Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46395 articles
Browse latest View live

RAIS DKT MAGUFULI MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea jambo na Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Othman Omar Makungu, , Naibu spika Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mhe George Mkuchika katika picha ya pamoja na viongozi wa dini na Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama baada ya kuhutubia wakati wa maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Jaji Mkuu Profesa Ibrahim Juma na Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Othman Omar Makungu, , Naibu spika Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mhe George Mkuchika katika picha ya pamoja na Majaji Wastaafu baada ya kuhutubia wakati wa maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Makamu wa Rais wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) Mhe. Godwin Ngwilimi baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya mwaka mpya wa mahakama ama Siku uya Sheria kwenye uwanja wa Mahakama kuu Ocean Road jijini Dar es salaam leo.

Picha na IKULU

IGP SIRO MGENI RASMI UZINDUZI WA CHAMA CHA WAMILIKI WA MBWA

$
0
0

Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Canine Association Ltd (TCAL) Sinare Sinare, akizungumz na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, leo wakati akitangaza uzinduzi rasmi wa Chama cha Wamiliki wa Mbwa utakaofanyika katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni siku ya jumamosi,Januria 3,2018. Mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakuwa Inspector General wa Polisi (IGP) Simon Siro. Kushoto kwake ni Wajumbe wa Kamati ya uzinduzi huo, Felicia Bulu na Deo Rweyunga. (kushoto) ni Kamanda wa Polisi Kikosi cha Mbwa na Farasi, Dkt. Egyne Emmanuel. Picha na Muhidin Sufiani (MAFOTO).
Mkutano ukiendela....



Na Amina Kasheba, Dar (DSJ).

INSIPEKTA wa polisi (IGP) Simon Siro atanatarajia kuwa mgeni ramsi katika uzinduzi wa chama cha mbwa kilichoundwa na Tanzani Acanine Assoation limited (TCAL) wafuga mbwa wa Mkoa wa Dar es salaam.

Uzinduzi huo unatarajia kufanyika Febuari 3 mwaka huu na kushirikishwa na wasio kuwa wanachama ili kuleta ushirikiano katika masuala ya wafugaji Tanzania.

Akizungumza na mwandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo Dar es salaam jana, Mkurungenzi wa kampuni ya Tanzania Acanine Association Limited (TCAL) Dk. Sinare Sinare, alisema dhumuni ya kuanzisha chama hicho ni kuwakutanisha wadau mbalimbali na wamiliki wa mbwa Tanzania ili kujenga ushirikiano baina ya wanachama wenyewe kwa lengo la kusimamia na kushauri kuhusu uzalishaji mbwa bora.

Aidha alisema wameamua kuanza kuhamasisha ufugaji bora wa mbwa ikiwa ni pamoja na kushawishi ufugaji unaojali maslahi a faida ya wanyama mbwa katika jamii na kutoa ushauri wa jinsi ya kusimamia ili kupata zao bora la Mbwa. 

“Dhumuni la kuanzisha chama hicho ni kuwakutanisha wadau na wamiliki wa mbwa Tanzania, ili waweze kuwa na sauti ya pamoja kama wamiliki wa Mbwa Tanzania, Aliongeza kuwa katika uzinduzi huo hakutakuwa na kiingilio ambapo mtu yoyote anaruhusiwa kuhudhuria na kujionea michezo mbalimbali ya Mbwa na Farasi.

Katika kusherehesha uzinduzi huo pia kutakuwa na maonyesho mbalimbali kutoka Kikosi cha mbwa ambao wataonyesha uwezo wa mbwa wao katika kulinda uslama wa raia na mali zao, pamoja na michezo ya farasi. 

Baada ya uzinduzi huo itakuwa ni sehemu ya maandalizi ya maonyesho makubwa ya mbwa yanayotarajia kufanyika Juni 6 mwaka huu na kushirikisha washiriki kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

Mohammed Enterprises yazindua shindano la Pindua Ushinde

$
0
0
Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) imezindua shindano la Zawadi ya Chini ya Kizibo (UTC) la “Pindua Ushinde” litakalofanyika kwa muda wa siku 45, linalotarajiwa kuisha Machi 10 mwaka huu.

Akizungumza na wanahabari katika uzinduzi wa shindano hilo, Mkurugenzi wa Masoko MeTL, Fatema Dewji ameeleza namna ya kushiriki shidano hilo, kwamba ili ujishindie zawadi, inatakiwa kununua maji ya Mo Maisha na Masafi yenye ujazo kuanzia Mili lita 600 hadi lita 1.7.

“Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania tunawaletea shindano la zawadi ya chini ya kizibo kwa bidhaa za maji. Hii ni kwa maji ya Mo Maisha na Masafi yenye ujazo kuanzia Mili Lita 600, lita 1 na lita 1.7 ambazo huja kwako katika chupa za plastiki. hii haijawahi kutokea popote nchini Tanzania,” amesema.Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL), Fatema Dewji akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa shindano la Zawadi ya Chini ya Kizibo (UTC) la “Pindua Ushinde”

Amesema, Pindua Ushinde inakupa fursa ya kujishindia zawadi ya Maji ya bure au pesa taslimu kuanzia Sh. 1,000 hadi 100,000, ambapo ili kujionea ulichoshinda, unatakiwa kupindua kizibo cha chupa ya maji ya Mo Maisha au Masafi.

“Maji ya Mo Maisha na Masafi ni safi na salama kwa afya yako na hutayarishwa katika mazingira bora ya usafi wa hali ya juu. Pia,chupa zetu ni safi na salama zilizorafiki kwa matumizi yako zimetengenezwa ili kukidhi viwango vya kimataifa. Kumbuka unapokunywa maji yetu unajiepusha na magonjwa yanayoenezwa kwa maji yasiyo safi na salama,” amesema.


 
Vile vile, Fatema Dewji amezindua Kampeni ya kutunza mazingira inayofahamika kwa jina la “Tanzania Safi” iliyolenga kuhakikisha ardhi haiharibiwi kwa uchafu wa chupa za plastiki.

“Tutatoa ushirikiano kuondoa chupa za plastiki zitakazoonekana mitaani ili zitumike kama malighafi katika uzalishaji viwandani. Hii si mara ya kwanza kufanya kampeni za utunzaji mazingira, awali MeTL ilifanya kampeni ya utunzaji mazingira kwa kusafisha ufukwe wa Coco Beach," amesema na kuongeza.

“Pia tuliendesha kampeni ya kuelimisha jamii namna ya kuepuka magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya maji yasiyo safi na salama ambapo wataalamu wa afya walielimisha jamii.”

Naye Meneja Mauzo wa Kiwanda cha A 1 kilicho chini ya MeTL kinachozalisha Maji ya Mo Maisha na Masafi, Godfrey Mangungulu amesema washindi wa maji bure na fedha kuanzia 1,000 hadi 50,000 watapewa zawadi zao waliponunua maji, na watakaoshinda zaidi ya fedha hizo watachukua bidhaa zao kwenye Kiwanda cha A1 kilichopo Kurasini.
“Tumeamua kurudisha fadhila kwa jamii, kwa zaidi ya miaka 20 tunauza bidhaa zetu , hivyo tumeamua kurudisha sehemu ya mauzo ya bidhaa zetu kwa jamii. MeTL tuajivunia bidhaa bora na usambazaji wetu unafika nchi nzima,” amesema.

WATANZANIA WATAKIWA KUACHA KUTUMIA VIPODOZI VISIVYOKUWA NA KIWANGO

BALOZI WA CUBA NCHINI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA KAMISHNA JENERALI JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI.

$
0
0
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akisalimiana na Balozi wa Cuba hapa nchini, Profesa Lucas Domingo Hernades Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Cuba alifika Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Kamishna Jenerali mapema leo asubuhi tarehe 01/02/2018.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye aliyeketi (mbele) akisoma taarifa na changamoto zinazolikabili Jeshi hilo Balozi wa Cuba hapa nchini, Profesa Lucas Domingo Hernades Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Cuba alifika Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Kamishna Jenerali mapema leo asubuhi tarehe 01/02/2018.

Balozi wa Cuba hapa nchini, Profesa Lucas Domingo Hernades akizungumza jambo wakati mazungumzo yao na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye (kushoto), Viongozi Waandamizi wa Jeshi hilo hawapo pichani na Katibu wa Balozi na Mkalima, Sultan Hamud Said (Kulia) Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam. Balozi huyo wa Cuba alifika Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Kamishna Jenerali mapema leo asubuhi tarehe 01/02/2018.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akiwa katika picha na Balozi wa Cuba hapa nchini, Profesa Lucas Domingo Hernades Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam wengine ni Kamishna wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Michael Shija wanne kutoka (kulia), Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Billy Mwakatage wa kwanza (kulia) na Kamishna wa Usalama Dhidi ya Moto, Jesuald Ikonko wa tano kutoka (kulia). Balozi huyo wa Cuba alifika Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Kamishna Jenerali mapema leo asubuhi tarehe 01/02/2018.

Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye akiagana na Balozi wa Cuba hapa nchini, Profesa Lucas Domingo Hernades Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam mara baada ya kumaliza mazungumzo yao mapema leo asubuhi tarehe 01/02/2018.Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji).

WAKAZI ELFU 16 KONDOA VIJIJINI WAONDOKANA NA KERO YA MAJI

$
0
0
Mmoja wa akina mama wa kijiji cha Mauno, Kata ya Bumbuta, Jimbo la Kondoa Vijijini akiongea na vyombo vya habari kuhusu furaha yao baada ya kisima cha maji kuzinduliwa hatua iliyowaondolea kero ya kutembea mwendo mrefu kutafuta maji
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, na Mbunge wa Jimbo la KOndoa Vijijini, Dkt. Ashatu Kijaji (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na wafadhili wa mradi wa kisima cha maji pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali ya kijiji na viongozi wa dini katika kijiji cha Mauno, wilayani Kondoa.
Wanakijiji wa Kijiji cha Mauno Wilayani Kondoa mkoani Dodoma wakichota maji baada ya kuzinduliwa rasmi kwa kisima cha maji kilichojengwa na wafadhili kutoka nchini Uturuki kupitia Ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini.
Wanakijiji wa Kijiji cha Mauno Wilayani Kondoa mkoani Dodoma wakichota maji baada ya kuzinduliwa rasmi kwa kisima cha maji kilichojengwa na wafadhili kutoka nchini Uturuki kupitia Ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini.
Wakazi wa kijiji cha Mauno wakiwa wamemwangusha ng’ombe kwa ajili ya kupata kitoweo ikiwa ni namna ya kujipongeza na kusherehekea baada ya kuzinduliwa kwa kisima cha maji kilichojengwa na wafadhili kutoka nchini Uturuki.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango

Na Benny Mwaipaja, Kondoa

ZAIDI ya wakazi elfu 16 wa vijiji vitatu vya Mauno, Makiranya na Kinyasi-Majengo, katika Jimbo la Kondoa Vijijini mkoani Dodoma wameondokana na adha ya kukosa maji baada ya kuzinduliwa kwa visima viatu vya maji vilivyojengwa kwa msaada wa wahisani kutoka nchini Uturuki kupitia ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa visima hivyo katika Kijiji cha Mauno, Kata ya Bumbuta, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kondoa Vijijini Dokta Ashatu Kijaji, amesema kuwa kuzinduliwa kwa visima hivyo kunalifanya jimbo lake lifikishe visima 41 hatua ambayo amesema itapunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la maji katika jimbo lake.

Dkt. Kijaji ameushukuru Ubalozi wa Uturuki kwa kuratibu msaada huo wa zaidi ya Dola za Kimarekani elfu 36, sawa na shilingi milioni 81, zilizotumika kuchimba visima hivyo pamoja na kuweka miundombinu mingine zikiwemo jenereta zinazotumika kusukuma maji hayo na kuwezesha upatikanaji wa maji hayo.

“Hivi sasa ujenzi wa visima 15 kati ya 25 vinavyojengwa na Serikali kupitia Wizara ya Maji unaendelea huku wahisani wakiwa wametujengea visima 36 hivyo kufikisha idadi ya visima 61 katika kipindi cha miaka miwili tu tangu Serikali ya Awamu ya Tano ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli aingie madarakani hali ambayo haijawahi kutokea na lengo letu ni kuhakikisha kuwa vijiji vyote 84 vinapatiwa huduma ya maji ifikapo mwaka 2020” Alisisitiza Dkt. Kijaji

Diwani wa Kata ya Bunbuta Bw. Bashiru Mtolo na mkazi mmoja wa kijiji hicho Bi. Khadija Hussein wamesema kuwa tatizo la maji katika kijiji cha Mauno lilikuwa kubwa na kuwalazimisha wanawake na watoto kwenda umbali mrefu kusaka maji kwa ajili ya matumizi yao ya majumbani pamoja na kunywesha mifugo.

“Tunaushukuru Ubalozi wa Uturuki kwa msaada wao huu mkubwa na Mbunge wetu kwa ufuatiliaji wake wa karibu uliowezesha kupatikana kwa visima hivi na vingine ambavyo vimesaidia kwa kiwango kikubwa kutatua kero ya maji na tunaamini mpaka kufikia mwaka 2020, matatizo ya maji katika wilaya yetu ya Kondoa litakuwa historia” alisema Diwani Mtolo.

Naye Mwakilishi na Mwambata wa Ubalozi wa Uturuki hapa nchini Sheikh Muhammad Cicek ameeleza kuwa msaada wa Dola elfu 36 zilizotumika kujenga miradi hiyo mitatu ya visima vya maji umetolewa na wahisani mbalimbali wa Uturuki ikiwa ni kuenzi uhusiano wa muda mrefu kati ya Uturuki na Tanzania.

Alisema kukamilika kwa miradi hiyo ya maji kutasadia kuwawezesha akina mama na wananchi wa Kondoa kwa ujumla kufanya shughuli nyingine za maendeleo badala ya kutumia muda mwingi kutafuta maji ambayo hata hivyo hayakuwa safi wala salama.

UONGOZI WA CCM MKOA WA PWANI WALAANI VIKALI VITENDO VYA WATU WANAOHUJUMU ZAO LA KOROSHO

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani Ramadhani Maneno akizungumza jambo na baadhi ya viongozi wa chama kikuu cha ushirika (CORECU) hawapo pichani baada ya kufanya ziara katika ofisi zao kupata taarifa ya baadhi ya watu wanaohujumu zao la korosho.
Mwenyekiti wa chama kikuu vha ushirikika Mkoa wa Pwani (COORECU) Rajab Ng’onoma akitoa ufafanuzi kwa viongozi wa CCM Mkoa wa Pwani kuhusiana na mwenendo mzima wa zao la korosho pamoja na changamoto amabzo zinawakabili katika utendaji wao wa kazi.
Baadhi ya wajumbe wa bodi ya CORECU wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa chama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Pwani mara baada ya kumalizika kwa kutano wa kujadili masuala mbali mbali ya zoa la korosho.PICHA ZOTE NA VICTOR MASANGU




VICTOR MASANGU-PWANI

SAKATA la kuhujumu zao la korosho linalofanywa na baadhi ya wanunuzi,wakulima,pamoja na viongozi wa vyama vya ushirika hatimaye limechukua sura mpya baada ya uongozi wa chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani kuamua kuliingilia kati suala hilo kwa lengo la kuweza kuwabaini wale wote ambao wanahusika kwa namna moja au nyingine ili waweze kuchukulia hatua kali za kisheria.

Uamuzi huo wa CCM mkoa wa Pwani umekuja kufuatia kuwepo kwa taarifa ya kuibuka vikundi vya watu wachache ambao wana lengo la kukwamisha juhudi za serikali ya awamu ya tano kutokana na kuamua kufanya vitendo vya kuhujumu zao hilo kwa kuweka mawe,michanga, na takataka katika magunia ya korosho kitu ambacho ni kinyume kabisa na sheria na taratibu za nchi.

Akizungumza katika ziara ya kushitukiza katika ofisi za Chama kikuu cha ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) kwa ajili ya kupata ufafanuzi juu ya jambo hilo Mwenyekiti mpya wa CCM Mkoa Ramadhani Maneno alisema kuwa suala hilo limemchukiza sana hivyo hawezi kulifumbia macho na atalivalia njuga kwa lengo la kuweza kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya tano Dk. John Pombe Magufuli ya kupambana na watu ambao ni wezi na mafisadi.

“Sisi kama chama cha CCM mkoa wa Pwani tumeamua kuja hapa kwa ajili ya kupata maelekezo juu ya suala hili la baadhi ya watu ambao wanahujumu zao la korosho kwa kweli na kwa kuwa tunatelekeza ilani ya chama kwa kweli hatuwezi kulivumilia tutahakikisha tunashirikiana na vyombo vya dola katika kulifanyia kazi suala hili la kuwapata wale ambao wanajihusisha,”alisema Maneno.

Naye mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) kutokea Mkoa wa Pwani Haji Jumaa alisema kuwa lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanatekeleza ilani ya chama ipasavyo ili kuweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi wote hususan kuweza kuwatetea wakulima waweze kupata haki zao za msingi wanazostahili bila ya kuzulumiwa na watu wachache.

Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika Mkoa wa Pwani (CORECU) Rajab Ng’onoma amesema wamekuwa wanakabiliwa na changamoto ya kushuka kwa ubora wa korosho ambao umesababishwa na mambo mabali mbali yakiwemo ukosefu wa maghala ya kuhifadhia,ukosefu wa vifungashio,pamoja na baadhi ya vyama ya ushirika kupokea korosho mbichi hivyo kupelekea wanunuzi kugoma kununua na kujikuta wanadaiwa madeni makubwa.

HIVI karibuni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kujionea shughuli mbali mbali za mfumo unaotumika katika uuzaji wa zao la korosho aliweza kubaini kuwepo kwa baadhi ya magunia yaliyokuwa na korosho kuwekewa uchafu wa aina mbali mbali ukiwemo, mawe, mchanga, pamoja na matakataka mbali mbali.

KAMISHNA MKUU KICHERE AWATAKA WAFANYAKAZI SIRARI KUENDELEA NA UTOZAJI WA KODI STAHIKI

$
0
0
Na: Veronica Kazimoto-Sirari

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Charles Kichere amewataka Wafanyakazi wa taasisi mbalimbali wakiwemo wa mamlaka hiyo wanaofanya kazi katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha Sirari kilichopo wilaya ya Tarime mkoani Mara kufanya kazi kwa ushirikiano na kuhakikisha wanaendelea kutoza kodi stahiki.

Akizungumza wakati wa ziara yake kituoni hapo, Kamishna Mkuu Kichere alisema nchi inaendeshwa kwa kodi za ndani hivyo ni muhimu kila taasisi iliyopo eneo hilo kutimiza wajibu wake katika suala zima la ukusanyaji wa kodi.

“Wote mnajua umuhimu wa kodi na pia mnafahamu kuwa, kwa kupitia kodi hizi, Serikali inajenga miundombinu ya barabara, umeme, inasomesha wanafunzi, inajenga shule, inalipa mishahara ya wafanyakazi wake na mambo megine mengi. Hivyo, mfanye kazi kwa bidii na kwa weledi ili mkusanye kodi inayotakiwa kukusanywa kwa mujibu wa sheria bila kumuonea mtu yeyote.” alisema Kichere.

Kichere aliongeza kuwa, wafanyakazi wote kituoni hapo wana wajibu wa kukusanya kodi ili kuisaidia nchi kupiga hatua kimaendeleo kwa kutumia mapato yanayokusanywa nchini kupitia kodi mbalimbali.Aidha, Kamishna Mkuu huyo amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mara na Kamati yake ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Tarime kwa ushirikiano wanaoutoa kwa TRA.

“Nachukua fursa hii kukushukuru wewe Mhe. Mkuu wa Mkoa pamoja na Kamati yako ya Ulinzi na Usalama na pia napenda kumshukuru Mkuu wa Wilaya ya Tarime Mhe. Glorious Luoga kwa ushirikiano mkubwa mnaoutoa kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania,” amesema Kichere.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Malima alisema kwamba, mkoa wake umepanga utaratibu wa kufanya kikao kila mwezi ili kupitia taarifa ya ukusanyaji mapato mkoani humo.

“Kwa mkoa wa Mara kituo hiki cha Sirari ni muhimu sana na kina maslahi makubwa hususani katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali, hivyo sisi kama mkoa tumejipanga kila mwezi kukaa pamoja kupitia taarifa ya TRA ili kupata viashiria vya maeneo muhimu ya ukusanyaji mapato ndani ya mkoa wetu,” alisema Malima.

Naye Kaimu Meneja Msaidizi wa Forodha wa Mkoa wa Mara Laurent Kagwebe ameushukuru uongozi wa mkoa wa Mara kwa ushirikiano mkubwa wanaoutoa katika suala zima la ukusanyaji mapato mkoani humo na kusema kuwa ushirikiano huo ukiendelea, kuna dalili njema za kuongezeka kwa makusanyo hapo baadae.

“Nikili wazi kuwa, nimekuwa nikipata ushirikiano mkubwa sana kutoka kwa Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya mkoani hapa na kama ushirikiano huu ukiendelea, nina imani kuwa, makusanyo yataongezeka kwa kiasi kikubwa,” amefafanua Kagwebe.

Kituo cha Huduma kwa Pamoja cha Sirari kina jumla ya wafanyakazi 86 kutoka taasisi mbalimbali za Serikali ambapo pamoja na mambo mengine, wafanyakazi hao wana jukumu la kulinda afya za wananchi kwa kukagua bidhaa zinazoingizwa nchini kupitia kituo hicho, kulinda usalama wa raia pamoja na kukusanya mapato ya Serikali.

Klabu za Fema Hip zasema "Ukatili wa kijinsia sasa Basi"

$
0
0
Mkuu wa Maendeleo na Ushirika kutoka Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallstig akikabidhi zawadi kwa mwalimu Kahwa Mpunami wa Misungwi High ambao wameshinda (BEST FEMA CLUB OF THE YEAR 2017) Klabu Bora ya mwaka 2017 kutoka shule ya sekondari ya Myunzi Korogwe Tanga baada ya kutangazwa mshindi katika kipengele hicho katika kongamano la kujadili namna ya kupunguza ukatili wa Kijinsia kwa watoto wa kike likiwa na kauli mbiu ya "Ukatili wa Kijinsia sasa BASI" na kushirikisha Klabu mbalimbali za FEMA kutoka mikoa mbalimbali nchini Tanzania , Kongamano limemalizika leo na lilikuwa likifanyika kwenye hoteli ya Seascape Mbezi Beach jijini Dar es salaam kwa siku nne mfurulizo, Kongamano hilo limehusisha pia mafunzo ya mambo mbalimbali. , Katika picha anayeshuhudia ni Dr. Minou Fuglesang Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Femina Hip Tanzania.
Mkuu wa Maendeleo na Ushirika kutoka Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallstig akikabidhi zawadi kwa Mayombo Lutego ambaye ameshinda (BEST FEMA CLUB MENTOR OF THE YEAR 2017) .kutoka shule ya Sekondari ya Misungwi mkoani Mwanza baada ya kutangazwa mshindi katika kipengele hicho katika anayeshuhudia ni Dr. Minou Fuglesang Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Femina Hip Tanzania.
Upendo Abisai kutokamwanachama wa Youth For Change Project uliopo chini ya Plan International Tanzania akitoa mada katika kongamano hilo kutoka kushoto ni watoa mada wengine Lydia Charles Mtangazaji wa Kipindi cha Fema TV Show na Fema Radio Show, Mkuu wa Maendeleo na Ushirika kutoka Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallstig, Amabilis Batamula Mkurugenzi wa Habari Femina Hip na Koshuma Mtengeti Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Childrens Dignity Forum (CDF)
Koshuma Mtengeti Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Childrens Dignity Forum (CDF) akitoa mada katika kongamano hilo kutoka kulia ni Lydia Charles Mtangazaji wa Kipindi cha FEMA TV SHOW, Mkuu wa Maendeleo na Ushirika kutoka Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallstig na Amabilis Batamula Mkurugenzi wa Habari Femina Hip.
Nicodemus Nangale kutoka shule ya sekondari Minaki kulia na Patrick Okilindi kutoka Shule ya Sekondari Arusha wakisoma habari iliyomhusu mmoja wa vijana kutoka Mkoa wa Mara aliyebadilisha maisha yake baada ya kumnyanayasa mke wake kwa kumpiga mara kwa mara.
Amabilis Batamula Mkurugenzi wa Habari Femina Hip akichangia mada katika kongamano hilo.
Halima Shariff Mjumbe wa Bodi ya Femina Hip akijadiliana jambo na Lydia Charles Mtangazaji wa kipindi cha Fema TV Show na Fema Radio Show katika kongamano hilo kushoto ni Dr. Minou Fuglesang Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Femina Hip Tanzania.
Lydia Charles Mtangazaji wa kipindi cha Fema TV Show na Fema Radio Show na Mkuu wa Maendeleo na Ushirika kutoka Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallstig wakijadili jambo katika kongamano hilo kutoka kushoto ni Dr. Minou Fuglesang Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Femina Hip Tanzania na Halima Shariff Mjumbe wa Bodi ya Femina Hip.
mmoja wa wanachama wa Klabu za Fema Hip akiuliza swali kwa watoa mada wakati kongamano hilo lilikendelea.

Amabilis Batamula Mkurugenzi wa Habari Fema Hip akifafanua jambo katika kongamano hilo.



Baadhi ya wanafunzi shule mbalimbali za sekondari nchini kutoka klabu za Fema Hip wakifuatilia mada katika kongamano hilo.



Lydia Charles Mtangazaji wa kipindi cha Fema TV Show na Fema Radio Show akihitimisha mjadala katika kongamano hilo kabla ya kutoa zawadi kwa washindi mbalimbali.



Baadhi ya viongozi mbalimbali kutoka klabu za Fema Hip zilizopo katika shule za sekondari hapa nchini wakiwa katika kongamano hilo.



Baadhi ya wafanyakazi wa Femina Hip wakifuatilia mada katika kongamano hilo.



Mkuu wa Maendeleo na Ushirika kutoka Ubalozi wa Sweden nchini Tanzania Bw. Ulf Kallstig akizungumza na vijana mbalimbali wananchama wa klabu za Fema Hip wakati wa kongamano hilo.



Baadhi ya wafanyakazi wa Femina Hip wakifuatilia mada katika kongamano hilo.



Picha mbalimbali hapa chini zikionyesha baadhi ya wafanyakazi na wanafunzi wanachama wa klabu za Femina Hip wakiwa katika picha za pamoja.



...........................................................................

Kongamano la kumi la Fema Clubs kutoka kote nchini limemalizika leo jijini Dar es Salaam likiwa limekutanisha wanafunzi zaidi ya mia moja pamoja na walimu wao. Hawa ni wawakilishi kutoka mikoa yote ya Tanzania.

Hili ni tukio ambalo shirika la Femina Hip hulifanya kila mwaka kama sehemu ya kuwaongezea uwezo vijana wanachama wa Clubs za Fema na pia walimu wao walezi, katika kutekeleza azma ya kuleta mabadiliko ya tabia na kujenga kizazi kinachozingatia mitindo bora ya maisha.

Kila mwaka kongamano huongozwa na mada maalum, na kwa mwaka huu kauli mbiu ni Ukatili wa Kijinsia Sasa Basi. Kauli mbiu hii inaakisi mkazo unaowekwa na shirika pamoja na wadau wake kupambana na matukio na tabia ambazo huwaumiza watu kwa sababu ya jinsi zao. Toleo jipya la jarida la Fema limesheheni simulizi za kweli na uzoefu wa watu ambao ama walifanya ukatili au walifanyiwa, lakini sasa wanasimama na kutuhimiza sote kuukataa ukatili wa kijinsia. Toleo hili lilizalishwa pamoja na wadau mbalimbali ikiwemo UNICEF, CDF na Plan International, na kama anavyosema Mkurugenzi Mkuu wa Femina Hip, Dr Minou Fuglesang, “Juhudi zetu hizi ni sambamba na juhudi za serikali kutokomeza ukatili dhidi ya wananawake na watoto kama zilivyoainishwa katika mpango wa kitaifa uliozinduliwa mwaka jana.”

Mafunzo na mijadala ambayo ilifanyika wakati wa kongamano hili ililenga kuwaandaa wana Fema Club kuwa vinara wa mabadiliko, kuongoza mchakato muhimu wa kuelimisha jamii zao na kuhamasisha tabia zinazopingana na ukatili huu.

Femina Hip inaamini katika usawa, usawa wa kijinsia na kwamba hakuna mwenye haki ya kumbagua au kumuumiza mtu mwingine kwa sababu ya jinsi yake, rangi au kwa kuwa ana ulemavu.

“Tunaamini katika mabadiliko, mitazamo chanya na mabadiliko ya tabia. Ni jukumu la Femina Hip kuwawezesha vijana kupata taarifa zinazoweza kuwahamasisha kuleta mabadiliko chanya katika jamii zao, wakahoji mila zenye madhara na wakajenga kizazi chenye usawa na ustawi wa sasa na baadae,” anasema Amabilis Batamula, mmoja wa wawezeshaji.

Baada ya siku tatu za mafunzo na mijadala, siku ya nne ya kongamano ni siku ya kusherehekea mafanikio na kuwapongeza wale ambao walifanya vizuri zaidi mwaka jana, 2017. Tunzo zilitolewa kwa Club bora kitaifa, mwalimu mlezi bora wa club kitaifa, mtandao bora wa Club za Fema, mlezi bora wa mtandao wa Club za Fema na Club bora kwa kila mkoa.

Washindi na vipengele vilivyowapa ushindi ni kama ifuatavyo BEST FEMA CLUB OF THE YEAR 2017 ilijishindia Klabu ya MISUNGWI HIGH FEMA CLUB, MWANZA Katika kipengele cha BEST FEMA CLUB MENTOR OF THE YEAR 2017 amejishindia Bw. MAYOMBO CHARLES LUTEGO wa MNYUZI SECONDARY SCHOOL, TANGA na katika kipengele cha BEST FEMA CLUBS NETWORK imejishindia klabu ya KILIMANJARO FEMA CLUBS NETWORK na mwisho ilikuwa ni kipengele cha BEST FEMA CLUBS NETWORK MENTOR ambapo amejishindia Bw.RENATUS SANGI wa MARA NETWORK

IGP SIRRO MGENI RASMI UZINDUZI CHAMA CHA MBWA

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Canine Association Ltd (TCAL) Sinare Sinare, akizungumz na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo, leo wakati akitangaza uzinduzi rasmi wa Chama cha Wamiliki wa Mbwa utakaofanyika katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni siku ya jumamosi,Januri 3,2018. Mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakuwa Inspector General wa Polisi (IGP) Simon Siro. Kushoto kwake ni Wajumbe wa Kamati ya uzinduzi huo, Felicia Bulu na Deo Rweyunga. (kushoto) ni Kamanda wa Polisi Kikosi cha Mbwa na Farasi, Dkt. Egyne Emmanuel. Picha na Muhidin Sufiani (MAFOTO).
Mkutano ukiendelea.



Na Amina Kasheba, Dar (DSJ)

MKURUGENZI wa Kampuni ya Tanzania Acanine Association Limited(TCAL),Dk. Sinare Sinare amesema Februari 3 mwaka huu wanatarajia kuzindua rasmi Chama cha Mbwa nchini ambapo mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo atakuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Dk.Sinare amesema lengo la kuanzishwa kwa chama hicho ni kuwakutanisha wadau na wamiliki wa mbwa nchini ili wajenge ushirikiano miongoni mwao.

"Tunaomba wadau wote wakiwamo wanaofuga na wasiofuga mbwa tukajumuika pamoja.Pamoja na mambo mengine kwa kutumia chama hiki pia tutakuwa na kazi ya kusimamia na kushauri kuhusu uzalishaji wa mbwa bora,"amesema Dk.Sinare.

Ameongeza wanataka kuona wamiliki wa mbwa na wadau wote wanakuwa na sauti ya pamoja na siku ya uzinduzi hakutakuwa na kiingilio, mtu yoyote ataruhusiwa kuhudhuria na kujionea michezo ya Mbwa na Farasi,"amesema.

Akielezea zaidi kuhusu uzinduzi huo, Dk.Sinare amesema Kikosi cha Mbwa cha Polisi nacho kitaonesha uwezo wa mbwa wao katika kulinda usalama wa raia na mali zao.

"Baada ya kuzindua chama hicho tutaanza maandalizi ya kuandaa maonesho makubwa ya mbwa yatakayofanyika Juni 6 mwaka huu na nchi mbalimbali kutoka Barani Afrika watashiriki maonesho hayo,"amesema Dk.Sinare.


HALMASHAURI MASWA YASHAURIWA KUWEKEZA KIWANDA CHA BIDHAA ZA NGOZI

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akivaa viatu vilivyotengenezwa katika Kiwanda cha kutengeneza bidhaa za Ngozi kilichopo Senani Wilayani Maswa wakati wa Ziara yake ya kukagua viwanda vidogo wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka(wa tatu kushoto) akiwa pamoja na viongozi wakuu wa Wilaya ya Maswa wakielekea katika Kiwanda kidogo cha kutengeneza bidhaa Ngozi katika Kijiji cha Senani kata ya Senani wakati wa ziara yake ya kukagua viwanda vidogo wilayani humo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kushoto) akifuatilia hatua mbalimbali za utengenzaji wa viatu vya ngozi kwenye kiwanda cha kutengeneza bidhaa ngozi kilichopo Kijiji cha Senani kata ya Senani wakati wa ziara yake ya kukagua viwanda vidogo wilayani Maswa.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (kushoto) akizungumza na baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Njiapanda wilayani Maswa, wakati alipotembelea eneo ambalo kitajengwa kiwanda kidogo cha kutengeneza ungalishe kitakachomikiwa na shule za Msingi 30 za Maswa,wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda vidogo wilayani humo.

………………….

Na Stella Kalinga, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu

Halmashauri ya Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu imeshauriwa kuwekeza katika kiwanda cha kutengeneza bidhaa za ngozi ikiwemo viatu, mikoba na mikanda kinachomilikiwa na kikundi cha Usindikaji Ngozi Senani kilicho kata ya Senani wilayani Maswa, ili kuongeza thamani ya ngozi zitokanazo na mifugo.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda vidogo katika wilaya MASWA.

Mtaka amesema katika kutekeleza Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano ya Tanzania ya Viwanda , Halmashauri ya Maswa inapaswa kuwekeza katika viwanda vinavyoanzishwa na vikundi ili kuviwezesha katika upatikanaji wa malighafi ya kutosha, kuongeza thamani ya mazao ya mifugo pamoja na kilimo ili viwanda hivyo viweze kuzalisha kwa tija.

“Tungehitaji kuwa mkoa ambao utawekeza sana katika viwanda vidogo na ndiyo maana tulianza dhana ya Wilaya moja bidhaa moja kiwanda kimoja na sasa tunakwenda kwenye Kijiji Kimoja Bidhaa Moja Kiwanda kimoja; tunataka kupunguza uagizwaji wa bidhaa kutoka nje ya Mkoa” alisema Mtaka.Aidha, ameitaka Halmashauri hiyo kuwasaidia wanakikundi kuweka mifumo mizuri ya kutengeneza soko la bidhaa zinazozalishwa katika kiwanda hicho ikiwa ni pamoja na kuuza katika minada yote ya wilaya hiyo na kuimarisha soko la nje.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt.Fredrick Sagamiko amesema Halmashauri itahakikisha kiwanda hicho kinapata malighafi ya kutosha ambapo amebainisha kuwa Halmashauri imeingia mkataba na Chuo cha DIT Mwanza kuhakikisha kuwa inazalisha malighafi(ngozi) kwa wakati kwa ajili ya kiwanda hicho.

Akiwa Malampaka ambapo alitembelea Mradi wa Ghala na Mashine ya kukoboa mpunga na kupanga madaraja, Mtaka amekipongeza Chama cha Ushirika Bumala AMCOS kwa kuanzisha kiwanda, huku akiwataka wananchi wa eneo hilo kujiandaa kiushindani katika biashara, kwa kuwa hivi karibuni Serikali inatarajia kuanza ujenzi wa bandari ya nchi kavu itakayoenda sambamba na ujenzi wa Reli ya Kisasa(Standard Gauge).

“Ni lazima mjiandae kiushindani katika biashara, miaka mitatu ijayo katika Mipango ya Serikali Malampaka haitakuwa kama ilivyo, hapa ni mahali ambapo Standard Gauge ikianza bidhaa zitakuwa zikisafirishwa kwa wingi; nimeshaongea na Mkurugenzi kuwa eneo hili lipimwe na Halmashauri imiliki eneo la uwekezaji” alisisitiza Mtaka.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka alitembelea eneo la ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza ungalishe katika Kijiji cha Njiapanda, ambacho kitamilikiwa na shule 30 za Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, kinachoanzishwa kwa lengo la kuongeza kipato cha shule na halmashauri, kutoa ajira kwa wananchi na kuboresha lishe za watu.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Afisa Elimu Msingi Wilaya ya Maswa, Mwl. Mabeyo Bujimu amesema shule za msingi 30 wilayani humo zitanufaika kwa kulima viazi lishe na kukiuzia kiwanda hicho kama malighafi pamoja na kuuza bidhaa zitakazozalishwa na kiwanda.

Huu ni mwanzo wa ziara ya Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ambayo amepanga kutembelea viwanda vidogo vilivyopo katika wilaya zote za mkoa huo.

RC RUVUMA AWATAKA VIONGOZI WA DINI KUSIMAMIA VYEMA MAADILI YA WAUMINI WAO

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa RUVUMA BI CHRISTINA MNDEME amewataka viongozi wa dini mkoa humo kusimamia vyema maadili ,unywaji pombe uliokithiri pamoja na matumizi ya madawa ya kulevya amesema hayo wakati akizungumza na viongozi wa dini katika ikulu ndogo mjini songea habari kamili hii hapa video yake

UHAMIAJI YATOA UFAFANUZI KUHUSU 'UZUSHI'UNAOENEZWA KWENYE MITANDAO YA KIJAMI

TAARIFA YA UPIMAJI KANSA KWA WENYE UALBINO

$
0
0

Kaka na dada wetu,

@imetoshafoundation wa kushirikiana na Umoja wa watu wenye ualbino Tanzania, na Taasisi ya Kansa ya Ocean Road, tumeandaa upimaji wa Kansa kwa watu wenye ualbino waishio jijini Dar es Salaam ikiwa ni jitihada zetu katika kujaribu kupunguza vifo vya watu wenye ualbino vinavyosababishwa na saratani ya ngozi. 

Watu wengi hufariki baada ya kugundua ugonjwa ukiwa umwshaenea mwilini, na inawezekana kuutibu ukiwa bado haujafikia hatua mbaya.
Hivyo basi kama unamjua mtu mwenye ualbino umpe taarifa kwamba kuna upimaji wa BURE Ocean Road kwa siku mbili, ili kutambua afya yake na kuanza kupata tiba kabla ugonjwa haujamuathiri.
Sambaza ujumbe, tuokoe maisha

KAIMU KATIBU IDARA YA VYUO,VYUO VIKUU AKABIDHI KADI 1500 KWA KATIBU HAMASA SENETI YA DAR

$
0
0
Kaimu Katibu wa Idara ya Vyuo na Vyuo Vikuu Ndugu Daniel Zenda akikabidhi  kadi 1500 za wanachama wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kwa Katibu wa Hamasa Seneti ya mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Juakali Kuwanya katika hafla iliyofanyika leo Makao Makuu ya UVCCM, Upanga  jijini Dar es Salaam.

Zenda amesema, kadi hizo amezikabidhi ili zigawiwe kwa wananchama wapya ambao wamekuwa wakijiunga kwa wingi katika Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake, kutokana na mwamko mkubwa wa wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuunga mkono CCM kutokana na kuvutiwa na Utendaji kazi  wa Rais John Magufuli na Serikali yake ya awamu ya tano

Imetolewa na 
Uvccm Seneti Mkoa Dsm.

maadhimisho siku ya maahakama yafana Njombe

$
0
0
Mawakili wa Kujitegemea Mkoani Njombe Wamewatupia Lawama Watoa Maamuzi Katika Muhimili wa Mahakama Kwakuwa na Visingizio Mbalimbali Vinavyosababisha Mashauri ya Watuhumiwa Kuahirishwa Mara Kwa Mara na  Kusababisha Kuongeza Gharama Katika Uendeshaji  Kesi.

Akitoa taarifa katika Maazimisho ya  Kilele Cha Wiki ya Sheria Ambayo Kimkoa Imefanyika Katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Njombe Wakili wa Kujitegemea Bwana Barnaba Mwangi Kupitia Taarifa ya Chama Cha Wanasheria Afrika Mashariki Anasema Miongoni Mwa Changamoto Kubwa Inayowakwamisha ni Visingizio Vinavyofanywa na Baadhi ya Mahakimu Kwa Kuahirisha Kesi Mara Kwa Mara Bila Sababu za Msingi Jambo Linalo Minya Upatikanaji wa Haki Kwa Wakati.

John Kapokolo ni Hakimu Mfawidhi  wa Makahama ya Hakimu Mkazi Njombe Ambaye Anasema Kuwa Mfumo Mpya wa TEHEMA Utakapoanza Kufanya Kazi Katika Muhimili wa Mahakama Kama Ambavyo Kauli Mbiu ya Wiki Sheria Inasema Basi Huenda Ikawa Muarobaini wa Kupatikana Kwa Haki Kwa Wakati na Kwa Weledi Mkubwa.
Miongoni Mwa Changamoto Zilizotajwa na Hakimu Kapokolo Katika Taarifa Yake ni Pamoja na Gharama Kubwa ya Upimaji wa Maeneo ya Mahakama za Mwanzo Hoja Inayotolewa Majibu na Mgeni Rasmi Katika Maazimisho Hayo Mkuu wa Mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka.

Baadhi ya Wadau Mkoani Njombe Akiwemo Mexon Sanga Hapa Anasema Anaamini Mfumo wa TEHEMAUtakwenda Kusaidia Sana Katika Upatikanaji wa Haki Kwani Hata Yeye Amekuwa Muhanga wa Namna Vyombo Vya Dola Vinavyo Shindwa Kuheshimu Muhimili wa Mahakama na Kuwakandamizi Wananchi.
Kaulimbiu ya Wiki ya Sheria Kwa Mwaka Huu Inasema ''Matumizi ya TEHEMA Katika Utoaji Haki Kwa Wakati na Kuzingatia Maadili"Kaulimbiu Inayokwenda Kuweka Bayana Kila Ushahidi Unaotolewa Mahakamani Kwa Njia ya Kunakiliwa Kwa Sauti na Video Bila Ubabaishaji Kama Inavyofanyika Katika Vikao Vya Bunge.

HOTUBA YA RAIS DKT.JOHN MAGUFULI KWENYE SHEREHE YA MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA MAHAKAMA

Tatu Mzuka yazindua kampeni ya Valentine, ‘Ukishinda, Unayempenda naye Anashinda’

$
0
0
 Mkuu wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, Sebastian Maganga,akizungumza mapema leo mbele ya Waandishi wa Habari kuhusu kampuni hiyo kuzindua kampeni mpya ya Valentine  ‘Ukishinda, Unayempenda naye Anashinda’  , ambayo inaanza rasmi leo hadi februari 18,2018.Pichani kulia ni Msanii wa muziki wa kizazi kipya aitwae Nandy pamoja na Aslay (kushoto) ambao wamechaguliwa kuwa mabalozi wa kampeni hiyo
 Msanii mahiri wa Muziki wa Kizazi kipya Aslay akighani moja ya wimbo walioimba pamoja na msanii mwenzake aitwaye Nandy 'subah lakheri' kama sehemu ya kionjo kwa wanahabari walioshiriki mkutano huo mapema leo jijini Dar.
 Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia yaliyokuwa yakijadiliwa kwenye mkutano huo
 Wasanii mahiri wa muziki wa kizazi kipya Aslay na Nandy kwa pamoja wakiimba wimbo wao wa 'subah lakheri'mbele ya wanahabari waliofika kwenye mkutano huo mapema leo jijini Dar
 Picha ya pamoja


• Zaidi ya milioni 300 kutolewa katika msimu huu wa Valentine

 Kampuni ya mchezo wa bahati nasibu, Tatu Mzuka, leo wamezindua kampeni mpya ya Valentine, ambayo inaanza rasmi leo hadi tarehe 18 ya mwezi wa pili.

Kampeni hiyo yenye kauli mbiu, ‘Ukishinda, Unayempenda Naye Anashinda’ imelenga kuhakiksha inashamirisha msimu wa Valentine kwa watanzania kupata fursa ya kujishindia mamilioni lakini pia wawapendao pia kupata fursa ya kushinda.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkuu wa Mawasiliano wa Tatu Mzuka, bwana Sebastian Maganga, alisema Tatu Mzuka imekuwa na utaratibu wa kuwa na kampeni zinazoendana na misimu ya sherehe za kitanzania.

‘Kwa msimu huu wa Valentine peke yake, zaidi ya shilingi MILIONI 300 zitatolewa kwa washindi wetu watakaocheza kuanzia tarehe 1 hadi 18 ya mwezi huu’ alisema Maganga.

Kama sehemu ya kampeni hiyo pia, Maganga alisema pia KILA SIKU kwa siku 18 kiasi cha MILIONI 10 zitakuwa zinatolewa, ambapo MILIONI 5 itakuwa ya mshindi na MILIONI 5 itakuwa ya mtu ambaye mshindi atamchagua.

‘Lakini pia kubwa kuliko, ukicheza kuanzia leo hadi tarehe 18 utapata pia fursa ya bure kuingia kwenye Valentine SUPA MZUKA Jackpot, ambapo mamilioni yatatolewa kwa washindi, ambapo pia mamilioni ya ziada yatakwenda kwa wanaowapenda’ alisema Maganga.

Kwa upande mwingine, Maganga aliwatambulisha Aslay na Nandy kama mabalozi wa kampeni hii, ambao pia watakuwa na matamasha makubwa katika msimu huu wa Valentine ambayo yatafanyika katika mikoa ya Tanga, Arusha na Dar.

‘Tunaomba mashabiki wetu wacheze Tatu Mzuka katika kipindi hiki, kwani wakishinda pia watapata fursa ya kuhudhuria matamasha yetu pamoja na kukaa sehemu ya watu maalumu pia watapata fursa ya kupiga picha na sisi na mambo mengine kibao’ alisema Aslay.

Akizungumza katika uzinduzi huo, msanii Nandy alisema anaamini kila mtu ana mtu anayempenda na ndio maana amefurahia kampeni hii kwani inawakumbusha watannzia misingi yetu ya upendo.

Namna ya kucheza Tatu Mzuka kipindi hiki cha Valentine ni rahisi kwa kutuma shilingi 500 hadi 30,000 kwenda namba ya kampuni 555111, na kumbukumbu namba ni namba zako tatu za bahati zikufuatiwa na neno PENDA, na hiyo itakupa fursa za kushinda kila saa, kila siku na pia kuingia kwenye SUPA MZUKA JACKPOT pamoja na kupata fursa ya kuhudhuria matamasha ya Nandy na Aslay.

WAZIRI MPINA AKAMATA MELI YA MALAYSIA , AIPA SIKU SABA KULIPA FAINI MILIONI 770/-

$
0
0
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amekamata meli ya uvuvi mali ya Kampuni ya Buah Naga 1 ya nchini Malaysia na kuitoza faini ya Dola za kimarekani 350,000 sawa na Sh.milioni 770 kwa kosa la kukutwa na mapezi ya samaki aina ya papa yenye uzito wa kilo 90 bila miili yake.

Ambapo hiyo ni kinyume cha Kanuni ya 66 ya kanuni za Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu pamoja na kifungu cha18 (2) cha Sheria ya Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu ya mwaka 1998 na marekebisho yake ya mwaka 2007.

Meli hiyo ilikamatwa Januari 26 mwaka huu baada ya kufanyika ukaguzi uliosimamiwa na kikosi maalum cha kupambana na kudhibiti uvuvi haramu na utoroshaji wa samaki na mazao yake wakati ikifanya shughuli za uvuvi katika ukanda wa Bahari Kuu kati ya Mkoa wa Lindi na Mtwara.Pamoja na kukutwa na mapezi hayo ya papa, meli hiyo ilikutwa pia na bastola aina ya Bereta ikiwa na risasi 10 bila ya kuwa na nyaraka za umiliki wake.

Akizungumza mjini Mtwara ambako meli hiyo ndiko inakoshikiliwa na Serikali Waziri Mpina ameagiza fedha hizo zilipwe ndani ya siku saba huku akitoa onyo kali kwa wamiliki wa meli waliopewa leseni za uvuvi wa Bahari kuu kufuata masharti ya vibali vyao na katika zama hizi za utawala wa Rais, Dk.John Magufuli watachukuliwa hatua kali zaidi.

"Enzi za Serikali ya Awamu Tano ya Rais Magufuli mtakaguliwa na kupekuliwa kuliko wakati wowote, hivyo ni vizuri mkatii sheria za nchi kwa mujibu wa leseni zenu,"amesema Mpina huku akisilizwa na Kapteni wa meli hiyo Han Ming Chuan  raia wa Taiwan.

Mpina amesema meli hizo zimekuwa zikitumika pia kufadhili biashara nyingine haramu ikiwemo kusafirisha dawa za kulevya ,usafirishaji haramu wa  binadamu na biashara ya silaha.Pia zinatumika kutorosha nyara za Serikali ikiwemo meno ya tembo, samaki na madini.

Aidha Waziri Mpina amesema kitendo cha wamiliki wa meli hiyo kuwakata samaki hao mapezi na kisha kutupa miili yao baharini kimeleta athari kubwa kwa Taifa kwani samaki hao wangeweza kutumika kwa matumizi mengine ya binadamu na kuchochea uchumi wa nchi.

Hivyo, ameridhia faini hiyo iliyotozwa na Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu ya Sh.milioni 770 na kuagiza kilo 90 za mapezi ya samaki na samaki wasioruhusiwa wataifishwe na kugawiwa kwa wananchi wa maeneo jirani ya Manispaa ya Mtwara. "Siku nyingine Serikali ikikamata meli iliyofanya makosa ya aina hiyo itataifishwa pamoja na vitu vyote vitakavyokuwemo kwa mujibu wa Sheria za nchi,"amesisitiza.

Waziri Mpina ameagiza wenye meli hizo kuzingatia masharti ya leseni zao zinazotaka kuwepo na asilimia 10 ya mabaharia wa kitanzania ndani ya meli zinazoingia kuvua katika Bahari kuu upande wa Tanzania.

Kwa upande wa Kamishna wa Oparesheni wa Mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za kulevya, Luteni Kanali Fredrick Milanzi amesema meli hiyo baada ya kukaguliwa imekutwa na mapezi kilo 90 ya samaki aina ya papa na bastola yenye risasi 10 ambayo inaendelea kushikiliwa na Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Mtwara hadi hati za umiliki zitakapowasilishwa.

Pia mwenye meli atatakiwa kuhakikisha anawasafirisha mabaharia kurudi nchi zao kwa madai hawataki kuendelea kufanya kazi kutokana na kukiukwa kwa mikataba yao ya kazi.Aidha samaki wasioruhusiwa kuvuliwa kwa mujibu wa leseni ya uvuvi iliyopewa meli hiyo ( Bychatch) watabaki kuwa ni wa Tanzania na watauzwa kwa mnada na fedha zitakazopatikana kiasi cha sh milioni 12 zitaingizwa kwenye Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu (DSFA).

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bahari Kuu, Hosea Mbilinyi amesema hatua zinachukuliwa kwa sasa zimelenga kudhibiti uvuvi haramu na utoroshaji wa samaki na mazao yake nje ya nchi na kwamba operesheni hizo ni endelevu na hazitambakiza mtu hata mmoja.

Wakati huohuo, Wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Divisheni ya Mashtaka Makao Makuu Dar es Salaam, Wankyo Simon amesema makosa hayo adhabu yake ni kubwa na wanapaswa kuzingatia muda uliotolewa na Waziri wa kulipa faini.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina pamoja na Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Mtwara Francis Mkuti wakionesha baadhi ya Samaki waliovuliwa na Meli hiyo.
 Hosea Mbilonyi Kaim Mkurugenz mamlaka ya Usimamiz wa Bahari Kuu  DFSA akimuonesha waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina shehena ya Samaki  tani 4.5 wasiotakiwa kuvuliwa ambao wanatakiwa Kupigwa Mnada Siku Yoyote.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akilekea katika Meli Buah Naga one kukagua Samaki walivuliwa kinyume na Taratibu..

Rais Magufuli afanya uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Viewing all 46395 articles
Browse latest View live




Latest Images