine kwani sio rahisi kughushi .Akizungumzia ving’amuzi alisema ,serikali kupitia TCRA iliondoa baadhi ya channel kwenye baadhi ya visimbuzi. 

Odiero alifafanua, Azam, Dstv na Zuku huduma wanatoa kwa kulipisha hivyo hawaruhusiwi kubeba channel za ndani. Watumiaji wa internet hadi sasa nchini wapo milioni 22 ,luninga zipo 34 ,vituo vya redio zaidi ya 150 kutoka kituo kimoja kilichokuwepo mwaka 1961.
Mkuu wa kanda ya Mashariki (TCRA) Lawi Odiero akizungumza.kwenye maonyesho hayo

TPDC KUONGEZA VITUO VYA KUJAZA GESI ASILIA KATIKA MAGARI-MUSOMBA

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli nchini ( TPDC), linatarajia kuongeza vituo 10 hadi 20 kwa Dar es salaam -Mtwara -Lindi, vya kujaza gesi asilia kwenye magari yaliyowekewa mfumo huo ambapo kipo kituo kimoja Ubungo ,kwa miaka kumi sasa ambacho hakikidhi mahitaji. 

Ili kufikia malengo yake ya kuongeza vituo vingi katika maeneo mbalimbali limejipanga kuruhusu na kukubaliana na watu binafsi wenye vituo vya mafuta kuweka gesi kwenye vituo vyao .

Akitembelea maonyesho ya bidhaa za viwandani yanayoendelea viwanja vya sabasaba, Pichandege Kibaha Pwani, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini ( TPDC), Kapuulya Musomba, alisema mwamko wa watumiaji upo vizuri tatizo hakuna vituo mikoani. 

Alieleza mwaka ujao wa fedha wataongeza vituo hivyo na sasa wapo kwenye hatua ya manunuzi. Musomba alisema ,wataanza kuongeza vituo viwili ama vitatu Dar es salaam na kuendelea maeneo mengine, na kusema watatangaza tenda ili wawekezaji na watu binafsi wajitokeze kufanikisha hilo. 

"Gesi asilia ikitumika kwenye magari inaweza kupunguza zaidi ya nusu ya gharama mafuta na kuleta unafuu katika sekta ya usafirishaji nchini,Hata hivyo alitaja mpango mwingine ni kuwafikia wananchi 120,000 ambao watafaidika na raslimali ya gesi lakini wanakwenda kwa awamu kulingana na fedha wanayoipata. 

"Gesi kwa ajili ya majumbani tumeanza Dar es salaam na Mtwara, na kuhusu viwandani tumeshaanza Pwani, Dar es salaam na Mtwara kwa njia ya mabomba "Musomba alielezea,mwaka huu wa fedha kufikia 2019 watapeleka Kibaha kwa mitungi kwa kuwa mabomba hayajafika kwa kujazia Dar es salaam kisha kuwafikishia wananchi. 

Alifafanua kwa wale wa mikoa mingine wameshaanza utafiti wa kina kuona kama watoa bomba Dar es salaam, Kibaha, Bagamoyo, Chalinze, Tanga litembee kwenye mikoa kama nane na kwa kushirikiana na wadau watafikia lengo hilo. Nae Mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo alisema ,wakati ujenzi wa bandari mpya Bagamoyo ukianza watahitaji gesi kutokana na ujenzi kuambatana na viwanda vingi. 

Ndikilo alibainisha awamu ya kwanza ya ujenzi huo utaendana na ujenzi wa viwanda 190 ambapo awamu ya pili utakuwa na takriban viwanda 1,000 hivyo gesi itahitajika pia. 
Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli nchini ( TPDC),  Kapuulya Musomba, (wa kwanza kulia) akieleza jambo. (picha na Mwamvua Mwinyi)

EALA SWEARS IN NEW EX-OFFICIOMEMBER

$
0
0
The Deputy Minister for Foreign Affairs and EAC, United Republic of Tanzania, Hon Dr Damas D. Ndumbaro takes the oath of allegiance to the House, flanked in background by Hon Dr Ngwaru Maghembe and Hon Simon Mbugua (right) .


The EALA Speaker, Rt Hon Ngoga Karoli Martin congratulates Dr Damas Ndumbaro, who joins the bench as an ex-officio Member of EALA
A Section of the House pay attention as EALA proceedings continue







The Deputy Minister for Foreign Affairs and EAC, United Republic of Tanzania, Hon Dr Damas D. Ndumbaro (left) is led to the House by Hon Dr Ngwaru Maghembe, Hon Pamela Massaay and Hon Simon Mbugua(partially hidden)
……………………..

East African Legislative Assembly, Arusha, Tanzania:

The new Deputy Minister for Foreign Affairs and East African Co-operation, United Republic of Tanzania, Hon Dr Damas Ndumbaro, this afternoon took Oath of Allegiance as an Ex-OfficioMember of the Assembly.

Hon Dr Ndumbaro was sworn in by the Clerk to the Assembly at a brief ceremony witnessed by the Speaker and Members of EALA in line with the Rule 5 of the Rules and Procedures of the Assembly. The Rule 5(4) of the Rules of Procedure says in part that: “No Member can sit or participate in the proceedings of the House until the Oath or Affirmation of Allegiance to the Treaty is taken”.

Rule 5(5) specifically states that “when a Member first attends to take his or her seat other than at the first Sitting of a new House, he or she shall be brought to the table by two Members and presented by them to the Speaker who shall then administer the Oath or Affirmation of Allegiance”.

Hon Dr Ndumbaro was ushered in to the House by EALA Members, Hon Simon Mbugua, Hon Pamela Massaay and Hon Dr Ngwaru Maghembe. EALA Speaker, Rt Hon Ngoga Karoli Martin congratulated Hon Dr Ndumbaro upon his swearing in – as he assumes his ex-officio role in the regional August House.

Hon Dr Ndumbaro was appointed to Cabinet by H.E. John Pombe Joseph Magufuli in September 2018 replacing Hon Dr Susan A. Kolimba who was dropped. The new Deputy Minister will serve in the Foreign Affairs and EAC Co-operation ministry position under Amb Dr Augustine Mahiga.

Prior to the appointment as Deputy Minister for State, East African Affairs, Hon. Dr Ndumbaro was and still is Member of Parliament for Songea Urban Constituency in Ruvuma region, United Republic of Tanzania. Hon Dr Ndumbaro, a lawyer by training is an advocate of the High Court of Tanzania and Zanzibar. He is a registered Arbitrator at the Tanzania Institute of Arbitration.

Between 2016 and 2017, Hon Dr Ndumbaro was Dean of Faulty at the Open University of Tanzania. The new Deputy Minister also served as Senior Legal Counsel, Corporate Secretary and Deputy Managing Director at the Tanzania-Zambia Railway Authority (TAZARA). His work career started at the Air Tanzania Holding Corporation where he was Legal Consultant for 3 years (2003-2006).

Hon Dr Ndumbaro holds a Doctor of Philosophy in Law obtained from the Open University of Tanzania, a Masters of Law and a Bachelor of Law, both obtained from the University of Dar es Salaam.

MKUTANO WA MAJAJI WAKUU NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA WAFANYIKA MJINI LILONGWE NCHINI MALAWI

$
0
0
Pichani kulia ni Mheshimiwa Jaji Mkuu Prof Ibrahim Hamis Juma akiwa sambamba na Mheshimiwa Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Othman Chande (kushoto) walipokwenda kumtembelea mheshimiwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi Ben Mashiba nyumbani kwake jana jijini Blantyre,nchini Malawi.
Majaji wakuu nchi za kusini mwa Afrika wakiwa katika picha ya pamoja,wakati wa Mkutano wao Mjini Lilongwe nchini Malawi
Viewing all 46334 articles
Browse latest View live




Latest Images