Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga (katikati) akimkabidhi cheti cha Stashahada cha Kuhitimu Mafunzo ya Kilimo na Ufugaji,Rais wa Chuo cha chuo cha Kilimo na ufugaji cha Kaole,Glorious Kalabamu (kushoto) katika Mahafali ya tatu ya chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani jana. Kulia ni Mjumbe wa Baraza la Wazazi la CCM Mkoa wa Pwani,Dk.Zainab Gama na Mkuu wa Chuo hicho,Sinami Simba. Picha zote na Elisa Shunda
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga (katikati) akimkabidhi cheti cha Stashahada cha Kuhitimu Mafunzo ya Kilimo na Ufugaji,Rais wa Chuo cha chuo cha Kilimo na ufugaji cha Kaole,Asnat Kasukuru (kushoto) katika Mahafali ya tatu ya chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani jana. Kulia ni Mjumbe wa Baraza la Wazazi la CCM Mkoa wa Pwani,Dk.Zainab Gama na Mkuu wa Chuo hicho,Sinami Simba (mwenye shati la bluu).
NA ELISA SHUNDA,BAGAMOYO
UMOJA wa wazazi taifa ya Chama cha Mapinduzi CCM, imeahidi kuendelea kusaidia kuboresha chuo cha Kilimo na ufugaji cha Kaole ili kiendane na adhi ya kuwa chuo bora kitakachotambulika kitaifa na kimataifa pamoja na kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya Tano wa kuelekea kwenye manufaa ya uchumi wa viwada nchini.
Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam, na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa wa Wazazi Taifa kutokea Zanzibar, Najma Murtaza Giga alipokuwa mgeni rasmi katika mahafari ya tatu ya chuo hicho yaliyofanyika Chuoni kaole-Bagamoyo mkoani Pwani.
Giga ambaye pia ni mbunge na mwenyekiti wa kamati ya Bunge kwenye bunge la jamuhuri ya muungano wa Tanzania, amewapongeza walimu na watumishi mbalimbali waosimamia chuo hicho kwa kufanya kazi kwenye werefi mkubwa wa kuongeza idadi ya wahitimu katika chuo hicho kwa mwaka huu kufikia 108 tofauti na mwaka jana ambao wahitimu walipungua kufikia 72.
‘’ki ukweli chuo chetu kinachosimiwa na umoja wa wazazi taifa ya chama cha mapinduzi CCM, kinapaswa kijitangaze na kipewe sapoti kubwa hasa kwa wazaz, walezi, wadau na serikali kwa ujumla ili kiwe na hadhi kama vyuo vingine na kiiendane na kasi ya serikali ya awamu ya tano ya Dr. John Magufuli” alisema Giga.
Akizungumzia kuhusiana na suala la ajira katika serikali ya awamu ya tano, Giga aliwataka watafunzi wanaosoma katika chuo hicho na wale waliohitimu kwamba wasiwe na wasiwasi kuhusiana na suala hilo kwani najira kwao itapatikana pia hakusita kuwatakawanafunzi hao kwamba wasikimbilie kuajiriwa peke yao bali wahakikishe wanakuwa na m binu mbadala wa kujiajiri na kutoa elimu hiyo kwa vijana wengine waliopo mitaani.
Hata hivyo Katibu mkuu huyo wa wazazi taifa kutokea Zanzibar, ametoa kiasi cha zaidi ya sh. Milioni 1.5 ni ahadi yake aliyoaidi hivi karibuni hivyo zitakwenda kununulia madawati katika chuo hicho.
Kwa upande wake mkuu wa chuo hicho, Sinani Simba amesema chuo hicho kinatoa kozi mbalimbali ikiwemo kozi ya Kilimo na Miufugo ngazi ya Astashahada na Shahada (Cheti na Diproma).
Amezungumzia kuhusu kilimo, Simba amesema chuo cha Kaole cha Kilimo na Mifugo kinachomilikiwa na umoja wa wazazi Taifa , hamesema tangu chuo kicho kianzishwe Desemba 15 mwaka 2015 hakijawai kutambulika vizuri ndani ya jamii ingawa kuna azina tosha ya wataalu na walimu, hivyo chuo hicho kinampango wa kujitangaza zaidi kusudi kiweze kuwa chuo cha kimataifa.
Akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wenzake, Exavery Mwakilema amesema chuo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo suala la ukosefu wa ajira kwa wanafunzi wanaomaliza chuoni hapo, Upungufu wa vitambu katika maktaba, Mifugo hasa ng’ombe wa maziwa na vifaa vya michezo.
Jumla ya wahitimu 108 wa mwaka wa tatu wa ngazi Cheti na diploma katika fani ya Kilimo na Mifugo leo wamehitimu masomo yao katika chuo hicho na huku wakiahidi wanaporudi ulaiyani watakuwa mabalozi bora kwa kutoa elimu kwa vijana wenzao .
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga (katikati) akiwaongoza wahitimu kuingia katika viunga vya chuo kuanza sherehe za mahafali hiyo.
Wahitimu wakicheza na kufurahi wakati wakiingia katika viunga vya chuo cha Kilimo na mifugo cha Kaole cha Umoja wa wazazi wilayani Bagamoyo tayari kuanza hafla hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga akizungumza katika sherehe za mahafali ya chuo hicho. Kushoto ni Mkuu wa Chuo hicho,Sinani Simba na Mjumbe wa Baraza la Wazazi CCM Mkoa wa Pwani,Dk.Zainab Gama.
Baadhi ya wahitimu wa ngazi ya Astashahada na Stashahada wakimsikiliza kwa umakini Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga (hayupo pichani) wakati akizungumza katika mahafali hayo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani,Jackson Mtuka akizungumza katika mkutano huo.
Baadhi ya wahitimu wa ngazi ya Astashahada na Stashahada wakimsikiliza kwa umakini Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani,Jackson Mtuka (hayupo pichani) wakati akizungumza katika mahafali hayo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Mkoa wa Pwani,Gama Juma Gama akizungumza katika mkutano huo.
Baadhi ya wananchi na ndugu waliohudhuria katika shughuli hiyo ya mahafali wakifuatilia kwa umakini matukio yote yanayofanyika katika viunga vya chuo hicho.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM wa Wilaya ya Bagamoyo,Abubakar Mlawa akizungumza katika mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu wa ngazi ya Astashahada na Stashahada wakifuatilia kwa umakini matukio yanayoendelea katika eneo hilo.
Mwanafunzi na Msoma Risala kutoka upande wa Wanachuo Wahitimu,Exavery Mwakilema akisoma changamoto zinazoikabili chuo hiko.
Wahitimu wa Masomo ya Mifugo wakila kiapo katika mahafali hayo.
Burudani zikiendelea chuoni hapo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi wa CCM Kibaha Mjini,Edwin shunda akimpongeza msanii aliyekuwa akiburudisha katika mahafali hayo.
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga akicheza muziki na wahitimu katika mahafali hayo.
Wahitimu wakicheza muziki aina ya kwaito katika mahafali hayo.
Mgeni Rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga akiwa kwenye picha ya pamoja na wakufunzi na wageni waalikwa baada ya kumalizika kwa shughuli hiyo ya mahafali ya tatu ya Chuo cha Kilimo na Ufugaji cha Kaole Bagamoyo.
Mkuu wa Chuo cha Kilimo na Ufugaji cha Kaole kilichopo Bagamoyo,Sinani simba,akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga na wageni waalikwa wengine kuhusu maendeleo ya chuo hicho na historia yake tangu kuanzishwa kwake na mazingira yake kwa ujumla.
mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga akiwa katika picha ya pamoja na Wahitimu na wageni waalikwa.
mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga akiwa katika picha ya pamoja na wananchi na ndugu mbalimbali wa wahitimu.
Mkuu wa Chuo cha Kilimo na Ufugaji cha Kaole kilichopo Bagamoyo,Sinani simba,akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa kutoka Zanzibar,Najma Murtaza Giga na wageni waalikwa wengine kuhusu wanachuo wanavyofanya mazoezi kwa vitendo katika shamba darasa lililopo chuoni hapo.