Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

TANESCO yang'ara Sherehe za Mei Mosi 2018, IRINGA

$
0
0
Rais Dk John Pombe Magufuli akimkabidhi cheti Mfanyakazi Bora wa Shirika la Umeme nchini Tanesco, ambaye ni Fundi Mchundo Endure Kiswaga kutoka kituo cha kufua Umeme Pangani Tanga.
Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ni miongoni mwa maelfu ya wafanyakazi waliojitokeza kwa wingi Mjini Iringa katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani MEI MOSI ambapo kitaifa iliadhimishwa mkoani humo na kuongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli.
Mwanadada mfanyakazi wa Tanesco akionesha utalaam wake wa kuunga waya za umeme katika nguzo kubwa wakati gari lao la maonesho likipita mbele ya mgeri rasmi katika uwanja wa Samora mjini Iringa.
Magari ya Tanesco yakiwa katika maandamano hayo ya Mei Mosi mjini Iringa.
Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ni miongoni mwa maelfu ya wafanyakazi waliojitokeza kwa wingi Mjini Iringa katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani MEI MOSI ambapo kitaifa iliadhimishwa mkoani humo na kuongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli.
Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) ni miongoni mwa maelfu ya wafanyakazi waliojitokeza kwa wingi Mjini Iringa katika sherehe za siku ya Wafanyakazi Duniani MEI MOSI ambapo kitaifa iliadhimishwa mkoani humo na kuongozwa na Rais Dk John Pombe Magufuli.

INTRODUCING Ommy Dimpoz featuring Seyi Shay - Yanje (Official Music Video)

UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA

$
0
0

Ubongo Learning ambalo ni shirika linaloongoza barani Afrika kwa maudhui ya elimu ya kuburudisha kwa watoto, leo imeandaa mkutano wake wa mwaka ambao ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana kutokana na mabadiliko katika soko la ajira.

Kwa kipindi cha miezi 6 sasa, Ubongo Learning, shirika lisilo la kibiashara ambalo ndiyo lilibuni katuni za kuelimisha za Ubongo Kids, limekuwa likifanya utafiti juu ya uwezo wa kupata ajira na usimamizi wa fedha miongoni mwa vijana nchini Tanzania. 

Lengo la mradi huu, uliofadhiliwa na Data for Local Impact (DLI), ni kuelimisha vijana, haswa wasichana jinsi ya kutumia maelezo, taarifa na takwimu zinazopatikana ili kufanya maamuzi bora juu ya maisha yao ya mbeleni, na zaidi ya hilo kupitia ujuzi wa masala ya kifedha. Vipindi vya televisheni vya Ubongo vinatazamwa na zaidi ya watu milioni 6.4 kila mwezi, hivyo kuvifanya kuwa vipindi vya watoto vyenye watazamaji wengi kuliko vyote Afrika Mashariki na kuwa sehemu nzuri sana kuwasilisha maswala muhimu kwa vijana.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano huo, Meneja Masoko Ubongo Learning Iman Lipumba alisema licha ya kuwa na Maendeleo makubwa ya kuhakikisha wasichana wanaandikishwa shule za msingi, lakini bado jamii nyingi nchini Tanzania bado zinawapendelea wavulana kielimu (hususan kwenye elimu ya shule za sekondari na vyuo vikuu) zaidi ya wasichana.

 Zaidi ya hilo, utafiti wetu unaonyesha kuwa wavulana wanashawishiwa zaidi kusoma masomo ya sayansi, hesabu na ukandarasi, taaluma ambazo zinahitajika sana katika soko la ajira, na wasichana wanashauriwa kuingia kwenye masomo ya sanaa na hatimaye kufanya kazi za utoa huduma ambazo huenda zikapotea katika miaka michache ijayo.


‘Tunahitaji kubadilisha hali hii. Sisi tunaamini kuwa kama vijana watapatiwa maelezo na taarifa hizi tangu awali, itawasaidia kufanya maamuzi bora kitaaluma ili kujaza nafasi zinazoongezeka kweney soko la ajira nchini Tanzania’ alisema Lipumba.

Kwa miaka 10 iliyopita, stashahada ya sheria au digrii yoyote nyingine kutoka chuo kikuu ingemhakikishia kijana kazi bora. Lakini, katika dunia ya leo, mabadiliko ya kasi kubwa katika teknolojia yamebadilisha kabisa maisha yetu, haswa jinsi tunavyofanya kazi. Wakati ajira katika taaluma zilizozoeleka kama vile sheria, utawala na biashara zinapungua, fursa za ajira katika IT, ukandarasi na kazi za kisanii kama vile kuendesha masoko kidijitali zinaongezeka kwa kasi kubwa sana. 

Tena, asili mia 65 ya watoto wanaoanza shule za msingi leo watakuja kuingia kwenye taaluma au kazi ambazo hazijawahi kuwepo kabisa. Hivyo, Ubongo Learning inajishughulisha na kuwawezesha vijana wa Tanzania kuwa na vipaji vitakavyohitajika ili kuwa na mafanikio katika mazingira yenye kasi na kutokuwa na uhakika wa

Likiwa shirika lisilo la kibiashara, Ubongo Learning linaanda maudhui ya kielimu ya kufurahisha na yenye kulenga na kuendana na maeneo au nchi maalum, maudhui ambayo yanawasadia watoto kujifunza na kutumia mafunzo hayo kubadilisha maisha yao. Shirika linafikia mamilioni ya familia barani Afrika kupitia teknolojia zinazopatikana kirahisi kama vile televisheni, redio na simu za mkononi.

Vile vile, Ubongo Learning imetengeneza katuni zinazofundisha vijana taaluma nyingine zenye thamani kubwa kama vile kuandika programu za kompyuta, jinsi ya kuhakiki taarifa za mtandaoni pamoja na utunzaji akiba, kupanga matumizi na kujipatia kipato. Pia tunafanya kazi na wadau wengine kama vile DLI amabo nao wanajishughulisha na kuelimisha vijana ili kuwapatia vipaji mbali mbali kuwawezesha kupata mafanikio.
 Mwakilishi wa Catholic Relief Service,Priyanka Jagtap, akiwasilisha mada katika mkutano wa mwaka wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Ubongo Learning linalojishughulisha na elimu ya kuburudisha watoto. Mkutano huo ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana  kutokana na mabadiliko katika soko la ajira leo jijini Dar es Salaam
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Ubongo Learning linalojishughulisha na elimu ya kuburudisha watoto, Nisha Lagon, akiwasilisha mada katika  mkutano wake wa mwaka ambao ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana  kutokana na mabadiliko katika soko la ajira leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mwakilishi wa Catholic Relief Service,Priyanka Jagtap.
Mwakilishi wa BBC Media Action ,Doreen Bangapi,akichangia mada katika katika mkutano wa mwaka wa wadau wa mwaka wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Ubongo Learning linalojishughulisha na elimu ya kuburudisha watoto. Mkutano huo ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana  kutokana na mabadiliko katika soko la ajira leo jijini Dar es Salaam



Msekwa Apongeza Utendaji wa rais Magufuli

$
0
0
Jonas Kamaleki-MAELEZO 

Spika wa Bunge mstaafu, Mhe. Pius Msekwa amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli anafanya kazi vizuri katika kuiletea nchi maendeleo hasa kwa kulinda na kusimamia rasilimali . 

Msekwa alisema hayo jana katika mahojiano na shirika moja la utangazaji la kimataifa yaliyofanyika Ukerewe, mkoani Mwanza. "Mwenye macho haambiwi tazama, yanayofanywa na Rais Magufuli yanaonekana wazi hata yanatoka kwenye vyombo vya habari badala ya kubaki kwenye kumbukumbu za serikali", alisema Msekwa. 

Kuhusu demokrasia nchini, Msekwa amesema kuwa hali ya demokrasia nchini inaridhisha kwani viongozi muda wao wa kukaa madarakani ukiisha wanaondoka. Wanaominya demokrasia ni wale wanaong'ang'ania madarakani baada ya kipindi chao kuisha, jambo ambalo kwa Serikali ya Tanzania halipo. Tangu Serikali ya Awamu ya Tano imeingia madarakani mambo mengi yamebadilika na kuwa bora zaidi. Mfano, nidhamu ya watumishi na uwajibikaji serikalini imeongezeka na hivyo ukiritimba na urasimu umepungua. 

Huduma za Afya zimeboreshwa kwa kujenga na kukarabati hospitali, zahanati na vituo vya afya. Hii pia ni pamoja na upatikanaji wa dawa hospitalini kupitia bohari ya dawa ya serikali (MSD). Kwa kujali afya za Watanzania, Serikali imeongeza bajeti ya dawa kutoka bilioni 39 hadi bilioni 268, jambo ambalo limefafanya upatikanaji wa dawa kuongezeka. 

Mambo mengine ambayo Mzee Msekwa anasema kuwa yanashamirisha utendaji wa Rais Magufuli ni pamoja na kupambana na rushwa na ufisadi, kujenga na kuboresha miundombinu ikiwemo ya barabara, madaraja, umeme , viwanja vya ndege na ujenzi wa reli ya kisasa yenye viwango vya kimataifa (Standard Gauge Railway). 

Kwa kipindi kifupi ambacho Rais Magufuli ameingia madarakani, serikali imeweza kununua ndege 7 ambazo tatu kati yake zimeshawasili nchini na zinafanya kazi, nne zinatarajiwa kuingia nchini mwaka huu (2018). 

Elimu bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari inatolewa, jambo ambalo limefanya wanafunzi wengi kujiandikisha kuanza darasa la kwanza kwa mwaka juzi, jana na mwaka huu 2018. Uhamasishaji wa uchumi wa kati unaotokana na viwanda ni jambo jingine ambalo Serikali ya Awamu ya Tano imelitilia mkazo. Hili ni dhahiri kwa kuongeza umeme katika gridi ya Taifa hadi kufikia megawati 1,451 mwaka 2018 na kuzidi kuongeza umeme. 

Ongezeko la umeme hadi kufikia zaidi ya megawati 5000 linatarajiwa ifikapo mwaka 2020, kwa mujibu wa Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani. Ujenzi wa mradi wa umeme wa Stieglers Gorge, utaleta mapinduzi makubwa katika upatikanaji wa nishati ya uhakika ya umeme kwa kuzalisha megawati 2100, ambao utachagiza ujenzi wa viwanda.

WAFANYAKAZI TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) WASHIRIKI SHEREHE ZA MAADHIMISHO SIKU YA WAFANYAKAZI DUNIANI

$
0
0
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiwa katika maandamano ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa jana katika uwanja wa Uhuru mkoani Dar es Salaam.
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakijiandaa kushiriki katika maandamano ya maadhimisho ya sherehe ya siku ya wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa jana katika uwanja wa Uhuru mkoani Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) walioshiriki Maadhimisho ya sherehe ya siku ya Wafanyakazi Duniani kitaifa yaliyofanyika jana katika uwanja wa Samora mkoani Iringa. 
Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakipita mbele ya mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya sherehe ya siku ya wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa jana katika uwanja wa Uhuru mkoani Dar es Salaam.
Baadhi ya Wafanyakazi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakijiandaa kushiriki katika maandamano ya maadhimisho ya Sherehe ya Siku ya Wafanyakazi Duniani kitaifa yaliyofanyika jana katika uwanja wa Samora mkoani Iringa.Picha na JKCI

UBUNGO YAPONGEZWA KWA UTOAJI MIKOPO KWA ASILIMIA 100, YAJIANDAA KUANZISHA VIWANDA

$
0
0
Emmanuel Masaka,Globu ya jamii

SERIKALI kupitia  Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi) Joseph Kakunda ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es Salaam kwa kuwa Halmshauri ya kwanza na ya mfano kwa kutoa fedha za mikopo ya wanawake na vijana kwa asilimia 100, kutoka katika
mapato ya ndani.

Hivyo Naibu Waziri ameitaka Wizara ya TAMISEMI kuandikia Manispaa ya Ubungo barua ya pongezi,kwani maeneo mengine ni jambo ambalo linaonekana kugumu kutekelezeka lakini Ubungo
wameweza.

Manispaa ya Ubungo juzi wamezindua mchakato wa ugawaji wa mikopo ya Sh.bilioni 1.94 ,wakati ina mwaka Mmoja tu tangu kuanzishwa kwake.Akizungumza  fedha hizo Meya Ubungo Boniface Jacob 
,amesisitiza mikopo itatolewa kwa vigezo bila kuangalia dini,kabila wala chama cha mtu.

"Waosema mikopo ni Ilani ya CCM,wajiulize mbona kwingine kuna Halmashauri za CCM lakini hakuna mambo haya mazuri? Hivyo watu wajue kuna viongozi  makini na imara wanatoka chama cha Chama cha Upinzani upinzani na ndio msingi na chachu ya mafanikio,"amesema Jacob.

Jacob ametoa rai kwa vijana kuomba mikopo hiyo,kwani idadi ya akina mama ni kubwa kuliko idadi ya vijana,huku akiahidi Mei mwaka huu halmashauri kuanzisha viwanda vidogo kwa ajili ya kuwasaidia vijana suala la ajira.Risala iliyosomwa kwa mgeni rasmi imeeleza Halmashauri ya Ubungo imeidhinisha kutoa fedha kwa vikundi 364 ambapo vikundi 119 ni vya vijana na vikundi 245 ni vya wanawake.Jumla watakaonufaika na mikopo hiyo ni wananchi 11,312.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI,Joseph Kakinda akiwa ameambatana na viongozi wa Ubungo wakitembelea mabanda ya wajasiria mali mara baada ya uzinduzi wa ugawaji wa mikopo kwa vikundi vya wakina Mama na Vijana,walemavu leo jijini Dar as Salaam.Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI,Joseph Kakinda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Ubungo wakitembelea katika hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa mikopo kwa vikundi vya wakina Mama na Vijana,walemavu leo jijini Dar as Salaam.

HAFTRADE YAUNGA MKONO ELIMU BURE KWA KUJENGA MADARASA MAWILI HANDENI MJINI

$
0
0

TAASISI isiyo ya kiserikali ya Haftrade Iliyopo Handeni Mjini mkoani Tanga imeamua kujenga madarasa mawili katika wilaya hiyo ili kuungana na Serikali katika mpango wa elimu bure.

Akizungumza katika ziara ya kukagua ujenzi wa madarasa mwishoni mwa wiki iliyopita Handeni Mjini mkoani Tanga Mkurugenzi wa Taasisi ya Haftrade Thecla Mingwa amesema ujenzi wa madarasa hayo upo hatua za mwisho na lengo lao ni kuona wanafanzi wanakaa kwenye mazingira mazuri ya kusomea.

Mingwa amesema Hafrade ina wanachama hai 20 mpaka sasa na kufafanua taasisi yao imesajaliwa kwa ajili ya shughuli za kijamii ikiwemo, elimu,mazingira,afya na maji vijijini. " Taasisi yangu ya Hafrade wakati ikiendelea kusimamia ujenzi huo mkakati wake kutafuta wadau kwa ajili ya ujenzi wa mabweni ya shule ya sekondari ya Kwenjugo, pia kutoa elimu pamoja na kupanda miti ya matunda na mikorosho" amesema Mingwa.

Amesisitiza mikakati yao mingine ni kutoa huduma zao katika maeneo mengi zaidi huku wakidhamiria kuendelea kushirikiana na Serikali ya Awamu ya tano.Aidha amesema mikakati yao mingine ni kuwa na mashamba makubwa kwa ajili ya shughuli za kilimo.uyaendesha kwa kilimo .Alisema Hafrade inashirikiana na Shirika la Save Children katika shughuli zake mbalimbali katika kuleta maendeleo.

"Hafrade inatoa huduma zake Handeni Mjini yenye Kata, 12 ambazo ni Chanika, Kidereko, Konje, Kwamagome,Kwediyamba,Kwenjugo Mangaribi ,Kwenjugo Mashariki,Mabanda,malezi ,mlimani, msasa na vibaoni,"amesema.Mingwa amesema katika utendaji wa shughuli zake Haftrade imegawanyika katika idara nne ambazo ni idara ya elimu, idara ya Afya, idara ya mazingira, na idara ya maji na inaendesha shughuli zake kwa kushirikiana na Serikali kuakikiasha malengo na mikakati iliyopangwa inatumia.

Ametaja baadhi ya kazi ya idara hizo kuwa ni Idara maji kulinda vyanzo vya maji, idara ya mazingira kuandaa maeneo ya shamba kwa ajili ya kilimo cha shamba darasa.cha mihogo na korosho.
 Wanachama wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Haftrade Ikikagua ujenzi wa Vyoo na madarasa ambayo wanajenga Katika kata ambazo wanaosimamia mradi Wilaya ya Handeni mjini mkoani Tanga  jana Picha na Heri Shaaban
 

MAJI YANAYOTIRIRIKA MITAANI KUTOKA VIWANDANI YAPIMWE KEMIKALI.

$
0
0

NA WAMJW-DAR ES SALAAM.

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeitaka  Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuchukua hatua ya kupima maji yanayotiririka mitaani kutoka viwandani kubaini kama yana kemikali ambazo zinaathiri wananchi au hazina madhara yoyote.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ys Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam.

"Bodi hii ninayoizindua leo inatakiwa kuhakikisha  majibu ya watu wanaokuja kuleta vipimo vyao yatoke mapema na haraka iwezekanavyo ili kupunguza msongamano wa wateja wenu" alisema Dkt. Ndugulile.

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa Mamlaka hiyo inatakiwa kushirikiana na kufanya  mazungumzo na Taasisi ya Chakula na Dawa TFDA na TBS ili kutoingiliana katika majukumu kwani kuna kuna kipengele cha majukumu yao kinafanana katika kusimamia ubora wa chakula.

Aidha Dkt. Ndugulile ameitaka Mamlaka hiyo kuisimamia kikamilifu sheria ya uchafuzi wa Mazingira ili kuepusha wananchi na magonjwa ya kuambukiza na yasioambukiza. Kwa upande wake Mkemia Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo Dkt. Fidelis Mafumiko amesema kuwa wanaiomba Serikali kutatua changamoto ya upungufu wa mitambo ya kufanyia kazi katika mamlaka hiyo.

Aidha Dkt. Mafumiko amesema kuwa Bodi hiyo iliyozinduliwa leo ipo tayari kufanya kazi kwa manufaa ya  Watanzania japo mamlka hiyo ina upungufu wa Watumishi kutoka watumishi 400 mpaka kufikia watumishi 220.

Bodi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali imezinduliwa leo ikiwa na Wajumbe saba ambao ni Mwenyrkiti wa bodi hiyo Prof. Esther Jason, Katibu Dkt. Fidelis Mafumiko,  Dkt. Eliud Eliakimu,  Dkt. Samwel Gwamaka, Dcp. Hussein Laiser, Bi. Irene Leisure na Bw. Pius Mponzi. 
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu ambae alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Otilie Gowelle.kulia ni Mwenyekiti wa bodi hiyo Dkt Esther Jason.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi Dkt. Esther Jason mwongozo wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Wapili kushoto ni Mkurugenzi wa Mafunzo na Rasilimali watu ambae alimwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt. Otilie Gowelle.
 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile akisisitiza jambo mbele ya Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mku na viongozi wengine wa Srikali wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu.
Mwenyekiti wa Bodi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Esther akiongea akitoa neno mbele ya viongozi wa Serikali na Waandishi wa Habari wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu.

 Picha ya pamoja ikiongozwa na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndegulile wakati wa uzinduzi wa Bodi Tendaji ya Kwanza ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali leo jijini Dar es salaam

WAJASIRIAMALI WANAWAKE 200 MKOANI KIGOMA WAPATIWA MAFUNZO KUWAIMARISHA KIUCHUMI

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel, Kigoma

WANAWAKE 200 ambao ni wajasiriamali mkoani Kigoma wanataraja kupata mafunzo yatakayosaidia kuwaimarisha kiuchumi na lengo ni kuhakikisha wanapata maendeleo katika mkoa huo na Taifa kwa ujumla hasa kipindi hiki cha kutekeleza sera ya Tanzania ya viwanda.

Awali akifungua rasmi mafunzo hayo jana mkoani humo na yanatarajiwa kudumu kwa siku 10 katika halmashauri zote mkoani hapa Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Kigoma Gaden Machunda ametoa msisitizo kwa akina mama kujikita katika ujenzi wa viwanda.

Aidha Machunda amewataka akina mama kuzingatia misingi ya ujasiriamali pamoja na kuwa na nidhamu na biashara wanazozifanya huku akiwataka wauzaji wa hoteli na migawa kuwa nadhifu ili kuwavutia wateja.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya AJ General Company amesema lengo la mradi huo ni kuwawezesha wanawake na kusaidia kutekeleza Ilani ya Serikali ya awamu ya 5  kuelekea ujenzi wa Tanzania ya viwanda.Ambapo amesema wanawake watainuka kiuchumi kupitia mpango huu na wanawake watapata mikopo isiyokuwa na masharti kama ilivyokuwa hapo awali lakini pia kuwezesha bidhaa zinazozalishwa mkoani hapa kupata soko nje ya nchi.

Katibu wa Umoja wa Wanawake mkoani Kigoma (UWT) Edina Kuguru amesema wao kama viongozi wa wanawake wamejipanga kuhakikisha wanawake wote mkoani hapa wanaondokana na mfumo wa kuwategemea wanaume.Amesema mikakati waliyonayo ni kutoa elimu ya ujasiriama na jinsi ya kutumia fedha wanazopewe zinatumika ipasavyo na kuwatafutia masoko kwani wana mipango ya kuanzisha viwanda vya mihogo kwa kuwa zao hilo linalimwa sana mkoani Kigoma.

Mmoja wa wajasiriamali wa Mkoa wa Kigoa Maisala Barakabise amesema wanawake wa mkoa huo wanajitahidi kufanya biashara kwa kutumia mitaji yao na wao ndio walezi wa familia na ni wathubutu.Hivyo wakiwezeshwa wanaweza zaidi na kuongeza wamekuwa wakiibua fursa nyingi.

Amesema changamoto wanazokumbana nazo katika kutafuta kipato na kujiondoa katika dimbwi la umasikini ni mitaji modogo.Mjasiriamali mwingine Sakina Kabeza amesema wanawake wa Kigoma ni wachapakazi na wanajituma na kufafanua kipindi cha nyuma fursa zilikuwa ni chache lakini kwa sasa Awamu ya tano imejipanga kikamilifu kutoa fursa kwa wanawake wote.

"Na endapo wanawake wa Kigoma wakipatiwa elimu na mitaji wanaouwezo wa kufanya vitu vya tofauti na wanao uwezo wa kuchangamkia fursa kujikwamua kimaisha,"amesema.Aidha ameipongeza taasisi hiyo iliyojitokeza na kutoa elimu na mikopo kwa wanawake mkoani Kigoma.

Wito kwa jamii kuondokana na mila potofu,Jamii yaaswa kupeana elimu

$
0
0
Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu Halotel Bwana Trieu Thanh Binh na baadhi ya wafanyakazi wa kampuni hiyo wakikabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya Kijamii kwa baadhi wa wauguzi leo wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea watoto walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) na kuwapelekea mahitaji hayo.
Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu Halotel Bwana Trieu Thanh Binh akikabidhi msaada wa mahitaji mbalimbali ya kijamii yenye kwa baadhi wa wauguzi leo wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea watoto walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) na kuwapelekea mahitaji 
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Halotel Stella Pius akikabidhi moja ya msaada wa mahitaji mbalimbali ya kijamii kwa mmoja wa wazazi wakati wafanyakazi wa kampuni hiyo walipowatembelea watoto walioko katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI)na kuwapelekea mahitaji hayo.

Kuwepo kwa mila potofu katika jamii ya watanzania ni moja na ya jambo ambalo limekuwa ni kikwazo katika juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali pamoja na taasisi mbalimbali za kijamii katika kupunguza au kutokomeza kabisa matatizo ya kiafya ambayo huwapata watoto wachanga wanaozaliwa na walio na umri chini ya miaka mitano.

Watoto wengi katika rika hilo huwa katika athari ya kuzaliwa au kupata magonjwa ambayo ni kuwa na vichwa maji, pamoja na mgongo wazi, ikiwa ni magonjwa ambayo huweza kuepukwa endapo tu jamii nzima ya watanzania wataweza kupatiwa elimu sahihi ya namna ya kuepuka au kuzuia magonjwa hayo na endapo kutabainika watoto wenye matatizo hayo jamii isiweze kuwaficha kutokana na imani potofu.

Hayo yamebainishwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya upasuaji katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) Bwana Laurent Lemeri Mchome, wakati akiongea na waandishi wa habari baada ya wafanyakazi wa kampuni ya simu ya Halotel walipowatembelea watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi pamoja na wazazi/walezi wao waliolazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa ajili ya kuwapa mahitaji mbalimbali ya kijamii kama sehemu ya msaada wao kama wafanyakazi. 

“Akiongea baada ya kukabidhiwa msaada huo, kwa niaba ya madaktari na wauguzi wodini hapo Dr Laurent Mchome amesema kila mwaka Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) tumekuwa tukitoa matibabu kwa wagonjwa zaidi ya 350 nchi nzima kupitia kampeni ya watoto wenye vichwa maji na mgongo wazi. Pia tumekuwa tukiweka kambi ya kutibu watoto kila mkoa kwa kila kanda nchini na changamoto kubwa ni kwamba jamii kubwa ya watanzania hawana elimu ya kutosha kuhusu magoinjwa haya kuwa yanatiwa na watoto hupona kabisa”.

“Naomba nitoe wito kwa jamii hasa kwa wale ambao wanafahamu kuhusu ugonjwa wa vichwa maji na mgongo wazi wanapoona jamii ambayo ina watoto wenye matatizo haya wasiogope bali wawape ushauri kuwaleta hospitali kwasababau matibau yanafanyika na watoto wanapona kabisa” Aliongeza Dr Mchome. 

Akizungumza wakati wa kukabidhi mahitaji hayo Naibu Mkurugenzi wa Kampuni ya Halotel. Bwana Trieu Thanh Binh amesema kuwa katika kuhakikisha tunasaidia sekta hii ya afya nchini, tumeona ni vyema kuja kuwatembelea watoto hawa na kujumuika nao siku hii ya leo kwa kuwapa misaada hii ya kijamii ambayo ambapo nimwendelezo wa kampeni ya kusaidia jamii yenye uhitaji, ili waweze kuimarika katika afya yao wanapoendelea kupata matibabu wodini hapa. Hii ni pamoja ya kuonesha upendo kwao na kutambua thamani yao katika jamii ya watanzania.

“Tunatambua changamoto mbalimbali ambazo ziko katika kuwapa matibabu watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi wawapo wodini wakisubiri wakisubiri kupata matibabu upasuaji hivyo nitoe wito kwa taasisi zingine mbalimbali, makampuni na watu binafsi kuweza kujitolea na kuwasaidia mahitaji mbaliambali ikiwa ni katika kujali na kutambua thamani ya afya yao aliongeza bwana Binh.”

Kwa upande wa Uongozi wa Taasisi ya Tiba ya Mifupa (MOI) , Afisa Uhusiano Bwana Patrick Mvungi alisema “ Tumefarijika sana kwa kupokea msaada huu kutoka Kampuni ya simu ya Halotel na wafanyakazi wake, tunawashukuru sana kwa kuthamini afya za watoto hawa lakini pia kwa kuunga mkono jitihada za kuisaidia sekta ya afya nchini. Hii ni hatua mpya na kubwa kwetu sisi katika kuimarisha ushirikiano wetu na Halotel kwa kiwango cha juu hasa katika kuboresha sekta ya afya kwa ujumla”.

Licha ya kampuni ya simu ya Halotel kupiga hatua kubwa katika kusambaza huduma za mawasiliano na kutoa huduma zenye ubora wa hali ya juu nchini nzima, kampuni hii imekuwa ikijihusisha na kutoa misaada mbalimbali kwa jamii ya watanzania. Hii ni katika kuonesha jinsi inavyothamini na kujali jamii ya watanzania kwa nyanja mbalimbali, ikiwemo kuboresha sekta ya afya na elimu kama moja ya kipaumbele cha kampuni ya hii kwa maendeleo ya watanzania na nchi kwa ujumla.

RAIS DKT.MAGUFULI ANATARAJIA KUWA MGENI RASMI TUZO ZA CTI MEI 4

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania CTI, Leodgar Tenga, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam,leo mchana wakati akitangaza rasmi \tarehe ya kutoa Tuzo za Rais za Viwanda zinazotarajia kufanyika Mei 4 mwaka katika Hoteli ya Serena, ambapo mgeni rasmi anatarajia kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. Katikati ni Mwenyekiti wa CTI, Dkt. Samuel Nyantahe na Makamu wa pili wa Mwenyekiti CTI, Shabbir Zavery. Picha na Muhidin Sufiani (MAFOTO)


Na Leandra Gabriel, Mafoto Blog, Dar

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dkt John Pombe Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tuzo za Rais za Mzalishaji bora wa Viwandani (PMAYA) za mwaka 2017 zinazotarajiwa kufanyika Mei 4 mwaka huu, jijini Dar es Salaam.

Shindano hilo la PMAYA zinazoandaliwa na Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) hutoa tuzo kwa viwanda vilivyofanya vizuri katika mwaka uliopita likiwahusisha wanachama wa CTI na wasio wanachama.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam,mchana huu, Mkurugenzi mtendaji wa CIT Leodger Tenga amesema kuwa tarehe 7 Desemba mwaka jana walizindua shindano la mzalishaji bora wa kampuni na tayari kampuni 36 ziliweza kujitokeza kwenye mchakato huo ukiwa umeenda vizuri na washindi wamepatikana ambao watakabidhiwa zawadi zao siku hiyo ya ijumaa, Mei 4.
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Machapisho wa Shirikisho la Viwanda Tanzania CTI, Thomas Kimbunga, akitangaza utaratibu wa upatikanaji wa washiriki wa tuzo hizo,wakati wa mkutano huo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage, ambao ni sehemu ya waratibu mkutano huo, Teddy Mapunda, akiongoza mkutano huo,
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Machapisho wa Shirikisho la Viwanda Tanzania CTI, Thomas Kimbunga, akitangaza utaratibu wa upatikanaji wa washiriki wa tuzo hizo,wakati wa mkutano huo. kutoka (kushoto) ni Meneja Masoko wa Kampuni ya Alaf Tanzania, Theresia Mmary, Makamu wa pili wa Mwenyekiti wa CTI, Shabbir Zavery, Mwenyekiti wa CTI, Dkt. Samuel Nyantahe na Mkurugenzi Mtendaji, Leodgar Tenga.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda Tanzania CTI, Dkt. Samuel Nyantahe, akizungumza na waandhishi wa habari kuhusu tuzo hizo.


Kwa upande wa mwenyekiti wa shirikisho hilo Dkt. Samwel Nyantahe ameeleza kuwa shirikisho hilo ni la wamiliki wa viwanda nchini ni kwa lengo la kuweka mazingira ya uzalishaji nchini na shindano hilo linatoa nafasi ya kutangaza bidhaa kwa wafanyabiashara na kupata nafasi ya kukutana na Rais na kuzungumza naye ikiwa ni muhimu kwa kuwa tunaelekea katika uchumi wa viwanda.

Mashindano hayo yanahusisha zaidi ya sekta 18 na makampuni 36 na kuna zawadi maalumu kwa washindi wa matumizi bora ya nishati katika viwanda vyao.

Mkurugenzi wa machapisho wa (CTI) Thomas Kimbunga ameeleza kuwa namna ya kushiriki ilikuwa katika makundi matatu ya viwanda yaani vile vikubwa, vidogo na vya kati na washiriki wameshindanishwa kulingana na makundi waliyoshindania na vigezo katika kila kundi ni pamoja na mazingira, mahusiano kazini na kuendeleza wafanyakazi sambamba na suala la ubora wa bidhaa kwa kuthibitishwa na TBS.

Aidha ameeleza kuwa shindano hilo litatasaidia kuongeza ufanisi hasa katika utendaji kazi katika sekta mbalimbali za viwanda pia washiriki watapata nafasi ya kujua maeneo waliyofanya vizuri na kupata nafasi ya kuboresha vyema bidhaa zao.Baadhi ya vigezo ambavyo vimezingatiwa ni pamoja na faida kwa jamii, afya na usalama, uuzaji wa bidhaa nje ya nchi, utendaji kiuchumi, utendaji kiteknolojia na matumizi bora ya nishati.
Sehemu ya wanahabari wakiwa bize kurekodi hotuba ya Mwenyekiti huyo.
Wanahabari wakiwa kazini.....
Baadhi ya wageni waalikwa katika mkutano huo....
Mwakilishi wa Hoteli ya Serena ambao ni moja kati ya wadhamini, Meneja wa mikutano na matukio, Alex Maboko, akizungumza jambo.

RAIS DKT. MAGUFULI AFANYA ZIARA WILAYA YA KILOLO MKOANI IRINGA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Luhota pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi  Kalambo zilizopo Iringa vijijini wakati alipokuwa njiani kuelekea Wilayani Kilolo kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la Msingi la Hospitali ya Wilaya ya Kilolo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Iringa vijijini katika eneo la Ndiwili (hawaonekani pichani) wakati alipokuwa njiani kuelekea Wilayani Kilolo kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la Msingi la Hospitali ya Wilaya ya Kilolo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Ipogolo mkoni Iringa wakati akitokea Kilolo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahi kwa kuimba nyimbo na vijana chipukizi wa Kilolo mara baada ya kuhutubia wananchi waliofika kwenye sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa. PICHA NA IKULU

RAIS MAGUFULI,MBUNGE MAVUNDE NA DC NDEJEMBI WATIMIZA AHADI YAO YA KUCHANGIA SHULE YA MSINGI VEYULA-JIJINI DODOMA

$
0
0
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akishiriki kuchimba msingi wa ujenzi wa madarasa shule ya msingi Veyula.

 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akishiriki kuchimba msingi wa ujenzi wa madarasa shule ya msingi Veyula pamoja na wananchi.
 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akimkabidhi fedha Kaimu Mkuu wa wilaya wa Dodoma Deogratias Ndejembi ikiwa ni mchango wake kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Veyula(katikati) ni Mkurugenzi wa jiji la Dodoma Godwin Kunambi.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akimkabidhi saruji Kaimu Mkuu wa wilaya wa Dodoma Deogratias Ndejembi ikiwa ni mchango wake kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Veyula.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akishiriki ushushaji mifuko ya sarufi
Kaimu Mkuu wa wilaya wa Dodoma Deogratias Ndejembi akizungumza na wananchi kuhusu ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya msingi Veyula.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungunza.
Wananchi walioshiriki uchimbaji msingi
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde na Kaimu Mkuu wa wilaya wa Dodoma Deogratias Ndejembi.
Kaimu Mkuu wa wilaya wa Dodoma Deogratias Ndejembi akichimba msingi vyumba vya madarasa shule ya msingi Veyula.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akiteta jambo na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi

...............................................................
Rais Dk.John Pombe Joseph Magufuli leo amewasilisha mchango wake wa  10,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya Shule ya Msingi Veyula iliyopo Jijini Dodoma ikiwa ni ahadi aliyoitoa kwa wananchi  wakati aliposimama kuwasilimia akitokea katika hafla ya Ufunguzi wa Barabara ya Dodoma-Babati.

Mchango huo umewasilishwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Deogratious Ndejembi ambaye pia amechangia Tsh 1,000,000 kutimiza ahadi yake na kuwashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kuanza kuchimba Msingi wa ujenzi wa madarasa na kutumia fursa hiyo kuwataka watendaji wote kusimamia zoezi la ujenzi kwa ufanisi na kumwagiza Lt Col Matina Mkuu wa Kikosi cha JKT Makutupora kusimamia ukamilishwaji wa ujenzi wa madarasa hayo ndani ya wiki tatu.

Aidha,Mbunge Wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe.Anthony Mavunde na DC Ndejembi waliungana na wananchi katika zoezi la uchimbaji msingi na baadaye Mh Mavunde alikabidhi kiasi cha Tsh 5,000,000  mifuko ya Saruji 100 na kuahidi kuongeza Tsh 5,000,000 ya ziada mapema wiki ijayo ikiwa ni mchango kutoka kwa marafiki wa Mbunge huyo,na pia alitumia fursa hiyo kumshukuru Mh Rais kwa kusaidia ujenzi wa madarasa hayo.

Naye Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi amewahakikishia wananchi kwamba Halmashauri ya Jiji la Dodoma italipia vifaa na gharama zote za kupaua madarasa hayo ikiwa ni sehemu ya mchango wa Jiji.

RAIS DKT MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA YA KILOLO, ATEMBELEA CHUO KIKUU KISHIRIKI CHA UALIMU CHA MKWAWA MJINI IRINGA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi wengine akipatiwa maelezo kutoka kwa msimamizi wa ukandarasi wa TBA  juu ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa kabla ya kuweka jiwe la msingi la mradi huo leo Mei 2, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na viongozi wengine akipiga makofi baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la  ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa leo Mei 2, 2018*

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana  na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo Mhe. Asia Juma Abdallah  kwenye sherehe ya kuweka jiwe la  la msingi la  ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa leo Mei 2, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa  mkoani Iringa alipotembelea leo Mei 2, 2018 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zwadi kutoa kwa Rasi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa  mkoani Iringa alipotembelea leo Mei 2, 2018. Kulia ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam na Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo, Profesa Bonaventure Rutinwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya  wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Mkwawa  mkoani Iringa alipotembelea leo Mei 2, 2018.

GGM na TACAIDS kuzindua Kilimanjaro Challenge 2018

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko (kushoto)  akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa zoezi la upandaji wa Mlima Kilimanjaro  (Kilimanjaro Challenge 2018), litakalo kwenda sambamba na kuendesha harambee kuchangisha fedha  kwa mwaka 2018 kwa ajili ya kusaidia mapambano ya kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI nchini. Kulia ni Makamu wa Rais miradi endelevu wa Kampuni ya AngloGold Ashanti, GGM, Simon Shayo.








Sehemu ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.
Makamu wa Rais miradi endelevu wa Kampuni ya AngloGold Ashanti, GGM, Simon Shayo (kushoto)  akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa zoezi la upandaji wa Mlima Kilimanjaro  (Kilimanjaro Challenge 2018), litakalo kwenda sambamba na kuendesha harambee kuchangisha fedha  kwa mwaka 2018 kwa ajili ya kusaidia mapambano ya kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI nchini. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko.
Watendaji wa MGODI wa Dhahabu wa Geita (GGM) na  Tume ya Kuthibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) wakijadili jambo mara baada ya kumaliza mkuatano wa waandishi wa habari mapema leo.
Watendaji wa MGODI wa Dhahabu wa Geita (GGM) na  Tume ya Kuthibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) wakiwa katika picha ya pamoja  mara baada ya kumaliza mkuatano wa waandishi wa habari mapema leo.







Dar es Salaam: Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) kwa kushirikiana na Tume ya kuthibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) inatarajia kuzindua zoezi la upandaji wa mlima Kilimanjaro (Kilimanjaro Challenge 2018),  na kuendesha harambee ya kuchangisha fedha kwa mwaka 2018 kwa ajili ya afua za UKIMWI nchini. Shughuli hii inatarajiwa kufanyika tarehe 4 Mei 2018 mwaka huu katika Hoteli ya Hyatt Regency Kilimanjaro iliyopo jijini Dar es Salaam.

Mgeni rasmi katika uzinduzi huo anatarajiwa kuwa Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ambapo atafanya zozezi la ugawaji wa fedha zilizokusanywa mwaka mwaka jana 2017 zilizopatikana baada ya wadau mbalimbali kupanda na  kuendesha baiskeli kwa kuzunguzuka Mlima Kilimanjaro .

Kilimanjaro Challenge against HIV & AIDS ni mfuko unachangia juhudi za serikali  katika mapambano dhidi ya UKIMWI na kutoa elimu kwa jamii kuhusu maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI (VVU).

Kilimanjaro Challenge ni mfuko muhimu unaoshirikiana na taasisi za nje na ndani ya nchi katika kuendeleza mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kwa jamii ya Kitanzania na Dunia kwa ujumla ili kuwapa matumaini ya kuhakikisha jamii inabaki bila kuathiriwa na VVU/UKIMWI katika miaka ijayo.

Mfuko huo pia unalenga kuisaidia Serikali kukabiliana na VVU//UKIMWI sambamba na kutoa nafasi kwa watalii wa ndani na nje kuupanda mlima Kilimanjaro.

Takwimu zilizotolewa na Tume ya Kuthibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS), zimeonesha kupungua kwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka asilimia 5.1 %  mwaka 2011/ 2012 hadi asilimia 4.7% mwaka 2016/17.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa TACAIDS, Dkt. Leonard Maboko anasema, “ Mwaka wa 2016, inakadiriwa kuwa watu milioni 1.5 nchini wanaoishi na VVU na UKIMWI hadi sasa watu 225 wanapata maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa siku. Ugonjwa huu umewaathiri zaidi vijana na watoto yatima zaidi. Tunahitaji kubadilisha hali hii. Lengo la kukusanya fedha ni kuweza kusaidia serikali ya Tanzania katika jitihada zake kufikia sifuri tatu. Sifuri katika maambukizi mapya, sifuri ya unyanyapaa, sifuri katika vifo vitokanavyo na UKIMWI. 

TACAIDS kwa kushirikiana na Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) na wadau wengine kwa kupitia mpango huu wa Kili Challenge tunapenda kutoa mchango na ushirikiano wetu kwa Taifa ili kutunisha mfuko utakaowezesha kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa huu. Tuna matumaini ya kujenga timu imara yenye hamasa ya kupambana na janga hili. Tunatoa wito kwa makampuni na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi, wajitokeze ili tusaidiaane kutunisha mfuko wa Kili Challenge na mwishowe kufikia malengo yetu ya kuhakikisha tunakuwa na kizazi kisicho na maambukizi ya VVU/ UKIMWI,” alisema Dkt. Leonard Maboko.

“Watoto watakaoshiriki katika zoezi la Kilimanjaro Challenge mwaka huu ni wa kiume na wa kike wenye umri kuanzia miaka 13. Watoto hao yatima kutokana na tatizo la VVU/ UKIMWI wamesaidiwa na Kituo cha kulea watoto yatima cha Moyo wa Huruma Orphanage Center kilichopo Geita.

Changamoto kubwa inayotokana na janga hili ni pamoja na maelfu ya watoto yatima wanaohitaji misaada baada ya wazazi wao kufariki, wajane wasiokuwa na kipato, pamoja na wazee wanaolazimika kuwalea wajukuu walioachwa na watoto wao ambao walifariki kutokana kwa ugonjwa huo.


MZEE MAJUTO KUELEKEA INDIA KWA MATIBABU SIKU YA IJUMAA

MKONGWE NDIMARA ATAKA SERIKALI KUTOPEWA SABABU YA ‘KUBANA’ WAANDISHI WA HABARI

$
0
0
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit (wa pili kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Charles Stuart (wa pili kulia), Mkurugenzi Mkazi wa Taasisi ya Friedrich Ebert Stiftung Tanzania, Andreas Quasten (kushoto) pamoja na Afisa Utawala Msaidizi na Itifaki wa ofisi za Unesco Dar es Salaam, Rahma Islem (kulia) wakati wa kongamano la maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deo Ndenjembi akisalimiana na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit (kulia) mara baada ya kuwasili kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari zinazofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Kushoto ni Afisa Utawala Msaidizi na Itifaki wa ofisi za Unesco Dar es Salaam, Rahma Islem
 Mshehereshaji wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, Innocent Mungy (katikati), Mshauri wa Utawala Bora na Haki za Binadamu wa Ubalozi wa Sweden nchini, Anette Widholm Bolme (kushoto) pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Gasirigwa Sengiyumva wakipitia ratiba ya maadhimisho hayo yanayofanyika katika hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akisalimiana na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit mara baada ya kuwasili kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Wengine katika picha ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deo Ndenjembi (wa pili kushoto), Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Salome Kitomari (wa tatu kushoto), Afisa Utawala Msaidizi na Itifaki wa ofisi za Unesco Dar es Salaam, Rahma Islem (wa pili kulia) pamoja na Mshehereshaji wa kongamano hilo, Innocent Mungy (kulia).
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai (wa tatu kulia) akiongozana na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit (kulia), Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Salome Kitomari (wa pili kulia) pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deo Ndenjembi (kushoto) kuelekea kwenye mabanda ya maonyesho mara baada ya kuwasili kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akipitia nakala ya gazeti la Majira huku akipata maelezo kutoka kwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Majira, Imma Mbuguni (wa pili kulia) wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Kulia ni Meneja Usambaza wa Gazeti la Majira, Sophia Mshangama.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mjenga Uwezo wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Deogratius Bwire kuhusu shughuli mbalimbali zinazofanywa na mtandao huo  mara baada ya kuwasili kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari zinazofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Deo Ndenjembi (wa pili kushoto) na Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Salome Kitomari (wa tatu kushoto)
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akipokea nakala ya gazeti la Mwananchi kutoka kwa wafanyakazi wa Mwananchi Communications wakati akitembelea mabanda ya maonyesho kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akipata maelezo kutoka kwa Mmoja wa Wakurugenzi na Mmiliki wa Gazeti la Jamhuri Deodatus Balile wakati alipokuwa akitembelea mabanda ya maonyesho kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akipokea majarida na machapisho mbalimbali ya Umoja wa Mataifa kutoka Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo wakati alipotembelea banda la UN kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena mjini Dodoma.
 Afisa Programu wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Paul Mallimbo akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai kuhusiana na kitabu cha Maadili ya Uandishi wa Habari wakati alipokuwa akitembelea banda la Baraza la Habari Tanzania (MCT) kwenye kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma. Kulia ni Afisa Logistic wa Baraza hilo, Athuman Mbegu.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano tayari kuanza kwa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mshehereshaji wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, Innocent Mungy akiwakaribishwa meza kuu, wanahabari na wadau wa habari kwenye kongamano la  maadhimisho hayo yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Meza kuu kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Salome Kitomari, Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari nchini (UTPC), Jane Mihanji.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai akifungua kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit akitoa salamu za Unesco wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa Habari nchini (UTPC), Jane Mihanji akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai kufungua kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo akizungumzia malengo ya maendeleo endelevu na jukumu la waandishi wa habari kutumia nafasi zao kutoa taarifa kuhusu malengo hayo kwa jamii ili yatekelezeke kwa urahisi, katika kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mtaalamu wa Masuala ya Vyombo vya Habari na Mkufunzi wa kujitegemea, Rose Haji Mwalimu akiongoza mjadala kuhusu mada: Wajibu wa Uongozi, Vyombo vya Habari na Sheria katika kuhakikisha haki inatendeka na kuonekana inatendeka wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Mwandishi wa Habari Nguli, Ndimara Tegambwage na mwezeshaji wa mada inayohusu; Wajibu wa Uongozi, Vyombo vya Habari na Sheria katika kuhakikisha haki inatendeka na kuonekana inatendeka: wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Wakili na Mwandishi wa Habari ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi ya MISA-TAN, James Marenga akichangia mada wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Nashera jijini Dodoma.
 Mdau wa Habari Ernest Sungura akishiriki kuchangia maoni katika mjadala uliowasilishwa na mwandishi nguli Ndimara Tegambwage (hayupo pichani) wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Habari Unesco nchini, Nancy Kaizilege (kulia) na Mshauri wa Utawala Bora na Haki za Binadamu wa Ubalozi wa Sweden nchini, Anette Widholm Bolme wakati wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.





Pichani juu na chini Sehemu ya washiriki ambao ni wahariri, waandishi wa habari, wadau wa tasnia ya habari na wageni waalikwa waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wakiwemo wahariri, wadau wa habari na waandishi wa habari waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa habari na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, Ubalozi wa Umoja wa Ulaya pamoja na wamiliki wa vyombo vya habari vya kijamii waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja waandishi wa habari wakonge (Veterans) waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
 Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja mameneja wa redio za kijamii waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.
Mgeni rasmi Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Job Ndugai katika picha ya pamoja wanafunzi wa Dodoma College of Journalism waliohudhuria kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini yanayofanyika katika Hoteli ya Morena jijini Dodoma.


Na Mwandishi wetu, Dodoma
WAANDISHI wa habari wanapaswa kuandika na kutangaza habari zao kwa weledi na kuzingatia maadili ili kuepuka kuandika habari zinazoipa serikali sababu ya kufungia vyombo vyao.
Kauli hiyo imetolewa mwandishi wa habari mkongwe nchini Tanzania Bw. Ndimara Tegambwage wakati akitoa mada ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania kwenye kongamano la maadhimisho ya siku ya Uhuru Wa Vyombo vya Habari Duniani ambayo nchini Tanzania yanafanyika kitaifa mkoani Dodoma.
Kila Mei 2-3 kila mwaka ni siku za kimataifa ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani.
Aidha katika mada yake hiyo Ndimara alisema Serikali barani Afrika zimekuwa zikikosa uvumilivu na kunyima uhuru vyombo vya habari licha ya kuwa uhuru huo unatambuliwa na katiba za mataifa ya Afrika.
Bw. Ndimara amebainisha kuwa, wakati serikali za Africa zikitoa haki ya kusajili vyombo vya habari hususani Radio, Runinga na Magazeti, serikali zinapokosolewa huvifungia vyombo hivyo kwa tuhuma za kukiuka maadili jambo ambalo alidai kuwa si la ukweli.
Mkongwe huyo wa tasnia ya habari nchini Tanzania amebainisha kuwa serikali nyingi barani Afrika zimekosa uvumilivu na kutumia nguvu nyingi kunyamanzisha wanahabari.
Huku akinukuu hotuba ya Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai ambaye ameonya kuwepo kwa wananchi wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya aliwataka waandishi wa habari kuwa makini kutokana na sheria mbalimbali zinazowazunguka zinaohitaji weledi wa hali ya juu katika kuhabarisha.
Awali akitoa hotuba ya ufunguzi wa kongamano la maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari nchini Tanzania, Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amesema Tanzania inautambua mchango wa vyombo vya habari katika kurahisisha mawasiliano ya jamii na kuharakisha maendeleo lakini inakwazwa na kuwepo kwa baadhi ya vyombo vya habari na wanahabari ambao huandika habari nyingi za kutungwa na za uongo.
Katika hotuba hiyo alilaani matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii akitaja kuwa inaongoza kwa kuwa na habari nyingi za kujitungia na zenye upotoshaji na kwamba Bunge ni mhanga wa upotoshaji wa habari zinazoandikwa na baadhi ya waandishi katika mitandao ya kijamii.
Akizungumzia ufanisi wa vyombo vya habari na wanahabari wenyewe Spika Ndugai aliwataka waandishi kuwa marafiki na kuacha tabia za kudharauliana  na kushauri ipo haja ya kuwekana sawa kwa maslahi mapana zaidi ya kitaaluma na jamii kwa ujumla.
Pia alizungumzia vyombo vya habari kusaidia mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi na kusema kalamu ikitumika vyema itasaidia sana mapambano hayo.“Wajibu mwingine wa vyombo vya habari ni mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi, lakini zoezi  hili huwa na matokeo chanya kama litazingatia ukweli na maadili yaliyopo” alisema Spika Job Ndugai na kuongeza kuwa bunge linajua changamoto zilizopo na kwamba wapo tayari kutoa ushirikiano.
“Bunge letu linajua changamoto ambazo baadhi ya wanahabari mnazipitia, tuko tayari kushirikiana nanyi kuona tasnia yetu ya habari inaboreshwa”  alisema Ndugai.
Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkazi wa Unesco ambaye pia ni Mshauri wa Masuala ya Mawasiliano Kanda ya Afrika Mashariki ofisi ya Unesco Nairobi, Jaco Du Toit amesema vyombo vya habari ni muhimu kwa maendeleo kwa hiyo ni lazima viwe huru ili viweze kutekeleza kazi yake.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA-TAN), Salome Kitomari, alieleza kusikitishwa kwake na matukio yanayoashiria kubinya uhuru wa vyombo vya habari  na pia kuitaka serikali kuwajibika katika kuwalinda waandishi wa habari.Wawakilishi wa radio jamii Tanzania wanasema pamoja na kufanyakazi kubwa ya kuelimisha jamii vijijini, serikali haijavipatia kipaumbele kama inavyofanya kwa vyombo vikubwa na vya kitaifa.
Akizungumza na waandishi wa habari Kiongozi wa Kituo cha Habari cha mkoani Radio FM cha visiwani Pemba Bw. Maalim Ali Abass alisema Radio za vijijini zinapokumbwa na kosa lolote la kitaaluma mema mengi wanayofanya kwa kujitolea husahaulika haraka na kujikuta katika hekaheka na serikali.

RAIS DKT MAGUFULI AWAANDALIA CHAKULA CHA JIONI WAZEE WA IRINGA, VIONGOZI WA DINI NA SIASA, TUCTA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwakaribisha wazee wa Kihehe kwenye hafla ya chakula cha jioni aliyowaandalia wao pamoja na viongozi wa dini, siasa na wa TUCTA katika Ikulu ndogo ya mjini Iringa usiku wa Mei Mosi
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasikiliza Naibu Chifu wa Wahehe Gerald Malangalila akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi wakielezea historia ya Iringa katika hafla hiyo
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahigaakisimulia  historia ya machifuIringa katika hafla hiyo
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwakaribisha wazee wa Kihehe kujipatia  chakula cha jioni aliyowaandalia wao pamoja na viongozi wa dini, siasa na wa TUCTA katika Ikulu ndogo ya mjini Iringa usiku wa Mei Mosi
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na wageni wengine wakimsikikiza Mbunge wa Iringa mjini kwa tiketi ya CHADEMA Mch. Peter Msigwa akiongea machache wakati wa hafla hiyo ya  chakula cha jioni  Ikulu ndogo ya mjini Iringa usiku wa Mei Mosi

Madiwani wa kata mbalimbali za mji wa Iringa waliohamia CCM kutoka CHADEMA wakijitambulisha kwenye hafla hiyo. Picha na IKULU

DC KIGAMBONI AWAONDOLEA TAHARUKI WANANCHI WA KIBADA KUBOMOLEWA NYUMBA ZAO

$
0
0
  Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni  Mh.Hashim Mgandilwa mwenye kofiaakizungumza na wakazi wa Kibada kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jana.
 Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mh.Hashim Mgandilwa akisistiza kuwa Sheria itafuatwa kuhakikisha wananchi wanapata haki yao.
 Mkuu wa wilaya ya Kigamboni Mh.Hashim Mgandilwa na wananchi wa kibada wakisoma ra,mani ili kubaini mipaka .
 Diwani wa Kata ya Kibada Mh.Amin Sambo  akishiriki kuchimba eneo linalodaiwa kuwa na jiwe la mpaka kwenye eneo la mkazi wa Kibada wakati walipokuwa wakitafuta mawe ya Mipaka.
 Kamati ya ulinzi na usalama na waanchi wakizulu kwenye moja ya nyumba iliyowekwa alama ya kubomoa na wakala wa barabara Tanroads ili kubaini mpaka uliopo.
  Mthamini wa Manispaa ya Kigamboni Bw.Mpoki Daimon  akifafanua taratibu za uthamini na ulipwaji fidia kwa wananchi wa Kata ya Somangila Mtaa wa Dege.
Baadhi ya wananchi na wataalamu mbalimbali  walishirki kwenye mkutano huo wa hadhara Kibada.

FREE STOPOVERS OFFERED BY ETIHAD TO ALL ECONOMY CLASS GUESTS FROM THE MIDDLE EAST, AFRICA & PAKISTAN

$
0
0
Abu Dhabi, United Arab Emirates – Etihad Airways is offering one night’s free accommodation in Abu Dhabi to all guests travelling in Economy Class from destinations* in the Middle East, Africa and Pakistan, and stopping over in the nation’s capital.

The offer is valid from 1 May 2018 until 15 September 2018 and the travel period is until 30 September 2018. The hotels included in the offer are the Radisson Blu on Yas Island and the Yas Island Rotana.

Mohammad Al Bulooki, Etihad Airways’ Executive Vice President Commercial, said: “Etihad Airways is delighted to invite guests to experience Abu Dhabi, a city which has so much to offer every type of traveller, especially during a short stopover.

“Five million guest arrivals were recorded in Abu Dhabi in 2017, proving that the emirate continues to attract greater numbers of leisure visitors each year.”

Guests can take advantage of world-famous leisure and business attractions, including miles of beautiful white sand beaches, theme parks such as Yas Waterworld, Ferrari World Abu Dhabi and the soon-to-be-launched Warner Bros. Theme Park.

There are unforgettable desert safari expeditions, arts and cultural institutions such as Manarat Al Saadiyat and the Louvre Museum; exquisite local and international dining, world-class golf, and Yas Marina Circuit.Abu Dhabi also offers a wide range of shopping opportunities to suit all tastes with a large choice of popular outlets and brands.

The city boasts a selection of spacious high-end shopping malls such as Yas Mall, Abu Dhabi Mall, Marina Mall, and The Galleria – one of the world’s most luxurious shopping centres.Etihad Airways has been running stopover programmes since 2011 and offering guests a variety of services including airport meet & assist, transportation, accommodation, tours, and visa processing services.

For further details on the deals, guests can visit etihad.com; Etihad Contact Centre; Etihad Retail Shops; or the airline’s trade partners.

* The countries in the offer are South Africa, Pakistan, Saudi Arabia, Morocco, Egypt, Jordan, Nigeria, Kuwait, Tanzania, Kenya, Bahrain, Oman, Sudan, Lebanon.
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images