Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live

MAMIA WAMZIKA MKE WA MWANDISHI WA HABARI WA GAZETI LA MWANANCHI MKOANI TANGA

$
0
0
 Sehemu ya waandishi wa habari mkoani Tanga wakiwa nyumbani kwa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi mkoani Tanga,Burhan Yakub ambaye alifiwa na mkewe wakati wa mazishi ambayo yamefanyika leo Makaburi ya Magomeni Jijini Tanga
Sehemu ya waombolezaji wakiwa wamelibeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mke wa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Mkoani Tangawakilipeleka makaburini tayari kwa ajili ya maziko.
 Sehemu ya waombolezaji wakiwa msibani eneo la Magomeni Jijini Tanga
 Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali Jijini Tanga wakiwa msibani leo katikati mwenye tisheti ya mistari ni Mwandishi Mwandamizi wa ITV na Radio One mkoani Tanga,William Mngazija kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Tanga,Hassan Hashim
 Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Mkoani Tanga,Burhan Yakub kushoto ambaye amefiwa na mkewe akiwa na ndugu jamaa wakati wa msiba huo nyumbani kwake eneo la magomeni Jijini Tanga.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella akiingia kwenye eneo la Msiba leo
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella katikati akiwa eneo la msibani Magomeni Jijini Tanga kulia ni Katibu Itikadi na Uenezi CCM wilaya ya Tanga,Lupasio Kapange

 Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kushoto akisalimiana na wananchi waliokuwepo msibani mara baada ya kuwasili
Wananchi wakifukia mwili wa aliyekuwa mke wa Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Mwananchi mkoani Tanga,Burhan Yakub
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akisalimiana na Katibu wa CCM mkoa wa Tanga,Allan Kingazi wakati wa mazishi hayo
  Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto,Ummy Mwalimu akisalimiana na Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga,Alhaj Mustapha Selebosi
Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoani Tanga,Hassan Hashimn akiteta jambo na wandishi wa habari mkoani Tanga wakati wa msiba huo(Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

MAMIA YA WAKAZI DAR KUMUAGA MWANAHABARI JUSTINE LIMONGA

$
0
0

 Waombolezaji na wanahabari wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mwanahabari wa Uhuru FM, Justine Limonga, wakati ukiwasili Viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuagwa kabla ya kufanyika mazishi yake Makaburi ya Saku yaliyopo nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam leo.
 Katibu  wa Itikadi na Uenezi  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamphrey Polepole, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza la mwanahabari, Justine Limonga.
 Waombolezaji wakisubiri kubeba jeneza lenye mwili wa marehemu kwenda eneo maalumu ilipo kufanyika ibada hiyo.
 Familia ya marehemu ikiwa kwenye ibada hiyo.
 Kwaya ya Mtakatifu Kizito ya Parokia ya Kutukuka kwa Msalaba Kizuiani, ikitoa burudani.
 Katekista wa Parokia ya Kutukuka kwa Msalaba Kizuiani,  Philo Mbunda, akitoa mahubiri.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Ibada ikiendelea
 Mwanamuziki Nguri, John Kitime akizungumzia jinsi alivyomfahamu marehemu Limonga.
 Mwakilishi wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA), Moni Nyangasa, akizungumza kwenye ibada hiyo.
 Msemaji wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Alfred Lucas, akizungumza kwenye ibada hiyo.
 Mbunge wa zamani wa Temeke, Abbas Mtemvu akimzungumzia marehemu Limonga.
 Mbunge wa Mbagala,  Issa Mangungu, akizungumza.
 Waombolezaji wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM, Angel Akilimali, akizungumza katika ibada hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM, Angel Akilimali, akiwapa pole wafiwa.


Mwanamuziki nguri, Hussein Jumbe, akiimba wimbo maalumu aliomtungia mwanahabari Justine Limonga.

Dotto Mwaibale na Kulwa Mwaibale

Katibu  wa Itikadi na Uenezi  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hamphrey Polepole, ameongoza mamia ya waombolezaji katika ibada ya kuaga mwili wa mwanahabari, Justine Limonga iliyofanyika Viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam leo mchana.

Akizungumza katika ibada hiyo, Polepole alisema CCM na tasnia ya habari imepoteza mtu muhimu ambaye alikuwa bado akitegemewa.

"Tumempoteza mtu muhimu ambaye alikuwa akitegemewa kama chama tutaangalia namna ya kuisaidia familia yake," alisema Polepole.

Mkurugenzi wa Nduvini Auto Garage, Alhaji Ahmed Msangi alizungumza jinsi alivyomfahamu marehemu ambapo aliahidi kampuni yake kwa kipindi hiki cha kufunguliwa kwa shule itawanunulia vifaa vya shule, sare na kuwalipia karo wakati wakisubiri kukaa na familia kuona namna ya kuwazesha watoto hao kielimu.

Kaimu Mkurugenzi wa Uhuru FM, Angel Akilimali alisema kifo cha mwanahabari huyo aliyekuwa mwajiriwa wao kimeacha pengo kubwa ambalo halitazibika.

Alisema Limonga alikuwa mhariri na mbunifu na aliweza kuongoza vipindi mbalimbali ambavyo vilipendwa na wasikilizaji wa Uhuru FM ambapo aliahidi stahiki zote za marehemu kama mwajiriwa zitapatikana kwa wakati.

Katika ibada hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, dini, siasa wanamuziki na wanahabari na wananchi iligubikwa na majonzi na baadhi ya watu kushindwa kujizuia kulia.

Akitoa mahubiri kwenye ibada hiyo Katekista wa Parokia ya Kutukuka kwa Msalaba Kizuiani,  Philo Mbunda alisema mwenzetu Limonga amemaliza kazi ya hapa duniani je sisi tuliobakia tumejiandaeje?

Mbunda alisema kila mtu anapaswa kujitafakari maisha yake ya kiroho kabla ya kifo na hivyo ndivyo Mungu wetu anavyohitaji.

Limonga alifariki dunia Desemba 30, mwaka jana katika Hospitali ya TMJ alikolazwa akitibiwa na ameacha mjane na watoto wawili ambapo mazishi yake yamefanyika leo katika Makaburi ya Saku yaliyopo Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA KIBIASHARA NCHINI ARGENTINA

TRA YAZINDUA KAMPENI YA USAJILI WA WALIPAKODI

MILIONI 400 ZA OFISI YA RAIS – TAMISEMI KUJENGA NA KUKARABATI KITUO CHA AFYA MALANGALI HALMASHAURI YA MUFINDI

$
0
0
HALMASHAURI ya Wilaya ya Mufindi itatumia jumla ya shilingi Milioni Mianne (400) kujenga na kufanya ukarabati mkubwa wa kituo cha Afya Malangali, kilichopo kata ya Malangali Halmashauri ya Wilayani Mufindi, ikiwa ni mkakati wa Serikali kuimarisha sekta muhimu ya Afya hususani Afya ya Mama na Mtoto.

Ujenzi na ukarabati wa kituo hiki cha Afya, unaotarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa, unafanyika baada ya Ofisi ya Rais – Tamisemi, kutoa kiasi cha Shilingi Milioni mianne (400) kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya kituo hicho ili kiweze kukidhi haja ya kutoa huduma bora za Afya kwa zaidi ya Wananchi elfu arobaini na nane (48,000) wa Tarafa ya Malangali watakao pewa rufaa kutoka kwenye Zahanati za Vijiji.

Matumizi ya kiasi hicho cha fedha, ni pamoja na kujenga jengo la kisasa la Maabara, Nyumba ya Mganga, kukamilisha ujenzi unaoendelea wa chumba cha upasuaji sanjari na kufanya ukarabati mkubwa wa Wodi maalum ya wazazi / Mama na Mtoto.

Ujenzi na ukarabati wa kituo, utatekelezwa kwa mfumo wa (Force Account) ambapo, Halmashauri itatumia Mafundi wenyeji watakaothibitishwa kuwa na uwezo unaokubalika wa kutekeleza jukumu hili kwa kipindi kisichozidi miezi mitatu, badala ya mtindo uliozoeleka wa kutumia Wakandarasi. Pia, ili kuhakikisha mradi huu unatekelezwa kwa viwango vinavyokubalika, Ofisi ya Mkurugenzi mtendaji, imeunda Vikosi kazi vitatu (03) vikijumuisha Maofisa kutoka idara mbalimbali maalum kwa kuratibu na kusimamia mradi huu kwa kuzingatia wakati na ubora.

Aidha, kwa kuwa uboreshaji wa kituo hiki, utatekelezwa kwa mfumo wa (Force Account) kama ambavyo imefafanuliwa hapo juu, Mkurugenzi Mtendaji anawahamasisha wananchi wote wa Tarafa ya Malangali kujitolea nguvu kazi pindi itakapohitajika wakati wa utekelezaji wa mradi huu kwa ustawi wa Afya ya kila mkazi wa Tarafa ya Malangali na Halmashauri ya Mufindi kwa ujumla.

Imetolewa na,

Ndimmyake Mwakapiso,
Ofisa Habari na Mawasiliano Halmashauri ya (W) Mufindi.
Profesa Riziki Shemdoe, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mufindi.
 

MAENDELEO HAYANA MIPAKA YA VYAMA-DKT MWANJELWA/

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akishiriki ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Iyera wakati akiwa ziarani Mkoani Mbeya, Jana 2 Januari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikabidhi mifuko 20 ya saruji kwa ajili ya kuongeza nguvu katika ujenzi wa vyumba vya madarasa shule ya Sekondari Iyera wakati akiwa ziarani Mkoani Mbeya, Jana 2 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akichanganya udongo wakati akishiriki ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Iyera wakati akiwa ziarani Mkoani Mbeya, Jana 2 Januari 2018. Wengine (Kulia) aliyeshika jembe ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe Paul Ntinika na Kushoto ni Diwani wa Kata ya Iyera (CHADEMA) Mhe Charles Mkera
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akipanga mawe kwenye msingi wa darasa ishara ya mafundi kuanza haraka ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Iyera wakati akiwa ziarani Mkoani Mbeya, Jana 2 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akimpongeza Diwani wa Kata ya Iyera (CHADEMA) Mhe Charles Mkera kwa kushirikiana na serikali na kuhamasisha wananchi katika ushiriki wa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Iyera wakati akiwa ziarani Mkoani Mbeya, Jana 2 Januari 2018.

Na Mathias Canal, Mbeya


Maendeleo ni mchakato wa kujenga jamii endelevu, yenye kujiamini,  kujituma na uwezo wa kushiriki, kwa misingi ya usawa na kuheshimiana, katika kubuni, kuandaa na kutekeleza mipango ya kujiletea “maendeleo” na kutumia matokeo ya kazi zao.


Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa amekuwa mwalimu mzuri wa somo la Uraia Mkoani Mbeya akifundisha kuhusu umoja na mshikamano huku akisisitiza kuwa Maendeleo ni dhana pana kwa wananchi na hayapaswi kufanywa kwa mipaka ya vyama vya siasa.


Mhe Mwanjelwa ameyasema hayo Jana 2 Januari 2018 wakati akizungumza na wananchi na mafundi wanaojenga majengo ya Shule ya Sekondari Iyera ili kutatua changamoto ya kuwa na vyumba vingi vya madarasa kwa ajili ya kuhimili wingi wa wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.


Amewasisitiza mafundi hao kujenga madarasa hayo kwa haraka na viwango vya hali ya juu kwani shule zinatarajiwa kufunguliwa hivi karibuni huku shule hiyo ikiwa na upungufu wa vyumba vinne vya madarasa.


Mhe Mwanjelwa alisema kuwa tangu serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli kutangaza utoaji elimu bure kuanzia ngazi ya shule ya msingi hadi sekondari kumekuwa na ongezeko kubwa la wananfunzi wanaojiunga na masomo ikiwa ni pamoja na kurejea shuleni kwa wananafunzi waliokata tamaa ya kuendelea na masomo.


Alisifu juhudi za Uongozi wa Wilaya ya Mbeya kwa kushirikiana kwa pamoja na wananchi katika shughuli za maendeleo huku akiipongeza Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa kufanya vyema na hatimaye kuongoza kwa ufaulu wa wanafunzi dhidi ya Halmashauri zingine za Mkoa wa Mbeya.


Sambamba na hayo pia Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa ameongeza nguvu kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule hiyo ya Sekondari Iyera kwa kuchangia mifuko 20 ya saruji.

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI LATOA ONYO KALI KUHUSU UNUNUZI WA VIFAA VYA ZIMAMOTO

$
0
0
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeundwa na linatekeleza majukumu yake chini ya Sheria ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji namba 14 ya mwaka 2007 (Fire and Rescue Force Act No. 14 of 2007). Majukumu makubwa ya Jeshi hili ni kuokoa Maisha na Mali katika majanga yatokanayo na moto, mafuriko, tetemeko la ardhi, ajali za barabarani pamoja na majanga mengine.

Sambamba na majukumu hayo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linafanya ukaguzi kwenye vyombo vya usafiri na usafirishaji, na kutoa ushauri uwekaji wa vifaa vya kinga na tahadhari. Ukaguzi huu unafanyika kwa mujibu wa sheria namba 14 ya mwaka 2007 ikisomwa pamoja na kanuni ya Vyeti na Usalama wa moto Mwaka 2008 na marekebisho ya mwaka 2014 (Fire and Rescue Force Safety Inspections and Certificates Regulations of 2008 GN.106 and its Amendment GN 63 of 2014.)

Pamoja na kanuni ya tahadhari dhidi ya moto kwenye majengo ya mwaka 2015 (Fire and Rescue Force Fire Safety Precaution in Building Regulations of 2015 GN 516.) Kwa kuzingatia majukumu hayo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linajulisha umma kuwa, halifanyi biashara ya kuuza vifaa vya kuzimia moto wala kuvifanyia matengenezo (service) vifaa hivyo pamoja na mifumo ya kinga na tahadhari dhidi ya moto. Bali Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linasimamia na kuhakiki ufungwaji wa vifaa hivyo.

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatoa rai kwa wamiliki wa majengo na vyombo vya usafiri na usafirishaji, wafanyabiashara na wananchi wote kuhakikisha wananunua au kufanyia matengenezo (service) vifaa na mifumo ya kinga na tahadhari dhidi ya moto kwa Mawakala waliosajiliwa kuuza vifaa vya Zimamoto (Fire Dealers) kwa mujibu wa sheria ya Jeshi.

Imetolewa na;
Ofisi ya Habari na Elimu kwa Umma
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
03 Januari, 2018

KHERI APOKELEWA MWANZA KWA KISHINDO

$
0
0
Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James kulia akisalimiana na Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Ndg:Anthony Dialo mara baada ya kuwasili katika ofisi za Ccm Mkoa wa Mwanza.
Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akiteta jambo na Mwenyekiti wa Ccm mkoa wa mwanza Dr. Anthony dialo.
Kaimu katibu mkuu wa Umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi Shaka Hamdu Shaka akizungumza na Wanachama wa CCM Mkoa mwanza katika Ofisi za CCM Mkoa wa Mwanza.
Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akizungumza na wanachama wa chama cha mapinduzi mkoa wa mwanza akielekea Uwasha wa CCM KIRUMBA.
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Ilemela na Naibu waziri wizara ya Ardhi Dkt Angelina Mabula alipowasili katika mapokezi  Uwanja wa CCM Kirumba
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akisalimia na mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ilemela
Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akiwasalimia na wanachama wa chama cha mapinduzi na jumuiya zake Uwanja wa Ccm kirumba.
wanachama wa Ccm Wakipugia mikono
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akivikwa skafu mara baada ya kuwasili Uwanja wa CCM Kirumba
 zoezi likiendelea
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akiwasalimia Wanachama wa CCM na Jumuiya zake waliohudhulia katika  uwanja wa CCM Kirumba
 
 vijana wa CCM wakionyesha ukomavu wao
Sehemu ya Viongozi


 kikundi cha ngoma toka bujoro kikitumbuiza
 Mwanachama wa CCM Akiwa amebebelea kipeperushi kwa uso wa furaha
 Sehemu ya madiwani na viongozi wilaya ya ilemela
 Viongozi meza kuu wakifuatilia mkutano
Katibu wa CCM Mkoa wa mwanza Ndg:raymond akizungumza katika mkutano
 Mama mzazi wa Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akitoa shukrani kwa wana CCM .
 Mbunge wa jimbo la Ilemela na naibu waziri wa Ardhi Dkt Angelina Mabula akizungumza katika mkutano wa kumpongeza kwa ushindi na kumkaribisha Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akipokea taarifa za pongezi kwa wazee wa kata ya kirumbo
 Mkuu wa mkoa wa mwanza John mongela akizungumza
 wazee wa mkoa wa mwanza wakimsimika Utemi Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akinyanyua silaa juu mara baada ya kusimikwa.(PICHA NA FAHADI SIRAJI)


Makamu mwenyekiti wa UVCCM akizungumza.
 Kaimu katibu mkuu wa Umoja wa vijana wa CCM Shaka Hamdu Shaka akizungumza na viongozi pamoja na Wanachama wa CCM na Jumuiya zake mkoa wa Mwanza wakati akimkaribisha Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James kuzungumza.(PICHA NA FAHADI SIRAJI)
 Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James akizungumza na Viongozi pamoja na wanachama wa CCM na jumuiya zake mkoa wa mwanza (PICHA NA FAHADI SIRAJI)
wanachama wakifurahia hotuba ya Mjumbe wa Kamati kuu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Kheri D James(PICHA NA FAHADI SIRAJI)





Zawadi ya vijana kata ya Kirumba (PICHA NA FAHADI SIRAJI)







MKAZI MIWNGINE WA TEMEKE MIKOROSHINI AIBUKA NA KITITA CHA MILIONI 50 ZA TATUMZUKA.

$
0
0
  Katibu Tawala wilaya ya Temeke, Ndugu Hashim Komba akikabdhi  mfano wa hundi kwa mshindi wa mchezo wa bahati nasibu wa Tatumzuka  Enirisha Kilango mapema leo kwenye ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Temeke.Enirisha Kilango ambaye ni Mkazi wa Temeke Mikoroshini anaejishughulisha na biashara zake ndogo ndogo alijishindia milioni 50 mwishoni mwa wiki
Enirisha Kilango ambaye ni Mkazi wa Temeke Mikoroshini anaejishughulisha na biashara zake ndogo ndogo akizungumza mapema leo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) ndani ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke,kufuatia ushindi wake wa kujinyakulia milioni 50 mwishoni mwa wiki katika mchezo huo wa kubahatisha.
 Katibu Tawala wilaya ya Temeke, Ndugu Hashim Komba akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Temeke, mbele ya Waandishi wa habari  (hawapo pichani) mapema leo,kabla ya kukabidhi mfano wa hundi kwa mshindi wa mchezo wa bahati nasibu wa Tatumzuka kwa mshinidi aliyejinyakulia Enirisha Kilango aliyejishindia milioni 50 mwishoni mwa wiki .

Ndugu Komba amewashukuru Tatumzuka kwa kuendelea kuwawezesha wananchi wa wilaya hiyo ya Temeke kupitia mchezo huo wa bahati nasibu,kwa kumpata mshindi mwingine ndani ya wilaya hiyo kwa mara nyingine tena,Komba amewasisitizia wananchi wake kuendelea kucheza zaidi na zaidi kwani mchezo ambao upo kisheria na hauna makando kando yoyote,ukishinda umeshinda kweli na fedha zako unakabidhiwa.

Mh Komba aliongeza kuwa kama Tatumzuka itawapatia shilingi Milioni Tano ambayo  imepatikana mara baada ya mshindi huyo kupatikana,basi watazitumia fedha hizo kuimarisha suala la ulinzi na usalama, tutakwenda kujenga kituo cha polisi na kuzitumia fedha hizo kununua mabati ili kukamilisha ujenzi wa vituo hivyo.

WADAU WAPONGEZWA KWA KUTIMIZA MIAKA 50 YA NDOA ( 1967-2017)

$
0
0
 Bwana. Hamisi Kambona na Mkewe Bibi. Hawa Salimu wakiwa katika hafla fupi ya kuadhimisha miaka hamsini (50) ya ndoa yao iliyofanyika Disemba 30, 2017 nyumbani kwake Mkoani Morogoro. Bwana. Hamisi Kambona na Bibi. Hawa Salimu walifunga ndoa mwaka 1967. Watoto, Marafiki, Ndugu na Jamaa wanawapongeza sana, wanawatakia heri nyingi na Mungu aendelee kuwabariki.

NAIBU MEYA JIJI LA MBEYA (CHADEMA) AAHIDI USHIRIKIANO NA WATEULE WA RAIS MAGUFULI AMSIFU MHE MWANJELWA KUSHIRIKIANA NA VYAMA VYA UPINZANI

$
0
0

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018. Picha Zote Na Mathias Canal
Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Mhe Fanuel Kyanula ambaye ni Diwani wa Kata ya Sinde akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua hatua zilizofikiwa katika ujenzi wa Vyumba vya madarasa Shule ya Sekondari Sinde kabla ya kuzungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018
Baadhi ya wananchi wakimlaki Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa mara baada ya kuwasili kwa ajili ya Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018.
Diwani wa Kata ya Manda Mkoani Mbeya Mhe Newton Mwakijobe akitoa salamu za wananchi wa Kata yake kwenye mkutano wa wananchi wa kata jirani ya Sinde kabla ya Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa kuzungumza na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo Jana Januari 2, 2018


Na Mathias Canal, Mbeya


IMEBAINIKA kuwa tofauti za kiitikadi baina ya madiwani katika Halmashauri nyingi nchini, zimekuwa ni kikwazo kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye tija kubwa kwa wananchi.

Tofauti hizo zimekuwa chanzo kikubwa katika utekelezaji wa miradi inayobuniwa na Halmashauri husika, au inayoletwa na Serikali Kuu na wafadhili. Mitazamo ya kisiasa, tofauti ya uwakilishi wa vyama na ubinafsi, ndio sababu kuu.

Katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya inayoongozwa na Meya na Naibu Meya wanaotokana na vyama vya upinzania hali imekuwa tofauti kwani asilimia kubwa ya madiwani wanaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli tofauti kabisa na Halmashauri zingine.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana 2 Januari 2018 uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina, Kata ya Sinde Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Mhe Fanuel Kyanula ambaye ni Diwani wa Kata ya Sinde alisema kuwa utendaji wa Rais Magufuli ni faida ya watanzania wote hivyo kuna kila sababu ya wananchi kuunga mkono juhudi za serikali yake.

Kyanula alisema kuwa pamoja na kuwa kiongozi anayetokana na chama cha upinzani lakini serikali ni moja hivyo anaungana na wateule wote wa Rais Magufuli katika kutekeleza dhamira ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo huku akimtaja Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa kama kiongozi wa mfano katika Mkoa wa Mbeya hivyo kuahidi kushirikiana nae kwa karibu.

Naibu Meya huyo amempongeza Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa kwa kuchangia jumla ya mifuko 40 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Iyera (Mifuko 20) na Shule ya Sekondari Sinde (Mifuko 20) zilizopo Jijini Mbeya.

Alimtaja Mhe Mwanjelwa kwamba amekuwa mwalimu mzuri wa somo la Uraia Mkoani Mbeya akifundisha kuhusu umoja na mshikamano huku akisisitiza kuwa Maendeleo ni dhana pana kwa wananchi na hayapaswi kufanywa kwa mipaka ya vyama vya siasa.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa yupo ziarani Mkoani Mbeya ambapo amesifu Uongozi wa Wilaya ya Mbeya kwa kazi kubwa katika utendaji ikiwemo kuanza mchakato wa ujenzi wa vyumba vya madarsa ili kuikabili changamoto ya wingi wa wananfunzi waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2018.

MAKAMU WA RAIS AHUDHURIA MSIBA WA MKE WA KANGI LUGOLA

$
0
0



 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola alipofika kutoa pole ya msiba wa mke wa Kangi Lugola, Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.
4
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa mke wa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Kangi Lugola, Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.
7
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiifariji familia ya Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Kangi Lugola wakati alipoenda kuwapa pole ya msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola nyumbani kwao klabu ya reli, Gerezani, jijini Dar es Salaam.
9
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.Kangi Lugola wakati alipoenda kutoa pole ya msiba wa mke wake Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.
16
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapa pole watoto wa  marehemu Mary Lugola , mke wa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola aliyefariki siku ya tarehe 01, Januari, 2018 katika hospitali ya Rabininsia jijini Dar es Salaam.
10
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa msibani kwa Kamishna Msaidizi wa Polisi marehemu Mary Lugola mke wa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola, wengine pichani ni Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. January Makamba (wa kwanza kushoto), Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Joseph Malongo (wa pili kulia) na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Butamo Phillip.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
……………..
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo tarehe 3, Januari, 2018 amehani msiba wa Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola ambaye ni Mke wa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola.

NEC YATANGAZA TAREHE YA KUFANYIKA KWA UCHAGUZI MDOGO KATIKA JIMBO LA SIHA NA KINONDONI PAMOJA NA KATA 4 ZA TANZANIA BARA

$
0
0
Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Hamid Mahmod Hamid 
 
Subira Kaswaga – NEC

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa uchaguzi mdogo katika majimbo ya Siha mkoani Kilimanjaro na Kinondoni mkoani Dar es Salaam pamoja na Kata nne za Tanzania Bara utafanyika Februari 17, 2018 kufutia waliokuwa Wabunge katika majimbo hayo kujivua Uanachama na kukosa sifa za kuendelea kuwa wabunge.

Taarifa ya Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Hamid Mahmod Hamid imeeleza kuwa pamoja na Majimbo hayo,pia Kata nne za Isamilo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza, Manzase Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Madanga Halmashauri ya Wilaya ya Pangani mkoani Tanga na Kimagai Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma zitafanya Uchaguzi mdogo

Aidha, Jaji Mkuu (Mst. Zanzibar) Hamid Mahmoud Hamid amesema kuwa, Tume inaendesha uchaguzi huo baada ya kupokea barua kutoka kwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Mh. Job Ndugai kuhusu uwepo wazi wa jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam na Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro.

Jaji Mahmoud amesema kuwa, barua hiyo ilieleza kuwa majimbo hayo yapo wazi baada Maulid Mtulia aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kujivua uanachama wa CUF na Dr. Godwin Mollel wa jimbo la Siha kujiuzulu uanachama wa CHADEMA na hivyo wote kukosa sifa za kuwa Wabunge.

Pia, ameeleza kuwa Tume ilipokea taarifa kutoka kwa Waziri mwenye dhamana ya Serikali za Mitaa ikiitaarifu Tume uwepo wa nafasi wazi za Udiwani katika kata nne za Tanzania Bara.

“Baada ya kupokea barua hizo Tume kwa kuzingatia vifungu vya 37(1) na 46(2) vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi sura ya 343 pamoja na kifungu cha 13(3) cha Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa sura ya 292 inatangaza kuwa majimbo mawili na kata nne zipo wazi” alisema Jaji Mahmoud.

Ameeleza kuwa, fomu za uteuzi kwa majimbo hayo mawili na kata nne itakuwa kati ya tarehe 14 – 20 Januari, 2018, uteuzi wa wagombea utafanyika tarehe 20/01/2018, na Kampeni za uchaguzi mdogo zitafanyika kuanzia tarehe 21/01 – 16/02/2018 na siku ya uchaguzi itakuwa tarehe 17/02/2017.

Vilevile, Jaji Mahmoud amevikumbusha Vyama vya Siasa na wadau wote wa uchaguzi kuzingatia sheria, kanuni, taratibu, miongozo na maelekezo yote wakati wa uchaguzi huo mdogo.

TONY ELUMELU FOUNDATION ACCEPTING APPLICATIONS FOR 4th CYCLE OF $100M ENTREPRENEURSHIP DEVELOPMENT PROGRAMME

$
0
0
APPLICATION DEADLINE: March 1, 2018
PROGRAM DATES: May 1 –  December 2018
/Volumes/THE OMISORE/2018 Application Drive - Graphic Designs/2018 Application Drive - BRANDING_Email Signature/Email  Signature.jpg
  LAGOS, NIGERIA – Africa’s largest philanthropy supporting entrepreneurship – The Tony Elumelu Foundation (TEF) is now accepting applications for business ideas that can transform Africa.
To apply, complete the online application at www.application.tonyelumelufoundation.org The deadline is midnight(WAT) on 1 March 2018.
The Programme provides critical tools for business success, including:
• Training: 12 weeks of intensive online training which guides creating and managing a business
• Mentoring: A world-class mentor to guide during the early transformation stages of the business
• Funding: $5,000* in seed capital to prove the concept, plus access to further funding
• Network: Access to the largest network of African start-ups and TEF’s own global contacts
The Programme, in its 4th cycle, is TEF’s 10-year, $100 million commitment to identify, train, mentor and fund 10,000 African entrepreneurs by 2024. 
TEF Founder, serial entrepreneur and philanthropist Tony O. Elumelu, CON said:
“When we launched the TEF Programme and committed $100 million to empowering Africa’s entrepreneurs, I knew we would create impact, but I never imagined it would be impact of this magnitude. We have unleashed a movement of African entrepreneurs -- a force so strong, so inspiring, that I am confident they will collectively transform Africa. We need Africa’s best and brightest entrepreneurs to come learn, grow their businesses and build our continent.”
1,000 entrepreneurs will be selected based on the viability of their idea, including: market opportunity; financial understanding; scalability; and leadership and entrepreneurial skills demonstrated in the application.
Eligibility:
1. The business must be based in Africa
2. The business must be for profit
3. The business must be 0-3 years old
4. Applicants must be at least 18 and a legal resident or citizen of an African country
CEO of the Foundation, Parminder Vir OBE said:
“We encourage women, French and Portuguese speakers to apply. Our 3,000 alumni are already growing their businesses and improving lives. If you have a transformational business or an idea, we have an opportunity for you.”
###
For more information or to apply, visit:  http://tonyelumelufoundation.org/programme/faqs/
* $5,000 seed capital is paid based on the official Central Bank of Nigeria naira equivalent value at the date of selection for the programme.
About The Tony Elumelu Foundation
Established in 2010, The Tony Elumelu Foundation (TEF) is the leading philanthropy in Africa championing entrepreneurship and entrepreneurs across the continent. The Foundation’s long-term investment in empowering African entrepreneurs is emblematic of Tony Elumelu’s philosophy of Africapitalism, which positions Africa’s private sector, and most importantly entrepreneurs, as the catalyst for the social and economic development of the continent. The Foundation’s flagship initiative, the TEF Entrepreneurship Programme, is a 10-year, $100 million commitment to identify, train mentor and fund 10,000 entrepreneurs, capable of changing the face of business across Africa.www.tonyelumelufoundation.org/teep @tonyelumeluFDN

NEC YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA KINONDONI NA SIHA PAMOJA NA KATA 4


VIBWANGA NA VITUKO VYATAWALA UCHAGUZI NAIBU MEYA DAR

$
0
0
* Meya wa Temeke, Ubungo nusura kuzichapa
 
Na Said Mwishehe, Blogu ya jamii

VITUKO, Vibweka, vitimbi na kila aina ya kejeli zimetawala wakati wa uchaguzi wa Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam.

Ilikuwa kama wanaigiza filamu lakini kumbe ndio ilikuwa namna ya kufanya uchaguzi huo ambao kwa sehemu kubwa majibizano yalichukua nafasi kubwa.

Uchaguzi wa kumpata Naibu Meya wa Jiji la Dar es Saalam umefanyika leo mchana na ulihusisha mgombea wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Mariam Lorida na mgombea wa Chama cha Wananchi(CUF) Mussa Kafana.

ILIKUWA HIVI
Kabla ya uchaguzi huo kufanyika, vibweka, vitimbi na majibizano yalitawala kati ya Vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi(Ukawa)dhidi ya upande wa CCM.

Ukawa hawakuwa tayari uchaguzi huo kufanyika kwani mgombea wao hakuwepo ukumbini huku CCM wakiona ipo haja ya kufanyika uchaguzi wa kumpata Naibu Meya ili shughuli za kimaendeleo zifanyike.

Wakati mjadala huo unaendelea Meya wa Jiji la Dar es Salaam Issaya Mwita hakuwepo ukumbini.Hivyo CCM na Ukawa wakawa wanalumbana aidha kufanyika au kutofanyika uchaguzi huo.
Wakati wanalumbana ziliibuka baadhi ya kauli ambazo CCM hawakuridhika nayo na hasa ile iliyodaiwa kutolewa na Meya wa Ubongo Boniphance Jacob baada ya kudai huenda mgombea wao ametekwa.
Kauli ambayo iliwakera baadhi ya wajumbe wa upande wa CCM na hasa Meya wa Temeke Abdallah Chaurembo kutaka Jackob afute kauli yake.

MEYA UBUNGO, TEMEKE NUSURA WAZICHAPE
Baada ya matokeo kutangazwa Meya Jackob alimkaba koo Meya wa Temeke Chaurembo.Sababu ni pale Chaurembo alipotaka kusogelea karatasi za kura.

Hivyo kukaibuka malumbano baina ya pande mbili, kiasi cha baadhi  askari polisi waliokuwa wamevaa kiraia kuamua kuingilia kati ili amani iendelee.

UKAWA WASHANGILIA
Matokeo ya uchaguzi huo yaliibua shangwe kwa Ukawa kwani ushindi huo wameamini umemeliza kiu yao ya kuitaka nafasi hiyo.Kwa mujibu wa nafasi ya Naibu Meya kila baada ta miezi sita wanafanya uchagizi.Hivyo Kafana amerudi tena kwenye nafasi hiyo.

CCM WATAFUTA MCHAWI
Ushindi wa mgombea wa Ukawa ukasababisha CCM kuanza kutafuta nani amewasaliti kwani kwa idadi ya washiriki walikuwa idadi sawa.Hivyo kwa matokeo hauo kuna Diwani wa CCM amewasaliti wenzake .Hali iliyoibua maswali.
  Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob  na Meya wa Manispaa ya Temeke Abdalah Chaurembo (aliyekaa chini) wakiwa wanaamuliwa na madiwani wengine  wakati wa uchaguzi wa kumtafuta Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam leo ambapo  uchaguzi huo ulijawa visa, vituko na vurugu za hapa na pale.
Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mussa Kafana (CUF) akiwa amelala ndani ya ukumbi wa Karimjee wakati wa  Uchaguzi wa kumtafuta  Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam uliofanyika leo jijini Dar es salaam na kuibuka mshindi baada ya kumshinda Mariam Rolida diwani wa  CCM kwa kura ya 12 dhidi ya 10.

 Meya wa Manispaa ya Temeke, Abdalah Chaurembo akizuiwa kuongoza kikao na Diwani wa Chadema Patrick Asenga wakati wa mchakato wa uchaguzi wa kumtafuta Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam.
 Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob (wa kwanza kulia) akizungumza na Madiwani wa Chama cha Mapinduzi wakati wa mkutano wa kumtafuta Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam leo.
  Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mussa Kafana akiwa anawasili katika ukumbi wa uchaguzi huku ameshikiliwa na madiwani wenzake  kufanikisha uchaguzi wa Naibu Meya wa Jiji.

MAGONJWA YASIYO YAKUAMBUKIZA YACHANGIA ASILIMIA 27 YA VIFO VYOTE NCHINI

$
0
0
Kaimu Mkurugenzi magonjwa yasiyo yakuambukiza Dkt. Sarah Maongezi akipokea tuzo ya Elimu kwa jamii kutoka kwa Mwenyekiti wa TANCDA Dkt. Tatizo Waane mapema leo katika ukumbi wa Hospitari ya Saratani ya Ocean Road, Wapili kutoka kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TANCDA Andrew Swai.
Kaimu Mkurugenzi magonjwa yasiyo yakuambukiza Dkt. Sarah Maongezi akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo katika picha) katika kikao kilichofanyika mapema leo katika ukumbi wa Hospitari ya Saratani ya Ocean Road kikihusu tuzo ya Elimu kwa jamii waliopata kutoka Shirikisho la kimataifa la magonjwa yasiyo yakuambukiza mwishoni mwa mwaka katika mkutano wa kimataifa uliofanyika katika falme zakiarabu, pembeni yake ni Mwenyekiti wa TANCDA Dkt. Tatizo Waane.

Kaimu Mkurugenzi magonjwa yasiyo yakuambukiza Dkt. Sarah Maongezi akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo katika picha) katika kikao kilichofanyika mapema leo katika ukumbi wa Hospitari ya Saratani ya Ocean Road kikihusu tuzo ya Elimu kwa jamii waliopata kutoka Shirikisho la kimataifa la magonjwa yasiyo yakuambukiza mwishoni mwa mwaka katika mkutano wa kimataifa uliofanyika katika falme zakiarabu. ………………………………………………………………….

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yasema kuwa magonjwa yasiyo yakuambukiza yanachangia kiasi kikubwa katika vifo vyote vinavyotokea hapa nchini.

Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa magonjwa yasiyokuwa yakuambukiza Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Dkt. Sarah Maongezi wakati akipokea tuzo kutoka kwa TANCDA waliopata mwishoni mwa mwaka huu kutoka katika Shirikisho la Kimataifa la Magonjwa yasiyo yakuambukiza.

“Muongeze juhudi katika kupambana na magonjwa hayo ambayo yanachangia asilimia27 ya vifo vyote hapa Tanzania” Alisema Dkt Maongezi.

Dkt Maongezi aliendelea kusema kwamba Serikali imedhamiria kwa nia kabisa katika kupambana na magonjwa haya kwa kuamua kushirikiana na Asasi mbali mbali nchini ili kutimiza azma hiyo ya kupambana na magonjwa haya.

“Serikali pekee yetu hatuwezi na ndio maana tukashirikiana na Asasi kama TANCDA inayojumuisha vyama vingine kama vile, Taasisi ya Saratani, Taasisi ya Magonjwa ya Moyo, Taasisi ya Mfumo wa Hewa na Taasisi ya Kisukari ambazo kwa ujumla zimejenga ushirikiano katika kupambana na magonjwa haya” Aliongeza Dkt. Maongezi.

Aidha Dkt. Maongezi amewahasa TANCDA kuongeza juhudi na kasi zaidi katika kupambana na magonjwa haya ili kuisaidia jamii kubwa ya Watanzania inayoangamia kutokana na kukosa elimu juu ya magonjwa hayo.

Dkt. Maongezi amewashukuru Waandishi wa Habari wote kwa mchango mkubwa wanaoendelea kuutoa katika kuisaidia jamii ya Tanzania hususani katika kupambana na Magonjwa yasiyo yakuambukiza kwa kuandika Makala za magazetini na vipindi vya Redioni na Tv, na kuwahasa kuendelea kufanya kazi hivyo ya kuelimisha jamii kwa juhudi.

Nae Makamu Mwenyekiti wa TANCDA Pro Andrew Swai ametoa wito kwa Asasi hizo kufanya tafiti zaidi katika maeneo mbali mbali bila kusahau vijijini, ili kuweza kufahamu idadi kamili ya watu waliohathirika na maradhi hayo na kurahisisha kufikisha ujumbe katika maeneo hayo.

“TANCDA inatakiwa kujitanua ili waweze kuwafikia watu wote, pia ule ujumbe unaopelekwa uweze kuwafanya watu ili aweze kubadilika”. Alisma Prof. Andrew Swai

TRA YARAHISISHA USAJILI WA WALIPAKODI.

$
0
0


Kamishna wa Kodi za Ndani Elijah Mwandumbya wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea kituo maalum kilichoteuliwa na mamlaka hiyo kilichopo Chanika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kampeni ya usajili wa walipakodi.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampeni ya usajili wa walipakodi inayofanyika nchi nzima kwa lengo la kuongeza idadi ya walipakodi, kupanua wigo wa ulipaji kodi na kuongeza mapato ya Serikali.
Mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (kulia) Bi. Regina Urio akimhudumia mfanyabiashara (kushoto) aliyefika katika kituo maalum kilichoteuliwa na mamlaka hiyo kilichopo Chanika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusajili na kupata Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN). (PICHA ZOTE NA MPIGA PICHA WETU).



Na: Veronica Kazimoto,-Dar es Salaam.

Wafanyabiashara wanaostahili kulipa kodi kwa njia ya makadirio, watalipa robo ya kwanza ndani ya siku tisini (90) kuanzia siku waliyosajiliwa tofauti na utaratibu uliokuwepo wa kulipa kodi hiyo kabla mfanyabishara hajaanza kufanya biashara husika.

Hayo yamesema leo na Kamishna wa Kodi za Ndani Elijah Mwandumbya wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) alipotembelea kituo maalum kilichoteuliwa na mamlaka hiyo kilichopo Chanika jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kampeni ya usajili wa walipakodi.

Kamishna Mwandumbya amesema kuwa, hapo awali wafanyabiashara walitakiwa kulipa robo mwaka ya kwanza mara baada ya kusajili na kupata Namba ya Utambulisho ya Mlipakodi (TIN) suala lililosababisha baadhi ya watu kushindwa kulipa kutokana na msingi mdogo wa biashara zao.

“Niseme tu kwamba, TRA tumeamua kuboresha huduma zetu kwa kuhakikisha kuwa, walipakodi wapya wanalipa makadirio yao ndani ya miezi mitatu tofauti na ilivyokuwa hapo awali ambapo mfanyabiashara alitakiwa kulipa kabla ya kuanza biashara yake”, alisema Mwandumbya.

Naye Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa mamlaka hiyo Richard Kayombo, amewataka wananchi wanaoishi maeneo hayo kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kujiandikisha na kusema kuwa, zoezi hilo katika kituo hicho litadumu kwa muda wa wiki moja.

“Tukitoka Manispaa ya Ilala tutaelekea Temeke na baadaye tutaendelea kufungua vituo katika maeneo mbalimbali na wakati huo huo ofisi zetu zinaendelea na kazi hii ya usajili kama kawaida” alisema Kayombo.

Mamlaka ya Mapato Tanzania inafanya kampeni ya usajili wa walipakodi nchi nzima kwa lengo la kuongeza idadi ya walipakodi, kupanua wigo wa ulipaji kodi na kuongeza mapato ya Serikali.

RAIS MAGUFULI AAGANA NA GAVANA WA BENKI KUU YA TANZANIA (BOT) ANAYEMALIZA MUDA WAKE PROF. BENNO NDULU PAMOJA NA KUKUTANA NA GAVANA MTEULE WA (BOT) PROF. FLORENS LUOGA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Gavana mteule wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Profesa Florens Luoga aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na na Gavana mteule wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Profesa Florens Luoga mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo  na Gavana mteule wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Profesa Florens Luoga wa kwanza (kushoto) pamoja na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu wa kwanza (kulia) mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na na Gavana mteule wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Profesa Florens Luoga wa kwanza (kushoto) pamoja na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu wa kwanza (kulia) mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) anayemaliza muda wake Profesa Benno Ndulu Ikulu jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

WAZIRI MKUU AOMBOLEZA MSIBA WA MKE WA NAIBU WAZIRI KANGI LUGOLA

$
0
0


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimfariji  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola  kwenye msiba wa  mkewe MarehemuKamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola Gerezani Railyways Club jijinio Dar es salaam leo January 3, 2018 (PICHA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
PMO_4794
Waziri Mkuu. Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo alipofika Gerezani Railways Club jijini Dar es salaam leo January 3, 2018  kwenye msiba wa Marehemu Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyekuwa mke wa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola aliyefariki jana.
PMO_4800
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ,akitoa pole kwa wafiwa alipofika Gerezani Railways Club jijini Dar es salaam leo January 3, 2018  kwenye msiba wa Marehemu Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyekuwa mke wa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola aliyefariki juzi tarehe 1/1/2018.
PMO_4808
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ,akitoa pole kwa wafiwa alipofika Gerezani Railways Club jijini Dar es salaam leo January 3, 2018  kwenye msiba wa Marehemu Kamishna Msaidizi wa Polisi Mary Lugola aliyekuwa mke wa  Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola aliyefariki juzi tarehe 1/1/2018.
Viewing all 46343 articles
Browse latest View live




Latest Images