Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46396 articles
Browse latest View live

TANZANIA YASIFIWA UN KWA MAGEUZI YA RAIS DKT MAGUFULI-DKT MAHIGA


Kesi ya uhujumu uchumi dhidi ya aliyekuwa mhasibu wa TRA yapigwa kalenda.

$
0
0
Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

Upande wa mashtaka katika kesi ya uhujumu uchumi inayowakabiki watu watatu akiwemo Mhasibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Reuben Mwakasa, umeieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa shauli hilo bado haujakamilika.

washtakiwa hao ambao walifikishwa majakamani hapo wiki iliyopita na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Respicius Mwijage wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kuisababishia hasara TRA ya sh. bilioni 29.

Mbali na Mwakasa, mkazi wa Msagara, Moshi, Kilimanjaro, washitakiwa wengine ni Meneja wa Tema Enterprises, Ephraim Magete, mkazi wa Kigamboni, Dar es Salaam na mfanyabiashara Elizabeth Massawe, mkazi wa Makongo Juu.

Mwendesha mashtaka wakili wa serikali mwandamizi Mutalemwa Kishenyi amedai mahakamani hapo kuwa kesi leo imekuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi bado haijakamilika.

Awali wakisomewa hati ya mashtaka na wakili wa Serikali Mkuu, Faraja Nchimbi, ilidaiwa, kati ya Novemba 22, 2013 na Agosti 21, mwaka huu, katika maeneo mbalimbali wilaya za Temeke na Ilala.

washitakiwa hao kwa pamoja kwa vitendo vyao waliisababishia mamlaka hiyo hasara ya kiasi hicho kwa kukwepa kulipa kodi kwenye mamlaka hiyo.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Octoba 11, mwaka huu.

REBECCA AMOS AJISHINDIA KITITA CHA MILIONI 60 ZA TATU MZUKA

$
0
0
  Meneja Mawasiliano wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akizungumza mapema leo mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu namna mchezo huu wa Tatu Mzuka unavyobadili maisha ya watu,huku akimtaja Rebecca Amos (pichani kulia),mkazi wa Yombo Vituka aliyejishindia kitita cha shilingi milio 60,picha shoto ni rafiki wa mshindi wa Tatu Mzuka kwa wiki hii,Agness Swai

Maganga  alisema kuwa Droo inayofanyika mara moja katika Juma si aina pekee ya kupata washindi katika mchezo huu, kwa kuwa kila mtu anapocheza Tatu Mzuka anapata pia nafasi ya kushinda mara 200 ya kiasi alichotumia kucheza kila saa. Droo hizi za kila saa kwa sasa zinatoa washindi ambao wanapata hadi kiasi cha shilingi milioni 300,000 katika Juma, kwa washindi mbalimbali nchini Tanzania.”
 Rebecca Amos (pichani kulia),mkazi wa Yombo Vituka aliyejishindia kitita cha shilingi milio 60 za Tatu Mzuka,akitoa ushuhuda wake kuhusiana na mchezo huo na hatimaye nae kuibuka mshindi wa mamilioni.Rebecca amewaasa watu wengine kucheza mchezo huo kwani mmoja wao anaweza akaibuka mshindi na kubadilisha kabisa mfumo wake wa kimaisha kupitia fedha atakazo kuwa ameshinda 
Meneja Mawasiliano wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi mshindi Rebecca Amos ,mkazi wa Yombo Vituka aliyejishindia kitita cha shilingi milioni 60,mapema leo jijini Dar.

Kwa mara nyingine mchezo wa Bahati Nasibu wa Tatu Mzuka, mchezo unaojinyakulia umaarufu mkubwa nchini Tanzania, umetangaza mshindi wake wa droo kubwa ya Juma la nane ambaye amejishindia kitita cha shilingi za Kitanzania milioni 60. Mshindi huyu si mwingine bali Bi. Rebecca Amos mkazi wa Yombo Vituka, jijini Dar es Salaam. 

Bi Rebecca, mwenye umri wa miaka 22, ameibuka na ushindi huu mnono katika mchezo uliofanyika Jumapili iliyopita na kurushwa mubashara katika televisheni.

Kufuatia zawadi hii ya iliyotolewa Juma hili na aina ya washindi wanaoibuka, mchezo wa Tatu Mzuka ni dhahiri umeendelea kuleta mageuzi makubwa katika eneo la michezo ya Bahati Nasibu hapa nchini. Hii inatokana na aina ya washindi wanaopatikana na pia uwezo Tatu Mzuka kutoa zawadi za washindi zinazofikia kiasi cha shilingi milioni 2 kila saa kwa saa 24 kwa siku. Ushindi huu unatolewa ilhali kiasi cha kushiriki katika mchezo huu kikiwa ni kuanzia shilingi 500 tu huku droo za kusaka washindi zikifanyika kila saa.

Akizungumza na vyombo vya habari kuhusu namna mchezo huu wa Tatu Mzuka unavyobadili maisha ya watu, Meneja Mawasiliano wa Tatu Mzuka Sebastian Maganga alisema; “Droo inayofanyika mara moja katika Juma si aina pekee ya kupata washindi katika mchezo huu kwa kuwa kila mtu anapocheza Tatu Mzuka anapata pia nafasi ya kushinda mara 200 ya kiasi alichotumia kucheza kila saa. Droo hizi za kila saa kwa sasa zinatoa washindi ambao wanapata hadi kiasi cha shilingi milioni 300,000 katika Juma, kwa washindi mbalimbali nchini Tanzania.”

Bw. Maganga pia aliongeza kuwa, “tumeongeza kipengele cha ziada katika Tatu Mzuka ambacho kinaitwa ‘Cheza na Washkaji, shinda na washkaji’. Katika kipengele hiki, mshindi wa droo kubwa anapata pia nafasi ya kutaja majina matatu ya rafiki zake ambao nao hujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 1 kila mmoja.”

Bi. Rebecca pia amefanikiwa kutaja majina matatu ya rafiki zake ambao wamejinyakulia kiasi cha shilingi milioni 1 kila mmoja. Washindi hao wa ziada wa Bi. Rebecca walikuwa ni mpenzi wake wa miaka mitano Bw. Ramathan Majiran na marafiki zake wawili tangu shule ya Msingi Agnes na Amina.

Washindi hawa wa nyongeza nao hawakuamini ushindi wao hadi pale fedha za ushindi ziliporushwa katika simu zao. Amina alikimbia kwa furaha kutoa fedha zile na kushangilia akiwa kazishika mkononi huku Agnes alishangaa kuona fedha hizo zikiingia kwenye simu yake kupitia MPESA wakati akipata mlo wa mchana. “Nilijawa furaha kubwa sana ambayo ilinifanya kutoendelea kula,” anasema Agnes.

Bi. Rebecca mshindi wa droo ya nane, ni mama wa motto mmoja ambaye hana ajira kwa sasa. Anaishi na wazazi wake ambao anawategemea kwa kila kitu.

“Nimekuwa na ndoto, ndoto kubwa tu lakini sikuwahi kuota bkuwa ipo siku nitafanikiwa kushika fedha nyingi kiasi hiki. Sasa naweza kuanzisha biashara, kuwasaidia wazazi wangu na pia kuwa na uwezo wa kumhudumia mwanangu. Kipi cha ziada ambacho binadamu anaomba kupata zaidi ya hiki?” Bi. Rebecca alisikika akisema.

Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO katika Siku ya Kimataifa ya Ufikivu Habari Sept 28

$
0
0
 Katika ulimwengu wa uchangamano, ufikivu wa habari ni muhimu katika kujenga jamii yenye maarifa, iliyo shirikishi na endelevu. Huu ndio ujumbe wa Siku ya Kimataifa ya Ufikivu Habari kwa Wote (IDUAI), ukizingatia jukumu muhimu ambalo ufukivu wa habari hufanya katika kuendeleza Agenda ya 2030 ya Maendeleo Endelevu. 

Ufikivu habari ni haki ya msingi. Inawawezesha wanawake na wanaume kuelewa na kushiriki katika kujenga na kushirikiana ujuzi wanaohitaji ili watoe mchango kikamilifu katika jamii yao. Raia wenye taarifa sahihi huifanya serikali iwajibike. 

Ufikivu Habari ni dereva wa uvumbuzi na ubunifu, kuongeza fursa kwa wote, hasa kwa wasichana na wanawake. Ufikivu habari huanza na kujitolea kwa Serikali kutengeneza, kueneza na kutekeleza sera na sheria zinazohusu haki ya habari na kuhakikisha kuheshimiwa kwa haki hii ya kibinadamu. Hii inahitaji utaratibu wa ufanisi wa utekelezaji na utamaduni wa uwazi katika aina zote za taasisi. 

Wananchi wanahitaji pia kuwa na fikra pana, ujuzi wa kusoma na ujuzi wa kidigitali ambao unahitajika kufikia, kuchambua na kutumia habari kwa njia tofauti, nje na ndani ya mitandao. Hii ndiyo maana UNESCO inaziomba serikali zote na washirika kutumia uwezo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ili kusaidia kufikia Lengo la 4, Elimu Endelevu inayolenga kuhakikisha "elimu shirikishi, sawa na ya ubora na kukuza fursa za elimu isiyo na mwisho kwa wote; Ufikivu wa Habari pia unajumuisha kukuza uandaaji wa maudhui yanayofaa, yenye kulenga jamii husika na yanayopatikana kwa lugha mbalimbali. Yote hii inahitaji sera zenye ufanisi na ushirikiano mzuri katika ngazi zote.  Siku ya Kimataifa ya Ufikivu Habari kwa Wote pia ni fursa ya kurejea ahadi yetu ya uhuru wa kujieleza na usalama wa waandishi wa habari. Vyombo vya habari huchukua nafasi muhimu katika kuwezesha ufikivu wa habari kwa wananchi na katika kufuatilia masuala muhimu ya kijamii na wakati huo huo vikiwaelimisha wafuatiliaji kwa kuwapa ufahamu na ujuzi. 

Haiwezekani kuwepo kwa ufikivu wa habari kwa wote bila kuwepo kwa vyombo vya habari vilivyo huru. Ufikivu wa habari sio tu ni lengo peke yake; pia ni mchangiaji muhimu katika utekelezaji wa malengo mengine yote ya Maendeleo Endelevu. Kwa hiyo ni muhimu tuendeleze juhudi zetu ili kuhakikisha kuwa kila mwanamke na mwanamume wanafurahia ufikivu kamili wa habari.

Marekebisho ya sheria katika sekta ya madini hayatambuliki na kufanya sekta hiyo kukosa mabadiliko –CAG Ripoti

$
0
0
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

OFISI ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali(CAG) imebainisha kuwa kipengele cha kutotambua marekebisho ya sheria kilichomo kwenye mikataba ya madini kimekuwa kikichangia kutoonekana kwa mabadiliko katika sekta hiyo.

Hayo yamebainishwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu wa Nje wa ofisi ya CAG, Johannes Kisiri wakati wa kutoa mada kuhusu ukaguzi wa hesabu za mashirika ya umma katika sekta ya gesi kwenye warsha ya asasi za kiraia na waandishi wa habari, amesema mikataba mingi ya madini na gesi kuna kipengele ambacho sio muafaka kwa faida ya taifa ambacho kinasema ‘ yatakayobadilika kwenye sheria hayataathiri makubaliano ya awali,” amesema

Kisiri amesema ukaguzi umegundua kuwa Kampuni ya Tanzanite One Tanzania Limited(TML) iliyoingia mkataba wa kuchimba madini ya tanzanite na Shirika la Madini la Taifa(Stamico) imekuwa ikiizuia madini hayo kampuni ya Sky Associates Vila ya bila kuishirikisha stamico.

Amesema ushauri wa CAG kuhusiana na mradi kuazalisha umeme katika Korongo la Stiegler ambao ulikuwa unasimamiwa na Mamlaka ya Uendelezaji Bonde la Rufiji (RUBADA) umefanyiwa kazi kutokana ripoti ya CAG ilianisha kuwa RUBADA haikuwa na uwezo wa kifedha wa kuenesha mradi huo na kushauri kufanywa na taasisi za umma zenye uwezo kama tanesco,” amesema

Mradi huo ambao ungekuwa na manufaa sana kwa gharama za dola za marekani bilioni 2.4 (sawa na Sh trilioni 6) na kutakiwa kuzalisha megawati 2,100 ambapo Bunge limefuta sheria iliyoanzisha RUBADA kupisha taasisi nyingine kuendesha mradi huo.

Mradi huu ulipangwa kutekelezwa katika vipindi vya awamu tatu, ambapo awamu ya kwaza ungezalisha megawati 300, ya pili 600 na awamu ya mwisho ni megawati 300 ambayo ingekamilika mwaka 2028.

Kisiri amesema mikataba inailazimisha tanesco kununua umme kwa Sh 544.65 kwa uniti moja kutoka kampuni binafsi na kuuza kwa Sh 279.35 kwa uniti
 Mkurugenzi Msaidizi wa Ufatiliaji na Tathimini wa CAG, Wendy Masoyi akizungumza katika ufunguzi wa warsha warsha ya Nne ya Asasi zisizo za Kiserikali na waandishi wa habari katika kupata toleo maalum kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30, 2016 iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa kitengo cha mawasiliano serikalini wa Ofisi ya CAG, Sarah Reuben akineonesha muundo wa kitabu cha machapisho ya ukaguzi wa CAG kwa mwaka ulioshia Juni 30 ,2016 kwa wana warsha hawapo pichani iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mkaguzi wa Serikali za Mitaa wa CAG Temeke, Angel Moshi akitoa mada kwa wana warsha hawapo pichani juu ya miradi mbalimbali iliyoangaliwa katika ukaguzi wa CAG kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30 , ilifanyika jijini Dar es Salaam.
 Sehemu ya wadau wakifatilia taarifa katika warsha ya toleo maalum kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30 ,2016 iliyohusisha Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani pamoja na Dar es Salaam.
Picha pamoja wadau katika warsha ya toleo maalum kwa mwaka wa fedha ulioshia Juni 30 ,2016 iliyohusisha Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani pamoja na Dar es Salaam.

RAIS NA MWENYEKITI WA CCM DKT MAGUFULI AENDESHA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 Kikao hicho kimehudhuriwa na wajumbe wote wa Halmashauri Kuu,wakiwemo Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Alli Mohamed Shein,Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kassim Majaliwa na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Alli Idd.
 Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)Ndg. Phili Mangula akikaribishwa ukumbini katika kikao cha Kamati Kuu ya Chama hicho kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt John Pombe  Magufuli akiwasili ukumbini kuongoza kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
  Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini  Dar es Salaam. Kushoto ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai na nyuma ya Makamu  wa Rais ni Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa na Spika wa Baraza wa Wakilishi la Zanzibar
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akisalimiana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini Dar ss Salaam.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Rodrick Mpogolo kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichoanza leo Jumatano ya Septemba 27, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam.

FCS YAWEZESHA AZAKI ZA ZANZIBAR KUFANYA MAFUNZO YA UTETEZI MOROGORO

$
0
0
Meneja wa Kitengo cha Kujenga Uwezo kutoka Foundation for Civil Society, Edna Chilimo, akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wana Asasi za Kiraia kutoka Visiwa vya Zanzibar yaliyofanyika katika ukumbi wa New Savoy mjini Morogoro. 

Makundi washiriki wa mafunzo hayo ni Azaki kutoka Zanzibar na Pemba ambapo wanashiriki mafunzo ya Utetezi na Ushawishi wa Sera kutoka kwa mashirika ya MVIWATA (Muungano wa Vyama vya Wakulima Wadogo Tanzania) na MPLC (Morogoro Para-Legal Center). Mashirika haya mawili yamebobea katika Ushawishi na Utetezi wa haki za kumiliki ardhi kwa makundi mbalimbali mkoani Morogoro. Picha zote na Muhidin Sufiani (MAFOTO).
Mshauri Mwelekezi wa Mradi wa Sera kutoka The Foundation for Civil Society Zanzibar, Salma Maulidi, akiendesha mafunzo hayo ndani ya ukumbi wa New savoy Morogoro.
Mkulima Mwezeshaji wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania MVIWATA Morogoro, Marcelina Kibena akiendesha mafunzo kwa washiri kutoka asasi za Kiraia za Visiwani Zanzibar yaliyofanyika katika Ofisi za MVIWATA zilizopo Viwanja vya Nane Nane mjini Morogoro.
Ofisa Miradi wa Morogoro Para-Legal Center (MPLC) Sakina Nyumayo, akifafanua jambo kwa washiriki hao wakati wa mafunzo.
Baadhi ya washiriki katika ukumbi wa Ofisi za MVIWATA viwanja vya Nanenane.
Baadhi ya washiriki katika ukumbi wa Ofisi za MVIWATA viwanja vya Nanenane, Morogoro Para-Legal Center.



Ofisa Miradi wa Morogoro Para-Legal Center, Augustino Ernest akifafanua jambo kwa washiriki kuhusu utendaji wa majukumu ya kikazi wakati walipotembelea katika ofisi hiyo.
Wakati wa maswali

Umakini wa kusikiliza

Ofisa Miradi wa Morogoro Para-Legal Center, Augustino Ernest akifafanua jambo kwa washiriki kuhusu utendaji wa majukumu ya kikazi wakati walipotembelea katika ofisi hiyo.
Mshauri Mwelekezi wa Mradi wa Sera kutoka The Foundation for Civil Society Zanzibar, Salma Maulidi, akiendesha mafunzo hayo ndani ya ukumbi wa New savoy Morogoro.
Hata hapa ntasikia kwa umakini tu.
Umakini wa kusikiliza
Akijibu baadhi ya maswali kutoka kwa washiriki
Umakini wa kurekodi kumbukumbu ya mafunzo
Mafunzo yakiendelea.....
Washiriki wakijieleza jinsi walivyoelewa na kupata elimu kutoka kwa wenzao MVIWATA na MPLC.
Washiriki wakijieleza jinsi walivyoelewa na kupata elimu kutoka kwa wenzao MVIWATA na MPLC.
Waashiriki wakijieleza jinsi walivyojifunza na kuelewa mengi kutoka kwa wenzao.
Mafunzo yakifungwa rasmi siku ya kwanza.

Miss Vyuo Vikuu sasa kufanyika Oktoba mwishoni

$
0
0
Dar es Salaam. Mashindano ya kumsaka mrembo wa vyuo vikuu vya Tanzania “Miss Higher Learning Institution 2017” yaliyopangwa kufanyika kesho Ijumaa ( Septemba 29) kwenye ukumbi wa King Solomoni, Namanga jijini yamehairishwa.

Kuhairishwa kwa mashindano hayo kumetokana na sababu za kalenda na waandaaji kufikia makubaliano ya kusogeza mbele mpaka mwishoni mwa mwezi ujao.Mashindano hayo yameandaliwa na kampuni ya Glamour Bridal Tanzania baada ya kupewa idhini ya waandaaji wa Miss Tanzania, Lino International Agency kwa kushirikiana na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata).

Mkurugenzi wa Glamour Bridal Tanzania Muba Saedo alisema kuwa hatua hiyo imefikiwa kwa lengo la kuboresha zaidi na hatua hiyo itawawezesha kufanya mashindano yenye upinzani wa hali ya juu kutokana na idadi ya vyuo mbalimbali vilivyothibitisha.

“Tumelazimika kusogeza mbele mashindano kutokana na sababu ambazo zipo nje ya uwezo wetu, warembo wataendelea na kambi chini ya mkufunzi wao Clara Michael na ba matron, Blessing Ngowi,” alisema Saedo.

Mbali ya Taasisi ya Ustawi wa Jamii (ISW), mashindano hayo yatashirikisha vyuo vya Taasisi ya Uhasaibu Dar es Salaam (TIA), IFM, CBE, UDOM, Tumaini – Makumira na Taasisi ya Uhasibu wa Arusha (IAA) na Chuo Kikuu Cha Ardhi.

Saedo alivitaja vyuo vingine kuwa ni Mzumbe, Chuo Kikuu cha Iringa, Tanzania Aviation University College na Magogoni.
 Warembo wa wanaowania taji la mrembo wa vyuo vikuu vya Tanzania “Miss Higher Learning Institution 2017” wakiwa katika picha ya pamoja. Shindano hilo lililopangwa kufanyika Septemba 29, limehairishwa mpaka mwishoni mwa mwezi ujao.
Warembo wa wanaowania taji la mrembo wa vyuo vikuu vya Tanzania “Miss Higher Learning Institution 2017” wakiwa katika picha ya pamoja. Shindano hilo lililopangwa kufanyika Septemba 29, limehairishwa mpaka mwishoni mwa mwezi ujao.

IGP SIRRO AFANYA UKAGUZI WA KUSTUKIZA HOSPITALI YA POLISI

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akisalimiana na maafisa wa Jeshi hilo alipowasili Hospitali ya Polisi iliyopo barabara ya Kilwa, kwa lengo la kuzungumza na uongozi na kujionea namna ya utoaji wa huduma za afya kwa wateja.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro (wa pili kulia), akimjulia hali mmoja kati ya wagonjwa wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya Polisi iliyopo barabara ya Kilwa, alipofanya ukaguzi wa ghafla katika hospitali hiyo kwa lengo la kuzungumza na uongozi na kujionea namna ya utoaji wa huduma za afya kwa wateja.
 Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akimsikiliza Kamanda wa Kikosi cha Afya (SACP) Paul Kasabago, alipofanya ukaguzi wa ghafla katika Hospitali ya Polisi iliyopo barabara ya Kilwa, kwa lengo la kuzungumza na uongozi na kujionea namna ya utoaji wa huduma za afya kwa wateja.

ASILIMIA 95 YA MIRADI YA KUBORESHA UMEME WA TANESCO DAR ES SALAAM IMEKAMILIKA:MHANDISI MGAYA

$
0
0
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO), limesema, tayari asilimia 95 ya uboreshaji miradi ya umeme katika jiji la Dar es Salaam, imekamilika.

Meneja Mwandamizi wa TANESCO Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Mhandisi, Mahende Mgaya, (pichani juu), amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo Septemba 27, 2017 na kwamba ifikapo Desemba mwaka huu wa 2017, wananchi na wakazi wa Dar es Salaam wataona ile hali ya kukatika kwa umeme, mara kwa mara imebadilika.

“Tulikuwa na jumla ya miradi mipya 18 ya kuboresha vituo vya umeme jijini Dar es Salaam ili viweze kutoa umeme wa kutosha na wa uhakika, hadi sasa, vituo vinane vimekamilika kabisa na vinafanya kazi, vimebaki vituo 10 ambavyo navyo viko katika hatua za mwisho za kukamilika, na ifikapo Desemba, 2017 vituo vyote 18 vitakuwa vinafanya akzi.” Alitoa hakikisho Mhandisi Mgaya.

Alisema, kufuatia kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na idadi ya watu jijini Dar es Salaam, mahitaji ya nishati ya umeme nayo yameongezeka na hivyo Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), iliamua kuchukua hatua za haraka kuboresha vituo vyake vya umeme ikiwa ni pamoja na kujenga vipya ili kukidhi mahitaji halisi ya umeme.

“Wafadhili kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika, (AfDB, World Bank, Finland, na Japan), walijitokeza na kufadhili miradi hiyo.”Alifafanua.

Kazi hiyo ya kuboresha vituo hivyo ambavyo ni pamoja na Mbagala, Kurasini, Kigamboni, Ilala Mchikichini, Kisutu, Mikocheni, Gongolamboto, na maeneo mengine imekuwa ikifanyika tangu miaka miwili iliyopita lakini kutokana na matatizo ya hapa na pale, ikiwa ni pamoja na mapingamizi ya wananchi kuzuia utekelezaji wa miradi hiyo, na wakandarasi, kumepelekea ucheleweshaji.

Maeneeo ambayo yamekuwa yakiathirika zaidi na hali hiyo ya kukatika kwa umeme mara kwa mara ni pamoja na Wilaya ya Temeke, Kigamboni, Ubungo na baadhi ya maeneo ya wilaya ya Kinodnoni.

“Nichukue fursa hii kuwaomba radhi wananchi, hususan wateja wetu, kutokana na hali hii ya kukatika kwa umeme, lakini napenda pia waelewe kuwa hali hiyo inatokana na kazi ambayo tumekuwa tukiifanya, na mara nyingi umeme tunakata siku za weekend, kwa vile shunguli nyingi za kiofisi zinakuwa zimepungua na hivyo inakuwa fursa nzuri kwetu kufanya kazi.” Alifafanua Mhandisi Mgaya.

Alisema, wananchi wanataka umeme, tena ulio bora na wa uhakika, ndio maana TANSCO imeamua kuchukua hatua madhubuti za kuboresha na kujenga vituo vipya vya kupoza na kusambaza umeme ikiwa ni pamoja na kujenga lini mpya za kusafirisha umeme.“Hatu hizi zote lazima ziwe na changamoto za hapa na pale, lakini kwa kiasi kikubwa TANESCO inaelekea kulitatua tatizo hilo la umeme jijini Dares Salaam na Mkuranga.”. Alisisitiza.

Wakandarasi na mafundi wa TANESCO wakiwa kazini Moja ya vituo ambavyo vimefungwa mitambo mipya ili kuboresha upatikanaji wa umeme jijini Dar es Salaam. Kituo cha kupoza na kusambaza umeme cha Kisutu.

MHE KINGU AWAOMBEA MAJI WAKAZI WA JIMBONI KWA LISSU

$
0
0

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Ikungi mara baada ya kupita Ofisi za Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu akielekea Manispaa ya Singida kwa ajili ya mapumziko, Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu (Kushoto) akimfatilia kwa makini Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe wakati wa kikao cha pamoja na watumishi wa Wilaya ya Ikungi, Mwingine ni Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Ikungi Ndg Elieza


Na Mathias Canal, Singida

Pamoja na Changamoto mbalimbali ambazo zinawakabili wananchi katika Jimbo la Singida Mashariki Wilayani Ikungi Mkoani Singida lakini uhaba wa upatikanaji wa huduma ya maji ni kikwaz kikubwa kwa wananchi kwani wanatumia umbali na muda mrefu kutafuta maji.

Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi Mhe Elibariki Kingu ametoa ombi hilo mbele ya Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe wakati akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Ikungi kwenye kikao kilichofanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu.

Mhe Kingu alisema kuwa Jimbo lake lina changamoto ya maji ambayo kwa kiasi kikubwa serikali inaendeleza juhudi za kuzitatua, huku akisema kuwa katika Jimbo jirani la Singida Mashariki linaloongozwa na Mhe Tundu Lissu hali ni mbaya zaidi katika upatikanaji wa miundombinu ya maji kwa wananchi wake.

Alisema kuwa hivi karibuni alipita katika jimbo hilo na kujionea adha inayowakumba wananchi jambo amablo lilimfanya kujipanga kuwaombea maji wananchi hao katika kipindi cha Bunge lijalo. Alisema kuwa wananchi hao wamebaki wakiwa utadhani hawana muwakilishi wa Jimbo kwa kipindi cha miaka 10 jambo ambalo linafanya kuteseka na huduma za utafutaji maji kwa kutumia muda mwingi na umbali mrefu.

Aidha, Mhe kingu alisema kuwa pamoja na changamoto ya upatikanaji wa maji Katika Jimbo la Singida Mashariki lakini pia jimbo hilo linakumbwa na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu ambayo ni pamoja na uhaba wa vyumba vya madarasa, Nyumba za walimu, Maabara, Matundu ya vyoo na mabweni.

Hata hivyo alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu kwa kuanzisha mkakati wa pamoja wa kuanzisha Mfuko wa Elimu Ikungi utakaowashirikisha wananchi pamoja na wadau wa elimu kuchukua hatua madhubuti ili kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto na hatimaye kuwafanya wanafunzi waweze kuongeza ufaulu.

Naibu waziri wa maji na Umwagiliaji Mhe Isack A. Kamwelwe ameanza ziara ya kikazi ya siku nne Mkoani Singida ambapo atatembelea na kukagua Miradi ya Maji na vyanzo vya uboreshaji upatikanaji wa maji.

WATANZANIA WAMETAKIWA KUENZI UTAMADUNI WETU KUKUZA FURSA ZA UTALII WA KIUTAMADUNI

$
0
0
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa pili kushoto) akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Ulinzi na Usalama mara baada ya kuwasili Wilayani Mbulu kwa ziara ya kikazi ya siku mbili wilayani humo.
Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga akimkaribisha Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura kuongea na wananchi waliokuwa katika tamasha la utamaduni katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom mara baada ya kuwasili Wilayani humo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili wilayani humo.
Baadhi ya Washiriki wa tamasha la utamaduni katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom, wilaya ya Mbullu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (hayupo pichani) alipotembelea kituo hicho.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akitoka ndani kujionea moja ya nyumba za asili ya Wabantu Wanyiramba na Wanyisanzu iliyopo Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura akicheza ngoma na washiriki wa tamasha la utamaduni alipotembelea Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa pili kulia) akipata maelezo ya utamaduni wa kabila la Wadatoga katika Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) kilichopo Haydom.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura (wa nne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wasichana wa kabila la Datoga na kusisitiza Watanzania kuenzi utamaduni wetu kwa kuurithisha kwa vijana wetu. Wa nne kushoto ni Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei Massay.(Picha na Eleuteri Mangi, WHUSM, Mbulu)



Na Eleuteri Mangi, WHUSM, Mbulu

Watanzania wametakiwa kuenzi mila na desturi ambazo ni chanya wazitunze na kuzitumia ili kujenga jamii yenye maadili mema nchini kwa manufaa ya kizazi cha sasa na baadaye.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Anastazia Wambura alipotembelea Kituo cha Pembe Nne za Utamaduni (4CCP) Haydom wilaya Mbulu mkoani Manyara ambapo amejionea utajiri wa kiutamaduni wenye fursa za utalii wa kiutamaduni.

“Nimetembelea nyumba za asili zilizopo hapa katika kituo hiki nimefurahishwa sana na utajiri wa kiutamaduni uliopo hapa, wazee walizingatia maadili katika kuwalea watoto wao kulingana na mila na desturi zao, ni vema tuenzi utamaduni wetu, huo ni msingi wa maadili mema ya jamii” alisema Naibu Waziri Wambura

Akitolea mfano wa maadili mema yanayopaswa kurithishwa aliyojionea katika kituo cha 4CCP na namna ambavyo watoto waliheshimu nyumba za wazazi wao, Naibu Waziri Wambura amesema kuwa kwa mujibu wa mila na desturi za Kitanzani suala la ulevi na utumiaji wa tumbaku kwa vijana ilikuwa ni mwiko hadi kijana afikie umri wa utu uzima ambapo anaweza kuwa na maamuzi sahihi katika maisha yake yenye kuwa na tija kwa familia.

“Kabla ya kuoa kijana alikuwa haruhusiwi kutumia tumbaku na kunywa pombe, bali kijana akioa na kuwa na watoto wawili kwa mujibu wa mila za makabila ya yaliyopo Mbulu aliruhusiwa kuingia katika kundi la watu wazima na kuruhusiwa kutumia vitu mbalimbali ikiwemo tumbaku na kinywaji cha pombe. Hapa kuna jambo la Watanzania kujifunza na kutunza ili kuondokana na mmomonyoko wa maadili” alisema Naibu Waziri Wambura.

Mila za jamii zilizo njema zinapaswa kutunzwa na kuendelezwa ili ziweze kusaidia vijana na jamii kwa ujumla kuweka mawazo yao katika shughuli za maendeleo pamoja na kupatia familia zao mahitaji ya kila siku.

Naibu Waziri Wambura alisisitiza kuwa mila hizo hazitakiwi kuachwa bali zainatakiwa kuenziwa, kutunzwa, kuendelezwa na kuhifadhiwa kwa manufaa ya sasa ziweze kuchangia katika kukuza utalii wa kiutamaduni ambao ni moja ya vyanzo vya mapato kwa wanajamii na taifa kwa ujumla.

Aidha, Naibu Waziri Wambura alisema kuwa wilaya ya Mbulu ni tajiri katika masuala ya utamaduni na kuongeza kuwa wilaya hiyo ni mdau muhimu katika sekta ya michezo na utamaduni ambazo zinapaswa kuendelezwa kwa manufaa ya taifa.

Kwa upande wake Mbunge wa Mbulu Vijijini Flatei Massay amesema kuwa wilaya hiyo imekuwa na utamaduni wa kufanya tamasha la utamaduni kila mwaka ambapo mwaka huu lilifanyika tarehe 21 hadi 23 mwezi Septemba na inaedelea kuimarisha umoja, mshikamano na ushirikiano miongoni mwa jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo hatua inayopelekea makabila yote kuwa mstari wa mbele katika kudumisha amani ya nchi.

Mbunge huyo aliyataja makabila yanayotokana na makundi makuu manne yanayopatikana wilaya ya Mbulu kuwa ni pamoja na Wairaqw ambao ni jamii ya Wakushi, Wahadzabe jamii ya Khoisan, Wanyiramba na Wanyisanzu jamii ya wabantu na Wadatooga jamii ya Kiniloti.

Naye Mkuu wa wilaya ya Mbulu Chelestino Mofuga amemhakikishia Naibu Waziri Wambura kuwa wilaya hiyo itaendelea kuenzi sekta ya utamaduni kwa kuwa na tamasha la utamaduni linalokutanisha makabila yote wilyani humo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uanuwai wa Utamaduni duniani ambayo hufanyika mwezi Mei tarehe 21 kila mwaka.

Hatua hiyo inatokana na Tanzania kusaini mkataba wa azimio la Umoja wa Mataifa (UN) kuenzi utamaduni na kuheshimu tamaduni za watu wengine chini unaosimamiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Mwaka 2002 Umoja wa Mataifa uliamua kuanzisha maadhimisho ya siku ya Utamaduni Duniani kutokana na kuongezeka kwa migogoro, mapigano na kupotea kwa maisha ya watu na mali zao iliyokuwa inatokea sehemu mbalimbali duniani mwishoni mwa miaka ya 1990.

MPANGO WA TAIFA WA DAMU SALAMA WAKABIDHI CHUPA ZA DAMU 300 HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI

$
0
0
 Mpango wa Taifa wa Damu salama kanda ya mashariki Dar es Salaam jana ulikabidhi chupa za Damu 300 kwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.  Akizungumza wakati wa makabidhiano Afisa uhusino Mpango wa Taifa wa Damu Salama Bw. Rajab Mwenda alisema chupa hizo za Damu zitasaidia kuokoa maisha ya wahitaji hospitali na zimepatikana kutokana na kampeni ya kukusanya Damu ambayo imeanza wiki hii ambapo mkoa wa Dar es Salaam mpaka jana ulikuwa umeisha kusanya zaidi ya  chupa za damu 500.  
 Bw. Rajab alitumia fursa ya makabidhiano kuwashukuru Jumuiya ya Khoja shia kwa mwitikio wao mkubwa wa kuchangia Damu kwa hiari siku ya Ashura 24/9/2017.  Siku ya Ashura ni siku ambayo Jumuiya ya Khoja shia kila mwaka huwa wanaadhimisha kifo cha Imam Hussein kwa kuchangia Damu. Pia alitoa wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kuchangia damu kama Ishara ya kuunga mkono jitihada za Mpango kuhamasisha jamii kuchangia Damu ili kupunguza vifoo vinavyoweza sababishwa na uhaba wa Damu
Mwakilishi wa Hospitali ya Muhimbili Bw. Hamisi Shabani Kubiga alishukuru Mpango wa Taifa wa Damu salama kwa kugawia Hospitali ya muhimbili kiasi hicho cha chupa za Damu, chupa hizo zitasaidia kutibu kina Mama na watoto wenye uhitaji wa Damu, Majeruhi wa ajali na magonjwa mengine alisema Bw. Hamisi

RC MAKONDA ATANGAZA NEEMA KWA WAMILIKI WA VIWANDA VIDOGO, DAR

INTRODUCING RAPSAM - TUGENDE (OFFICIA VIDEO)


MAKAMISHNA WA UPELELEZI WA KODI AFRIKA MASHARIKI WAKUTANA DAR

$
0
0
Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala akisalimiana na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala kabla ya kuanza kwa mkutano wa watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs) 
Washiriki wa mkutano huo wakianza kwa kumtanguliza Mungu kwanza. 
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa akisoma hotuba ya Kamishna Mkuu wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa makamshina na watendaji waandamizi wa Mamlaka za mapato za jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofanyika jijini Dar es Salaam leo. 
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (kushoto) akibadilishana mawazo na baadhi ya watendaji waandamizi wa mamlaka hiyo wakati wa mapumziko ya Mkutano wa Mamlaka za mapato za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa makamishna wapelelezi kwa maswala ya kodi uliofunguliwa jijini Dar es Salaam leo Septemba 27 2017. Kutokea (kushoto) ni Kaimu Naibu Kamishna wa Upelelezi wa Kodi, Salim Kessi, Kaimu Naibu Kamishna Upelelezi wa Kodi, Eustacio Makala na Meneja Elimu kwa mlipa kodi, Diana Masala. 
KAIMU Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Gerald Mwanilwa (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano huo. 
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo. 
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo.

WAFANYABIASHARA SOKO LA ILALA MCHIKICHINI JIJINI DAR ES SALAAM WAPEWA ELIMU YA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

$
0
0
Mwezeshaji wa kisheria kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG), Amina Mussa akitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia kwa wafanyabiashara wa Soko la Ilala Mchikichini Dar es Salaam leo. 
Mfanyabiashara Shikei Ngosi, akielezea changamoto zinazotokana na ukatili wa kijinsia katika soko hilo.
Mwezeshaji Khadija Mohamed akitoa elimu ya upingaji wa ukatili wa kijinsia.
Mfanyabiashara, Mussa Ibrahim, akichangia jambo.
Juma Mohamed akichangia jambo.
Mfanyabiashara wa nguo katika soko hilo, Godrey Milonge akielezea changamoto za ukati wa kijinsia katika soko hilo.
Mwezeshaji wa Sheria kutoka Soko la Temeke Stereo, Batuli Mkumbukwa akichangia jambo.
Mwezeshaji Sheria,wa Soko la Kigogo Kisambusa, Mariam Rashid akitoa mafunzo
Mwezeshaji wa Sheria katika Soko la Ilala Mchikichini, Consolata Cleophas akitoa elimu hiyo.
Mfanyabiashara, Johnson Stephano akisoma moja ya kijarida kinachoelezea ukatili huo.
Mafunzo yakiendelea.
Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Suzan Sitha, akiwaeleza jambo wafanyabiashara wa soko hilo kuhusu kukomesha ukatili wa jinsia.



Na Dotto Mwaibale

WAFANYABIASHARA katika Soko la Ilala Mchikichini wamepatiwa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa jinsia masokoni .

Katika hatua nyingine wafanyabiashara wanaume wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia na wanawake wametakiwa kwenda kushitaki ofisi za masoko husika ili sheria ichukue mkondo wake kwa wahusika waweze kujirekebisha.

Mwito huo umetolewa na Mwezeshaji wa Sheria masokoni, Khadija Mohamed kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG) wakati wanasheria wa shirika hilo wakitoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wafanyabiashara wa Soko la Ilala Mchikichini Dar es Salaam leo hii.

"Wakina baba mnapofanyiwa vitendo vya kijinsia na wanawake katika masoko msione haya nendeni kushitaki kwa viongozi wa masoko ili watuhumiwa waweze kukamatwa na kujirekebisha" alisema Mohamed.

Mohamed alisema vitendo vya ukatili wa jinsia hawafanyiwi wanawake pekee bali hata wanaume wamekuwa wakifanyiwa lakini wanaona aibu kwenda kushitaki.Mwezeshaji wa Sheria Batuli Mkumbukwa alisema vitendo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo vimeshamiri hivyo alitoa mwito kwa wafanyabiashara wa soko hilo kuviacha. 

Mkumbukwa alisema ili kumaliza vitendo hivyo kwa makosa madogo madogo kama kutoa lugha ya matusi, kumshika mtu maunoni bila ya ridhaa yake mtuhumiwa amekuwa akipewa adhabu pamoja na kupigwa faini lakini kwa kosa la ubakaji adhabu yake ni kifungo cha maisha au miaka 30.

Mariam Rashid, ambaye ni mwezeshaji wa kisheria kutoka EfG alitaja ukatili wa kijinsia unaofanyika katika masoko ni ukatili wa kingono, uchumi, kisaikolojia na kimwili.Baadhi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo vinafanyika katika soko hilo ni pamoja na wafanyabiashara kuwashika sehemu za siri wateja wao wa kike maarufu kama kunawa, kukojoa kwenye chupa za maji na kwenda kuziweka kwenye meza za 

wafanyabiashara, lugha za matusi, kujambisha na kutolipa fedha baada ya kuuziwa chakula na mama lishe.Wafanyabiashara katika soko hilo walisema kuwa kukithiri kwa vitendo hivyo vya ukatili wa kijinsia katika soko hilo kwa namna moja au nyingine vinachangiwa na wanawake wenyewe kutokana na tamaa zao kwa kuvaa nguo fupi na kujilengesha kwa wanaume ili wapate bure bidhaa wanazozitaka.

"Wanawake wanabakwa na kushikwa maungoni kwa kupenda wenyewe wala hawalazimishwi" alisema Juma Mohamed mfanyabiashara.

Ofisa Mradi wa Mpe Riziki si Matusi kutoka EfG, Susan Sitta alisema lengo la kutoa mafunzo hayo ni kuwaongezea uelewa wafanyabiashara ili waweze kuacha kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia katika masoko ili kutoa fursa kwao kufanya biashara zao bila ya kuwa na bugudha.

Alisema mradi huo umefadhiliwa na Shirika la United Nations Trust Fund na kuwa unafanyika katika masoko ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na Temeke.

WATEJA WA CBA BENKI WAENDELEA KUNUFAIKA NA PROMOSHENI YA"WEKA AMANA USHINDE"

$
0
0
  Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani, akizungumza na waandishi wa habari, wakati wa kuchezeshwa droo ya tatu ya ya promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zinaendelea kushindaniwa na wateja wa benki hiyo, Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi na kushoto ni Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo.
 Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani, akibonyeza kitufe cha kompyuta kwa ajili ya kuchezesha droo ya kuwapata washindi wa promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zinaendelea kushindaniwa na wateja wa benki hiyo , Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi na kushoto ni Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo.
 Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo, akimuonesha Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani (katikati) na Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi, mshindi wa droo ya tatu ya ya promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zitashindaniwa na wateja wa benki hiyo, mara baada ya kuchezeshwa, Dar es Salaam jana.
Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki wa Benki ya CBA kwa wateja binafsi, Julius Konyani, akizungumza na mmoja wa washindi aliyejishindia kitita cha shilingi Milioni 2/- kwenye droo ya tatu ya ya promosheni ya akiba inayojulikana kama ‘Weka amana ushinde’ zaidi ya milioni 20 zinashindaniwa na wateja wa benki hiyo, Dar es Salaam jana. Kulia ni Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Abdallah Hemedi na kushoto ni Mkuu wa Mauzo na Mahusiano ya Kibenki wa CBA, Godson Biyengo.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO AL HAMISI SEPTEMBA 28,2017

Tigo yaleta mageuzi ya elimu Mkoani Tabora Yatoa msaada wa mfumo wa elimu kwa njia ya mtandao kwa shule mbili za sekondari Tabora

$
0
0

Meneja wa Tigo kanda ya ziwa kusini, Gwamaka Mwakilembe akizungumza na waandishi wa habari na wanafunzi wa shule ya wasichana Tabora kabla ya makabidhiano ya huduma ya intaneti ya Tigo kwenye shule hiyo



Mwalimu mkuu wa shule ya wasichana ya Tabora, Lydia Mwampamba akizungumza na waandishi wa habari na wanafunzi wa shule ya wasichana Tabora kabla ya makabidhiano ya huduma ya intaneti ya Tigo kwenye shule hiyo




Kaimu Katibu Tawala mkoa Tabora, Nathalis Linuma akizungumza na waandishi wa habari na wanafunzi wa shule ya wasichana Tabora kabla ya makabidhiano ya huduma ya intaneti ya Tigo kwenye shule hiyo


Kaimu Katibu Tawala mkoa Tabora, Nathalis Linuma akikata utepe kuzindua huduma ya Tigo eSchool shule ya sekondari wasichana Tabora. Kulia mkuu wa shule, Lydia Mwampamba , kushoto Afisa elimu mkoa, Suzana Nyarubamba na nyuma Meneja wa Tigo kanda ya ziwa kusini, Gwamaka Mwakilembe    


Mtaalam wa mtandao toka Shule, Direct Rajabu Mgeni akitoa maelezo kwa mgeni rasmi namna ya kutumia huduma ya Tigo eSchool.

 Picha




Kaimu Katibu Tawala mkoa Tabora Nathalis Linuma akipata maelezo toka kwa wanafunzi wa shule ya sekondari wasichana Tabora jinsi ya kutumia huduma ya Tigo eSchool kwenye komputa, Pembeni mwenye fulana ya bluu ni Meneja wa Tigo kanda ya ziwa kusini, Gwamaka Mwakilembe.

Mgeni Rasmi kaimu Katibu Tawala mkoa wa Tabora Nathalis Linuma akiwa kwenye picha ya pamoja na walimu, wanafunzi na uongozi wa Tigo mara baada ya uzinduzi


Viewing all 46396 articles
Browse latest View live




Latest Images