Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

WAZIRI UMMY AZINDUA MAABARA HAMISHIKA ZA TFDA


DK. KIGWANGALLA ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA ZIWA MANYARA NA KUKAGUA SHUGHULI MBALIMBALI ZA UHIFADHI NA UTALII

$
0
0
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akisalimiana na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Manyara, Noelia Myonga alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiongozwa na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga (wa pili kushoto) kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akizungumza na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akiteta jambo na  Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga kuhusu hifadhi hiyo alipoitembelea jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiongozwa na Mhifahdi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara, Noelia Myonga kwenda kuangalia kivutio cha Maji ya Moto ya Asili ndani ya hifadhi hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akigusa maji ya moto ya asili ambayo ni kivutio cha kipekee cha utalii kilichopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. Maji hayo yanakadiriwa kuwa na nyuzi joto 80 ambapo imeelezwa kuwa baadhi ya watalii huweza kuchemsha mayai katika maji hayo. Nyuma yake anayeshuhudia ni Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akionyeshwa maeneo ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara na Mhifadhi Mkuu wa hifadhi hiyo, Noelia Myonga alipoitembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa ‘Lodge’ ya AndBeyond Lake Manyara Tree, Mei Saimon (kulia) kuhusu ‘lodge’ hiyo ambayo ipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akisikiliza maelezo kutoka kwa Meneja wa ‘Lodge’ ya AndBeyond Lake Manyara Tree, Mei Saimon (kulia) kuhusu mazingira ya nje ya ‘lodge’ hiyo ambayo ipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
 Waziri, Dk. Kigwangalla akikagua miundombinu ya lodge hiyo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa pili kulia) akikagua mazingira ya Lodge’ ya AndBeyond Lake Manyara Tree ambayo ipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. Kulia kwake ni Meneja wa hoteli hiyo, Mei Saimon. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya miundombinu ya kupumzikia wageni katika Lodge’ ya AndBeyond Lake Manyara Tree ambayo ipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara alipotembelea hifadhi hiyo jana mkoani Arusha kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. Kulia kwake ni Meneja wa hoteli hiyo, Mei Saimon. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua baadhi ya miundombinu ya kupumzikia wageni katika Lodge’ hiyo ya AndBeyond Lake Manyara Tree ambayo ipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (wa tatu kulia waliosimama) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Nyumba ya Kulala Wageni ya AndBeyond Lake Manyara Tree Lodge ambayo ipo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara wakati alipotembelea hifadhi hiyo jana kwa ajili ya kukagua shughuli mbalimbali za uhifadhi na utalii kwa lengo la kuimarisha uhifadhi endelevu na utalii nchini. 
Simba katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Baadhi ya miundombinu ya daraja katika hifadhi hiyo ambayo huwarahisishia watalii kuona wanyamapori mbalimbali.
Pundamilimilia
Ndege na nyati katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Ndege aina mbalimbali wanapatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Mtoto wa Tembo katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara.
Baadhi ya Tembo katika Hifadhi ya Taifa ya Ziwa Manyara. (PICHA NA HAMZA TEMBA - WIZARA YA MALIASILI NA UTALII)

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMAPILI LEO NOVEMBA 5,2017

Maginga Business Holdings Company Ltd yadaiwa kukwamisha ujenzi wa barabara ya Namelock –Sunya

$
0
0
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo (katikati) akimskiliza Meneja wa TARURA Wilaya ya Kiteto Eng.Gerald Matindi akielezea hali ya ujenzi wa barabara ya Namelock-Sunya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kwanza kushoto) akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magesa, Mbunge wa Kiteto Mhe.Emanuel Papiyani na Mwenyekiti wa Ccm Wilaya wakikagua ujenzi wa barabara ya Namelock –Sunya eneo linalojengwa na Mkandarasi Maginga Business Holdings Company Ltd ya mjini Dodoma.

Muonekano wa barabara ya Namelock –Sunya eneo linalojengwa na Mkandarasi Maginga Business Holdings Company Ltd ya mjini Dodoma ambaye yuko site kwa miezi minne sasa lakini hali ya ujenzi wa barabara hiyo ikiwa hairidhishi.
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa kata ya Engusero –Wilayani Kiteto wakati wa ziara yake ya kazi Wilayani hapo.

DC SHINYANGA AFUNGUA MKUTANO MKUU WA KLABU YA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA SHINYANGA 2017

$
0
0

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro leo Jumamosi Novemba 4,2017 amefungua mkutano mkuu wa wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC) mwaka 2017.
Mkutano huo mkuu wa SPC ulikuwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali ya kujenga klabu na masuala kadha kadha kuhusu tasnia ya habari.
Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Katemi Hotel mjini Shinyanga,Matiro alisema kalamu ya mwandishi wa habari ni fimbo hivyo kuwataka wazitumie vyema kwa ajili ya maendeleo katika jamii.
Alisema kutokana na kwamba waandishi wa habari ni wadau wakubwa wa maendeleo ni vyema wakawa wazalendo kwa kutangaza fursa za maendeleo katika mkoa wa Shinyanga.
“Serikali inatambua mchango wa waandishi wa habari,naomba tushirikiane katika kuwaletea maendeleo wananchi,sisi viongozi wa serikali tutaendelea kuwahamasisha wakurugenzi katika halmashauri za wilaya kuwapa taarifa sahihi pale mnapohitaji”alieleza Matiro.
Katika hatua nyingine aliwaasa waandishi wa habari kujiendeleza kielimu ili kuongeza umahiri na ufanisi katika kazi zao lakini pia kukabiliana na sheria ya huduma za habari ya mwaka 2016 inayotaka mwandishi wa habari awe na kiwango cha elimu kuanzia ngazi ya diploma.
Matiro aliwasisitiza waandishi wa habari kuandika habari za maendeleo ya mkoa wa Shinyanga huku akiwaomba kutangaza fursa za uwekezaji katika viwanda kuunga mkono jitihada za serikali katika kuifanya Tanzania kuwa ya viwanda.
“Tutakuwa na kiwanda cha nyama katika manispaa ya Shinyanga hivi karibuni,kutokana na kuwa na kiwanda hicho kinahitajika kiwanda kingine cha ngozi,naomba wadau kuja kuwekeza katika kiwanda cha ngozi”,aliongeza.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde waandishi wa habari mkoani humo wanaunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano chini ya Mheshimiwa rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuwaletea maendeleo wananchi.
“Waandishi wa habari ni daraja kati ya serikali na wananchi,hivyo kupitia kalamu zetu tupo tayari na tumekuwa tukishirikiana na viongozi wa serikali kufanikisha utekelezaji wa sera mbalimbali ikiwemo hii ya kujenga uchumi wa viwanda”,alisema Malunde.
“Ili kufanikisha haya,waandishi wa habari tunaomba ushirikiano kutoka katika mamlaka mbalimbali zinazohusika kwani baadhi ya viongozi wa serikali hawapendi kushirikisha vyombo vya habari katika kutekeleza mambo yanayogusa jamii”,aliongeza.
Aidha Malunde aliwataka waandishi wa habari kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya uandishi wa habari na sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya huduma za habari mwaka 2016 ambayo imekuwa mwiba kwa uhuru wa vyombo vya habari.
Viongozi wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Mwenyekiti Kadama Malunde (wa pili kutoka kushoto,akifuatiwa na Katibu Mtendaji Stephen Wang'anyi na katibu Msaidizi Ali Lityawi) wakimpokea mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro (kushoto) ili kushiriki katika mkutano mkuu wa SPC,2017 uliofanyika katika ukumbi wa Katemi Hotel Novemba 4,2017.Picha zote na Patrick Mabula na Frank Mshana - Shinyanga Press Club
Mgeni rasmi wakati wa mkutano mkuu wa wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC) mwaka 2017,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro akizungumza katika mkutano huo.Wa kwanza kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Shaaban Alley na katibu mtendaji wa SPC,Stephen Wang'anyi wakimsikiliza mkuu huyo wa wilaya.
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde akitoa hotuba fupi wakati wa mkutano mkuu wa wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (Shinyanga Press Club – SPC) mwaka 2017.Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.Kulia ni Katibu Msaidizi wa SPC,Ali Lityawi
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde akiwasisitiza waandishi wa habari kuzingatia maadili ya uandishi wa habari na kutoogopa kufichua maovu yanayofanyika katika jamii
Wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga wakiwa ukumbini
Katibu Mtendaji wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga Stephen Wang'anyi akisoma taarifa ya mafanikio ya klabu hiyo tangu mwaka 2015 mpaka Oktoba 31,2017
Wanachama wa SPC,Kareny Masasy na Marco Mipawa (kushoto) wakifuatilia yaliyokuwa yanajiri ukumbini
Wanachama wa SPC wakifuatilia kilichokuwa kinaendelea ukumbini
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde akitoa neno wakati wa majadiliano ya ajenda mbalimbali wakati wa mkutano huo.Kulia ni Mweka Hazina wa SPC,Stella Ibengwe.
Picha ya pamoja,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro na wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga (SPC) wakati wa mkutano mkuu wa SPC 2017
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro na baadhi ya wajumbe wa kamati ya utendaji ya SPC
Picha ya pamoja, mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro (katikati),Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Kadama Malunde (kulia) na Katibu Mtendaji wa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Shinyanga,Stephen Wang'anyi
Picha zote na Patrick Mabula na Frank Mshana - Shinyanga Press Club

WANANCHI SIMIYU WAENDELEA NA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

$
0
0
 Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikao 12 ya Tanzania inayoendelea na zeozi la kuwasajili wananchi kwa lengo la kuwapatia Vitambulisho vya Taifa.

Kwa sasa zoezi hilo limeingia kwenye awamu ya pili ya Usajili katika wilaya zote za mkoa huo ambazo ni Bariadi, Meatu, Busega, Maswa na Itilima huku mwitikio wa watu ukiwa mkubwa.

wanaoshiriki kwenye zoezi hilo ni wananchi wote wenye umri wa miaka 18 na kuendelea, wageni na Wakimbizi.

Pichani ni Maafisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiwachukua alama za Kibaiolojia wananchi wa mkoa wa Simiyu Kijiji cha  Mwakiboro wakati zoezi la Usajili likiendelea .
Zoezi la Usajili likiendelea katika Kijiji cha Kilulu wilayani Bariadi 

Wananchi wa Kijiji cha Mwakiboro mkoani Simiyu wakisubiri kupatiwa huduma ya Uandikishwaji Vitambulisho vya Taifa.
 

DC KIBONDO AWAAGIZA MADIWANI KUHAMASISHA WANANCHI KUIBUA VITUO VYA AFYA KATIKA KATA ZAO.

$
0
0
Na Rhoda Ezekiel Kigoma.

WILAYA ya Kibondo inakabiliwa na upungufu wa vituo vya Afya, ambapo katika Wilaya nzima kuna vituo vya afya viwili hali inayopelekea Wananchi wa Wilaya ya Kibondo kukosa vituo vya kwenda kutibiwa na kupelekea ongezeko la vifo kwa Wananchi kutokana na kukosa huduma.

Kufuatia hali hiyo Mkuu wa Wilaya ya Kibondo Luis Bura amewaagiza Madiwani kuhakikisha wanawahamasisha Wananchi katika kata zao kuibua vituo vya Afya kwa kuanzisha ujenzi Wa vituo hivyo na Halmashauri kumalizia ujenzi huo ili kuhakikisha vituo vya Afya katika Wilaya hiyo vinaongezeka.

Akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani Juzi Mkuu huyo alisema jambo la aibu sana kwa Wilaya hiyo kuwa na vituo vya Afya viwili na halmashauri isipochukua hatua ya kurekebisha vituo hivyo vitarudi kuwa zahanati, na amemuagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri kuhakikisha anaongeza mbinu ya kuibua vituo hivyo angalau Wilaya hiyo kuwa na vituo 10 kwa kuanzia.

Aidha Bura alisisitiza Madiwani kupatiwa Vitambulisho vya bima ya afya ili na wao waweze kuwahamasisha wananchi kuchangia mfuko wa bima ya Afya (CHF) na waweze kupatiwa matibabu bure na kupunguza gharama za matibabu.

"Halmashauri inatakiwa kuingiza bajeti ya vituo vilivyo ibuliwa na kuanza kuvijenga katika kata husika,kata ya Busunzu, Burungu, Budohoko na Kibondo Mjini inatakiwa angalau kuwa na vituo vya Afya kumi inasikitisha sana sijui itakapo fika 2020 mtaenda kuwambia nini Wananchi maana hakuna kitu kizuri mtakacho fanya kama kuwasaidia wananchi kuwaboreshea huduma za afya",alisema Bura.

Hata hivyo Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kibondo, Juma Mnwele alisema mpaka sasa wamepata milioni 500 kwaajili ya ukarabati wa zahanati ya Mabamba ilikuwa kituo cha Afya na kuwasaidia Wananchi wa Wilaya wanapata huduma ya Afya nzuri kama Serikali ya Awamu ya tano ilivyo kusudia kuboresha vituo vya Afya.

Aidha Mnwele aliwaomba madiwani kpamoja na wenyeviti wa kamati za maendeleo kuwashawishi wataalamu kufanya matumizi bora na uangalizi wa fedha za miradi ya Afya na kufuatilia kwa kufuatilia na kuthibiti ilikuzuia ubadhilifu kwa Watendaji wasio waaminifu kama kutajitokeza viashiria vya rushwa.

Aidha Mkurugenzi huyo alimshukuru Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania John Mgufuli jwa zawadi ya vifaa tiba pamoja na vitanda sita na magodaro yake vilivyotolewa katika hospitali ya Wilaya hiyo ,na kuipongeza Serikali ya awamu ya tano kwa jitihada za kuboresha huduma ya Afya kwa kuwawezesha Wananchi kupata huduma stahiki na kupunguza vifo vya mama na mtoto vitokanavyo.

DC WA HANDENI MH GODWIN GONDWE APOKEA MSAADA WA VIFAA VYA UJENZI WA ZAHANATI WENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 14.7

$
0
0
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe amepokea msaada wa vifaa vya ujenzi wa zahanati wenye thamani ya Shilingi Milioni 14.7 za Kitanzania kutoka Darworth Ltd, Mwekezaji wa kiwanda cha usindikaji matunda, kama shukurani baada ya kupewa ardhi yenye ukubwa wa ekari 10 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda hicho Kitongoji cha Mkomba katika Kijiji cha Michungwani Wilayani Handeni..

Akizungumza wakati wa mapaokezi ya vifaa hivyo Mkuu wa Wilaya amewataka Viongozi ngazi ya Kata kuhakikisha wanasimamia na kutumia vifaa kwa kadri ilivyokusudiwa na kwamba asitokee mtu yeyote kupindisha matumizi au kusimamisha ujenzi wa zahanati hiyo ambayo itakuwa na manufaa kwa wananchi wote.

Ameongeza kuwa yote hayo yanafanywa kwaajili ya wananchi wa Handeni na kwamba maendeleo hayana itikadi, hivyo roho ya maendeleo iliyopo waishikilie ili wasonge mbele kwa pamoja kwakuzingatia kuwa wanatekeleza ilani ya chama cha mapinduzi.

Gondwe amesema kuwa Mh.Rais ameagiza kuwepo kwa maeneo yanayotengwa rasmi kwaajili ya viwanda , na sisi kama viongozi tumejumuika kwa pamoja kusimamia agizo la Mh.Rais, kwa Handeni ni wajibu wetu kuhakikisha tunaendelea kutenga maeneo kwaajili ya viwanda kama ambavyo kiwanda hiki kitakavyojengwa.

“Asitokee mtu akauondoa umoja huu, huu ni mwanzotu, viongozi tunakazi ya kuhakikisha vifaa hivi vilivyoletwa vinafanye kazi yake na wananchi waone matunda ya rasilimali yao” amesema Gondwe

Kadhalka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni Bw. William Makufwe ameahidi kusimamia na kuhakikisha vifaa vyote vinatumika ipasavyo na kutoa ushirikiano kwa mwekezaji ili kufikia malengo ya ukamilishaji wa kiwanda cha kusindika matunda.

Kwa upande wake mwekezaji John Kessy kutoka kamupni ya Darworth Ltd amesema kuwa ujenzi wa kiwanda utakuwa si wa manufaa kwa wananchi wa michungwani tu, bali na hata kwao wawekezaji na ndiomaana wameona vyema kuchangia ujenzi wa zahanati sababu hata wafanyakazi watakaokuwa wanafanya kazi kwenye kiwanda watanufaika na huduma za afya zitakazotolewa hapo.

Aliongeza kuwa watafurahishwa kama vifaa hivyo vitasaidia kufikia lengo lililokusudiwa kwakuwa huo ni mwanzo na kwamba watendelea kufanya kazi bega kwa bega kwa kushirikiana na Serikali ili kufikia uchumi wa Tanzania ya Viwanda.

Mkuu wa Wilaya amepokea vifaa ambavyo ni Mabati (ya geji 28) 200, nondo Tani3,mifuko 200 ya saruji na mabomba lora 3 ambayo yatatumika kusambaza maji kutoka kwenye zahanati hadi kiwandani na kufanya jumla ya Mil.14.7, hatua ya ujenzi kwa sasa ipo kwenye michoro ambapo kiwanda kinatarajiwa kujengwa kuanzia Januari 2018 na kukamilika Desemba 2018. Mapokezi hayo yalijumuisha viongozi mbalimbali kuanzia ngazi ya Wilaya hadi ya Kata.


Imetolewa na:
Kitengo cha Teknolojia,Habari na Mawasiliano.
Halmashauri ya Wilaya ya Handeni
4/11/2017

 Mkuu wa Wilaya ya Handeni MH. Godwin Gondwe  (mwenye koti jeusi akipokea nondo kutoka kwa mwekezaji John Kessy kwa ishara ya kupeana mikono na viongozi wengine wakishuhudia
 Mkuu wa Wilaya ya Handeni  kulia name Mwekezaji upande wa Kushoto akipokea mfuko wa saruji kuwakilisha mifuko mingine  ,pembeni ni viongozi mbalimbali wa Halmashauri
 Mapokezi ya mabomba kwa ajili ya kusambazia maji,  Mkuu wa Wilaya ya Handeni  mwenye koti jeusi akipokea kutoka kwa mwekezaji John Kessy, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh Godwin Gondwe akizungumza na uongozi wa Kata kwenye ofisi ya Kijiji cha Michungwani.
 Mkurugenzi Mtendaji Bw. William Makufwe akizungumza kabla ya mapokezi ya vifaa na kumkaribisha mwekezaji Kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Handeni
 Mwekezaji John Kessy kutoka kampuni ya Darworth Ltd  akishukuru uongozi wa Wilaya kwa ushirikiano wanaoutoa katika kufanikisha Ujenzi wa kiwanda cha juice za matunda.
 Viongozi wakipokea nondo kwa pamoja

Miaka Miwili ya Rais Magufuli, Mageuzi Makubwa Yafanyika

MAAMUZI YA TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI YA RUFAA 15 ZA WAGOMBEA WA UDIWANI

$
0
0
Kwa kuzingatia Kifungu cha 44(5) cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 ikisomwa pamoja na Kanuni ya 28(1)(2) ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani) za mwaka 2015 Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilipokea Rufaa kumi na tano (15) kutoka kwa Wagombea Udiwani wa Halmashauri mbalimbali zenye Uchaguzi Mdogo wa Madiwani.

Kati ya Rufaa hizo kumi na tano (15), Rufaa 9 ziliwasilishwa na Wagombea ambao hawakuridhishwa na maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi waliowaengua kutoka katika orodha ya wagombea wa Udiwani katika Kata mbalimbali.

Aidha, Kati ya Rufaa kumi na tano (15), Rufaa sita (6) ziliwasilishwa na Wagombea ambao hawakuridhishwa na maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi ya kuwaruhusu wagombea wenzao kuendelea kugombea udiwani katika Halmashauri mbalimbali.

Kuanzia tarehe 03 hadi 04 Novemba, 2017, Tume kwa mujibu wa Kanuni ya 29 ya Kanuni za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Uchaguzi wa Madiwani) za mwaka 2015, ilipokea, ilijadili na kufanya maamuzi ya Rufaa hizo. Yafuatayo ndiyo maamuzi ya Tume:

Kuhusu Rufaa tisa (9) za wagombea waliokata Rufaa kupinga maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi kuwaondoa katika kugombea Udiwani, Tume imekubali Rufaa zao na kuwarejesha katika kugombea udiwani katika Kata husika kuanzia tarehe ya leo 04 Novemba, 2017.

Kuhusu Rufaa sita (6) za wagombea waliokata Rufaa kupinga maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi ya kuwaruhusu wagombea wenzao wa Udiwani kuendelea na Kampeni za Udiwani, Tume imezikataa Rufaa na imekubaliana na Maamuzi ya Wasimamizi wa Uchaguzi. Hivyo, wagombea sita (6) waendelee kuwa wagombea.

Taarifa rasmi za maamuzi ya Tume zimetumwa kwa Wasimamizi wa Uchaguzi ili wawapatia wahusika maamuzi ya Tume.

Imetolewa leo tarehe 04 Novemba, 2017 na;

NAIBU WAZIRI WA NISHATI, SUBIRA MGALU ATEMBELEA MIRADI YA UMEME CHAMAZI-DOVYA NA MBANDE WILAYANI TEMEKE

$
0
0
Naibu waziri wa Nishati, Mhe. Subira Mgalu, (kulia), akizungumza jambo mbelke ya viongozi wa Tanesco mkoa wa Temeke na wa serikali ya Mtaa, alipotembelea miradi ya umeme huko Cghamazi, Dovya, Mbagala jijini Dar es Salaam, leo Jumapili Novemba 5, 2017.

NAIBU Waziri wa Nishati Mhe. Subira Mgalu leo Jumapili Novemba 5, 2017 amefanya ziara ya kutembelea miradi 7 ya umeme inayotekelezwa na Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), huko Chamazi-Dovya kwa Mzala 1-3, Mbande kwa Masister na Chamazi Vigoa, Mbagala jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri amefuatana na Kaimu Mkurugenzi, TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka na viongozi wengine wa Shirika hilo.
Kwa mujibu wa Kaimu Meneja Uhusianom wa TANESCO, Bi. Leila Muhaji, miradi hiyo saba ni pamoja na ule wa Chamazi Dovya ambao unajumuisha miradi mitatu, (3), Mbande kwa Masister, Miradio 4 na hivyo kufanya jumla ya miradi saba lengo likiwa ni kuwapatia umeme Wananchi wote wa Chamanzi Dovya ambao hawajapata umeme.

“Miradi hii imekamilika na na kila mradi tumefunga transfoma mbili (2).” Alisema Bi. Leila.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, (wapili kushoto), Meneja Mwandamizi wa TANESCO Kanda ya Dar es Salaam na Pwani Mhandisi Mahende Mgaya, (wakwanza kushoto) wakimsikilzia Meneja wa TANESCO Mkoa wa Temeke, Mhandisi Jahulula, wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo.
Naibu waziri Mgalu, akiangalia ripoti ya utekelezaji wa miradim hiyo, iliyokuwaikisomwa na Meneja wa TANESCO Mkoa wa Temeke, Mhandisi Jahulula Maendeleo.

Waziri Mwakyembe awataka wataalam wa Michezo kuleta matokeo Chanya katika sekta ya Michezo nchini.

$
0
0
Na Lorietha Laurence-WHUSM

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amewataka wakufunzi 128 ambao ni wataalam wa michezo kuzingatia kwa makini yote waliojifunza na kuyafanyia kazi ili kuleta matokeo chanya kwenye sekta ya michezo nchini .

Akizungumza katika ufungaji wa mafunzo hayo Wilayani Kyela Mkoani Mbeya ambapo Mhe. Dkt. Mwakyemba alieleza kuwa sekta ya michezo ni ajira na chanzo kikubwa cha mapato hivyo wakufunzi hao wakasimamie vyema waliyojifunza na kuyafanyia kazi kwa ajili ya maendeleo ya michezo nchini.

“Michezo ni ajira na chanzo kikubwa cha mapato hivyo msimamie vyema yote mliyojifunza na kuyafanyia kazi ipasavyo ili kuleta matokeo chanya kwa jamii yetu kwa kuwa na wacheza bora wa kimataifa”amesema Mhe. Mwakyembe.Aidha ameongeza kwa kueleza kuwa mbali ya kuwa michezo ni ajira pia ni kinga bora inayosaidia katika kuimarisha afya na hivyo kujiepusha na maradhi mbalimbali jambo ambalo ni muhimu kwa jamii.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji Baraza la Michezo la Taifa (BMT) Bw. Mohamed Kiganja ameeleza kuwa Baraza lake limejipanga kutoa mafunzo ya wataalam wa michezo hayo kwa nchi nzima na hivyo kuzishauri Halmashauri kuchangamkia fursa hiyo kwa kujiandaa na kuwasilisha maombi mapema ili kuyafanyia kazi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kyela. Dkt. Hunter Mwakifuna alimshukuru Waziri Mwakyembe kwa mchango wa hali na mali katika kukamilisha mafunzo hayo na kuahidi kuwatumia wakufunzi hao katika kufundisha michezo Wilayani hapo.

Nao Wahitimu wameishukuru serikali kwa jitihadi iliyofanta ya kuwaandalia mafunzo hayo na kuahidi kuwa walimu na mabalozi bora katika sekta ya michezo kwa kuibua na kuendeleza vipaji vya wachezaji katika ngazi mbalimbali.

Mafunzo hayo yalifanywa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ilianza tarehe 23 hadi 28 Oktoba huku awamu ya pili ikiwa ni kuanzia 29 Oktoba hadi tarehe 4 Novemba mwaka huu chini ya uratibu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Chuo cha Michezo Malya cha Mkoani Mwanza lengo ikiwa ni kuhakikisha Tanzania inakuwa na wataalam wa kutosha katika sekta ya michezo.

WAZAZI MBURAHATI SACCOS YAIVA, KUPATA HATI YA USAJILI HIVI KARIBUNI

$
0
0
 Mwenyekiti wa muda wa Wazazi Mburahati Saccos, John Mapunda akifungua mkutano wa wanachama wa Saccos hiyo, uliofanyika kwenye ukumi wa Jengo la Kitegauchumi la CCM, Mburahati, Dar es Salaam, jana. 

Amesema ameamua yeye na wenzake kuanzisha ushirika huo wa Akiba na mikopo siyo kwa maslahi ya kisiasa bali kuwasaidia kuwasaidia kiuchumi wanachama wa Jumuiya ya Wazazi katika Kata ya Mburahati ili nao waweze kuwa na maisha bora wakiwa ni miongoni mwa Watanzanaia wenye mahitaji hayo. Kushoto ni Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo ambaye alifika kwenye mkutano huo kutoa mafunzo ya namna bora ya kuanzisha na kuendesha Saccos. Kulia ni Mhazini wa muda Boniface Chigenda na Katibu wa muda Sofia Kiroboto.
 Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo akitoa mafunzo ya namna bora ya kuanzisha Saccos na kuifanya idumu wakati wa mkutano huo. Amesema Saccos hiyo kwa sasa imeshatimiza masharti yote ya kupatiwa usajili na inapatiwa usajili huo hivi karibuni, alisema katika Kadirio lake Saccos hiyo inatarajia kupata zaidi ya Sh. milioni 13 kutokana na ada na michango ya wanachama ambao hadi sasa wamefikia 68, pia kufanya matumizi ya zaidi ya Sh. milioni 13 na kubaki na ziada ya zaidi ya Sh. milioni 29.
 Kitabu au Masharti ya Saccos hiyo
 Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo, akionyesha orodha ya wananchama 68 waliokwishajiunga na Saccos hiyo. Kulia ni Mwenyekiti wa muda John Mapunda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuia ya Wazazi Kata ya Mburahati.
 Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo akifafanua jambo wakati akionyesha orodha hiyo 
 Baadhi ya wanachama wa Saccos hiyo wakisikiliza Ofisa huyo kwa makini  Mwenyekiti wa muda wa Saccos hiyo John Mapunda akitoa nafasi kwa wanachama kuuliza maswali
 Mwanachama wa Saccos hiyo Dismas Shirima akiuliza swali.
 Mwanachama wa Saccos hiyo Mtindi Mbega akiuliza swali
 Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo (kushoto), akimsikiliza kwa makini Mwanachama wa Saccos hiyo Justin Kaijage wakati akiluzwa swali
 Mwenyekiti wa muda wa Saccos hiyo John Mapunda na Katibu wake Sofia Kiroboto wakifuatilia kwa karibu wakati wanachama wakiuliza maswali
 Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo akijibu maswali
 wanachama ukumbini
 Wanachama ukumbini
 Wanachama ukumbini 
 Wanachama wakichangamkia kulipa ada 
 Wanachama wakichangamkia kulipa ada
Mtoto wa mmoja wa wanachama wa SACCOS akijiburudisha kwa soka wakati mkutano ukiendelea
Ofisa Ushirika wa Manispaa ya Ubungo Emmanuel Philipo (kulia) akiagana na wanachama waanzilishi wa Saccos hiyo, Dickson Tungaraza, baada ya kikao kumalizika. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

DC URAMBO: WAKULIMA 4,268 WAJIANDIKISHA KULIMA PAMBA MSIMU UJAO.

$
0
0

NA TIGANYA VINCENT-RS –TABORA

JUMLA ya wakulima 4,268 wilayani Urambo wamejiandikisha kulima zao la Pamba katika msimu wa kilimo unatarajia kuanza wakati wowote mwezi huu.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Angelina Kwingwa wakati akitoa taarifa ya maandalizi ya kilimo hocho kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey ambaye anazungukia vijiji mbalimbali vinavyolima pamba kwa ajili ya utoaji wa elimu juu ya ulimaji bora.Alisema kuwa idadi ya wakulima wanatoka Kata 15 ambao wamo katika vijiji 49 wameleta makisio yao ya kulima zao hilo na kuongeza wakifanikiwa kulima zinaweza kupatika zaidi tani 2000.

Kwingwa alisema kuwa maandalizi yanakwenda vizuri ambapo wanatarajia kupata mbegu ambazo zimependekezwa na Bodi ya Pamba zisizokuwa na Manyoa tani 31.2 kwa ajili ya kusambaza kwa wakulima kwa ajili ya kuanza kilimo hicho.Naye Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mwanri aliwaonya wakulima na wafanyabiashara kutoingiza mbegu za manyoya ambazo zimepigwa marufuku na kuongeza kuwa mkulima atakayepanda mbegu hizo atalazika kuzing’oa.

“Hapa mbegu tutakayopanda ni UKM08 na sio nyingine …nikikutana mtu amepanda mbegu iliyopigwa marufuku ya manyoa nitavuruga shamba lake na kuwachukulia hatua watu ambao watakuwa wamebainika kuingiza mbegu hiyo” alisisitiza Mwanri.

Alisema kuwa wakulima wanatakiwa kuzingatia ushari wa kitaalamu ikiwemo umbali kutoka shimo moja hadi jingine na mstari moja hadi mwingine ili waweze kuwa na idadi ya miche inayotakiwa na 20,000 hadi 22,000 katika ekari moja.

Mwanri alisema kuwa idadi hiyo itawawezesha wakulima kupata kilo kuanzia 1000 hadi 1200 kwa ekari moja ambapo itakuwa ni zaidi ya zile walizokuwa wakipata za 250 hadi 300 wakati wakilima bila kutumia utaalamu na mbegu bora.Aliongeza kuwa mtu yoyote atakayetaka kulima zao hilo ni vema akazingatia Sheria na taratibu zinazoongoza zao hilo ili asije akajikuta katika matatizo ya kushitakiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora  yuko katika ziara maalumu ya kutembelea maeneo yote yanayolima zao la pamba kutoka wilaya za igunga, Nzega, Uyui, Kaliua na Urambo kwa lengo la kuwahamasisha watu washiriki kilimo hicho na vile vile kutoa elimu juu ya kilimo bora kitakacho wasaidia kuzalisha mazao mengi na ya ziada.

NAIBU WAZIRI NISHATI SUBIRA MGALU ASEMA VIJIJI 54 MKOANI PWANI KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME WA REA AWAMU YA TATU

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara mpya ya nishati Subira Mgalu akizungumza na watendaji wa shirika la umeme Tanesco Mkoa wa Pwani pamoja na wakandarasi baada ya kukagua mradi wa REA awamu ya tatu uliopo maeneo ya sofu mlandizi Wilayani Kibaha mkoani Pwani alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja kwa ajili ya kujionea mwenendo mzima wa ujenzi.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Naibu Waziri wa nishati Subira Mgalu wa kati kati akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Tanesco Mkoa wa Pwani Martin Madulu wa kushoto katika alipotembelea kituo cha usambazaji wa umeme kilichopo Mlandizi.
Naibu Waziri wa Wizara mpya ya nishati Subira Mgalu akipata ufafanuzi kutoka kwa wakandarasi wa mradi wa umeme wa REA awamu ya tatu katika eneo la Msufini Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.
Naibu waziri mpya wa Nishati Subira Mgalu akisikiliza kwa umakini maelezo kutoka kwa Meneja wa tanesco Mkoa wa Pwani Martin Madulu wa kushoto mara baada ya kutembelea kituo cha umsambazaji wa umeme kilichopo Mlandizi ikiwa ni ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua miradi ya nsihati ya umeme 


NA VICTOR MASANGU, PWANI

VIJIJI vipatavyo 54 katika mkoa wa Pwani ambavyo wananchi wake walikuwa katika hali ya sintofahamu kutokana na kukaa gizani kwa kipindi cha muda mrefu hatimaye wanatarajia kupata na kunufaika na nishati ya umeme wa uhakika ifikapo mwezi machi mwaka 2018 baada ya kukamilika kwa mradi wa kusambaza umeme vijiji (REA) awamu ya tatu.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa wizara ya nishati Subira Mgalu baada ya kufanya ziara yake ya kikazi ya siku moja katika Wilaya ya Bagamoyo pamoja na Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani kwa ajili ya kutembelea baadhi ya miradi ya REA ambayo inatekelezwa kwa awamu ya tatu pamoja na kujionea changamoto mbali mbali zinazowakabili.

Pia Magalu amesema kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli ni kuhakikisha inapeleka huduma ya uhakika kwa wananchi wake pamona na maeneo mengine yenye kutoa huduma za kijamii na kubainisha kuwa wanatarajia ifikapo mwaka 2021 vijiji vtote nchini view vimefikiwa na huduma ya nishati ya umeme.

Aidha Naibu Waziri huyo alipotembelea kituo cha uzalishaji wa umeme kilichopo maeneo ya Mlandizi aliliagiza Shirika la ugavi wa umeme Tanesco kuhakikisha wanajipanga vizuri ili kuweza kupunguza malalamiko ambayoyamekuwa yakitolewa na baadhi ya wananchi kuunguza vitu vyao majumbani kutokana na tatizo la kukatika katika umeme kila mara bila ya kutoa taarifa.

“Jamani viongozi wangu wa Tanesco kumekuwepo na baadhi ya malalamiko ambayo yamekuwa yakitolewa na wateja kuhusina na hii hali ya kukatika katika kwa umeme mara kwa mara bila ya taarifa hali amabyo inasababisha wakati mwingine wananachi hao kuunguza vitu vyao hivyo katika hili mimi nawaomba mbadilike na mlifanyie kazi katika kuhakikisha lawama hizi zinaondoka kabisa na nina imani mtalifanyia kazi,”alisema Mgalu.

Kwa upande wake Meneja wa Shirika la ugavi wa umeme (Tanseco ) Mkoa wa Pwani Martin Madulu amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo wa REA awamu ya tatu utakuwa ni mkombozi mkubwa katika suala zima la nishati ya umeme kwani wanatarajia kuwafikiza zaidi ya wateja 5000, na kuongeza kuwa mradi huo umegharimu kiasi cha shiingi bilioni 5.

Meneja Madulu aliongeza kuwa lengo la Tanesco ni kuhakikisha kwamba wanaboresha zaidi huduma ya nishati ya umeme hususan katika maeneo ya vijijini kwa lengo la kuweza kuwafikia wananchi wengie ambao wataweza kupata fursa ya kutumia nishati hiyo katika kuendeshea shughuli zao mbali mbali za kimaendeleo.

Mhandisi mkuu ambaye anayesimamia miradi ya umeme wa vijijini (REA) katika Mkoa wa Pwani Leo Mwakatobe amesema licha ya kujitahidi katika kunga miundombinu mipya kwa ajili ya nishati hiyo wanakabiliwa na chanagmoto kubwa ya kuwepo kwa baadhi ya wananchi kugoma kuhama kwa ajili ya kupata njia ya kupitsiha mradi huo hivyo kuwapa wakati mgumu katika utekelazaji wa majukumu yao.

“Katika miradi hii ya kusambaza umeme vijijini kwa kweli baadhi ya maeneo bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya wananchi kuwa wagumu kupisha eneo kwa ajii ya kuweza kupata njia ya kupitisha nishati ya umeme, hivyo inatupa wakat mgumu sana katika kufanya kazi zetu na wengi wao wanadai fidia ya kulipwa lakini katika maradi huu hauna fidia kitu kikubwa ni kutupa ushirikiano katika kufanikisha zoezi hili,”alisema Mhandisi Mwakatobe.

KUKAMILIKA kwa mradi wa umeme vijijini awamu ya tatu (REA) katika Mkoa wa Pwani utaweza kuvinufaisha vijiji vipatavyo 154 ambavyo baadhi ya vingine vilishapatiwa umeme huo katika awamu ya kwanza pamoja na ya pili.

Ben Pol awaamsha Wabunge vitini kwenye Tamasha la Tigo Fiesta Dodoma

$
0
0

Wabunge wa bunge la Tanzania wakicheza pamoja na msanii Ben Pol(mwenye shati nyeupe) kwenye Tamasha kubwa la Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma usiku wa kuamkia jana.
Msanii Ben Pol akipongezwa na Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Antony Mavunde kwenye jukwaa la Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia jana uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Msanii Mimi Mars mdogo wa Vanessa Mdee akifanya yake kwenye Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia jana uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.




Msanii Vanessa Mdee akitoa burudani kwenye Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia jana, uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Darassa akitoa burudani kwa maelfu ya wakazi wa Dodoma mapema usiku wa ijumaa
JUX  akitoa burudani kwenye Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia jana, uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Msanii mkongwe Alli Kiba akiwapa burudani mashabiki wake waliofurika kwenye Tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika usiku wa kuamkia jana uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.

Wateja wa Tigo Dodoma wafurika kujinunulia tiketi kwa Tigo Pesa kushuhudia Tamasha la Tigo Fiesta

$
0
0

Mtoa huduma ya mauzo wa duka la Tigo Dodoma mtaa wa CDA, Alli Mshana akimhudumia mteja aliyefika kupata huduma dukani mapema mwishoni wa wiki hii.
Mteja wa Tigo, Mwajuma Hassan akikabidhiwa simu na msanii Jux huku wasanii Roma na Ben Pol wakishuhudia makabidhiano hayo yaliyofanyika duka la Tigo Dodoma mara baada ya wasanii kutembelea duka hilo. Ndani ya msimu huu wa Tigo Fiesta kampuni ya Tigo imeweka punguzo la bidhaa mbalimbali kwenye maduka yake yote nchini.
Wateja waliofurika Duka la Tigo mtaa wa CDA Dodoma wakipata huduma za Tigo Pesa kwa kununua tiketi za Tamasha la Tigo Fiesta Dodoma.
Wasanii Mimi Mars na Country Boy wakimkabidhi mteja wa Tigo, Kiyoya Shem tiketi ya kushuhudia tamasha la Tigo Fiesta Dodoma mapema mwishoni wa wiki iliyopita.
Wasanii Genevieve na Nedy Music wakiwa na mteja wa Tigo, Bruno Mpangala mara baada ya kujishindia tiketi ya kwenda kushuhudia tamasha la Tigo Fiesta litakalofanyika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma
Wateja waliofurika kupata huduma za Tigo Pesa kwa kununua tiketi za kushuhudia tamasha la Tigo Fiesta Dodoma

RC RUVUMA AMWAGIZA MKANDARAS KUMALIZA UJENZI WA GHALA LA KOROSHO.

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa RUVUMA, CHRISTINE MNDEME amemwagiza Mkandarasi SKYCITY LIMITED, anayejenga ghala la kuhifadhia korosho wilayani TUNDURU kumaliza ujenzi huo mapema ili kupisha ujenzi wa kiwanda cha kubangua korosho.

RC MNYETI AKAGUA UJENZI UKUTA UNAOZUNGUKA MIGODI YA MADINI YA TANZANITE MIRERANI.

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti, ameanza rasmi kazi Mkoani humo kwa kukagua ujenzi wa ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais John Magufuli. 

Mnyeti alitembelea eneo hilo na mwenyeji wake mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo. Alipongeza kasi ya maandalizi ya ujenzi huo kwani kila sehemu aliyokagua ambapo ukuta utapita aliwakuta vijana hao wa JKT wana ari na hamasa ya utendaji kazi. 

"Kwa namna vijana wetu wanajeshi wanavyoonekana kwenye maeneo yote niliyopitia wanaonyesha wataimaliza kazi hii ndani ya muda mfupi tofauti na agizo la miezi sita lililotolewa na Rais Magufuli," alisema Mnyeti.Aliwaahidi kutoa ushirikiano kwa jambo lolote lile watakalokuwa wanalitaka kwenye serikali ili kuhakikisha agizo hilo la Rais Magufuli linatekelezeka kwa wakati husika. 

Kamanda wa operesheni ukuta Mirerani, Kanali Festus Mang'wela alimhakikishia mkuu huyo wa mkoa kuwa vijana wote wanaojenga ukuta huo watafikishiwa ujumbe huo wenye lengo la manufaa ya kulinda afya zao. Kanali Mang'wela alisema ukuta huo wenye kilometa 24.5 na urefu wa mita tatu kwenda juu unatarajiwa kuanza kujengwa rasmi Novemba 6 mwaka huu. 

Alisema wanatarajia mkuu wa JKT Meja jenerali Michael Isamuhyo ndiye atakuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo wa ukuta wanaotarajia kuujenga kwa muda usiopungua miezi sita. Alitoa shukrani kwa serikali ya wilaya ya Simanjiro kwa ushirikiano mkubwa wanaowapa askari hao wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo la maandalizi ya ujenzi wa ukuta huo. 

Katibu Tawala wa wilaya ya Simanjiro, Zuwena Omary akisoma taarifa ya Wilaya hiyo kwa mkuu wa mkoa huo alisema wanashirikiana ipasavyo katika maandalizi ya ujenzi wa ukuta huo. Alisema serikali ya wilaya ya Simanjiro na uongozi wa JWTZ wamekuwa na mawasiliano ya mara kwa mara ili kuhakikisha zoezi hilo linafanyika ipasavyo na kwa wakati muafaka. 

Alisema ukuta huo utachangia kudhibiti utoroshwaji wa madini hayo ambayo huuzwa yakiwa ghafi au kusanifiwa na kuuzwa na madalali na wanunuzi wa ndani na nje ya nchi. Alisema katika utekelezaji wa agizo la Rais Magufuli, wamefanikisha uanzishwaji wa ujenzi wa ukuta na kupatikana eneo la mnada wa madini ya Tanzanite Mirerani. 

"Hadi hivi sasa imeshafanyika minada minne ya madini ya Tanzanite jijini Arusha na serikali kuu na halmashauri ya wilaya ya Simanjiro zikapata kodi ya mapato na kodi ya huduma ila minada ijayo itafanyika Mirerani," alisema Omary. 
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti (wa pili kushoto) akitembelea kambi ya wanajeshi wanaojenga ukuta wa kuzunguka madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro (kushoto) ni Mkuu wa wilaya hiyo Zephania Chaula na (wapili kulia)  ni msimamizi wa ujenzi huo kanali Festus Mang'wela kwenye ziara yake ya kwanza Mkoani humo.  
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti (kushoto) akimsikiliza msimamizi wa ujenzi wa ukuta unaojengwa kuzunguka madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro, Kanali Festus Mang'wela, (katikati) baada ya kutembelea zahanati ya kijiji cha Naisinyai ambapo madaktari wa JWTZ wanatoa huduma za afya. 
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti (kulia) akikagua maandalizi ya ujenzi wa ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro. 
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti (kushoto) akikagua maandalizi ya ujenzi wa ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro. 
Mkuu wa Mkoa wa Manyara Alexander Mnyeti (kushoto) akikagua ramani ya ujenzi wa ukuta unaozunguka migodi ya madini ya Tanzanite Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro.

SEMINA YA WABUNGE WA KAMATI TATU ZA BUNGE

$
0
0
 Ndugu Serafine Tamba akitoa mada kuhusu Mchakato wa Utungaji Sheria katika Semina ya Wabunge wa Kamati ya Kamati ya Katiba na Sheria, Kamati ya Sheria Ndogo na Kamati Mambo Nje, Ulinzi na Usalama.
 Wajumbe wa Kamati tatu za Bunge wakifuatiliana mada kuhusu mchakato wa Utungaji Sheria kutoka kwa Ndugu Serafine Tamba  katika Semina ya Wabunge iliyofanyika Mjini Dodoma. Wajumbe wa Kamati zilizohudhuria Semina hiyo ni Kamati ya Katiba na Sheria, Kamati ya Sheria Ndogo na Kamati Mambo Nje, Ulinzi na Usalama.
 Baadhi ya Wajumbe wa Kamati za Bunge zilizoshiriki Semina kuhusu Mchakato wa Utungaji Sheria wakifuatilia mada katika Semina iliyofanyika Mjini Dodoma.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo, Mheshimiwa Andrew Chenge akitoa mchango wake Katika Semina ya Wabunge iliyofanyika Mjini Dodoma. Wajumbe wa Kamati zilizohudhuria Semina hiyo ni Kamati ya Katiba na Sheria, Kamati ya Sheria Ndogo na Kamati Mambo Nje, Ulinzi na Usalama.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Balozi Adadi Rajabu akizungumza katika Semina ya Wabunge wa Kamati ya Katiba na Sheria, Kamati ya Sheria Ndogo na Kamati Mambo Nje, Ulinzi na Usalama iliyofanyika Mjini Dodoma.Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria Mohamed Mchengelwa
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images