Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live

DKT.CHAULA:TOENI ELIMU KWA JAMII KUHUSU UMUHIMU WA BIMA YA AFYA

$
0
0
1
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Zainabu Chaula akikagua stoo ya dawa kituo cha afya cha Katoro kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mkoani Geita leo alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa vituo vya afya nchini.
2
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Zainabu Chaula akiongea na baadhi ya wagonjwa alipotembelea kituo cha afya cha Katoro kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita , Mkoani Geita leo alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa vituo vya afya nchini.
2C4A2135
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Zainabu Chaula akikagua eneo la kujenga kituo cha afya katika Zahanati ya Katete iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Mkoani Geita leo alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa vituo vya afya nchini.
............................

Na. Angela Msimbira OR-TAMISEMI GEITA

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia Afya Dkt. Zainabu Chaula amewaagiza viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kuwa bima ya afya nchini.Dkt. Chaula ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua ukarabati na ujenzi wa vituo vya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mkoani Geita.

Amesema kuwa Watanzania hawatafanikiwa kielimu na kiuchumi kama hawatakuwa na afya bora hivyo ni jukumu la viongozi wote nchini kuhakikisha wanawahimiza wananchi kuwa na utaratibu wa kukata bima ya afya kwa ajili ya familia zao.Amesema Bima ya afya inamsaidia mwananchi pale anapougua gafla na kukosa fedha za matibabu hivyo ni muhimu Wanganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanatoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa kukata bima ya afya nchini.“Inasikitisha kuona wananchi wengi hawajui umuhimu wa kukata bima ya Afya, nawaagiza Viongozi wote kutoa elimu ipasavyo kwa wananchi ili waelewe umuhimu wa kuwa na bima ya afya kwenye familia zao” Amefafanua Dkt. Chaula.

Dkt. Chaula amewaagiza viongozi hao kuwahimiza wananchi kukata bima ya afya kwa ajili ya kuimarisha afya zao kwa sababu ni muhimu na inasaidia familia pindi zinazopata maradhi na kuhitaji huduma za afya.Kuhusu ukarabati na ujenzi wa vituo vya afya nchini Dkt. Zainabu Chaula amewapongeza wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato kwa kuchangia nguvu kazi katika ujenzi wa vituo vya afya ili kuunga mkono juhudi za Serikali na kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.

Dkt. Chaula amewahamasisha wananchi wa Kata ya Bwina, Halmashauri ya Wilaya ya Chato kuchangia nguvukazi ili kuanza ujenzi wa Kituo cha afya cha eneo hilo ambacho kitaungwa Mkono na Serikali.Amesema Serikali inajenga miundombinu ya afya kwa kuchagua maeneo yaliyopo mbali na kuyajenga kimakakati ili kuwapunguzia adha wananchi ya kutembea umbali mrefu kutafuta huduma za afya lengo likiwa ni kuweza kutoa huduma bora kwa jamii Aidha Dkt. Chaula amekamilisha ziara yake ya siku tatu katika Mkoa wa Geita ambapo ametembelea Vitio vya afya na Zahanati za Halmashauri ya Wialaya ya Geita na Chato Mkoani hapo.

PANGANI YAANDIKA HISTORIA SIKU YA WAZEE DUNIANI

$
0
0

 NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso kushoto akila na wazee wilayani Pangani IKIWA ni kilele cha siku ya wazee Duniani ambako kiwilaya yalifanyika kwenye viwanja vya Bomani wilayani humo
 MKUU wa wilaya ya Pangani,Zainabu Abdallah katika akiwa na wakazi wa mji wa Pangani wakati wa maadhimisho hayo
NAIBU Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wazeeAfisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gipson George akizungumza katika maadhimisho hayo
 Afisa Tawala wa wilaya ya Pangani Gipson George kushoto akishirikiana na wananchi wengine kubeba chakula kwa ajili ya kugawa kwa wazee
 Wazee wakipatiwa vipimo
 Wazee wakiwa kwenye maadhimisho hayo

 Sehemu ya wazee wilayani Pangani wakiwa kwenye maadhimisho hayoi
 sehemu ya vyakula walivyoandaliwa wazee


NA MWANDISHI WETU, PANGANI.

IKIWA ni kilele cha siku ya wazee Duniani kwa wiki nzima iliyopita jana ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Pangani,Mbunge wa Jimbo hilo na Halmashauri imefanya kampeni ya “Nashukuru Mzee” ambayo imeacha alama kubwa na kuandika historia katika wilaya ya Pangani.

Maadhimisho hayo yalifanyika kwenye viwanja vya Bomani Pangani na baadae kujumuika kwa chakula cha pamoja nyumbani kwa Mkuu wa wilaya ya Pangani.
Akizungumza katika maadhimisho hayo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah alisema wanawashukuru wazee hao kwa kazi nzito walioifanya hadi sasa kuijenga wilaya hiyo na Taifa kwa ujumla.

“Kuwapa zawadi ya uhakika ambayo ni sekta ya afya kama jambo muhimu zaidi kwao nyakati hizi ikiwa ni kuhakikisha wazee wote ndani ya siku wanapata vitambulisho vyao vya matibabu bure kama inavyoelekeza sera ya wazee”Alisema.

“Lakini pia matibabu, upasuaji, vipimo na matibabu bure maalumu toka kwa wataalamu ndani na nje ya Pangani kwa wiki hii hadi kilele huku vipimo vya macho na ambao watapatikana na tatizo watapatiwa miwani”Alisema.
Hata hivyo alisema wataendelea kuwajengea uwezo na kuwapa tumaini jipya na mikakati sambamba na kusikiliza changamoto ambazo zinawakabilia

Kwa upande wake,Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso aliitaka jamii kuwaenzi wazee na kuwathamani kutokana na kuwa na mchango mkubwa kwao

BENKI YA KILIMO YAOMBWA KUSAIDIA ZAO LA CHAI WILAYANI LUSHOTO

$
0
0



 Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. January Lugangika (wapili kushoto) akizungumza na ugeni kutoka Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ulipomtembelea Ofisini kwake wilayani Lushoto kuzungumzia fursa za uwekezaji katika kilimo. Wanaomsikiliza ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kushoto), wengine ni Afisa Biashara Mwandamizi wa TADB, Eunice Mbando (kulia) na Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo, Bw. Tito Kayugyuma (wapili kulia).
IMG_7031
Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. January Lugangika akihimiza jambo wakati wa kikao.
IMG_7032
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine akifafanua jambo wakati akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Bw. January Lugangika (hayupo pichani).
IMG_7033
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kulia) akiwa katika mazungumzo na Katibu Tawala wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Nicodemas Tambo (katikati). Anayesikiliza ni Afisa Ushirika wa Wilaya hiyo, Bw. Tito Kayugyuma (kushoto).
IMG_7034
Katibu Tawala wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Nicodemas Tambo akizungumza wakati wa kikao hicho alitumia fursa hiyo kuiiomba Benki ya Kilimo kuwaelimisha wakulima wa wilaya hiyo juu ya uwepo fursa za mikopo ya gharama nafuu kutoka TADB.
IMG_7076
Katibu Tawala wa Wilaya ya Lushoto, Bw. Nicodemas Tambo (kushoto) akiagana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imeombwa kusaidia uzalishaji wa zao la chai wilayani Lushoto mkoani Tanga ili kuchagiza shughuli za kiuchumi na kunyanyua kipato cha wakulima wadogo wadogo wilayani humo humo.
Ombi hilo limetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. January Lugangika wakati akizungumza na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine alipotembelea Ofisini kwake.

Bw. Lugangika alisema kuwa Serikali imejipambanua katika kukufua viwanda hasa vyenye kusaidia wakulima wadogo wadogo kupitia ununuzi wa malighafi akilitaja zao la chai kuwa ni la kipaumbele katika kuchagiza juhudi hizo za Serikali.“Benki ya Kilimo ikisaidia kufufua viwanda vyetu vya chai itawanufaisha wakulima wetu wanaolima chai hivyo kuweza kunyanyua kipato cha wakulima wilayani kwetu,” alisema.

Aliongeza kuwa wilaya ya Lushoto imejaliwa kuwa na eneo kubwa la uzalishaji zao la chai hivyo kuongeza tija katika kuendeleza zao hilo.Akizungumza wakati wa kikao hicho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Bw. Japhet Justine alisema TADB ipo tayari kuchagiza uzalishaji wa mazao ya kimkakati yenye masoko ya uhakika ikiwemo zao la chai na yenye kulenga kunyanyua hali za maisha ya wakulima wadogo wadogo nchini.Aliongeza kuwa TADB ipo tayari kusaidia juhudi za wilaya ya Lushoto katika kuwasaidi wakulima walio kwenye vikundi vya ushirika au skimu za uzalishaji wa mazao ya kilimo wilayani humo.

“TADB ipo tayari kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini nchini,” alisema.Bw. Justine aliongeza kuwa Benki  ya Kilimo imelenga kutekeleza kwa vitendo Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Kilimo (ASDP 2) kwa kuwasaidia wakulima wadogo wadogo nchini kwa kuwapatia mikopo ya gharama nafuu ili kuongeza uzalishaji wa malighafi kwa ajili ya viwanda hivyo kuchagiza dhana ya Tanzania ya Viwanda.

Naye, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Bw. Nicodemas Tambo aliiomba Benki ya Kilimo kuwaelimisha wakulima wa wilaya hiyo juu ya uwepo fursa za mikopo ya gharama nafuu kutoka TADB.“Nawaomba muwaelimishe wakulima wetu ili wachangamkie fursa za huduma zenu ili waweze kulima kibiashara,” alisema.

RAIS DK.SHEIN AWAZAWADIA WANAFUNZI WALIOFAULU VIZURI KIDATO CHA NNE NA SITA

$
0
0

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimzawadia Mwanafunzi Biubwa Khamis Ussi (kushoto) kidato cha Sita Skuli ya SOS aliyepata point 3 Sayansi ,katika hafla ya kuwazawadia Wanafunzi waliomaliza kidato cha Nne na Sita 2017-2018 na kupata Daraja la Kwanza na kula nao pamoja Chakula cha Mchana leo katika viwanja vya Ikulu Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimzawadia Mwanafunzi Fahad Rashid Salum(kushoto) kidato cha Sita Skuli ya Lumumba aliyepata point 3 Sayansi, katika hafla ya kuwazawadia Wanafunzi waliomaliza kidato cha Nne na Sita 2017-2018 na kupata Daraja la Kwanza na kula nao pamoja Chakula cha Mchana leo katika viwanja vya Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]02/10/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimzawadia Mwanafunzi Hamdoun Sabri Hamdoun (kushoto) kidato cha Sita Skuli ya SOS katika hafla ya kuwazawadia Wanafunzi waliomaliza kidato cha Nne na Sita 2017-2018 na kupata Daraja la Kwanza na kula nao pamoja Chakula cha Mchana leo katika viwanja vya Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 02/10/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) mara alipowasili katika Viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar katika hafla ya kuwazawadia na kuwapongeza wanafunzi wa kidato cha Nne na Sita waliofaulu na kupata Daraja la kwanza pamoja kula nao Chakula cha Mchana leo,(kulia) Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Mhe.Riziki Pembe Juma,[Picha na Ikulu.]02/10/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimzawadia Mwanafunzi Mwalim Kombo Mwalim (kushoto) kidato cha Sita Skuli ya SOS katika hafla ya kuwazawadia Wanafunzi waliomaliza kidato cha Nne na Sita 2017-2018 na kupata Daraja la Kwanza na kula nao pamoja Chakula cha Mchana leo katika viwanja vya Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 02/10/2018.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akitoa hutuba yake kwa Viongozi,Walimu na Wanafunzi wa Kidato cha Nne na Sita waliofaulu na kupata Daraja la kwanza katika Sherehe za kuwazawadia na kuwapongeza pamoja na kula nao chakula cha mchana katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.]02/10/2018.
Makamanda wakuu wa Vikosi vay SMZ wakiwa katika Sherehe za kuwazawadia wanafunzi wa Kidato cha Nne na Sita waliomaliza masomo na kupata daraja la Kwanza pamoja na kula chakula cha mchana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar leo[Picha na Ikulu.]02/10/2018.
Wanafunzi wa Kidato cha Sita wakiwa katika Sherehe za kuwazawadia wanafunzi wa Kidato cha Nne na Sita waliofaulu masomo na kupata daraja la Kwanza pamoja na kula chakula cha mchana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.]02/10/2018.
Wanafunzi wa Kidato cha Nne wakiwa katika Sherehe za kuwazawadia wanafunzi wa Kidato cha Nne na Sita waliofaulu masomo na kupata daraja la Kwanza pamoja na kula chakula cha mchana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) katika viwanja vya Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.]02/10/2018.

MKURUGENZI MTENDAJI TIC AITA WAWEKEZAJI JNIA-TBIII

$
0
0




Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bw. Geoffrey Mwambe (aliyenyoosha mkono ukutani), wakati akipata ufafanuzi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (katikati) na Mkurugenzi wa Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha kwenye ukumbi wa mikutano wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII).
DSC_2314
Mafundi (kulia juu ya mashine) wakiwa wanaendelea na ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, wakati wa ziara ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela na wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bw.Geoffrey Mwambe pamoja na msafara wao, leo walipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi huo.
DSC_2318
Mhandisi Barton Komba wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) anayesimamia mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), akielekeza jambo wakati wa ziara ya Wakurugenzi kutoka Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bw. Geoffrey Mwambe (wapili kushoto) na wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (watatu kulia) leo walipofanya ziara ya kuangalia maendeleo ya mradi huo.
 DSC_2343
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bw. Geoffrey Mwambe (alinyoosha mikono) leo akijaribu kueleza kwa vitendo katika ziara yake aliyoambatana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (watatu kushoto) walipotembelea ujenzi wa mradi unaoendelea wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, tayari ujenzi umefikia asilimia 82.
DSC_2437
Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Bw. Paul Rwegasha (wa pili kulia) akitoa maelezo mbalimbali mbele ya Wakurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bw. Geoffrey Mwambe (wapili kushoto) na wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (watatu kulia) walipotembelea jengo la tatu la abiria la JNIA leo kuangalia maendeleo ya ujenzi huo unaotarajiwa kukamilika Mei 2019. 
DSC_2279
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Richard Mayongela (kushoto) leo akiteta na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Bw. Geoffrey Mwambe kabla ya kuanza kwa ziara ya kutembelea mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII).

MBIO ZA ROTARY DAR MARATHON ZAPIGA HODI

$
0
0
Dar es Salaam. Mwaka huu unaweka alama ya maadhimisho ya miaka 10 ya Mbio za Rotary Dar, tukio la hisani ambalo limekuwa likiweka rekodi kubwa katika usajili kila mwaka.

Kupitia mbio hizo,miradi mbalimbali ya huduma za kijamii imekuwa ikitekelezwa kwa miaka tisa mfululizo iliyopita kupitia fedha ambazo huwa zinachangwa ikiwemo upandaji miti zaidi ya 26,000,utoaji wa huduma ya maji safi ya kunywa shuleni,

Ujenzi wa wodi ya saratani ya watoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kituo cha maendeleo ya ujasiriamali Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Mwaka huu, matembezi ya hisani na mbio za Rotary Dar zinalenga kukusanya fedha kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa kliniki maalum katika Hospitali ya CCRBT itakayowezesha utoaji huduma na kupunguza gharama zinazotolewa kwa watu wenye ulemavu.

Mbio za Rotary Dar ni juhudi za pamoja baina ya klabu nane za Rotary jijini Dar es Salaam ambazo zimekuwa zikiungwa mkono kwa ufadhili mkubwa wa Benki M na Pepsi.

Akizungumza kuhusu tukio hilo, Mwenyekiti wa Bodi wa Mbio za Rotary Dar, Bi. Sharmila Bhatt amesema, "Tunaamini ushirikiano wa kimkakati tuliokuwa nao na Benki M ulikuwa na mafanikio makubwa jambo lilopelekea muelekeo mzuri na kutoa motisha kwa wafadhili wengine katika ambao wanatuunga mkono mwaka huu," alieleza na kuongeza kuwa, "mwaka huu Pepsi nao wameongeza hatua nyingine zaidi kwa ajili ya kutangaza michezo Tanzania kwa kutoa ufadhili wa jumla kwa Mtanzania mwanaume na mwanamke atakayefanya vizuri katika mbio za kilomita 42.2, ambapo watapelekwa kushiriki mbio za Beirut Marathon nchini Lebanon.

Haya ni mafanikio makubwa kwa Mbio za Rotary Dar, kukubalika na kuweza kutoa Watanzania watakaoshiriki riadha kwa kupewa ufadhili kwa ajili ya mbio za Kimataifa".

Pia alitaja wadau wengine muhimu katika ufadhili huo wa Mbio za Rotary Dar kuwa ni Ashton Media, Toyota, ALAF, Zoom Tanzania, Resolution Insurance,Clouds Media Group, Azam Media, Plasco Limited, Insignia, Night Support, Ashers na Soft Tech.

Bi. Bhatt alitumia pia fursa hiyo kumtambulisha Balozi wa Mbio za Rotary Dar 2018, msanii wa kike anayevuma zaidi nchini Bi. Vanessa Mdee al-maarufu Vee-Money ambaye atashiriki katika matembezi na mbio hizo ikiwemo kutoa hamasa na motisha kwa washiriki wa tukio hilo ili wajitokeze kwa wingi.

Akizungumza na waandishi wa habari, Bi.Vanessa ameeleza kuupokea ubalozi huo kwa moyo mweupe huku akiahidi kuunga mkono tukio hilo.

"Ninafarijika sana kupewa fursa kubwa kama hii na nimeamini kuwa ninaweza kufanya jambo kuhusiana na tukio hili kwa jamii. Ninaahidi kututumia ushawishi wangu ili kuvutia washiriki wengi zaidi. Nikitambua kuwa kila mshiriki atakayeshiriki katika tukio hili, uchangiaji wake utawezesha kusaidia wengine,"amesema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mbio za Rotary Dar 2018, Rotarian Catherinerose Barretto aliwahakikishia Watanzania kuwa, kila kitu kinaenda vizuri, kama kilivyopangwa. Aliongeza kuwa, Oktoba 14, 2018 itakuwa siku ya kumbukumbu kwa michezo na siku ya tukio la kifamilia katika historia ya Tanzania.

Kwa mujibu wa Bi. Barretto miaka 10 ya Mbio za Rotary Dar zinatarajiwa kuwavutia zaidi ya washiriki 16,000.

Amesema, tukio hilo litahusisha matembezi ya familia kilomita tano, matembezi ya kilomita tisa, mbio za kilomita 21.1, mbio za kilomita 42.2, baiskeli na shughuli nyingine nyingi za kufurahisha.
"Tunatarajia kuwa na washiriki kutoka Kenya,Uganda, Rwanda, Malawi, Afrika Kusini na Ethiopia, "amesema.

Bi. Barretto alikumbushia kuwa, kauli mbiu ya tukio hilo itaendelea kuwa, "Ponya Maisha, Badilisha Jamii" ikiwa ni mwaka wa tatu wakichangisha fedha kwa ajili ya kuisaidia Hospitali ya CCBRT iweze kutoa huduma kwa ufanisi zaidi.

Kwa mujibu Mkurugenzi wa Uendeshaji wa CCBRT, Bi. Brenda Msangi kujengwa kwa kiliniki ya kisasa hospitalini hapo kutasaidia kuimarisha juhudi za utoaji huduma ikiwa matarajio yao ni kuhudumia Watanzania wengi zaidi miaka ijayo.

"Mbio za Rotary Dar kila wakati zimekuwa zikifikiria namna ya kuisaidia hospitali yetu katika uendeshaji wa shughuli zetu. Na matokeo yake ni kuwa jamii kubwa ya Watanzania inanufaika kupitia moyo wao wa kujitoa,"amesema

Msanii wa kike anayetamba zaidi nchini, Vanessa Mdee al-maarufu Vee-Money ambaye pia ni Balozi wa wa Mbio za Rotary Dar kwa mwaka huu akizungumza leo (Oktoba 02, 2018) jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kutangaza rasmi maandalizi ya mbio za Rotary Dar zitakazofanyika Oktoba 14 mwaka huu (Siku ya Mwalimu Nyerere). Vanessa atashiriki mbio za Rotary Dar kwa mwaka huu lakini pia atatumia ushawishi alionao kuwahamasisha watu wengi zaidi kushiriki. Pamoja nae ni Mwenyekiti wa Bodi wa Mbio za Rotary Dar, Bi. Sharmila Bhatt (kulia) na Mkurugenzi Uendeshaji wa CCBRT, Brenda Msangi (kushoto).
Mkurugenzi Uendeshaji wa CCBRT, Brenda Msangi (kushoto) akionyesha kipeperushi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo (Oktoba 02, 2018) jijini Dar es Salaam kuelezea baadhi ya huduma maalumu zinazotolewa na hospitalini hapo wakati wa hafla ya kutangaza rasmi maandalizi ya mbio za Rotary Dar zitakazofanyika Oktoba 14 mwaka huu (Siku ya Mwalimu Nyerere). Pamoja nae ni Msanii Vanessa Mdee al-maarufu Vee-Money (katikati) ambaye pia ni Balozi wa wa Mbio za Rotary Dar kwa mwaka huu na Mwenyekiti wa Bodi wa Mbio za Rotary Dar, Bi. Sharmila Bhatt (kulia).
Mwenyekiti wa Bodi wa Mbio za Rotary Dar, Bi. Sharmila Bhatt (kulia) akizungumza leo (Oktoba 02, 2018) jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kutangaza rasmi maandalizi ya mbio za Rotary Dar zitakazofanyika Oktoba 14 mwaka huu (Siku ya Mwalimu Nyerere). Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mbio za Rotary Dar, Catherinerose Barretto, Mkurugenzi Uendeshaji wa CCBRT, Brenda Msangi na Msanii Vanessa Mdee al-maarufu Vee-Money ambaye pia ni Balozi wa wa Mbio za Rotary Dar kwa mwaka huu.
Mwenyekiti wa Bodi wa Mbio za Rotary Dar, Bi. Sharmila Bhatt (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Uendeshaji wa CCBRT, Brenda Msangi baada ya mkutano na waandishi wa habari leo (Oktoba 02 2018) jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kutangaza rasmi maandalizi ya mbio za Rotary Dar zitakazofanyika Oktoba 14 mwaka huu (Siku ya Mwalimu Nyerere). CCBRT ndio mnufaika mkubwa wa fedha zinazokusanywa kutokana na mbio za Rotary Dar ambapo kwa mwaka mbio hizo zitakusanya fedha kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa kliniki maalum katika Hospitali ya CCRBT itakayowezesha utoaji huduma na kupunguza gharama zinazotolewa kwa watu wenye ulemavu.
Mwenyekiti wa Bodi wa Mbio za Rotary Dar, Bi. Sharmila Bhatt (katikati) na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya mbio za Rotary Dar, Catherinerose Barretto wakifurahia jambo na Vanessa Mdee al-maarufu Vee-Money ambaye ni Balozi wa Mbio za Rotary Dar kwa mwaka huu baada ya mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo (Oktoba 02, 2018) jijini Dar es salaam. Madhuni ya mkutano huo yalikuwa ni kutangaza rasmi maandalizi ya mbio za Rotary Dar zitakazofanyika Oktoba 14 mwaka huu (Siku ya Mwalimu Nyerere).

Benki ya NMB yaisaidia sukos, dmf vifaa vya kukabiliana na maafa /majanga

$
0
0
Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba (wa pili kuklia) akizungumza na wanahabari kabla ya kukabidhi mahema nane ambayo yatolewa na NMB ambayo yatatumiwa na taasisi hiyo wakati inazunguka kwa jamii kutoa elimu namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali pindi yanapotekea.
Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation, Sukos-DMF, Bw. Suleiman Kova (Kamanda mstaafu wa Jeshi la Polisi) moja ya fulana zilizotolewa na NMB kwa ajili ya Sukos-DMF.
Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation, Sukos-DMF, Bw. Suleiman Kova (Kamanda mstaafu wa Jeshi la Polisi) moja ya fulana zilizotolewa na NMB kwa ajili ya Sukos-DMF.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation, Sukos-DMF, Bw. Suleiman Kova (wa pili kulia) akizungumzia taasisi yake inavyofanya kazi zake kabla ya kupokeaa msaada huo toka NMB. Kutoka kushoto ni Msanii wa uigizaji, Salim Ahmad 'Gabo', Meneja Mwajiri wa Cops Security (T) Ltd, Ibraahim Mcherecheta na Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba (wa kwanza kulia).


BENKI ya NMB imetoa msaada wa mahema maalum pamoja na fulana zitakazotumiwa na Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation-Sukos-DMF wakati inazunguka kwa jamii kutoa elimu namna ya kukabiliana na majanga mbalimbali pindi yanapotekea. Vifaa hivyo ambavyo ni mahema maalum nane pamoja na fulana zitakuwa zikitumiwa siku ya tarehe 6 Octoba ikiwa ni siku maalumu kabisa ya kuadhimisha siku ya maafa /majanga duniani. 

Akizungumza katika tukio hilo la kukabidhi msaada huo, Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba alisema tukio hilo ni mwendelezo wa benki hiyo katika kuisaidia jamii hivyo wanatambua na kuguswa na majanga na maafa yanayowakumba wananchi ambao ni jamii wanaoihudumia.

"Ni ada yetu NMB kuisaidia jamii inayotuzunguka kupitia kitengo maalumu cha CSR...tumekuwa tukifanya hivi maeneo mbalimbali..hususani sekta ya elimu, afya na huduma nyingine muhimu kwa jamii. NMB inaamini msaada huu utatasidia jamii kupatiwa elimu ya kujikinga na majanga unaweza kupunguza athari ya majanga hayo hata yanapotokea," alisema Bi. Lilian Kisamba alipokuwa akikabidhi msaada huo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Sukos-DMF, Suleiman Kova.

Alisema NMB itaendelea kuisaidia jamii katika maeneo mbalimbali kwa kuwa hakuna maendeleo ya kiuchumi pasipo na jamii salama na pia hakuna biashara inayoweza kufanya vema pasipo na jamii salama. Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Sukos-DMF, Suleiman Kova (Kamanda mstaafu wa Jeshi la Polisi) alisema taasisi yake ya Sukos-DMF kwa kushirikiana na Benki ya NMB na wadau wengine imepanga kufanya uzinduzi wa mahema maalum ambayo yatakuwa yakitumika katika shughuli za kutoa hifadhi kwa wahanga wakati yanapotokea maafa.

Alisema zoezi hilo litakwenda sambamba na washiriki kufanya mazoezi (jogging) kuanzia eneo la uwanja wa taifa kuelekea viwanja vya Kituo cha Vijana cha Jakaya Kikwete na pia kutakuwa na tukio la washiriki kuchangia damu kwa ajili ya wahitaji, huku akisisitiza elimu ya kukabiliana na majanga kwa taasisi hiyo utakuwa ni mradi endelevu.

"Tunapenda kuwajulisha wananchi pamoja na wadau mbalimbali wajitokeze kwa wingi Oktoba 6, 2018 katika Viwanja vya Jakaya M. Kikwete kituo cha vijana vilivyopo Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam. Siku hiyo kutakuwa na maadhimisho maalum ya taasisi ya Sukos ambapo tutazindua mahema maalum yenye lengo la kutoa hifadhi kwa wahanga wakati wa maafa," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Sukos-DMF, Suleiman Kova.

Taasisi ya Suleman Kova Security inayosaidia kutoa elimu kwa umma kujikinga na majanga (Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation-Sukos-DMF). Taasisi hiyo inajihusisha na usimamizi, utoaji elimu na uhamasishaji jamii kuhusiana na namna ya kukabiliana na maafa mbalimbali ikiwa ni kuunga mkono Serikali harakati za kutoa elimu kwa jamii kuyakabili majanga anuai.

Wadau wengine watakaoungana na Sukos-DMF katika maadhimisho yao ni pamoja na Mpango wa Taifa wa Damu salama, Kampuni ya Coka cola, Kampuni ya Cops Security Ltd na vyombo vya habari kuhamasisha jamii.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation, Sukos-DMF, Bw. Suleiman Kova (wa pili kulia) akizungumzia taasisi yake inavyofanya kazi zake kabla ya kupokeaa msaada huo toka NMB. Kutoka kushoto ni Msanii wa uigizaji, Salim Ahmad 'Gabo', Meneja Mwajiri wa Cops Security (T) Ltd, Ibraahim Mcherecheta na Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba (wa kwanza kulia).
Msanii wa uigizaji, Salim Ahmad 'Gabo' ambaye ni Balozi wa Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation, Sukos-DMF akizungumza na wanahabari. Kutoka kushoto ni Afisa Mahusiano Mpango wa Taifa wa Damu Salama, Raya Hamad, Meneja Mwajiri wa Cops Security (T) Ltd, Ibraahim Mcherecheta, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Suleman Kova Security and Disaster Management Foundation, Sukos-DMF, Bw. Suleiman Kova na Meneja Mradi, Uwajibikaji kwa Jamii wa Benki ya NMB, Lilian Kisamba.

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu NIDA


TUGHE YAIPONGEZA WCF KWA KUWAANDALIA MAFUNZO YA UELEWA WA SHERIA YA FIDIA KWA WAFANYAKAZI

$
0
0
KATIBU Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya TUGHE taifa, Bw. Hery Mkunda, akizungumza kwenye semina ya mafunzo ya siku moja iliyoratibiwa kwa pamoja kati ya TUGHE na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), mjini Morogoro kwa lengo la kuwajengea uwezo viongozi na watendaji wa chama hicho kuhusu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.

NA K-VIS BLOG, MOROGORO
KATIBU Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya TUGHE taifa, Bw. Hery Mkunda, ameupongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa kuandaa mafunzo kwa ajili ya viongozi na watendaji wa chama hicho kuhusu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
Bw. Mkunda aliyasema hayo Mjini Morogoro Oktoba 1, 2018  wakati wa semina ya siku moja ya kuwajengea uwezo viongozi na watendaji wa TUGHE na kuwapa elimu kuhusu wajibu na haki za waajiri na wafanyakazi katika kutekeleza sheria hiyo.
Semina hiyo ya mafunzo ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio ya Mkutano Mkuu wa kwanza  wa Wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) uliofanyika mjini Arusha Mwaka jana (2017) ambapo pamoja na mambo mengine wadau walielekeza Mfuko kutoa mafunzo kwa makundi mbalimbali vikiwemo vyama vya wafanyakazi.
“Tuna wanachama takriban 70,000 kwa hiyo TUGHE sio jeshi dogo ni kubwa sana na hawa hapa ni watendaji wetu kutoka nchi nzima na ndio wanaohusika moja kwa moja na wanachama, naomba nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwa WCF kwa kuandaa semina hii.” Alisema Katibu Mkuu huyo wa TUGHE Bw. Mkunda.
Alisema watendaji na viongozi wa TUGHE Tanzania nzima ambao wameshiriki mafunzo hayo, wakielewa vema majukumu ya Mfuko itawezesha viongozi hao kueneza elimu hiyo kwa wanachama wao.“Kwa makatibu wetu wa mikoa ambao ndio wanaosimamia haki na maslahi ya wafanyakazi sehemu zao za kazi itakuwa ni rahisi sana kuhakikisha kwamba wafanyakazi ambao ni wanachama wetu wanapata haki zao ambazo Mfuko unatakiwa kutoa endapo wanapata madhara yatokanayo na kazi kama kuumia, kuugua au kufariki wakati wakitekeleza wajibu wao wa kazi” alisema Bw. Mkunda.
Akitoa neno la utangulizi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Mkurugenzi wa Uendeshaji Bw. Anselim Peter alisema, semina hiyo ya mafunzo ni muendelezo wa hatua ya Mfuko kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ambayo ni wadau wa Mfuko na nia kubwa ni kuwajengea uelewa wa madhumuni ya kuanzishwa kwa Mfuko, Sheria na jinsi Mfuko unavyofanya kazi. 

Alisema katika kipindi cha zaidi ya miaka miwili tangu Mfuko uanze kutekeleza majukumu yake, kumekuwepo na mafanikio makubwa ya kutimiza jukumu kuu la kuanzishwa kwa Mfuko la kupokea madai na kulipa fidia na hadi sasa Mfuko tayari umekwishalipa fidia zaidi ya shilingi bilioni 4.4.
Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi  Sekta ya Hifadhi ya Jamii Nchini (SSRA) Dkt. Irene Isaka, aliwataka viongozi na watendaji wa Chama hicho kuhakikisha wanachama wao wanafahamu wajibu na haki zao katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF). 

Dkt. Isaka ameyasema hayo katika hotuba ya ufunguzi wa mafunzo ya Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi kwa viongozi na watendaji wa TUGHE taifa na mikoa   iliyosomwa kwa niaba yake na Mkurugenzi wa Utafiti na Tathmini SSRA, Joseph Mutashubilwa mjini Morogoro Jumatatu Oktoba 1, 2018.“ Kwa kufanya hivi tutakuwa tunaepusha migogoro na tunadumisha mahusiano mazuri sehemu za kazi hali itakayowavutia wawekezaji kuja nchini kwa wingi na hivyo kutimiza dhamira ya Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.” Alisema. 

Dkt. Isaka pia amewataka washiriki hao wa mafunzo kusambaza elimu watakayoipata kwa kuwafikia na kuwapa elimu hiyo wanachama wa chama hicho na kumtaka kila kiongozi/ mtendaji aliyeshiriki awe na mpango kazi utakaoonesha idadi ya wanachama alionao katika eneo lake na namna atakavyowafikishia elimu hiyo ambayo ni muhimu kwao kuifahamu.

“ Nina imani kwa kufanya hivi tutakuwa tumewasaidia kwa kiasi kikubwa wanachama wetu kuujua Mfuko, kazi zake na pia kufahamu nini wanapaswa kufanya baada ya kupata matatizo wakati wakiwa wanatekeleza majukumu ya mwajiri” alifafanua. Akinukuu kifungu cha 72 (4) cha Sheria ya Fidia kwa wafanyakazi, Mkurugenzi Mkuu huyo wa SSRA alisema kifungu hicho cha sheria kinatamka nafasi ya uwakilishi wa vyama katika kamati za afya na usalama mahali pa kazi ambapo mwajiri anatakiwa kutunza kumbukumbu hizo na kamati inatakiwa kukagua ili kuona kama hilo linafanyika. Hayo yote ni katika kuhakikisha kwamba upo ushirikishwaji baina ya viongozi/watendaji na Serikali katika kulinda afya za wafanyakazi sehemu za kazi.
 KATIBU Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya TUGHE taifa, Bw. Hery Mkunda, akizunumza wakati wa udunguzi.Naibu Katibu Mkuu wa TUGHE, (Afya), Mhandisi Amani Msuya, akizungtuzma wakati wa semina hiyo.
 Baadhi ya viongozi wa TUGHE walioshiriki mafunzo hayo, wakisikilzia mada zilizokuwa zikitolewa na wataalamu wa WCF kuhusu shughuli za Mfuko.
 Katibu Mkuu wa TUGHE Mkoa wa Morogoro akizungumza.
 Katibu wa TUGHE Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Simon E. Elias Msuya akziunguzma.
 Washiriki ambao ni makatibu wa TUGHE wa mikoa yote Tanzania Bara pamoja na watendaji kutoka chama hicho makao makuu, wakisikiliza mada.
 Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter akitoa somo kuhusu shughuliz a Mfuko.
 Katibu w aTUGHE Mkoa wa Iringa, Bi. Rose Lamosai, akizungumza.

 Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter, (kushoto), akibadilishana mawazo na Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma, Mchenya M. John
Naibu Katibu Mkuu wa TUGHE taifa (AFYA), Bw. Amani Msuya, akizunhumza wakati wa kufunga mafunzo hayo. Katikati ni Mkurugenzi wa Uendeshaji WCF, Bw. Anselim Peter na kushoto ni Meneja wa huduma za Sheria Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bw. Kitandu Ugula

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA KITUO CHA WATOTO WENYE ULEMAVU WA AKILI CHA MIYUJI DODOMA

$
0
0

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia watoto wenye ulemavu wa akili wakati alipotembelea Kituo cha watoto hao, cha Miyuji Cheshire House cha jijini Dodoma, Septemba 2, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipotembelea Kituo cha Watoto Wenye Ulemavu wa Akili cha Miyuji Cheshire House cha jijini Dodoma, Oktoba 2, 2018. Wapili kushoto ni Naibu Waziri , Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira ambaye pia ni Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde, watatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge, kulia ni mwakilishi wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Padri, Onesmo Wisi na wapili kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo hicho, Peter Mavunde. (Picha na Ofisi a Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhi zawadi ya keki kwa watoto wa Kituo cha Watoto Wenye Ulemavu wa Akili cha Miyuji Cheshire House jijini Dodoma, Septemba 2, 2018. Kushoto ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde, kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo hicho, Peter Mavunde na wapili kushoto ni mwakilishi wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Padri, Onesmo Wisi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua shamba la zabibu la Kituo cha Watoto Wenye Ulemavu wa Akili cha Miyuji Cheshire House kilichopo Miyuji jijini Dodoma, Oktoba, 2, 2018. Watatu kulia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinith Mahenge, wapili kulia ni Mwakilishi wa Askofu wa Jimbo Katoliki la Dodoma, Padri Onesmo Wisi na wanne kushoto ni Mwalimu wa Kituo hicho, Josephine Baharia.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Dodoma Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde wakati alipowasili kwenye Kituo cha Watoto Wenye Ulemavu wa Akili cha Miyuji Cheshire House cha jijini Dodoma, Oktoba 2, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

TCCIA YAWEKA MIPANGO MKAKATI WA KUTATUA MATATIZO YA WAFANYABIASHARA

$
0
0
CHAMA cha wafanyabiashara, viwanda na kilimo nchini TCCIA ,imeweka mipango mikakati katika kutekeleza maazimio yaliyotolewa na serikali kufuatia tathimini kwamishi ya miaka mitano ambapo imelenga kuboresha shughuli mbalimbali za biashara,viwanda na kilimo.

Kimeweka utaratibu wa kuwawezesha wakulima wa korosho kwa kuwapatia nyenzo bora kwa kuwa zao hilo limechukua nafasi kubwa miongoni mwa mazao ya biashara katika kuliongezea pato Taifa kwa takribani miaka mitatu mfululizo.Maazimio hayo yalitolewa jana jijini Dar es Salaam kwenye  mkutano wa bodi ya wakurugenzi wa TCCIA uliowashirikisha wadau kutoka ngazi ya kata wilaya mkoa na taifa katika kujadili masuala mbalimbali yanayowakwamisha wafanyabiashara .

Makamu wa rais TCCIA upande wa kilimoa bw. Joseph Kaungwa alisema kuwa kumejitokeza vikwazo vingi ambavyo vimechangia kukwamisha shughuli za kibashara viwanda na kilimo visisonge mbele vikiwemo kodi na tozo mbali mbali.Pia alisema kutowapa nyenzo bora pamoja na pembejeo uwezeshi na masoko ya uakika yenye kukidhi matakwa ya bidhaa zizalishwazo na wakulima ambazo kimsngi uwapatia wakati mgumu kipindi cha kuandaa mashamba na kipindi cha mavuno.

Kwa upande wake makamu wa rais TCCIA katika masuala ya biashara bwa. Julias kaijage alisema kuwa chama hicho kimeweko mifumo ya uendesheji ambayo ni bodi katika kujadili maazimio mbalimbali na kuwezesha wafanyabiashara kujipatia manufaa .

“Wakati nchi ikielekea kwenye uchumu wa kati tunawataka wafanyabiashara kuachana na masuala ya uchuuzi ambayo hayana nafasi katika kuwaletea maendelo, ‘alisema Kaijage.Nae mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Mtwara Bw.Swallah Saidi alisema wamewafundisha wakulima namna ya kuifadhi korosho ili ziweze kupata bei nzuri katika soko la kimataifa ambapo itawapatia wakulima kipato cha kutosha.

“Tumezalisha zaidi ya tani laki tatu kwa lengo la kuongeza uzalishaji na kuitangaza korosdho katika masoko ya nnje ambapo kurosho ya Tanzania imekuwa bora zaidi katika nchi zinazolima zao hili afrika.
Kulia ni Kaimu Rais wa Chama cha wafanyabiashara wenye viwanda na Killimo (TCCIA) Octavian Mshiu akichangia baadhi ya maazimio yaliyotolewa na wanacha katika mkutano wa bodi ya wakurugenzi TCCIA jijini Dar es Salaam jana . Picha na Nicolas Gilliard.
Washiriki wakiwa katika mkutano wa bodi ya wakurugenzi TCCIA jijini Dar es Salaam jana . Picha na Nicolas Gilliard.
Baadhi washiriki wakiwa katika pica ya pamoja mara baada ya kuamaliza mkutano wa bodi ya wakurugenzi TCCIA jijini Dar es Salaam jana . Picha na Nicolas Gilliard.

NMB YASHEREHEKEA UZINDUZI WA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA NA WATEJA WAKE

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja iliyofanyika NMB Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Mmoja wa wateja wa Benki ya NMB, Isaac Joseph Kessy akikabidhiwa cheti na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki, Ruth Zaipuna. Kulia ni Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam, Badru Idd na Kushoto ni Meneja wa NMB Mlimani City Seka Urio.

Baadhi ya wateja wa Benki ya NMB wakiwa kwenye uzinduzi wa Wiki ya huduma kwa wateja.

Mmoja wa wafanyakazi wa Benki ya NMB kutoka kitengo cha ‘HR Support’ (kulia) akiwasilisha mada namba kitengo hicho kilivyofanikiwa kutoa huduma zake ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja wa NMB.
Mada mbalimbali zikijadiliwa na wafanyakazi wa NMB ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja wa NMB.

Mada mbalimbali zikijadiliwa na wafanyakazi wa NMB ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja wa NMB.

Sehemu ya wafanyakazi wa NMB wakiwa katika majadiliano Makao Makuu ya NMB ikiwa ni sehemu ya maadhimisho uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja wa NMB.

Baadhi ya wafanyakazi wa NMB kutoka kitengo cha ‘HR Support’ makao makuu ya benki hiyo wakikata keki kujipongeza kwa kitengo hicho kutimiza mwaka mmoja kwa mafanikio ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya uzinduzi wa wiki ya huduma kwa wateja wa NMB.

Keki ikiandaliwa na kitengo cha ‘HR Support’ makao makuu ya Benki ya NMB tayari kwa kuliwa na washiriki. 

MAAFISA MAENDELEO YA JAMII KIGOMA WANOLEWA UELEWA KUHUSU UALBINO-

$
0
0

Mashirika ya Under The Same Sun, CEFA Tanzania na GNRC Tanzania, yaendelea kuelimisha jamii kuhusiana na ualbino
.Mradi wa HAKI YETU wakutana na Maafisa Maendeleo na ustawi wa jamii .Kigoma na kuzungumza madhara ya kuwatenga watu wenye ualbino
Maafisa Maendeleo ya Jamii, na ustawi wa jamii Kigoma wapigwa msasa uelewa kuhusu Ualbino

Maafisa Maendeleo ya Jamii, na ustawi wa jamii, kutoka manispaa ya kigoma Ujiji leo wamehudhuria mafunzo ya uelewa kuhusu ualbino na elimu ya Amani na maadili iliyotolewa na mradi wa Haki Yetu mkoani Kigoma.

Mradi huo umekua ukiendeshwa tangu Aprili,2018 katika Mikoa ya kigoma na maeneo ya jirani kwa ushirika wa wadau Mbalimbali lengo lao likiwa ni kutoa msaada kwa jamii kuelewa zaidi kuhusu ualbino, kupunguza imani potofu, kuwajengea watu wenye ualbino misingi ya kujiamini ualbino pamoja na kutengeneza jamii shirikishi isiyokuwa na ma waa ya ubaguzi wa aina yoyote kwa watu wenye ualbini 

Katika mradi huu misingi muhimu ambayo imekua ikiwekewa msisitizo ni pamoja na kuzingatia utu, kuwapa nafasi watu wenye ualbino bila kuwabagua, kushirikiana nao kwenye maswala ya elimu na uchumi lengo likiwa ni kujenga Taifa bora 

Mradi wa Haki Yetu unatekelezwa na Mashirika ya Under The Same Sun, CEFA Tanzania na GNRC Tanzania, ukilenga kuelimisha jamii kuhusiana na ualbino.
 Pichani juu na chini ni Maafisa Maendeleo ya Jamii, na ustawi wa jamii, kutoka manispaa ya kigoma Ujiji leo wamehudhuria mafunzo ya uelewa kuhusu ualbino na elimu ya Amani na maadili iliyotolewa na mradi wa Haki Yetu mkoani Kigoma.




















 

ACACIA kukusanya milioni 340 kuboresha elimu nchini

$
0
0
Kampuni ya uchimbaji wa madini Tanzania – Acacia inatarajia kukusanya zaidi ya Sh milioni 340 kwa kupitia mashindano ya mbio za baiskeli kwa ajili ya kuboresha upatikanaji wa elimu kwa jamii zinazozunguka migodi yetu katika kanda ya ziwa. 

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo nchini, Asa Mwaipopo, Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben alisema mashindano hayo wameyapatia jina la ‘Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge’ na yanaenda sambamba na mpango wa kampuni wa kujenga jamii endelevu. 

Alisema mpango huo unaofahamika kwa jina la ‘CanEducate’,unatoa kipaumbele katika kuhakikisha jamii zetu – hasa watoto wa kike - wanapata elimu bora kama njia moja wapo ya kujikwamua na umaskini na kufanikisha dhamira ya serikali ya kuinua uchumi na hali za maisha ya watanzania kama ilivyoainishwa kwenye Dira ya Maendeleo 2025. 

“Fedha hizo zitasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia maskini na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwapatia sare na vifaa vingine vya shule ikiwemo vitabu na vifaa mbalimbali. 

“Pia zitaelekezwa katika kusaidia wanafunzi wa kidato cha tano na sita wanaotoka kwenye maeneo yanayozunguka migodi yetu kwa kuwalipia ada za mitihani, gharama za malazi na usafiri. Wanafunzi wengi wa ngazi hii husafiri umbali mrefu kufika shule zinazotoa elimu kwa ngazi hiyo ya ‘A Level’.” Alisema. 

Ali hasa sasa mpango huo wa CanEducate ulioanza mwaka 2011, umetumia kiasi cha Sh milioni 494 kwa kuwadhamini wanafunzi 3936, na kuziwezesha kwa njia mbalimbali shule zaidi ya tisa. 

“Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Acacia imeelekeza Zaidi ya asilimia 38 ya bajeti yake ya kutelekeza miradi ya kijamii, katika kutelekeleza miradi ya elimu. Baadhi ya miradi ya elimu iliyotelekezwa na Acacia mwaka 2017, ni pamoja na ujenzi wa madarasa, mabweni ya kisasa kwa ajili ya wanafunzi wa kike na ukarabati wa maktaba sita kwenye shule zinazozunguka migodi yetu,” alisema. 

Aidha, alisema Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo atazindua rasmi wa mashindano ya Acacia Imara Pamoja Cycle Challenge utafanyika Oktoba 5, mwaka huu na mashindano yenyewe yatafanyika Novemba 3, 2018 jijini Mwanza. 

“Tunatoa wito kwa kampuni na wadau mbalimbali kujitokeza katika kuchangia kufikia lengo letu ili kwa pamoja tuweze kuleta tumaini la thamani kwa wanafunzi wenye ndoto ya kupata elimu nzuri na kufikia malengo yao, na baadae kuja kulisaidia taifa. 

Naye Rais wa Chama cha Baiskeli Tanzania, Godfrey Mhagama alitoa wito kwa wananchi na makampuni mbalimbali kujitokeza katika mbio hizo na kufadhili mpango huo ili kuiwezesha jamii kupata huduma mbalimbali za kielimu. 

“Acacia wamekuwa na sisi tangu mwaka 2014, na sasa tumeingia mkataba wa miaka miwili tena, hakika wametusaidioa sana hasa sisi washiriki wa mchezo huu wa basikeli kwa kutupatia vifaa mbalimbali vya usalama na hata misaada mingine ambayo huwa tunawaomba,” alisema. 

Aidha, baadhi ya wanufaika wa mpango wa CanEducate, Dk. Husein Mwanga ambaye ni mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili, alisema mpango wa CanEducate ulimwezesha kusoma shahada ya uzamivu katika masuala ya usalama kazini. 

“Walinifadhili masomo yangu Afrika kusini kwa muda wa miaka minne, na sasa nimerudi nyumbani kuitumikia nchi yangu, hakika mpango huu umeisaidia Tanzania kupiga hatua kubwa kielimu,” amesema. 

Naye Dismas Kalitenge alisema licha ya mpango huo kumwezesha kulipia baadhi ya gharama katika Shahada ya Uhandisi wa madini aliohitimu mwaka katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, pia sasa amepata ufadhili wa msomo ya Shahada ya Uzamivu nchini Canada. 

“Nilihangaika sana kupata ufadhili ila nawashukuru ACACIA kwa kunidhamini kwenda kusomea uhandisi wa madini, nina hakika nikirudi nitaisaidia nchi yangu kupiga hatua kubwa kimaendeleo katika sekta ya madini,” alisema. 

Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben (katikati), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu wa mashindano ya mbio za baiskeli zinazojulikana kwa jina la ‘Imara Pamoja Cycle Challenge’. Kulia ni Mshauri Mkuu wa Kitengo cha Jamii endelevu – ACACIA, Siama Paul na kushoto ni Rais wa Chama cha Baiskeli Tanzania, Godfrey Mhagama. 
Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben (katikati), kulia kwake ni Mshauri Mkuu wa Kitengo cha Jamii endelevu – ACACIA, Siama Paul na kushoto ni Rais wa Chama cha Baiskeli Tanzania, Godfrey Mhagama wakiwa na baadhi ya wanufaika wa mpango wa uwezeshaji wanafunzi wasio na uwezo wa kumudu gharama za elimu ‘CanEducate’. Kampuni hiyo inatarajia kuzindua mbio za baiskeli zinazojulikana kwa jina la ACACIA Imara pamoja kwa lengo la kukusanya fedha za kuboresha sekta ya elimu nchini.
Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben (katikati), kulia kwake ni Mshauri Mkuu wa Kitengo cha Jamii endelevu – ACACIA, Siama Paul, wakimsikiliza mmoja wa wanufaika wa mpango wa kuwawezesha wanafunzi wasio na uwezo wa kumuda gharama za elimu – CanEducate, Jeremiah Nambali ambaye ambehitimu Shahada ya uhandisi wa madini katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam baada ya kuwezeshwa na mpango huo unaoratibiwa na Kampuni ya ACACIA kwa kushirikiana na taasisi ya CanEducate.


Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben (katikati), akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu wa mashindano ya mbio za baiskeli zinazojulikana kwa jina la ‘Imara Pamoja Cycle Challenge’. Kulia ni Mshauri Mkuu wa Kitengo cha Jamii endelevu – ACACIA, Siama Paul na kushoto ni Rais wa Chama cha Baiskeli Tanzania, Godfrey Mhagama.
Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben (katikati), kulia kwake ni Mshauri Mkuu wa Kitengo cha Jamii endelevu – ACACIA, Siama Paul na kushoto ni Rais wa Chama cha Baiskeli Tanzania, Godfrey Mhagama wakiwa na baadhi ya wanufaika wa mpango wa uwezeshaji wanafunzi wasio na uwezo wa kumudu gharama za elimu ‘CanEducate’. Kampuni hiyo inatarajia kuzindua mbio za baiskeli zinazojulikana kwa jina la ACACIA Imara pamoja kwa lengo la kukusanya fedha za kuboresha sekta ya elimu nchini.
Meneja Uboreshaji tija kutoka Kampuni ya uchimbaji wa madini nchini Tanzania – ACACIA, Janeth Ruben (katikati), kulia kwake ni Mshauri Mkuu wa Kitengo cha Jamii endelevu – ACACIA, Siama Paul, wakimsikiliza mmoja wa wanufaika wa mpango wa kuwawezesha wanafunzi wasio na uwezo wa kumuda gharama za elimu – CanEducate, Jeremiah Nambali ambaye ambehitimu Shahada ya uhandisi wa madini katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam baada ya kuwezeshwa na mpango huo unaoratibiwa na Kampuni ya ACACIA kwa kushirikiana na taasisi ya CanEducate.

JENERALI MSTAAFU MWAMUNYAGE ATEMBELEA MIRADI MBALIMBALI YA MAJI YA DAWASA

$
0
0
Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Taka na Maji safi (DAWASA) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange ametembelea miradi mbalimbali na ujenzi wa matanki ya kuhifadhia maji  inayosimamiwa na Mamlaka hiyo leo Jijini Dar es Salaam.

Ziara hiyo ya kwanza toka kuteuliwa kwake Mwamunyage ametembelea mradi wa maji wa Bunju, Mabwepande, Salasala, Wazo na Kibamba hadi Kisarawe.

Jenerali Mstaafu ameambatana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasa Mhandisi Cyprian Luhemeja na baadhi ya viongozi wa bodi hiyo katika kukagua miradi na  hatua iliyofikia.

Akitembelea miradi hiyo ya Maji itakayosaidia upatikanaji wa maji wa takribani Lita milioni sita kwenye Kila tanki  kwa siku, Jenerali Mstaafu Mwamunyange amefurahishwa na hatua kubwa iliyofikiwa na Dawasa katika kuhakikisha mkoa wa Dar es Salaam na baadhi ya Maeneo ya Mkoa wa Pwani yanapata maji salama na ya uhakika.

Katika mradi wa Salasala unaosimamiwa na Kampuni ya Jain Irrigation Systme ambao upo katika hatua ya mwisho unatarajiwa kuzinduliwa mwishoni mwa mwezi Oktoba utakaowezesha kupatikana kwa wateja wapya 40,000.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasa) Mhandisi Cyprian Luhemeja  (wa pili Kulia) akiwa ameambatana na Mwenyekiti wa Bodi ya Dawasa Jenerali Mstaafu Davis Mwamjnyange (wa kwanza kushoto) wakiwa wanakagua moja ya Tanki la kuhifadhia maji wakati wa ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya Mamlaka hiyo Leo Jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Majinsafi na Maji Taka (Dawasa) Mhandisi Cyprian  Luhemeja  akimuelezea moja ya mradi wa maji kwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Dawasa Jenerali Mstaafu Davis Mwamjnyange katika ziara yake iliyofanyika Leo Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Taka na Maji safi (DAWASA) Jenerali Mstaafu Davis Mwamunyange (katikati) akisikiliza maelezo kutoka kwa wakandarasi wa mradi huo kutoka kampuni ya Jain Irrigation System  wakati wa ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya Mamlaka hiyo Leo Jijini Dar es Salaam.


RAIS DKT. MAGUFULI AWAAPISHA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI, SKAUTI MKUU WA TANZANIA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea saluti toka kwa Ndg. Mwantumu Bakari Mahiza muda mfupi baada ya kumuapisha kuwa Skauti Mkuu wa Chama Cha Skauti Tanzania. Aliyeketi ni Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe aliyemuapisha kuwa Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Hafla hii imefanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi baada ya kuongea machache kwenye hafla ya kuwaapisha Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe na Skauti Mkuu wa Tanzania Ndg. Mwantumu bakari Mahiza Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo wakati  Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaj Ali Hassan Mwinyi akiongea machache kwenye hafla ya kuwaapisha Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe na Skauti Mkuu wa Tanzania Ndg. Mwantumu Bakari Mahiza Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018.
\
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Skauti Mkuu wa Tanzania Ndg. Mwantumu bakari Mahiza Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe kuwa Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na Mdhamini wa Chama cha Skauti Tanzania Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi Rais wa Chama cha Skauti na Waziri wa Elimu, sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Technolojia Dr. leonard Akwilapo,  Skauti Mkuu Ndg. Mwantumu Bakari Mahiza, Mama Anna Abdallah, Mwenyekiti wa Chama cha Skauti nchini Mhe. Abdulkadir Shah na makamishna wa Skauti na Girl Guide  kwenye hafla ya kuwaapisha Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe na Skauti Mkuu wa Tanzania Ndg. Mwantumu Bakari Mahiza Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na Rais Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai, waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga, naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro, Katibu Mkuu kiongozi Balozi John Kijazi na Skauti Mkuu Ndg. Mwantumu Bakari Mahiza pamoja na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama  baada ya kuwaapisha Katibu Mkuu Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe na Skauti Mkuu wa Tanzania Ndg. Mwantumu Bakari Mahiza Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 20 Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 3, 2018. Picha na IKULU

WAZIRI MPANGO APOKEA RIPOTI TATHMINI YA UTENDAJI WA PPRA

$
0
0

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango akizungumza wakati alipokuwa akipokea ripoti ya tathmini ya utendaji ya Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kwa mwaka wa fedha 2017/18 leo jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango akizungumza wakati alipokuwa akipokea ripoti ya tathmini ya utendaji ya Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kwa mwaka wa fedha 2017/18 leo jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Balozi Matern Lumbanga akiwasilisha ripoti ya tathmini ya utendaji wa PPRA kwa mwaka wa fedha 2017/18, leo jijini Dodoma.Kushoto ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Mhandisi. Ayoub Kisuwi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti na Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Balozi Matern Lumbanga akiwasilisha ripoti ya tathmini ya utendaji wa PPRA kwa mwaka wa fedha 2017/18, leo jijini Dodoma.Kushoto ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Mhandisi. Ayoub Kisuwi.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa ununuzi wa Umma (PPRA) wakifuatilia ripoti ya tathmini ya utendaji wa PPRA kwa mwaka wa fedha 2017/18, leo jijini Dodoma.
Baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa ununuzi wa Umma (PPRA) wakifuatilia ripoti ya tathmini ya utendaji wa PPRA kwa mwaka wa fedha 2017/18, leo jijini Dodoma.
Baadhi ya watendaji kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia kikao baina ya Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango (hayupo pichani) na Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) leo jijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango akizindua ripoti ya tathmini ya utendaji ya Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kwa mwaka wa fedha 2017/18 leo jijini Dodoma.Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA Balozi Matern Lumbanga.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango(mwenye tai nyekundu) akiteta jambo na wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) mara baada ya kupokea ripoti ya ripoti ya tathmini ya utendaji ya PPRA kwa mwaka wa fedha 2017/18 leo jijini Dodoma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA Balozi Matern Lumbanga.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Phillip Mpango(mwenye tai nyekundu) akiteta jambo na wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) mara baada ya kupokea ripoti ya ripoti ya tathmini ya utendaji ya PPRA kwa mwaka wa fedha 2017/18 leo jijini Dodoma. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA Balozi Matern Lumbanga.

Wiki ya Huduma kwa Wateja wa Tigo

$
0
0
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Tigo, Mwangaza Matotola (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja ambapo wafanyakazi wa Tigo waliwatembelea wateja mitaani na kukusanya maoni yao kuhusu huduma zake. Kulia ni Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa pamoja na wafanyakazi wa kitengo cha huduma kwa wateja.
 Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa (kati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja ambapo wafanyakazi wa Tigo waliwatembelea wateja mitaani na kukusanya maoni yao kuhusu huduma zake. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Tigo, Mwangaza Matotola pamoja na wafanyakazi wa kitengo cha huduma kwa wateja .
 Msaidizi wa Huduma za Tigo, Plasidia Jameson (kati) pamoja na Msaidizi wa Ubora wa Huduma za Tigo, Kejiya Thangal (kulia) wakielezea baadhi ya huduma za Tigo kwa mfanyabiashara wa soko la Mwenge, Dismas Msauthi (kushoto), hii ikiwa kwa nia ya kuboresha utoaji huduma kama sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
 Afisa wa Huduma kwa Wateja wa Tigo, Wilfred Nestory (kushoto) akielezea baadhi ya huduma za Tigo kwa wafanyabiashara wa soko la Mwenge, Joseph Luseba (kulia)  na Samuel Gervas (kati), hii ikiwa kwa nia ya kuboresha utoaji huduma kama sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
 Meneja Mauzo wa Tigo – Kinondoni, Aznat Mboya (kushoto) akikusanya maoni na kuelezea baadhi ya huduma za Tigo kwa Juma Ibrahim mkaazi wa Mlalakuwa na Mohammed Sultan wa Manzese Dar es Salaam kwa nia ya kuboresha utoaji huduma, hii ikiwa kama sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.
Kiongozi wa Timu wa Huduma kwa Wateja ya Tigo, Jackson Jerry (kulia) pamoja na Meneja Mauzo wa Tigo – Kinondoni Aznat Mboya (aliyesimama kati) – Kinondoni, Aznat Mboya (kushoto) wakikusanya maoni na kuelezea baadhi ya huduma za Tigo kwa Elizabeth Simon wa Mwenge Dar es Salaam kwa nia ya kuboresha utoaji huduma, hii ikiwa kama sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja.

RAIS MAGUFULI ATOA UJUMBE KWA SKAUTI MKUU WA TANZANIA, MWANTUMU MAHIZA

BODI YA BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAHITIMISHA ZIARA YAKE YA KUKAGUA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA UBIA WA KILIMO TANZANIA.

$
0
0


Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafasi (TPSF) Bw. Salum Shamte ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa Baraza la Kilimo Tanzania (ACT) akimuonyesha Mwenyekiti wa Baraza la kilimo Tanzania (ACT) Dkt Sinare Yusuph (katikati) Barua kutoka Benki ya Kilimo inayokataa kuwapatia Mkopo wakulima wa Kijiji cha Minepa Wilayani Ifakara kwa kile walichodai mpaka wakulima hao wawe na hati miliki ya Mashamba hayo kitu kinachotajwa kuwa si sahihi, ambapo wajumbe wa bodi wameazimia kulifanyika kazi suala hilo.
Afisa Mauzo wa Kampuni ya Lonagro inayojihusisha na uuzaji wa zana za Kilimo hifadhi Bw Ray Travas akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Baraza la Kilimo Tanzania waliofika ofisini kwake Mjini Arusha ambapo alisema bado kuna mwitikio mdogo kwa wakulima kutumia zana za kisasa katika kilimo kutokana na uzalishaji wao kuwa mdogo huku pia wakikwamishwa na bei za mazao ambazo zimekuwa chini zaidi.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafasi (TPSF) Bw. Salum Shamte ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa Baraza la Kilimo Tanzania (ACT),akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Tanzania Bi Janeth Bitegeko na wakulima mbalimbali katika moja ya ziara ya wajumbe wa bodi ya ACT kukagua miradi inayosimamiwa na Ubia wa Kilimo Tanzania (TAP).
Mkurugenzi wa kampuni ya Siza Agro Processing iliyoko Mjini Mufindi inayojishughulisha na kukoboa na kupaki kwa viwango tofauti bidhaa za mchele na unga akiwaonyesha wajumbe wa Bodi bidhaa ya Mchele inayozalishwa na Kiwanda chake, ingawa kwa sasa anasema shughuli za uzalishaji katika kiwanda hicho chenye mashine za kisasa unasuasua.
Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya baraza la kilimo wakiwa ndani ya ghala la kuhifadhia mazao lililojengwa na ACT/TAP aktika kijiji cha katurikila wialyani Mufindi Mkoani Iringa.

Kaimu Mkurugenzi wa halimashuari ya Arumeru Bi grace Mbilinyi akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Baraza la Kilimo Tanzania walipotembelea ofisini kwake ambapo ameshukuru kwa miradi inayotekelezwa na ACT wilayani humo ikiwemo ya ujenzi wa maghala ya kuhifadhia mazao.

Mjumbe wa bodi ya bazaar la kilimo Tanzania Bw. Enock Ndondole akiwasisistiza wakulima wa kijiji cha Minepa Wilayani Ifakara Mkoani Morogoro umuhimu wa kusambaza teknlojia wanayoitumia kwenye Kilimo cha Mpunga ya Kilimo shadidi ili wakulima wengi zaidi waweze kutumia teknlojia hiyo ambayo inamfanya mkulima kupata mazao mengi zaidi.
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live




Latest Images