Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46396 articles
Browse latest View live

RAIS MAGUFULI AREJEA NCHINI AKITOKEA NCHINI UGANDA ALIPOHUDHURIA MKUTANO WA 19 WA WAKUU WA NCHI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

$
0
0



Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa MKoa wa Mwanza John Mongella mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.


Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) MKoa wa Mwanza ndugu Anthony Dialo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa ndugu Kheri Jamesn mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Naibu Waziri wa Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Angelina Mabula mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akitazama ngoma mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akizungumza na baadhi ya Viongozi na Wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa MKoa wa Mwanza mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Ardhi,nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula,Mkuu wa MKoa wa Mwanza John Mongella na wacheza ngoma waliofika kumlaki uwanjani hapo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza akitokea Nchini Uganda alipohudhuria mkutano wa 19 wa wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.


PICHA NA IKULU.

OSHA YASISITIZA KADA YA USALAMA KAZINI KUTAMBULIKA RASMI

$
0
0
Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) unakusudia kuishawishi serikali na waajiri katika sekta binafsi hapa nchini kuitambua kada ya Usalama na Afya mahali pa kazi na kuiweka katika mfumo rasmi wa ajira.

Mpango huo uliwekwa wazi na Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA Bi.Khadija Mwenda, alipowahutubia wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi katika hafla ya kufunga kozi hiyo Februari 23,2018 jijini Dar es salaam. Kozi hiyo pamoja na nyingine zinazohusu Usalama na Afya kazini hutolewa na Wakala huo wa serikali.

Mtendaji Mkuu huyo alisema kwasasa kada ya maofisa Usalama Mahali pa Kazi (Safety Officers) bado haitambuliki katika mfumo rasmi wa ajira hapa nchini jambo linalopunguza ufanisi katika kusimamia utekelezaji wa Sheria Na. 5 ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003.

”Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi ya mwaka 2003, inawataka waajiri kuunda Kamati za Usalama na Afya katika sehemu zao za kazi ambazo wajumbe wake ni wawakilishi wa wafanyakazi ambao kimsingi wana majukumu yao mengine tofauti na kusimamia masuala ya usalama na afya mahali pa kazi. Hivyo jukumu la kusimamia usalama na afya wa wafanyakazi wenzao katika sehemu za kazi husika linakuwa ni la ziada,” alisema Bi. Mwenda.

Aliongeza: “Hivyo tunaamini kwamba endapo kada hii itaingizwa katika mfumo rasmi wa ajira katika sekta zote, waajiri wote watalazimika kuajiri wataalam wa masuala ya usalama na afya mahali pa kazi ambao jukumu lao kuu litakuwa ni kusimamia afya na usalama wa wafanyakazi wote wanapokuwa kazini.”

Aidha, Kiongozi huyo mkuu wa taasisi aliwaasa wahitimu wa mafunzo hayo kwenda kuwa mabalozi wazuri wa OSHA kwa kutumia ipasavyo elimu waliyoipata katika kuimarisha hali ya usalama na afya kwenye maeneo ya kazi wanakotoka na hivyo kuongeza tija na kukuza pato la Taifa.“Tunatarajia kwamba mtatuwakilisha vema katika sehemu mbali mbali za kazi mnakokwenda kufanya kazi kwa kuyatekeleza yale yote mliyojifunza katika mafunzo haya,” alisema kiongozi huyo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mafunzo, Utafiti na Takwimu wa OSHA, Bw. Joshua Matiko, aliwapongeza wahitimu hao kwakujituma na kuwa na nidhamu katika kipindi chote walipokuwa wakipatiwa mafunzo hayo.“Ninawaasa msiridhike na mafunzo haya mliyoyapata kwasasa bali mnapaswa kujiendeleza zaidi kwa kusoma kozi nyingine zitakazowawezesha kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi zaidi. Kwa mfano, kuna mafunzo mengine ya namna ya kufanya utambuzi wa vihatarishi katika sehemu za kazi yatatolewa hivi karibuni huko jijini Mwanza hivyo mnakaribishwa kushiriki,” alieleza Matiko.


OSHA ni msimamzi mkuu wa Usalama na Afya za wafanyakazi wanapokuwa kazini ambapo husajili sehemu za kazi, kufanya kaguzi za usalama na afya katika sehemu husika na kutoa mafunzo ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi.

Habari imeandikwa na Eleuter Mbilinyi
Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akiwahutubia wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Mafunzo, Utafiti na Takwimu wa OSHA, Bw. Joshua Matiko, akiongea na wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, akiwahutubia wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakati wa hafla ya kufunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam.
Wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakifuatilia hotuba ya Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, wakati wa hafla ya kufunga kozi hiyo iliyofanyika katika ofisi za Wakala jijini Dar es Salaam.
Wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakifuatilia hotuba ya Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, wakati wa hafla ya kufunga kozi hiyo iliyofanyika katika ofisi za Wakala jijini Dar es Salaam.
Wahitimu wa Kozi ya Taifa ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi wakifuatilia hotuba ya Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda, wakati wa hafla ya kufunga kozi hiyo iliyofanyika katika ofisi za Wakala jijini Dar es Salaam.

TAARIFA YA KUSITISHA MATUMIZI YA ADA MPYA KWA WAANDAAJI WA MBIO ZA MARATHON

$
0
0
SHIRIKISHO la Riadha Tanzania (RT), limepokea tamko la Baraza la Michezo la Taifa (BMT), kuhusu mada tajwa hapo juu Februari 20, 2018 kwa barua yenye Kumbukumbu namba: BMT/A/2/Vol. 18/69, pia kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

BMT imeagiza kusitishwa ada hizo hadi Machi 5 itakapotoa maelekezo mengine baada ya kukutana na RT na waandaaji.

Sisi RT tumefedheheshwa na uamuzi huo na jinsi njia iliyotumiwa na BMT katika kulishughulikia tatizo linalodaiwa kuwa malalamiko ya waandaaji wa marathon kudai kuwa tozo hizo ni kubwa, tofauti na wanachokiandaa au kukifanya.

Kwani tuliamini, kutokana na miongozo ya kiutendaji, BMT ingekuwa mstari wa kwanza kulinda matakwa ya Katiba ya RT kiutendaji.

Tuliamini BMT inajua mamlaka ya utendaji ya RT, hivyo kabla ya kufikia uamuzi huo, ingetuita RT kwanza na kujadili hicho kinachodaiwa kuwa malalamiko, ndipo ingefikia kuanza kuchukua hatua.

KUPANDISHWA ADA;

Kutokana na mwenendo usioridhisha kwa muda mrefu kuhusu uandaaji wa mbio za Marathon kiholela, ambao ulikuwa haufuati taratibu zinazotakiwa, hata BMT yenyewe ni shahidi kutokana na matamshi mbalimbali ya Watendaji wake, RT iliamua kuchukua hatua kwa mujibu wa Katiba yake kama msimamizi mkuu wa mchezo wa Riadha nchini.

Mnamo Septemba 16, 2017 RT ilitoa mwito kwa waandaaji wa mbio za Marathon na kukutana katika moja ya kumbi za Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ambako takribani waandaaji 28 - 30 walijitokeza.

Katika kikao hicho ambacho kilikuwa cha wazi na huru, RT iliwaeleza waandaaji kuhusiana na utaratibu mzima wa uandaaji wa mbio za Marathon na utaratibu mpya unaotakiwa kuanza kutumika kuanzia January 2018, ikiwamo kujisajili na kuzitenga mbio hizo katika makundi manne ya A, B, C na D kulingana na ukubwa wa mbio husika na kila kundi na gharama zake.

RT ilifikia uamuzi huo baada ya tathmini za kiufundi na uzoefu wake kama msimamizi mkuu wa mchezo wa riadha hapa nchini.

Katika kikao hicho yalifanyika majadiliano ya kina na waandaaji hao kutoa maoni yao kuwa viwango vya kwanza vilivyowasilishwa na RT vilikuwa vikubwa sana na kuomba kutazamwa upya.

RT ilipokea maoni hayo na Kamati Tendaji kuketi na kuvipitia upya na kisha kuja na mapendekezo mapya (siku hiyo hiyo), ambayo yaliridhiwa na pande zote katika kikao hicho.

RT ilisisitiza na kuwafafanulia wahusika kuwa, Marathon ni biashara na kama mdau ana nia njema ya kukuza na kuendeleza mchezo wa raidha kuna matukio mengi tu na si marathon pekee.

Kiufundi, waandaaji walishauriwa ili kuepuka gharama ambazo hawawezi kuzimudu, wajikite kuandaa mashindano ya Uwanjani ‘Track and field’ na mbio chini ya Kilomita 21, ambayo ni bure kabisa, zaidi ya kuhakikisha wamejisajili.

SINTOFAHAMU:

Baada ya maazimio hayo hatukuwahi kusikia au kupata malalamiko rasmi wala maoni kutoka kwa muandaaji yeyote kuhusiana na maamuzi yaliyofikiwa katika kikao cha Septemba 16, 2017 Uwanja wa Taifa.

Lakini cha kushangaza, tukasikia kuna malalamiko yamepelekwa BMT kuhusiana na uamuzi halali wa kikao cha Septemba 16, 2017 baina ya RT na Waandaaji.

Tuliamini kama kuna nia ya kweli na si ovu juu ya RT, hao waliokimbilia BMT wangeweza kuja tena RT na hoja zao na wangeona hakuna ufumbuzi, ndipo wangeenda ngazi nyingine. Tofauti na kilichofanyika na kwa masikitiko makubwa BMT kulibeba na kukimbilia kutoa uamuzi bila hata ya kuketi na chombo husika kilichopewa dhamana ya kusimamia mchezo wa riadha nchini.

Kwa kuonyesha BMT haikujipa muda kulijua jambo kwanza kwa kina kabla ya kuchukua hatua yoyote, ndio maana hata katika taarifa yake imenukuu vikao ambavyo katika kumbukumbu ya RT havipo.

Sehemu ya barua ya BMT inanukuu;

“Kufuatia malalamiko yanayotolewa na waandaaji wa mashindano hayo ya marathon kufuatia kupandishwa kwa ada za kuendesha mbio hizo, hayo yamesemwa kupitia kikao kilichokaliwa Oktoba 7, 2017 kati ya Msajili, uongozi wa RT na wadau wa mashindano hayo"

“Katika kikao cha Oktoba 7, pamoja na mambo mengine uongozi wa RT ulifahamishwa na Msajili wa Vyama na Klabu za Michezo nchini, umuhimu na ulazima kwa kufuata sheria, kwa waandaaji wa mashindano ya marathon kusajiliwa kama wakuzaji na mawakala wa michezo kwa mujibu wa kanuni ya 19 (1), (2), na (3)”.

RT katika kumbukumbu zake, haijawahi kuwa na kikao (specific kwa agenda ya kanuni za waandaaji wa marathon na msajili), kama ilivyoelezwa hapo juu, kuhusu taratibu RT ilihimizwa kufuata utaratibu kama vyama vyote vya michezo vinavyohimizwa na msajili.

UAMUZI WA RT

Kwanza unasisitiza uamuzi uliofikiwa katika kikao na waandaaji Septemba 16, 2017 Uwanja wa Taifa uko pale pale. BMT haiwezi kuipangia RT ada kama ambavyo haiwezi kuipangia TFF ada za viingilio nk. RT ni chombo huru na lenye majukumu makubwa ya kuhakikisha taifa letu linaleta medali za ushindi, ni jukumu la RT kujitafutia vyanzo halali vya mapato ili tusiitegemee serikali kwa kila jambo.

Tunasisitiza waandaaji wote kuhakikisha wanalipa ada kulingana na makundi yaliyopangwa na kujisajili kabla ya kuendesha matukio yao.

Pili kutokana na Kalenda ya RT, itakuwa ni ngumu Kamati ya Utendaji kuhudhuria kikao kilichoitishwa Machi 5 na BMT huko Moshi Kilimanjaro.

Sababu ni kutokana na wito mfupi wa kikao hicho, wajumbe wengi wametawanyika sehemu mbalimbali kutokana na majukumu ya kichama ikiwemo kushughulikia kambi za Taifa.

Kumbukumbu: BMT mara nyingi ilishawahi kutuhimiza tukae na waandaaji ili tupunguze msururu wa mbio za marathon ambazo hazina tija kwa taifa,

Uhalali: Chama cha waandaaji mbio sio mdau wa RT kwa maana haitambuliki rasmi kwetu, wadau halali wa RT ni waandaaji wa mbio moja moja waliojisajili na RT na kulipa ada (annual fee) pamoja na ada ya usajili.

Muundo: Categorization (madaraja) ya mbio ni jambo la kawaida duniani kote (standard practice all over the world - how can TZ be an exception? New York, Boston na London Marathon ni Lebel A wakati mbio zingine ni B,C nk.

Mwisho, tunaiomba BMT kuangalia namna ya kushughulikia masuala hususan ya kiufundi na uhuru wa kikatiba wa vyama vya michezo, ili kuepusha misigano ambayo itarudisha nyuma maendeleo ya michezo hususan riadha.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki michezo yetu.

Imetolewa na:

Wilhelm Gidabuday

Katibu Mkuu RT

24/20/2018

KUNA WATU WANAJIDAI WANASHAHADA ZA UCHUMI KUMBE MAMBUMBU WA UCHUMI-Dk MPANGO

$
0
0

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAZIRI wa Fedha na Mipango,Dk.Philipo Mpango amesema kuna baadhi ya watu nchini wamekuwa wakijidai wana shahada za uchumi lakini kiuhalisia ni mambumbu wa uchumi.

Pia amesema kutungwa kwa sera au kufanyika kwa maamuzi yasiyoendana na taaluma ya uchumi kunakopelekea kuumiza wananchi masikini kutokana na uwepo wa wachumi feki ambao wanapewa nafasi serikalini ,vyuoni hata kwenye sekta binafsi.

Amesema ili kukabiliana na changamoto hizo na nyingine iko haja nchi kuwa na jJumuiya ya Wachumi au chama hai cha wachumi na chenye nguvu kwani ni muhimu sana.Dk.Mpango amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anazindua rasmi chama cha Jumuiya ya Wachumi (EST) ambapo ametoa sababu tatu za umuhimu wa jumuiya hiyo.

Amefafanua sababu ya kwanza tasnia ya uchumi ina nafasi ya pekee katika kazi ya kujenga nchi kijamii,kiuchumi na hata kisiasa."Wachumi tunategemewa tuwe viongozi .Bila shaka waumini wenzangu wa John Maynard Keynes kuna maneno amewahi kuyasema na naomba nimnukuu.

Amesema hivi mawazo ya wachumi na wanafalsa wa siasa ,yawe sahihi au so sahihi yana nguvu kuliko inavyoeleweka kwa wengi."Watu wanaojiamini kwamba wako guru na ushawishi wa wanataaluma ,kiuhalisia watu hao ni watumwa wa mchumi fulani marehemu," amesema Dk.Mpango wakati ananukuu manneo ya Keynes.

Amesema sababu ya pili inatokana na ukweli siku za usoni hazifahamiki mia kwa mia na wao wachumi hawana anasa ya kufanya majaribio ya maisha ya watu katika maabara kama wenzao wa upande wa sayansi asilia.Ameongeza endapo watafanya majaribio na misingi ya uchumi jumla kiuhalisia bila shaka moto utawaka kwa maana ya mfumuko wa bei kupanda,thamani ya sarafu kuanguka, uzalishaji kushuka, wananchi kukosa huduma za msingi.

Pia vijana kukosa ajira na mambo mengine mengi ambapo athari zake ni kuchochea maandamano mitaani ambayo yamesabaabisha serikali nyingi kuanguka.Hivyo ili kuepuka kufanya makosa makubwa kupita kiasi mbadala wa maabara kwa wananchi ni uwepo wa jukwaa la mijadala ya kukosoana na kubadilishana mawazo kuhusu Sera na mwenendo wa uchumi wa Taifa.

Wakati sababu ya tatu,Dk.Mpango anasema ni jumuiya hai ya kusimamia kazi za wachumi hapa nchini.Matokeo take kumewepo na wachumi feki,kukosekana kwa udhibiti wa vyeti.Pia uwepo wa Stashahada na Shahada zinavyopatikana au kutengenezwa kwenye mitandao ya kompyuta na matokeo yake kuharibika kwa sofa za wachumi wazuri wa Tanzania.

"Kuna msemo unasema samaki mmoja akioza basi wote wameoza.Hivyo kupitia jumuiya hii ya wachumi naomba sana safari hii tufanye tofauti kwa kurekebisha hali hii na natumaini itakuwa no kwa mara ya mwisho.

" Baadhi yenu mtakumbuka Jumuiya ya Wachumi Tanzania kwa mara ya kwanza ilisajiliwa Novemba 15 mwaka 1996 na ikapewa hati ya usajili Juni 26 mwaka 2013 na Wizara ya Mambo ya Ndani.

"Baadhi ya malengo makuu ya kuanzishwa kwa jumuiya hiyo ni kulinda tasnia ya wachumi nchini,kuwaunganisha wachumi, kusimamia weledi wa wachumi,kuhamasisha na kuimarisha utafiti na uchambuzi wa taarifa," amesema Dk.Mpango.

Ameongeza kupitia Sera na mipango mbalimbali ya maendeleo ya Serikali kwa ujumla na kisekta na kuimarisha uhusiano na taasisi nyingine.Dk.Mpango amesema hata hivyo imepita miaka takriban 20  kuanzia mwaka 1998 hadi hivi sasa ambayo jumuiya imekuwa mfu au haionekani kuwepo au kutoa mchango wowote kwa nchi yetu kama ilivyokusudiwa.

Amesema matarajio yake kuanzia leo Tanzania itakuwa na Jumuiya ya Wachumi yenye nguvu itakayojengwa juu ya misingi ya weledi na utaalam,elimu na ujuzi,bidii,uzalendo ,uwazi na uwajibikaji.Pia anapenda kuona Jumuiya ya wachumi ambayo itajinasibisha kwa umahiri wa kukuza utafiti wa kiuchumi,maendeleo ya nchi na mafunzo ya wachumi kazini.

Amesema anataka kuona Jumuiya yenye kuratibu jukwaa la mijadala kuhusu sera za kiuchumo na maendeleo ya Taifa.Ametumia nafasi hiyo kuwatambua na kuwapongeza wachumi wazalendo ambao wameiweka nchi yetu ya Tanzania katika ramani ya dunia ya wachumi mashuhuri.

Amesema wa kwanza ni Profesa Justian Rweyemamu,wa pili ni Rais mstaafu ,Dk.Jakaya Kikwete na watatu ni Gavana mstaafu wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT)Profesa Benno Ndulu .

"Hawa kwa maoni yangu wanastahili tuzo na napenda Jumuiya ya Wachumi mpya itafakari vigezo na namna bora ya kuwatambua na kuwaenzi wachumi hawa ," amesema Dk.Mpango na kuongeza" Na vilevile kutambua wachumi wengine wenye sifa kama hizo na hata wachumi chipukizi ili kutambua vipaji vyao".
Mkurugenzi wa Kituo Cha Uwekezaji TIC na Mwenyekiti wa Kamati Uzinduzi wa Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Wachumi Tanzania Economics Society Of Tanzania (EST) Bw. Godfrey Mwambe akipokea katiba ya Chama hicho kutoka kwa Vick Msima Meneja Msaidizi Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki (BOT)kwa ajili ya uzinduzi rasmi wa jumuiya hiyo kwenye ukumbi wa BOT leo jijini Dar es salaam, ambapo Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango katikati anayeshuhudia ndiye aliyezinduam, Kulia ni Gavana wa Benki Kuu (BOT)Profesa Florens Luoga.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango katikati akizindua katiba ya chama hicho kwa kushirikiana na Gavana wa Benki Kuu (BOT)Profesa Florens Luoga na mawaziri pamoja na viongozi mbalimbali wachumi wakishiriki katika zoezi hilo.
Baadhi ya wachumi wakiwa katika uzinduzi wa jumioya hiyo leo kwenye ukumbi wa BOT jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango katikati akionyesha katiba ya chama hicho na Gavana wa Benki Kuu (BOT)Profesa Florens Luoga na mawaziri pamoja na viongozi mbalimbali wakishiriki katika zoezi hilo.
Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango katikati pamoja na Gavana wa Benki Kuu (BOT)Profesa Florens Luoga na mawaziri pamoja na viongozi mbalimbali wachumi wakionyesha katiba ya Jumuiya hiyo baada ya kuzinduliwa rasmi leo jijini Dar es salaam..
Picha mbalimbali zikionyesha washiriki mbalimbali wa mkutano huo wa uzinduzi ambao ni wachumi na wanachama wa (EST)
Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango katikati akiwa katika picha ya pamoja na Gavana wa Benki Kuu (BOT)Profesa Florens Luoga na mawaziri pamoja na viongozi mbalimbali wachumi walioshiriki katika uzinduzi huo.
Waziri wa Fedha na Mipango Dk. Philip Mpango katikati akiwa katika picha ya pamoja na Gavana wa Benki Kuu (BOT)Profesa Florens Luoga na mawaziri pamoja na viongozi mbalimbali wachumi walioshiriki katika uzinduzi huo.

Meya Mwita awasilisha Mpango wa bajeti bilioni 75.2, 2018/ 2019

$
0
0
MSTAHIKI Meya wa jiji la Dar es Salaam , Isaya Mwita leo amewasilisha mpango wa bajeti wa mwaka 2018 hadi 2019 ambapo jumla ya shilingi bilioni 75.2 zitatumika kwa mwaka huo.

Hata hivyo mpango huo umepitishwa kwa kauli moja na Madiwani wote wa halmashauri hiyo huku wakimpongeza kwa kusema kuwa jiji limepata Meya anayejali maslahi ya maendeleo katika halmashauri hiyo.

Halmashauri hiyo imeandaa mpango huo kwa kuzingatia taratibu zinazotakiwa kufuatwa na mamlaka za Serikali za mitaa katika utayarishaji wa makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha wa 2018 na 2019.

Akizungumzia mpango huo kwenye mabaraza la Madiwani na waandishi wahabari , Meya Mwita amesema kuwa jiji limekadiria kukusanya na kutumia shilingi bilioni 75.2 ambapo itatokana kwenye vyanzo mbalimbali vya mapato ikiwemo bilioni 18.1 zinatarajiwa kukusanywa kutoka kwenye vyanzo vya vyandani.

Aidha amefafanua kuwa mapato mengine yatapatikana kutokana na halmashauri kubuni vyanzo vingine vya mapato sambamba na kuboresha mikakati ya ukusanyaji wa mapato.

Amefafanua kuwa utekelezaji wa bajeti hiyo umelenga kutekelaza mradi wa ujenzi wa kituo cha mabasi cha Mbezi Luis,kuboresha miundombinu ya Dampo,ujenzi wa vyoo vya Umma na kuhakikisha utoaji wa huduma usiokua na usumbufu kwa wananchi.

Amesema halmashauri pia imepanga kutumia asilimia 65 ya mapato ya ndani sawa na shilingi bilioni 11.7 kwa ajili ya kuchangia miradi mbalimbali ya maendeleo ,shilingi bilioni 1.08 zitatumika kwa ajili ya mfuko wa wanawake ,vijana na walemavu.

Akizungumzia suala la utalii ,Meya Mwita amesema kuwa katika bajeti hiyo zaidi ya bilioni mbili zimetengwa ili kuboresha sekta ya hiyo ikiwemo kununua mabasi ,kutengeneza na kuboresha vivutio mbalimbali vilipo jijini hapa.

Ameongeza kua kuboreshwa kwa sekta hiyo kutaongezea pato la Taifa pamoja na kutoa ajira kwa vijana waliosomea masuala ya utalii ambao kwa kiasi kikuba hawana ajira.

“ Kama jiji la Dar es Salaam tumeona ni wakati muafaka sasa wakuweka nguvu kwenye sekta ya utalii, ambayo kwa kiasi kikubwa kitakuwa ni kivutio kwa wageni kuja hapa ,maanye ni kwamba jiji litapata fedha nyingi kupitia mpango huo” amesema Meya Mwita.

Imetolewa leo Februali 24

Na Christina Mwagala Afisa habari Ofisi ya Meya wa jiji.

DK.KAMANI AWAONYA VIONGOZI VYAMA VYA USHIRIKA NCHINI

$
0
0
Na Said Nwishehe,Globu ya Jamii

MWENYEKITI wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika,Dk.Titus Kamani amesema Serikali kupitia tume hiyo ni awaelekeza viongozi wa Vyama vya Ushirika kutojihusisha kuuza mali za vyama hivyo pasipo kuzingatia sheria.

Hivyo amesema hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaobainika kuuza mali za vyama hivyo na kufafanua ili kudhibiti hali hiyo Ofisi za Mrajisi wa vyama vya ushirika imekuwa ikichukua hatua ikiwa pamoja na kuwaondoa viongozi wanaokiuka sheria.

Dk.Kamani amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati anaelezea udhibito wa mali za ushirika na mpango wa makusanyo na mauzo ya mazao makuu matano ya kimkakati kupitia mfumo wa ushirika.

Amesema vyama vya ushirika nchini vinaendeshwa kwa kuzingatia sheria ya vyama vya ushirika namba 6 ya mwaka 2013.Hivyo vyama vinapaswa kuzingatia sheria wanapotekeleza majukumu yao.Dk.Kamani amesema Serikali kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika inaelekeza viongozi wa vyama hivyo kuwa makini kuzingatia sheria.

Amefafanua vyama vina haki ya kumiliki mali na kuuza mali hizo pale itakapoona inafaa kwa kuzingatia shetia iliyopo.Pia mali zinazomilikiwa na vyama zinapaswa kuwa zimerasimishwa ili kuleta uhalali wa umiliki.

Dk.Kamani amesema pamoja na uwepo wa taratibu za kisheria zinazoelekeza namna ya ununuzi ,uuzaji na urasimishaji wa mali zake,baadhi ya viongozi wa vyama wamekuwa hawazingatii na matokeo yake wamekuwa wakiingia kwenye migogoro na wanaushirika.

Amesema kutokana na uzito wa jambo hill la umiliki wa mali, mwaka 2016 akiwahutubia wananchi wa Jiji la Mwanza, Rais Dk.John Magufuli alieleza jinsi viongozi wa vyama vya Ushirika wanavyohujumu vyama na kujinufaisha.

Hivyo alitoa maelekezo yakiwamo ya kurejeshwa kwa mali zote za vyama vya vikuu vya Ushirika vya NCU (1984)Ltd na Shirecu (1984)Ltd zilizouzwa kinyemela ambapo kutokana na agizo hill hadi sasa kati ya mali za NCU ,7 tayari zimerejeshwa na kati ya mali 2 za Shorecu zote zimerejeshwa .

"Kwa dhati ya moyo wangu,nawashukuru na kuwapongeza viongozi wetu wakuu wa nchi kwa imani kubwa waliyonayo juu ya Ushirika kwa kuutetea na kuhakikisha unatumika kumkomboa mwananchi wa kipato cha chini," amesema Dk.Kamani.Amesema pia Serikali inawakumbusha wakurugenzi wa halmashauri za majiji ,manispaa ,wilaya na miji kuhakikisha vinakodi maghala kwa ajili ya kuhifadhi pamba.

Hiyo ikiwa ni maandalizi kwa vyama vya Ushirika katika msimu wa mwaka 2018/2019 kama yalivyo maelekezo ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

IDARA YA UHAMIAJI WAFANYA USAFI KITUO CHA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM, SHULE YA MSINGI MATUMAINI

$
0
0

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

IDARA ya Uhamiaji nchini imefanya usafi katika Kituo cha watoto wenye mahitaji maalumu na Shule ya Msingi ya Matumaini ya Jeshi la Waokovu ‘Salvation Army’ iliyopo Kurasini jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam baada ya kumaliza kufanya usafi katika shule hiyo,kwa niaba ya Kamishina Jenerali wa Idara hiyo , Kamishina wa Utawala na Fedha, Edward Chogera amesema tangu kutangzwa Siku ya Jumamosi ni ya kufanya usafi Idara yai imekuwa ikifanya jitihada za kufanya usafi huo katika maeneo ambayo yana mchango kwa jamii.

Amesema shule ya Matumaini na kituo ni sehemu muhimu kutokana na watoto wanaosoma hapo kuwa na mahitaji maalumu.Kituo hicho hakiwezi kufanya chenyewe kutokana na mazingira ya watoto hao.Ameongeza mbali ya kufanya usafi katika kituo hicho wametoa pia msaada wenye thamani sh.500,000 ambao umetokana na wafanyakazi wa idara na wadau wenye ni njema kusaidia kundi maalumu ya kituo cha Jeshi la Uokovu .

Aidha amesema katika kipindi kijacho wamepanga kuwafikia watu wengine katika kufanya usafi ikiwa ni sehemu ya wafanyakazi kujua jamii inayowazunguka.Msaada waliotoa ni , Mchele, Maharage sukari , Mafuta ya kula , Sabuni za kuogea , Unga wa mahindi na mafuta ya kupakaa kwa wanafunzi wenye Ualbino .

Kwa upande wake Mkurugenzi wa kituo hicho,Timoth Sinana amesema licha kupata elimu,watoto wamekuwa wamekuwa wakiendelezwa kwenye mambo mbalimbali yakiwamo ufundi nguo na kuendeleza vipaji vyao.Amesema wanafunzi hao wamekuwa bora kimkoa katika suala la vipaji.
Kamishina wa Utawala na Fedha wa Idara ya Uhamiaji , Edward Chogera akizungumza wanafunzi na walimu pamoja na walezi wa kituo na shule ya Matumaini ya Jeshi la Waokovu Salvation Army mara baada ya kumaliza usafi katika kituo hicho jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Kituo cha Jeshi la Waokovu pamoja shule ya Matumaini, Timoth Sinana akizungumza kuhusiana na historia ya shule hiyo tangu ilipoanzishwa mwaka 1969 pamoja na mafanikio ya shule hiyo .
Msaada uliotolewa katika kituoa hicho ni , Mchele, Maharage sukari , Mafuta ya Kula , Sabuni za Kuogea , Unga wa Mahindi pamoja na mafuta ya kupakaa kwa wanafunzi Wenye Ualbino .  
Baadhi wa wafanyakazi katika shule ya msingi ya matumaini na kituo cha jeshi la Waokovu

SERIKALI YA AWAMU YA TANO HAIKO TAYARI KUONA MWANANCHI ANAONEWA, ANANYANYASWA'

$
0
0
Naibu waziri wa madini Stanlaus Nyongo Akizungumza na Wakazi Wa Kijiji Cha Nyakabale wakati wa ziara yake Mkoani Geita. 
Naibu waziri wa madini Stanlaus Nyongo akishiriki zoezi la kupanda mawe ya dhahabu. 
Naibu waziri wa madini Stanlaus Nyongo akizungumza na diwani wa kata ya Mgusu Patory Ruhusa. 
Naibu Waziri Akimsikiliza Pili Mwaluko Anaefanya Kazi Ya Uchenjuaji Madini kwenye mtaa wa Nyakabale. 
Wananchi wakiwa kwenye Mkutano wa pamoja na Naibu Waziri wa madini Stanlaus Nyongo.


Na,Joel Maduka,Geita. 


NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema Serikali ya Awamu ya Tano haiko tayari kuona mtu akilalamika ,kunyanyaswa au kunyimwa haki yake.

Ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyakabale, Kata ya Mgusu wilayani Geita wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani humo ya kuzungukia maeneo ya uchimbaji na kusikiliza kero za wananchi walizunguka kwenye baadhi ya maeneo ya mgodi wa Geita(GGM).

Hatua hiyo ya Naibu Waziri Nyongo imekuja baada ya kusikia malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuhusu mgodi wa GGM kushindwa kuwalipa fidia kwa muda mrefu licha ya kuwepo kwa maagizo mengi  yaliyotolewa na  baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakifika mkoani humo.

 Amesema mtu mwingine yuko tayari kuona Mtanzania mwenzake akikandamizwa ilimradi yeye aendelee kulinda maslahi yake binafsi, na kwamba miaka hiyo imeshapita na muda uliopo kwa sasa ni kufanya kazi za kuwatumikia wananchi ambao ni wanyonge.

“Tukikaa kwenye viyoyozi hatuambiwi ukweli na wamiliki wa migodi lakini tunapo fika katika eneo husika tunapata ukweli , unakuta mtu kazaliwa hapo, kakulia hapo amejenga ana watoto.Halafu mtu anakuondoa kwa madai kuwa upo kwenye leseni yake ,hiyo haingii akilini na kama unahitaji eneo langu njoo tukae tumalizane unipe changu mimi nisepe inakuwa nilipe nisepe,”amesema Nyongo.

Amewataka watu wa mgodi huo kuwalipa wananchi hao ama waondoke wawaachie wananchi hao eneo lao waendelee kuchimba na si kuwazuia ikiwa hawafanyi shughuli za uchimbaji kwa sasa.

Ameongeza  au wawaache waendelee kufanya shughuli za bila kubuguziwa, mgodi ulikuja kama neema za Mungu, hivyo isiwe mgodi huu kazi yake kuwanyanyasa wananchi.

Awali akitoa malalamiko kwa Naibu Waziri, Mwananchi wa Nyakabale kwa niaba ya wenzake Joseph Kihengu amemwambua Naibu Waziri kuwa wanailaumu serikali iliyopita.

Amefafanua inawezekana wakati wanabinafsisha mgodi huu na wao walbinafisishwa humo bila kujua.

“Mheshimiwa kipindi cha nyuma usingeweza kupata umati kama huu, umati huu umetokana na imani ya Serikali ya awamu ya tano waliyo nayo,hivyo iwaangalie kwa jicho la tatu ili watu Wanyakabele wajue hatima ya maeneo ambayo yapo ndani ya bikoni mgodi wa GGM”Amesema Joseph.

Katika hatua nyingine akina mama wa Nyakabale wakiwakilishwa na Godliva Mgini waliutupia lawama mgodi huo wa GGM kwa kuwafilisi kwa kukilaghai kikundi chao cha Baraka baada ya kuwaahidi kuwawezesha kuanzisha mradi ufungaji wa nguruwe 100.

Ambapo amedai waliambiwa wasombe mawe ili wajenge na kujikuta wakighalamia kiasi cha Sh.800,000, baadae wakatokomea kusiko julikana na kuwaacha maskini zaidi.

Nae Makamu wa Rais GGM, Saimon Shayo amesema “Tunatambua majirani hivyo niseme tu baadhi ya maneno yaliyoelezwa hapa mengine yanafahamika na  mengine ni mageni ndo tunayasikia na mangine tunahitaji kama mgodi kukaa na kuyapatia ufumbuzi”.

Aidha amesema kuna baadhi ya watu wa Nyakabale vigingi vyao vipo ndani ya mgodi na kimsingi jambo hilo lipo wazi pia kuna watu wana haki ya ardhi kisheria suala na kwamba suala hilo ni namna ya kukaa pamoja na kujadili kwasasa.

DC TEMEKE AHIMIZA WAENDESHA BODABODA KUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI

$
0
0
Na Emmanuel ,Globu ya Jamii

MKUU wa Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam, Felix Lyaniva amewataka madereva wa pikipiki na Bajaj kuwa makini na kuzingatia sheria za usalama barabarani ikiwemo kuvaa kofia ngumu na viatu wakati wanapoendesha vyombo vya moto.

Amesema lengo ni kuepuka ajali zinazosababishwa na madereva wazembe na kuwataka kufanya kazi kwa kuzingatia sheria zilizopo.

Lyaniva ameyasema hayo leo, wakati wa utambulishaji rasmi wa mfumo wa namba utakaowatambulisha madereva pikipiki na bajaji katika vituo vyao mbalimbali katika katika Kata ya Kibondemaji, Mbagala Jijini Dar es salaamu uliofadhiliwa na Diwani wa Kata hiyo Abdallah. 

Diwani huyo ameshirikiana na Kampuni ya Tanzania Motorcycle and Bajaji Association (TAMOBA) kwa ajili ya kuzisajili Pikipiki na Bajaji katika mfumo wa GPS utakaowawezesha kujua Pikipiki iliyoibiwa ipo eneo gani na kuweza kupatikana kwa haraka zaidi.

Akizungumza zaidi Lyaniva amewapiga marufuku mgambo wa wilaya hiyo kutokamata pikipiki na Bajaj kwani wengi wao wamekuwa wakikamata pikipiki hizo bila ya kuzingatia sheria.

Amesena kazi ya kukamata bodaboda itafanywa na askari wenye weledi na wenye kujua sheria za usalama barabarani.Lyaniva pia amewapongeza TAMOBA kwa kuwafikia madereva bodaboda na bajaj kwani walikuwa na wasiwasi wa kuibiwa vyombo vyao na kuporwa na majambazi.

Ameongeza Diwani huyo ameleta maendeleo makubwa na mazuri katika Kata hiyo na pia TAMOBA imeleta usalama mzuri kabisa wa kisasa kwa kuwa madereva hao watafanya kazi zao wakiwa hawana wasiwasi wa kuibiwa Pikipiki zao na mali zao wawapo katika majukumu yao hayo pamoja na abiria wao.

Naye Diwani wa Kata ya Kibondemaji, Abdallah Mtinika amewashukuru TAMOBA kwani wameweza kumpatia refrector 300 kwa ajili ya madereva pikipiki katika kata yake hiyo na kuahidi kushirikiana na Bodaboda hao wa Kata yake.

Kwa upande wake, Ofisa Utumishi wa TAMOBA Erasto Lahi amesema Kampuni hiyo ilianzishwa rasmi mwaka 2006 na lengo ni kuwalinda madereva wa pikipiki na Bajaj na vyombo vyao.

Hivyo ameahidi kila bodaboda atapata sare ili kutambulika pia kuingizwa katika mfumo wa utambulishi utakaowatambua na kueleza mfumo huo utasaidia kuokoa gharama za kulipia Bima kubwa kwa kuwa kipengele cha hofu ya usalama wa chombo chake kitafanyiwa kazi masaa 24 labda iwe kwa sababu zingine, mfumo huu unawahakikishia wamiliki kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi watakuwa salama.

“Kila atakayesajiliwa na Kampuni hii atasajiliwa na mfumo maalum wa GPS utakaowezesha kujua Pikipiki iliyoibiwa ipo wapi, inatumiwa na nani na kuwezesha kui-lock hapohapo ilipo."Mtu aliye katika mfumo huu atapata msaada wa kulindwa kwenye mfumo muda wote saa 24, hivyo mmiliki wa chombo muda wowote akihitaji taarifa za chombo kilipo, kilipopita na kinapoelekea atazipata," amesema.

Amesisitiza pia mfumo huu utaunganishwa na Jeshi la Polisi moja kwa moja ili kuharakisha zaidi huduma za kiusalama.

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Katibu wa Bodaboda Kata hiyo ya Kibondemaji Hassan Habibu amemshukuru Diwani huyo ambae ni mlezi wao na kueleza changamoto wanazokutana nazo ni pamoja na baadhi ya askari shirikishi maarufu kama mgambo kuwakamata nyakati za usiku bila utaratibu wa kisheria na kuwapiga kwa kutumia magongo bila ya kujua makosa yao.

Pia kutopata mikataba ya uhakika kutoka kwa wamiliki wa pikipiki hizo wanazoziendesha.


Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mhe Felix Lyaniva akizungumza na madereva wa pikipiki na Bajaj juu ya kuzingatia sheria za usalama Barabarani ikiwemo kuvaa kofia ngumu na viatu wakati wanapoendesha vyombo vya moto,leo jijini Dar es Salaam.(picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii)
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Kate Sylivia Magdalena Kamba akizungumza na akizungumza na madereva wa pikipiki na Bajaj juu ya kufanya kazi kwa kuzingatia sheria zilizopo, leo jijini Dar es Salaam.

Afisa Utumishi wa TAMOBA Bw. Erasto Lahi akizungumza na madereva wa pikipiki na Bajaj juu ya kuzisajili Pikipiki na Bajaj katika mfumo wa GPS utakaowawezesha kujua Pikipiki iliyoibiwa ipo eneo gani na kuweza kupatikana kwa haraka zaidi, le,jijini Dar es Salaam.
Semu ya madereva wa pikipiki na Bajaj piki na Bajaj wakiwa kwenye mkutano utambulishaji rasmi wa mfumo wa namba utakaowatambulisha madereva pikipiki na bajaji katika vituo vyao mbalimbali vya Kata ya Kibondemaji, Mbagala Jijini Dar es salaamu.

BENKI YA CRDB YADHAMINI MKUTANO MKUU WA GS1

$
0
0
 Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (wa pili kulia), akishiriki maandamano ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa Taasisi ya GS1 jijini Dar es Salaam. Maandamano yakielekea ukumbini. 
 Brass Band ikiongoza maandamano hayo. 
Mwenyekiti wa Bodi ya GS1 Tanzania, Gideon Mazara (wa kwanza kulia), akiwashiriki maandamano wakati wa kuingia ukumbini katika Mkutano Mkuu wa Mwakwa wa taasisi hiyo.
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya CRDB, Frederick Nshakanabo, Mkurugenzi wa Huduma Mbadala wa Benki ya CRDB, Philip Alfred na Msaidizi wa Mkurugezi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Kenny Kasigila.
 Maandamano kuelekea katika ukumbi wa mikutano. 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati), akipokea maandamano ya washiriki wa mkutano wa GS1. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akimkabidhi cheti cha shukrani Mkurugenzi Mtendaji wa Benki wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, kwa kutambua udhamini wa benki ya CRDB katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Global Standard (GS1), taasisi hiyo inajishughulisha na uwekaji wa Barcodes katika bidhaa za kitanzania ili ziweze kukubalika katika soko la kimataifa na pia kuwa mdau wa kufanikisha sekta ya viwanda nchi mkutano huo ulifanyika jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi ya GS1 Tanzania, Gideon Mazara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei,akizungumza katika Mkutano wa Mkuu wa Taasisi ya GS1 ambao ni watumiaji wa Simbomilia (Barcodes).
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto), akiwa na baadhi ya watendaji wa benki hiyo katika mkutano wa Mwaka wa taasisi ya GS1.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benmki ya CRDB, Tully Mwambapa akiteta jambo na Mkurugenzi wa Fedha wa Benki hiyo, Frederick Nshakanabo, katika mkutano huo. 
Mkutano ukiendelea.
Washiriki wa mkutano huo.

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI IBADA YA MISA TAKATIFU ILIYOFANYIKA KATIKA KANISA LA KIGANGO CHA MLIMANI WILAYANI CHATO

$
0
0
  Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akishiriki Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita Februari 25, 2018.
 Rais Mhe. Dkt John Pombe Magufuli akipiga makofi baada ya mahubiri kutoka kwa Padre Alex Bulandi wakati wa Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita Februari 25, 2018.
Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia waumini wa kanisa hilo mara baada ya kukaribishwa na Padre Alex Bulandi wakati wa Ibada ya misa Takatifu katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25, 2018.
  Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akimshukuru Padre Alex Bulandi baada ya kusalimia wakati wa Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.
 Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Chato Mhe.Medradi Kalemani akiwasalimia waumini wa kanisa wakati wa Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.
 Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiagana na Padre Alex Bulandi baada ya Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.
 Rais Mhe.Dkt John Pombe Magufuli akiagana na Waziri wa Nishati amabaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chato Mhe. Medrad Kalemani mara baada ya Ibada ya misa Takatifu iliyofanyika katika kanisa la kigango cha Mlimani (Parokia teule ya mlimani)lililopo Wilayani Chato Geita.Februari 25,2018.


PICHA NA IKULU.

WANANCHI 300 WA KITONGOJI CHA KINACHERE,HANANG WAANZA UJENZI WA KISIMA NA TENKI LA KUHIFADHIA MAJI YA MVUA

$
0
0
Na Jumbe Ismailly -HANANG    


WANANCHI  300 wa Kitongoji cha Kinachere,kata ya Sirop,tarafa ya Simbay,wilayani Hanang,Mkoani Manyara kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Hanang wameanza ujenzi wa kisima na tanki la kuhifadhia maji ya mvua ili waweze kuondokana na adha ya kufuata huduma hiyo  umbali wa zaidi ya mita 400 kutoka kwenye makazi yao.
Mwenyekiti mstaafu wa Kijiji hicho,Peter Qwendo alisema mradi huo utakapokamilika unatarajia kugharimu zaidi ya shilingi milioni 49 na kwamba kati ya kiasi hicho cha fedha nguvu za wananchi ni asilimia kumi ya gharama za mradi huo kwa kufanyakazi ya kukusanya mawe,mchanga,kokoto,kuchota maji na kumwagilia.
Aidha Qwendo ambaye pia ni mmoja wa watu waliokwenda nchini Kenya kupata mafunzo juu ya usimamizi wa shughuli hiyo,alisema wananchi hao wanaoishi katika kaya 107 wamekuwa wakiifuata huduma hiyo katika Kitongoji cha Ghata kilichopo umbali wa takribani kilomita 14 kwenda na kurudi.
Kwa upande wake Msimamizi wa Mpango wa afya wa Kijiji cha Nangwa,Apolei Wilbrod aliweka bayana kwamba wafadhili wa mradi huo ni Medical Missionary Of Mary Nangwa wanaoendesha huduma za kliniki ya mama na mtoto katika wilaya ya Hanang. 
Kwa mujibu wa Wilbrod mradi huo ulioanza tangu mwaka 2014 kwa miradi ya aina nne,kabla ya kuanza kwa mradi huo wa tano na madhumuni yake yalikuwa kuwasaidia wananchi waliopo kwenye maeneo hayo na kwamba unaotarajiwa kukamilika katika kipindi cha mwezi mmoja na utagharimu jumla ya shilingi milioni 49,700,000/=.
Hata hivyo Msimamizi huyo wa mradi alitumia pia wasaa huo kutoa wito kwa wadau wengine kujenga utamaduni wa kushirikiana wakati wote na jamii kwa kufurahia miradi husika ili iweze kuwasaidia wananchi.
Mbunge wa jimbo la Hanang,Dk.Mary Nagu aliyetembelea mradi huo kwenye ziara yake inayoendelea katika jimbo hilo alibainisha kuwa utaratibu mzuri waliojiwekea ni kwamba wananchi wanalazimika kuchangia asilimia kumi na Halmashauri asilimia kumi.
Hata hivyo mbunge huyo aliunga mkono wananchi hao kwa kuwaahidi kuwapatia malori matano ya mchanga na atawasiliana na Halmashauri ili kufahamu imechangia kitu gani katika mradi huo.
“Mradi umechelewa hela zimekuja zikakaa sasa basi tuonyeshe kwamba na sisi tunataka maji kwani maji ni uhai,hamtaki maji,mmenionyesha mnataka kwa sababu mmejitolea na kazi inaenda kwa kasi sana.”alisisitiza Mbunge huyo wa Jimbo la Hanang.
Ramadhani Hamisi ni fundi wa kujenga kisima na tenki la maji katika mradi huo anaweka bayana kwamba tenki hilo litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kujaza lita laki moja za maji na wanatarajia kukamilisha kujenga katika kipindi cha mwezi mmoja.
ananchi wa Kitongoji cha Kinachere,kata ya Sirop,Tarafa ya Simbay wakifanya kazi za mikono kuhakikisha mradi huo unakamilika katika kipindi cha mwezi mmoja na kuanza kunufaika na huduma ya maji safi na salama.
bunge wa Jimbo la Hanang,Dk.Mary Nagu akiungana na wananchi wa Kitongoji cha Kinachere kufanyakazi za kukusanya na kusomba mchanga wa kujengea kisima pamoja na tenki la kuhifadhia maji ya mvua na kuahidi kuchangia lori tano za mchanga.
Mbunge wa Jimbo la Hanang,Mkoani Manyara,Dk.Mary Nagu(wa kwanza kutoka kushoto) akikagua ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji ya mvua linalojengwa juu ya mawe.
mafundi wa kujenga kisima wakiendelea na kazi ya kusuka nondo za kisima kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wake katika kipindi cha mwezi mmoja.(Picha zote Na Jumbe Ismailly)
Ni Mbunge wa Jimbo la Hanang,Mkoani Manyara,Dk.Mary Nagu(wa kwanza kutoka kushoto) akipata maelezo mafupi ya mradi wa ujenzi wa kisima na tenki la kuhifadhia maji ya mvua kutoka kwa msimamizi wa mradi huo,Apolei Wilbrod.

Watoto 6 Wawashiwa Vifaa vya Usikivu (Cochlear Implant)

$
0
0
Watoto sita ambao wamewekewa vifaa vya usikivu Januari mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo wameanza kusikia kwa mara ya kwanza baada ya kuwashiwa vifaa hivyo.

Kuwashwa kwa vifaa hivyo kumeleta furaha kwa wazazi kwani wameshuhudia watoto wao wakisikia sauti kwa mara ya kwanza na hivyo kuwajengea matumaini ya watoto hao kuanza maisha mapya.

Zoezi la kuwawashia vifaa hivyo (Switch On) limefanyika leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na wataalaam kutoka Medel Austria ambao ndio wasambazaji wa vifaa hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari , Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio Dkt. Edwin Liyombo amesema watoto hao walifanyiwa upasuaji wa upandikizaji kifaa cha usikivu Januari mwaka huu ambapo zaidi ya asilimia 80 ya upasuaji huo ulifanywa na watalaam wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .

‘’Watoto hawa wataanza maisha mapya ya kusikia sauti mbalimbali katika mazingira yanayowazunguka baada ya kuunganisha vifaa hivi na kuviwasha’’. Amesema Dkt. Liyombo

Akifafanua amesema mbali na watoto hao sita lakini pia watoto wengine watano ambao walifanyiwa upasuaji huo mwaka jana na wengine sita ambao walifanyiwa upasuaji huo nchini India nao wamekuja kufuatiliwa maendeleo yao ili kubaini changamoto zinazowakabili na kupewa ushauri wa kitaalam. 

Akielezea ukubwa tatizo Dkt. Liyombo amesema takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) zinaonesha kuwa katika watoto 1,000 wanaozaliwa, inakadiriwa kuwa watoto watano wanazaliwa na tatizo kubwa la usikivu .

Pia amesema MNH ipo kwenye mchakato wa kuanzisha utaratibu wa kuwachunguza watoto wachanga ili kubaini mapema wenye matatizo yakutosikia.

Kwa upande wake Muwakilishi kutoka Medel Fayaz Jafar amesema upasuji huo umekua na mafanikio makubwa kwakua katika awamu hiyo kumekua na mabadiliko kwani asilimia kubwa ya upasuaji umefanywa na watalaam wa MNH na kwamba hatua hiyo ni ya kuridhisha.

Huduma ya Upandikizaji wa kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) ilizinduliwa Juni 7 , 2017 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu hivyo Tanzania imekuwa nchi ya pili kutoa huduma hiyo katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki baada ya Kenya. Aidha Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma hiyo kupitia Hospitali ya Umma ambayo ni Muhimbili yenye hadhi ya ubingwa wa hali ya juu.
Mtaalam wa Huduma ya Usikivu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mathayo Majogoro Alfred (katikati) akiunganisha kifaa cha usikivu cha nje na cha ndani ili mtoto Matilda Katobesi aweze kusikia kwa mara ya kwanza. Kulia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo akifuatilia na kushoto ni mama wa mtoto huyo, Angelina Cosmas.
Mtoto Matilda kwa mara ya kwanza leo tarehe 24, Januari, 2018 akianza kutamka baadhi ya maneno baada ya kufundishwa na mtaalamu wa sauti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo wa Muhimbili akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuwasha kwa mara ya kwanza vifaa vya usikivu kwa watoto waliofanyiwa upasuaji na kupandikizwa vifaa hivyo katika hospitaili hiyo. Kuanzia kushoto ni Mkuu wa Idara ya Macho, Dkt. Baruani, Katibu wa Umoja wa Watoto na Wazazi Wanaonufaika na Vifaa vya Usikivu nchini, Bupe Mwakalambile na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Wateja, Bwana Aminiel Aligaesha.
Wazazi wakisubiri kuashwa kwa mara ya kwanza kwa vifaa vya usikivu katika hospitali hiyo.
Mtaalamu wa Sauti, Fayaz Jaffer akionyesha kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) kwa waandishi wa habari ambacho kinapandikizwa kwa mtoto mwenye tatizo la kusikia. Kulia ni Paul Khalil kutoka Kampuni ya Medel. Kuanzia kushoto ni Dkt. Edwin Liyombo, Dkt. Baruani, Bi. Bupe Mwakalambile na Bwana Aminiel Aligaesha wakiwa kwenye mkutano huo leo.

Watoto 6 Wawashiwa Vifaa vya Usikivu (Cochlear Implant)

$
0
0
Watoto sita ambao wamewekewa vifaa vya usikivu Januari mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo wameanza kusikia kwa mara ya kwanza baada ya kuwashiwa vifaa hivyo.

Kuwashwa kwa vifaa hivyo kumeleta furaha kwa wazazi kwani wameshuhudia watoto wao wakisikia sauti kwa mara ya kwanza na hivyo kuwajengea matumaini ya watoto hao kuanza maisha mapya.

Zoezi la kuwawashia vifaa hivyo (Switch On) limefanyika leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na wataalaam kutoka Medel Austria ambao ndio wasambazaji wa vifaa hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari , Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio Dkt. Edwin Liyombo amesema watoto hao walifanyiwa upasuaji wa upandikizaji kifaa cha usikivu Januari mwaka huu ambapo zaidi ya asilimia 80 ya upasuaji huo ulifanywa na watalaam wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .

‘’Watoto hawa wataanza maisha mapya ya kusikia sauti mbalimbali katika mazingira yanayowazunguka baada ya kuunganisha vifaa hivi na kuviwasha’’. Amesema Dkt. Liyombo

Akifafanua amesema mbali na watoto hao sita lakini pia watoto wengine watano ambao walifanyiwa upasuaji huo mwaka jana na wengine sita ambao walifanyiwa upasuaji huo nchini India nao wamekuja kufuatiliwa maendeleo yao ili kubaini changamoto zinazowakabili na kupewa ushauri wa kitaalam. 

Akielezea ukubwa tatizo Dkt. Liyombo amesema takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) zinaonesha kuwa katika watoto 1,000 wanaozaliwa, inakadiriwa kuwa watoto watano wanazaliwa na tatizo kubwa la usikivu .

Pia amesema MNH ipo kwenye mchakato wa kuanzisha utaratibu wa kuwachunguza watoto wachanga ili kubaini mapema wenye matatizo yakutosikia.

Kwa upande wake Muwakilishi kutoka Medel Fayaz Jafar amesema upasuji huo umekua na mafanikio makubwa kwakua katika awamu hiyo kumekua na mabadiliko kwani asilimia kubwa ya upasuaji umefanywa na watalaam wa MNH na kwamba hatua hiyo ni ya kuridhisha.

Huduma ya Upandikizaji wa kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) ilizinduliwa Juni 7 , 2017 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu hivyo Tanzania imekuwa nchi ya pili kutoa huduma hiyo katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki baada ya Kenya. Aidha Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma hiyo kupitia Hospitali ya Umma ambayo ni Muhimbili yenye hadhi ya ubingwa wa hali ya juu.
Mtaalam wa Huduma ya Usikivu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mathayo Majogoro Alfred (katikati) akiunganisha kifaa cha usikivu cha nje na cha ndani ili mtoto Matilda Katobesi aweze kusikia kwa mara ya kwanza. Kulia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo akifuatilia na kushoto ni mama wa mtoto huyo, Angelina Cosmas.
Mtoto Matilda kwa mara ya kwanza leo tarehe 24, Januari, 2018 akianza kutamka baadhi ya maneno baada ya kufundishwa na mtaalamu wa sauti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo wa Muhimbili akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuwasha kwa mara ya kwanza vifaa vya usikivu kwa watoto waliofanyiwa upasuaji na kupandikizwa vifaa hivyo katika hospitaili hiyo. Kuanzia kushoto ni Mkuu wa Idara ya Macho, Dkt. Baruani, Katibu wa Umoja wa Watoto na Wazazi Wanaonufaika na Vifaa vya Usikivu nchini, Bupe Mwakalambile na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Wateja, Bwana Aminiel Aligaesha.
Wazazi wakisubiri kuashwa kwa mara ya kwanza kwa vifaa vya usikivu katika hospitali hiyo.
Mtaalamu wa Sauti, Fayaz Jaffer akionyesha kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) kwa waandishi wa habari ambacho kinapandikizwa kwa mtoto mwenye tatizo la kusikia. Kulia ni Paul Khalil kutoka Kampuni ya Medel. Kuanzia kushoto ni Dkt. Edwin Liyombo, Dkt. Baruani, Bi. Bupe Mwakalambile na Bwana Aminiel Aligaesha wakiwa kwenye mkutano huo leo.

Watoto 6 Wawashiwa Vifaa vya Usikivu (Cochlear Implant)

$
0
0
Watoto sita ambao wamewekewa vifaa vya usikivu Januari mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo wameanza kusikia kwa mara ya kwanza baada ya kuwashiwa vifaa hivyo.

Kuwashwa kwa vifaa hivyo kumeleta furaha kwa wazazi kwani wameshuhudia watoto wao wakisikia sauti kwa mara ya kwanza na hivyo kuwajengea matumaini ya watoto hao kuanza maisha mapya.

Zoezi la kuwawashia vifaa hivyo (Switch On) limefanyika leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kushirikiana na wataalaam kutoka Medel Austria ambao ndio wasambazaji wa vifaa hivyo.

Akizungumza na waandishi wa habari , Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio Dkt. Edwin Liyombo amesema watoto hao walifanyiwa upasuaji wa upandikizaji kifaa cha usikivu Januari mwaka huu ambapo zaidi ya asilimia 80 ya upasuaji huo ulifanywa na watalaam wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili .

‘’Watoto hawa wataanza maisha mapya ya kusikia sauti mbalimbali katika mazingira yanayowazunguka baada ya kuunganisha vifaa hivi na kuviwasha’’. Amesema Dkt. Liyombo

Akifafanua amesema mbali na watoto hao sita lakini pia watoto wengine watano ambao walifanyiwa upasuaji huo mwaka jana na wengine sita ambao walifanyiwa upasuaji huo nchini India nao wamekuja kufuatiliwa maendeleo yao ili kubaini changamoto zinazowakabili na kupewa ushauri wa kitaalam. 

Akielezea ukubwa tatizo Dkt. Liyombo amesema takwimu za Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO) zinaonesha kuwa katika watoto 1,000 wanaozaliwa, inakadiriwa kuwa watoto watano wanazaliwa na tatizo kubwa la usikivu .

Pia amesema MNH ipo kwenye mchakato wa kuanzisha utaratibu wa kuwachunguza watoto wachanga ili kubaini mapema wenye matatizo yakutosikia.

Kwa upande wake Muwakilishi kutoka Medel Fayaz Jafar amesema upasuji huo umekua na mafanikio makubwa kwakua katika awamu hiyo kumekua na mabadiliko kwani asilimia kubwa ya upasuaji umefanywa na watalaam wa MNH na kwamba hatua hiyo ni ya kuridhisha.

Huduma ya Upandikizaji wa kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) ilizinduliwa Juni 7 , 2017 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia , Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu hivyo Tanzania imekuwa nchi ya pili kutoa huduma hiyo katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki baada ya Kenya. Aidha Tanzania imekuwa nchi ya kwanza kutoa huduma hiyo kupitia Hospitali ya Umma ambayo ni Muhimbili yenye hadhi ya ubingwa wa hali ya juu.
Mtaalam wa Huduma ya Usikivu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mathayo Majogoro Alfred (katikati) akiunganisha kifaa cha usikivu cha nje na cha ndani ili mtoto Matilda Katobesi aweze kusikia kwa mara ya kwanza. Kulia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo akifuatilia na kushoto ni mama wa mtoto huyo, Angelina Cosmas.
Mtoto Matilda kwa mara ya kwanza leo tarehe 24, Januari, 2018 akianza kutamka baadhi ya maneno baada ya kufundishwa na mtaalamu wa sauti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Pua, Koo na Masikio, Dkt. Edwin Liyombo wa Muhimbili akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuwasha kwa mara ya kwanza vifaa vya usikivu kwa watoto waliofanyiwa upasuaji na kupandikizwa vifaa hivyo katika hospitaili hiyo. Kuanzia kushoto ni Mkuu wa Idara ya Macho, Dkt. Baruani, Katibu wa Umoja wa Watoto na Wazazi Wanaonufaika na Vifaa vya Usikivu nchini, Bupe Mwakalambile na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Huduma kwa Wateja, Bwana Aminiel Aligaesha.
Wazazi wakisubiri kuashwa kwa mara ya kwanza kwa vifaa vya usikivu katika hospitali hiyo.
Mtaalamu wa Sauti, Fayaz Jaffer akionyesha kifaa cha usikivu (Cochlear Implant) kwa waandishi wa habari ambacho kinapandikizwa kwa mtoto mwenye tatizo la kusikia. Kulia ni Paul Khalil kutoka Kampuni ya Medel. Kuanzia kushoto ni Dkt. Edwin Liyombo, Dkt. Baruani, Bi. Bupe Mwakalambile na Bwana Aminiel Aligaesha wakiwa kwenye mkutano huo leo.

serikali yatakiwa kuzitambua kazi za wanawake katika mipango ya Taifa

$
0
0

NA VICENT MACHA - DAR ES SALAAM.

SERIKALI imetakiwa kuzitambua kazi za kutoa huduma zinazotekelezwa na wanawake na kuziingiza katika Mipango ya Taifa kwani zinaweza kusaidia kuongeza pato la Taifa.

Hayo yamesemwa mapema leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia (TGNP) Bi. Lilian Liundi alipokuwa akitoa Mhuktasari wa Kongamano la Wanawake na Uongozi.

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika siku ya jumanne ya tarehe 27 Mlimani City jijini Dar es salaam, likihudhuriwa na wanawake mbalimbali walio katika nafasi za uongozi na waliostaafu.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa kuna haja ya serikali kuzitambua shughuli mbalimbali zinazotolewa na wanawake kama huduma kwa lengo la kujipatia kipato kwani uchunguzi umebaini kuwa wanawake hutumia muda wa masaa 10 mpaka 15 kwa siku kwa shughuli hizo hivyo wanakosa muda wa kufanya shughuli za kujipatia kipato.

Aidha Mkurugenzi huyo aliendelea kusema kuwa lengo kuu la Kongamano hilo ni wanawake kwa pamoja kuweza kujadili namna gani wataweza kuongeza nafasi za uongozi na maamuzi kwani bado hawajaweza kufikia lengo ambalo ni 50 kwa 50.

Lakini pia kuweza kusherekea, kupongezana na kuajadili changamoto mbalimbali anazokutana nazo mwanamke katika Nyanja ya elimu, afya na umiliki wa ardhi swala ambalo bado ni changamoto kubwa kwa wanawake wengi hivi sasa. Bi. Lilian aliendelea kusema kuwa kutakuwa na kuenzi na kukumbuka mchango uliotolewa na wanawake ambao walikuwa katika ngazi za uongozi maamuzi kuanzia ngazi ya jamii mpaka taifa.

Mgeni Rasmi katika Kongamano hilo anatarajiwa kuwa Waziri msataafu Mama Marry Nagu, lakini pia kutakuwa na wadau zaidi ya 250 wanawake kwa wanaume viongozi wa sasa na wastaafu katika kuhakikisha kongamano hilo linaleta tija kwa jamii yetu.
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi akitoa ufafanuzi wa jambo fulani mapema leo jijini Dar es salaam katika mkutano na waandishi kuhusu kongamano la Wanawake Uongozi. 
Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Lilian Liundi wa katikati akiwa na jopo la wafanyakazi wa shirika hilo pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki katika kuandaa Kongamano la Wanawake na Uongozi. 
Waandishi wa habari wakiendelea na kazi yao.
                        

SOLOMONI MUKUBWA,CHRISTINA SHUSHO WATHIBITISHA KUNOGESHA TAMASHA LA PASAKA 2018 KANDA YA ZIWA

$
0
0

Waimbaji wa nyimbo za Kiroho (Injili), Afrika Mashariki na Kati Christina Shusho na Solomon Mukubwa wanatarajiwa kuwaburudisha kiroho vilivyo,watakapokuwa wakitumbuiza katika jukwaa la Tamasha la Pasaka 2018,ambalo safari hii linafanyika Kanda ya Ziwa,mkoa wa Mwanza na Simiyu. 

Akiwatangazia Mashabiki wa Tamasha la Pasaka jijini Dar Es Salaam hapo jana,Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw, Alex Msama alisema kuwa mbali ya uzinduzi wa Mwimbaji Nyota wa nyimbo za Injili,Rose Muhando pia waimbaji hao wamethibitisha kuzindua na kuzitangaza nyimbo zao mpya.

Msama amesema kuwa Waimbaji hao wana  nyimbo nzuri na zenye kumuimbia,kumsifu na kumtukuza Mungu,nyimbo ambazo anaamini zitavuta hisia za wengi watakapozikia.

"Solomoni Mukubwa na Shusho wote hawa hawajasikika muda mrefu katika majukwaa,hivyo wakazi wa Kanda ya Ziwa wakae mkao wa kuzifurahisha roho na wajitokeze kwa wingi katika maonesho hayo yatakayofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Aprili 1 na Uwanja wa Halmashauri mjini Bariadi mkoani Simiyu Aprili 2 mwaka huu",alisema Msama.
Mkurugenzi wa Msama Promotions Ltd,Alex Msama akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na maandalizi ya tamasha la pasaka linalotarajiwa kurindima Kanda ya Ziwa.

KATIBU CHADEMA KATA YA MAILMOJA ATIMKIA CCM

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani

WIMBI la baadhi ya viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) limezidi kuwakumba hapa nchini baada ya katibu wa CHADEMA kata ya MailMoja Mjini Kibaha Mohamed Hashim kuhamia CCM.

Pamoja na hayo wanachama wengine wa CHADEMA na ACT Wazalendo wapatao tisa nao walirejea CCM na kukabidhi kadi zao kwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Pwani Ramadhan Maneno.

Hayo yalijiri Kongowe wilayani Kibaha wakati Maneno alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa wilayani humo.Maneno alisema, kwa sasa wapinzani wameshatambua vyama hivyo kuwa hakuna jipya hivyo wameamua kumuunga mkono Rais Dk John Magufuli ambaye anatatua kero na changamoto zilizokuwa zinawasumbua wananchi.

“Hichi ndicho kielelezo cha kumkubali kiongozi wetu wao wenyewe wameona kinachofanyika na kasi na mabadiliko ya kimaendeleo iliyopo,” alisema Maneno.Alisema kuwa wanaCCM wanapaswa kukiimarisha chama kwa kuhakikisha wanalipa ada zao kwa wakati kwani ili mwanachama awe hai lazima alipe ada zake .

“Tunawanachama 38,000 kwenye Mji wa Kibaha lakini waliolipa ada ni wanachama 8,000 pekee ,,:;si sawa lazima wanachama watakeleze jukumu lao hilo ili kujenga chama,” alisisitiza Maneno.Alielezea kwa sasa viongozi waendelee kuhamasisha wananchi kujiunga CCM kwani mtaji wa chama ni kuongeza wanachama wapya.

Maneno alibainisha mkoa umejipanga kushika dola kwenye uchaguzi wa serikali za Vijiji na Mitaa mwaka 2019 ikiwa kama sehemu ya kujipima kabla ya mwaka 2020 kwenye uchaguzi mkuu.Aidha aliwataka viongozi kuanzisha madawati ya kusikiliza malalamiko ya wanachama na wananchi ili wapate mahali pa kutoa madukuduku yao na kueleza changamoto mbalimbali zikiwemo zile za kimaendeleo.

Maneno alitoa rai kwa viongozi wake kwenye wilaya za mkoa huo kuisimamia serikali ili iweze kutekeleza ilani ya chama kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi.Kwa mujibu wake, wasimamizi wakuu wa ilani ni viongozi ambao wanapaswa kushirikiana na watendaji wa serikali katika kukabili na kutatua changamoto za wananchi.

“Kwa sasa ilani inayotekelezwa ni ya CCM hivyo sisi ndiyo wasimamizi wakuu tunapaswa kuisimamia na kuhakikisha ahadi zote tulizo ahidi wananchi zinatekelezwa ili kuwaletea maendeleo wananchi,” alisema Maneno.Maneno alisema kuna miradi mingi ambayo endapo haitasimamiwa au kufuatiliwa na viongozi wa chama tawala inaweza isikamilike kwa wakati endapo hakutakuwa na ushirikiano na viongozi wa chama.

Nae Hashim alisema ameamua kurudi CCM baada ya kuona kuwa kwenye chama hicho hakuna demokrasia ya kweli na kujaa malumbano ambayo hayana tija kwa wananchi.Kwa upande wake ,mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Maulid Bundala alieleza ,viongozi wa ngazi za juu tayari wameshafanya kazi kubwa ya kukijenga chama pamoja na serikali na wao wajibu wao ni kuendeleza maboresho.

Bundala alisema mbali ya kuhimiza maendeleo kwa kushirikiana na chama wanaendelea kushirikiana vema na Halmasahuri ambao ndiyo watekelezaji wa miradi ya maendeleo.Akiwa wilayani hapo ,Maneno alitembelea soko la vyakula na bidhaa mbalimbali la Maili Moja maarufu kama Loliondo pamoja na ujenzi wa stendi mpya ya mabasi ambayo iko kwenye hatua za mwisho.
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani, Ramadhani Maneno akizungumza jambo na baadhi ya  viongozi ,wa CCM Mjini Kibaha na halmashauri ya mjini hapo wakati wa ziara yake mjini humo .
 Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani, Ramadhani Maneno akisalimiana na  baadhi ya  viongozi ,wa CCM Kata ya Kongowe na Mjini Kibaha kabla ya mkutano nao ,kuzungumzia masuala mbalimbali ya Chama wakati wa ziara yake mjini humo .(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Pwani, Ramadhani Maneno akipokea kadi kutoka kwa katibu wa CHADEMA kata ya MailMoja Mohamed Hashim aliehamia CCM wakati mwenyekiti huyo alipokuwa akizungumza na baadhi ya wanachama na viongozi ,katika mkutano huo wanachama wengine Tisa kutoka upinzani walijiunga na Chama hicho.(picha na Mwamvua Mwinyi)

STENDI YA KISASA MAILMOJA - KIBAHA KUKAMILIKA MACHI

$
0
0
Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

STENDI ya mabasi ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani inatarajiwa kukamilika Machi baada ya mkandarasi wa kuongezewa muda kutokana na mradi huo kukumbwa na changamoto kadhaa.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Renatus Makoye msimamizi wa ujenzi wa stendi hiyo kutoka kampuni ya Mhandisi alipokuwa akielezea maendeleo ya ujenzi huo kwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoani Pwani Ramadhani Maneno ambaye alikwendakukagua mradi huo .Alisema awali mradi huo ulitarajiwa kukamilika Novemba mwaka jana.

Makoye alisema kuwa stendi hiyo ambayo imegharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.9 itakuwa ikihudumia wasafiri wa mabasi ya kwenda mikoani pamoja na mabasi madogo ya Daladala yanayofanya safari zake ndani ya mkoa imefikia hatua za mwisho.

"Awamu ya kwanza ilikuwa ni ujenzi wa fensi, choo na kituo cha polisi, awamu nyingine ni ujenzi wa sehemu ya mabasi kupaki na sehemu za magari binafsi," alisema Makoye.Alieleza ujenzi huo umezingatia viwango ambapo sehemu ya mabasi makubwa ujenzi wake ni kiwango cha zege huku ile ya mabasi madogo imejengwa kiwango cha lami.

Mwenyekiti wa CCM mkoani humo, Ramadhan Maneno aliishukuru serikali kwa kuwa na taasisi na benki ya dunia ambao ndiyo waliofadhili wa ujenzi huo.Alielezea kwamba thamani ya fedha zimetumika kwa usahihi.

Maneno alisema ujenzi wa mradi wa stendi utainua uchumi wa mkoa wa Pwani na kuwataka watumiaji wa stendi hiyo kuitunza ili iweze kudumu na kutoa huduma nzuri.Kwa upande wake mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha Jeniffer Omolo alisema baadhi ya majengo yatajengwa ikiwa ni pamoja utawala litajengwa na vibanda vya kukatia tiketi sehemu za abiria kusubiria mabasi, migahawa na majengo ya huduma mbalimbali za kijamii.

Omolo alisema baadhi ya majengo hayajajengwa kutokana na fedha kutokuwa ya kutosha kuweka vitu vyote hivyo .Alisema lengo lao ni kuwa na stendi ya kisasa ambayo ina huduma zote.
 Hali halisi ya ujenzi unavyoendelea katika stendi Mpya ya kisasa inayojengwa mjini Kibaha Mkoani Pwani.(picha na Mwamvua Mwinyi)
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoani Pwani ,Ramadhani Maneno (wa tatu kutoka kulia) akimsikiliza mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Jennifer Omolo (wa pili kutoka kulia)wakati alipokuwa akitoa taarifa ya miradi ya soko la Loliondo na ujenzi wa stendi Mpya ya kisasa katika ziara ya siku moja aliyoifanya mwenyekiti huyo mjini humo.

DIAMOND SOMA NILOCHOANDIKA KUHUSU WEWE NA ZARI, NAMUOMBA MUNGU ASIKURUDISHE ULIKOANZIA

$
0
0
Na said Mwishehe,Globu ya Jamii

NI ngumu kuzungumzia mahusoano ya kimapenzi ya watu wengine lakini kuna wakati unaamua kufumba macho na kuziba masikio useme japo kidogo.

Nikiri mahusiano ya kimapenzi wakati mwingine hukumbwa nachangmoto nyingi.Mungu nisaidie nifikishe ujumbe kwa ufasaha.Hata hivyo siri ya mtungi aijue kata.Wengine huwa ni wa kupata taarifa...bwana umesikia jamaa ameacha mpenzi au mke.

Wakati mwingine unaweza kuambiwa ndugu yangu yule mshikaji wako kaachwa na mkewe au mpenzi wake.Ni mambo ya kawaida kusikia waliokuwa na mapenzi moto na pengine kuwa ya mfano wa kuigwa yamefika tamati.Hata hivyo swali la msingi huwa watu wanataka kujua kwanini waliokuwa wanapendana wameachana.Hivyo sababu ndio huibua mjadala kwenye jamii.

Tena usiombe walioachana wakiwa ni watu maarufu na wenye kukubalika na kupendwa zaidi.Nikiri kwenye maisha yangu ya uandishi yaliyoanza rasmi mwaka 2001,sikuwahi kabisa kuandika chambuzi au maoni inayozungumzia wapenzi kuachana.

Sikuwa na sababu ya kufanya hivyo kwani ni maisha binafsi ya watu wawili walioamua kupenda na kukaa pamoja na hatimaye wakaamua kuachana.Kwa mazingira ya aina hiyo unatoa maoni au kuandika uchambuzi il iweje?Hivyo huwa napotezea na ndio maana hata hili la juzi la Mkuu wa Wilaya fulani(jina kapuni) kutumia mitandao ya kijamii kumpongeza mumewe kuongeza mke wa pili kichwani kwangu halikunisumbua maana halina uhusiano na maendeleo ya Watanzania.

Ingawa aliyesema ni kiongozi wa umma na matendo yake wakati mwingine yana nafasi ya kuigwa na wengine hasa yale matendo mema.Nikiri kabla kuvunja mwiko huu wa kutoandika habari za uhusiano wa kimapenzi,niliamua kufanya mawasiliano ya kutosha na halmashauri ya ubungo wangu mwisho wa siku moyo,mwili na akili vikakubaliana si dhambi kuelezea walau kidogo.

Naomba niombe radhi kwa nitakaowakwaza kwa namna yoyote ile kwani kwenye maisha yetu haya lile ambalo wewe unaliona haliko sawa kwa mwingine anaona zuri na kulipa maksi za juu.Ndio maisha ya binadamu yalivyo.Hivyo niombe msamaha kwa yule ambaye kwa namna moja au nyingine nitamkwaza.

Naomba nianze kwa kuelezea masikitiko yangu makubwa baada ya kusikia taarifa za Nasibu Abdull maarufu Diamond kuachana na mpenzi wake ambaye ni mama wa watoto wake wawili Zarinah Hassan a.k.a The Boss Lady.Sitaki kusema kama Diamond kaachwa au kaacha lakini kwa lugha nyepesi ni kwamba wawili hao penzi limefika mwisho.

Yaani kama nitatumia moja ya wimbo za Diamond niseme penzi la Diamond na Zar sasa Zilipendwa.Inasikitisha sana lakini ndio hivyo.Kwanini wameachana? Ni swali gumu kulijibu ila fahamu tu hakuna mapenzi tena kwa sasa kati yao.Taarifa za wawili hao kuamua kuachana zilianza kusambaa kwenye mitandao ya kijamii kama utani.Si unajua tena mambo ya wasanii wetu kuna wakati unaweza kuumiza kichwa kumbe wenzio wanatafuta kiki.

Hata hivyo nikaanza kumtafakari Diamond,alikotoka,alipo na hatua ambayo amefikia kwenye muziki huo. Nikaanza kujiuliza ni kweli taarifa za kuachwa ni kitafuta kiki?Kichwa changu hakikukubali kirahisi.Nikasema ngoja nikae kimya maana unaweza kuzungumzia jambo hewa na kibaya zaidi huwa sina utaratibu wa kuzungumzia mapenzi ya watu.

Nikawa nasubiri maana nikiri tu binfasi ni miongoni kwa mashabiki wa muziki wa Diamond ,imefikia hatua kuishi na bango lenye nembo ya WCB kwangu ni jambo la kawaida.Basi bwana kama unavyojua msanii unayempenda lazima utafuatilia na maisha yake. Na kazi yangu hii ya kuandika andika imenifanya nifuatilie maisha ya wasanii mbalimbali maana wanafanya kazi nzuri na naifurahia.

Maana maisha tunayoishi nayo yametawaliwa na changamoto nyingi za kimaisha,hivyo nyimbo za wasanii zimekuwa sehemu ya tulizo la moyo.Juzi sasa nikapata jibu, kweli Zari na Diamond wameachana.Ujue kwanini ?Nimemsikia Zari kwa masikio yangu akielezea kufika mwisho kwa penzi lao.Ameeleza sababu kadhaa na zote kwangu lawama nazielekeza kwa Diamond. Amevuruga penzi kwa mikono yake.

Wakati naandika nikaanza kukumbuka mashairi ya wimbo wa Nandy unaosema Kivuruge.Kuna sehemu anaomba "Umekuwa kivuruge unavuruga sana". Yale maneno ya wimbo huo yafanye sasa ndio anaimba Zari.Acha niendelee Diamond amesahau alikotoka,maisha ambayo amepitia kwenye masuala ya mahusiano.Kabla ya kukutana na Zari Diamond amepita kwenye msururu wa warembo.

Ama kweli mwenye asili haachi asili.Ukijumlisha umaarufu ,fedha ,kipaji na mafaniko akajisahau ndugu yangu Boy from Tandale kwani ameanza kurudi kule kule.Leo Zari ameshindwa kuvumilia.Zari anasema wakati anahojiwa na BBC kuwa amevumilia ameshindwa.Diamond amekuwa akifanya mambo ya kumvunjia heshima.Ile stori ya kuzaa na binti mwenye uzuri wake Hamisa Mobeto ilimuumiza sana The Boss Lady.Ndivyo anavyosema.

Akajipa moyo kuwa huenda Diamond atajifunza na kuacha kumbe wapi.Zari anasema wakati akiendelea kufikiria aina ya maisha ya mzazi mwenzake kwenye mambo ya mahusiano ghafla anaona zile picha akiwa amekumbatiana na Wema Sepetu.

Usiniulize kwanini?Kwani hujui kama Diamond kabla ya kuwa na Zari ameishi sana na Wema.Basi tena Diamond akiwa na Wema hapa juzi kati ameeleza mengi na kuwaambia mashabiki wake yeye na Wema hawana matatizo tena na ni marafiki wakubwa.Kumbe Zari anamsikia .Unajua kilichoafuata? Moyo wa Zari ukasema sasa basi.Cha kwanza akaamua kudhibiti mawasiliano ya Diamond yasimfikie.Kwa kifupi amekata mawasiliano.Hataki tena kuwasiliana na Diamond.Pata picha nini kinaendelea.Itoshe kusema nimemsikia Zari akizungumzia kumuacha Diamond na kwamba sasa atajikita kwenye shughuli zake binafsi.

Kauli hiyo kimsingi ndio imenisukuma kivunja mwiko wa kuandika habari za mahusiano ya mapenzi ya watu na baada ya leo sitaandika tena.Iko hivi nayaangalia maisha ya Diamond baada ya kuachana na Zari.Nakumbuka historia yake Diamond kwenye mambo ya mapenzi anapokuwa na binti wa Kitanzania haikuwa vizuri.

Diamond aliyekuwa na Wema sawa alikuwa tayari maarufu lakini baada ya kuingia kwenye mikono ya Zari ,Diamond akaanza kuonekana msanii anayejua nini anachokifanya kwenye muziki.Akapiga hatua kiasi cha kumshangaza kila mmoja wetu.Diamond wakati akiwa na Wema alitambata na nyimbo kadhaa kikiwamo kibao chake cha Mbagala ambacho ndicho kilimtambulisha rasmi.

Alipokuwa na Zari ,Diamond akaanza kuwa msanii mkubwa na wa kimataifa.Dunia leo hii inamjua Diamond.Ametambulika kila mahali kutokana na kipaji chake kwenye muziki wa kizazi kipya.Kama ukitaka ushahidi wa uwezo wa Diamond usiniulize mimi Said Mwishehe,nenda kawaulize akina DJ Khalifa,Chris Brown ,Neyo na hata wale akina Morgan Heritage waliomba naye wimbo wa Halleluya.

Huku wengine tukianza kubishana kuhusu uwezo wa Diamond tunapoteza muda maana wenye muziki wao wanamjua.Ila ndio hivyo tena amefanikiwa kupenya kwenye muziki lakini ameshindwa kupenya kulinda penzi lake kwa Zari.Unaweza kujiuliza Diamond nini kimemtokea,ni utoto? Hapa kwani ni mtu mzima.

Unaweza kujiuliza ni ulimbukeni wa mapenzi?Hapana kwani Diamond si limbukeni.Unaweza kujiuliza amepitiwa na shetani?Hapana kwani nani amemuona Shetani.Unaweza kujiuliza ameharibu penzi kwa sababu ya uzuri wa Wema na Hamisa?Akili yangu inakataa kabisa maana kwa Zari anakila kitu.Ni mrembo,anavutia, ana akili na kubwa zaidi ana sifa zote za kuwa mke.

Diamond amekosea sana kumvunjia heshima Zari kwa kurudi kwenye kupiga picha za kukumbatiana na watu alipokuwa ana mahusiano nao huko nyuma.Tangu Zari awe na Diamond aamekuwa makini sana kuilinda nyumba yake.Amejitahidi kutunza heshima ya Diamond, amejitahidi kuwathibitisha Watanzania yeye ni mwanamke sahihi kwa Diamond.

Kwa bahati mbaya aliyepewa heshima zote hakuona.Sijui ni upofu? Hapana. Diamond ni msanii anayejua nini anachokifanya na kwenye hili huenda anajua anachokifanya.Lakini ukweli amekosea sana tena sana,Diamond kuachana na Zari umefanya kosa kubwa.Kibaya zaidi ni kwa sababu za kitoto kabisa.Ulishindwa nini kufanya mambo yako kwa siri.Kuna wanaume wangapi wana nyumba ndogo na bado wanaheshimu nyumba zao.

Sawa Diamond moja ya nyimbo yake amesema "Sikomi" tena ukaongeza licha ya mateso haya.Brother umemkosea sana kuachana na Zari.Leo huenda hata Tiffah na Nillan waliokuwa wamezoea kukuona kila wanapofumbua macho sasa wanaanza kuona tofauti.Ndio maana baba yupo kwake na mama yupo kwake.

Angalia unavyoingiza watoto kwenye shida.Kisa picha za kukumbatiana na aliyekuwa mpenzi wako.Ulishindwa kutafakari?Mbona kwenye nyimbo unatafakari kabla na ndio maana ukatuteka wengi na kuwa upande wako.Umeshindwaje kutafakari unayoyafanya kwa Zari.

Diamond unakumbuka kuna wakati Zari alipost picha kwenye mitandao wake wa kijamii akiwa na mwanaume mwenye bwawa la kuogolea akiwa Afrika Kusini.Nakumbuka ulikuja juu na ukaweka post ukisema ndio maana unakulaga tu.Sijui ulikuwa na maana gani.Zari akaitolea ufafanuzi ile picha kuwa alikuwa ni ndugu yake na picha hiyo ilipigwa na mke wa huyo ndugu.

Ukasemehe na maisha yakaendelea.Sasa pata picha wewe tukio moja tu lilikutesa,je wewe unayoyafanya kwake unamtesa kwa kiasi gani.Naomba unisamehe Diamond,naomba mashabiki wako nao wanisamehe huenda nachokiona mimi ni kibaya kwa wengine kikawa poa na wanakupongeza.

Hata hivyo naangalia maisha yako kimuziki.Nikiri naanza kupata wasiwasi na sikuombei mabaya lakini kama naanza kuona unarudi ulikotokea.Naomba Mungu nachowaza kisiwe maana umeliwakilisha vema taifa kwenye tasnia ya muziki wa kizazi kipya.Tunahitaji kuona ukiendelea kubaki keleleni kwenye muziki. Chondechonde angalia namna ya kuomba radhi kwa Zari.

Na kuomba radhi si kosa au dhambi bali ni njia ya kujisahihisha na kujiimarisha.Kuna hatari ya mipango yako mingi kushindwa kuendelea kama ulivyoipanga.Najua unao mameneja wenye uwezo mkubwa wa kukusimamia lakini nyumba ikiyumba na kazi nayo inayumba.Kumbuka ile kauli kwenye mafanikio ya mwanaume nyuma kuna mwanamke.Hivyo kwenye mafanikio yako nyuma yako yupo Zari.

Tulizoea kila wiki tunasikia nyimbo mpya kutoka kwako lakini sasa wiki imekata.Unajua kwanini?Nyumba haiko sawa.Utajipa moyo kuwa yatapita na wanawake wako wengi sawa.Ila kumbuka hata wakiwa wengi kiasi gani lakini hatakuwa wa aina ya Zari.

Ni salamu zangu kwako Diamond,Simba,Boy from Tandale na majina mengine mengi .Hata lila Chib Dangote.Nihitimishe kwa kueleza tu ni mtazamo tu na nilichoandika si sheria,kanuni wala taratibu.Nikuombe Diamond soma nilichaondika kuhusu wewe na Zari.

Ni mawazo tu yamejikusanya kichwani na kwa ujinga wangu nikaona acha niyaandike yaonekane.Alamsiki.Jumapili iwe njema kwetu sote.

UKITAKA KUWASILIANA 0688534011
Viewing all 46396 articles
Browse latest View live




Latest Images