Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUJIUZULU NDG. LAZARO NYALANDU


KAMANDA MUSILIM ATANGAZA MDHAMINI KUELEKEA WIKI YA NENDA KWA USALAMA MKOA WA DAR ES SALAAM

$
0
0
KAMANDA wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, kamishina msaidizi mwandamizi wa jeshi la polisi (SACP) Fortunatus Musilim,  akizungumza na waandishi wa habari (hawapo picha) wakati akimtangaza rasmi mdhamini mkuu wa Wiki ya Nenda kwa usalama mkoa wa Dar es Salaam, inayotarajia kuanza Nov 18 hadi 25 kwenye Viwanja vya Biafra jijini. Kushoto kwake ni Mkuu wa Matawi na Mitandao wa Benki ya StanBic, ambao ni wadhamini, Mussa Kitoi (kulia) ni Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Teddy Mapunda. Picha na Muhidin Sufiani

WAZIRI MKUU MAJALIWA AZUNGUMZA NA BAADHI YA WATANZANIA WAISHIO NCHINI CANADA

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na baadhi ya watanzania waishio nchini Canada, kwenye hoteli ya The Ritz-Carlton Toronto Oktoba 31, 2017PMO_6468
Watanzania waishio nchini Canada,wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipo kutana nao  kwenye hoteli ya The Ritz-Carlton Toronto Oktoba 31, 2017.Picha na Ofisi ya Waziri MkuuPMO_6467

NEMBO YA MIAKA 10 YA SWAHILI FASHION WEEK YAZINDULIWA LEO JIJINI DAR ES SALAAM

$
0
0
Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii.

Baraza la Sanaa la Taifa nchini, leo Novemba 1, limezindua nembo ya miaka 10 ya wiki ya maonyesho ya mitindo ya ‘Swahili fashion week and Awards’, yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Desemba 1 hadi 3 mwaka huu, jijini Dar es Salaam. 

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa wa Basata, Vivian Shalua amesema maonyesho hayo yanalenga kuinua uchumi wa nchi, kukuza lugha ya Kiswahili na kupanua fursa ya masoko Tanzania na Afrika Mashariki.Aidha, Shalua amesema, maonyesho hayo ya mitindo ni moja ya maonyesho yanayozalisha ajira za kudumu na hata za muda na pia kuzalisha pato na kuongeza fedha za kigeni kwa kuuza nguo nje ya nchi.

“Nawapongeza sana waandaji wa maonyesho ya mitindo ‘Swahili Fashion week and Awards’ kwani ni mashindano pekee ambayo hayajawahi kusimama hata mara moja tangu kuanzishwa kwake mwaka 2008” amesema Shalua. Aidha amewaasa wanamitindo wote ambao wanafanya kazi zao kinyemela bila ya kupitia Basata kwa minajili ya kukwepa kulipa kodi mwisho wao umefika, waache mara moja kwani serikali hii ya awamu ya tano haitawaacha bure. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Swahili Fashion Week na mbunifu mbunifu mkongwe, Mustapha Hassanali amesema maonyesho haya ya Swahili fashion week yatasaidia kutekeleza pia juhudi za Rais Pombe Magufuli katika sera ya kuwa na Tanzania ya uchumi wa viwanda kupitia bidhaa za nguo zinazotengenezwa nchini.

Amesema, hatua hii kubwa ya kusherehekea miaka kumi itaendelea kuwa kivutio katika maonyesho yote ya mitindo nchini Tanzania huku wabinifu wa ndani na wale wakimataifa wakipata hisia za dhati kwani Swahili fashion week ni jukwaa la kwanza lenya ubunifu kwa wabunifu wa mitindo Africa nzima kwa kuonyesha mavazi yao ulimwenguni kote.

Amesema, maonyesho ya Swahili week mwaka huu yatafanyika katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa kuanzia tarehe 1-3 Desemba na pia yatakuwa na wabunifu zaidi ya 50 kutoka nchi mbali zikiwemo, Nigeria, Malawi, Kenya, Uganda, Kenya na nyinginezo ambapo wajasiliamali watapata fursa ya kuonyesha kazi zao za mikono.

“Tunaomba wadau wajitokeze kwa wingi kusherehekea nasi siku hii muhimu kwa kuwaunga mkono wabunifu wetu wa mitindo vile vile watashuhuhudia mitindo ya kipekee katika maonyesho haya”, amesema Hassanali.Kwa upande wake, Meneja mradi wa Swahili Fashion Week, Glory Urrasa amesema katika sherehe hizo, wanakazania kuboresha sekta ya ukuaji wa mitindo kwa Africa Mashariki wananchi wakishuhudia ukuaji mzuri wa wabunifu wa mitindo,

“Tofauti na miaka iliyopita, maonyesha haya ya kumi yanajumuisha na utoaji wa tuzo katika siku zote tatu za maonyesho huku tukisisitiza jamii kuwa mitindo ni pato linalozalisha tasnia ya ubunifu na kukuza dhana ya bidhaa za Africa. amesema Urrasa.
 Mkurugenzi wa Swahili Fashion Week, Mustapha Hassanali akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa nembo ya miaka 10 ya wiki ya maonyesho ya mitindo ya ‘Swahili fashion week and Awards’, yatakayofanyika kuanzia Desemba 1 hadi 3 mwaka huu, jijini Dar es Salaam. 
Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa wa Basata, Vivian Shalua akizungumza na waandisishi wa habari na kuzindua wiki ya maonyesho ya mitindo ya ‘Swahili fashion week and Awards’ yatakayofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Swahili Fashion Week, Mustapha Hassanali na kulia ni Mkurugenzi wa Uzalishaji Vipindi wa Azam TV, Charles Hillary.
 Baadhi ya wanamitindo wakifuatilia jambo kwenye mkutano wa uzinduzi wa nembo ya miaka 10 ya wiki ya maonyesho ya mitindo ya ‘Swahili fashion week and Awards’ yatakayofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa wa Basata, Vivian Shalua akizindua nembo ya miaka 10 ya wiki ya maonyesho ya mitindo ya ‘Swahili fashion week and Awards’ leo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa wa Basata, Vivian Shalua akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Swahili Fashion Week, Mustapha Hassanali  pamoja na baadhi ya wanamitindo wa hapa nchini.

SPIKA NDUGAI, KATIBU WA BUNGE, NDG. KAGAIGAI WATEMBELEA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII.

$
0
0
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakifuatilia kikao cha pamoja cha kamati hiyo walipotembelewa na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai, katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai kwa lengo la kuangalia jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake. katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Chuo kikuu cha Dodoma, uliopo Mjini Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Chuo kikuu cha Dodoma, uliopo Mjini Dodoma. kushoto ni katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai na kulia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mheshimiwa, Sebastian Kapufi.
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen kagaigai akizungumza na Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa lengo la kuangalia jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake katika kikao kilichofanyika leo ukumbi wa Chuo kikuu cha Dodoma, uliopo Mjini Dodoma. wa tatu kulia ni Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mheshimiwa, Sebastian Kapufi.
 Wajumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, wakifuatilia kikao cha kamati hiyo walipotembelewa na Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai na katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai kwa lengo la kuangalia jinsi kamati hiyo inavyotekeleza majukumu yake katika kilichofanyika leo ukumbi wa Chuo kikuu cha Dodoma, uliopo Mjini Dodoma. kushoto ni Mheshimiwa Mary Chatanda, katikati ni Mheshimiwa Atupele Mwakibete na kulia ni Mheshimiwa Neema Mgaya.
 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akiwasili na kupokelewa na  Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Ndg. Sebastian Kapufi (kulia) kabla ya kuanza kikao na kamati hiyo kilichofanyika leo ukumbi wa Chuo kikuu cha Dodoma, uliopo Mjini Dodoma.(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Mwili wa aliyekuwa mtangazaji wa Uhuru Fm Violet Mzindakaya umeagwa leo Jijini Dar Es Salaam

RAIS DK.SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA WIZARA YA NCHI OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA IDARA MAALUM ZA SMZ

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya NchI Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017 kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja.
 Baadhi ya Makamanda wa Idara mbali mbali za SMZ wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani), alipozungumza na Uongozi wa Wizara  ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017 kilichofanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.
 Katibu Mkuu wa Wizara  ya Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Radhia Rashid Haroub (kulia) alipokuwa akisoma taarifa ya Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017 katika kikao cha siku moja    kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).
 Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ  Mhe.Haji Omar Kheir (katikati) alipowasilisha Muhtasari wa  Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza Julai- Septemba 2017, wakati wa kikao cha siku moja cha  Uongozi wa Wizara hiyo kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani)wengine ni  Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abdulhamid Yahya  Mzee (kulia) na Naibu Waziri wa Wizara  hiyo Mhe.Shamata Shaame Khamis.
Kamishna wa Vyuo vya Mafunzo Zanzibar, Ali Abdalla Ali akitoa maelezo kuhusi Taasisi yake wakati wa kikao cha Uongozi wa Waziri wa  Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa,Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja,chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) akiwepo na Mkuu wa JKU Kanali Ali Mtumwenio Ali. (Picha na Ikulu)

KINONDONI YAIPONGEZA HAZINA KWA KUONGOA DAR

$
0
0
WILAYA ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, imeelezea siri ya kuwa ya kwanza kitaifa kwenye matokeo ya darasa la saba mwaka huu, huku ikiipongeza shule ya Hazina ambayo imekuwa ya kwanza kwa Mkoa wa Dar es salaam.

Ofisa Elimu Wilaya ya Kinondoni, Kiduma Mageni, alisema jana kuwa matokeo hayo ni matunda ya ushirikiano mzuri baina ya viongozi wa Wilaya hiyo, wamiliki wa shule, walimu na wanafunzi.Alisema hii ni mara ya kwanza kwa Wilaya yake kuwa ya kwanza kitaifa na kwamba hata kiwango cha ufaulu walichofikia hawakuwahi kukifikia hivyo ni mafanikio ya kujivunia.

“Haya ni matunda ya ushirikiano wetu, tunafanyakazi kama timu moja kuanzia wazazi, uongozi wa Wilaya, kata, uongozi wa shule hivyo tunaahidi kuendelea na ushirikiano huu na mimi kama kiongozi wa elimu wa Wilaya nitahakikisha tunazidi kuwa juu,” alisema.

Aliipongeza shule ya Hazina kwa kushika nafasi ya kwanza kwa Wilaya ya Kinondoni, wa kwanza Mkoa wa Dar es salaam kwa kundi la shule zenye zaidi ya wanafunzi 40 na vile vile kushika nafasi ya saba kitaifa.Alisema shule za umma nazo zimefanya vizuri sana kwenye matokeo hayo ingawa zilikuwa na idadi kubwa ya wanafunzi huku akisifu mpango wa elimu bure kuwa chachu ya mafanikio hayo.

Naye Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Patrick Cheche, alisema kwa miaka zaidi ya 10 tangu kuanzishwa kwa shule hiyo wamekuwa wakipata mafanikio makubwa mwaka hadi mwaka kwenye matokeo ya kitaifa.Alitoa mfano kuwa shule imekuwa ikipata matokeo mazuri kitaaluma kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa na hadi Taifa na kumekuwa na mabadiliko channya kila mwaka ambapo mwaka huu imefanikiwa kuongoza wilaya ya Ilala, nafasi ya kwanza mkoa na nafasi ya saba kitaifa.

Alisema wamefanikiwa kufungua shule nyingine maeneo ya Bunju ijulikanayo kama New hazina ikiwa ni mipango yao ya kuboresha elimu kuendana na malengo ya millennia.

Cheche alisema malengo yao ni kuendelea kufundisha kwa bidii sana ili kuendelea kushika nafasi za juu katika mitihani ya kitaifa na kusaidia watoto wengi wa Tanzania kupata elimu bora.
Ofisa Elimu wa Manispaa ya Kinondoni, Kiduma Mageni akimkabidhi zawadi mwanafunzi wa Shule ya Msingi Hazina, Emma James kwenye mahafali ya shule hiyo. Anayefuata ni Mkuu wa shule hiyo, Patrick Cheche.
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Hazina wakionyesha moja ya michezo yao kwenye mahafali ya shule hiyo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Ofisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Kiduma Mageni.
 Wanafunzi wa Shule ya Msingi Hazina iliyoko Magomeni jijini Dar es Salaam , wakiwa kwenye shindano ya kujibu maswali ya papo kwa papo wakati wa mahafali ya shule hiyo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Ofisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, Kiduma Mageni


DKT. MWAKYEMBE: KAZI ZA SANAA NA FILAMU ZIKIDHI SOKO KIMATAIFA

$
0
0
Na Genofeva Matemu, WHUSM, Dodoma.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe ameitaka Bodi ya Filamu pamoja na Baraza la Sanaa la Taifa kuendelea kusimamia kazi za sanaa na filamu ili ziweze kukidhi soko la ndani na la kimataifa.

Waziri Mwakyembe amesema hayo leo Mjini Dodoma wakati wa kikao cha wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii kujadili maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu.

“Bodi ya Filamu na BASATA wamekua wakifanya kazi nzuri ya kukinua vipaji katika tasnia ya filamu na muziki nchini. Ni wajibu wenu sasa kuendelea kusimamia tasnia hizo ili ziweze kukidhi matakwa ya nchi yetu pamoja na kuitangaza nchi kimataifa” amesema Mhe. Mwakyembe
Kwa upande wake Mhe. Grace Tendega amezitaka taasisi hizo kuweka mikakati thabiti ya kusimamia tasnia ya filamu na muziki hatua itakayowasaidia wanatasnia hizo kuboresha maudhui ya maadili katika kazi filamu na muziki.

Naye Mhe. Kasuku Bilago ameitaka Serikali kuwekeza zaidi katika sekta ya filamu nchini kwani sekta hiyo inayofasi kuhimu katika kuinua uchumi wa nchi kwa kasi zaidi kama ilivyo katika nchi za wenzetu
Aidha, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii Mhe. Peter Selukamba amewataka wajumbe wa kamati hiyo kuwa na ushirikiano na Serikali katika kubadili mtazamo wa kukuza sekta ya filamu na muziki nchini.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii Mhe. Peter Selukamba (kushoto) akifungua kikao cha wizara na kamati hiyo kujadili  maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu leo Mjini Dodoma. Kulia ni Katibu wa Kamati hiyo Bi. Pamela Palangio
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza wakati wa kikao cha wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii kujadili maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu leo Mjini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi. Suzan Mlawi.
  Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fissoo akiwasilisha taarifa ya Bodi ya Filamu wakati wa kikao cha wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii kujadili  maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu leo Mjini Dodoma. 
 Mhe. Grace Tendega (kulia) akichangia mada wakati wa kikao cha wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii kujadili maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu leo Mjini Dodoma. Kushoto ni Mhe. Sikudhani Chikambo
  Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza akiwasilisha taarifa ya Basata wakati wa kikao cha wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii kujadili maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu leo Mjini Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bibi. Suzan Mlawi (kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Nicholaus Willium (kushoto) wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao cha wizara na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo na Huduma na Jamii kujadili maendeleo ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) pamoja na maendeleo ya Bodi ya Filamu leo Mjini Dodoma.  
Picha na: Genofeva Matemu - WHUSM

NAIBU WAZIRI WA AFYA ATEMBELEA MFUKO WA TAIFA YA BIMA YA AFYA LEO

$
0
0

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile amewataka Mfuko wa taifa wa bima ya afya nchini (NHIF) kuhakikisha watanzania wote wanapaya huduma ya bima ili kuweza kupata matibabu kwa urahisi na wakati sahihi.

Hayo yamesemwa leo alipotembelea makao makuu ya mfuko huo na kujionea namna wanavyofaya kazi zao ikiwemo kuhifadhi nyaraka za madai kutoka katika vituo tofauti vya afya.

Dr Ndungulile amesema, NHIF wanatakiwa kujitanua zaidi ikiwemo kujitangaza na amewasifu kwa huduma nzuri wanazozitoa kwa wananchi pamoja na kutoa vifaa tiba kwa wateja wao.

"napenda niwapongeze NHIF kwa hatua kubwa mliyofikia ya kutoa huduma kwa watanzania na nimesikia kutoka kwa mkurugenzi kuwa mpaka sasa mna asilimia 31  ya watanzania wote lakini mikakati yenu ni kufika asilimia 50  kwa mwaka 2020,"amesema Dr Ndungulile.

Ameongezea katika kuhakikisha wateja wanapata huduma nzuri basi yale malalamiko yanayotolewa na baadhi ya vituo vya afya kucheleweshewa malipo yao asingependa ayasikie tena, wanatakiwa kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa wakati na kuwalipa kile wanachostahili.

 Naye  Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga amesema kuwa wao kama mfuko wa bima kwa sasa wanatoa huduma katika vituo vingi vya afya na pia wameweza kupata idadi kubwa ya wateja wapya.

Konga amesema kuwa, kwa sasa NHIF wanatoa huduma za matibabu ya magonjwa mbalimbali ikiwemo kutoa vifaa tiba, kusafishwa kwa figo, upasuaji na mengineyo.
Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile akipata maelezo ya namna Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) wanavyohifadhi nyaraka zao katika makabati maalumu na yanaweza kudumu kwa zaidi ya miaka saba, Kulia ni Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga 
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga akimuelezea Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile mikakati yao ilikoanzia na mpaka walipo sasa kwenye utoaji wa huduma za kiafya, pia katika kuendeleza kutoa huduma bora kwa wateja wao ikiwemo kuongezeka kwa wateja wa huduma ya bima kufikia aailimia 50 ya watanzania kwa mwaka 2020.
 Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile akielezewa jinsi wanavyoweza kushughulikia simu zote za wateja wanazopiga kwa ajili ya kupata huduma, na wanapata takribani simu 200 kwa siku  kutoka kwa wateja tofauti kushoto ni  Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga 
Kaimu Mkurugenzi wa Masoko wa Utafiti wa Mfuko wa taifa ya Bima ya Afya Angela Mziray akielezea jambo kwa Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile  
 Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile akiwa ametembelea sehemu mbalimbali wakati alipotembelea makao makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bma ya Afya (NHIF) leo Jijini Dar es Salaam
 Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile  akiwa anasaini katika kitabu cha wageni.
 Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile  akiwa anazungumza na wafanyakazi wa kanda ya Dar es salaam leo wakati  alipotembelea makao makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bma ya Afya (NHIF) na kuwataka waendelee kuitangaza vyema mfuko huo na waje kufikia malengo waliyoyapanga.
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Benard Konga  akikambidhi kijarida chenye maelezo yahusuyo Mfuko wa taifa wa bima ya Afya kwa  Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile alipotembelea makao makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bma ya Afya (NHIF) na kuzungumza na wafanyakazi wa mfuko huo kutoka kanda ya Dar es Salaam leo.
 Kaimu Mweenyekiti wa Chama cha wafanyakazi Rose Gabriel akitoa neno la Shukrani kwa Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile  wakati alipotembelea makao makuu ya Mfuko wa Taifa wa Bma ya Afya (NHIF) na kuzungumza na wafanyakazi wa mfuko huo kutoka kanda ya Dar es Salaam leo.
Naibu  Waziri wa Afya Wizara ya Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dr Faustine Ndungulile  akiwa katika picha ya pamoja na watendaji wa Mfuko wa Taifa wa Bma ya Afya (NHIF) leo Jijini Dar es Salaam.Picha Zote na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

VIJUSO VYA MAGAZEETI YA LEO ALHAMIS NOVEMBA 2,2017

MPANGO WA UENDESHAJI WA KIJINSIA KWA AJILI YA MWITIKIO WA UKIMWI TANZANIA BARA WATAMBULISHWA RASMI KWA MKOA WA SINGIDA

$
0
0
ratibu wa Jinsia kutoka TACAIDS Jacob Kayombo na Afisa Jinsia kutoka TACAIDS Judith Luande wakijadili baadhi ya maoni, maswali na mapendekezo ya wajumbe ambao ni timu ya kudhibiti Ukimwi ya Mkoa wa Singida wakati wa Mafunzo juu ya mpango wa uendeshaji wa kijinsia.
Mjumbe wa mafunzo juu ya mpango wa uendeshaji wa kijinsia Afisa wa Serikali za Mitaa Hussein Mwatawala akipitia fomu zitakazotumika katika kukusanya taarifa za masuala ya Kijinsia mkoani Singida.


Serikali kupitia Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) imeandaa Mpango wa uendeshaji wa Kijinsia kwa ajili ya mwitikio wa Masuala ya Ukimwi ambao umetambulishwa rasmi kwa timu ya Kuthibiti Ukimwi Mkoani Singida.

Mratibu wa Jinsia Kutoka TACAIDS Jacob Kayombo ameongoza mafunzo hayo kwa timu ya kuthibiti Ukimwi Mkoa wa Singida ambapo amewaeleza kuwa mafunzo hayo yatawasaidia kuratibu na kutoa dira katika utekelezaji wa program mbalimbali za Ukimwi kwa ngazi ya Mkoa.

Kayombo amesema Mafunzo hayo yamelenga kuutambulisha mpango huo pamoja na fomu zitakazotumika katika ukusanyaji wa taarifa zihusuzo jinsia na Ukimwi.“Mafunzo haya tunayotoa yamejikita katika kuufafanua mpango huu utakavyotumika pamoja na namna ambavyo fomu hizi zitatumika kukusanya taarifa za jinsia na Ukimwi kwa Mkoa wa Singida na jinsi ambavyo taarifa hizo zitasaidia kufanya maamuzi sahihi kuhusu masuala ya Ukimwi”, amesema Kayombo.

Ameongeza kuwa matarajio yanayotegemewa baada ya mafunzo hayo kutolewa ni kuona masuala yote ya kijinsia yanapewa kipaumbele katika program mbalimbali za Ukimwi.Kayombo amesisitiza kuwa mpango huu utakuwa ni mwongozo wa wadau wa masuala ya Ukimwi ili waweze kutekeleza shughuli zao kwa kuzingatia usawa wa kijinsia hasa katika kuweka mikakati ya kuthibiti Ukimwi yenye uelekeo wa Usawa wa kijinsia.

Amebainisha kuwa mpango huu ambao umedumu katika kipindi cha mwaka 2016 mpaka 2018 una mwelekeo mpya wa program za ukimwi wenye kuzingatia masuala ya kijinsia pamoja na kuondoa changamoto zitokanazo na mila na desturi potofu za masuala ya kijinsia.

Naye Mjumbe wa mafunzo hayo Afisa wa Serikali za Mitaa Hussein Mwatawala amesema mafunzo hayo yametoa mwanga na mwelekeo utakawaosaidia katika kusimamia wadau wanaotekeleza shughuliza Ukimwi ili wazingatie usawa wa kijinsia mkoani hapa.

Mwatawala amesema maafisa waliopata mafunzo hayo wamepewa elimu ya kutosha juu ya mpango na wameufahamu vema kazi iliyobaki ni kuhakikisha masuala ya usawa ya kijinsia yanapewa kipaumbele katika kila program ya Ukimwi inayotekelezwa na wadau mkoani hapa.Mpango wa uendeshaji wa masuala ya Kijinsia 2016-2018 umeanzishwa kwa lengo la kutoa mwongozo kwa wadau wa masuala ya Ukimwi ili watekeleze program zao katika mtazamo wa usawa wa kijinsia.

Mpango huu unashughulikia tofauti za kijinsia zikiwemo ukatili wa kijinsia, unyanyapaa na ubaguzi ili kulinda haki za watu wote wakiwemo wanaume,wanawake,wasichana na wavulana ili wapate huduma za uzuiaji wa maambukizi ya VVU, tiba, matunzo na msaada.

Aidha mpango huu unahusianishwa na Mkakati wa tatu wa taifa wa kuthibiti Ukimwi 2013-2018 na Mkakati wa tatu wa kuthibiti VVU na Ukimwi wa Sekta ya Afya 2013-2017 ambapo mikakati hiyo ina kanuni ambazo zinajumuisha usawa wa kijinsia na ulinzi wa haki za binadamu.

HITILAFU YA MFUMO WA KUPOKELEA GESI KINYEREZI I, TATHIMINI YAONYESHA MATENGENEZO MAKUBWA YANAHITAJIKA, MAFUNDI WAKO KAZINI: TANESCO

$
0
0
Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji, TANESCO

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
TATHMINI iliyofanywa na Wahandisi wa Shirika la Umeme Tanzania, (TANESCO), kufuatia mfumo wa kupokea gesi asili kwenye mitambo ya kufua umeme, Kinyerezi I jijini Dar es Salaam kupata hitilafu, imebaini matengeenzo makubwa yanahitajika kufanyika ili kuhakikisha mfumo unarudi katika ubora wake..

Kwa mujibu wa taarifa ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Mhandisi Dkt. Tito Mwinuka, iliyosambazwa kwa vyombo vya habari leo Novemba 1, 2017, imesema kufuatia mfumo huo kupatwa na hitilafu majira ya mchana Oktoba 32, 2017, hatua ya kwanza iliyochukuliwa na wataalamu wa TANESCO ni kuzima mitambo ili kuruhusu kazi ya usafishaji kuondoa gesi hiyo kufanyika.

”Baada ya usafishaji wa Mitambo kukamilika, matengenezo yalianza usiku wa kuamkia leo Novemba 1, 2017, kwa kutumia wataalamu wa ndani wa Shirika pamoja na Mkandarasi wa kampuni ya JACOBSEN ELEKTRO AS.” Taarifa hiyo ya TANESCO ilisema.

Taarifa hiyo iliendelea kusema, “Kutokana na ukubwa wa matengeenzo na uangalifu wa hali ya juu unaotakiwa katika kazi hii hususan suala la usalama wa mitambo pamoja na watumishi wa Shirika waliopo katika eneo la mitambo, hatua za tahadhari zimechukuliwa.” Taarifa hiyo ilisema.

Aidha taarifa imefafanua kuwa kutokana na Mitambo hiyo kuzimwa ili kuruhusu kazi ya marekebusho ya hitilafu hiyo kukamilika kwa wakati, kutakuwa na upungufu wa umeme katika maeeno mbalimbali ya nchi.
“Uongozi wa Shirika unawaomba radhi wateja wake na wananchi kwa ujumla kwa maeneo ambayo bado yanakosa huduma ya umeme katika kipindi hiki cha matengenezo hayo na tutaendelea kuwaarifu wananchi jinsi kazi ya matengenezo inavyoendelea hadi kukamilika kwake.” Taarifa hiyo ilisema

KAMPENI YA WANAWAKE NA ARDHI YAZIDI KUWAFIKIA WATU WENGI ZAIDI

$
0
0
Katika kuendelea na kampeni ya Wanawake na Ardhi wadau mbalimbali wamekutana jijini Dar es salaam kujadili juu ya 'Nafasi ya Wanawake katika Michakato ya usimamizi wa ardhi' warsha iliyowahusisha wawakilishi kutoka Wizara ya Ardhi, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo, Mashirika na wawakilishi wa wakulima na wafugaji.
Kwa ujumla warsha hiyo ililenga malengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na: kuelewa michakato ya mabadiliko mbalimbali ya taratibu za usimamizi wa Ardhi(Mfano marejeo ya sera ya Taifa ya ardhi) na athari chanya au hasi kwa wanawake wa Tanzania,kusambaza ujumbe wa kampeni ya wanawake na ardhi kama ulivyokusanywa kutoka kwa wadau ambao ni wakulima wadogo wanawake,wafugaji na mashirika mbalimbali, pia kupata fursa ya kuipatia Serikali maoni ya wanawake katika marejeo ya sera ya ardhi ya Taifa.
 Bi. Wiyagi Kisandu kutoka WLAC akitoa mada juu ya uelewa wa maswala ya kijinsia kwa jamii na wanawake kwa ujumla, ambapo alisema kuwa ni muhimu Serikali na wadau wengine washirikiane kuwapa elemu ya haki miliki ya ardhi ili iwe rahisi hata kipindi cha mchakato wa kushughulikia kupata hati hizo uwe rahisi.
 Bi. Naomi Shardrack Mratibu wa Miradi ya Ardhi kutoka Shirika la Kimataifa la Oxfam akielezea kuhusu dhana ya kuwawezesha wanawake kumiliki rasilimali ardhi, pia alielezea utafiti wa maswala ya umiliki wa ardhi uliofanywa na shirika la Oxfam na namna mifumo dume inavyo wakandamiza wanawake katika kumiliki Ardhi.
 Bw. Stephano Mpangala kutoka RUDI akielezea kisa mkasa kilichohusu mzee Kuzenza Magoso(80) ambaye alikuwa na wake sita(6), kwa kutambua umuhimu wa hati milki ya ardhi aliwapatia  wake zake wote hati za kumiliki ardhi ili kuondoa migogoro ambayo ingeweza kujitokeza mbeleni.
Bi.Elisa Simioni   Aliyewahi kushiriki shindano la Mama wa chakula linaloendeshwa na Shirika la Kimataifa la  Oxfam Tanzania akieleza kisa mkasa cha  namna akina amama  walivyoweza kushiriki kikamilifu katika kupigania na kurejesha msitu  kijijini kwao ambao ulivamiwa na kutumika vibaya
 Bw. Adam Ole Mwarabu akielezea zaidi juu ya Kisa mkasa alichozungumzia Bi. Elisa Simion kuhusu uharibifu wa misitu na kusisitiza kuwa licha ya akina mama hao kupigania msitu isiharibiwe, lakini pia akina mama takribani 100 walikwenda kulala katika msitu huo kwa lengo la kuonesha kuwa hawakufurahishwa na uharibifu huo, na mpaka sasa hakuna tena wavamizi katika eneo hilo.
 Bi. Rehema Abdallah mhamasishaji wa umiliki wa ardhi kwa wanawake, alisema kuwa wao wapo tayari katika kushiriki kuchangia gharama za mchakato wa kuhakikisha wanapata hati miliki za ardhi kwa kuwa ni kitu cha muhimu.
 Mh. Yannick Ndoinyo  Diwani wa kata ya Ololosokwani- Longido akielezea namna wakina mama walivyopewa nafasi kubwa katika kumiliki ardhi.
 Dr. Adam Nyaruhume Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro, alieleza kuwa ni muhimu kuwajulisha na kuwaelimisha wanakijiji hasa kuhusiana na maswala ya mipango na matumizi ya ardhi pamoja na umilikishwaji wa ardhi, pia aliwapongeza Asasi ya RUDI kwa kufanya vizuri katika mipango na matumizi ya ardhi katika maeneo mbalimbali wanayoyashughulikia.
 Bw. Joseph Rutaizibwa, Mchumi Mwandamizi kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi akitoa ushauri kuwa Baraza la Taifa la Uwekezaji Wananchi kiuchumi lishirikishwe katika michakato hii muhimu inayohusu maswala ya ardhi.
 Bi. Eva Mageni akielezea changamoto mbalimbali ambazo wanakutana nazo wanawake hasa katika umilikishwaji wa ardhi.
 Bi. Rosada Msoma Afisa Maliasili Mkuu kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii,alisema kuwa Wizara inatoa ushirikiano wa karibu kwa wananchi katika kuhakikisha kuna utunzaji bora wa maliasilizetu.
 Wawakilishi mbalimbali kutoka Wizara ya Ardhi,Wizara ya Kilimo,Wizara ya Mifugo, Wawakilishi wa wakulima na wafugaji, Asasi za Kiraia za Nchini pamoja na za kimataifa,na wadau wengine wakiwa katika makundi mbalimbali kujadili mipango mikakati ya kuendeleza haki za wanawake katika rasilimali ardhi nchini
 Bi. Anne Manangwa Mtafiti kutoka TNRF akitoa mapendekezo kwa niaba ya Asasi za Kiraia ambapo kati ya mambo waliyo omba yafanyiwe kazi katika kampeni  ya wanawake na ardhi ni pamoja na, Elimu itolewe kwa njia ya vyombo vya habari juu ya kumiliki ardhi, haki za wanawake katika kumiliki ardhi pamoja na ushirikishwaji wa wanawake katika kuandaa Sera,uandaaji wa mikakati pamoja na kutunga Sheria.
 Bi. Marcelina Kibena Mwakilishi kutoka MVIWATA, wao katika kikundi chao walitoa maoni kuhusu kutambua makundi mbalimbali kupitia elimu itasaidia kuondoa mfumo dume,kuhamasisha wanawake katika kushika nyadhifa mbalimbali za maamuzi, vyombo vya habari kuandaa programu mbalimbali za uelewa kuhusu kumiliki ardhi na mgawanyo wa rasilimali kuanzia ngazi ya kijiji.
Wadau mbalimbali wakiwemo wawakilishi kutoka Wizara ya Ardhi, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo, Care International,WLAC,PINGOs,UCRT,FFH,LANDESA,PWC,NES
na ILRI pamoja na waendeshaji wa kampeni hiyo Shirika la Kimataifa la Oxfam Tanzania pamoja na TALA wakiwa katika warsha hiyo .

DC WILAYA YA NYANG'WALE ASEMA BILA YA KUWEPO USALAMA WA CHAKULA NCHINI HAKUNA KITAKACHOWEZA KUFANYIKA

$
0
0
 Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale mkoani Geita
 Mkuu wa Wilaya ya Nyang'wale Mkoa wa Geita,  Hamim Buzohera Gwiyama (katikati), akizungumza na watafiti wa kilimo kutoka  Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera, Ukiriguru Mwanza, Ilonga mkoani Morogoro na Waandishi wa Habari kabla ya kukabidhiwa mbegu bora za mahindi na mhogo kwa ajili ya kuzipanda kwenye mashamba darasa katika vijiji vinne wilayani humo leo hii. Kulia ni Diwani wa Kata ya Nyugwa, Ndozi Manual na kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Fabian Sospeter ambaye alikabidhiwa mbegu hizo na kuhutubia wananchi kwa niaba ya mkuu huyo wa wilaya.
 Wananchi wakiwa kwenye mkutano wa uzinduzi wa upandaji wa mbegu katika mashamba darasa uliofanyika Kata ya Nyugwa wilayani humo.
 Diwani wa Kata ya Nyugwa, Ndozi Manual, akizungumza katika uzinduzi huo.
 Katibu Tawala wa wilaya hiyo, Fabian Sospeter, akihutubia wananchi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi, akimkabidhi mbegu ya mhogo aina ya Mkombozi Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Fabian Sospeter kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo.
 Mtaalamu wa Mazao ya Mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibula, akiwaelekeza wananchi wa Kata ya Nyugwa jinsi ya upandaji wa mbegu ya mhogo aina ya Mkombozi kwenye shamba darasa.
 Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Fabian Sospeter akipanda mbegu ya mhogo aina ya Mkombozi kwa niaba ya mkuu wa wilaya hiyo.
 Mtafiti kutoka  Kituo cha Utafiti wa Kilimo  cha Ilonga, mkoani Morogoro, Ismail Ngolinda akitoa maelekezo kwa wakulima wa Kijiji cha Kakora  jinsi ya upandaji wa mbegu ya mahindi aina ya Wema 2109 yanayostahimili ukame. Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Kilimo wa Wilaya ya Nyang'wale,Gudala Kija Tabu na katikati ni mkulima wa kijiji hicho.
 Wananchi wa kijiji cha Kakora wakiwa wamesimama mbele ya shamba la mahindi ambalo mahindi yake ni duni kutokana na mimea yake kushambuliwa na wadudu.
 Mkulima Pendo Sangoma akishiriki kupanda mbegu ya Wema katika shamba darasa katika Kijiji cha Kakora wilaya humo. Kushoto ni Ofisa Ugani, David Makabila kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.
 Watoto, Michael  na Getruda Bundala wa Kijiji cha Kakora wakiwa wamebeba mbegu ya mahindi aina ya Wema wakati wa uzinduzi wa shamba darasa katika kijiji hicho.
 Ofisa Ugani wa Kijiji cha Nyang'wale, akitoa maelekezo kwa watafiti wa kilimo kuhusu masuala ya kilimo.
Mshauri wa Jukwaa la Matumizi ya Bioteknolojia katika Kilimo (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange, akizungumza na viongozi wa Kijiji cha Kanegele, maofisa ugani na watafiti kabla ya kupanda mbegu ya mhogo katika shamba darasa kwenye kijiji hicho. Wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa kijiji hicho, Makoye Malikwisha.

Na Dotto Mwaibale, Nyang'wale, Geita

MKUU wa Wilaya ya Nyang'wale Mkoa wa Geita Hamim Buzohera Gwiyama amesema bila ya kuwepo kwa usalama wa chakula nchini bado kutaendelea kuwepo na changamoto nyingi za maendeleo na kuwa pasipo chakula hakuna kitakachoweza kufanyika.

Hayo yalisema na Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Fabian Sospeter  kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo, Hamim Gwiyana wilayani humo jana wakati akipokea mbegu bora za mahindi aina ya Wema na mhogo aina ya Mkombozi kutoka Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB) kwa ajili ya kuanzisha mashamba darasa ya mbegu katika vijiji vya Kakora, Nyang'wale, Kanegele na Nyugwa.

"Bila ya kuwepo kwa chakula cha kutosha hakuna kitu kitakachoweza kufanyika kwani shughuli zote zitasimama hivyo ni muhimu kuhimizana katika kilimo chenye tija kama tunavyo himizwa na wataalamu wetu kutoka COSTECH, Kituo cha Utafiti wa Kilimo Ukiriguru Mwanza na Maruku mkoani Kagera" alisema Gwiyama.

Alisema usalama wa kujilinda na adui hauna shida kwani mtu anaweza kuandaa jeshi lake la kukabiliana na adui huku akiwa na silaha nzito lakini sio usalama wa chakula ambao unahitaji maandalizi ya kutosha na watu kujituma na kufanya kazi kwa bidii hasa za kilimo chenye tija.

Alisema kukosekana kwa chakula mara nyingi kunachangiwa na tabia za baadhi ya watu kuharibu mazingira kwa kukata miti hovyo hivyo kusababisha mvua kushindwa kunyesha  na maeneo mengi kuwa na ukame.

Alisema katika wilaya yake njaa imechangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi kuwa watoro na kushindwa kumaliza shule na kuwa kukosekana kwa chakula kwa watu ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.


Diwani wa Kata Nyugwa, Ndozi Manual akizungumza kwa niaba ya wananchi wa vijiji hivyo aliwata wananchi kuyatunza mashamba darasa hayo kwa kuwa ni mali yao baada ya kuletewa na COSTECH na OFAB na kuwa baada ya kupata mbegu bora wanatarajia kupata mavuno mengi.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi akizungumza kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, alisema kuwa kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala yote yanayohusu  Sayansi na Teknolojia na kusimamia tafiti zote za kisayansi katika maeneo mbalimbali na kuhakikisha matunda ya tafiti hizo yanawafikia walengwa.

Alisema mbegu hizo walizozikabidhi ikiwamo ya mahindi yanayostahimili ukame ya Wema 2109 na mhogo zimefanyiwa utafiti na zitapandwa katika mashamba darasa na baadae kusambazwa kwa wakulima wengine ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mbegu bora kutokana na wakulima kukabiliwa na mbegu ambazo zilikuwa na magonjwa. 

Dk. Bakari aliwataka wakulima na maofisa ugani kuyatunza mashamba darasa hayo ili kazi kubwa iliyofanyika isipotee bure na baada ya muda mfupi watarudi kuangalia maendeleo yake

JE WAJUA KUTELEKEZA ARDHI NI PAMOJA NA HAYA.

$
0
0
Na  Bashir  Yakub. 

Kuna  mambo ambayo  yafaa  tujihadhari  nayo  sana  hasa  kipindi  hiki. Wengi wamefutiwa  umiliki wa  ardhi. Takwimu  za kufutiwa ni kubwa sana kipindi hiki kama ulikuwa hujui. Kwa  watu  wanaonunua  ardhi  na  kwenda  kuishi  nje  ya  nchi  hili  lawahusu  sana kabla hamjapoteza ardhi zenu.  

Najua  unachojua kuhusu  kutelekeza ardhi  ni pengine  kutokujenga,  au  kutoitumia  kama ilivyopangiwa matumizi, nk. Ni kweli lakini  hiyo ni maana  finyu  ya kutelekeza ardhi. Maana  ni  zaidi ya hiyo,  na  hapa tutaona  ili  ujihadhari na  uwezekano wa  kupoteza  ardhi  yako.

1.MAMBO  AMBAYO  UKIFANYA  UTAHESABIKA  KUTELEKEZA  ARDHI.

Mambo  haya  yameelezwa   na  Sheria  Namba  4  ya  ardhi  ya  1999 kifungu  cha  51(1).

( a ) Kutokulipa  kodi, tozo  au  ushuru  wowote  ambao  upo  kisheria  kwa  ajili  ya  ardhi  ni  kutelekeza  ardhi  kwa  mujibu  wa  sheria hiyo.  Mnazijua  kodi  za  majengo,  kodi  za  ardhi  nk.  Hizi  ni  muhimu  sana  na  kimsingi  ndizo  zinazoeleza  uhai  wa  ardhi  yako.

Ikiwa hulipi  hizi  hata  kama  eneo  hilo  umejenga  kiwanda  kinachofanya  kazi  saa  24  siku  7  za  wiki  bado  mbele  ya  macho  ya  sheria  unahesabika  kutelekeza  ardhi.  Dawa  ya  kuepuka  hili  ni  ndogo.  Lipa  hizo  kodi  na  tozo  kwa  mujibu  wa  sheria. Yamkini  hizi  huwa si  pesa  nyingi  sana ya  kumshinda  mmiliki  kulipa.

( b ) Jengo  ndani  ya  ardhi  kuwa  gofu  ni  kutelekeza  ardhi  kwa  mujibu  wa  sheria.  Lakini  pia   katika eneo  hilo  sheria  imetumia  neno “disrepair”.  Maana   yake  kutokufanya  ukarabati.  Kwa  tafsiri  hii  ni  kuwa  kumbe  hata  kutokufanyia  majengo  yetu ukarabati  nako ni  kutelekeza  ardhi. 

Utaona  katikati  ya  miji  yetu  majengo ya  zamani machafu,  yaliyopauka. Japo  ndani  mwake  watu  wanaishi  na  maofisi  yamo  bado kwa tafsiri  ya  neno  “disrepair”  ni  kuwa  jengo  hilo  limetelekezwa.  Na  sheria  imeeleza  zaidi  kuwa itakuwa  mbaya  zaidi  ikiwa  jengo  hilo  linahatarisha  afya  au maisha  ya  watumiaji  wake , majirani  au  hata  wapita  njia. 

                   KUSOMA  ZAIDI  sheriayakub.blogspot.com

RC MNDEME AWAASA VIONGOZI WA MKOA WA RUVUMA KUSHIRIKIANA KULETA MAENDELEO KWA WANANCHI

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma B.Christina Mndeme amewataka viongozi wa mkoa wa Ruvuma na wilaya kuhakikisha wanashirikana katika kuuletea maendeleo mkoa,uki kiwataka kumpa ushirikiano zaidi .

MKUU WA WILAYA YA MONDULI, NDUGU IDD KIMANTA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA HUDUMA ZA KIBENKI

$
0
0

Mkuu wa wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha,Idd Kimanta(kushoto) akizungumza na Mameneja wa benki ya NMB mara baada ya kuwasili eneo la Mto wa Mbu kufungua tawi jipya litakalowahudumia wanaochi na taasisi mbalimbali,kutoka kushoto ni Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini,Saria Mlay,Meneja wa tawi la Mto wa Mbu,Happiness Patrick,Meneja wa tawi la Clock Tower,Manyolizu Masanja ,Meneja wa tawi la Business Center,Said Parseko na Meneja wa tawi la Karatu,Elizabeth Chawinga
Mkuu wa wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha,Idd Kimanta  akizungumza wakati wa ufunguzi wa tawi la benki ya NMB eneo la Mto wa Mbu ambalo linachangia asilimia 70 ya mapato yote ya wilaya hiyo.
Baadhi ya mameneja waliohudhuria uzinduzi wa tawi la Mto wa Mbu wilayani Monduli.
Mkuu wa wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha,Idd Kimanta  akizindua tawi la benki ya NMB eneo la Mto wa Mbu kushoto ni Meneja wa NMB kanda ya Kaskazini,Saria Mlay na Meneja wa tawi hilo,Happiness Patrick.
Mkuu wa wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha,Idd Kimanta  akipata huduma za kibenki kwenye tawi jipya baada ya uzinduzi .
Baadhi ya mameneja waliohudhuria uzinduzi wa tawi la Mto wa Mbu wilayani Monduli wakibadilishana mawazo.
Burudani ya ngoma kutoka kundi la Maasai Simba ikitumbuiza.

SERIKALI YATAIFISHA NG’OMBE 6648 MISENYI KAGERA

$
0
0
NA MWANDISHI MAALUM MISENYI

Akiwa katika muendelezo wa ziara zake za oparation kamata mifugo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Mpina Ameagiza kukamilisha taratibu za Uhamiaji na Mahakama kupitia mwanasheria mkuu wa Serikali wa Wilaya ya Misenyi Pamoja na Uhamiaji, ili kuweza kupigwa mnada kwa idadi ya ng’ombe 6648 walioingia nchini kinyemela toka nchi jirani ya Uganda na kukamatwa.

Waziri mpina alisema uvamizi wa kundi kubwa kama hilo la wanyama linaweza kusabisha madhara makubwa katika mazingira kama vile mmomonyoko wa ardhi, kuharibifu wa vyanzo vya maji, kumaliza malisho ya mifugo iliyoko nchini, kusababisha migogogoro ya mara kwa mara kwa wakulima na wafugaji na hata kuleta maambukizi ya magonjwa ya wanyama. “Sisi kama Serikali hatuwezi kuruhusu hali hii iendelee na mimi kama Waziri Mwenye dhamana nina jukumu la kuhakikisha tunalinda lasimali hii ya malisho” Alisema Mpina.

Mpina alisema suala hili haliingiliani na Ushirika wa Afrika Mashariki kwani Ushirika huo upo kisheria hivyo wavamizi wanaoingiza mifugo kinyemela nchini toka nchi jirani ni wahalifu kama wahalifu wengine. “Kwa hiyo naangiza ng’ombe hawa 6648 waliokamatwa hatua ziendelee na ambao hawajakamatwa wakamatwe na wataifishwe na Serikali.”Alisisitiza Waziri Mpina.

Kwa upande wa upande wake mkuu wa Wilaya ya Misenyi Kanali Denis Mwila alisema kuwa zoezi la kutathmini ng’ombe katika wilaya yake bado linaendelea na taratibu za kisheria zinafuatwa.

Alipokuwa Mkoani Kagera Mapema Leo Mpina alitembelea mabwawa ya mradi wa samaki yaliyopo Wilayani Muleba katika kijiji cha Luhanga na kusema Serikali ina nia ya kukomesha kabisa uvuvi haramu ikiwa ni pamoja na kuwasaka wavuvi haramu kule waliko na kuwa na nyenzo.

Aidha, akiwa Bukoba Mjini Mpina alitembelea kiwanda cha kuchakata samaki cha Suprime Fish Ltd na kuagiza wamiliki wa viwanda vya samaki nchini kuhakikisha wanachukua hatua za haraka kufufua viwanda hivyo na kuongeza uzalishaji kwani Serikali imeshaanza kuchukua hatua ya kuhakikisha samaki wanapatikana kwa wingi nchini. 

Aliyeshika Samakai aina ya Sato ni Waziri Mpina alipotembelea Mradi wa Mabwawa ya Samaki wa Luhanga Wilayani Muleba.
Waziri Mpina katika Picha akivua samaki aina ya kambale alipotembelea Mradi wa mabwawa ya samaki wa Luhanga Wilayani Muleba.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akiiongea na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Misenyi mara baada ya zoezi la kutaifisha ng'ombe.
Katika Picha ni sehemu ya ng'ombe 6638 waliotaifishwa na serikali baada ya kuingia nchini kinyemela kutoka nchi jirani ya uganda ng'ombe hao wanasubiri maamuzi ya Mhakama kwa ajili ya Kupigwa mnada.

MAJABA ALIVYOPOKELEWA KWENYE NYUMBA YAKE BUNJU B JIJINI DAR

$
0
0


 Nyumba iliyopo Bunju B ilivyokuwa kabla ya makabidhiano jana. Mkurugenzi wa Mkuu wa Global Group, Eric Shigongo (wa kwanza kulia) na George Majaba (wa pili kulia) pamoja na Meneja Mkuu wa Global, Abdallah Mrisho wakijadiliana jambo. ... Shigongo akizungumza machache mbela ya nyumba hiyo kabla ya kumkabidhi George Majaba jana. Mara baada ya kukata utepe, Shigongo akifungua nyumba hiyo. Ndani ya nyumba kushoto, George Majaba, Afisa Masoko, Jimmy Haroub, Mkurugenzi Mtendaji, Eric Shigongo, mke wa Majaba, Meneja Mkuu, Abdallah Mrisho na Mhariri Mwandamizi, Elvan Stambuli wakifurahia mandari ya nyumba. George Majaba akiwa na majirani zake wapya wa Bunju B kwenye nyumba yake mpya, hapo walikuwa wakimkaribisha. Majaba akizungushwa kuoneshwa mandari ya nje ya nyumba yake mpya.

Msafara wa magari ukiongozwa na pikipiki zaidi ya tano ulitokea makao makuu ya Global Group Sinza Mori Dar, huku Mshindi wa Shindano la Nyumba Awamu ya Pili, George Majaba akiwa kwenye gari la wazi aina ya BMW huku mke wake akiwa kwenye gari lingine na watoto wao . 

Msafara ulipita Barabara ya Shekilango, ukaingia Barabara ya Ali Hassani Mwinyi kisha ukaingia New Bagamoyo, njiani kwa kuwa kulikuwa na gari la matangazo, watu walikuwa wamejipanga kumshuhudi Majaba aliyejawa na tabasamu akipita akiwa kwenye gari hilo la wazi. 

 Msafara ulipofika Tegeta umati ulikuwa mkubwa na wengi waliokuwa wakimuona Majaba walikuwa hawaamini macho yao kwani yeye mshindi alikuwa akiwapungua mkono na msafara ukawa unaenda kwa mwendo wa polepole, hali iliyofanya baadhi ya wananchi kumkaribia mshindi na walisikika wakisema ‘Hongera, Hongera!” Lakini abiria waliokuwa kwenye mabasi ya daladala nao walionekana wakitoa vichwa vyao madirishani na kumpongeza Majaba ambaye mara zote alikuwa na tabasamu usoni. 

 Hali ilikua hivyo hivyo msafara ulipofika Boko na baada ya kufika Bunju msafara ulisimama kabla ya kuingia Barabara ya Mabwepande ambapo kwa mwendo mfupi tu msafara uliingia kwenye nyumba mpya ya Majaba. Mara baada ya kufika, Meneja Mkuu, Abdallah Mrisho alitambulisha kwa wageni na wenyeji waliofika kushuhudia makabidhiano hayo na kisha akampa nafasi Mkurugenzi Mtendaji wa Global Group, Eric Shigongo kusema machache. “Kifupi leo tunamkabidhi nyumba yake Bwana Majaba. 

Ni jambo linalofurahisha kuona yupo hapa na familia yake ya mke na watoto watatu, hivyo bila kupoteza muda karibuni tufungue nyumba,” alisema Shigongo. Baada ya kusema maneno hayo Shigongo, Majaba na mkewe walishika utepe na Shigongo akaukata kuashirika kuwa sasa wamekabidhiwa nyumba yao. 

 Baadaye Majaba na watu wengine wakiongozwa na Shigongo waliingia ndani na kuoneshwa kila chumba, baadaye nje na uani ambako kulikuwa na nafasi kubwa na Shigongo alimuambia mke wa Majaba kwamba eneo hilo anaweza kufanyia miradi kama ya kufuga. Wenyeji walimkaribisha Majaba na baadaye wakapiga picha ya pamoja huku wakimpongesha kwa kushinda nyumba hiyo. Shughuli hiyo iliisha saa moja kasoro robo jioni. 

HABARI NA ELVAN STAMBULI, PICHA MUSSA MATEJA.
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images