Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

WAKULIMA WILAYANI HAI WASIFU MRADI WA N2AFRICA KWA MBEGU BORA ZA MAZAO YA MAHARAGE

$
0
0
Na Mathias Canal, Kilimanjaro

Wakulima wadogo katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro wameipongeza Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) yenye makao makuu yake nchini Nigeria kwa teknolojia walizoanzisha za kutafiti wadudu waharibifu na aina mpya ya mbegu za maharagwe aina ya Jesca, Lyamungo 90 na Uyole njano wanazozitoa kwa wakulima.

Wakulima hao wamesema kuwa mbegu hizo zimepelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya mbogamboga jamii ya mikunde huku katika Wilaya hiyo uzalishaji wa maharagwe ukiwa ndio ukombozi kwa wakulima kufuatia mafunzo na mbinu bora za kisasa wanazopatiwa na wataalamu wa (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA.

Wakizungumza kwa niaba ya wakulima wengine 30 katika Wilaya ya Hai Wanufaika wa mradi wa N2AFRICA Hashim Abdallah mkazi wa kitongoji cha Landi na Lucy David mkazi wa Kitongoji cha Madukani Kata ya weruweru wanasema kabla ya mradi huo walikuwa wanapanda kilo 60 za mbegu katika heka moja na mavuno ya gunia 3 mpaka 5 ambapo hivi sasa matarajio ya mavuno yao yataongezeka maradufu kwani wanatumia kilo 30 za mbegu kwenye heka moja na kuvuna gunia 10 mpaka 15.

Wakulima hao wameomba mafunzo ya kutengeneza mbegu bora za kilimo cha mbogamboga na mafunzo ya jinsi ya kuhifadhi mbegu hizo ili waweze kuendeleza uzalishaji wao wenyewe badala ya kuomba tena mbegu kutoka katika mradi huo wa N2AFRICA.

Pia wameiomba Taasisi ya (IITA) kupitia mradi wake wa N2AFRICA unaojihusisha na usambazaji wa teknolojia ya mazao jamii ya mikunde kuwasaidia kutafuta masoko ili kuboresha zaidi ufanisi wa mauzo yao mara baada ya mavuno. 

Wakulima hao walisema kuwa Wakulima wadogo nchini Tanzania huzalisha asimia 70 ya chakula ingawa karibu nusu yao hawazalishi chakula cha kutosha kwa ajili ya mauzo. 

Aidha, walisema Wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu wa teknolojia ya kilimo cha kisasa, kukosa uwezo wa kujipatia pembejeo bora na kukosa huduma za kiufundi za ughani zinazoweza kuwasidia kukuza kilimo pamoja na ukosefu wa mafunzo jambo ambalo kwa sasa wameanza kunufaika nalo kupitia mradi wa N2AFRICA.

Kwa upande wake Afisa Kilimo (Mazao) Halmashauri ya Wilaya ya Hai Bi Matrida R. Massawe alisema kuwa upatikanaji mbegu bora za maharagwe zilizotolewa na mradi wa N2AFRICA zimekuwa na tija kubwa kwa wakulima kwani mavuno yameongezeka kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na msimu wa mavuno uliopita.

Alisema kuwa Mradi huo umetatua changamoto ya uduni wa kilimo kwa wakulima kwani walikuwa wakilima pasina kufuata mbinu bora za kilimo hivyo upatikanaji huo wa mbegu bora na mbinu za uongezaji rutuba kwenye udongo umekuwa mkombozi kwa wakulima kwani wanazalisha na kuuza mazao yao kwa faida kubwa.

Massawe aliwahimiza wakulima kuendelea kujifunza kanuni bora za kilimo na kuzingatia ushauri wa kitaalamu unaotolewa na mradi wa N2AFRICA katika uzalishaji wa mazao kwani kilimo kisichozingatia utaalamu na kanuni bora za kilimo hakiwezi kuwa na tija katika jamii.

Hata hivyo Mwaka 2017 katika msimu wa kilimo mafunzo yameendelea kutolewa na Mradi wa N2AFRICA kwa wakulima wa maharagwe ambapo wakulima 30 wamepata mafunzo ya mbegu daraja la kuazimiwa. 

Aliwasihi wakulima kutumia fursa hiyo kupitia mradi wa N2AFRICA ili kuweza kuboresha kilimo cha maharagwe ambapo pia amewapongeza wadau hao wa kilimo wa N2AFRICA na kuwaomba kuendeleza kilimo hicho katika maeneo yote ya Wilaya ya Hai ili kunufaisha wakulima wengi zaidi.

Mradi wa N2AFRICA unaendeshwa na na Taasisi ya Kimataifa ya kilimo cha Kitropiki katika ukanda wa joto makao makuu yake ni nchini Nigeria chini ya ufadhili wa Bill na Melinda Gates na kuongozwa na Chuo Kikuu cha Wagenigen cha Uholanzi.

Lucy David akielezea jinsi alivyonufaika Mbegu za maharagwe zilizotolewa na Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA

Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah akiwa shambani kuendelea na shughuli zake za kusafisha majani katika shamba lake kabla ya mavuno.

Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) wakikagua shamba la Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah.

Muonekano wa mazao ya maharagwe yakiwa shambani kabla ya mavuno

Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) walipotembelea ofisi ya Afisa Kilimo, Umwagiliaji na ushiriki wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Ndg David Lekei

Afisa kilimo (Mazao) wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Bi Matilda Massawe akielezea jinsi wakulima walivyonufaika na mradi wa N2AFRICA katika Wilaya ya Hiyo.

Muonekano wa shamba la maharagwe lililolimwa kwa kufuata mbinu bora na za kisasa za kilimo


Muonekano wa shamba la maharagwe lililolimwa bila kufuata mbinu bora za kilimo

Hashim Abdallah akielezea jinsi alivyonufaika Mbegu za maharagwe zilizotolewa na Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA

Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) wakikagua shamba la Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah.
Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mwantumu Abdillah akiwa shambani kuendelea na shughuli zake za kusafisha majani katika shamba kabla ya mavuno.
Mkulima wa zao la maharagwe Lucy David Katika Kitongoji cha Madukani, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro akielezea mafanikio aliyoyapata kutokana na Mradi wa N2AFRICA, Wengine ni Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) walipomtembelea shambani kwake.

Kampuni ya matangazo ya Kwanza yatangaza neema kwa watangazaji na wachapishaji

$
0
0
 Meneja Bidhaa  wa Kwanza Advertising Network, Leon John akieleza namna ya jukwaa hilo litakavyofanya kazi ambapo mtandao huo utaunganisha kampuni za uzalishaji, wachapishaji mtandaoni
Baadhi ya wachapishaji (Blogers) wakifuailia kwa makini uzinduzi huo katika hafla iliyofanyika mapema leo katika Hoteli ya Hyatt
Meneja wa Masoko ya Digitali kutoka kampuni TECNO ambayo ni miongoni mwa kampuni zilizomo kwenye jukwaa hilo, Bw. Kelvin Boniface(wa kwanza kushoto) akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali wakati wa mkutano huo.
Mkurugenzi mtendaji wa KONCEPT na katibu wa Tanzania Blogers Network  Bw. Krantz Mwantepele (wa kwanza kulia) akichangia jambo kuhusu uelewa wake juu ya watumiaji wa mitandao ya kijamii hasa upande wa Blog.Meneja bidhaa kutoka Kwanza Advertising Network, Leon John (wa kati kati)


Meneja Mawasiliano wa  Kwanza Advertising Network, Herman Mkamba akieleza vigezo vitakavyotumika kuchagua mitandao na Blog zitakazo jiunga kwenye jukwaa hili.
Afisa Mtendaji mkuu wa Kwanza Edwin Bruno (mwenye suti katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wageni waaalikwa katika hafla ya uzinduzi wa Kwanza Advertising Network mapema leo katika Hoteli ya Hyatt Regency.
 Meneja Bidhaa  wa Kwanza Advertising Network, Leon John akifanya mahojiano na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa Kwanza Advertising Network.

Dar Es Salaam Septemba 18, 2017: Kampuni ya matangazo ya Kwanza Advertising Network, leo imezindua huduma mpya, itakayowezesha biashara mbali mbali na watangazaji kuwafikia mamilioni ya wateja kupitia simu za mkononi, tovuti na mtandao wa intaneti
Akiongea wakati wa hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Hotel jijini Dar Es Salaam, Afisa mtendaji mkuu wa Kwanza Advertising Network Edwin Bruno alisema, huduma hiyo itakuwa na uwazi wa hali ya juu kwa kuwa itamwezesha mtangazaji kuona namna ambavyo tangazo la biashara yake linavyosoma na hivyo kujua ni watu wangapi wameliona na kulisoma
“Kwanza imewezesha blogers wa Tanzania wakati pia ikitumia tovuti zenye kutembelewa na watu wengi kuongeza thamani kwa watangazaji kulingana na wateja wao,” alisema Bruno na kuongeza kuwa Kwanza ni mtandao wa kipekee unao mhakikishia mtangazaji faida kwa kila tangazo analoliweka kwenye mtandao huo.
Bruno alifafanua kuwa, lengo la Kwanza ni kuhakikisha kuwa wateja wake (watangazaji) wanatumia kikamilifu fursa zilizopo katika ulimwengu wa kidijitali kutangaza biashara zao kupitia njia za kisasa za utangazaji ambazo ni pamoja na matumizi ya mtandao.
Zaidi alifafanua kuwa, Kwanza inatumia nyenzo za kisasa ambazo humpa taarifa mteja juu ya watu walioliona au kulisoma tangazo lake na pia kumwonyesha tovuti ambazo tangazo lake limesomwa kwa wingi zaidi.
Alieleza kuwa, Kwanza imegundua namna ambavyo inaweza kuwasaidia watangazaji na wachapishaji kutengeneza fedha kwa njia ya mtandao.


Kwanza inatoa nafasi kufikia wateja wengi kwa watangazaji na pia kipato kikubwa kwa wachapishaji .Watangazaji kila mara hutafuta namna ya kuwafikia wateja wao kwa kiwango kikubwa na hii ni nafasi kubwa kwa wachapishaji wa Tanzania kutumia fursa hii kwa makini kutengeneza kipato zaidi.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 20, 2017

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ATEMBELEA KWANDA CHA VIGAE CHA TWYFORD CHA CHALINZI MKOANI PWANI

$
0
0
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na viongozi wa serikqli na Chama Tawala CCM baada ya kutembelea kiwanda cha vigae cha TWYFORD kilichopo Chalinze mkoani Pwani Septemba 19, 2017. Kushoto ni Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua ufungaji mitambo ya kiwanda cha vigae cha TWYFORD kilichopo Chalinze mkoani Pwani Septemba 19, 2017. Kulia kwake ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarest Ndikilo na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho, Bw. Jack Fen.picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

MWAKILISHI KUTOKA BENKI YA DUNIA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MABORESHO WA HUDUMA ZA KIMAHAKAMA

$
0
0
Na Mary Gwera, Mahakama

Mwakilishi ‘Practice Manager’ kutoka Benki ya Dunia (WB), Bw. George Larbi ameisifu Mahakama kwa utekelezaji wake wa Mradi wa Maboresho wa huduma za Kimahakama.

Bw. Larbi aliyasema hayo mapema Septemba 19, alipokutana na Mhe. Jaji Mkuu ofisini kwake Mahakama ya Rufani-Dar es Salaam ambapo alipata nafasi ya kuongea na Mhe. Jaji Mkuu na Viongozi wengine wa Mahakama akiwemo Mtendaji Mkuu na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

“Mradi huu unaotekelezwa na Mahakama ni mradi wa mfano ambapo mafanikio yake yanatarajiwa kuigwa nan chi nyingine,” alisema Bw. Larli.

Bw. Larli ambaye amewasili nchini kutokea Washington D.C zilipo ofisi cha Benki ya Dunia amefanya ziara yake kwa lengo la kuangalia maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ambao unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Mahakama ya Tanzania na Benki ya Dunia (WB).

Alisema Mradi huu unaotekelezwa na Mahakama ni Mradi wa pili kwa nchi za Afrika ambapo Benki ya Dunia inashirikiana moja kwa moja na Mahakama katika kuboresha huduma ya utoaji haki.

Maeneo muhimu yanaotekelezwa na Mradi wa Benki ya Dunia (WB) ni pamoja na; Mapambano dhidi ya Rushwa; ni kwa jinsi gani Mahakama pamoja na wadau wengine wanaweza kushirikiana katika kupiga vita vitendo vya rushwa.Maeneo mengine ni ushirikishaji wa wadau katika masuala yote ya utoaji haki na kusogeza huduma ya utoaji haki karibu na wananchi.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibarhim Hamis Juma (kulia) akiongea neno na Bw. George Larbi kutoka Benki ya Dunia (katikati) wa kwanza kushoto ni Bw. Denis Biseko 'Co-Team Task Leadear' wa Mradi wa Maboresho ya Huduma za Kimahakama.
 Bw. George Larbi, kutoka Benki ya Dunia (WB) (katikati) akiongea na Mhe. Jaji Mkuu (kulia).
 Mhe. Jaji Mkuu (aliyeketi wa kwanza kulia) akiwa pamoja na Wageni kutoka Benki ya Dunia (wawili walioketi katikati) wa tatu kutoka kushoto ni Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga, wa pili kushoto ni Msajili Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mradi wa Maboresho wa Huduma za Mahakama, Mhe. Zahra Maruma.
 Ukaguzi: Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Mahakama cha Mahakama-Kisutu unaojengwa kwa fedha za Benki ya Dunia Bw. George Larbi kutoka Benki ya Dunia pia alipata fursa ya kutembelea Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Mafunzo cha Mahakama unaofanyika katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa sasa kazi ya upakaji rangi katika jengo hilo inaendelea.
 Mafundi wakiendelea na kazi ya upakaji rangi katika jengo la Kituo cha Mafunzo linalojengwa Kisutu-Dar es Salaam (Picha na Mary Gwera, Mahakama)

MILIONI MIA MOJA NA TISINI (190,000,000) ZATUMIKA KUTIBU UGONJWA WA KIPINDUPINDU HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA

$
0
0
Afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya akizungumza na viongozi wa vijiji wa tarafa ya pawaga kuhusu uboreshaji wa vyoo bora kwa lengo la kutatua tatizo la ugonjwa wa kipindupindu ambalo limekuwa likijitokeza mara kwa mara katika tarafa hiyo walianza kutoa elimu kwa viongozi wote na baadae wakahamia kwa wananchi.
Afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya akizungumza na mama moja ambaye hana choo bora na kutundikiwa bendera ilikuwa inamuonyesha kuwa hana choo bora katika kijiji cha mboliboli tarafa ya pawaga mkoani Iringa.
Afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya akisimamia zoezi la utundikaji wa bendera kwa wasio na vyoo bora


Na Fredy Mgunda,Iringa.

Halmashauri ya wilaya ya Iringa imetumia shilingi milioni mia moja na tisini (190,000,000 ) kupambana na tatizo la milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu katika tarafa ya pawaga na Idodi mkoani Iringa na ni miongoni mwa halmashauri 156 zinazotekeleza kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira Tanzania bara.

Akizungumza wakati wa utoaji elimu ya matumizi ya vyoo bora katika tarafa ya pawaga afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya aliwataka wananchi kuanza kutumia vyoo bora ili kumaliza tatizo la milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu ambao umekuwa ukiwakumba mara kwa mara.

“Jamani chanzo mmoja wapo cha mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ni matumizi ya vyoo ambavyo sio bora hivyo mnatakiwa kutumia vyoo bora na kutoa elimu kwa wananchi wenu maana nyinyi ndi wenye wananchi na leo tunawapa hii elimu nyie viongozi tunaomba muifikishe elimu kwa wananchi”alisema Nkya

Nkya alisema walitoa elimu ya uboreshaji wa miundombinu ya vyoo na kunawa mikono kwa kutumia maji tiririka kwa sabuni mara ya kutoka chooni kwa ngazi ya kaya na shule za msingi na sekondari,Vyuo,taasisi za kidini,taasisi binafsi,taasisi za kiserikali kama ofisi za serikali na vituo vya afya lengo likiwa ni kutokomeza kabisa ugonjwa wa kipindupindu.

“Ukiangalia hadi sana tumefanikiwa kuzifikia jumla ya kaya 24 zilizotekeleza kampeni hiikupitia wadau mbalimbali kama wizara ya afya,wizara ya maji,wizara ya elimu (RWSSP),halmashauri ya wilaya ya Iringa,UNICEFU,SNV na WARID na jumla ya kata nne ambazo ni ilolompya,Mlenge,Mboliboli na Itunundu zimeanza kutekeleza rasmi kampeni hii kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018” alisema Nkya

Mwezi wa pili hadi mwezi wan ne mwaka 2016 ndio kulitokea mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika halmashauri ya wilaya ya Iringa ambapo kata za Mboliboli na Mlenge zilikumbwa na ugonjwa huo huku vijiji vya Luganga,Mnadani,Idodi na Mafuruto vilikuwa na idadi ndogo ya wagonjwa wa kipindupindu.

Aidha Nkya alisema kuwa mikakati ya halmashauri ya wilaya ya Iringa kuzitambua kaya na taasisi zisizo na vyoo bora,kutambua vibarua na wamiliki wa mshamba ya mpunga,kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa usafi wa mazingira vijijini na kutoa elimu ya usafi wa mazingira kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa kipindupindu kisitokee tena katika halmashauri hiyo.

“Tumepeana maagizo ya kutekeleza kama kuwawekea bendera nyekundu kaya na taasisi zote ambazo hazina vyoo bora,kutoa muda maalumu wa kuboresha vyoo vyao vinginevyo kuna faini ambayo itatolewa kwa kaya na taasisi ambazo zitakuwa hazijaboresha vyoo vyao” alisema Nkya

Nyamiki Kimsau ni mwananchi wa kijiji cha Usolanga pawaga alisema kuwa kuwa ugonjwa kipindupindu umekuwa sugu katika kijiji hicho kutokana na wananchi wemgi kutokuwa na vyoo bora ambavyo vinakidhi kuishi na afya bora.

“Wananchi tukiwa tunafanya usafi na kuwa na vyoo bora basi tunaweza kuepukana na milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu hivyo naomba serikali kuwa wakali kwenye swala la kuwa na vyoo bora ili kuondokana na aibu ambayo imekuwa inatutafuna kwa muda sasa” alisema Kimsau

Naye Mwaita Bin jumbe alisema kuwa kweli wananchi wa kijiji cha mboliboli hawana vyoo bora kutokana na ugumu wa maisha hivyo wanaomba kupewa muda ili waweze kuboresha vyoo bora lakini swala la ugonjwa wa kipindupindu bado unawakumba kila mara.

“Jamani tunaomba viongozi mtoe elimu ya kutosha kwa wananchi ili wajue umuhimu wa kuwa na vyoo bora tofauti na hali iliyopo hivi sasa” alisema Bin jumbe

Hamis Matyame ni kijana wa kijiji cha mboliboli aliita serikali ya kijiji kutafuta njia mbadala ya kuwachimbia vyoo bora wazee ambao hawana uwezo wa kifedha na guvu kazi kwa sababu wasipo saidiwa ugonjwa wa kipindupindu hauta koma katika tarafa ya pawaga.

“Mimi kama kijana napenda kuwasaidia wazee kuboresha vyoo ila hapa kijijini kuna wazee wengi hivyo pekee yangu siwezi hivyo naiomba serikali kutafuta njia mbadala kuwasaidia hawa wazee” alisema Matyame

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI AELEKEA MKOANI ARUSHA KWA AJILI YA ZIARA YA KIKAZI

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 20 Septemba, 2017 ameondoka jijini Dar Es salaam kuelekea mkoani Arusha kwa ziara ya kikazi.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro KIA,Rais Dkt. Magufuli ataanza ziara yake Mkoani Manyara kwa kufungua barabara ya Kia - Mererani yenye urefu wa kilomita 26, na kuzungumza na wananchi wa mkoa huo.

Tarehe 23 Septemba 2017, Rais Dkt. Magufuli atatunuku Kamisheni kwa Maafisa wanafunzi wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar Es salaam , Rais Dkt. Magufuli ameagwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mhe. Paul Makonda.

Jaffar Haniu
Naibu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar Es Slaam.
20 Septemba 2017. 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akielekea kupanda ndege kwenda mkoani Arusha kwa ajili ya ziara ya kikazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati akielekea kupanda ndege kwenda mkoani Arusha kwa ajili ya ziara ya Kikazi. PICHA NA IKULU
 

TAARIFA YA KIFO CHA ASKARI WA JWTZ


JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI NCHINI LATOA TAMKO

WALIMU WA SAYANSI LINDI WAIOMBA SERIKALI KUWASAIDIA

$
0
0

Walimu wa masomo ya Sayansi mkoani Lindi wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka za kuandaa na kuimarisha miundombinu bora kwa shule za Sekondari zinazofundisha masomo hayo ili kuendeleza na kufufua vipaji vya wanafunzi.

Akizungumza kwa niaba ya walimu hao wakati wa ziara iliyofanywa na wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara katika shule za mkoa huo,   Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mchinga iliyopo  mkoani humo, Bw. Makopa Selemani , amesisitiza kwa Serikali kuona namna ya kujenga maabara  nyingi za sayansi ambazo zitakuwa na vifaa na kuongeza walimu wa Sayansi ambao wameonekana kuwa ni wachache katika mkoa huo.

"Tunaiomba Serikali kutazama kwa jicho la pekee shule za mkoa huu hususan zenye michepuo ya sayansi kwani si kwamba wanafunzi hawapendi masomo haya bali miundombinu hairidhishi", amesema Mwalimu Mkuu.
Aidha, Mwalimu Mkuu ameongeza kuwa ili kuwasaidia wanafunzi wa kike katika mkoa huo serikali iwajengee mabweni wanafunzi hao ili kuepusha kupata vishawishi kwani wengi wao wanaishi mbali na shule.

Mwalimu Mkuu Selemani, ameelezea baadhi ya mikakati ya shule yake katika kuhamasisha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi ikiwemo kufanya vikao vya mara kwa mara na wanafunzi hao ili kujadili changamoto zao na kuzitatua.

Ametoa wito kwa Wizara kufanya ziara za mara kwa mara katika shule mbalimbali nchini ili kuhamasisha wanafunzi husasan wa kike kupenda na kujifunza masomo ya sayansi ambayo yameonekana kuwa ni vikwazo katika mkoa huo.

Kwa upande wake, Mhandisi  kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi Liberatha  Alphonce,  amewasisitiza wanafunzi  wa kike mkoani humo kuanza kujituma na kujijengea misingi imara ya kupenda masomo ya sayansi wakiwa katika ngazi za awali ili kufikia malengo yao.

Amefafanua kuwa masomo ya Sayansi yanatoa fursa za kujiajiri na urahisi wa kupata mikopo kwa wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na elimu ya juu.Naye, mwanafunzi Shamira Salum, kutoka shule ya Sekondari ya Mchinga, ameiomba serikali kuongeza walimu na vifaa katika shule za mkoa huo ili kuweza kutimiza malengo yao ya kuwa wahandisi na madaktari wa baadae.
Ziara ya wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara imelenga kutoa elimu na kuhamasisha wanafunzi wa kike nchini kusoma masomo ya sayansi ambapo pamoja na mambo mengine wahandisi hao wametembelea shule ya sekondari ya Mchinga, Lindi, Mkonge na Mingoyo ambazo zipo mkoani Lindi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
 Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha Alphonce, akionesha mfano wa picha iliyochorwa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi (hawapo pichani), ili kuhamasisha wanafunzi kupenda masomo ya sayansi.
 Wahandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, wakisikiliza maoni kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi walipotembelea shule hiyo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
 Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi, wakionesha ndoto zao kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, walipotembelea shule hiyo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
 Mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Lindi, akitoa maoni yake kuhusu changamoto  zinazokabili shule  yao kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi, wakimsikiliza Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha Alphonce (hayupo pichani) wakati akitoa mada kuhusu uhamasishaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.

Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Rahma Mwinyi, akigawa zawadi ya madaftri kwa wanafunzi wa shule ya Mkonge mkoani Lindi ili  kuhamasisha wanafunzi  hao kupenda masomo ya sayansi.
 Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya walimu pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi.

WAZIRI KAIRUKI AELEKEZA MTUMISHI ALIYEHAKIKIWA KWA CHETI TOFAUTI NA MAJINA ANAYOLIPWA MSHAHARA KUONDOLEWA KWENYE PAYROLL

$
0
0

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akitoa maelekezo wakati wa ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuangalia namna zoezi la uhakiki wa vyeti vya watumishi wa umma lilivyofanyika.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) akipokea taarifa ya utendaji kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alipofanya ziara ya kikazi katika mkoa wa Pwani kwa lengo la kuangalia namna zoezi la uhakiki wa vyeti vya watumishi wa umma lilivyofanyika.
 Baadhi ya watendaji wa Sekretarieti ya Mkoa wa Pwani wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb) alipofanya ziara ya kikazi katika Mkoa wa Pwani kwa lengo la kuangalia namna zoezi la uhakiki wa vyeti vya watumishi wa umma lilivyofanyika.



HATIMAYE MGOGORO KATI YA WALIOKUWA WAFANYAKAZI YA KAMPUNI YA CEYTUN NA WAMIKILI WAKE UMEMALIZIKA NA WAMELIPWA MADAI YAO.

$
0
0
Na Tiganya Vincent
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amefanikiwa kumaliza mgogoro kati ya waliokuwa wafanyakazi 11 wa Kampuni ya Ujenzi ya Ceytun iliyokuwa ikipanua Uwanja wa Ndege wa Tabora na wamiliki wake juu ya kulipwa madai ya malipo ya muda wa ziada na mapunjo ya mishahara.
Mgogoro huo ulimalizika jana mjini Tabora baada ya Wamiliki wa Kampuni hiyo kukubali na kulipa madeni ya wafanyakazi wake ambapo  malipo yalifanyika mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Wilaya ya Tabora.
Hatua hiyo ilifikiwa baada ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kuamuru kuwang’anywa Hati za kusafiria za viongozi wake wawili wa Kampuni hiyo na kuzuiwa kwa vifaa vyake vya  ujenzi baada ya kuonekana kuwa anataka kuondoka bila kulipa malipo ya wafanyakazi hao.

Akizungumza mara baada ya Kampuni hiyo kuwalipa waliokuwa  wafanyakazi wake Mwanri alisema kuwa amelizika na kazi iliyofanyika na hivi sasa wanaweza kuchukua hati zao za kusafiria na wako huru kuondoa vifaa vyao vya ujenzi kwa sababu wamemalizana na watumishi hao bila kinyongo.

Aliomba Kampuni hiyo ikipata kazi nyingine isisite kuwapa ajira waliokuwa wafanyakazi wake licha ya mvutano uliotokea na kuongeza kuwa kilichotekea ndio mwanzo wa kuboresha mahusiano katika siku za baadaye.
Mwanri alisema kuwa uungwana waliouonyesha kukabali kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao na waliokuwa wafanyakazi wao umeonyesha ni Kampuni inayostahili kuendelea kupewa kazi nyingine hapa nchini.
Aliwataka kutofunga milango kwani inawezekana wapo waliokuwa wafanyakazi wao ambao walisahaulika na wameshaondoka na pindi watakapokuja na vielelezo vinavyoonyesha kuwa bado wanadai basi wasaidiwe na walipwe haki zao.

Kwa upande Meneja Mradi wa Kampuni ya Ujenzi ya Ceytun  Ercan Kavaic alisema kuwa hana kinyongo na mfanyakazi yoyote yule na yko tayari kufanyakazi na mtu yoyote akipata kazi nyingine.
Alisema kuwa Kampuni yake ilikuwa ikihakikisha kila mtumishi anapofikia ukomo wa mkataba wake inamwongeza mshahara wa mwezi mmoja zaidi ya ule uliopo katika mkataba na kumpa cheti cha kutambua mchango wake katika kushiriki Kampuni yake.

Kavaic alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa kufanikisha kumalizika kwa tofauti baina ya Kampuni yake na waliokuwa wafanyakazi wake na kuweza kufika muafaka wa kulipa fedha nusu ya zile ambazo walikuwa wamesama za shilingi milioni 20 baada ya uchambuzi walikuta madi ni milioni 10.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi wenzake ambaye ni fundi umeme John Mathew alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Wilaya ya Tabora kwa kusimamia hadi haki yao imepatikana na kuonyesha moyo wao wa uzalendo wa kushughulikia matatizo ya wananchi hata ikibidi kwa nguvu kubwa.

Pia alimshukuru Meneja Mradi wa Kampuni ya Ujenzi ya Ceytun Bw. Kavaic kwa kubali kukaa meza moja ambayo ndio iliyolea makubaliano na wao kuweza kupata haki yao na wao walisema wako tayari kufanyakazi naye endapo atapewa jukumu jingine la upanuzi wa uwanja wa ndege kama alivyoelekeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wawekezaji wazungumzia ushindani unavyoathiri bidhaa za ndani

$
0
0
 Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Dairies Limited mkoani Iringa, Bwana Fuad Abri akitoa mada juu ya uendeshaji wa kiwanda chake na ubia wao na Kituo cha Kuendeleza kilimo Nyanda za juu kusini mwa Tanzania (SAGCOT) alipotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo,Mifugo , Maji na Umwagiliaji. Lengo la ziara ya Kamati hiyo ni kujionea na kujifunza juu ya Kongani ya Ihemi na shughuli za SAGCOT.
Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Dairies Limited, Bwana Fuad Abri (kulia)akitoa maelekezo ya uendeshaji wa kiwanda chake alipotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo,Mifugo , maji na umwagiliaji. Ikiwa ni sehemu ya ziara ya kamati hiyo kujionea na kujifunza juu ya kongani ya Ihemi na shughuli mbalimbali za Mpango wa Kuendeleza Kilimo Nyanda za juu kusini mwa Tanzania(SAGCOT). Wapili kulia ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni mbunge wa Maswa Magharibi, Bwana Mashimba Ndaki. Watatu kulia ni Mjumbe wa kamati ambaye pia Mbunge wa viti Maalum Bibi Khadija Hassan Aboud. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT , Bwana Geoffrey Kirenga.

Na Mwandishi Wetu, Iringa.

WAWEKEZAJI katika sekta ya kilimo na mifugo wamelalamikia ushindani unaoletwa na bidhaa kutoka nje kutokana na serikali kushindwa kuzidhibiti kwa njia ya kupunguza kodi na tozo mbalimbali katika uzalishaji.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana wawekezaji hao ambao pia ni sehemu ya wabia wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo, Mifugo, Maji na Umwagiliaji katika Kongani ya Ihemi mkoani Iringa na Njombe, walisema ipo haja serikali ikaangalia suala hilo kwa jicho pana ili kulinda bidhaa za ndani.

Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Dairies Limited kilichopo mkoani hapa, Bwana Fuad Abri alisema haiwezekani Tanzania iwe nchi ya pili kwa idadi ya ng’ombe barani Afrika baada ya Ethiopia lakini bado inapitwa katika uzalishaji na uingizaji maziwa nchini.

“Wenzetu Kenya wanazalisha lita 1,500,000 za maziwa kwa siku lakini Tanzania inazalisha lita 120,000 kwa siku. Wakati huohuo sisi tunawapita kwa umbali katika idadi ya ng’ombe, kama hiyo haitoshi bidhaa za maziwa kutoka mataifa jirani zinaingia kwa wingi na kutoa ushindani mkubwa na bidhaa za ndani,” alisema Bw. Abri.

Alisisitiza kuwa zipo namna nyingi za kuzuia ushindani huu kwa sababu Serikali ya Kenya inashirikiana kwa kiasi kikubwa na wazalishaji maziwa na ndiyo maana wana uwezo wa kusafirisha nje kwa bei shindani.

“Katika biashara hii ya maziwa kitu kikubwa kinachotakiwa kuangaliwa ni namna gani unapata maziwa yako, bei utakayonunulia ikupe faida lakini faida yenyewe iwe katika soko shindani,” alisema Bw. Abri.

Wabunge hao wakiongozwa na mwenyeji wao Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT, Bwana Geofrey Kirenga ambapo kwa upande wao waliongozwa na kaimu mwenyekiti wa kamati Bwana. Mashimba Ndaki, walitembelea kiwanda cha kuzalisha chakula cha mifugo na ufugaji kuku wa nyama na mayai, Silver Land kilichopo mkoani hapa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho, Bwana Jack Bennie alisema mbali ya kuwepo na utaratibu wa kulipa kiasi kidogo cha kodi kutokana na utaratibu wa kiuwekezaji lakini bado bidhaa za kuku na chakula cha mifugo vinaathiri soko kutokana na kuzalishwa chini ya kiwango lakini vingine vinaingia nchini na kuuzwa kwa bei ndogo inayovuruga ushindani.

“Tumeamua kufanya uwezekazi mkubwa katika sekta hii ya mifugo, lakini kuna tatizo la ushindani usioendana na uhalisia ambapo bidhaa kutoka nje zilituathiri kwa kiasi kikubwa, tunashukuru kwa sasa serikali imezuia kuingiza vifaranga vya kuku kutoka nje, tunaomba washikilie hapohapo kwa sababu kukosekana kwa vifaranga hivyo kumesaidia wazalishaji wa ndani kupata soko,” alisema Bwana Bennie. Akizungumzia hali hiyo mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo Dkt. Immaculate Sware alisema wawekezaji wakubwa namna hiyo ni fursa kwa watanzania hivyo serikali haina budi kuangalia namna ya kuwatengenezea mazingira mazuri ya biashara ili walipe kodi vizuri lakini pia wanufaishe jamii.

“Tumetembelea miradi mingi iliyo katika ubia na SAGCOT, mradi huu wa Silverlands ni mkubwa kwa hiyo tunapopata muda wa kusikiliza kero zao inakua jambo jema kujua namna ya kuzifikisha ili zitatuliwe na kusaidia jamii ambayo ndiyo wanufaika kwa njia nyingi ikiwemo kupata ajira na kupata huduma au bidhaa,” alisema Dkt. Sware.

SAGCOT imeamua kuwatembeza wajumbe wa kamati hiyo ya bunge ili kuona shughuli zinazofanyika katika kongani ya Ihemi ambayo ni miongoni mwa kongani sita zilizopo katika kituo hicho. Maeneo mengi waliyotembelea ni ile inayosimamia mnyororo wa ongezeko la thamani katika mazao ya nyanya, viazi mviringo, soya na maziwa.

RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA BARABARA YA KILOMITA 26 YA KIA-MERERANI MKOA WA MANYARA LEO

$
0
0

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akizinfdua rasmi barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017.

Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na viongozi wengine akikata utepe kuzindua barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017.



Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia maelfu ya wananchi wa Mererani wakati wa kuzindua barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017.





Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Mbulu,Hason Kamoga baada ya kuzindua barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017. Picha na IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akilakiwa kwa furaha na Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Joel Bendera alipowasili kuzindua barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia maelfu ya wananchi alipowasili Mererani kuzindua barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017.
Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipeana mikono na Mbunge wa Simanjiro Mhe. James Ole Milya kwenye sherehe ya kuzindua barabara ya lami ya kilomita 26 kutoka Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa kilimanjaro (KIA) katika mkoa wa Kilimanjaro hadi Mererani mkoani Manyara leo Septemba 20, 2017.

KATIBU MTENDAJI BODI YA FILAMU AWATAKA WATANZANIA KUJIANDAA TAMASHA LA JAMAFEST

$
0
0
Binagi Media Group.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Tanzania Bi.Joyce Fisso amewataka watanzania kujiandaa na kutumia vyema fursa ya kuwa wenyeji wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki (JAMAFEST) litakalofanyika nchini mwaka 2019.

Akizungumza na BMG hii leo, Bi.Fissoo ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la JAMAFEST 2017 lililomalizika Kampala nchini Uganda, amesema tamasha hilo linatoa fursa kubwa kwa watanzania kuonyesha ngoma na bidhaa mbalimbali za kiutamaduni na hivyo kukuza soko lao la ndani na nje ya nchi.

Aidha Bi.Fissoo amefurahishwa kwa namna watanzania walivyoshiriki vyema kwenye tamasha la mwaka huu nchini Uganda na kubainisha kwamba walitia fora kwenye maonyesho ya tamasha hilo yaliyofanyika kwenye viwanja vya Kokolo.

Katika kilele cha Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki JAMAFEST mwaka 2017 nchini Uganda, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania, Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe alipokea bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama ishara ya Tanzania kuwa mwenyeji wa tamasha hilo ambalo kwa mara ya kwanza liliasisiwa nchini Rwanda mwaka 2013.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu nchini Tanzania ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi Tamasha la JAMAFEST Bi.Joyce Fisso (mwenye bendera) akijiandaa kupongea cheti cha pongezi kutoka kwa Waziri wa Wizara ya Afrika Mashariki ya Uganda Mhe.Ali Kivejinja kwenye kilele cha Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki JAMAFEST lililofanyika Kampala nchini Uganda Septemba 14,2017.
Naibu Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Balozi Elibariki Maleko (wa pili kulia) akipokea cheti cha pongezi kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi.Joyce Fissoo kwenye kilele cha Tamasha la JAMAFEST ambapo Tanzania ilishiriki vyema kwenye tamasha hilo lililofikia tamati Septemba 14,2017 nchini Uganda.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nchini, Mhe.Dkt.Harrison Mwakyembe alipokea bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kama ishara ya Tanzania kuwa mwenyeji wa Tamasha la Utamaduni na Sanaa Afrika Mashariki JAMAFEST mwaka 2019 ambapo kwa mara ya kwanza tamasha hilo liliasisiwa mwaka 2013 nchini Rwanda.

UBA bank Tanzania yazindua kituo cha huduma kwa wateja cha Masaa 24 Siku 7 za wiki

$
0
0
Mkuu wa Kitengo cha Huduma bora za benki ya UBA, Ms Queen Odunga (Kushoto) akizungumzia namna ya Kituo cha huduma kwa Wateja kitakachokuwa kikifanya kazi kwa masaa 24 kila siku katika kuhakikisha kuwa UBA Tanzania inaendelea kutoa huduma bora na zenye kuendana na matakwa ya wateja wa UBA Tanzania. Uzinduzi huo umefanyika Mapema leo katika ofisi za makao makuu ya benki hio zilizopo barabara ya Mwl Nyerere, Jijini Dar Es Salaam.Pembeni ni Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya UBA Tanzania, Bw Peter Makau.
 Mkuu wa idara ya Uendeshaji wa Benki ya UBA Tanzania, Bw Chriss Byaruhanga akizungumzia juu ya Uzinduzi wa Kituo Kipya cha Huduma kwa Wateja cha Benki ya UBA Tanzania Kitakachokuwa kikifanya kazi kwa Masaa 24 kila siku. 
 
 Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya UBA Tanzania, Mr Peter Makau akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)mapema leo wakati wa kuzindua kituo cha huduma kwa wateja cha benki ya UBA Tanzania kitakachofanya kazi kwa masaa 24 kila siku.
Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa benki ya UBA Tanzania, Bi Brendansia Kileo akifafanua Juu ya huduma nyingine zinatolewa na benki hiyo huku lengo kubwa likiwa ni kuwafikia wateja wengi zaidi na kutoa huduma bora zaidi kwa wateja wao.
Dar Es Salaam, Benki ya UBA Tanzania leo (Jumatano) imezindua kituo cha Huduma Kwa Wateja Cha Masaa 24 Kila Siku. Kituo hiko kitakuwa kikifanya kazi kwa masaa 24 kila siku huku lengo likiwa ni kuendelea kutoa huduma bora kwa wateja wao na wasio wateja muda wote pale ambapo mteja anahitaji huduma kutoka benki hio.
Kituo hiko cha Huduma kwa Wateja kwa Masaa 24 kitakuwa kikitoa huduma pia kupitia mitandao yao ya Kijamii ya Facebook, Twitter, BBM, E-mail na kupitia simu ya meza. 
Ili mteja aweze kupatiwa huduma anapaswa kuwasiliana nao kwa njia mojawapo kati ya hizi kwa kutumia barua pepe (e-mail: CFC@ubagroup.com, Kupitia mtandao wa twitter Mteja anaweza kuwasiliana nao kupitia https://www.twitter.com/ubacares na kupitia facebook unaweza kuwasiliana nao kwa kutembelea https://www.facebook,com/ubaTanzania na instagram https://www.instagram.com/ubacares
Vilevile mteja anaweza kuwasiliana nao moja kwa moja kupitia namba ya simu ya +255 764 700 782 na kwa wale wanaotumia BBM basi wanapatikana kupitia BBM channel C00211246
Pamoja na kuzindua kituo hiko cha huduma kwa wateja kwa masaa 24 siku 7 za wiki vilevile UBA Tanzania wanatarajia kufungua matawi mapya manne ili kupanua wigo na kuwafikia wateja wengi zaidi na kuwasogezea huduma karibu.

SHABIKI WA YANGA MKOANI RUVUMA , AFUNGUKA MAZITO BAADA YA YANGA KUTOKA SALE YA 1-1

$
0
0
Shabiki wa Yanga mkoani Ruvuma maarufu kwa jina la Bakule Bakule atokwa na machozi baada ya time yake ya Yanga kutoka sale ya kufungana moja moja na Maji Maji , asema maandalizi yalifofanywa na Maji Maji yalikuwa kwa ajili ya kuwaangamiza Yanga ila kwa Simba hatafanya hivo.

Idara ya hekaheka ya Leo Tena Clouds yafanyika Duka jipya la Tigo Mwanza

$
0
0

Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds fm, Geah Habib akiendesha kipindi chake ndani ya duka jipya la Tigo mkoani Mwanza hii leo. Hii ni sehemu ya shamrashamra za msimu wa Tigo fiesta 2017.
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena cha Clouds fm, Geah Habib akiendesha kipindi chake ndani ya duka jipya la Tigo mkoani Mwanza hii leo. Hii ni sehemu ya shamrashamra za msimu wa Tigo fiesta 2017.

Wafanyakazi wa Tigo wakiendelea kutoa Huduma
Msimamizi wa duka la Tigo Barbara ya Nyerere mkoani Mwanza, Neema Mossama akizungumzia jinsi gani wateja wa Tigo wataweza kunufaika na huduma zao ndani ya msimu huu wa Tigo fiesta.

WATU WAWILI WAMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI WILAYA YA NAMTUMBO MKOANI RUVUMA

$
0
0

Watu wa wili wamefariki dunia katika ajali ya gari aina ya loli lenye namba za usajili T782 CMC katika kijiji cha Utwango. Barabara ya Songea – Namtumbo . Wilaya ya Namtumbo Mkoani Ruvuma. Waliofariki ni dereva wa Gari hilo ambaye bado hajafahamika jina lake mwingine ni kondakta wa gari hilo aliyejulikana kwa jina la Abiud Daudi

KUMBUKUMBU YA MIAKA 20 YA KIFO CHA RAMADHANI NYAMKA

$
0
0

Familia ya Ramadhani  Hassan Nyamka wanakumbuka kifo cha baba yao mpendwa Ramadhani Nyamka aliyefariki Septemba 20 1997.

Ni miaka 2o toka kuondoka kwa Ramadhani Nyamka ambaye aliwahi kuwa Mwemyekiti wa Chama Mkoa Dar es Salaam na Meya wa Jiji la Dar es salaam mwaka 1978-82.

Unakumbukwa na watoto wako Zuberi, Ibrahim, Sophia, Halima, Shami, Mariam, Maendeleo, Shaban na Mikidadi,  wake zao Mama Shami na Mama Mzee pamoja na wajukuu zako Zainab, Umrathi, Nuru, Salum, Hafidha, Sara na familia nzima kwa ujumla.

Tunazidi kukuombea kwa Allah azidi kukupa kauli thabiti na makazi mema Akhera.

Allahuma Amin.


Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images