Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46384 articles
Browse latest View live

Marais Kenyatta, Akufo-Addo watoa somo kwa vijana Afrika

$
0
0
Na MWANDISHI WETU

-Lagos, Nigeria

MARAIS Uhuru Kenyatta wa Kenya na Nana Akufo-Addo wa Ghana wamewataka vijana Bara la Afrika kuwa wabunifu na kumchangamkia fursa za kiuchumi ili kuiweza kusaidia nchini zao.

Kauli hizo wametoa hivi karibuni jijini Lagos nchini Nigeria kwenye jukwaa la nne la kila mwaka lililoandaliwa na Taasisi ya Tony maarufu Tony Elumelu Foundation (TEF), Entrepeneurship Forum.

Rais Uhuru Kenyatta, aliwahimiza vijana kutoka bara la Afrika kutumia ubunifu wao ili kuleta mabadiliko.“Viongozi vijana wabunifu kutoka Afrika wanapigana na mabadiliko yenye nia njema kwa kutumia teknolojia. Kuwa bora iwezekanavyo kwa familia, jamii, taifa yako lakini muhimu wewe mwenyewe,” amesema 

Rais Uhuru alisisitiza ushauri wake kwa vijana kufanya kazi ili kuwa bora kwa taaluma ambayo wamechagua.Tukio hilo ni fursa pekee ya kukusanya vipaji vya biashara kwa vijana, kujenga mitandao yenye nguvu na kupeleka ujumbe kwa watunga sera kwamba sekta binafsi iliyo mahiri na inawajibika inauwezo wa kuleta mabadiliko ya kiuchumi.

Baada ya kupata mafunzo ya miezi tisa, ushauri na ufadhili, jumla ya vijana 4,470 walifaidika na programu hiyo iliyoshuhudia zaidi ya vijana laki tatu wakituma maombi. Mwasisi wa jukwaa hilo, Tony Elumelu, alisisitiza kuendelea kujitolea kuhakikisha maendeleo ya uchumi Afrika kwa kusaidia mafunzo ya kizazi kipya cha wajasiriamali ambao mafanikio yao yanaweza yakabadili bara hili ikwemo kutengeneza ajira. 

“Ujasiriamali ni muhimu kufungua maendeleo ya uchumi katika bara letu. Naamini kwa dhati mafanikio yanaweza yakaleta demokrasia na kama tunaweza kubadili tamaa na kuwa fursa, hiki kizazi cha ajabu kinaweza kufanikiwa kwa kila jambo,” alisema Tony Elumelu.Naye Rais wa Ghana, Nana Akudo-Addo, aliwasisitizia wawakilishi wa sekta ya umma kuhimiza, kusaidia na kuiga kazi inayofanywa na Taasisi ya Tony Elumelu.“Hakuna kinachobadilika au kujiendeleza kivyake. Watu lazima waamke, waonge, wajadili na kubadilisha mada,” alisema Rais Nana Akufo-Addo.

Tangu kuanzishwa kwa taasisi hiyo, imeweza kuwasaidia wajasiriamali Waafrika kutoka pembe zote za Bara la Afrika na washindi katika mashindano mbalimbali katika jukwaa la mwaka huu walipata ufadhili wa dola za Marekani 5000 (takribani Shilingi milioni 11.4 kila mmoja). 
Mwasisi wa jukwaa hilo, Tony Elumelu (kushoto), akiwa na Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, kwenye jukwaa la TEF wakichambua kuhusu hali uchumi na umuhimu wa vijana Afrika kuwa wabunifu jijini Lagos, Nigeria
Mwasisi wa jukwaa hilo, Tony Elumelu (kushoto), akiwa na Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, wakiwa na kijana mshiriki wa kongamano kutoka nchini Ghana baada ya kijana huyu kutaka ufafanuzi kwa Rais wake wa namna vijana wanavyopewa kipaumbele katika ujenzi wa uchumi wa nchi hiyo.
Mwasisi wa jukwaa hilo, Tony Elumelu, akiwa na Rais wa Ghana, Nana Akufo-Addo, wakiwa watendaji wa Taasisi wa Tony Emelu Foundation wakati wa uzinduzi wa tovuti ya taasisi hiyo jijini Lagos, Nigeria
Baadhi ya waandishi wa habari kutoka nchi za Afrika wakiwa kwenye majadiliano wa maofisa Uhusiano wa Benki za UBA, jijini Lagos
Mshiriki wa kutoka Tanzania, Kinshaga akionesha bidhaa kwa washiriki wa jukwaa la TEF jijini Lagos, Nigeria

MAKAMU WA RAIS AENDELEA NA ZIARA WILAYANI KISARAWE

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimu wananchi mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara za lami Kisarawe mjini, Makamu wa Rais yupo wilayani Kisarawe ikiwa sehemu ya ziara yake ya siku sita ya kukagua na kuhamasisha shughuli za kimaendeleo mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Kisarawe ,Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais  TAMISEMI Mhe. Selemeni Jafo mara baada ya kukagua ujenzi wa mradi wa tenki la maji litakalokuwa na uwezo wa kubeba lita milioni 6 katika eneo la Mnarani Kisarawe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

PANGANI WAJIWEKA TAYARI KWA ZIARA YA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA.

$
0
0

MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Pangani Seif Ally akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kulia ni Katibu wa CCM wilaya ya Pangani
Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani (DAS) Hassani Nyange akizungumza katika kikao hicho
Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gibson George akizungumza katika kikao hicho Sehemu ya wajumbe wa kikao hicho


NA MWANDISHI WETU,PANGANI.

MKUU wa wilaya ya Pangani mkoani Tanga Zainabu Abdallah amewataka viongozi na wananchi wa wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kwenye mapokezi ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anayetarajiwa kuanza ziara wilayani humo Octoba 29 mwaka huu.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya Habari Mkuu wa wilaya hiyo mara baada ya kumalizika kikao cha maandalizi ya ziara hiyo aliwataka wananchi hao wakiwemo viongozi kujitokeza kwa wingi eneo la Mkwaja kwenye mapokezi hayo.

Alisema baada ya mapokezi hayo Waziri Mkuu anatarajiwa kuzungumza na wananchi kwenye maeneo ya Sakura,Mwera na Bomani Pangani mjini huku wananchi wakitakiwa kujumuika kwenye mikutano hiyo kwa wingi.

Hata hivyo aliwataka wananchio kutumia fursa hiyo kwenda kumsikiliza Waziri Mkuu na kuwasihi wale watakaopata nafasi endapo itatolewa kuitumia kusema kwa niaba ya wana Pangani wengi na kueleza changamoto zao na kuzungumza na kiongozi wao aliekuja kwa ajili yao.

Katika hatua nyengine Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Abdallah kwenye muendelezo wa tamaduni ya ushirikiano na mshikamano wa viongozi katika wilaya ya Pangani amekutanisha pamoja viongozi wote kwa kushirikisha Kamati ya ulinzi na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya,Halmashauri ya Wilaya ikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Seif Ally,Mkurugenzi na wakuu wote wa Idara,Taasisi zote,Ofisi ya Mbunge,Kamati ya siasa ya chama Tawala(CCM),Madiwani wote,NGO’s,Viongozi wa Dini na viongozi wengine wote.

Lengo ni kuunganisha nguvu ya pamoja na kujiweka tayari kupokea ugeni mkubwa na wa heshima unaotarajiwa kutua wilayani hapa October 29 mwaka huu siku ya Jumatatu.
.

Bodi ya wadhamini ya NSSF yatakiwa kuweka mifumo bora ya kielektroniki ili kudhibiti mapato.

KAMPUNI YA CRJE YA CHINA YAUNGA MKONO JUHUDI ZA RC MAKONDA KWA KUJENGA OFISI MBILI ZA WALIMU

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda jana amezindua ujenzi wa Ofisi moja Kati ya ofisi mbili za kisasa katika shule ya msingi Vijibweni katika Manispaa ya Kigamboni ikiwa ni ahadi alizoahidiwa na Kampuni ya Ujenzi ya CRJE iliyoguswa na Kampeni ya Makonda ya Ujenzi wa Ofisi 402 za walimu katika jiji la Dar es salaam.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika shule ya msingi Vijibweni ambako ni moja ya shule ambayo ofisi za walimu zitajengwa Makonda amesema kuwa moja kati ya vitu vinavyomnyima usingizi ni kuona walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu ikiwemo kufanya kazi chini ya miti na kwenye korido na lengo la kuanzisha kampeni hiyo ni kuhakikisha thamani walimu inarejea.

Aidha Makonda amesema uwepo wa mazingira bora ya kufanyia kazi kwa walimu Ndio chachu ya kuongezeka kwa ufaulu ambapo amewapongeza walimu na watendaji wa elimu kwa kuifanya Dar es salaam kuongoza kitaifa katika matokeo ya mtihani wa Darasa la Saba.Pia Makonda amesema kuwa ofisi hizo zitakuwa na mahitaji yote muhimu ikiwemo ofisi ya mwalimu mkuu, mwalimu mkuu msaidizi, ukumbi wa mikutano, ofisi ya walimu wote, chumba cha mitihani, chumba cha mhasibu, mapokezi, stoo, Vyoo na Bafu.

Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Sarah Msafiri amesema kuwa kama watendaji wataendelea kuunga mkono jitihada za Mh. Rais na Mkuu wa Mkoa katika suala zima la elimu ili kuhakikisha watoto wanapata elimu iliyo bora na walimu wanafanya kazi zao katika mazingira ya kuridhisha.Diwani wa kata ya Vijibweni na Mstahiki Meya wa jiji la Dar es salaam Isaya Mwita amesema kuwa anashukuru kwa kufanya kazi na viongozi kwa ushirikiano bila kujali itikadi za vyama.

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi Vijibweni amemueleza Mkuu wa Mkoa kuwa shule hiyo haina ofisi yoyote ya walimu hivyo wamekuwa wakifanyia kazi chini ya miti na kwenye korido ambapo wamemshukuru kwa kuwaletea mfadhili wa kuwajengea ofisi ya kisasa.
Wanafunzi wa Shule ya msingi vijibweni waliohudhuria katika uzinduzi wa ujenzi wa ofisi mbili za walimu za kisasa jana jijini Dar es Salaam.
RC Makonda akiwa ameongozana na baadhi ya viongozi wa maispaa ya Kigamboni akikagua madarasa ya wanafunzi wa Shule ya msingi ya vijibweni katika uzinduzi wa ujenzi wa ofisi za walimu ikiwa ni muendelezo wa ilani yake kujenga ofisi hizo 402 hapa Jijini Dar es Salaam.
RC Makonda akiwapungia wanafunzi mkono wa kwaheri Mara baada ya zoezi la uzinduzi wa ujenzi wa ofisi kumalizika jana  Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza jana na wageni waaliohudhuria wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa ofisi mbili za kisasa za walimu wa Shule ya msingi ya vijibweni iliyopo katika manispaa ya Halmashauri ya Kigamboni Jijini Dar es Salaam akitimiza ahadi aliloahidiwa na kampuni ya ujenzi ya CRJE kutoka nchini China iliyoguswa na kampeni ya RC Makonda ya kujenga ofisi 402 za walimu.

Mtanzania Rebeca Gyumi aibuka kidedea tuzo ya haki za binadamu ya UN

$
0
0
Rebeca Gyumi, mwanaharakati wa haki za wanawake na wasichana nchini Tanzania pamoja na watu wengine wawili na shirika moja la kiraia, wameshinda tuzo ya mwaka huu ya haki za binadamu

Washindi hao wametangazwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Maria Fernanda Espinosa ambaye kupitia ukurasa wake wa Twitter amewapongeza kwa mchango wao wa kusongesha mbele haki za binadamu. 

Hii ni tuzo ya 10 ambayo mwaka huu inaendana na miaka 70 ya tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa ambapo washindi hao watapokea tuzo hizo tarehe 10 mwezi disemba mwaka huu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani. 

Taarifa ya ofisi ya Kamishna wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa imefafanua kazi za washindi hao akitolea mfano Rebeca Gyumi. 

Bi. Gyumim muasisi na mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya Msichana Initiative nchini Tanzania, kwa miaka 8 amekuwa akihoji uhalali wa ibara ya 13 na 17 ya sheria ya ndoa yam waka 1971 nchini Tanzania ambayo inahurusu mtoto wa kike kuolewa akiwa na umri wa miaka 14 na 15 kwa ridhaa ya wazazi au mahakama. 

Taarifa hiyo inasema “Bi. Gyumi alishinda kesi hiyo mbele ya Mahakama Kuu ya Tanzaina mwaka 2016.” Mshindi mwingine ni Asma Jahangir mwanaharakati mwanasheria wa Pakistani ambaye amefariki dunia mwaka huu. 

Marehemu Jahangir kwa miongo mitatu amekuwa akitetea haki za wanawake, wasichana, watoto na makundi madogo ya kidini na maskini nchini mwake ambapo alifungua kituo cha msaada wa sheria. Ingawa hivyo alikuwa akikumbwa na misukosuko lakini alikuwa na uwezo wa kushinda kesi zilizokuwa na utata. 

Kwa upande wake, mshindi mwingine Joênia Wapichana au Joênia Batista de Carvalho, mwanaharakati wa haki za watu wa jamii ya asili nchini Brazil, ni mwanamke wa kwanza wa jamii hiyo kuwa mwanasheria. “Baada ya kuwasilisha mbele ya tume ya haki za binadamu ya nchi za Amerika, Bi. Wapichana alikuwa mwanasheria wa kwanza wa jamii ya asili kuingia Mahakama Kuu ya Brazil. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA >>>>>>

TANGAZO KUHUSU MAHAFALI YA 12 CHUO KIKUU CHA ARDHI

WAKAAZI WA MWANZA WAPATA VIBE LA TIGO FIESTA

$
0
0
 
 Mshindi wa Tigo Fiesta Supa Nyota mkoa wa Mwanza 2018, Elisayo akiwa kwenye jukwaa la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jana  uwanja wa CCM Kirumba
 
 Msanii anayechipukia, Jollie akiwa kwenye steji ya Tigo Fiesta Vibe Kama Lote usiku wa kuamkia jana uwanja wa CCM Kirumba

 Msanii Nandy akitumbuiza kwenye steji ya Tigo Fiesta Vibe Kama Lote usiku wa kuamkia jana uwanja wa CCM Kirumba
  Msanii Nedy na skwadi lake  akitumbuiza kwenye steji ya Tigo Fiesta Vibe Kama Lote usiku wa kuamkia jana uwanja wa CCM Kirumba

  Kundi la Weusi lilkipagawasha mashabiki kwenye Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote lililofanyika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza usiku wa kuamkia jana.

 
 Kundi la Weusi lilkipagawasha mashabiki kwenye Tamasha la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote lililofanyika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza usiku wa kuamkia jana.

Wakaazi wa jiji la Mwanza na Vitongoji vyake usiku wa kuamkia jana waliweza kukonga mioyo yao kwa burudani kabambe kwenye Tamasha kubwa nchini la Tigo Fiesta Vibe Kama Lote lililofanyika uwanja wa CCM Kirumba.
Wasanii mbalimbali wakiwemo Weusi, Rostam, Country Boy, Nandy, Fid Q, Richie Mavoko, Jux,WhoZu Nedy Music na wengine wengi waliweza kufanya kile mashabiki walikuwa wanatarajia.

Mwamba wa kanda ya Ziwa Fareed Kubanda maarufu kama Fid Q aliwateka vilivyo wanamwanza hasa kwa wimbo wake FRESH, Fid Q ambaye ni mwenyeji wa Mwanza ilimbidi arudie wimbo huo pendwa mbele ya mashabiki.Vibe la Tigo Fiesta liliamshwa zaidi na kundi la Weusi lililowajumuisha Joh Makini, Nikki wa Pili , Lord Eyez na G Nako walioweza kukaa jukwaani kwa muda mrefu bila kuchosha mashabiki kwa nyimbo lukuki zikiwemo SWAGIRE,NiCome na kadhalika.

Nae Msanii anayeng’ara kwa sasa, WhoZu aliweza kuwakamata mashabiki kwa wimbo wake HUENDI MBINGUNI amabo ameupiga kwa mahadhi ya Reggae. Kwa upande wa kundi la Rostam linalowajumuisha Roma na Stamina kama kawaida yao wao ndio wanaofunga jukwaa, waliweza kufunga shoo kwa nyimbo zao nyingi.

Nao Wadhamini wa Tamasha hilo Kampuni ya Tigo, Mkurugenzi wa Kanda ya Ziwa, Uthmaan Madata alisema ‘Mbali na muziki, wateja wa Tigo pia wanaweza kuvuna hadi mara mbili ya thamani kwa vifurushi vya intaneti watakavyonunua kupitia *147*00#. Promosheni ya Data Kama Loteitahakikisha kuwa mashabiki wanaweza kufuatilia habari na matukio yote ya msimu wa Tigo Fiesta 2018 – Vibe Kama Lote; au kufurahia kuperuzi kwenye mtandao wenye kasi zaidi wa 4G+,’ Madata alisema.

Wateja wote wa Tigo pia wanaweza kuvuna hadi TSH 10 millioni, zawadi za kila wiki za TSH milioni moja, ama zawadi za kil asiku za TSH 100,000 kwa kushiriki katika shindano la Tigo Fiesta 2018 – Chemsha Bongo. Ushiriki katika shindano hilo unapatikana kwa kutuma neno MUZIKI kwenda 15571 au kwa kutembelea tovuti ya http://tigofiesta.co.tz

Tamasha hilo litaendelea jumapili hii kwenye uwanja wa Karume mjini Musoma.


MAKAMU WA RAIS AKATAA KUZINDUA STENDI KUU MPYA YA MAILMOJA KIBAHA

$
0
0
NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA 

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amekataa kuzindua stendi kuu mpya ya Mailmoja Kibaha mkoani Pwani, akiwa katika ziara yake mkoani humo. 

Hatua hiyo ameifikia kutokana na kupata wasiwasi wa utekelezaji wa mradi kuwa na baadhi ya mapungufu ambapo amedai baada ya kufanya uchunguzi wiki mbili ama tatu zijazo atakwenda kuuzindua. Akizungumza katika stand hiyo, Samia alieleza, kuna minong’ono wameisikia kuhusu mradi huo hivyo ni jukumu lake kuibeba na atakapo jiridhisha atarudi kwa mara nyingine . 

Hata hivyo, alisema atakutana na mkuu wa wilaya, mkurugenzi na mkuu wa mkoa kuzungumzia suala hilo. “Msishtuke kwa hili ni kawaida kwa kuchukua hatua za aina hii ili kujiridhisha kwa maslahi ya halmashauri, mkoa na watumiaji kijumla “Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni sikivu na kusikia malalamiko ya wananchi, tumepata malalamiko kidogo kuhusu stand hii, serikali ni ya uwazi na ukweli hivyo sitofungua stendi “alisisitiza Samia. 

Samia alimpongeza mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kibaha, Jennifer Omolo na mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama na wahusika waliohusika kufanikisha mradi huo. Nae waziri wa nchi ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na serikali za mitaa -TAMISEMI ,Selemani Jafo alisema yeye kama waziri wapo wataalamu wanaohakiki lakini ameridhishwa na kazi hiyo . 

“Kwani kila kazi ina changamoto za kibinadamu, hasi na chanya, lakini wamejitahidi “alisema Jafo. Jafo alieleza, mradi huo umepata msaada wa mkopo nafuu kutoka bank ya Dunia ambao wamepata fedha za kimarekani dollar milioni 255 .# Alielezea , wanagusa miji 18 na wanachokifanya wanagusa stendi tisa, barabara za miji kwa kiwango cha lami na madaraja makubwa ya kisasa. 

Wakitoa kero ya stand hiyo, madereva pikipiki walidai eneo lililotengwa kwa ajili yao halina sehemu ya kujikinga hivyo kusababisha usumbufu wakati wa mvua na jua. Mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kibaha, Jennifer Omolo alisema katika stendi ndogo ya awali walikuwa wakikusanya ushuru sh. 950.000 kwa siku ambapo sasa wanakusanya sh. milioni 1.6 .Alisema mradi huo umegharimu sh. bilioni 2.9 na walishamlipa mkandarasi bilioni 2.7 ,stendi hiyo itakuwa na mabanda kumi ya kukatia tiketi, mawakala 40 ,eneo la tax, na wafanyabiashara ndogondogo wanaojiingizia kipato kwa kuuza biashara zao wapo 100 . 

Samia akiwa katika ziara yake Kibaha vijijini na mjini pia alipata fursa ya kutembelea mradi wa reli ya kisasa ya standard gauge kujionea namna unavyoendelea.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Meneja Uzalishaji Mhandisi Farid M. Abdallah wakati akikagua shughuli za ujanzi wa Reli ya Kisasa “Standard Gauge” katika kijiji cha Soga wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua stendi mpya ya mabasi Kibaha . Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais

WAZIRI LUKUVI ALITAKA SHIRIKA LA NYUMBA NHC KUWA MFANO KATIKA KUSIMAMIA NA KUTUNZA NYUMBA ZAKE

$
0
0
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuwa mfano katika, kuhifadhi, kutunza na kujenga nyumba bora za gharama nafuu kwa ajili ya kuziuza au kuzipangisha kwa wananchi wakiwemo watumishi wa umma.

Aidha, amelitaka shirika la NHC kuwa mfano kwa taasisi nyingine zinazojishughulisha na ujenzi kwa kujenga nyumba bora na wakati huo kuwapangisha wananchi kwa malipo ya kodi ya mwezi mmoja mmoja badala ya utaratibu uliozoeleka wa kupangisha kwa malipo ya kipindi cha miezi sita au mwaka mzima na kuepuka kutumia ‘vishoka’ wakati wa kupangisha nyumba zake.

Lukuvi aliyasema hayo jana alipolitembelea Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika mkoa wa Kilimanjaro wakati wa mwisho wa ziara yake ya kushughulikia migogoro ya ardhi katika wilaya za Hai, Moshi na Same mkoani Kilimanjaro.

Alisema, Shirika la Nyumba la nyumba NHC lazima liwe na mkakati mzuri wa ukarabati nyumba zake na kubainisha kuwa haiwezekani Shirika kubwa kama hilo kuwa na nyumba nyingi katika maeneo ya vitovu vya miji huku nyingi ya nyumba hizo zikiwa zimechoka na kusisitiza kuwa hataki kusikia NHC inakuwa na nyumba za aina hiyo.

Amelitaka Shirika kujipanga vizuri na kuhakikisha linashirikiana vizuri na ofisi za Mikoa na Halmashauri kwa lengo la kujenga nyumba za gharama nafuu kwa ajili ya watumishi na wakati huo kutangaza shughuli zake kwa kuwa NHC ina Kampuni yake ya ujenzi iliyosheheni wataalamu wa fani mbalimbali sambamba na kuwa na uwezo wa kujenga majengo mbalimbali kama vile Shule, Hospitali, Vituo vya Afya na Vyuo.

Aidha, Lukuvi amelitaka Shirika la NHC kuimarisha kitengo chake cha huduma kwa wateja na kujiwekea utaratibu wa kuwatembelea wapangaji wake kwa lengo la kufahamu changamoto zinazowakabili katika nyumba na kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo.

Kwa upande wake Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa mkoa wa Kilimanjaro Juma Kiaramba alimueleza Lukuvi kuwa Shirika la NHC katika mkoa huo liko kwenye mazungumzo na halmashauri ya Manispaa ya Moshi kwa ajili ya ujenzi wa nyumba 25 za gharama nafuu na mradi huo utagharimu jumla ya shilingi bilioni 1.4 na utachukua miezi kumi na nane mpaka kukamilika.

Kwa mujibu wa Kiaramba, NHC mkoa wa Kilimanjaro pamoja na kufanya ukarabati wa majengo yake katika mkoa huo, kwa sasa Shirika iko kwenye mazungumzo na taasisi mbalimbali mkoani humo ikiwemo halmashauri ya Same kwa ajili ya kujenga nyumba za gharama nafuu ingawa kumekuwa na chanagamoto kubwa ya uhaba wa ardhi katika maeneo kadhaa ya mkoa huo.

MWAKILISHI MTEULE WA JANG’OMBE AKABIDHIWA CHETI CHA USHINDI

$
0
0
NA IS-HAKA OMAR,ZANZIBAR

MWAKILISHI mteule wa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Jang’ombe Ndugu Ramadhan Hamza Chande leo amekabidhiwa rasmi Cheti cha udhibitisho wa ushindi wa nafasi ya Uwakilishi wa Jimbo hilo.

Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Wilaya ya Mjini iliyopo Maisara na kuudhuriwa na Viongozi na Wanatendaji wandamizi Tume hiyo na CCM.Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Cheti hicho Mwakilishi mteule huyo Ramadhan Hamza ameahidi kufanya kazi kwa uadilifu na kwa kufuata miongozo na taratibu zote za kisheria kwa maslahi ya wananchi wote wa Jimbo hilo. 

Amewashukuru wananchi na wanachama wa CCM wa Jimbo hilo kwa kumpatia ridhaa yangu kuongoza Jimbo hilo kupitia utaratibu halali wa kidemokrasia. “Nitawatumikia kwa uadilifu wananchi wote wa Jang’ombe bila ya ubaguzi wowote kwani naamini bila yenu nyinyi kuridhia kunipa nafasi hii nisingeweza kushinda katika mchakato huu wa kisiasa uliokuwa na ushindani mkubwa.Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015/2020 tayari nishakabidhiwa muda wowote nitaanza kutekeleza mpango kazi wangu kwa lengo la kutekeleza ahadi nilizoahidi katika kampeni.”,ameeleza Chande.

Kwa upande wake aliyekuwa Msimamizi Mkuu wa Uchaguzi wa Jang’ombe ambaye pia ni Afisa wa ZEC Wilaya ya Mjini Bi.Mwanapili Khamis Mohamed amemsisitiza kiongozi huyo kufanya kazi zake kwa majibu wa taratibu na kanuni za kisheria ili kutimiza matakwa ya wananchi waliomchagua. 

Mwakilishi huyo aliyeshinda nafasi hiyo jana kwa kura 6,581 sawa na asilimia 90.5 katika Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Jang’ombe uliofanyika kwa amani bila ya kujitokeza matukio ya uvunjifu wa sheria za Uchaguzi na nchi kwa ujumla.
AFISA wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Wilaya ya Mjini Mwanapili Khamis Mohamed (kulia) akimkabidhi Cheti cha udhibitisho wa Ushindi wa nafasi ya Uwakilishi Mwakilishi mteule wa Jimbo la Jang’ombe Ramadhan Hamza Chande (kushoto) , aliyekuwa Wakala wa Mgombea wa CCM katika Uchaguzi huo Rajab Uweje Yakoub (wa pili kushoto).
ALIYEKUWA Wakala wa Mgombea Uwakilishi wa CCM Ndugu Rajab Uweje Yakoub (wa pili kushoto) akisaini Cheti cha udhibitisho wa ushindi wa Uwakilishi cha Mwakilishi mteule wa CCM Jimbo la Jang’ombe.
MWAKILISHI mteule wa Jimbo la Jang’ombe Ramadhan Hamza Chande akionyesha Cheti cha udhibitisho wa ushindi wa Uwakilishi kupitia Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo uliofanyika Jana.

SHONZA: SERIKALI ITAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO WASANII KUKUZA SOKO LA TASNIA YA SANAA

$
0
0
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mjasiriamali wa sanaa za uchongaji, Ras Jeshi Beku alipotembelea banda la Msanii huyo wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Mjasiriamali wa sanaa za uchongaji, Ras Jeshi Beku alipotembelea banda la Msanii huyo wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza (kulia), akitazama kikoi kilitengenezwa na Msajiriamali Esther Mwita alipotembelea banda la Msanii huyo wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utanmaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akitazama moja shati lilitengtenezwa na Mjasiriamali Monica Matemba alipotembelea banda la Mjasiriamali huyo wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akitazama chungu kilitengenezwa na mmoja wa Wajasiariamali alipotembelea banda la Mjasiriamali huyo wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akitazama chungu kilitengenezwa na mmoja wa Wajasiariamali alipotembelea banda la Mjasiriamali huyo wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akijaribu moja ya vidani vilivyotokana na kazi za wajasiriamali wasanii mara baada ya kutembelea alipotembelea banda la Mjasiriamali wakati wa kufunga tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fisoo, Mwenyekiti wa Bodi wa Taasisi hiyo Prof. Frowin Paul Nyoni na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano katika Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) Geofrey Tengeneza, wakibadilishana mawazo wakati wa kufungwa kwa Tamsha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza, akisoma moja ya vitabu wakati alipotembelea moja wa mabanda ya wajasiriamali wakati wa kufungwa kwa Tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Msanii wa sanaa ya uchongaji, Amiri Amasha akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya wasanii na wajasiriamali katika kilele cha Tamsha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Mkuu wa Magofu ya Kaole- Bagamoyo Mkoani Pwani, Siyawezi Hungo (katikati) akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza wakati alipotembelea Banda la Taasisi hiyo katika kilele cha Tamasha la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kutembelea Banda la Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza Nchini wakati wa kilele cha Tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. Kulia kwakeni Katibu Mtendaji wa Bodi hiyo, Joyce Fisoo na Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof. Frowin Paul Nyoni. 

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Joyce Fisoo akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya vitambulisho rasmi vya Bodi hiyo kwa watayarishaji na waandajii wa filamu mbalimbali nchini kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza wakati alipotembelea banda la Bodi hiyo katika kilele cha Tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo jana Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Kikundi cha Ngoma cha Bagamoyo Players kinachoongozwa na Wakufunzi wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) wakitoa burudani ya ngoma kwa wageni mbalimbali waliohudhuria kilele cha Tamasha la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo Pwani jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza akihutubia wageni mbalimbali waliohudhuria kilele cha Tamasha la 37 la Sanaa nas Utamaduni Bagamoyo jana Jumamosi Oktoba 27, 2018, Wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani. 

(PICHA NA MAELEZO) 

…………………………………

Na Mwandishi Wetu,MAELEZO

Bagamoyo

NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza amesema Serikali itaendelea kuwajengea uwezo, umahiri na ubunifu wasanii wa Tanzania kupitia Mradi wa Utambuzi wa Wasanii wa Sanaa za Ufundi (TASIP) ili kukuza soko la tasnia hiyo katika ngazi ya kitaifa na kimataifa.

Akifunga Tamasha la 37 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo, Wilayani Bagamoyo, Mkoani Pwani jana (Jumamosi Oktoba 27, 2018), Shonza alisema malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kuwa tasnia ya sanaa nchini inapiga hatua kubwa zaidi na kuwafanya wasanii kunufaika na kazi zao.

Aliongeza kwa kuzingatia kuwa Wizara yake inasimamia na kutekeleza sera ya sanaa nchini, Serikali itahakikisha kuwa kuipitia mradi wa TASIP unawafikia na kuwatambua wasanii wote nchini na kuwawezesha kuwa na utambulisho rasmi utawaozesha kupata mitaji na mikopo ya kuendesha shughuli zao.

“Mwaka jana nilizindua mradi huu wa TASIP na mwaka huu tumeanza kushuhudia mafanikio makubwa kupitia program hii, kwa kuwa wapo baadhi ya wasanii waliotambuliwa na kusajiliwa na wameanza kupata mikopo kutoka mabenki hatua inayowezesha kupata kutatua baadhi ya changamoto katika kuendesha shughuli zao” alisema Shonza.

Naibu Waziri Shonza alisema Serikali itaendelea kutoa msukumo kwa wafadhili mbalimbali kuweza kuunga mkono Tamasha la Sanaa na Utamduni Bagamoyo linalofanyika kila mwaka nchini, kwa kuwa Tamasha hilo linawezesha wasanii wa Tanzania wanapata uzoefu wa masuala mbalimbali kutoka kwa wasanii wenzao wa mataifa mbalimbali ya nje na hivyo kuweza kuongeza ubunifu katika kazi zao.

Kwa mujibu wa Shonza alisema kwa kutambua umuhimu wa Tamasha hilo, Serikali itaendelea kuijengea Tasasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBA) kwa ili kuwa na uwezo kuweza kuzalisha wasanii na wakufunzi wenye ubora katika ngazi ya kitaifa na kimataifa kwani Taasisi hiyo imekuwa kiungo muhimu cha uzalishaji wa wasanii katika mataifa mbalimbali ya kigeni.

SERIKALI HAITAMWONEA HURUMA MTU YEYOTE ATAKAYEKAMATWA AKIJIHUSISHA NA UVUVI HARAMU-NAIBU WAZIRI ULEGA

$
0
0
 Serikali imepiga marufuku uvuvi haramu na kuteketeza  nyavu aina ya makokoro 35 , makila 6 na nyavu za zenia 25 zilizokuwa zikitumiwa na wavuvi haramu katika bwawa la Nyumba ya Mungu lililopo wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kagongo kata Lang’ata leo,Naibu Waziri wa mifugo na Uvuvi  Abdalah Ulega  amesema serikali haitamwonea huruma mtu yeyote atakayekamatwa akijihusisha na uvuvi haramu kwani serikali  imekua ikipoteza kiasi kikubwa cha mapato kutokana na uvuvi huo.

“Hatuna utani na mtu asiye na huruma na rasilimali za nchi hii, Tanzania ndio nchi yenye  sehemukubwa  yenye maji kuliko sehemu nyingine lakini bado tunaagiza samaki kutoka nchini china, tumeagiza sato., perege hadi kibua wa kichina, tusipotokomeza leo bwawa litakuwa historia kwa vizazi vijavyo” amesema Ulega

Kwa  upande wake mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira  alisema uwepo wa bwawa hilo umekuwa msaada mkubwa kwa wananchi katika eneo hilo na sasa ni wakati wa wananchi kuwa walinzi kwa kila mmoja ili kutokomeza uvuvi haramu.“Hebu leo amueni kabisa kwamba  biashara ya samaki ndio mfumo wa maisha yenu, Ninyi mkifanya hivyo sisi hatutahitaji kufunga hili bwawa , wakati wote tutahitaji kuongeza kizazi cha samaki na kuleta wataalamu kupima kiwango cha samaki tulichonacho” alisema Mghwira

 Kwa upande wake Dismas Gondwe mkazi wa kijiji cha kigongo kata ya Lang’ata amesema  uvuvi haramu katika bwawa hilo unatokana na kukosekana kwa utaratibu maalumu unaowaelekeza  wavuvi kuendesha  shughuli zao katika bwawa hilo.

Gondwe ameiomba serikali kuwawezesha  wavuvi wa bwawa la Nyumba ya Mungu zana  harali ambazo serikali inazitambua.

Naibi Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na wavuvi wa kijiji cha Kagongo kata ya Lang`ata mkoa wa Kilimanjaro kuhusu serikali kutokumuonea huruma mtu yoyote ambaye atajihusisha na shughuli za uvuvi  haramu.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG Kilimanjaro)
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akiteta jambo na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira.
 Naibi Waziri Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,  Abdallah Ulega (wakwanza kulia) kwa kushirikiana na  Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mghwira na  Mkuu wa wilaya ya Mwanga Aarron Mbogho wakiteketeza zana haramu zilizokua zikitumika katika uvuvi haramu kwenye bwawa la Nyumba ya Mungu.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG Kilimanjaro)
 Sehemu ya wavuvi wa kijiji cha Kagongo kata ya Lang`ata mkoa wa Kilimanjaro wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega.
Zana haramu zilizokua zikitumika katika uvuvi haramu zikiteketezwa

NEWS ALERT: LAWRENCE MASHA NA MBUNGE CHEGENI WASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI WILAYANI RUNGWE KWA TUHUMA ZA KUFANYA VURUGU KWA MWEKEZAJI WA MATUNDA MKOANI MBEYA

$
0
0
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Lawrence Masha pamoja na Mbunge wa Jimbo la Busega Raphael Chegeni na vijana wengine 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya wakituhumiwa kufanya vurugu kwenye nyumba ya mwekezaji wa matunda ya Parachichi Peter Cruise na kutoa vyombo vyake nje kinyume cha taratibu. 

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya kosa hilo Oktoba  27, 2018  majira ya saa tatu asubuhi kwenye makazi ya mwekezaji yaliyopo katika eneo la Rungwe Mission na kuharibu mali hali iliyozua mabishano makali kabla jeshi la polisi kufika eneo la tukio na kuwakamata watuhumiwa ambao watafikishwa mahakama mara baada ya uchunguzi kukamilika. 

Masha na wenzake wanadaiwa kufika nyumbani kwa mwekezaji huyo kwa kuvunja mlango wa nyumba na kisha kutoa vyombo nje kwa nguvu .

 Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Ulrich Matei amethibitisha  kukamatwa kwa watu hao na kueleza kuwa hana taarifa za ujio wao licha ya (watuhumiwa hao) kudai wanakwenda kutekeleza amri ya mahakama inayowapa uhalali wa kumwondoa mwekezaji huyo kwenye makaazi hayo.

MANINJA walipovamia jukwaa la sherehe za Miaka 20 ya TWANGA PEPETA


RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WANUNUZI WA KOROSHO JIJINI DAR ES SALAAM NA KUTOA MSIMAMO WA SERIKALI KUHUSU BEI YA KOROSHO

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wanunuzi wa zao la Korosho katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam na kutoa msimamo wa Serikali kuhusu bei ya Korosho kuwa isipungue shilingi 3000 kwa kilo moja. 
Wadau na Wanunuzi wa Korosho wakiwa wanasikiliza Maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati alipokutana nao na kuzungumza nao jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

KILUWA GROUP YAWAPOKEA WADAU WAKE WA UWEKEZAJI KUTOKA CHINA,WADHAMIRIA KUWEKEZA KWENYE BIDHAA ZA NGOZI

$
0
0

 Mwenyekiti wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa ( wa nne kulia) pamoja na ujumbe wake wakiwa na wageni wao katika picha ya pamoja kwenye moja ya chumba maalum cha kufikia Wageni katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,mara baada ya kuwasili Oktoba 27,2018 jijini Dar kutoka nchini China .Kampuni hiyo yenye ujumbe wa watu wa Watano umekuja nchini kwa mwaliko wa kampuni ya Kiluwa Group Ltd kufanya mazungumzo mbalimbali yakiwemo ya kutafuta fursa za uwekezaji ikiwemo pia kuonana na uongozi wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC).
 Mwenyekiti wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa  pamoja akipokea zawadi aliyoletewa na mgeni wake,Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong mara  kwenye moja ya chumba maalum cha kufikia Wageni katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,mara baada ya kuwasili Oktoba 27,2018 kutoka nchini China.
 Mwenyekiti wa Makampuni ya Kiluwa Group Ltd,Mohamed Kiluwa  pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong wakimsikiliza Meneja wa kampuni ya Kiluwa Group Ndugu Madoweka (ambaye ni mkalimani wa lugha ya Kichina),akifafanua jambo kurahisisha mawasiliano kwa mgeni wao Ndugu Mayi Hong akiwa ameambatana na ujumbe wake wa watu wanne kutoka kwenye kampuni yake ambayo inajishughulisha na uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa za ngozi nchini China.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group,Naima Kiluwa akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong,mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,jijini Dar  Oktoba 27,2018.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiluwa Group,Naima Kiluwa pichani kati akiwa ameambatana na Wageni wake mara baada ya kuwapokea jana uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakitokea nchini Chaina,Pichani kulia ni Mkurugenzi Mtendani wa kampuni ya Yinengda New Material Technology,Mayi Hong.kampuni hiyo inajishughulisha na uzalishaji/utengenezaji wa bidhaa za ngozi nchini China.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 29,2018.

SWEDEN YASAINI MAKUBALIANO MAPYA NA SHIRIKA LA FEMINA, YATOA BILIONI 4.5 KUENDELEZA MPANGO MKAKATI 2018/20

$
0
0
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
UBALOZI  wa Sweden nchini umesaini makubaliano na shirika la Femina Hip ikiwa ni msaada wa kutekeleza mpango mkakati wa Femina Hip kwa mwaka 2018/2019. Katika makubaliano hayo  jumla ya shilingi bilioni 4.5 zimetolewa kwa shirika hilo ili kuendelea kukuza elimu ya afya ya uzazi, haki, uwezeshaji kiuchumi na uraia kwa vijana nchini. Makubaliano hayo yametiwa saini na Mkuu wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden nchini Ulf Kallstig na mwanzilishi na Mkurugenzi mtendaji wa Femina Hip Dkt. Minou Fuglesang katika ofisi za ubalozi wa Sweden leo jijini Dar es salaam.

Akizungumza na vyombo vya habari wakati wa makubaliano hayo Ulf Kallstig amesema kuwa mchango wa Sweden utaboresha mipango ya Femina Hip inayolenga kuwawezesha vijana kutoka kona zote nchini hasa katika kuwajengea juhudi za kuwawezesha, kuboresha maisha ya vijana nchini na kuwajengea tabia ya uwajibikaji.

Aidha amesema kuwa, "Vijana wana jukumu muhimu katika kuiendesha Tanzania kuelekea taifa la uchumi wa kati wa viwanda na ni muhimu kwetu kuzishirikisha sauti za vijana katika mijadala ya kimaendeleo inayolenga kuhakikisha malengo ya maendeleo endelevu yanafanikiwa pamoja na ari ya ushirikishwaji na ustawi wa Tanzania" ameeleza Ulf.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Femina Hip Dkt. Minou Fuglesang amesema kuwa, " Femina Hip inashukuru kwa ushirikiano na ubalozi wa Sweden, tutaendelea kuchangia kazi zinazofanywa na serikali ya Tanzania katika kuhakikisha kwamba katika kizazi hiki cha vijana hususani wasichana wanalindwa na kusaidiwa kuwa raia wema wenye kuwajibika ipasavyo" ameeleza Dkt. Minou.

Dkt. Minou amesema kuwa, asasi za kiraia ni chombo muhimu na zina nafasi ya kipekee katika kuwapa sauti wananchi na kwa Femina kwa miaka mingi imekuwa chombo kinachoaminiwa kwa kuimarisha kitengo cha uhamasishaji na ushirikiano kwenye mitandao ya shule za sekondari na mashirika ya ndani katika kufikisha ujuzi muhimu vijana kila kona nchini.

Mkurugenzi wa habari wa Femina Amabilis Batamula amesema kuwa, wakielekea miaka 20 ya Femina wanaishukuru sana serikali ya Tanzania na Sweden kwa kuwaunga mkono na  hadi sasa wanawafikia watu Milioni 15 kwa mwaka na kuna  zaidi ya klabu 2340 za Fema kwa  katika shule za sekondari kote nchini.

Aidha Batamula ameishukuru serikali kwa kuruhusu na kutambua mchango wa asasi za kiraia  ikiwepo Femina katika kuwajenga vijana katika ujenzi wa taifa.

Pia amesema kuwa katika wiki ya vijana iliyohitimishwa kitaifa Mkoani Tanga, mgeni rasmi Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Ummy Mwalimu alipendekeza uwepo wa Klabu za Fema katika shule zote za serikali na binafsi nchini na wao wanasubiri mwitiko kutoka kwa vijana katika shule mbalimbali nchini.

Mwisho ameushukuru ubalozi wa Sweden kwa kuwa marafiki wazuri kwa Serikali na Femina na kwa msaada walioupata leo utawasaidia sana vijana.
Mkurugenzi mtendaji wa Femina Hip Dkt. Minou Fuglesang akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam ambapo ametoa shukurani kwa ubalozi wa  Sweden kwa  kuonyesha ushirikiano ambao utaiwezesha shirika la Femina kuendekeza juhudi za kuwawezesha kuboresha Maisha ya  vijana wa Tanzania na kuwajengea tabia ya uwajibikaji.
  Mkuu wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden Ulf Kallstig pamoja na Mkurugenzi mtendaji  wa Femina Hip Dkt.Minou Fuglesang leo Jijini Dar es Salaam katika ubalozi wa  Sweden wakisaini mkataba wa makubaliano Mapya ya shilingi bilioni 4.5 za Kitanzania na shirika la Femina Kwa kipindi cha mwaka 2018-2020 ili kuboresha  mipango ya shirika hilo.
Mkuu wa Ushirikiano wa Maendeleo wa Ubalozi wa Sweden Ulf Kallstig wakikabidhiana mkataba huo na Mkurugenzi mtendaji wa Femina  Dkt Minou Fuglesang pamoja na  Mkurugenzi  wa  habari wa shirika hilo Amabili  Batamula baada ya zoezi la utiaji saini kumalizika leo Jijini Dar es Salaam katika ubalozi wa Sweden.

Makamu wa Rais afungua maonyesho ya wiki ya Viwanda mkoani Pwani

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRL) Masanja Kadogosamara baada ya kutembelea banda la kampuni inayotengeneza reli mpya ya kisasa ya YAPI MERKEZ wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya wiki ya Viwanda mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji  wa benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela Tuzo ya Udhamini Mkuu wa maonyesho ya Viwanda mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji  wa benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela cheti ya Udhamini Mkuu wa maonyesho ya Viwanda mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea zawadi maalum ya kumpongeza kwa kufanya ziara yenye mafanikio mkoani Pwani toka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo (kushoto) mara baada ya ufunguzi wa wiki ya maonyesho ya Viwanda mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi na wadhamini wa maonyesho ya Wiki ya Viwanda mkoani Pwani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Viewing all 46384 articles
Browse latest View live




Latest Images