Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

Rais Magufuli amtumia salamu za Rambirambi Mhe. Rais Kenyatta kufuatia ajali ya barabarani


SALAMU ZA MWAKA MPYA KUTOKA KWA MHE. NAIBU WAZIRI WA AFYA Dkt. Faustine Ndugulile

$
0
0
SALAMU ZA MWAKA MPYA ZA MHE. NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO ZIKISISITIZA JUU YA WAJIBU WA WATOA HUDUMA ZA AFYA NA MABARAZA YA KITAALUMA PAMOJA NA HAKI ZA WANANCHI KUPATA HUDUMA BORA ZA AFYA.
Ndugu Wananchi,
Nachukua fursa hii kuungana nanyi nyote kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutufikisha salama siku hii ya leo tunapoanza mwaka mpya 2018. Hii ni neema pekee ambayo Mwenyezi Mungu  ametujaalia  kwani kuna wengi walitamani kuifikia siku hii lakini hawakubahatika. Hivyo, nawatakieni nyote kheri na fanaka katika mwaka huu mpya.
Napenda kutumia fursa hii pia kuwashukuru na kuwapongeza Wanataaluma na Watoa huduma za afya wote kwa kuendelea kutoa huduma kwa ari, juhudi, uaminifu na uadilifu licha ya changamoto mbalimbali wanazokutana nazo katika utendaji kazi wa kila siku.  Nami nawatia shime na hamasa ili muendelee na moyo huo wa kuwahudumia na kuwatumikia Wananchi.
Natambua kuwa  Sera yetu ya Afya inataka tuijenge jamii yenye afya bora na ustawi ambayo itachangia kikamilifu katika maendeleo ya mtu binafsi pamoja na yale ya Taifa.  Aidha, Sera na Sheria zetu mbali mbali zinatambua umuhimu na nafasi ya Mabaraza ya kitaaluma katika kuboresha na kusimamia viwango vya maadili ya wanataaluma walio chini ya Wizara yangu. Jambo hili ni muhimu sana hususan tukizingatia ongezeko la minong’ono, manung’uniko na hata malalamiko kutoka kwa wananchi dhidi ya baadhi ya  watoa huduma ambao wanakiuka taratibu au miiko ya kazi zao na hivyo kuathiri ubora wa utoaji huduma.
Nimeona kama sehemu ya salamu zangu za mwaka mpya wa 2018, nitoe maelekezo yatakayoweza kutusaidia kuboresha utoaji huduma katika sekta ya afya kupitia Watoa Huduma za Afya na Mabaraza ya Kitaaluma na pia kuwakumbusha wananchi juu ya haki yao ya msingi ya kupata huduma bora za afya na wajibu wao wa kuhakikisha hilo linatokea.
  • Wanataaluma wa Afya:
Nawakumbusha Wanataaluma wote katika Sekta ya afya, yaani Madaktari, Wauguzi, Wakunga, Wafamasia, Wataalam wa Maabara, Madaktari na Wataalam wa Afya ya Kinywa na Meno, Wataalam wa Mionzi, Wataalam wa viungo bandia na Wafiziotherapia,  kwamba taaluma hizi ni za Kuheshimika sana (Noble), na hivyo kazi na majukumu mnayoyatekeleza yamejengwa  katika  misingi ya kuaminiwa (Trust) na Jamii, na kwamba  kuaminiwa  huko ndio kiini cha heshima ya taaluma hizi. Hivyo, ni wajibu wa kila mwanataaluma kutekeleza majukumu yake akiongozwa na msingi huu mkuu, pamoja na misingi mingine ya kimaadili ambayo ni: HURUMA, UKWELI, FARAGHA, USIRI, UAMINIFU, USAWA, HAKI, UTU na MAHUSIANO MEMA.
Aidha, naendelea kuwakumbusha kuwa, utekelezaji wa majukumu yenu siku zote ni lazima uzingatie matakwa ya Katiba ya Nchi ambayo ndiyo Sheria Mama. Mkumbuke kuwa Dira Kuu katika  utekelezaji wa wajibu wenu kama wanataaluma ni uzingatiaji wa haki, heshima, usawa na utu kwa wote wanaokuja mbele yenu kupata huduma za kitaaluma. Vile vile mkumbuke kuwa siku zote mnao wajibu wa kutekeleza majukumu yenu ya kitaaluma kwa kuzingatia Sheria nyingine za nchi,  Kanuni, Sera, pamoja na  Miongozo iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria za Nchi, pamoja na Miongozo na Matamko  ya Kimataifa ambayo tumeridhia kuyatekeleza na kuyazingatia.
Aidha, nawakumbusha Wanataaluma wote Waandamizi na Viongozi katika Sekta ya Afya kwamba ni wajibu wao kuhakikisha kuwa Wanataaluma na watoa huduma wote walio chini yao wanazingatia na kufuata Sheria, Kanuni, Weledi (Professionalism) pamoja na Maadili (Ethics) ya taaluma au kazi zao na kuchukua hatua stahiki za nidhamu, kwa mujibu wa Sheria, kunapotokea ukiukwaji. Pia kila Mwanataaluma ana wajibu wa kuhakikisha kuwa Wanataaluma wanaomzunguka wanatekeleza majukumu yao kwa misingi hii iliyotajwa na ana wajibu wa kutoa taarifa kwa Mamlaka husika pindi panapotokea ukiukwaji au kuonekana viashiria vyake. Jambo hili ni muhimu sana ili kama Wanataaluma msikubali kazi nzuri inayofanywa na wengi iharibiwe na wakorofi wachache miongoni mwenu.
  • Mabaraza ya Taaluma
Natumia fursa hii pia kuyakumbusha Mabaraza yote ya Kitaaluma yaliyo chini ya Wizara yangu kuhakikisha kuwa wanasimamia kikamilifu Sheria zinazosimamia Wanataaluma wao. Hii ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa  mtu yeyoye anayetaka kutoa huduma za kitaaluma ni lazima awe na elimu na ujuzi  unaokubalika, na atambulike kwa kupewa usajili na leseni ya kufanya kazi za kitaaluma. Dhima ya Wizara ni kuona kuwa jamii inapata huduma zilizo sahihi, salama na zenye ubora unaokubalika. Hivyo, Mabaraza yana wajibu wa kuchukua hatua stahiki kwa yeyote atakayebainika kukiuka Sheria na taratibu zilizowekwa.
  • Wanajamii
Napenda kuwajulisha wanajamii wote kuwa mnayo haki ya kupata huduma za afya zilizo salama, bora na ambazo zinazingatia misingi ya usawa, haki na zinazozingatia heshima na utu wa binadamu.  Pia, mnayo haki ya kupata taarifa sahihi kuhusu hali ya afya au ugonjwa, na kupata ushauri au tiba kwa wakati na kwa gharama zinazokubalika. Hivyo, wanajamii mnao wajibu wa kutoa taarifa wakati wowote mnapobaini kuwepo kwa viashiria au vitendo vya ukiukwaji wa maadili, sheria na taratibu zilizowekwa kwa misingi ya Sheria za Nchi.  Kati ya vitendo visivyo kubalika ni pamoja na rushwa, ubadhirifu wa mali za umma, wizi, lugha chafu, matusi, dharau, mavazi yasiyo na heshima, ulevi, matumizi ya madawa ya kulevya, uropokaji wa siri za wagonjwa, unyanyasaji wa kijinsia, matumizi mabaya ya simu za mkononi na tabia nyingine zote zinazofanana na hizi.
Hitimisho na Maagizo,
Nahitimisha salamu zangu kwa kutoa maagizo yafuatayo:
  • Wanataaluma na Watoa Huduma,
  1. Kila Mwanataaluma na mtoa huduma anapaswa kuvaa kitambulisho chenye jina lake kamili  wakati wote awapo eneo la kazi. Hii ni pamoja na uvaaji wa sare nadhifu za kazi.
  2. Viongozi wa kila kituo cha kutolea huduma za afya wahakikishe kuwa kuna Masanduku ya kutolea maoni yanayoonekana kwa uwazi na urahisi, na kwamba maoni yanayotolewa yanafanyiwa kazi ipasavyo.
  3. Viongozi wa kila kituo cha kutolea huduma za afya wahakikishe kuwa kuna Ofisi za kuwasilisha malalamiko zilizo karibu ili kufikiwa na wateja wote wenye uhitaji.
  1. Viongozi wa vituo vya kutolea huduma za afya wanapaswa kuweka wazi namba zao rasmi za simu kwenye mbao za matangazo ambazo mwananchi atazitumia kutoa taarifa au kuwasilisha maoni au malalamiko.
  2. Mganga Mkuu wa Kituo, Mganga Mkuu wa Wilaya, Mganga Mkuu wa Mkoa au Kiongozi mwenye mamlaka katika utoaji wa huduma za afya ana wajibu wa kuwasilisha malalamiko dhidi ya mwanataaluma anayetuhumiwa katika Baraza la Taaluma husika pindi panapotokea vitendo vya ukiukwaji wa weledi (Professionalism) na maadili (Ethics).
  • Mabaraza ya Taaluma
Kila Baraza la taaluma pamoja na Wawakilishi wao waliopo katika Wilaya, Mikoa na ngazi ya Taifa waweke wazi utaratibu wa kisheria wa uwasilishwaji wa malalamiko na taratibu za Uchunguzi wa vitendo viovu dhidi ya wanataaluma. Hii ni pamoja na kuweka wazi namba za simu na anuani za barua pepe (e-mails).
  • Wanajamii kwa ujumla:
    1. Nawasihi Wanajamii kuwaheshimu na kuwathamini Watoa huduma za Afya nchini
  • Nawasihi wanajamii wote kutoa taarifa, maoni au malalamiko dhidi ya wanataaluma au watoa huduma wanaokiuka misingi ya Taaluma zao, au wanaotoa huduma kinyume na Taratibu zilizopo kwa:
  • Uongozi wa kituo husika,
  • Mganga Mkuu wa Wilaya,
  • Mganga Mkuu wa Mkoa,
  • Ofisa wa TAKUKURU,
  • Baraza la Taaluma Husika,
  • Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, au
  • Katibu Mkuu OR-TAMISEMI, au kwa
  • Kiongozi yeyote wa Serikali, ili awasilishe taarifa hizo kunakostahili.
Aidha ni vema taarifa itolewe kwa kumtaja mhusika ili kurahishisha ufuatiliaji.
Nawatakieni nyote Kheri na Afya Njema kwa mwaka mpya wa 2018.
Ahsanteni sana.
Dkt. Faustine Ndugulile (Mb)
NAIBU WAZIRI WIZARA YA AFYA,
MAENDELEO YA JAMII, JINSIA,WAZEE NA WATOTO.
31/12/2017.

MWONGOZO WA UFUGAJI NA UPATIKANAJI WA MASOKO YA SUNGURA

$
0
0

Umeanza kufuga sungura na unakabiliwa na changamoto mbalimbali za ulishaji na magonjwa?

Au unataka kuanza ufugaji wa sungura na hujui jinsi ya kufanya?

Kubwa zaidi ni hili; unataka kufuga au unafuga, lakini HUJUI WAPI PA KULIPATA SOKO LA SUNGURA?

Yawezekana ulipata mafunzo, ukalipa fedha nyingi kununua mabanda, mbegu na chakula, lakini waliokupatia mafunzo wakati huo wamekukimbia na hata unapowatafuta ili wakusaidia changamoto zinazokukabili hawaonekani.

Yawezekana pia umeingia kwenye mikataba mbalimbali na baadhi ya watu waliokuaminisha kwamba wao wanalo soko la sungura - wengine wakakwambia wanasafirisha kupeleka Arabuni au Kenya - lakini mpaka sasa hawakusaidii lolote japo walikuahidi watakupatia na wataalam wa kuwahudumia wanapoumwa.
Umechanganyikiwa kwa kuona kwamba umepoteza muda na rasilimali zako kwenye ujasiriamali ambao waliokufundisha wamekukimbia na ukiwapigia ama hawapatikani au wanakujibu kwa ujeuri.

Usijali, hujapotea bado na sasa ondoa hofu kabisa. ANZA MWAKA MPYA KWA FIKRA MPYA ZENYE MAENDELEO!

PIGA NAMBA HII +255 656 331974 ILI KUPATA MWONGOZO HUU kwa kuchangia BEI NDOGO TU YA SHS. 20,000/= ili uweze kupata nakala hii kwa njia ya mtandao popote ulipo.

Utajifunza mengi ndani ya mwongozo huu ambayo ni pamoja na ufugaji bora, uhudumiaji, utafutaji wa masoko, MAGONJWA kujua dalili zake, jinsi ya kuyatibia na namna ya kuyakinga!

Kumbuka tu kwamba, biashara yoyote unahitaji vitu vikuu vitatu au vinne: Elimu sahihi ya biashara unayotaka kuifanya; SOKO – nani wateja wa bidhaa zako?; Mtaji wa biashara; na Muda.

Kwa kuwa unatumia gharama hasa katika mtaji, ni vyema ukapata elimu sahihi pamoja na kujua namna ya kutafuta masoko, kinyume chake utakuwa unafanya kazi ya Muhanga, mnyama ambaye kazi yake ni kuchimba mashimo halafu anashindwa kuishi!

Epukana na madalali wanaoweza kukupotosha ambao wao wanatafuta fursa tu ili wapige dili hasa baada ya kukuuzia mbegu na mabanda halafu wanakuteleza.


WASILIANA NA DANIEL MBEGA KWA SIMU HII +255 656 331974 ILI UPATE NAKALA YAKO SASA!!

Wateja watatu wajishindia TSH 15 milioni, 10 milioni na 5 milioni!

$
0
0





Meneja wa Wateja wa Tigo Pesa, Mary Rutta (kulia) akiongea kwa njia ya simu na moja wa washindi wa promosheni ya Tumia Tigo Pesa na Ushinde iliyofanyika usiku wa kuamkia mwaka mpya katika ofisi za Tigo ambapo Lugano Thomas Mlimi wa Dar es salaam, Kulthum Salim Ally wa Ruvuma na Maria Josef Maligisa wa Lindi walijinyakulia shilingi milioni 15, milioni 10 na milioni 5 katika promosheni hiyo. Katikati ni Meneja wa Mapato wa Tigo, Arnold Ngakashi na kushooto ni Mwakilisi wa Bodi ya Michezo ya Bahati na Sibu Tanzania, Ally Abdallah.


Wengine 150 wajinyakulia zawadi za TSH 1 milioni na 500,000 kila mmoja!

‘Nimeanza mwaka mpya nikiwa milionea!’ alisema Lugano Thomas Mlini, ambaye ni dereva na mkaazi wa Mbezi Makonde, jijini Dar es Salaam alipotaarifiwa kuwa amejishindia shilingi milioni 15 kutoka Tigo.

Kupitia huduma yake ya Tigo Pesa, kampuni ya simu inayoongoza ya Tigo imewageuza Watanzania watatu kuwa matajiri wapya kwa mwaka 2018.

‘Ndoto zangu za kuanzisha biashara sasa zimetimia! Ahsanteni sana Tigo’ alisema Kulthum Salim Ally, mkulima na mkaazi wa Tunduru, Ruvuma ambaye naye alijinyakulia kitita cha shilinigi 10 milioni katika drooo kabambe ya promosheni ya Tumia Tigo Pesa na Ushinde iliyofanyika siku ya mkesha wa kuamkia mwaka mpya, katika ofisi ya makao makuu ya Tigo jijijni Dar es Salaam.

‘Nilienda kulala nikiwa maskini na sasa nimeamka nikiwa tajiri’ alisema Mariam Josef maligisa, Mkulima na mkaazi wa Nagangu, Lindi aliyeamka kutoka usingizini ili kupokea simu yake na kutaarifiwa kuwa naye amejishindia TSH 5 milioni kutoka Tigo.

Akitangaza washindi katika droo hiyo ya kuukaribisha mwaka mpya, Meneja wa Wateja wa Tigo Pesa, Mary Rutta alisema, ‘Tigo pesa ni zaidi ya huduma ya kufanya malipo. Ni sehemu ya maisha. Kwa hiyo leo tumewawezesha wateja wetu kutumiza ndoto zao za msimu wa sikukuu na Mwaka Mpya kupitia huduma ya Tigo Pesa.

Alibainisha kuwa Tigo imetoa jumla ya shilingi 120 milioni kwa watu 153 kutoka maeneo mbali mbali ya nchi. Wateja walishinda zawadi nono za kila siku baada ya kutumia huduma ya Tigo Pesa.

‘Pia tunajivunia mchango wetu katika kufanikisha upatikanaji wa huduma za kifedha nchini. Kupitia Tigo Pesa, tunawawezesha mamilioni ya Watanzania kutuma na kupokea zaidi ya TSH 1.7 bilioni kila mwezi. Hii inawawezesha wateja wenyewe pamoja na jamii, huku ikichangia ukuaji wa uchumi wa nchi,’ aliongeza.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Masoko wa Tigo, Willima Mpinga alisema kuwa,’Tigo inawatakia Watanzania wote Mwaka Mpya wenye furaha na mafanikio. Tigo ni mtandao unaowaelewa zaidi wateja na kujibu mahitaji ya soko. Tulizindua promosheni ya Tumia Tigo Pesa na Ushinde kwa dhumuni kuu la kuwawezesha wateja wetu kushinda pesa zitakazowawezesha kutimiza malengo yao ya mwisho mwaka.’

Tigo Pesa ni huduma ya kifedha kwa njia ya simu ya pili kwa ukubwa nchini. Tigo Pesa ina mtandao mpana zaidi wa wakala na watoa huduma zaidi ya 70,000 waliosambaa nchini kote. Tigo Pesa pia ilikuwa ndio huduma ya kwanza Afrika Mashariki iliyowezesha wateja kutuma fedha kwenda nchi nyingine kwa kutumia viwango na fedha za nchi husika.

Tigo ndio kampuni inayoongoza kwa mageuzi ya kidigitali ikijivunia huduma bora za sauti, SMS, intaneti yenye kasi ya juu zaidi ya 4G iliyosambaa katika miji 24 nchini, pamoja na huduma za kifedha. Mtandao wa Tigo pia ni maarufu kwa promosheni na ofa zake bunifu kwa wateja.

Tigo ilianza kutoa huduma zake Tanzania mwaka 1995 na kwa miaka mitatu sasa ndio kampuni ya simu inayokua kwa kasi zaidi nchini. Kwa sasa Tigo ndio kampuni ya simu ya pili kwa ukubwa nchini ikiwa na wateja zaidi ya 11.6 milioni.

MPINA ASHEREHEKEA SIKUKUU YA MWAKA MPYA KWA KUSHIRIKIANA NA WANANCHI WA JIMBO LA KISESA KUHAMASISHA KILIMO BORA CHA ZAO LA PAMBA

$
0
0
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina akishirikiana na wakulima wa Kijiji cha Itinje Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu kupalilia shamba la pamba lililopandwa kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo wakati wa mapumziko yake ya sikukuu ya Mwaka Mpya jimboni kwake mapema leo.
 Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akishirikiana baadhi ya wananchi wa jimbo la Kisesa Wilaya Meatu mkoani Simiyu kupalilia shamba la pamba ikiwa ni sehemu ya uhamasishaji kilimo cha kuzingatia mbinu bora za kilimo ikiwemo kupanda kwa mistari pamoja na kutochanganya zao hilo na mazao mengine alipokuwa kwenye mapumziko ya sikukuu ya mwaka mpya jimboni kwake.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina akishirikiana mkulima wa Kijiji cha Itinje jimbo la Kisesa Wilaya Meatu mkoani Simiyu Mama Sagwa Njile kupalilia zao la pamba lililopandwa kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo wakati wa mapumziko ya sikukuu ya Mwaka Mpya jimboni kwake leo

UVCCM YAPONGEZA MIRADI YA AFYA TABORA.

$
0
0

Na Mwandishi wetu,Tabora

Umoja wa Vijana wa CCM umesema umeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi ya afya inayotokana na ahadi katika ilani ya uchaguzi katika halmshauri za wilaya mji wa Nzega na Nzega vijijini mkoani Tabora. Pia Umoja huo umeeleza kikubwa kasi hiyo inatokana na kuwepo kwa mashirikiano makubwa kati ya viongozi wa chama,halmashauri za wilaya na serikali kuu.

Matamshi hayo yametamkwa jana na Mwenyekiti wa Taifa wa UVCCM Kheri Denise james mara baada ya kumaliza kutembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya cha Kazogolo katika halmashauri ya mji wa Nzege .

Kheri alisema kitendo cha serikali ya awamu ya tano kupeleka jumla ya shilingi milioni mia tano toka serikali kuu oktoba mwaka huu kwa ajali ya ujenzi wa kituo hicho ni kielelezo kuwa serikali inajali maisha ya wetu wake .

"UVCCM tumeridhishwa na ujenzi wa miradi ya afya katika halmashauri za mji wa Nzega na halmashauri ya nzega vijijini.Ilani ya uchaguzi ya chama imetekelezwa kwa vitendo. Hii ndiyo tafsiri halisi ya hapa kazi "Alisems Kheir .Aidha alisema kazi ya kuwatumikia wananchi haina mjadala badala yake inamhitaji kila kiongozi dhamana kuwa nafasi yake kuwajibika na kuwatumikia wananchi.

"Kuimarika kwa huduma za jamii na watu kupata huduma bora ndiyo malengo ya kisera yanayotakiwa kufanikishwa. Tuna wajibu kila mmoja kwa nafasi yake kumsaidia Rais na serikali yale "Alisisitiza  Kheri akiwa mkoani Tabora ametembelea mradi mkubwa wa usambazaji maji toka

ziwa Victoria mkoani mwanza kupitia shinyanga hadi Tabora,kuona maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya kazogolo na kuzumgumza na wananchi katika halmashsuri ya mji wa nzega na nzega vijiijini.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipokelewa na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi Nzega- mkoa wa Tabora akiwa anaelekea Mwanza kwa ajili ya mapokezi yake baada ya kuchaguliwa na mkutano mkuu wa 9 wa UVCCM kuwa mwenyekiti mpya wa UVCCM 2017-2022.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James wa tatu toka Kushoto akivikwa Skafu mara baada ya kuwasili katika Ofisi za CCM Wilayani Nzega.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akikagua kikundi cha ngoma mara baada ya kupokelewa.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akisaini Kitabu cha Mauzulio ya Wageni.
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Bi Tabia Maulid Mwita Akizungum,za na Wanachama wa Chaa cha Mapinduzi Wilayani Nzenga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akizungumza na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi na Jumuiya zake Wilayani nzega mkoa wa Tabora.
Wanachama Wilayani Nzega Wakimsikiliza
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice Jameswa tatu toka kushoto akizungumza jambo na M..mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya shillingi billioni 600 utakaotokea Ziwa Victoria na kunufaisha wananchi wapatao milioni 1.1 wa mikoa ya Shinyanga (vijiji 39) na zaidi Tabora (vijiji 89).


Baadhi ya Vifaa vya Ujenzi wa mradi mkubwa wa maji wenye thamani ya shillingi billioni 600 utakaotokea Ziwa Victoria na kunufaisha wananchi wapatao milioni 1.1 wa mikoa ya Shinyanga (vijiji 39) na zaidi Tabora (vijiji 89).
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akitunza fedha katika kikundi cha ngoma ya Asili alipowasili Wilaya ya Nzega Vijijini kuzungumza na Viongozi mbali mbali wa chama.
Viongozi wamsikiliza
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipata maelezo toka kwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Nzega Ndugu Amos Kanuda na Mkuu wa wilaya ya Nzega Ndugu Godfrey William Ngupula,alipotembelea kituo cha afya cha Zogolo kilichopo Halmashauri ya mji wa Nzega kinachotegemewa zaidi kuhudumia wananchi wa mji wa Nzega yenye watu wasiopungua laki mmoja. Ujenzi unaolenga kuboresha utoaji wa huduma katika kituo hiki ulikadiriwa kugharimu shillingi milioni 500 ukiwa ni ufadhili wa mfuko wa World Bank.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Kheri Denice James akipokelewa na Wanachama wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Shinyanga akitokea Tabora kuelekea mwanza.(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)

MHE MWANJELWA AWATAKA WANANCHI MBEYA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI KWA VITENDO

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akiwasihi waumini kumuunga mkono na kumuombea Rais Magufuli wakati akitoa salamu kwenye ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akimlisha chakula mmoja ya wazee waliohudhuria ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa pamoja na Viongozi wengine wakiongoza maombi wakati wa ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.

 Miongoni mwa wazee waliohudhuria ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.

 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akifanyiwa maombi na viongozi wa dini wakati wa ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akishiriki chakula cha mchana na wazee waliohudhuria ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.


Na Mathias Canal, Mbeya


Wananchi Mkoani Mbeya wametakiwa kuunga mkono kwa vitendo juhudi za uwajibikaji wa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli.


Mwito huo umetolewa Leo 1 Januari 2018 na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa wakati akitoa salamu kwenye ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya.


Alisema kuwa Rais Magufuli na serikali anayoingoza anawathamini kwa kiasi kikubwa wazee kote nchini kwani kwa umri wao ni sehemu ya turufu muhimu kimawazo na busara katika utendaji ndio maana Mke wake Mhe Mama Janeth Magufuli hushirikiana na wazee waliopo katika makundi mbalimbali katika huduma za kijamii.


Alisema kuwa serikali hii ya awamu ya Tano inayochagizwa na kauli mbiu isemayo "HAPA KAZI TU" inawakumbusha na kuwahamasisha wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kuinua haraka uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.


Katika ibada Hiyo Mhe Mwanjelwa ameshiriki chakula cha mchana na wazee waliohudhuria ibada Hiyo ya siku ya wazee kutoka Kata ya Manga na Sinde ikiwa ni ishara ya mapokezi mema ya Mwaka Mpya 2018. 


Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo aliongoza waumini wa kanisa la Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) kumuombea Rais Magufuli sambamba na serikali kwa ujumla ili wananchi waendelea kujivunia matunda ya Rais Magufuli ambaye Duniani kote anasifika kwa umakini na ushupavu.


Alisema kuwa zoezi hilo linapaswa kuwa endelevu kwa kanisa hilo kushirikiana kwa Karibu na wazee huku akisema kuwa litakuwa jambo zuri na muhimu zaidi endapo litafanyika kwa ajili ya wazee wa Mkoa mzima wa Mbeya.


"Wazee ni Tunu, kuwa Mzee ni Baraka kwani hata vijana ni wazee wajao, Lakini niwasihi kuendelea kuwatumia wazee kwa ushauri wa kijamii pia kidini lakini zaidi Mwaka Mpya 2018 uwe Mwaka wa Mafanikio kwetu sote:" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa


Mhe Mwanjelwa Alisifu uongozi wa kanisa hilo kwa kumualika kushiriki nao katika ibada hiyo huku akiwapongeza kwa kufanya ibada ya kiroho lakini pia ibada ya kimwili kwa ushirikishaji wa jamii.


Naye Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) Mchungaji Capson Masimbani alimpongeza Mhe Mwanjelwa na kusema kuwa ni kiongozi mwenye kujali wananchi pasina kubagua itikadi za dini zao.


Alisema kuwa ni Viongozi wachache nchini ambao wana unyenyekevu kama yeye huku akimsihi kuendelea na busara na hekima Hiyo.


Sambamba na hayo Mhe Naibu Waziri wa Kilimo aliunga mkono juhudi za kanisa hilo kwa kuandaa sherehe hiyo ya siku ya wazee kwa kuwapatia mifuko 66 ya sukari wazee hao.

WAZIRI MKUU ATOA KADI ZA CHF KWA WAZEE 4,000

$
0
0
*Ahimiza wakazi wa Ruangwa wajiunge na bima hiyo

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakazi wa wilaya ya Ruangwa wajiunge na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili waweze kumudu gharama za matibabu bila kulazimika kuwa fedha taslimu.

Ametoa wito huo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa mji wa Ruangwa na vijiji vya jirani katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya CWT, mjini Ruangwa, mkoani Lindi.

“Leo hii nimetoa kadi za CHF kwa wazee 4,000 wa wilaya hii. Ninaishukuru Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kutenga fedha na kuwalipia wazee hawa ili wanufaike na bima hii ya afya kama ambavyo imeelekezwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi.”

“Ninatoa wito kwa wananchi wengine walipie sh. 15,000 kwa mwaka ili wapatiwe kadi kwa ajili ya watu sita wa familia zao; yaani mhusika, mwenza wake na watoto wanne. Bima hii inasaidia kwa vile unapata matibabu hata kama huna fedha taslimu,” alisema.

Waziri Mkuu alikabidhi kadi kwa Mzee Issa Juma Ngalapa, mkazi wa kata ya Nachingwea pamoja na Mzee Suleiman Stola Lihepa wa kijiji cha Kilimahewa, kata ya Nachingwea kwa niaba ya wazee wote waliotakiwa kupatiwa kadi hizo.

Akitoa ufafanuzi juu ya mpango huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Bw. Andrea Chezue alisema mpango wa kutoa kadi za bima ya afya kwa wazee wameuita ‘CHF Endelevu’ kwa sababu walifanya tathmini na kubaini kuwa matibabu yao yana gharama, na yasipolipiwa, dawa zitaisha au wazee hao hawataweza kupatiwa huduma.

“Katika Halmashauri tulifanya utambuzi wa wazee wa kuanzia miaka 60 na kuendelea kwenye vijiji vyote na kubaini kuwa kuna wazee 4,000. Tukaamua Halmashauri iwalipie sh. 15,000 kwa kila wazee sita kama ilivyo katika kaya ili tuweze kuchangia gharama za matibabu yao,” alisema.

“Mzee akipatiwa kadi hii, inakuwa ni ya kudumu, anaitumia miaka yote. Si ya kulipia kila mwaka kama zilivyo zile nyingine. Hadi sasa tumeshatoa kadi kwa wazee 2,700 na tunaendelea kutengeza kadi hadi tukamilishe zote. Tumepanga kuwa kila mwaka, tutafanya utambuzi wa wazee katika vijiji vyote ili wale wanaofikisha umri huo, nao pia waingizwe kwenye mpango huu,” alisema.



IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATATU, JANUARI MOSI, 2018.

Sahara Group Hinges Future on Synergy, Diversification

$
0
0
Leading African energy and infrastructure conglomerate, Sahara Group has reinforced its commitment to sustaining its growth and expansion across global markets through diversification, collaboration and innovation

The energy giant which currently has operations in over 13 countries across four continents, made this assertion in its second Sustainability Report tagged: “Sustainability Through Synergy.

The Report which highlights activities in 2016 within Sahara Group’s Power, upstream, downstream, midstream and infrastructure divisions was presented in accordance with the Sustainability Reporting Standards of the Global Reporting Initiative (GRI).

According to Executive Director and Co-founder Sahara Group, Tonye Cole, the report reaffirms the organisation’s commitment to transparency and business integrity.

“We are delighted to be leading the charge for a paradigm shift that aligns business reporting in Africa with global best practice. Sahara continues to demonstrate how businesses can grow from humble beginnings to become conglomerates through diversification, collaboration, innovation and resilience. The Sahara story, since we commenced business in 2016 has been driven by creativity and an endless passion for daring the impossible,” he said.

He added: “The 2016 sustainability report covers critical aspects of our business and we believe such reports are required to safeguard the future of African businesses and enhance their competitiveness globally.”

Notable highlights in the report include key investments and innovation in the power sector, where Sahara Group has emerged as one of the largest privately owned power institutions in Sub-Saharan Africa. The report also highlights the adoption of a Supply Chain Efficiency strategy that is expected to drive synergy, growth and sustainability of its businesses across the entire energy value chain.

In addition to providing information on the various business divisions, the report also sheds light on Sahara Group’s core values, people, economic performance, stakeholder engagement, health and safety records as well as the activities of Sahara Foundation – the Group’s corporate responsibility vehicle.

Sahara Foundation which hitherto had implemented several projects in Health, Education, Capacity Building, and the Environment, adopted the extrapreneurship platform in 2016 to enable it empower more beneficiaries through shared platforms.

The report captures the admission of Sahara Group into the Vanguard Board of the World Economic Forum Partnering Against Corruption Initiative (PACI). The Board is responsible for developing strategies for designing corruption out of countries and regions through various initiatives.

Sahara Group is currently working on a new initiative with the PACI community towards helping to Rebuild Trust and Integrity in Businesses with a major focus on Nigeria and Africa as a whole.

In line with its membership of the Private Sector Advisory Group of the United Nations Sustainable Development Goals Fund (SDGF), Sahara has been working with various partners to promote the implementation of the 17 SDGs of the United Nations.

Sahara Group is partnering with the SDGF, The Kaduna State Government and other agencies of the United Nations, on project “Food Africa” which seeks to empower young farmers, eradicate poverty, provide employment, reduce wastage and improve sustainable food production in Nigeria. The plan is to replicate the project across the continent.

Intended for regional and global audiences, including regulators, stakeholders, financial service providers, multi-lateral institutions, civil societies, customers, the media and the general public, the Sahara Group sustainability report is available for download via the media section of its website, www.sahara-group.com and its social media platforms.

The report:

http://www.sahara-group.com/sahara-group-hinges-future-on-synergy-diversification.html

ZAIDI YA BILIONI 1.2 ZIMETENGWA NA WAKALA WA BARABARA NCHINI TANROAD KWA AJILI YA UJENZI WA BARABARA KUTOKA ULANGA HADI KURUNGU

$
0
0

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akikabidhi kadi ya bima ya Afya kwa mmoja wazee waliokatiwa bima ya afya na Naibu Waziri huyo, Salehe Mgonza katika Mkutano uliofanyika Mkuranga.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akiwa na viongozi wa chama na serikali akikabibidhi mikokoteni kwa kikundi cha Umoja waendesha mikokoteni wilaya ya Mkuranga.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza juu ushirikiano katika ulinzi na usalama pamoja na kuwapeleka shule wanafunzi wa kuanza darasa la kwanza.


Mganga mkuu Wilaya ya Mkuranga Dkt.Steven Mwandambo (kushoto)akijibu swali mbele ya Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega picha na Emmanuel Massaka,Globui ya jamii.
Baadhi ya Madiwa wani kwakiwa katika mkutano huu
sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano huu.

ZAIDI ya shilingi bilioni 1.2 zimetengwa na Wakala wa barabara nchini TANROAD kwa ajili ya Ujenzi wa Barabara kutoka Ulanga hadi Kurungu wilayani mkuranga katika Mkoa Pwani.

Akizungumza na wananchi wilayani humo jana katika mkutano wa hadhara wa kufunga mwaka 2017 na kukaribisha 2018 Mbunge wa Jimbo hilo Abdalla Ulega ambaye pia ni Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi,alisema tayari serikali imeshatenga fedha hizo.

Ulega aliwaeleza wananchi wa jimbo hilo kuwa katika miaka miwili ya uongozi wake yapo mambo mengi ambayo ameyafanya, lakini barabara ni kero kubwa kwa wanamkuranga hivyo katika juhudi zake amefanikiwa kupata fedha hizo kwa ajili ya kuaza ujenzi huo.

"Ndugu zangu wanamkuranga mwanenu napambana kwelikweli kwa maana najuwa niliahidi na nyie mlinituma na mmeendelea kunituma nami staki kuwaangusha, hivyo kuazia January hadi Februari mwaka huu 2018 ujenzi wa barabara hii ambayo nimetaja itaaza ujenzi. "alisema Ulega

Pia aliongeza kuwa anajuwa kwamba changamoto ya barabara imekuwepo kwa muda mrefu na viongozi mbalimbali wamepita lakini aliwaeleza wasubiri utekelezaji wake kuanzia miezi hiyo.  Akizungumzia eneo la afya wilayani humo,Ulega  aliwaeleza wananchi hao kuwa kwa muda mrefu hospitali ya wilaya ilikuwa haina kipimo cha X-ray lakini kwa jitihada zake amefanikisha kupata kipimo hicho na kitakabidhiwa hospitalini hapo hivi karibuni.

Alisema mbali na hilo lakini pia hospitali hiyo ilikuwa na kero karibu tatu hadi nne ikiwamo na ukosefu wa madawa, huduma ya maji, lakini hivi sasa kero hizo zimeondoshwa kwa kiwango kikubwa.

"Wazee bila shaka sasa mambo yanakwenda vizuri ukilinganisha na tulikotoka na tunaendelea kuboresha huduma hii ikiwamo na kufungua vituo vya afya kwa lengo la kupunguza msongamano katika hospitali ya wilaya. "alisema Waziri Ulega

Pia alisema kuna ongezeko kubwa la Zahanati kutoka 35 hadi kufikia 40 katika vijiji vyote 125 ndani ya wilaya hiyo, nakudai kuwa lengo kufikia 2020 zifikie zahanati 50.

Akizungumzia Elimu Ulega aliwataka wazazi kusimamia suala zima la watoto kwenda shule ambapo alidai kutokana na hamasa ya elimu bure Wilaya ya mkuranga imefanikiwa kutoa mtoto aliyeshika nafasi ya pili kitaifa.

Aliongeza kuwa kutokana na juhudi zinazofanywa na wazazi kwa lengo la kuhakikisha elimu wilayani humo inastawi, ameweza kuchangia saruji mifuko 100 na mabati 100 katika kuunga mkono katika ujenzi wa madarasa Katika shule ya msingi mkuranga mjini

Kwaupande wake Mkuu wa wilaya hiyo Firbeto Sanga akizungumza katika mkutano huo aliwataka wananchi hao kuendelea kutoa ushirikiano ndani ya wilaya hiyo ili kukomesha vitendo vya kiharifu.Aliwataka kuwatambua wageni wanaongia kwenye wilaya hiyo nakutoa taarifa sahihi lakini huku akiwakumbusha kupeleka watoto shule wenye umri wa kusoma na kamwe wasisubiri kusukumwa na serikali.

WAZIRI MKUCHIKA ATEMBELEA TPSC TAWI LA MTWARA

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (kushoto) akiwasili chuo cha Chuo Cha Utumishi wa Umma Tanzania (TPSC) Tawi la Mtwara ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake za kutembelea matawi ya chuo hicho nchini kulia ni Mkurugenzi wa TPSC Tawi la Mtwara Dkt. Emmanuel Shindika,ziara hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (katikati) akipata maelezo kutoka Mkurugenzi wa TPSC Tawi la Mtwara Dkt. Emmanuel Shindika (kushoto) akiwa katika moja ya madarasa ya chuo hicho tawi la Mtwara ikiwa ni mwendelezo wa ziara zake za kutembelea matawi ya chuo hicho nchini, ziara hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki.Wengine pichani ni watumishi wa chuo hicho.
Kwaya ya TPSC tawi la Mtwara ikitoa burudani mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (Hayupo pichani), aliyefanya ziara fupi chuoni mwishoni mwa wiki sambamba na kupokea taarifa ya tawi na kusikiliza changamoto za watumishi na wanachuo.
Baadhi ya wanachuo wa Chuo cha Utumishi wa Umma TPSC tawi la Mtwara, wakimsikiliza kwa makini waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Kapteni Mstaafu George Mkuchika (Hayupo pichani), aliyefanya ziara fupi chuoni hapo mwishoni mwa wiki sambamba na kupokea taarifa ya chuo na kusikiliza changamoto za watumishi na wanachuo.

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA FAMILIA YA NGUZA VICKING IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0

 Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza wakiwasili viunga vya  Ikulu jijini Dar Leo Januari 2, 2018 kumshukuru Rais Magufuli kwa msamaha wake alioutoa kwao dhidi ya kifungo cha maisha walichokuwa wakitumikia gerezani tangia walipohukumiwa miaka 13 iliyopita.
Rais Dkt John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na Familia ya  Mwanamuziki Nguza Vicking “Babu Seya” na wanae Johnson Nguza “Papii Kocha”, Francis Nguza na Michael Nguza wakipata sala ya pamoja,mara baada kuwasili viunga vya  Ikulu jijini Dar Leo Januari 2, 2018 kumshukuru Rais Magufuli kwa msamaha wake alioutoa kwao dhidi ya kifungo cha maisha walichokuwa wakitumikia gerezani tangia walipohukumiwa miaka 13 iliyopita.

DK. MNDOLWA AKABIDHIWA RASMI OFISI LEO, AAHIDI KUUNDA KAMATI KUTAFUTA UFUMBUZI DHIDI YA KUMOMONYOKA KWA MAADILI KATIKA JAMII YA KITANZANIA

$
0
0
 Mwenyekiti Mstaafu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Abdallah Bulembo (kushoto) akikabidhi nyaraka zenye orodha ya mali za Jumuiya hiyo kwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo, Dk. Edmund Mndolwa, leo Januari 2, 2018, Makao Makuu ya Jumuiya jijini Dar es Salaam. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Zanzibar  Abdallah Haj Haidar.
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa akisalimiana na Katibu Mkuu wa Jumuia hiyo Seif Shabani Mohamed alipowasili Makamo Makuu ya Jumuiya hiyo kwa ajili ya makabidhiano hayo
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa  akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar Najma Giga wakati wa hafla hiyo
 Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Dk. Mndolwa akizungumza na Mwenyekiti wa Jumuia hiyo Mstaafu Abdallah Bulembo wakati wa hafla hiyo. Kulia ni Makamu Menyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Zanzibar Abdallah Haj Haidar
 Mwenyekiti mstaafu wa Jumuiya ya Wqzazi Tanzania Abdallah Bulembo akionyesha Katiba ya Jumuiya hiyo kabla ya Kumkabidhi Mwenyekiti mpya wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Dk Edmund Mndolwa. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hizo Zanzibar Abdallah Haj Haidar
 Mwenyekiti Mstaafu wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Abdallah Bulembo (kushoto) akikabidhi nyaraka zenye orodha ya mali za Jumuiya hiyo, kwa Mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo, Dk. Edmund Mndolwa, leo Januari 2, 2018, Makao Makuu ya Jumuiya jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Seif Shabani Mohammed na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Zanzibar  Abdallah Haj Haidar. 
 Bulembo akiendelea kukabidhi nyaraka
 Dk. Mndolwa na Bulembo wakisaini nyaraka za makabidhiano
 Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania  Zanzibar  Abdallah Haj Haidar na Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Seif Shabani Mohammed wakisaini nyaraka upande wa mashahidi
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania Edmund Mndolwa akizungumza baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi
 Dk Mndolwa na Bulembo wakifurahia jambo baada ya makabidhiano ya ofisi
Watumishi wa Jumuiya ya Wazazi Makao Makuu wakiwa kazini wakati wa makabidhiano hayo ya ofisi baina ya Dk Mndolwa na Bulembo PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

Na Bashir Nkoromo.

Mwenyekiti mpya wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Dk. Edmund Mndolwa ameahidi kuunda Kamati ya  kutathmini namna Jumuiya hiyo inakavyolishughulia kwa ufanisi tatizo la kuporomoka kwa maadili katika jamii hapa nchini.

Dk. Mndolwa ametoa ahadi hiyo leo, hayo wakati akikabidhiwa rasmi Ofisi na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mstaafu Abdallah Bulembo, hafla iliyofanyika Makao Makuu ya Jumuiya ya Wazazi Tanzania jijini Dar es Salaam.

"Katika hotuba ya Mwenyekiti wa CCM Rais Dk. John Magufuli alitutaka sisi viongozi wa Jumuiya hii tusikae kimya wakati vitendo vya kuporomoka kwa maadili katika jamii ikiwemo wasanii wa kike kuonyesha sehemu za miili yao zinazotakiwa kusitiriwa. Sasa hili ni agizo lazima mimi na viongozi wenzangu tulipe kipaumbele katika kulifanyika kazi.

Kwa hiyo baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi leo hii, miongoni mwa mipango yangu Kama Mwenyekiti ni Kuunda Kamati itakayojikita kwa undani kuhakikisha tunapata njia bora za kudhibiti kuporomoka kwa maadili katika jamii ya Watanzania", alisema Dk Mndoldwa.Alisema, pia atahakikisha katika zama za uongozi wake, Jumuiya ya Wazazi inainuka na kujitegemea vya kutosha kiuchumi ili iondokane na adha ya kuwa ombaomba.

"Jumuiya hii ianazo mali nyingi, kinachotakiwa hapa ni kuhakikisha fedha zinazotokana na mali au miradi hii zinaingia kwenye hazina ya Jumuia badala ya kupotelea mifukoni mwa wajanja wachache, tukifanikiwa kuthibiti bila shaka tutakuwa na fedha za kutosha", alisema Dk. Mndolwa.

Akimzungumzia Bulembo, Dk Mndolwa amesema, alikuwa kiongozi bora ambaye ameisaidia kwa kiasi kikubwa Jumuiya ya Wazazi, na kwamba katika jitihada zake ameiboresha Jumuia hiyo kwa karibu asilimia tisini.

"Nimejifunza mambo mengi kwa Bulembo, mojawapo ni uvumilivu, huyu ni mvumilivu kiasi kwamba itanibidi kuiga uvumilivu wake ili na mimi nistaafu kwenye Jumuiya hii nikiwa safi kama yeye," Alisema Dk. Mndolwa.

Kwa Upande wake Bulembo aliwataka viongozi wapya wa Jumuiya hiyo kuthamini sana Waaandishi wa habari kwa kuwapa ushirikiano kila unapohitajika na kwamba yupo tayari kutoa ushauri pale utakapohitaji.

Aliwaasa viongozi wapya kuendeleza mazuri yaliyofanywa na uongozi uliopita huku wakiachana na mabaya yaliyofanyika wakati huo.

"Namna nzuri ya kuongoza ni kuwa karibu na unaowaongoza, msikae nao mbali mnaowaongoza na ikiwa kutakuwa na jambo miongozi mwenu viongozi ambalo haliendendi vizuri utatuzi wake uwe kwenye vikao si kwingineko", Alisema Bulembo.

UBOVU MAGARI MAPYA YA POLISI WAISHITUA WIZARA MAMBO YA NDANI

$
0
0

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani Masauni Yusuph Masauni (kulia) akitoa maelekezo kwa maofisa wa polisi wakiongozwa na Kamishina wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi Albert Nyamhanga(kushoto)baada ya kukagua magari ya polisi leo katika bandari ya Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani akitafakari jambo baada ya kukagua magari ya polisi yaliyopo Chuo cha Polisi Kurasini Dar es Salaam leo baada ya kufanya ziara yenye lengo la kufuatilia kukabidhiwa kwa magari 53 kwa Jeshi la Polisi yaliyokuwa bandarini.
Naibu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Masauni Yusuph Masauni (wa kwanza kulia) akipata maelezo kutoka kwa moja ya maofisa wa Bandari ya Dar es Salaam leo kuhusu uwepo wa magari 119 ya Jeshi la Polisi ambayo yanasubiri kukabidhiwa kwa polisi. Masauni amefanya ziara bandarini hapo kufuatilia agizo la Rais,Dk.John Magufuli la kutaka magari ya polisi ya polisi yaliyopo bandarini yakabidhiwe.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Masaun Yusuph Masauni akiwa mbele ya gari jipya lililopo Chuo cha Polisi Kurasini jijini Dar es Salaam baada ya kulifanyia ukaguzi. Gari hilo ni moja kati ya magari 53 mapya yaliyokabidhiwa kwa Jeshi la Polisi nchini.
 
*Masauni aunda kamati maalumu kufanya uchunguzi upya

Na Said Mwishehe, Blogu ya jamii

NAIBU Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Masauni Yusuph Masauni ameagiza kuundwa kamati maalumu kuchunguza magari 53 ya polisi yaliyopo Chuo cha Polisi jijini Dar es Salaam. Amesema mbali ya kuchunguza kwa kina magari hayo,pia ipo haja kupitiwa kwa mkataba wa ujio wa magari hayo Kwani kuna maswali mengi ya kujiuliza ambayo lazima yapate majibu yake.

Masauni ametoa agizo la kuundwa kwa kamati hiyo leo, baada ya kufanya ziara Katika Bandari ya Dar es Salaam ili kuangalia iwapo agizo la Rais ,John Maguful limetekelezwa la kutaka magari ya polisi yaliyopo bandarini yakabidhiwe kwa Jeshi la Polisi nchini. Masauni amesema kimsingi agizo la Rais limetekelezwa kwa magari 53 kukabidhiwa Polisi lakini amebaini kati ya magari hayo matano ni mabovu kutokana na kuwa na hitilafu mbalimbali licha ya kuwa mapya.

"Baada ya kufanyikaa ukaguzi wa awali kwa magari 53,matano kati ya hayo ni mabovu. Na ukaguzi uliofanywa ni wa waletaji na polisi bado hawajafanya ukaguzi wao."Ukisiliza taarifa kuhusu magari haya kuna maswali yanaibuka. Hivyo Wizara ya Mambo ya Ndani inatoa maagizo ya kuundwa kamati maalumu itakayoshirikisha watalaamu kutoka taasisi tofauti kuchunguza magari yote 53,"amesema Masauni.

Amefafanua mkataba kuhusu magari hayo ya polisi unaeleza idadi ya magari yote kwa ajili ya Polisi ni 777 na yaliyopo hadi sasa ni 53 ambayo tayari yamekabidhiwa na magari 119 bado yapo bandarini."Hivyo niagize pia magari ambayo bado yapo bandarini nayo utaratibu ufanyike na kisha kukabidhi kwa jeshi la polisi kwani tunakabiliwa na uhaba wa magari,lazima tusimamie yatoke haraka wakati ukaguzi wa kina ukiendelea,"amesema.

Amesisitiza ni vema kubaini ubora wa magari hayo na kamati itakayochunguza itakuwa huru na itakapokamilisha itatoa taarifa rasmi itakayokuwa na maelezo muhimu ya ubora na uwezo wa magari hayo ya polis. Alipoulizwa iwapo magari hayo ni mapya, amejibu kwa mujibu wa mkataba magari yanatakiwa kuwa mapya na ndio maana amepata mashaka baada ya kubaini kuna magari yanahitilafu.

Kuhusu thamani ya magari yote kwa mujibu wa mkataba, Kamishna wa Fedha na Lojistiki Albert Nyamhanga amesema ni dola za Marekani 29,606,100.

TRA YATOA UTARATIBU WA KUSAJILI WALIPA KODI WADOGO


RAIS DKT JPM AOMBOLEZA MSIBA WA MKE WA NAIBU WAZIRI KANGI LUGOLA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini kitabu cha maombolezo alipofika Gerezani Railways Club jijini Dar es salaam leo January 2, 2018  kwenye msiba wa Marehemu Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyekuwa mke wa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola aliyefariki jana.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitoa mkono wa pole kwa wafiwa alipofika Gerezani Railways Club jijini Dar es salaam leo January 2, 2018  kwenye msiba wa Marehemu Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyekuwa mke wa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola aliyefariki jana.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli    akimfariji  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola  kwenye msiba wa  mkewe MarehemuKamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola Gerezani Railyways Club jijinio Dar es salaam leo January 2, 2018 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na  wanafamilia alipofika Gerezani Railways Club jijini Dar es salaam leo January 2, 2018  kwenye msiba wa Marehemu Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyekuwa mke wa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola aliyefariki jana.

PICHA NA IKULU

RUSHWA IMECHANGIA WAKANDARASI KUJENGA BARABARA CHINI YA KIWANGO-DC HAPI

$
0
0
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akionesha sehemu   ya Udongo ambao umechanganyika na takataka zilizokuwa chini ya barabara ya Msasani CCBRT ,ambayo imekuwa ikimeguka kila siku kutokana na mkandarasi wa awali  aliojenga barabara hiyo kuipitisha juu ya udongo wenye takataka na kusababishia hasara kwa serikali kila Mwaka.DC Hapi alieleza kuwa ujenzi  huo wa awali umeiingiza Serikali Hasara kutokana na baadhi ya watendaji wa Serikali kula rushwa na kufumbia macho ujenzi huo wa barabara juu ya dampo. 
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akiwaonya wakazi wa Tandale kwa Tumbo juu ya utupaji taka hovyo katika mitaro ya Maji iliyopo pembezoni mwa barabara,kama ionekanavyo pichani ikiwa imejaa maji taka na kuhatarisha afya za wakazi wa eneo hilo.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akionesha barabara ya Magomeni Kondoa inayokarabatiwa na Wakala wa Barabara nchini Tarura  mara baada ya kuwa na Mashimo mengi na kufanya kushindwa kupitika
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akichota sehemu ya udongo uliokuwa ukisumbua barabara ya Msasani CCBRT ambao ulikuwa umechanganyika na Taka.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi akikagua barabara ya kuelekea Sleepway Masaki Jijini Dar es Salaam ambayo imeharibika na Mashimo Makubwa na sasa inakarabatiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni.

DK. KIGWANGALLA NA MKURUGENZI MKAZI WA UNDP KUANZISHA KIKOSI KAZI CHA KUCHUNGUZA TUHUMA ZA UJANGILI WA TEMBO KATIKA HIFADHI YA RUAHA

$
0
0
Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Bi. Natalie BOUCLY wamekubaliana kuanzisha kikosi kazi cha pamoja cha kuchunguza tuhuma zilizotolewa hivi karibuni na kituo cha habari cha ITV LONDON kuhusu ujangili wa Tembo katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha iliyopo Mkoani Iringa.

Dk. Kigwangalla na Mkurugenzi huyo, wamefikia makubaliano hayo leo Januari 2, 2018 wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi ndogo ya Wizara ya Maliasili na Utalii, Mpingo House Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Waziri Kigwangalla amemueleza Mkurugenzi huyo kuwa Wizara yake inaandaa mikakati mbalimbali ya kuongeza idadi ya watalii nchini na mapato ikiwemo kuwashirikisha wananchi kuandaa mwezi maalum wa Urithi wa Tanzania pamoja na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato kwa njia za kielektroniki katika vituo mbalimbali ya Utalii.

Kwa upande wake, Mkurugenzi huyo amemuahidi Waziri Kigwangalla kuendelea kumpa ushirikiano katika nyanja mbalimbali za kuendeleza Utalii nchini na uhifadhi wa misitu na wanyamapori kwa ujumla.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa hapa nchini (UNDP), Bi. Natalie BOUCLY katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo, Mpingo House Jijini Dar es Salaam leo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa hapa nchini (UNDP), Bi. Natalie BOUCLY wakati wa mazungumzo yaliyofanyika leo katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo, Mpingo House Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akiagana  na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa hapa nchini (UNDP), Bi. Natalie BOUCLY baada ya mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo, Mpingo House Jijini Dar es Salaam leo.

MFANYABIASHARA AJENGA ZAHANATI YENYE VIFAA VYA KISASA NA KUIKABIDHI SERIKALINI

$
0
0
 Mfanyabiashara, Emmanuel Mallya (katikati) akisaini hati na mkataba wa zahanati EB, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Michael Kilawila kwenye hafla hiyo ya makabidhiano. Kushoto ni mke wa Bw. Mallya, Bi. Marry Mallya akishuhudia makabidhiano hayo.
 Mfanyabiashara, Emmanuel Mallya (kushoto) akimkabidhi hati na mkataba wa zahanati EB Zahanati Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Michael Kilawila kwenye hafla hiyo ya makabidhiano.

Na Mwandishi Wetu, Moshi
MFANYABIASHARA na mzaliwa wa Kijiji cha Uchau Kaskazini wilaya ya Moshi Vijijini, Emmanuel Mallya, ameikabidhi serikali zahanati ikiwa na vifaa vya kisasa vikiwamo vitanda vya wagonjwa vinavyotumia nishati ya umeme.

Zahanati hiyo inayojukana kwa jina la EB zahanati, imejengwa na mfanyabiashara huyo kwa kutumia nguvu zake mwenyewe bila kuhusisha msaada kutoka Halmashauri ya wilaya ya Moshi wala serikali kuu.

Akizungumza katika hafla fupi ya kuikabidhi zahanati hiyo kwa serikali, mfanyabiashara huyo alisema wazo la kujenga zahanati hiyo lilitokana na kuwepo na changamoto za umbali wa huduma za afya kwa wananchi wa eneo hilo.

Alisema changamoto hiyo ilipelekea kuwepo na vifo vya watu wengi vilivyochangiwa na umbali wa upatikanaji wa vituo vya afya na kwamba changamoto hizo ndizo zilizomsukama kuona haja ya kujenga zahanati hiyo.

Alitoa wito kwa mamlaka husika kuitunza zahanati hiyo pamoja na vifaa vitakavyotumika katika kuwahudumia wagonjwa huku akitoa wito kwa watu wengine wenye uwezo kujitolea katika kuwahudumia wananchi wasio nacho.

“Utajiri unatokana na moyo wa mtu alionao, unaweza ukawa na utajiri na usiwe na moyo wa kuwasaidia wengine, kila mtu amepewa karama na mwenyezi Mungu, muhimu hapa ni namna ya kuzitambua hizo karama,” alisema.

Kabla ya ujenzi huo ulioanza julai mwaka 2013, familia iliyokuwa ikishi mahali ilipojengwa shule hiyo iliridhia ombo la mfanyabaishara huyo la kuachia eneo hilo na kupelekwa kwenye eneo jingine kwa ushirikiano wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Kimasio.

Aliwapongeza familia hiyo kwa kukubali ombi lake la kuliachia eneo hilo na kuongeza kuwa, bila familia hiyo kuridhia kuondoka katika eneo hilo ndoto zake za kujenga zahanati katika eneo hilo zingeishia ukingoni.

Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini, Anthony Komu alihimiza usimamizi wa karibu wa zahanati hiyo kwa wale watakakuwa wasimamizi baada ya aliyeijenga kuikabidhi kwa serikali.

"Mhehsimiwa Mkuu wa Wilaya, uzoefu unaonyesha kuwa, miradi mingi inayojengwa na wafadhili imekuwa ikiharibika kutokana na kutokuwepo na usimamizi wa karibu, ni rai yangu kuwa tuitunze zahanati hii isijekuwa mazalia ya popo kama ambavyo tumekuwa tukishuhudia kwa baadhi ya zahanati na vituo vya afya,” alisema.

Alisema mfanyabiashara huyo ametenda wema wa hali ya juu kwa wananchi wa Wilaya ya Moshi Vijijini na Vunjo kwa ujumla  na kwamba wema huo kamwe hautafutika ndnai ya mioyo ya wananchi hao. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Michael Kilawila, alitoa wito kwa wananchi wa wilaya hiyo kuchangishana kwa kile kidogo walichonacho ili wanunue gari la wagonjwa ambalo litahudumia zahanati hiyo kwa muda wa saa 24.

Alisema uwepo wa gari la wagonjwa katika zahanati hiyo utarahisisha kuwapeleka wagonjwa katika Hospitali kubwa ikiwamo ya Kibosho, Mawenzi na KCMC kwa wale ambao watahitaji kupewa rufaa.

Alisema maendeleo yanahitaji umoja na mshikamano na kuonya kuwa maendeleo hayana itikadi yoyote ya kisiasa kwani zahanati hiyo itahudumia wananchi wote bila kujali huyu ni wa chama gani.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa wilaya ya Moshi, Kippi Warioba alipongeza moyo ulioonyeshwa na mfanyabiashara huyo wa kusaidia watu wenye mahitaji. Pia alitoa wito kwa serikali ya kijiji hicho kuanza mazungumzo na wananchi wanaoishi karibu na zahanati hiyo kuachia maeneo yao ili zahanati hiyo ipanuliwe na kufika hadhi ya kituo cha Afya.

Alitoa wito kwa kila mtu kuchangia chochote alichonacho ndani ya jamii na si lazima iwe pesa na kuwapongeza walioachia eneo ilipojengwa zahanati hiyo wametoa mchango mkubwa sana kwa jamii.

ANZA MWAKA MPYA WA 2018 NA MALENGO HAYA

$
0
0
Na Jumia Travel Tanzania

Baada ya pilikapilika za msimu wa sikukuu na sherehe za kuuaga mwaka 2017 na kuukaribisha mwaka 2018, huu ni muda muafaka kwako wa kujiwekea malengo mapya.
Malengo hutofautiana kulingana na kitu gani unataka kukifanikisha ndani ya kipindi cha muda fulani. Kwa mfano, kuacha kula aina ya vyakula fulani au vinywaji kutokana na kuvitumia kipindi cha sikukuu; kubana matumizi ili kukusanya kiasi fulani cha pesa; au kufanya mazoezi ya kutosha ili kurudia ile hali yako ya zamani kabla ya sikukuu, nakadhalika.

Kukurahisishia baadhi ya malengo ambayo unaweza kujiwekea mwanzo huu wa mwaka, Jumia Travel imemekukusanyia malengo yafuatayo machache ambayo yanaweza kukufaa endapo utayazingatia.
Punguza muda wa kuangalia luninga, soma zaidi vitabu. Kuna faida nyingi za kusoma vitabu kuliko watu wanavyofikiria kama vile kuongeza maarifa juu ya masuala mbalimbali, kupata ujuzi pamoja na kuburudisha. Kwa mujibu wa wataalamu kusoma vitabu huimarisha afya ya akili yako pamoja na kukuongezea namna ya kuwasiliana na kuwaelewa watu. Hivyo basi, kama ulikuwa unatumia muda mwingi zaidi kutazama luninga basi jaribu kuutumia pia kwa kusoma vitabu.
Lala mapema. Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, ukosefu wa usingizi unaweza kusababisha hatari ya kupata magonjwa kama vile kisukari, ugonjwa wa moyo, utapiamlo na msongo wa mawazo. Mwaka huu mpya jaribu kujiwekea utaratibu wa kulala mapema, weka kengele ya kukumbusha na hakikisha unaizingitia ili angalau ulale masaa 7 au 8.

Jaribu kuwa mbali na simu yako. Nadhani unaweza kuwa umeona mara kadhaa namna simu ya mkononi inavyowafanya watu kutokuwa makini au kuutoa muda wao kikamilifu katika baadhi ya shuguli. Unaweza kukuta kwenye kusanyiko la familia au kikao na mtu muhimu lakini simu inakuwa chanzo cha kuondoa umakini. Jaribu kulidhibiti hilo kwa kuizima kila unapokutana na watu muhimu au tukio kwa kipindi cha muda fulani au hata siku nzima pia kama ikiwezekana.

Weka akiba. Hakuna jambo ambalo lina changamoto kama kujiwekea akiba ya fedha. Wengi wetu hatujui namna ya kudhibiti matumizi ya pesa tunazozipata. Tunajikuta tunaweka hifadhi ya pesa baada ya matumizi kitu ambacho sio sahihi. Inashauriwa kwamba weka akiba ya fedha kwanza ndipo utumie kiasi kilichobakia. Na hakikisha unajitahidi kutumia kiasi ambacho umekwishajiwekea bajeti ili usiitumie akiba uliyojiwekea.

Punguza muda unaoutumia mitandaoni. Ni vizuri kutumia muda mtandaoni kwani unakupatia fursa ya kupata taarifa, maarifa pamoja na kujuana na watu tofauti. Lakini kutumia muda mwingi huko kunaweza kuwa na madhara kwako bila ya kutarajia. Wataalamu wamegundua kwamba kutumia muda mwingi mitandaoni kunaweza kuathiri afya ya akili yako, wanadai kwamba kunaweza kupelekea mtu kutojiamini kutokana na yale yanayoendelea mitandaoni.
Punguza madeni. Mwaka huu ufanye usiwe na madeni mengi yasiyo na tija ambayo hunyonya fedha zako na kukufanya kutotimiza malengo yako. Hakikisha kwamba unamaliza kulipa madeni uliyonayo ili uwe huru kifedha. Haukatazwi kukopa na ni jambo la busara wakati mwingine kwani hukuwezesha kufanikisha jambo ambalo hauna uwezo nalo kwa wakati uliopo. Lakini hakikisha unakopa kwa ajili ya jambo la maendeleo na siyo starehe.

Tumia muda zaidi na familia yako. Inawezekana mwaka ulioisha haukupata muda wa kutosha wa kutumia pamoja na familia yako badala yake ulikuwa umetingwa na kazi au marafiki. Wengi wetu huwa tunagundua ni jambo jema kutumia muda na familia hususani kwenye kipindi cha sikukuu. Unaweza kulibadili hilo kwa kujiwekea malengo mapema. Unaweza kupanga labda kila baada ya mwezi mmoja, miezi mitatu au minne.
Tabasamu, kutana na watu zaidi! Kuwa na furaha ni chaguo lako. Changamoto kwenye maisha lazima zitakuwepo, lakini ni chaguo lako aidha kuziruhusu zikuathiri au la. Jumia Travel inaamini kwamba mwaka huu mpya ufanye uwe wa pekee kwa kubadili mtazamo juu ya maisha yako, kutana zaidi na watu, badilishana mawazo, huwezi kufahamu kwani kwa kuzungumza zaidi na watu kunaweza kukufungulia milango ya fursa kwenye maisha yako!

Heri ya mwaka mpya 2018 na uwe wenye mafanikio tele kwako!

Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images