Quantcast
Channel: JIACHIE
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AAGIZA WAENDESHA BODABODA WOTE KUNUNUA KOFIA NGUMU NDANI YA MWEZI MMOJA

$
0
0

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akizungumza na waendesha bodaboda na baiskeli 'daladala' leo mjini Shinyanga.Kulia ni Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule.Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Mheshimiwa Josephine Matiro akizungumza wakati wa kufunga kikao hicho.
Mkazi wa Shinyanga Mjini akieleza shida yake kwa Waziri wa Mambo ya Ndani,Mheshimiwa Mwigulu Nchemba baada ya kikao kufungwa.


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ameagiza waendesha bodaboda wote nchini kuhakikisha kuwa wanakuwa na kofia ngumu ‘Helmet’ ndani ya mwezi mmoja baada ya hapo hatua kali zitachukuliwa. 

Mheshimiwa Nchemba ametoa agizo hilo leo Jumamosi Agosti 26,2017 mjini Shinyanga wakati akizungumza na waendesha bodaboda na baiskeli 'daladala' zaidi ya 300 wanaofanya shughuli zao katika manispaa ya Shinyanga. 

Alisema kosa la kutovaa kofia ngumu litawahusu wamiliki wa bodaboda,waendesha bodaboda pamoja na abiria ambao kwa pamoja watawajibika kila mmoja kwa nafasi yake. 

“Hili litafsiriwe vizuri kila eneo katika nchi yetu,kwanza kabisa kama mmiliki hajaweka kofia mbili,bodaboda ikikutwa haina kofia mbili,tatizo lile linaenda kwa mmiliki,pili kama mwendesha bodaboda amepewa kofia mbili halafu akaamua kuziacha huyo ana kosa”,alieleza. 

“Tatu, kama mwendesha bodaboda ana kofia zote mbili lakini mbebwaji/abiria hataki kuvaa kofia,mwacheni mwenye pikipiki aende na pikipiki yake,huyo mbebwaji atakuwa na kosa la kuhatarisha maisha yake ili kila mmoja atimize wajibu wake”,aliongeza Nchemba. 

Mheshimiwa Nchemba pia alisisitiza umuhimu wa abiria wanaopanda katika bodaboda kukaa mkao wa kiume ili kuepusha ajali za barabarani. 
Katika hatua nyingine Waziri huyo amepiga marufuku ukamataji wa bodaboda unaofanywa na askari polisi kwa kufukuzana na waendesha bodaboda kwani inachangia kutokea kwa ajali. 

“Tumeelekeza ukamataji wa kistaarabu,ukamataji huu wa kistaarabu ufanyike kwa nyinyi mtimize wajibu ili kuwe na tofauti ya aliyekosa na ambaye hajakosa,na sisi askari lazima tutofautishe aliyekosa na ambaye hajakosa ili tuwe marafiki na hawa watu”,alisema Nchemba. 

“Tunafanya haya kwa ajili ya maisha yenu,hatuna upendo zaidi ya kuokoa maisha yenu,hatutaki watu wapoteze maisha kwa sababu ya uzembe wa waendesha bodaboda ama abiria”,aliongeza Nchemba. 

Naye Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule alisema kikao hicho cha Waziri wa Mambo ya Ndani ni sehemu ya utekelezaji wa majukumu ya jeshi la polisi katika zoezi la utoaji elimu kuhusu masuala ya usalama barabarani. 

“Hivi karibuni katika mkutano wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga,uliolenga kusikiliza kero za wananchi,kuna mambo yaliibuliwa ikiwemo la waendesha bodaboda kutofahamu matumizi mazuri ya Mzunguko wa barabara ‘Round About’ hivyo tunatoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya Round about”,alieleza Kamanda Haule. 

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mheshimiwa Zainab Telack,alisema ajali za barabarani zimepungua kutokana na waendesha bodaboda kuendelea kuzingatia sheria za usalama barabarani. 

Mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini,Mheshimiwa Stephen Masele (CCM) aliwataka waendesha bodaboda kufuata sheria za usalama barabarani na askari polisi waache kutumia nguvu kubwa kukabiliana na waendesha bodaboda.
MSIKILIZE HAPA WAZIRI MWIGULU NCHEMBA AKITOA MAAGIZO LEO SHINYANGA
ANGALIA PICHA ZA MATUKIO
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akiwasisitiza waendesha bodaboda kuzingatia sheria za usalama barabarani.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akizungumza.
Waendesha bodaboda na baiskeli mjini Shinyanga wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Ndani,Mheshimiwa Mwigulu Nchemba.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akizungumza na waendesha bodaboda na baiskeli.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga,Mheshimiwa Zainab Telack akizungumza wakati wa kikao hicho.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule akizungumza wakati wa kikao hicho.
Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule akieleza namna jeshi la polisi linafanya ili kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua mkoani Shinyanga.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Shinyanga,Anthony Masanzu akisisitiza jambo wakati kikao hicho.
Mbunge wa jimbo la Shinyanga Mjini,Mheshimiwa Stephen Masele (CCM) akizungumza katika kikao hicho.
Kikao kinaendelea.
Mmoja wa waendesha akiuliza swali kwa waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mheshimiwa Mwigulu Nchemba.

Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

DKT. SHEIN KATIKA HAFLA YA KUCHANGIA MFUKO WA MAENDELEO YA UWT ZANZIBAR.

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipowasili katika hafla ya Chakula cha Hisani kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar iliyofanyika jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 27/08/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipowasili katika hafla ya Chakula cha Hisani kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar iliyofanyika jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 27/08/2017.
Baadhi ya Viongozi mbali mbali na Wafanyabishara waliohudhuria katika hafla ya Chakula cha Hisani kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar iliyofanyika jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.] 27/08/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akiwa na Viongozi mbali mbali katika hafla ya Chakula cha Hisani kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar iliyofanyika jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,ambapo kikundi cha Taarab cha Culture Muzical Club kilitumbiza katika hafla hiyo,[Picha na Ikulu.] 27/08/2017.
Baadhi ya Viongozi mbali mbali na Wafanyabishara waliohudhuria katika hafla ya Chakula cha Hisani kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar wakipata burudani ya Muziki uliopigwa na Kikundi cha Culture Muzicul Club jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.] 27/08/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akimkabidhi Cheti Bw.Jacob Moywaywa kutoka Hotel ya Breezes Beach akiwa ni miongozi mwa wachangiaji wa kiwango cha juu katika kuchangia Mfuko wa Maendeleo ya UWT Zanzibar katika hafla ya chakula cha hisani iliyofanyika jana ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]27/08/2017.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akimkabidhi Cheti Mkurugenzi Mkuu Abdukadir Mohamed Bujeti kutoka MECCO akiwa ni miongozi mwa wachangiaji wa kiwango cha juu katika kuchangia Mfuko wa Maendeleo ya UWT Zanzibar katika hafla ya chakula cha hisani iliyofanyika jana ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]27/08/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akimkabidhi Cheti Bw.Ali Kilupy kutoka Kendwa Roky Hotel akiwa ni miongozi mwa wachangiaji wa kiwango cha juu katika kuchangia Mfuko wa Maendeleo ya UWT Zanzibar katika hafla ya chakula cha hisani iliyofanyika jana ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.]27/08/2017.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) alipokuwa akipokea zawadi maalum kutoka kwa Dkt.Maua Abeid Daftari Mwenyekiti wa kamati ya kuhamasisha uchangiaji wa mfuko wa maendeleo ya UWT katika hafla ya Chakula cha hisani cha kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja jana,[Picha na Ikulu.] 27/08/2017.

:DC TUNDURU APIGA MARAFUKU NGOMA ZA UNYAGO.

$
0
0
Mkuu wa wilaya ya Tunduru JUMA HOMERA ,amepiga marafuku kwa wazazi wote kuto kujihusisha na masuala ya kimila hususani katika kushiriki ngoma za usiku hali inayopelekea kutokea kwa mimba za utotoni.

MFUKO WA MAENDELEO WA JUMUIYA YA UWT ZANZIBAR WACHANGIWA

$
0
0
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akitia saini Picha yake iliyochorwa ambayo ilipigwa mnada kwa Viongozi na Wafanyabiashara mbali mbali na kununuliwa kwa shingi za Kitanzania Milliomi tatu,ambayo Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya Mecco Bw.Abdukadir Mohamed Bujet (kulia) ameinunua picha hiyo katika hafla ya Kuchangia Mfuko wa Maendeleo ya UWT Zanzibar iliyofanyika jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) alipokuwa akikabidhi Picha ya Mji wa Zanzibar Kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ikiwa ni miongoni mwa Picha mbali mbali zilizopigwa mnada kufanikisha kuchangia Mfuko wa maendeleo ya UWT Zanzibar hafla iliyofanyika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni Mjini Unguja,(kushoto) Mama Asha Suleiman Mke Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein iliyochorwa ikipigwa mnada kwa Viongozi na Wafanyabiashara mbali mbali waliohudhuria katika hafla ya Kuchangia Mfuko wa Maendeleo ya UWT Zanzibar iliyofanyika jana katika ukumbi wa Zamani wa Baraza la Wawakilishi Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 26/08/2017.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA CUBA

$
0
0

*Asisitiza nia ya kufungua ubalozi nchini humo

 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Cuba, Bi. Gladys Bejarano na kumuhakikishia ufunguzi wa ofisi za ubalozi wa Tanzania nchini humo.

Amesema Tanzania inayatambua na kuyathamini mahusiano mazuri ya kidiplomasia, kisiasa, kiuchumi, kielimu, kiafya na kiutamaduni kati yake na Cuba, hivyo inatarajia kufungua ubalozi nchini humo ili kurahisisha utendaji wa kazi za kibalozi.

Waziri Mkuu alikutana na Bi. Gladys jana jioni (Jumamosi, Agosti 26, 2017) wakati alipokuwa akihitimisha ziara yake ya kikazi nchini Cuba. Malengo ya ziara yalikuwa ni kuimarisha na kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

“Tunatambua mahusiano mazuri yaliyopo kati Tanzania na Cuba, ambayo yalikuwepo kuanzia Serikali ya Awamu ya kwanza chini ya uongozi wa Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Nyerere, hivyo lazima tufungue ofisi za ubalozi na tutamleta balozi wetu hapa.”

Pia Waziri Mkuu ameishukuru Serikali ya Cuba kwa ujenzi wa kiwanda cha dawa za kuulia vijidudu vya maralia pamoja na ufadhili wa masomo ya udaktari inaoutoa kwa wanafunzi wa Kitanzania ambao wanasoma katika vyuo mbalimbali nchini humo.

Hata hivyo aliiomba Serikali hiyo iendelee kutoa ufadhili wa masomo kwa madaktari hao hadi ngazi ya shahada ya uzamili kwa sababu Serikali ya Tanzania inawahitaji madaktari bingwa wengi kwani walioko nchini ni wachache.

Kwa upande wake, Bi. Gladys alimshukuru Waziri Mkuu kwa kufanya ziara nchini Cuba na alimuhakikishia kwamba uhusiano wa Serikali yake na Serikali ya Tanzania utaendelea kuimarishwa kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Alisema Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli inafanya jitihada kubwa za kuhakikisha uchumi wake unakua kwa kasi jambo ambalo ni tofauti na mataifa mengine. “Nawapongeza kwa hatua za kimaendeleo mnazozifanya.”

Makamu huyo wa Rais alisema Serikali ya Cuba itaendelea kushirikiana na Tanzania katika uboreshaji wa Sekta za Afya, Utamaduni, Kilimo, Uchumi na Elimu. Kuhusu ombi la kuongeza ufadhili wa shahada ya uzamili kwa madaktari  alisema amelipokea na atalifanyia kazi.

Awali Balozi wa Tanzania nchini Canada, ambaye anasimamia na nchi ya Cuba, Balozi Jack Zoka alisema Serikali ya Cuba ni miongoni mwa nchi zinazoshirikiana na Tanzania katika uboreshaji wa shughuli za maedndeleo, hivyo uwepo wa ofisi za ubalozi nchini humo utazidi kuimarisha mahusiano.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMAPILI, AGOSTI 27, 2017.
  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo ya Kikazi na Makamu wa Rais wa Cuba, Bi. Gladys Bejarano. katika Mji wa Havana Nchini Cuba jana August 26/2017.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo ya Kikazi na Makamu wa Rais wa Cuba, Bi. Gladys Bejarano. katika Mji wa Havana Nchini Cuba jana August 26/2017.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

DKT MAHENGE KUWAFUNDA MAAFISA UGANI MOANI RUVUMA.

$
0
0
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma DKT BILINITH MAHENGE amewataka wadau wa kilimo na mafisa ugani kuhakikisha wanatoa taarifa sahihi juu ya uzalishaji wa zao la soya ambalo limeonekana kuwa na tija katika mikoa ya mbeya,njombe na ruvuma kutokana na hali ya hewa iliyopo katika mikoa hiyo.

KUNDI LA NYOTA YA ASUBUHI KUFANYA VIDEO NA CHRISTIAN BELLA

WIZARA YA ARDHI YATAMBULISHWA NA KOREA MRADI WA KUCHORA RAMANI ZA KIJIOGRAFIA

$
0
0
 Timu ya utambulisho wa Mradi wa kuchora Ramani za kijiografia kutoka Korea na baadhi ya watendaji wa Idara ya Upimaji wa Ramanni (Wizara ya Ardhi) katika Mkutano wa utambulisho wa Mradi.
Ugeni kutoka Taasisi ya Taifa ya Kijiografia- Korea, waliofika kutambulisha Mradi wa kuchora Ramani za kijiografia utakaoanza 2018, katika picha ya pamoja na baadhi ya watenfaji wa Wizara ya Ardhi.

Ugeni wa Wakorea, kutoka Taasisi ya Taifa ya masuala ya kijiografia umetambulisha rasmi mradi wa kuchora ramani za kijiografia kwa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Ugeni huo uliopokelewa na Idara ya Upimaji na Ramani katika Wizara ya Ardhi, umehusisha timu ya Maafisa kumi kutoka nchini Korea. Akizungumza na wawakilishi wa Idara ya Upimaji na Ramani; Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Taasisi hiyo; Bwn. Hynu-Hee Joo amesema mradi huo unaojumuisha nchi tatu, yaani Tanzania, Zambia na Msumbiji unategemewa kuanza rasmi 2018.

Mradi wa kuchora ramani za kijiografia upo chini ya ufadhili wa nci ya Korea kupitia Benki ya Dunia na Umoja wa Kamisheni ya Afrika.

Na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

MPOGORO AFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA MAKATIBU WA UVCCM MIKOA YA TANZANIA BARA NA VISIWANI.

$
0
0



Naibu katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi ndugu Rodrick mpogoro akifungua Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaam.
Mwenyekiti wa umoja wa Vijana na mjumbe wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi Ndg:Sadifa Juma khamisi akizungumza katika Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaam
Kaimu katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi shaka Hamdu Shaka akizungumza katika Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaam

washiriki wa mafunzo elekezi wakifuatilia mafunzo 
mshiriki Katibu wa umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa kirimanjaro ndg; abdulrahim hamid akiuliza swali wakati wa Mafunzo elekezi kwa makatibu wa umoja wa Vijana wa CCM mikoa ya Tanzania bara na Visiwani katika ukumbi wa kamati kuu ofisi ndogo ya Ccm Lumumba dar es salaa.(PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI)

MTUHUMIWA WA UJAMBAZI AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI WAKATI AKITOROKA MKOANI SINGIDA.

$
0
0
Mkazi wa kijiji cha Shiponga – Hanang Mkoani Manyara anayedaiwa kuwa jambazi, Hamisi Athumani (32), amefariki dunia baada ya kupigwa risasi kiunoni na askari polisi wakati akiwa katika harakati ya kutoroka.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani hapa, ACP Debora Magiligimba, amesema tukio hilo limetokea Agosti 25 mwaka huu saa nane mchana, huko katika kijiji cha Mgori tarafa ya Ngimu wilaya ya Singida.

Amefafanua kuwa Hamisi (marehemu) alipigwa risasi na askari polisi wakati akijaribu kuwatoroka mara baada kuonyesha bunduki aina ya rifle yenye namba 7358 na risasi zake tano.

Amesema bunduki hiyo iliyokuwa imekatwa mtutu na risasi zake tano zilikuwa zimefichwa kwenye soksi, vitu hivyo vilikuwa vilihifadhiwa kwenye mfuko wa sandarusi, na kufichwa chini ya jiwe.

ACP Magiligimba amesema Agosti 23 mwaka huu, mtuhumiwa alikamatwa na wananchi wa kijiji cha Ngamu, na kufikishwa katika kituo cha polisi cha kijiji hicho kwa tuhuma ya kujihusisha na matukio ya ujambazi.

“Kesho yake mtuhumiwa alihojiwa na kukiri kujihusisha na matukio ya ujambazi wa kutumia silaha katika mikoa mbalimbali. Pia aliahidi kuwapeleka askari kuwaonyesha mahali alikoificha silaha anayoitumia kwenye matukio hayo ya ujambazi”, amesema ACP Magiligimba.

Kamanda huyo amesema Agosti 25 mwaka huu saa sita mchana, askari polisi wakiwa na mtuhumiwa, walikwenda katika pori la kijiji cha Mgori mahali alipokuwa ameficha bunduki hiyo aina ya rifle.

“Mara tu baada ya kuwaonyesha askari hao silaha hiyo na wakati askari wanaendelea kufanya upekuzi katika eneo hilo, mtuhumiwa alijaribu kutoroka askari kwa kukimbia” amesema na kuongeza;

“Askari mmoja alifyatua risasi tatu hewani akimtaka asimame, lakini hakutii. Ndipo alipompiga risasi moja iliyompata sehemu ya kiunoni”.

Amesema jereha hilo la risasi lilisababisha mtuhumiwa Hamisi avuje damu nyingi, na hivyo kufariki dunia wakati akikimbizwa hospitali ya mkoa kwa matibabu.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida linaendelea kutoa wito kwa wananchi waote kutoa taarifa zitakazosaidia kubaini wahalifu katika maeneo yao ili hatua ziweze kuchukuliwa kudhibiti vitendo vya kihalifu”, amesema kamanda huyo.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Singida ACP Debora Magiligimba akionyesha bunduki aina ya rifle iliyokuwa ikimilikiwa na mtuhumiwa wa ujambazi Hamisi Athumani (32) mkazi wa Shiponga-Hanang mkoa wa Manyara anayedaiwa kuitumia kwenye matukio ya ujambazi. 
Picha/habari na Nathaniel Limu

HOTUBA YA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI - KAMBI MAALUM YA VIJANA WA CCM

VIJUSO VYA MAGAZETI YA JUMATATU LEO AGOSTI 28,2017

KUTANA NA MWANAMKE ALIYE JITOLEA KUMTIBU MUME WAKE MARADHI MAZITO

$
0
0
Maisha ya ndoa huja na changamoto nyingi sana. Moja kati ya changamoto kubwa wanazo zipata wanandoa ni pale mmoja kati ya wanandoa hao anapo patwa na mtihani wa kuugua maradhi mazito kama vile kisukari au kiharusi.
Jambo hili linapotokea ndoa huyumba kwa kiasi kikubwa sana na mwisho wa siku huweza kufikia hatua ya kuvunjika kabisa.
Hata hivyo si wanandoa wote huwakimbia wenzi wao pindi wanapo patwa na matatizo makubwa hususani maradhi mazito. Mfano mzuri ni kwa mwanadada Tina ( 33 ) mkazi wa Tabata jijini Dar Es Salaam.
Wakati baadhi ya wanawake huwakimbia waume au wapenzi wao pindi wagunduapo kuwa waume au wapenzi wao hao wanakabiliwa na maradhi mazito kama vile kisukari, moyo, kiharusi nakadhalika, hali ni tofauti kwa mwanadada Tina.
Mwanadada huyu , licha ya kuendelea kuiheshimu na kuitunza ndoa yake, lakini pia amejitolea bega kwa bega kushiriki katika tiba dhidi ya maradhi mazito yanayo msumbua mume wake.
Tina anameapa kuwa atahakikisha anapambana hadi tone la mwisho la damu yake ili mradi tu mumewe aweze kupona maradhi hayo mazito yanayo msumbua.
JE NI MARADHI GANI HAYO ? NA JE TINA ANASHIRIKI VIPI KATIKA KUHAKIKISHA MUMEWE ANAPATA TIBA DHIDI YA MARADHI YANAYO MSUMBUA ?
Kuyafahamu yote haya BONYEZA :https://neemaherbalist.blogspot.com/2017/08/kutana-na-mwanamke-aliye-jitolea_26.html

Taasisi ya Women On Wheel - Africa yatoa mafunzo ya udereva kwa wanawake

$
0
0
Bw. Martin Gabone Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Women On Wheel - Africa akizungumza na wanawake akina mama kwa wasichana wakati wa semina ya iliyoandaliwa na Taasisi hiyo kwa ajili ya kuwapa mafunzo ya udereva wa kibiashara ambao utawawezesha kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji.

Bw. Martin Gabone amesema Semina hii ina lengo la kuwaandaa wanawake watanzania na Afrika kwa ujumla kupata ujuzi katika taaluma ya udereva wa kibiashara ambapo wanawake hawa watapata mafunzo maalum katika programu ya Women On Wheel - Africa ili kujiwezesha na kujitegemea kiuchumi kupitia taaluma hii ya udereva wa kibiashara na wenye tija kwa maisha yao na taifa kwa ujumla wake.

Women On Wheel - Africa inawakaribisha wanawake akina mama kwa wasichana kujisajiri ili kujiunga na mpango huu muhimu ambapo mafunzo yanatarajiwa kuanza mwezi wa tisa mwaka huu 2017 jijini Dar es salaam katika ofisi za taasisi ya
Kwa mawasiliano zaidi unaweza kutumia namba hizi
OFISI ZA TAASISI HIYO ZIPO KINONDONI ADA ESTATE KARIBU NA BAKWATA HIGH SCHOOL
AF2AF3
Baadhi ya washiriki wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika katika ofisi za Women On Wheel - Africa Kinondoni.
AF4
Baadhi ya washiriki wakiwa katika semina hiyo iliyofanyika katika ofisi za Women On Wheel - Africa Kinondoni.
AF5
Bw. Martin Gabone Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Women On Wheel - Africa akisisitiza jambo wakati akizungumza na wanawake akina mama kwa wasichana wakati wa semina ya iliyoandaliwa na Taasisi hiyo kwa ajili ya kuwapa mafunzo ya ujasiriamali na kuwawezesha kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji.
AF6AF7
Mjasiriamali Bi Tedy Daniel mmoja wa washiriki wa semina hiyo akifafanua jambo kwa wanasemina wenzake wakati wa mafunzo hayo.
AF8
Bw. Martin Gabone Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Women On Wheel - Africa akiwaelekeza jambo baadhi ya washiriki wakati wa semina ya iliyoandaliwa na Taasisi hiyo kwa ajili ya kuwapa mafunzo ya ujasiriamali na kuwawezesha kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji.

MUONEKANO WA OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU INAYOENDELEA KUJENGWA MKOANI DODOMA

$
0
0
Muonekano wa jengo jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu linaloendelea kujengwa mkoani Dodoma.
Muonekano wa jengo jipya la Makao Makuu ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu linaloendelea kujengwa mkoani Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa akikagua ujenzi wa ofisi hiyo unaoendelea mkoani Dodoma. Wa kwanza kulia ni Mhandisi John Ainainyi Njau kutoka Benki ya Dunia nchini Tanzania.
Mkandarasi wa majengo kutoka kampuni ya Hainan International Ltd inayojenga Ofisi ya Taifa ya Takwimu mkoani Dodoma akitoa maelezo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina chuwa wakati alipotembelea kukagua ujenzi wa ofisi hiyo.
Baadhi ya Wakurugenzi na Maafisa waandamizi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) walioambatana na Mkurugenzi Mkuu wa ofisi hiyo Dkt. Albina Chuwa (hayupo pichani) kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo jipya la Makao Makuu ya ofisi hiyo mkoani Dodoma. (PICHA ZOTE NA VERONICA KAZIMOTO).

VODACOM YAANGUSHA KIAMA CHA MAGOLI 7-1 DHIDI YA HUAWEI KATIKA MCHEZO WA KIRAFIKI

$
0
0
 Wachezaji wa timu ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC, wakishangilia ushindi wao  baada ya kuiadhibu timu ya wafanyakazi wa Huawei mabao 7-1 wakati wa mchezo wa kirafiki ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.
 Mshambuliaji  hatari wa timu ya Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao akifunga goli wakati wa mchezo wa kirafiki na  Kampuni ya Huawei  uliofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam.Vodacom Tanzania PLC iliibuka na ushindi wa magoli 7-1.
 Mkurugenzi Mtendaji  wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Farreo (jezi no.9) na  nahodha wa timu ya kampuni hiyo, Ngayama Matongo (wapili kushoto) wakishangilia ushindi  dhidi ya  timu ya kampuni ya Huawei wakati wa mchezo wa kirafiki baina ya kampuni hizo,uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania Plc ilishinda magoli 7-1
 Mshambuliaji wa timu ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC, (kushoto) Astrid Mapunda akimtoka beki wa timu ya wafanyakazi wa Huawei , wakati wa mchezo wa kirafiki baina ya kampuni hizo, uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania Plc ilishinda magoli 7-1.

Kikosi cha timu ya  wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC, wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, Ian Ferrao(katikati) aliyeshika mpira wakipozi kwenye picha kabla ya kuanza kwa mchezo wa kirafiki dhidi ya  kampuni ya Huawei  uliofanyika kwenye viwanjwa vya Gymkhana jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Vodacom Tanzania iliilaza Huawei  magoli 7-1.

 Mkurugenzi Mtendaji  wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Farreo (kushoto)  akimshuhudia Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huawei  Mengdong Gao,(kulia) akimkabidhi jezi  nahodha wa timu ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania Plc, Ngayama Matongo (katikati) wakati wa mchezo wa kirafiki baina ya kampuni hizo,uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania Plc ilishinda magoli 7-1.
 Mkurugenzi Mtendaji  wa Vodacom Tanzania Plc, Ian Ferrao (kushoto) akisaini mpira wa mfungaji bora wa mchezo wa kirafiki kati ya Vodacom na Huawei uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, ambapo Vodacom Tanzania Plc iliiadhibu Huawei magoli 7-0.Kulia ni  Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huawei  Mengdong Gao. 
 Mabeki wa timu ya Vodacom Tanzania PLC wakimdhibiti mshambuliaji wa timu ya Huawei, Li Kun , wakati wa mchezo wa kirafiki baina ya kampuni hizo, uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania iliibuka kidedea kwa magoli 7-1
 Wachezaji wa timu ya Vodacom Tanzania PLC, wakipeana mbinu za ushindi  wakati wa mapumziko ya mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya wafanyakazi wa kampuni ya Huawei, uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania PLC, ilishinda magoli 7-1
Mfungaji bora wa mechi ya kirafiki kati ya Vodacom Tanzania PLC na Huawei,Kungwi Michael akionesha kiatu cha dhahabu cha ufungaji bora na kikombe mara baada ya kutangazwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania, ilishinda magoli 7-1.
 
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni Huawei Mengdong Gao (kulia)  akimkabidhi  mchezaji wa timu ya Vodacom Tanzania PLC, Kungwi Michael tuzo ya ufungaji bora  baada ya mchezo wa kirafiki baina ya kampuni hizo,uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam, Vodacom Tanzania, ilishinda magoli 7-1 . Kushoto ni nahodha wa timu hiyo, Ngayama Matongo.

YALIYOJIRI KWENYE UZINDUZI WA MFUKO WA ELIMU WILAYANI IKUNGI

$
0
0
BMG Habari, Pamoja Daima!
Jumamosi iliyopita, Agost 19,2017 Wilaya ya Ikungi mkoani Singida ilizindua rasmi “Mfuko wa Elimu Ikungi” ulioanzishwa wilayani humo kwa lengo la kusaidia utatuzi wa kero za elimu ikiwemo uhaba wa maabara, madarasa, vyoo pamoja na nyumba za waalimu.

Katika uzinduzi huo, pia zilifanyika shughuli kadhaa ikiwemo uzinduzi wa ligi ya soka ya “Ikungi Elimu Cup 2017” yenye lengo la kuhamasisha wananchi pamoja na wadau mbalimbali kuchangia Mfuko wa Elimu Ikungi, uzinduzi wa zoezi la ufyatuaji wa matofali ambapo kila Kata wilayani Ikungi imeazimia kufyatua matofali elfu kumi.

Karibu kwa dakika chache kutazama yaliyojiri kwenye uzinduzi huo ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt.Rehema Nchimbi ambaye aliwakilishwa na Katibu Tawala mkoani humo Dkt.Angeline Lutambi huku mwenyeji wake akiwa ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi na mlezi wa Mfuko wa Elimu Ikungi, Mhe.Miraji Jumanne Mtaturu. Tazama video hapo chini.

HIZI NDIO MECHI KUBWA ZA WATANI WA JADI BARANI AFRIKA

$
0
0
Na Jumia Travel Tanzania

Miongoni mwa matukio yanayosisimua zaidi kwenye mchezo wa soka ni mipambano ya watani wa jadi. Katika nchi nyingi barani Afrika ukiwauliza kwa harakaharaka mashabiki wengi wa soka ni mechi zipi huwa wanazisubiria sana utawasikia wanakutajia michezo kama vile Real Madrid na Barcelona, Manchester United na Manchester City, Inter Milan na AC Milan, Liverpool na Manchester United, Chelsea na Arsenal au Bayern Munich na Borussia Dortmund.
Kutokana na umaarufu wa soka la nchi za Ulaya imekuwa ni rahisi kwa mechi zao kufuatiliwa kwa urahisi ukilinganisha na huku Afrika. Lakini hiyo haimaanishi kwamba bara la Afrika nalo halina michezo ya namna hiyo ambayo ikiwa inakaribia homa miongoni mwa mashabiki huwa juu kuliko kawaida.

Ukweli ni kwamba mechi za namna ya mifano iliyotajwa hapo juu zipo na zimekuwa zikichezwa kwa miaka mingi tu.kw au pengine inawezekana ukawa unazisikia tu lakini haujui umuhimu uliopo pindi zinapokutana. Jumia Travel imekukusanyia orodha ya mechi kali za mpira wa miguu ambazo timu zikikutana kunakuwa ni patashika, presha na vimbwanga vya kila aina.  
Orlando Pirates dhidi ya Kaizer Chiefs (Afrika ya Kusini) -  Soweto derby. Kama yalivyo mapambano mengine ya watani wa jadi, mchezo huu ni zaidi ya mpira wa miguu kwani ni uhasama hasa. Mchezo ambao umpewa jina la ‘Soweto derby’ huzikutanisha timu za Orlando Pirates na Kaizer Chiefs mara kadhaa ndani ya mwaka katika jiji la Johannesburg. Uhasama wa timu hizi mbili unakuja kutokana na kuwa zote zinatokea sehemu moja. Kaizer Chiefs ilianzishwa na aliyekuwa mmojawapo wa wachezaji wa Orlando Pirates, Kaizer Motaung.
   
Wydad Casablanca dhidi ya Raja Casablanca (Morocco) - Casablanca derby. Hakuna ubishi kwamba nchi za Afrika ya Kaskazini zimebarikiwa kuwa na vipaji lukuki vya mpira wa miguu ambapo mpaka hivi sasa vinaliwakilisha vema bara hili sehemu mbalimbali duniani. Katika mji wa Casablanca kwenye nyakati tofauti za mwaka kunakuwa na mchezo mkali ambao huzikutanisha timu za Wydad Casablanca na Raja Casablanca ambao pia hujulikana kama ‘Casablanca derby’. Mchezo wa watani wa jadi hawa mara nyingi hupigwa katika uwanja wa Mohammed V Stadium ambapo licha ya kuonyesha nani ni fundi wa kusakata kandanda lakini pia ni juu ya nani ni bora katika anga za kuliwakilisha jiji na nchi kwa ujumla.  
Al Ahly dhidi ya Zamalek (Misri) - Cairo derby. Linapokuja suala la mchezo wa soka basi mashabiki wa timu za Al Ahly dhidi ya Zamalek ni nambari moja kwa kuzishangilia timu zao. Mojawapo ya mitanange mikali kabisa ya soka ambayo hutawaliwa na presha na msisimko mkubwa ni pindi timu hizi zinapokutana ambao pia umepewa jina la ‘Cairo derby.’ Inapofikia siku ya mechi hii hali ya hewa ya jiji zima la Cairo hubadilika kutokana na homa ya mchezo huo. Mbali na kuwa ushindani huwa ni wa kisoka lakini kwa upande mwingine ni wa kisiasa zaidi.
    
Club Africain dhidi ya Espérance Sportive de Tunis (Tunisia) - Tunis derby. Katika jiji la Tunis kwenye ratiba tofauti za mchezo wa soka huzikutanisha timu mbili zinazowakilisha jiji hilo za Club Africain na Espérance Sportive de Tunis. Ushindani mkubwa katika mchezo huu umekuwa na historia tofauti ambapo hapo awali ulihusishwa na matabaka kama vile ilisemekana timu ya Espérance ilikuwa ikimilikiwa na serikali na tabaka la juu la watu wa mji wa Tunisia huku Club Africain ikimilikiwa na watu maarufu wa matabaka tofauti. Lakini hiyo imebadilika na ikawezekana kutokuwa na ukweli ndani yake kwani unaweza kukuta watu wa familia moja wanashabikia hizo kwa wakati mmoja.
  
Simba S.C. dhidi ya Young Africans S.C. (Tanzania) - Dar es Salaam au Kariakoo derby. Tukiachana na umaarufu wa mchezo wa mpira wa miguu katika nchi za Afrika ya Kuskazini pia katika kalenda za soka barani Afrika huwa inapigwa mechi kali sana kwenye ukanda wa Afrika ya Mashariki baina ya timu za Simba na Young Africans au Yanga ambazo zote hutokea jiji la Dar es Salaam. Mbali na timu hizo kukutana katika michezo kadhaa ya ligi kuu pia kuna michezo mingine ni pamoja na ngao ya jamii, kombe la shirikisho la mpira wa miguu, kombe la mapinduzi ne mingineyo. 
Kama ni mgeni kwenye jiji la Dar es Salaam basi ikifika siku ya mchezo huo utajua homa ya watani wa jadi wa timu hizo mtaani kwani utawatambua mashabiki wa timu hizo kwa mbwembwe, tambo na shamrashamra kwa kuvalia jezi za rangi nyekundu na nyeupe (Simba) huku Yanga ni (kijani na njano). 

Uhasama wa timu hizo ambazo zinatokea katika eneo moja la Kariakoo si tu kuhusu mpira bali ni heshima juu ya nani ni mfalme na bingwa wa kusakata kandanda nchini Tanzania na kuliwakilisha taifa kwenye anga za kimataifa. Mchezo baina ya timu hizi mbili huwa unapigwa kwenye uwanja wa taifa ambao unao uwezo wa kukusanya mashabiki takribani 60,000.
USM Alger dhidi ya MC Alger (Aljeria). Mchezo huu wa watani wa jadi kama ilivyo mingine huzitenganisha familia na majirani na wakati mwingine huisha kwa ugomvi na vurugu baina ya mashabiki wa pande mbili. Uhasama baina timu ya hizi mbili unahusishwa kwa kiasi kikubwa na historia ya nchi hiyo wakati wa harakati za kudai uhuru. Katika sehemu mbalimbali za nchi ya Aljeria mchezo baina ya timu hizi mbili hubakia kuwa ni tukio la kitaifa kutokana na kuzungumziwa na kupewa nafasi kubwa kwenye vyomo tofauti vya habari.

TP Mazembe dhidi ya FC Lupopo (R.D Congo). Jina la TP Mazembe sio geni miongoni mwa mashabiki wengi wa soka nchini Tanzania kutokana na wachezaji wa hapa nyumbani Mbwana Samata ambaye alifanikiwa kujitwalia taji la mchezo bora wa ndani wa Afrika na Thomas Ulimwengu kuchezea pale. Katika jiji la Lubumbushi kila mwaka kunakuwa na tukio kubwa la mchezo wa soka ambalo huwakutanisha watani wa jadi kati ya TP Mazembe na FC Lupopo.

Gor Mahia dhidi ya AFC Leopards (Kenya) - Nairobi au Mashemeji derby. Shamrashamra na tambo za mashabiki wa mchezo wa mpira miguu katika mitaa mbalimbali ya jiji la Nairobi huonekana wazi pindi timu za Gor Mahia na AFC Leopards zinapokutana. Mchezo huu ambao una historia ya muda mrefu kwenye soka nchini Kenya huchukuliwa kama ni siku kubwa ambapo mashabiki licha ya kuonyesha uhasama mkubwa lakini ni sherehe, likizo na huchukuliwa kama siku maalum.
Asec Mimosas dhidi ya Africa Sport Abidjan (Ivory Coast) - Abidjan derby. Miongoni mwa tukio baya kutokea pindi timu hizi mahasimu zinazotokea katika jiji la Abidjan nchini Ivory Coast ni mwaka 2001 ambapo vurugu zilitokea ambapo mtu mmoja alifariki huku 30 wakijeruhiwa. Timu ya Asec Mimosas inajivunia kwa kutoa vipaji vikubwa kabisa vya soka nchini humo na duniani wakiwemo Kolo Toure, Didier Drogba na Gervinho.

Al-Merreikh dhidi ya Al-Hilal (Sudani). Uhasama wa timu hizi mbili zinazotokea kwenye jiji la Omdurman nchini Sudan ambapo mnamo mwaka 1934 timu ya Al-Merreikh iliifunga Al-Hilal kwa mabao 2 bila ya majibu ambapo kulikuwa hakuna uwanja enzi hizo. Uhasama baina ya timu hizo mbili pia huchochewa kwa kiasi kikubwa na idadi ya wachezaji kila timu iliyo nayo kwenye kikosi cha timu ya taifa.      
Ipo michezo mingine mingi tu ya watani wa jadi kwenye soka lakini hiyo ndiyo mikubwa ambayo inasubiriwa na kuangaliwa zaidi. Jumia Travel inaamini kwamba sasa utakuwa umeijua na utaanza kuifuatilia kwani kuna burudani nyingi ulikuwa ukiikosa kwa kutoifuatilia. Mechi hizo kutokupewa nafasi kubwa na vyombo vya habari tofauti barani Afrika kama ilivyo kwa ile ya Ulaya haimaanishi kwamba haina ushindani mkubwa.

MAHAFALI YA 6 YA GENIUS KINGS YAFANA JIJINI DAR

$
0
0
Mkurugenzi Mkuu wa Shule ya Genius Kings Nusery& Primary School, Machage Kisyeri, (Kulia) akisoma hotuba.
Mwalimu Mkuu wa shule, Aloyce Siame (kushoto) akimkabidhi risala Profesa Joseph Kahamba , ambaye alikuwa mageni rasmi wakati wa mahafali hayo.Katikati ni Mkurugenzi wa shule Julius Rutabanja.
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Aloyce Siame (kulia) akikabidhiwa zawadi ya kikombe na Profesa Joseph Kahamba.
Paroko msaidizi wa Roho Mtakatifu Parokia ya Segerea Velence Kisaka (kulia) akibarikia shule hiyo baada ya kufanya ibada kwa ajili ya kuwaombea wanafunzi wa darasa la saba wanaojiandaa na mitihani ya taifa.
Mwalimu wa Dini ya Kiislam Shekhe Hussein Abdalah akiongoza swala kwa ajili kawaombea watoto wa darasa la saba katika shule hiyo.
Mgeni rasmi akiangalia wanafunzi wakifanya majaribio ya sayansi.
Wahitimu wakitoa burudani kwa wazazi na wageni waalikwa.
Kikosi cha scout shuleni hapo wakifanya mambo yao
Wanafunzi wakionyesha kipaji cha kucheza ngoma za asili.
*Wahitimu waaswa kwenda na kasi ya sayansi na teknolojia
Wakati serikali ya Tanzania inao mkakati wa kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda,wanafunzi wanaohitimu masomo wametakiwa kujiona sehemu ya mkakati huo na kusoma kwa bidii kupata ujuzi wa taaluma mbalimbali ikiwemo kutoogopa kusoma masomo ya hesabu na sayansi.
Ushauri huo umetolewa na daktari bingwa nchini wa magonjwa ya nevu (Neurosurgery) kutoka Chuo Kikuu cha Muhimbili,Profesa Joseph Kahamba, wakati wa mahafali ya darasa la saba ya msingi ya Genius Kings yaliyofanyika Segerea jijini Dar es Salaam .
Profesa Kahamba alisema kuwa nchi yetu bado inakabiliwa na changamoto ya kuwa na wataalamu waliobobea katika nyanja mbalimbali ambapo aliwataka wanafunzi wanaohitimu masomo na waliopo mashuleni na vyuoni kujipanga kuhakikisha wanapata utaalamu wa fani mbalimbali tayari kwa kutumikia taifa la Tanzania.
“Wanafunzi waliopo mashuleni na vyuoni mnapaswa kujipanga kwa kuhakikisha mnasoma kwa bidii na kupata ujuzi wa fani mbalimbali kwa kuwa mapinduzi ya kuendeleza taifa letu yanayoendelea yanahitaji wataalamu wa fani mbalimbali na wanaotegemewa kuchukua majukumu hayo hawatoki nje ya nchi bali ni nyinyi vijana wa kitanzania”Alisema Profesa Kahamba.
Aliongeza kusema kuwa kinachotakiwa kwa wanafunzi waliopo mashuleni na vyuoni kujibidisha kusoma kwa bidii na kupata taaluma za fani mbalimbali na wahakikishe wanajiamini na kuhakikisha ndoto zao walizojiwekea zinatimia na wanakuwa na uzalendo wa kuitumikia nchi na kuleta maendeleo chanya katika jamii kupitia elimu waliyoipata.
Profesa Kahamba aliupongeza uongozi wa shule ya Genius Kings kwa kufanya uwekezaji katika sekta ya elimu kwa kuwa umelenga kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha elimu nchini na kuleta mabadiliko wenye jamii kwa kuwa elimu ni njia pekee ya kuleta maendeleo kwa haraka katika ujenzi wa taifa . “Naupongeza uongozi wa shule kwa kuwekeza katika elimu na nawapongeza wazazi ambao wanawekeza katika elimu kwa kusomesha watoto wao maana elimu bora katika jamii inachangia kuleta mabadiliko ya nchi haraka”.Alisema
Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw. Aloyce Siame, alisema kuwa katika kipindi cha miaka 10 tangu shule ianzishwe imeweza kushikilia rekodi ya kufanya vizuri kwa kufaulisha wanafunzi wa darasa la saba na la nne kwa kiwango cha juu na kuingia katika shule tano bora wilayani Ilala na shule bora 20 mkoani Dar es Salaam mfululizo hali ambayo imewajengea hari ya kuzidi kufanya vizuri kwa mwaka huu na miaka ijayo.
“Moja ya mtazamo wa shule hii ni kuifanya kuwa shule bora ya mfano inayotoa elimu bora nchini kuanzia shule ya awali na shule ya msingi na sekondari.”Tumejipanga kuhakikisha lengo hili linatimia na tunatoa shukrani kwa serikali,wazazi na wadau wote ambao wameonyesha kutuunga mkono katika kipindi hiki cha awamu ya kwanza ya mwanzo ya miaka 10 na kuwezesha mafanikio haya kupatikana”.Alisema.
Kwa upande wake,Mkurugenzi mkuu wa shule hiyo ,Bw.Machage Kisyeri,aliwapongeza wahitimu kwa kufikia hatua hiyo na aliwataka watumie elimu waliyoipata kujipanga zaidi kwa masomo ya sekondari ambayo yanawakabili mbele yao. “Maisha sio lelemama mnapaswa kupambana zaidi katika hatua inayofuatia na kuhakikisha msingi wa elimu imara tuliyowapatia unawaongoza kuelekea katika kupata mafanikio ya kitaaluma popote pale mtakapokwenda”Alisisitiza.
Aliongeza kuwa shule imejizatiti kuunga mkono jitihada za serikali za kuboresha elimu nchini ambapo kuanzia mwezi Januari mwakani itaanza kutoa elimu ya sekondari katika shule yake mpya iliyojengwa sehemu ya Mataya wilayani Bagamoyo katika mkoa wa Pwani.
Kuhusiana na changamoto wanazokabiliana nazo alisema kuwa zipo changamoto za kawaida kinachotakiwa ni ushirikiano baina ya wazazi,walimu,na wadau wanaosimamia elimu ili kuhakikisha mafanikio yanapatikana na elimu ya Tanzania inazidi kupanda “Walimu wakiwezeshwa vizuri na kupewa ushirikiano wa kutosha naamini shule nyingi za Tanzania zitatoa elimu bora kwa kuwa tunao walimu wengi wazuri ambao wakitumiwa ipasavyo tutasonga mbele”.Alisema.

NAIBU WAZIRI WA AFYA KUZIPIGA JEKI HOSPITALI ZA MKOA WA RUVUMA.

$
0
0
Watanzania wametakiwa kuchunguza afya zao mara kwa mara iliwaweze kujua hali ya afya zao na kuondokana na magonjwa ambayo yanaweza kuwapata hasa yale ambayo si ya kuambukizwa ilikuweza kubaini afya zao kwa kuwa yanachukua kipindi kirefu mpaka mtu aje kugundulika kuwa anadalili za magonwa hayo. Kampeni hiyo ya uchunguzi kwa magonjwa ya saratani ya mlango wa kizazi.matiti,kifua kikuu na magonjwa yasiyo ambukizwa yamefanyika katika uwanjwa wa majimaji yakiongozwa na naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia na watoto HAMIS KIGWANGALA.
Viewing all 46373 articles
Browse latest View live




Latest Images