Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

WAZIRI MKUU: VIWANDA 3,306 VYAANZISHWA NCHINI

$
0
0
 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano imetekeleza kaulimbiu yake ya kujenga uchumi unaotegemea viwanda na kwamba hadi kufikia Februari 2018, viwanda vipya 3,306 vimekwishaanzishwa nchini.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Aprili 4, 2018) Bungeni mjini Dodoma, wakati akiwasilisha taarifa ya mapitio ya utekelezaji wa kazi za Serikali kwa mwaka 2017/2018 na mwelekeo wa kazi za Serikali kwa mwaka 2018/2019 kwenye mkutano wa 11 wa Bunge.

Amesema Serikali inahamasisha uwekezaji katika viwanda kwa kutoa vivutio vya kodi na visivyo vya kodi kwa wawekezaji mahiri (strategic investors); kuendeleza na kuboresha miundombimu wezeshi kama vile barabara, reli, bandari, umeme na maji. “Serikali itaendelea kuhuisha sera, sheria na kanuni pamoja na kufuatilia utendaji wa viwanda vilivyobinafsishwa na kuchukua hatua stahiki kwa wamiliki walioenda kinyume na mikataba ya mauzo,” amesema. 

Waziri Mkuu amelieleza Bunge kwamba mikoa na Halmashauri zote nchini zimeelekezwa kutenga maeneo ya uwekezaji kwa ajili ya viwanda na kwamba katika mwaka 2018/2019, Serikali itatoa kipaumbele katika kutekeleza miradi ya kielelezo, uanzishwaji wa kanda maalum za kiuchumi pamoja na kuboresha mazingira ya biashara na kuvutia uwekezaji katika sekta ya viwanda. 

Akitoa ufafanuzi kuhusu ushiriki wa sekta ya hifadhi ya jamii kwenye ujenzi wa uchumi wa viwanda, Waziri Mkuu amesema pamoja na miradi mingine NSSF na PPF kwa kushirikiana na Jeshi la Magereza wanatekeleza mradi mkubwa wa uzalishaji wa sukari mkoani Morogoro. 

“Lengo la mradi huo ni kuzalisha tani 250,000 za sukari na umeme megawati 40. Mradi huo unatekelezwa katika shamba la Mkulazi lililopo Ngerengere lenye ukubwa wa hekta 63,000 na shamba la gereza la Mbigiri lenye ukubwa wa ekari 12,000 lililopo Dakawa,” alisema. 

“Hadi sasa ekari 2,000 za mashamba ya miwa zimetayarishwa katika eneo la Mkulazi na ekari 1,100 zimepandwa miwa. Lengo la Serikali ni kukamilisha awamu ya kwanza ya ufungaji wa mitambo ya kiwanda cha Mbigiri ifikapo mwezi Desemba, 2018 ili uzalishaji uanze mwaka 2019,” alisema na kuongeza kuwa miradi hiyo itakapokamilika, itazalisha zaidi ya ajira 100,000. 

Waziri Mkuu alisema tangu kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo Juni 2017, ajira za moja kwa moja 780 na ajira zisizo za moja kwa moja  24,000 ikijumuisha wakulima wadogo wa mbegu na kilimo cha nje zimezalishwa.

Akifafanua kuhusu ujenzi wa barabara kuu, Waziri Mkuu alisema Serikali inaendelea kuboresha mtandao wa barabara nchini ambapo katika kipindi cha Julai 2017 hadi Februari 2018, ujenzi wa Km. 776.45 za barabara kuu kwa kiwango cha lami umekamilika na Km. 1,760 zinaendelea kujengwa. Pia barabara zenye urefu wa Km. 17,054 zilikarabatiwa katika kipindi hicho.

Kuhusu ujenzi wa madaraja, Waziri Mkuu alisema madaraja ya Kilombero na Kavuu ujenzi wake umekamilika na kwamba ujenzi unaoendelea hivi sasa ni wa madaraja ya Sibiti, Mto Mara, Lukuledi, Ruhuhu, Momba na Mlalakuwa. Alisema madaraja mengine 996 katika maeneo mbalimbali nchini yamekarabatiwa.

Kuhusu jitihada za Serikali kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es Salaam, Waziri Mkuu alisema hadi kufikia Februari 2018, ujenzi wa barabara ya juu katika eneo la TAZARA ulikuwa umefikia asilimia 70 na ujenzi wa barabara za juu katika makutano ya Ubungo (Ubungo Interchange) umeanza. 

“Maandalizi ya awamu ya pili hadi ya nne ya mradi wa ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka yanaendelea. Katika mwaka 2018/2019, Serikali imepanga kujenga kilometa 597 za barabara kuu na za mikoa kwa kiwango cha lami na kilometa 72 za kiwango cha lami zitakarabatiwa,” alisema. 

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kuliarifu Bunge juu ya uanzishwaji wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tanzania Rural and Urban Roads Agency – TARURA) kwa lengo la kurahisisha huduma za usafirishaji na kuongeza kasi ya wananchi kujiletea maendeleo. 

Alisema TARURA imepewa jukumu la kusimamia ujenzi na matengenezo ya mtandao wa barabara zenye urefu wa kilometa 108,946.2 za vijijini na mijini. “Katika mwaka 2017/2018, TARURA imesimamia matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilomita 4,183.3, madaraja 35, makalavati makubwa 43 na madogo 364 na drift nne,” alisema.

Waziri Mkuu aliliomba Bunge likubali kupitisha sh. 143,618,762,698 zikiwa ni makadirio ya mapato na matumizi ya fedha ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zilizopo chini yake pamoja na Mfuko wa Bunge kwa mwaka 2018/2019 ambapo sh. 74,527,321,698 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. 69,091,441,000 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo. 

Vilevile, Waziri Mkuu aliliomba Bunge liidhinishe sh. 125,521,100,000 kwa ajili ya Mfuko wa Bunge ambapo sh. 117,205,487,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida na sh. 8,315,613,000 ni kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
JUMATANO, APRILI 4, 2018

Gawio la Airtel Money kwa wateja lafikia bilioni 14.8,

$
0
0
Airtel Tanzania imetoa gawio linalofikia shilingi bilioni 14.8 hadi sasa kwa wateja wake na mawakala nchi nzima ikiwa ni sehemu ya faida waliyoipata tangu mwaka 2015. 

Hili limebainishwa na Mkurugenzi wa masoko wa Airtel Tanzania, Isack Nchunda kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Airtel wakati akitangaza gawio la robo hii ambalo ni shilingi bilioni 1.8. 

“Tangu tuanze kugawa sehemu ya faida yetu kwa wateja mwaka 2015, tumeshatoa jumla ya shilingi bilioni 14.8 na huwa tunagawa kila robo ya mwaka na kuhakikisha wateja na mawakala wanapokea fedha hizi kupitia akaunti zao za Airtel Money na wana uhuru wa kutumia fedha hizi wanavyotaka,” alisema. 

Kwa mujibu wa Nchunda, hii ni mara ya sita mfulululizo kwa Airtel Tanzania kugawa sehemu ya faida kwa wateja wake tangu mwaka 2015. “Bwana Pesa hutoa gawio hili kwa wateja wa Airtel Money na mawakala kulingana na salio la mteja kila siku,” aliongeza. Aliwashukuru wateja wa Airtel kwa kuendelea kutumia Airtel Money na kuifanya iwe huduma yenye tija na maarufu zaidi na kuongeza kuwa hadi sasa wana zaidi ya maduka 100 maalum kwa kutoa huduma ya Airtel Money ambayo yanafanya huduma hii iwe ya kuaminika zaidi na rahisi kupatikana. 

“Maduka haya ya Airtel Money huhakikisha mawakala wana salio la kutosha muda wote ili wateja wasipate usumbufu wanapohitaji huduma hiyo,” alisema. Kwa upande wake, Meneja wa Airtel Money, alisema kuanzia leo, wateja wa Airtel Money na mawakala watapata gawio linalofikia shilingi bilioni 1.8 kupitia akaunti zao za Airtel Money na wanaweza kutumia gedha hizo wanavyotaka ikiwemo kulipia huduma mbalimbali kama vifurushi vya mtandao, muda wa maongezi na LUKU. 

Alitoa wito kwa mawakala wa Airtel Money kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma bora kwa wateja ili kampuni hiyo iendelee kutoa gawio kwa wateja wake kila robo ya mwaka. “Airtel Money imejizatiti kuendelea kutoa huduma  bora na nafuu ambayo ni suluhisho kwa biashara za aina yoyote,” alisema na kuongeza kuwa Airtel inashirikiana na biashara zaidi ya 400 na ziadi na benki 30 katika kutoa huduma za kifedha. 

Airtel ina zaidi ya mawakala 50,000 nchi nzima na inaendelea kutanua wigowake ili kuhakikisha huduma za kifedha zinapatikana katika miji na vijijini.

JUMUIYA YA UMOJA WA WAZAZI TANZANIA MKOA WA DAR ES SALAAM, YAADHIMISHA KWA KISHINDO MIAKA 63 YA KUANZISHWA KWA UMOJA HUO

$
0
0
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akimkabidhi Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) Cheti cha Skurani kutoka Umoja huo Wilaya ya Kigamboni kutambua mchango mkubwa wa hali na mali ambao amekuwa akiutoa kwa jumuiya hiyo, wakati wa Kongamano la Maadhimisho ya miaka 63 ya Umoja wa Wazazi Tanzania, lililoandaliwa na Umoja huo mkoa wa Dar es Salaam, katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, leo 
MWANZO⤋
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akishuka katika gari lake baada ya kuwasili kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, kuadhimisha miaka 63 ya kuzaliwa Umoja wa Wazazi Tanzania.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akikaribishwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Kate Kamba baada ya kuwasili eneo la Ukumbi wa wa Mikutan wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere. Kulia ni Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Lugano Mwafongo
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akisalimiana na Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam, Lugano Mwafongo baada ya kuwasili eneo la Ukumbi wa wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akisindikizwa na viongozi kwenda ukumbini baada ya kuwasili eneo la Ukumbi wa mikutano wa mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe, na kutoka kulia ni Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi mkoa huo Lugano Mwafongo na Mwenyekiti wa CCM mkoa huo Kate Kamba 
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akipata maelezo ya awali kutoka kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam Frank Kamugisha baada ya kuwasili katika chumba cha Wageni maarufu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam, Lugano Mwafongo (kushoto) akiwa na Katibu wa CCM mkoa huo Saad Kusilawe wakati wa mazungumzo hayo.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akiwaunga mkono wajumbe waliokuwa wakimshangilia baada ya kuwasili ukumbini kwenye Kongamano la miaka 63 ya kuzaliwa kwa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam, yaliyoandaiwa na Umoja huo mkoa wa Dar es Salaam. Kulia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa dar es Salaam Frank Kamugisha.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akiwa na viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam, tayari kushiriki kongamano hilo
 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Mwinyimkuu Sangaraza akifungua pazia la kongamano hilo kwa kufanya utambulisho
 "Jamani sare maalum ya sherehe hizi ilichelewa kidooogo, lakini ninayo imeshafika hii hapa" akasema Sangaraza na kuwaacha wajumbe na mgeni rasmi wakicheka
 Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala akisalimia baada ya kutambulishwa
 Wajumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Jumuiya ya umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam wakisalimia baada ya ktambulishwa. Kutoka Kushoto ni Katibu wa Uchumi na Fedha habib Nasser, Mwafongo na Kamugisha
 Wazee wa Jumuiya ya Umoja wa wazazi mkoa wa Dar es Salaam (mstari wa mbele) wakiwa kwenye kongamano hilo
 Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam, Lugano Mwafongo akizungumza kwenye kongamano hilo.
 Wajumbe wakimshangilia Mwanfongo wakati akifanya utambulisho
 Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Jumiya ya Umoja huo Mzee Mkali akisalimia baada ya kutambulishwa
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Frank Kamugisha akitoa nafasi ya kufanywa dua na maombi kabla ya kongamano kuanza rasmi
 Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Sheik Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) akiomba dua kabla ya kongamano kuanza
 Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Sheik Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) akiomba dua kabla ya kongamano kuanza
 Wajumbe wakipokea dua ya Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Sheik Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) kabla ya kongamano kuanza
 Katibu wa Elimu, Malezi na Mazingira wa Jumiya ya Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Wilson Tobola akisoma maombi kabla ya kongamano hilo kuanza
 Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Lugano Mwafongo akisoma taarifa ya maadhimisho ya miaka 63 ya Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania wakati wa Kongamano hilo
 Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Lugano Mwafongo akimkabdhi taarifa hiyo Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo baada ya kuisoma
 Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam Beatrice Mandia akizungumzia maadili wakati wa kongamano hilo
 Katibu wa Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam Habib Nasser akitangaza Wajumbe wa Baraza la Uchumi na fedha kwenye kongamano hilo  
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana mkoa wa Dar es Salaam akisalimia  
 Mjumbe wa Baraza la Utekelezaji la Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam ndugu Busolo akizungumza kwenye kongamano hilo 
 Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania mkoa wa Dar es Salaam, Mzee Mkali akizungumza kwenye kongamano hilo
 Vijana wa Vyombo vya Habari vya CCM Jumanne Gude wa Gazeti la Uhuru na mwenzake kutoka Uhuru FM wakiwa makini wakati wakichukua taarifa kwenye kongamano hilo
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Kate kamba akizungumza  katika kongamano hilo
 Mwenyekiti wa Jumuiya wa Umoja wa Wazazi mkoa wa Dar es Salaam Frank Kamugisha akimkaribisha mgeni rasmi kuzungumza kwenye kongamano hilo
 Baadhi ya wajumbe ukumbini
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akizungumza na wajumbe wakati wa kongamano hilo
 Baadhi ya wajumbe ukumbini
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akimkabidhi Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) Cheti cha Skurani kutoka Jumuiya ya Umoja huo Wilaya ya Kigamboni kutambua mchango mkubwa wa hali na mali ambao amekuwa akiutoa kwa jumuiya hiyo, wakati wa Kongamano hilo.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akimkabidhi Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) Cheti cha pongezi kutoka Jumuiya ya Umoja huo mkoa wa Dar es Salaam, wakati wa kongamano hilo
 Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba) akifurahia baada ya kupewa Cheti cha Skurani kutoka Jumuiya ya Umoja huo Wilaya ya Kigamboni kutambua mchango mkubwa wa hali na mali ambao amekuwa akiutoa kwa jumuiya hiyo. 
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akimkabidhi Doto Msawa Cheti cha Skurani kutoka Jumuiya ya Umoja huo Wilaya ya Kigamboni kutambua mchango mkubwa wa hali na mali ambao amekuwa akiutoa kwa jumuiya hiyo
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akiendelea kukabidhi tuzo za shukrani na pongezi kwa viongozi mbalimbali
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akiendelea kukabidhi tuzo za shukrani na pongezi kwa viongozi mbalimbali
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akiendelea kukabidhi tuzo za shukrani na pongezi kwa viongozi mbalimbali, anayekabidhiwa ni katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akiendelea kukabidhi tuzo za shukrani na pongezi kwa viongozi mbalimbali, Anayekabidhiwa ni Ndugu Busoro
 Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam akimpongeza Busoro
 Frank Nkinda (kulia) ambaye ni Msaidizi wa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akiwa ukumbini
 Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe akizungumza kutoa neno la shukurani mwishoni mwa kongamano hilo
PICHA ZA PAMOJA⇩


 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo akiagana na wajumbe baada ya kongamano hilo
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Rodrick Mpogolo  akiagana na Mjumbe wa Kamati ya Uchumi na Fedha wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tanzania, mkoa wa Dar es Salaam, Abdulkadir Sharif (Scaba Scuba)  mwishoni mwa kongamano hilo.
Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Saad Kusilawe (kushoto) akiondoka ukumbini mwishoni mwa kongamano hilo la Maadhimisho ya miaka 63 ya kuanzishwa kwa  Umoja wa Wazazi Tanzania, lilioandaliwa na Jumuiya ya Umoja huo mkoa wa Dar es Salaam. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

KONGAMANO LA MAADHIMISHO YA MIAKA 63 YA JUMUIYA YA WAZAZI TANZANIA

$
0
0
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini .

KAMPUNI ya Kilimanjaro SAR ya mkoani Kilimanjaro imeanza rasmi shughuli za utafutaji na uokoaji kwa wapandaji wa Milima miwili ya Kilimanjaro na Meru kwa kutumia ndege aina ya Helkopta. 

Kilimanjaro SAR inakua kampuni ya kwanza kuweka historia katika bara la Afrika ya utoaji wa huduma hiyo muhimu na maada kwa maisha ya wapandaji wa Milima ikizingatiwa asilimia 75 ya magonjwa uwapo mlimani yanatokana na mbadiliko ya Hali ya Hewa kulingana na urefu wa Mlima.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Afisa mtendaji mkuu wa Kampuni ya Kilimanjaro SAR,Ivan Braun raia wa Denmark ameeleza kuwa kuanza kwa shughuli hiyo kutasaidia aliyepata matatizo akiwa mlimani kuhudumiwa ndani ya dakika 5 baada ya kupokea simu ya hitaji la msaada.

“Kampuni hii itatoa huduma kamili ya uokoaji wa dharura kwa wapanda Mlima,Takwimu zinaonyesha zaidi ya watalii 45,000 hutamani kupanda kilele cha mlima mrefu Africa, kwa bahati mbaya hofu juu ya usalama wa maisha yao imekua kizuizi kwao kutimiza ndoto hii.”imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

“Mabadiliko chanya sasa yamepatikana kutoka katika huduma za uokoaji zisizo na ufanisi mpaka zenye ubora wa hali ya juu.”alieleza Braun ambaye ni mtaalamu wa kupanda Milima.Alisema mbali na kuwa na Helikopta bora na zenye uwezo wa juu maalumu kwa huduma hiyo ya utafutaji na uokoaji pia ina timu maalumu ya madaktari wa kimataifa na wasaidizi wa kliniki.

“Kampuni hii inaleta usalama katika maana pana zaidi kwa kuanzisha kliniki ya kwanza Afrika maalumu kwa matibabu ya magonjwa yatokanayo na mlima.Kampuni ya Kilimanjaro SAR itahakikisha inaifanya Kilimanjaro kuwa sehemu salama zaidi ya utalii Africa.”alisema Braun.

Kuanza kwa utolewaji wa huduma hiyo kutasaidia sekta ya Utalii nchini kupata suluhu ya Changamoto ya muda mrefu ya utoaji wa msaada wa kitabibu, utafutaji na uokoaji wa wageni wanaopata matatizo wakati wa kupanda Mlima Kilimanjaro na Meru .

Hivi karibuni kampuni ya Kilimanjaro SAR iliingia makubaliano na Hospitali ya St Joseph ya mjini Moshi kuanza kutoa huduma za kitabibu kwa wagonjwa watakao pata matatizo wakati wa kupanda Milima hiyo zoezi lililoenda sambamba na uzinduzi wa Kliniki ya kwanza Afrika ya magonjwa yatokanayo na muinuko wa juu.Katika uzinduzi huo mgeni rasmi ,Mkuu wa wilaya ya Moshi ,Kippi Warioba alisema hii ni fursa mpya kwa sekta ya Utalii kuutangaza vyema Mlima Kilimanjaro kwamba kwa kiasi kikubwa itasaidia katika kuongeza idadi ya Watalii. 

Hata hivyo kuanza kwa huduma hiyo muhimu kwa sekta ya Utalii nchini ,bado ipo changamoto ya matumizi ya uwanja mdogo wa ndege wa Moshi hali inayowalazimu kutumia uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA).
Moja ya ndege aina ya Helkopta ilipowasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya utoaji wa Huduma ya Utafutaji na uokoaji kwa wapanda Milima
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Kilimanjaro SAR ya mkoani Kilimanjaro Ivan Broun akionekana mwenye tabasamu mara baada ya moja ya ndege aina ya Helkopta kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) kwa ajili ya utoaji wa Huduma ya Utafutaji na uokoaji kwa wapanda Milima.

Mwalimu Rufiji ashinda pasaka mzuka jackpot ya milioni 260.

$
0
0



Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akizungumza na wanahabari  mapema leo jijini Dar wakati wa kumtambulisha mshindi
Pasaka Mzuka Jackpot Edward Msenga (Kulia) na kumpongeza kwa ushindi mkubwa wa kujishindia kiasi cha Shiling Milion 260. Kushoto ni Mkaguzi kutoka michezo ya Bahati Nasibu  Bakari Maggid.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga  akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 260 kwa
mshindi wa Pasaka Mzuka Jackpot Edward Msenga .

Mshindi wa
Pasaka Mzuka Jackpot Edward Msengi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kutambulishwa na kushukuru kwa kupata fedha hizo na kuwataka watanzania waamini kuwa mchezo huo unatenda haki.


Tatu Mzuka, mchezo wa namba unaoongoza nchini leo umetangaza na kumtambulisha kwa wana habari mtanzania aliyebahatika kushinda milioni 260 kwenye Pasaka Mzuka Jackpot ambayo ilionyeshwa mubashara kupitia ITV, Clouds TV na TV 1 jumapili ya Pasaka.

Edward Msengi (56), ambaye anatokea Rufiji, Pwani ndiye aliyebahatika kuondoka na kitita cha shilingi milioni 260 ambayo ni jackpot kubwa kuwahi kutolewa kwa mshindi mmoja katika nchi hii.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Bwana Sebastian Maganga alimtambulisha mshindi na kumpongeza kwa ushindi huo mkubwa. “ Sisi Tatu Mzuka tunayo furaha kiasi kwamba tumeamua kumleta mshindi Dar es salaam ili kushiriki pamoja nanyi katika tukio hili kubwa” . Msengi ambaye ni mzaliwa wa mkoa wa Singida na baba wa watoto wanne alikuwepo kudhihirisha furaha yake na kuhadithia safari yake aliyopitia mpaka kushinda kitita kikubwa cha milioni 260.

“ Nimekuwa nikicheza Tatu Mzuka kwa muda sasa. Nina furaha kubwa sana. Sikuwahi hata kuota kama ningeweza kupata fursa kubwa kama hii. Ninategemea kujenga nyumba nzuri kwa ajili ya familia yangu na kuwekeza katika biashara pamoja na kuhakikisha kwamba watoto wangu wote wapo katika shule nzuri” alisema Bwana Msengi
 
Mbali ya tukio hilo adhim,Maganga aliufahamisha umma juu ya ujio wa  kampeni ya mwezi April ijulikanayo kama Mzuka FULL CHARGE.

“Maisha ni kusaidiana ndio maana unaposhinda Tatu Mzuka na kuwa ‘FULLCHARGE’; tunakupa fursa ya kumbusti mtu mwingine ambaye utamchagua. Shinda milioni 6 kila saa na upate nafasi ya kuingia kwenye jackpot ya milioni 10 kila siku na milioni 60 jumapili hii ili umbusti yoyote unayemtaka”

Rais Magufuli atuma salamu za rambirambi kufuatia vifo vya watu 12 katika ajali huko Igunga Tabora

DC JOSEPH MKIRIKITI “WAKURUGENZI SIMAMIENI MATUMIZI YA FEDHA ZA MISITU”

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa,Joseph Mkirikiti, amewataka Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Mkoa wa Lindi kusimamia na kuhakikisha Maafisa Misitu wanaandaa mpango kazi na kuwasilisha taarifa ya matumizi ya fedha ambazo wamepokea na kuzifanyia kazi kutoka kwa Mfuko wa Misitu Tanzania( TaFF). 

Mkirikiti amesema hatua hiyo itaziwezesha Halmashauri kurejeshewa fedha kwaajili ya utekelezaji wa shughuli za upandaji miti kwa mwaka wa fedha 2017/2018. 

” Fedha hizo zinazopaswa kurejeshwa katika Halmashauri ni zinazotoka na wafanyabiashara wa mazao ya misitu ambapo wanapaswa kulipa tozo ya asilimia 5 ya makusanyo kutoka misitu ya asili kwa ajili ya kugharamia shughuli ya upandaji miti Wilayani” amesema Mkirikiti. 

Ameongeza kuwa kwa mujibu wa muongozo huo wa uvunaji na biashara ya mazao ya misitu, tozo ya asilimia tano ya fedha za upandaji miti inatozwa kwenye mazao ya misitu kama vile kuni, mkaa, magogo, na nguzo.

“Kuna fedha ambazo zinapaswa kurudishwa katika halmashauri zetu kwa ajili ya kuratibu shughuli hizi ila watu mnaohusika mnafanya uzembe wa kutokutekeleza majukumu yenu ,Wakurugenzi msiwafumbie macho hawa watu wanaotaka kuturudisha nyuma, Kila mtumishi wa serikali azingatie majukumu yake na hakikisheni hizo fedha kwa Halmashauri ambazo hamjazipata watu wenu wawasilishe vitu vinavyotakiwa ili zipatikane” amesema Mkirikiti.

Naye Mtendaji wa mradi Usimamizi Shirika rasimali za uvuvi Thomas Chale amesema shirika la Uhifadhi wa Mazingira Duniani (WWF), watashirikiana na viongozi kuhakikisha mazingira ya Mkoa wa Lindi na Wilaya zake yanatunzwa kama inavyopaswa. 
Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa,Joseph Mkirikiti akishiriki katika zoezi la kupanda Miti

Rais Magufuli kuzindua Nyumba za Polisi Arusha ,April 7

$
0
0
Na.Vero Ignatus ,Arusha.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pohn Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa nyumba za polisi na vituo vya polisi Jijini Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi jijini hapa DCP Charles Mkumbo amesema kuwa kutakuwa na uzinduzi wa vituo viwili cha Utalii na Diplomasia na kingine ni Kituo cha daraja la kati kilichopo Murieti Jijini Arusha.

Kamanda Mkumbo amesema kuwa kutakuwepo pia na maonyesho mbalimbali ya  Jeshi la Polisi linavyofanya kazi za kuwahudumia wananchi ambapo maonesho hayo yatafanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid .

Amewataka wananchi kutokuwa na hofu kwani hali ya usalama Jijini hapa umeimarishwa na amewaomba wajitokeze kwa wingi katika sherehe hizo.
Kituo chaPolisi cha Utalii na Diplomasia kinachotarajiwa kuzinduliwa April 7 Jijini Arusha.Picha na Vero Ignatus Blog.

Baadhi ya Nyumba za Polisi zinazotarajiwa kuzinduliwa na Mh.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Magufuli

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yazindua ugawaji endelevu wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu

$
0
0
Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe Hamad Rashid leo amezindua ugawaji endelevu wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu kwa jamii hapa Zanzibar. 

‘Leo kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, tunayo furaha kubwa kutangaza ugawaji wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu kwa kila mama mjamzito ambaye ataudhuria kliniki kwa mara ya kwanza na watoto wanaopata chanjo ya surua. Vile vile kila Mzanzibari ataweza kupokea chandarua kutoka kituo cha afya kwa kutumia koponi ambayo ataipata kutoka kwa mjumbe wa sheha,’ alisema Hamad Rashid.

Kampeni Endelevu ya ugawaji vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu una lengo la kufanya upatikanaji kwa rahisi vyandarua kupitia vituo vya afya. Ugawaji endelevu wa vyandarua ni mradi unaoendeshwa kwa pamoja na shirika la Johns Hopkins Center for Communication kupitia mradi wa VectorWorks kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani – USAID .
,
kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria na kuratibiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Kitengo cha kumaliza Malaria Zanzibar - ZAMEP . ‘Serikali inatoa shukrani kwa washirika wa Maendeleo ya afya, Watu wa Marekani, Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya WHO, Global Fund na wengine wote, aliongeza Mh Rashid.

‘Zanzibar imedhamiria kumaliza ugonjwa wa malaria kwa kusambaza vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu jambo ambalo litafanya upatikanaji wake kuwa rahisi. Upatikanaji kwa urahisi wa vyandarua ni hatua moja muhimu kwenye kupambana na ugonjwa wa malaria’, alisema Mhe Rashid akiongeza kuwa kupitia mradi huu unaozinduliwa leo, kila mama mjamzito na watoto wenye umri wa mwaka mmoja watapata vyandarua bila Malipo yoyote. Vile vile alitoa wito kwa kila Mzanzibari kubadailisha chandarua chake cha zamani kwa kupata kopuni kutoka kwa Shehia kisha kutembelea kituo chochote cha Afya kupata chandarua.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miradi kutoka VectorWorks Waziri Nyoni alisema ‘Tunayo furaha kufanya kazi pamoja na Kitengo cha kumaliza Malaria Zanzibar - ZAMEP kuendesha programu hii yenye lengo la kumaliza malaria Zanzibar. Ugawaji wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu pamoja na koponi unaendeshwa na kitengo cha Serikali cha kusambaza vifaa tiba pamoja, Zanzibar Central Medical Store (CMS). 

Kupitia mfumo huo, vyandarua na koponi zitakuwa zikipelekwa kwenye vituo vya afya na CMS, huku Mfumo wa Taarifa ukihusisha vitengo vingine vya afya kupitia HMIS, alisema Nyoni. Nyoni aliongeza kuwa VectorWorks pamoja na ZAMEP, HMIS, CMS wameandaa utaratibu ambao unahakikisha kila chandarua na kuponi inahesabiwa.

Leo tunasherekea hatua nyingine muhimu kwenye historia ya kumaliza malaria Zanzibar kwa kuzindua ugawaji endelevu wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu kwa kila mama mjamzito na mtoto wenye umri wa mwaka mmoja wa kupata bure chandarua pamoja na kila Mzanzibari. Vyandarua hivi vitawapa usingizi mzuri lakini pia muhimu ni kinga dhidi ya malaria, aliongeza Nyoni.

Haya ni mafanikio makubwa kwa Zanzibar, alisema Mhe Rashid. ‘Tumepiga hatua kubwa dhidi ya mapambano na malaria kwa miaka mitano iliyopita. Tumeweza kupunguza ugonjwa wa malaria kuwa chini ya Asilimia moja. Lengo letu kama serikali kuendeleza juhudi hizi, na kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na washiriki wetu kwenye Maendeleo ya afya, malaria inaweza kuwa sio tishio kabisa kwa Zanzibar’, alisema Mhe Rashid.

Ugawaji wa vyandarua vyenye dawa ya muda unaongozwa na Wizara ya Afya Zanzibar kupitia Central Medical Stores, Kitengo cha kumaliza malaria Zanzibar (ZAMEP), Sekta ya afya ya uzazi na kitengo cha usimamizi wa taarifa. Kampeini imefadhiliwa na Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria. Uratibu wa kitaalam wa programu hii unafanywa na mradi wa VectorWorks. 

VectorWorks ni mradi wa miaka mitano (2014-2019) wenye lengo kuongeza upatikanaji wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu na vidhiti vingine vya malaria. VectorWorks inaongwa na Johns Hopkins Center for Communication Programs –CCP. Washirika wa mradi ni pamoja na PSI Tanzania, Tropical Health na chuo kikuu cha Tulane.

Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid akiongea na waandishi wa habari jana Zanzibar baada ya kuzindua ugawaji endelevu wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu ikiwa ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kupambana na ugonjwa wa Malaria chini ya ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria. 
Waziri wa Afya wa Zanzibar Hamad Rashid akiongea na waandishi wa habari jana Zanzibar baada ya kuzindua ugawaji endelevu wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu ikiwa ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kupambana na ugonjwa wa Malaria chini ya ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria. 
Naibu Meneja wa Kitengo cha Kupambana na Malaria Zanzibar Faiza Bwanaheri akiongea na waandishi wa habari leo Zanzibar baada ya kuzindua ugawaji endelevu wa vyandarua vyenye dawa ya muda mrefu ikiwa ni juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuendelea kupambana na ugonjwa wa Malaria chini ya ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani – USAID kupitia Mfuko wa Raisi wa Marekani wa kudhibiti malaria. Kushoto ni Mkurugenzi wa Miradi kutoka VectorWorks Waziri Nyoni.

URAFIKI WA TANZANIA,CHINA NI WA DAMU,LAZIMA UDUMISHWE NA KULINDWA-BALOZI MAHIGA

$
0
0
*Balozi wa Wang Ke aongoza Jumuiya ya marafiki wa China ,Tanzania kuwakumbuka waliopoteza maisha wakati wa ujenzi wa reli ya Tazara


Na Said Mwishehe,Globu ya jamii


 SERIKALI ya Tanzania imeungana na Jamhuri ya Watu wa China katika kumbukumbu ya vifo vya Wachina 70 waliofarika wakati wa ujenzi wa reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA).

Watanzania waliongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Kikanda na Afrika Mashariki, Balozi Dk. Augustino Mahiga huku ikiwakilishwa na Balozi wao nchini, Wang Ke. Kumbukumbu hiyo, imeandaliwa na Jumuia ya Marafiki wa Tanzania na China ambayo Mwenyekiti wake Dk.Salim Salim na Katibu wake ni Joseph Kahama.

Kabla ya kuweka mashada kwenye makaburi kwenye makaburi ya wachina hao ambao wengi wao ni wataalamu na wahandisi katika ujenzi wa reli, ilitolewa historia fupi ya vifo vyao.

Akizungumza baada ya kuweka mashada, Balozi Mahiga alisema ujenzi wa reli hiyo ulithibitisha urafiki wa kutoka moyoni kati ya nchi hizo mbili na kufafanua ujenzi wake ulifungua milango kwa China kujenga viwanda vingine kama UFI na Kiwanda cha Nguo cha Urafiki.

"Wakati wa ujenzi huu damu zilimwagika, wachina wamepoteza maisha na wengine wamebaki na ulemavu wa kudumu...hivyo urafiki wetu sisi na China ni wa damu," amesema.


Naye, Balozi Wang amesema nusu ya karne iliyopita, kupitia ombi la Rais wa Tanzania, Julius Nyerere na Rais wa Zambia, Kenneth Kaunda, viongozi wa kizazi cha China, Mwenyekiti Mao Zedong na Waziri Mkuu, Zhou Enlai walifanya maamuzi ya kimkakati na kihistoria kusaidia ujenzi wa TAZARA.

"Wafanyakazi na mafundi Wachina 50,000 waliitikia wito wa taifa na waliungwa mkono na wenzao kutoka Tanzania na Zambia, walishinda vigumu na vikwazo vingine kumalizia ujenzi wa TAZARA yenye urefu wa kilomita 1,860 ndani ya miaka sita na kuufanya kuwa  mradi wa kihistoria wenye umaarufu duniani,"alisema.

Amesema wafanyakazi na mafundi 65  Wakichina walipoteza maisha na walizikwa katika ardhi ya Afrika mbali na nyumbani kwao.

"TAZARA imekuwa ikifahamika kwa dunia kama reli ya ukombozi iliyowasaidia watu wa Afrika kupata Uhuru na Ukombozi...na pia reli ya urafiki ikiwakilisha urafiki wa ndani kati ya Wachina na Waafrika,"amesema.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mfuko wa Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku amesema ipo haja kwa Tanzania na China kuendelea kudumisha urafiki wao.

"Wakati ule Mwalimu Nyerere kabla ya kwenda kuomba China watujengee reli alianza kuomba kwa nchi moja ya Magharibi sihitaji, anaetaka kuijua aje nitamnong'oneza. Nchi hiyo ilimjibu Nyerere hivi; ujenzi wa reli ya Tanzania na Zambia upitie Zanzibar. Nyerere akaondoka tukaenda China na baada ya kufika huko Mwalimu ikabidi aongee na waziri mkuu wa nchi hiyo, Zhou Enlai.

"Tena wakati anaomba hakwenda moja kwa moja alizunguka lakini hakujibiwa chochote ila wakati tunataka kuondoka tulienda kuaga kwa Rais wa China ambaye alikubali ombi letu. Kwa hiyo huu ni urafiki wa damu,"amesema.
 Mnara wa Makaburi ya Wachina waliokuwa wakijenga Reli ya Tazara  ambao walifariki wakati wa ujenzi wa reli hiyo miaka zaidi ya 40 iliyopita.
 Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga akitoa heshima  na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, kwenye Mnara wa makaburi ya Wachina waliofkuja kutengeneza Reli ya Tazara
 Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga akiwa na Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, wakiweka mashada kwenye moja ya kaburi la wakandarasi waliofika nchini kujenga reli ya Tazara
 Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga  akihutubia Viongozi na wakazi wa Jiji la Dar es Salaam waliofikakatika sherehe ya kitamaduni ya watu wa china ya kuwakumbuka mafundi waliojenga reli ya Tazara.
  Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, akihutubia na kutoa historia fupi ya ushirikiano wa Tanzania na China ulivyoasisiwa na Mwalimu Nyerere.
 Waziri wa Katiba na Sheria , Profesa Paramagamba Kabudi akiweka maua kwenye kaburi la wataalamu wa kichina waliokuwa wanajenga reli ya Tazara.
 Kibao kinacho elezea utambulisho wa Makaburi ya Wataalam wa Kichina Gongolamboto
 Katibu  wa Mfuko wa Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku akieleza namana Mwalimuj Nyerere alivyoweza kuomba reli kwa kiongozi wa China Mau Sentum
  Waziri wa Mambo ya Nje Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi  Agustine Mahiga  na  Balozi wa China Nchini Tanzania, Wang Ke, pamoja na Viongozi wengine wakiwa wamesimama nyimbo za Taifa za mataifa yote mawili zilivyokuwa zikiimbwa.
 watu waliofika katika Sherehe za utamaduni za kuwakumbuka Wataalamu na Wakandarasi walikuwa wanjenga reli ya Tazara  kutoka china  wakitoa heshima zao kwenye mnara wa kaburi hilo
Baadhi ya Wazee walioshiriki kujenga Reli ya Tazara kwa kushirikiana na Wachina miaka 40 iliyopita.
--

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA MJASILIAMALI WA SANAA ZA MIKONO

$
0
0
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimasikiliza  mjasiriamali Robinson Mungule anayeuza kazi za sanaa ya mikono katika ufukwe za Nungwi mkoa wa Kaskazini Unguja. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na mjasiriamali Robinson Mungule anayeuza kazi za sanaa ya mikono katika ufukwe za Nungwi mkoa wa Kaskazini Unguja. ( Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

AIRTEL MONEY YAGAWA BILIONI 14 KWA WATEJA WAKE HADI SASA, YATANGAZA GAWIO JIPWA

$
0
0
Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania, Jackson Mmbando, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu gawiwo la bilioni 1.8 la robo ya mwaka kwa wateja wa Airtel Money. katikati ni Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Tanzania, Isack Nchunda na Meneja wa Airtel Money, Ibrahim Marando.
Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Tanzania, Isack Nchunda, akitangaza gawiwo la bilioni 1.8 la robo ya mwaka kwa wateja wa Airtel Money wakati kizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Kulia ni Meneja wa Airtel Money, Ibrahim Marando.

Airtel Tanzania imetoa gawio linalofikia shilingi bilioni 14.8 hadi sasa kwa wateja wake na mawakala nchi nzima ikiwa ni  sehemu ya faida waliyoipata tangu mwaka 2015.

Hili limebainishwa na Mkurugenzi wa masoko wa Airtel Tanzania, Isack Nchunda kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Airtel wakati akitangaza gawio la robo hii ambalo ni shilingi bilioni 1.8.

“Tangu tuanze kugawa sehemu ya faida yetu kwa wateja mwaka 2015, tumeshatoa jumla ya shilingi bilioni 14.8 na huwa tunagawa kila robo ya mwaka na kuhakikisha wateja na mawakala wanapokea fedha hizi kupitia akaunti zao za Airtel Money na wana uhuru wa kutumia fedha hizi wanavyotaka,” alisema.

Kwa mujibu wa Nchunda, hii ni mara ya sita mfulululizo kwa Airtel Tanzania kugawa sehemu ya faida kwa wateja wake tangu mwaka 2015. “Bwana Pesa hutoa gawio hili kwa wateja wa Airtel Money na mawakala kulingana na salio la mteja kila siku,” aliongeza.

Aliwashukuru wateja wa Airtel kwa kuendelea kutumia Airtel Money na kuifanya iwe huduma yenye tija na maarufu zaidi na kuongeza kuwa hadi sasa wana zaidi ya maduka 100 maalum kwa kutoa huduma ya  Airtel Money ambayo yanafanya huduma hii iwe ya kuaminika zaidi na rahisi kupatikana.

“Maduka haya ya Airtel Money huhakikisha mawakala wana salio la kutosha muda wote ili wateja wasipate usumbufu wanapohitaji huduma hiyo,” alisema. 

Kwa upande wake, Meneja wa Airtel Money, alisema kuanzia leo, wateja wa Airtel Money na mawakala watapata gawio linalofikia shilingi bilioni 1.8 kupitia akaunti zao za Airtel Money na wanaweza kutumia gedha hizo wanavyotaka ikiwemo kulipia huduma mbalimbali kama vifurushi vya mtandao, muda wa maongezi na LUKU.

Alitoa wito kwa mawakala wa Airtel Money kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma bora kwa wateja ili kampuni hiyo iendelee kutoa gawio kwa wateja wake kila robo ya mwaka.

“Airtel Money imejizatiti kuendelea kutoa huduma bora na nafuu ambayo ni suluhisho kwa biashara za aina yoyote,” alisema na kuongeza kuwa Airtel inashirikiana na biashara zaidi ya 400 na ziadi na benki 30 katika kutoa huduma za kifedha.

Airtel ina zaidi ya mawakala 50,000 nchi nzima na inaendelea kutanua wigowake ili kuhakikisha huduma za kifedha zinapatikana katika miji na vijijini.

TBL YAJIKITA KUINUA KILIMO KWA NJIA YA UBUNIFU WA MIRADI YA KISASA

$
0
0
 Na Humphrey Shao, GLobu ya Jamii

KAMPUNI ya Bia nchini(TBL) ambayo ni moja kati ya wanafamilia AB InBev imeandaa shindano linalowahusisha matumizi ya ubunifu na teknolojia kwa wakulima.


Shindano hilo lililozinduliwa jana, litafikia tamati Mei 10 mwaka huu, tukio litakalofanyikia ukumbi wa Mlimani City ambapo washindi watatu watapatikana.


Akizungumza kwenye uzinduzi wa shindano hilo, linalofanyika kwa ushirikiano na Mradi wa masuala ya Teknolojia na Ubunifu Bits & Bytes,  Mkurugenzi Mtendaji wa TBL, Roberto Jarrin, alisema lengo ni kuwatambua na kuwaendeleza wakulima wanaolima kibunifu.


Alisema, kilimo cha kibunifu kinawanufaisha wakulima kwa kuwa wanapata faida ile ile iliyokusudiwa kwa kuwa kinaokoa mazao na mbegu kupotea wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna.



“Tanzania Breweries tumeona nafasi ambayo kilimo inayo katika kuendeleza uchumi wa nchi na hilo linaweza kufanikiwa kwa kutumia teknolojia na ubunifu katika kilimo, hivyo shindano hili linalenga kuwafikia wakulima wengi zaidi”alisema Roberto Jarrin.


Kwa upande wake Mwanzilishi mwenza wa Bits and Bytes  Zuweina Farah, alisema katika kuhakikisha kilimo chenye kuhusisha ubunifu na teknolojia unafanikiwa mnamo April 9 watakua SUGECO, na tarehe 10 na 12 watashiriki kwenye kongamano la kilimo biashara mkoani Morogoro.


Aliongeza pia Arusha mnamo April 12 na 13 katika Chuo cha ufundi Arusha kutakuwa na mjadala kuhusiana na kilimo ikiwa pamoja na kutembelea miradi tofauti ya Twende. Huku April 14 hadi 15  itashirikiana na AIESEC kwa Dar na mipango mingine kufanyiwa kazi kufikisha ujumbe kwa wabia tofauti kwenye eneo hili..


 Mkurugenzi wa Tasisi Bits and Bytes,Lilian Madeje  akizungumza na Waandishi wa habari juu mradi wa ubunifu wa  kuinua kilimo nchini
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia nchini(TBL),Roberto Jarrin, akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya udhamini wao wa kuwezesha bunifu za Kilimo
 Waandishi wa Habari waliohudhulia Mkutano huo wakifatilia kwa makini hotuba ya Mkurugenzi wa TBL

AJALI YA MAGARI KUGONGANA YAUA WATU 12, YAJERUHI 46

$
0
0
Ajali hii imetokea majira ya saa mbili usiku wa jana huko kijiji cha Makomero wilaya ya Igunga Mkoa wa Tabora ambapo Basi lenye namba za usajili T.983 DCE mali ya Kampuni ya CITY BOY likiendeshwa na EMANUEL ATUPENDA CHITEMO mkazi likiwa linatokea Ngara Mkoa wa Kagera kuelekea Mkoa wa Dar es salaam liligongana na gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T.486 ARB lilokuwa linaendeshwa na SALUMU ABDALAH KALAMBO na kusababisha vifo vya abiria 12 huku 46 wakijeruhiwa.

Akiongea na waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandamizi WILBROD MUTAFUNGWA ameeleza kwamba Abiria 12 walipoteza Maisha huku wengine 46 wakijeruhiwa na kati yao aliwataja abiria watatu ambao hali zao ni mbaya na wawili wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mkoa wa Mwanza na mmoja Nkinga Mission wilaya ya Igunga.

Kamanda Mtafungwa ameeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Gari aina ya Fuso kupasuka tairi ya mbele upande wa kulia na kusababissha kukatika kwa mfumo wa usukani likiwa katika mwendo mkali baada ya kuyaingia mashimo mawili yaliyo katikati ya barabara na kusababisha kupoteza mwelekeo na kisha kuligonga basi la abiria lililokuwa likipishana nalo.
Gari kampuni ya CITY BOY mara baada ya kupata ajali.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora alipowatembelea na kuwajulia hali majeruhi katika Hospitali ya Igunga.

MAANDALIZI YA UZINDUZI WA UKUTA KUZUNGUKA MIGODI YA TANZANITE MEREARNI YAKAMILIKA

$
0
0
Waziri wa Madini Mhe. Anjellah Kairuki akifurahia jambo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Venance Mabeyo kabla ya kikao cha majumuisho kuhusu maandalizi ya uzinduzi wa ukuta kuzunguka mgodi wa Tanzanite Mirerani Mkoani Manyara unaotarajiwa kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 6 Aprili 2018.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Hussein Mwinyi akipokelewa na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Venance Mabeyo kabla ya kikao cha majumuisho kuhusu maandalizi ya uzinduzi wa ukuta kuzunguka mgodi wa Tanzanite Mirerani Mkoani Manyara unaotarajiwa kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 6 Aprili 2018.
PIX7.Mafundi wakiwa katika hatua za mwisho kukamilisha maandalizi ya uzinduzi wa ukuta kuzunguka mgodi wa Tanzanite Mirerani Mkoani Manyara unaotarajiwa kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 6 Aprili 2018.
Mmoja wa mafundi akiendelea na kazi ya kuandaa eneo litakapowekwa jiwe la msingi wakati wa uzinduzi wa ukuta kuzunguka mgodi wa Tanzanite Mirerani Mkoani Manyara unaotarajiwa kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 6 Aprili 2018.
Sehemu ya geti la kuingia katika eneo la mgodi wa Tanzanite kama inavyoonekana katika picha.

TFDA YAWAPA WADAU MIONGOZO YA USAJILI WA VIWANDA

$
0
0
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imekutana wadau wenye nia ya kuwekeza katika viwanda vya dawa kwa ajili ya kupata miongozo ya kufanya kiwanda kiweze kujengwa na kuanza kuzalisha dawa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo ,Adam Fimbo amesema kuwa kuwakutanisha wadau hao umetokana mkutano wa Mawaziri wa Viwanda , Biashara na uwekezaji pamoja Wizara ya Afya, Maendeleo Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto ambapo TFDA imeona ni muda mwafaka katika kuweza kuwapa muongozo wadau jinsi ya kuweza kuanzisha viwanda hivyo.

Fimbo amesema kuwa TFDA kazi yake kubwa ni kuangalia usalama wa dawa tangu inapozalishwa mpaka inaingia sokoni ikiwa lengo ni kumlinda mlaji na dawa hizo.Aidha amesema kuwa baada ili kiwanda cha dawa kiweze kusajiliwa na kuzalisha dawa hizo lazima vigezo vilivyokwa vizingatiwe.

Fimbo amesema baada ya kupata michoro na kuanza kuzalisha dawa usajili hauzidi siku 15 kutokana na hatua zote zilizofanyika TFDA inakuwa imepitia.
Hata hivyo amesema kuwa hakuna uarasimu wowote katika kusajili dawa au kiwanda nia kumlinda mlaji kwa dawa anazotumia.

“Bila kuwa na usalama wa dawa unaweza ukaua watu ndio maana TFDA tuka kwa ajili ya kazi hiyo ya kuangalia usalama wa dawa za ndani na zinazoingia”amesema Fimbo.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Adam Fimbo akizungumza na waandishi habari kuhusiana na kukutana na wadau wenye nia ya kuwekeza katika viwanda vya dawa kupata miongozo ya kufanya kuwekeza katika sekta hiyo, leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Mkaguzi wa Viwanda vya Dawa wa TFDA, Proche Patrick akiwapitisha katika miongozo wadau wenye nia ya kuwekeza katika viwanda vya dawa leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Msajili wa Dawa wa TFDA, Dk. Shani Maboko akizungumza na wadau wenye nia ya kuwekeza katika viwanda vya dawa jinsi ya usajili wa dawa unavyofanyika katika mamlaka hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wadau wenye nia ya kuwekeza katika viwanda vya dawa wakisikiliza mada zinazotolewa na TFDA . leo jijini Dar es Salaam

MAHAKAMA YA TANZANIA YAINGIA MAKUBALIANO NA SHIRIKA LA POSTA KUSAMBAZA NAKALA ZA HUKUMU

$
0
0
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang’ombe, akizungumza wakati wa hafla ya kusaini mkataba kati ya Posta na Mahakama ya Tanzania wa huduma ya Posta Mlangoni inayotolewa na shirika hilo. Hafla hiyo, imefanyika katika Ofisi za Mahakama ya Rufani, jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Katanga na kushoto ni Mwanasheria Mkuu wa TPC, Zuhura Pinde. Waliosimama nyuma yao, ni baadhi ya Maofisa waandamizi wa Posta na Mahakama.
Msajili wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati (kulia), akizungumza katika hafla hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang’ombe na katikati ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Katanga. Wengine nyuma kutoka kushoto ni Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji Biashara wa TPC, Fadya Zam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TPC, Elia Madulesi, Mtendaji wa Mahakama Kuu, Leonard Magacha, Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Solanus Nyimbi.
Msajili wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati (kulia), akizungumza katika hafla hiyo, jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang’ombe na katikati ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Katanga. Wengine nyuma kutoka kushoto ni Kaimu Meneja Mkuu Uendeshaji Biashara wa TPC, Fadya Zam, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TPC, Elia Madulesi, Mtendaji wa Mahakama Kuu, Leonard Magacha, Msajili wa Mahakama Kuu, Ilvin Mugeta na Mtendaji wa Mahakama ya Rufani, Solanus Nyimbi. 
Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Katanga akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Mwanasheria wa Mahakama ya Tanzania, Peace Mpango (kulia), akisaini mkataba huo, huku akiangaliwa kwa makini na Mwanasheria Mkuu wa TPC, Zuhura Pinde. 
Mwanasheria Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Zuhura Pinde, akisaini akisaini mkataba huo, huku akiangaliwa kwa makini na Mwanasheria wa Mahakama ya Tanzania, Peace Mpango.
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang’ombe (kushoto) na Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Hussein Katanga (kulia), wakibadilishana mkataba huo, mara baada ya kusainiwa katika hafla hiyo.
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania (TPC), Hassan Mwang’ombe, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla hiyo, jijini leo.
Msajili wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika hafla hiyo.

Kamishna wa Nishati Afanya Ziara katika kiwanda Cha Mita Za LUKU Cha Inhemeter Tanzania Limited

$
0
0
 eneja Mwandamizi wa kiwanda cha kuzalisha mita za LUKU cha Inhemeter Tanzania Limited, Will Tang (kulia) akielezea majukumu ya kiwanda hicho kwa Kamishna wa Nishati, Mhandisi Innocent Luoga (kushoto) katika ziara yake aliyoifanya katika kiwanda hicho kilichopo jijini Dar es Salaam  tarehe 03 Aprili, 2018.
Picha Na 2
Kamishna wa Nishati, Mhandisi Innocent Luoga (katikati) akitoa maelekezo kwa  uongozi wa kiwanda hicho. Kushoto ni Mshauri Mkuu wa Kiwanda hicho, Mhadisi Dkt. Adelhelm Meru na kulia ni Meneja Mwandamizi wa kiwanda hicho,Will Tang.
Picha Na 3
Mafundi wakiendelea na kazi ya kutengeneza mita katika kiwanda hicho.
Picha Na 4
Kutoka kushoto mbele Meneja Mwandamizi wa kiwanda cha kuzalisha mita za LUKU cha Inhemeter Tanzania Limited, Will Tang Kamishna wa Nishati, Mhandisi Innocent Luoga, Mshauri Mkuu wa Kiwanda hicho, Mhadisi Dkt. Adelhelm Meru na Msimamizi wa Utawala wa kiwanda hicho, Khilna Chohan wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho.
Picha Na 5
Baadhi ya mita  za LUKU zinazotengenezwa na kiwanda hicho
Picha Na 6
Mtambo maaalum wa kupima ubora wa mita katika kiwanda hicho.
……………..
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Tarehe 03 Aprili, 2018 Kamishna wa Nishati, Mhandisi Innocent Luoga alifanya ziara katika kiwanda cha kuzalisha mita za LUKU cha Inhemeter Tanzania Limited kilichopo jijini Dar es Salaam.
Lengo la zira hiyo lilikuwa ni kuangalia utendaji kazi wa kiwanda hicho pamoja na kutatua changamoto zilizopo katika kiwanda hicho.
Akizungumza katika ziara hiyo Mshauri Mkuu wa Kiwanda hicho, Mhadisi Dkt. Adelhelm Meru alisema  kiwanda hicho kilichoanzishwa Februari mwaka huu kina uwezo wa kuzalisha mita 500,000 kwa mwaka na kusisitiza kina uwezo kwa kuzalisha hadi mita milioni moja kulingana na mahitaji ya soko.
Dkt Meru aliendelea kusema kuwa, kiwanda kimeanza kuzalisha mita kidogo na kuiomba serikali  kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya usambazaji wa miundombinu ya umeme vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kutoa oda za mita nyingi ili waanze kuzalisha mita nyingi za kutosha kulingana na soko.
“Mita tunazotengeneza zina ubora wa hali ya juu zenye kuendana na mazingira ya aina yoyote, tunaunga mkono juhudi za Serikali kuelekea kwenye uchumi wa viwanda kwa kusambaza vifaa kwa ajili ya wakandarasi wanaojenga miundombinu ya umeme nchini,”alisema Dkt. Meru.
Wakati huohuo Meneja Mwandamizi wa Kampuni hiyo, Will Tang aliomba Serikali kutoa kipaumbele kwa matumizi ya vifaa vya umeme vinavyotengenezwa na viwanda vya ndani ya nchi.
Naye Mhandisi Luoga aliuhakikishia uongozi wa kiwanda hicho kuwa Serikali kupitia Wizara ya Nishati inaunga mkono juhudi za kiwanda hicho na kusisitiza kuwa ipo tayari kutumia bidhaa zake katika miradi ya umeme vijijini.
“Mara baada ya kuthibitisha ubora wa bidhaa zenu, mnatakiwa kujiandaa kupokea oda kubwa kutoka TANESCO na REA kwa mwaka,” aliongeza Kamishna Luoga.
Alisema katika kuhamasisha Sera yake ya Uchumi wa Viwanda, Serikali ya Awamu ya Tano inatoa kipaumbele cha matumizi ya bidhaa za ndani hususan katika miradi ya umeme nchini kwa kuwa viwanda vya ndani vitaongeza mapato, ajira na hata kurahisisha upatikanaji wa bidhaa hizo kwa bei nafuu nchini.
Akielezea hatua kadhaa zilizochukuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Nishati kwenye uhamasishaji wa  uwekezaji wa viwanda vya ndani, Mhandisi Luoga alieleza kuwa, Serikali imepiga marufuku uingizaji wa nguzo za umeme kutoka nje ya nchi pamoja na bidhaa nyingine zinazopatikana hapa nchini.
“Tunataka ifike mahali mita za LUKU, transfoma, nyaya na vifaa vingine vyote vya umeme vitoke ndani ya nchi tu na kukuza uchumi wa viwanda,” alisisitiza Mhandisi Luoga.
Hata hivyo Mhandisi Luoga alielekeza kampuni hiyo kukaa pamoja na Wizara, TANESCO na REA na kupanga namna ya kushirikiana katika utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme nchini

WATUMISHI WA SEKTA YA UJENZI WATAKIWA KUJITATHIMINI

$
0
0
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa, akizungumza na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Sekta ya Ujenzi (hawapo pichani), wakati wa ufunguzi wa baraza hilo lililofanyika mkoani Morogoro.
Mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhanga (katikati), akizungumza na wajumbe wa baraza hilo pamoja na wawakilishi kutoka Taasisi zilizo chini ya sekta hiyo katika kikao cha baraza la wafanyakazi, mkoani Morogoro.
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Bi. Elizabeth Tagora akiwasilisha rasimu ya bajeti na mpango wa utekelezaji wa sekta hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2018/19 kwa wajumbe wa baraza la wafanyakazi, mkoani Morogoro.
Baadhi ya wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) wakifuatilia maelekezo ya mgeni rasmi ambaye ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani), wakati wa ufunguzi wa kikao cha baraza hilo kilichofanyika mkoani Morogoro.
Katibu wa baraza la wafanyakazi (Sekta ya Ujenzi), Bw. Vendeline Massawe, akitoa neno la shukrani kwa wajumbe wa baraza kwa kumchagua kushika nafasi hiyo mara baada ya katibu wa zamani kupata uhamisho, Mkoani Morogoro.
Mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhanga (katikati), pamoja na viongozi wengine wakishiriki kuimba nyimbo ya ‘Solidarity forever’ kuonyesha mshikamano katika utendaji kazi wakati wa Kikao cha baraza la wafanyakazi, Mkoani Morogoro.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Sekta ya Ujenzi mara baada ya kufungua kikao cha baraza hilo kilichofanyika Mkoani Morogoro.

…………………

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amewataka wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa Sekta ya Ujenzi kujitathimini yale waliyoazimia kutekeleza kwa mwaka wa Fedha 2017/18 kama yamefikia lengo ili kuweza kusaidia kuboresha utendaji na kutafutia ufumbuzi masuala ambayo yanakwamisha ufanisi wa kazi na kuwezesha mazingira wezeshi kwa wafanyakazi.


Prof. Mbarawa amesema hayo mkoani Morogoro, wakati akifungua kikao cha baraza la wafanyakazi ambapo pamoja na mambo mengime amesisitiza umuhimu wa baraza hilo katika kuhakikisha kuwa waajiri na watumishi wanatambua wajibu na haki zao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kuleta matokeo chanya katika utendaji kazi wenye tija, staha na upendo.

“Ni matarajio yangu kuwa kila mjumbe kwa nafasi aliyonayo katika baraza hili atatumia fursa hii kutoa michango ya mawazo ili iweze kuwa mwongozo mzuri wa kutekeleza majukumu kwa ufanisi”, amesema Prof. Mbarawa. 

Aidha, ametoa wito kwa wajumbe hao kuhakikisha kuwa Wizara inashiriki kikamilifu katika kutekeleza azma ya Serikali ya kuwajengea watanzania miundombinu bora na imara ili kuifanya Tanzania iwe nchi ya viwanda na hivyo kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya kuifanya nchi yetu iwe na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.

Profesa Mbarawa, amewataka wajumbe hao kujadili kwa kina Rasimu ya Bajeti na Mpango wa utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2018/19 ili kuweza kuleta tija na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi Waziri Prof. Mbarawa, Mwenyekiti wa baraza hilo ambaye ni Katibu Mkuu wa Sekta ya Ujenzi Mhandisi Joseph Nyamhanga, amesema kuwa mabaraza ya wafanyakazi yameanzishwa kwa madhumuni ya kuishauri Serikali katika ngazi ya Wizara, Idara na Taasisi za Umma kuhusu usimamizi wa rasilimali watu, utekelezaji wa majukumu kwa ufanisi na weledi kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya utumishi wa umma. 

Ameongeza majukumu mengine kuwa ni kulinda haki na wajibu wa waajiri na wafanyakazi; kutoa ushauri kuhusu kujenga hali bora za kazi; maslahi ya Wanyakazi na kusimamia haki na ustawi katika sehemu za kazi.

WAKULIMA KUNUFAIKA NA KILIMO CHA PAMBA GEITA

$
0
0
Na Joel Maduka,Geita

Serikali imewahakikishia mazingira yaliyo salama wakulima wa zao la pamba ikiwa ni pamoja na kununuliwa kwa zao hilo bila ya kukopwa kwa msimu wa pamba ambao unatarajia kuanza tarehe 1 Mei mwaka huu .

Hayo yameelezwa na kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru , Charles Kabeho wakati akifungua mradi wa zao la pamba katika kijiji cha Nyamalimbe Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo alisema serikali imejipanga kuhakikisha mkulima wa pamba mwaka huu ananufaika na zao hilo.

“ Zao la Pamba linamanufaa kwa mkulima na serikali kwani zao ambalo linatengeneza nguo kuliko kusubili kuletewa mitumba kutoka nje hivyo tulithamini zao hili kwani linasaidia pia kuondoa umaskini katika familia”Alisisitiza Kabeho.

Mussa Kabehe ambaye ni Mkulima wa zao hilo alisema kwa sasa kutokana na hali ya hewa na mvua kunyesha kwa wingi wamekuwa na matumaini machache ya kupata pamba Nyingi kwani asilimia kuwa zimeharibikia shambani na kwamba awana matarajio ya kuzalisha pamba Nyingi zaidi ingawa kwa mwaka huu wengi walijitokeza kulima pamba.

Kiongozi huyo wa mwenge pia amefungua miradi 12 katika Halmashauli ya Wilaya ya Geita iliyo gharimu kiasi cha shilingi bilioni tano na milioni miatatu ambapo pia kiongozi huyo aliwakumbusha wananchi wa kijiji hicho kutojihusisha na suara la rushwa kwa ni adui wa haki.
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Charles Kabeho akizungumza na kuwasisitiza wakulima wa zao la Pamba kuwekaza nguvu zaidi kulima zao hilo wakati alipoweka Jiwe la Msingi kwenye mradi wa shamba la pamba kijiji cha Nyamalimbe Wilayani Geita. 
Baadhi ya pamba zikiwa shambani kabla ya kuvunwa. 
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Charles Kabeho,akiweka jiwe la msingi kwenye shamba la pamba kwenye kijiji cha Nyamalimbe. 
Watoto ambao ni yatima wakipewa zawadi na Kiongozi wa mbio za mwenge Charles Kabeho kwenye Kijiji cha Bujura wilayani Geita.
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images