Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

AQRB YATAKIWA KUJITANGAZA - MAJALIWA

$
0
0
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amezungumzia juu ya umuhimu wa Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), kutangaza huduma wanazotoa za ujenzi ili kuwawezesha wananchi kuelewa na kuzitumia huduma hizo na hivyo kuboresha Sekta ya Ujenzi hapa nchini.

Akifungua semina ya siku mbili ya maadhimisho ya ishirini na tisa ya elimu endelevu kwa Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi jijini Dodoma, Waziri Mkuu amewataka wataalam hao kujiendeleza kitaaluma ili watoe huduma bora zaidi zinazouwiana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

‘Ongezeni wigo wa huduma zenu ndani na nje ya nchi ili huduma za ujenzi bora wa makazi katika miji na majini ziwe endelevu na zenye gharama stahiki”, amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.Waziri Mkuu ameisisitiza bodi ya AQRB kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya sayansi na mafunzo ya ujenzi ili kuongeza idadi ya wanataaluma wanaoweza kujiajiri na kuajiri watu wengine.

Aidha, amehimiza Wizara ya Ujenzi kushirikiana na Wizara ya Afya na Tamisemi katika ujenzi wa vituo vya afya vya kisasa katika mikoa na halmashauri mbalimbali nchini.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kulia), akikata utepe kuashiria makabidhiano ya mashine 10 za kufyatulia matofali zilizotolewa na Bodi ya Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), kabla ya kufungua semina ya 29 ya wataalam hao, Mkoani Dodoma. Wa tatu kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akimsikiliza mwanafunzi wa mwaka  wa 4 wa kozi ya Usanifu Majengo, Kutoka Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), Mwita Mgaya, kuhusu ujenzi wa kisasa wa majengo wakati Waziri Mkuu huyo alipotembelea banda  la chuo hicho kabla ya kufungua semina ya 29 ya wataalam hao, Mkoani Dodoma, kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.
 Wajumbe wa Semina ya Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Wakimsikiliza Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (hayupo pichani), wakati akifungua mkutano huo wa siku 2 uliowakutanisha wataalam kujadili Mustakabali wa Viwanda nchini na namna ya kutunza majengo ya kale mkoani Dodoma.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akifungua semina ya 29 ya Bodi ya Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi (AQRB), Mkoani Dodoma, wa kwanza kulia ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa  (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Wasanifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi baada ya kufungua semina ya 29 ya wataalam hao, Mkoani Dodoma. Wa tatu kushoto ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa.


NEWS ALERT: CHINA YAIPIGA JEKI TANZANIA YA BILIONI 146.47 KWA UJENZI WA CHUO KIKUU CHA USAFIRISHAJI NA UPEMBUZI YAKINIFU UJENZI WA RELI YA STANDARD GAUGE

$
0
0

Na Benny Mwaipaja, WFM-Dar es Salaam

Serikali ya Tanzania imetiliana saini na Serikali ya China mkataba wa msaada wa kiasi cha Shilingi Bilioni 146.47. Mkataba huo umesainiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dotto James na Balozi wa China nchini Wang Ke Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo Katibu Mkuu alisema kuwa fedha hizo ni msaada na siyo mkopo na zitatumika katika miradi miwili ya miundombinu. Mradi wa kwanza ni ujenzi wa Chuo Kikuu cha Usafirishaji cha Taifa (NIT) ambacho kitajengwa Mabibo Jijini Dar es Salaam kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 62 sawa na takriban Shilingi bilioni 138.3.

Mradi wa pili ni kwa ajili ya kusaidia upembuzi yakinifu na upembuzi sanifu wa mradi wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa (SGR), ambapo kiasi cha Sh. bilioni 3.2 kimetengwa kwa ajili hiyo.

Bw. Doto James alisema kwa sasa mradi wa ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha Kimataifa umeanza kwa awamu mbili ambazo moja ni kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro, na kuanzia Morogoro hadi Makutopora-Dodoma, upembuzi yakinifu utakaofanywa na Serikali ya China ni kwa maeneo mengine ya ujenzi wa Reli hiyo kuanzia Dodoma, Tabora hadi Mwanza na Kuanzia Kaliua hadi Kigoma.

"China imetusaidia miradi mingi ikiwemo mradi wa maji Chalinze, Ujenzi wa uwanja wa Michezo wa Taifa, Mradi wa teknolojia za Kilimo mkoani Morogoro, Kituo cha upasuaji wa moyo na mafunzo, Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Nyerere pamoja na misaada ya dawa na vifaa tiba" alieleza Bw. James

Kwa upande wake Balozi wa China hapa nchini, Wang Ke, Alisema kuwa China inategemea kuona kuwa msaada huo utasaidia kuimarisha maendeleo na kuisaidia Tanzania kupata maendeleo haraka.

Aidha alisema China itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kutekeleza miradi mbalimbali ya kimaendeleo ambayo itawasaidia Watanzania na kuendeleza urafiki uliopo kati ya nchi hizi mbili.

Balozi Wang Ke, amesema Pia Serikali ya China na Tanzania zinaendelea majadiliano kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, na kuongeza kuwa majadiliano hayo yatakapokamilika nchi yake itasaidia ujenzi wa bandari hiyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Usafirishaji Taifa (NIT) Prof. Zacharia Mganilwa ameishukuru Serikali ya China kwa msaada huo na kusema kuwa msaada huo utaisaidia chuo hicho kuweza kutoa wataalamu wa kutosha kuweza kushiriki katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo sekta ya anga.

Amebainisha kuwa Chuo hicho Kikuu kitatoa mafunzo kwenye fani muhimu na zinazohitajika ikiwemo ufundi wa reli, masuala ya anga na sekta nyingine mtambuka kwa kutoa wataalamu waliobobea watakao changia kufanikisha azma ya Serikali ya uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake Kaimu Naibu Mkurugenzi Uendeshaji wa Shirika la Reli Tanzania-TRC, Bw. Focus Msasani ameeleza kuwa msaada huo wa shilingi bilioni 3.22, utasaidia kuipunguzi serikali gharama ilizokuwa izitumie kwa kazi hiyo kenye mradi mkubwa wa kihistoria wa ujenzi wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa.
 Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Mhe. Wang Ke wakitia saini mkataba wa msaada wa kifedha ambapo serikali ya China itaisaidia Tanzania jumla ya shilingi Bilioni 146.47  kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji pamoja na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard gauge. Hafla hii fupi imefanyika Ofisi za Hazina jijini Dar es salaam leo  Jumamosi Mei 19, 2018
 Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Mhe. wang Ke wakibadilishana mikataba baada ya kuitia saini makubaliano ambapo serikali ya China itaisaidia Tanzania jumla ya  shilingi Bilioni 146.47  kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji pamoja na  upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard gauge. Hafla hii fupi imefanyika Ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam leo  Jumamosi Mei 19, 2018 
Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James akiagana na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Mhe. Wang Ke baada ya wawili hao kutia saini kwa niaba ya nchi zao wa mkataba wa msaada wa kifedha ambapo serikali ya China itaisaidia Tanzania jumla ya shilingi Bilioni 146.47 kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Usafirishaji  pamoja na  upembuzi yakinifu wa ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard gauge. Hafla hii fupi imefanyika Ofisi za Hazina jijini Dar es salaam leo  Jumamosi Mei 19, 2018. Picha na IKULU.

DONGOBESH FC YAICHAPA STAND FC YA HAYDOM GOLI 1-0 NA KUTINGA NUSU FAINALI KOMBE LA KURUGENZI CUP 2018

$
0
0
 Mchezaji wa timu ya Dongobesh FC Antipas Vicent akiwa amebebwa juu juu na mchezaji mwenzake mara baada ya kumalizika kwa mchezo katika yake na timu ya Stand FC ya Mjini Haydom ambapo mchezaji huyo ndiye aliyeifungia timu yake goli 1-0 na timu ya Dongobeshi kufanikiwa kuingia nusu fainali katika michuano ya Kurugenzi Cup 2018 linaloandaliwa na Halmashauri ya wilaya ya Mbulu, Mchezo huo umefanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Haydom.ikidhaminiwa na Kiwanda cha maziwa cha ASAS cha Iringa.
 Wachezaji wa timu ya Dongobash FC wakisikiliza maelezo ya Mmoja wa Waratibu wa michuano hiyo Bw. Phars Nyanda wakati akiwapa utaratibu mara baada ya mchezo huo kumalizika.
 Benchi la Ufundi la Timu ya Dongobesh FC likinyanyuka juu na kushangilia mara baada ya kuifunga timu ya Stand FC ya mjini Haydom katika mchezo uliofanyika leo jioni kwenye uwanja wa Shule ya Msingi ya Haydom.
 Golikipa wa timu ya Stand FC ya mjini Haydom akisaidiwa na wenzake mara baada ya kuumia wakati wakiwania mpira uliokuwa unaingia golini mwake katika mchezo huo.
 Hekaheka golini mwa timu ya Stand FC ya mjini Haydom wakati wachezaji wa timu ya Dongobesh FC wakiliandama goli la wapinzani wao.

CRDB BANK WALIVYOSHIRIKI NA KUTOA HUDUMA KWENYE MAONESHO YA WAJASIRIAMALI WA ILALA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Meneja Biashara wa CRDB Bank, Tawi la Vijana, Zaituni Manora, akitoa sera za benki hiyo kwa wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, wakati wa ufunguzi wa maonesho yao, yaliyofunguliwa na Mkuu wa Wilaya Ilala, Sophia Mjema, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya wafanyakazi wa CRDB Bank, wakiwa katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.  
Baadhi ya wafanyakazi wa CRDB Bank, wakiliandaa gari la kutolea huduma za kibenki katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo. 
Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo akimwelekeza mmoja wa wananchi aliyefika kwenye banda la benki hiyo katika maonesho hayo, jinsi ya kujaza fomu za miamala ya kifedha ya benki hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa CRDB Bank, wakiwa katika picha ya pamoja ndani ya banda lao katika maonesho hayo, wakiwa tayari kutoa huduma kwa wajasiriamali pamoja na wananchi kwenye maonesho hayo, Viawanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.   
Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo akiwapatia maelezo baadhi ya wananchi waliofika kwenye banda la benki hiyo katika maonesho hayo, jijini Dar es Salaam leo.
Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo (kulia), akimpatia maelezo mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Ilala, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (kushoto), wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya huduma za kifedha pamoja na ya wajasiriamali kabla ya kuyafungua. 
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema (kushoto), akimwuliza jambo Ofisa Mikopo wa CRDB Bank, Josephat Shimo (kulia), akiwa kwenye banda la benki hiyo, wakati akitembelea mabanda mbalimbali ya huduma za kifedha pamoja na ya wajasiriamali kabla ya kuyafungua maonesho hayo.  
Ofisa Huduma kwa wateja wa CRDB Bank, Makao Makuu, Richard Tangazo (kushoto), akimpatia maelezo mmoja wa wajasiriamali aliofika kwenye banda la benki hiyo, katika maonesho hayo.
Mgeni rasmi katika ufunguzi wa maonesho ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, akiwa meza kuu pamoja na baadhi ya Madiwani wa Manispaa ya Ilala kabla ya kuyafungua maonesho hayo.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omar Kumbilamoto, akizungumza wakati akimkaribisha mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema kuzungumza katika ufunguzi wa maonesho hayo. 
Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, akizungumza na wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala, wakati akiyafungua maonesho yao, viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii, Diwani wa Gongolamboto, Jakob Kisi, akimkabidhi cheti cha kutambua mchango wa CRDB Bank, Meneja Biashara, Tawi la Vijana, Zaituni Manora, wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo. CRDB Bank, ni moja ya waliodhamini na kufanikisha maonesho hayo ya wajasiriamali wa Manispaa ya Ilala.

JAFO ATOA SIKU TANO KWA HALMASHAURI 10 KUJIELEZA KUHUSU MATUMIZI YA FEDHA ZA MIRADI YA AFYA

$
0
0
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Selemani Jafo akifungua kikao kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotekelezwa chini ya Mamlaka za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kilichowajumuisha Makatibu Tawala kutoka mikoa yote nchini.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mhandisi Mussa Iyombe akimkaribisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Selemani Jafo kufungua kikao kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotekelezwa chini ya Mamlaka za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kilichowajumuisha Makatibu Tawala kutoka mikoa yote nchini.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Makatibu Tawala za Mikoa.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Selemani Jafo akivishwa beji ya heshima kutokana na utendaji kazi wake.
 Wajumbe wa kikao kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotekelezwa chini ya Mamlaka za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kilichowajumuisha Makatibu Tawala kutoka mikoa yote nchini.
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Dk.Zainab Chaula akizungumza katika kikao kazi juu ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotekelezwa chini ya Mamlaka za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kilichowajumuisha Makatibu Tawala kutoka mikoa yote nchini.
...................................................................................................

Zulfa Mfinanga na Magdalena Stanley

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Seleman Jafo ametoa siku tano
kwa wakurugenzi na waganga wakuu wa halmashauri 10 nchini kutoa
maelezo ya kina kwa nini halmashari hizo hazijafika asilimia kumi ya
matumizi ya fedha za miradi ya afya.

Jafo ameyasema hayo leo wakati akifungua kikao kazi juu ya utekelezaji
wa miradi ya afya inayotekelezwa chini ya Mamlaka za Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa kilichowajumuisha Makatibu Tawala kutoka mikoa yote
nchini.

Amesema halmashauri hizo zimeshindwa kutumia fedha zilizotolewa kwa
ajili ya miradi ya afya kama inavyotakiwa ambapo matumizi yake
yanaonekana kuwa chini ya kiwango, huku akizitaja halmashauri hizo kuwa
ni halmashauri ya wilaya ya Karatu, Mpimbwe, Mbulu Dc, Songwe,
Simanjiro, Mkinga, Mkuranga, Namtumbo, Nzega Dc pamoja na Kilindi.

“Halmasharu hizi zina kila dalili ya kupata hati chafu, naagiza hadi kufika
siku ya Jumatano niwe nimepata majibu ya kuridhisha ni kwanini
hawajatumia fedha walizopewa kama maelezo yanavyotaka, tukiacha
kufanya kazi kwa mazoea tutapata matokeo mazuri, lakini kwa hali hii
tusitegemee matokeo mazuri kwa baadhi ya maeneo” Alisema Jafo

Kuwa upande mwingine Waziri Jafo aliwaagiza Makatibu Tawala hao
kuwaelekeza wakurugenzi wa halmashauri nchini kuwekeana malengo na
watumishi wao kwa kuwafanya tathmini ya uwajibikaji kila mwaka ili
kuongeza ufanisi na uwajibikaji kazini kwani bado wapo baadhi ya
watumishi wanafanya kazi kwa mazoea.

Amesema kuwa iwapo mtumishi wataonekana amefanya kazi chini ya
kiwango cha alama 50 kama ni mkuu wa idara atawajibishwa kwa
kushushwa cheo, na yule ambaye ataonekana kufanya vizuri zaidi alishauri
anastahili kupewa zawadi ya mfanyakazi bora wakati wa maadhimisho ya
siku ya wafanyakazi Duniani-Mei Mosi.

Aidha Waziri Jafo amesema kwa sasa kipaumbele cha utoaji wa fedha
kwa ajili ya miradi ya maendeleo zitatolewa kwa kuzingatia kipimo cha
matokeo mazuri kwa halmashauri husika, kwani kwa kufanya hivyo
itasaidia kuongeza uwajibikaji.

Wakati huo huo Waziri huyo aliagiza halmashauri zote nchini kuweka
mfumo wa matumizi ya mfuko wa afya ya jamii wa CHF iliyoboreshwa
sambamba ya kuhimiza matumizi ya ukusanyaji wa mapato wa njia ya
kimtandao ili kuepuka upotevu wa fedha za serikali.

Akizungumzia mafanikio ya mfuko huo Mratibu wa mfuko wa afya ya jamii
TAMISEMI, Nkinda Shekalaghe amesema kuwa hadi sasa mfuko huo
haujafikia lengo lililowekwa na serikali la kuunganisha wananchi kwa
asilimia 30 hadi kufikia mwaka 2015, kwani kwa mwaka 2016/2017
wamefikia asilimia 24.

Alitaja baadhi ya changamoto zinazoukabili mfuko huo kuwa ni pamoja na
utayari wa wananchi kujiunga na mfuko, huduma duni za afya, kutokuwepo
kwa mfumo rasmi wa utoaji wa taarifa pamoja na kiwango kidogo cha
uchangiaji ambapo amesema tayai wameshachukua hatua mbalimba
katika kukabiliana na changamoto hizo.

SERIKALI YAKANUSHA KUONGEZEKA KWA DENI LA TAIFA

KAMATI YA KUDUMU BUNGE YA ARDHI NA MAENDELEO YA MAKAZI YATEMBELEA MRADI WA KURASIMISHA MAKAZI KIMARA KILUNGURE

$
0
0
 Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi, akizungumza na Wananchi wa kata ya Kilungule mara alipofanya ziara na Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi na Maliasili kujionea namna mradi wa urasimishaji makazi ulivyofanyika katika eneo hilo.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili , Nape Nnauye akizungumza na Wakazi wa Kilungule wakati walipofanya ziara kukagua mradi wa urasimishaji Ardhi unaotekelezwa na Wizara ya Ardhi
 Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kilungule A,Emanuel Komba akizungumza jinsi mradi huo ulivyokuwa rafiki kwa wakazi wa eneo hilo .
 Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili , Nape Nnauye katika eneo Kilungule A mahali ambapo watu wa eneo hilo wamerasimishwa makazi yao.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili , Nape Nnauye akiwa na baadhi ya Wabunge ambao ni Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu na Ardhi na Maliasili
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Ardhi Maliasili , Nape Nnauye akiwa na Waziri wa Ardhi William Lukuvi  pamoja na Wajumbe wa kamati hiyo

DC LUSHOTO AWATAKA MADIWANI KUKAGUA MIRADI INAYOTEKELEZWA KWENYE MAENEO YAO

$
0
0
 MKUU wa wilaya ya Lushoto January Lugangika akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani cha Halmashauri ya Bumbuli ambacho kwa mara ya kwanza kilifanyika eneo la makao makuu ya Kwehangara
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bumbuli Peter Nyalali akizungumza katika kikao cha robo ya mwaka cha Baraza la Madiwani kilichofanyika eneo Jipya la Makao Makuu ya Halamshauri hiyo Kwehangala kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Amiri Sheiza
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bumbuli Amiri Sheiza akizungumza katika kikao hicho kwa kuwataka wananchi kuwa wamoja kuhakikisha halmashauri hiyo inbapata mafanikio kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauti ya Bumbuli Peter Nyalali
 Mkurugenzi wa Halmashauti ya Bumbuli Peter Nyalali kushoto akiwa na Mwenyekiti wa Halma shauri ya Bumbuli Amiri Sheiza wakifuatilia hoja mbalimbali kwenye kikao hicho
 Mkuu wa wilaya ya Lushoto January Lugangika kulia akipitia makabrasha kwenye kikao hicho
 Sehemu ya madiwani wakifuatilia kikao hicho
 Sehemu ya wananchi waliopata fursa ya kuhudhuria baraza hilo 

MKUU wa wilaya ya Lushoto mkoani Tanga January Lugangika amewataka madiwani wa halmshauri ya Bumbuli kuhakikisha wanashiriki katika kukagua miradi inayotekelezwa kwenye maeneo mbalimbali ili kuiepusha kujengwa chini ya kiwango na hivyo kukosa tija kwa wananchi.

Agizo hilo alilitoa juzi wakati akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani cha kawaida cha robo tatu kilichofanyika kwa mara ya kwanza katika makao makuu mapya ya halmashauri hiyo eneo la Kwehangara.

Alisema iwapo madiwani hao watashindwa kukagua miradi hiyo inatoa mwanya kwa wakandarasi kushindwa kuitekeleza kwa viwango vinavyotakiwa hali inayopelekea kukosa tija na thamani halisi ya fedha zinazotumika. “Ndugu zangu madiwani hakikisheni mnakagua miradi ya maendeleo hili ndio jukumu lenu la msingi kwani msipofanya hivyo ndipo wakandarasi wanafanya miradi hiyo isiwe na tija na hivyo matokeo yake gharama inayotumika inakosa thamani yake”Alisema DC Lugangika.

Aidha pia alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Peter Nyalali kuweka utaratibu mzuri kwa madiwani ili waende kukagua miradi inayotekelezwa hususani miradi ya maji ambayo imekuwa ikihujumiwa kutokana na wakandarasi”Alisema.Nay kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bumbuli Amiri Sheiza alisema wanamshukuru Rais John Magufuli kwa kuwasaidia kuwatatulia mambo mawili makubwa kwao kuyapatia ufumbuzi.

Alisema suala la kwanza ni ujenzi wa Jengo la Halmashauri eneo la Kwehangara na pili ni ufunguzi wa kiwanda cha Mponde katika mambo hayo ameonyesha namna anavyotujali.“Hivyo tunamuomba Mungu amuongezee hekima na busara katika kuiendesha nchi na pia napenda kumthibitishia Rais kwamba wananchi, Baraza la Madiwani pamoja na kupishana kifikra bado tupo pamoja kufanya kazi bila kubaguana”Alisema.


Hata hivyo alionya kuwa mtu ambaye ataanzisha vimaneno kuhusu suala hilo watamchukulia hatua kali kwa sababu atakuwa hana nia njema na wananchi wa halmashauri hiyo katika kuwaletea maendeleo.


“Nionyesha mtu yoyote atakayeleta vimaneno kuhusu suala hili sisi hatutamvumilia tutamchukulia hatua kali kwani wana Bumbuli na mbunge wetu sote pamoja “Alisema.

(Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

HALI YA UPATIKANAJI WA DAWA MKOANI MBEYA NI ASILIMIA 91.5

$
0
0
 Ofisa Mauzo wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Mbeya, Rhoda Joseph (kushoto) na Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ilembo, Sk.Bwire Biseko (kulia), wakihesabu dawa wakati wa makabidhiano yaliyofanyika kituo hapa jana wilaya ya Mbeya Vijijini. Katikati ni mwanakamati ya Afya wa Kijiji cha Ilembo.
 Ofisa Mauzo wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Mbeya, Rhoda Joseph, akimkabidhi dawa mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Afya wa Kijiji cha Ilembo wakati wa zoezi la kukabidhiwa dawa hizo. Kulia ni Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ilembo, Sk.Bwire Biseko.
 Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Ilembo, Sk.Bwire Biseko akiangalia dawa hizo baada ya kukabidhiwa.
 Baadhi ya wafanyakazi wa MSD Kanda ya Mbeya wakionesha ishara ya mshikamano baada ya kuandaa mzigo wa dawa kwa ajili ya kwenda kuzisambaza kwenye vituo vya afya mkoani Mbeya.
 Baadhi ya wafanyakazi wa MSD Kanda ya Mbeya wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuandaa mzigo wa dawa kwa ajili ya kwenda kuzisambaza kwenye vituo vya afya mkoani humo.

Na Dotto Mwaibale, Mbeya

UPATIKANAJI wa dawa na vifaa tiba na vitendanishi vya maabara mkoani Mbeya umefikia asilimia 91.5 kwa mwezi huu wa Mei, kutokana na ongezeko la bajeti ya dawa kwa mwaka fedha 2017/2018.

Imeelezwa katika mwaka huo wa fedha bajeti imeongezeka kwa asilimia 20.6  kwa hospitali za wilaya na asilimia 51 kwa zahanati na vituo vya afya.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Dkt.Yahya Msuya ameeleza hayo wakati maofisa wa Bohari ya Dawa (MSD) walipotembelea wateja wa vituo vya Afya vitatu, vya Wilaya ya Mbeya vijijini wakati wa kusambaza dawa za mgawo wa mwisho wa mwaka wa fedha wa 2017/2018. 

Dkt. Msuya alisema ongezeko la asilimia 91.5 la upatikanaji wa dawa umeimarisha huduma za afya na na kupunguza malalamiko ya wananchi kuhusu kukosekana kwa dawa.

"Hospitali ya Rufaa ya Mbeya inahudumia wagonjwa wapatao 400 kwa siku; upatikaji wa dawa kwa sasa ni wa uhakika na uwepo wa maduka ya MSD  ni chachu ya kuimarika kwa huduma," alisema.

Alisisitiza kuwa utekelezaji wa agizo la serikali, la kutoa dawa za malaria bure kwa wananchi pamoja na dawa za msaada katika vituo vya afya na hospitaliti linafanyika.

Mfamasia wa Wilaya ya Mbeya, Apolinary Mwakabana alisema  pamoja na upatikanaji wa dawa kuridhisha kwa asilimia 91.5, jitihada zinahitaji ili kuwa na dawa zote, kwani  asilimia 9 ya dawa zinazokosekana hulazimika kuzitafuta nje ya bohari.

Alisifu ushirikiano wa kikanda uliopo kati ya halmashauri na MSD katika huduma hususani  kukiwa na mahitaji ya dharula.

Naye Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya cha Ilembo kilichopo Mbeya vijijini Sk.Bwire Biseko, alisema kwa siku kituo hicho kinahudumia wagonjwa 107 kutoka vijiji 10, vyenye wakazi zaidi ya wakazi 17,000.

Alisema uboreshaji wa huduma za afya katika upatikanaji wa dawa na vifaa tiba umeimarisha uchumi na huduma za afya kwa kuwa watu wengi hawamudu gharama za matibabu kutoka nje ya hospitali.

Ubia Enock ni kati ya wakazi ambao walijitokeza katika kamati ya afya ya Kijiji cha Ilembo kushuhudia makabidhiano ya dawa hizo ambapo alisisitiza haja ya serikali kuboresha huduma kwa watu wanaotumia bima za afya.

WASAIDIZI WA MAKAMU WA RAIS WATOA FUTARI KWA WATOTO YATIMA WA KITUO CHA RAHMAN DODOMA

$
0
0
Wasaidizi wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wametoa futari kwa kituo cha watoto Yatima cha Rahman kilichopo Chang’ombe Dodoma.

Kituo hicho chenye watoto 120 ambao kati ya hao 75 ni yatima ambapo hupatiwa Elimu ya Dini na Lugha.

Wasaidizi hao ambao waliwakilishwa na Kaimu Katibu wa Makamu wa Rais Bi. Maulidah Hassan na Msaidizi wa Masula ya Siasa Ndugu Nehemia Mandia kwa pamoja walisema imekuwa utamaduni wao kukutana, kuzungumza na kusaidia watoto yatima, watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na walemavu na wameahidi kuendelea kusaidia kila inapowezekana. 

Nae mwanzilishi wa Kituo hicho Bi. Rukia Hamisi ameshukuru kwa wasaidizi wa Mheshimiwa Makamu wa Rais kufika ofisini kwake na ameomba Mheshimiwa Makamu wa Rais akipata nafasi naye afike kituoni kwani watoto wanampenda sana pili alishukuru kwa futari.




RAIS DK. SHEIN AKUTANA NA BALOZI MPYA WA CANADA, CUBA

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na mgeni wake Balozi Mpya   wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Canada pia akiiwakilisha Tanzania nchini Cuba Mhe. Alphayo Kidata  alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kujitambulisha (Picha na Ikulu).
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na  mgeni wake Balozi  Mpya wa    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Canada pia akiiwakilisha Tanzania nchini Cuba Mhe. Alphayo Kidata  alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo kujitambulisha.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na  mgeni wake Balozi   Mpya wa    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Canada pia akiiwakilisha Tanzania nchini Cuba Mhe. Alphayo Kidata  baada ya mazungumzo yao alipofika kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza  la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akiagana na  mgeni  wake Balozi   Mpya wa    Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Canada pia akiiwakilisha Tanzania nchini Cuba Mhe. Alphayo Kidata  baada ya mazungumzo yao alipofika kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar leo.

RAIS DKT. MAGUFULI AWAPONGEZA WABUNGE STEPHEN MASELE (MAKAMU WA RAIS BUNGE LA AFRIKA) PAMOJA NA MBONI MHITA (RAIS WA CAUCUS YA VIJANA YA BUNGE LA AFRIKA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM)

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wabunge, wa kwanza kushoto Stephen Masele ambaye amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika aliyeambatana na Mbunge mwingine Mboni Mhita (kulia) ambaye pia  amechaguliwa kuwa Rais wa Caucus ya vijana ya Bunge la Afrika katika uchaguzi uliofanyika Afrika ya Kusini wiki iliyopita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kuwapongeza wabunge hao wa Tanzania waliochaguliwa kushika nafasi za juu katika Bunge la Afrika.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge wa Shinyanga mjini Stephen Masele ambaye amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika mara baada ya kumaliza mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mbunge Mboni Mhita kwa  kuchaguliwa kuwa Rais wa Caucus ya vijana ya Bunge la Afrika katika uchaguzi uliofanyika Afrika ya Kusini wiki iliyopita. 
Makamu wa Rais wa Bunge la Afrika Stephen Masele akizungumza na Wanahari Ikulu jijini Dar es Salaam. Kulia ni Rais wa Caucus ya vijana ya Bunge la Afrika Mboni Mhita PICHA NA IKULU

SPIKA NDUGAI AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU, MHE. JAJI WARIOBA OFISINI KWAKE JIJINI DODOMA.

$
0
0
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akizungumza na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Jaji. Joseph Sinde Warioba (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma. 
Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto) akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu. Mhe. Jaji. Joseph Sinde Warioba (kulia) alipowatembelea jana katika Ofisi ya Bunge Jijini Dodoma. Katikati ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai 
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akiteta jambo na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Jaji. Joseph Sinde Warioba (kulia) alipomtembelea leo Ofisini kwake Jijini Dodoma. 
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Jaji. Joseph Sinde Warioba (kulia) akisalimiana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama (wa pili kushoto), wa pili kulia ni Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai na kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson walipokutana leo katika Ofisi ya Bunge Jijini Dodoma.(PICHA NA DEONISIUS SIMBA - OFISI YA BUNGE)

WAZIRI MKUU MAJALIWA AZINDUA MRADI WA UUNGANISHWAJI WA UMEME WA GRIDI YA TAIFA KWA MIKOA WA LINDI NA MTWARA

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akifunua kitambaa kuashiria uzinduzi wa mradi wa uunganishwaji umeme wa Gridi ya Taifa kwa mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Mahumbika Mkoani Lindi leo Mei 21, 2018. Kushoto ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi. Mradi huo sasa umeondoa kero ya muda mrefu ya upatikanaji wa umeme ulio bora na wa uhakika kwenye mikoa hiyo ya Kusini.


WAZIRI Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amewahakikishia watanzania wote kuwa Serikali itafikisha umeme kila kona na kila kijiji.

Waziri Mkuu aliyasema hayo mara baada ya kuzindua mradi wa uunganishwaji wa umeme wa Gridi ya Taika kwa mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye hafla iliyofanyika Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Mahumbika mkoani Lindi leo Mei 21, 2018.

Hata hivyo aliwataka kuwa wavumilivu kwani mipango ya serikali ambahyo ni kuhakikisha umeme unafika sio tu maeneo ya mijini bali pia kwenye vijiji vyote vya Tanzania.“Kitendo kinachofanyika hapoa leo ni ushahjidi wa ahadi hiyo ya serikali na ninachowaomba Watanzania ni kuwa na subira kwani serikali inatekeleza ahadi ilizotoa kuhakikisha watanzania wanapata umem wa uhakika na wa bei nafuu.”

Akizungumzia uzinduzi huo ambao sasa umetoa sukuhisho la uhaba wa umeme kwenye mkoa huo wa Lindi Waziri Mkuu alitoa maagizo kwenye halmashauri zote mkoani humo kuhakikisha maeneo yote nyeti ya huduma za kijamii yanafikishiwa umeme ikiwemo shule na hospitali.“Hatutarajii kuwa na eneo lenye shida ya umeme, hapa ni umeme masaa 24, na tafsiri ya serikali kuwa hapa ni umeme wa uhakika na wa kutosha ndio hii ambayo leo hii tumezindua.” Alisema.

Alisema sera ya serikali ni ya uchumi wa viwanda,na kwamba, wale watu wanaotaka kuwekeza viwanda vya Korosho, Salfa na vifaa mbalimbaki kwenye mkoa wa Lindi sasa ni wakati wao kwenda mkoani humo na kuwekeza kwani hivi sasa kuna umeme wa uhakika.Aidha Waziri Mkuu aliwaasa wananchi kuwa walizni wa miundombinu ya umeme, na kuwataka wanapoona vitendo vya watu wakihujumu mkiundombinu basi taarifa za kuwashughulikia watu hao ni vema zikatolewa kwa vyombo husika ili kuchukua hatua.

“Naomba vifaa vyote vinavyoletwa kwenye maeneo yenu, kwenye vijiji vyenu basi tuvilinde ili hatimaye tuweze kunufaika na uimarishwaji wa miundombinu ya umeme.” Aliasa Wazir Mkuu.Kupitia mpango w REA, yaani umeme vijijini Serikali imepunguza kutoka Shilingi 380,000/= hadi shilingi 27,000/= tu.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,(katikati) na viongozi wengine wa serikali wakiwemo mawaziri akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mradi wa kuunganishwa umeme wa Gridi ya Taifa kwa mikoa ya Lindi na Mtwara kwenye kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Mahumbika Mkoani Lindi leo Mei 21, 2018. 
Waziri Mkuu Majaliwa akimpongeza Waziri Dkt. Kalemani.
Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, (wapili kulia), akiwa na viongozi wengine, wakiimba wimbo wa taifa baada ya kufanya uzinduzi.
Waziri Mkuu Majaliwa, na viongozi wengine, akipatiwa maelezo ya ,mradi huo na mmoja wa wataalamu wa TANESCO, kwenye kituo cha Mahumbika.
Waziri Mkuu Majaliwa, akitoa hotuba yake 
Waziri Mkuu Majaliwa, akitoa hotuba yake
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, akitoa hotuba yake
Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka, akitoa maelezo ya mradi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi, akitoa hotuba yake
Waziri Dkt. Kalemani, (katikati), akisindikizwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt. Tito Mwinuka.

Taasisi ya Mo Dewji yatoa msaada kwa watoto wenye saratani

$
0
0

Taasisi ya Mo Dewji imetoa msaada kwa watoto wanaopatiwa matibabu ya magonjwa ya saratani katika kituo cha Tumaini la Maisha katika hospitali ya Taifa Muhimbili, Jijini Dar es Salaam.

Msaada ambao umetolewa ni unga wa ngano, khanga na sabuni za kuogea, kufua na kunawia mikono.

Akikabidhi msaada huo, Kaimu Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Belinda Paul alisema taasisi yao itaendelea kuwa na utaratibu wa kutoa msaada katika kituo hicho ili kuwafariji watoto ambao wanapatiwa matibabu.

Alisema hiyo sehemu ya kwanza kutoa msaada kwani wamekuwa na utaratibu wa kusaidia jamii kutokana na uhitaji uliopo hivyo kwa kufanya hivyo wanaamini watakuwa wamegusa maisha ya Watanzania wengi.

Aidha, Paul amewataka watu wengine wenye uwezo kuweka utaratibu wa kusaidia watu wengine wenye uhitaji kama watoto waliopo katika kituo cha Tumaini la Maisha.

Kaimu Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Belinda Paul akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto ambao wanapatiwa matibabu katika kituo cha Tumaini la Maisha.

Kaimu Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Belinda Paul akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasimamizi wa kituo cha Tumaini la Maisha wakati walipokuwa wakikabidhi msaada katika kituo hicho.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (USDM) ambao wanalipiwa gharama za masomo na Taasisi ya Mo Dewji wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wanaopatiwa matibabu katika kituo cha Tumaini la Maisha.


MAKAMPUNI 380 KUONESHA BIDHAA ZAO KATIKA MAONESHO MAKUBWA YA KIMAITAFA UTALII YA KARIBU KILIFAIR MJINI MOSHI.

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kilifair Ltd ,Tom Kunkler akizungumza mbele ya waandishi kuhusu tukio la Maonesho ya Kimatifa ya Utalii ya KAribu Kilifair yanayotaraji kufanyika mjini Moshi ,June 1 hadi 3 mwaka huu.
Viongozi wa Kampuni ya uokoaji ya Kilimanjaro SIR wakifuatilia maelezo juu ya manesho hayo yaliyokuwa yakitolewa kwa wanahabari.
Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Kilifair inayoratibu maonesho ya Karibu  Kilifair ,Dominic Shoo akizungumzia tukio hilo kubwa la Kitalii.
Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia maelezo yaliyokuwa yakitolewa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Uokoaji ya Kilimanjaro SIR ,Ivan Brown akizungumza wakati wa kikao na wanahabri kuhusu tukio hilo.
Baadhi ya Wanahabari.
Meneja Mauzo wa Shirika la Ndege la Ethiopian Airlines ,Fitsimt Dejene ambao ni miongoni mwa wadhamini wa Maonesho ya Kimataifa ya Karibu Kilifair yanayotaraji kufanyika mjini Moshi. 
Waratibu wa Maonesho ya Karibu Kilifair wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wadhamini wa maonesho hayo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini .

MAKAMPUNI 380 yanayojishughulisha na Utalii yanataraji kushiriki Maonesho ya Kimataifa ya Karibu Kilifair huku kampuni ya Kilifair Ltd inayoratibu maonesho hayo ikitangaza kuandaa safari za kifamilia zitakazoshirikisha watu kutoka nchi mbalimbali Duniani kujionea vuvitio vya utalii kwa lengo la kuvitangaza kimataifa.

Maonesho ya kimataifa ya Utalii yaliyopewa jina la Karibu Kilifair yanafanyika kwa mwaka wan ne sasa yakiwakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya Utalii wa Tanzania na nje ya nchi ,kwa lengo la kutangaza bidhaa mbalimbali za Utalii ikiwemo vivutio mbalimbali.

Kwa mara ya kwanza Kampuni ya Kilimanjaro SIR inayojishughulisha na ukoaji wa wageni waliopata matatizo katika maeneo yenye miinuko kama Mlima Kilimanjaro na Meru inataraji kushiriki katika maonesho hayo huku Shirika la ndege la Ethiopian Airlines likitangaza kutumia maonesho hayo kutangaza vivutio vya Utalii kwa wageni watakaosafiri na ndege wa shirika hilo.

Maonesho ya Karibu Kilifair yanayoratibiwa na Kampuni ya Kilifair Ltd awali yalijukiana kama Kilifair yakidhaminiwa na Kampuni mbalimbali za ndani na nje ya nchi .

SERIKALI HAITAJIUSISHA NA UPANGAJI WA ADA KWA SHULE BINAFSI-NAIBU WAZIRI WILLIAM OLE NASHA

SERIKALI YAHIMIZA HALMASHAURI KUBUNI MIRADI YA KIMKAKATI ILI KUJIONGEZEA MAPATO

$
0
0
Serikali imeeleza kuwa Uchukuaji wa baadhi ya vyanzo vya mapato katika halmashauri ulifanyika kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti iliyoridhiwa na Bunge ya mwaka 2015 kifungu namba 58 ikiwa na lengo la kuongeza ufanisi wa ukusanyaji na matumizi ya mapato hayo.

Hayo yameelezwa Bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) alipokuwa akijibu swali la Msingi la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Suzana Mgonukulima, aliyependekeza itungwe sheria ya kuibana serikali ikiwa haitarejesha fedha zilizotokana na vyanzo vya mapato vilivyopo kwenye Miji, Halmashauri, Manispaa na Majiji zitakazokusanywa na kuwekwa kwenye Mfuko Mkuu wa Serikali.

Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Bajeti, mgao wa fedha kutoka katika Mfuko Mkuu wa Serikali utazingatia bajeti iliyoidhinishwa, upatikanaji na mtiririko wa fedha, utekelezaji mpango wa ununuzi na mpango wa kuajiri hivyo hakuna Fungu litakaloruhusiwa kufanya matumizi ya aina yoyote mpaka kuwe na fedha za kulipa matumizi husika.

“Usimamizi wa Mapato hayo kwa mujibu ya Sheria ya Bajeti ya Mwaka 2015 Kifungu namba 58 unazingatia mapato kuingizwa kwenye Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Fedha za Serikali, aliyepewa mamlaka ya kukusanya mapato ya Serikali atawajibika katika ukusanyaji wenye ufanisi, utunzaji wa hesabu, utoaji wa taarifa na kuzuia ufujaji wa mapato”, alisema Dkt. Kijaji. 

Alisema Usimamizi wa mapato na matumizi umebainishwa vizuri na hivyo hakuna haja ya kutunga sheria nyingine ya kuibana Serikali ikiwa haitapeleka fedha kwenye, Miji, Halmashauri, Manispaa na Majiji.

Aidha akijibu swali la nyongezai la Mhe. Mgonukulima kuhusu kutokuwa na usawa katika utoaji wa fedha za maendeleo katika Wilaya, Dkt. Kijaji alisema kuwa tarehe 5 Mei, 2018 Serikali ilizindua Mkakati wa kuziwezesha Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza miradi yenye kuchochea upatikanaji wa Mapato ili ziweze kujitegemea hivyo ni vema Halmashauri zikabuni miradi ya maendeleo itakayoongeza mapato.

Akieleza kuhusu utaratibu wa malipo ya Kodi ya Majengo kutoka katika Halmashauri nchini Naibu Waziri Dkt. Kijaji, alisema kuwa Majengo yasiyofanyiwa tathimini yanatakiwa kutozwa kiwango sawa cha Sh. 10,000 na majengo ya juu (ghorofa) yanatakiwa kutozwa kiwango sawa cha Sh. 50,000.

Alisema majengo yaliyofanyiwa tahimini ndiyo yanayoweza kulipiwa kodi zaidi ya kiasi hicho, hivyo wakurugenzi wa Halmashauri wanapaswa kuzingatia utaratibu huo uliowekwa katika ukusanyaji wa kodi hiyo, alieleza Dkt. Kijaji.

Imetolewa na;
Benny Mwaipaja
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango

WAZIRI MWAKYEMBE AKABIDHI MAGARI FAINALI YA SHIKA NDINGA YA EFM TANGANYIKA PARKER'S

$
0
0
 Waziri wa Habari, Sanaa , Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe akizungumza wakati wa kuhitimisha fainali za shindano la Shika Ndinga linaloendeshwa na kituo cha Radio cha Efm na Tv , Kwa kuwapongeza kuwa kituo cha kwanza kuwakumbuka wasikilizaji wake kwa kuwawezesha kuwa Wajasiliamali.
 Waziri wa Habari, Sanaa , Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, akikabidhi zawadi ya Gari kwa Mshindi wa shindano la Shika Ndinga kwa Wanaume, ambaye ametokea mkoa wa Tanga.
 Waziri wa Habari, Sanaa , Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe  akikabidhi Zawadi ya Gari kwa Mshindi wa Shika Ndinga kwa Wanawake, ambaye anatokea Mkoa wa  Mwanza
 Meneja wa Kituo Cha Radiio cha EFM na Tv E ,Dennisi Busulwa(Sebo) akizungumza na wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliofika kushuhudia fainali za shindano la Shika Ndinga katika Viwanja vya Tanganyika Parker's Dar es Salaam.
 Watangazaji wa Kipindi cha Ubaoni kutoka Radio ya Efm, Mpoki na Dokii wakishangilia na wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliofika katika fainali za shindano hilo katika Viwanja vya Tanganyika Parker's
 Washiriki wa Shindano la Shika Ndinga kwa Wanawake  wakiwa katika harakati za kujaza Vikombe katika hatua ya kwanza ya shindano hilo.

Majaji wa Shindano la Shika Ndinga wakiwa wamesimama tayari kwa ajili ya kutizama mchezo utakavyoendelea uwanjani
 Washiriki wa Kiume wakiwa katika hatua ya Mwisho ya kushika ndinga hili waweze kutwaa gari kwa atakayebaki mpaka mwisho
 Mmoja ya Washiriki kutoka mkoa wa Mtwara aliyotolewa katika hatua ya kwanza akitoa machozi mara baada ya kuenguliwa kwenye shindano.

Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar es Salaam wakifatilia shindano la Shika ndinga.
--

WIKI YA UBUNIFU YAANZA RASMI KUMBI ZA COSTECH JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
 Kiongozi wa HDIF, Tanzania,David McGinty  akizungumza na Wahariri  na Waandishi wa Vyombo Mbalimbali vya habari pamoja na wadau wa Masuala ya Sayansi wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Ubunifu kwa Vijana inayofanyika katika Kumbi Mbalimbali za Costech Jijini Dar es Salaam chini ya ufadhili wa UKAID na HDIF.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH),Dkt Amos Nungu akizungumzia kuhusu wiki ya Ubunifu kwa Vijana iliyoanza katika Kumbi mbali mbali za Costech, ambapo wanufaika wataonesha kazi zao kwa kuwasilisha katika makongamano yatakayokuwa yanaendelea  chini ya ufadhili wa HDIF kwa kushirikiana na UKAID
Naibu Kiongozi wa HDIF Tanzania, Joseph Manirakiza akieleza namna HDIF ilivyoweza kutoa ruzuku kwa wanufaika wa miradi mbalimbali ya ubunifu wakati wa ufunguzi ya wiki ya ubunifu inayoendelea katika kumbi mbalimbali za COSTECH.
Baadhi ya wanufaika wa Mradi huo wakifuatilia kwa ukaribu hotuba mbalimbali zinazotolewa na wadau wa masuala ya ubunifu.
Mtaalamu wa Masuala ya Mawasiliano kutoka HDIF , Hannah Mwandoloma akiwa pamoja na baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari wakisikiliza mawasilisho juu ya wiki ya Ubunifu.
Wanufaika wa Wiki ya Ubunifu wakiwa katika Picha ya Pamoja na Viongozi wa COSTECH, HDIF na UKAID


Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images