Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live

JIJI LA TANGA LAZIZIMA KWA MSIMU WA TIGO FIESTA 2017 USIKU WA IJUMAA HII

$
0
0
Msanii Aslay akitumbuiza mashabiki waliofurika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga kwenye Tamasha kubwa la Tigo Fiesta usiku wa kuamkia jumamosi.
Msanii mkongwe wa Taarabu Khadija Kopa  na msanii wa bongo fleva, Ben Pol kwa pamoja wakiwa kwenye jukwaa la tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga usiku wa kuamkia jumamosi.
RosaRee akiwa katika jukwaa la Tigo Fiesta

Msanii  Zaidi yao akiimba na mashabbiki zake katika Tamasha la Tigo Fiesta Mkoani Tanga.
Msanii wa bongo fleva, Nandy akiwa kwenye jukwaa la tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga usiku wa kuamkia jumamosi.

Barclays Bank Tanzania launches its ultra-modern branch in Moshi

$
0
0
 Kilimanjaro Regional Commissioner, Ms. Anna Mghwira (centre), cuts a ribbon to officially open a new branch of Barclays Bank Tanzania in Moshi last weekend. Looking on the right is  Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed; on the left,  BBT Moshi Branch Manager, Ibrahim Omari  and Moshi District Commissioner, Kipi Warioba.
 Kilimanjaro Regional Commissioner, Ms. Anna Mghwira (centre), listens to Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed (left) during the opening ceremony on BBT Moshi branch. Looking on are Moshi District Commissioner, Kipi Warioba (right), BBT Moshi Branch Manager, Ibrahim Omari (second right),  and Barclays Tanzania Head of Customers Network, John Beja (second left).
 limanjaro RC. Anna Mghwira (left), being welcomed by Barclays Bank Tanzania Head of Marketing and Corporate Relations, Arona Luhanga.
Barclays Bank Tanzania Managing Director, (third left), poses for a memento photograph with some Moshi branch officials after the ceremony. 
 Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed giving his welcoming remarks during the opening ceremony of BBT Moshi branch in Moshi, Kilimanjaro last weekend.

Moshi District Commissioner, Kipi Warioba (second left), talking to Barclays Bank Tanzania Managing Director, Abdi Mohamed (right), during the official opening ceremony of BBT Moshi branch last weekend. Looking on are, Barclays Tanzania Head of Customers Network, John Beja (left), and Moshi Municipal Mayor, Raymond Mboya.

NELLY KAZIKAZI ATWAA TAJI LA MISS HIGHLEANING 2017,

$
0
0
 Miss Highlearning 2017, Nelly Kazikazi, akipunga mkono kwa furaha akiwa na washindi wenzake baada ya kutangazwa rasmi na kuvishwa Taji katika shindano la Miss Vyuo Vikuu lililofanyika usiku wa kuamkia jana kwenye Ukumbi wa King Solomon Namanga Dar es Salaam. Kulia ni mshindi wa pili, Queen Elizabeth Makune (kushoto) ni mshindi wa tatu,  Melody Thomas. Picha Zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO)
 Shindano hilo pia lilipambwa na burudani kutoka kwa wasanii tofauti kama JK Comedian Jukwaani, Msaga sumu na Barnaba Boy.
 Sehemu ya wageni waliofika kushuhudia shindano hilo wakiwa katika meza za VIP
 Shoo ilianza kama hivi kwa kufungua na shoo ya pamoja
 Hatimaye warembo walianza kupita jukwaani na vazi la ubunifu....
 
 
 
 
 Msaga Sumu akitoa burdani
 Hatimaye Warembo walianza kupita jukwaani wakia na vazi la Ufukweni

 Majaji wakijadiliana jambo
 Dj John Dilinga naye akionyesha shoo, kuigiza umiss

 Miss Talent akinyesha jinsi alivyochukua taji hilo.
 Hatimaye ukafika muda wa Warembo kupita jukwaani na vazi la usiku.
 Ulifika muda wa Barnaba Boy kuwarusha wadau wa urembo ukumbini hapo
 Dj Denso kutoka Mafoto City Sound akiwarusha kwa ngoma za Barnaba alipopanda jukwaani
 Huku ni nyumba ya Stage warembo wakishoo love
 Barnaba Boy akiwachezesha warembo kwa ngoma zake
 Warembo wakiwa nyuma ya stage nao wakifuatilia shoo ya Barnaba Boy
 Hawa ndiyo warembo wote walioshiriki shindano hilo
 Mkurugenzi na mratibu wa shindano hilo, Joseph Musendo akizungumza jukwaani, akiwa na msaidizi wake
 Ilipoanza kutangazwa tatu bora
 Miss Highlearning 2016, Laura Kway, akimvisha Taji Miss Highlearning 2017, Nelly Kazikazi, baada ya kutangazwa mshindi.
Miss Highlearning 2017, Nelly Kazikazi, akipunga mkono kwa furaha baada ya kutangazwa mshindi.

SERIKALI YATENGA MILIONI 700 ZA MAJI MIRERANI

$
0
0
Serikali imetenga shilingi milioni 700 milioni kwa ajili ya kuanzisha mradi wa maji kwenye Mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara utakaopunguza kero ya maji kwenye eneo hilo.

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Isack Kamwelwe ameyasema hayo kwenye ziara yake ya siku moja Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara. Waziri Kamwelwe alisema radi huo wa maji utasababisha asilimia 85 ya wananchi wa mji huo kupata maji ya uhakika.

Alisema mradi huo unatarajiwa kuanza wakati wowote kuanzia sasa kwani fedha za mradi huo zimeshatengwa tayari. limuagiza meneja wa mamlaka ya maji safi Babati (Bawasa) mhandisi Idd Msuya kuhakikisha mradi huo wa Mirerani unaanza na kukamilika ndani ya muda wa miezi sita.

"Baada ya Rais John Magufuli kufanya ziara yake hivi karibuni kwenye mji mdogo wa Mirerani alitoa ahadi ya kupatiwa maji wananchi wa eneo hilo hivyo nikiwa Waziri mwenye dhamana hiyo amehakikisha agizo hilo limetekelezwa," alisema Waziri Kamwelwe. Alisema baada ya Rais Magufuli kuagiza maji ya uhakika yapatikane Mirerani na zoezi la ujenzi wa ukuta wa kuzunguka machimbo ya Tanzanite kuanza, yeye kama Waziri aliamua ashughulikie suala la maji Mirerani.

Kwa upande wake, meneja wa Bawasa, mhandisi Idd Msuya alitoa ahadi kwa Waziri kuwa watasimamia ipasavyo mradi huo wa maji na kuhakikisha unaanza ndani ya muda wa miezi sita. Mkuu wa wilaya ya Simanjiro Zephania Chaula alimshukuru Waziri Kamwelwe kwa kuitembelea kwa mara ya pili Simanjiro na kuahidi neema ya maji kwenye miji ya Mirerani, Orkesumet na kijiji cha Naisinyai.

Chaula alisema wilaya hiyo ina vipaumbele vitatu vya elimu, afya na maji, hivyo ziara hiyi imekuwa na manufaa makubwa kwao kwani kipaumbele chao kimojawapo cha maji kitapatiwa ufumbuzi. "Umekuwa Waziri mchapakazi tangu ukiwa Naibu wa Wizara hii na kila tukikupigia simu juu ya mradi wa maji wa kutoka mto Ruvu hadi Orkesumet ulikuwa unatupa ushirikiano wa kutosha," alisema mhandisi Chaula.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Jackson Sipitieck akimshukuru Rais Magufuli kumpandisha cheo Waziri Kamwelwe kuwa Waziri kamili wa Wizara hiyo, ambaye awali alikuwa Naibu Waziri wa wizara hiyo.

Sipitieck alisema Waziri Kamwelwe ni mchapakazi mahiri kwani hii ni mara yake ya pili kufika wilayani Simanjiro kwa ajili ya kutatua changamoto ya maji. Alimshukuru Waziri Kamwelwe kwa kufuatilia ipasavyo mradi mkubwa wa maji kutoka mto Ruvu hadi Orkesumet kwani utasaidia wananchi na mifugo kupata maji ya uhakika.

"Pia tunashukuru kwa kukubali ombi letu la kututengea fedha kwa ajili ya ujenzi wa eneo la bwawa la Langai linalotegemewa na wafugaji wa kata tatu za Langai, Loiborsoit na Naberera ambalo lilipasuka na kusababisha maji kupungua ghafla na kukauka," alisema Sipitieck.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Zuwena Omary alisema wananchi wa eneo hilo wanategemea vyanzo mbalimbali vya matumizi ya maji ikiwemo mto, mabwawa, chemchem, mifereji na visima vifupi na virefu.
Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe akizungumza juu ya utekelezaji wa miradi mitatu ya maji kwenye Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, (kushoto) ni Mkuu wa wilaya hiyo mhandisi Zephania Chaula na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Jackson Leskar Sipitieck. 

 Katibu Tawala wa Wilaya ya Simanjiro Zuwena Omary akisoma taarifa ya Wilaya hiyo kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe.
 Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, mhandisi Zephania Chaula akimshukuru Waziri wa Maji na Umwagiliaji mhandisi Isack Kamwelwe kwa utekelezaji wake wa miradi ya maji Simanjiro.

WALIMU 10 WASTAAFU SIMANJIRO WAPATIWA MABATI 200

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha walimu Tanzania (CWT) Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara mwalimu Abraham Kisimbi akizungumza juu ya Chama hicho kuwapatia walimu 10 wastaafu hundi ya shilingi milioni 3.4 kwa ajili ya ununuzi wa mabati 200 kwenye mkutano mkuu wa walimu wa wilaya hiyo. 
 Mwalimu mstaafu na Mwenyekiti Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la ECLAT Peter Toima akizungumza kwenye mkutano mkuu wa walimu wa Simanjiro juu ya mipango na mikakati mbalimbali ya shirika lake ya ujenzi wa baadhi ya shule za wilaya hiyo. 
 Mwenyekiti wa Chama cha walimu Tanzania (CWT) mwalimu Abraham Kisimbi akizungumza juu ya changamoto mbalimbali zinazowakabili walimu wa wilaya hiyo.


Chama cha walimu Tanzania (CWT) Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, kimewakabidhi walimu 10 wastaafu hundi ya sh3.4 milioni kwa ajili ya ununuzi wa mabati 200. 

Mwenyekiti wa CWT Wilayani Simanjiro mwalimu Abraham Kisimbi aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika mji mdogo wa Orkesumet. Mwalimu Kisimbi alisema lengo la kuwapa mabati hayo ni kuwawezesha walimu hao wastaafu wajenge nyumba zao baada ya kumaliza utumishi wao serikalini. 

Alisema wamewapa walimu hao wastaafu 10 mabati 200 ambapo kila mmoja atapata mabati 20 yatakayowasaidia kuezeka nyumba zao watakazojenga na kuanza maisha yao ya ustaafu. "Tumeona badala ya kuwapa mabati na kuhangaika kusafirisha kila mmoja tumempa hundi ya sh340,000 ili akanunue mabati 20 kule anapoishi," alisema mwalimu Kisimbi. 

Aliwataka walimu hao kutumia fedha hizo kwa malengo yaliyopangwa ili wakafanikishe maisha yao kipindi hiki ambacho watakuwa wamestaafu kazi zao za ualimu na kuanza maisha mengine. 

Mwalimu Nazama Tarimo akisoma risala ya CWT alisema wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo walimu kutopandishwa madaraja na kutolipwa madai yao. Mwalimu Tarimo alisema kutembelea umbali mrefu na msongamano wa wanafunzi madarasani kunasababisha walimu kushindwa kufikia asilimia 80 ya ufaulu kwa wanafunzi wa eneo hilo. 

Alisema walimu wa mijini na vijijini wanatakiwa kupatiwa mtaala mmoja ili kuwawezesha kutoa elimu bora kwa wanafunzi wao. Mwalimu mstaafu Peter Toima ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la ECLAT alisema kwa kutambua thamani ya elimu ameiunga mkono serikali kwa kukarabati, kukarafati na kujenga madarasa mapya kwenye shule mbalimbali. 

Toima alisema kupitia shirika lake la ECLAT wamewezesha uanzishwaji wa shule ya kwanza yenye kidato cha tano na cha sita, pekee wilayani humo ya Emboreet. Alisema wamekuwa wanaiunga mkono serikali kwenye ujenzi wa miundombinu ya majengo ya madarasa ya shule ili serikali iwezesha walimu na vitabu.

Ni Wakenya Rock City Marathon 2017

$
0
0
Abrahamu Too kutoka Kenya ameibuka mshindi wa kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza jana baada ya kumaliza kwa muda wa saa 02:22:45, akifuatiwa kwa karibu na mshiriki mwenzake kutoka nchini humo Moris Motima aliyetumia muda wa saa 02:23:19

Kivutio katika mbio hizo ilikuwa ni Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza ambae mbali na kuzindua mbio hizo pia alishiriki katika mbio za km 3 akiambatana na viongozi wengine wa serikali.

Nafasi ya tatu katika mbio hizo pia ilichukuliwa Mkenya George Onyacha aliyetumia muda wa saa 02:23:27, ikiwa sekunde chache nyuma ya mpinzani wake.

Katika mbio hizo zilizoanzia na kuhitimishwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini humo ilishuhudiwa nafasi ya kwanza hadi ya saba zikishikwa na wakimbiaji kutoka nchini Kenya huku nafasi ya nane ikienda kwa Mtanzania Paschal Mombo alietumia muda wa saa 02:30:43.

Akizungumzia siri ya ushindi wake, mbali na kusifia uratibu mzuri wa mbio hizo uliomuwezesha kukimbia bila changamoto yoyote Too alisema ni kujituma kufanya zaidi mazoezi na kukaa kambini muda mrefu ili kufanya vizuri katika michuano ya mwaka huu.

“Maandalizi ya mwaka huu ni mazuri na washiriki wameendelea kuongezeka mwaka hadi mwaka jambo linalotufanya wanariadha kujiwekea mikakati mizuri ili kuweza kukabiliana na ushindani mkali uliopo katika mbio hizi na ninashukuru Mungu nimefanikiwa,” alisema.

Upande wa wanawake mshindi wa kwanza ni Mkenya Alice Gradys Otero aliyetumia muda wa saa 02:48:18 akifuatiwa na Mkenya mwenzie Tecla Chebet  aliyetumia saa 02:54:28 huku nafasi ya tatu ikishikwa na Mkenya Flavious Kwamboka alietumia muda wa saa 02:57:32.
Mtanzania Brabuelia Bryton kutoka mkoani Moshi alishika nafasi ya sita kwa upande wa wanawake katika mbio hizo akitumia saa 03:14:41

Washindi wa kwanza katika mbio hizo zilizofanyika kwa mara ya nane jijini humo  waliibuka na kitita cha Sh 4 milioni kila mmoja, washindi wa pili Sh 2 mil na washindi watatu Sh Mil 1.

Kwa upande wa mbio za km 21 Peter Limo kutoka Kenya aliibuka mshindi wa kwanza baada ya kumaliza kwa muda wa saa 01:05:24, akifuatiwa kwa karibu na mshiriki mwenzake kutoka nchini humo George Wayaki aliyetumia muda wa saa 01:05:50

Nafasi ya tatu katika mbio hizo pia ilichukuliwa Mtanzania Chacha Boy aliyetumia muda wa saa 01:05:59, ikiwa sekunde tisa tu nyuma ya mpinzani wake.

Upande wa wanawake mshindi wa kwanza ni Mkenya Dorifin Omare aliyetumia muda wa saa 01:17:12 akifuatiwa na Mkenya mwenzie Alice Mogiare aliyetumia saa 01:18:30 huku nafasi ya tatu ikishikwa na Mkenya Maiselina Issa alietumia muda wa saa 01:19:55.

Mtanzania Siatha Romanus kutoka mkoani Arusha alishika nafasi ya sita kwa upande wa wanawake katika mbio hizo akitumia saa 01:25:58
Katika mashindano hayo ilishuhudiwa washiriki ambao pia ni wadhamini wa mbio hizo kutoka  makampuni ya PUMA, Tiper, NSSF, RedBull,  Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), New Mwanza Hotel, EF Out door, CF Hospital, KK Security, na kampuni ya uchapishaji ya SDS wakishiriki kikamilifu katika mbio za KM 5 sambamba na watu wenye ulemavu wa ngozi yaani Albino.

Akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi, Naibu Waziri Shonza alisema aliwapongeza washiriki na waandaaji wa mbio hizo na kutoa wito kwa wadau mbalimbali kushirikiana kwa pamoja ili kurejesha hadhi ya mchezo wa riadha nchini.

“Tanzania inaweza kurejea katika ramani ya dunia kwenye michezo kama tukijikita katika maandalizi mazuri ya kuibua na kuviendeleza vipaji vya vijana wetu nchini hasa kuanzia ngazi ya shule za msingi.” Alisema.

Naye Rais wa Shirikisho la riadha nchini (RT) ambae pia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bw Anthony Mtaka mbali  mbali na kuwapongeza waandaaji wa mbio hizo alisema licha ya wingi wa washiriki kutoka ndani ya nchi bado taifa linakabiliwa na uhaba wa wanaridha wa mbio ndefu yaani km 42 na wachache wanaofanya vizuri kwenye mbio hizo wamekuwa wakishindwa kushiriki mbio kama hizo zinazofanyika ndani ya nchini.

Abrahamu Too kutoka Kenya akimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye mbio za km 42 Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza jana baada ya kumaliza kwa muda wa saa 02:22:45, akifuatiwa kwa karibu na mshiriki mwenzake kutoka nchini humo Moris Motima aliyetumia muda wa saa 02:23:19.

 Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza akizungumza na waandishi wa habari kabla ya kuzindua mbio za Rock City Marathon zilizofanyika jijini Mwanza jana  ambapo alikimbia mbio za km 3 akiambatana na viongozi wengine wa serikali.
 Baada ya uzinduzi kazi ikaanza!
 Mbali na kuzindua mbio hizo pia Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza (wa pili kulia)alishiriki kikamilifu katika mbio mbio za km 3 akiambatana na viongozi wengine wa serikali.

 Mbali na washiriki kutoka ndani ya nchin pia pia washiriki kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo China na Marekani nao hawakuwa nyuma.

Rais wa Shirikisho la riadha nchini (RT) ambae pia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bw Anthony Mtaka akizungumza kwenye warsha ya kukabidhi zawadi kwa washindi ambapo pamoja na mambo mengine aliwapongeza waandaaji wa mbio hizo kampuni ya Capital Plus Internantional (CPI).


Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza ( katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa kwanza hadi wa tatu wa mbio za Km 42 (waliosimama nyuma) mara baada ya kuwakabidhi zawadi pamoja na medali. Wengine ni pamoja na Rais wa Shirikisho la riadha nchini (RT) ambae pia ni Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bw Anthony Mtaka(wa tatu kushoto), waandaaji pamoja na viongozi wa mchezo huo.

 Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza (Kushoto) akikabidhi zawadi kwa washindi wa mbio za Km 42 kwa upande wa wanawake ambapo washindi wa kwanza hadi watano wote walitoka nchini Kenya.
 Naibu Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo, Bi Juliana Shonza (Kushoto) akikabidhi zawadi kwa washindi wa mbio za Km 5 ambazo zilikuwa mahususi kwa washiriki wenye ulemavu wa ngozi pamoja na washiriki kutoka kwenye mashirika mbalimbali (corporate race)
Meneja Mahusiano Mkuu wa Kampuni ya kuhifadhi mafuta nchini Tiper, Bw Emanuel Kondi (kulia) akikabidhi zawadi kwa mmoja wa washindi wa mbio hizo. Kampuni ya Tiper ni moja ya wadhamini wakubwa wa mbio hizo ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo kuisaidia Serikali kutangaza utalii kupitia michezo pamoja na kuinua ya michezo kupitia riadha.

 Baadhi ya washindi wa mbio hizo, waandaaji na viongozi wa mchezo wa Riadha wakiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja Huduma kwa wateja Kanda ya Ziwa kutoka  kampuni ya ndege ya Precision Air, Bi Isabella Mwalwiba mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao. Kampuni ya Precision ni miongoni mwa wadhamini wakubwa wa mbio hizo.
 Baadhi ya washindi wa mbio hizo wakipokea zawadi zao kutoka kwa muwakilishi wa kampuni ya CF Hospital ya jijini Mwanza.zawadi zao. CF Hospital ni miongoni mwa wadhamini  wa mbio hizo.
 Baadhi ya washindi wa mbio hizo, waandaaji na viongozi wa mchezo wa Riadha wakiwa kwenye picha ya pamoja na Meneja Kanda  wa  kampuni ya Ulinzi ya KK Security, Bi Levina Vedasto  mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao. Kampuni ya KK Security ni miongoni mwa wadhamini wakubwa wa mbio hizo ambapo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi waliwahakikishia washiriki uwepo wa ulinzi na Usalama.
 Baadhi ya washiriki kutoka ndani na nje ya nchi wakifurahia medali zao!
Baada ya ushindi ilikuwa ni furaha tupu! 

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AFUNGUA DARAJA LA WAENDA KWA MIGUU LA FURAHISHA JIJINI MWANZA

$
0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella pamoja na viongozi mbalimbali akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha liliopo jijini Mwanza.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella pamoja na viongozi mbalimbali akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha liliopo jijini Mwanza. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaMhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa pamoja na viongozi mbalimbali akivuta utepe kwenye jiwe la ufunguzi kuashiria ufunguzi wa wa Daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha liliopo jijini Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaMhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa mara baada ya kufungua daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha jijini Mwanza.

 Sehemu ya wananchi waliohudhuria ufunguzi wa daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha jijini Mwanza.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi kabla ya ufunguzi wa daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha jijini Mwanza.


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma na kikundi cha ngoma za asili cha jijini Mwanza mara baada ya ufunguzi wa daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha jijini Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia pamoja na wananchi waliohudhuria katika sherehe za ufunguzi wa wa daraja la Waenda kwa miguu la Furahisha jijini Mwanza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wakati akiwaaga mara baada ya ufunguzi wa Daraja hilo la Furahisha.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaMhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwapungia mkono wananchi waliopo chini ya Daraja la Furahisha(hawaonekani pichani )
Mara baada ya ufunguzi wa daraja hilo.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kabla ya ufunguzi wa daraja hilo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwaaga wananchi katika eneo la Daraja la Furahisha jijini Mwanza mara baada ya ufunguzi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mkewe Mama Janeth Magufuli wakipanda ngazi za Daraja hilo jipya la Furahisha jijini Mwanza. 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaMhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Miundombinu kutoka chama cha CUF Zuberi Kuchauka mara baada ya kuhutubia wananchi katika eneo la Furahisha jijini Mwanza.Picha namba 16. Sehemu ya Daraja la Furahisha. PICHA NA IKULU.


WADAU WA MAENDELEO WAKUTANA NA MAAFISA WA SERIKALI NA TASAF MJINI DSM.

$
0
0
 MMoja wa maafisa wa TASAF Bw. Hamis Kikwape (aliyeshika kipaza sauti) akiwasilisha taarifa baada ya kurejea kutoka Zanzibar na Morogoro akiwa na wadau wa maendeleo.
 Baadhi ya wadau wa maendeleo,maafisa wa serikali na watendaji wa TASAF wakiwa katika kikao cha pamoja cha kufuatilia utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini.
 Mmoja wa maafisa wa TASAF Bi. Tumpe Lukonge (aliyeshika kipaza sauti) akiwasilisha taarifa ya ziara kwa wajumbe wa kikao kazi cha wadau wa maewndeleo,maafisa wa serikali na watendaji wa TASAF ,kinachojadili utekelezaji wa  Mpango wa Kunusuru Kaya masikini.

Baadhi ya wadau wa maendeleo,maafisa wa serikali na watendaji wa TASAF wakiwa katika kikao cha pamoja cha kufuatilia utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini.

Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga (kulia) akiwa na Kiongozi wa Shughuli za TASAF katika benki ya Dunia Bw. Muderis Mohamed wakiwa katika kikao kazi hicho.
 

NA ESTOM SANGA-TASAF.

Wadau wa Maendeleo,Maafisa wa Serikali na Watendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF wanakutana jijini Dar es salaam baada ya kutembelea maeneo kadhaa ya Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini nchini.

Vikao kazi hivyo vilivyoanza kwenye makao makuu ya TASAF mjini Dar es salaam vitapitia taarifa zilizopatikana kwenye maeneo yaliyotembelewa na wadau hao wa maendeleo na maafisa wa serikali ili kuona Mafanikio na Changamoto za utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya Masikini unaohudumia takribani kaya milioni MOJA NA LAKI MOJA nchini kote.

Wakiwa katika maeneo hayo ya utekelezaji wajumbe walipata fursa ya kukutana na baadhi ya walengwa wa Mpango huo na kuona shuhuda mbalimbali za namna Mpango huo unavyoendelea kupunguza adha ya umasikini kwa kutumia fedha wanazozipata kuanzisha shughuli za kiuchumi na kujiongezea kipato.

Miongoni mwa miradi iliyoanzishwa na walengwa ni pamoja na ufugaji wa kuku wa kienyeji, mbuzi,nguruwe na hata ng’ombe wa maziwa na kuboresha makazi yao kwa kujenga nyumba za matofali na kuezeka kwa mabati tofauti na hali waliyokuwa wakikabiliwa kabla ya kuingizwa kwenye shughuli za Mpango.

Vikao kazi hivyo vinavyoambatana na ziara kwenye maeneo ya Utekelezaji wa Mpango hufanywa kila baada ya miezi SITA kwa lengo la kuboresha huduma kwa walengwa na kusaidia nia ya serikali ya kujenga mazingira wezeshi kwa wananchi kukuza mapato yao kwa kuanzisha miradi midogo midogo kulingana na mazingira yao.

Mikoa ambayo wadau hao wa maendeleo na maafisa wa serikali na TASAF wametemebelea ni pamoja na Tabora, Kigoma, Njombe,Ruvuma,Kilimanjaro, Morogoro, na Zanzibar.Baada ya vikao hivyo taarifa ya maendeleo ya utekelezaji na mapendekezo yakayofikiwa itawasilishwa serikalini.



NAIBU SPIKA TULIA ACKSON AWASHUKURU WADAU, AZINDUA TAMASHA LA TULIA TRADITIONAL DANCES FESTIVAL 2018

$
0
0
 
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tulia Trust na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam, leo wakati akitangaza rasmi kuzindua Tamasha la 'Tulia Traditional Dances Festival 2018' linalofanyika kila mwaka Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya, pamoja na kuwashukuru wadhamini waliofanikisha Tamasha lililofanyika Mwezi Septemba mwaka huu Tukuyu. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Utamaduni, Lilly Beleko, aliyemwakilisha Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo (kulia) ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Air Tanzania, Ladislaus Matindi. Picha na Muhidin Sufiani

NAIBU WAZIRI LUGOLA AFANYA ZIARA ENEO LA TANDALE KWA MTOGOLE NA KUZINDUA OPERESHENI YA MIEZI MIWILI YA KUSAFISHA MITO NCHI NZIMA

$
0
0


Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola akizungumza na waandishi wa habari na wakazi wa eneo la Tande kwa Mtogole wakati wa ziara ya waziri huyo ya kuzindua operesheni ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola akikagua eneo la Mto Ng’ombe eneo la Tandale kwa Mtogole wakati wa ziara ya waziri huyo ya kuzindua operesheni ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola akisafisha eneo la Mto Ng’ombe kuashiria uzinduzi wa operesheni maalum ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.
Eneo la Mto Ng’ombe likiwa limejaa taka ngumu kama zilivyokutwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola wakati wa ziara ya waziri huyo ya kuzindua operesheni ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.


Picha na Eliphace Marwa – Maelezo

MATUKIO KATIKA PICHA ZA KIKAO CHA KAMATI YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA MJINI DODOMA

$
0
0
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala, Mheshimiwa George Mkuchika akisoma Taarifa ya Maboresho ya Mfumo wa Utumishi na Mshahara Serikalini (MCMIS) wakati Kamati hiyo ilipokutana na Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mjini Dodoma. Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Laurean Ndumbaro.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa akifuatilia majadiliano ya Wajumbe wa Kamati yake wakati Kamati hiyo ilipokutana na Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala kwa ajili ya kupokea na kujadili Taarifa ya Maboresho ya Mfumo wa Utumishi na Mshahara Serikalini (MCMIS), Kulia kwake ni Katibu wa Kamati hiyo, Eunike Shirima.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakiwa katika kikao na Watendaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala ambapo leo walijadili Taarifa ya Maboresho ya Mfumo wa Utumishi na Mshahara Serikalini (MCMIS), Kulia kwake ni Katibu wa Kamati hiyo, Eunike Shirima.

Wafanyakazi 143 Wa Ofisi Ya Rais Utumishi Wahamia Dodoma Awamu Ya Pili

$
0
0
Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bibi. Dorothy Aidan Mwaluko akiagana na Kiongozi wa msafara wa magari yaliyobeba mizigo ya ofisi hiyo ikiwa ni muendelezo wa zoezi la kuhamia Dodoma leo Jijini Dar es Salaam. Jumla ya wafanyakazi 143 wameagwa katika awamu hii ya pili, ambapo awamu ya kwanza waliondoka wafanyakazi 78. Katikati mwenye miwani Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bibi. Jane Kajiru.
Gari lililobeba nyaraka na vifaa vya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora likijiandaa kuondoka katika viwanja vya ofisi hiyo iliyopo Magogoni leo jijini Dar es Salaam. Jumla ya wafanyakazi 143 wameagwa katika awamu hii ya pili, ambapo awamu ya kwanza waliondoka wafanyakazi 78.
Baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwapungia mikono ya kwaheri madereva wa magari yaliyobeba mizigo ya ofisi hiyo ikiwa ni muendelezo wa zoezi la kuhamia Dodoma leo Jijini Dar es Salaam. Jumla ya wafanyakazi 143 wameagwa katika awamu hii ya pili, ambapo awamu ya kwanza waliondoka wafanyakazi 78.

Picha na: Frank Shija – MAELEZO

DKT.FAUSTINE NDUGULILE AFUNGUA MKUTANO WA NNE WA CHAMA CHA WATAALAMU WA MAGONJWA YA FIGO MJINI DODOMA

$
0
0
Naibu Waziri wa Afya,maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto dkt.Faustine Ndugulile akiongea kwenye mkutano huo wa wataalamu wa magonjwa ya figo nchini.Mkutano huo wa siku mbili unafanyika kwenye Hotel ya Morena Mjini Dodoma na kuhudhuriwa na wataalamu mbalimbali kutoka Hospitali nchini,Wadau wa Maendeleo pamoja na wataalamu wengine kutoka nchi za Kenya,Sudan,India pamoja na Norway
Makamu wa Rais wa Chama cha wataalamu wa magonjwa ya Figo Tanzania (NESOT), Dkt.Paschal Ruggajjo akiongea dhima kubwa ya mkutano huo ni teknolojia ya upandikizaji wa viungo nchini ili kuweza kuhudumia wagonjwa takribani milioni 23.
Baadhi ya Wataalamu wa magonjwa ya figo waliohudhuria mkutano huo.Mkutano huo ni wa siku mbili ambapo watajadili dhana mbalimbali ya ugonjwa wa figo ikiwemo kutoa elimu kwa umma ili kuweza kukabiliana na magonjwa ya figo pamoja na upandikizaji.Tanzania imekua ikipeleka wastani wa wagonjwa thelathini na tano(35) kwa mwaka nje ya nchi kwa ajili ya kupandikiza figo na gharama ya kupandikiza nje ya nchi ikiwemo India ni shilingi milioni 75 hadi 77 kwa mtu mmoja ikiwemo kupandikiza,nauli pamoja na malazi
Makamu wa Rais wa cChama hicho akimpa zawadi mmoja wa wataalamu wa figo ambaye amefanya tafiti na kuwasilisha mada ya katika mkutano huo Profesa Ainory Gesase ambaye ni mkufunzi wa Chuo cha Sayansi ya Tiba.
Picha ya pamoja ya Mgeni Rasmi wa mkutano huo Dkt.Ndugulile akiwa na wataalamu wa figo nchini pamoja na wadau wengine wa ndani ya nchi na nje ya nchi.
Naibu Waziri akisalimiana na washiriki wa Mkutano huo mara baada ya ufunguzi.Dkt.Ndugulile alisema Serikali mgonjwa mmoja anahitaji wastani wa shilingi za kitanzania 37,620,504 kwa mwaka kwa ajili ya kulipia gharama za kusafisha damu nchini
Mashine za kusafisha figo(Dialysis Machine) ambazo zimefungwa kwenye hospitali nchini.Serikali imefunga mashine katika hospitali nchini ikiwemo UDOM (10),Hospitali ya Muhimbili (42), Hospitali ya Rufaa Mbeya(5), Hospitali ya Rufaa Bugando (10), KCMC(10),Hospitali ya Misheni Serian(10),Hospitali ya NSK Arusha(5),TMK(10),Regency(15),Hurbert Kairuki(5), Aga Khan(10) na Access(10).Mashine hizo zina uwezo wa kuhudumia wagonjwa 783 kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) na 391 kwa huduma ya malipo ya papo kwa papo


Picha zote na Wizara ya Afya

Waziri Mwakyembe azindua Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru

$
0
0
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ambayo yanalenga kuonyesha namna mashujaa wa Tanganyika walipambana kupata uhuru, maonyesho ambayo yatafanyika kwa muda wa mwezi mmoja katika Makumbusho ya Taifa- Nyumba ya Utamaduni jijini Dar es Salaam. Uzinduzi wa maonyesho hayo ambao ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU), kwa lengo ya kuendeleza juhudi za Uhifadhi wa Hifadhi ya Urithi Tanzania,hususani ya Ukombozi wa Afrika yanasimamiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO). Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa maonyesho hayo, Dkt. Mwakyembe alisema mradi huo wa kuhifadhi historia ya Ukombozi wa bara la Afrika ni muhimu kwa Tanzania kwani unaweza kusaidia kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea nchini kuliko ilivyo sasa kwani inawapa nafasi wageni ya kuona mambo tofauti na yaliyozoeleka pindi wanapokuja nchini. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru. “Tuna mradi ambao utatupeleka mbali sana Watanzania, Afrika Kusini, Namibia, Angola hata wao wametuambia tusije shangaa sehemu hiyo ikawa inaleta watalii wengi zaidi kuliko wanaokuja kuangalia tembo na simba, urithi wa Afrika tumekabidhiwa na bara la Afrika ni wajibu wetu Watanzania kuusukuma huu mradi maana tumeshachelewa, Watanzania wengi labda hawaelewi mwaka 2011 kwa kushirikiana na UNESCO tulipeleka ombi AU la mradi huu wa bara la Afrika na wakaubariki huu mradi na wakaamua makao makuu yawe Tanzania na sisi tukachagua Dar na hapa kitajengwa kituo kikubwa kitakuwa na historia ya Ukombozi wa Afrika, sisi ndiyo viongozi wa huu mradi,” alisema Dkt. Mwakyembe. Alisema ili kufanikisha mradi huo tayari wameanza kuchukua hatua mbalimbali ili kuhakikisha pindi watakapojenga kituoambacho kitatumika kuhifadhi vitu mbalimbali ambavyo vilitumika katika kipindi cha ukombozi wa bara la Afrika kuwe na taarifa nyingi kuhusu bara la Afrika. “Tunawatumia wazee walio na historia ya ukombozi wa Afrika tumehoji zaidi ya wazee 100 na tunaendelea na hilo zoezi na tumebaini maeneo zaidi ya 200 Tanzania ambayo yanahitaji kuhifadhiwa, ni wajibu wangu kupeleka muswada bungeni ili tuyahifadhi na kuyalinda kwa kutumia sheria,” alisema Waziri Mwakyembe. Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru. Kwa upande wa Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer alisema ni muhimu kwa bara la Afrika kuwa na maonyesho ambayo yanaelezea historia ya bara hilo ili yatumike kuelezea kizazi cha sasa na kijacho namna nchi za Afrika zilipambana kupata uhuru na wao kama EU wataendelea kusaidia miradi mbalimbali yenye lengo ya kutunza urithi wa bara la Afrika. “Ni jambo la kujivunia kwa Umoja wa nchi za Ulaya kusaidia kufanikisha mradi huu … EU tumekuwa tukisaidia miradi mingi na hii yote ni kwa ajili ya kutunza utamaduni na urithi wa bara la Afrika, tumesaidia miradi mbalimbali nchini ikiwepo ya Olduvai na Ngorongoro na tutaendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kuendeleza maeneo ya kihistoria,” alisema. Afisa Mpango Kitaifa wa UNESCO, Nancy Kaizilege akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru. Naye Mkurugenzi Mkazi wa UNESCO kanda ya Afrika Mashariki na Afisa Mwakilishi wa Unesco Dar, Ann Therese Ndong- Jatta katika hotuba yake iliyosomwa na Afisa Mpango Kitaifa wa UNESCO, Nancy Kaizilege alisema ni jambo zuri kuwepo na makumbusho ambayo yanaeleza historia ya bara la Afrika na yatawza kuwapa nafasi watu mbalimbali kutoka mataifa ya nje ya bara la Afrika kuona na kujifunza historia ya Afrika. “Makumbusho haya ni muhimu kwasababu ni sehemu ya ukumbusho wetu kwa baadae, kupitia makumbusho haya tutaona historia ya bara la Afrika, historia ya mwanadamu na safari ya kutafuta uhuru ilivyokuwa,” alisema Kaizilege. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe na Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer wakikata utepe katika uzinduzi wa Maonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru.Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa ameongozana na Balozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya nchini (EU), Roeland Van de Geer na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuangalia vitu mbalimbali vya kihistoria ambavyo vimewekwa katikaMaonyesho ya Mashujaa na Mapambano ya kupata Uhuru.

TAARIFA YA SHUKURANI

$
0
0
 FAMILIA YA MAREHEMU MZEE MOHAMED NASSOR KISSOKY NA FAMILIA YA MAREHEMU BRIGEDIA JENERALI JUMA MOHAMED PONGWE TUNATOA SHUKRANI ZETU ZA DHATI KWA NDUGU JAMAA NA MARAFIKI NA WOTE MLIOTUFARIJI NA KUSHIRIKIANA NASI KWA NJIA MOJA AU NYINGINE WAKATI WA MARADHI NA KATIKA MSIBA WA MPENDWA WETU DA BEBBY MARIAM JUMA PONGWE. 

SI RAHISI KUMSHUKURU KILA MTU MMOJA MMOJA. 

TUNAOMBA MPOKEE SHUKRANI ZETU ZA UPENDO. NASI HATUNA UWEZO WA KUWALIPA ISIPOKUWA YEYE MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA NDIYE ATAWALIPA KWA KADRI ATAKAVYOONA INAFAA.AMEENA! TUNAPENDA KUWAFAHAMISHA KUWA HITIMA (DUA) YA KUMUOMBEA MAREHEMU ITAFANYIKA JUMAPILI 05/11/2017 SAA SABA ADHUHURI. 

MWENGE  MLALAKUWA KUPITIA UWANJA WA NGOME SACCOS KUELEKEA MAKAZI YA RAIA. KUTAKUWA NA MABANGO YA KUELEKEZA. "INNA LILLAH WA INNA ILLAH RAJ'IUN".

RC GEITA KUWAPIMA MAOFISA UGANI UWEZO WA UTENDAJI KAZI ZAO ZA KILIMO

$
0
0

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, akimkabidhi mbegu bora ya mahindi, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel Lughumbi  wakati wa uzinduzi wa mashamba darasa ya mbegu za mahindi, mhogo na viazi lishe uliofanyika nje ya viwanja vya ofisi ya mkoa huo jana. Kushoto ni Mshauri wa Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo   (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange.
 Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel Lughumbi akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kukabidhiwa mbegu hizo za mahindi zinazokabiliana na ukame  Wema.






 Ofisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, David Makabila akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Isamilo kabla ya uzinduzi wa shamba darasa la mbegu ya mahindi. Kutoka kushoto ni Mtafiti kutoka COSTECH, Dk.Beatrice Lyimo, Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti cha Maruku mkoani Kagera, Jojianas Kibula, Mtafiti Bestina Daniel na Mshauri wa Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo   (OFAB), Dk.Nicholaus Nyange.
 Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga Kilosa mkoani Morogoro,  Ismail Ngolinda, akitoa maelezo ya jinsi ya kupanda mbegu ya mahindi.
 wananchi wa Kijiji cha Isamilo wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Mkulima Hernick Elias wa Kijiji cha Isamilo akizungumzia changamoto za kilimo walizonazo
 Watafiti wakifanya vipimo kabla ya uzinduzi wa shamba la mbegu za mahindi katika kijiji cha Isamilo.
 Wakulima wa Kikundi cha Nguvumoja cha Kijiji cha Isamilo wakiwa shambani wakati wa uzinduzi huo.
 Mkulima wa Kijiji cha Isamilo, Salome Renatus akizungumza na waandishi wa habari.
  Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga Kilosa mkoani Morogoro,  Ismail Ngolinda, akionesha namna ya ujimbaji wa mashimo kabla ya upandaji wa mbegu za mahindi.
 Ofisa Ugani wa Kijiji cha Isamilo, Issa Pegeege, akionesha jinsi ya uwekaji mbolea kabla ya kupanda mbegu ya mahindi Wema.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari (kulia), kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, akiongoza wakulima kupanda mbegu ya mahindi kwenye shamba darasa katika Kijiji cha Isamilo.
 Mkulima wa Kijiji cha Kikundi cha Nguvu moja katika Kijiji cha Kamhanga, Hamisi King akitoa maelekezo wakati wa uzinduzi wa shamba darasa la mahindi katika kijiji hicho.
 Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga Kilosa mkoani Morogoro,  Ismail Ngolinda, akionesha namna ya ujimbaji wa mashimo kabla ya upandaji wa mbegu za mahindi katika Kijiji cha Isamilo. 
 Wakulima na wananchi wa Kikundi cha Kasimpya katika Kijiji cha Mnekezi kilichopo Kata ya Kaseme wakisubiri maelekezo namna ya kupanda mbegu za mahindi katika shamba darasa.
 Diwani wa Kata ya Kaseme, Andrew Kalamla akizungumza na wananchi katika uzinduzi wa shamba darasa hilo.
 Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mnekezi.
 Mwakilishi wa Mkoa wa Geita, Emiri Kasagala, akihutubia katika uzinduzi huo kwa niaba ya mkuu wa mkoa huo, Robert Gabriel
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, akipanda mbegu wakati wa uzinduzi wa shamba darasa katika Kijiji cha Mnekezi. Kulia ni Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa, Emiri Kasagala.

Na Dotto Mwaibale, Geita

MKUU wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel Lughumbi amesema ataanzisha utaratibu wa kuwapima maofisa ugani wa mkoa huo utendaji kazi wao ili kujua uwezo wa kila mmoja wao.

Hayo ameyasema  wakati Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), ilipokuwa ikimkabidhi mbegu bora za mahindi, mihogo na viazi lishe ikiwa ni siku yake ya kwanza kufanya kazi katika mkoa huo tangu ateuliwe na Rais Dk.John Magufuli kushika wadhifa huo.

"Kilimo ni muhimu sana hasa katika kipindi hiki ambacho nchi inaingia katika uchumi wa kati wa viwanda hivyo nitaweka utaratibu wa kuwapima maofisa ugani wote wa mkoa huu ili niweze kujua utendaji kazi wao" alisema Lughumbi.

Lughumbi aliwataka maofisa ugani mkoani humo kuacha kukaa maofisi kwenye viyoyozi badala yake waende walipo wakulima kushirikiana nao kuwapa elimu ya kilimo ili kujikomboa kiuchumi kupitia kilimo.

Mkuu huyo wa mkoa ameahidi kununua viatu vya shambani 'gambuti' na koti na kuwa mara moja ataanza kutembelea wakulima katika maeneo yao ili kujua changamoto zao na kusema anapenda kuona mkoa wa Geita unakuwa namba moja kwa kilimo hapa nchini.

Akizungumza kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH wakati wa kukabidhi mbegu hizo, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi na Viumbe Hai wa COSTECH, Dk.Bakari Msangi alisema kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala yote yanayohusu  Sayansi na Teknolojia na kusimamia tafiti zote za kisayansi katika maeneo mbalimbali na kilimo na kuhakikisha zinawafikia walengwa.

Alisema mbegu hizo walizozikabidhi zimefanyiwa utafiti na zitapandwa katika mashamba darasa na baadae kusambazwa kwa wakulima wengine ili kuondoa changamoto ya kukosekana kwa mbegu bora kutokana na wakulima kukabiliwa na mbegu ambazo zilikuwa na magonjwa kama batobato na ukame.

Akizungumzia mbegu bora ya viazi lishe alisema mbegu hiyo viazi vyake vinavitamini A ya kutosha ambayo ni muhimu kwa watoto na hiyo itawasaidia baadhi yao kuto kwenda Hospitali kuipata badala yake wataipata kwa kula viazi hivyo.

Msangi aliwaomba maofisa ugani pale wanapokuwa na changamoto mbalimbali za kazi yao wasisite kwenda COSTECH ili kusaidiana na kupeana mbinu mbalimbali za kilimo.

Mkulima wa Kijiji cha Isamilo, Hermick Elias alisema kukosekana kwa mbegu bora, wataalamu wa kilimo na kutofikiwa na pembejeo za kilimo kwa wakati ni moja ya sababu ambayo imewarudisha nyuma katika masuala ya kilimo lakini wanaamini kwa mbegu hizo walizoletewa na COSTECH itakuwa nu mkombozi kwao kwa kupata chakula na ziada watauza na kujipatia fedha za kuwasaidia.

Alisema kwa kilimo walichokuwa wakikifanya ekari moja walikuwa wakipata mahindi kuanzia magunia nane hadi tisa lakini kwa maelezo ya watafiti hao wa kilimo iwapo watatumia mbegu hiyo bora wataweza kupata magunia kuanzia 25 hadi 30.

Mkulima Salome Renatus aliipongeza serikali na COSTECH kwa kuwapelekea mbegu hizo hivyo wanatarajia kupata mazao yenye tija tofauti na awali.

Mbegu hizo zitapandwa katika mashamba darasa katika wilaya zote za mkoa wa Geita, Nyang'wale, Mbogwe,Chato na Bukombe.

NAIBU WAZIRI ULEGA AWATAKA WAFUGAJI WA OLOLOSOKWAN KUWA WATULIVU KUSUBIRI UTATUZI WA MGOGORO WAO NA HIFADHI

$
0
0
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wafugaji wa Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha juu ya kuwa watulivu wakati suala la mgogoro kati yao na hifadhi likiwa linashughulikiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega amewataka wafugaji wa Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha kuwa watulivu wakati suala la mgogoro kati yao na hifadhi likiwa linashughulikiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Naibu Waziri Ulega ameeleza hayo jana katika mkutano na wafugaji hao uliofanyika kwenye Kata ya Ololosokwan wilayani humo.

“Wakati tunamsubiri Waziri Mkuu atoe maelekezo naomba msiharibu hali ya hewa hii ndiyo rai yetu.Au kuna yeyote anayepinga jambo hili? Aliwauliza wafugaji hao na kujibiwa hakuna na wote wapo pamoja na Serikali.

“Hatua hii itaturahishishia sisi kwa sababu wizara inaliangalia jambo hili kwa ukaribu kutokana sehemu kubwa ya nchi wafugaji wamekuwa malalamiko makubwa sana ikiwamo kufilisia mifugo yao pindi inapoingia hifadhini na kusababishiwa umasikini,”amesema Ulega.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka alimweleza Ulega kwamba ukosefu wa malisho ni mojawapo ya changamoto inayowakabili wafugaji hao kutokana maeneo machache yaliyopo.

Hata hivyo, Ulega alihaidi kulishughulikia changamoto hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa pamoja watatafuta mashirika kwa ajili kuangalia namna ya kuboresha malisho hayo ili kuleta ahueni kwa wafugaji hayo.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akisalimina na wazee wa Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Mmoja wa wafungaji Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega wilayani Ngorongoro mkoani Arusha.
 Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka akizungumza na wananchi wa kata ya Ololosokwan mkoani Arusha.
Wanana wa kata ya Ololosokwan wilayani Ngorongoro mkoani Arusha,wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega. Picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii,Arusha.

MWENYEKITI (CWT) MUFINDI OBI KIMBALE WALIMU TUNAISHI KWENYE MAPAGALE TUNAOMBA VIWANJA

$
0
0
 Na Fredy Mgunda,Mufindi

Chama cha walimu wa Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa kimemuomba mkurugenzi kuwakopesha viwanja walimu ili kujikwamuamua na mazingira magumu wanayokumbana katika nyumba wanazoishi.

Hayo yalisemwa na mwenyekiti chama cha walimu wa Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi Obi Kimbale alisema kuwa walimu wamekuwa wakiishi katika nyumba chakavu au mbali na mazingira ya shule kitu kinachosababisha kushuka kwa uwezo wa walimu kufundisha.

Kimbale alisema kuwa walimu hawana pesa za kununua moja kwa moja viwanja hivyo kwa njia ya kuwakopesha inawezekana kutokana kuwa ni waajiliwa wa serikali na mishahara yao inajulikana na ni rahisi kuresha mkopo huo.

“Sisi walimu ukitaka kujua mimi nalipwa shilingi ngapi ni rahisi tu kwa kuwa mishahara ya serikali mara nyingi inajulikana hasa pale mtumishi unapoenda kukopa mahali ndio maana tunaiomba serikali itusaidie kukopa viwanja kuwa kuwa tunauwezo wa kulipa kwa awamu tatu” alisema Kimbale
Aidha Kimbale aliwatupia lawama maafisa elimu na walimu wakuu wa shule kwa kuwanyima ruhusa bila kuwa na sababu maalum. 

“Wakurugenzi amekuwa ametoa kibali upewe ruhusa lakini viongozi waliochini ya mkurugenzi wanatuwekea vipingamizi ambavyo havieleweki kitu kinachozua utata mkubwa baina ya viongozi na walimu ambao sio viongozi” alisema Kimbale

Kimbale alimpongeza wakurugenzi wa halmashauri ya mufindi na mji wa mafinga kwa kuwajali walimu kwa kuwapa ruhusa pale inapotakiwa tofauti na hali ilivyo kwa hawa viongozi wa chini yake.

“Unakuta siku ya wanawake duniani au siku ya walimu duniani bado walimu wananyimwa ruhusa wakati muda huo mkurugenzi amewaruhusu walimu kuhudhuria sherehe hizo kitu kinachoongeza ukakasi baina ya watendaji wa nafasi za juu na watendaji wa nafasi za chini” alisema Kimbale


Kimbale aliwapongeza walimu wa manispaa ya Iringa kwa kuendelea kufanya kazi kwa kujituma licha ya kukumbana na changamoto mbalimbali ikiwepo kunyimwa ruhusa.

Akijibu hoja hizo mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Williamu alisema haelewi kwanini mara kwa mara swala hilo linakuwa linajirudia maana tulishalitafutia ufumbuzi hapo awali.

Sasa naenda kuandika barua rasmi kwa wakurugenzi ili kutatua kabisa tatizo hilo maana hata kwangu imekuwa kero na mwazoni nilijua wakuu wa shule ndio tatizo kumbe maafisa elimu ndio tatizo naenda kulishughulikia kwa haraka sana swala hili” alisema Williamu

Williamu aliwataka maafisa elimu na wakuu wa shule wote wa wilaya ya Iringa kuwapa ruhusa walimu pale ambapo wanapata matatizo maana hakuna haja ya kumnyima ruhusa mtu akiwa anashida na watakiwa kuzifahamu siku za kitaifa ambazo ni lazima walimu wahudhurie wanapaswa kutoa ruhusa bila kipingamizi.

“Kunasiku kama siku ya mwalimu,siku ya wanawake na siku nyingine za kitaifa walimu wanapaswa kupewa ruhusa kwenda kuhudhuria tukio hilo kutokana na umuhimu wake” alisema Williamu

Williamu alisema kuwa mkurugenzi ndio mwajili sasa hao maafisa elimu na wakuu wa shule wanatoa wapi hiyo jeuri ya kuwanyima ruhusa ambayo viongozi wa ngazi za juu wanajua kuwa kunakitu kinafanyika cha taifa.

Williamu aliwataka viongozi wa walimu kuandika barua ya kuomba viwanja ili waweze kulishughulikia swala hilo likiwa kwenye maandishi.

“Andikeni barua yenye idadi na majina ya walimu wanaotaka viwanja ili kuondoa kasumba ya kusema wanaotaka ni kikukindi cha walimu wachache tu na bila kufanya hivyo swala lenu la kuomba viwanja litakuwa gumu kulitafutia ufumbuzi” alisema Williamu
Williamu aliwaomba walimu wawewavumilivu katika kipindi wacholishughulikia swala hilo kwa kuwa sio jambo la kukurupuka linahitaji utulivu wa kutosha ili kufanikishwa swala walimu kupata viwanja.

Naye afisa elimu wa wilaya ya Mufindi alisema kuwa watawatafuta hao maafisa ambao wanawanyima ruhusa walimu wakati swala hilo lilishatafutiwa ufumbuzi.

“Jamani sisi huku sheria tulishaiweka kwenye matukio muhimu ya kitaifa walimu wapewe ruhusa sasa sijui ili sawala limetoka wapi naomba nikitoka hapa nitazungumza na wakuu wa shule pamoja na maafisa elimu wenzangu”
Mwenyekiti chama cha walimu wa Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi Obi Kimbale akizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
mkuu wa wilaya ya Mufindi Jamhuri Williamuakizungumza na waandishi wa habari wakati wa mkutano mkuu wa chama cha walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

KISHINDO CHA MSIMU WA TIGO FIESTA CHAACHA GUMZO MOSHI

$
0
0
Wasanii Banarba na Gnako wakishiriki uzinduzi wa huduma mpya ya Tigo ya TUMEKUSOMA ambayo ni namba maalum (code number) itakayowawezesha wateja wa Tigo kuingia kwenye menyu na kupata huduma mbalimbali. Uzinduzi huo ulifanyika kwenye tamasha la Tigo Fiesta lililofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.
Msanii Bright akiwa kwenye jukwaa la Tigo Fiesta liliofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.
Chege akiburudisha kwenye jukwaa la Tigo Fiesta liliofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.
Msanii Bright akiwa kwenye jukwaa la Tigo Fiesta liliofanyika uwanja wa Majengo Manispaa ya Moshi usiku wa kuamkia jumatatu.
Umati wa wakazi wa Moshi wakiwa wanashuhudia burudani iliyokuwa inatolewa na wasanii .
Gigy Money akiwa katika jukwaa la Tigo Fiesta mapema usiku wa kuamkia jumatatu



Jux akiburudisha wakazi wa Moshi mapema usiku wa kuamkia jumatatu katika jukwaa la Tigo Fiesta .





TIGO Fiesta 2017 imefana vilivyo mkoani Kilimanjaro ambapo wasanii mbalimbali wa Bongo fleva wamefanya vilivyo katika viwanja vya Majengo katika Manispaa ya Moshi kwa kutoa burudani ya kukata na shoka kwa wakazi wa manispaa hiyo.

Katika kuhakikisha kuwa kila mkazi wa Moshi anafurahia vilivyo tamasha maalumu la Tigo Fiesta 2017 ambapo mdhamini mkuu wa tukio hilo la aina yake Tigo Tanzania leo wametangaza namba maalumu ya wateja ambayo ni *147*00# hii inajulikana kama TUMEKUSOMA ambayo  wateja wataweza kufanya kuitumia katika huduma mbalimbali za Tigo.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika tamasha maalumu la Tigo Fiesta 2017 katika Manispaa ya Moshi, Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Tigo Tanzania, William Mpinga alifafanua kuwa, namba hiyo mpya (Code number) itatumika kwa wateja wa Tigo kote Tanzania katika kupata huduma mbalimbali za mtandao huo.


Tofauti na matukio  yaliyotangulia, washiriki wote kutoka mtandao wowote kwa tamasha la mwaka huu mbali na kupata huduma ya kulipia kiingilio kwa huduma ya Tigo-Pesa, pia wamepata burudani kabambe kutoka kwa wasanii mbalimbali wa muziki kutoka Tanzania.

Wasanii waliotumbuiza katika Tigo Fiesta katika viwanja vya Majengo katika Manispaa ya Moshi ni pamoja na Rich Mavoko, Chege, Nandy, Maua, Vanessa, Jux, Ben Pol, Rostam, Weusia, Darassa,Lulu Diva, Rosa Lee, Mimi Mars, OMG, Gigy Money,  Asley na wasanii wengineo.


Jukwaani Msanii Rosa Ree aliingia kama Malkia na kiti chake nakuwafanya mashabiki wapagawe na wimbo wake Mchagamchaga na nyingine,
Msanii Aslay kama ilivyokawaida yake mashabiki waliweza kuimba nae mwanzo mwisho wa nyimbo zake zote, wimbo wake mhudumu ndio uliwapagawisha zaidi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya kaskazini, Henry Kinabo amewataka watanzania kutumia huduma mbalimbali zitolewazo na Tigo kwa kuwa faida inayotokana na huduma inasasaidia huduma mbalimbali za kijamii zikiwemo elimu, afya na nyinginrezo ikiwamo mtandao wa intaneti.

“Nawashauri watanzania wote kutumia huduma mbalimbali bora zitolewazo na Tigo  kwani sehemu kubwa ya faida tunayopata tunairudisha kwa jamii kupitia huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu hasa huduma ya intaneti kwashule mbalimbali, mbali madawati tuliyoto mwaka jana..” alifafanua Kinabo.  

UNDANI KUHUSU SHEREHE ZA HALLOWEEN KILA IFIKAPO OKTOBA 31

$
0
0

Na Jumia Travel Tanzania

Inawezekana utakuwa umesikia watu au kusoma kwenye mitandao ya kijamii kuhusu sherehe za Halloween lakini ukawa hauelewi. Mbali na hapo inawezekana pia umekutana na matangazo kadhaa yakikutana kushiriki kwenye sherehe za sikukuu hiyo sehemu kadhaa za starehe hususani vilabu vya usiku hapa nchini.
Kutokana na utandawazi uliosababisha dunia kuwa kijiji tumejikuta kwa namna moja ama nyingine tukishiriki matukio mbalimbali kwa wakati mmoja. Baadhi ya matukio hayo huwa hatuelewi maana yake kwa undani zaidi. Kwa mfano, Halloween kwa namna inavyosherehekewa ni kama ina uhusiano na sherehe za kishetani.

Ikiwa sehemu mbalimbali duniani zimeshaanza maandalizi ya sherehe za Halloween ambazo hufanyika kila ifikapo Oktoba 31 ya kila mwaka, Jumia Travel ingependa kukufahamisha juu ya maana halisi ya sherehe hii.  
Japokuwa umaarufu wa sherehe ya Halloween umetokana na nchi ya Marekani lakini ukweli ni kwamba wanahistoria wanaamini sherehe hii ilianzia nchini Ireland na kusambaa nchi za jirani za Scotland, Uingereza, Ufaransa na baadaye sehemu zingine duniani.

Na kudhihirisha kwamba Marekani inasherehekea sherehe hii kikamilifu, inaaminika kwamba ni sherehe ya pili kwa ukubwa wa kibiashara ndani ya mwaka. Katika kipindi hiki takwimu zinaonyesha kwamba wamarekani hutumia zaidi ya dola bilioni 5 kuadhimisha sherehe hii. Na kwa kuongezea robo ya mauzo yote ya peremende au pipi ya mwaka hufanyika ndani ya kipindi hiki nchini humo.
Halloween ina maana gani na kwanini husherehekewa kila ifikapo Oktoba 31 ya mwaka?

Maana halisi ya neno Halloween ni siku ya mkesha wa siku ya watakatifu wote ambayo huadhimishwa kila ifikapo Novemba mosi. Halloween pia ni ufupisho wa neno ‘Allhalloween, All Hallows’ Evening na All Saint’s Eve’ ambapo husherehekewa kila ifikapo Oktoba 31 ya kila mwaka.

Asili ya Halloween ilitokana na sherehe ya ‘Samhain’ iliyokuwa ikiadhimishwa na watu wa kale wa Ireland au ‘Waseltiki’ kama wanavyojulikana.

Samhain ni sherehe ya wapagani wa kiseltiki ikimaanisha ‘Mwisho wa Majira ya Joto’ ambayo huadhimishwa mwisho wa msimu wa mavuno.

Hiki kilikuwa ni kipindi ambacho walikuwa wakiwasha moto kuuzunguka na kisha kuvalia mavazi yanafanana na ya mashetani ili kuepekana na mizimu inayosemekana huwa inarandaranda usiku huo.

Katika karne ya nane, Papa Gregory III alisema kwamba Novemba mosi itakuwa ni siku ya kuwakumbuka watakatifu na wafia dini wote. Na hapo ndipo ‘Siku ya Watakatifu Wote’ ilipoanzia na jioni yake ilikuwa ikijulikana kama ‘All Hallows’ Eve’ na baadaye kuwa Halloween.
Halloween imepata umaarufu mkubwa kadiri muda unavyokwenda na kuwa kipindi cha kufanya biashara kwa wingi ambapo watoto na watu wazima husherehekea kwa kuvalia mavazi ya kuogofya kama mizimu au mashetani na kwenda kuhudhuria sherehe zinazoandaliwa.

Kwanini watu huvalia mavazi ya kuogofya usiku wa Halloween?

Utamaduni ambao umekuwepo kwa miaka mingi katika kusherehekea Halloween ni pamoja na kuvalia mavazi ya kutisha kama mizimu au mashetani.
Washerehekeaji hufanya hivyo kutokana na asili ya sherehe hii ambapo inaamini kwamba katika mkesha wa siku ya Oktoba 31 kuamkia Novemba mosi mashetani, wachawi na mizimu huwa inarandaranda mitaani kusherehekea kuanza kwa msimu wao - kipindi cha majira ya baridi. Inasemekana kwamba huranda mitaani na kuwachezea watu, kuwatisha, kuwadhuru na kuwafanyia hila mbalimbali kadiri wanavyopenda.

Njia pekee kwa watu waliokuwa wanaogopa kutishwa na mizimu hiyo ni kuwapatia vitu ambavyo walikuwa wanavipendelea, mara nyingi huwa ni vyakula vitamu na zawadi nzuri kama vile peremende kwa kuviacha milangoni.

Au, njia nyingine iliyokuwa ikitumika, kwa watu ambao walikuwa wanaogopa, ni kwa kuvalia mavazi kama yao na kisha kurandaranda mitaani, lengo ni kwa mizimu hiyo kutowatambua na kuwafananisha binadamu hao na wenzao.
Je unajiuliza kama usherehekee sikukuu ya Halloween? Kumekuwa na dhana tofauti juu ya sherehe hii ambayo kwa namna moja ama nyingine zimekuwa zikihusishwa na ushetani na ushirikina. Hii inategemea namna wewe mwenyewe utakavyosherehekea na kwa malengo gani na kama itaathiri vipi imani yako. Kwa makala haya, Jumia Travel inaamini kwamba utakuwa umefahamu machache kuhusiana na sherehe hii ambayo inazidi kushika kasi kadiri miaka inavyokwenda.
Viewing all 46401 articles
Browse latest View live




Latest Images