Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46389 articles
Browse latest View live

Article 5


Tony Elumelu mourns with Sierra Leone. Donates $500,000

$
0
0
Following the August 14 unprecedented disaster, Tony Elumelu, Founder of Tony Elumelu Foundation and Chairman of United Bank for Africa (UBA), yesterday, Wednesday 23 August, paid a state visit to the people and Government of Sierra Leone to commiserate over the great loss caused by devastating mudslides and floods that have claimed hundreds of innocent lives and left many more still missing.
Elumelu in the company of former President of Nigeria Olusegun Obasanjo and Sierra Leonean Presiden Ernest Koroma visited some of the survivors at the Connaught Hospital in Freetown upon arrival in the country. Later on at the Sierra Leonean Statehouse, he made a donation of USD$250,000 on behalf of the Tony Elumelu Foundation and another USD$250,000 on behalf of staff, management and Directors of United Bank for Africa (UBA) as emergency aid grants for victims of the mudslides.
Speaking in solidarity with Sierra Leone, Elumelu charged the world and the African private sector to rally around the ongoing rehabilitation and relief efforts. “For me, the little token we are giving is what it is, little, but symbolic. At a time like this, the world must come together to support the victims of this unfortunate disaster. It is not a situation that one prays to be in, but in the event that it does happen, we should all rally to support one another.”
Continuing, he urged the rest of the world not to turn a blind eye to Sierra Leone’s plight: “We have on our hands a humanitarian disaster of high proportions. It requires the attention of the entire world. We have buried over 600 lives and many hundreds more are still missing. We must turn the global spotlight on Africa. The world must stand with Africa just as in the past, Africa has stood with the world.”
The UBA Chairman reassured Sierra Leoneans of the Bank’s steadfast support. “United Bank for Africa (UBA) will continue to play its role in helping small and medium scale enterprises, and women, especially from the affected areas, to enable them rebuild their economic lives. 
The Sierra Leonean President, moved by this act, commended Elumelu’s unwavering presence in the country’s times of need, stating: “In you we have a brother and someone we can rely on.” He praised the consistency of the Founder of the Tony Elumelu Foundation (TEF). “You have always provided us with support. United Bank for Africa (UBA) was here immediately after the war to provide us with banking services to support our rebuilding efforts. Again, during our fight against Ebola, you were here through the United Bank for Africa (UBA) and the Tony Elumelu Foundation (TEF) and provided us with great support. And now again, you have come to support us.”
Elumelu’s donation will support the victims, some of whom are in hospital needing food, clothing and medicine. The much-needed assistance will also go towards the ongoing recovery efforts and the construction of permanent settlements for the affected persons.
The Sierra Leonean mudlslides is the third catastrophe to devastate the West African country in the past two decades. 

KAMPUNI GUILIN PHARMACEUTICALS TANZANIA LIMITED YAZINDU TAWI HAPA NCHINI KWAAJILI YA KUTENGENEZA NA KUSAMBAZA DAWA ZA KUKABILIANA NA UGONJWA WA MALARIA.

$
0
0
Katibu Mkuu wa wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya (wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja  mara baada ya uzinduzi wa tawi la kampuni mpya ya kimataifa toka nchini China iitwayo Guilin Pharmaceuticals Tanzania Limited itakayotengeneza na kusambaza dawa za kukabiliana na ugonjwa wa Malaria kali iitwayo Artesun nchini Tanzania. (Wa pili kulia ni Mwakilishi Mkuu wa China kwenye masuala ya uchumi na biashara nchini Tanzania (wa pili kushoto) Makamu mkuu wa Rais wa kampuni ya Guilin Pharmaceutical Tanzania Lily Su (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Ashok Pandey.
 Katibu Mkuu wa wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya (wa kwanza kushoto) akizungumza waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uzinduzi wa tawi la kampuni mpya ya kimataifa toka nchini China iitwayo Guilin Pharmaceuticals Tanzania Limited itakayotengeneza na kusambaza dawa za kukabiliana na ugonjwa wa Malaria kali iitwayo Artesun nchini Tanzania. (wa pili kulia ni Mwakilishi Mkuu wa China kwenye masuala ya uchumi na biashara nchini Tanzania (wa pili kushoto) Makamu mkuu wa Rais wa kampuni ya Guilin Pharmaceutical Tanzania Lily Su (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Ashok Pandey.
 Katibu Mkuu wa wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Mpoki Ulisubisya akipitia baadhi ya nakara za karatasi zilipewa katika uzinduzi wa uzinduzi wa tawi la kampuni mpya ya kimataifa toka nchini China iitwayo Guilin Pharmaceuticals Tanzania Limited itakayotengeneza na kusambaza dawa za kukabiliana na ugonjwa wa Malaria kali iitwayo Artesun nchini Tanzania.

TMT YAIBANA MCHENGA, BINGWA WA SPRITE BBALL KINGS KUJULIKANA JUMAMOSI

$
0
0
 Nahodha wa timu Mchenga BBall Stars Mohamed Yusuf akiwa anajaribu kuwatoka wachezaji wa timu ya TMT katika mchezo wa nne kati ya mitano katika fainali ya Sprite BBall Kings uliyopigwa kwenye viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Ulimalizika kwa TMT kutoka na ushindi wa pointi 80-79.


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.


Timu ya TMT imefanikiwa kurejesha furaha kwa mashabiki zake baada ya kuwafunga Mchenga BBall Stars kwa pointi 80-79 mchezo wa nne kati ya mitano katika fainali ya Sprite BBall Kings uliyopigwa kwenye viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

TMT imefanikiwa kushinda mchezo huo wa pili kati ya minne na kuzima matumaini ya Mchenga ga kutwa ubingwa mapema baada ya kuwa tayari wakiwa wameshashinda michezo miwili kati ya mitatu.

Katika mchezo wa kwanza Mchenga walitoka na ushindi wa pointi 101- 70 za TMT, mchezo wa pili TMT wakashinda kwa pointi 82-79, na mechi ya tatu Mchenga wakashinda kwa alama 87-82 za TMT.

Kutokana na matokeo hayo timu ya TMT imeweza kusimamisha ubingwa uliokuwa unategemewa na Mchenga BBall Stars kwa siku ya juzi na kupelekea kwenda katika Game 5 siku ya Jumamosi Ijayo.

Pamoja na hayo, mechi hiyo iliweza kuonyesha utofauti na ufundi mkubwa kutokana na timu zote mbili kujifua vizuri na kusababisha kumaliza mchezo kwa tofauti ya pointi moja.

Manahodha wa timu zote mbili wamewaahidi mashabiki wao kuja kwa wingi siku ya Jumamosi kwa ajili ya kushuhudia mchezo huo wa mwisho na wenye kutoa hatma ya bingwa Sprite BBall Kings 2017 na kila mmoja akijinasibu kufanyia makosa pale walipokosea ili waweze kuondoka na kitita cha shiling milion 10.

Mchenga na TMT zitakutana tena Septemba mbili (Jumamosi) ya mwaka huu kucheza game 5 ambapo mchezo huo ndiyo utakoweza kuamua mshindi ni nani kati ya wawili hao.
Nahodha wa timu Mchenga BBall Stars Mohamed Yusuf akiwa anajaribu kumtoka nahodha wa  timu ya TMT Isihaka Masoud katika mchezo wa nne kati ya mitano katika fainali ya Sprite BBall Kings uliyopigwa kwenye viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam. Ulimalizika kwa TMT kutoka na ushindi wa pointi 80-79.

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AZINDUA NYUMBA ZA MAKAZI YA ASKARI MAGEREZA, GEREZA KUU ARUSHA

$
0
0
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha, leo Agosti 28, 2017(Wa pili kulia) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa(wa tatu toka kulia) ni Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mhe. Gobless Lema.
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kutoa hotuba fupi ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akitoa hotuba mbele ya Maofisa na askari wa Magereza Mkoani Arusha katika hafla ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha. 
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(katikati) akikagua nyumba za askari Magereza zilizojengwa kwa kutumia fedha iliyopatikana katika miradi ya Shirika la Magereza(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha, Khamis Nkubasi.
 Muonekano wa nyumba zilizozinduliwa za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
 Baadhi ya Maafisa na Askari wa Magereza Mkoani Arusha waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha. 
 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa akimpongeza Mkuu wa Magereza Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Khamis Nkubasi mara baada ya uzinduzi wa nyumba hizo(katikati) ni Naibu Kamishna wa Magereza, Tusekile Mwaisabila.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo(kulia) alipomtembelea ofsini kwake leo kabla ya uzinduzi rasmi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Maafisa na Askari ambao ni mafundi ujenzi waliojenga nyumba hizo(waliosimama) mara baada ya hafla ya uzinduzi wa nyumba hizo. Wengine walioketi ni Kamishna Jenrerali wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa tatu toka kushoto), wa pili kushoto ni  Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mhe. Gobless Lema(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba(Mb) akisalimiana na Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza Mkoani Arusha alipowasili katika viwanja vya Gereza Kuu Arusha katika ziara Maalum ya uzinduzi wa nyumba za makazi ya askari wa Gereza Kuu Arusha leo Agosti 28, 2017 ambapo nyumba hizo zimejengwa hivi karibuni na Uongozi wa Jeshi hilo kwa kutumia fedha iliyopatikana katika miradi ya Shirika la Magereza. Kushoto kwa Waziri ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini Dkt. Juma Malewa.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AMUAGA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE CUBA

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiagana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba Bi. Ana Teressa .jana Agosti 27/2017 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Havana ,baada ya kumaliza ziara ya kikazi Nchini Cuba. Katikati ni Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

RPC MSANGI AWAAASA WAANDISHI WA HABARI KUTUMIA KALAMU ZAO VIZURI ILI KULINDA AMANI YA NCHI

$
0
0
Na David John Mwanza

JESHI la Polisi mkoa wa Mwanza limeaasa waandishi wa habari nchini,  kuhakikisha wanatumia kalamu zao kwa uweledi na uadilifu mkubwa katika kuhabarisha umma, mambo muhimu ya nchi na kwamba waepuke kutumiwa na watu wachache ambao mara zote hawalitakii mema Taifa.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Rpc Mohamed Msangi wakati wa mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi ambaye aliongozana na Naibu katibu kuu wa Taasisi ya kutetea haki za binadamu nchini TAHURA Habibu Rajabu jana.

Kamanda Msangi mbali na mambo mengine alisema kuwa waandishi wa habari wanadhamana kubwa katika kuhakikisha Taifa linaendelea kuwa salama kwani kama kalamu zao zitatumika vibaya ni rahisi kuvunja usalama ambao umejengwa na waasisi wa Taifa.

"Nitowe wito kwa waandishi wa habari ni vema wakaongeza uzalendo na uchungu kwa nchi yao na hasa kuhakikisha mnatumia kalamu zenu kwa ustadi wa hali ya juu na kuepuka kutumiwa na watu ambao hawalitakii mema taifa,".alisema Msangi

Aliongeza kuwa katika suala la kulinda amani linatakiwa kwa kila mtanzania, kwani hata mwandishi wa habari ni mtanzania na pindi usalama utakapokosekana haitajalisha nafasi ya mtu hivyo lazima waandishi wa habari wanatakiwa kuwa wazalendo la kuhakikisha wanapigania taifa lao kwa nguvu zote.

Msangi alifafanua kuwa watanzania wasidanganywe kwani uhuru ambao unapatikana hapa nchini huwezi kupata mahala pengine popote hivyo ni lazima kujiepusha na watu ambao wanataka kujipatia umaalufu kwa mgono wa watu wengine wakiwemo wandishi wa habari.

Akizungumzia hali ya usalama katika mkoa wa mwanza Kamanda Msangi alisema jiji hilo lipo salama na watu wanaendelea na shughuli zao kama ilivyo maeneo mengine huku akikiri kuwepo kwa matukio madpmadogo ambayo kimsingi jeshi la Polisi linaendelea na uperesheni zake za kila siku.

"Mwanza iki shwari na hata ninyi wenyewe mnaona kama watu wanaendelea na kazi zao japo matukio madogo madogo hayakosekani hususani uwizi wa pikipiki na kadhalika lakini askari wangu wako wanaendelea na majukumu yab kuhakikisha mambo yanaendelea kuwa salama."alisema Msangi.

Pia aliwataka wananchi wa mwanza ma tanzania kila mtu kujitambua na zaidi kuhakikisha kauli ya viwanda wanaipiokea kwa kufanya kazi huku akibainisha wao kama mkoa wameshatenda maeneo kwa ajili ya kukaribisha uwekezaji kwa manufaa ya nchi huku akisisitiza kwa kuzitaka taasisi za haki za binadamu kuwa makini kupokea malalamiko ya watu pasipo kuyachunguza kwa kina.

"Nivema taaisis za zinateteta haki za binadamu kufanya kazi zao kwa uweledi na kuhakikisha malalamiko wanayoletewa wanayafanyia kazi kabla ya kuchukua hatua ambazo mwisho wa siku zinaleta madhara kwa wananchi husika.alisema Msangi.

Ambapo kwa upande wake Naibu katibu mkuu wa Tahura Habibu Rajabu aliunga mkono kauli ya RPC Msangi huku akishauri kwamba wananchi wajitahidi kuleta malalamiko kwa wakati na si kusubiri muda mwingi umepita lakini hata wakileta ukifanya uchunguzi kwa kina unakuta alalamiko mengi ni yakweli lakini mengine ni siasa tu.

IGP SIRRO AFUNGUA MAFUNZO YA KIJESHI MKOANI KILIMANJARO

$
0
0
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro, akizungumza na baadhi ya askari wa Jeshi hilo wanaoshiriki mafunzo ya wiki mbili ya kuwajengea Uwezo na Ujasiri wakati wanapotekeleza majukumu yao muda mfupi kabla ya kufungua rasmi mafunzo hayo yanayofanyika katika chuo cha Polisi Moshi CCP mkoani Kilimanjaro jana. Picha na Jeshi la Polisi.
Baadhi ya askari wa Jeshi la Polisi nchini kikosi cha kutuliza Ghasia (FFU) wanaoshiriki mafunzo ya wiki mbili ya kuwajengea Uwezo na Ujasiri wakati wanapotekeleza majukumu yao wakiwa tayari kumuonyesha Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (hayupo pichani), moja ya mbinu mahiri za kukabiliana na matishio ya kiuhalifu na wahalifu, mafunzo hayo yanayofanyika katika Chuo cha Polisi Moshi CCP. Picha na Jeshi la Polisi.

Wataalamu wa afya kutoka China watembelea Hospitali ya Muhimbili leo

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza na ujumbe kutoka China Leo. Ujumbe huo umejadiliana na uongozi wa MNH jinsi watakavyotoa huduma ya matibabu kwa wagonjwa.
Wataalamu wa afya kutoka China wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa MNH leo.
Baadhi ya wakurugenzi wa MNH wakifuatilia mazungumzo hayo leo.
Watalaamu na baadhi ya wakurugenzi wa MNH wakiwa kwenye picha ya pamoja leo.

KAMATI YA BAJETI YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA MIRADI YA MAXCOM AFRICA KATIKA VITUO VYA DART.

$
0
0
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Max Com Africa Juma Rajabu  akimuonyesha Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia namna ya  mfumo wa kutumia kadi unavyo fanya kazi katika vituo vya Mabasi yaendayo haraka katika kituo cha Mabasi ya haraka cha Feri jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia, akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa haabari juu ya ziara yao ya kutembelea mradi wa ukusanyaji fedha katika kituo cha Feri cha mabasi yaendayo Haraka
 Mbunge wa Ileje na mjumbe wa Kamati ya Bajeti, Janeth Mbene akipanchi tiketi katika kituo cha mabasi yaendayo haraka kilichopo Feri Jijini Dar es Salaam wakati wajumbe wa kamati hiyo ilipotembelea miradi ya Maxcom Africa
 Mbunge wa Rombo , Joseph Selasini akipanchi tiketi katika kituo cha mabasi yaendayo haraka kilichopo Feri Jijini Dar es Salaam wakati wajumbe wa kamati hiyo ilipotembelea miradi ya Maxcom Africa
 Mkuu wa Kitengo cha Biashara Kutoka Maxmalipo Bw. Deogratius Lazari Akifafanua Jambo kwa wabunge  wa kamati ya Bajeti walipotembelea Mradi wa ukusanyaji mapato wa Max Malipo katika Vituo vya Mabasi ya Endayo Haraka
 Kaimu Mtendaji Mkuu DART, Ronald Lwakatare, akifafanua Jambo kwa wabunge  wa kamati ya Bajeti walipotembelea Mradi wa ukusanyaji mapato wa Max Malipo katika Vituo vya Mabasi ya Endayo Haraka.
 Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano la Tanzania na Wajumbe wa kamati ya Bajeti wakiangalia miundombinu ya mradi wa mabasi yaendayo harakajijini Dar es Salaam.

WANAWAKE WA SINGIDA WAHIMIZWA KUACHA WOGA, WAPIGANIE HAKI ZAO.

$
0
0
Wanawake Mkoani Singida wamehimizwa kujenga utamaduni wa kujiamini na kuondoa woga, ili waweze kufanikiwa kupigania haki zao za msingi, ikiwemo ya haki ya kumiliki ardhi.

Wito huo umetolewa na diwani wa kata ya Mungumaji Hassan Shabani Mkata, wakati akichangia mada juu ya haki ya umiliki wa ardhi kwa wanawake kwenye mafunzo yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa kituo cha walimu mjini hapa.

Mafunzo juu ya haki ya mwanamke kumiliki ardhi yaliandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Singida IR Vicoba Net Work (SIRVICONET) na kufadhiliwa na shirika la The Foundation for Civil Society kwa ajili ya wanawake wa Singida.

Mkata amefafanua kuwa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua uhalali wa umiliki ardhi kwa wanawake, isipokua wanawake wenyewe wanakosa haki hiyo kutokana na woga wao uliopitiliza.

Amesema umefika wakati sasa wanawake wawe mstari wa mbele kupingania haki zao na kutokomeza mila kandamizi, ziliyopitwa na wakati ambazo zinawakandamiza kwamba hawana haki ya kumiliki ardhi.

“Kwa hilo wanawake watafanikiwa tu endapo wataondoa woga, wakajiamini na wakaunganisha nguvu zao. Nasisitiza, wanawake wanapaswa kutambua kuwa wanahaki sawa na wanaume, katika kumiliki ardhi”, amefafanua.

Naye mwezeshaji wa mafunzo hayo Afisa Ardhi kutoka Manispaa ya Singida, Lilian Msasi amesema ardhi ni mali ya umma na imekabidhiwa kwa rais, kwa niaba ya Watanzania wote.

“Raia wote…. wanawake na wanaume wana haki sawa ya kupata, kumiliki, kutumia na kugawana ardhi. Miliki za ardhi zilizopo zinatambuliwa na kulindwa kisheria”, amesema Msasi.

Msasi amesema mwanamke ana haki sawa na mwanaume katika kupata, kumiliki, kutumia na kugawa ardhi. Haki hiyo imetamkwa kwenye kifungu cha tatu (92) cha sheria ya ardhi mjini na sheria ya vijiji za mwaka 1999.

Kuhusu sifa za kuomba haki ya kumiliki ardhi, Lilian amesema kuwa ni mtu ye yote mwanamke au mwanaume, mtanzania mwenye umri wa miaka 18 na kuendelea anaweza kupatiwa hati ya kumiliki ardhi.

“Pia kikundi cha watu ambao sio raia wa Tanzania, wanaweza kuomba haki ya kumiliki ardhi (delivative righs), kwa ajili ya uwekezaji”, amesema.

Ameongeza kuwa kwa vile wanawake ni watumiaji wakuu wa ardhi, vyombo vinavyohusika na masuala ya usimamizi na utendaji wa ardhi, vihakikishwe kuwa wanawake na wanaume wanashirikishwa ipasavyo katika masuala yahusuyo ardhi

Awali Mratibu wa Shirika la SIRVICONET, Happy Francis, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo zaidi wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya kata, maafisa watendaji wa kata na maafisa maendeleo ya jamii, ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

Ameongeza kuwa dhamira ya SIRVICONET ni kuwezesha wanachama wake kuwa na nguvu kiuchumi katika kupambana na umaskini, ujinga na maradhi na kuwa na mahusiano mazuri miongoni mwao.
 Mratibu wa shirika la Singida IR Vicoba Net work (SIRVICONET) Happy Francis, akitoa ufafanuzi wa jambo kuhusu mafunzo juu ya umiliki ardhi kwa wanawake. Mafunzo hayo yamefanyikia kwenye ukumbi wa mikutano kituo cha walimu barabara ya Nyerere mjini hapa.
 Baadhi ya washiriki wa mafunzo juu ya umiliki wa ardhi kwa wanawake yaliyoandaliwa na shirika la SIRVICINET na kufadhiliwa na shirika la The Foudation For Civil Society.
Mwezeshaji Lilian Msasi, akitoa mafunzo juu ya umiliki wa ardhi kwa wanawake yaliyoandaliwa na shirika la SIRVICONET na kufadhiliwa na shirika la The Foundation For Civil Society.

RAIS DKT MAGUFULI ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA TAKUKURU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

$
0
0

 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wafanyakazi wa Makao Makuu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Upanga jijini Dar es salaam leo Agosti 28, 2017 . Wengine ni Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora)Mhe. Angela Kairuki, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dr. Laurean Ndumbaro, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bw. Valentino Mlowola, na Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa TAKUKURU Bw. Alex Mfungo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wafanyakazi wa Makao Makuu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Upanga jijini Dar es salaam leo Agosti 28, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bw. Valentino Mlowola
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza kwa risala nzuri Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bw. Valentino Mlowola alipowatembelea makao makuu yao Upanga jijini Dar es salaam leo Agosti 28, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bw. Valentino Mlowola alipowatembelea makao makuu yao Upanga jijini Dar es salaam leo Agosti 28, 2017. Wengine ni Waziri wa Nchi ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora) Mhe. Angela Kairuki na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma Dkt. Laurean Ndumbaro. Picha na IKULU

JKCI KUENDELEA KUPOKEA MADAKTARI KUTOKA CHINA.

$
0
0
Na.Agness Moshi na Bushiri Matenda-MAELEZO.

Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) inatarajia kupokea madaktari wengine wanne kutoka China kwa ajili ya kuendelea kusaidiana na madaktari wazawa katika taasisi hiyo baada ya madaktari wengine wanne kutoka China kumaliza muda wao. 
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi hiyo Dkt.Peter Kisenge katika hafla ya kuwaaga madaktari wanne kutoka China waliomaliza muda wao wa utumishi hapa nchini ambao walikua wakishirikiana naTaasisi hiyo kwa takribani miaka miwili.  

“Wanarudi nchini China baada ya kumaliza muda wao, Tunawashukuru kwa kushirikiana nasi kwa kipindi chote walichokua nasi tunaishukuru Serikali ya China kwa misaada mbalimbali wanayotupatia ikiwemo ujenzi wa jengo la Taasisi ya Moyo, madaktari,wataalam pamoja na vifaa tiba”, alisema Dkt.Kisenge.
Dkt.Kisenge aliongeza kuwa hivi karibuni Taasisi inatarajia kupokea madaktari wengine wanne kutoka China kwa ajili ya kuendelea kushirikiana nao   katika utoaji huduma ili kuweza kuifanya Taasisi hiyo ya kimataifa.
Naye Kiongozi wa timu ya Madaktari kutoka China kwa Mkoa wa Dar Es Salaam Dkt.Sun Long amesema kwa miaka miwili waliyofanya kazi na Taasisi hiyo wamefanikiwa kufanya oparesheni  takribani 373 jambo ambalo limesaidia kupunguza  gharama za matibabu na idadi ya wagonjwa wa Moyo kwenda kutibiwa nje ya Nchi kama vile India.
“Sasa hakuna haja ya kutumia fedha nyingi kwa ajili ya matibabu ya Moyo, Matibabu yote yanapatikana katika taasisi hii, hakuna Matata, Hapakazi Tu”, alisisitiza Dkt. Long.

Aidha, Dkt.Long amesema kuna haja ya nchi hizi mbili kuendelea kushirikiana ili kuendelea kusaidiana katika utoaji huduma ikiwa ni pamoja na kubadilishana wataalam ili kukuza uwezo katika utoaji huduma.
Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa jopo la madaktari waliomaliza muda wao Dkt. Gu Zhigiang ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kujitegemea katika matibabu ya magonjwa ya Moyo kwa wananchi wake na ameshukuru ushirikiano walioupata kutoka kwa taasisi hiyo kwa kipindi chote walichofanya kazi hapa nchini. 
“Ninamshuru kila mmoja na ninafurahi kuhudumia Nchi hii nzuri, ninatumaini tutaendelea kushirikiana zaidi”, alisema Dkt. Gu Zhigiang.
Dkt. Gu Zhigiang ameongeza kuwa anatarajia kukua kwa ushirikiano baina ya nchi hizi mbili kwani tunaelekea kuadhimisha miaka 50 ya ushirikiano kati ya Serikali ya China na Tanzania.

UJENZI WA KIVUKO KIPYA KIGONGO BUSISI WAANZA RASMI

$
0
0
Na Alfred Mgweno (TEMESA MWANZA)

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu, ameshiriki katika zoezi la kuweka msingi wa ujenzi wa kivuko kipya kitakachotoa huduma ya usafiri katika Ziwa Victoria kati ya Kigongo na Busisi Mkoani Mwanza. 

Zoezi hilo linaloashiria kuanza rasmi kwa ujenzi huo limefanyika Pasiansi katika eneo linalotumika kwa ajili ya ujenzi wa meli, vivuko na boti linalomilikiwa na Kampuni ya Songoro Marine Transport Limited ya Mwanza iliyoshinda zabuni ya kujenga kivuko hicho kwa gharama ya Shilingi Bilioni 8.9 za kitanzania. 

Tukio hili la kihistoria lilihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Ukodishaji Mitambo na Huduma za Vivuko kutoka TEMESA Mhandisi Japhet Y. Maselle, Mhandisi Amos Mutahiwa kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Bwana Salehe Songoro Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Songoro, na wafanyakazi wa Kampuni ya Songoro na wale wa TEMESA.

Akiongea baada ya zoezi hilo, Dkt. Mgwatu amesema wakazi wa Mwanza wana kila sababu ya kujivunia kuanza kwa ujenzi wa kivuko hicho kwani kitakapokamilika kitasaidia kurahisisha usafiri wa abiria na mali zao na hivyo kuimarisha uchumi wao. Aidha Dk. Mgwatu amemtaka Mkandarasi kuhakikisha anamaliza kujenga kivuko ndani ya muda uliopangwa kwenye mkataba na kuzingatia ubora wa hali ya juu. 

Pia ameishukuru Serikali kwa kuendelea kutenga fedha za maendeleo kwa ajili ya miradi ya vivuko kwa lengo la kuboresha huduma za usafiri. Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Songoro ameahidi kukamilisha mradi huo kwa wakati huku akisisitiza kuwa kampuni yake imejipanga vyema kufanya kazi kwa kasi kwa kuwa malighafi kwa ajili ya ujenzi wa kivuko tayari ipo kwenye eneo la ujenzi.

Kivuko hicho kipya kitakapokamilika kitafanya idadi ya vivuko vinavyotoa huduma katika eneo la Kigongo Busisi kufikia vinne vikiwemo vile vya MV. Sengerema, MV. Misungwi, pamoja na MV. Sabasaba.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu akiwa ameshikilia vifaa vya kuchomelea vyuma kuashiria kuanza kuweka msingi wa kivuko ‘’Keel Laying’’ katika eneo la Pasiansi ikiwa ni kumbukumbu ya kuanza rasmi kwa ujenzi wa kivuko kipya kitakachotoa huduma kati ya Kigongo na Busisi Mkoani Mwanza. Ujenzi wa kivuko hicho unatarajiwa kukamilika ifikapo Januari 2018 na utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.9.


Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu akichomelea vyuma kuashiria kuweka msingi wa kivuko ‘’Keel Laying’’ katika eneo la Pasiansi ikiwa ni kumbukumbu ya kuanza rasmi kwa ujenzi wa kivuko kipya kitakachotoa huduma kati ya Kigongo na Busisi Mkoani Mwanza. Ujenzi wa kivuko hicho unatarajiwa kukamilika ifikapo Januari 2018 na utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.9.




Meneja wa Miradi wa Kampuni ya Kizalendo ya MS. Songoro Marine Transport Limited ya Jijini Mwanza Major Songoro (kushoto) akitoa maelezo kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (kulia) kuhusu kuanza kwa mradi wa ujenzi wa kivuko kipya cha Kigongo na Busisi Mkoani Mwanza. Ujenzi wa kivuko hicho unatarajiwa kukamilika ifikapo Januari 2018 na utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.9.
Meneja wa Miradi wa Kampuni ya Kizalendo ya MS. Songoro Marine Transport Limited ya Jijini Mwanza Major Songoro (kulia) akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (kushoto) michoro itakayotumika katika Ujenzi wa kivuko kipya cha Kigongo na Busisi Mkoani Mwanza. Ujenzi wa kivuko hicho unatarajiwa kukamilika ifikapo Januari 2018 na utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.9.
Meneja wa miradi wa Kampuni ya Kizalendo ya MS. Songoro Marine Transport Limited ya Jijini Mwanza Major Songoro (kulia) akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (katikati) michoro itakayotumika katika Ujenzi wa kivuko kipya cha Kigongo na Busisi Mkoani Mwanza. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Songoro Bwana Salehe Songoro. Ujenzi wa kivuko hicho unatarajiwa kukamilika ifikapo Januari 2018 na utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.9.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kizalendo ya MS. Songoro Marine Transport Limited ya Jijini Mwanza Bwana Salehe Songoro (wa pili kulia aliyenyoosha mkono) akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu (wa tatu kushoto) mojawapo ya malighafi itakayotumika katika ujenzi wa kivuko kipya cha Kigongo na Busisi. Ujenzi wa kivuko hicho unatarajiwa kukamilika ifikapo Januari 2018 na utagharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.9.

PICHA ZOTE NA ALFRED MGWENO (TEMESA MWANZA)

KAMATI YA BUNGE LA TANZANIA YATEMBELEA MRADI WA MAXCOM


WATANZANIA TUENDELEE KUICHANGIA TAASISI YA JKCI: DKT.TULIA

$
0
0
Na Agness Moshi na Bushiri Matenda –MAELEZO.

Watanzania na wadau  mbalimbali wa sekta ya Afya nchini wameombwa kuendelea  kuisaidia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ili iendelee kufanya kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora. 

Hayo yamesemwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Mfuko wa Tulia Trust Mhe.Tulia Akson, wakati akikabidhi msaada  runinga nne na katoni mbili za maziwa vyenye thamani ya  shilingi 1,000,000 vilivyotolewa kwa watoto waliopo kwenye  Taasisi hiyo kwa  ushirikiano na Dstv, TSN na Kampuni ya Twincity.
 Dkt.Tulia amesema msaada  wa runinga unatimiza ahadi waliohaidi kwa taasisi hiyo na unamaana kubwa sana kwa sababu utawasaidia watoto wanaokaa hospitalini hapo kwa muda mrefu  kujifunza ,na kuwaburudisha  kwa kipindi chote cha matibabu ya awali  kabla ya kufanyiwa upasuaji.
“Watoto hawa wanakaa muda mrefu hospitalini wakitibiwa hivyo wanashindwa kujumuika na wenzao kwa michezo jambo ambalo linawafanya wahisi upweke  kwa kuwapatia runinga kutawasaidia kuondoa hali hiyo , kuwaburudisha na kuwapa nafasi ya  kujifunza kupitia vipindi mbalimbali vinavyorushwa na king’amuzi cha DSTV”, alisema Dkt.Tulia
 Naye Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt.Mohammed Janabi amesema kuwa si watoto tu watakaofaidika kwani hata wazazi wao wataweza kujua mambo mbalimbali  yanayoendelea Nchini kwa kuangalia taarifa za Habari zitakazokua zinaonyeshwa kupitia chaneli mbalimbali. 
 “ Sio watoto wote wanaokuja hapa wanatatizo la moyo peke yake wengine wanakuja wakiwa na Magonjwa mengine  ambapo inabidi  tuanze kuwatibia kwanza magonjwa hayo ambapo wakati mwingine yanachukua muda mrefu  hivyo basi kwa kipindi chote hicho runinga hizi zitakua zikiwapa burudani, elimu kwa masomo mbalimbali kama vile kiingereza, hesabu  kwa watoto wakubwa na kwa wale wadogo wataburudika kupitia katuni”,alisema Dkt.Janabi.
 Dkt.Janabi ameongeza kuwa msaada wa maziwa waliopewa utasaidia kuimarisha afya za watoto wadogo wanaotibiwa kwani wapo wengine wamekuja wakiwa na Afya duni ,wengine wana magonjwa ya utapia mlo hivyo kupelekea kuchelewa kupatiwa matibabu.
Aidha,Dkt.Janabi amemshukuru Dkt.Tulia kupitia Mfuko wake wa Tulia Trust kwa kuendelea kuhamasisha wadau mbalimbali kuipatia misaada Taasisi hiyo. 
 Kwa upande wake mtoto Mwamvita Hassani mwenye umri wa miaka 13 kutoka wilayani Kondoa kwa niaba ya watoto wanaotibiwa kwenye Taasisi hiyo ametoa shukrani zake kwa Naibu Spika na wadau waliowapa misaada hiyo.

“Ninawashukuru sana kwakutuletea Tv na Maziwa,Tumefurahi na tunawaombea watuletee Tv zingine”, alisema Mwamvita.
Dkt.Janabi  amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia upatikanaji wa vitanda kwa ajili ya Taasisi hiyo kwani wanakabiliwa na  changamoto mbalimbali ikiwemo swala la upungufu wa vitanda kwa wagonjwa kwani wanavitanda 128 tu ambavyo havikidhi mahitaji kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaofika kwa ajili ya matibabu.

TAARIFA YA HALI YA HEWA KUTOKA MAMLAKA YA HALI YA HEWA (TMA).

WATANZANIA TUENDELEE KUICHANGIA TAASISI YA JKCI: DKT.TULIA

$
0
0
Na Agness Moshi na Bushiri Matenda –MAELEZO.

Watanzania na wadau  mbalimbali wa sekta ya Afya nchini wameombwa kuendelea  kuisaidia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ili iendelee kufanya kazi kwa ufanisi na kutoa huduma bora. 

Hayo yamesemwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Mfuko wa Tulia Trust Mhe.Tulia Akson, wakati akikabidhi msaada  runinga nne na katoni mbili za maziwa vyenye thamani ya  shilingi 1,000,000 vilivyotolewa kwa watoto waliopo kwenye  Taasisi hiyo kwa  ushirikiano na Dstv, TSN na Kampuni ya Twincity.
 Dkt.Tulia amesema msaada  wa runinga unatimiza ahadi waliohaidi kwa taasisi hiyo na unamaana kubwa sana kwa sababu utawasaidia watoto wanaokaa hospitalini hapo kwa muda mrefu  kujifunza ,na kuwaburudisha  kwa kipindi chote cha matibabu ya awali  kabla ya kufanyiwa upasuaji.
“Watoto hawa wanakaa muda mrefu hospitalini wakitibiwa hivyo wanashindwa kujumuika na wenzao kwa michezo jambo ambalo linawafanya wahisi upweke  kwa kuwapatia runinga kutawasaidia kuondoa hali hiyo , kuwaburudisha na kuwapa nafasi ya  kujifunza kupitia vipindi mbalimbali vinavyorushwa na king’amuzi cha DSTV”, alisema Dkt.Tulia
 Naye Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Dkt.Mohammed Janabi amesema kuwa si watoto tu watakaofaidika kwani hata wazazi wao wataweza kujua mambo mbalimbali  yanayoendelea Nchini kwa kuangalia taarifa za Habari zitakazokua zinaonyeshwa kupitia chaneli mbalimbali. 
 “ Sio watoto wote wanaokuja hapa wanatatizo la moyo peke yake wengine wanakuja wakiwa na Magonjwa mengine  ambapo inabidi  tuanze kuwatibia kwanza magonjwa hayo ambapo wakati mwingine yanachukua muda mrefu  hivyo basi kwa kipindi chote hicho runinga hizi zitakua zikiwapa burudani, elimu kwa masomo mbalimbali kama vile kiingereza, hesabu  kwa watoto wakubwa na kwa wale wadogo wataburudika kupitia katuni”,alisema Dkt.Janabi.
 Dkt.Janabi ameongeza kuwa msaada wa maziwa waliopewa utasaidia kuimarisha afya za watoto wadogo wanaotibiwa kwani wapo wengine wamekuja wakiwa na Afya duni ,wengine wana magonjwa ya utapia mlo hivyo kupelekea kuchelewa kupatiwa matibabu.
Aidha,Dkt.Janabi amemshukuru Dkt.Tulia kupitia Mfuko wake wa Tulia Trust kwa kuendelea kuhamasisha wadau mbalimbali kuipatia misaada Taasisi hiyo. 
 Kwa upande wake mtoto Mwamvita Hassani mwenye umri wa miaka 13 kutoka wilayani Kondoa kwa niaba ya watoto wanaotibiwa kwenye Taasisi hiyo ametoa shukrani zake kwa Naibu Spika na wadau waliowapa misaada hiyo.

“Ninawashukuru sana kwakutuletea Tv na Maziwa,Tumefurahi na tunawaombea watuletee Tv zingine”, alisema Mwamvita.
Dkt.Janabi  amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia upatikanaji wa vitanda kwa ajili ya Taasisi hiyo kwani wanakabiliwa na  changamoto mbalimbali ikiwemo swala la upungufu wa vitanda kwa wagonjwa kwani wanavitanda 128 tu ambavyo havikidhi mahitaji kutokana na idadi kubwa ya wagonjwa wanaofika kwa ajili ya matibabu.

ZANZIBAR YAIPONGEZA BODI YA UTALII TANZANIA

$
0
0

Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii, Bw. Geofrey Meena akitoa maelezo kwa wajumbe wa kamati ya Baraza la wawakilishi ya Maendeleo ya Wanawake, Habari na Utaliiya Zanzibar walipotembelea ofisi za Bodi ya Utalii, Dar es Salaam.
Mjumbe wa Kamati ya Baraza Wawakilishi ya Maendeleo ya Wanawake, Habari na Utalii ya Zanzibar akitumia lugha ya alama kutafsiri jambo kwa moja ya mjumbe wa Baraza Hilo.
Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo wa Zanzibar, Mhe. Rashid Ali Juma (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Maendeleo ya Wanawake, Habari na Utalii ya Zanzibar.

Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Maendeleo ya Wanawake, Habari na Utalii ya Zanzibar wameitembelea Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) kwa lengo la kudumisha ushirikiano na kujifunza mbinu mbalimbali zinazotumiwa na Bodi katika kuvitangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ndani na nje ya nchi.

Meneja Masoko wa Bodi ya Utalii, Bw. Geofrey Meena alitoa ufafanuzi wa kina kuhusu shughuli zinazofanywa na Bodi ikiwa pamoja na namna inavyoshirikiana na Balozi za Tanzania zilizopo katika nchi mbalimbali, Mabalozi wa Hiari wa Utalii wanavyosaidia kutangaza utalii wa Tanzania katika nchi zao, Namna Bodi inavyoshirikiana na vyombo mbalimbali vya Habari vya ndani na nje katika kutayarisha vipindi vya utalii wa Tanzania. 
 
Aidha Bw, Meena alisisitiza kuwa mialiko ya Timu maarufu za mchezo wa mpira wa miguu kuwa moja ya njia yenye manufaa makubwa katika kuitangaza Tanzania

Ujumbe huo uliyongozwa na Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo wa Zanzibar, Mhe. Rashid Ali Juma ambaye alionyesha kuridhishwa na juhudi zinazofanywa na Bodi, alisema “ziara yetu imekuwa ni ya mafanikio kwani tumeweza kujifunza mikakati inayotumiwa na Bodi katika kutekeleza jukumu lake la kutangaza utalii wa Tanzania hasa Utalii wa Ndani”.
 
 Pia ujumbe huo uliipongeza Bodi kwa kuwa na mipango madhubiti ya utangazaji pamoja na kutengeneza video maalumu inayotumika kuvitangaza vivutio hivyo katika matukio mbalimbali ya kimataifa.

Ziara hiyo Ilifanyika tarehe 28/08/2017.

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMANNE LEO AGOSTI 29,2017

Viewing all 46389 articles
Browse latest View live




Latest Images