Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

WIZARA YA MALIASILI, ARDHI NA TAMISEMI KUAMUA HATMA YA MGOGORO WA PORI LA AKIBA MKUNGUNERO – DK. KIGWANGALLA

$
0
0


Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi aliyekuwa akimunesha mpaka wa kijiji hicho na Pori la Akiba Mkungunero wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Na Hamza Temba - Kondoa, Dodoma
..........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla jana tarehe 7 februari, 2018 ametembelea Pori la Akiba Mkungunero katika Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma na kuwataka wananchi wanaozunguka pori hilo kusubiri uamuzi wa Serikali  utakaoshirikisha Wizara yake,  Wizara ya Ardhi na Tamisemi katika kujibu maombi yao ya kutaka kupewa sehemu ya ardhi katika pori hilo kwa ajili ya kuendesha shughuli za kibinadamu.

Dk. Kigwangalla ambaye aliongozana na Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, alitembelea vijiji vinne vya Ikengwa, Keikei Tangini, Keikei na Kisondoko na kufanya mikutano ya hadhara kwa ajili ya kujiridhisha na  kujifunza juu ya mgogoro uliopo baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero.

"Nimefika hapa leo kujifunza juu ya mgogoro huu, nimejionea hali halisi lakini pia nina maelezo ya wataalamu ambayo yapo kwenye maandishi naomba niende nikayasome, niyatafakari ili niweze kushauriana na wenzangu na mwisho wa siku tuweze kuja na suluhu ya namna ya kuondokana na changamoto ambazo zimekuwepo.

"Niwaombe sana wakati Serikali inaendelea kutafuta suluhu ya mgogoro huu ni vema tukafuata sheria zilizopo, tuzingatie mipaka iliyowekwa ili tusiingie kwenye migogoro, lakini kwa sasa siwezi kwa namna yeyote ile kutamka neno la kujibu maombi ya mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji na wananchi yaliyotolewa hapa leo.

"Kama Serikali tutakaa, Wizara yangu, Wizara ya Ardhi na Tamisemi ili tujue kiini cha mgogoro huu tufanye uamuzi kuwa ni maeneo gani yaongezwe katika hifadhi kwa ajili ya wananchi au ni vitongoji vipi vifutwe, tutaleta majibu, na jambo hili tutalifanya kwa uadilifu mkubwa bila kumuonea mtu ili kumaliza mgogoro huu," alisisitiza Dk. Kigwangalla.

Awali akimkaribisha Waziri huyo kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Ikengwa, Mbunge wa jimbo hilo, Dk. Ashatu Kijaji alisema kutokana na ukweli kuwa Serikali ya awamu ya tano inasikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi, ni vema Waziri huyo akatumia hekima na kuangalia uwezekano wa kuwapa wananchi hao Kilomita 12 za mraba kutoka kwenye hifadhi hiyo kwa ajili ya kuendesha shughuli zao za kibinadamu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi alisema mgogoro baina ya vijiji hivyo na Pori la Akiba Mkungunero ulinza mwaka 2006 kufuatia zoezi la kuanzishwa kwake  pamoja na lile na uwekagi wa vigingi vya mpaka  na vijiji jirani kutoshirikisha wananchi na viongozi wa halmashauri za vijiji hoja ambayo ilipigwa na Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso

Aidha alisema wananchi wa vijiji hivyo wanakabiliwa na uhaba wa maeneo ya kilimo na ufugaji, hivyo akamuomba Waziri huyo pamoja na Serikali kwa ujumla kutumia busara  kuwamegea wananchi wa vijiji hivyo eneo la Kilomita 12 za mraba kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji.

Naye Meneja wa Pori hilo, Emannuel Bilaso alisema Pori la Akiba Mkungunero lilianzishwa kwa tangazo la Serikali Na. 307 la mwaka 1996 baada ya kupandishwa hadhi kutoka Pori Tengefu. Alisema mchakato wa kupandisha hadhi pori hilo ulishirikisha wananchi na viongozi wa vijiji na wilaya ambapo mihutasari mbalimbali ilisainiwa.

Alisema pori hilo linakabiliwa na changamoto mbalimbali zinazochochea mgororo huo ikiwemo kijiji kimoja cha Kisondoko  kusajiliwa kimakosa ndani ya hifadhi hiyo pamoja na malalamiko mbalimbali ya wananchi kuwa hawakushirikishwa kwenye uanzishwaji wa pori pamoja na madai mengine kuwa pori hilo limeingilia mipaka ya vijiji hivyo.

Pori la Akiba Mkungunero ambalo lina ukubwa wa Kilimita za Mraba 557.9 lina umuhimu mkubwa kiuchumi na kiikolojia kwa kuwa ni chanzo muhimu cha mto Tarangire ambao ni uhai wa hifadhi ya Taifa ya Tarangire na ikolojia nzima ya ziwa Manyara. Pori hilo pia ni sehemu ya mapito na mazalia ya wanyamapori pamoja na makazi ya wanyamapori adimu duniani.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kondoa muda mfupi baada ya kuwasili wilayana humo jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa ramani ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na Mrasimu Ramani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Peter Nyange (kulia) wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kulia) akiteja jambo na Meneja wa Pori la Akiba Mkungunero, Emannuel Bilaso wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akiteta jambo na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ikengwa, Mohammed Tabahi wakati wa ziara yake ya kikazi jana katika Pori la Akiba Mkungunero Wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akipokea mabango ya malalamiko kutoka kwa wananchi wa kijiji cha Kisondoko kuhusu Pori la Akiba Mkungunero na vijiji jirani wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kisondoko wilayani Kondoa jana.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero na mmoja wa wahifadhi wa Pori hilo wakati wa ziara yake ya kikazi katika pori hilo jana Wilayani Kondoa Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kubaini changamoto za mgogoro wa mipaka kati ya pori hilo na vijiji jirani ili kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu ambapo alisema Wizara yake kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi na TAMISEMI zitakaa pamoja kutafuta suluhu ya mgogoro huo. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

MBARAWA AMKABIDHI NAIBU SPIKA MWONGOZO WA WATUMIAJI HUDUMA NA BIDHAA ZA MAWASILIANO

$
0
0

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa pili kushoto) akimkabidhi Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (wa pili kulia) Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano kwa niaba ya Wabunge. Wakishuhudia watatu kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Mawasiliano Mhandisi Anjelina Madete na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma.
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akionesha Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kwa niaba ya Wabunge. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto) akimweleza Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (wa kwanza kulia) umuhimu wa Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano kwa Wabunge mara baada ya kumkabidhi Mwongozo huo kwa niaba ya Wabunge ili waweze kusoma, kuelewa na kuelimisha wananchi namna ya kutumia vema huduma na bidhaa za mawasiliano nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba (wa kwanza kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson (wa kwanza kulia) kuhusu Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kwa niaba ya Wabunge. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma

MSTAHIKI MEYA SELEBOSI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI LEO JIJINI TANGA

$
0
0


Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga(CCM) Alhaji Mustapha Mhina Selebosi akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani leo kwenye ukumbi wa Halmashauri kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudi Mayeji kushoto ni Naibu Meya wa Jiji hilo,Mohamed Haniu
Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudio Mayeji akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji hilo,Alhaji Mustapa Mhina Selebosi anayefuata ni Naibu Meya Mohamed Haniu na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga,Meja
Naibu Meya Mohamed Haniu akizungumza katika kikao hicho kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi
Waheshimiwa madiwani wa Jiji la Tanga wakifanya dua kabla ya kuanza kikao hicho
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi katika akiwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia na Naibu Mstahiki Meya Mohamed Haniu wakipitia taarifa mbalimbali wakati wa kikao hicho leo
Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi katika akisisitiza jambo kwenye kikao hicho kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji na kushoto ni Naibu Meya wa Jiji la Tanga ,Mohamed Haniu
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Hamisi Mkoba akipitia kabrasha wakati wa kikao hicho


Katibu wa CCM wilaya ya Tanga katika akifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa kikao hicho









Baadhi ya waheshimiwa maduwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho kwa umakini




Sehemu ya wataalamu katika halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho







Diwani wa Kata ya Maweni (CCM) Calvas Joseph akiuliza swali katika kikao hicho

















Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga(CCM) Alhaji Mustapha Mhina Selebosi akizungumza wakati akifungua kikao cha Baraza la Madiwani leo kwenye ukumbi wa Halmashauri kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudi Mayeji kushoto ni Naibu Meya wa Jiji hilo,Mohamed Haniu




Mkurugenzi wa Jiji la Tanga,Daudio Mayeji akizungumza katika kikao hicho kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji hilo,Alhaji Mustapa Mhina Selebosi anayefuata ni Naibu Meya Mohamed Haniu na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga,Meja




Naibu Meya Mohamed Haniu akizungumza katika kikao hicho kulia ni Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi






Waheshimiwa madiwani wa Jiji la Tanga wakifanya dua kabla ya kuanza kikao hicho







Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi katika akiwa na Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji kulia na Naibu Mstahiki Meya Mohamed Haniu wakipitia taarifa mbalimbali wakati wa kikao hicho leo







Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Mhina Selebosi katika akisisitiza jambo kwenye kikao hicho kulia ni Mkurugenzi wa Jiji la Tanga Daudi Mayeji na kushoto ni Naibu Meya wa Jiji la Tanga ,Mohamed Haniu







Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Hamisi Mkoba akipitia kabrasha wakati wa kikao hicho





Katibu wa CCM wilaya ya Tanga katika akifuatilia mijadala mbalimbali wakati wa kikao hicho









Baadhi ya waheshimiwa maduwani wa Halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho kwa umakini




Sehemu ya wataalamu katika halmashauri ya Jiji la Tanga wakifuatilia kikao hicho







Diwani wa Kata ya Maweni (CCM) Calvas Joseph akiuliza swali katika kikao hicho




Sehemu ya waheshimiwa madiwani wa Jiji la Tanga wakiangalia makabrasha kabla ya kuanza kikao hicho









Sehemu ya wataalamu kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga wakiwa makini kufuatilia taarifa mbalimbali kulia ni Ramadhani Possi (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)


Sehemu ya waheshimiwa madiwani wa Jiji la Tanga wakiangalia makabrasha kabla ya kuanza kikao hicho

Sehemu ya wataalamu kwenye Halmashauri ya Jiji la Tanga wakiwa makini kufuatilia taarifa mbalimbali kulia ni Ramadhani Possi (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

JAFO ASHUSHA NEEMA YA LAMI CHANG’OMBE, AMFAGILIA MAVUNDE KWA UCHAPAKAZI WAKE

$
0
0

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
jiwe la msingi la soko la Chang'ombe
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk.Binilith Mahenge akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Baadhi ya bidhaa zilizopo soko la Chang'ombe
Soko lenyewe la Chang'ombe
Viongozi mbalimbali katika uzinduzi wa Soko la wafanyabiashara wadogo wadogo wa Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Wafanyabishara wa Soko la Chang'ombe Manispaa ya Dodoma.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akitembelea soko la Chang'ombe mara baada ya kuzindua.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo akisalimiana na wananchi na wafanyabiashara wa soko la Chang'ombe.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI), Mhe.Selemani Jafo, amemfagilia Mbunge wa Jimbo la Dodoma Anthony Mavunde kwa jitihada zake za kuwaletea maendeleo kwa wananchi wake, huku akiuagiza Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) kuhakikisha katika bajeti yao ya mwaka 2018/19 wanaingiza kwenye mpango ujenzi wa barabara ya lami Chang’ombe hadi Chuo cha Mipango.

Jafo ameyasema hayo leo alipokuwa anazindua soko jipya la kisasa kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo kata Chang’ombe lililojengwa na Serikali kwa kusaidiana na wafanyabiashara na Mbunge Mavunde ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Vijana.

Ujenzi wa soko hilo ulianza mwaka 2017 na kukamilika mapema mwaka huu na litakuwa na wafanyabiashara wa bidhaa mbalimbali takribani 342 na limegharimu kiasi cha Sh.Milioni 70.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Waziri Jafo amesema katika ziara zake za miradi ya maendeleo alizotembelea katika Manispaa ya Dodoma, Mbunge Mavunde ameonekana kushiriki katika kila sekta kwa kusaidiana na wananchi.

“Katika kila taarifa ya mradi wa maendeleo inayosomwa,unaonesha Mbunge wenu Mavunde amechangia kwa kweli nimpongeze sana kwa kushiriki kuleta maendeleo kwa wananchi wake, ni mchapakazi.Nawapongeza katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 mlilamba dume kila eneo ninaloenda nakuta nyayo zake, Naahidi kumpa ushirikiano wa kutosha,”amesema jafo

Amesema katika ujenzi wa soko hilo Mbunge huyo amesaidiana na wananchi na kufanikisha kukamilisha ujenzi wake na kuahidi kuendelea kuboresha miundombinu ya Dodoma ili iendane na hadhi ya Makao Makuu ya nchi.

Waziri Jafo amesema Serikali inawekeza miundombinu ya hali ya juu katika mkoa wa Dodoma ikiwemo mtandao wa barabara za lami katika maeneo mbalimbali pamoja na taa za barabarani ikiwa ni pamoja na ujenzi wa dampo la kisasa.“Kwa kuwa serikali inahamia Dodoma hivyo basi miundombinu mbalimbali lazima iendelee kujengwa na kurekebishwa,” Amesisitiza Mhe. Jafo

Aidha Waziri jafo amewapongeza wananchi kwa kushirikiana na Halmashauri ya Manispaa kukamilisha ujenzi wa soko la kisasa na kwamba limejengwa kwa gharama nafuu sio kama masoko mengine yanayojengwa kwa gharama kubwa.

Pia ameupongeza Uongozi wa Mkoa wa Dodoma pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge na Mkurugenzi wa Manispaa Godwin Kunambi kwa jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi.

Amemuagiza Mkurugenzi Kunambi kukamilisha masoko mbalimbali pamoja na kuanza kutumika kwa machinjio ya kuku yaliyopo soko la majengo ipasavyo kwa kuwa kuna taarifa kuku wanaenda kuchinjwa maeneo mengine na kuacha machinjio ya eneo hilo.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mavunde amesema ujenzi wa soko hilo ni ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2015 na kwamba yataendelea kujengwa masoko ya kisasa yanayoendana na hadhi ya Makao Makuu ya Nchi.

“Pia kipekee niwashukuru wananchi wangu hasa wafanyabiashara kwa kuchangia ujenzi wa soko hili, pia na Mbunge wa jimbo la Mbarali Mhe.Haroun alinisaidia hapa kifusi malori 70 kwa ajili ya kushindilia chini.Niliahidi kuwatumikia na sitawaangusha nitakuwa nanyi bega kwa bega nanyie nawaomba mniunge mkono,”amesema Mavunde

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amempongeza Mavunde kwa kazi anayoifanya ya kuwaletea wananchi maendeleo na kuwataka wananchi kumuunga mkono ili aweze kuwatumikia ipasavyo.Kadhalika, Mkurugenzi Kunambi amesema Manispaa imepangwa vizuri kwa kuwa kila kata imetengewa eneo kwa ajili ya soko na kwamba Manispaa hiyo imejipanga kutengeneza masoko hayo.

Aidha amesema mwezi Machi mwaka huu utaanza ujenzi wa stendi kubwa ya kisasa ya mabasi yaendayo mikoani na soko la kisasa katika eneo la Nzuguni.

MKUU WA WILAYA YA KIBAHA ASSUMPTER MSHAMA ATOA SIKU TISINI KWA MWEKEZAJI KURUDISHA HEKARI 5000 KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA LUKENGE

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama akizungumza na umati wa wananchi wa kijiji cha Lukenge kata Magindu hawapo pichani katika mkutano wa adhara ambao aliuandaa kwa ajili ya kuweza kutatua mgogoro wa aradhi kati ya wananachi hao na mwekezaji ambao umedumu kwa kipindi kirefu
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama akiwa anatoka kwenye mkutano na wananchi wa kijiji cha lukenge alipokwenda kwa ajili ya kumaliza sakata la mgogoro baina ya wananachi hao pamoja na mwekezaji.
Baadhi ya wananchi wa kijiji cha lukenge wakiwa wanamsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama wakati wa mkutano wa adhara ambao uliandaliwa kwa ajili ya kusikiliza mgogoro uliopo katia ya wananchi na mwekezaji.
Wananchi wa kijiji cha lukenge wakiwa wameshika mabango yaliyokuwa yameandikwa ujumbe wa kumkataa mwekezaji huyo, ambapo walipita mbele kwa ajili ya kuweza kumuonyesha Mkuu wa Wilaaya ya Kibaha.
PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU



NA VICTOR MASANGU, KIBAHA PWANI

SERIKALI wilayani Kibaha,Mkoa wa Pwani imemtaka mwekezaji ambaye alichukua eneo lenye ukubwa wa hekari zipatazo 5000 za ardhi bila ya kuzingatia sheria na taratibu kuzirudisha kwa kipindi cha siku tisini kutokana na kushindwa kuliendeleza kwa kipindi cha zaidi ya miaka nane kama walivyokubaliana katiba mkataba na wananchi wa kijiji cha lukenge kata ya Magindu.

Sakata la mgogoro wa ardhi baina ya wananchi hao na mwekeaji limechukua sura mpya kufuatai Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama baada ya kupokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi hivyo kumtaka mwekezaji huyo kuzirudisha hekari hizo 5000 kwa wananchi ambazo alikuwa amepewa na serikali ya kijiji kwa ajili ya uwekezaji wa ufugaji wa kisasa wa ng’ombe pamoja na samaki lakini ameshindwa kutekeleza makubaliano aliyopatiwa hapo awali.

Akizungumza katika mkutano maalumu wa adhara ambao uliandaliwa kwa ajili ya kujadili sakata hilo Mkuu huyo wa Wilaya amesema eneo hilo mwekezaji huyo alipewa kwa ajili ya kuliendeleza lakini amekuwa akijinufaisha mwenywe na kuwanyonya wakazi wa eneo hilo bila ya kuwaletea maendeleo ya aina yoyote tofauti na makubaliano yao.

Kwa upande wake aliyekuwa Mwenyekiti wa zamani wa kijiji hicho cha Lukenge Seif Maleta ambaye kwa sasa amemaliza muda wake amesema kwamba eneo hilo la hekari 5000 hawakumuuzia mwekezaji huyo ila walimpatia kulitumia kwa muda tu kwa ajili ya kuweza kufanyia shughuli zake mbali mbali za ufugaji wa ng’ombe na samaki kwa makubaliano maalumu.

Naye mwekezaji huyo ambaye analalamikiwa na wananchi anayejulikana kw ajina la Tangono Kashima alisema kwamba eneo hilo la uwekezaji wa ng’ombe alilipata kwa kuzingatia taratibu za serikali ya kijiji kwa kuandika barua maalumu kwa ajili ya kuomba eneo hilo kwa ajili ya kufuga ufugaji wa kisasa wa ng’ombe pamoja na kuchimba bwawa kwa ajili ya ufugaji wa samaki

ENEO hilo la ardhi lililopo katika kijiji cha lukenge kata ya magindu katika halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani lina ukumbwa wa hekari zipatazo 5000 na kwa sasa limeingia katika mgogoro mkubwa baina ya wananchi pamoja na mwekezaji huyo kutokana na kukiuka kanuni na sheria za umiliki wa ardhi.

RC MNYETI AENDESHA HARAMBEE NA KUPATIKANA SHILINGI MILIONI 17 UJENZI WA MAABARA

$
0
0
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akizungumza na wanafunzi na walimu wa shule ya sekondari Bishop Hando iliyoshika nafasi ya kwanza kwenye mtihani wa kidato cha nne mwaka jana Wilayani Mbulu, ambapo aliwapa zawadi ya shilingi milioni moja walimu wa shule hiyo na wanafunzi aliwapa chakula, magunia 100 ya mahindi baada ya kushika nafasi hiyo.

Wanafunzi wa shule ya sekondari Bishop Hando ya Kata ya Masqaroda Wilayani Mbulu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti alipotembelea shule hiyo ambapo aliendesha harambee ya umaliziaji wa ujenzi wa jengo maabara na kupatikana shilingi milioni 17.5.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti akimsikiliza mwalimu wa shule ya sekondari Bishop Hando, ya Wilayani Mbulu Samuel Surumbu alipotembelea shule hiyo na kufanya harambee ya umaliziaji wa ujenzi wa jengo la maabara na kupatikana shilingi milioni 17.5 Wanafunzi wa shule ya sekondari
Wanafunzi wa shule ya sekondari Bishop Hando na wananchi wa Kata ya Masqaroda Wilayani Mbulu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti alipotembelea shule hiyo kwenye ziara yake ya siku saba ya kutembelea wilaya ya Mbulu, ambapo anakagua miradi ya maendeleo, kuwasikiliza wananchi na kuzungumza nao.

………………….

MKUU wa Mkoa wa Manyara, Alexander Pastory Mnyeti ameendesha harambee iliyopatikana sh17. 5 milioni ya umaliziaji wa jengo la maabara ya shule ya sekondari Bishop Hando ya Wilayani Mbulu.

Pia, Mnyeti amewapa zawadi ya sh1 milioni walimu wa shule hiyo na wanafunzi wakapewa magunia 100 ya mahindi ya chakula kwa kushika nafasi ya kwanza kwenye matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2017.Aliendesha zoezi hilo kwenye ziara yake ya siku saba ya kutembelea halmashauri ya wilaya ya Mbulu ambapo atakagua na kuzindua miradi ya maendeleo, kusikiliza kero na kuzungumza na wananchi.

Mnyeti akizungumza kwenye shule hiyo amemuagiza mkuu wa wilaya hiyo Chelestino Mofuga kuhakikisha maabara hiyo inakamilika ndani ya muda wa miezi mitatu.“Hata mimi niliwahi kuwa mkuu wa shule ya sekondari, natambua gharama za ujenzi zilivyo, hapa panahitajika sh40 milioni, sisi tumechangia sh17. 5 milioni sasa pambaneni mlimalize jengo hili,” alisema Mnyeti.

Mkuu wa wilaya hiyo Mofuga alimuhakikishia Mnyeti kuwa atafanikisha usimamizi wa umaliziaji wa maabara hiyo ndani ya miezi mitatu kama alivyoagiza.“Kupitia nafasi hii nakuagiza mtendaji wa kata ya Masqaroda na mtendaji wa kijiji kuendesha michango kwa wananchi ili tumalize jengo hili la maabara,” alisema Mofuga.Awali, mwalimu wa shule hiyo ya sekondari Bishop Hando, Samuel Surumbu alisema kiwango cha taaluma kwa wanafunzi kinafanikiwa kutokana na ufundishaji wa walimu na kuwepo kwa chakula shuleni.

Mwalimu Surumbu alisema pia wanasaidiwa kufundisha na walimu wengine wa kujitolea wanaofundisha masomo ya sayansi.Alisema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo wa upungufu wa majengo ikiwemo ofisi za walimu, nyumba za walimu na bwalo la kulia chakula.Diwani wa kata ya Masqaroda Peter Tarmo alimshukuru Mnyeti kwa kuendesha zoezi hilo lililofanikisha upatikanaji wa fedha hizo zitakazosaidia umaliziaji wa jengo hilo la maabara.

Huu mzigo hivi sasa utakuwa mwepesi tofauti na hapo awali, tutajipanga na wananchi wangu na wilaya yetu kuhakikisha maabara hii inakamilika,” alisema Tarmo.

MATUKIO KATIKA PICHA WAZIRI MKUU MAJALIWA AKIZUNGUMZA NA WABUNGE MJINI DODOMA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa, Bungeni mjini Dodoma Februari 8, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 8, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mbunge wa Konde, Khatib Said Haji kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma, Februari 8, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Februari 8, 2018
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wabunge, Murad Sadiq wa Mvomero (kulia), Suleiman Nchambi wa Kishapu (katikati) na Richard Ndassa wa Sumve kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Februari 8, 2018.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

Wawindaji wa Panya Rukwa Kukomeshwa

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akipanda mti katika shule ya msingi Mpwapwa, kata ya Mpwapwa Wilayani Sumbawanga ikiwa ni kampeni ya kufikisha miti Milioni 6 kwa Mkoa kwa mwaka 2017/2018.
Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule akisaidiana na mwanafunzi wa darasa la kwanza Shule ya Msingi Mpwapwa Joanita Mwanandenje kupanda mti ili kuwahamasisha wanafunzi kuwa na utamaduni wa kupanda miti na kufikisha miti milioni 3 kwa Wilaya ya Sumbawanga.
Mjumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa ACP George Kyando akijiandaa kuapanda mti katika Shule ya Msingi Mpwapwa ikiwa ni kampeni ya Mkoa kufikisha miti milioni 6 na kuhifadhi mazingira ya Mkoa.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akikabidhi miche kwa Didas Kosam M/kiti wa kitongoji cha Katupa, Kijiji cha Mpwapwa chenye vitongoji vinne. Ambapo kila kitongoji kilipewa miche 200.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo
Mjumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Rukwa, Afisa Uhamiaji Mkoa Carlos Haule akipanda mti nje ya Zahanati ya Mpwapwa ikiwa ni kuendeleza kuhamasisha kampeni ya upandaji miti Rukwa. 

……………

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Sumbwanga Dk. Khalfan Haule kuhakikisha anatafuta dawa ya kuulia panya wakiwa mashambani ili kuokoa miti kutokana na uchomaji wa misitu kwasababu ya uwindaji wa panya.

Amesema kuwa ameisikia changamoto hiyo ya uchomaji wa misitu kwasababu ya uwindaji wa panya kutoka kwa vijana mbalimbali wanaojishughulisha na mashamba ya upandaji miti pamoja na taarifa iliyosomwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga juu ya changamoto za kuendeleza misitu.

“DC tafuta dawa ya panya, wauliwe huko mashambani, ili panya wasiwepo na miti iokoke, mbona hamshangilii? Hawa panya tutawaua kwa sumu huko mashambani wasiwe chanzo cha mioto ambayo mnachoma huko kuwatafuta hawa panya ili wafie huko huko mashimoni msiwapate,” Alisisitiza.

Agizo hilo amelitoa katika muendelezo wa kampeni ya upandaji miti mijini na vijijini katika Kijiji cha Mpwapwa, kata ya Mpwapwa, Wilayani Sumbwanga baada ya kuwauliza wananchi wa Kijiji hicho juu ya changamoto aliyoisikia ya uchomaji wa moto misitu kutokana na kuwinda panya, japo wananchi walikataa.

Pia katika kuongezea hilo alimuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kuhakikisha anasimamia sheria ya hifadhi ya mazingira na kuwawajibisha wote wanaohusika na uharibifu wa mazingira.

Nae akisoma taarifa Mkurugenzi wa H/W ya Sumbawanga Nyangi Msemakweli alibainisha kuwa miongoni mwa changamoto ni muitikio mdogo wa uhifadhi wa mazingira pamoja na mila na tamaduni za wananchi za uwindaji wa panya hali inayosababisha uchomaji wa misitu wakati wa kiangazi.

“Changamoto nyingine ni baadhi ya viongozi wa serikali ya Kijiji kujihusisha na uuzajia wa maeneo yaliyotengwa kwaajili ya hifadhi ya Kijiji na usimamizi mdogo wa sheria ndogo za vijiji katika utunzaji wa misitu,” Alimalizia.

Mmoja wa vijana wanaojishughulisha na upandaji kiti wa kibiashara Julius Magaga alimweleza Mh. Wangabo kuwa chnagmoto inayowakatisha tamaa vijana wengi ni kutokana na uwindaji wa panya uliokithiri na kusababisha hasara katika misitu.

Kwa msimu wa 2017/2018 hadi 30/1/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Sumbwanga imepanda miti 830,527 ambayo ni sawa na 55.4% na ina misitu 92 yenye ukubwa wa jumla ya Hekta 49,179.6. Huku Mh. Wangabo akigawa miche 850 kwa kaya 850 za Kijiji cha Mpwapwa, Wilayani Sumbawanga.

ACACIA YAKABIDHI HUNDI BILIONI 1.1 ZA USHURU WA HUDUMA KAHAMA MJI NA MSALALA

$
0
0
Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu Acacia kupitia migodi yake ya Buzwagi na Bulyanhulu imekabidhi hundi za shilingi bilioni 1.1 kwa halmashauri ya wilaya ya Mji wa Kahama na Msalala mkoani Shinyanga kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa kipindi cha Mwezi Julai hadi Disemba mwaka 2017. 

Acacia imekabidhi hundi ya shilingi milioni 924,881,819.78 kwa halmashauri ya wilaya ya Mji wa Kahama zilizotolewa na mgodi wa Buzwagi na hundi ya shilingi milioni 153,591,456 kwa halmashauri ya wilaya ya Msalala zilizotolewa na mgodi wa Bulyanhulu na kufanya jumla kuwa shilingi bilioni 1.1. 

Meneja Mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu amekabidhi hundi hizo kwa mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurulu leo Alhamis Februari 8,2018 mjini Kahama. 

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo,Busunzu alisema mgodi wa Bulyanhulu pia ulipa shilingi 75,649,524 kwa halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya ushuru wa huduma kwa kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2017. 

Busunzu alisema kupungua kwa uzalishaji katika migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu kumesababisha kupungua kwa kiwango cha uchangiaji wa ushuru wa huduma katika miezi sita iliyopita ikilinganishwa na mwaka jana na mwaka juzi. 

Hata hivyo alisema Acacia imedhamiria kuendelea kuwa mdau mkubwa wa maendeleo kwa kuendelea kusaidia maendeleo ya biashara za wazawa pamoja na kushirikiana na serikali katika miradi endelevu ya muda mrefu kwenye jamii. 

Busunzu alieleza kuwa Acacia inaendelea kushirikiana na serikali ya mkoa na wilaya katika kutekeleza miradi miwili mikubwa ya miundombinu ya jamii katika eneo la maji na afya. 

“Bulyanhulu itafadhili shilingi bilioni 1.1 kwenye awamu ya pili ya kuboresha kituo cha afya cha Bugarama ili kuwezesha kufikia hatua ya kuwa hospitali ya wilaya,pia tumechangia shilingi bilioni 4.5 katika mradi wa ushirikiano wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika halmashauri ya Msalala na Nyang’wale”,aliongeza Busunzu. 

Naye Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu aliishukuru Acacia kwa kutoa ushuru wa huduma na kuwaomba kuendelea kushirikiana na halmashauri za wilaya katika kuwaletea maendeleo wananchi. 

Nkurlu aliwaagiza wakurugenzi wa halmashauri kutumia vizuri pesa zilizotolewa na Acacia ili zitoe matokeo chanya ikiwemo kutatua changamoto zinazowakabili wananchi. 

Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba alisema watazitumia pesa hizo kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo kuboresha huduma za afya wilayani humo. 
Katikati ni Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akikabidhi hundi ya shilingi153,591,456 kwa Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya wilaya ya Msalala katika kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2017. Kulia ni Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akikabidhi hundi hiyo ya shilingi milioni 153 kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Msalala Simon Berege 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkuru,Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu,Meneja wa Huduma na Mahusiano wa Acacia, Elias Kasitila na Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Msalala Simon Berege wakiwa wameshikilia hundi ya shilingi milioni 153. 
Katikati ni Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akikabidhi hundi ya milioni 924,881,819.78 kwa Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu kwa ajili ya malipo ya ushuru wa huduma kwa halmashauri ya wilaya ya Mji wa Kahama katika kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba 2017. Kulia ni Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akikabidhi hundi hiyo kwa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba 
Picha ya pamoja baada ya makabidhiano ya hundi mbili 
Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhi hundi zenye jumla ya shilingi bilioni 1.1 
Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akizungumza na waandishi wa habari ambapo alisema Acacia itaendelea kushirikiana na serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi 
Mkuu wa wilaya ya Kahama Fadhili Nkurlu akizungumza baada ya kupokea hundi zenye jumla ya shilingi bilioni 1.1 zilizotolewa na Acacia 
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba. 


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Dkt MWINUKA atembelea Kituo cha Kupoza,Kusambaza Umeme, Shinyanga

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka, ametembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.
Katika ziara hiyo, Dkt. Mwinuka amejionea shughuli mbalimbali zinazofanyika kituoni hapo. 

Kituo hicho ni mojawapo ya vituo vilivyofanyiwa upanuzi wakati wa utekelezaji wa Mradi wa njia ya Kusafirisha umeme ya msongo wa kilovolti 400 (Backbone) kutoka Mkoani Iringa hadi Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji TANESCO Dkt. Tito Mwinuka, akisaini Kitabu cha Kumbukumbu ya Wageni Wakati alipotembelea kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.
Muonekano wa kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Ibadakuli, kilichopo Mkoani Shinyanga.

WIZARA YA MALIASILI YAAGIZWA IRUDI KWA WANANCHI KUTOA MAJIBU

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii irudi kwenye maeneo yote yenye migogoro ya mipaka na iungane na Halmashauri za wilaya ili waweze kutoa majibu kwa wananchi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Alhamisi, Februari 8, 2018) wakati akijibu swali la mbunge wa Urambo, Bibi Margaret Sitta wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu Bungeni mjini Dodoma.

Bibi Sitta alitaka kujua Serikali imeweka taratibu na mikakati gani ya kumaliza migogoro ya mipaka inayoendelea katika maeneo mbalimbali ya hifadhi za misitu nchini kwa kuwa wananchi wanahitaji maeneo kwa ajili ya shughuli za kilimo na mifugo.

Waziri Mkuu amesema Serikali iliiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii iweke vigingi kwenye maeneo yote yanayozunguka hifadhi za misitu ili kuweka alama zitakazopunguza migogoro ya kuingiliana kati ya wananchi walioko kwenye vijiji na wahifadhi kwenye maeneo ya hifadhi ya misitu hiyo.

Amesema maagizo hayo yalitolewa baada ya kugundua kuwa kuna migogoro mingi kati ya wananchi walioko katika vijiji vya jirani na misitu iliyohifadhiwa kisheria ambayo ina ramani.

“Lakini tunatambua kwamba wanapoendelea na zoezi hilo la uwekaji alama, inaweza kutokea kijiji kikajikuta kipo ndani ya mipaka ya hifadhi na inaweza kusababisha kutoelewana kati ya wanakijiji na wenye mamlaka ya hifadhi.”

“Tuliwasihi wanakijiji wakati zoezi hili linaendelea na hata kama kijiji kitajikuta kimezungukwa na hizo alama, wanakijiji watulie ili kazi ya awali ikamilike na pale kwenye mgogoro, Serikali itarudi tena kuja kuangalia mgogoro huo na kufanya tathmini ya kina.”

Amesema Serikali iliiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii inapofanya kazi hiyo ya kuweka vigingi lazima ishirikishe mamlaka za halmashauri na kijiji husika na wao washiriki katika zoezi hilo ili kuondoa migogoro isiyokuwa ya lazima.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali ilishaielekeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi izitumie ranchi za NARCO na kugawa katika vitalu ili kubaini ukubwa wa eneo iliyonayo ndipo iweze kufanya uamuzi wa kugawa vitalu hivyo kwa wafugaji.

Ameyasema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Nkenge, Balozi Dkt. Diodorus Kamala aliyetaka kujua taarifa ya kamati iliyoundwa na Serikali kufuatilia migogoro ya ranchi zilizokuwa chini ya NARCO na wafugaji, itapelekwa lini bungeni ili iweze kujadiliwa.

Waziri Mkuu amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi iliunda tume ya kufuatilia maeneo yote ya ranchi za Taifa na kuyapima maeneo hayo lakini pia kujua ni akina nani wanayamiliki maeneo hayo, kubaini kama walipewa kihalali, na kama ni kweli wanamiliki mifugo yoyote kwenye maeneo tajwa.

Kuhusu kupelekwa bungeni kwa taarifa ya tume hiyo, Waziri Mkuu amemtaka Waziri wa Mifugo aikamilishe na kuiwasilisha Bungeni kama taratibu zinavyotaka ili kuwawezesha wabunge na wananchi wajue dira na mwelekeo wa Serikali wa namna ya kufuga mifugo hiyo kwa njia ambazo zitawaletea tija lakini kikubwa zaidi ni kumaliza migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
 

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
41193 - DODOMA.
ALHAMISI, FEBRUARI 8, 2018.

UNICEF YATOA MSAADA WA LAPTOP 200 KWA WIZARA YA AFYA ZANZIBAR

$
0
0
Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto UNICEF limetoa msaada wa Komputa aina ya Laptop 200 kwa Wizara ya Afya ya Zanzibar ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo.

Laptop hizo zenye thamani ya zaidi ya Shilingi Milioni 400 zimetolewa ikiwa ni mwendelezo wa UNICEF kuiunga mkono Serikali katika kuimarisha huduma za matibabu hasa ya akinamama na watoto.Akikabidhi Msaada huo katika Ukumbi wa Wizara hiyo Mnazi mmoja Mwakilishi wa UNICEF Zanzibar Francesca Morandin amesema upatikanaji wa taarifa sahihi ni jambo muhimu linalofaa kupewa kipaumbele.

Amesema uwepo wa taarifa sahihi za Wajawazito na watoto huisaidia Serikali kujua idadi ya ongezeko la watu wake hali inayopelekea kupanga mipango vyema ya matibabu kulingana na idadi ya watu husika.Amewataka Watendaji kwa ujumla kuunga mkono juhudi zinazotolewa na UNECO ili kuhakikisha afya za Watoto na Wajawazito zinaimarika.

Francesca ameongeza kuwa Shirika hilo la UNICEF litaendelea kuiunga mkono Zanzibar katika juhudi zake za kimatibu na kuipongeza Srikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kutoa matibabu bure kwa wananchi wake.

Amefahamisha kuwa Zanzibar inapiga hatua mbele kwa upande wa Matibabu na kupongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuwashajiisha Wajawajizito kushiriki huduma hizo muhimu katika maisha yao. “Zanzibar zaidi ya asilimia 99 ya Wajawazito hushiriki katika Kliniki mbalimbali walau mara moja katika kipindi chao cha ujauzito. Hii inawezekana kwamba imechangiwa na juhudi za Serikali za kuyafanya matibabu bure”Alipongeza Francesca.

Kwa upande wake Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo amelishukuru Shirika la UNICEF kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar hasa katika sekta ya Afya.

Amemuahidi Mwakilishi huyo kwamba Msaada uliotolewa utatumika vyema ili kutimiza malengo ya Shirika hilo.

“Cha bure mara nyingi vitu vya bure havitunzwi vyema lakini Laptop hizi lazima tujitahidi kuutumia vyema..Laptop ziendelee kudumu na taarifa zinazohitajika zote kuanzia Dawa, Wajawazito, Watoto nakadhalika zote ziwekwe kwenye mfumo unaotakiwa”Alisema Waziri Kombo.

Waziri Kombo amesema Zanzibar inaendelea kupokea pongezi kutoka pande zote za Dunia kwa namna Serikali inavyojitahidi katika kutoa huduma bora za matibabu na hivyo msaada huo utazidi kuimarisha huduma hizo.

Laptop hizo zitagawiwa katika Vituo vyote vya matibabu Unguja na Pemba ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo.

IMETOLEWA NA MAELEZO ZANZIBAR
Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo kushoto na akikabidhiwa Msaada wa Laptop 200 zenye thamani ya zaidi ya Shil.Millioni 400 kutoka kwa Mwakilishi wa UNICEF Zanzibar Francesca Morandin ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar

Mwakilishi wa UNICEF Zanzibar Francesca Morandin akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Msaada wa Laptop 200 zenye thamani ya zaidi ya Shil.Millioni 400 kwa Wizara ya Afya Zanzibar ili zisaidie kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo. Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar.
Waziri wa Afya wa Zanzibar Mahmoud Thabit Kombo akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Msaada wa Laptop 200 zenye thamani ya zaidi ya Shil.Millioni 400 kutoka shirika la UNICEF ili kuimarisha usimamizi wa mfumo wa taarifa za Afya kwa wizara hiyo.Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar

……………..

KISHAPU KUWAHAMISHIA WALIMU WA SEKONDARI KUFUNDISHA SHULE ZA MSINGI KUONGEZA UFANISI

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akizungumza katika kikao cha kijadili namna ya kuboresha sekta ya elimu kwa ujumla. Wengine pichani kushoto ni Kaimu Afisa Elimu Sekondari, Paul Kasanda na mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Diwani wa kata ya Mwaweja, Makanasa Kishiwa.2
Washiriki mbalimbali wakiwemo maafisa elimu kata, walimu wakuu shule za msingi na sekondari na baadhi ya wanafunzi wakiendelea kufuatilia kikao hicho.
3
Mwenyekiti wa kikao hicho ambaye pia ni Diwani wa kata ya Mwaweja, Makanasa Kishiwa akizungumza. Kushoto ni Afisa Elimu Sekondari, Paul Kasanda
4
Afisa Elimu Msingi, Sostenes Mbwilo akisisitiza jambo kwa washiriki wa kikao hicho (hawapo pichani).
5
Kaimu Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Paul Sheka akichangia katika kikao cha wadau wa elimu.
6
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akisisitiza  jambo wakati wa kikao cha kujadili namna ya kuboresha sekta ya elimu wilayani humo.
7
Washiriki wakiendelea kufuatilia kikao hicho.
……………..
Na Robert Hokororo, Ofisi ya Mkurugenzi
Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu ipo katika mchakato wa kuwahamishia walimu wa ziada wa masomo ya sanaa wa shule za sekondari kwenda kufundisha shule za msingi zenye upungufu.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Stephen Magoiga wakati akizungumza katika kikao kikao kilichowakutanisha wadau wa elimu wilayani Kishapu kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta ya elimu ya msingi na sekondari ili kuboresha viwango vya ufaulu.
Alisema mchakato huo unafanyika kutokana na maelekezo kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ili kuboresha ikama ya walimu baada ya kubaini upungufu au ziada kwa kila shule.
Kwa mujibu wa takwimu kutokana na uhakiki kuna ziada ya walimu wa masomo ya sanaa kwenye shule za sekondari na upungufu wa walimu wa sayansi na hisabati katika shule za msingi.
Kutokana na changamoto hiyo kwa kuanzia Kishapu itaanza kuwahamisha walimu wa ziada sekondari na kwenda kufundisha shule za msingi zilizo karibu na kuwa uhamisho huo hautaathiri mishahara na stahiki nyingine za walimu.
Akifafanua zaidi Magoiga alisema kuwa hilo ni zoezi la kawaida na kuwa walimu wengi katika shule za sekondari wana vipindi vichache kulinganisha na wale wa msingi na hivyo litasaidia kuleta ufanisi bila kuathiri utendaji.
“Mwalimu wa sekondari nikikuhamishia shule ya msingi kufundisha usijisikie vibaya na kujiona kama nimekushusha bali nimekuongezea majukumu mengine kwa mamlaka niliyo nayo, na ntapita nihakikishe unakuwepo kituo nilichokupangia kufundisha,” alisisitiza.
Aidha alihimiza ushirikiano baina ya wadau wote wa elimu ili kuwepo na maandalizi mazuri kwa wanafunzi wafanye vizuri katika masomo yao huku akisema wazazi wanapaswa kushiriki kikamilifu katika malezi ya watoto wao.
Wakichangia kwa nyakati tofauti baadhi ya madiwani akiwemo Mh. Lucas Nkende wa kata ya Mwamashele alisema mahudhurio hafifu ya wanafunzi ndi changamoto zinazoporomosha kiwango cha ufaulu.
Alishauri pawepo na mfumo mzuri wa kusimamia wanafunzi huku akisisitiza mamlaka iangalie walimu wenye uwezo wa kufundisha wanafunzi wa madarasa ya chini ambapo ndio msingi wa elimu.
Kikao hicho kimehusisha waheshimiwa madiwani, Mkurugenzi Mtendaji, maofisa elimu msingi na sekondari kutoka makao makuu na kata, wakuu wa shule za msingi na sekondari, wanafunzi na wadau kutoka Programu ya Kuinua Ubora wa Elimu (Equip). 

WANANCHI KONDOA WAIOMBA SERIKALI IWAREJESHEE SEHEMU YA ARDHI YAO PORI LA AKIBA MKUNGUNERO

$
0
0
 Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Ikengwa, Nade Laida, akibubujikwa machozi wakati wa mkutano kati ya wanakijiji na msafara wa Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala kutokana na kile kilichoelezwa kuwa mwanamke huyo ni mmoja wa waathirika wa mgogoro baina ya Pori la Akiba Mkungunero na wananchi wa vijiji vinavyozunguka pori hilo.
 Mmoja wa wakazi wa kijiji cha Keikei Tangini ambaye jina lake halikufahamika mara moja, akiwa ameshikilia bango linaloeleza kuwa mipaka ya Pori la Akiba Mkungunero imesogezwa kwenye kijiji chao.
 Naibu Waziri wa Fedha na Mipango ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini, Dkt. Ashatu Kijaji (katikati)  akizungunza wakati wa mkutano ulioitishwa na Waziri wa Maliaasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala katika kijiji cha Keikei Tangini ili kusikiliza malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Pori la akiba Mkungunero kuhusu kumegwa kwa maeneno yao na Pori hilo, wilayani Kondoa mkoani Dodoma.


Wakazi waishio jirani na Pori la Akiba la Mkungunero lililoko Wilayani Kondoa mkoani Dodoma, wameiomba Serikali iwarejeshee eneo la kilometa 12 kuanzia kwenye vijiji vyao kwenda ndani ya Pori hilo ambalo wanadai limechukuliwa kinyemela na Wizara ya Maliasili na Utalii na kuathiri maisha yao yanayotegemea kwa kiasi kikubwa kilimo na ufugaji.

Wakazi wa vijiji vya Ikengwa, Keikei Tangini, Keikei na Kisondoko, wametoa maombi hayo mbele ya Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangala wakati alipofanyaziara katika vijiji hivyo vinavyozunguka Pori hilo la Akiba ili kutatua mgogoro wa muda mrefu baina ya Pori hilo na wananchi wanaolizunguka.

Wananchi na viongozi wa vijiji hivyo wameeleza kuwa uwekaji wa mipaka ya Pori hilo haukuwa shirikishi na kwamba maeneo makubwa ya vijiji yaliyokuwa yakitumiwa na wananchi kwa shughuli zao za kilimo, ufugaji na makazi yametwaliwa na kusababisha mgogoro huo.

Malalamiko mengine ya wananchi hao ni kunyanyaswa na watumishi wa Pori la Akiba Mkungunero kwa kupigwa, kunyang'anywa mifugo yao, na baadhi yao kudai kuumizwa na baadhi ya wenzao kuuawa kwa risasi na askari wanaolinda Pori hilo.

Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini Dkt. Ashatu Kijaji, ameiomba Serikali kutumia busara na kurejesha eneo lililochukuliwa kimakosa kutoka kwa wananchi ili waweze kujiendeleza kiuchumi na kuishi kwa amani na utulivu.

"Najua wewe ni mwadilifu ndio maana umeaminiwa na Mhe. Rais, najua utawatendea haki wananchi wa vijiji hivi ili nao wajione ni wananchi halali katika Taifa lao huru la Tanzania tukienda hatua kwa hatua bila kuvunja sheria za nchi" alisisitiza Dkt. Kijaji

Amefafanua kuwa maeneo yaliyochukuliwa na Pori hilo yalikuwa yakitumiwa na wananchi kwa muda mrefu na kwamba mchakato wa kupandisha hadhi eneo hilo kutoka Pori Tengefu hadi kuwa Pori la Akiba la Mkungunero haukuwashirikisha wananchi.

Akijibu Hoja za Wananchi hao, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamis Kigwangala, pamoja na kutoa elimu kuhusu umuhimu wa uhifadhi kwa ustawi na maendeleo ya nchi, aliwahakikishia wananchi hao kwamba Serikali itatafuta njia ya bora ya kuumaliza mgogoro huo kwa maslahi ya pande zote mbili, wananchi na Serikali.

"Ni lazima tutafute mahali ambapo tutabalance, maslahi ya umma na maslahi mapana ya Taifa zima na niwahakikishie kuwa tutafanyakazi hiyo kwa uadilifu, uzalendo mkubwa, lakini zaidi kwa kuzingatia maslahi yenu wananchi wenzetu" Alisisitiza Dkt. Kigwangala.

Awali, Meneja wa Pori hilo, Emmanuel Birasso, alieleza kuwa mchakato wa kuanzisha Pori hilo la Akiba Mkungunero ulifuata taratibu za kisheria za uanzishwaji wa mapori ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wananchi jambo ambalo linapingwa na wananchi hao.

Alieleza kuwa mpaka sasa takriban kilometa 118 za mpaka wote wa Pori umesimikwa alama za mipaka na kuwaondoa watu wanaodaiwa kuvamia Pori hilo pamoja na kuimarisha ulinzi na doria.

Pori Tengefu la Mkungunero (Game Controlled Area) lilipandishwa hadhi na kuwa Pori la Akiba la Mkungunero mnamo mwaka 1996 kwa Tangazo la Serikali (GN) namba 307, likiwa na ukubwa wa kilometa za mraba 743.95.

Serikali Haitaivunja Taasisi ya Elimu ya Watu wazima Kwa Kuwa Bado Inahitajika

$
0
0
Serikali imesema iko tayari kupokea ushauri wa namna bora ya kuimarisha utendaji wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) kwa kuwa azma ya Serikali ni kuendeleza Taasisi hiyo kwani bado inahitajika na madhumuni ya kuanzishwa kwake yana tija kwa Taifa.

Akizungumza wakati akijibu Hoja za Wabunge na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Waziri wa Elimu Sayansi na Teknplojia Profesa Joyce Ndalichako amesema kuwa Bado Taasisi hiyo inahitajika hivyo Serikali inaangalia namna ya kuiboresha na si kuivunja kama ilivyopendekezwa.

“ Taasisi ya Elimu ilianzishwa kwa lengo la kutoa elimu kwa wale waliokosa katika mfumo rasmi na pia kutoa mafunzo endelevu hivyo bado kuna umuhimu wa kuendeleza Taasisi hii” Alisisitiza Prof. Ndalichako.

Akifafanua Prof. Ndalichako amesema kuwa Taasisi hiyo inaweza kuimarishwa zaidi ili kuendana na mahitaji ya sasa ikiwa ni sehemu ya mikakati ya Serikali kuimarisha na kukuza kiwango cha elimu nchini.

Akizungumzia mikakati yakuimarisha elimu nchini Profesa Ndalichako amesema kuwa kwa sasa Serikali inafanya ukarabati wa Shule Kongwe hapa nchini, vyuo vya Ualimu, na Ujenzi wa maktaba yakisasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 2500 kwa wakati mmoja hiyo ikiwa ni sehemu ya miradi yakuboresha elimu inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii yalipendekeza kuwa TEWW ivunjwe ambapo Serikali imesema kuwa Bado Taasisi hiyo inahitajika na ina tija hivyo kitakachofanyika ni kuiboresha zaidi ili kukuza elimu hapa nchini na Si kuivunja kama ilivyopendekezwa.

Taasisi hiyo imeanzishwa kwa sheria namba 139 ya mwaka 1989 na iko chini ya Wizara ya Elimu Sayansi na Teknoloji.
Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akionesha kwa wabunge baadhi ya Vitabu vyenye ubora unaotakiwa kwa matumizi ya wanafunzi ikiwa ni moja ya hatua zilizochukuliwa na Serikali katika kuimarisha elimu nchini ambapo pia alibainisha kuwa Serikali haitaivunja Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima badala yake inaangalia namna bora yakuimarisha Taasisi hiyo.


Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akisisitiza jambo kwa wabunge wakati akijibu hoja za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Bungeni Mjini Dodoma.

WATAKIWA KUWEKA MIKAKATI ENDELEVU KUBORESHA AFYA ZA WANAOWAHUDUMIA

$
0
0
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo akiwahutubia wataalamu wa afya wa Jeshi la Polisi kutoka maeneo mbalimbali nchini wakati wa ufunguzi wa semina iliyofanyika katika hoteli ya SG Resort iliyopo jijini Arusha.
Baadhi ya wataalamu wa afya wa Jeshi la Polisi kutoka katika vituo mbalimbali nchini wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa mkutano huo ambayo ulifunguliwa na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo kwa niaba ya IGP.

Mgeni rasmi wa ufunguzi wa semina kuhusiana na VVU na UKIMWI kwa wataalamu wa vituo vya afya vya Polisi nchini Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa semina hiyo. Kulia kwake ni Mganga Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Dr. Charles Msenga na kushoto kwake (aliyevaa suti) ni Mkurugenzi wa AIDS FREE Dr. William Nyagwa.
Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha



Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Wataalamu wa afya wa Jeshi la Polisi wametakiwa kujiweka tayari katika kujadili changamoto na kuibua mikakati endelevu ili waweze kuboresha huduma za afya kwa watu wenye uhitaji, askari pamoja na familia zao.

Hayo yamesemwa leo asubuhi katika hoteli ya SG Resort iliyopo jijini hapa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, wakati wa ufunguzi wa semina ya siku mbili ya wakuu wa vituo tiba vya Polisi Tanzania pamoja na wafanyakazi na watumishi wa JSI kuhusiana na uboreshaji utoaji wa huduma za afya katika kukabiliana na jukumu la kupambana na uzuiaji wa maambukizi ya VVU na UKIMWI.

Alitoa wito kwa Madaktari, Wauguzi na watumishi wengine wanaofanya kazi katika Zahanati na vituo vya afya kuendelea kuwatambua wenye maambukizi ya VVU na UKIMWI kwa kuwapima, kuwaanzishia dawa na kuhakikisha wote walioanza matibabu wanaendelea kutumia dawa kwa kipindi chote cha uhai wao.

Kamanda Mkumbo aliendelea kuwakumbusha washiriki wa mkutano huo kuendelea kuwahudumia wananchi kwa uadilifu na utunzaji mkubwa wa siri za wateja wanaopatiwa huduma za VCT/CTC ikiwa ni sehemu ya kiapo chao juu ya taaluma yao.

Naye Mganga mkuu wa Kikosi cha Afya cha Jeshi la Polisi nchini Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Msenga, alisema kwamba lengo la semina hiyo ambayo inawezeshwa na JSI/AIDS FREE ni kujitathmini namna ya utoaji huduma bora kwa askari, familia zao pamoja na wananchi wengine wanaotumia vituo hivyo.

Alisema kwamba ubora wa huduma ambao wanatoa umekuwa ukiongezeka siku hadi siku ambapo wataalamu hao wa afya wamekuwa wakihakikisha kwamba wagonjwa wote wenye matatizo wanapatiwa dawa na walioacha dawa wanafuatiliwa na kuendelea kuhudumiwa.Alisema vituo vyao vya Afya vimekuwa vikitoa Ushauri Nasaha na Kupima (VTC) lakini pia kwa wagonjwa wamekuwa wakipata huduma za Uangalizi pamoja na kupewa dawa (CTC) hali ambayo imesaidia watu wengi kujitokeza kupima na kufahamu afya zao.

Awali akizungumza katika Semina hiyo iliyojumuisha washiriki 50 kutoka vituo mbalimbali vya afya vya Polisi nchini, Mkurugenzi wa AIDS FREE Dr. William Nyagwa, alisema kwamba shirika hilo lisilo la kiserikali linataka siku za usoni UKIMWI uwe historia na kuwataka wana semina hao kuendelea kujitoa kufanya kazi hiyo huku akiwahakikishia kwamba wao wapo nyuma yao.

Aidha alitoa wito kwa askari pamoja na familia zao kujitokeza kwa wingi kupata huduma kupitia vituo hivyo vya afya kwani kwa mgonjwa itakuwa rahisi kuhudumiwa na kuwahakikishia kwamba wataalamu wanaotoa huduma katika vituo vya afya wamekula kiapo hivyo wasiwe na wasiwasi juu ya usiri.Dr. Nyagwa alisema Semina hiyo pia itatoa uhuru kwa washiriki wote kuelezea changamoto zinazowakabili katika maeneo yao ya kazi ili ziweze kutatuliwa.

MGODI BUZWAGI WAZINDUA MAKTABA SHULE YA SEKONDARI BUGISHA KAHAMA

$
0
0
Mgodi wa dhahabu wa Acacia Buzwagi umezindua maktaba iliyogharimu shilingi milioni 22.4 kwenye shule ya sekondari Bugisha iliyopo katika kata ya Mondo wilayani Kahama mkoani Shinyanga kwa lengo la kusaidia wanafunzi na walimu kuchangia katika kuboresha ubora wa elimu inayotolewa.

Maktaba hiyo imezinduliwa leo Alhamis Februari 8,2018 na Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na kuhudhuriwa pia na Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu.

Hii ni maktaba ya pili katika wilaya ya Kahama kuzinduliwa na mgodi huo ambapo mwaka 2017 mgodi wa Buzwagi ulianzisha maktaba ya jamii katika kata ya Kagongwa ili kutoa rasilimali za elimu ya aina mbalimbali kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati uzinduzi huo, Meneja Mkuu wa Migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu,Benedict Busunzu maktaba hiyo itasaidia kuboresha upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi kutoka jamii inayouzunguka mgodi wa Buzwagi.
Alisema kupitia mpango wa Acacia wa maendeleo ya jamii wameamua kushirikiana na shirika la kimataifa la Read International kuboresha jengo moja la shule hiyo na kuliwekea samani kwa ajili ya matumizi ya maktaba.

“Read International ni wadau wetu wakubwa hasa katika masuala ya elimu na wamekuwa chachu ya kuleta maendeleo,kwa kutambua umuhimu wao tuliamua kukaa chini na kuamua kukarabati jengo moja na kulifanya maktaba ili vijana wetu wapate mahali pa kupatia maarifa zaidi”,alieleza.

Busunzu alisema Acacia itaendelea kuunga mkono sekta ya elimu nchini kwa njia ya kujenga miundombinu ya shule kama vile vyumba vya madarasa,nyumba za walimu,vyoo na maabara na kutoa misaada kwa wanafunzi kupitia vifaa vya elimu mfano vitabu,sare na ada kupitia programu ya CanEducate.

“Misaada inayotolewa na Acacia katika sekta ya elimu ni sehemu ya sera ya wajibikaji kwa jamii ya kampuni inayojikita katika kuhakikisha jamii inakuwa endelevu kupitia sekta ya elimu na sera hiyo inachangia moja kwa moja maono ya taifa hadi kufikia mwaka 2025 na malengo ya nchi ya kuleta maendeleo endelevu kwa kuhakikisha jamii inapata elimu iliyo bora”,alieleza.

Naye Mwakilishi wa shirika la Read International linalojihusisha na masuala ya elimu,Esther Kalwinzi mgodi wa Buzwagi ndiyo uliotoa shilingi milioni 22.4 kwa ajili kukarabati darasa kuwa maktaba.“Jumla ya vitabu 1,278 vimehifadhiwa katika maktaba hii ambayo itahudumia wanafunzi wapatao 290 na walimu 23 na jumla ya gharama za marekebisho ya jengo hili,vitabu na samani za maktaba ni shilingi 22,442,953”,alifafanua Kalwinzi.

Kwa upande wake,mgeni rasmi katika hafla hiyo,Mkurugenzi wa Mji wa Kahama,Underson Msumba aliushukuru mgodi huo kwa kuendelea kuwa karibu na jamii inayowazunguka na kushirikiana katika shughuli za maendeleo.

“Wakati mwingine huwa nafikiria bila mgodi Kahama ingekuwaje,kwa kweli mgodi umefanya juhudi nyingi katika kuboresha sekta ya elimu katika wilaya yetu,ninaamini uwepo wa maktaba hii utawafanya wanafunzi kufanya vizuri zaidi katika masomo yao”,alisema Msumba.

Aidha aliwataka wanafunzi kuzingatia masomo yao huku akisisitiza kuwa elimu ndiyo urithi pekee wa kudumu na wenye kubadilisha maisha yao.
Muonekano wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha lililoboreshwa na mgodi wa Buzwagi kwa kushirikiana na Read International - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba,meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu ,viongozi mbalimbali wa kata ya Mondo,walimu na wanafunzi wakiwa nje ya jengo hilo la maktaba kabla ya kuzinduliwa rasmi
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akikata utepe kuzindua rasmi jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha. Katikati ni Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu.Wa kwanza kushoto ni Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akifuatiwa na diwani wa kata ya Mondo Kija Peja
Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akionesha sehemu ya kuangalia orodha/aina ya vitabu vilivyopo katika maktaba hiyo
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia vitabu katika maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba na Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu wakisoma vitabu ndani ya maktaba ya shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Kahama,Underson Msumba akiangalia mandhari ya maktaba hiyo
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba,meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu ,viongozi mbalimbali wa kata ya Mondo,walimu na wanafunzi wakiwa nje ya jengo la maktaba baada ya uzinduzi
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba akiwasisitiza wanafunzi kuzingatia masomo yao
Meneja mkuu wa migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu Benedict Busunzu akielezea namna walivyoshirikiana na shirika la Read International katika kufanikisha ukarabati wa jengo hilo la maktaba
Mwakilishi wa shirika la Read International ,Esther Kalwinzi akizungumza wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa jengo la maktaba katika shule ya sekondari Bugisha
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kahama Mji Underson Msumba
Mkuu wa shule ya sekondari Bugisha Limbuzizi Magumba akiushuru mgodi wa Buzwagi kwa kutoa shilingi milioni 22.4 kwa ajili ya ukarabati wa maktaba katika shule yake
Wanafunzi wa shule ya sekondari Bugisha wakiimba shairi wakati wa hafla ya kuzindua maktaba katika shule hiyo
Mwanafunzi Tedy Martine akisoma risala akisoma risala kwa mgeni rasmi.Alizitaja miongoni mwa changamoto zilizopo katika shule hiyo kuwa ni upungu wa viti na meza hali inayowafanya wakae wawili wawili lakini pia upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi.
Diwani wa kata ya Mondo Kija Peja akiushukuru mgodi wa Buzwagi kwa kuendelea kusaidia jamii na kuomba ushirikiano uendelee kuwepo.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

SIDO YATANGAZA VITA KWA WADAIWA SUGU

$
0
0
 Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akitoa uamuzi wa wao kuwaweka kampuni ya udalali ya Yono Auction kwa ajili ya kwenda kukamata wadaiwa sugu wote. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Scholastica Kevela akitoa tamko la siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada kufidia deni. 
Meneja wa SIDO mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akiongoza wafanyakazi na viongozi wa Yono kupita mlango kwa mlango wakati wakizundua kampeni ya kudai madeni "LIPA DENI LAKO SIDO, KUWA MZALENDO'. 
Wakiingia katika moja ya ofisi za mdaiwa wa SIDO. 
Nae Mwenyekiti wa Kuatamia mawazo ya wabunifu, Joseph Mlay ameiunga mkono SIDO kwa hatua waliyochukua ya kuingia mlango kwa mlango katika kudai madeni yao. 

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoa wa Dar es Salaam imetangaza vita kwa wale wadaiwa sugu kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada. Kauli hiyo ameitoa leo jijini Dar es Salaam, Meneja wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga wakati akizindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wateja wao.

 "Leo tunazindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wadaiwa sugu wote wa SIDO hatutakuwa na huruma juu ya hili maana hawa ndiyo wanarudisha maendeleo ya shirika nyuma, kuna waliokopa, walipanga kama haujalipa deni lako ujue tunakupa siku 14 tu baada ya hapo sheria itachukua mkondo wake," amesema Mkurugenzi Maganga. 

Meneja Macdonald Maganga amesema wadaiwa ni wale waliopewa maeneo maalumu ya viwanda kwa ajili ya kufanyia kazi zao na waliopatiwa huduma ya fedha kwa mkopo na kushindwa kurejesha kwa wakati. “Kuna ambao wamekaa miaka mingi au miezi mingi bila kurejesha fedha kwetu kama shirika inatuathiri kwa sababu hatuwezi kuwahudumia wengine,” amesema Maganga. Maganga amesema wanadai jumla ya sh. milioni 350 kutoka kwa wadaiwa zaidi ya 77. 

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Scholastica Kevela amewashukuru SIDO kwa kuweza kuwapa kazi hiyo ya kuwakusanyia madeni na kuongeza kuwa hawata muonea huruma mdaiwa yeyote. 

Yono Auction Mart tunatoa siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada kufidia deni,". amesema Mama Kevela. 

“Kwa wadaiwa wote wa SIDO, wanaoishi kwenye viwanda na nyumba za SIDO bila kulipa pango, waliochukua mikopo na hawataki kurejesha kwa sababu wanazozijua wao, mkono wa Yono uko kazini ni vyema wakachukua hatua wakalipa ili kuondosha usumbufu,” amesema Kevela. 

Mdaiwa Masoud amedai hawafanyi makusudi kutolipa madeni ni kutokana na kodi kupanda kila mwaka huku hali ya biashara ikiwa mbaya. “Ukizingitia soko la ushidani na hali ya bidhaa unashindwa kuuza kwa wakati kwa hiyo tunalipa lakini hatulipi kwa wakati,” amesema. 

Amedai wamepangishwa kwa zaidi ya miaka 40 wakifanya shughuli zao na kama wangekuwa hawalipi kwa kipindi chote wangefukuzwa hivyo ameiomba serikali kutodhani kuwa wanapuuza kulipa madeni.

DC MATIRO AVUNJA KAMATI YA MAJI KATA YA DIDIA KWA UBADHIRIFU WA FEDHA

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ameivunja Kamati ya maji ya kata ya Didia iliyopo katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga kutokana na kufanya ubadhirifu kwenye mradi wa maji wa kisima kirefu. 

Kamati hiyo inadaiwa kutafuna pesa za mradi ulioanza kujengwa mwaka 2013/2014 na kukabidhiwa mwaka 2016 na kugharimu shilingi milioni 400.16 umeshindwa kuendelea kuhudumia wananchi mara baada ya kifaa kimoja kuharibika na kukosekana pesa za matengezo na kuufanya mradi kutaka kufa. 

Akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa kata ya Didia jana Februari 8,2018 mkuu wa wilaya aliamua kuvunja kamati hiyo na kuagiza wajumbe wa kamati hiyo wakamatwe. “Kamati hii kuanzia sasa nimeivunja na ninaagiza jeshi la jadi Sungusungu watu hawa watafutwe wakamate na wapelekwe Polisi sababu ni wahujumu uchumi na kisha wapewe muda wa kizirudisha pesa zote walizozitafuna kabla ya kuchukuliwa hatua zaidi za kisheria,” alisema Matiro. 

Hata hivyo mara baada ya kuivunja kamati hiyo ya maji, alisimamia zoezi la wananchi kuchagua viongozi wengine sita wa mpito kupitia mkutano huo wa hadhara kwa kuchaguliwa na wananchi wakiongozwa na mwenyekiti wake Katunge Njile, huku akiagiza viongozi wote wa vitongoji kuitisha mikutano ya hadhara na kuchagua wajumbe wawili wawili ambao wataunda kamati ya maji ya kudumu. 

Pia aliagiza kila kaya kwenye kata hiyo ya Didia yenye wakazi 4112 wachange shilingi 3000, fedha ambazo zitasaidia kununua kifaa kwenye mradi huo wa maji chenye gharama ya shilingi milioni 3.7, ili uanze kufanya kazi na kuondoa adha ya wananchi kutumia maji machafu sambamba na kumtua ndoo kichwani mwanamke. 

Naye aliyekuwa mwenyekiti wa kamati hiyo ya maji Selemani Msabaha, alikiri kuwa walishindwa kuendesha mradi huo mara baada ya pesa kukosekana ambapo mpaka sasa kwenye akaunti kuna shilingi 129,000. Kwa mujibu wa mkaguzi wa ndani wa halmashauri hiyo Sumbukeni Malela kamati hiyo ilikuwa ikikusanya hadi shilingi milioni 17 na walikuwa hawafanyi vikao na hakuna listi za manunuzi ya vifaa vinapoharibika na kwamba kiasi cha shilingi 984,600 hazijulikani zilipo. 
Mkuu wa wilaya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza na wananchi wa Kata ya Didia Shinyanga na kuivunja kamati ya maji kutokana na kufanya ubadhirifu wa fedha na kukwamisha mradi huo kutofanya kazi tena. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog 
Wananchi wa kata ya Didia wakimsikiliza mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro. 
Aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati ya maji iliyovunjwa kata ya Didia Selemani Msabaha akizungumza mbele ya Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro na wananchi na kukiri mradi huo wa maji Didia kuwa umeshidwa kuendelea kutoa huduma mara baada ya fedha za matengenezo Shilingi milioni 3.7 kukosekana 
Mkaguzi wa ndani wa halmashuri ya Shinyanga vijijini Sumbukeni Malela ,akieleza jinsi ubadhirifu wa fedha ulivyotumika kwenye mradi huo wa maji Didia.Picha zote na Marco Maduhu - Malunde1 blog

BoT YAWAASA WAANDISHI KUTOA UCHAMBUZI WA KINA TAARIFA ZA FEDHA ZA MABENKI

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi wa BoT, Tawi la Mtwara, Bi. Leticia Rweyemamu, akitoa hotuba ya kufunga semina ya sikju tano ya waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha, kwenye makao makuu ya tawi hilo Mkoani Mtwara leo Ijumaa Februari 9, 2018.


NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mtwara

SEMINA ya siku tano ya waandishi wa Habari za Uchumi, Biashara na Fedha iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania, Idara ya Uhussiano na Itifaki, imemalizika leo Februari 5, 2018 mkoani Mtwara.

Katika simian hiyo iliyofunguliwa mwanzoni mwa wiki na Naibu Gavana wa Benki Kuu anayeshughulikia Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC), Bw. Julian Raphael Banzi, waandishi hao wamejifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya mfumo mpya wa kuandaa Sera ya Fedha, (Financial Monetary Policy), mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia, mifuko ya dhamana kwa wajasiriamali na dhamana za serikali. 

Mambo mengine ambayo waandishi hao kutoka vyombo mbalimbali vikiwemo, Redio, Luninga, Magazeti na Blogs ni kanuni mpya za usimamizi wa bureaux de change, usimamizi wa mabenki na taasisi za fedha na dhamana kwa mikopo ya nyumba (Mortgage Finance). 

Waandishi hao pia wamepata wasaa wa kujifunza nafasi ya matawi ya BoT katika utekelezaji wa majukumu ya benki hiyo, fidia za interoperability katika kukuza huduma rasmi za fedha ili kujua kuna usalama gani wa fedha za wateja wanaotumia mifumo ya kufanya miamala ya kampuni za simu. 

Lakini pia wamejifunza kuhusu nafasi ya dodi ya ya amana katika ufilisi na kwa nini ulipaji fidia kwa wateja wa benki zilizofilisiwa unachukua muda mrefu, mafanikio na changamoto katika utekelezaji wa Sera ya Fedha Safi (Clean Money Policy), mafanikio na changamoto za dawati la kutatua malalamiko ya wateja wa benki na taasisi za fedha. 

Aidha waandishi hao pia walipata fursa ya kutembelea miradi ya kiuchumi inayotekelezwa na serikali na taasisi binafsi ya uchimbaji na uc hakataji wa gesi, huko Mnazi-Bay na Madimba. 

Akifunga semina hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa BoT tawi la BoT, Mkoani Mtwara, Bi. Leticia Rweyemamu, amewataka waandishi hao kutumia elimu waliyoipata ili kuhabarisha umma kwa usahihi kuhusu kazi za Benki Kuu, na kutumia faida waliyopata ya kukutana na wataalamu mbalimbali wa BoT ili wawatumie kupata ufafanuzi wa habari mbalimbali za kiuchumi ili kuandaa habari timilifu. 

“Nimejifunza kutoka kwenu kwamba ubora wa habari unategemea idadi ya watoa taarifa katika habari hiyo na ninatoa rai kuwa watumieni wataalamu hao ipasavyo ili kuzifanya taarifa zenu kwa wananchi ziwe bora zaidi.” Alisema Bi. Rweyemamu 

Aitoa wito kwa waandishi hao kutumia utaalamu kuelimisha umma kutumia huduma rasmi za kibenki ili kutunza fedha na kufanya miamala kwani ni muhimu kwa sababu licha ya kuhakikisha usalama wa fedha za mtyumiaji wa huduma hizo kuna uwezekano mkubwa wa kujikinga na upotevu wa fedha unaoweza kutokea kwa sababu mbalimbalin ikiwemo wizi. 

“Pia toeni uchambuzi wa kina kuhusu taarifa za fedha, (Financial Statements), za mabenki na taasisi za fedha ili kuwawezesha wananchi waliokuwa na amana au wangependa kuwekeza amana zao kuwa na taarifa sahihi kuhusu hali ya taasisi hizo ili kufanya maamuzi sahihi. 

“Haitoshi kuandika kuwa benki fulani imepata faida kiasi Fulani au hasara kiasi Fulani tu, ni vema wananchi wakapata taarifa mbalimbali zinazohusu ukwasi wa taasisi husimka, ikiwemo mali, madeni pamoja na mipango mbalimbali ya taasisi hizo za kifedha.” Alifafanua. 

Bi. Rweyemamu, amewahamasisha waandishi hao kutumia nafasi ya BoT kuhabarisha namna inavyoandaa na kutekeleza sera ya fedha ili kuhabarisha umma mwenendo wa uchumi na sekta ya fedha nchini ili hatimaye wafanye maamuzi sahihi ya kuhusu uwekezaji hapa nchini. 

Alivitaka vyombo vya habari kutumia nafasi kubwa katika kutoa taarifa zinazochangia maendeleo ya uchumi wa viwanda na kupunguza fursa kubwa inayotolewa kwa taarifa za kuburudisha tu, kwani kwa kufanya hivyo vyombo vya bhabari vitaisaidia serikali kuelezea mipango yake ya kueldekea uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025. 

“Kama alivyoeleza Naibu Gavana wakati akifungua semina hii, Benki Kuu inatambua mchango wa vyombo vya ahabari vyote ikiwemo redio, televisheni, magazeti na mitandao ya kijamii katika kutangaza habari za benki hiyo kwa manufaa ya umma.” Kwa upande wake, Kaimu Meneja Uhusiano na Itifaki wa BoT, Bi. Vicky Msina alisema BoT itaendelea kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari kwani kwa kufanya hivyo kunajenga uwezo wa waandishi kufanya uchambuzi wa taarifa mbalimbali na kuziandika kwa usahihi. 

“Nimefarijika sana kuwa pamekuwepo na uelewa mkubwa wa waandishi hawa kuhusu utekelezaji na majukumu ya Benki Kuu.” Alisema 
Kaimu Meneja wa Idara ya Uhusiano na Itifaki, BoT, Bi. Vicky Msina, akizungumza wakati wa hafla ya ufungaji wa semina hiyo.
Dkt. Suleiman Missango, Meneja Msaidizi-Idara ya Utafiti, Kurugenzi ya Sera za Uchumi na Utafiti, BoT, akiwasilisha mada kuhusu Government securities (Government Date Securities) , mwishoni mwa semina hiyo leo Februari 9, 2018.
Dkt. Suleiman Missango, Meneja Msaidizi-Idara ya Utafiti, Kurugenzi ya Sera za Uchumi na Utafiti, BoT, akiwasilisha mada kuhusu Government securities (Government Date Securities) , mwishoni mwa semina hiyo leo Februari 9, 2018.
Baadhi ya washiriki wakifurahia hotuba ya mgeni rasmi.
Bw. Abdueli Elinaza akitoa hotuba kwa niaba ya washiriki wa semina hiyo.
Meneja Msaidizi, Dawati la Kutatua Malalamiko ya wateja wa mabenki na taasisi za fedha, Benki Kuu ya Tanzania, (BoT) Bw.Ganga Ben Mlipano, akitambulishwa kwa wana semina kabla ya kuwasilisha mada ya mafanikio na changamoto za dawati hilo.
Meneja Msaidizi, Dawati la Kutatua Malalamiko ya wateja wa mabenki na taasisi za fedha, Benki Kuu ya Tanzania, (BoT) Bw.Ganga Ben Mlipano, akiwasilisha mada kuhusu mafanikio na changamoto za dawati la kutatua malalamiko ya wateja wa benki na taasisi za fedha.
Bw. Ganga akibadilishana maewazo na Bi.Vicky Msina, kabla ya kuwasilisha mada yake.
Mgeni rasmi, B. Leticia Rweyemamu, (kulia), akiongozana na Bibi.Leah Mzundu, Meneja Idara ya Uendeshaji Tawila BoT Mtwara, wakati akiwasili ukumbini kufunga semina.
Kutoka kushoto, Bi. Vicky Msina, Bi. Leticia Rweyemamu na Dkt. Suleiman Missango.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji na wana semina mwishonin mwa semina hiyo.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images