Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live

MFUMO MPYA WA KUANDAA MIPANGO NA BAJETI ZA MAMLAKA YA SERIKALI ZA MITAA (PLANREP) KUIMARISHA UTOAJI HUDUMA KWA WANANCHI TANZANIA

0
0
 Katibu Tawala wa Mkoa wa Dododma  Rehema Madenge akifungua mafunzo ya siku nane kwa wataalamu wa Afya, Mipango na Fedha kutoka Mikoa Mitano chini ya ufadhili wa mradi wa Uimarishaji Mifumo (PS3)

SERIKALI kuanzia sasa inaweza kuokoa zaidi ya Sh Bilioni tisa ambazo zilikuwa zikutumiwa na maofisa wake mbalimbali katika uandaaji wa mipango na bajeti katika Serikali za mitaa na Halmashauri kufuatia kuanza kwa matumizi ya mfumo mpya wa uandaaji mipango na bajeti utakaotekelezwa chini ya mradi wa uimarishaji wa mifumo ya sekta za umma (PS3). Anaandika Mroki Mroki wa DAILY NEWS Digital.

Mradi wa PF3 unatekelezwa na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID). BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI.

 Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo kwa  watazindua Mfumo mpya wa  kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa (PlanRep), Mratibu wa Mfunzo hayo, ambaye pia ni Mtaalaam wa Mifumo ya Tehama na Mawasiliano kutoka PS3, Desderi Wengaa, alisema katika mfumo wa zamani uliokuwa unatumika ulikuwa ukiwafanya watendaji wa serikali kutumia muda mrefu na gharama kubwa kuandaa mipango na bajeti zao lakini huu wa sasa utaokoa muda na gharama ambazo zinazidi bilioni tisa kila mwaka.

“Mradi huu kupitia mfumo wa PlanRep utasaidia san asana kuokoa gharama kwaa maana ya rasiliamali fedha zilizokuwa zinatumiwa na serikali takribani Sh milioni 60 kwa kila halmashauri na zaidi ya Sh bilioni nane hadi tisa au kumi kwa nchi nzima kwa kutumia mfumo huu ambao pia utawawezesha watendaji kufanya kazi za kutoa huduma katika maeneo yao badala ya kuzunguka katika vikao vya kuandaa bajeti,” alisema Wengaa.
Washiriki wa Mafunzo hayo ya namna ya kutumia Mfumo mpya wa  kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa (PlanRep),wakifuatilia hotuba za ufunguzi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa mradi pamoja na mgeni rasmi ambaye alikwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge.
Washiriki wa Mafunzo hayo ya namna ya kutumia Mfumo mpya wa  kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa (PlanRep),wakifuatilia hotuba za ufunguzi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa mradi pamoja na mgeni rasmi ambaye alikwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge.
Mwakilishi wa washiriki wa Mafunzo hayo, Dk Aisha Mahita akitoa neno la Shukrani kwaniaba ya washiriki wote.
Miongoni mwa wakufunzi wa mafunzo hayo ni timu ya kitaifa ya wakufunzi kutoka TAMISEMI, Sekretarieti za Mikoa, Wakala ya Serikali Mtandao (Ega), Ofisi ya Raisi Menejimenti na Utumishi wa Umma, Wizara ya Fedha na Mipango, PS3 pamoja na wizara zingine ikiwemo Wizara ya Afya. 

Zaidi ya watumiaji 1,500 watafundishwa juu ya mfumo wakiwakilisha ngazi tatu za Serikali.  Mafunzo haya yanajumuisha Maafisa Mipango, Wahasibu, Wachumi, Maafisa Tehama na Makatibu wa Afya wa Halmashauri.

Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma (PS3), ni Mradi wa miaka mitano unaotekelezwa katika mikoa 13 na Halmashauri 93 za Tanzania bara.  PS3 inafanya kazi katika sekta mbalimbali ili kuimarisha mifumo ya mawasiliano, utawala bora, fedha na rasilimali watu, hususani kwa jamii zenye uhitaji.

Washiriki wa Mafunzo hayo ya namna ya kutumia Mfumo mpya wa  kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa (PlanRep),wakifuatilia hotuba za ufunguzi zilizokuwa zikitolewa na viongozi wa mradi pamoja na mgeni rasmi ambaye alikwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge.
Meza kuu katika picha ya pamoja.

Wakazi wa Shinyanga na Geita kunufaika na uwekezaji mradi wa umeme

0
0

Kampuni ya Acacia, kwa ushirikiano na TANESCO, imejenga kituo cha kupozea umeme kilichopo katika mgodi wake wa dhahabu wa Bulyanhulu ambacho kimeweza kuongeza uhakika wa upatikanaji wa umeme katika maeneo ya mgodi huo.

Acacia imewekeza shilingi bilioni 5.5 katika mradi huo ambao utanufaisha maeneo yanayozunguka migodi ya Buzwagi na Bulyanhulu na maeneo mengine ikiwa ni pamoja na Kahama, Shinyanga, Msalala, na sehemu nyingine za Geita.

Ujenzi wa Kituo hicho ulianza Desemba 2016 na unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.
Haya ni maendeleo makubwa kwa viwanda na biashara zinazozunguka eneo hilo ambazo zitafaidika na uwepo wa umeme wa uhakika jambo litakalosaidia kuboresha ufanisi na kuongeza uzalishaji.

Mkuu wa kitengo cha miradi ya maendeleo wa mgodi wa Bulyanhulu, Jiten Divecha ameeleza kuwa tatizo la mabadiliko ya nguvu ya umeme limekuwepo kwa muda mrefu na limekua likisababisha uharibifu mkubwa wa mashine.“Ujenzi wa kituo hiki utasaidia kupunguza athari zinazotokana na kuongezeka au kupungua kwa nguvu ya umeme katika migodi yetu hivyo kuboresha shughuli za uzalishaji. Wakazi na viwanda vinavyotumia umeme katika wilaya ya Msalala mkoani Shinyanga na wilaya zingine za mkoa wa Geita zitafaidika na uwekezaji huu pia,” alisema Jiten.

Aliongeza: "Acacia inajitahidi kuleta manufaa ya kiuchumi ya pamoja kwa jamii zinazotuzunguka na wadau wake kupitia miradi endelevu."
Wakati wa ujenzi wa kituo hicho, ajira mbalimbali zilitolewa kwa jamii zinazozunguka mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu.
Akizungumzia fursa hiyo, David Nyanda alisema: “tunathamini sana ujenzi wa mradi huu kwa sababu tumepata fursa za ajira. Japokuwa fursa hizi ni za muda, tunaweza kupata mapato ili kuendesha familia zetu hasa katika kipindi hiki cha ukame.”

ETIHAD, ARGENTINA AIRLINE SIGN CODESHARE DEAL

0
0

Abu Dhabi, UNITED ARAB EMIRATES – Etihad Airways and Aerolíneas Argentinas have launched a new codeshare partnership.

Under the agreement, Etihad Airways customers are able to enjoy convenient connections via Rome and Madrid to Buenos Aires (EZE) and onwards to nine other popular Argentinian destinations – Córdoba (COR), Mendoza (MDZ), Rosario (ROS), Iguazú (IGR), Salta (SLA), Mar del Plata (MDQ), Bariloche (BRC), Trelew (REL) and Ushuaia (USH).

In turn, Aerolíneas Argentinas guests can have access to Etihad Airways’ network of over 100 destinations from its Abu Dhabi hub via the Italian and Spanish capitals.

Mohammad Al Bulooki, Etihad Airways Executive Vice President Commercial, said: “This codeshare demonstrates the importance of Argentina as a vital travel market for Etihad Airways in Latin America given the growing tourism, cultural and business opportunities that exist between the UAE and Argentina.

“We wish to give travellers flying Aerolíneas Argentinas the opportunity to enjoy the acclaimed service and hospitality for which Etihad Airways is renowned throughout the world. This codeshare will make the experience that much easier.”

Diego Garcia, Aerolíneas Argentinas Chief Commercial Officer, said: "This is a very good opportunity to consolidate and increase our offer to one of the most important hubs in the Middle East. It also allows us to improve our load factors, optimise the use of the fleet and strengthen the image of Aerolíneas Argentinas in the Asian market. We hope that this agreement will also be the gateway for many tourists to visit some of the most attractive landmarks in our country."

Codeshare agreements offer customers countless benefits, such as baggage check-in to their final destination and extra assistance during connections. Members of both airlines’ loyalty programmes – Etihad Guest and Aerolíneas Plus – will soon be able to earn and redeem miles on the codeshare flights.

About Etihad Aviation Group

Etihad Aviation Group (EAG) is a diversified global aviation and travel group comprising five business divisions – Etihad Airways, the national airline of the United Arab Emirates, Etihad Airways Engineering, Etihad Airport Services, Hala Group and Airline Equity Partners. The group has minority investments in six airlines: airberlin, Air Serbia, Air Seychelles, Alitalia, Jet Airways and Virgin Australia.

From its Abu Dhabi base, Etihad Airways flies to, or has announced plans to serve, more than 110 passenger and cargo destinations in the Middle East, Africa, Europe, Asia, Australia and the Americas. The airline has a fleet of over 120 Airbus and Boeing aircraft. In 2013, it placed firm orders for 204 aircraft, which included 71 Boeing 787s, 25 Boeing 777Xs, 62 Airbus A350s and 10 Airbus A380s. For more information, please visit: etihad.com

DC MTATURU AMWAGA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU 69 ZINAZOSHIRIKI MASHINDANO YA IKUNGI ELIMU CUP 2017

0
0
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji J. Mtaturu akifungua mipira aliyoigawa kwa timu zote shiriki za mashindano ya mpira wa miguu maarufu kama "IKUNGI ELIMU CUP 2017"
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji J. Mtaturu akionyesha moja ya mipira aliyoigawa kwa timu shiriki kwenye mashindano ya mpira wa miguu maarufu kama "IKUNGI ELIMU CUP 2017"

Baadhi za jezi zilizotolewa kwa ajili ya timu zote shiriki kwenye mashindano ya mpira wa miguu maarufu kama "IKUNGI ELIMU CUP 2017"
Na Mathias canal, Singida

Takribani timu 69 zinazoshiriki  mashindano ya mpira wa miguu maarufu kama “IKUNGI ELIMU CUP 2017” zimekabiziwa jezi pamoja na mipira kwa ajili ya utimilifu wa kuwa na vifaa vya michezo kwenye mashindano hayo jambo ambalo limeibua hisia chanya kwa kila timu kutaka kuibuka mshindi.

Akitoa vifaa hivyo vya michezo kwa ajili ya ushiriki wa timu hizo, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu alisema kuwa Ofisi yake kwa ushirikiano mkubwa na wadau wa elimu na wananchi kwa ujumla wamechangia vifaa hivyo vya michezo ikiwa ni sehemu ya kuongeza chachu ya hamasa katika mashindano na kufikisha zaidi ujumbe wa umuhimu wa waanchi kuchangia mfuko wa elimu.

Mashindano hayo yanayoshadihishwa na kauli mbiu isemayo CHANGIA, BORESHA ELIMU IKUNGI yanafanyika katika vijiji vyote 101 ambapo katika Jimbo la Singida Magharibi lenye kata 15 kila Kata itatoa timu mbili na Jimbo la Singida Mashariki lenye Kata 13 kila kata itatoa timu tatu hivyo kuwa na timu 69 zitakazopambana na kupatikana timu tatu bora.

Mhe Mtaturu alisema kuwa kunzishwa kwa mashindano hayo ni kusudio la kuifanya jamii kujihusisha na shughuli za maendeleo kwa kushirikiana na serikali, kuibua vipaji vya michezo katika Wilaya ili kukuza ajira na kufanya vijana waachane na utumiaji wa madawa ya kulevya.

Sababu zingine ni Kuunganisha jamii kuwa kitu kimoja hatimaye vijana na wananchi kuimarisha upendo, ajira na afya sambamba na kudumisha amani na mshikamano.

Mashindano hayo yanataraji kufika ukomo Septemba 19, 2017 huku zawadi zikitaraji kutolewa kwa washindi watano ambapo mshindi wa kwanza atapatiwa zawadi ya Kombe, Seti ya jezi, Mipira miwili na kitita cha shilingi 1,000,000/= , na mshindi wa pili atapatiwa Seti ya jezi, Mipira miwili na shilingi 750,000/=.

Mshindi wa tatu atapatiwa Mipira miwili na shilingi 450,000/= , Mshindi wa nne atapatiwa Mpira mmoja na Shilingi 200,000/= huku mshindi wa tano akipatiwa Mpira mmoja na Shilingi 100,000/=.

Aidha, kutakuwa na zawadi zingine kwa timu yenye nidhamu, Zawadi ya mfungaji bora, Zawadi ya Kipa bora, Zawadi ya mchezaji bora, huku wachezaji wengine 30 wakichaguliwa kuingia kambini kufundishwa mbinu za uchezaji bora.

Katika taarifa ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati wa uzinduzi wa ligi hiyo mbele ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Angelina M. Lutambi aliyemuwakilisha Mkuu wa Mkoa huo Mhe Dkt Rehema Nchimbi, alisema kuwa Idara ya elimu katika Wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa nyumba za walimu, Upungufu wa Walimu, Maabara ya Masomo ya sayansi kwa shule za sekondari, pamoja na vifaa vya kujifunzia na kufundishia.

Hivyo Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kwa ushirikiano na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo walianzisha mfuko wa elimu wilaya kwa mujibu wa sheria ndogo ya Halmashauri Wilaya ya Ikungi ya mwaka 2014 ambayo ilitolewa katika tangazo la serikali Na. 222 la tarehe 11 Julai, 2014 ili kuweza kukabiliana na changamoto za elimu ambazo zinaathiri mafanikio ya elimu katika Wilaya hiyo.

Kuanzishwa kwa mfuko wa elimu kumepelekea pia kufunguliwa kwa akaunti ya mfuko katika Benki ya NMB tawi la Ikungi kwa jina la Mfuko wa Elimu wa Wilaya ya Ikungi (Ikungi District Education Funds) akaunti Namba 52510000554.

Hata hivyo Mhe Mtaturu alitoa Rai kwa wadau wa elimu kuchangia mfuko wa elimu ili kukuza ufanisi wa elimu katika Wilaya hiyo ambao kwa kiasi kikubwa unategemea zaidi upatikanaji wa rasilimali fedha na nguvu kazi kutoka kwa wadau, wananchi, Taasisi, Mashirika, Makampuni mbalimbali yaliyopo ndani na nje ya nchi.

MWISHO

TUNDURU WAANZA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS KWA VITENDO.

0
0
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma Juma Homera .
Serikali ya Wilaya ya Tunduru imeanza kutekeleza kwa vitendo agizo la Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli la kujenga kituo cha Afya kila kata kwa nchi nzima, Ambapo wilaya hiyo tayari imenza ujenzi wa kituo cha Afya katika kata ya Nakayaya . Ujenzi wa kituo hicho cha Afya umefikia hatua ya kuezekwa na unatarajiwa kukamilika mwakani .Hii hapa video yenye habari hiyo.

ZIARA YA KAMATI YA BUNGE YA BAJETI DAR ES SALAAM KATIKA TAASISI ZA MUHIMBILI, DART NA IFM

0
0
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doroth Mwanyika akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti wakati wajumbe hao walipotembelea Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM). Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Prof. Lettice Rutashobya na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia.
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, Profesa Mohamed Janabi akiwaeleza masuala mbalimbali kuhusiana na huduma ambazo hospitali hiyo inazitoa kwa Kamati ya Bunge ya Bajeti ambayo pamoja na mambo mengine ilitembelea hospitalini hapo kujionea shughuli zinazofanywa ikiwemo upasauaji wa moyo kwa wagonjwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia akielekezwa jinsi ya kutumia risiti ya Mwendokasi kwa ajili ya kuingia kituoni kusubiri basi.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti wakiwa ndani ya Basi la Mwendo Kasi wakielekea Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam, wajumbe hao walikuwa wakikagua mfumo wa kukusanya fedha za nauli kwa mabasi hayo uliotengenezwa na Kampuni ya Maxcom.

MBAO FC YAJAZWA MILION 140 YA UDHAMINI NA KAMPUNI YA GF TRUCKS & EQUIPMENT LTD

0
0
Mkurugenzi wa Mtendaji kampuni ya GF Trucks & Equipment Imrani Karmali na Mwenyekiti wa Mbao Fc Solly Zephania Njashi wakionyesha hati ya makubaliano ya Mkataba ikiwa ni mkataba wa udhamini wa timu hiyo kwa mwaka mmoja wenye thamani ya Milioni 140 sambamba na basi la wachezaji.


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

UONGOZI wa klabu ya Mbao Fc umeingia mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya milioni 149 na kampuni ya GF Trucks & Equipments ikiwa ni udhamini wa timu hiyo kutoka Jijini Mwanza.

Kampuni hiyo imeridhishwa na maendeleo ya timu hiyo na kuamua kuwapatia udhamini kwani hawajawahi kushiriki katika udhamin i wa soka la Kiwango cha ligi kuu.

Mkataba huo uliosainiwa mbele ya waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Imrani Karmali amesema kuwa mkataba huo ni wa kihistoria kwani unaenda kuleta na kukuza maendeleo ya mpira wa miguu nchini.
Karmal amesema kuwa, madhumuni makubwa ni kukuza vipaji vya mpira wa miguu na wanatarajiwa kuisaidia Mbao Fc kufikia malengo yao msimu huu, " tunafahamu usafiri umekuwa ni tatizo kwa klabu nyingi ndogo za Ligi Kuu na hicho kimetupelekea kuanza na basi msimu huu ambapo katika mkataba wa milioni 140 utajumuisha sambamba na basi hilo la wachezaji lenye thamani ya milioni 70,".

"uwezo waliouonesha katika ligi kuu na hata kuingia fainali ya kombe la FA ulituhamasisha kuifuatilia kwa ukaribu sana na tuna imani kwa msaada wetu Mbao itaendelea kufanya vizuri na si hao tu bali hata ajira kwa vijana zitaongezeka,"amesema Karmali.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Mbao Fc, Solly Zephania Njashi ameusifu mkataba huo na kusema kuwa utazidi kuleta chachu ya maendeleo katika klabu yao na hata kupunguza gharama za mahitaji kwa wachezaji.

Njashi ameishukurui kampuni ya GF Trucks & Equipments kwa mkataba huo na kuwaahidi mashabiki na wapenzi wa Mbao kuwa mwaka huu wataendelea kufanya vizuri na kuendelea kusalia katika Ligi kuu msimu ujao.

Baada ya kusaini mkataba huo, kampuni ya GF Trucks & Equipments i iliwakabidhi mfano wa jezi zitakazovaliwa na timu ya Mbao tayari zikiwa zimeshaweka nembo ya kamouni hiyo.
Mwenyekiti wa Mbao Solly Zephania Njashi akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuingia makubaliano ya udhamini wa mkatabwa mwaka mmoja na na kampuni ya GF Trucks & Equipments wenye thamani ya Milioni 140, kushoto ni Mkurugenzi wa Mtendaji kampuni ya GF Trucks & Equipment Imrani Karmali 
Afisa Masoko wa Kampuni ya GF Trucks & Equipments Kulwa Bundala akizungumza na wanahabari baada ya kuingia mkataba na timu ya Mbao Fc wenye thamani ya Milioni 140 kwa mwaka mmoja.
Mkurugenzi wa Mtendaji kampuni ya GF Trucks & Equipment Imrani Karmali na Mwenyekiti wa Mbao Solly Zephania Njashi wakionyesha jezi za Mbao zitakazotumikia mwaka huu.

KAMISHNA WA MADINI AANZA ZIARA KANDA YA ZIWA

0
0
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (kulia), akifafanua jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Samwel Sweda (wa pili kutoka kushoto), alipofika ofisini kwake akiwa katika ziara ya kazi wilayani humo. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Eliud Mwaiteleke. Wengine ni Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Ziwa Viktoria-Magharibi, Mhandisi Yahya Samamba (kushoto kwa Mkuu wa Wilaya) na Mhandisi Rayson Nkya (wa kwanza kulia).
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (katikati), akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa viongozi wa Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza, Mrisho Masebu, kuhusu utendaji kazi wa Mradi huo.
Mmoja wa Viongozi wa Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza, Baraka Ezekiel (wa pili kutoka kulia), akifafanua jambo kwa Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (katikati) na Ujumbe wake. Kamishna Mchwampaka alitembelea Mradi huo Agosti 28 mwaka huu akiwa katika ziara ya kazi Kanda ya Ziwa.
Viongozi wa Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza, wakimwongoza Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (katikati), kukagua shughuli mbalimbali zinazofanyika katika mgodi huo. 
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (katikati), akiwa ameambatana na baadhi ya maafisa wa Wizara ya Nishati na Madini na wafanyakazi wa Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza, wakikagua sehemu mbalimbali za Mgodi huo.
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka (mwenye koti), akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza na Maafisa wa Wizara ya Nishati na Madini, mara baada ya kukagua Mgodi huo.
Shughuli za uchimbaji madini zikiendelea katika Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza.

Na Veronica Simba – Mwanza
Kamishna wa Madini Tanzania, Mhandisi Benjamin Mchwampaka, ameanza ziara ya kazi ya takriban juma moja katika mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa lengo la kukagua utekelezaji wa shughuli mbalimbali za sekta hiyo.
Katika siku ya kwanza ya ziara hiyo, Agosti 28 mwaka huu, Kamishna Mchwampaka alikutana na kuzungumza na wafanyakazi wa Ofisi ya Madini, Kanda ya Ziwa Viktoria-Magharibi pamoja na wafanyakazi wa Ofisi Ndogo ya Ukaguzi wa Madini Kanda ya Mwanza, iliyokuwa ikijulikana kama Wakala wa Ukaguzi Madini Tanzania (TMAA).
Akizungumza mara baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi wa Ofisi hizo mbili, Kamishna Mchwampaka aliwataka wafanyakazi hao kufanya kazi kwa bidii na kwa ushirikiano ili kufanikisha malengo ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuwaletea wananchi wake maendeleo ya dhati.
Katika hatua nyingine, akizuru Mradi wa Uchimbaji wa Kati wa Madini ya Dhahabu uliopo Ishokelahela wilayani Misungwi, Mkoa wa Mwanza, Kamishna Mchwampaka, alipongeza jitihada za watendaji wa Mradi huo unaomilikiwa na wazawa wazalendo kwa asilimia mia moja, kwa ubia kati ya Isinka Federation 2014 Mining Cooperative Society Limited na Kampuni ya kitanzania ya Busolwa Mining Limited.
Alisema kuwa, jitihada zinazooneshwa na wajasiriamali hao wazalendo zinapaswa kuigwa na watanzania wengine kote nchini kwani Mradi huo una maendeleo ya kuridhisha na kujivunia japokuwa bado haujaanza uzalishaji.
“Sisi kama Serikali tunafarijika sana tunaposhuhudia wananchi wazalendo wakiweka jitihada na kufanikiwa katika biashara za madini kama hivi mnavyofanya ninyi. Tunaahidi kuendelea kuwasaidia kadri iwezekanavyo ili muweze kufikia malengo yenu na kuchangia katika kuinua uchumi wa nchi.”
Kwa upande wao, baadhi ya viongozi wa Mradi huo, Baraka Ezekiel na Mrisho Masebu, waliahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa ubunifu ili mafanikio yao yaweze kuwahamasisha watanzania wengine.
Aidha, waliahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali kadri ipasavyo ikiwa ni pamoja na kulipa kodi zote stahiki pamoja na kufuata kanuni na sheria za madini zilizowekwa kwa mujibu wa sheria.
Kamishna Mchwampaka pia alipata fursa ya kuwatembelea na kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Samwel Sweda ambapo walikubaliana kushirikiana katika majukumu mbalimbali yanayohusu sekta ya madini kwa manufaa ya wananchi.
Hii ni ziara ya kwanza rasmi ya kikazi kwa Kamishna wa Madini, Mhandisi Mchwampaka tangu alipoteuliwa na Rais John Pombe Magufuli, kushika wadhifa huo, takribani miezi minne iliyopita.
Kamishna Mchwampaka anaendelea na ziara yake, ambapo katika siku ya pili atazuru Mkoa wa Geita.

Cheka akata rufaa BMT kupinga matokeo

0
0

Meneja wa bondia wa Cosmass Cheka, Juma Ndambile (kulia) akizungumzia matatizo yaliyompata bondia wake.
Cosmass Cheka akizungumzia hatua aliyochukuwa ya kukata rufaa BMT kupinga kufungiwa na matokeo ya pambano lake dhidi ya bondia Haidary Mchanjo.
 
Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Cosmas Cheka amekata rufaa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) kupinga matokeo na adhabu ya kufungiwa miezi sita na faini ya Sh200,000 iliyotangazwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC).

Cheka alisema hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari na kusema kuwa TPBC ilikuwa na njama dhidi yake ili kumtengenezea nafasi bondia Haidary Mchanjo katika ngumi za kulipwa nchini.

Alifafanua kuwa adhabu dhidi yake haikufuata sheria kwani kwanza hakupewa nafasi ya kusikilizwa kwa mujibu wa sheria, huku akimpa nafasi mwamuzi wa pambano hilo, Modest Rashid ambaye alitaka kupigana naye kuitwa na kujieleza katika kikao cha TPBC.

“Hata kwenye mahakama, lazima mtuhumiwa apewe nafasi ya kusikilizwa au kujitetea, mimi nilikuwa ulingoni na mwamuzi na mpinzani wangu Mchanjo, mwamuzi amenitolea maneno machafu sana, haikutosha akaamua kunikata pointi, niliandika barua ya kulalamika TPBC, hawajaniita na kuibuka na adhabu kwangu,” alisema Cheka.

Alisema kuwa pamoja na maamuzi hayo kutonifikia kimaandishi, nimeamua kuchukua hatua za haraka kwani tayari vyombo vya habari mbalimbali na mitandaa ya kijamii yamekwisha tangaza maamuzi hayo yaliyofanywa bila kufuata sheria kwani hawakunipa nafasi ya kusikilizwa kwa mujibu wa sheria.

Meneja wa bondia huyo, Juma Ndambile, alisema kuwa walichokifanya TPBC ni kumvunja nguvu bondia wake ili ashindwe kuendelea na mchezo wake.

Ndambile alisema kuwa TPBC ilionyesha nia ya kuhujumu matokeo hayo mapema kwa kuweka vipingamizi mbalimbali pamoja na kutakiwa kumlipa mwamuzi wa pambano wakati wao hawakuwa waandaaji.

“Niliwaambia kuwa pambano limeandaliwa na kampuni inayoiitwa dragon, sasa kwa nini mimi nilipe, pia niliambiwa nitafute hela ya glovu, niligoma, nadhani hiyo ndiyo imekuwa chanzo,” alisema Ndambile. Alisema kuwa ili kumpata mshindi sahihi, bora pambano hilo lilirudiwe ili mshindi apatikane kwa mujibu wa taratibu na siyo kwa njia iliyotumika ambayo lengo lake ni kuharibu rekodi na kutengenza za bondia mwigine

RC TABORA ATAKA MAELEZO ALIYECHOMA MOTO KATIKA CHUO CHA ARDHI

0
0
Na Tiganya Vincent.

SERIKALI Mkoa wa Tabora imeagiza kutafutwa na kuchukiwa hatua kali na kupata maelezo ya watu waliohusika na uchomaji moto katika maeneo ya Chuo cha Ardhi Tabora na kusababisha uharibifu mkubwa wa mistu asili na miti iliyokuwa imepandwa katika eneo hilo kama hatua za uhifadhi wa mazingira.

Kauli hiyo imetolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri baada ya kukuta eneo la Chuo hicho likiwa limeungua na moto wakati wa ziara ya ya kukagua vitalu vya kuoteshea miti ikiwa ni maandilizi ya zoezi la upandaji wa miti.

Alisema kuwa haiwezekani wananchi wanajitoa kwa moyo kupanda miti katika kampeni inayoendelea kisha watu wachache wanaamua kuua miti na kuharibu mazingira.

Mwanri aliongeza kuwa inasikitisha kuona hata sehemu za Taasisi za umma kama hiyo zinaacha moto unaunguza miti na wakufunzi wapo, wanachuo wapo bila kuchukua hatua ya kuuzima na kuwasaka waliohusika.

Alisema kitendo kinaonyesha jinsi wao nao wanahusika kwa namna moja au nyingine katika kuchangia uharibifu ulifanyika katika Chuo chako.
Kufuatia kitecho hicho Mkuu wa Mkoa alimwagiza Afisa Mazingira wa Manispaa ya Tabora kwenda kwa Mkuu wa Chuo kupata maelezo nini kilitokea na hatua zilizochukuliwa kwa wahusika na kama hawachukua hatua kwa wahusika basi Sheria za Mazingira zichukue mkondo wake.

Aliongeza kuwa pamoja na hatua hiyo zitakazochuliwa aliagiza uongozi wa Chuo hicho kuhakikisha wanarudishia miti yote iliungua mapema iwezekanavyo.“Nimesikitishwa na kitengo nilichokiona katika eneo la Chuo cha kuchoma moto na kuunguza miti ,kiwa kwa watu wasomi ambao wanatakiwa wawe mfano wa utunzaji wa mazingira wao ndio wanakuwa wa kwanza kuharibu mazingira kwa kuchoma moto…nimesikitishwa sana” alisema Mkuu huyo wa Mkoa.

Naye Afisa Mazingira wa Manispaa ya Tabora William Mpangala alisema hadi hivi sasa Ofisi yake imekwishakamata watu 27 kwa makosa ya uchomaji moto ovyo na kuwapiga faini ya kuanzia 50,000/-

Alisema kuwa viongozi wa Taasisi wafahamu kuwa kunapotokea moto katika maeneo yao wakishindwa kuwakamata wahalifu wao watawajibika kulipa faini ya uharibifu wa mazingira ya kuanzia shilingi 500,000/-.

Utamaduni wa uchomaji moto ovyo katika Mkoa wa Tabora unaoenekana kama kama jambo la kawaida wengine wakitaka malisho mapya ya mifugo na mengine wakati wa kuandaa mashamba na wakati wa kulina asali.
Jambo hilo limekuwa likimuumiza kichwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati mwingine kulizamika kuamuka usiku kuwavizia watu wanaowasha moto ovyo.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Tabora ameziagiza Halmashauri zote mkoani kuhakikisha vitalu vya miti waliyotayarisha kwa ajili awamu ya pili ya upandaji mkoani hapa inayomiti ya kutosha kwa kadri walivyokubaliana.
Alisema kuwa Manispaa ya Tabora inapaswa kuhakikisha imeotosha miche 500,000, Nzega Mji na Wilaya miche 500,000 na nyingine zilizobaki 250,000 kila moja.

Mwanri idadi hiyo ni nje ya ile ambapo kila mkazi wa Tabora atakiwa kupanda au kupandiwa na mzazi wake kama ni mtoto miti miwili kila mmoja.

Balozi Asha-Rose Migiro awatembelea Watanzania waishio Birmingham

0
0
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mheshimiwa Asha-Rose Migiro alifanya ziara ya kuwatemebelea Watanzania waishio katika mji wa Bimingham na vitongoji vyake tarehe 28/8/2017.

Pamoja na ziara hiyo, Mhe. Balozi Migiro alipata nafasi ya kushiriki katika uzinduzi rasmi wa Jumuiya ya Watanzania waishio katika mji huo wa Birmingham na Vitongoji vyake, ijulikanayo kama Watanzania wa Birmingham na nchi nyeusi -(Tanzanian's in Birmingham and Black Country - WBBC).

Mhe. Balozi aliwapongeza na kutoa wito kwa  Watanzania hao kuwa na kushirikiano wa karibu na Ofisi za Ubalozi kupitia Viongozi wao. Pia alihimiza umuhimu wa Wana diaspora kuwa wamoja na kushirikiana bila kubaguana.

Katika Mkutano huo, kulifanyika hafla ndogo ya kuchangia Jumuiya hiyo pamoja na chakula cha pamoja kwa kumshukuru Mhe.Balozi kwa kutenga muda wake na kuwatembelea.

Sambamba na hafla hiyo Mheshimiwa Balozi Asha-Rose Migiro pia alizindua rasmi Jumuiya hiyo, na kukabidhiwa Katiba yao itakayo tumika kuendesha shughuli za kila siku za Jumuiya hiyo.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Balozi Migiro akiwahutubia Watanzania waliohudhuria katika mkutano huo kushoto kwake ni katibu wa Jumuiya ya Watanzania waishio Birmingham na Black Country Dkt. Hassan Khalfan Hamidu, anayefuatia ni Mbunge kutoka jimbo la Stafford wa chama cha Conservative Jeremy John Lefroy na nyuma ya Balozi ni Mwambata wa Uhamiaji Ubalozini Bw. Magnus Ulungi.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Balozi akiwa na viongozi wa Jumuiya ya Watanzania waishio Birmingham Mwenyekiti wa WBBC Bw. Renatus Mgetta(Pili kulia), Katibu wa Baraza la Ushauri Brian M. Ngelangela.; Kutoka kushoto mwa picha ni Katibu Mwenenzi Dr. Dr. Othman M., Katibu wa Jumuiya Dr. Hassan Khalfan na Kiongozi wa Kamati ya Katiba, Uratibu na Mwongozo Bw. Nelson Kampa.
 Mbunge kutoka jimbo la Stafford wa chama cha Conservative Jeremy John Lefroy akihutubuia katika mkutano huo wa wanadispora.
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mhe. Balozi Migiro akijumuika na watanzania katika kucheza muziki
 Balozi Asha-Rose Migiro akizungumza na Mwenyekiti wa British Tanzania Society (BTS) Prof. Andrew Coulson wakati wa mkutano huo.
Mheshimiwa Balozi, akijumuhika na Watanzania hao katika chakula cha pamoja

Dawasa kujenga miundombinu ya majitaka jijini Dar es Salaam.

0
0

Na Agness Francis, Blogu ya Jamii.

UZALISHAJI wa Maji Safi kunahitaji kuwepo na miundombinu ya maji taka ambayo yanazalishwa na maji safi katika kutunza mazingira pamoja na afya kwa wananchi wanatumia maji safi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam, Mhandisi Romanus Mwang’ingo amesema kuwa wameanza kufanya utekelezaji wa miradi ya ukusaji na uondoshaji wa majitaka kwa kuanzisha miradi mitatu ya kisasa ya kusafisha majitaka hayo.

Amesema Miradi hiyo itakwenda sambasamba na uzalishaji wa mabomba ya kukusanya majitaka hayo kwa kujenga miundombinu katika maeneo ya Jangwani, Mbezi Beach pamoja na Kurasini.

Mwandisi Mwang’ingo amesema ujenzi wa miundombinu hiyo itaongeza kiwango cha kusafisha majitaka kwa asilimia 30 ifikapo 2020 kutoka kiwango cha asilimia 10 iliyopo sasa itakayogharimu Dola za Kimarekani Milioni 600 katika mwaka wa fedha 2017/2018.

Amesema mfumo wa majitaka wa Jangwani utakapokamilika utakuwa na uwezo wa kusafisha majitaka hayo mita za ujazo 200,000 kwa siku.

Mabomba yenye urefu wa kilomita 376 yatajengwa katika mradi utakaonzia kunazia Ubungo hadi Jangwani,Kinondoni, Mwananyamala, Msasani Katikati ya Jiji na Ilala.

Mhandisi Mwang’ingo amesema kuwa awamu ya kwanza ya ujenzi itahusisha sehemu sehemu itakayoweza kusafisha mita za ujazo 25,000 kwa siku na mabomba yenye urefu wa kilomita 17.43 yatakayojengwa eneo la magomeni.

Aidha katika awamu ya kwanza,bomba linalomwaga majitaka baharini litaacha kutumika na badala yake majitaka hayo yatakwenda kusafishiwa katika mtambo huo ambapo mtambo huu unajengwa kati ya ushirikiano wa Serikali ya Tanzania na Serikali ya Korea kupitia mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Exim ya Korea unaotarajiwa kugharimu Dola za Kimarekani milioni 90 ambazo tayari zimepatikana.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam, Mhandisi Romanus Mwang’ingo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari juu ya mikakati Dawasa ya maji safi na majitaka leo jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Maelezo,Rodney Thadeus kulia ni Meneja Mawasiliano Dawasa, Neli Msuya.
Meneja wa Mawasiliano wa Dawasa, Neli Msuya akizungumza juu miradi inajengwa na Dawasa katika maeneo mbalimbali Dar es Salaam na Sehemu ya mkoa wa Pwani leo jijini Dar es Salaam

PATAKUWA HAPATOSHI TRAVERTINE HOTEL-MAGOMENI

0
0

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MAKAMU WA RAISI WA KAMPUNI YA UTENGENEZAJI MELI UFARANSA

0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watu wote wenye nia ya kutaka kuwekeza katika miradi mbalimbali nchini Tanzania kuhakikisha wanafuata sheria, kanuni na taratibu.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumanne, Agosti 29, 2017) wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais (Uendelezaji Bishara) wa kampuni ya PIRIOU, Bw. Michel Perrin. Waziri Mkuu amekutana na Bw. Perrin jijini Paris nchini Ufaransa kupitia ofisi ya ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa. Kampuni ya PIRIOU inataka kuja nchini kuwekeza katika utengenezaji na ukarabati wa meli.

Akizungumza na muwekezaji huyo Waziri Mkuu alimshukuru kwa nia yake ya kutaka kuwekeza nchini, ambapo alimtaka afuate sheria, kanuni na taratibu za uwekezaji nchini. “Tanzania ni sehemu nzuri ya uwekezaji kwa sababu kuna fursa nyingi. Pia ni nchi yenye amani na utulivu wa kisiasa pamoja na mazingira mazuri ya uwekezaji hivyo nakukaribisha sana.”

Kwa upande wake Bw. Perrin amesema ameamua kuja kuwekeza nchini kwa kuwa Tanzania ni nchi salama na kwamba anauhakika wa kupata soko ndani ya nchi pamoja na mataifa jiraji. Amesema anaamini uwekezaji wake nchini Tanzania utakuwa na tija, hivyo ameahidi kufanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na Serikali na pia atahakikisha anafuata sheria zote za nchi.

Pia Bw. Perrin alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Balozi Samwel Shelukindo kutokana na ushirikiano anaompa kuhusu masuala ya uwekezaji nchini. Naye Balozi Shelukindo amesema atahakikisha anaendelea kutafuta wafanyabiashara mbalimbali na kuwashawishi waje kuwekeza katika sekta mbalimbali nchini

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU, JUMANNE, AGOSTI 29, 2017.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Makamu wa Raisi wa Kampuni (Uendelezaji Bibiashara) wa Kampuni ya PIRIOU ya utengenezaji na ukarabati wa meli nchini Ufaransa. Bwana Michel Perrin .kulia ni Balozi wa Tanzania Nchini Ufaransa Bwana Samweli Shelukindo.Waziri Mkuu amekutana naye leo Agost 29/2017 Parisi Ufaransa.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI, KARANI WA MARAZA MAREHEMU HASSAN RASHID SHEBUGE AKUMBUKWA

0
0
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan na Katibu Mkuu Kiongozi pamoja na mawaziri wakisimama kwa heshima kumkumbuka aliyekuwa Karani wa Baraza la Mawaziri Marehemu Hassan Rashid shebuge aliyefariki mwezi Julai mwaka huu, kabla ya kuanza kwa kikao hicho kilichofanyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 29, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza kikao cha baraza la Mawziri kulu jijini Dar es salaam leo Agosti 29, 2017

MIVARF yafanikiwa kupunguza umaskini wa kipato na kuimarisha uhakika wa Chakula

0
0

MCHUNGAJI WA GHANA KUTOA HUDUMA KATIKA KANISA LA MOTO HALISI LILILOPO TABATA SEGEREA KWA BIBI JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

0
0
 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akizungumza na waumini wa Kanisa la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International') lilopo Tabata Segerea kwa Bibi jijini Dar es Salaam mara baada alipo wasiri hapa nchini majira ya saa 6: 30 na kuzungumza machache na waumini wa kanisa hilo kuhusu huduma atakayoitoa kwa waumini hao.

MWAZILISHI na mchungaji Mkuu wa kanisa  la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International'), lililopo Tabata Segerea kwa Bibi
,Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana amewasili hapa kwaajili ya
  kuwaletea siku tatu za huduma ya ujazo wa upako.

Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumkaribisha hapa nchini mchungaji huyo kutoka nchini Ghana, Mchungaji Mwenyeji, Innocent Ikechukwu amesema kuwa wananchi wajitokeze ili kupata maada mbalimbali za ukombozi na mafanikio.

Amesema huduma zitatolewa kwa siku tatu kuanzia leo Jumanne saa 11:00 jioni hadi alhamisi ambapo wahapingani kabisa na muda wa kazi hapa nchini kutokana na muda huo watu wengi watakuwa wametoka makazini.

Huduma hiyo itatolewa kwa lengo la kusaidia wanachi wenye matatizo mbalimbali, ili kupata upanyaji na kumtumaini Mungu,pamoja na Ukombozi na Mafanikio ambapo wanawaalika watu mbalimbali kuhudhulia mkutano huo ambapo mtoa maada katika siku tatu mfululizo ili kujipatia huduma za ukombozi na mafanikio.

 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akiwapungia mkono waumini wa kanisa la Pure Fire miracles Ministries International jijin Dar es Salaam leo mara baada alipowasili jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mchungaji Mwenyeji, Innocent Ikechukwu.
 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akiwasalimia waumini wa Kanisa la Moto halisi jijini Dar es Salaam leo.
 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akisalimiwa na muumini wa kanisa la Moto halisi jijini Dar es Salaam leo.
Kikundi cha Mtalumbeta wakitumbuiza katika ujio wa
Mwanzilishi na mchungaji Mkuu wa kanisa  la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International') mara baada alipowasili hapa nchini jijini Dar es Salaam leo.
 Waumini wakanisa la Pure Fire miracles Ministries International' wakimshangilia na kumkaribisha
Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana mara baada alipowasili kanisani hapo jijini Dar es Salaam leo.
 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana wakimshangilia mwanzilishi wa kanisa lao mara baada alipowasili jijini Dar es Salaam leo.
 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akizungumza na waumini  mara baada alipowasili jijini Dar es Salaam leo kushoto ni Mkalimani.
 Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kuwasili katika Kanisa la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International') lilopo Tabata Segerea kwa Bibi jijini Dar es Salaam.
 Mchungaji Mwenyeji, Innocent Ikechukwuakizungumza wakati wa kumkaribisha  Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana mara baada alipo wasili kanisani hapo jijinio Dar es Salaam leo.
Pia amemshukuru kwa kuitikia wito wake kuja hapa nchini kutoa huduma ya neno la Mungu pamoja na ukombozi wa Mafanikio ya wanajamii watakao hudhuria katika huduma kanisani hapo.
Baadhi ya waumini wa Kanisa la Moto halisi (Pure Fire miracles Ministries International') lilopo Tabata Segerea kwa Bibi wakimuaga Mkuu wa Kanisa hilo, Dk. Enoch Aminu kutoka nchini Ghana mara baada ya kufika na kuongea na waumini hao.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.

WATU SITA WAFARIKI KWA AJALI YA LORI KIJIJI CHA KATIKA KIJIJI CHA KIJOTA, SINGIDA.

0
0
Watu sita wamefariki dunia huku wengine 42 wakijeruhiwa baada ya lori lenye namba za usajili T.806 AEL aina ya scania mali ya Abdalla Mussa (39) mfanyabiashara mkazi wa Mwenge mjini Singida, kuacha njia na kupinduka katika Kijiji cha Kijota, Singida.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Debora Magiligimba amesema ajali hiyo imetokea Agosti 27 mwaka huu saa 1.30 usiku katika kijiji cha Kijota wakati likitokea mnadani katika kijiji cha Mtinko Singida vijijini, likielekea Singida mjini.

ACP Magiligimba ametaja chanzo cha ajali kuwa ni uzembe wa dereva wa lori hilo Jumanne Kidanka (32) Kamanda huyo amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva ambaye hakuwa makini akiwa anaendesha lori hilo lililosheheni abira na mizingo mingi.

Amewataja waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni Haji Jumanne (35), Mikidadi Mohammed (40) wote wawili wakazi wa kijiji cha Mrama na Musa Salimu (30) mkazi wa kijiji cha Mwakiti.

ACP Magiligimba amewataja wengine kuwa ni Allen Mwangu (38) mkazi wa wilaya ya Ikungi, Lucas Stephano (40) mkazi wa kijiji cha Mrama na Sharifa Omari (19) mkazi wa kijiji cha Ilongero.

Ameongeza kuwa majeruhi 20 wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida, kumi wamelazwa hospitali ya misheni ya Mtinko na wanne ambao hali zao ni mbaya, wamelazwa katika hospitali ya misheni ya Hydom mkoani Manyara.

Ameeleza kuwa baadhi ya majeruhi walipatiwa matibabu na kurejea makwao huku wengine waliolazwa wamevunjika mikono, miguu na sehemu mbalimbali ya miili yao.

“Hawa wenye hali mbaya ni Fadhili Jumanne (33) mkazi wa Kibaoni mjini Singida, Mikidadi Hamisi, Jafari Hamisi na Idrisa Ibrahimu, wote wamevunjika miguu. Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye hospitali misheni Mtinko”, amesema.
 Mmoja wa majeruhi akipatiwa matibabu ya mkono katika hospitali ya Mkoa wa Singida mara baada ya kupata ajali ya lori iliyoua watu 6 katika kijiji cha Kijota Singida.
 Mmoja wa majeruhi akiwa amelazwa huku akiendelea kupatiwa matibabu ya mkono katika hospitali ya Mkoa wa Singida mara baada ya kupata ajali ya lori iliyoua watu 6 katika kijiji cha Kijota Singida.
Baadhi ya ndugu na jamaa wa majeruhi wa ajali ya lori iliyoua watu sita wakiwa nje ya wodi za wagonjwa katika hospitali ya Mkoa wa Singida.

NAIBU WAZIRI ANGELINA MABULA AFANYA ZIARA MKOANI GEITA, ASISITIZA UKUSANYAJI WA MAPATO YA ARDHI NA MAJENGO

0
0
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula,akiangalia ramani ya Kijiji cha Bukandwe ambacho kipo kwenye Wilaya ya Mbongwe Mkoani Geita. Mkuu wa Wilaya ya Mbongwe Mathar Mkupasi akiagana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula wakati alipotembelea kijiji cha Bukandwe. Mkuu wa Wilaya ya Bukombe ,Josephat Maganga akisoma taarifa fupi ya Wilaya ya Bukombe kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula akikagua na kupatiwa maelezo na afisa ardhi mteule Joseph Kimondo . Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula ,akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Bukombe.PICHA ZOTE NA JOEL MADUKA .
 
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula akiwasili kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Geita na akisalimiana na kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa huo Nyuma yake ni mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga 
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula,akisaini kwenye kitabu cha wageni ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Mbongwe. Mkuu wa Wilaya ya Mbongwe Mathar Mkupasi akisoma taarifa ya ardhi na maendeleo ya ukusanyaji wa mapato ambayo yanatokana na ardhi pamoja majengo yaliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya Hiyo. Watumishi wa halmashauri ya Mboongwe pamoja na kamati ya Ulinzi na usalama wakifuatilia kikao cha Naibu waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe Elias Kayandabila akionesha mchoro na ramani ya nyumba ambazo zinatarajia kujengwa na shirika la Nyumba la Taifa. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbongwe Elias Kayandabila akikabidhi ramani kwa meneja wa shirika la Nyumba Mwanza, Simiyu na Geita Mhandisi Benedict Kilimba . Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Angeline Mabula,akikagua mafaili kwenye ofisi za Ardhi za Wilaya hiyo.

DC WA BUHIGWE KANALI GAGUTI AFANYA UKAGUZI WA KUSHITUKIZA MPAKANI MWA TANZANIA NA BURUNDI

0
0

Na Rhoda Ezekiel

MKUU wa wilaya Buhigwe mkoa Kigoma, Kanali Marco Gaguti ameendesha zoezi la kustukiza la ukaguzi wa hali ya ulinzi na usalama wa mpaka wa Tanzania na Burundi na kuridhika kwamba hali ya ulinzi na usalama katika mpaka huo ni ya kuridhisha.

Katika ukaguzi huo uliofanyika juzi usiku, kiongozi huyo akiambatana na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo alitembelea vijiji vya Kibande,Nyamugali na Mnanila ambako aliambaa ambaa na ukingo wa Mto malagarasi unaotengenisha nchi za Tanzania na Burundi kuona hali halisi ya ulinzi na usalama na kuona hali ya usafirishaji wa bidhaa za magendo kupitia maeneo hayo.
Akizungumza na waandishi wa habari majira ya saa tisa alfajiri baada ya kukamilisha zoezi hilo, Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa ulinzi shirikishi uliowekwa kuanzia ngazi za vitongoji na uelimishaji jamii kuhusu hatua za kuimarisha ulinzi maeneo ya mpakani imekuwa na mafanikio makubwa na kwamba ofisi yake itaendelea kusimamia hali hiyo kuhakikisha ulinzi na usalama wa kudumu unakuwepo wakati wote.

Sambamba na kuangalia hali ya ulinzi na usalama pia zoezi hilo lilihusisha upekuzi katika baadhi ya nyumba zilizokuwa zinahisiwa kuhifadhi wahamiaji haramu na kutembelea maeneo ya mpaka ambayo yanatuhumiwa kwa usafirishaji wa bidhaa za magendo kwenda nchini Burundi na zinazotoka huko kuingia mkoani Kigoma.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa amekuwa akifanya ukaguzi huo mara kwa mara na kwamba mafanikio ni makubwa ingawa alikiri kuwepo kwa changamoto ya baadhi ya wananchi na viongozi wa vijiji katika maeneo hayo ya mpakani kushirikiana na wahalifu kutenda makosa ya uingizaji wa bidhaa zamagendo na wahamiaji haramu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya Buhigwe, Anosta Nyamoga alisema kuwa zoezi la ukaguzi wa mpaka wakati wa usiku limesaidia kupunguza vitendo vya usafirishaji wa bidhaa mbalimbali hasa mazao kwenda nchini Burundi bila kulipiwa ushuru.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa vitendo vya usafirishaji wa mazao na bidhaa bila kulipiwa ushuru vimekuwa vikiiokosesha mapato halmashauri yake na kwamba mkakati wa kuziba mianya ya upotevu huo wa mapato ya serikali inaendelea kufanyiwa kazi.
Viewing all 46205 articles
Browse latest View live




Latest Images