Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

Tigo Pesa Yapata Uthibitisho wa Huduma za Kifedha Kutoka Shirika la Kimataifa la GSMA (Action Requested)

$
0
0

‘GSMA Mobile Money Certification’ inatoa muongozo ili kuhamasisha utoaji wa huduma bora zaidi za kifedha kwa wateja wetu.

Dar es Salaam, 13 Aprili, 2018.  

Tigo Pesa, huduma ya kifedha kwa simu za mkononi inayoongoza nchini, imepokea uthibitisho wa kimataifa ujulikanao kama ‘GSMA Mobile Money Certification’.

Uthibitisho huu unatambua uwezo mkubwa wa Tigo Pesa katika kutoa huduma salama, kwa uwazi, za kuaminika na thabiti zinazokuza haki za wateja na kuzuia miamala ya kihalifu.

Tigo Pesa ni moja kati ya watoa huduma za kifedha kwa simu za mkononi wa kwanza kabisa duniani kupokea uthibitisho huu kutoka GSMA.

GSMA Mobile Money Certification’ ni mkakati wa kimataifa unaolenga kuleta huduma za kifedha salama, wazi na thabiti zaidi kwa mamilioni ya watumiaji wa huduma za kifedha kwa simu za mkononi duniani kote. Huku kukiwa na zaidi ya akaunti 690 milioni za fedha kwa simu za mkononi duniani, sekta ya simu za mkononi inaboresha maisha duniani na imewezesha mamilioni ya watu wasiokuwa na akaunti za benki kufikiwa na huduma rasmi za kifedha.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Afisa Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu za Mkononi wa Tigo, Hussein Sayed alisema, “Tigo Pesa inajivunia mchango wake mkubwa katika kufanikisha upatikanaji wa huduma rasmi za kifedha nchini kwa kutoa fursa kwa mamilioni ya Watanzania wasio na huduma za kibenki kuwa sehemu ya mfumo rasmi wa kifedha.’
Uthibitisho huu kutoka GSMA ni ishara tosha kuwa Tigo Pesa imepiga hatua kubwa kuhakikisha kuwa fedha za wateja wetu zipo salama, na kuwa haki zao zinalindwa. Kupitia taratibu zetu za kibiashara tunalenga kutoa huduma zenye viwango vya juu zaidi.  

GSMA imebainisha kuwa vigezo vinavyotumika kutoa uthibitisho huu vinazingatia viwango vya ubora wa kimataifa katika utoaji huduma za kifedha. Kabla ya kupokea uthibitisho huo, kila mtoa huduma wa fedha kwa njia ya simu za mkononi sharti afikie asilimia 100% ya vigezo vilivyowekwa. Watoa huduma wanaopokea uthibitisho huu ni wale tu waliofanikiwa kuonesha kuwa hatua za uendeshaji wa biashara zao ni miongoni mwa zile zilizo bora, zinazoaminika na kuwajibika zaidi katika mfumo mzima wa utoaji huduma za kifedha duniani.
“Tigo Pesa inajivunia kufikia vigezo vilivyotuwezesha kupokea uthibitisho huu kutoka GSMA. Hii inaonesha ubora na uwajibikaji katika huduma zetu. Vile vile inathibitisha kuwa tunaongoza katika mageuzi ya kidigitali na utoaji wa huduma za kifedha ulimwenguni,’ Hussein aliongeza.
Pamoja na azma ya Tigo kutoa huduma za kiwango cha kimatifa kwa wateja wetu, huduma yetu ya Tigo pesa imeboreshwa na kuwa mfumo kamili wa huduma za kifedha. Daima tupo mstari wa mbele katika ubunifu wa huduma katika soko hili; kwa mfano tulikuwa mtoa huduma wa kwanza duniani kuzindua huduma ya fedha kwa simu za mkononi iliyowezesha uhamishaji wa fedha kwenda mitandao mingine nchini. Pia tulianzisha huduma ya kwanza Afrika Mashariki iliyowezesha wateja kufanya miamala ya fedha kupitia simu za mkononi kwenda nje ya nchi kwa kubadili thamani ya fedha kwa sarafu ya nchi husika. Tigo pia ndio kampuni ya kwanza ya simu za mkononi kutoa gawio la faida kwa wateja wetu.
‘Uthibitisho huu wa GSMA unaashiria uendeshaji wa biashara yetu unazingatia mojawapo ya mifumo bora zaidi duniani. Tigo Pesa inaaminika na kuwajibika, hivyo ni mshirika bora wa kibiashara,’ Afisa huyo Mkuu wa Huduma za Kifedha kwa Simu za Mkononi wa Tigo alibainisha.

‘GSMA Mobile Money Certification’ unaonesha mwamko mkubwa kwa upande wa watoa huduma kuzuia utakatishaji wa fedha na ufadhili wa ugaidi; pamoja na kutoa huduma bora, za uhakika, salama na zisizokuwa na upendeleo kwa wateja na washirika wote wa kibiashara.


Dkt. Harrison Mwakyembe Atoa Maagizo Mazito kwa Uongozi wa StarMedia na TBC

Serikali Itaendelea kutenga Bajeti ya Kutosha kwa ajili ya Maendeleo ya SIDO-Mhe. Charles Mwijage

WAZIRI JENISTA MHAGAMA AFUNGUA MKUTANO WA WADAU KUJADILI NAMNA BORA ZAIDI YA UTEKELEZAJI WA SHERIA YA FIDIA KWA WAFANYAKAZI

$
0
0



  

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, DODOMA

SERIKALI ilianzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kwa lengo la kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanapata mafao bora na stahiki ya fidia tofauti na sheria ya zamani iliyotoa viwango vya chini vya fidia, lakini pia kuwawezesha waajiri kupata muda zaidi kushughulikia masuala yao ya uzalishaji na uendeshaji.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi , Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama mjini Dodoma mwishoni Aprili 13, 2018, wakati akifungua mkutano wa wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF-Tawi la Dodoma) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA-Tawi la Dodoma) na Chama cha Waajiri Tanzania, (ATE), kwa lengo la kujadiliana namna bora zaidi ya utekelezaji wa sheria ya fidia kwa wafanyakazi.

Mhe. Waziri alisema viwango vya juu vya malipo ya fidia kwa wafanyakazi walipokuwa wanaumia kazini kabla ya sheria ya kuanzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, ilikuwa ni shilingi 108,000/=kwa mfanyakazi aliyepata ajali au kuumia kazini, lakini pia sheria inasema kulikuwa na malipo mengine ya shilingi 83,000/= kwa mfanyakzi aliyefariki kwa ajali au ugonjwa kutokana na kazi aliyokuwa akifanya na malipo hayo yalitegemea pia mkataba wa ajira yake unasemaje.

“Serikali ilikuja na sheria mpya baada ya kuona viwango hivi kwa ubinadamu na kwa hali halisi, vilikuwa vimepitwa sana na wakati na wafanyakazi walikuwa wanapata fidia hiyo kwa kadhia kubwa sana na viwango hivyo haviendani na ukuaji wa uchumi na kwa wakati tulionao.” Alifafanua Mhe. Waziri.

Aidha Mhe. Waziri alisema, Mfuko unafaida kubwa sio tu kwa wafanyakazi bali pia kwa waajiri na taifa kwa ujumla ambapo wafanyakazi sasa wanauhakika wa kupata kinga ya kipato kutoakana na majanga ambayo yatasababishwa na ajali, magonjwa ama vifo kutokana na kazi wanazofanya, lakini waajiri nao watapata muda zaidi wa kushughulikia masuala yao ya uzalishaji na uendelevu wa biashara na shughuli zao kwani Serikali kupitia Mfuko itabeba mzigo wote wa gharama pindi mfanyakazi atakapofikwa na janga lolote awapo kazini.

“Pamoja na uchanga wake, Mfuko huu ambao umeanzishwa mwaka 2015 umeonyesha mafanikio makubwa katika kipindi kifupi kwani hadi sasa waajiri ambao wameshajisajili kwenye mfuko wetu ni 13,500 na wafanyakazi wao ambao wamepatwa na majanga wakiwa kazini wameshalipwa fidia na Mfuko fedha zisizopungua shilingi bilioni 2.52 kufikia Februari 2018.” Alibainisha.

Alisema Mfuko umekuja wakati muafaka kwani nchi inakwenda kwenye uchumi wa viwanda bila shaka kutakuwepo na ongezeko la ajali na magonjwa yanayotokana na uendeshaji wa shughuli katika viuwanda vyetu hivyo ni lazima kiwepo chombo kitakachosimamia majukumu haya ya fidia ili kuwapa nafasi pana waajiri kuendelea na shughuli zao za uzalishaji.


“Rais wetu wa Jamhuri ya uungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli kila wakati tunapokutana kwenye baraza la Wafanyabiashara Tanzania amekuwa akituagiza sisi wasaidizi wake, kama kuna jambo lolote linajitokeza na sekta binafsi inafikiri kwamba jambo hili bado halijaeleweka na haliko sawasawa ni wajibu wetu sisi mawaziri kuchukua hatua haraka za kukutana na kujadiliana na wadau na kushauriana na wadau husika ili kufikia muafaka na kuelewana ili kwenda pamoja na ndio maana leo tuko hapa.” Alifafanua Mhe. Waziri Jenista Mhagama.


Wakitoa ushuhuda mbele ya washiriki wa mkutano huo, Wafanyakazi waliopatwa na majanga ya kuumia au kufiwa na wenza wao, wameipongeza Serikali kwa kuanzisha Mfuko huo kwani umekuwa ni mkombozi kwa wafanyakazi.

“Mimi nilikatika mkono wakati nikitekeleza majukumu yangu ya kazi kwenye Kampuni ya Reli Tanzania, (TRL), na WCF imenilipa fidia ya mkupuo na inaendelea kunilipa pensheni ya kila mwezi, shilingi 170,000/= kwa maisha yangu yote nitakapokuwa hai.” Alisema Bw.Fortunatus Kiwale

Naye Mfanyakazi mwingine wa Kampuni ya Frank Pile International Project Limited ya jijini Dar es Salaam, Bw. Patrick Millinga, yeye alisema Mfuko umemlipa fidia ya zaidi ya shilingi milioni 31.9 baada ya kupoteza jicho lake la kushoto kutokana na kugongwa na kipande cha chuma wakati akitekeleza majukumu yake ya kazi.

Mwingine aliyetoa ushuhuda wa faida ya Mfuko kwa wafanyakazi, ni mama mjane, Bi. Petronila Mligo, ambaye yeye alifiwa na mumewe katika ajali ya gari wakati akirejea kituo chake cha kazi jijini Mwanza akitokea Dodoma.

“Mfuko umenilipa fidia ya mkupuo kutokana na kifo cha mume wangu, lakini pia ninaendelea kulipwa pensheni ya kila mwezi mimi na watoto wangu wawili, ambapo kila mtoto analipwa shilingi 175,000/= na mimi ninalipwa shilingi 375,000/=.” Alisema mama huyo mjane ambaye ni mwalimu.

Akiwasilisha mada mbele ya washiriki, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba alisema Mfuko unaendeshwa kwa msingi wa utatu ambapo katika bodi ya wadhamini ambayo ina uwakishi wa serikali, wafanyakazi na uwakilishi wa waajiri kama ambavyo Shirika la Kazi Duniani linavyotaka katika masuala haya ya fidia kwa wafanyakazi.

Alisema, katika mfumo wa zamani, mfanyakazi anapotoka au kwenda kazini endapo atapatwa na tatizo njiani sheria ya zamani haikumtambua, tofauti na sheria ya sasa ambapo inaeleza mfanyaakzi akiumia au akifikwa na umauti wakati akitoka kazini au akielekea kazini sheria ya sasa inataka afidiwe.

“Alisema Mfuko umeweka utaratibu ili kuhakikisha mfumo wa usajili wa waajiri unakuwa wa haraka na rahisi lakini pia kushughulikia masuala ya ulipaji fidia katika kipindi kifupi.” Alisema.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi , Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, akihutubia wakati wa mkutano wa wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF-Tawi la Dodoma) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA-Tawi la Dodoma), uliofanyika jengo la LAPF mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Mkuta huo ulioandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, ulilenga kutoa elimu zaidi kwa wadau na kujadiliana kuhusu namna bora zaidi ya uendeshaji wa shughuli za Mfuko huo kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw.Eric Shitindi, akitoa hotuba ya ukaribisho wakati wa mkutano wa wadau wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF-Tawi la Dodoma) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA-Tawi la Dodoma), uliofanyika jengo la LAPF mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Mkuta huo ulioandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, ulilenga kutoa elimu zaidi kwa wadau na kujadiliana kuhusu namna bora zaidi ya uendeshaji wa shughuli za Mfuko huo kuhsuu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi , Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, (Wanne kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, Bw. Masha Mashomba, (Wakwanza kushoto), wakisalimiana na wanufaika wa Fidia kwa Wafanyakazi wa (WCF), Bw. Patrick Millinga, (wakwanza kulia) na Bi. Petronila Mligo, (wapili kushoto), wakati wa mkutano wa wadau wa Mfuko, Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF-Tawi la Dodoma) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA-Tawi la Dodoma, na kufanyika jengo la LAPF mjini Dodoma. Mkuta huo ulilenga kutoa elimu zaidi na kujadiliana kuhusu namna bora zaidi ya uendeshaji wa shughuli za Mfuko huo. Wengine pichani ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, (Kazi, Vijana na Ajira), Mhe. Antony Mavunde, (watatu kulia), Mwakilishi wa ATE, Bw. Almasi Maige, (wapili kushoto) na Katibu Mtendaji wa TCCIA-Dodoma, Bw.Iddi Senga.

Mkutano ukiendelea

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi , Ajira, Vijana na Watu Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama,(katikati), na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Mashan Mshomba, (kulia), wakimsikiliza Niabu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Mhe. Antony Mavunde, wakati wa mkutano wa wadau wa Mfuko, Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, (TPSF-Tawi la Dodoma) na Chama cha Wafanyabiashara ya Viwanda na Kilimo (TCCIA-Tawi la Dodoma), uliofanyika jengo la LAPF mjini Dodoma mwishoni mwa wiki. Mkuta huo ulioandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu, ulilenga kutoa elimu zaidi kwa wadau na kujadiliana kuhusu namna bora zaidi ya uendeshaji wa shughuli za Mfuko huo kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi.

Baadhi ya washiriki

Baadhi ya washiriki

Baadhi ya washiriki
Washiriki wakifuatilia hotuba ya Mhe. Waziri.

Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba akiwa na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalaam Omar, (kushoto) na Mkurugenzi wa Uendeshaji, Bw. Anselim Peter, akijibu baadhi ya hoja zilizojitokeza wakati wa mkutano huo wa majadiliano na wadau.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Eric Shitindi, (kushoto), akiwa na Bw. Mshomba.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, (WCF), Bi. Laura Kunenge, akizungumza jambo wakati wa mkutano huo.

Mhe. Waziri Jenista Mhagama, akizungumza na waandishi wa habari.

Mhe. Waziri akiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wakati akiwasili ukumbini.

Mnufaika wa Fidia, Bi. Petronila Mligo, akitoa ushuhuda wa faida anayopata kutokana na uwepo wa Mfuko, baada ya kufiwa na mumewe akiwa kwenye safarin ya kikazi.

Bw. Patrick Millinga, naye akitoa ushuhuda kutokana na Fidia aliyopata kutoka WCF baada ya kupoteza jicho lake la kushoto wakati akitekeleza majukumu yake ya kikazi.

Mhe. Waziri Mhagama akisalimiana namnufaika mwingine wa Fidia, Bw. Fortunatus Kiwale


Picha ya kwanza ya pamoja.

Picha ya pili ya pamoja.

Ecobank Group washirikiana na MTN kuwezesha huduma zaidi za fedha barani Afrika

$
0
0
Pichani kuanzia Kushoto kwenda Kulia ni Charles Kie, Mkurugenzi Mtendaji wa, Ecobank Nigeria Ltd; Serigne Dioum, Mtendaji wa MTN’s , Hudma za kifedha kwa njia ya mtandao; Ade Ayeyemi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa, Ecobank Transnational Incorporated (ETI), Rob Shuter, Ofisa Mtendaji mkuu wa MTN na Patrick Akinwuntan, Mtendaji wa Ecobank Transnational Incorporated (ETI) Na Mwandishi wetu



KAMPUNI ya simu MTN imeingia ubia na moja ya benki inayoongoza barani Afrika ya Ecobank Transnational Incorporated (ETI) kuwezesha wateja wao kufaidika na huduma za kifedha zinazotolewa na makampuni hayo.

Imeelezwa kuwa MTN ikijivunia idadi kubwa ya wateja wanaotumia huduma zake mbalimbali; mtandao mkubwa wenye uhakika; bidhaa zenye ubunifu na huduma zake za kifedha kwa mtandao imeungana na Ecobank kuwezesha wateja wao kuanzisha kufungua akaunti na kupitisha miamala yao kupitia mtandao wa MTN.

Makampuni hayo mawili maarufu barani Afrika yametiliana saini mkataba wa makubaliano utakaowezesha kushirikiana katika kubuni na kuwezesha huduma za kifedha zenye ubora wa kiwango cha juu kati ya benki hiyo na mtandao wa simu wa MTN.

Miongoni mwa huduma zitakazotolewa ni kuwezesha miamala mbalimbali kufanyika kwa kutumia simu na akaunti za benki.

Kutumia mitaji iliyopo katika uwekezaji ndani ya Ecobank na MTN kuwezesha miamala ya kimataifa kufanyika kidigitali.

Aidha makubaliano hayo yatachochea ubunifu wa bidhaa mbalimbali katika upande wa hifadhi ya fedha kwa njia ya mtandao na ukopeshaji wake na kutoa nafasi ya malipo kwa njia ya mtandao kwa wateja, wafanyabiashara na mashirika mbalimbali.

Ade Ayeyemi, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Ecobank anasema: “ Mabadiliko ya kidigitali katika mifumo ya benki na simu kunatengeneza fursa za namna bora ya kuwezesha kutoa huduma za kifedha. Afrika inalazimika kwenda mbio katika digiti ili kuwezesha fursa zilizopo zitumike kuwatumikia wateja. MTN na Ecobank leo wamechukua hatua kubwa kuwezesha fursa hizo” .

Pia alisema kwamba mkakati wa benk hiyo wa kidigiti kwa muda mrefuj umelenga kuhakikisha nafuu ya uwezeshaji wa miamala katika soko. Akizungumzia ushirikiano huo Ofisa Mtendaji Mkuu na Rais, Rob Shuter alisema: “Ushirikiano kati ya mabenki na watoaji wa huduma za miamala kwa njia ya simu ni muhimu, hivyo uhusiano wetu wa muda mrefu na Ecobank umelenga kuwezesha huduma za fedha kuwafikia wananchi wengi na kwa urahisi zaidi. Tumefurahishwa na maafikiano haya kwani yametupeleka hatua nyingine, kwani ushirikiano wetu utawezesha ubunifu utakaowezesha huduma za fedha kupenya kila mahali katika bara hili.”

WANANCHI WATAKIWA KUJIUNGA NA MIFUKO YA AFYA JAMII ILI KUKWEPA GHARAMA ZA MATIBABU

$
0
0
RS TABORA

SERIKALI imezitaka jamii kujiunga na mifuko ya huduma za bima za jamii ili waweze kupata huduma ya tiba kwa gharama nafuu badala ya kutumia mtindo wa kulipa fedha taslimu wanapokwenda kutibiwa.

Kauli hiyo ilitolewa jana Wilayani Nzega na Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati akizungumza na wakazi wa Zogolo mara baada ya kukizindua.

Alisema kazi wananchi ambapo hajajiunga na Mifuko ya Afya ya Jamii(CHF) na mingine wanajikuta wakitumia fedha nyingi kwa ajili ya matibabu wakati wangekata Bima za viwango tofauti wangenufaika.

Waziri huyo alisema mtu akimkatia mtoto wake mdogo Bima ya Afya ya shilingi elfu 50 atapata huduma za matibabu mwaka mzima katika Hospitali yoyote hapa nchini zikiwemo za binafsi ambazo zina makataba na Serikali kupitia Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa. Aliwataka Madereva wa boda boda wilayani Nzega nao kujiunga na Bima kwa kulipia shilingi 76000 ili waweze kupata matatibu mwaka mzima popte pindi wanapopata ajali au wanapougua na kuongeza kuwa kwa kutegemea fedha taslimu ni gharama kubwa.

Waziri huyo aliwambia wakijunga pamoja na kutoa kiasi hicho atawaunganisha ili waweze kupata vitambulisho vya Bima ambavyo vitawaweze kupata matibabu kwa gharama nafuu na fedha nyingine kuzielekeza katika shughuli nyingine za maendeleo. “unapokwenda kufanyiwa upasuaji unaweza kutozwa shilingi 100,000/- lakini ukiwa umetoa shilingi elfu 30 kupitia kujiunga Mfuko wa Afya ya Jamii , utatumia kadi kupata huduma hiyo katika Hospitali yoyote bila kudaiwa chochote” alisisitiza Ummy

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa Aggrey Mwanri alisema kuwa mwitikio wa wananchi Mkoani humo kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) bado uko chini na kuongeza kuwa wameamua kuendesha elimu kupitia mikutano mbalimbali kwa lengo la kuongeza idadi inaongezeka.

Alisema kuwa sehemu kubwa ya wakazi ni wakulima ambao wanategemea mavuno ya msimu kujipatia kipato kwa ajili ya mahitaji mbalimbali ikiwemo matibabu na hivyo kupata shida wakati mwingine kwa kutokuwa na uwezo wa kulipia gharama kwa fedha tasilimu kwa kuwa fedha zinakuwa hazipo tena hadi mavuno mengine.

Mwanri alisema njia ya pekee ya kuwasaidia wakulima ni kuhakikisha wengi wao wamejiunga na Mfuko wa Jamii ambapo wakitoa shilingi 10,000 wanapata matibabu watu sita katika familia moja.

MTOTO WA MKULIMA WAZIRI MKUU MSTAAFU PINDA ATAJA MUAROBAINI WA KUZUIA UCHOMAJI MISITU

$
0
0

 Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda, "Mtoto wa Mkulima" akionyesha furaha yake baada ya kuzindua nembo ya "Malkia wa Asali" kwenye hoteli ya Morena mjini Dodoma leo Aprili 14, 2018.



NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, DODOMA

WAKATI kuna wimbi la uchomaji misitu ovyo hapa nchini, “Mtoto wa Mkulima, Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda ametoa “dawa” ya kuzuia uharibifu huo wa maliasili na si nyingine bali ni kufuga nyuki.

Waziri Mkuu huyo mstaafu ambaye alipenda kujitambulisha kama mtoto wa mkulima kutokana na mapenzi yake katika Kilimo, alitoa “elimu” hiyo leo Aprili 14, 2018 wakati akizindua nembo ya “Malkia wa Asali Tanzania” kwenye Hoteli ya Morena mjini Dodoma. 

“Sisi upande wa Katavi tulichofanya, nilmwambia mkuu wa Mkoa sisi kuchoma choama misitu ni “tradition” (utamaduni) yaani kuchoma ni jambo la kawaida na ukitaka kuzuia hili jaribu kutumia ufugaji wa nyuki kama silaha ya kuzuia uchomaji wa miti.” Alisema na kuendelea. 

Kwa hivyo alichofanya maeneo kama Inyonga, tulitenga maeneo na kuweka mabango yetu tukaweka wafugaji wa nyuki na kuwaambia ninyi ndio walinzi wetu na tangu tufanye hivyo kumekuwepo na hali nzuri sana, na uchomaji moto umepungua sana, alisema. 

Mheshimiwa Pinda alitoa mfano mwingine jijini Mbeya (Mbeya city), ambako mji umezungukwa na milima mizuri yenye misitu ambayo imekuwa ikiharibiwa na uchomaji moto mara kwa mara. 

“Alitokea baba mmoja Askofu Mwalyego siku moja akaja kuniambia baba mimi hii inanikera kama inavyokukera sana wewe, hivi nikijaribu ku-introduce ufugaji wa nyuki hapa itasaidia, nikamwambia try (jaribu), ameweka wafugaji wa nyuki kuzunguka milima pale Mbeya mjini na mimi nikamwambia I will buy all your honey na juzi nikawa namuuliza zoezi langu linakwendaje, akaniambia nina miaka miwili mitatu sijaona moshi kwenye lile eneo. 

Kutokana na uzoefu huo Mtoto wa Mkulima akatoa hakikisho kuwa “Hii ni silaha moja nzuri kwa sababu mtu akielewa halimpi shida hata kidogo.” Alisema. Mhe. Pinda pia alisema, ufugaji nyuki pia ni silaha ya kuzuia ujangili wa wanyama na kutolea mfano wa hifadhi ya misitu huko Kigoma na alipokutana na CEO pale masikitiko yake makubwa ilikuwa ni sula la ujangili na ushauri wangu nilimwambia akae na wafugaji nyuki, walau kuzunguka eneo hiulo la misitu. 

“Yule bwana alijaribu na nilipomtembelea mara ya pili aliruhusu wafugaji na mfugaji bwana ukimwambia ukimwambia ukiruhusu kuingia hapa mtu ambaye hatumjui tunakufukuza hapa unaondoka na anajua ndoo moja laki moja inamkosa hakubali na kwakweli wamefanya kazi nzuri na amewafanya sasa kama askari wa wanyamapori.” Alifafanua 

Akizungumzia faida ya asali, Mhe. Pinda alisema ni chakula kilichobeba virutubisho vyote ambavyo binadamu anahitaji lakini si hivyo tu, asali imekuwa na soko kubwa ulimwenguni na inaweza kuwa chanzo kimoja cha kukuza uchumi kwa wananchi na taifa kwa ujumla.

“Nawaomba sana waheshimiwa wabunge, mimi nilishatoka huko, lakini bwana Camara hapa anachohitaji ni visemeo juu ya umuhimu wa sekta hii, ni sekta ndogo lakini mchango wake unaweza kusaidia sana katika uchumi. 

Aidha Mheshimiwa Pinda alisema, nchi yetu imejaliwa kuwa na eneo kubwa sana la misitu kuliko nchi nyingi na kusikitishwa wakati alipokwenda Addis-Ababa Ethiopia ambapo aliposoma jarida, aliona eti Ethiopia ndio namba moja kwa uzalishaji asali barani Afrika, nikamwambia Camara hivi Ethiopia ina uoto gani wa asili wa kuizidi Tanzania? 

Alisema, mahitaji ya asali Tanzania ni zaidi ya tani 140,000 na anaamini ni zaidi lakini Tanzania inatoa asali kidogo sana, na Ethiopia wanazalisha tani 40,000 wakati yeye (Pinda) Tanzania inazalisha tani 24,000 tu. 

Nembo hiyo iliyozinduliwa ni ya kampuni ya Nyuki Safari ambayo iko chini ya Mtanzania Kaizirege David Camara na Mmarekani Mary Winzer Canning na lengo lake ni kuboresha bidhaa hiyo ya asli ili kuvutia soko. 
Mhe. Pinda akiangalia Mvinyo (wine), uliotengenezwa na kampuni ya Nyuki safari ikiwa na nembo mpya ya Malkia wa Asali. 
Mhe. Pinda akiungana na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Kuandikwa, (wapili kulia), Mbunge wa Urambo, Mhe. Margareth Sitta, (wakwanza kushoto), Mwanzilishi mwenza na Afisa Mkuu Mbunifu wa kampuni ya kuzalisha asali ya Nyuki Safari, Mary Winzer Canning, (wanne kushoto), na Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Profesa Silayo na mrembo aliyebeba nembo hiyo. 
Mhe. Pinda na wageni wengine wakishiriki kwenye uzinduzi wa nembo hiyo.
Mhe. Pinda wakati akitoa hotuba yake.
Mhe. Pinda katika picha ya pamoja na Waanzilishi wenza wa kampuni ya Nyuki Safari, Bw.Kaizirege David Camara, (kushoto), na Bi. Mary Winzer David Canning.
Bw. Kaizirege akizungumza.
Mhe. Pinda, (katikati), Mama Sitta ba Bi. Mary
Mkurugenzi wa Wilaya ya Chamwino, Bw.Paschal Masatu, akitoa hotuba yake
Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Profesa Silayo, akizungumza.

Balozi Luvanda awasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Sri Lanka

$
0
0
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda aliwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kisoshalisti ya Sri Lanka, Mheshimiwa Maithripala SIRISENA.

Hii ni hatua muhimu katika kuendeleza, kuimarisha na kukuza uhusiano wa kirafiki na ushirikiano mwema uliopo kati ya Tanzania na Sri Lanka ambao ulianza mnamo miaka ya tisini. Wakati huo, Sri Lanka ilikuwa inawakilishwa nchini Tanzania kupitia Ubalozi wake wa mjini Kampala, Uganda ambao baadaye ulifungwa na Tanzania ikiwakilishwa nchini Sri Lanka kupitia Ubalozi wake wa New Delhi. Kwa sasa Sri Lanka inakusudia kumteua Balozi wake mjini Nairobi ambaye pia ataiwakilisha nchi hiyo nchini Tanzania.

Katika hafla hiyo, Balozi Luvanda aliambatana na Mwambata Jeshi wa Tanzania nchini India, Col.Amri Salim MWAMI. Aidha, Balozi Luvanda alifanya mazungumzo na Mkuu wa Itifaki wa Sri Lanka pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Masuala ya Afrika, ambapo ameahidi kushirikiana kwa karibu na watendaji hao katika kudumisha uhusiano uliopo kati ya nchi hizi mbili na ambao utazinufaisha zaidi, hususan katika kuhakikisha uhaulishaji wa uzoefu, teknolojia na utaalam wa Sri Lanka kwa Tanzania kwenye sekta ya viwanda vya nguo, madini na vito mbali mbali na kilimo.

Sri Lanka ni nchi yenye uchumi unaoendelea ingawa imepitia kipindi kigumu cha vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa takriban miaka 25, vita ambavyo vilimalizika mwaka 2009.
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (kushoto) ambaye anawakilisha pia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kisoshalisti ya Sri Lanka akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mheshimiwa Maithripala SIRISENA, Rais wa nchi hiyo
Balozi Luvanda akisalimiana na maafisa waandanizi wa Ikulu ya Sri Lanka
Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda aliwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kisoshalisti ya Sri Lanka, Mheshimiwa Maithripala SIRISENA.

EPZA ,TCCAI KUSHIRIKIANA KATIKA KUHAMASISHA WAZAWA KUWEKEZA

Naibu Waziri akutana na kufanya mazungumzo na Spika EALA

$
0
0
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba na Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Mhe. Martin Ngoga wakisalimiana walipokutana kwa mazumgumzo katika Ofisi za Wizara Dodoma.

Mhe. Ngoga alimtembelea Naibu Waziri Mhe. Dkt. Kolimba Ofisini kwake ambapo walifanya mazungumzo kuhusu masuala mbalimbali ya Jumuiya. Mhe. Dkt.Kolimba katika mazungumzo hayo amemwahidi Spika wa EALA kuwa Wizara na Serikali kwa ujumla itatoa ushirikiano wa hali ya juu kwa Bunge hilo katika utelezaji wa majukumu yake.

Aidha kwa upande wake Spika wa EALA amesema kuwa,kwa sasa wamejipanga vizuri katika kuhakikisha wanadumisha ushirikiano na Mabunge ya Nchi wanachama na kutoa mrejesho kwa Nchi wanachama kuhusu masuala mbalimbali ya yanayojili katika Bunge hilo.

Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki linafanya vikao vyake mjini Dodoma kuanzia tarehe 9 hadi 28 Aprili, 2018 
Spika wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) Mhe. Martin Ngoga akisaini kitabu cha wageni mara baada kuwasili Wizarani Dodoma. 
Naibu Waziri Mhe. Dkt. Kolimba na Spika wa EALA Mhe. Dkt.Ngoga wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge wa EALA na Maafisa kutoka Wizarani na Bunge la EALA

KATIBU MKUU SIHABA NKINGA AFUNGUA KIKO CHA WAFANYAKAZI IDARA KUU MAENDELEO YA JAMII MJINI DODOMA

$
0
0
Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bibi. Sihaba Nkinga akizungumza na watumishi wa Idara Kuu anayoiongoza katika Kikao cha wafanyakazi kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma kilicholenga kukumbushana masuala mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utendaji kazi na huduma kwa wananchi.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bw. Raphael Nombo akifafanua masuala mbalimbalia ya Kiutawala na Kiutumishi kwa watumishi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii katika Kikao cha wafanyakazi kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma kilicholenga kukumbushana masuala mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utendaji kazi na huduma kwa wananchi.
Afisa Utumishi Bi. Daina Lumelezi akieleza yatokanayo na Kikao kilichopita kwa Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii na na watumishi katika Kikao cha wafanyakazi kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma kilicholenga kukumbushana masuala mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utendaji kazi na huduma kwa wananchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango Bi. Sophina Mjangu akiwasilisha Sura ya Bajeti kwa Mwaka 2018/2019 kwa watumishi wa Idara Kuu anayoiongoza katika Kikao cha wafanyakazi kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma kilicholenga kukumbushana masuala mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utendaji kazi na huduma kwa wananchi.
  
Baadhi ya watumishi wakifuatilia kikao kati yao na Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bibi. Sihaba Nkinga (hayupo pichani) kilichofanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma kilicholenga kukumbushana masuala mbalimbali ya kiutendaji ili kuboresha utendaji kazi na huduma kwa wananchi.Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

WILAYA GAIRO YAANZA KILIMO CHA MAZAO YA PAMBA, KOROSHO NA KAHAWA

$
0
0

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven akikagua shamba darasa la Mhe. Mchembe Mkuu wa Wilaya Gairo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven akiongea na wananchi Kijiji cha Kisitwi Gairo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven akikagua kiwanda cha mvinyo itokanayo na ndizi. Kiwanda hicho ni kati ya viwanda vipya 6 vilivyoanzishwa mwaka 2018.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Gairo Mhe. Rahel Nyangasi akiwa kwenye shamba darasa lake la zao la Pamba. 
 
Utekelezaji wa mazao ya kimkakati hasa Pamba msimu wa 2017/2018 kama ilivyoelekezwa na Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa Kassim watekelezwa kwa vitendo wilayani Gairo. 
 
Hayo yameelekezwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Kebwe Steven alipotembelea Wilaya ya Gairo mwanzoni mwa wili iliyopita ili kuhamasisha kilimo cha Pamba ambapo ekari moja ya pamba unapata shilingi milioni 1.4. Alidha Dkt. Kebwe alirudi wilayani Gairo kukagua utekelezaji wa maagizo yake ikiwemo kutembelea mashamba darasa ya viongozi akiwemo Mkuu wa Wilaya Mhe. Siriel Mchembe, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Rahel Nyangasi na Mkurugenzi Mtendaji Bi. Agnes Mkandya. 
 
Mhe. Mchembe alimpa taarifa Mkuu wa Mkoa kuhusu kilimo cha pamba ambapo hekta 181 zimelimwa, pembejeo zimepokelewa ikiwemo mbegu za pamba kilo 3,996 viuadudu mililita 120 na mabomba 10. Mbali na Pamba wilaya ya Gairo wameweza kulima zao la Korosho ekari 2,618 jumla ya miche 70,800 pamoja na zao la kahawa idadi ya miche 800 na mbegu gramu 3,000.
 
 Pamba, Korosho na Kahawa ni mazao ya kimkakati na ya kibiashara hapa wilayani Gairo ambapo mazao hayo yatawainua na wananchi kutoka uchumi wa chini kwenda uchumi wa kati kama ambavyo sera za awamu ya tano za Rais Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa akisisitiza. Mwisho wananchi wa Gairo walimshukuru sana Mkuu wa Mkoa, Dkt. Kebwe Steven kwa kazi kubwa anayofanya kuhamasisha Kilimo cha mazao ya kimkakati Wilaya ya Gairo.

Harmonize Ft Diamond Platnumz - Kwangwaru ( Official Video )

Mafundi Sanifu Wa Barabara Wafundwa Kuhusu Mazingira

$
0
0
Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Julius Chambo akifafanua jambo kwenye hafla ya ufungaji wa Mafunzo ya tathmini na usimamizi wa athari za mazingira katika miradi ya ujenzi wa barabara kwa mafundi sanifu yanayofanyika mkoani Morogoro.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya tathmini na usimamizi wa athari za mazingira katika miradi ya ujenzi wa barabara wakifuatilia hotuba ya ufungaji wa mafunzo hayo iliyotolewa na Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Julius Chambo.
Mhitimu wa mafunzo ya tathmini na usimamizi wa athari za mazingira katika miradi ya ujenzi wa barabara akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Julius Chambo mara baada ya kuhitimu mafunzo hayo.
Mwakilishi wa wahitimu wa mafunzo ya tathmini na usimamizi wa athari za mazingira katika miradi ya ujenzi wa barabara, Bw. Seth Rengia akiwasilisha maoni ya wahitimu wa mafunzo hayo kwa mgeni rasmi.
Mkurugenzi wa Usalama na Mazingira wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Eng. Julius Chambo (wa tatu kulia) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo ya tathmini na usimamizi wa athari za mazingira katika miradi ya ujenzi wa barabara yanayofanyika mkoani Morogoro.

AZAM WAIOMBA TFF WASOGEZA MBELE MECHI YAO DHIDI YA NJOMBE MJI

$
0
0
Na Agness Fracis,Blogu ya Jamii

UONGOZI wa Azam FC umeomba mchezo wao dhidi ya Njombe Mji usogezwa mbele kutokana na muda mchache waliopumzika baada ya kumalizana na Ruvu Shoting ya Mlandizi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Ofisa Habari wa Azam Jaffary Maganga amesema wameomba mchezo kusogezwa mbele ili kupata nafasi ya kujiandaa ikiwa ni jana wametoka ugenini kucheza na timu ya Ruvu shooting.

"Tumeandika barua Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania( TFF) kuomba mchezo dhidi ya Njombe Mji ya mkoani Njombe usogezwe mbele badala ya kuchezwa kesho ikiwa sheria za FIFA zinasema inatakiwa kupumzika saa 72 na si 48,"amesema.

Mchezo huo uliotarajiwa kuchezwa kesho katika dimba la Azam Complex Chamazi.
Ambapo kikosi hicho cha Azam kimerejea jana hiyo hiyo kutoka Mlandizi kuendelea kujifua na mazaoezi kukabilia na Njombe Mji katika mchezo wao ujao.

"Tumerejea jana usiku kutoka Uwanja wa Mabatini Mlandizi tulipomaliza tu mechi na kikosi kipo mazoezini kujiandaa nadhani nnajua Njombe Mji ni timu nzuri pia"amesema Jaffary Maganga.

Azam FC walikubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Ruvu Shoting na kuendelea kubaki nasafi ya 3 wakiwa na alama 45,huku vinara Simba wakiendelea kujikita Kileleni kwa alama 52 na Mabingwa watetezi Yanga wao wakishikilia nafasi ya pili kwa pointi 47,katika msimamo wa Ligi kuu Tanzania Bara.

BANDARI TANGA YAKABIDHI VITANDA 10 VYA KUJIFUNGULIA WAKINA MAMA WAJAWAZITO WILAYANI PANGANI

$
0
0
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimkabidhi vitanda 10 leo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kwa ajili ya kujifungulia wakina mama wajawazito ambavyo vimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) ,ambavyo vinagharimu kiasi cha milioni 12.2.Kushoto anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM).
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimkabidhi vitanda 10 leo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kwa ajili ya kujifungulia wakina mama wajawazito ambavyo vimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) ambavyo vinagharimu kiasi cha milioni 12.2 kushoto anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani .
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimkabidhi vitanda 10 leo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kwa ajili ya kujifungulia wakina mama wajawazito,ambavyo vimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA),vinagharimu kiasi cha shilingi milioni 12.2 .Kulia anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Daudi Mlahangwa 

Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimpongezwa na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso mara baada ya kukabidhi vitanda hivyo katika anayeshughudia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa.

Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa katika akimkabidhi Vitanda 10 vilivyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini TPA kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Daudi Mlahangwa kwa ajili ya wilaya ya Pangani kulia ni Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama akishughudia
Mganga mkuu wa wilaya ya Pangani (DMO) Juma Mfanga kulia akitolea vitanda 10 kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Daudi Mlahangwa vilivyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA)
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akiteta jambo na Mkuu wilaya ya Pangani Zainabu Issa katikati ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso
Sehemu ya vitanda 10 vilivyotolewa na TPA
(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

BANDARI TANGA YAKABIDHI VITANDA 10 VYA KUJIFUNGULIA WAKINA MAMA WAJAWAZITO WILAYANI PANGANI

$
0
0
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimkabidhi vitanda 10 leo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kwa ajili ya kujifungulia wakina mama wajawazito ambavyo vimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) ,ambavyo vinagharimu kiasi cha milioni 12.2.Kushoto anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM).
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimkabidhi vitanda 10 leo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kwa ajili ya kujifungulia wakina mama wajawazito ambavyo vimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA) ambavyo vinagharimu kiasi cha milioni 12.2 kushoto anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani .
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimkabidhi vitanda 10 leo Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah kwa ajili ya kujifungulia wakina mama wajawazito,ambavyo vimetolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA),vinagharimu kiasi cha shilingi milioni 12.2 .Kulia anayeshuhudia ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Daudi Mlahangwa 

Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akimpongezwa na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso mara baada ya kukabidhi vitanda hivyo katika anayeshughudia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa.

Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Issa katika akimkabidhi Vitanda 10 vilivyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini TPA kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Daudi Mlahangwa kwa ajili ya wilaya ya Pangani kulia ni Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama akishughudia
Mganga mkuu wa wilaya ya Pangani (DMO) Juma Mfanga kulia akitolea vitanda 10 kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani,Daudi Mlahangwa vilivyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari nchini (TPA)
Meneja wa Bandari ya Tanga,Percival Salama kushoto akiteta jambo na Mkuu wilaya ya Pangani Zainabu Issa katikati ni Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) Jumaa Aweso
Sehemu ya vitanda 10 vilivyotolewa na TPA
(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

Rais Magufuli Tanya uteuzi wa Majaji wa Mahakama Kuu 10, Naibu AG, Naibu DPP, Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali

SHEREHE ZA WAFANYAKAZI ZA MEI MOSI KITAIFA KUFANYIKA IRINGA

$
0
0
Na Francis Godwin
SHIRIKISHO   la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA) ambao  ni  waandaaji  wa  sherehe  za  wafanyakazi kitaifa  (MEI  MOSI) wamempongeza  Rais  Dkt  John Magufuli kwa  kukubali  mwaliko  wao  wa  kuwa  mgeni  rasmi katika sherehe  za  Mei  Mosi  ambazo mwaka huu zitakazofanyika  kitaifa  mkoani Iringa.
Rais wa shirikisho  la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA)  Tumaini  Vyamhokya alisema  leo  kuwa  katika  sherehe  hizo  za  wafanyakazi duniani kwa  Tanzania  zitafanyika  katika  mkoa  wa  Iringa kwenye  uwanja  wa  Samora  na  kuwa tayari  Rais Dkt  Magufuli  amekubali  kuwa  mgeni  rasmi.  Hivyo  aliwataka  wafanyakazi   kujitokeza  kwa  wingi  kushiriki sherehe  hizo  na  kuwa  kupitia sherehe  hizo  watapata fursa ya  kujua  mikakati ya  serikali  dhidi ya wafanyakazi  nchini japo  hadi  sasa  wanapongeza  hatua  iliyofikiwa na  serikali ya  kuwarejesha  kazini  wafanyakazi  waliokuwa  wamesimamishwa kazi  kutokana na elimu  yao ya  darasa la  saba.
Rais   huyo  alisema  kuwa  TUCTA  imefanya  jitihada  kubwa  za  kukutana na  serikali  kuwapigania  wafanyakazi hao  walioondolewa kazini   kutokana na  elimu   yao na  serikali  imesikiliza  na  imewarejesha  kazini. Alisema  kuwa  serikali  imeendelea  kufanya  jitihada  kubwa  kuongeza ajira  pamoja na  kusikiliza  kero  mbali mbali  za  wafanyakazi na  kuzipatia  majibu. Akielezea  juu ya maandalizi ya  sherehe  za mei  mosi  mkoani  Iringa  alisema  kwa  sehemu  kubwa   maandalizi yanakwenda  vizuri na  wamepata  ratibu ya  kuzunguka  wilaya  zote za  mkoa  wa Iringa kutoa elimu  pamoja na kututana na  wafanyakazi ili  kujua  changamoto  zao. 
 " TUCTA  inapenda  kuishukuru  serikali  ya  mkoa  wa Iringa kwa  kukubali  kupokea maadhimisho  haya  ya  Mei mosi 2018 TUCTA kwa  kushirikiana  na  serikali ya  mkoa wa  Iringa chini ya  mkuu wa  mkoa Amina Masenza pamoja na waziri  wa  nchi ofisi ya  waziri  mkuu  sera ,bunge  ,kazi ,vijana , ajira   na  watu  wenye  ulemavu Jenista Mhagama tumefanya maandalizi ya  kutosha"
Alisema  kabla ya  Mei  mosi  mambo  yakayofanyika  Iringa ni  pamoja na makongamano mawili ya  kimkoa na  moja la kitaifa  na kuwakongamano la kwanza  litafanyika April 23 katika  wilaya ya  Mufindi ambapo mgeni rasmi  atakuwa mkuu wa  wilaya ya Mufindi  Jamhuri  Wiliam wakati  kongamano la  pili  litafanyika  wilaya ya  Kilolo  April 25  na  mgeni  rasmi  ni mkuu wa  wilaya ya  Kilolo Asia Abdalah  huku April 27 litafanyika  kongamano la  kitaifa litakalohusu Tanzania ya  uchumi wa  viwanda kwenye  ukumbi wa  Kichangani ambalo  viongozi mbali mbali  wa  kitaifa  watashiriki. 

Aidha  alisema  kutakuwa na  michezo  ya  Mei  mosi ya fani mbali mbali itakayoanza April 16 hadi  April 30 katika uwanja wa  Samora kuwa  kwa  ajili ya  kuwafanya  wafanyabiashara na  wajasilia mali  kutumia  fursa ya  mei  mosi  Iringa maonyesho  ya  bidhaa mbali  mbali yatafanyika .
Rais  wa  shirikisho  la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA) Tumaini  Vyamhokya kulia  akiwa na  wajumbe  wenzake kwenye kikao hicho cha maandalizi mjini Iringa.




 Rais  wa  shirikisho  la  vyama huru    vya  wafanyakazi Tanzania  (TUCTA) Tumaini  Vyamhokya katikati akiongoza  kuimba  wimbo wa  wafanyakazi  wakati wa  kikao  na  waandishi wa habari mkoa  wa  Iringa kuelezea maandalizi ya  Mei  Mosi  kitaifa  yatakayofanyika  mkoani Iringa
Mkuu  wa  wilaya ya  Iringa  Richard Kasesela kulia  akiwapongeza  viongozi wa  shirikisho  la  vyama  vya  wafanyakazi
Wajumbe  wa TUCTA  wakiimba  wimbo  wa  wafanyakazi  leo
Wimbo   wa  kuwaunganisha  wafanyakazi

Makamu wa Rais kumwakilisha Rais DKt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Wakuu wa Serikali wa Jumuiya ya Madola (CHOGM) London

$
0
0
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameondoka nchini jana kwenda London, Uingereza kushiriki kwenye Mkutano wa Wakuu wa Serikali wa Jumuiya ya Madola (CHOGM) unaotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 16 hadi 20 Aprili, mwaka huu akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Mkutano huo ambao Kaulimbiu yake ni “Kuelekea Mustakabali wa Pamoja” utafanyika chini ya Uenyekiti wa Waziri Mkuu wa Uingereza, Mheshimiwa Theresa May na utafunguliwa na Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Malkia Elizabeth wa Pili wa Uingereza.
Majadiliano ya Mkutano wa CHOGM 2018 yatajikita kwenye maeneo manne makuu ya kipaumbele ambayo yatajadili namna Jumuiya ya Madola inaweza kufikia mustakabali wenye ustawi zaidi; mustakabali endelevu zaidi; mustakabali wenye haki zaidi; na mustakabali wenye usawa zaidi.
Mijadala katika maeneo hayo ya kipaumbele itahusisha masuala mbalimbali ikiwemo, kukuza zaidi biashara na uwekezaji baina ya nchi za Jumuiya ya Madola kwa manufaa ya nchi wanachama na Jumuiya nzima; kukuza na kuendeleza misingi ya demokrasia; ajenda ya mabadiliko ya tabia nchi na maendeleo endelevu pamoja na masuala ya uhalifu wa kimataifa kama vile ugaidi, uhalifu wa kimtandao na usafirishaji wa binadamu.
Jumuiya ya Madola ilianzishwa mwaka 1949 kupitia Tamko la London ambalo lilikuwa ni matokeo ya Mkutano wa Mawaziri Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Madola.  Jumuiya ya Madola ina wanachama 53 ambapo kati ya hizo, nchi 19 ni za Afrika, 7 ni kutoka Asia, 13 ni kutoka nchi za Carribean na Mabara ya Amerika, 11 ni kutoka eneo la Pacific na nchi 3 ni kutoka Ulaya.
Ujumbe wa Makamu wa Rais unajumuisha Mheshimiwa Dkt. Balozi Augustine Mahiga (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na viongozi wengine waandamizi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki.
Makamu wa Rais na ujumbe wake wanatarajia kurejea nchini Aprili 22, mwaka huu.
Imetolewa na:
Ofisi ya Makamu wa Rais
Dar es salaam
15/4/2018
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images